Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatatu ya Septemba 25


Joshua Nassari: Nipo Tayari Kujiuzulu Ubunge

0
0
Mbunge wa Chadema wa Arumeru Mashariki, Joshua Nassari ameweka rehani ubunge wake  baada ya Rais John Magufuli kumpokea aliyekuwa diwani wa chama hicho aliyejiuzulu akisema ni kwa sababu ya kuunga mkono juhudi za Rais.

Nassari amedai ana ushahidi wa kielektroniki unaoonyesha madiwani hao walivyopewa rushwa ili wajiuzulu nafasi zao.

Hata hivyo, diwani wa Kata ya Kimandolu, Mchungaji Rayson Ngowi ambaye amepokewa na Rais Magufuli juzi  baada ya kujiuzulu Chadema akizungumzia tuhuma hizo alisema madai hayo hayana ukweli wowote na kama Nassari ana ushahidi ni vyema angeutoa hadharani.

Ngowi aliwashauri Chadema mkoani Arusha watatue matatizo yaliyopo ndani ya chama hicho na wasitafute visingizio kwa kuwa yeye ameamua kujiuzulu kwa kuunga mkono juhudi za Rais Magufuli na hajapewa rushwa yoyote.

Diwani mwingine aliyejiengua katika chama hicho wa Kata ya Muriet, Credo Kifukwe alisema hakuna chochote alichopewa kama rushwa kwa lengo la kujiuzulu, akimshauri Nassari autoe hadharani ushahidi anaousema na si kushusha tuhuma zisizo na mashiko.

Akizungumza na waandishi wa habari jana mjini hapa, Nassari alisema ushahidi huo ameuhifadhi ndani ya ‘flash disc’ na yuko tayari kumkabidhi Rais Magufuli na vyombo vya uchunguzi.

Mbunge huyo alisema endapo ikithibitika kuwa ushahidi wake ni wa uongo yuko tayari kujiuzulu nafasi yake ya ubunge.

“Ninao ushahidi na kama Mheshimiwa Rais yuko tayari niko tayari kumpatia ninayo flash, ushahidi ninao kwa muda mrefu na tulijua watapokelewa juzi madiwani wawili lakini mmoja amekataa akaenda mmoja,” alisema Nassari. 
 
Alidai kwamba  kwa kipindi kirefu alipokuwa masomoni nchini Uingereza alikuwa akijiuliza ni kwa nini madiwani katika Mkoa wa Arusha wamekuwa wakijiuzulu na ndipo alipoamua kufanya uchunguzi wa kina.

Nassari akiwa ameambatana na Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema katika mkutano huo, alisema alianza kufanya uchunguzi Mei kwa kutumia vifaa vya kielektroniki alivyovinunua nchini Uingereza na kubaini kwamba baadhi ya madiwani wanaojiuzulu walipewa rushwa ya fedha, ahadi ya vyeo na ya makazi.

Alisema uchunguzi juu ya tuhuma za madiwani hao kujiuzulu aliufanyia ndani ya ofisi ya umma akisisitiza hakuna diwani wa Chadema mkoani Arusha ambaye amejiuzulu kwa kumuunga mkono Rais Magufuli bali wamepewa rushwa.

“Mheshimiwa Rais anapambana na rushwa lakini kuondoka kwa madiwani ni mfumo wa rushwa anaopambana nao niko tayari kujiuzulu nafasi yangu ya ubunge endapo ikithibitika ushahidi wangu ni wa uongo,” alisema Nassari.

Madiwani wapatao 10 wa Chadema wamejiuzulu kwa nyakati tofauti. Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Humphrey Polepole ameshawahi kunukuliwa akikanusha tuhuma za kupewa rushwa madiwani wanaojiengua kutoka Chadema na kujiunga na CCM.

Polepole Julai alikaririwa akisema iwapo Chadema ina viongozi wanaoweza kuhongwa na wakahongeka basi ni chama cha  ovyo kwa kuwa chama kilicho imara na watu wake wapo safi hawawezi kuhongeka.

Alitoa kauli hiyo mjini Bagamoyo alipohudhuria mahafali ya Shirikisho la Wanafunzi wa Vyuo Vikuu (Tahliso) Mkoa wa Pwani.

Peter Msigwa Kaachiwa kwa Dhamana, Kuripoti kwa RCO Leo

0
0
Mbunge wa Iringa Mjini (Chadema) Msigwa ameachiwa huru jana usiku  kwa dhamana baada ya kukamatwa akiwa kwenye mkutano wa hadhara.

Msigwa aliachiwa baada ya kudhaminiwa na wadhamini wawili Alex Kimbe pamoja na Mwenyekiti wa Bavicha Iringa  Leonce Marto , saa nne usiku .

Msigwa alishushwa  jukwaani kwa nguvu  akiwa anahutubia mkutano wa hadhara katika kata ya Mlandege Manispaa ya Iringa na anatuhumiwa kwa kosa la uchochezi dhidi ya vyombo vya usalama .

Marto  amesema  mikutano yake imefungiwa na hapaswi kuendelea na ziara yake katika kata nyingine  mpaka hapo OCD atakapo amua vinginevyo.

Leo  Mbunge anatakiwa kuripoti kwa RCO na huenda kesi ya uchochezi ambayo tayari imeshafunguliwa jalada lake ikapelekwa mahakamani .

Amesema  Mbunge huyo  atazungumza na vyombo vya habari leo mchana  kuweka wazi madhila yaliyompata wakati akitekeleza wajibu wake kwa wananchi.

Rais Magufuli Kuongoza Vikao vya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa - NEC Kwa Siku Mbili Dar

0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Taifa, anatarajia kuongoza kikao cha  Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) kwa siku mbili Jijini Dar es Salaam, Septemba 30 hadi Oktoba 1, 2017.

Kwa mujibu wa  taarifa iliyotolewa jana  Septemba 24 na Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Humphrey Polepole ameeleza kuwa, Kamati kuu ya Halmashauri ya Taifa (CC)  na Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) vinatarajia kuketi  Jijini Dar e Salaam kwa nyakati tofauti.

Rais Magufuli amemaliza ziara yake ya siku sita katika Mkoa wa Arusha.

0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli tarehe 25 Septemba, 2017 amemaliza ziara yake ya siku 6 katika Mkoa wa Arusha.

Akiwa njiani kuelekea uwanja wa ndege wa kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) Mhe. Rais Magufuli amesimamishwa na wananchi wa Sangsi nje kidogo ya Jiji la Arusha na wananchi wa Pacha ya Kia Mkoani Kilimanjaro na kuwahakikishia kuwa Serikali itaendelea kutatua kero za wananchi na kuwahudumia bila kuwabagua kwa misingi ya itikadi za kisiasa, dini na ukabila.

Mhe. Rais Magufuli amesema katika kutimiza azma hiyo Serikali inatekeleza miradi mikubwa ya maendeleo ikiwemo ujenzi wa barabara ya Usa River  – Arusha inayojengwa kwa gharama ya shilingi Bilioni 139, mradi wa maji wa Arusha utakaogharimu Shilingi Bilioni 42, mradi wa kusambaza umeme katika vijiji zaidi ya 200 na mingine mingi inayotekelezwa katika maeneo hayo.

“Nina uhakika nyinyi wakazi wa Arusha mnaona Arusha inavyobadilika, kabla ya kujengwa barabara hii kulikuwa kunatokea ajali nyingi, na kuna watu walikufa pale kwenye daraja, inawezekana wengine wameanza kusahau, wanaozaliwa sasa hivi wanaweza kuona haya sio chochote lakini hii ni ishara ya kupanda kwa uchumi wetu, uchumi unapopanda na miundominu inakuwa mizuri” amesema Mhe. Rais Magufuli.

Aidha, Mhe. Rais Magufuli amesikiliza kero mbalimbali za wananchi wakiwemo wafanyakazi ambao wamelalamikia kuhamishwa vituo vya kazi bila kulipwa stahiki zao na amerejea agizo lake la kupiga marufuku mfanyakazi yeyote kuhamishwa kituo cha kazi pasipo kulipwa stahiki zake.

Kuhusu kero za wananchi wa pacha ya Kia waliolalamikia tatizo la uhaba wa maji, kunyang’anywa maeneo ya biashara na waliokuwa walinzi wa uwanja wa ndege kudai haki zao Mhe. Rais Magufuli ameziagiza mamlaka husika kushughulikia matatizo hayo.

Mhe. Rais Magufuli amerejea Jijini Dar es Salaam.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Arusha
25 Septemba, 2017

Kwa Nini Wanaume Wengi Wanaupungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo?

0
0
Asilimia 45 ya wanaume wapo tofauti na wengine kwa kuwatimizia vyema wake au wapenzi Wao na kuwasababishia kutoka nje ya ndoa zao.

NINI CHANZO CHA HAYO?Kupiga punyeto,Ngiri,Vidonda vya tumbo,Magonjwa ya moyo,Presha,Kisukari,Korodani moja kuvimba,Msongo wa mwazo,Kufanyiwa tohara ukiwa mtu mzima n.k.DOKTA MANYANDA sasa kapata tiba sahihi ya tatizo la NGUVU ZA KIUME.

MUHAMA:Hii hutibu na kuponyesha kabisa tatizo la nguvu za kiume,utakuwa na uwezo wa kurudia tendo zaidi ya mara tatu bila kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dakika 15-20.DAWA hii imechanganywa miti 12.Hata wazee wenye umri mkubwa wanapona kabisa.OKO NDOA YAKO SASA. 

MANGUNGU MIX: Ndio tiba tosha kwa sasa ambayo hurefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo inch 1-8 na unene sentimita 1-5,dawa hii ipo ya kupaka na kunywa na haina madhara yoyote kwa mtumiaji.

NITOFAUTI NA ULIZO WAHI KUZITUMIA.Pia tuna dawa za kupatanisha mke,mme,mpenzi au bosi wako kwa mda mfupi sana,Uzazi,Kusafisha nyota,

Je unamali yako unauza hupati wateja?Wasiliana nami 0716-263605 

DOKTA MANYANDA ANAPATIKANA KASULU KIGOMA,Kwa wale wa mikoani huduma hii utaipata popote pale.

Ndugai: Tundu Lissu ana Bima ya Bunge, Hapaswi Kutibiwa kwa Michango

0
0
Spika wa Bunge la Tanzania, Job Ndugai amefunguka na kudai matibabu ya Mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lissu hayawezi kufanyika kwa kuchangishana michango kwa kuwa ana bima yake na haki zake ndani ya Bunge.

Spika Ndugai amebainisha hayo leo asubuhi wakati akizungumza kwenye kipindi cha East Africa Breakfast kutoka East Africa Radio baada ya kuulizwa swali kwamba kuna utaratibu gani endapo mbunge akiumia ama akiumwa akiwa kazini.

"Utaratibu ni kwamba wabunge wote wana bima pamoja na mimi mwenyewe, Mawaziri wote wana bima ndani ya bunge kwa sababu ni wabunge kwanza kabla ya kuwa Mawaziri. Kwa hiyo bima zao ndiyo zinazowahudumia na tunahudumiwa kupitia hospitali zote za serikali, tunalazwa kama watanzania wengine wowote wale. Ikitokea yanahitajika matibabu ya nje ya nchi, yatatoka mapendekezo katika hospitali ya Muhimbili kwamba matibabu ya huyo mtu  yanapaswa yakafanyikie nje ya nchi kutokana na upungufu wa jambo fulani hapa nchini", amesema Spika Ndugai.

Pamoja na hayo, Spika Ndugai aliendelea kwa kusema "Tukirudi kwa Mhe. Lissu ni kwamba tulikuwa wote hapa Dodoma, baada ya kuombwa na familia pamoja na Mhe. Mbowe kwamba ni vyema apelekwe kutibiwa katika hospitali ya Nairobi nchini Kenya tulikubaliana kwa pamoja kuwa ni vizuri aende huko. Lakini alienda huko kama vile ni hospitali binafsi ambayo ipo nje kidogo ya mkondo wetu wa kawaida. Kwa hiyo bado bima yake ipo hapa bungeni na utaratibu wa kumtibu upo".

Aidha, Spika Ndugai amesema bunge kwa ujumla haliwezi kumtupa Mhe. Lissu hata kidogo kuhusiana na masuala ya matibabu yake.

"Sisi kama bunge hatujamtupa mwenzetu na bahati nzuri serikali imetoa tamko lake kuwa halijamtupa, ni suala la kuwekana sawa tu badala ya matamko kwenye vyombo vya habari, magazeti ambayo yamekuwa yakipotosha tu na kuleta malumbano ambayo hayana sababu. Kwa hiyo wito wangu kwa wahusika wote ikiwa ni pamoja na familia ya Lissu, CHADEMA, uongozi wa bunge na serikali endapo tukikaa pamoja hakuna ambacho kitashindwa kuzungumzika, hatuwezi kumtibu mwenzetu kwa michango ya kuchangishana wakati ana bima yake na haki zake", amesisitiza Spika Ndugai.

Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH....Anatoa Pete za Bahati, Anasafisha Nyota, Anazuia Chuma Ulete na Mengine

0
0
Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH CHIEF SULTAN MAKATA Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika
Anatibu kwa Njia ya Simu Ukiwa Nchi Yoyote / Mkoa wowote
 
..JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na Chief Sultan Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO NDANI YA SAA 12 TU(LIMBWATA). Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine?Una Mpenzi wako ana Pesa na Unataka kumkamata? Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao Endapo utafata Atakacho kuelekeza.
 
Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.
Chief Sultan Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..
 
Anatibu kwa Kutumia Vitabu vya QUR-AN Dawa za Asili za Africa,Dawa za Kiarabu na Majini.Anatafsiri Ndoto. Kushinda BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA,Hutoa PETE ZA BAHATI inayoendana na NYOTA YAKO. Mvuto wa Mwili na BIASHARA, Kinga ya Mwili,ZINDIKO za Nyumba.HUZUIA CHUMA ULETE NA KUKUPA DAWA YA KUONGEZA FAIDA KWENYE BIASHARA. HURUDISHA MALI ZILIZOPOTEA AU KUDHULUMIWA.MIGUU Kufa GANZI.Kufungua KIZAZI kwa wale walio fungwa kwa njia za KISHIRIKINA. 

Anakupa Jini la Mali kwa yule anaehitaji Utajiri BILA MASHARTI.Humaliza Kabisa Tatizo la Nguvu za KIUME na Kurefusha Uume kwa Saizi Unayotaka,HUMALIZA KESI YA AINA YOYOTE NDANI YA SIKU 14. na mengi zaidi

Whatsapp/Calls 0658316976
0755911233
 
Tiba ni kwa Watu wenye Imani na Dini zote

Waziri wa Afya Aipiga Marufuku Muhimbili kutoa rufaa za nje hata kwa Rais Maguful

0
0
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu ametoa agizo kwa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) kuhakikisha haitoi rufaa ya matibabu nje ya nchi ikiwa wana uwezo wa kutibu maradhi husika hapa nchini.

Ummy amesisitiza wataalamu kutowaogopa wanasiasa ikiwa wana uwezo wa kumtibu mgonjwa hapa nchini haina ulazima wa kumwandikia rufaa nje ya nchi hata akiwa ni Rais John Magufuli.

Ametoa agizo hilo leo Jumatatu wakati akipokea msaada wa vifaa vipya kwa ajili ya vyumba viwili vya upasuaji vya watoto wadogo na wodi ya watoto ya upasuaji vyenye thamani ya Dola za Marekani 675,000 sawa na Sh1.5 bilioni,  kutoka kwa wataalamu na wahisani kutoka nchini Uingereza kupitia taasisi ya Archie Wood Foundation.

"Rais aliponiteua aliniagiza kwamba lazima niachane na rufaa za nje, hatuwezi kuachana nazo ikiwa magonjwa yanayoweza kutibiwa ndani yatatibiwa nje," amesema Ummy.

Amesema Watanzania wana imani na  Muhimbili  na hivi sasa wengi wanatoka hospitali za kulipia na kufuata matibabu ila changamoto iliyopo ni majengo lakini wapo mbioni kujenga jengo la ghorofa kwa ajili ya wagonjwa wa kulipia.

"Msitoe rufaa ya mgonjwa kama hamjajiridhisha kwamba mnaweza kumtibu hapa hata kama awe Rais, waziri au nani msitoe rufaa kwani maana yake mtakuwa mmeshindwa ni lazima ninyi mseme kwamba hamuwezi na sisi tutashughulikia," amesema.

Amewatahadharisha wataalamu hao na wanasiasa kwamba lazima wahakikishe kweli hawawezi kutibu na kwamba wizara ipo tayari na itawaunga mkono.

Msigwa Kulihitaki Jehi la Polisi

0
0
Mbunge wa Iringa Mjini(Chadema), Mchungaji Peter Msigwa amesema atalishitaki Jeshi la Polisi, kwa tuhuma za kuingilia majukumu yake ya kikazi pale anapokuwa akitimiza wajibu wake wa kibunge ikiwemo kuongea na wananchi.

Mchungaji Msigwa amesema atakata rufaa kwa sababu polisi wamezuia mikutano yake ya leo na kesho ambayo alitarajia kufanya katika kata za Kihesa na Kitwiru kwa madai ya kukiuka masharti alipohutubia katika Kata ya Mlandege.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Jumatatu, Mchungaji Msigwa amesema chombo pekee kinachoweza kumtia hatiani kwa kufanya uchochezi ni Mahakama na sio polisi.

“Jana walinikamata tangu saa 11:30 na kuanza kunihoji mpaka  saa 3:15 usiku kwa tuhuma za kufanya uchochezi lakini mimi nakataa sijafanya uchochezi kwa sababau hakuna mtu anaweza kunizuia kuongea na wananchi wangu, wanadai nimeleta hofu na kuvichonganisha vyombo vya dola na wananchi,” amesema Mchungaji Msigwa .

Amesema mpaka muda huu yupo nje kwa dhamana na tayari ameripoti polisi asubuhi leo Jumatatu amehojiwa lakini ameambiwa ataitwa tena kwa mahojiano zaidi.

“Mimi niko tayari hata kama wangeniweka ndani wiki mbili siogopi kwa sababu sitanyamaza nitaendelea kuongea na sitaacha kusema kilichomtokea Tundu Lissu na ili kuninyamazisha ni lazima waniue kwa sababu nishajiandaa kisaikolojia,” amesema Mchungaji Msingwa.

Akizungumzia hilo Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa, Julius Mjengi amesema walimkamata Msigwa kwa kuwa alikuwa anatoa maneno ya uchochezi kwa wananchi aliokuwa anawahutubia mkutano wa hadhara Kata ya Mlandege.

Mgengi amesema bado jeshi hilo linaendela na upelelezi juu ya tuhuma hizo na mara utakapokamilika watamfikisha mahakamani mbunge Msigwa.

Mwakyembe apiga marufuku tuzo za muziki na mashindano ya Miss Tanzania

0
0
Waziri wa Utamaduni Sanaa na Michezo Harrison Mwakyembe amepiga marufuku mashindano ya Miss Tanzania na tuzo za muziki kutokana na ubabaishaji wa waandaaji wa mashindano ya tasnia hizo.

Mwakyembe amesema mashindano ya Miss Tanzania yamegubikwa na ubabaishaji kwenye utoaji wa tuzo na kumekuwa na tabia ya kuchelewa kuwapa washindi zawadi wanazoahidiwa jambo linaloleta usumbufu.

Waziri huyo ameongeza kuwa watakaotaka kuandaa mashindano hayo ni lazima zawadi wanazoahidi kuwapa washindi zipekwe ofisini kwake.

”Kwa sasa tunanakaa chini na wadau wa burudani juu ya mashindano hayo ila tunataka tuzo ziwe na (guaranteed sustainability) muendelezo wa uhakika na sio kufanyika kwa kubahatisha”, alisema Mwakyembe.

Kwa mara ya mwisho mashindano ya za Miss Tanzania yalifanyika mwaka 2016 ambapo ilichukua takribani miezi 6 kwa Kamati ya shindano la Urembo la Miss Tanzania kumpatia mshindi zawadi yake.

Kwenye tuzo za muziki waziri Mwakyembe amesema tuzo hizo zinahitaji marekebisho kwani zilikuwa zikitegemea watu wachache kiasi kwamba wakinuna basi hakuna tuzo.

Makamu Wa Rais Afungua Mkutano Wa Siku 5 Wa Majaji Na Mahakimu Wa Nchi Za Jumuiya Ya Madola

0
0
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan leo amefungua mkutano wa  Majaji  na Mahakimu wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Madola akimwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa John Pombe Magufuli. Mkutano huo umefanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Benki Kuu ya Tanzania, Dar es Salaam.

Katika uzinduzi huo, Makamu wa Rais alipongeza mafanikio makubwa yaliyofikiwa na Chama cha Majaji na Mahakimu wa nchi wananchama wa Jumuiya ya Madola (CMJA). 

Makamu wa Rais alisema” jitihada zenu katika kuendeleza na kuimarisha viwango na uhuru wa mahakama na vilevile kuendeleza utawala wa sheria vimeendelea kuimarika na kuifanya jumuiya yenu kuwa imara zaidi”.

Kwa miaka mingi mmeendelea kuchochea na kuimarisha uhuru wa mahakama huku mkijitahidi kuendeleza utawala wa sheria katika nchi za jumuiya ya madola, alisema Makamu wa Rais.

Aidha, mkutano huo uliohudhuriwa na Majaji Wakuu wa Mahakama, majaji na mahakimu, Makamu wa Rais aliuasa mhimili wa Mahakama kuunga mkono jitihada za serikali katika mapambano ya kuondoa umaskini na rushwa ili kufikia maendeleo ya kweli. 

“Naamini kwamba nia ya kujenga mahakama yenye ufanisi, uwajibikaji na jumuishi haitafikiwa kama mahakama ya Tanzania itajitenga na jitihada za serikali za kuondoa umaskini na rushwa”, alisisitiza Makamu wa Rais.

Pia Makamu wa Rais alisisitiza kuwa rushwa huondoa uhuru wa mahakama na hivyo kupoteza utawala wa sheria.  Aliwataka washiriki wa mkutano huo kupambana na rushwa katika mahakama ili kuhakikisha haki na maendeleo vinapatikana.

Mwisho Makamu wa Rais aliwahakikishia washiriki wa mkutano huo kwamba serikali ya Tanzania itaendelea kuheshimu na kuimarisha uhuru wa Mahakama kwa  kuhakikisha inaendelea kupambana na kuondoa vitendo vya rushwa.  
 
Imetolewa na :-
Ofisi ya Makamu wa Rais

Jaji Mkuu wa Tanzania Ampongeza Jaji Mkuu wa Kenya Kwa Ujasiri wake wa Kulinda Uhuru wa Mahakama

0
0
Jaji Mkuu wa Kenya, David Maraga ametua nchini katika mkutano wa majaji na mahakimu akionekana kivutio kwa wengine.

Jaji huyo ni mmoja wa majaji wakuu 13 kutoka nchi mbalimbali duniani wanaohudhuria mkutano majaji na mahakimu wa nchi za Jumuiya ya Madola unaofanyika jijini Dar es Salaam kwa siku tatu..

Maraga amegeuka kivutio baada ya kushangiliwa na majaji waliohudhuria mkutano huo wakati alipotambulishwa na Jaji Mkuu wa Tanzania, Profesa Ibrahim Juma.

Profesa Juma amempongeza Maraga kwa kuwakilisha mfano bora wa kulinda uhuru wa Mahakama kwa nchi nyingine duniani.

Kiongozi huyo ameonekana akiwa ameambatana na walinzi wanne ambao wanamfuata popote anapotembea nje ya mkutano huo.

Hata hivyo, Maraga amekataa kuzungumza na vyombo vya habari kwa madai amekuja kuhudhuria mkutano huo na siyo kwa jambo jingine lolote.

Mkutano huo umefunguliwa leo Jumatatu na Makamu wa Rais, Samia Suluhu ukiwa na kauli mbiu "Kujenga Mahakama Shirikishi, Thabiti na Inayowajibika."

Jaji Maraga kwa siku za hivi karibuni amekuwa maarufu baada ya kutoa uamuzi wa kufuta Uchaguzi Mkuu wa Kenya uliokuwa umempa ushindi Rais Uhuru Kenyatta.

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Gazi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

0
0
Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Tupo Mbagala

Pata Tiba ya Tiba ya Tatizo la Nguvu Za Kiume........Inasaidia Kukufanya Urudie Mara 5 na kuchelewa kwa Dakika 20

0
0
TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO LINATIBIKA.Baada ya utafiti wa mda mrefu juu ya matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume na ukosaji wa hamu ya tendo la ndoa ama kushindwa kurudia tendo kwa haraka DR Magise imekuletea tiba ya matatizo hayo kwa kutumia dawa za: 
 
FUUl POWER:Ni dawa asili ya vidonge inayotibu tatizo la upungufu au ukosefu wa nguvu za kiume,dawa hii inamchanganyiko wakutosha wenyekuzalisha vichocheo vingi vya Hemone za Gestrogen vikiwemo vitamin B6&B1,vitamini E,pamoja na madini aina ya zinc vitakufanya kuwa na nguvu na mzunguko mzuri wa damu na kuongeza hamu na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya hatua nne au zaidi,na kuchelewa kufika kileleni zaidi dakka 20-30.
 
NYAMVA:Inarutubisha maumbile ya uume yani kurefusha na kunenepesha nchi 4-7 upana cm3-4 standard kiafya haijalishi umri wako hata kwa wazee ukiitumia maumbile yako yatabaki kuwa hivyo siku zote,Pia tunatibu Presha,kisukari siku7,ngiri,chango la tumbo tumbo kujaa gesi,kutopata choo vizuri

 TUPO TZ DAR ES SALAAM   MBAGALA RANGI TATU.HUDUMA HII UTALETEWA POPOTE ULIPO .WASILIANA NAMI 0783741788,0715741788 -DR MAGISE

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumanne ya Septemba 26

Daktari Atoa Uhahidi Mahakamani, Kadai Manji Yupo Hatarini na Anaweza Kufa Muda Wowote

0
0
Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Moyo kutoka Hospitali ya Aga Khan, Mustapha Bapumia (62) ameieleza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuwa anashangaa mtu mwenye umri mdogo kama Yusuf Manji (41) kuwa na vyuma vinne kwenye moyo.

Alieleza kuwa na vyuma vinne kwenye moyo ni hatari na kwamba anatembea katika kamba nyembamba.

“Kitaaluma huyu ni lazima ajiangalie sana yupo katika hatari anaweza kupoteza maisha muda wowote.”

Dk Bapumia ambaye ni shahidi wa tatu wa upande wa utetezi alimeeleza hayo jana Jumatatu mbele ya Hakimu Mfawidhi, Cyprian Mkeha wakati akitoa ushahidi katika kesi inayomkabili Manji ya kutumia dawa za kulevya aina ya Heroine.

Akiongozwa na Wakili Hajra Mungula kutoa ushahidi, Dk Bapumia alisema yeye kwa siku huwa anawaona wagonjwa 50 hadi 60 na kwamba Februari 21, 2017 ilikuwa ni mara ya kwanza Manji kupelekwa kwao akiwa na maumivu ya moyo.

Ameeleza kuwa wana utaratibu wa wagonjwa tete kuwapeleka katika kitengo cha dharura  na kwamba Manji walimpokea, wakamlaza, wakamchunguza na kuona ana tatizo sugu la moyo pamoja na kuwa na umri mdogo.

"Nikatafuatilia historia na kubaini licha ya kuzibuliwa kwa  mishipa yake mitatu India, Dubai na Marekani,  ilikuwa bado haijaziba lakini alikuwa bado anapata maumivu ya moyo," ameeleza shahidi huyo.

Ameeleza kuwa walimfanyia vipimo na vilionyesha tatizo lipo na kuna sehemu ya nne inahitaji kuzibuliwa na kwamba mgonjwa alikuwa wazi kuwa anatumia sigara na pombe.

Kutokana na hali hiyo ameeleza walimshauri mgonjwa ili waweze kuzibuliwa lakini akawaambia waache na akaomba dawa kwa kuwa familia yake ipo Marekani na matibabu yake mengi yanafanyika huko.

Shahidi huyo alieleza kuwa wao kama hospitali hawezi kufanya chochote bila ridhaa ya mgonjwa hivyo wakampatia dawa na akaruhusiwa Februari 24, 2017.

Alieleza kuwa siku hiyo hiyo alirejeshwa tena hospitalini hapo nyakati za saa mbili usiku akisumbuliwa na maumivu kwenye moyo, wakamlaza mpaka tarehe Machi 14, 2017 ambapo aliruhusiwa.

“Katika kipindi hicho Manji aliridhia na kuzibuliwa vyuma kwenye moyo.”

Ameeleza kuwa walimpatia dawa ikiwamo za  kupunguza kolestro (mafuta) kupunguza maumivu sugu ya mgongo pamoja na  kupunguza hofu ambazo zimo ndani ya Morphine na Benzodiazepines.

Kwa upande wake Manji akijitetea aliiomba Mahakama imuachie huru.

Akitoa ushahidi wake alieleza kuwa yeye ana matatizo ya moyo ya kurithi kutoka kwa babu zake ambao walikwishafariki kwa ugonjwa huo.

Ameeleza kuwa ugonjwa wa moyo ulimuanza akiwa na umri wa miaka 26 na kwamba mara nyingi amekuwa akitibiwa nje ya nchi ikiwamo India na Marekani na ana vyuma vitano kwenye moyo.

Akitoa ushahidi mahakamani hapo, Manji ameeleza kuwa kila baada ya miaka miwili anavibadilisha na kufanya uchunguzi vinafanya kazi vipi.

Akiongozwa na wakili wake, Hajra Mungula, Manji ameeleza kuwa katika ripoti zake za kati ya 2009 na 2016 haijawahi kutokea akaonekana kama anatumia dawa za kulevya.

Manji akiendelea kujitetea ameeleza kuwa anatumia vidonge 30 hadi 35 kwa siku.

Manji ameeleza kuwa polisi walikuwa wastaarabu wanampatia dawa na kwa upande wa  Magereza  vidonge vilikuwa katika kabati wanampatia.

Manji ameeleza kuwa Februari 8, 2017 alipata taarifa ya kutuhumiwa utumiaji wa dawa za kulevya na kuripoti kwa Mkuu wa Upelelezi wa Kanda Maalum (ZCO).

Baada ya kuipata taarifa hiyo ameeleza aliitisha mkutano na waandishi wa habari  kukanusha taarifa hiyo na Februari 9, 2017 alikwenda polisi kwa sababu anaheshimu jamuhuri na alitaka kazi ifanyike kwa haraka.

Ameeleza alivyokwenda alichukuliwa na kupelekwa kwa Mkemia Mkuu wa Serikali ambapo alikutana na Gwajima(Askofu Josephat) na akatoa sampuli ya mkojo.

Ameeleza kuwa baada ya hapo walikwenda kukagua nyumbani kwake walichukua kompyuta, credit card na visa card.

Amesema kuwa anashangaa kwanini walichukua hivyo vitu wakati havihusiani na kesi ya dawa za kulevya na kuliacha sanduku lililokuwa na sindano na vifaa tiba.

Aliongeza kuwa inajulikana kuwa kuna ugomvi wa kibiashara ambapo wanagombea kampuni ya Tigo na kwamba hiyo kesi ni propaganda na ni mchezo mchafu.

Amesema hiyo kesi imemuathiri yeye binafsi na baba yake alimuachia vitu viwili jina zuri na maadili kwa jamii.

Pia imemuaribia jina kwa jamii yake, msikitini anashindwa kwenda kusali, biashara pia na imeumiza watoto na imemfanya aachie Uenyekiti wa Klabu ya Yanga.

Amesema kuwa kutokana na kesi hiyo anaona aibu kukaa na viongozi ambao anafahamiana nao akiwamo Raila Odinga na rais mstaafu Benjamin Mkapa

Kesi hiyo imeahirishwa hadi leo itakapoendelea kwa ushahidi wa upande wa utetezi.

Awali Manji alidai kuwa yeye ni mshauri wa kampuni za familia na kwamba alikataa tuhuma za dawa za kulevya ili mahakama imsikilize na kutenda haki na kwamba dawa aina ya Morphine na Benzodiazepines ni sehemu ya dawa zake ambazo anatumia.

Mume Ajinyonga Baada ya Kumpiga hadi Kumuua Mkewe Akimtuhumu Kuchepuka Nje ya Ndoa

0
0
Mkazi wa Misungwi, Kwilokeja Boniface (35) amemuua mkewe Shija Luchagula (30), kwa kumnyonga kisha na yeye kujinyonga kwa kile kinachodaiwa wivu wa mapenzi.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Ahmed Msangi alisema jana  Jumatatu kuwa tukio hilo lilitokea jana katika kijiji cha Mwiligiligili wilayani Misungwi.

Alisema mwanaume alitoka shambani akakuta tairi nyingi za baiskeli kwenye uwanja wa nyumba yake ndipo ukazuka ugomvi baina yao akimtuhumu mkewe kutokuwa mwaminifu kwenye ndoa yao hivyo alianza kumpiga kwa fimbo kisha kumnyonga mpaka akafariki dunia.

Alisema baada ya kufanya hivyo na yeye alichukua jukumu la kujinyonga kwa kamba ili kukwepa mkono wa sheria.

“Kwa sasa polisi wanaendelea na uchunguzi kuhusiana na vifo hivyo na miili ya marehemu tayari imefanyiwa uchunguzi na kukabidhiwa kwa ndugu wa marehemu kwa ajili ya mazishi"

Mtoto wa Siku Moja Atupwa Chooni Jijini Mwanza......Polisi, Wananchi Wafanikiwa Kumukoa Akiwa Hai

0
0
Mtoto mchanga wa kike anayekadiliwa kuwa na umri wa siku moja ameokotwa kwenye shimo la choo kinachotumika katika mtaa wa Lumala Kata ya Kawekamo Wilayani Ilemela mkoani Mwanza akiwa hai baada ya kutupwa na mzazi wake.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Ahmed Msangi amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema baada ya muda mchache kupita toka kichanga hicho kutupwa kwenye shimo hilo la choo,  polisi walipata taarifa na kwenda kusaidia kumtoa mtoto huyo ambaye sasa amepelekwa hospitali ya Sekou Toure kwa matibabu zaidi.

"Inadaiwa kuwa baada ya muda mchache kupita toka mtoto alipotupwa, palikuwa na mtu aliyekwenda kujisaidia chooni ndipo akiwa chooni alisikia sauti ya mtoto mchanga akilia toka ndani ya shimo la choo. Inasemekana kuwa baada ya mtu huyo kusikia sauti hiyo ya mtoto akilia, alikwenda kutoa taarifa kwenye uongozi wa serikali za mtaa ambapo uongozi wa mtaa ulifika mahali hapo kisha ulitoa taarifa kituo cha polisi" alisema Msangi  na  kuongeza;

"Askari baada ya kupokea taarifa hiyo walifanya ufuatiliaji wa haraka hadi eneo la tukio na kushirikiana na wananchi waliokuwepo eneo hilo na kufanikiwa kutoa kichanga hicho cha mtoto toka ndani ya shimo la choo kikiwa hai. mtoto amepelewa hospitali ya mkoa ya sekou toure kupatiwa matibabu na hali yake inaendelea vizuri. Polisi wapo katika upelelezi na msako katika maeneo mbalimbali ya mkoa wa Mwanza, ili kuweza kubaini mzazi/wazazi wa mtoto huyo ambao wamefanya ukatili huo dhidi ya mtoto, ili baadae waweze kufikishwa kwenye vyombo vya sheria ili hatua stahiki za kisheria ziweze kuchukuliwa dhidi yao na iwe fundisho kwa wengine".

Kamanda Msangi ametoa wito kwa wazazi na walezi kuacha tabia ya kutenda ukatili dhidi ya watoto ikiwepo vitendo vya kutupa watoto kwani ni kosa la jinai na endapo mtu atabainika kufanya hivyo hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yake

UVCCM Wavurugana Jijini Mbeya

0
0
Wanachama wa Umoja wa Vijana (UVCCM) Mbeya mjini, wametishia kutotoa ushirikiano kwa Mwenyekiti mpya wa UVCCM, Stephano Halinga, aliyeshinda uchaguzi mwishoni mwa wiki kwa madai kuwa mchakato wa kumpata Mwenyekiti huyo ulikuwa na shinikizo.

Wakizungumza mara baada ya uchaguzi huo, baadhi ya wanachama hao ambao hawakuwa tayari kutaja majina yao walizielekeza lawama zao kwa Katibu wa UVCCM, Gerald Kinawiro na Katibu wa CCM Mbeya Mjini, Gerald Mwadallu kuwa walihusika na uteuzi wa Mwenyekiti mpya.

Akijibu tuhuma hizo Katibu wa UVCCM, Mbeya Mjini ambaye pia ni Mkurugenzi wa uchaguzi, Gerald Kinawiro, amedai kuwa, mchakato wa kuwapata wagombea unafanywa kwa kuzingatia kanuni na taratibu za chama, hivyo hujuma hizo hazina ukweli wowote na kama kuna mwanachama yeyote mwenye malalamiko afike kwenye ofisi za chama.

Katika kiny’ang’anyiro cha kumpata Mwenyekiti wa UVCCM Mbeya mjini Stephano Halinga alipata kura 178, Farida Ngoyi kura 61 na Omari Omari kura 60.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images