Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Jeshi la Polisi Makao Makuu na TCRA Wazungumzia Makosa ya Mtandaoni na Hatua Ambazo Mwananchi Anatakiwa Kuchukua

$
0
0

Msemaji wa Jeshi la Polisi nchini Kamishina Msaidizi wa Polisi (ACP) Barnabas Mwakalukwa amewataka wananchi kwa ujumla wanaofanyiwa vitendo vya uhalifu mitandaoni wasiende TCRA bali wanapaswa kutoa taarifa katika jeshi la polisi.

ACP Mwakalukwa amebainisha hayo wakati alipokuwa anazungumza katika mkutano wa pamoja na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kuhusu suala zima la uhalifu wa makosa ya mitandao ambapo kwa sasa limeshika kasi kubwa

"Chochote kinachofanyika ambacho ni kosa jinai nawaomba msiende Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), kwa watoa huduma wa mitandao ya simu mbalimbali wala katika vyombo vya kutolea habari bali unapaswa uje katika kituo cha polisi utoe taarifa zako kama ni kosa la jinai kwa sababu mkienda huko uchunguzi utakuwa shida kwa maana wewe mwenyewe utaweza kusababisha hata yule aliyekutendea uhalifu atoroke", amesema ACP Mwakalukwa na kuongeza;

"Kutokana na kukua kwa teknolojia vitu vingi vimekuwa vikifanyika 'online' kwa hiyo hii mitandao ya kijamii imeonekana ni muhimu sana kwenye maendeleo, lakini pia imebadilisha mbinu ya kufanya uhalifu katika mitandao ya kijamii kwa kutumiwa na baadhi ya watu kutapeli, hata kutishia kuua, hivyo jeshi la polisi limejipanga kwa ajili ya kushughulikia makosa ambayo yanatokana na mtandao", amesema Mwakalukwa.

Kwa upande wake,Kaimu Mkurugenzi wa TCRA, Thadayo Ringo amesema analishukuru jeshi la polisi kwa kuweza kuwasaidia katika kuwatatulia changamoto mbalimbali hasa za kiusalama huku akiwataka wananchi watakaopata matatizo katika mtandao kwenda kutoa taarifa polisi ili waweze kuwasaidia kabla ya kufika kwao.

Spika Ndugai Awatahadharisha wabunge kuhusu Usalama Wao na Kutokaa Baa Muda Mrefu

$
0
0
Spika Ndugai leo amewausia wabunge wanzake kuwa makini na usalama wao kwa kuchukua hatua zaidi za kujilinda, ikiwemo kutokaa baa mpaka usiku wa manane ili kujiepusha na matatizo mbali mbali yatakayoathiri usalama wao. .

Akizungumza muda mfupi leo Ijumaa kabla ya kuahirishwa kwa Bunge, Ndugai aliwataka wabunge kutokaa sana katika mabaa.

“Yaani tuchukue hatua tu katika maisha yetu kama mnavyosikia matukio ni mengi katika nchi yetu. Ni vizuri usalama unaanza na wewe mwenyewe kwanza,”amesema.

Amesema vyombo vya usalama vinavyowalinda vinakuwa vinaongezea kidogo na kuwataka kutazama nyendo zao za namna ambavyo wanaishi.

“Kwa wale tuliozoea sana saa 7 ndio tunarudi nyumbani  basi tuanze kurudi mapema kidogo. Lakini pia tuangalie usalama wa familia zetu na tuwaambie wapigakura naona siku hizi watoto wanapotea, watoto wanauawa,”amesema.

Amewataka wabunge kuwapelekea huo ujumbe kuwa wawe makini na watoto wao wakati wa kwenda shule na maeneo mengine kwa kuhakikisha wanajua mtu anayewapeleka shule na kuwachukua.

“Hayo mambo yanayofanana na hayo. Ushauri ni wa ujumla tu,”amesema.

Aliwataka wabunge kuendelea kumuombea Tundu Lissu na wale watakaopata nafasi ya kwenda kumuona jijini Nairobi wampelekee ujumbe.

Amesema pia wabunge wawaombee wenzao ambao wamekwenda kumuuguza mbunge huyo lakini wanatukana kwa sababu hawajui watendalo.

Ushauri huo umekuja siku chache baada ya Lissu kujeruhiwa kwa kupigwa risasi nyumbani kwake Area D mjini Dodoma.

Waziri Mkuu Atuma Ujumbe kwa 'Watu Wasiojulukana; Wanaofanya Matukio ya Kihalifu Nchini

$
0
0

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema serikali haitafumbia macho matukio ya mashambulizi wanayofanyiwa watu mbalimbali wakiwepo viongozi na kuwataka wabunge na wananchi kuendelea kuwa wavumilivu wakati jeshi la polisi likiendelea kufanya uchunguzi.

Waziri Majaliwa amesema hayo wakati akiahirisha vikao vya mkutano wa nane wa bunge la 11, na kusema vyombo vya dola vinaendelea kufanya uchunguzi ili kuwabaini watu wasiojulikana wanaojihusisha na vitendo hivyo  ili sheria iweze kuchukua mkondo wake.

"Serikali haitofumbia macho matukio ya kihalifu yanayotokea nchini, vyombo vya dola tayari vimeshaagizwa kuhakikisha wanawatafuta wanaohusika na vitendo vya kihalifu na kukamatwa ili hatua za kisheria zichukuliwe dhidi yao", amesema Waziri Majaliwa.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Kamati ya kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje Ulinzi na Usalama Mhe. Adad Rajabu ameliomba bunge kuongeza muda ili kuweza kukamilisha kazi ya kufanya uchunguzi wa matukio ya kujeruhiwa, kuvamiwa pamoja na kufuatiliwa kwa baadhi ya wabunge ili kuweza kukamilisha kazi hiyo.

Aidha Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amehairisha vikao vya bunge leo hadi  Septemba 7 mwaka huu ambapo litafunguliwa tena.

Jeshi la Polisi Lapiga Marufuku Maombi ya Kumuombea Tundu Lissu Yaliyotangazwa na CHADEMA

$
0
0
Kamishna Kanda maalumu ya Dar es salaam, Lazaro Mambo Sasa amepiga marufuku maandamano na maombi yanayotaka kufanywa na CHADEMA siku ya Jumapili kumuombea Tundu Lissu kwenye uwanja wa TP Sinza Dar es Salaam na kusema hiyo siyo sehemu ya maombezi.

Lazaro Mambo Sasa amesema hayo leo wakati akifanya mahojiano na waandishi wa habari na kusema kuwa hawezi kuruhusu mkusanyiko wa watu na kuwataka watu ambao wanataka kumuombea Tundu Lissu kwenda kwenye nyumba za ibada na kumuombea lakini si kufanya mkusanyiko huo ambao wao CHADEMA wanataka kufanya.

"Hatutaruhusu mkusanyiko wowote usio na kibali, yapo maeneo ambayo kimsingi yanaendesha maombi hayo, yapo makanisa ipo misikiti na mahali pengine ambako pengine ni rasmi kwa shughuli hiyo.

"Kupitia kwenu nasema hakutakuwa na kusanyiko hilo, yapo maneno ambayo yanaendelea kutolewa kupitia taarifa zao walizotoa ambayo maneno hayo kimsingi kila anayesikiliza anajua nia yao ni nini. 

"Na sisi tukishaona kuna viashiria vya uvunjifu wa amani hatuwezi kuhurusu mkusanyiko wa watu kwa hiyo mkusanyiko wa maombi hayo ni marufuku, tunaruhusu mwenye uwezo hata wa kukesha kanisani aende kwani ni mahali rasmi kwa maombi" alisisitiza Mambo Sasa

Aidha Kamanda Mambo Sasa ametolea ufafanuzi juu ya wanachama wa CUF ambao waliomba kufanya maandamano siku ya Jumapili Septemba 17, 2017 kwa ajili ya kuwapokea baadhi ya wabunge saba wa chama hicho ambao wameapishwa siku ya karibuni bungeni na kusema jambo hilo haliwezekani na yoyote ambaye atakiuka maagizo hayo basi ataishia mikononi mwa polisi.

"Sambamba na hilo naomba niseme kwa wale wanachama wa CUF ambao wameomba tarehe 17 kuwapokea wabunge wa CUF wanaotoka kuapishwa Dodoma walikuwa wameomba kufanya maandamano waanzie Kimara kuelekea Buguruni tumeshatoa maelekezo kuhusu hilo kuwa maandamano hayaruhusiwi na yoyote atakaye jaribu kufanya maandamano ataishia mikononi mwa polisi" alisema Kamanda Mambo Sasa

Baraza la Vijana CHADEMA (BAVICHA) leo asubuhi lilitoa taarifa kwa umma kuwa siku ya Jumapili litafanya maombezi ya kitaifa kwenye uwanja wa TP uliopo Sinza Darajani kumuombea Mbuge Tundu Lissu ambaye alishambuliwa na risasi na watu wasiojulikana ili aweze kupona kwa haraka na kurudi kuendelea na shughuli zake, jambo ambalo limepigwa na jeshi la polisi.

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Gazi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0
Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Tupo Mbagala

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumamosi ya Septemba 16

Waziri Mkuu Awaasa Watendaji Wa Taasisi Zinazosimamia Mazao Ya Biashara

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewataka viongozi wa taasisi zilizopewa dhamana ya kusimamia mazao makuu matano ya biashara ambayo ni ya pamba, tumbaku, korosho, chai na kahawa kutekeleza majukumu yao ipasavyo.

Amesema mazao hayo ni muhimu sana katika kuwezesha mkakati wa Serikali ya Awamu ya Tano wa kufikia uchumi wa viwanda kwani ndiyo mhimili wa kutoa malighafi za kuendesha viwanda husika na yana mnyororo mpana wa uzalishaji ambao una fursa ya kutoa ajira nyingi.  

Waziri Mkuu ametoa kauli hiyo jana (Ijumaa, Septemba 15, 2017) Bungeni mjini Dodoma alipowasilisha hotuba yake ya kuahirisha Mkutano wa Nane wa Bunge. Amesema Serikali imejipanga kuimarisha usimamizi katika uzalishaji na uuzaji wa mazao hayo.

Alisema Serikali itahakikisha kuwa kila taasisi iliyopewa dhamana ya kusimamia mazao hayo, inatekeleza majukumu yake ipasavyo sambamba na kuhakikisha kwamba Watendaji wake wanafanya kazi hiyo kwa uadilifu na ufanisi mkubwa.

Alisema jitihada hizo zinalenga kuwawezesha wakulima wengi hususan wa vijijini ambao ni takriban asilimia 75 ya Watanzania wote, kulima kilimo cha kisasa, chenye tija na cha kibiashara, hivyo kuondokana na umaskini wa kipato.

“Vilevile, kuwawezesha wakulima kupata mbinu za kisasa za kuyafikia masoko ya uhakika ya mazao yao ili kupata bei nzuri ambayo itawakwamua kiuchumi. Mazao mengine ya kibiashara yatakayotiliwa mkazo ni katani, ufuta, alizeti, mbaazi na ngano.”

Alisema kwa kipindi kirefu uzalishaji wa mazao hayo ulishuka kulitokana na changamoto mbalimbali ikiwemo ya baadhi ya viongozi wa vyama vya Ushirika kushindwa kutekeleza vyema wajibu wao, wizi, dhuluma kwa wakulima na pia ushiriki mdogo wa Maofisa Kilimo katika kusimamia kilimo cha kitaalam.

Wakati huo huo, Waziri Mkuu amesema jumla ya vijana 1,000,000 wamelengwa kupata urasimishaji  ujuzi kati ya mwaka 2017 na 2021 kupitia Mpango wa Kutathmini na Kurasimisha Ujuzi uliopatikana nje ya Mfumo Rasmi wa Mafunzo.

Alisea Serikali imeamua kuchukua hatua hiyo ili kuwawezesha vijana ambao ndiyo nguvu kazi wachangie kikamilifu katika kujenga uchumi wa Taifa. “Hadi sasa tayari vijana wengi wanaendelea kunufaika na mpango huu kutoka mikoa mbalimbali.”

Miongoni mwa faida za mpango huo ni pamoja na kuwasaidia mafundi waliojifunza kupitia sehemu za kazi kupata kazi zenye staha na kuwajengea uwezo wa kushiriki na kushindana kikamilifu katika soko la ajira. Pia kuinua tija mahali pa kazi na kusaidia waajiri/wenye makampuni kukidhi viwango katika eneo la rasilimali watu.

Waziri Mkuu alisema mpango huu unafadhiliwa kwa asilimia 100 na Serikali na unatekelezwa kwa pamoja na Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi ( VETA)

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
  

Tanzania yakanusha vikali kuwa na uhusiano na Korea Kaskazini

$
0
0
Serikali imekanusha vikali taarifa kutoka Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kuwa ina mahusiano ya kibiashara na Korea Kaskazini ambayo imewekewa vikwazo vya kiuchumi na baraza hilo.

Hayo yamesemwa jana jijini Dar es salaam na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Augustine Mahiga, alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari, ambapo alisema kuwa licha ya uhusiano uliokuwepo awali, lakini tangu mwaka 2014, Tanzania imepunguza uhusiano wa kibiashara na kidiplomasia na nchi hiyo.

“Hatuna ugomvi na Korea Kaskazini, lakini kwa mpango wake wa kutengeneza makombora ya masafa marefu ya nyuklia sio mzuri kwa heshima na usalama wa duniani, ndiyo maana tukaanza kuchukua hatua za kupunguza mahusiano.” alisema Dkt.Mahiga

Aidha, Dkt. Mahiga aliongeza kuwa uhusiano huo wa kibiashara ulikuwepo kabla ya vikwazo vilivyowekwa hivi karibuni na Baraza la Umoja wa Mataifa

Tanzania na Uganda ni miongoni mwa baadhi ya nchi zinazochunguzwa na Umoja wa Mataifa kwa tuhuma za kwenda kinyume na vikwazo vilivyowekwa na Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa dhidi ya Korea Kaskazini.

Ripoti ya uchunguzi huo ilitolewa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa tarehe 9 mwezi wa Septemba. Baraza la Usalama la Umoja ikisema linachunguza tuhuma za Tanzania kuingia mikataba ya kijeshi na Korea Kaskazini inayogharimu dola za kimarekani milioni 12.5

CHADEMA Yapingana na Jeshi la Polisi

$
0
0
Baraza la vijana CHADEMA (BAVICHA) limepinga kauli alizotoa Kamishna Kanda maalumu ya Dar es salaam, Lazaro Mambosasa kuhusu maombi yao kitaifa kumuombea Mbunge Tundu Lissu na kusema wao hawajapanga kuandamana bali watafanya maombi kumuombe Lissu.

Akiongea jana  na waandishi wa habari Katibu Mkuu (BAVICHA) Taifa, Julius Mwita alisema kuwa wameshangazwa na kusikitishwa na kauli kadhaa alizozitoa Mambosasa kuhusu maombi yao na kusema ametafsiri ndivyo sivyo kauli zao kwani wao hawajapanga kufanya maandamano.

"Tumeshangazwa na kusikitishwa na kauli kadhaa alizozitoa Mambosasa akionesha kuwa amezuia maombi hayo kwa sababu alizodai kuwa yatakuwa ni maandamano na kinyume cha taratibu. Tungependa kusema shughuli yetu ya Jumapili haijapangwa kuhusisha wala haitahusisha maandamano yoyote kama ambavyo SACP Mambosasa ametafsiri. "

Julius Mwita aliendelea kuweka wazi kwamba wameamua kukutana kwenye uwanja huo ili kutoa nafasi kwa watu wa imani zote kuweza kukutana na kufanya sala na dua kwa pamoja.

"Tumesema wazi katika taarifa yetu kwa jeshi hilo wilayani Kinondoni, kuwa shughuli ambayo tumeiandaa inahusu maombi ambayo yatahusisha watu wa imani za dini mbalimbali ambao kimsingi hawawezi kukutana ndani ya nyumba moja ya ibada lakini wote hao wanaweza kukutana sehemu moja, mahali pa wazi na kuomba dua/ sala kwa utulivu pamoja" alisema Julius Mwita

Mwita amesema wao wanaendelea na maandalizi ya shughuli hiyo kama kawaida kwa kuwa waanamini hakuna utaratibu wala sheria ambayo wamevunja na kumtaka Mambosasa aipokee hiyo barua ya maombi yao kisha aitafakari na kulinganisha na kauli zake alizozitoa leo mbele ya waandishi wa habari.

"Tunaelewa sheria na taratibu za nchi zinazosimamia mikusanyiko mbalimbali haziwapatii Polisi mamlaka yoyote ya kuzuia mikusanyiko au kutoa kibali cha mikusanyiko, bali sheria na taratibu hizo zimeelekeza wahusika wa shughuli hiyo kutoa taarifa Polisi na kueleza siku, mahali, muda na wahusika wa mkusanyiko husika." 

Mwita aliendelea kutoa ufafanuzi juu ya jambo hilo na kudai

"Baada ya kusikia kauli ya SACP Mambosasa, tunatoa wito kama ifuatavyo tunamsihi SACP Mambosasa apate nakala ya barua yetu ya taarifa kuhusu shughuli hiyo ambayo tumepeleka mamlaka za kipolisi kama sheria inavyoelekeza, ili aweze kutafakari uzito wa shughuli hiyo ya maombi ya Kitaifa ya Vijana kisha alinganishe na kauli zake alizotoa leo" alisema Mwita

Mbali na hilo Katibu Mkuu wa (BAVICHA) Julius Mwita alisema wao wanaendelea na maandalizi na kuwataka watu wenye mapenzi mema na taifa na ambao wameguswa na tukio la kinyama na kikatili la kupigwa risasi kwa Mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lissu kuhakikisha wanafika Jumapili Sinza Darajani katika uwanja wa TP kwa ajili ya maombezi hayo na kusema jambo hilo si la kisiasa kama ambavyo Mambosasa amekuwa akisema.

Serikali Yaapa Kupambana na Wanaojihusisha na Mapenzi ya Jinsi Moja

$
0
0
Serikali imesema inapambana kwa nguvu zote na vitendo vya mapenzi ya jinsi moja na kwamba, mwanamume atakayethibitika kufanya vitendo vya kike ataadhibiwa kisheria.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk Hamisi Kigwangalla alisema hayo jana Ijumaa alipojibu swali la Mbunge wa Viti Maalumu (Chadema), Susan Lyimo.

Mbunge huyo alisema kumekuwa na biashara kati ya wanaume na wanawake lakini pia ipo ya watu wa jinsi moja. “Nataka kufahamu hao wanachukuliwa hatua gani?” alihoji Lyimo.

Naibu waziri alisema sheria inakataza watu wa jinsi moja kufanya mapenzi  kinyume cha maumbile na pia inakataza wanaume kufanya vitendo vya jinsi ya kike.

Alisema kuna adhabu kali hutolewa na sheria hiyo kwa mtu anayebainika kufanya vitendo hivyo na kwamba, adhabu yake ni kifungo cha hadi zaidi ya miaka 30 jela.

“Tumekuwa tukipambana kwa nguvu zetu zote na makundi haya ambayo yamekuwa yakishiriki katika vitendo vya mapenzi ya jinsi moja, kuyahamasisha ama kuyahalalisha  au kuyafanya kuonekana kama ni vitu vya kawaida katika nchi yetu,” alisema.

Dk Kigwangalla alisema wamefanikiwa kwa kiasi kikubwa kwa kufanya operesheni nchi nzima. Amesema taasisi mbalimbali ambazo zilikuwa na mwelekeo wa kutekeleza afua za kinga katika sekta ya afya wamezifuta na kuzibadilisha.

Katika swali la msingi, Mbunge wa Geita Mjini (CCM), Costantine Kanyasu alihoji kazi ya kuwakamata wanawake wanaojiuza imefanikiwa kwa kiasi gani nchini.

Dk Kigwangalla alisema tatizo hilo ni kubwa katika mikoa ya Dar es Salaam, Mwanza, Arusha, Mbeya na Dodoma.

“Kitendo cha mwanamke kuishi akitegemea kipato chake au sehemu ya kipato chake kutokana na ukahaba ni kosa la kisheria,” alisema.

Naibu waziri alisema katika kutekeleza sheria ipasavyo, viongozi katika mikoa ukiwemo Mkoa wa Dar es Salaam wamekuwa wakikamatwa na kuchukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria ya wanawake wanaojiuza.

Alisema Wizara ya Afya kwa kushirikiana na Ofisi ya Rais Tamisemi na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi wataendelea kuhakikisha wanawake wanaojihusisha na biashara hiyo wanaendelea kukamatwa ili kulinda heshima, utu na hadhi ya wanawake wa Tanzania.

Kutana na Mtaalamu wa Kusafisha Nyota........Anatoa Mvuto wa Biashara, Kupandishwa Cheo, Kurudishiwa Mali Uliyoibiwa na Mengne

$
0
0
Kutana na Mtaalamu wa Kusafisha Nyota........Anatoa Mvuto wa Biashara, Kupandishwa Cheo, Kurudishiwa Mali Uliyoibiwa na Mengne
 
Kutana Maajabu ya Mtabibu MAALIM MOHAMEDI MASUDI Mganga wa Waganga Sasa Yupo Mikoa Yote Tanzania
Pia anatoa Tiba kwa Njia ya Simu ukiwa popote Pale Tanzania au Nje ya Tanzania..
MAALIM MOHAMEDI MASUDI ni Mtabibu na Mtafiti wa Dawa za Asili ya Africa, na Duniani Katika utoaji wa Tiba za Asili..
 
Je unasumbulia na Mapenzi..?
(Umeachwa na Umpendae awe Mume/ Mke au mpenzi na Anaishi na Mtu Mwingine na Bado Unampenda?) Umejaribu sehemu Nyingi bila Mafanikio?Wasiliana na MAALIM MOHAMEDI MASUDI Akusaidie Kumshika Umpendae Asikusaliti(LIMBWATA) Kumtawala Mpenzi wako kwa sababu Maalum..Anauwezo wa Kusambalatisha Mahusiano yao ndani ya siku Moja tu.
Je Unasumbuliwa na Madeni?
Biashara yako Haina wateja?
Unatatizo la kutokushika Mimba na umehangaika sehemu nyingi bila mafanikio?
Wasiliana na MAALIM MOHAMEDI MASUDI Kwa Majibu ya Maswali yako..

Anasafisha NYOTA na Kutoa PETE za BAHATI kuendana na NYOTA yako. UTAJIRI USIO NA MASHARTI.(Magic Wallet_Pochi ya Maajabu Isio Isha Hela)
KUWA MAARUFU na KUJULIKANA
Kupandishwa CHEO na HESHIMA Mahala pa KAZI.
Utapewa Nguvu ya Kujilinda na MALI ZAKO zako na Mwili wako.. Huzuia Chuma Ulete katika Biashara.. Hurudisha MALI zilizo Potea au KUDHULUMIWA.

Mvuto wa Biashara na Mwili wako.
Hutibu kabisa Nguvu za Kiume na Kurefusha Uume kwa saizi Unayotaka.
Magonjwa Sugu(Miguu Kufa Ganzi, kisukari, Presha, Pumu nk.
Wasiliana nae kwa namba
0655516982
0688856265
0621898709(Whatsapp)

Kwa Nini Wanaume Wengi Wanaupungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo?

$
0
0
Asilimia 45 ya wanaume wapo tofauti na wengine kwa kuwatimizia vyema wake au wapenzi Wao na kuwasababishia kutoka nje ya ndoa zao.

NINI CHANZO CHA HAYO?Kupiga punyeto,Ngiri,Vidonda vya tumbo,Magonjwa ya moyo,Presha,Kisukari,Korodani moja kuvimba,Msongo wa mwazo,Kufanyiwa tohara ukiwa mtu mzima n.k.DOKTA MANYANDA sasa kapata tiba sahihi ya tatizo la NGUVU ZA KIUME.

MUHAMA:Hii hutibu na kuponyesha kabisa tatizo la nguvu za kiume,utakuwa na uwezo wa kurudia tendo zaidi ya mara tatu bila kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dakika 15-20.DAWA hii imechanganywa miti 12.Hata wazee wenye umri mkubwa wanapona kabisa.OKO NDOA YAKO SASA. 

MANGUNGU MIX: Ndio tiba tosha kwa sasa ambayo hurefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo inch 1-8 na unene sentimita 1-5,dawa hii ipo ya kupaka na kunywa na haina madhara yoyote kwa mtumiaji.

NITOFAUTI NA ULIZO WAHI KUZITUMIA.Pia tuna dawa za kupatanisha mke,mme,mpenzi au bosi wako kwa mda mfupi sana,Uzazi,Kusafisha nyota,

Je unamali yako unauza hupati wateja?Wasiliana nami 0716-263605 

DOKTA MANYANDA ANAPATIKANA KASULU KIGOMA,Kwa wale wa mikoani huduma hii utaipata popote pale.

Pata Tiba ya Tiba ya Tatizo la Nguvu Za Kiume........Inasaidia Kukufanya Urudie Mara 5 na kuchelewa kwa Dakika 20

$
0
0
TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO LINATIBIKA.Baada ya utafiti wa mda mrefu juu ya matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume na ukosaji wa hamu ya tendo la ndoa ama kushindwa kurudia tendo kwa haraka DR Magise imekuletea tiba ya matatizo hayo kwa kutumia dawa za: 
 
FUUl POWER:Ni dawa asili ya vidonge inayotibu tatizo la upungufu au ukosefu wa nguvu za kiume,dawa hii inamchanganyiko wakutosha wenyekuzalisha vichocheo vingi vya Hemone za Gestrogen vikiwemo vitamin B6&B1,vitamini E,pamoja na madini aina ya zinc vitakufanya kuwa na nguvu na mzunguko mzuri wa damu na kuongeza hamu na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya hatua nne au zaidi,na kuchelewa kufika kileleni zaidi dakka 20-30.
 
NYAMVA:Inarutubisha maumbile ya uume yani kurefusha na kunenepesha nchi 4-7 upana cm3-4 standard kiafya haijalishi umri wako hata kwa wazee ukiitumia maumbile yako yatabaki kuwa hivyo siku zote,Pia tunatibu Presha,kisukari siku7,ngiri,chango la tumbo tumbo kujaa gesi,kutopata choo vizuri

 TUPO TZ DAR ES SALAAM   MBAGALA RANGI TATU.HUDUMA HII UTALETEWA POPOTE ULIPO .WASILIANA NAMI 0783741788,0715741788 -DR MAGISE

Baa, Migahawa na Vilabu vya Pombe Vyafungwa kwa Ugonjwa wa Kipindupindu

$
0
0
Mkuu wa Wilaya ya Mbarali Mh. Reuben Mfune ameagiza bar zote, migahawa, vilabu vya pombe na grocery kufungwa kwa siku zisizojulikana kutokana na ugonjwa wa kipindupindu kuzidi kusambaa wilayani humo.

Mkuu wa wilaya ametoa taarifa hiyo kupitia Afisa habari wa wilaya hiyo Daudi Nyingo na kuwataka wananchi kuwa makini na matumizi ya maji ya mito na mifereji kwani yameathiriwa na vijidudu vya kipindupindu.

"Wananchi wote wa wilaya ya Mbarali mnatangaziwa kuwa hali ya ugonjwa wa Kipindupindu bado ni mbaya sana wilaya hapa, hivyo basi biashara zote za migahawa, vyakula vyote vinavyotembezwa, minada, vilabu vya pombe, bar, grocery zote, pamoja na mikusanyiko yote inayohusiana na sherehe, vyote vimefungwa hadi hapo mtakapotangaziwa tena"

Mkuu wa Wilaya ya Mbarali amesema kuwa mtu yoyote ambaye atakiuka maagizo hayo atachukuliwa hatua kali za kisheria

"Aidha mashine zote zitakazobainika kusaga vimea au unga wa pombe za kienyeji hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yao Vilevile mnakumbushwa kwamba, maji yote ya mito pamoja na mifereji yameathiriwa na vijidudu vya Kipindupindu, hivyo basi wananchi wote mnaagizwa kuchemsha maji au kutumia vidonge vya 'water guard' pamoja na kufanya matumizi sahihi ya vyoo" alisema Mfune

Hadi kufia Septemba 15, 2017 jumla ya wagonjwa 628 wamepatikana huku jumla ya watu nane wamefariki kutokana na ugonjwa wa Kipindupindu wilayani Mbarali jijini Mbeya.

Mabasi yakamatwa usiku wa manane kwa mwendokasi

$
0
0
Mabasi saba ya abiria yamekamatwa  na kutozwa faini kwa kosa la mwendokasi na kutofuata sheria za usalama barabarani huku wakihatarisha maisha ya abiria.

Kamatakamata hiyo  ambayo imesimamiwa na Kamanda wa kikosi cha usalama barabarani   Fotunatus  Muslim akiwa na timu ya viongozi na askari  mkoa wa Morogoro imefanyika usiku wa kuamkia leo.

Zoezi la ukamataji mabasi hayo limefanyika eneo la Dumila Wilaya ya Kilosa mkoani hapa, zoezi lilichukua takribani masaa mawili ambapo mabasi hayo yamezuiwa kuondoka mpaka asubuhi huku yakitozwa faini.

Kamanda Muslim amesema jeshi hilo halitakubali kuona maisha ya watanzania yakipotea  kutokana na uzembe wa baadhi ya madereva.

Amesema  kikosi hicho cha usalama barabarani kimeahidi kupambana na madereva wa mabasi ya abiria hasa nyakati za usiku kwani ndio wamekuwa wakiendesha kwa mwendokasi huku wakidai  serikali muda huo inakuwa imelala.

Mabasi ya abiria zaidi ya saba yanayofanya safari kati ya mkoa wa Mara (Musoma) Dar es salaam, na Mwanza- Dar es salaam yamekaguliwa na kutozwa faini.

Muslim amesema  madereva wengi wamekuwa wakifuata sheria za barabarani nyakati za mchana kwa kuhofia kukamatwa kutokana na tochi zilizopo na inapofika nyakati za usiku madereva hao wamekuwa wakitumia mwanya wa kuendesha kwa mwendo kasi.

 Akizungumzia dhamira ya Polisi  Muslim amesema ni kuwalinda raia na mali zao na kuwataka askari wa usalama barabarani kuacha kufanya kazi kwa mazoea.

Amesema doria ni endelevu na sasa itakuwa kwa nchi nzima kwa usiku na mchana huku akiwataka madereva hao kuacha kudanganyika kwa madai kuwa tochi usiku hazifanyi kazi usiku na kwamba tochi sasa zitakamata mpaka usiku.

"Nimekuja na slogani ya Kamata hii ni kwa wale madereva wasiotii na kufuata sheria na tutapambana nao kila wakati na nyakati zote na hiyo itasaidia abiria kusafiri salama na matumizi ya barabarani kuwa bora," amesema kamanda Muslim

Mmoja wa abiria aliyejitambulisha kwa jina la Leon Mwete aliyekuwa katika moja ya basi yaliyokamatwa eneo hilo la Dumila amesema zoezi hilo ni zuri na linafaa kuendelea.

Amesema hii itapunguza ajali za barabarani na kwamba kwa sasa uendeshaji wa madereva wengi ni mzuri ukilinganisha na zamani.

Naye kamanda wa kikosi cha usalama barabarani mkoa wa Morogoro Boniface Mbao ameeleza kuwa yeye akiwa msimamizi mkuu ataendelea kusimamia na kufanya oparesheni za usiku na mchana kama maelekezo yaliyotolewa.

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Gazi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0
Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Tupo Mbagala

Nyumba ya Zitto Kabwe yawaka moto

$
0
0
Nyumba ya Mbunge Kigoma Mjini Zitto Kabwe iliyopo Kibingo, Kata ya Mwandiga mjini Kigoma imeungua moto jioni ya leo ambapo mpaka sasa chanzo cha moto huo hakijafahamika.

Hayo yamethibitishwa na Afisa habari wa chama cha ACT, Abdalla Khamis na kusema ni kweli tukio hilo limetokea lakini siyo katika nyumba ambayo anaishi Mbunge Zitto Kabwe.

"Ni kweli nyumba ya Zitto imeungua moto jioni ya leo lakini siyo nyumba ambayo anaishi yeye binafsi, bali ni nyumba ambayo imejengwa katika kiwanja kimoja na nyumba anayoishi kwa sasa", amesema Abdalla.

Habari Zilizopo Katika Nagazeti ya Leo Jumapili ya Septemba 17

Spika Job Ndugai Ajibu Tena Mapigo ya Wabunge anaodai Wanamdhalilisha

$
0
0
Spika wa Bunge, Job Ndugai amefunguka na kusema kuwa yeye hana tatizo lolote na Mbunge Zitto Kabwe, Saed Kubenea na Godless Lema ila amedai yeye ni binadamu hivyo mtu anapomnyanyasa na kumdhalilisha hutumia mamlaka aliyonayo kufanya maamuzi.

Ndugai amesema kuwa yeye kama kiongozi wa Bunge anamamlaka na madaraka makubwa kuliko hata yaliyoandikwa na kusisitiza kuwa anao uwezo wa kumsimamisha Mbunge asiongee chochote bungeni mbaka muda wa mbunge huyo utakapokwisha.

"Siyo kila kitu huandikwa katika mahusiano ya kikazi lakini kiongozi wako wa kazi ana mamlaka na madaraka makubwa kuliko hata yaliyoandikwa si kila jambo lazima liwe ni kanuni, narudi tena nimesikia watu wakibisha bisha ninao uwezo kama spika, zipo kanuni zinamruhusu Spika wa Bunge kwa kadri anavyoona inafaa kwa busara yake namna gani aongoze bunge, huwezi kuwa unatukana bunge unamtukana huyo spika halafu huyo huyo Spika anakupa nafasi uzungumze kwa sababu yeye ni malaika? Mimi ni binadamu mwenye damu na nyama kama wengine" alisema Ndugai

Spika wa Bunge aliendelea kutoa ufafanuzi juu ya baadhi ya wabunge ambao wamekuwa wakitumia mitandao ya kijamii kupotosha umma au kumzungumza mambo ya bunge kwa njia isiyo na staa kupitia mitandao hiyo ya kijamii na kumdhalilisha yeye na kusema yeye pia atatumia mamlaka yake kuona anafanya nini juu ya wabunge hao.

"Kwa jinsi unavyoninyanyasa na kunidhalilisha mbele ya watu na mimi nitatumia madaraka yangu na mamlaka niliyonayo niliyopewa na nchi na Mungu kuona nini nifanye katika mamlaka niliyonayo" alisisitiza Ndugai

Spika wa Bunge Job Ndugai alisema kuwa ana uwezo wa kumzuia mbunge Zitto Kabwe asizungumze chochote ndani ya bunge kwa kipindi chote cha ubunge

Mbunge wa CCM amtembelea Tundu Lissu Nairobi

$
0
0
Mbunge wa Singida Kaskazini Mhe. Lazaro Samuel Nyalandu amemtembelea Mbunge wa Singida Mashariki Mhe. Tundu Lissu jijini Nairobi nchini Kenya kumjulia hali kufuatia mbunge huyo kupigwa risasi na watu wasiojulikana Septemba 7, 2017 akiwa mjini Dodoma.

Lazaro Nyalandu amesema kuwa kwa niaba ya watu wa Singida na Watanzania wote ametoa salamu za pole kwa mke wa Tundu Lissu kwa kuwa bado hajapata nafasi ya kumuona kiongozi huyo na kusema anasubiri kama ataweza kupata nafasi ya kumuona  kama madaktari wataruhusu.

"Nimefika hospitali ya Nairobi mapema leo (jana) kumjulia hali Mh. Tundu Lissu. Madaktari wanaendelea kumfanyia matibabu, na bado hatujaruhusiwa kumuona. 

"Kwa niaba ya wana Singida na Watanzania wote, nimetoa salaam za pole kwa mke wake, na bado nasubiri uwezekano wa kuweza kuonana naye usiku  endapo madaktari wataruhusu" alisema Nyalandu

Aidha Mbunge huyo amewataka Watanzania kijumla kuendelea kumuombe Mbunge Tundu Lissu ili aweze kupona na kurejea nchini akiwa mzima wa afya njema

"Cha muhimu zaidi, sote tuendelee kumuombea Mungu amtendee wema, na kumponya katika majira haya ya kujaribiwa kwake. Katika yote ndani ya yote, ikawe heri kwake" alisema Nyalandu

Mbunge Tundu Lissu alishambuliwa kwa risasi na watu wasiojulikana Septemba 7, 2017 akiwa Makao Makuu ya nchi jijini Dodoma na baadaye kusafirishwa kupelekwa jijini Nairobi Kenye kwa matibabu ambapo mpaka sasa yupo huko akiendelea kupata matibabu.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live


Latest Images