Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Pata Tiba ya Tiba ya Tatizo la Nguvu Za Kiume........Inasaidia Kukufanya Urudie Mara 5 na kuchelewa kwa Dakika 20

$
0
0
TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO LINATIBIKA.Baada ya utafiti wa mda mrefu juu ya matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume na ukosaji wa hamu ya tendo la ndoa ama kushindwa kurudia tendo kwa haraka DR Magise imekuletea tiba ya matatizo hayo kwa kutumia dawa za: 
 
FUUl POWER:Ni dawa asili ya vidonge inayotibu tatizo la upungufu au ukosefu wa nguvu za kiume,dawa hii inamchanganyiko wakutosha wenyekuzalisha vichocheo vingi vya Hemone za Gestrogen vikiwemo vitamin B6&B1,vitamini E,pamoja na madini aina ya zinc vitakufanya kuwa na nguvu na mzunguko mzuri wa damu na kuongeza hamu na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya hatua nne au zaidi,na kuchelewa kufika kileleni zaidi dakka 20-30.
 
NYAMVA:Inarutubisha maumbile ya uume yani kurefusha na kunenepesha nchi 4-7 upana cm3-4 standard kiafya haijalishi umri wako hata kwa wazee ukiitumia maumbile yako yatabaki kuwa hivyo siku zote,Pia tunatibu Presha,kisukari siku7,ngiri,chango la tumbo tumbo kujaa gesi,kutopata choo vizuri

 TUPO TZ DAR ES SALAAM   MBAGALA RANGI TATU.HUDUMA HII UTALETEWA POPOTE ULIPO .WASILIANA NAMI 0783741788,0715741788 -DR MAGISE

Selemani Jafo awataka Wakuu wa Wilaya kuitumia vizuri sheria ya kuweka ndani watu

$
0
0
Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Selemani Jafo amewatakaa Wakuu wa Wilaya kuitumia vizuri sheria ya kumuweka mtu ndani kwa saa 48 pasipo uonevu wowote.

Jafo ameitoa kauli hiyo  Mjini Dodoma alipokuwa akifunga mafunzo ya Uongozi ya Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi wa Majiji, Manispaa na Halmashauri kutoka mikoa ya Mbeya, Iringa, Rukwa, Njombe, Ruvuma, Songwe, Shinyanga na Dar es Salaam, Yalioanza Septemba 11, mwaka huu.

"Fanyeni kazi kwa kufuata mipaka yenu ya kazi, kwani ndilo jambo pekee litakalo waepusha na migogoro katika maeneo yenu ya kazi," amesema Jafo.

Amesema , viongozi hao wanapaswa kufanya kazi pasipo kumuonea au kumpendelea mtu kwa namna yoyote ile, bali wakawe mifano kwa kujenga uhusiano mzuri na watumishi wanao waongoza pamoja na wananchi.

Jafo amewataka kwenda kufanya mabadiliko katika maeneo mbalimbali, ikiwa ni pamoja na vita dhidi ya rushwa na dawa za kulevya, usimamizi wa miradi ya maendeleo,matumizi ya mfumo wa kielektroniki katika ukusanyaji wa mapato ya Serikali pamoja na kusimamia uwajibikaji wa watumishi wa umma.

Wakati wakiendelea na mafunzo hayo, Katibu Mkuu Kiongozi Mhandisi John Kijazi amewatembelea Wakuu hao wa Wilaya na kuwapa miongozo ya utendaji kazi pamoja na mipaka ya kazi yao ili kuepuka migogoro katika maeneo yao ya kazi.

Naye, Mkuu wa Kitengo cha Mafunzo kutoka Taasisi ya Uongozi, Kadari Singo alizitaja mada walizofundishwa viongozi hao kuwa ni pamoja na muundo wa Serikali, namna ya kumbadili kiongozi, utunzaji wa nyaraka na siri za Serikali, manunuzi, matumizi sahihi ya vyombo vya usalama, usalama wa nchi pamoja na mambo ya uchaguzi.

Zitto anena nyumba yake kuteketea moto

$
0
0
Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe amewataka wananchi kuwa watulivu wakati Jeshi la Polisi likiendelea na uchunguzi kubaini chanzo cha moto ulioteketeza nyumba yake.

Nyumba hiyo iliteketea jana Jumamosi alasiri na hakuna madhara kwa binadamu yaliyotokea isipokuwa mali zote zilizokuwamo ndani zimeteketea.

“Tumepata ajali kidogo. Nyumba yangu ninayoishi katika eneo la Kibingo, mji mdogo wa Mwandiga, Kigoma imeteketea kwa moto jioni hii. Alhamdulillah, kuwa hakuna binaadam aliyeumia,” aliandika Zitto katika ukurasa wake wa Facebook.

Alisema analishukuru Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, majirani zake na wananchi wenzake kwa ushirikiano walioutoa ili kuzima moto huo.

“Kwa sasa Jeshi la Polisi wanafanyia kazi kujua chanzo cha ajali. Naomba wananchi wawe watulivu wakati Polisi wanaendelea na uchunguzi husika,” alisema Zitto.

Nyumba hiyo aliyoijenga wakati akigombea ubunge kwa mara ya kwanza iko kiwanja kimoja na nyumba yake ya sasa.

Msaidizi wa mbunge huyo, Nyembo Mustafa alisema Zitto hakuwa anaishi kwenye nyumba hiyo baada ya kujenga nyingine kubwa kwenye kiwanja hicho.

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo Apiga Marufuku Watumishi wa Umma Kukamatwa Hovyo

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo amepiga marufuku viongozi wa Serikali kuwakamata na kuwaweka rumande watumishi wa umma bila kufuata sheria na taratibu za utumishi.

Gambo alisema juzi kuwa siku za hivi karibuni kumejitokeza matukio ya baadhi ya viongozi kuwaweka rumande watendaji wa Serikali bila kufuata taratibu.

“Kama mtendaji alikosea kuna taratibu zake, kuna masuala ya kiutumishi, kuna ya kijinai na ya uchunguzi, hivyo ni busara kufuata taratibu,” alisema.

Gambo aliwataka viongozi kutumia vyombo vilivyowekwa na Serikali kutatua matatizo ikiwamo, Taasisi za Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) na pia kufuata sheria za utumishi wa umma.

Pia, aliwataka watumishi wa umma mkoani Arusha kufanya kazi kwa kushirikiana na kuepuka majungu kwa kuwa wote wanawajibika kwa wananchi.

“Fanyeni kazi kwa ushirikiano na kuheshimiana ili kuepusha migogoro isiyo ya lazima katika halmashauri zenu na wilaya kwa jumla,” alisema Gambo.

Awali, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Arusha Vijijini, Wilson Mahera alisema wamejipanga kutatua kero za watumishi na wananchi ili kuhakikisha wanapata maendeleo.

Mahera alisema katika bajeti iliyopita Sh580 milioni zilitumika kuboresha miundombinu katika sekta ya elimu kama kujenga nyumba za walimu, madarasa na kukabiliana na upungufu mwingine.

Alisema katika bajeti ya mwaka 2017/18 pia, mikakati imewekwa kukabiliana na kero mbalimbali za watumishi na wananchi.

Mahera alisema mapato ya ndani yanayotarajiwa kukusanywa ni zaidi ya Sh3 bilioni huku Sh39 bilioni zikitoka Serikali Kuu.

Katiba Pendekezwa Yahofiwa Kuyeyuka.....Jukata Watilia Shaka Maandalizi, Wataka Mabadiliko Muhimu Kabla ya 2020

$
0
0
Jukwaa la Katiba Tanzania (Jukata) limeitaka Serikali ifanye mabadiliko ya msingi katika Katiba kabla ya kuingia kwenye maandalizi ya uchaguzi mkuu ujao.

Jukata imesema mabadiliko hayo ya msingi  yafanyike iwapo  hakuna uwezekano wa kukamilisha mchakato wa Katiba Mpya kabla ya uchaguzi wa mwaka 2020, kama ambavyo dalili zinazidi kuonyesha.

Akizungumza na waandishi wa habari jana Jumamosi jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mtendaji wa Jukata, Hebron Mwakagenda alisema kwa hali ilivyo dalili ya kupatikana Katiba Mpya hakuna, kutokana na kutotengwa bajeti kwa ajili ya mchakato huo.

Alisema ipo haja ya kurekebisha angalau mambo ya msingi ambayo yamelalamikiwa na wananchi kwa kipindi kirefu.

Alisema kutokana na hilo yafanyike mabadiliko muhimu katika Katiba iliyopo ikiwamo kuwapo na uhuru kamili ya tume ya uchaguzi Zanzibar.

Aliyataja mabadiliko hayo ni kuwa na uhuru kamili wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi na Tume ya Uchaguzi Zanzibar.

Alisema mabadiliko hayo pia yaangalie kuwapo kwa fursa ya mgombea huru katika uchaguzi, ikiendana na kutokuwa na masharti makali yanayokatisha tamaa.

Alisema pia Katiba ibadilishwe na iwe na nafasi ya kuhoji matokeo ya uchaguzi wa Rais mahakamani na pia kuwezesha vyama vya siasa kuungana kikatiba na kisheria kwa lengo la kusimamisha mgombea mmoja.

“Hili siyo la vyama vya upinzani pekee, hata chama tawala CCM itafikia mahali kitahitaji kuungana na vyama vingine kusimamisha mgombea mmoja."

“Siasa zinabadilika sana na chenyewe ni kama kipo ukingoni, hivyo hili liangaliwe na lipewe nafasi kwenye Katiba,” alisema Mwakagenda.

Aliyataja mabadiliko mengine ni kurejesha mfumo wa ushindi katika uchaguzi wa Rais kwa kigezo cha kupatikana kwa kura zisizopungua 50 jumlisha moja.

Mlipuko wa bomu waua watoto watatu Jijini Arusha

$
0
0
Watoto watatu waliokuwa wakichunga ng'ombe wamefariki dunia baada ya kulipukiwa na bomu walilolichezea wakidhani ni mpira.

Tukio hilo lilitokea Ijumaa jioni katika Kijiji cha Nafco kilichopo Kata ya Loksale wilayani Monduli mkoa Arusha.

Mwenyekiti wa kijiji hicho, Julius Mhale amesema watoto hao wanatarajiwa kuzikwa kesho Jumatatu.

Amesema eneo lilikolipuka bomu hutumiwa na Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) kwa mazoezi.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Charles Mkumbo amethibitisha tukio hilo na kuahidi kutoa taarifa rasmi.

Watano Watiwa Mbaroni kwa Kumuombea Tundu Lissu

$
0
0
Jeshi la Polisi jijini Dar es salaam, linawashikilia watu watano kwa tuhuma za kuratibu shughuli za maombezi maalum kwa ajili ya mbunge Tundu Lissu, katika viwanja vya TIP Sinza.

Akizungumza na waandishi wa habari Kamanda wa Polisi mkoa wa Kinondoni Murilo Jumanne aliyekuwa eneo la tukio, amesema wameamua kuwakamata watu hao kwa kuwa wanatishia amani na utulivu wa nchi.

"Wale wenye nia mbaya ambao bila shaka wana ajenda binafsi ajenda ambazo kimsingi zina uelekeo wa kutishia masuala ya amani, mimi kama Kamnda wa Polisi mkoa wa Kinondoni, siwezi kukubali hali hiyo itokee kwenye eneo langu, watu wanaendelea na shughuli zao na wachache wakiwa wamevaa nguo za kawaida lakini wameficha tishirt ndani, wanafika sehemu wanaanza kuzitoa", amesema Kamanda Jumanne.

Kamanda Jumanne ameendelea kwa kuwataka wananchi kuacha kufanya mikusanyiko ya aina hiyo, na iwapo wanahitaji kufanya ibada waende kwenye sehemu za ibada.

Jana Jeshi la polisi Kanda maalum lilitoa taarifa ya kupiga marufuku kusanyiko lolote lisilo halali kumuombea Mbunge Tundu Lissu ambaye yuko Nairobi kwa matibabu, na kusema ni kuhatarisha hali ya amani.

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Gazi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0
Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Tupo Mbagala

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatatu ya Septemba 18

Majaliwa atoa onyo kali kwa viongozi Serikalini Wasio na Mashamba

$
0
0
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa amepiga marufuku Viongozi wa Serikali wasiokuwa na mashamba ya mikorosho kutojihusisha na biashara ya uuzaji wa zao hilo.

Ametoa agizo hilo hii jana wakati wa ufunguzi wa mkutano wa wadau wa korosho uliofanyika mkoani Tanga, ambapo amewataka viongozi hao kutoingilia biashara ya zao hilo kwakuwa haliwahusu.

“Kama huna shamba, huwezi kuwa na korosho, unauza umepata wapi. Jukumu lenu ni kufuatilia, kukemea na kuchukua hatua stahiki penye udhaifu na si vinginevyo,”amesema Majaliwa

Amesema kuwa kama viongozi hao wanahitaji kuuza korosho watumie muda huu ambao Serikali inahamasisha watu wafungue mashamba mapya nao watumie fursa hiyo na kulima.

Hata hivyo, ameongeza kuwa ni vyema kila mdau akahahakikisha anatimiza wajibu wake ipasavyo kama ni mkulima alime kwa kuzingatia stadi za kilimo na mnunuzi azingatie taratibu zilizopo.

Tanzania yasamehewa deni la Bilioni 445 na Brazil

$
0
0
Serikali ya Brazil imeisamehe Tanzania deni Dola 203milioni ambazo sawa Bilioni 445 ambalo limetokana na mkopo uliotolewa kwaajili ya ujenzi wa barabara ya Morogoro-Dodoma mwaka 1979.

Balozi wa Tanzania Nchini Brazil Dk Emmanuel Nchimbi amesaini mkataba huo kwaniaba ya Tanzania huku Wakili wa Hazina ya Taifa Dk Sonia Portella Nunes akisaini kwa niaba ya Serikali ya Brazil.

Balozi Nchimbi ameishukuru Serikali ya Brazil kwa msamaha huo ambao amesema umeunga mkono jitihada za Rais Dk. John Magufuli kujenga uchumi imara wa Tanzania.

Balozi Nchimbi pia ameuhakikishia Serikali ya Brazil utayari wa Tanzania katika kuimarisha ushirikiano wa kibiashara na uchumi na Brazil.

Hivyo kuanzia sasa kampuni za Brazil zinaruhusiwa kukopa katika Benki za Brazil kwa ajili ya kutekeleza miradi nchini Tanzania lakini pia Serikali ya Tanzania inaruhusiwa kuanzisha majadiliano ya miradi mipya ya maendeleo.

Polisi Wataja Chanzo cha nyumba ya Zitto Kabwe Kuwaka Moto

$
0
0
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kigoma, Ferdinand Mtui amesema kuongezeka joto katika betri za sola ndio chanzo cha moto uliounguza Nyumba ya Mbunge wa Kigoma mjini, Zitto Kabwe juzi jioni.

Nyumba hiyo ipo mtaa wa Kibingo, mji mdogo wa Mwandiga katika wilaya ya Kigoma mkoani Kigoma.

Amesema  joto hilo limesababisha mlipuko wa moto kwenye betri za sola na hivyo nyumba kushika moto na kuteketea yote.

Polisi wanamshikilia mlinzi wa nyumba hiyo, Norbert Joseph kwa mahojiano zaidi ili kubaini kama kuna uzembe wowote uliofanywa na kusababisha moto kuwaka.

Msaidizi wa Zitto anayeifahamika kwa jina la  Nyembo Mustafa ametaja  thamani ya hasara iliyosababishwa na moto huo kwamba ni Sh 45 milioni.

Mbunge Musukuma akamatwa na polisi Geita

$
0
0
Polisi mkoani Geita wanamshikilia Mbunge wa jimbo la Geita vijijini Joseph Kasheku (Musukuma) kutokana na vurugu zilizotokea eneo la mgodi wa GGM Septemba 14 mwaka huu.

Mbunge Msukuma na madiwani wa wilaya ya Geita walifunga barabara zinazoingia kwenye mgodi wa GGM wakishinikiza kulipwa dola 12 milion zinazotokana na kodi ya huduma.

Kamanda wa polisi mkoani hapa Mponjoli Mwabulambo jana alithibitishwa kukamatwa kwa Msukuma na kusema askari walimkamata katika eneo la CCM mjini Geita.

Kamanda amesema  kukamatwa kwa Musukuma ni mwendelezo wa Polisi  kuwakamata watu wote waliohusika katika vurugu zilizotokea Septemba 14.

Amesema tayari wamekamata madiwani wengine wawili na wananchi  watano na kwamba jeshi hilo bado linaendelea na uchunguzi na msako wa kuwakamata wote walioshiriki.

“Bado tunaendelea na msako na hawa ni wahalifu kama wahalifu wengine na sheria lazima ichukue mkondo wake na  Musukuma tumemkamata sio kwamba amekuja mwenyewe ”amesema

Kamanda amesema kwa sasa wanaendelea na mahojiano na wakikamilisha sheria itachukua mkondo wake na kwamba kosa la jina halina kikomo na wote walioshiriki vurugu za kufunga barabara lazima wakamatwe na kufikishwa kwenye vyombo vya sheria .

Hadi sasa jeshi la polisi mkoani Geita linawashikilia madiwani kumi wa halmashauri za wilaya ya Geita waliofunga barabara  zinazoingia mgodi wa GGM na kuharibu miundo mbinu ya maji yaliyotengenezwa na GGM kwa ajili ya shughuli za mgodi na wananchi wa mji wa Geita  katika kijiji cha Nungwe jambo ambalo ni kinyume na sheria.

Mgogoro wa madiwani na GGM
Madiwani wa halmashauri mbili za wilaya ya Geita juzi walifunga barabara za kuingia  katika mgodi wa dhahabu wa GGM wakishinikiza kulipwa dola 12milion zinazotokana na ushuru wa huduma kuanzia mwaka 2004 hadi 2013.

Madiwani hao wanadai fedha hizo ni haki yao kwa mujibu wa sheria kwasababu mgodi ulipaswa kulipa ushuru wa huduma wa 0.03 toka mwaka 2004 hadi 2013 na hawakulipa na badala yake walilipa dola 200,000 kwa kipindi chote kinyume na sheria.

Msimamo huo wa madiwani unapingwa na uongozi wa mgodi wanaodai  kuwa mgogoro uliopo unasababishwa na kupingana kwa sheria ambazo zote zimetungwa na bunge.

Meneja mawasiliano ya jamii Manase Ndoroma amesema  sheria ya madini iliwaruhusu kulipa  dola 200,000 kwa mwaka huku sheria ya baraza la madiwani ikiwa imepitisha malipo ya 0.3 jambo ambalo limesababisha mgogoro na kwamba suluhisho pekee ni kwenda mahakamani.

Tayari serikali mkoani hapa imewataka madiwani hao kuwa watulivu na kumsubiri Naibu Waziri wa Wizara ya Nishati na Madini, pamoja na kamishna wa madini  kufika mkoani hapa leo  Jumatatu kwa lengo la kutafuta ufumbuzi wa mgogoro huo.

Polisi yatoa ufafanuzi Vifo vya Watoto Watatu Waliofariki kwa Bomu Arusha

$
0
0
Kamanda wa polisi Arusha Charles Mkumbo amewataka viongozi waliopo karibu na kambi za mazoezi ya kijeshi kuweka utaratibu wa kuwakumbusha wananchi kutoa taarifa pindi wanapoona vitu wasivyovijua hasa vyenye asili ya chuma ili kuepusha madhara.

Kamanda Mkumbo ametoa hadhari hiyo alipokuwa akizungumzia tukio la vifo vya watoto watatu wakazi wa kata ya Loksale wilayani Monduli vilivyosababishwa na mlipuko wa bomu walilookota wakati wanachunga mifugo na kuanza kulichezea kama mpira ambalo lililipuka na kuwajeruhi vibaya miguuni.

Akizungumza kwa njia ya simu kamanda Mkumbo amesema licha ya kuwa tukio hilo ni la bahati mbaya lakini lingeweza kuepukika kama watoto hao wangeweza kutoa taarifa ya kitu walichokiona.

Kamanda Mkumbo amesema kuwa watoto hao  wangeweza kufanya hivyo kama wangekuwa wanakumbushwa na wazazi wao mara kwa mara wanapokwenda machungani.

Kwa upande wa Mkuu wa wilaya ya Monduli Bw. Iddy Kimanta aliyezungumza na ITV kwa njia ya Simu amesema watoto hao wote ni wanafunzi wa shule ya msingi Nafko na wawili akiwemo Landisi Setabau miaka 12 na Samweli Nyandusi miaka 9 walikuwa wanasoma darasa la kwanza wakati mwingine aliyetajwa kwa jina la Seuri Losila miaka alikuwa darasa la tatu.

Viongozi wa eneo lililopotokea tukio hilo wamesema kimsingi tukio hilo ni bahati mbaya kwani kwa muda mrefu wananchi wamekuwa wakielimishwa juu ya kufuata maelekezo na mara nyingi wamekuwa wakitoa ushirikiano ikiwa ni pamoja kutoa taarifa wanapoona mabaki ya vyuma.

Kwa mujibu wa viongozi hao katika maeneo mengi ya wafugaji wakati wa likizo watoto huwasaidia wazazi wao kuchunga mifugo na pia wakati wote wamekuwa wakitoa taarifa wanapokutana na vitu kama hivyo na wahusika wamekuwa wakifika mara moja na kuvichukua.

Askari Polisi Wawili Wahukumiwa Miaka 35 Jela

$
0
0
Mahakama Kuu ya Tanzania imewahukumu askari Polisi wawili wa kutoka kituo cha Oysterbay jijini Dar es Salaam na watu wengine sita kwenda jela miaka 35 kwa makosa mawili ya kukutwa nyara za serikali na kujihusisha na mtandao wa ujangili.

Hayo yamesemwa na Wakili wa Serikali, Salimu Msemo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari mjini Dodoma, ambapo aliwataja polisi hao wa zamani waliokutwa na hatia ni wenye namba D 8656 CPL Senga Nyembo na G 553 PC Issa Mtama washtakiwa walikutwa na meno 70 ya tembo yenye thamani ya Sh. milioni 800.

Wengine sita waliokuwa nao wote wamekutwa na hatia ni pamoja na Prosper Maleto, Seif Mdumuka, Amri Bakari, Said Mdumuka, Ramadhan Athuman na Musa Mohamed.

Aidha, amesema kuwa washtakiwa hao walikutwa na kosa hilo katika eneo la kituo cha ukaguzi cha Kauzeni lililopo Wilaya ya Kisarawe mkoani Pwani kabla ya kufikishwa kortini na kukumbana na adhabu hiyo.

Hata hivyo, ameongeza kuwa katika kosa la kwanza, washtakiwa walihukumiwa kwenda jela miaka 20 kila mmoja na faini kwa kila mmoja, wakati katika kosa la pili, washtakiwa wawili ambao ni hao polisi, walihukumiwa miaka 15 kwenda jela.

Jinsi Punyeto Inavyo Sababisha Ukosefu Na Upungufu Wa Nguvu za Kiume

$
0
0
Ukosefu  na/ama  upungufu  wa  nguvu  za  kiume, ni  tatizo  linalo  wakabili  mamilioni  ya  wanaume  duniani.  Zipo  sababu  nyingi  zinazo  sababisha  tatizo  la  ukosefu  wa  nguvu  za  kiume.  

Miongoni  mwa  sababu  hizo  ni  pamoja  na  maradhi  kisukari, presha,shinikizo  la  damu, moyo, figo, matatizo  kwenye  mishipa  ya  ubongo  &  mishipa  ya  uti  wa mgongo, matatizo  kwenye  mishipa itumikayo  kusafrisha damu  mwilini, maradhi  ya  ngiri,  pamoja  na   upigaji  punyeto  kwa  muda  mrefu.

Katika  makala  yetu  ya  leo, tutaangalia  namna   suala  la  upigaji  punyeto linavyo  athiri  nguvu  za  kiume.

Kabla  hatujaangalia  namna  suala la upigaji  punyeto linavyo  maliza  nguvu  za  kiume, ni  vyema  tukafahamu  kwanza  kuhusu  SAYANSI  YA  MFUMO  WA  NGUVU  ZA  KIUME.

Kufahamu   kuhusu   SAYANSI  YA  MFUMO  WA  NGUVU  ZA  KIUME  tafadhali  tembelea :

Ukisoma  vizuri  kuhusu  mfumo  wa  nguvu  za  kiume, utagundua  kuwa   Suala  la  nguvu  za  kiume  ni  suala  la  kimfumo.  Ili  mwanaume  awe na nguvu  za  kiume, aendelee  kuwa  na  nguvu  za  kiume na  azilinde  nguvu  zake za  kiume, ni  lazima  ogani  zote zinazo  husika  na  mfumo  wa  nguvu  za  kiume  ziwe  na  afya  njema  na  ziwe  na  ushirikiano   thabiti  na  wenye  afya.

Vile  vile , utagundua  kuwa , mambo  makuu  muhimu  katika   mfumo  wa  nguvu  za  kiume  ni  kama  ifuatavyo:

i.Mishipa  imara  ya  ubongo  na  yenye  afya  njema

ii. Mishipa  imara  ya  uti  wa  mgongo  (  spinal  cords )

iii.Mishipa  imara  itumikayo  kusafirisha  damu  mwilini  (  Blood Vessels )

iv. Mfumo  imara  wa  usafirishaji  damu  mwilini

v. Mishipa  ya  uume  iliyo  imara  na  yenye  afya  njema

vi. Uhusiano  imara  na  wenye  afya  kati  ya  mishipa  ya  fahamu  iliyopo  katika  ubongo, mishipa  ya  kwenye  uti  wa  mgongo  pamoja  na  misuli & mishipa  ya  kwenye  uume.

Hivyo  basi, ili  mwanaume  aweze  kuwa  na  nguvu  imara  za  kiume, na  aendelee  kuwa  na  nguvu  hizo ni  lazima  mambo  yote  muhimu  katika  mfumo  wa  nguvu za  kiume  yawe  imara  pasi na  hitilafu  yoyote.

Hitilafu  yoyote  katika  mambo  hayo, itasababisha  ukosefu na/ama  upungufu wa  nguvu  za  kiume  kwa  mwanaume  huyo.  Pale inapotokea    hitilafu  ama  mapungufu  katika  ogani  zaidi  ya  moja  kati  ya  zilizo  tajwa hapo  juu, basi  tatizo  kwa  muhusika  huwa  kubwa  mara  dufu.

JINSI  PUNYETO  INAVYO  SABABISHA  TATIZO  LA  UKOSEFU &  UPUNGUFU  WA  NGUVU  ZA  KIUME.
Mwanaume   anapopatwa na  wazo  la  kufanya  tendo  la  ndoa, ubongo  hutoa  ishara  kwenye  mishipa  ya  uti  wa  mgongo  ambayo  nayo  husafirisha  taarifa  hadi  kwenye  mishipa &  misuli  ya  uume.

Mishipa  ya  uume inapopokea  taarifa  hiyo, hutanuka. Na  mishipa  ya  uume  inapotanuka, hufanya  mambo  mawili  muhimu  sana :

i.Husababisha  mishipa  ya  ateri  kupanuka  na  hivyo  kuruhusu  damu  kuingia kwa  kasi  sana   ndani  ya  mishipa  ya  uume  na  hivyo  kuufanya  uume  usimame  na  kuwa  imara  bara bara.

ii. Huibinya na  kuiziba  mishipa  ya  vena  na  hivyo  kuzuia  kunyonya  ama  kufyonza  damu  iliyo  ingia  ndani  ya  mishipa ya  uume.  (  KAZI  KUBWA  YA  MISHIPA  YA  VENA  ILIYO  KARIBU NA  MISHIPA  YA  UUME  NI KUHAKIKISHA  HAKUNA  DAMU NDANI YA  MISHIPA  YA  UUME. HIVYO  BASI  DAMU  INAPOINGIA  NDANI YA  MISHIPA  YA  UUME, MISHIPA  YA  VENA  HU “SENSE” JAMBO  HILO  KWA  HARAKA  NA HIVYO  KUIFYONZA  DAMU  HIYO  KUTOKA KWENYE MISHIPA  YA UUME  YA  KUITOA  NJE YA MISHIPA  YA  UUME.  NA  DAMU INAPOKOSEKANA  NDANI  YA  MISHIPA  YA  UUME, HUUFANYA  UUME  KUSINYAA  NA  KULEGEA )

Mtu  anayepiga  punyeto  husababisha  mambo  yafuatayo  katika  mwili  wake :

1. Huuwa  nguvu  ya  mishipa  & misuli ya  uume ambayo  ndio  inayo husika  na  kusimama  kwa  uume

2. Mishipa  ya   uume  inapo  sinyaa  na  kukosa  nguvu  yake  ya  asili, husababisha  mambo  yafuatayo :

i.Huondoa  uwezo  wa  mishipa  &  misuli  ya  uume  kutanuka, na  hii  ndio  sababu  inayo  wafanya  waathirika  wa  punyeto  kutumia  nguvu  nyingi  sana  katika  kuufanya  uume  usimame.

ii.Huondoa  uwezo  wa  mishipa &  misuli  ya  uume  kuibana  na  kuiziba  mishipa  ya  vena, na  hii ndio  sababu  inayo  fanya  waathirika  wa  punyeto  kufika  kileleni  haraka  sana, kwani damu  inayo  ingia  kwenye misuli  ya  uume   hufyonzwa  ndani ya  muda  mfupi sana. 
 
 Hii  hutokea  kwa  sababu  mishipa na  misuli  ya  uume inakuwa  imelegea,na  mishipa  ya  vena inakuwa  imepwaya, hivyo  msuguano wowote ule  hufanya  mishipa  ya  vena  kufunguka  na  kufyonza  damu  kutoka  kwenye mishipa  ya  uume  na hivyo  kuufanya  uume  kusinyaa  ndani ya dakika ama sekunde  chache sana.

3. Vile  vile  punyeto  hufanya  uume  kusinyaa na  kurudi ndani  na  kuufanya  uonekane kama  uume  wa  motto mdogo.

Kwa  ufupi  punyeto  husababisha  ukosefu  wa  nguvu  za  kiume  kwa  sababu  kuu  zifuatazo :

i.Kwanza   hudhoofisha  na  kuharibu  mishipa  ya  uume,  ambayo  ndio  hufanya  uume kusimama.

ii.Pili  hudhoofisha  utendaji  kazi  wa  mishipa  ya  ateri, ambayo  ndio  hutumika  kama  njia  ya  kusafirisha  damu kupeleka kwenye  misuli  ya  uume  na  ivyo  kuufanya  uume  usimame

iii. Tatu, punyeto  hupelekea  kuvuja  kwa  mishipa  ya  vena  na  hivyo  kusababisha  damu  kufyonzwa  kwa  haraka  sana  kila  iingiapo ndani  ya  misuli ya  uume  na  matokeo  yake  ni  uume   kusimama  kwa  muda  mfupi  sana  wakati wa  tendo  la  ndoa.

iv. Punyeto  huathiri  mtiririko  wa  damu  kwenda  kwenye  mishipa  ya  uume, kwa  sababu  hudhoofisha  misuli &  mishipa  ya  uume  pamoja  na mishipa ya  ateri  ambayo  ndio  hutumika  katika  kusafirisha  damu kwenda  kwenye  uume

DALILI  ZA  MTU  ALIYE  ATHIRIWA  NA  PUNYETO
Dalili  kuu  za  mtu  aliye athiriwa  na  punyeto  ni  kama  ifuatavyo:

i.           Uume  kusinyaa  na  kuwa  kama  wa  mtoto
ii.         Uume kurudi  ndani
iii.       Uume  kusimama  ukiwa  legelege
iv.       Kufika  kileleni  haraka  wakati  wa  tendo  la  ndoa.

TIBA   YA   NGUVU  ZA  KIUME  KWA MTU  ALIYE  ATHIRIKA  NA  PUNYETO.
Dawa   asilia  ya  nguvu  za  kiume iitwayo JIKO  ni tiba  bora  na  ya  uhakika  kabisa  kwa  mtu  aliye  athiriwa   na  punyeto.  Dawa  hii, pamoja  na  mambo  mengine  mengi, husaidia  kufanya  mambio  yafuatayo  katika  mwili  wa  mwanaume  aliye  athiriwa  na  punyeto :

i.Kuimarisha  mishipa  & misuli  ya  uume  ulio  legea na  hivyo  kuurejeshea  uwezo wake wa  asili

ii. Hutibu   tatizo  la  uume  kurudi  ndani

iii.Humaliza  tatizo  la  kusimama  kwa  uume  ukiwa  legelege

iv.Hutibu  na  kuponya  kabisa  tatizo  la  kufika  kieleleni  haraka.

BEI  YA  DAWA  :  Dawa  hii  inapatikana  kwa  gharama  ya  SHILINGI  ELFU  THEMANINI  TU (Tsh. 80,000/=)

MAHALI  INAPOPATIKANA :  Dawa  hii  inapatikana  katika  duka  la  dawa  asilia  liitwalo  NEEMA  HERBALIST  &  NUTRITIONAL  FOODS  CLINIC  lililopo  jijini  DAR  ES  SALAAM  katika  eneo  la  UBUNGO   nyuma  ya  jengo  la  UBUNGO  PLAZA   karibu  na SHULE  YA  MSINGI  UBUNGO  NATIONAL  HOUSING.

Kwa  wateja  wasio  weza  kufika  ofisini  kwetu. Watafikishiwa  dawa  mahali  popote  walipo  jijini  DAR  ES  SALAAM.

Kwa   wateja  waliopo  mikoani  watatumiwa  dawa  kwa  njia  ya  MABASI

Kwa  wateja  waliopo   Zanzibar  wata fikishiwa  dawa  kwa  njia  ya  usafiri  wa boti.

Na  kwa  wateja  waliopo  UGHAIBUNI  watatumiwa  dawa  kwa  njia  ya  POSTA  ama  DHL.

MAWASILIANO :  WASILIANA  NASI   KWA  SIMU  NAMBA  0766  53  83  84.

Kwa  taarifa  zaidi  kuhusu  huduma  zetu, tutembelee kila  siku  kwenye  blogu  yetu :

Je,una Upungufu Wa Nguvu Zakiume,kukosa Hamu Ya Tendo La Ndoa,kufika Kileleni Mapema Na Kushindwa Kurudia ????

$
0
0

Tatizo la kukosa au kupungukiwa nguvu za kiume na maumbile madogo ya kiume husababishwa na mambo mengi kama,KISUKARI,NGIRI,CHANGO,TUMBO KUUNGURUMA,MAUMIVU YA KIUNO,UNENE KUPITA KIASI,KUJICHUA nk.

Upungufu wa nguvu za kiume husababisha tendo la ndoa kutofanyika kwa kujiami nakwa usahihi nahivyo husababisha ndoa, mahusiano mengi kuvunjika.

BAADHI YA DALILI ZA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NI,
1 KUKOSA HAMU YA TENDOL LA NDOA 
2 UUME KISIMAMA KWA KULEGEA 
3 KUWAHI KUFIKA KILELENI 
4 KUSHINDWA KURUDIA TENDO LA NDOA WAKATI 
5 KUCHOKA SANA BAADA YA ROUND YAKWANZA NAKUKINAI TENDO LA NDOA KABISA.

TUMIA 3 POWER KWA TATIZO LA UKOSEFU(UPUNGUFU)WA NGUVU ZA KIUME NAHAMU YA TENDO LA NDOA.FINA HUBORESHA MAUMBILE YA KIUME KWA KUNENEPESHA KWA SAIZI UIPENDAYO HAIJARISHI UMRI.

PIA KUNA DAWA ZA KURUDISHA MPENZI KWA MUDA MFUPI SANA NAZAKUPATA KAZI,KESI,KUDHULUMIWA,NK 

WASILIANA NA SHEIKH OMARY AKUTATULIE MATATIZO YAKO HATA KAMA UMEHANGAIKA SANA PASIPO MAFANIKIO 

 SIMU; NO 0767145357/0629034550.

Zitto Kabwe afunguka alichoambiwa na Lissu hospitalin

$
0
0
Mbunge wa Kigoma Mjini Zitto Kabwe amefunguka na kudai amerudi nchini akiwa na unyenyekevu mkubwa zaidi kwa sababu ya nguvu na ujasiri alioonyeshwa na Mbunge Tundu Lissu pindi alipokwenda kumjulia hali katika hospitali ya Nairobi nchini Kenya.

Zitto ameeleza hayo kupitia ukurasa wake wa facebook asubuhi ya leo na kusema japo Lissu ameumizwa sana lakini hakuacha kumuonyesha ucheshi licha ya kuwa na maumivu makali aliyokuwa nayo katika mwili wake.

"Siku mbili hizi nilizoenda kumuona Lissu zimeniacha nikiwa mawazo sana, nimerudi nchini nikiwa kwenye unyenyekevu zaidi kwa sababu ya nguvu na ujasiri ambao ndugu yangu amenionesha licha ya kuwa kwenye maumivu makali. Siyo mara nyingi hapa nchini kusikia tukiongelea ujasiri lakini namfikiria lissu na vile nilivyojisikia nikiwa pamoja naye Nairobi, najua hivyo ndivyo alivyo", ameandika Zitto.

Pamoja na hayo, Zitto ameendelea kwa kusema "waliomshambulia wamemuumiza kweli na bado wakati tuliokuwa naye amenionesha shukrani, ari na pia ucheshi. Huo ni ujasiri, alichopitia na anachoendelea kupitia Lissu siyo kitu rahisi kwa mtu yeyote kutafakari. Kufikiria hali ile kungeniacha niumie moyo kama asingesema maneno haya kwangu kuwa  'tumeshinda. Tumeshashinda", amesisitiza Zitto.

Mbunge Tundu Lissu alishambuliwa kwa risasi na watu wasiojulikana Septemba 7, 2017 akiwa Makao Makuu ya nchi mjini Dodoma na baadaye kusafirishwa kwenda jijini Nairobi Kenya kwa ajili ya kupatiwa matibabu kufuatia majeraha aliyopata, ambapo mpaka sasa yuko huko kwa matibabu.

VIDEO: Msigwa, Lema watema cheche Nairobi wakihojiwa kuhusu Tundu Lissu

$
0
0
Wabunge wawili wa Chadema wametumia mahojiano nje ya nchi kuzungumzia matatizo ya Tanzania wakisema hayawezi kumalizwa na mtu mmoja bali kwa mifumo imara ya mihimili ya Mahakama, Bunge na Serikali.

Wakizungumza katika mahojiano na Kituo cha Televisheni cha KTN cha Nairobi, Kenya  jana Jumapili walisisitiza umuhimu wa kuwa na Katiba Mpya ili kuipa nguvu mihimili hiyo.

Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema alisema ufisadi ambao Rais John Magufuli anaushughulikia sasa ulifanywa na watendaji waliokuwa chini ya Chama cha Mapinduzi (CCM).

Alisema chama hicho kimeongoza nchi tangu Tanzania ilipopata Uhuru, hivyo ufisadi huo ulifanywa na viongozi waliokuwa chini ya chama hicho.

“Ili tuwe na mfumo wenye nguvu tunatakiwa kubadilisha Katiba ili tuwe na Mahakama na Bunge huru,” alisema.

Lema alisema kumtegemea mtu mmoja hakuwezi kuleta mafanikio kama ambayo yamefikiwa na Kenya.

Alisema Katiba ikibadilishwa na kuwa na vipengele mbalimbali, vikiwemo vya kuwa na Tume Huru ya Uchaguzi na kumshtaki Rais akitoka madarakani Tanzania itakuwa imepiga hatua.

Alisema mabadiliko ya Katiba nchini Kenya si tu yataisaidia katika siasa bali katika kukuza uchumi wao.

“Uamuzi wa Mahakama ya Juu ya Kenya kufuta matokeo ya Rais si tu yatawasaidia kisiasa bali yatajenga imani hata kwa wawekezaji,” alisema.

Alisema wawekezaji wataongezeka nchini Kenya kwa sababu wanakuwa na imani na Mahakama.

Kwa upande wake, Mbunge wa Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa alisema Rais ana nguvu kuliko mihimili mingine na amekuwa akitoa maelekezo kwa mihimili hiyo.

“Bunge la Tanzania limetekwa na Serikali, wenzetu CCM wako wengi kuliko sisi wapinzani, wakikaa kwenye Party Caucus (vikao vya chama) yao wanaamua mambo yenye manufaa kwa chama chao,” alisema.

Alisema madhara ya wabunge wa CCM kufanya uamuzi wenye manufaa kwa chama hayawaathiri wapinzani tu, bali Watanzania kwa jumla.

Wabunge hao wako jijini Nairobi kumjulia hali Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu aliyelazwa katika Hospitali ya Nairobi baada ya kupigwa risasi Septemba 7 mwaka huu akiwa nyumbani kwake Area D, mjini Dodoma.

==>Wasikilize hapo chini

Upelelezi kesi ya Aveva, Kaburu umekamilika

$
0
0
Upelelezi wa awali katika kesi ya utakatishaji fesha inayowakabili Rais wa Simba SC, Evans Aveva na Makamu wake, Geofrey Nyange ‘Kaburu’ umekamilika katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.

Wakili wa Serikali, Nassoro Katuga amemueleza Hakimu Mkazi Mkuu, Victoria Nongwa leo September 18, 2017 kuwa, upelelezi wa awali wa kesi hiyo umekamilika ambapo jalada la kesi limepelekwa kwa Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) ili alisome na kueleza kama anaona umekamilika au la.

Baada ya kuelezwa hayo, Hakimu Nongwa aliahirisha kesi hiyo hadi September 27, 2017.

Aveva na Kaburu wanashtakiwa na TAKUKURU wakikabiliwa na tuhuma za kughushi nyaraka za Klabu ya Simba na kutakatisha fedha kiasi cha dola za Marekani 300,000 (zaidi ya Sh milioni 650) na wamekuwa rumande tangu Juni 29, mwaka huu.

Upelelezi uliokuwa unafanyiwa kazi ni nyaraka za kughushi maandiko zilizokuwa zimepelekwa kwa mtaalam kufanyiwa uchunguzi ili kubaini makosa hayo.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images