Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Darasa la saba wafeli hesabu za la Darasa pili

$
0
0
Wanafunzi wa darasa la saba wameshindwa kufanya hesabu za darasa la pili baada ya kubainika ni asilimia 69 pekee wanaoweza kufanya hesabu hizo. Pia asilimia 48 tu ya darasa la tatu  wanaweza kufanya hesabu za darasa la pili

Aidha, asilimia 38 ya wanafunzi wa darasa la tatu ndiyo wanaoweza kusoma hadithi ya kingereza ya darasa la pili na asilimia 82 ya wanafunzi wa darasa la saba wamebainika kuweza  kusoma hadithi ya Kiingereza ya darasa la pili.

Utafiti huo kwa mujibu wa taasisi ya Twaweza ulifanyika katika wilaya 159 ukishirikisha sampuli ya watoto 112,455 wenye miaka kati ya saba hadi 16.

Akizindua ripoti hiyo jana Desemba 3 katika shule ya msingi mazoezi afisa tawala wilaya ya Monduli, Sharif Mziray alisema kwamba serikali imeipokea ripoti hiyo kwa mikono miwili na imewasaidia kuwafungua mambo mengi.

Mziray, alisema  kwamba serikali inaichukulia ripoti hiyo kama changamoto na kuanzia sasa watatengeneza mazingira wezeshi kwa walimu na wanafunzi ili kujenga mazingira bora ya watoto kujifunza.

“Hii ni changamoto kwetu sisi kama serikali ya wilaya lakini wazazi pamoja na walimu mna changamoto ya kuhakikisha mnaweka mazingira mazuri ya watoto kujifunza”alisema Mziray

Hata hivyo, mratibu wa programu ya Uwezo wilayani Monduli, Mohammed Nkinde alisema  kwamba wilaya hiyo imeshika nafasi ya 43 kati ya 159 katika ngazi ya kitaifa na nafasi ya 4 katika ngazi ya mkoa  katika uwezo wa watoto kujifunza.

Nkinde, alisema kwamba mahudhurio ya walimu na ufundishaji kwa ujumla upo chini wilayani Monduli kwa kuwa kiwango cha mahudhurio wilayani humo kinaonyesha kuwa ni asilimia 86 ya mahudhurio ya walimu na asilimia 75 ya mahudhurio ya wanafunzi kiwango ambacho hakiridhishi.

“Hii inaonyesha kwamba muda wa wanafunzi na mwalimu kukutana au kufundisha darasani wakati wa muda wa shule ni mdogo na hivyo wanafunzi hawapati muda unaopaswa kufundishwa ili waweze kujifunza stadi za msingi” alisema  Nkinde

Ofisa maadili na nidhamu kutoka tume ya utumishi wa walimu wilayani humo, Rhoda Msemo alikemea tabia ya baadhi ya wazazi ambao hawakubahatika kwenda shule kutokagua madaftari ya watoto wao na kusema tabia hiyo haifai.

“Kuna baadhi ya wazazi hawakupata bahati ya kwenda shule hivyo wanawaogopa watoto wao hata kukagua home work (kazi za nyumbani) hawakagui hii si sawa kagueni kazi zao hawa watoto msiwaogope” alisema Msemo

Simba Kicheko Tu....Haya Ndo Mambo 10 Bilionea Mohammed Dewji Atakayoanza Nayo Baada ya Kukabidhiwea Timu Hiyo

$
0
0
Bilionea Mohammed Dewji ameipokea kwa mikono miwili ishu yake ya ushindi kuwa mwekezaji mpya Simba na ametoa ahadi zake 10 kuhakikisha zinafanyika kuleta mabadiliko makubwa.

Mo Dewji ameshinda zabuni ya kuwa mwekezaji wa Simba kwa dau la Sh bilioni 20 alizoweka ‘mezani’ na hakukuwa na mtu yoyote aliyejitokeza kushindana naye kama ilivyokuwa ikielezwa awali.

MOJA:
Kambi ya Simba itajengwa upya kabisa na itakuwa ni hosteli ya kisasa yenye vyumba hadi 35. 30 vitakuwa kwa ajili ya wachezaji na vitano kwa ajili ya benchi la ufundi.
 
MBILI:
Simba sasa itafaidika kwa kuwa na gym yake ya kisasa, bwawa kubwa la kuogelea kwa ajili ya mazoezi na sehemu ya kupumzika kwa wachezaji.
 
TATU:
Wachezaji, makocha na viongozi watakuwa na mgahawa wao wa kisasa kabisa.
 
NNE:
Mo Dewji anaamini timu lazima iwe na viwanja vya mazoezi. Hivyo ataanza na viwanja viwili, kimoja nyasi asilia na kingine nyasi bandia.
 
TANO:
Mo Dewji ameahidi kuwekeza katika soka la vijana akianza na wale wenye umri wa chini ya miaka 14, 16 na 18 na lengo ni kuwakuza.
 
SITA:
Mo Dewji amesema atasimamia wachezaji kuitambua thamani ya Simba kwa kujituma hasa.

SABA:
Simba itaanza kufanya mambo kimataifa kwa kuitangaza na kuikuza brand ikiwa ni pamoja na kutengeneza vifaa mbalimbali kama fulana, kofia, vishika ufunguo na kadhalika.

NANE:
Ameahidi kutenga kitita cha  Sh milioni 500 ambazo zitatumiwa na benchi la ufundi katika mipango yao kama kambi na kadhalika pia Sh bilioni moja kwa ajili ya usajili.

TISA:
Kushindana na timu kubwa Afrika na sio Tanzania pekee.

KUMI:
Kurejesha Simba katika historia ya kimataifa

TBA Yakiri Kubomoka kwa Mabweni Mapya ya UDSM Yaliyozinduliwa na JPM

$
0
0
Mkurugenzi wa Wakala wa Majengo nchini Mhandisi Elius A. Mwakalinga, amekiri picha zinazosambaa mitandaoni zikionyesha majengo mapya ya mabweni ya UDSM yana nyufa ni za majengo hayo, huku akisema ni kitu cha kawaida kwa majengo makubwa.

Mwakalinga amesema kutokea kwa nyufa hizo ni moja ya hatua za 'expansion joint' ambazo hutumiwa kwenye ujenzi wa majengo, lakini majengo hayo yamekidhi vigezo vyote na vipimo wakati wa ujenzi wake.

"Kila design tunayofanya ya majengo sasa hivi tunatumia expansion joint, majengo mengi makubwa huwa inatumia hiyo, hivyo ni common na sio creck kubwa sana kama inavoonekana kwenye picha, nilienda ile jana usiku kukagua tukakuta hiyo hali, ni process za majengo ili yaweze kusatle, hivyo watu wawe na amani kabisa wala wasiwe na hofu", amesema Bwana Mwakalinga.

Mwakalinga ameendelea kwa kusema kwamba watu wanaosambaza picha hizo bila kutaka ufafanuzi kutoka kwake wanafanya makosa kwani wanawatia watu hofu kwa jambo la kawaida kwenye hatua za ujenzi, huku wakilaumu kitu ambacho hawana uhakika nacho.

Kauli ya Polepole Baada ya Mbunge wa CUF Kujiuzulu na Kutangaza Kuhamia CCM

$
0
0
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Humphrey Polepole  amesema Chama cha Mapinduzi (CCM) hakitampokea yeyote anayetaka kurudi ndani ya chama hicho bila kufuata utaratibu. 

Kauli hiyo imekuja baada ya aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Kinondoni(CUF), Maulid Said Abdallah Mtulia kutangaza kujiuzulu nafasi zake zote za uongozi alizokuwa akizishikilia kwenda CCM.

Polepole aliyasema hayo wakati akiwahutubia wananchi wa CCM mkoa wa Mara katika uchaguzi wa Mwenyekiti wa Mkoa wa Chama.

“Ameamua kule aliko haoni itikadi,haoni siasa, haoni mwelekeo, Chama kina baba wawili huwezi kuwa na nyumba ina baba wawili alafu utasikiliza watoto watamsikiliza nani, basi amehama,” alisema Polepole.

“Sasa mimi niko hapa Musoma mimi nitumie fursa hii anayemuunga mkono ni Rais wetu ambaye ni mwana CCM kwelikweli na ndiye Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi ikimpendeza afuate utaratibu akiona mazuri ya Rais yule asione vinaelea kwa mazuri yale asione vimeshushwa vimeundwa na wanaounda mambo mazuri ya Magufuli ni Chama cha Mapinduzi.”

Wanafunzi Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) Wazungumzia Sakata la Hosteli Yao Mpya Kuanza Kubomoka

$
0
0
Baadhi ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) wameingia hofu baada ya mabweni wanayoishi kuwa na nyufa.

Mabweni hayo yanayotumiwa na wavulana katika jengo la Block A yana nyufa sehemu mbalimbali kuanzia chini hadi ghorofa ya tatu.

Mbunge wa serikali ya wanafunzi (Daruso), Simon Masenga amesema nyufa hizo zilianza kuonekana wiki mbili zilizopita.

Amesema walitoa taarifa kwa meneja wa hosteli lakini majibu waliyopewa ni kuwa majengo hayo yako chini ya Wakala wa Majengo Tanzania (TBA).

Mbunge mwingine wa serikali ya wanafunzi, Kumbusho Dawson amesema leo Jumatatu Desemba 4,2017 kuwa majengo hayo yana upungufu, ukiwemo wa maji kutuama kwenye bafu na kutokuwa na makabati.

"Tumelalamika kwa meneja wa mabweni kuhusu upungufu katika majengo haya na majibu tunayopewa ni kuwa bado yako chini ya TBA," amesema Dawson.

Majengo hayo yaliyojengwa na TBA kwa miezi minane yakielezwa kugharimu Sh10 bilioni yalizinduliwa Aprili 15,2017.

Ujenzi ulifanyika ikiwa ni utekelezaji wa agizo la Rais John Magufuli la kumaliza tatizo la malazi kwa wanafunzi wa UDSM.

Picha zinazoonyesha nyufa kwenye majengo hayo zilianza kusambaa mitandaoni jana Jumapili Desemba 3,2017.

Bunduki ya Mbunge Joshua Nassari Yaanza Kuchunguzwa

$
0
0
Wakati mbunge wa Arumeru Mashariki (Chadema), Joshua Nassari akilihusisha tukio la kuvamiwa nyumbani kwake na watu wasiojulikana na masuala ya kisiasa, polisi inashikilia bunduki ya mwanasiasa huyo kwa uchunguzi.

Polisi mkoani Arusha imesema imeanza uchunguzi wa kina wa kuwasaka washukiwa, huku ikichunguza silaha ya Nassari aina ya shotgun, ikisema tukio hilo lina utata kutokana na mazingira lilivyotokea.

Kamanda wa polisi wa mkoa, Charles Mkumbo amesema  kuwa wameanza uchunguzi wa kina ili kubaini endapo kulikuwa na tukio au la.

“Tunaifanyia uchunguzi bunduki yake, tunataka kujiridhisha endapo kulikuwa na tukio au la,” alisema Mkumbo.

Hata hivyo, kamanda huyo alisema msako unaendelea ili kuwabaini washukiwa na kwamba hawajapata maganda ya risasi zinazodaiwa kutumika katika uvamizi huo.

Juzi Nassari aliwaambia waandishi wa habari kuwa nusu saa baada ya kuwasili nyumbani kwake alisikia hali isiyo ya kawaida ndani ya uzio wa nyumba na baadaye kulisikika milio ya risasi. Alisema mbwa wake aliyekuwa akibweka alinyamaza, hali iliyomfanya achukue silaha yake kujihami.

“Nilipiga risasi tano, kisha kukawa kimya nikaenda kuwaamsha vijana wanaonisaidia hapa nyumbani kuwaeleza tukio lililotokea kisha nikaondoka.”

Alisema waliofanya tukio hilo hawakujua kama ana silaha kwa sababu mwaka 2014 wakati wa uchaguzi wa Serikali za mitaa, bastola yake ilichukuliwa na polisi na hadi leo haijarudishwa, hivyo kuwa na silaha nyingine kulimsaidia kujibu mapigo.

Katika tukio hilo, Nassari alisema aliwajibu watu hao kwa kupiga risasi tano hewani huku wenyewe wakipiga 12 na moja ilimpata mbwa wake ambaye alimzika juzi katika maeneo ya nyumba anayoishi.

Hivi karibuni mbunge huyo aliwasilisha makao makuu ya Takukuru ushahidi wa CD aliodai kuwa unawahusisha madiwani wa Chadema mkoani Arusha kushawishiwa kuhamia chama tawala.

CUF ya Maalim Seif Yachekelea Maulid Mtulia kujiuzulu Ubunge

$
0
0

Uamuzi wa Maulid Mtulia kujivua ubunge na uanachama haujakishtua chama chake cha CUF, badala yake kimesema bado wengine wawili ambao kingependa waondoke haraka.

Hilo lilisemwa jana na katibu mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad ambaye anaongoza upande mmojapo kati ya mbili zinazokinzana. Upande mwingine unaongozwa na Profesa Ibrahim Lipumba.

Naibu katibu mkuu wa CUF (Zanzibar), Nassor Ahmed Mazrui amesema kuwa, Mtulia ni mmoja wa wabunge watatu wanaomuunga mkono Profesa Lipumba.

“Hatukutarajia kama Mtulia ataondoka wakati huu, bali tulijua ataendelea kudumu. Lakini kama ameondoka ni faraja kwetu kwa sababu katika mipango yetu tulishamuondoa,” alisema Mazrui.

“Tunawaombea dua wale wawili waliobaki waondoke hata leo kwa sababu kuendelea kukaa kwao ndani ya CUF ni kukidhoofisha chama hiki.”

Mazrui aliwataka wabunge kutoshangaa endapo wenzao hao watatangaza kujiuzulu nafasi zao akidai kuna mipango inaendelea kupangwa ili kufanikisha mchakato huo.

“Narudia tena na waondoke, tena waondoke haraka. Ninawahakikishia wana CUF kuwa chama hiki kipo imara na wasiwe na hofu,” alisema Mazrui.

Alisema CUF ni taasisi imara na kati ya wabunge 40, watatu alidai wamekuwa wakikivuruga chama hicho kwa kushirikiana na Profesa Lipumba.

Akizungumzia kuondoka kwa Mtulia, alisema wakati mwingine akifa mgonjwa uliyemuuguza muda mrefu unamshukuru Mungu.

“Tunamshukuru Mungu maana tumeuguza vya kutosha. Haikuwa bahati yetu,” alisema.

CUF ya Lipumba Yawaomba radhi wapiga kura Kinondoni Baada ya Mbunge wake Maulid Mtulia Kujiuzulu

$
0
0
Chama cha Wananchi  (CUF), upande wa Profesa  Ibrahim  Lipumba kimewaomba radhi wapiga kura wa jimbo la Kinondoni  baada ya aliyekuwa mbunge  wa jimbo hilo kupitia chama hicho, Maulid Mtulia kujiuzulu.

Kauli imetolewa  leo, Jumatatu  Desemba 4, 2017 na Mkurugenzi  wa Habari, Uenezi na Mawasiliano ya Umma, Abdul  Kambaya wakati akizungumza  na wanahabari kwenye makao makuu ya chama hicho Buguruni.

Amesema CUF iliwaaminisha wakazi wa Kinondoni  kwa kumpeleka Mtulia kugombea jimbo hilo kwa kuwa ni mtu makini na mambo mengi alishaanza kuyatekeleza ikiwamo kuzuia bomoa bomoa lakini wanasikitika kujiuzulu kwake.

"CUF  haikutarajia kuingia katika uchaguzi mdogo hasa jimbo la Kinondoni  kabla ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020 labda kingetokea kifo. Tunawaomba radhi wakazi wa Kinondoni," amesema Kambaya.

Kambaya amesema sababu za kujiuzulu  alizozitoa Mtulia ni za msingi kwake lakini kwao hazina maana wala mashiko.

Desemba 2, Mtulia alitangaza kujiuzulu nafasi ya ubunge huku akisema amefikia uamuzi huo bila kushawishia na mtu yoyote na ameamua kuhamia CCM.

Rais Magufuli Akutana Na Mwakilishi Mkazi Wa Benki Ya Dunia, Aendesha Baraza La Mawaziri Ikulu Jijini Dar Es Salaam Leo

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Joseph Magufuli akiwa na Mkurugenzi Mkazi wa Benki ya dunia nchini Bi. Bella Bird aliyekutana na kufanya naye mazungumzo Ikulu jijini Dar es salaam leo Novemba 4, 2017

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Joseph Magufuli aakiendesha kikao cha Baraza la Mawari  Ikulu jijini Dar es salaam leo Novemba 4, 2017
PICHA NA IKULU

Tundu Lissu atuma salamu wiki ya msaada wa sheria....Awataka Watanzania Wasichoke Kumuombea

$
0
0
Rais wa Chama cha Wanasheria wa Tanganyika (TLS), Tundu Lissu ametumia maadhimisho ya wiki ya msaada wa sheria kuwaomba wananchi kumwombea apone na kurudi nchini aendelee kutoa mchango wake katika taaluma ya sheria.

Lissu tangu Septemba 7 amelazwa katika Hospitali ya Nairobi nchini Kenya anakopatiwa matibabu baada ya kushambuliwa na kujeruhiwa kwa risasi akiwa katika makazi yake Area D mjini Dodoma.

Akizungumza leo Jumatatu Desemba 4,2017 katika ufunguzi wa wiki ya msaada wa sheria, mwakilishi wa TLS, John Seka amesema Lissu anawasalimia wananchi.

“Rais wa TLS, Tundu Lissu anawasalimia sana, anaendelea kupata nafuu ila anawaomba Watanzania waendelee kumwombea ili apone haraka,” amesema Seka.

Amesema Lissu ambaye pia ni mbunge wa Singida Mashariki (Chadema) ana hamu ya kurudi nyumbani aendelee kutoa mchango wake wa kisheria kwa wananchi.

Kuanzia leo hadi Desemba 8,2017 wananchi wanapata fursa ya kupata msaada wa kisheria katika migogoro inayowakabili.

Seka ametoa wito kwa wananchi kufika katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam na mikoani kupata huduma ya msaada wa kisheria.

Amesema baada ya wiki hiyo kumalizika, wananchi watatakiwa kufika ofisi za TLS kupata msaada wa kisheria kwa kuwa hilo ni moja ya majukumu ya chama hicho.

Mtulia Atua Rasmi CCM na Kukabidhiwa Kadi....... Awajibu Wanaomtuhumu Kusaliti Upinzani

$
0
0
Aliyekuwa  Mbunge wa Kinondoni kupitia Chama Cha Wananchi (CUF), Maulid Mtulia leo Jumatatu Desemba 4, 2017 amekabidhiwa rasmi kadi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) mapema leo katika ofisi za chama hicho.

==>YALIYOSEMWA NA MAULID MTULIA MARA BAADA YA KUKABIDHIWA KADI YA CCM LEO
“Nimejivua nyadhifa zangu zote ya Ubunge wa Kinondoni na vyeo vyote nilivyokuwa navyo CUF na kuamua kujiunga na CCM kutokana na kuridhishwa na CCM ya sasa na utendaji wa Rais Dk. Magufuli.

“Mimi ni mgeni na salamu ninayoijua ya CCM ni CCM Oyeee. Nimejiunga na CCM ili kuunga mkono kazi nzuri inayofanywa na Rais Dk. Magufuli. Nimetoka kwenye chama chenye migogoro mingi, nimekuja kwenye chama chenye amani, haki na Demokrasia ya kweli. Ningekuwa Mbunge kupitia CCM ningefanya mengi makubwa zaidi,” alisema Mtulia.

“Sijaja CCM kutafuta cheo bali nimetumia haki yangu ya kidemokrasia ya kujiunga na chama chochote kile ninachokitaka. Kila jambo nililokuwa namwomba Rais tena hadharani (mfano wakati wa ufunguzi wa maghorofa) ameyatekeleza kwa kiwango kikubwa.

“Nawashangaa Viongozi wa Upinzani wanaopinga na kususa mambo ya Serikali na shughuli za Bunge, hizo shida za Wananchi Nani atawatatulia endapo wanawasusia wenye mamlaka? Nipo tayari kuwa hata Balozi wa nyumba kumi na ikishindikana nitaenda kuvua samaki nyumbani Rufiji.

“Nawahaidi wana CCM watafurahia uwepo wangu na watanufaika nami ndani ya CCM. Nawaambia wana Kinondoni wasikosee, wachague Mbunge anayetokana na CCM. Wachague CCM siku zote,”  alisema Mtulia

IMETOLEWA NA;
Idara ya Uhamasishaji na Chipukizi
UVCCM Taifa.

Mahakama Yagoma Kufuta Mashtaka 20 ya Gugai wa Takukuru

$
0
0
Mahakama ya Hakimu Mkuu mkazi Kisutu imekataa kuyafuta mashtaka 20 ya utakatishaji fedha kati ya 43 yanayomkabili aliyekuwa mhasibu wa TAKUKURU Godfrey Gugai na wenzake na kusema kuwa mashtaka hayo kwa sasa yana nguvu kisheria.

Akitangaza uamuzi huo wa mahakama Hakimu Mkazi Kiongozi Thomas Simba amesema uamuzi wake huo unahitimisha mjadala aliouahirisha aliposikiliza kesi hiyo kwa mara ya kwanza Novemba 16 kama je mashtaka ya utakatishaji fedha katika hati ya mashtaka ya Gugai na wenzake yaendelee au la.

Mara baada ya kutoa maamuzi hayo Hakimu Simba ameahirisha kesi hiyo hadi Desemba 18 mwaka huu baada ya upande wa mashtaka ukiongozwa na wakili Vitalis Peter kusema kuwa upelelezi haujakamilika ambapo watuhumiwa wanatetewa na wakili Alex Mgongolwa.

Godfrey Gugai na wenzake watatu walifikishwa katika mahakama hiyo ya Kisutu wakikabiliwa na makosa 43 ikiwemo kutakatisha fedha,udanganyifu pamoja na umiliki wa mali nyingi kwa Gugai kinyume na kipato chake halisi ambapo makosa mengi yanamhusu Gugai pekee yake.

Kutokana na uamuzi uliotolewa safari hii na Hakimu Simba Washtakiwa wote wamerudishwa rumande kwa kuwa  mashtaka wanayokabiliwa nayo,ya utakatishaji fedha,hayana dhamana na kesi yao itasomwa tena mahakamani hapo Desemba 18.

Benki ya Dunia yajipanga kukuza uchumi wa Tanzania na kupunguza umasikini

$
0
0
Mwakilishi wa Benki ya Dunia katika nchi za Tanzania, Burundi, Malawi na Somalia Bi. Bella Bird amemhakikishia Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli kuwa benki hiyo imejipanga kuendelea kutoa mikopo nafuu kwa miradi mbalimbali ya maendeleo hapa nchini ili kukuza uchumi na kupunguza umasikini.

Bi. Bella Bird ametoa kauli hiyo leo tarehe 04 Desemba, 2017 Ikulu Jijini Dar es Salaam na kubainisha maeneo ya kipaumbele kuwa ni miundombinu hususani barabara na reli, kuongeza uzalishaji na usambazaji wa nishati ya umeme, Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) na elimu kwa kujielekeza katika ubora na kuhakikisha idadi ya wanaopata elimu inaongezeka.

Maeneo mengine ni kuboresha sekta ya afya, kuongeza upatikanaji wa maji, usimamizi bora wa ardhi, mawasiliano, huduma za fedha jumuishi, vituo vya pamoja vya Serikali na kusaidia familia masikini.

Bi. Bella Bird amempongeza Mhe. Rais Magufuli kwa usimamizi mzuri wa miradi ya maendeleo inayotekelezwa na Benki ya Dunia na amemuahidi kuwa benki hiyo itaendelea kushirikiana kwa karibu na Tanzania katika utekelezaji wa miradi mingine.

“Mwaka uliopita Benki ya Dunia imetoa mikopo nafuu yenye thamani ya Dola za Marekani Bilioni 1.2 (Shilingi Trilioni 2.7) kwa Tanzania, fedha hizi zimekwenda katika miradi mbalimbali na tunafurahi kuwa miradi hiyo inakwenda vizuri na wananchi wanafurahia, kwa sasa tunapanga namna tutakavyotoa mikopo kwa ajili ya kuunga mkono juhudi za maendeleo katika kipindi kijacho” amesema Bi. Bella Bird.

Kwa upande wake Mhe. Rais Magufuli ameishukuru Benki ya Dunia kwa ushirikiano wake na Tanzania katika maendeleo na amemhakikishia Bi. Bella Bird kuwa Serikali itazisimamia vizuri fedha zote zinazotolewa na benki hiyo ili zilete matokeo yanayotarajiwa.

Mhe. Rais Magufuli ameongeza kuwa maeneo yote ambayo benki hiyo imeyataja kuwa kipaumbele katika fedha zitakazotolewa kuanzia sasa ni muhimu kwa ustawi wa Tanzania na amesisitiza kuwa fedha zitakazotolewa kwa mkopo zielekezwe katika maendeleo na sio vinginevyo.

“Naishukuru sana Benki ya Dunia kwa kutuunga mkono, nitafurahi kuona mnaendelea kutupatia fedha ambazo zinaelekezwa kwenye miradi ya maendeleo na kuleta manufaa mapana na endelevu, badala ya kugawa fedha kwa watu na baadaye nchi inakuja kuzilipa kwa kukusanya kodi za wananchi” amesisitiza Mhe. Rais Magufuli.

Wakati huo huo, Mhe. Rais Magufuli leo ameongoza kikao cha Baraza la Mawaziri Kilichofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam.
 
Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam
04 Desemba, 2017

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumanne ya Disemba 5

UDSM Yasema marekebisho katika jengo la Kitalu A lenye nyufa yanaweza kufanyika wakati jengo likiwa linatumika.


Mwandishi wa Mwananchi apotea katika mazingira ya kutatanisha Kibiti

Mwanafunzi Aliyesambaza Picha za Nyufa Hostel za UDSM Atiwa Mbaroni

$
0
0
Mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Kumbusho Dawson anashikiliwa na polisi akituhumiwa kusambaza picha kuonyesha nyufa kwenye majengo ya hosteli.

Dawson ambaye ni mbunge wa serikali ya wanafunzi (Daruso) alikamatwa jana Jumatatu Desemba 4,2017 mchana.

Makamu wa Rais wa Daruso, Anastazia Anthony amethibitisha kukamatwa kwa mbunge huyo jana saa saba mchana.

"Ni kweli Kumbusho alikamatwa jana mchana  na kupelekwa kituo cha polisi cha Chuo Kikuu kwa ajili ya kuhojiwa lakini ilipofika saa tisa alasiri polisi walisema hawana uwezo wa kumuhoji hapa hivyo wakampeleka Oysterbay," amesema Anastazia.

Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa alipotafutwa amesema hana taarifa kuhusu tukio hilo. Alisema anasubiri atakapofikishiwa taarifa atazitoa kwa umma.

Godbless Lema, Jerry Muro Wazidisha Utata Safari Ya Mnyika Kuhamia CCM

$
0
0
Licha ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kukaririw jana kikikanusha fununu zilizozagaa mitandaoni zikielekeza kuwa Mbunge wa Kibamba (Chadema), Mhe. John Mnyika anatazamiwa kuhamia Chama cha Mapinduzi (CCM), bado ishara zimezidi kuonesha kuwa safari ya kinara huyo wa upinzani kuelekea CCM imezidi kuiva.

Tetesi hizo zimegonga vichwa vya mitandao ya kijamii jana jioni  baada ya kada wa CCM, Jerry Muro kutumia mtandao wa kijamii wa Instagram kwa kuweka picha ya Rais, Dkt. John Pombe Magufuli na John Mnyika na kuandika maneno kadhaa kama ifuatavyo;

“Wanakuita mvulana, basi nenda kwa Baba ukadeke kidogo kule ulikua unakomazwa tu, #safarimojamatata.”
Wakati wengi wakitafakari maneno ya Jerry Muro, Mbunge wa Arusha Mjini (Chadema) naye ametumia mtandao wa kijamii kuandika machache yaliyotafsiriwa kama maneno yanayoongelea sakata la Mnyika kutimkia CCM. 

==>Lema ameandika yafuatayo;

.

Ijue Sayansi ya Kusimama na Kusinyaa kwa UUme ( Sayansi ya Nguvu za Kiume)

$
0
0

Ukosefu  na/ama  upungufu wa  nguvu  za  kiume, ni tatizo linalo  wakabili  mamilioni  ya  wanaume duniani.

Tatizo  la  ukosefu/upungufu  wa  nguvu  za  kiume ni  nini  ?

Ukosefu  ama  upungufu  wa  nguvu za  kiume  ni  ile  hali  ya  mwanaume  kutokuwa  na  uwezo  wa kufanya  tendo  la  ndoa  kwa  ukamilifu

HATUA  MBILI  MUHIMU  KATIKA  KUSIMAMA  KWA  UUME
Ili  mwanaume   aweze  kufanya  tendo  la  ndoa  na  andelee  kufanya  tendo  la  ndoa, ni  lazima  uume wake  upitie  hatua  kuu  mbili  kama  ifuatavyo :

Hatua  ya  kwanza, ni  lazima  uume  wake  uweze  kusimama  barabara  na  kuwa  mgumu  kama  msumari.

Na  hatua  ya  pili  ni  lazima, uume  wake  uendelee  kusimama  kwa  muda  mrefu  wakati  wa  tendo  la  ndoa.  Hatua  zote  mbili  zinapo  kamilika, ndipo  tunapo  pata  kitu  kinaitwa STRONGER  AND  LONGER  ERECTION

JINSI  HATUA  ZA  KUSIMAMA  KWA  UUME  ZINAVYO  TOKEA.

1. HATUA   YA  KWANZA:

DAMU  KUTIRIRIKA  KWA  KASI KUINGIA  NDANI  YA  MISHIPA  YA  UUME  NA  KUUFANYA  UUME  KUSIMAMA  NA  KUWA  MGUMU.

Unapopata  wazo  la  kufanya  tendo  la  ndoa, mishipa  ya  fahamu iliyopo  kwenye  ubongo,  hupeleka  ishara  kwenye  mishipa  ya  uti  wa  mgongo, ambayo  nayo  hupeleka  taarifa  hadi  kwenye  mishipa  ya  uume. Taarifa  inapofika  kwenye  mishipa  ya  uume  huifanya  mishipa hiyo  ku-relax  na  hatimaye   kufanya  mishipa  ya  ateri  kufunguka  na  kutanuka. Mishipa  ya  ateri  inapo  tanuka  na  kufunguka, huruhusu  damu  kuingia  kwa  kasi  ndani  ya  mishipa  ya  uume  na  hivyo  kuufanya  huume  kusimama.

Ni  muhimu  kujua  kuwa, mishipa  ya  uume  inapo relax  hupelekea  kuisukuma na  hatimaye  kuiziba  mishipa  ya  vena  iliyo  karibu  na  mishipa  ya  uume  na  hivyo  kuiondolea  uwezo  wa  kunyonya  damu  iliyomo  ndani  ya  mishipa  ya  uume  na  kuipeleka  sehemu  nyingine  za  mwili.

N.B: Kazi  kubwa  ya  mishipa  ya  vena  ni  kunyonya  damu  iliyomo  ndani  ya  mishipa  ya  uume  na  kuipeleka  katika  sehemu  nyingine  za  mwili.  Au  kwa  lugha  nyingine  unaweza  kusema, kazi  kubwa  ya  mishipa  ya  vena  ni  kuhakikisha  hakuna  damu  kwenye  mishipa  ya  uume.
 
2. HATUA  YA  PILI  :
DAMU  KUENDELEA  KUHIFADHIWA  KATIKA  UUME  WAKATI  UUME  UKIWA  UMESIMAMA  NA  HIVYO  KUUFANYA  UUME  UENDELEE  KUDUMU  KATIKA TENDO LA NDOA   KWA  MUDA  MREFU.

Uume  ulio  simama, ili  uendelee  kusimama, ni  lazima  mishipa  ya  vena  isiwe  na  uwezo   wa  kunyonya  damu  kutoka  katika  mishipa  ya  uume  na  kuipeleka  katika  sehemu  nyinginezo  za  mwili. .

Mishipa  ya  Vena  ndio  inayo  husika  na  kunyonya  damu  kutoka  kwenye  mishipa  ya  uume na  kupeleka  sehemu  nyingine  za  mwili.  Ili  uume  uendelee  kusimama  lazima  mishipa  hii  ya  vena  iwe imezibwa. Ili  iweze  kuzibwa   ni  lazima  misuli  laini  ya  kwenye  uume  iwe - ime  relax na  hivyo  kuifanya  mishipa  ya  vena  kushindwa  ku  nyonya damu  kutoka  kwenye  uume.

Endapo  mishipa  ya  vena  itazibuka , basi  itanyonya  na  kutoa  damu yote  kutoka  kwenye  mishipa  ya  uume uliosimama  na  kuipeleka  sehemu  nyinginezo  za  mwili  na  hatimaye  uume  huo ulio simama  na  utasinyaa  mara  moja.

JINSI  UUME  UNAVYO  SIMAMA  NA  KUSISIMKA.
Tumeisha  zifahamu  hatua  mbili  muhimu  katika  kusimama  kwa  uume

Jinsi  Uume  unavyo  simama: Katika  uume  kuna chemba  yenye  mishipa  laini  sana, ambayo  ndio  huufanya  uume  kusimama.

Mishipa  hii  ipo kama  sponji  hivyo  huweza  kunyauka  na  kutanuka.

Damu  inapoingia  ndani  ya  mishipa  hii  huufanya  uume  kusimama  na  kuwa  mgumu  kama  msumari.

Damu  inapoendelea  kuhifadhiwa  ndani  ya  mishipa  hii  wakati  wa  tendo  la  ndoa, huufanya  uume  uendelee  kusimama.

Mwanaume  unapo  patwa  na  wazo la  kufanya  tendo  la  ndoa, mishipa  ya  fahamu  iliyo  kwenye  ubongo  hupeleka  ishara  kwenye  uti  wa mgongo, ambao  nao  hufikisha   taarifa  kwenye  mishipa  ya  uume.

Taarifa  ikisha  fika  kwenye  mishipa  ya  uume, huifanya  mishipa  ya  uume  ku-relax  na  mishipa  ya  uume  inapo  relax, hufanya  mambo  makuu  mawili;

i. Kwanza  hufanya  mishipa  ya  ateri  kufunguka na  hivyo  damu  kutiririka  kwa  kasi  sana  kuingia  kwenye  mishipa  ya  uume

( Mishipa  ya  ateri  ndio  inayo  tumika  kama  njia  ya  kuingiza  damu  kwenye  uume. Bila  mishipa  ya  ateri  imara  na  yenye  afya, damu  haiwezi kuingia  kwenye  mishipa  ya  uume, na  damu  isipoweza kuingia  kwenye  mishipa  ya  uume, basi  uume  hauwezi  kusimama )

ii.Pili huibana  mishipa  ya  vena  na  hivyo  kuizuia    kunyonya  damu  kutoka  kwenye  uume  na  kuipeleka  kwenye  sehemu nyingine  za  mwili. Matokeo  yake  kuufanya  uume  uendelee  kusimama  kwa  muda  mrefu  wakati  wa  tendo  la  ndoa.

Kumbuka ,kazi  kubwa  ya  mishipa  ya  neva  iliyo  karibu  na  mishipa ya  uume, ni kunyonya  damu kutoka  ndani  ya  mishipa  ya  uume  na  kuipeleka  kwenye  sehemu  nyingine  za  mwili. Kwa  lugha  nyingine, kazi  kubwa  ya  mishipa  ya  vena  ni  kuhakikisha  hakuna  damu  kwenye  mishipa  ya  uume ulio simama.

Kadri  damu  inavyo  zidi  kuingia  ndani  ya mishipa  ya  uume, ndivyo  uume  unavyo  zidi  kuwa  mgumu  na  kukakamaa.

Na  kadri  damu  inavyo  hifadhiwa  ndani  ya  mishipa  ya  uume, ndivyo  uume  unavyo endelea  kusimama  wakati  wa  tendo  la  ndoa kwa  muda mrefu.

Baada  ya  kumaliza  kufanya  tendo  la  ndoa,mishipa  ya  uume inarudi  katika  hali  yake  ya  kawaida (inanyauka ), ikisha  nyauka, mishipa  ya  ateri  inanyauka  pia, vena  zinafunguka  na  kunyonya  damu  katika  mishipa  ya  uume  na  kuirejesha  katika  sehemu nyinginezo  za  mwili  na  hatimaye  uume  kurudi  katika  hali  ya  kawaida  ( Flaccid ).

Hali  hii  itaendelea  kujirudia  kwa  kadri  utakavyo  kuwa  ukiendelea kufanya  tendo  la  ndoa.

Mambo  Muhimu  Katika  Kuufanya Uume  Usimame na  Kuendelea  kudumu  katika  kusimama  kwa  muda  mrefu wakati  wa  tendo  la  ndoa.

Ili  uume  uweze  kusimama  imara  kama  msumari na  uendelee  kusimama  imara  na  kwa  muda  mrefu  wakati  wa  tendo la  ndoa, ni  lazima  mambo  yafuatayo yawepo.

1. Mishipa ya   uume iliyo  imara  na  yenye  afya  njema.

2. Mfumo   mzuri  wa damu  katika   mwili  mzima.

3.Mtiririko  imara  wa  damu kuingia  na  kutoka  ndani  ya  mishipa  ya  uume.

4. Ushirikiano  wenye  afya  kati  ya  mishipa  ya  fahamu  ya  kwenye  ubongo  (nerves), mishipa  ya  kwenye  uti  wa  mgongo  pamoja  na  mishipa  ya  kwenye  uume.

Ili  mwanaume  aweze  kuwa  imara  katika  tendo  la  ndoa, ni  lazima  mambo  manne  niliyo yataja  hapo  juu  yawe  sawa  sawa  bila  hitilafu  yoyote. Kinyume  chake, mwanaume  hawezi  kuwa  na  nguvu  za  kiume.

MAMBO   YANAYO SABABISHA   UKOSEFU/UPUNGUFU  WA  NGUVU  ZA  KIUME.
Tumeshajua   nguvu za  kiume  ni  nini, jinsi  uume  unavyo  simama, hatua  za  kusimama  kwa  uume, pamoja  na  mambo  yanayo  fanya  uume  uweze  kusimama  na  kuwa  na  uwezo  wa  kuendelea  kusimama  wakati  wa  tendo  la  ndoa.

Ni  vyema  tukajua  mambo  yanayo  sababisha  kushindwa  kusimama  kwa  uume, mambo  yanayo  sababisha  uume  ushindwe kuendelea  kusimama  kwa  muda  mrefu  wakati  wa  tendo  la  ndoa   pamoja  na  mambo  yanayo  fanya  mtu  ashindwe  kurudia  tendo  la  ndoa.

Yafuatayo  ni  mambo  yanayo  sababisha  ukosefu wa  nguvu  za  kiume.

1. MAGONJWA  YANAYO  SHAMBULIA  MFUMO  WA  DAMU  PAMOJA  NA  MISHIPA  YA  DAMU.

Damu  ndio  nishati  inayo wezesha  kusimama  kwa  uume  na kuufanya  kuwa  mgumu na  imara  kama  msumari.

Damu  ndio  nishati  inayo weza   kuufanya  uume uendelee kusimama  wakati  wa  tendo  la  ndoa.

Damu  ndio  nishati  inayo  upa  uume  uimara  na  uwezo  wa  kurudia  tendo  la  ndoa  zaidi  ya  mara  moja.

Hivyo  basi  ili  uume  uweze  kuwa  imara na  wenye  nguvu, pamoja  na  kuwa  na  uwezo  wa  kumudu  na  kustahimili   tendo  la  ndoa  wakati  wowote , basi  ni  lazima   mwanaume  awe  na mfumo  imara  wa  damu  utakao  ruhusu  kutiririka  kwa  damu  kwenda  katika  sehemu mbalimbali  za  mwili  ikiwamo  uume.

Ili  mfumo  uweze  kuwa  imara  ni  lazima  mhusika  awe  na  damu  ya  kutosha, na  pili  awe  na  mishipa  ya  damu  yenye  afya.

Katika  mwili  wa  mwanadamu,kuna  mishipa  inayo  tumika  kusafirisha  damu  kutoka  katika  sehemu moja  ya  mwili kwenda  katika  sehemu  nyingine  ya  mwili  ikiwemo  uume. Mishipa  hiyo  ni  kama  vile  vena (veins), atery ( ateri) na  capillary  ( kapilari )

Mishipa  hii  ya  damu  inapaswa  kuwa  imara  na  yenye  afya  njema  wakati  wote.   Mishipa  hii  ikipatwa  na  hitilifu, basi  itazuia  kusafirishwa  kwa  damu  katika  sehemu  mbalimbali za  mwili  wa  mwanadamu  na  hatimaye  kufanya  suala  la  kuwa  na  nguvu  za  kiume  kwa  mhusika  kuwa  ugumu  kwa  sababu   ya  kushindwa  kupeleka  damu  kwenye  mishipa  ya  uume.

Magonjwa  kwenye  mishipa  ya  damu  huzuia   kutirika  kwa  damu kwenye  ogani  muhimu   kama  vile  moyo, ubongo na  figo.

VIASHIRIA  VYA  MAGONJWA  KWENYE  MISHIPA  YA  DAMU.
Utajuaje  kwamba  una  magonjwa  kwenye  mishipa  yako  ya  damu ?

Ukiwa  una  matatizo  yafuatayo ya  kiafya, ni  ishara  kwamba, una  magonjwa  kwenye  mishipa  yako  ya  damu:

1.  Kolestrol ( Ama  lehemu  kwenye  damu )
Kolestrol  nyingi  kwenye  damu, huzuia  kutiririka  kwa  damu. Kolestrol  ikizidi  kwenye  damu,  hupelekea  kuziba   mishipa  ya  ateri  ambayo  kazi  yake  ni  kupeleka  damu  kwenye  uume. Matokeo  yake  ni  mhusika  kutokuwa  na  uwezo  wa  kusimamisha  uume  wake barabara  kwa  sababu uume  hauwezi  kusimama  bila  damu  kuingia  ndani  ya  mishipa  ya  uume. 
 
 Hivyo  basi pamoja  na  dawa  ya  nguvu  za  kiume, yakupasa  kutibu  kolestrol. Unaweza  kuondoa  kolestrol  kwenye  damu  kwa  kutumia  dawa  mbali  za  asili  kama  vile mdalasini,uwatu, habbat sodah  etc.  Jinsi  ya  kujitibu  kolestrol  kwa  kutumia dawa asilia  tafadhali  tembelea


2.      Shinikizo  Kubwa  la  Damu
Shinikizo  Kuu la  Damu husababisha  mishipa  ya  ateri  ambayo  hutiririsha  damu  iingiayo  kwenye  uume  kuziba  na  kushindwa kutanuka  kwa  kiwango  inachotakiwa  kutanuka.

Pia  huifanya  mishipa  laini  katika  uume   kushindwa  ku-relax  na  hivyo  kushindwa  kuizuia  mishipa  ya  vena  ya  kunyonya  damu  kutoka  kwenye  mishipa  ya  uume  na  kuipeleka  kwenye  maeneo  mengineyo  ya  mwilini.

Matokeo  yake  kunakuwa hakuna  kiasi  cha  kutosha  cha  damu  iingiayo  kwenye  uume  na  hivyo  kufanya  uume  ushindwe  kusimama.

Vile  vile  hata  kiasi  kidogo  cha  damu  kinacho  ingia  kwenye  uume, kinashindwa  kuendelea  kuhifadhiwa  ndani  ya  uume  wakati uume  ukiwa  umesimama, na  matokeo yake  ni  uume  kusinyaa  ndani  ya  kipindi kifupi  sana  tangu  usimame.

Pamoja  na kutumia  dawa  ya  nguvu  za  kiume, unapaswa   pia  kutumia  dawa  asilia  kujitibu  tatizo  la  shinikizo  kuu  la  damu.

Kufahamu  jinsi  ya  kujitibu  tatizo  la shinikizo  la  damu  kwa  njia  ya  asilia, tembelea :


3.  Ugonjwa  wa  kisukari :
 Ugonjwa  wa  kisukari  ni  miongoni  mwa  vyanzo  vikuu  vya  tatizo  la  ukosefu wa  nguvu  za  kiume.  Kusimama  kwa  uume  kunategemeana  na  kutiririka  kwa  damu  mwilini. Kisukari  huathiri  mishipa  ya  damu pamoja  na  usambazaji  wa  damu  kwenye  ogani  muhimu  mwilini  kama  vile  moyo, ubongo, figo  na  uume.

Kiukweli, mwanaume  mwenye  kisukari  yupo  katika  risk  kubwa  ya  kupatwa  na  tatizo  la  ukosefu  wa  nguvu  za  kiume,m tena  katika  kiwango  kikubwa  sana.

Unashauriwa pamoja  na kutumia  dawa  ya  nguvu  za  kiume, tumia  pamoja  na  dawa  mbalimbali  za  asili  kwa  ajili  ya  kubalance  sukari  yako mwilini. 
 
Zipo  dawa  mbalimbali  za  asili  zinazo  saidia  kubalance  kiwango  cha  sukari  mwilini. Dwa  hizo  ni  pamoja na mdalasini, unga  wa  uwatu, mbegu  za  uwatu, manjano, majani  ya  manjano,mbegu  za  katani, nakadhalika. Namna  ya  kutumia  dawa  hizo  kujitibu  tatizo  la  sukari, tafadhali  tembelea :http://neemaherbalist.blogspot.com/2015/07/jitibu-kisukari-presha-shinikizo-la.html

4. Magonjwa  ya  figo
Tatizo  la  ugonjwa  wa  figo  huathiri  vitu vingi  ambavyo  ni  muhimu  sana  katika  kuufanya  uume  uweze  kusimama  na  kuendelea  kudumu  katika  kusimama.

Tatizo  la  figo, huathiri  homoni, huathiri kutiririka   kwa  damu  kwenda  kwenye  mishipa  ya  uume. Huathiri  mfumo  wa mishipa  ya  neva  pamoja  na  nishati  ya  mwili mzima.

Pamoja  na  dawa  ya  kutibu  tatizo  la  nguvu za  kiume, unapaswa  pia, kutibu  tatizo  la  figo. Kufahamu  jinsi  ya  kujitibu  magonjwa mbalimbali  ya  figo  kwa  kutumia  dawa mbalimbali  asilia, tembelea :http://neemaherbalist.blogspot.com/2015/07/jitibu-kisukari-presha-shinikizo-la.html

5.        Ugonjwa  wa  moyo
Moyo  ndio  supplier  mkubwa  wa  damu  katika  sehemu  mbalimbali  za  mwili.  Ugonjwa  wa  moyo  hupunguza  uwezo  wa  moyo  kusambaza  damu  kwenye  mishipa  mbalimbali  ya  damu  na  hivyo  kuathiri  utendaji  kazi  wa  mishipa ya  damu  kama  vile  ateri  na  vena. Matokeo  yake  ni  mishipa  hiyo  kushindwa  kupeleka  damu  ya  kutosha  katika  uume  pamoja  na  kushindwa  kuifanya  mishipa  ya  uume  kurelax na  matokeo  yake,. Ukosefu  wa nguvu  za  kiume. Hivyo  basi, pamoja  na  dawa  ya  nguvu  za  kiume, unapaswa  pia   kutibu  tatizo  la  moyo. Kufahamu  jinsi  unavyo  weza  kutibu ugonjwa  wa  moyo  kwa  dawa  asilia, tembelea :


6.  Kupwaya  kwa  mishipa  ya  vena.
Kazi  kubwa  ya  mishipa  ya  vena  kwenye  uume   kunyonya  damu  iliyomo  ndani  ya mishipa  ya  uume  na  kuipeleka  katika sehemu  nyingine  za  mwili.  Mishipa  ya  vena iliyopo  karibu  na  uume  kazi  yake  kubwa  ni kuhakikisha  hakuna  damu  yoyote  kwenye mishipa  ya  uume. ( KUMBUKA  KUWA  DAMU NDIO  HUFANYA  UUMU  USIMAME, HIVYO CHOCHOTE  KILE  KITAKACHO  FANYA  DAMU ISIKAE  NDANI  YA  MISHIPA  YA  UUME , KITAFANYA  UUME  USINYAE  )

Ili  uume  uendelee  kusimama  ni  lazima, mishipa  ya  vena  isiwe  na  uwezo  wa kunyonya  damu  kutoka  kwenye  mishipa  ya uume  kupeleka  nje  ya  mishipa  ya  uume.

Na  ili  mishipa  ya  vena  isiwe  na  uwezo  wa   kunyonya  damu  kutoka  kwenye   mishipa ya  uume  ulio  simama  na  kuipeleka  kwenye sehemu  nyingine  za  mwili,  ni  lazima mishipa  ya  uume  iwe  imara  na  thabiti  isiyo na  hitilafu  yoyote  ile.

Mishipa  ya  vena  ikipwaya, mwanaume hutokuwa  na  uwezo  wa  kusimamisha  uume wako, na  ikitokea  umefanikiwa kuusimamisha  basi  utasimama  ukiwa legelege  sana  na  utasinyaa  ndani  ya  muda mfupi  sana, kwa  sababu  damu  iliyo  ingia ndani  ya  uume  wako  na  kuufanya  usimame, itanyonywa  ndani  ya  muda  mfupi  sana  na kutolewa  nje  ya  mishipa  ya  uume  na  hivyo kuufanya  uume  wako  usimame.

 Tatizo  la  kupwaya  kwa  mishipa  ya  vena linasababishwa  na  kupiga  punyeto  kwa muda  mrefu  pamoja  na  ugonjwa  wa kisukari.

KUPIGA  PUNYETO  KWA  MUDA  MREFU: Kupiga  punyeto  kwa  muda  mrefu  ni  moja kati  ya  vyanzo  vikuu  vya  tatizo  la  la ukosefu  wa  nguvu  za  kiume.  Asilimia kubwa  ya  vijana  wenye  tatizo  la  ukosefu wa  nguvu  za  kiume, linasababishwa  na upigaji  wa  punyeto  kwa  muda  mrefu.

JINSI  PUNYETO  INAVYO  SABABISHA UKOSEFU  WA  NGUVU  ZA  KIUME.

Unapopiga  punyeto  unakuwa  unaiminya mishipa  ya  uume   ambayo  ndio  inaufanya uume  usimame.

Matokeo  yake  unaifanya  mishipa  hiyo  ilegee na  kutokuwa  na  uwezo  wa  kusimama  tena.

Mishipa  ya  uume  iliyo  legea  kutokana  na upigaji  punyeto, huleta  madhara  yafuatayo  :

i.           Huondoa  uwezo  wa  mishipa  ya  uume kurelax.

( Unapopata  wazo  la  kufanya  tendo  la ndoa, mishipa  ya  uume  ina relax  , mishipa  iki  relax  husababisha  mishipa ya  ateri  kupanuka  na  kuruhusu  damu kingie  ndani  ya  mishipa  ya  uume  na hatimaye  kuufanya  uume  usimame  na kuwa  mgumu)
 
ii.Mishipa   ya  kiume  ikishindwa  ku relax husababisha  mishipa  ya  ateri  kuziba

iii. Mishipa  ya  ateri  ikiziba, damu  haiwezi kutiririka  kuingia  kwenye  mishipa  ya uume, na  hata  ikitokea  damu  imeingia ndani  ya  mishipa  ya  uume  basi huingia  kiasi  kidogo sana   tena  kwa presha  ndogo  sana  hivyo  basi  hata kama  uume  utasimama   basi utasimama  ukiwa  legelege  sana

iv. Mishipa  ya  uume  ikishindwa  kurelax basi  haitakuwa  na  uwezo  wa  kuipush na  kuiziba  mishipa  ya  vena  ambayo ndio  hunyonya  damu  kutoka  kwenye mishipa  ya  uume  ulio  simama. 
 
Matokeo  yake  basi, damu  kidogo  iliyo ingia  ndani  ya  mishipa  ya  uume  na kuufanya  uume  kusimama, hunyonywa na  kutolewa  nje  ya  mishipa  ya  uume ndani  ya  sekunde  chache  sana  na hivyo  kuufanya  uume usinyae  ndani ya  muda  mfupi  sana.

v. Mishipa  ya  uume  kulegea

vi. Uume  kurudi ndani  na  kusinyaa  na kuwa  kama  uume  wa  mtoto

6. Tatizo  la  unene  kupita  kiasi : Tatizo  la unene  na  uzito  kupita  kiasi  ni  miongoni mwa  mambo  yanayo  sababisha  upungufu wa  nguvu  za  kiume. Unene  kupita  kiasi humuweka  mtu  katika  hatari  ya  kupatwa na  magonjwa  kama  vile  kisukari, presha, moyo  na  shinikizo  kuu  la  damu. 
 
Na magonjwa  ya  kisukari, moyo,presha  na shinikizo  la  damu  husababisha  upungufu na ukosefu  wa  nguvu  za  kiume, na  hivyo kumuweka  muhusika  katika  hatari  kuu  ya kupatwa  na  tatizo  la  ukosefu/upungufu  wa nguvu  za  kiume.

Hivyo  basi  kwa  wewe  mwenye  tatizo  la unene  na  uzito  kupita  kiasi , pamoja  na kutumia  tiba  ya  nguvu  za  kiume,  ni  vyema ukafanya  na  mpango  wa  kupunguza  unene na  uzito  wako.

JINSI  YA  KUPUNGUZA  UZITO  NA  UNENE KWA  KUTUMIA  TIBA  ASILIA, TAFADHALI TEMBELEA:


7.   Matatizo  Katika  mfumo  wa  Ubongo

Uume  hauwezi  kusimama   bila  ya  kuwa  na ushirikiano  na  ubongo.  Ili mtu  uume  uweze kusimama, mtu  lazima  apate  wazo  la kufanya  tendo  la  ndoa  (UBONGO  UNA HUSIKA  HAPO ), akishapata  wazo, ubungo hupeleka  ishara  kwenye  mishipa  ya  fahamu iliyopo  katika  uti  wa  mgongo  ambayo  nayo hupeleka  taarifa  kwenye  mishipa  ya  uume then  uume  usimama.   
 
Hivyo  basi  ili  mtu  aweze  kuwa  na uwezo  wa kusimamisha  uume  wake  ni lazima  kuwa  na  mawasiliano  mazuri  na  imara  kati  ya mishipa  ya  fahamu ( ubongo ), mishipa  ya  kwenye  uti  wa  mgongo   na  mishipa  ya  kwenye    uume.  Bila ushirikiano  kati  ya  vitu  hivyo  vitatu, uume hauwezi  kusimama.

Magonjwa  yanayoweza  kuathiri  ushirikiano  kati  ya  mishipa  ya  ubongo  na  mishipa  ya  uume, yanaweza  kusababisha  kushindwa  kusimama  kwa  uume.

Magonjwa  hayo  ni  pamoja  na  kiharusi,kupoteza  kumbukumbu  (  Alzheimer ), multiple  sclerosis pamoja  na  ugonjwa  wa  Parkinson.

Ni  vyema  mgonjwa  akatibiwa  kwanza magonjwa  hayo  kabla  ya  kuanza  kutumia dawa  ya  nguvu  za  kiume.  Kufahamu  jinsi ya  kujitibu  magonjwa  tajwa  hapo  juu  kwa njia  asilia,tafadhali  tembelea

Mambo   mengine  yanayo  sababisha  ukosefu na  upungufu  wa  nguvu  za  kiume, ni pamoja  na  maumivu & majeraha  kwenye  uti wa  mgongo,  chango  la  kiume , ngiri  na matatizo  katika  homoni.

 VIASHRIA  VYA  MTU  MWENYE  TATIZO  LA UKOSEFU/UPUNGUFU  WA  NGUVU  ZA KIUME.

Mtu  mwenye  tatizo  la  ukosefu  wa  nguvu  za kiume  huwa  na  dalili  zifuatazo ;

1. Kushindwa  kabisa  kusimamisha  uume wake

2. Uume  kusimama  ukiwa  legelege

3. Kuwahi  kumaliza  tendo  la  ndoa

4. Mwanaume  kutokuwa  na uwezo  wa kufanya  tendo  la  ndoa  katika  baadhi ya  staili  ( Mara  nyingi   mwanaume huyu huwa  na  uwezo  wa  kufanya tendo  la  ndoa    staili  moja  tu ).  Hapa mwanaume  anakuwa  na  uwezo  wa kufanya  tendo  la  ndoa  kwa  staili  ya   “ missionary” pekee.  Ikibadilishwa   staili, mwanaume  anakuwa hana  tena  uwezo wa  kusimamisha  uume  wake  japo katika  hali  ya  u lege  lege

5. Uume  kutokuwa  na  uwezo  wa kusimama  wenyewe   bila kushikwashikwa  ama  kutomaswa kwa muda  mrefu.

6. Uume  kusinyaa  ukiwa  ndani  ya mwanamke.

7. Uume  kusinyaa, pindi  inapotokea activity  yoyote  ya  kiungo  ama  ogani nyingine  ya  mwanaume  wakati  wa tendo  la  ndoa. Kwa  mfano, wakati  wa tendo  la  ndoa, ikitokea  mwanaume amekohoa  au  kupiga  chafya, uume  nao unasinyaa.

8. Uume  kusinyaa  mara  tu  baada  ya kutolewa  ndani  ya  uke ( Kwa  mfano kama  unafanya  tendo  la  ndoa, halafu uume  ukatoka  nje, kitendo  cha kuushika  kuurudisha ndani, tayari  una sinyaa )

9. Kutokuwa  na  uwezo  wa  kurudia  tendo la  ndoa.

10.  Kupatwa  na  maumivu  wakati  wa tendo  la  ndoa.

VIASHIRIA  VYA  MWANAUME  ASIYE  NA TATIZO  LA UKOSEFU  WA  NGUVU  ZA KIUME.

Mwanaume  asiye  na  tatizo  la  ukosefu  wa nguvu  za  kiume, huonyesha  ishara  zifuatazo ;

i.Uume  husimama  ukiwa  imara  kama msumari.

ii.Hukaa  kifuani  kwa  muda  mrefu  ( Wastani  ni  kati  ya  dakika  20  hadi  45 )

iii.Huweza  kurudia  tendo  la  ndoa  zaidi ya  mara  tatu  bila  misuli  ya  uume kuchoka.

iv.Huweza  kufanya  tendo  la  ndoa  kwa staili  yoyote  ile

v.Uume  husimama  wenyewe  bila kushikwa  shikwa  wala  kuwa stimulated  kwa  namna  yoyote  ile

vi.Kwa  ufupi  anakuwa  na  uwezo  wa kufanya na  kukamilisha  tendo  la  ndoa kwa  uukamilifu  mkubwa.

TIBA  ASILIA  YA  TATIZO  LA UKOSEFU/UPUNGUFU  WA  NGUVU  ZA KIUME.

Dawa  asilia  ya  JIKO   ni  dawa  asilia  inayo tibu  na  kuponyesha  kabisa  tatizo  la ukosefu  wa  nguvu  za  kiume.

                              MFUMO   WA  DAWA
Dozi  ya  dawa  ya  JIKO ni  mkusanyiko  wa dawa  nne  asilia  zenye  uwezo  mkubwa  sana katika kutibu  na  kuponyesha  kabisa  tatizo la  ukosefu/upungufu  wa  nguvu  za  kiume.

Dawa  hizi  zipo  katika  mfumo  wa  MIZIZI  na UNGA  UNGA.

JINSI   DOZI  YA  DAWA  YA  JIKO  INAVYO FANYA  KAZI.
Dozi  ya  dawa  ya  JIKO  inafanya  kazi zifuatazo  katika  mwili  wa  mwanadamu.

KAZI  INAYO  FANYWA  NA  DAWA  YA  JIKO .
Dawa  ya  JIKO  inasadia  katika  mambo makuu yafuatayo:
1.  Inasaidia   kuimarisha  mishipa  ya  uume  ulio legea  na  hivyo  kuufanya  uume  uwe  na uwezo  wa  kusimama  barabara  kama msumari  wakati  wa  tendo  la  ndoa.

2. Inasaidia  kusafisha  mishipa  ya  kwenye uume  na  hivyo  kusaidia  katika  kuongeza kasi  ya  msukumo  wa  damu  kwenye mishipa  ya  kwenye  uume.

3. Huongeza  damu  mwilini

4. Husaidia  kuongeza  msukumo (pressure)  wa damu  kwenye  mishipa  ya  uume  na  hivyo kuufanya  uume  kuwa  na  nguvu  za  ajabu.

5. Huipa  misuli  ya  uume  uwezo  wa  kuziba  wa kuizuia  mishipa  ya  vena   kunyonya  damu kwenye  mishipa  ya  uume  wakati  wa  tendo la  ndoa  na  matokeo  yake  kukupa  uwezo wa  kufanya  tendo  la  ndoa  kwa  muda  mrefu

               ( Kuzuia  hali  ya  kufika  kileleni haraka  )

6. Husaidia  kurelax  mind  na  hivyo  kumfanya mtu  awe  na  uwezo  wa  kuconcentrate  wakati wa  tendo la  ndoa   bila  kuathiriwa  na msongo  wa  mawazo

7.  Hurejesha, kuimarisha  na  kuboresha ushirikiano  kati  ya  mishipa  ya  fahamu  ya  kwenye  ubongo  (nerves), mishipa  ya  kwenye  uti  wa  mgongo  pamoja  na  mishipa  ya  kwenye  uume
8. Humfanya  mwanaume  awe  na  uwezo  wa kurudia  tendo  la  ndoa  mara  nyingi  zaidi bila  kuchoka.
9. Husaidia  kuongeza  hamu  ya  tendo  la  ndoa.10. Husaidia  kuurudisha  nje  uume  ulio ingia ndani.
11. Husaidia  kutibu  side effects  za  punyeto na  matumizi  ya  muda  mrefu  ya dawa  kali za  (za  kizungu ) za  kuongeza  nguvu  za kiume.

12. Husaidia  kutibu  chango  la  kiume.

13.Dawa  hii  huwasaidia  hata  wanawake wanao sumbuliwa  na  tatizo  la  ukosefu  wa hamu ya  tendo  la  ndoa.

BEI  YA  DAWA:  Dozi  ya  dawa  ya  JIKO inapatikana  kwa  gharama  ya  SHILINGI ELFU  THEMANINI  TU  (Tshs.80,000/=)

MAHALI  TUNAPOPATIKANA :
Dozi  ya  dawa  ya  JIKO, inatolewa  na  duka  la dawa  asilia  la  NEEMA 

HERBALIST  &   NUTRITIONAL  FOODS  CLINIC. Tunapatikana jijini  DAR ES  SALAAM, katika  eneo  la UBUNGO     karibu  na  SHULE  YA MSINGI  UNGUNGO  NATIONAL  HOUSING  NYUMA  YA  JENGO  LA  UBUNGO  PLAZA.

Kwa  wasio  weza  kufika  ofisini  kwetu, tunatoa huduma  ya kuwapelekea  dawa  mahali  walipo ( DELIVERY )

Kwa  wateja  waliopo  nje  ya  DAR  ES  SALAAM, watatumiwa  dawa  kwa  njia  ya  mabasi, wateja  waliopo  Zanzibar, watatumiwa  dawa kwa   njia  ya  boti  na  kwa  wateja  waliopo Ulaya, America  na  Arabuni, watatumiwa dawa  kwa  njia  ya  DHL  au POSTA.

WASILIANA  NASI  KWA  SIMU  NAMBA

0766  53  83  84.
Na  kwa  maelezo  zaidi  kuhusu  huduma  zetu, endelea  kutembelea:

Mbwa wa Polisi Wamuumbua Jamaa Aliyetengeneza Tukio FEKI la Kuvamiwa na Majambazi

$
0
0
Mfanyakazi  wa kampuni ya saruji ya Simba Cement, Edward Ngassa amekamatwa na Jeshi la Polisi mkoani Dodoma kwa tuhuma za kutengeneza tukio la uongo la kuporwa Sh. milioni 20.4 na majambazi jana.

Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi mkoa wa Dodoma, Gilles Muroto, mbwa wa polisi mwenye mafunzo ndiye aliyegundua udanganyifu huo wa Ngassa nyumbani kwake.

Kamanda Muroto alisema mtuhumiwa huyo alitengeneza tukio la uongo kwamba ameporwa fedha na majambazi katika eneo la Uhindini karibu na mgahawa wa Sunja.

Kufuatia ripoti ya tukio hilo, Muroto alisema, timu ya upelelezi ilifanya uchunguzi wa kina na kubaini kwamba hakukuwa na tukio la uporaji katika eneo hilo.

“Katika uchunguzi huo tulienda kumpekua kwa kina mtuhumiwa nyumbani kwake na kufanikiwa kukamata fedha zote alizoiba akiwa ameficha kwenye ndoo ndogo ya plastiki na kuweka udongo kisha kupanda ua juu yake ili zisikamatwe kirahisi,” alisema.

Muroto alibainisha kuwa waliweza kuzifichua fedha hizo kwa kutumia mbwa ambaye alikuwa akinusa kwenye maeneo yote na kuzikuta kwenye ndoo ya ua.

“Huyu mtuhumiwa alimpigia simu mwajiri wake akidai kuwa wakati anaelekea benki kuna pikipiki ya majambazi ilimzuia kwa mbele na kumpora hizo fedha,” alisema Muroto.

Katika hatua nyingine, Kamanda Muroto alisema watu wawili wamekamatwa kwa wizi wa betri tatu za minara ya mawasiliano katika eneo la Chang’ombe na Chuo Kikuu cha Dodoma (Udom).

“Watuhumiwa Eliezel Muhongole ambaye ni fundi na mfanyakazi wa kampuni ya Halotel na Alfredy Mlugu mkulima na mkazi wa Mpunguzi walikamatwa kwa wizi huu,” alisema Muroto.

Mbali na hilo, Muroto alisema watu watatu wanashikiliwa na polisi mkoani humu kwa kukamatwa na vipande vinne vya meno ya tembo vyenye uzito wa kilo 16 na thamani ya Sh. milioni 33.2.

Aliwataja waliokamatwa kuwa ni mkazi wa Dar es salaam Hussein Henry (40), na Mussa Ramadhani (35) na Abdalah Ramadhani (32) wote wakazi wa Kondoa.

“Hawa walikamatwa wakiwa wamepakia meno haya ya tembo kwenye pikipiki yenye namba za usajili MC516 BDC aina Fekon wakitokea Kondoa wakielekea Dodoma mjini,” alisema.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images