Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Gazi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0
Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Tupo Mbagala

Msigwa: Tuko Wabung Wanne CHADEMA Tunaowindwa

$
0
0
Mbunge wa Iringa Mjini kwa tiketi ya CHADEMA Peter Msigwa amefunguka na kutaja majina ya wabunge wengine wa nne ndani ya CHADEMA ambao wamekuwa wakiwindwa na watu wasiojulikana ili kushambuliwa kama alivyoshambuliwa Mbunge Tundu Lissu.

Msigwa amesema hayo leo akiwa jijini Nairobi nchini Kenya ambapo yupo huko kwa ajili ya kumuangalia Mbunge Tundu Lissu aliyeshambuliwa kwa risasi Septemba 7 mwaka huu mjini Dodoma

 Msigwa ametumia nafasi hiyo kutoa taarifa kwa vyombo vya usalama kuwa hata wao wanatafutwa na watu wasiojulikana ili kupigwa risasi.

"Usalama wetu upo mashakani niwaambie usalama wa taifa, nimwabie Mkuu wa Majeshi, nimwabie IGP pamoja na Rais mwenyewe tunawindwa wabunge wengine wanne wa CHADEMA akiwepo Mhe. Freeman Mbowe, mimi vijana wale walinifuata wiki mbili zilizopita Iringa, Mhe Godbless Lema alifuatwa Arusha, Halima Mdee na Mhe. Mbowe tupo kwenye orodha hiyo ya kuuwawa" alisema Mchungaji Msigwa

Aidha Mchungaji Msigwa ameendelea kusema licha ya vitisho hivyo wao wataendelea kuzungumza na kukemea mambo ambayo yapo kinyume na utaratibu na sheria za nchi na kusema hawataogopa.

"kwa hiyo hizo roho zetu tumeziweka mikononi mwenu lakini tunasema kwamba hatutanyamaza tutakosoa, tukakemea, na kupinga uonevu wowote katika nchi yetu, kwa haya mambo hamtatutisha wala kutunyamazisha tunaendelea kusonga mbele" alisema Mchungaji Msigwa.

Peter Msigwa: Ndugai Alipaswa Kuwa GEREZANI Muda Huu na Sio Bungeni

$
0
0
Mbunge wa Iringa mjini kwa tiketi ya CHADEMA, Mchungaji Peter Msigwa ameibuka na kumvaa Spika wa Bunge Mhe.Job Ndugai kwa kumwambia hana sifa ya kuwa kiongozi wa kusimamia nidhamu ndani ya bunge bali alipaswa kuwa gerezani muda huu.

Peter Msigwa ameleza hayo mchana wa leo alipokuwa mjini Nairobi nchini Kenya kumjulia hali Mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lissu aliyeshambuliwa kwa kupigwa na risasi na watu wasiofahamika katika siku za hivi karibuni na kupelekea kuamsha hisia za watu wengi juu ya jambo hilo ambalo halikuwahi kutegemewa kutokea Tanzania nchi yenye amani na usalama wa kutosha.

"Ninaomba mumuogope Mungu kwa sababu tunaleta mchezo na maisha ya Watanzania, mnataka kutunyamazisha ili tusiseme. Tutasema mpaka mwisho wetu kwa sababu uhai wetu na usalama wa taifa letu umetishiwiwa kwa kiwango cha juu sana lakini Mhe. Ndugai wewe kama spika unasifa gani ya kutuambia sisi tuwe na adabu ndani ya bunge wakati wewe mwenyewe kipindi cha kampeni ulionekanaa ukipiga watu hadharani na fimbo, ulitakiwa uwe gerezani na siyo kutusimamia nidhamu ndani ya bunge", amesema Msingwa.

Pamoja na hayo, Msigwa ameendelea kwa kusema "Nakuchukulia Mhe. Job Ndugai kama wewe ni adui, yaani wewe ni adui wa usalama wa taifa la Tanzania kwa sababu unasababisha muhimili wa bunge uwe dhaifu kutokana na serikali ya Tanzania imekuteka na kukupa maagizo na kulifanya bunge liwe butu, lishindwe kusimamia maamuzi na kulisimamia serikali. Nasema haya kwa ujasiri mkubwa sina kitu cha kuogopa tena kama ndugu yetu ameshapigwa risasi na tumeshaambiwa tunaofutwa ni sisi hivyo hatuna cha kuogopa kusema jambo lolote", amesisitiza Msigwa.

Kwa upande mwingine, Mchungaji Msigwa amedai muda mwingine wanashindwa hata kuwaambia watoto wao kuwa Mhe. Job Ndugai ni kiongozi wao wa bunge kwa kuwa wanatishwa, wanafukuzwa pamoja na kupigwa pingu huku akisisitiza kuwa yupo tayari kufukuzwa bungeni lakini hatoweza kukaa kimya.

Halima Mdee Agoma Kujisalimisha kwa DCI

$
0
0

Mbunge wa jimbo la Kawe jijini Dar es salaa Halima James Mdee amesema hajaenda kuripoti kwa DCI kama ilivyotakiwa kwa sababu yeye hajaitwa rasmi.

Mdee amesema DCI ametoa tangazo la ujumla, lakini yeye binafsi hajapewa wito wowote, hivyo hawezi kwenda kutokana na taarifa hiyo.

"Mimi nimesikia tangazo la ujumla, wakiniita in personel Halima njoo nitaenda na hakuna popote kwenye kauli yao iliposema Halima Mdee njoo, lakini siwezi kwenda kwa 'general statement', amesema Halima Mdee

Juzi Jeshi la Polisi liliwataka watu wote waliopost kwenye mitandao ya kijamii kuhusu askari wao aliye nchini Nairobi wakimuhusisha na kumfuatilia  Tundu Lissu nchini Kenya kwenye matibabu na kutakiwa kuripoti wenyewe kwa DCI, kabla ya kitengo cha sheria za makosa ya mtandaoni hakijawachukulia hatua zaidi.

Mbunge wa CCM Asimulia Alivyowadhamini CHADEMA Kupata Ndege ya Kumbeba Tundu Lissu Kumpeleka Kenya

$
0
0
Mbunge wa Mpendae (CCM) Salim Hassan Turky amefunguka na kusema CHADEMA ndiyo imelipa gharama za ndege iliyombeba Tundu Lissu kutoka Dodoma kwenda Kenya na kusema yeye aliwadhamini wakati huo kwa kuwa hawakuwa na fedha taslimu za kulipa

Salim Hassan Turky ametoa ufafanuzi huo leo baada ya kuwepo kwa taarifa kuwa Mbunge huyo ndiye aliyelipia gharama za ndege iliyombeba Tundu Lissu kutoka Dodoma kwenda Kenya kwa matibabu, taarifa ambayo imetolewa na Spika wa Bunge jambo ambalo CHADEMA wamelipinga na kusema Spika anapotosha umma juu ya jambo hilo. 

“Tusifanye tukio la Tundu Lissu kuwa la siasa. Mimi binafsi tukio zima la mbunge mwenzangu limenisikitisha sana limenisononesha sana. Nikiwa kama kamishna wa Bunge lakini pia ni binadamu kuna kuzaliwa na kufa,”amesema.

“Kwa hiyo tukio hilo lilipotokea tuliitwa na makamishna wote na Spika wetu wakiwemo Mbowe (Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani) Msigwa na timu yake. Kwanza ndege ilikuwepo pale Airport ambayo ilikuwa imeshaagizwa na Bunge iko stand by kumpeleka moja kwa moja Muhimbili.”

Amesema walichoamua ni kuwa aende moja kwa moja Nairobi nchini Kenya lakini ndege hiyo haikuwa na kibali cha kwenda nchini humo na kwamba ili uweze kwenda nchini humo unalazimika kuwa na marubani wawili.

Hata hivyo, amesema Spika Ndugai alihangaika kupata kibali cha ndege iliyokuwepo uwanjani ili iweze kumpeleka mgonjwa Nairobi.

“Wakati mambo yote tayari rubani wa ndege akasema kuna kitu kinaitwa landing Instrument ambayo ile ndege haina kwa hiyo haitaweza kuruka,” amesema.

Amesema kutokana na majibu hayo waliingiwa na sitofahamu watafanya nini lakini yeye aliingia katika uzoefu wake aliopewa na Mungu kwa kutafuta ndege kwa ndugu zake ambao wanafanya nao biashara sana.

“Nikawaambia ndege ipo wakatoa nauli zao za ghali ghali kwa sababu tunajuana wakakubali kutusaidia kwa dola 9,200 pamoja na ambulance (gari la wagonjwa) mimi ndio niliyoita kwa kubaliana na Mbowe na Msigwa kwamba Turky haya mambo yasimamie baadaye…na ndicho kilichofanyika,” amesema.


Aidha Turky aliendelea kueleza kuwa walipofika nchini Kenya siku ya pili walipaswa kuwa ametoa fedha hizo lakini haikuwa hivyo mpaka leo Septemba 14, 2017 majira ya saa sita mchana alipowasiliana na wahusika aliambiwa kuwa CHADEMA walikuwa wameshalipa hizo fedha.

Mbali na hilo Turky amesema kuwa kauli ambayo Spika wa Bunge Job Ndugai ameisema leo bungeni haikuwa na tatizo kwani alikuwa amesema yeye ndiye amelipa hiyo fedha lakini CHADEMA wangekuja kuirudisha kwake, jambo ambalo anadai kama leo wasingeweza kulipa CHADEMA basi angelipa yeye fedha hizo kwa watu hao halafu yeye angekuja kumalizana na CHADEMA.

Pia katika kauli ambayo ametoa Mbunge wa Iringa Mjini Peter Msigwa amesema kuwa fedha hizo za ndege iliyombeba Tundu Lissu kutoka Dodoma kwenda Nairobi nchini Kenya imelipwa na Watanzania ambao walikuwa wanachangia fedha za matibabu kwa Lissu pamoja na CHADEMA wenyewe na si mbunge wa CCM.

Update Toka kwa Mbowe: Tundu Lissu Kwa Sasa Anaweza Kuongea na Kula Kidogo

$
0
0
Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe amesema kuwa hivi sasa Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu anaweza kuongea na kula kidogo.

Akizungumza na waandishi leo Alhamisi jijini Nairobi, Mbowe amesema taarifa za kwamba Lissu amepata maambukizi katika kifua ambayo yanatishia maisha yake siyo za ukweli.

Mbowe amesema hali ya Lissu inabadilika kila siku hivyo amewahakikishia wananchi kuwa anaendelea kurejea katika hali yake.

Amesema Lissu ameweza kuonana na baadhi ya waliomtembelea kwa maelekezo ya madaktari ambao wanamtibu.

"Pamoja na kwamba kuna watu wengi wanataka kumuona lakini ni wachache wanaoruhusiwa kumuona kwa kuwa madaktari wanataka apumzike,"amesema Mbowe.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 15

Misukule Wa Nguvu Za Kiume

$
0
0
IMESIMULIWA  NA  DOKTA  MUNGWA  KABILI
SIMU  :  0744  -  000  473 .

MISUKULE   WA  NGUVU  ZA  KIUME
Msukule  ni nini ?
Msukule  ni  mtu  au  sehemu  ya  mtu  iliyo  chukuliwa  na  kufichwa kichawi  kwa  lengo  la  kutumikishwa  kazi  na  shughuli  mbalimbali   za kichawi.

Misukule  wengi  wanao  chukuliwa , huchukuliwa  kwa  lengo  la  kutumikishwa  kwenye  mashamba, biashara,migodi, uvuvi, masokoni, madukani, ulinzi  na  kwenye  shughuli  mbalimbali  za  kichawi.

Kwa  ufupi  misukule  wengi  huchukuliwa  kwa  sababu  ya   masuala  ya  mali  na  utajiri  wa  kichawi.

Misukule  wengine  huchukuliwa  kwa  ajili  ya  kufanya  kazi  ya  chuma  ulete. Hawa  ni  maarufu  miongoni  mwa  wale  ndugu  zangu  wanao pewa  utajiri  wa  punje  za  kuku.

Kwa  msio fahamu  kuhusu  utajiri  wa  aina  hii  ni  kwamba,  kuna  vijiji  fulani  vipo katika  wilaya  mbili  maarufu  huko  nyanda  zap  juu  kusini, hutolewa  utajiri  wa  kichawi  maarufu  kama  utajiri  wa kudonoa  ama  utajiri  wa  kuku, ama utajiri  wa  kuuza  miaka.

Mtu  anayefanyiwa  kafara  hii   huingia  agano  maalumu  la  kichawi   la  kuuza  haki  yake  ya  kuishi  duniani.

Mtu huyu  atatazamwa  kichawi  ili kubaini  amebakiza  miaka  mingapi  ya  kuishi  hapa  duniani.

Kama  amebakiza  miaka  ishirini  basi  ataingizwa   katika mkataba  na  wachawi  kutoa  sadaka  baadhi  ya  miaka  yake .   Mfano   katika  miaka  ishirini  iliyo baki,  anaweza  akaambiwa  atoe  miaka  kumi  au  kumi  na  tano  au  minane .

Kitakacho  amua  idadi  ya   miaka  ya  kuishi  ya  mtu huyo  ni jini aliye  katika  mfumo  wa  kuku.

Zitachukuliwa  punje  za  mchele  zitawekwa  ardhini  halafu  kuku  huyo  ataanza  kudonoa  punje  moja  baada  ya  nyingine.

Idadi  ya  punje  atakazo  donoa  kuku  huyo  ndio  idadi  ya  miaka  ambayo  mtu  huyo  ataishi. Kama  miaka  ya  kuishi  ya  mtu  huyo  ni  ishirini  halafu kuku  akadonoa  punje  kumi  na  mbili, basi  maana  yake  ni kwamba  mtu huyo  ataishi  miaka  kumi  na  mbili  ya  utajiri  mkubwa  halafu  miaka  minane  iliyo  baki  ataenda  kuitumikia  kama  msukule.

Kinacho  tokea  hapo  ni  kwamba, muda  wa  mtu  huyo unapomalizika, mtu  huyo  anachukuliwa  kama  msukule  na  kwenda  kutumikishwa  kwenye  migodi  iliyopo  huko  Congo   au kutumika  katika  kuhamisha  mali  za  mtu  ambae  muda  wake  wa  kuishi  kitajiri  umekwisha  kwenda  kwa  mtu  mpya  ambae  anakuwa  ameingia  kwenye  mkataba  huu  wa  utajiri  wa  kichawi.

  Nitalizungumzia  kwa  kina  suala  hili  katika  makala  zangu  zijazo.

Kama  nilivyo  dokeza  hapo  awali, msukule  anaweza  kuchukuliwa  kama  mtu  mzima, au  sehemu  ya  mtu  kama  vile  akili, nyota  ya  mtu, nguvu  za  kiume, mbegu  za  uzazi  kwa  wanaume  au  mayai  ya  uzazi  kwa upande  wa  wanawake , jicho moja , macho  yote  mawili  nakadhalika.

Msukule  huitwa  jina  tofauti  kulingana  na  sehemu  ya  mwili  wake  iliyo  chukuliwa  msukule.   Kwa  mfano, mtu  aliye  chukuliwa  akili  zake  huitwa  ndondocha

Watu  wengi  wanafahamu  kuhusu  watu  kamili  walio  chukuliwa  misukule lakini  hawajui  kuhusu  watu  ambao  wamechukuliwa  nguvu  za  kiume.

NI   NANI   HAWA   MISUKULE  WA  NGUVU   ZA  KIUME  ?
Msukule  wa  nguvu  za  kiume  ni  mwanaume  mwenye  kusumbuliwa  na maradhi  ya  nguvu  za  kiume  yanayo  tokana  na  kurogwa.

Msukule  wa  nguvu  za  kiume  ni  mwanaume  ambaye  nguvu  zake  za kiume  zimechukuliwa   na  kufichwa  kichawi  kwa  lengo  la   kutumikishwa  kama  msukule.

Msukule  wa  nguvu  za  kiume  ni  mwanaume  ambae  nguvu  zake  za kiume  zimetolewa  kafara  kwa  ajili  ya  mali, biashara  na  utajiri  wa  kifisadi  ama  utajiri  wa  kichawi.

  AINA  ZA  MISUKULE  WA  NGUVU  ZA  KIUME

 Misukule  wa  nguvu  za  kiume  wapo  wa  aina  kuu  mbili  :

AINA  YA  KWANZA

MISUKULE  WA  NGUVU  ZA  KIUME  AMBAO  WAO  WENYEWE  WAMEZITOA  KAFARA  NGUVU  ZAO  ZA  KIUME.
Aina  hii  ya  misukule  haijulikani  na  wengi  lakini  kiuhalisia  wapo  wanaume  wengi  sana  ambao  wao  wenyewe  kwa  ridhaa  yao  wenyewe  wameamua  kutoa  kafara  nguvu  zao  za  kiume  kwa  lengo  la  kupata  mali  na  utajiri.

Hapa  mwanaume  anaenda  kwa  mganga  kwa  ajili  ya  kupata  mali  na  utajiri, anapewa  sharti  la  kutoa   nguvu  zake  za  kiume  ili  awe  tajiri.

Mwanaume  huyo  atatakiwa  kutoa  mbegu  zake  za  kiume  ambazo  zitatengenezwa  kichawi  na  kutumika  kama  kafara  ya  mali  na  utajiri.

Kafara  hii  huwa  ni  kafara  nzito  sana !

Kwa  maana  nyingine,mwanaume  aliye  ingia  katika   mkataba  huu  wa  kichawi, anakuwa  ameingia  mkataba  wa  kutoa  watoto  wake  ambao  bado  hawajazaliwa.

Mara  nyingi  mkataba  huu  huwa  ni  kuwadumu  yaani  mwanaume  huyo  atakuwa  hivyo  hivyo  katika  siku  zote  za  maisha  yake  na  huwa  na  masharti mazito  na  inapo tokea  mwanaume  huyo  akakiuka  mojawapo kati  ya  masharti  atakayo  pewa, adhabu  yake  huwa  nzito.

Wanaume  walio  katika  kundi  hili  wao  hawana  shida  kabisa  na  suala la  wao  kutokuwa  na  nguvu  za  kiume  kwa  sababu  tayari  wanajua  nini  chanzo  cha  tatizo  lao.

Maelezo  kuhusu  wanaume  walio  katika  kundi  hili  ni  marefu  sana kiasi siwezi  kuyaelezea  yote  hapa, ila  nina  ahidi  nitakapo  pata  muda  siku  za  mbeleni  nitaelezea  kwa  kina.

MISUKULE   WA  NGUVU  ZA  KIUME  AMBAO  NGUVU  ZAO  ZIMECHUKULIWA  KICHAWI BILA  RIDHAA  YAO   WALA  BILA  KUJUA.

Idadi  kubwa  ya  misukule  wa  nguvu  za  kiume  ipo  kwenye  kundi hili. Hawa  ni  wanaume  ambao  nguvu  zao  za  kiume  zimeibwa  ama kuchukuliwa  na  kufichwa  kichawi  kwa  ajili  ya  kutumikishwa  kichawi.

Ni  wanaume  ambao  nguvu  zao  za  kiume  zimechukuliwa  bila  ridhaa  yao .

Ni  wanaume  ambao  nguvu  zao  za  kiume  zimechukuliwa  bila  wao  kujua  kama  nguvu  zao  zimechukuliwa .

Wachawi  wana  amini  kuwa, njia  bora  na  ya  uhakika  ya  kuiba  kichawi ama  kuchukua  kitu  cha  mtu kichawi   bila  ridhaa  yake  ni  kukichukua  kitu  hicho  bila  mhusika  kujua  kama  kitu  chake  kimechukuliwa.

Huamini  pia   ili  jambo  hili  liweze  kufanikiwa  ni  lazima  umbadilishie  mhusika  na  kitu  kingine  kinacho  fanana  na  kitu  ulicho  kichukua  kutoka  kwake  ili  mhusika  asijue  kama  kitu  chake  kimechukuliwa.

Wakati  wanaume  walio  katika  kundi  la  kwanza  nguvu  zao  za  kiume  wamezitoa  kwa  ridhaa  yao  wenyewe   kwa  ajili  ya  kupata  mali, fedha  na  utajiri  wa  kichawi, wanaume  walio  katika  kundi  hili  la  pili, nguvu  zao  zimechukuliwa  bila  ridhaa  yao  wala  bila  wao  kujua  na  kama  hiyo  haitoshi  watu  wengine  wananufaika  nazo  bila  wahusika  kujua chochote kinacho  endelea.

Wanaume  hawa  ndio  wanaume  walio  katika  kundi  baya zaidi  kwa  sababu  wao  wanakuwa  hawajui  chochote  kinacho  endelea  kuhusu  nguvu  zao.

Na  kwa  kuwa  wanakuwa hawajui  chanzo  cha  tatizo  lao, basi  hubaki  kuhangaika  na  kuteseka  katika  maisha  yao  yote.

Mara  nyingi  wanakuwa  wana  amini  maradhi  yao  ya  nguvu  za  kiume  yamesababishwa  na  mambo mbalimbali  kama  vile  maradhi  ya  kisukari, presha, ngiri, chango  la  uzazi  nakadhalika, lakini  kiukweli, maradhi  yao  yanakuwa  yamesababishwa  na   kurogwa.  Nguvu  zao  zinakuwa  zimechukuliwa  kwa  ajili  ya  kutumikishwa  kichawi.

  NI KATIKA  MAZINGIRA  YAPI  NGUVU  ZA  KIUME  ZA  MTU  ZINAWEZA  KUCHUKULIWA  KICHAWI.
 Nguvu  za  kiume  huwa  zinachukuliwa kichawi   kupitia  mbegu  za  kiume  za  mwanaume  aliye  kusudiwa.

Mbegu  hizo  zaweza  kuwa  zimetoka  kwa  kulazimishwa  au  zaweza  kuwa  zimetoka  kwa  ridhaa  ya  mwanaume  husika.

Vile  vile  mbegu hizo  zaweza  kuwa  zimetoka  bila  mwanaume  husika  kujua  au  bila  kuwa  na  uweze  wa  kucontrol zisitoke .

Matumizi  na  mahitaji  ya  mbegu  za  kiume  yatategemea  na  namna  ambavyo  mbegu  hizo  zimepatikana. Kila  namna  ina  matumizi  yake  ingawa  zote  hutumika  katika  matumizi  mbalimbali  ya  kichawi.

MBEGU  ZA  KIUME  AMBAZO  ZIMETOKA  KWA  KULAZIMISHWA

Hizi   ni mbegu  zinazo  toka  baada  ya  mwanaume kufanya  punyeto. Wachawi  wanazihitaji  sana  mbegu  za  namna  hii  kwa  ajili  ya  kufanya  mambo yao  ya  kichawi  na  moja  kati  ya  matumizi  ya  mbegu  hizi  ni  katika  ulozi  wa  mapenzi.  Kumvuta  mwanaume  kimapenzi  kwa  nguvu. Kijana  unae  jishughulisha  na  biashara  hii  nakushauri  uache  mara  moja.

MBEGU    ZA  KIUME  AMBAZO  ZIMETOKA  KWA  RIDHAA  YA KE

Hizi ni mbegu zinazo  toka  baada  ya  mwanaume  kufanya  mapenzi na  mwanamke.

MBEGU  ZINAZO  TOKA  BILA  MWANAUME  KUJUA AU BILA  KUWA  NA  UWEZO  WA  KUZI CONTROL

Hizi  ni mbegu zinazo  toka pindi mwanaume  anapokuwa  anafanya  mapenzi  na  jinni  mahaba  usingizini.  Wachawi  wanazihitaji  sana  mbegu hizi  kwa  ajili ya  matumizi  yao  ya  kichawi.  Unashauriwa  kutosema  kwa  mwanamke  ambae  umelala  nae kama umeota  usiku  unafanya  mapenzi  na  mwanamke  halafu ukamwaga  au umeamka  asubuhi  umekuta  mbegu zimetoka zenyewe.

NGUVU  ZA  ZINAWEZA  KUCHUKULIWA  VIPI  KICHAWI?

Najua  utakuwa  unajiuliza  na  kushangaa, nguvu  za  kiume  za mtu  zinaweza  kuchukuliwa  vipi  au katika  mazingira  yepi.

Nguvu  za  kiume  zinaweza  kuchukuliwa  katika  namna , njia  na  mazingira  tofauti tofauti.  Yafuatayo  ni  mazingira   ambayo nguvu  za  kiume  zinaweza  kuchukuliwa  kichawi.

NGUVU  ZAKO ZA  KIUME  ZINAWEZA  KUCHUKULIWA  KUPITIA  MCHEPUKO  WAKO

Hii  hutokea  mara  nyingi  sana  na  nnaweza  kusema  idadi  kubwa  ya  wanaume  ambao  nguvu  zao  zimechukuliwa  kichawi    ni  kupitia  michepuko  yao.

Kinacho  tokea  hapa  sio  kwamba  mchepuko  wako  ndio  ana  zifunga  nguvu  zako, la  hasha  isipokuwa  mchepuko  anakuwa  ameenda  kwa  wachawi  kuomba  ndumba  za  kukufunga   kimapenzi na  kukutuliza  au / na  ndumba  za  kukufanya  ukienda  kutembea  na  mwanamke  mwingine  usisimame. Yeye  lengo  lake  linakuwa  ni zuri  lakini katika  mchakato  wa  lengo  lake  hilo  linaweza  kutokea suala  la  kufunga  nguvu  zako.

Mganga  atamwambia  huyo  mchepuko  wako, NENDA  KALETE  MBEGU  AMA  SHAHAWA  ZA  HUYO MWANAUME  ULIYE  KUJA  KUMREKEBISHA.

Mbegu  zako  za  kiume  atazichukua  katika  mazingira  yafuatayo :

Mosi :  Kama  huwa  mnafanya  tendo  la  ndoa  bila  kinga, ukisha  kojoa  atajifuta  na  kitambaa  maalumu  atakacho  pewa  kisha  atakipeleka  kwa  mtaalamu.

Pili :   kama  huwa  mnatumia  kinga, ataomba  akufute  na  kitambaa  kwenye  uume  wako  mara  baada  ya  kumaliza  kufanya  tendo.

Au  kama  ataona  utamstukia  anaweza  hata  asihangaike  kukufuta  nazo  ila  atakacho kifanya  ataenda  kumwaga  chooni  au  kwenye  dustbin , dawa  maalumu  ya  kichawi  ambayo  atakuwa  amepewa  na  mganga.

Kumwaga  dawa  kwenye  dustbin au  chooni  kutategemea  na  wewe  kondomu  yako  umeitupa  wapi  baada  ya  tendo.

Kama  uliitupa  kwenye  dustbin  basi, hiyo dawa  ataimwaga  kwenye  dustbin. Atakutegea  umeenda  bafuni au chooni, basi  atamwaga  dawa  hiyo  kwenye  dustibin

Na  kama  kondom yako  iliyo tumika  utaenda  kuitupa  chooni basi  dawa  hiyo  ya  kichawi  itaenda  kutupwa  chooni pia.

Dawa  hiyo ni dawa  ya  kijini  ambayo  kazi  yake  ni  kuchukua mbegu  zilizotupwa  jalalani  au  chooni  na   kuzipeleka  kwa  wachawi  kwa  ajili  ya  matumizi  mbalimbali  ya  kichawi.

Dawa  hii  inayo tupwa  chooni  au  kwenye  dustbin huwa  inatupwa  kwa  lengo  la  kwanza kwenda  kuzikomboa  shahawa  ambazo  zimetupwa  kwenye  dustbin au  chooni  kutoka  kwa  majini  wa  jalalani  na  chooni kisha  kuzipeleka  mahali  zilipo kusudiwa.

Hii ni kwa  sababu, chooni  na  kwenye  dustbin pia  kuna  majini  wachafu . Ukitupa  mbegu  zako  chooni  au  kwenye  dustbin maana  yake  ni kwamba  unakuwa  umefungamanisha  nyota  yako  na  majini  wachafu  wa  chooni  au  jalalani.

Ni nuksi kubwa  sana  kutupa  kondomu  iliyo tumika  chooni  au  jalalani  au kwenye  dustbin,  kwani  majini  wa  maeneo  hayo  watakuingia  kupitia  mbegu  zako  na watajifungamanisha  na  nyota  yako  na  nafsi  yako.

Dalili  utaanza  kuziona  kupitia  kwenye  udhaifu  wa  nguvu  zako  zap  kiume  ambao utaendana  na  kufifia  kwa  nyota  yako  kwa  kasi ya  ajabu.

Mambo  yako  yote  yatakuwa  machafu  kama  choo  au  jalala. Kuanzia  kazi, biashara,mahusiano, afya  yako ikiwemo  nguvu  zako  za  kiume.

Mchepuko  wako  akisha  zipeleka  mbegu zako  kwa  mganga, mganga  ataziweka  kwenye  chungu au kibuyu  maalumu , zitapikwa  pamoja  na  dawa  maalumu  za kichawi  kwa  ajili  ya  kuzipima au kupima  nyota  yako kupitia  mbegu  zako.

Mganga  akigundua  nyota  ya  mwanaume  husika  ipo  juu  basi  atazichukua  mbegu hizo  haraka  sana  na  kuzitengeneza  kichawi   kwa  ajili  ya  ima  kuwauzia  wachawi ama  wafanya  biashara   wanaonunua  misukule  ya  nguvu  za  kiume kwa  ajili shughuli  zao  mbalimbali  ima  kukutengeneza  ndondocha.

Kwenye  kumtengeneza  ndondocha  mwanaume  kwa  kutumia  mbegu  zake  za  kiume   huwa  inakuwa  hivi, huyo  mwanamke  akisha  zichukua  mbegu  hizo  na  kuzipeleka  kwa  mganga, inafanywa  kafara  maalumu  ya  mnyama, halafu hizo  mbegu  zinapikwa  na  dawa  maalumu  za  kichawi  halafu huyo mwanamke  anachanjiwa  kwenye  pande  kuu  saba  za  mwili  wake.

Ni  uchawi  mzito  sana  huu. Matokeo  yake  ni kumfanya  mwanaume  huyo kuwa  ndondocha  na  zezeta  kwa  mwanamke  huyo. Pesa  zote  anazo  zipata  mwanaume  huyo  anakuwa  anazipeleka  kwa  mwanamke  aliye tengeneza  uchawi  huo.

Mbegu  za  kiume  za  mwanaume  zinaweza  kuchanganywa  na  dawa  maalumu  za  kichawi, akalishwa  kinyonga  na  kuunguzwa  mzima mzima, halafu  mwanaume  huyo  akailishwa  dawa  hiyo  huku  lengo   likiwa  ni kumtenganisha  na  familia  yake  na  kuwa  anawageuka  na  kuwabadilikia  kama  kinyonga.

Njia  nyingine  mbegu  zako za  kiume  zinaweza  kuchukuliwa  kwa  njia  ya  jini mahaba. Unaota  usiku unafanya  mapenzi  na  jini  mahaba  hadi  unafika  kileleni, kumbe  lengo lilikuwa  ni  kuchukua  mbegu zako  za  kiume.

Njia  nyingine  mbegu  zako  za  kiume  zinaweza  kuchukuliwa  kwa  njia  ya  kufanya  mapenzi  na  mwanamke  mchawi  ambae  anataka  kuiba  nyota  yako  au  kuchukua  msukule  nguvu  zako.

Mwanamke  huyu  ataingia  nyumbani kwako  usiku wa manane  kichawi  na  kufanya  nawe  mapenzi  kwa  lengo  la  kuchukua  mbegu zako.

Wakati mwingine  inaweza  kutokea  umeota  usiku  unafanya  mapenzi  na  mwanamke  unaye  mfahamu  au  usie  mfahamu hadi  kufika  kileleni. Ukiota  ndoto  hii jua  unachezewa  mchezo  huu  mchafu.

Wakati mwingine  mbegu  zako  zinaweza  kuchukuliwa  kwa  njia  ya  kufanya  mapenzi  kichawi  na  tunge  la  kike.

Tunge  la  kike  litakuja  kichawi  hadi  nyumbani  kwako  na  kufanya  mapenzi  na  wewe. Litapata  ujauzito  wako  halafu  mtoto  atazaliwa.  Huyu mtoto  atakae  zaliwa  ndo atakae  enda  kutumika  kama  ndondocha  kwenye   biashara  mbalimbali  kama  vile  maduka  nakadhailka.

Njia  hii  ndio  inayo  tumiwa  sana  na  wachawi  na  wanaume  wengi  wameumizwa  kupitia  njia  hii.

Njia  nyingine  ni pale  nguvu  za  kiume  zinapo  chukuliwa  wakati  mtoto  akingali  mchanga. Njia  ni  hatari  sana  na   ndio  maana  inashauriwa  mama  mjamzito  kuwa  makini  na  mwangalifu sana  katika  siku kumi na  nne  za mwanzo  baada  ya  kujifungua  mtoto  wa  kiume.

Ni katika  kipindi  hicho cha  siku  kumi na  nne  zap   mwanzo  ambazo  wachawi  huzitumia   kutafuta  kuiba  nyota  ya  mtoto  huyo  wa  kiume  kupitia  nguvu  zake  za  kiume.

Nyota  hii  huwa  inaibwa  kupitia  nguvu  zake  za  kiume  na  huwa  zinachukuliwa  kupitia  kitovu  chake. Ndo maana  unatakiwa  kuwa  makini  sana  na  kitovu  cha  mtoto  wako  wa  kiume  kisiangukie  uume  wake  wakati  kinadondoka.

Katika  kupambana  na mtihani  huu  baadhi  ya  wazazi  huwa  wanavikata  wenyewe  vitovu  vya  watoto  wao  wa  kiume  na  huwa  wanatumia  mafuta  ya  nazi, nyoya  la  kuku  na  dawa  maalumu  za  jadi.

Narudia  kwa  mara  nyingine  tena  unapaswa  kuwa  makini  sana katika  kipindi  hiki.

Wachawi  kupitia  taaluma  yao  ya  kichawi  wanaweza  kubaini  nyota  ya  mtoto  na  kujua  atakuja  kuwa  nani .

Ii kuzuia mtoto  huyo  asije  kuwa vile alivyo pangiwa  na  Mwenyezi  Mungu, wachawi  hulazimika  kuiba  nyota  ya mtoto  husika  na  kuiuza  kwa  watu  wengine na  moja  kati ya  njia  kuu  wanazo  weza  kutumia  katika  kufanikisha  nia  yake  ovu  ni kuiba  nguvu  za  kiume  za  mtoto  huyo  kwa  njia  za  kichawi.

Pia  wanaume  wengine  nguvu  zao  zimechukuliwa  tangu wakiwa  tumboni  mwa  mama  zao. Wachawi  wanaamini  ya kwamba, ukitaka  kukuiua  kitu  basi  kiue  kabla hakijazaliwa. Hapo ndipo  linapo kuja  suala  la  kuiba  nguvu za watoto  wa  kiume  tangu  wakiwa  tumboni  mwa  mama  zao.

Ukitaka  kujua  kama  mtoto  wako  nguvu zake  zimeibwa  tangu  akiwa  tumboni ishara  ya  kwanza  ni  pindi  kitovu cha  mtoto  huyo  kinapo mdondokea  kwenye  uume  wake.

Vilevile Mbegu  zako  za  kiume  zinaweza  kuchukuliwa  kupitia  kujichua.. Mbegu  za  mwanaume  zinazo  toka wakati wa  kujichua  hujulikana  katika  ulimwengu  wa  waganga  kama  MBEGU ZILIZO  TOKA  KWA  KULAZIMISHWA.

Haijalishi  unapo fanya  punyeto  unafuta  kwenye  karatasi, gazeti, kitambaa  au  unaacha zidondoke  kwenye  sakafu  ya  bafuni na  kumwagia  maji  lakini  jua, wachawi  kwa  kushirikiana  na  majini  huwa  wanachukua  mbegu  za  kiume  zinazo  toka  baada  ya  kujichua..

Kama  huwa  unajichua  usiku chumbani  kwako kitandani, asubuhi  baada  ya  kuamka  au  bafuni  ama  chooni , basi  jua  wachawi  huchukua  mbegu  zako  na  kuzitumia  kwenye  mambo yao  ya  kichawi.

 MAMBO  AU TABIA  ZINAZO  WEZA  KUFANYA  MBEGU  ZAKO  ZA  KIUME  ZICHUKULIWE  NA  WACHAWI.

Yafuatayo  ni  mambo  yanayo weza  kusababisha  mbegu zako  za  kiume  zichukuliwe.

i.  Kufanya  mapenzi  na  wanawake  wanao  uza  miili  yao  “ HUKO  HUWA  ZINACHUKULIWA  SANA  “

ii. Kuwa  na  michepuko. Mwanaume  fahamu  unapokuwa  na  michepuko  unakuwa  unakaribisha  nafasi  ya  wewe  kufanyiwa  ulozi  wa  kimapenzi.  Hii ni kwa  sababu  michepuko wengi  huwa  wanatumia  uchawi kuwatuliza  wanaume  wanao tembea  nao. Sasa  ikitokea  bahati  mbaya  mchepuko  wako  katika  kutafuta  ndumba  za  kukutuliza, akakutana  na wachawi  wanao  tumia  mbegu  za  kiume  katika  shughuli  zao  basi  ndugu  yangu jua  umekwisha.

iii.Kutupa  kondom  kwenye  dustbin au chooni  mara  baada  ya  kufanya  tendo  la  ndoa.

iv.Kufanya  punyeto    “  WANAO FANYA  SHUGHULI  HII  NAWAHURUMIA  SANA  KWANI  NI MOJA  KATI  YA  WAHANGA  WAKUU  WA  UCHAWI  HUU HUKU WAO  WAKIAMINI  KUWA SHIDA  YAO  IMESABABISHWA NA  PUNYETO.

v.Wanaume  walio lelewa  na  mama  za  kambo  ambao  ni  washirikina. Wanaume  wengi  ambao  nimewatibu  tatizo  hili  wametoka  katika  familia  walizo lelewa  na  mama  wa  kambo.

Hii  mara  nyingi  hutokea  pindi  mama  wa  kambo  anapokuwa  haja bahatika  kupata watoto  wa  kiume,au hajabahatika  kupata  watoto halafu baba  ana  mali nyingi.

Akisukumwa  na  hofu  ya  kukosa  mali  ya  mumewe  mwanamke  huyu anaweza  kushawishika  kwenda  kwa  waganga  kuwadhibiti  watoto wake  wa  kambo  wa  kiume. Mganga  ataomba  nguo  za ndani za  watoto  hawa  au  mkojo  au nguo iliyo  kojolewa  au  atampa dawa  ya  kuwalisha  kwenye  chakula  au  kuwatega.

Kama  watoto  ni  wakubwa  mama  huyu  anaweza  kushirikiana  na  binti ambapo binti  atajilengesha  kwa  kijana  aliye  kusudiwa  wataanzisha  uhusiano  wa  kimapenzi  na  kisha  kutumia  fursa  hiyo  kupata  mbegu  za  kiume  za mwanaume  husika. HATA  HIVYO  HII HAIMAANISHI KUWA  AKINA  MAMA  WA  KAMBO WOTE NI  WABAYA. JAMBO HILI HUTOKEA  KWA  BAADHI  YA  AKINA  MAMA  WA  KAMBO NA SIO WOTE. WAPO AKINA  MAMA  WA  KAMBO  AMBAO NI WAZURI  KULIKO  HATA  MAMA  WAZAZI.

vi. Kugombana  ama  kuachana  na  mchumba  au  mke . Mke  anaweza  kwenda  kukutengeneza  ili  kukukomoa.

vii. Kuoa mwanamke  mshirikina. Katika  kutafuta  ndumba  zap  kukutuliza  anaweza  kukutana  na  suala  la  kutakiwa  apeleke  mbegu  zako.

viii. Wakati  mwingine  unaweza  kufanyiwa  hivi  kwa  sababu  una  maisha  mazuri. Mtu anakufanyia  uchawi  huu  kwa  lengo  la  kuchukua  nyota  yako  na  kwenda  kuitumikisha  kama  msukule  wa  biashara  mali  na  utajiri.

ix. Kukataa  mtoto

x. Kufuta  uchumba  na  kuoa  mwanamke  mwingine

xi. Kutembea  na  mke  wa mtu

xii. Kugombea  mpenzi  au  mchumba.

Mtu  anaweza  kukuroga  nguvu  zap  kiume  ili  kukukomoa, kwa  mfano

 Porini  kuna  mti  unatoa  vitunda  vidogo  vyenye  rangi  mbili  nyeusi  na  nyekundu.

Mti  huu  huwa  ni  dawa  ya  maradhi  ya  mgolo  ama  bawaziri

Una  majani  matamu  kama  sukari  ambayo  wakati  wa  njaa  huweza  kutumika  kutengenezea  chai  na  pia  huweza  kutumika  kutengeneza  chai  kwa  watu  wenye  kusumbuliwa  na  maradhi  ya  kisukari.

Vipande  saba  vya  mti  huu vinachukuliwa  halafu  wanachukuliwa   wanyama  wa  aina  tatu  tofauti   wafugwao  wanachinjwa kisha  damu  yao  inachanganywa  pamoja  na dawa  zitokanazo  na  miti  ya  porini  aina  saba  halafu  vinaenda  kupikwa  porini  kisha  zinafungwa  kwenye  chombo  maalumu  na  kuzikwa  kwenye  makaburi  saba  tofauti  kwa  muda  wa  siku  saba  saba   na  njia  panda  saba  tofauti  tofauti  kwa  muda  wa  siku  saba  kisha  zinazikwa  kwenye  milima  miwili  tofauti  kwa  muda  wa  siku  saba.

Baada  ya  hapo, linachukuliwa  bawa  la  ndege  mmoja  wa  porini. Huyu ndege  anatumiwa  sana  na  wachawi  “  NDEGE  HUYU  SIO  BUNDI  WALA  SULULI  WALA  MKATA  SANDA’.

Ndege  huyu  ana  sifa  moja  kubwa  katika  ulimwengu  wa  wachawi.  Nayo  ni  kwamba, ukichukua  nyoya  lake  ukaliweka  kwenye  mto wa  kwenye  kitanda  alicholalia  mgonjwa, basi  mgonjwa  huyo hatopona  bali  atakufa  na  kama  utaliweka  chini  ya  mto  alio lalia  mtoto  mchanga  basi  mtoto  huyo atadumaa, hatokua.

Bawa  la  ndege   huyu  ndio  linatumika  kama  kalamu  ya  kuandikia  majina  ya  mkusudiwa  pamoja  na  manuizo.

Majina  na  manuizo  yakiisha  kuandikwa,  miti  hiyo  saba  inaenda  kutupwa  barabarani  kwenye  barabara  saba  tofauti.

Miti  hiyo  ikigongwa  na  gari  tu  basi  na  mwanaume  aliye  kusudiwa  anaanza  kuugua  maradhi  ya  nguvu  za  kiume.

Maradhi  huanza  taratibu  na  baadae  huhitimu  na  kuwa  sugu  ambapo  mhusika  anaweza  kufikia  hatua  ya  kuwa  hanithi  kabisa.

KWANINI  WACHAWI  HUZICHUKUA  MSUKULE  NGUVU  ZA  KIUME

Kama  nilivyo  sema  hapo awali  wachawi  huchukua  kichawi  nguvu  za  kiume  kwa  ajili  ya  kwenda  kuzitumikisha  kama  misukule  kwenye  biashara, mali  na  utajiri.

KUNA  UHUSIANO  GANI  KATI  YA  NGUVU  ZA  KIUME  NA  DAWA  ZA  UTAJIRI  MALI  NA  BIASHARA ?

 Najua  lazima  utakuwa  umejiuliza  swai  hili, yafuatayo   ni majibu  ya  swali  hili.

Nguvu  za  kiume  zina  uhusiano  mkubwa  sana  na  damu. Nguvu za  kiume  ni damu  na  damu  ndio  nguvu  za  kiume.

Damu  ndio  uhai  wa  mwanadamu. Damu ndio roho ya  mwanadamu  na  roho  ya  mwanadamu  ndio damu. Damu  huishi ndani  ya  roho  ya  mwanadamu  na  roho  ya  mwanadamu  huishi  ndani  ya  damu  ya  mwanadamu.

Roho  ya  mwanadamu  hubeba  akili  na nafsi. Na  nafsi ya  mwanadamu  hubeba  nyota  ya  mwanadamu.  Nafsi  ya  mwanadamu  hubeba  akili  ya  mwanadamu . Hisia  za  mwanadamu,  Silka za mwanadamu, Hulka  za mwanadamu  na  utashi  wa  mwanadamu.

Uanaume  au unamke  ni  nafsi  anayo zaliwa  nayo mwanadamu. Nguvu  za  kiume  ndio  nafsi ya kwanza  ya  mwanaume. Hiyo ndio  inayo mfanya  awe  mwanaume  au  ajione  mwanaume.

Unapo chukua  nyota ya  mwanaume  ambayo  ndio  nafsi ya  mwanaume  ambayo  ndani  yake  ipo akili ya  mwanaume ambayo  ndio  nguvu  za  kiume  za  mwanaume  unakuwa  umechukua  nafsi  ya  mwanaume  huyo ambayo ndio  nyota  yake.

Nguvu  za  kiume  ndio  chanzo  cha  uhai  wa  mwanadamu.

Nguvu  zap  kiume  za mwanaume  zinasimama  badala  ya  nafsi ya  mwanaume.

Unaposema  fulani  ni damu  yangu  maana  yake  ni kwamba  fulani  ni roho  yako  ambae  amekuja  duniani  kupitia  nguvu  za  kiume.

Katika  ulimwengu  wa  waganga  na  wachawi, nguvu  za  kiume  ni  kielelezo cha  uhai  wa  mwanaume  husika.

Nguvu  za  kiume  ni  kielelezo cha  ukamilifu  wa  mwanaume.

Hivyo  wachawi  wanapo chukua  nguvu  za  kiume  za mtu kwa  lengo  la  kuzitumikisha  kichawi,hufanya hivyo  wakiwa  wanajua  wanacho kifanya.

UFANYE  NINI  KUEPUKA  NGUVU  ZAKO KUCHUKULIWA  MSUKULE

Kitu kikubwa cha kufanya  ni kuhakikisha  unakuwa  na  kinga  kubwa ambayo itawafanya  wachawi  wasiwe  na  uwezo  wa  kuchukua  nguvu  zako msukule.

Vile  vile  unatakiwa  kujiepusha  na  tabia  hatarishi  ambazo  nimezieleza  hapo juu. Tabia  hizo ni  tabia  zitakazo  kuweka  katika  hatari  kubwa  ya  nguvu  zako  kuchukuliwa  kichawi.

UTAJUAJE  KUWA NGUVU  ZAKO  ZA  KIUME  ZIMECHUKULIWA  KICHAWI

Endapo utaonyesha  dalili  zifuatazo  basi  jua  tatizo lako la  nguvu  za  kiume  limechukuliwa  kichawi  au  zipo kwenye  mpango  wa  kuchukuliwa.

1.Ukiwa  na  mwanamke  mmoja  unakuwa  na  nguvu  lakini  ukienda  kwa  wanawake  wengine  unakuwa  hauna  nguvu.

2.Umetumia  tiba  mbalimbali  zap  nguvu  za  kiume  lakini  huponi  wala  kupata  nafuu  yoyote.

3.Mpenzi, mchumba  au mke  wako  anakudharau  kwa  sababu  ya  kutokuwa  na  nguvu  za  kiume.

4.Mpenzi  wako  anakukimbia  kwa  sababu  hauna  nguvu  za  kiume

5.Mpenzi   au mke  wako  anatoka  nje  ya  ndoa  au  mahusiano  na  mwanaume  ambae  unamzidi  fedha  na  maisha  kwa  ujumla.

6.Umekuwa  addicted  na  tabia  ya  kujichua  na  unashindwa  kuacha.

7.Kuachana  na  kila  mwanamke  unayekuwa  nae  katika  mahusiano

8.Kutodumu katika  mahusiano

9.Kuwa  na matatizo  ya  uzazi

10. Kufanikiwa  chini  ya  kiwango : Kwa  sababu  suala  hili huwa  linaenda  na  kuchukuliwa  nyota  basi  hata  mafanikio  unayo  yapata  huwa  yanakuwa  chini  ya  kiwango.

11.Kutojiamini  wakati  wa  tendo  la  ndoa. Unashindwa  kujiamini  kwa  sababu  unakuwa  na  wasiwasi  na  uanaume wako.

12. Kuishiwa  nguvu  zap  kiume

13.Maumbile  kunyauka  na  kusinyaa  na  kuwa  kama  ya  mtoto

14. Maumivi wakati  wa  tendo  la  ndoa

15. Kutokuwa  na  uwezo  wa  kurudia  tendo  la  ndoa

16.Maumivu  ya  mgongo

17.Kukosa  hamu  ya  kufanya  tendo  la  ndoa.

18.Unaota  unafanya  mapenzi  na mtu usie mjua NAKADHALIKA.

TIBA  KWA MTU MWENYE  MARADHI  YA  NGUVU  ZA  KIUME  YANAYO  TOKANA  NA  KUROGWA.

Kuwa  na  maradhi  ya  nguvu  za  kiume  yanayo  tokana  na  kurogwa  maana  yake  ni  kwamba ile  sehemu  ya  kwenye  nafsi  na  akili  ya  mwanaume  ambayo  inahusika  na  utashi, hisia  na   maamuzi  sahihi, inakuwa  imechukuliwa  kichawi  kwa  lengo  la  kutumikishwa  kichawi  na  badala  yake  linawekwa  jinni  maalumu  la  kichawi  ambalo  sasa  ndio  linasimama  kama  mbadala  wa nafsi  yako.

Jinni  hili  ndio  litakalo  kuwa  lina  control utashi , hisia  na  maamuzi  yako.

Jinni  huyu mchafu  anakuwa  ameamrishwa  na  kuapishwa kwa  damu   kufanya  makazi  yake  katika nafasi yako. Anakuwa  anautumia  mwili  wako  kama  sehemu  yake  ya  makazi.  Maamuzi  utakayo  kuwa  unaya fanya  kwa  kiasi  kikubwa  yatakuwa  na utashi  na  mapendeleo  ya    jinni  huyu.

Jinni  huyu huwa  na  sifa  zifuatazo : Kwanza  hakujui  vizuri, hajui unapenda  nini, hajui  hupendi  nini, hajui utashi  wako  ni  nini  wala  hajui  hisia  zako zipo wapi  , yeye  anacho  jua  ni kufuata  maelekezo  aliyopewa  ambayo  ni  kukaa ndani  ya  nafsi  yako  na ku ku -control.

Kwa  kuwa  jinni  huyu  hajui  wewe  unapenda  kitu gani  wala  hajui  kuhusu  utashi  wako  wala  hisia  zako  zipo  wapi, hata  unapokuwa  katika  mazingira  ambayo  kikawaida  ulitakiwa  kusisimkwa  kimahaba unajikuta  unashindwa  kusisimka.  Hii  ni kwa  sababu  unakuwa  sio  wewe  bali yeye.

Mfano  mzuri  unakuta  mwanaume   katika  siku  zap  nyuma akiwa  faragha  na  mke  wake  halafu mke  wake  akawa  katika  hali  ya  ufaragha, basi  mwanaume  “ atakasirika  “  kweli kweli na  atafanya  tendo  la  ndoa  vizuri kabisa.

Lakini cha  ajabu  ghafla  hali  inaanza  kuwa  tofauti, upo na  mkeo faragha  halafu  jogoo  anashindwa  kuwika. Na  wewe  unadhani  una  stress  au  labda  una  kisukari  au ulifanyaga  sana  punyeto ulipokuwa  shuleni  au  una  lehemu  mbaya nakadhalika.

Sababu  ya  kushindwa  kwako   ni hiyo, kuna roho chafu imekaa  kwenye  nafsi yako, hiyo roho ndio inayo  control  hisia  zako na  utashi  wako.  Haijui  kama  wewe  ni mwanaume  au  mwanamke, haijui  unapenda  nini  haupendi  nini, haijui hisia  zako  zipo wapi ndio  maana  unapokutana  na  mke  wako, unashindwa  kufanya  unacho  takiwa  kufanya.

Wakati mwingine  jinni  huyu mbali  na  kutokukujua  lakini  pia  anaweza  kuwa  hapendi  kabisa  ngono  ya  aina  yoyote  ile  iwe  ni  ngono  halali yani mke  na  mume  au  ngono  haramu  yani  mwanaume  na  mchepuko.

Hivyo unapokuwa  unataka  kufanya  tendo  la  ndoa, jinni  huyu anakuwa  anakuzuia kwa  kukata  mawasiliano  yako kwenye  ubongo  na  kukuondolea  msisimko.

Hii ni kwa  sababu  jinni  huyu  sasa ndio   anaekumiliki kama  chombo chake  na  hawezi  kukuacha  mpaka  siku  unaondoka  duniani  au  labda  itokee  aondolewe  kwa  nguvu.

Tendo  la  ndoa  linakuwa  linampa  kero  kubwa . Anakuwa  hapendi  kukuona  ukiwa  unafanya  tendo  hilo, hivyo akiona  unataka  tu kufanya  anakuzuia  kwa  njia niliyo ieleza  hapo juu, matokeo  unaishia  kupoteza  hamu  ya  tendo  la  ndoa  na  hata  ikitokea  umefanya  unafanya  kwa  muda  mfupi na  kumaliza  na kushindwa  kurudia  kabisa  huku  ukimuacha  mwenzi wako  akiwa  bado  hajapanda  mlima.

Wakati mwingine  jinni  huyu anaweza  kuwa  jinni  mahaba   ambae  anakuwa  amefungishwa  ndoa  nawewe   bila  ridhaa  yako.

Jinni  huyu  atakuwa  anafanya  mapenzi  na  wewe  na  kumaliza  nguvu  zako  zote. Na  kwa kuwa  jinni  huyu  atakuwa  anakupenda  na  kuwa  na  wivu na  wewe ili kukuzia  usiende  nje  basi  atafunga  nguvu  zako  za  kiume.

 TIBA  YA  TATIZO  HILI  NI  KWANZA  KUMUONDOA  HUYU  JINI,  KUONDOA  UCHAFU  AMBAO UMEPANDWA  KWENYE  MWILI  WAKO, KUONDOA  UUME  WA  KICHAWI   AMBAO  UMEPANDWA  KWENYE  MWILI  WAKO  KAMA  MBADALA  WA  UUME  WAKO  ULIO CHUKULIWA  NA KISHA  KUKUSAFISHA  HALAFU  MWISHO  KUKUPIKIA  DAWA  MAALUMU  AMBAYO  ITARUDISHA  NGUVU  ZAKO  NA  KUKUFANYA  UFURAHIE  MAISHA  YAKO YA  NDOA  KAMA  ZAMANI.

MAKALA  HAYA  YAMEANDALIWA  NA  DOKTA  MUNGWA  KABILI. ANAPATIKANA  KWA  SIMU  NAMBA 

0744   -  000   473

KUSOMA  MAKALA  ZAKE  MBALIMBALI  KUHUSU  ULIMWENGU USIO ONEKANA, TEMBELEA  :  www.mungwakabili.blogspot.com

Waziri Mkuu Aipa SOMO Wizara ya Nishati na Madini

$
0
0
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa ameitaka Wizara ya Nishati na Madini kuboresha mikakati yake kwa ajili ya kudhibiti uchimbaji na biashara ya madini nchini ili kuleta tija kwa maendeleo.

Miongoni mwa mikakati hiyo, ni kuvutia wawekezaji, kuandaa wataalamu na kuboresha mifumo.

Majaliwa aliyasema hayo jana wakati wa Mkutano wa 37 wa Mawaziri wa Nishati na Madini wa nchi wananchama wa Kituo cha Madini cha African Minerals and Geoscience Centre (AMGC), licha ya mambo mengine ulijadili mchango wa sekta ya madini kwenye uchumi wa Afrika.

Waziri mkuu alisema licha ya Tanzania kuwa na utajiri mkubwa wa madini, sekta hiyo haina tija kwenye maendeleo ya uchumi kwa wananchi wake hasa waishio karibu na migodi.

“Changamoto kubwa ni namna tunaweza kuwa na sekta ya madini, inayoweza kutoa mchango stahiki na kuwafanya wananchi wote kunufaika na kupata maendeleo,” alisema Majaliwa.

Alisema hivi sasa hali hairidhishi kwa kuwa maeneo mengi ya machimbo yameharibiwa, huku wakazi wake wakiachwa maskini.

“Mfano, Tanzania licha ya kuwa tajiri wa madini ya dhahabu, almasi, tanzanite, shaba na chuma, mchango wa sekta hiyo ni asilimia 4.8 tu ya pato la Taifa, hivyo kuna haja ya kuongeza usimamizi,” alisema.

Pia, alihimiza kutumia kituo hicho kwa ajili ya kufanya utathmini na uongezaji thamani wa madini nchini, badala ya kuyasafirisha yakiwa ghafi.

“Kituo hiki (AMGC) kinafanya utafiti, kinafundisha wataalamu na kina maabara za kisasa kwa ajili ya uhakiki na uongezaji thamani madini,” alisema

Wakati huohuo, Naibu Waziri wa Nishati, Dk Medard Kalemani alisema aliagiza kampuni za madini na wachimbaji wadogo mwakani zitaanza kupeleka madini kwa ajili ya kufanya tathmini ya viwango, badala ya kuyasafirisha nje ya nchi.

“Nitoe wito kwa kampuni zote za madini zianze kuleta madini yao katika kituo hiki, ili yaanze kutathminiwa, badala ya kupeleka nje ya nchi,” alisema Dk Kalemani.

Dk Kalemani alisema, hatua hiyo ni utekelezaji wa msimamo wa Serikali wa kudhibiti madini na kutaka yafanyiwe uchenjuaji na uongezaji thamani ili kuongeza pato la nchi.

Naye Mkurugenzi Mkuu wa AMGC, Ibrahim Shaddad alisema kituo hicho kinaundwa na nchi nane wanachama na kwamba, wanatarajia kuzipokea nchi nyingi zaidi kwa ajili ya kuimarisha utendaji.

Katika Mkutano huo,Tanzania ilikuwa Mwenyekiti ambapo ulihudhuriwa na Mawaziri,Makatibu Wakuu,Wakurugenzi kutoka Wizara ya madini pamoja na Mashirika mbalimbali ya Kimataifa sanjari na kuadhimisha miaka 40 tangu kuanzishwa kwa kituo hicho mwaka 1977.

Ufafanuzi wa Bunge kuhusu gharama za ndege iliyompelekea Tundu Lissu Nairobi

Unasumbuliwa na Kiharusi,Ngiri au Kifafa?......Unatatizo la Nguvu za Kiume, Kuachika au Tatizo la Uzazi? . Kutana na Mtalaamu Huyu Akusaidie

$
0
0
SASA YUPO DAR;Anadawa ya kumvuta mpenzi wako popote alipo kwa masaa 6 tu na kumtuliza asitoke kwako

Je, unaugomvi usioisha na mpenzi wako na unaachwa mara kwa mara? Njoo upate dawa ufurahie penzi tulivu la umpendae.

Anadawa za nguvu za kiume, kuimarisha mishipa iliyolegea, kuongeza homoni na kukufanya udumu katika tendo hadi dakika 45 na unaweza kurudia tendo hata mara 4 bila kuchoka.

Anatibu Busha bila kupasua,uzazi, mshipa wa ngiri,kiharusi,kifafa,kuondoa majini machafu nakadhalika.

Mpigie kwa simu: 0755505099

CCM Wampongeza Mbunge wao wa CCM aliyekodi ndege Ya Kumsafirisha Tundu Lissu

$
0
0
Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimempongeza mwanachama wake aliyejitolea kudhamini ndege iliyomsafirisha Mbunge wa Jimbo la Singida Mashariki, Tundu Lissu kwenda jijini Nairobi nchini Kenya kwaajili ya matibabu.

Katika taarifa hiyo, imesema kuwa wamechukua hatua hiyo ya kumpongeza Mbunge wa Jimbo la Mpendae, Salim Hassan Turky kwa kuonyesha upendo, utu na mshikamano na kuweka kando tofauti za kisiasa.

“Kwa dhati kabisa tunampongeza mwanachama wetu na mbunge wa Jimbo la Mpendae, kwa kuonyesha utu na kuweka kando itikadi za kivyama kumsaidia Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu,” amesema Polepole kupitia taarifa hiyo

Hata hivyo, Polepole ameongeza kuwa wameamua kumpongeza mbunge huyo kwa kuonyesha uzalendo wa hali ya juu, kwani katika matatizo ni vyema itikadi za kisiasa zikawekwa pembeni ili kuweza kutatua kile ambacho kinakuwa kinawakabili.

Waliokamatwa na mzigo wa almasi yenye thamani ya sh. 32.3 bilioni wapandishwa kizimbani Mahakama ya Kisutu leo

$
0
0
Baada ya Serikali kuanza kuwashughulikia wale wote wanaohujumu uchumi wa nchi na kuiibia nchi rasilimali zake, watuhumiwa waliokamatwa na mzigo wa Almasi zenye thamani ya shilingi bilioni 32.3 katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA), wamefikishwa katika Mahakama ya Kisutu leo asubuhi Septemba 15.

Mzigo huo wa Almasi uliokuwa unatoka mgodi wa Mwadui ulizuiliwa na Serikali kwa lengo la kuufanyia tathmini upya ili kujua thamani halisi baada ya thamani iliyokuwa imetajwa awali kutiliwa mashaka na Serikali.

Baada ya kubainika kuwa wahusika walidanganya thamani, Jeshi la Polisi liliwashikilia watuhumiwa wanne huku uchunguzi na hatua nyingine za kisheria zikifuatwa baada ya kuzuiwa kwa mzigo huo.

Mgodi wa Mwadui unamilikiwa kwa ubia kati ya Serikali na Kampuni ya Petra Diamonds ya Afrika Kusini ambapo Serikali ina hisa 25% na Petra Diamonds ina hisa 75%.

Kwa Nini Wanaume Wengi Wanaupungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo?

$
0
0
Asilimia 45 ya wanaume wapo tofauti na wengine kwa kuwatimizia vyema wake au wapenzi Wao na kuwasababishia kutoka nje ya ndoa zao.

NINI CHANZO CHA HAYO?Kupiga punyeto,Ngiri,Vidonda vya tumbo,Magonjwa ya moyo,Presha,Kisukari,Korodani moja kuvimba,Msongo wa mwazo,Kufanyiwa tohara ukiwa mtu mzima n.k.DOKTA MANYANDA sasa kapata tiba sahihi ya tatizo la NGUVU ZA KIUME.

MUHAMA:Hii hutibu na kuponyesha kabisa tatizo la nguvu za kiume,utakuwa na uwezo wa kurudia tendo zaidi ya mara tatu bila kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dakika 15-20.DAWA hii imechanganywa miti 12.Hata wazee wenye umri mkubwa wanapona kabisa.OKO NDOA YAKO SASA. 

MANGUNGU MIX: Ndio tiba tosha kwa sasa ambayo hurefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo inch 1-8 na unene sentimita 1-5,dawa hii ipo ya kupaka na kunywa na haina madhara yoyote kwa mtumiaji.

NITOFAUTI NA ULIZO WAHI KUZITUMIA.Pia tuna dawa za kupatanisha mke,mme,mpenzi au bosi wako kwa mda mfupi sana,Uzazi,Kusafisha nyota,

Je unamali yako unauza hupati wateja?Wasiliana nami 0716-263605 

DOKTA MANYANDA ANAPATIKANA KASULU KIGOMA,Kwa wale wa mikoani huduma hii utaipata popote pale.

Mbowe: Hali ya Tundu Lissu Inatia Matumaini, Hofu ya Kumpoteza Haipo Tena

$
0
0
Mwenyekiti wa CHADEMA Mhe. Freeman Mbowe amefunguka na kusema kuwa ile hofu iliyokuwepo Mbunge Tundu Lissu aliyeshambuliwa na risasi kuwa huenda angepoteza maisha imezidi kupungua na kudai madaktari wanatoa matumaini makubwa hali yake inaimarika.

Freeman Mbowe amesema hayo leo kupitia kwenye mitandao yake ya kijamii na kusema kuwa Mbunge huyo sasa anaweza kuzungumza japo anaendelea kupatiwa matibabu na kudai pia ataendelea kufanyiwa upasuaji mwingine.

Aidha Mbowe amewataka wananchi kutosikiliza taarifa za watu wengine kuhusu hali ya mgonjwa na kusema taarifa rasmi juu ya hali ya mgonjwa itatolewa na wao ambao wapo na mgonjwa Nairobi Kenya.

"Kuhusu hali ya Mhe. Lissu, kwa sasa ile hofu ya kupoteza maisha imezidi kupungua, madaktari sasa wanatoa matumaini makubwa kuwa hali yake sasa inaimarika. 

"Yale yote yaliyokuwa yanatishia pengine uhai wake, usalama wake, yamepungua kwa kiasi kikubwa na madaktari wanatoa matumaini makubwa. 

"Sasa hivi, Mhe Lissu anaweza kuzungumza, nimezungumza nae, japo bado anapatiwa matibabu na ataendelea kwenda 'theatre' kwa ajili ya upasuaji na kutibu majeraha mbalimbali aliyoyapata. 

"Anazungumza na anatoa salamu kwa Wanaafrika Mashariki, anatoa salamu kwa Watanzania, niseme tu kwamba sisi ambao tuko nae muda wote ndo tunajua hali halisi ya mgonjwa" alisema Freeman Mbowe

Mbali na hilo Freeman Mbowe amedai kuwa Mbunge huyo hana athari zozote zile kwenye kifua chake kama ambavyo baadhi ya taarifa zinasema kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii na kudai Mwanasheria Mkuu huyo wa CHADEMA yupo imara.

"Mhe. Lissu hana 'infection' ya kifua, kwa sasa yuko vizuri yuko imara, bado ni 'critical' lakini bado yuko stable. Tuendelee kumuombea kila siku, wakati wote, aweze kupona kwa haraka na kuruhusiwa kutoka hospitali" alisema Mbowe

Mbunge Tundu Lissu alishambuliwa kwa risasi na watu wasiojulikana Septemba 7, 2017 akiwa Makao Makuu ya nchi mjini Dodoma na baadaye kusafirishwa kwenda jijini Nairobi Kenya kwa ajili ya kupatiwa matibabu kufuatia majeraha aliyopata, ambapo mpaka sasa yuko huko kwa matibabu.

Breaking News: Mahakama ya Kisutu Yamwachia Huru Askofu Gwajima

$
0
0
Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima amefutiwa kesi ya kushindwa kutunza silaha baada ya  upande wa mashitaka  kushindwa kuthibitisha mashtaka hayo, na kuamuru arudishiwe mkoba wenye silaha yake.

Gwajima na wenzake watatu wamefutiwa mashtaka hayo mbele ya hakimu mbele ya Hakimu Mkazi Kisutu, Cyprian Mkehe.

Katika kesi hiyo ambayo Gwajima alikuwa akisimamiwa na Wakili Peter Kibatala, washtakiwa hao walikuwa wakidaiwa kuwa Machi 29, 2015 katika Hospitali ya TMJ iliyopo Mikocheni A walikutwa wakimiliki Bastola aina ya Berretta yenye namba ya siri CAT 5802 bila ya kuwa na kibali toka kwa mamlaka inayohusika na silaha na milipuko.

Ilidaiwa kuwa washtakiwa hao walifanya kosa hilo kinyume na kifungu cha 32 (1) na cha 34 (1) (2) na(3) cha sheria ya Silaha na Milipuko sura ya 223 iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2010.

Pia, walidaiwa kuwa siku ya tukio washtakiwa hao pia walikutwa wakimiliki isivyo halali risasi tatu za bastola pamoja na risasi 17 za bunduki aina ya Shotgun.

Wazee wa Mkoa wa Kigoma wakerwa na kauli ya Spika wa Bunge, Job Ndugai.

$
0
0
Wazee wa Kigoma wakiwakilishwa na Mwenyekiti wa Ngome ya Wazee ya Chama cha ACT Wazalendo, Alhaj Jaffar Kasisiko wamesikitishwa na kauli aliyotoa Spika Ndugai kuwa anaweza kumzuia Zitto Kabwe asiongee chochote mpaka ubunge wake utakapokwisha.

Wazee hao wanasema kitendo cha Spika kumzuia Zitto Kabwe kuongea bungeni ni sawa na kuwazuia wao wasiongee na shida zao zisiweze kutatuliwa na kudai inaonekana hiyo kauli imeshafanyiwa kazi na kitendo cha kumwita Zitto kwenye Kamati ni sawa na kupoteza muda tu na kudai jambo hilo halimtendei haki kijana wao Zitto Kabwe na wao wenyewe.

Aidha wazee hao wamemtaka Spika Job Ndugai na viongozi wengine wasiwe na kiburi na watazame mambo ambayo yanawaunganisha kwa pamoja. 

CHADEMA Kufanya Maombi Maalumu Kitaifa ya Kumuombea Tundu Lissu Jumapili Hii

$
0
0

Makamu Mwenyekiti wa Baraza la Vijana CHADEMA taifa (BAVICHA), Patrick ole Sosopi amefunguka na kusema wao kama chama wameamua kuwakutanisha wanachama wao mbalimbali wa imani tofauti kwa ajili ya kufanya maombezi ya kitaifa kumuombea Mbunge Lissu.

Akiongea na waandishi wa habari leo Makao Makuu ya CHADEMA, Sosopi amesema kuwa jambo hilo halihusiani na mambo ya kisiasa bali wameamua kukutana kwa lengo la kuombea taifa katika mambo mbalimbali ikiwa pamoja na kuliombea jeshi la polisi ili wafanye kazi zao kwa kufuata misingi ya haki na usalama zaidi.

"Madaktari wamefanya kazi kubwa sana kuendelea kuokoa maisha ya Tundu Lissu na sisi tumekaa na kufikiri kwamba ni bora tukutane ili kwa pamoja tuweze kufanya maombezi, tunajua chama chetu kina kila aina ya watu wenye imani mbalimbali ya dini, hivyo Baraza tumeandaa maombo maalum kwa ajili ya Mhe. Tundu Lissu na kuita 'Tanzania National youth Prayer for Lissu' tutafanya maombi hayo ya kitaifa na kutoa wito kwa watu wote, jambo hili si la kisiasa na wala halina sura ya kisiasa " alisisitiza Sosopi

Aidha Sosopi amesema kuwa wanategemea kufanya maombezi hayo siku ya Jumapili jijini Dar es Salaam maeneo ya Sinza Darajani viwanja vya TP na kudai kwamba mpaka sasa wamefanya maandalizi yote ikiwa pamoja na kuandika barua kwa taasisi zote za dini kuweza kufika kwa ajili ya maombezi hayo.

Mbali na hilo Sosopi amedai kuwa kwa kuwa wanaamini jambo hilo halina sura ya kisiasa hivyo wanategemea kuona jeshi la polisi nchini likifika kwa lengo la kutoa ulinzi kwa raia ambao watafika kwa ajili ya maombezi hayo na si vinginevyo.

"Naomba jambo hili lisitafsiriwe vibaya sisi, kama viongozi wa kisiasa tutakwenda pia kusikiliza maombi na si kwenda kuongea chochote, tutakwenda uwanjani kwa sababu sisi kama CHADEMA hatuna kanisa wala msikiti kufanya maombezi hayo ndiyo maana tunakwenda uwanjani hapo, tunaamini hapo ni sehemu sahihi kuweza kuwakutanisha watu wetu wote bila kujali itikadi zao" alisema Sosopi

Pata Tiba ya Tiba ya Tatizo la Nguvu Za Kiume........Inasaidia Kukufanya Urudie Mara 5 na kuchelewa kwa Dakika 20

$
0
0
TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO LINATIBIKA.Baada ya utafiti wa mda mrefu juu ya matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume na ukosaji wa hamu ya tendo la ndoa ama kushindwa kurudia tendo kwa haraka DR Magise imekuletea tiba ya matatizo hayo kwa kutumia dawa za: 
 
FUUl POWER:Ni dawa asili ya vidonge inayotibu tatizo la upungufu au ukosefu wa nguvu za kiume,dawa hii inamchanganyiko wakutosha wenyekuzalisha vichocheo vingi vya Hemone za Gestrogen vikiwemo vitamin B6&B1,vitamini E,pamoja na madini aina ya zinc vitakufanya kuwa na nguvu na mzunguko mzuri wa damu na kuongeza hamu na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya hatua nne au zaidi,na kuchelewa kufika kileleni zaidi dakka 20-30.
 
NYAMVA:Inarutubisha maumbile ya uume yani kurefusha na kunenepesha nchi 4-7 upana cm3-4 standard kiafya haijalishi umri wako hata kwa wazee ukiitumia maumbile yako yatabaki kuwa hivyo siku zote,Pia tunatibu Presha,kisukari siku7,ngiri,chango la tumbo tumbo kujaa gesi,kutopata choo vizuri

 TUPO TZ DAR ES SALAAM   MBAGALA RANGI TATU.HUDUMA HII UTALETEWA POPOTE ULIPO .WASILIANA NAMI 0783741788,0715741788 -DR MAGISE

Dereva wa Mbunge wa CHADEMA ashambuliwa kwa mapanga

$
0
0
Suezi Dan Maradufu (45), dereva wa Mbunge wa Tarime Vijijini, John Heche ameshambuliwa na watu wasiofahamika usiku wa kuamkia leo na kumjeruhi usoni.

Akiwa amelazwa katika hospitali ya Mji wa Tarime, Maradufu amesema jana Alhamisi saa mbili usiku akitoka nyumbani kwake kwenda kwa  mbunge alivamiwa na watu wawili waliomjeruhi kwenye paji la uso.

Maradufu amesema alikuwa akienda kwa Heche ili wasafiri kwenda Nairobi nchini Kenya kumwona Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu aliyelazwa jijini humo baada ya kushambuliwa na kujeruhiwa kwa risasi nyumbani kwake Area D, mjini Dodoma.

Dereva huyo amesema baada ya kuvamiwa  na watu hao, walimpiga kwa shoka kwenye paji la uso na walipora begi lake la nguo.

Mrimi Zabron ambaye ni katibu wa mbunge Heche anayemuuguza dereva huyo amesema alifikishwa hospitali saa nane usiku.

Amesema kwa usaidizi wa ndugu wa Heche alifikishwa hospitali na ameshonwa nyuzi sita kwenye jeraha.

Zabron amesema safari ya Heche iliyokuwa ifanyike jana saa nne usiku, imefanyika leo asubuhi.

Amesema mbunge huyo amesafiri na kaka yake ambaye ni Katibu wa Chadema Mkoa wa Mara, Chacha Heche.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images