Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Waziri Ummy Alaani Kitendo Cha Mwalimu Kumpa Mimba Mwanafunzi Wa Darasa La Saba Wilaya Ya Kalambo Mkoani Rukwa

$
0
0
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy A. Mwalimu (Mb) amepokea kwa masikitiko makubwa kitendo cha mwalimu mmoja wa Shule ya Msingi Samanzi, iliyoko kijiji cha Samanzi, Kata ya Kisumba, wilaya ya Kalambo mkoani Rukwa kumpa ujauzito mwanafunzi wa darasa la saba (jina limehifadhiwa), na kushindwa kufanya mtihani wa kuhitimu elimu ya msingi. Mhe. 

Waziri amesema kitendo hicho ni ukatili na unyanyasaji dhidi ya mtoto wa kike na ni ukiukwaji wa Haki za Msingi za Mtoto ikiwemo haki ya Kuendelezwa na Kulindwa.

Waziri Ummy amewaasa walimu kuacha tabia ya kuwa na mahusiano ya kingono na wanafunzi maana shule kama taasisi, ni chombo madhubuti cha kujenga uelewa kwa jamii kuhusu ulinzi na usalama wa Mtoto katika jamii. 

Aidha, amewataka walimu,  walezi na jamii kuhakikisha wajibu wa kuwalinda na kuwalea watoto bila uwanyanyasaji na ukatili wa aina yoyote. 

Ameongeza kuwa, inapotokea mwalimu amehusishwa na tuhuma ya kumpa mimba mtoto wa kike kitendo hicho kinatia doa dhamana ya mwalimu na nafasi ya shule katika malezi ya mtoto.

Waziri Ummy, ameitaka jamii kuboresha ushirikiano wa wazazi, walezi na walimu maana wanamchango mkubwa katika makuzi na maendeleo ya watoto. 

Kadhalika, amesisitiza kutambua kuwa madhara ya mwalimu kumpa mimba mwanafunzi anamfanya kuwa mwathirika wa vitendo vya ukatili katika maisha yake yote.

Aidha, Waziri Ummy ameelekeza vyombo vya dola mkoani Rukwa kuhakikisha suala hili linachunguzwa kikamilifu na kumfikisha mtuhumiwa mbele ya vyombo vya sheria ili haki iweze kutendeka.

Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

22/09/2017

Msemaji wa Serikali: "Wamekufa watu Wangapi Kibiti Hatukuita Wazungu?"

$
0
0
Baada ya viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kusikika wakidai vyombo vya usalama kutoka nje ya nchi vije kufanya uchunguzi wa shambulio la MbungeTundu Lissu, Msemaji mkuu wa Serikali Dkt. Hassan Abbaas amefunguka na kuhoji watu wangapi wamekufa na wazungu hawakuja.

Kupitia ukurasa wake wa twitter Dkt. Abbas amehoji kwa kuandika "Waje wazungu? Wamekufa watu wangapi Kibiti hatukuita wazungu?Lakini hatujui pia hata hao wazungu kwao makosa ya jinai pia yamewazidi nguvu?

Hata hivyo Dkt Abbas ameongeza kwamba tabia ya kutuhumiana kunapotokea kosa la jinai ambalo limetendwa kwa mtu yoyote au mwanasiasa siyo vizuri kwani kufanya hivyo kunakufanya uwe mshukiwa namba moja wa tukio.

Ameongeza kwamba kwamba ni "busara vyombo vya dola vikaachwa vifanye kazi yake kwanza na siyo kutuhumu".

Chama cha Demokrasia na Maendeleo kupitia viongozi wake wamekuwa wakitaka serikali iruhusu vyombo vya kimataifa waje nchini kufanya uchunguzi juu ya shambulio la Tundu Lissu aliyepigwa risasi na waru wasiojulikana Septemba 7 akiwa nje ya nyumba yake Area D' Dodoma alipokuwa akitokea bungeni mchana.

Waziri wa Afya Atoa Ufafanuzi Mwingine Sakata la Tundu Lissu

$
0
0
Waziri Ummy Mwalimu amejibu tuhumu zinazotolewa na baadhi ya watu dhidi ya serikali baada ya kutaka kuombwa kugharamia matibabu ya Lissu, na kusema kwamba serikali imelazimika kufanya hivyo kwa sababu mgonjwa alijitoa kwenye utaratibu wa serikali.

Ummy Mwalimu ambaye ni Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, ametoa maelezo hayo leo kwenye ukurasa wake wa twitter, na kusema kwamba serikali isingeweza kuingilia kati bila kuombwa na familia ya Tundu Lissu, kwani mgonjwa alishatolewa kwenye utaratibu wa serikali kwa kupelekwa Nairobi, na hiyo sio mara ya kwanza kwa serikali kufanya hivyo.

"Mgonjwa alitolewa kwenye utaratibu wa serikali alipopelekwa Nairobi, sasa gharama/tiba zaid yahitajika, serikali inaingiaje bila ridhaa ya familia? Na hii sio mara ya 1 kutokea. Mzee wetu S.Sitta (RIP), alikwenda matibabu London kwa utaratibu binafsi kisha alileta maombi serikali ishiriki", ameandika Ummy Mwalimu.

Waziri Ummy Mwalimu ameendelea kwa kuandika akisema kwamba mgonjwa ni Mbunge anayehitaji matibabu zaidi, lakini kwa kuwa sasa hivi yupo nje ya utaratibu wa serikali, ili serikali iweze kushiriki ni lazima yawepo maombi ya kufanya hivyo.

Hapo juzi serikali ilitoa tamko ikisema kwamba watakubali kusimamia matibabu ya Tundu Lissu popote duniani iwapo familia yake itaomba kufanya hivyo, na sio vinginevyo, kitendo ambacho kimeibua sintofahamu nyingi kwa baadhi ya wananchi wakiilaumu serikali kwa kutojali matatizo ya Tundu Lissu.

Mbowe Atoa Sababu Kwa Nini Hawajafungua Kesi Yoyote Dhidi ya Shambulio la Tundu Lissu

$
0
0
Mwenyekiti wa Chama cha demokrasia na Maendeleo, Mh. Freeman Mbowe amefunguka na kujibu hoja za kwa nini mpaka sasa CHADEMA hawajafungua kesi kutokana na shambulio Tundu Lissu  ambapo amesema ni kutokana na kuwa kipaumbele chao cha kwanza ni kuokoa maisha ya Lissu.

Mh. Mbowe ameyasema hayo wakati akizungumza jana na wanahabari ambapo amesema kuwa baada ya tukio la Lissu kutokea akili na mawazo ya Chadema yalikuwa kwenye kuokoa maisha ya Lissu na wanasubiri mambo yakiwa sawa wataangalia kufanya lolote linalowezekana kwan wakati huo.

"Kwa nini Chadema hatujafungua kesi? Kesi unafungua kwa nani? Anayechunguza ni nani? Chadema tumeshafungua kesi nyingi ya akiwepo Ben Saanane msaidizi wangu aliye[potea kusikojulikana, Kesi ya nyani unapeleka kwa Tumbili. Priority yetu sisi ni kumuokoa Lissu na siyo Kesi. Kupigania maisha yake ndicho kitu tuliona kinachofaa kufanywa na ndicho tunachofanya mpaka sasa", amesema.

"Ninaamini tu mambo yakikaa sawa vichwa vyote hivi vya Chadema vitajua kama tunaweza kufungua kesi au kitu gani kingine ambacho kinafaa kufanywa endapo tu afya ya Mh. Lissu ikishaimarika" ameongeza

Akizungumzia kwanini mpaka leo dereva wa Lissu hajarudi nchini ili kwenda kuripoti polisi kama jinsi jeshi la polisi lilivyoagiza, Mbowe amesema kwamba kijana huyo atarudishwa nchini pindi tuu wataalamu wa afya wanaomhudumia wakitoa ripoti afya yake kama iko salama na wao hawapo kwa ajili ya kumficha.

"Wiki iliopita nilisema dereva wa Mh. Lissu yupo Nairiobi kwa ajili ya matibabu ya kisaikolojia. Hatukuona kama ni busara kumtelekeza wakati alikuwepo kwenye matatizo na boss wake. Madaktari wakituthibitishia kuwa yuko timamu atarudi nchini kwani hatuko kwa ajili ya kumficha mtu. Yule kijana ni kama mtoto wa Lissu, dereva na mlinzi wake, wana miaka mingi pamoja tangu Lissu anagombea ubunge kwa mara ya kwanza" amesisitiza.

Ameongeza pia dereva atakuja kuzungumza nini kilitokea na yeye alijiokoaje naamini aliyekuwa anashambulia alikuwa hajalenga kumuacha hai mtu hata mmoja hivyo mimi siyo msemaji sana wa dereva wake Lissu lakini akipona ataelezea mwenyewe kila kitu.

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Gazi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0
Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Tupo Mbagala

Rais Magufuli atoa kamisheni 422

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa nchi Dkt. John Pombe Magufuli, leo amewatunuku kamisheni maafisa wa Jeshi 422 ambao wamehitimu mafunzo mbali mbali kwenye chuo cha Jeshi Monduli mkoani Arusha.

Tukio hilo ambalo limefanyika katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid Arusha Mjni, limehudhuriwa na viongozi mbali mabali wa kitaifa na mafisa wa Jeshi nchini pamoja na wananchi mbali mbali wa mkoa wa Arusha.

Kabla ya kuwatunuku kamisheni maafisa hao wa jeshi, Rais Magufuli alikagua gwaride maalum, na kutoa zawadi kwa maafisa wa jeshi watano waliofanya vizuri zaidi kwenye masomo yao.

Tukio hilo la Rais Magufuli kuwapa Kamisheni Maafisa wa Jeshi katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid ni la kwanza kufanyika katika uwanja wa wazi badala ya viwanja vya jeshi wilayani Monduli.

Rais Magufuli Atangaza Ajira 3000 za Wanajeshi

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa nchi Dkt. John Pombe Magufuli, ametangaza kutoa ajira kwa wanajeshi 3000 wapya mwaka huu, ili jeshi la Tanzania liweze kuwa na askari wa kutosha.

Rais Magufuli ametoa taarifa hiyo leo alipokuwa akihutubia umma mara baada ya kuwapa kamisheni maafisa wa Jeshi, katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid mkoani Arusha, huku akitaka wahusika kutowasahau vijana waliohitimu mafunzo ya JKT.

"Lakini pia leo tumepata maofisa 422, unapokuwa na jeshi la maofisa lazima kuwepo na 'junior officers', huwezi ukawa na jeshi lote lina maofisa, kwa kutambua hili natangaza rasmi kwamba nitatoa nafasi 3,000 za kuajiri wanajeshi wapya, na hawa wataoajiriwa muzingatie na wale ambao wamemaliza JKT, lengo ni kuhakikisha jeshi letu linakuwa na maaskari wa kutosha na la kisasa zaidi", amesema Rais Magufuli.

Leo Rais Magufuli ametoa kamisheni kwa Maafisa wa Jeshi 422 waliohitimu mafunzo katika chuo cha Monduli, hafla ambayo imekuwa ya kwanza kufanyika katika uwanja wa umma,

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumapili ya Septemba 24


Ndege za kijeshi za Marekani zapaa karibu na Korea Kaskazini kuonyesha ubabe

$
0
0
Ndege za kijeshi za Marekani zimepaa karibu na pwani ya mashariki ya Korea Kaskazini katika kuonyesha ubabe wa kivita, idara ya ulinzi nchini Marekani pentagon imesema.

''Hatua hiyo ni kuonyesha kuwa rais Trump ana njia tofauti za kijeshi kushinda vitisho vyovyote'' , msemaji Dana White alisema.

Marekani na Korea Kaskazini zimerushiana cheche za maneneo katika kipindi cha hivi majuzi.

Katika Umoja wa mataifa siku ya Jumanne, bwana Trump alisema kuwa ataiangamiza Korea Kaskazini iwapo Marekani italazimika kujitetea na washirika wake.

''Hili ni eneo ambalo jeshi lolote halifai kupitia na ni ndege za kijeshi za Marekani ambazo zimeweza kulifikia katika karne ya 21, licha ya tabia mbaya ya Korea Kaskazini'', alisema Bi White.

Tangazo hili lilijiri muda mfupi kabla ya waziri wa kigeni wa Korea Kaskazini kutoa hotuba yake katika umoja wa mataifa.

Mapema siku ya Jumamosi , tetemeko lenye ukubwa wa 3.4 katika vipimo vya Ritcher lilisikika karibu na kituo cha kujaribia makombora cha Korea Kaskazini na kuzua hofu kwamba taifa hilo huenda lilitekeleza jaribio jingine la kombora lake.

Lakini wataalam wamesema kuwa lilikuwa tetemeko la ardhi.

Jipatie Riwaya ya Kusiimua ya President Wife Toka kwa Mtunzi Makini

$
0
0
NI JUMAPILI NYINGINE, NINAKUSOGEZEA OFA HII KABAMBE YA PUNGUZO LA BEI KWA VITABU(Soft Copy) VYANGU VYOTE,.

Jipatie ofa ya kitabu cha PRESIDENT WIFE(Shadow of D.F.E) kwa sh 5000 kupitia mitandao ya Whatsapp 06570725588 na Email eddazariaM@gmail.com 
Pia unaweza kusoma kitabu cha SHE IS MY WIFE  kwa sh 5000/=.

VITABU VINGINE AMBAVYO VIPO KWENYE OFA LEO JUMA PILI NI.
1. AIISSII U KILL ME(Hi inauzwa kila episode moja sh 250)
2. AM NOT A DOCTOR sh 7000/=
3. MY LIFE sh 7000/=
4.HARD DAY sh 4000/=
5. SEX DEALERS sh 3000/=
6. MY MOM'S FRIEND sh 6000/=
7. SORRY MADAM D.F.E- 5000/=
8. SHE IS MY WIFE- 5000/=
PIA JIUNGE KWENYE GROUP LANGU LA ADITHI YA POWER NA AIISSII U KILL ME LEGACY WAHTSAPP UJIPATIE OFA YA EPISODE 28 BUREE. ADA GROUP NI SH 3000 KWA MWENZI.

MALIPO YOTE YA VITABU NA ADA YA GROUP UNANALIPIA KWA MPESA 0768516188 JOYCE MBWAMBO au TIGOPESA 0657072588 AZARIA MSULWA au AIRTEL MONEY 0682630798 AZARIA MSULWA.

WASILIANA NAMI 0657072588 AU 0768516188 
KARIBUNI SANA TENA SANA

Mke wa Tundu Lissu, Dreva Wake Wafunguka kwa Mara ya Kwanza

$
0
0
Kwa mara ya kwanza, Alicia Magabe ambaye ni mke wa Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), Tundu Lissu amezungumzia tukio la mumewe kushambuliwa kwa risasi na kudokeza kwamba haliwezi kuwa limetokana na sababu nyingine isipokuwa kazi ambazo amekuwa akizifanya.

Pia amezungumzia kuhusu afya yake na kueleza kuwa bado siyo nzuri na kuwaomba Watanzania waendelee kumuombea.

Mbali ya Alicia ambaye pia ni mwanasheria, dereva wa Lissu naye amezungumza akisema ameathiriwa kwa kiasi kikubwa na tukio hilo huku akiahidi kuripoti polisi mara baada ya kurejea nchini.

Lissu ambaye pia ni Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), amelazwa katika Hospitali ya Nairobi tangu alipopelekwa huko baada ya kupigwa risasi akiwa ndani ya gari nje ya nyumba yake mjini Dodoma mchana wa Septemba 7 akitokea bungeni.

“Watanzania wote wanajua Lissu maisha yake yote amekuwa ni mtetezi wa wanyonge na tukio hili amelipata kutokana na kazi zake hizo hivyo nawaomba tumuombee tu,” alisema.

“Ninachoweza kusema hali ya mheshimiwa Lissu sio nzuri ingawa ni tofauti na tulivyomleta hapa, hivyo naomba Watanzania kuendelea kumuombea.”

Aliwashukuru Watanzania kwa michango, na maombi yao kwa Lissu akisema hiyo inaonyesha ni jinsi gani wanathamini mchango wake kwa jamii.

Alipoulizwa kuhusu kauli ya Serikali kwamba ipo tayari kugharimia matibabu ya Lissu popote ikiwa itaombwa na familia hiyo, Alicia ambaye pia ni wakili alisema kwa sasa hana maoni.

“Katika hili no comment (sina maoni) ndio tumesikia jana amezungumza na kwa kuwa jambo hili siyo la uamuzi wa mtu mmoja, mimi sina cha kusema,” alisema.

Hata hivyo, alisema anashukuru kazi kubwa ambayo inafanywa na madaktari wa Hospitali ya Nairobi na kusema wanaridhishwa na matibabu ambayo anapatiwa kwa sasa.

Kauli  ya  Dereva wa Lissu
Mbali ya Alicia, dereva wa Lissu ambaye ndiye mtu pekee waliyekuwa wote siku ya tukio hilo, Simon Bakari naye alizungumza kwa mara ya kwanza kuhusu tukio hilo na kudokeza kwamba limevuruga na hana kumbukumbu sahihi.

Dereva huyo ambaye naye anaendelea kupatiwa matibabu ya kisaikolojia katika hospitali hiyo ya Nairobi alisisitiza, “Kwa sasa siwezi kuzungumza vizuri tukio hili kwani nadhani sina kumbukumbu vizuri.”

Alipoulizwa kuhusu wito wa polisi wa kwenda kutoa maelezo, alisema atafanya hivyo pindi atakaporejea nchini baada ya matibabu.

“Nilisikia polisi wamenitaka nikatoe maelezo lakini sijisikii vizuri na bado napata matibabu. Nitakwenda,” alisema.

Serikali Yaondoa Masharti Sakata la Matibabu ya Tundu Lissu

$
0
0
Msemaji wa Serikali Dkt. Hassan Abbas amefunguka na kusema kuwa hakuna masharti yoyote serikali imeweka ili Mbunge wa Singida Mashariki Mhe. Tundu Lissu apatiwe matibabu na kusema wanasubiri maombi ili waweze kugharamia matibabu ya Lissu.

Msemaji wa serikali amesema hayo jana kupitia mtandao wake wa twitter siku moja baada ya Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe kusema kuwa alipata taarifa kutoka kwa wasaidizi wa Spika wa Bunge kuwa wapo tayari kugharamia matibabu ya Tundu Lissu kwa masharti ya kuwa mgonjwa lazima apelekwe India, wapate barua ya maombi na kupata ripoti ya madaktari jambo ambalo Mbowe anasema alilikataa na kusema hawezi kufanya hivyo.

Kufuatia kuwepo kwa taarifa hizo ndipo Msemaji wa Serikali ameibuka na kusema kuwa hakuna masharti yoyote ambayo wameyaweka na kusema serikali ipo tayari kugharamia matibabu ya Tundu Lissu na kuwa wao wanasubiri barua kujua gharama za matibabu.

"Hakuna sharti lolote, tunasisitiza tena na bado tunasubiri, leteni barua rasmi tujue gharama na itifaki nyingine za tiba. Tutagharamia" alisema Dkt. Abbas

Aidha Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mh. Ummy Mwalimu aliendelea pia kufafanua jambo hilo kuwa Mbunge Tundu Lissu aliondolewa kwenye utaratibu wa serikali alipopelekwa nchini Kenya hivyo anadai ili serikali iweze kuingia katika gharama za kulipia matibabu lazima wapate ridhaa ya familia.

"Mgonjwa alitolewa kwenye utaratibu wa Serikali alipopelekwa NRB. Sasa gharama/tiba zaid yahitajika. Serikali inaingiaje bila ridhaa ya familia? Mgonjwa ni Mbunge, anahitaji matibabu zaidi. Lakini kwa kuwa sasa yupo nje ya utaratibu wa Serikali, Serikali kushiriki ni lazima yawepo maombi" alisisitiza Ummy Mwalimu

Je,una Upungufu Wa Nguvu Zakiume,kukosa Hamu Ya Tendo La Ndoa,kufika Kileleni Mapema Na Kushindwa Kurudia ????

$
0
0
Tatizo la kukosa au kupungukiwa nguvu za kiume na maumbile madogo ya kiume husababishwa na mambo mengi kama,KISUKARI,NGIRI,CHANGO,TUMBO KUUNGURUMA,MAUMIVU YA KIUNO,UNENE KUPITA KIASI,KUJICHUA nk.

Upungufu wa nguvu za kiume husababisha tendo la ndoa kutofanyika kwa kujiami nakwa usahihi nahivyo husababisha ndoa, mahusiano mengi kuvunjika.

BAADHI YA DALILI ZA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NI,
1 KUKOSA HAMU YA TENDOL LA NDOA 
2 UUME KISIMAMA KWA KULEGEA 
3 KUWAHI KUFIKA KILELENI 
4 KUSHINDWA KURUDIA TENDO LA NDOA WAKATI 
5 KUCHOKA SANA BAADA YA ROUND YAKWANZA NAKUKINAI TENDO LA NDOA KABISA.

TUMIA 3 POWER KWA TATIZO LA UKOSEFU(UPUNGUFU)WA NGUVU ZA KIUME NAHAMU YA TENDO LA NDOA.FINA HUBORESHA MAUMBILE YA KIUME KWA KUNENEPESHA KWA SAIZI UIPENDAYO HAIJARISHI UMRI.

PIA KUNA DAWA ZA KURUDISHA MPENZI KWA MUDA MFUPI SANA NAZAKUPATA KAZI,KESI,KUDHULUMIWA,NK 

WASILIANA NA SHEIKH OMARY AKUTATULIE MATATIZO YAKO HATA KAMA UMEHANGAIKA SANA PASIPO MAFANIKIO 

Pia sheikh omary anatibu busha bila opresheni,kisukari,ngiri,presha vidonda vya tumbo,korodani kuvimba,na anatoa dagu za utajiri kwa wanaohitaji bila masharti yoyote magumu.ANAPATIKANA MBAGALA ZAKIEM,NAUTALETEWA POPOTE ULIPO.

 SIMU; NO 0767145357/0629034550.

Kwa Nini Wanaume Wengi Wanaupungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo?

$
0
0
Asilimia 45 ya wanaume wapo tofauti na wengine kwa kuwatimizia vyema wake au wapenzi Wao na kuwasababishia kutoka nje ya ndoa zao.

NINI CHANZO CHA HAYO?Kupiga punyeto,Ngiri,Vidonda vya tumbo,Magonjwa ya moyo,Presha,Kisukari,Korodani moja kuvimba,Msongo wa mwazo,Kufanyiwa tohara ukiwa mtu mzima n.k.DOKTA MANYANDA sasa kapata tiba sahihi ya tatizo la NGUVU ZA KIUME.

MUHAMA:Hii hutibu na kuponyesha kabisa tatizo la nguvu za kiume,utakuwa na uwezo wa kurudia tendo zaidi ya mara tatu bila kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dakika 15-20.DAWA hii imechanganywa miti 12.Hata wazee wenye umri mkubwa wanapona kabisa.OKO NDOA YAKO SASA. 

MANGUNGU MIX: Ndio tiba tosha kwa sasa ambayo hurefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo inch 1-8 na unene sentimita 1-5,dawa hii ipo ya kupaka na kunywa na haina madhara yoyote kwa mtumiaji.

NITOFAUTI NA ULIZO WAHI KUZITUMIA.Pia tuna dawa za kupatanisha mke,mme,mpenzi au bosi wako kwa mda mfupi sana,Uzazi,Kusafisha nyota,

Je unamali yako unauza hupati wateja?Wasiliana nami 0716-263605 

DOKTA MANYANDA ANAPATIKANA KASULU KIGOMA,Kwa wale wa mikoani huduma hii utaipata popote pale.

Bunge Laijibu Hospitali ya Kenya Anakotibiwa Tundu Lissu

$
0
0
Ofisi ya Bunge imetoa uthibitisho wa nyaraka kuonyesha kuwa fedha zilizochangwa na wabunge zimewasilishwa hospitalini anakotibiwa Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu.

Lissu aliyeshambuliwa na kujeruhiwa kwa risasi nyumbani kwake Area D mjini Dodoma Septemba 7, anaendelea na matibabu katika Hospitali ya Nairobi nchini Kenya.

“Napenda kusisitiza kuwa fedha zilizochangwa na wabunge Sh43 milioni kwa ajili ya kusaidia matibabu ya Mheshimiwa Tundu Lissu tayari zimetumwa katika Akaunti ya Hospitali ya Nairobi anakopatiwa matibabu,” imesema taarifa iliyotolewa leo Jumapili na Kitengo cha Habari, Elimu kwa Umma na Mawasiliano cha Bunge.

Fedha hizo zimetumwa kupitia Benki Kuu ya Tanzania (BoT).

Bunge limesema fedha hizo ambapo kwa mujibu wa viwango vya kubadilishia fedha vya BoT kwa siku hiyo ili kuwa ni sawa na Shilingi ya Kenya 1,977,120.58.

“Kiasi hicho cha Fedha kilitumwa Septemba 20, 2017 kwenda Benki ya Barclays, Tawi la Hurlringham, Akaunti Namba 0451155318 yenye jina la Kenya Hospital Association.


Tundu Lissu Aikataza Familia Kuandika Barua ya Matibabu Serikalini

$
0
0
Familia ya mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lissu, imesema imezuiliwa kuandika barua kwa ajili ya kuiomba serikali kugharamia matibabu ya mbunge huyo kwa madai amehaidi suala hilo atakuja kulishughulikia yeye mwenyewe hivi karibuni.

Hayo amebainisha kaka wa mbunge huyo ambaye pia ni msemaji wa familia, Alute Mughwai baada ya kupita siku kadhaa tokea serikali ya Tanzania kupitia Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu kutoa kauli yao ya kusema mgonjwa ni mbunge ambaye anayehitaji matibabu zaidi lakini kwa kuwa yupo nje ya utaratibu wa serikali na ili serikali iweze kushiriki ni lazima yawepo maombi ya kufanya hivyo.

"Majira ya saa nne hivi niliweza kuzungumza na Mhe. Tundu Lissu akiwa hospitalini Nairobi baada ya kumjulia hali nilimueleza taarifa ya Mhe. Waziri kwamba tuandike barua ili aweze kupata matibabu kwa gharama za serikali, akanijibu kuwa jambo hilo atalizungumzia yeye mwenyewe siku za hivi karibuni. Kwa sababu yeye anaamini ni mbunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye anahaki zote anazostahili kulipwa, kama mbunge ikiwa ni pamoja na kupatiwa matibabu endapo ataugua au atapatwa na maradhi", amesema Alute.

Pamoja na hayo, kaka wa Lissu ameendelea kwa kusema "Mpaka hivi sasa jeshi letu la polisi halijaweza kumkamata mshtakiwa yeyote juu ya tukio la Lissu wakati jambo hilo lilitokea mchana kweupe na watu wengi walishuhudia. Sasa mazingira hayo yametupa wasiwasi kama tukio hilo litachunguzwa kikamilifu, hatuna wasiwasi na uwezo wa polisi wetu kufanya huo uchunguzi lakini shida yetu ni utayari".

Aidha, Alute amesema wameshamuandikia barua Mwanasheria Mkuu wa serikali ili waweze kupatiwa msaada wa kiuchunguzi zaidi dhidi ya tukio hilo lililomtokea ndugu yake.

"Barua tumeandika Septemba 16, mwaka huu kwenda kwa Mwanasheria Mkuu wa serikali maana ndiyo mamlaka inayopaswa kuchukua hatua za kuombwa msaada wa kiupelelezi kwa niaba ya serikali yetu huko nje ya nchi, na hiyo barua nimeinakili kwa Mhe. Waziri Sheria na Mambo ya Katiba", amesisitiza Alute.

Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu alishambuliwa na risasi nje ya nyumba yake mjini Dodoma wakati akitokea Bungeni na watu wasiojulikana Septemba 7, 2017 na mwishowe kukimbiziwa katika hospitali ya Nairobi nchini Kenya kwa ajili ya kupatiwa matibabu zaidi.

Pata Tiba ya Tiba ya Tatizo la Nguvu Za Kiume........Inasaidia Kukufanya Urudie Mara 5 na kuchelewa kwa Dakika 20

$
0
0
TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO LINATIBIKA.Baada ya utafiti wa mda mrefu juu ya matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume na ukosaji wa hamu ya tendo la ndoa ama kushindwa kurudia tendo kwa haraka DR Magise imekuletea tiba ya matatizo hayo kwa kutumia dawa za: 
 
FUUl POWER:Ni dawa asili ya vidonge inayotibu tatizo la upungufu au ukosefu wa nguvu za kiume,dawa hii inamchanganyiko wakutosha wenyekuzalisha vichocheo vingi vya Hemone za Gestrogen vikiwemo vitamin B6&B1,vitamini E,pamoja na madini aina ya zinc vitakufanya kuwa na nguvu na mzunguko mzuri wa damu na kuongeza hamu na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya hatua nne au zaidi,na kuchelewa kufika kileleni zaidi dakka 20-30.
 
NYAMVA:Inarutubisha maumbile ya uume yani kurefusha na kunenepesha nchi 4-7 upana cm3-4 standard kiafya haijalishi umri wako hata kwa wazee ukiitumia maumbile yako yatabaki kuwa hivyo siku zote,Pia tunatibu Presha,kisukari siku7,ngiri,chango la tumbo tumbo kujaa gesi,kutopata choo vizuri

 TUPO TZ DAR ES SALAAM   MBAGALA RANGI TATU.HUDUMA HII UTALETEWA POPOTE ULIPO .WASILIANA NAMI 0783741788,0715741788 -DR MAGISE

Polepole: Magufuli ni Mwanaume wa Shoka Aliyeweza Kuitikisa Afrika Nzima

$
0
0
 Maono ya Mwalimu kwa Uongozi wa Awamu ya V
Mwalimu Nyerere alipata kusema katika kitabu cha Afrika Today and Tomorrow katika ukurasa wa 84 “…Africa is yet to liberate itself – to attain Economic liberation – gaining control over, and having responsibility for our economic development strategy and macro economic policies in order to be able to provide for, at least, decent basic standard of living for all our people. Unless this is done our political independence will always be in danger – who controls money, they say, also controls politics.”


Tafsiri yangu ya maneno haya Mwalimu Nyerere anasema “Afrika bado inahitaji kujikomboa – ili kufikia Uhuru wa Kiuchumi – ili kuwa na udhibiti, na wajibu katika mikakati ya maendeleo yetu kiuchumi na sera zetu za kiuchumi ili tuweze kuwapatia watu wetu angalau kiwango cha msingi na chenye utu cha ustawi wa maisha yao. Kama hili lisipofanyika uhuru wetu wa kisiasa bado utakuwa mashakani/hatarini – mwenye kuzidhibiti fedha, wanasema, hudhibiti siasa pia.”

Mwalimu alipata kuyasema haya mwaka 1999 na bado alikuwa ameona mbali sana. Mwalimu alikuwa anatukumbusha kazi kubwa ambayo kipindi kile mwaka 1999 ilikuwa haijakamilika na akiutizamia wakati ujao kwamba bado kazi hiyo ilipasa kukamilishwa – Ukombozi wa Kiuchumi unaotuletea Uhuru wa Kiuchumi kwa Taifa letu la Tanzania.

Kipindi fulani yeye mwenyewe Mwalimu alipata kuamini hakika kwamba uhuru wa Tanzania haungalikuwa mkamilifu mpaka Bara lote la Afrika kukombolewa. Mwalimu akasema mapambano yao ya kulikomboa bara la Afrika yalikamilika mwaka 1994 walipofanikiwa kuufuta ukaburu Afrika Kusini.

Mwalimu Nyerere anaandika Mwaka 1999 kwamba sasa (1999) na kuliko kipindi kingine kabla, anaamini kwa nguvu kubwa kwamba Uhuru wa kisiasa wa Bara la Afrika hautakuwa kamili isipokuwa watu wa Afrika wachukue na kushika kwa mikono yao udhibiti wa uchumi wao badala la kuuacha uchumi wa Afrika katika mikono ya nguvu za kigeni.

Aidha Mwalimu anabashiri na kwa lugha ya kiingereza akisema “This is the Challenge of the new generation of leaders in Africa” akimaanisha kwa kiswahili “Na hii ndiyo changamoto ambayo kizazi kipya cha viongozi wa Afrika wanayo” Tafsiri ni yangu.

Mwalimu anaendelea kusema “Viongozi wa kizazi chake waliweza kutenda kilichowezekana kipindi kile. Viongozi wapya ni lazima wafanikiwe katika utume wao mpya ambao ni ukombozi wa kiuchumi na kushindwa kufanikiwa katika utume huu kutamaanisha kuuachia uhuru wa nchi zao, wa wananchi wao na kukubali hali ilivyo sasa ya utegemezi wa kiuchumi.

Mwalimu Nyerere alikiri kwamba Uongozi wa Afrika unaweza kuwekwa katika mafungu matatu;

Mosi, Viongozi waliopambana kuhakikisha Afrika inakuwa huru, Pili, viongozi waliohangaika na mdororo wa uchumi uliotokana na sera mbovu na zisizotaarifiwa na uhalisia wa Afrika miaka ya 80 na 90. Wapo pia viongozi ambao walidumbukia katika ama rushwa kubwa na kuvuruga Uongozi wa nchi mbalimbali Afrika au matukio ya Mapinduzi ya kijeshi kwa kisingizio cha kupambana na ufisadi katika nchi hizo. Kwa bahati nzuri kizazi hiki kinaelekea kwisha.

Tatu, ni awamu mpya ya viongozi inayoibuka, hii ni awamu ambayo tutashuhudia kuongezeka kwa viongozi waadilifu na wazalendo wanaochukua Uongozi wa nchi za Afrika. Awamu hii ndio ambayo inakuja kusafisha masalia ya Uongozi usiowajibika na chembechembe za uzembe. Awamu hii itatoa Uongozi bora ambao utaweza kusema HAPANA kwa wale ambao wanacheza na mambo yetu ya ndani katika nchi zetu.

Aidha Mwalimu Nyerere anaendelea kusema viongozi hawa wa awamu mpya wanajua matakwa ya wananchi wao, ni aina mpya ya viongozi wanaotoa aina mpya ya Uongozi. Viongozi hawa wamenia kukamilisha mapambano ya ukombozi – ukombozi wa kiuchumi.

Wajibu Mkuu Mwalimu Nyerere anaeleza wa Maendeleo ya Afrika unabaki kwa waafrika wenyewe. Msaada wowote utakuwa ni nyongeza tu katika jitihada za waafrika wenyewe. Na kama kutakuwa na uhusiano wowote basi lazima mahusiano haya yajengwe katika namna ambayo yatanufaisha waafrika kwa haki na sio katika misingi ya unyonyaji. Mwalimu anamaliza kwa kusema “shime sote tuungane mikono kuiokoa Afrika dhidi ya unyonyaji wowote baadaye”.

Baada ya rejea na nukuu hizi za Mwalimu napenda kujadili CCM MPYA TANZANIA MPYA na ukweli kwamba uhuru wa kiuchumi ni mapambano na asilani hautakuja katika sahani ya fedha. Tafakuri yangu nimeigawa katika vipindi tatu, Mosi, Tulikotoka ni mbali, Pili, Tuliko sasa na Tatu, Tunakokwenda.

Tulikotoka ni mbali
Serikali za Awamu ya Kwanza na ya Pili zimepambana sana kuleta maendeleo ya Taifa la Tanzania, kwanza ya ujenzi wa Taifa Moja Imara na madhubuti linaloitwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Tanganyika na Zanzibar kwa pamoja tumezirithi kutoka kwa wakoloni lakini Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ujenzi wake tumeufanya wenyewe. Mwaka 1964 ni mwaka muhimu katika ujenzi wa Taifa na kisha baada ya hapo tunalo zoezi endelevu la kujenga Taifa hili.

Ujenzi wa Taifa la Tanzania haukuwahi kuwa rahisi na umepitia changamoto na mitihani mingi sana. Natafakari katika pande la ardhi ambalo kuna watu wenye lugha na makabila tofauti tofauti zaidi ya 120, na kila kabila likiwa na utamaduni wake, desturi zake na Uongozi wake (Machifu).

Hili Mwalimu Nyerere alianza na viongozi waliofuatia baada yake wakaendelea nalo na leo tunajivuna Tanzania ndio nchi pekee katika Afrika ambayo watu wake wana lugha moja ya Taifa ambayo sio ya kabila mojawapo.

Mitihani ilianza mwaka 1964, wakati wa uamuzi wa kihistoria wa kuunganisha nchi mbili zilizokuwa huru kwa maana ya Tanganyika na Zanzibar na kuunda nchi moja mpya na huru ilopewa jina “Jamhuri ya Muungano wa Tanzania”. Wahisani wetu wakubwa wa maendeleo kipindi hicho Ujerumani Magharibi hawakupendezwa na uamuzi huu na wakatishia kuvunja uhusiano nasi.

Kabla hatujatishika tukajitathimini kama Taifa, heshima yetu na umuhimu wa tunu yetu ya UMOJA. Kwa kauli moja tukavunja uhusiano na Ujerumani Magharibi na kurudisha msaada wa fedha ambao tayari ulikuwa umetolewa kwetu. Funzo hapa ni haijalishi tunapitia wakati gani lakini wakati wote tunapaswa kulinda heshima na umoja wa Taifa letu.

Mtihani wa pili ulikuwa mwaka 1965, hii ilikuwa baada ya kikundi cha watu wachache kujitangazia uhuru kule Zimbabwe ya leo (Unilateral Declaration of Independence). Tanzania iliamini katika uhuru wa kweli na wa wengi nchini humo. Tukawaeleza waingereza kwamba tabia ile ni mbaya na haikubaliki na kwa kuwa Uingereza ndiye dada mkubwa katika familia ya Jumuiya ya Madola tukamtaka achukue hatua dhidi ya utawala wa wachache uliojitangazia uhuru chini ya bwana Smith.

Waingereza walisua sua na hata baada ya nchi za Afrika kulaani vikali kitendo kile bado hawakuchukua hatua kali na stahiki. Kati ya Nchi za Afrika huru ni Tanzania na Ghana tu ndio zilizovunja mahusiano na Uingereza, kitendo hiki kililenga kupeleka ujumbe kwamba hatuukubali unyonyaji wa aina yoyote iwe Tanzania au nje ya Tanzania na hasa kwa mataifa rafiki kipindi kile.

Mwaka 1970-75 tukapata ukame mkubwa katika nchi yetu, wakati hali hiyo ikiendelea tukatoka na mikakati ya kupambana na hali hiyo kwa kuanzisha skimu kadhaa za umwagiliaji ili kuongeza uzalishaji wa chakula nchini. Haikuwa kazi rahisi, ilitaka Chama, Serikali na Umma wa Wananchi kuwa na uelewa wa pamoja wa hali iliyokuwa inatukabili na kusimama imara pamoja ili kukabiliana nayo.

Tukavuka salama, na mwaka 1977 tukaandika historia nyingine kubwa ya kuunganisha vyama vya TANU na ASP na kuzaliwa Chama Cha Mapinduzi (CCM).
 
Mwaka mmoja baadaye tukaingia katika Vita dhidi ya Nduli Iddi Amin, vita ya Kagera. Vita hii ilitupa heshima kubwa maana tuliipigana wenyewe na licha ya kwamba Nduli alisaidiwa na mataifa mengine lakini Wananchi wa Tanzania na Jeshi letu la Wananchi (JWTZ) tukamfurushia mbali hadi nje ya mipaka yetu. Vita ya Kagera licha ya heshima kubwa ilituacha katika wakati mgumu sana kiuchumi maana tulitumia karibia hifadhi yetu yote ya fedha za kigeni ambayo hutumika kuagiza bidhaa muhimu kutoka nje.

Kuna kipindi tulifika tukabaki na akiba isiyozidi wiki mbili ya Mafuta ya Magari, ulikuwa wakati mgumu sana. Huwa nafananisha Uongozi wa Nchi kama Uongozi wa familia inayojitahidi sana kujikwamua kihali na kiuchumi licha ya changamoto mbalimbali. Baba au Mama anaweza kurudi nyumbani na chakula hakuna na ilhali watoto hujua baba au mama lazima awe na uwezo wa kuleta chakula nyumbani. Nadhani Mama na Baba wote wataungana na mimi kwamba hakuna wakati mgumu ambapo watoto wanakutegemea uwawezeshe na hauko katika uwezo wa kuwezesha lakini unapambana uwawezeshe maana hawawezi amini kwamba baba au mama hawezi kuwezesha mahitaji yao.

Miaka ya Themanini (80) ikawa na Changamoto zaidi na ukiongeza na masharti gandamizi ya Taasisi za Kifedha za Kidunia zijulikanazo kwa kiingereza kama “Britton Woods Institutions”. Wakatulazimisha Serikali isifanye tena uzalishaji na iachane na umiliki wa mashirika ya umma, wakalazimisha tushushe thamani ya fedha yetu (shilingi ya Tanzania) na wakatueleza ili tupate misaada kutoka kwao kwanza ni lazima turidhie masharti haya niliyoyataja kwa uchache na tukubali kutekeleza programu za kurekebisha uchumi wetu (Structural Adjustment Programmes – SAPs).

Kibaya zaidi na kwasababu tulikuwa na msimamo wa kuendelea na Mapambano ya kuukomboa Uchumi wetu dhidi ya mikakati ya kinyonyaji ya kibeberu iliyokuwa inatambulishwa na Taasisi hizi za kifedha za kidunia, waliamua pia kutuhujumu waziwazi.

Hujuma ya uchumi wetu ilikuwa kutoka nje na ikiratibiwa kimkakati kabisa na ilikuwa pia kutoka ndani ikiratibiwa kwa ustadi na vibaraka wa mabeberu, watanzania wachache waliokosa uadilifu, uaminifu, uzalendo na mapenzi ya dhati kwa Taifa letu.

Vilikuwepo viwanda zaidi ya 400 na migodi kadhaa, lakini viwanda na migodi inapojiendesha kila baada ya muda huhitaji vipuri, basi kila tulipoagiza vipuri kutoka kampuni za nje walitoa visingizo mbalimbali, mara kampuni zimeuzwa au kampuni ilishafilisika na kadhalika na kadhalika. Hivyo baada ya muda viwanda vingi vilikosa vipuri na kulazimika kusimama na watu kupoteza ajira. Hali kama hiyo ilitokea katika migodi kadhaa na ikailazimu serikali kuweka mpango wa kuifunga migodi hiyo.

Hata pale tulipoamua kampuni yetu ya kizalendo Nyumbu itengeneze vipuri hapa hapa nchini basi mataifa makubwa yalififisha dhamira njema ya kampuni za kizalendo kwa kutoa misaada ili kampuni za ndani zishindwe kufanya biashara, zishindwe kujiendesha na hatimaye kuanguka.

Changamoto ziliongezeka sana kwasababu tulisimamia haki huku tukiendelea kupinga udhalimu. Ililazimu serikali itafute mbinu mbadala ya kujiendesha na ndipo mawazo kama ujenzi wa bwawa la kuzalisha umeme la Stiegler’s Gorge likaja lakini uwezo wa kujenga hatukuwa nao wakati huo.

Mwalimu Nyerere alijua huenda katika pwani yetu tunaweza kuwa na gesi au mafuta na akazungumza na nchi fulani za Magharibi ili kuja kufanya utafiti wa uwepo wa mafuta na gesi. Wataalamu wa kimagharibi wakaja na wakafanya utafiti na kusema hakuna dalili yoyote ya mafuta au gesi.

Mwalimu alikuwa mvumilivu na hakuwa mtu wa kukata tamaa, na alizungumza na marafiki zetu wa India ambao walikuja hapa na wakachoronga maeneo machache ya pwani ya Tanzania (Pwani na Lindi) na hatimaye gesi ikapatikana, wakamwambia imepatikana na wakalipua kisima kimoja na kikawaka moto bila kuzimika kwa miezi mitatu. Mwalimu Nyerere akawaambia wakizibe kisima hicho na pasijulikane pahala pale mpaka watakapokuwa tayari hapo baadaye.

Kuna kipindi tulipokuwa tukifanya mashauriano (negotiations) katika masuala ya kiuchumi ili “mabwana wakubwa” ama walegeze kamba au watusaidie, ilitubidi sisi kusafiri kuwafuata, mfano, kule Ulaya katika vikao vya Paris Club, vikao hivi wanakaa matajiri wa dunia na mataifa makubwa. Mzee Cleopa David Msuya alishiriki kule, ilikuwa lazima uwafuate Ulaya mabwana wakubwa kule, na kuna kipindi aliwafuata na aliishia mapokezi, ubeberu bila kugangamala una jeuri, kiburi na dharau sana.

Napenda watu wajua safari yetu imekuwa yenye milima na mabonde lakini kitu kimoja cha kujivuna tumebaki na Taifa moja. Ni wajibu wetu kukumbushana tulikotoka ni mbali na hasa vijana na watoto wetu.

Tulipo sasa
Tanzania iko katika awamu ya Tano ya Uongozi wake tangu kuasisiwa kwake. Baada ya vipindi viwili vya awamu ya Nne, CCM iliamua kufanya Mageuzi Makubwa ambayo yanahakikisha chama hiki kinabaki kuwa Chama cha Wanachama na kinachoshughulika na shida za watu wetu.

Mageuzi ya CCM yanalenga pia kuhakikisha katika kila mawanda haki ya watanzania inapatikana. Taifa hili ni tajiri sana na linaweza kujitosheleza ndani lakini tumeshindwa kwa muda mrefu kujenga uwezo wa ndani ili kutimiza ndoto hii ya kujitegemea ama kwa unyonge au wakati mwingine kwa uzembe wa baadhi yetu.

Chama Cha Mapinduzi baada ya kujitathimini kikatafuta mtu ambaye ataweza kuishika agenda ya Mageuzi ya CCM, na ieleweke Mageuzi ya CCM yatatoa mwelekeo kwa Mageuzi ya Serikali ili sote tuweze kukidhi na kuweka jitihada kubwa ya kutosheleza mahitaji na matarajio ya msingi ya watanzania.

Mtu huyu ambaye ameaminiwa kwanza na wana CCM kisha watanzania ni Ndugu yetu John Pombe Joseph Magufuli, mtanzania kweli kweli na mwenye uchungu wa kuhujumiwa kwetu. Mtu ambaye CCM ilimleta (Ndg. Magufuli) ilipasa awe mtu ambaye hatatuonea soni, hataleta urafiki, hataona haya kutuambia hapa na pale tulikosea.

Chama Cha Mapinduzi (CCM) kilitafakari na kuamua kutuletea Ndg. Magufuli ili pia aweze kutusimamia kwa haki tena pasina kujiona mnyonge hata mbele ya wabwana wakubwa wa ndani na nje ya nchi.

Leo Afrika nzima inazizima kwamba yuko mwanaume ambaye ameweza kusema imetosha “enough is enough” sio haki na ni unyonyaji kuchukua madini yetu katika namna ambayo haki yetu inapokwa. Ndugu Magufuli ana amini sana katika sekta binafsi na hasa katika ujenzi wa uchumi wa viwanda sambamba na sekta ya umma, lakini ana amini zaidi katika sekta binafsi inayojiendesha kwa kanuni za maadili ikiwemo kulipa kodi. Ana amini katika uwekezaji kutoka nje, lakini unaotambua kwamba sisi ni Taifa huru na tunayo haki ya kunufaika kutokana na utajiri wa rasilimali zetu.

Ndugu Magufuli ana amini kwa hakika uwekezaji kutoka nje unapaswa kujengwa katika misingi ya haki na usawa na kwamba kila upande una wajibu Tanzania na wawekezaji, Tanzania iweke mazingira ya uwekezaji hasa wa viwanda na wawekezaji watende sawa sawa na kanuni za kidunia za maadili ikiwemo kutokuiba kwa ujanja ujanja, kutokwepa kodi, kutosafirisha pesa kwenda nje “capital flight” wakati zinawezwa kutunzwa hapa na kadharika.

Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimemleta ndugu Magufuli wakati muafaka wakati tunamhitaji zaidi mtu kama yeye. Ukisoma Maelezo na Nukuu za Mwalimu Nyerere katika maelezo yangu ya awali juu ya Maono ya Mwalimu Nyerere utaungana nami kusema ile aina ya Uongozi mpya katika bara la Afrika, Tanzania tumekuwa kinara wa kwanza na wengine watafuata ili bara la Afrika lirejeshe heshima yake ya uhalisia na asili.

Wiki ijayo nitaeleza kuhusu tunakokwenda na kwanini Ndugu Magufuli ni zawadi na tumtumie katika kipindi hiki cha mpito na cha kunyooshana nidhamu ili maisha yetu katika miaka mikuu 75 “The Great 75 Years” iwe rahisi na yenye mafanikio makubwa hii ni kati ya Mwaka 2025 na Mwaka 2100. Huu ni wakati wa siasa za Maendeleo na sio siasa za Madaraka.

Makala hii imeandikwa na Humphrey Polepole, Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) mwenye dhamana ya Itikadi na Uenezi

Mbunge Peter Msigwa akamatwa na polisi Mkoani Iringa

$
0
0
Mbunge wa Iringa Mjini Peter Msigwa (Chadema) amekamatwa na polisi leo Jumapili jioni baada ya kushushwa jukwaani kwenye mkutano wa hadhara katika Kata ya Mlandege mkoani Iringa.

Mwenyekiti wa Baraza la Vijana wa Chadema Iringa Mjini (Bavicha), Leonce Marto amesema  kuwa mbunge huyo alikamatwa saa 11:24 jioni na Mkuu wa Upelelezi wa Mkoa (RCO) aliyekuwa ameambatana na polisi wengine kisha wakampeleka ofisi za mkoa za jeshi hilo.

“Kutoka Mlandege mpaka ofisini kwa kamanda wa mkoa amebadilishwa kwenye magari matatu. Tunahisi atakuwa anasafirishwa ingawa bado anahojiwa. Yupo ndani, sisi tunaendelea kumsubiri nje,” amesema Marto.

Mwenyekiti huyo alibainiha  kwamba mpaka wakati huo (saa 12:30 jioni) jeshi hilo halikubainisha sababu za kumshikilia Msigwa.

“Alikuwa na kibali cha kufanya mkutano katika kata tatu kuanzia leo Jumapili mpaka Jumanne. Alianza kuzungumza saa tisa alasiri ilipofika saa 11:24 jioni, RCO akiwa na polisi wengi wakamshusha jukwaani na kuondoka naye,” alisema Marto bila kufafanua sababu za kukamatwa.

Ongeza Hips, Makalio Na Mapaja, Kuwa Mweupe Na Softi...... Ongeza Maumbile Ya Kiume, Nguvu Na Hamu Ya Tendo

$
0
0
Natural beauty product Tunakuletea bidhaa bora zenye matokeo ya uhakika na haraka zisizo na kemikali wala madhara. Zimetengenezwa kwa mimea na matunda na kudhibitishwa kiafya. 
 
             NB. Matokeo ni uhakika na garantii na risiti
🍉🌿🍅🍍🍒🍉🍓🍅🍒
          BIDHAA ZETU:-
  
1.Kurefusha nywele na kuzuia kukatika ovyo @130,000/=
2.Kuongeza shepu (hips, makalio na mapaja) kwa:-
(a)BOTCHO MULT-PLUS 10× @200,000/=
(b)Vidonge  @180,000/=
(c)BOTCHO 10× ya kupaka @170,000/=
3.Kuwa mweupe na softi mwili mzima kwa:-
(1)Mafuta  @130,000/=
(11)Vidonge @150,000/=
4. Kupunguza unene na manyama uzembe @150,000/=
5.Kuongeza uume pamoja na nguvu za kiume kwa:-
(a)SHARK POWER gely ya kupaka (Inaongeza inch 6-7) @150,000/=
(b)Vidonge kwa ajili ya kuongeza nguvu na hamu ya tendo la ndoa hata kwa wenye kisukari @150,000/=
(C)HANDSOME UP ORIGINAL- kifaa cha kuongeza maumbile kwa size uipendayo @250,000/=
6.Kuondoa mvi milele zisiludi tena @150,000/=
7.Kuongeza unene wa mwili mzima na uzito pamoja na hamu ya kula  @130,000/=
8.Kupunguza tumbo (kitambi) na nyama za pembeni kwa:-
(a)Dawa ya kunywa au kupaka @130,000/=
(b)Mkanda wa kawaida @120,000/=
(c)Micro-computer belt wa umeme @200,000/=
9.Kupunguza  maziwa na kuyasimamisha hata kwa walionyonyesha @130,000/=
10.Kushepu miguu (CHUPA YA BIA) na kuondoa vigimbi @130,000/=
11.Kuondoa mipasuko mwilini (michirizi) @120,000/=
12.Kurudisha usichana  (bikra) @120,000/=
        Wasiliana nasi :- (+255)
             0759029968 au.       
                0659618585
 
  TAHADHARI: Hakikisha unapata risiti yenye muhuri halisi wa NATURAL BEAUTY pamoja na garantii ili kukuhakikishia kufanikiwa kwako.
👉🏻Ili kuona bidhaa zaidi na shuhuda za waliotumia bidhaa zetu. ...............
     Follow us on instagram  @natural2162
@natural2162
            
                              [ WELCOME ALL]
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live


Latest Images