Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Majeruhi watatu ajali ya Wanafunzi Arusha Kurejea Nchini Kesho Kutwa

$
0
0
Watoto watatu walionusurika kwenye ajali ya basi la wanafunzi wa Shule ya Lucky Vincent ambayo ilipoteza maisha ya wanafunzi 32, wanatarajia kurejea nchini August 18, 2017 baada ya kupatiwa matibabu Marekani.

Mbunge wa Singida Kaskazini Lazaro Nyalandu ambaye alikuwa mstari wa mbele kusimamia shughuli ya kuwasafirisha, amesema ratiba ya mapokezi itaanza mapema zaidi ambapo itakuwa saa Moja asubuhi katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro, ‘KIA’ ambapo Makamu wa Rais Samia Sulu Hassan atawaongoza Watanzania.

”Watawasili tarehe 18, 2017 wiki hii wakiwa wanaletwa na ndege ile ile iliyowachukua na ratiba inaanza mapema kidogo saa moja asubuhi, wananchi na wanafamilia wanatarajiwa wawe wamefika uwanja wa KIA, Kutakuwa na viongozi mbalimbali na tunatarajia makamu wa Rais kuwa mgeni rasmi.”  Amesema  Lazaro Nyalandu.

Bodaboda Wapigwa Marufuku Kubeba Wanafunzi na Watoto Chini ya Miaka 10

$
0
0
Jeshi la Polisi  August 15, 2017 limetoa tamko la kupiga marufuku Waendesha Bodaboda kubeba watoto wenye umri wa chini ya miaka 10 na kwamba atakayekiuka agizo hilo pamoja na mzazi aliyeruhusu mwanawe kubebwa watachukuliwa hatua za kisheria ikiwa ni pamoja na faini, kifungo au vyote viwili.

Kamishna Msaidizi wa Polisi ambaye pia ni Afisa Mnadhimu wa Kikosi cha Usalama Barabarani, Theopista Malya, amesema kuwa watoto wamekuwa kwenye hatari kubwa wakipandishwa kwenye Bodaboda na wakati mwingine waendesha bodaboda hubeba watoto zaidi ya mmoja jambo ambalo ni lazima likemewe.

Aidha, alisema kuwa Jeshi hilo limeandaa kipindi maalumu cha Radio kitakachorushwa na Clouds FM kila siku ya Jumatano saa 2:00 Usiku kikiwa na lengo la kuongeza elimu kwa waendesha Bodaboda katika kuzingatia Usalama Barabarani pindi wanapofanya shughuli zao.

Mwenyekiti wa Taasisi ya Mabalozi wa Usalama barabarani (TSA), John Seka alisema kipindi hicho kitalenga kuwapa elimu waendeshaji wa bodaboda.

Pia, alitumia nafasi hiyo kuwataka wafuate sheria zilizowekwa na Sumatra ili waepukane na mkono wa sheria.

Paulina Shayo ambaye ni mwakilishi kutoka WAT Saccos alisema kuwa wanatoa mikopo kwa bodaboda na kwamba mikopo hiyo itawasaidia kuwa wamiliki halali wa vyombo hivyo.

Mtoto Mchanga wa Miezi 6 Aliyejeruhiwa na Polisi Afariki Dunia

$
0
0
Mtoto wa miezi sita aliyejeruhiwa na maafisa wa polisi baada ya kutangazwa kwa matokeo ya uchaguzi yaliozua utata nchini Kenya amefariki, kulingana na familia yake.

Samantha Pendo alikuwa mahututi tangu siku ya Ijumaa baada ya kupata majeraha ya kichwa wakati polisi walipovamia nyumba yao katika mtaa wa mabanda magharibi mwa mji wa Kisumu.

Babake Joseph Abanja , ameliambia gazeti la Daily Nation: "Nataka haki kwa mwanangu,hakuwa akiandamana , babake hakuwa akiandamana pia.Mamake hakuwa akiandamana na badala yake walimuua.

''Nilifanya nilivyoambiwa kwenda kupiga kura na kurudi nyumbani'.Walitufuata hapa na kutupiga''.

Takriuban watu 24 waliuawa katika ghasia ambazo zilizuka baada ya uchaguzi wa tarehe 8 mwezi Agosti kulingana na shirika moja la haki za kibinaadamu

Kiongozi wa upinzani Raila Odinga alisema kuwa uchaguzi huo ulifanyiwa udanganyifu ili kumsaidia rais aliyepo madarakani Uhuru kenyatta kushinda.

Hatahivyo wachunguzi wa kimataifa wanasema kuwa uchaguzi huo ulikuwa huru na wa haki.

Umoja wa Mataifa Wakataa Ombi la Raila Odinga

$
0
0
Afisa wa Umoja wa Mataifa, amekataa ombi la kiongozi wa Muungano wa Upinzani nchini Kenya Nasa, Raila Odinga la kutaka umoja huo kufanya tathmini mpya ya uchaguzi mkuu wa Agosti 8.

Msemaji wa Umoja wa Mataifa, Farhan Haq, ameunga mkono kauli ya Katibu Mkuu, Antonio Gutrres, ya kuwataka wanasiasa wa Kenya wanaopinga matokeo ya uchaguzi kufikisha masuala hayo mbele ya taasisi zenye mamlaka ya kutoa maamuzi Kikatiba.

Bw. Haq amesema, Umoja huo utafuatilia kauli za Bw. Odinga kuhusu uchaguzi mkuu huku gazeti la Washington Post likisema uchaguzi wa Kenya ulikuwa huru na wa haki.

Mpinzani Mkuu wa Lungu atoka jela

$
0
0
Kiongozi mkuu wa upinzani nchini Zambia, Hakainde Hichilema aliyekuwa amewekwa mahabusu akikabiliwa na shtaka la uhaini ameachiliwa huru asubuhi hii.

Hichilema ameachiwa huru baada ya Mwendesha Mashtaka kumfutia mashtaka kiongozi huyo aliyekuwa mahabusu tangu Aprili mwaka huu.

"Mwendesha Mashtaka Mkuu ameamua kusitisha mchakato wa kesi kwa mamlaka ya kikatiba aliyonayo. Kwa hiyo, anaachiwa huru kuanzia sasa,” amesema Jaji wa Mahakama Kuu, Charles Chanda.

Hichilema na wenzake walikamatwa kwa madai ya kutaka kuhatarisha maisha ya Rais Edgar Lungu baada ya kiongozi huyo na wafuasi wake kukataa kupisha msafara wa rais huyo.

Habari za kuachiwa huru zilivuja tangu mwishoni mwa wiki, ikielezwa kwamba ni kutokana na juhudi zilizofanywa na Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Madola Patricia Scotland ambaye alifanya ziara nchini Zambia kuangalia hali ya siasa. Katibu huyo alikutana na kufanya mazungumzo na Rais Lungu na pia alimtembelea Hichilema katika gereza la Mukobeko.

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Gazi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0
Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Tupo Mbagala

Jipatie ofa ya kitabu cha PRESIDENT WIFE......Ni Riwaya Kali ya Kusisimua

$
0
0
Jipatie ofa ya kitabu cha PRESIDENT WIFE(Shadow of D.F.E) kwa sh 5000 kupitia mitandao ya Whatsapp 06570725588 na Email eddazaria G.Msulwa.
Pia unaweza kusoma kitabu cha SORRY MADAM season one pamoja na SHE IS MY WIFE kila kimoja utakipata pia kwa sh 5000.
 
HIZI NI BAADHI YA STORY NILIZO ZIANDIKA NA ZINAPATIKANA
1. AIISSII U KILL ME
2. AM NOT A DOCTOR sh 10000
3. MY LIFE sh 10000
4.HARD DAY sh 4000
5. SEX DEALERS sh 3000
6. MY MOM'S FRIEND sh 7000
NA NYINGINE NYNGI. 

KARIBUNI SANA NA NINAOMBA MUZIDI KUENDELEA KUNIUNGA MKONO KATIKA KIPAJI CHANGU HICHI CHA UANDISHI.
WASILIANA NAMI 0657072588 AU 0768516188
KARIBUNI SANA TENA SANA

Mwanaume Amuua Mpenzi Wake Kisha na Yeye Kujiua Dar

$
0
0
Binti mmoja aliyefahamika kwa jina la Maria Pius amezikwa leo makaburi ya Mwananyamala kwa Kopa baada ya mpenzi wake kumuua kwa kumpiga na kitu chenye nchi kali kisha mwili wake kuutupa kwenye shamba huko Chanika jijini Dar es Salaam.

Inasemekana siku ya Jumatatu mwanaume huyo ambaye jina lake halijafahamika alimpiga binti huyo na vitu vyenye ncha kali kwa kinachoelezwa kuwa ni wivu wa mapenzi mpaka alipopoteza maisha kisha muaji huyo aliandika ujumbe unaosema wasimatafute muuaji kwani amemuua yeye, kisha ujumbe huo aliuweka kwenye kifua cha binti huyo pamoja na simu mbili, simu ya mtuhumiwa pamoja na simu ya binti huyo.

Baada ya watu kugundua kuwa binti huyo ameuawa na kutoa taarifa kwenye vyombo vya dola inadaiwa siku ya kesho yake ambayo ni jana mwanaume huyo aliyedaiwa kufanya mauaji hayo naye aliamua kujitoa uhai kwa kujitumbukiza kwenye kisima cha maji na kupoteza maisha.

Baadhi ya ndugu na majirani wa binti huyo waliopo Mwananyamala sehemu ambayo alikuwa akiishi kabla ya kwenda huko Chanika na kuanza maisha na mwanaume huyo wamesema binti huyo alikuwa anaishi na mwanaume huyo Chanika lakini mwanaume huyo walikuwa hawamfahamu kwani hajawahi kujitambulisha kwao na wala binti huyo hajawahi kumpeleka.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Alhamisi ya August 17

Akamatwa na Polisi kwa kumpaka mwanae kinyesi

$
0
0
Mtu mmoja anashikiliwa na Jeshi la Polisi kwa kosa la kumfanyia ukatili mtoto wake wa kumpaka mavi ya mbuzi kwenye majeraha aliyoungua na  moto wilayani Nyamagana.

Kwamba tarehe 15.08.2017 majira ya saa 16:30hrs jioni katika Mtaa wa Chakechake – Mkuyuni Wilaya ya Nyamagana Jiji na Mkoa wa Mwanza, Sospeter Rajabu miaka 42, mvuvi na mkazi wa mtaa wa Chakechake – Mkuyuni, anashikiliwa na jeshi la polisi kwa kosa la kumfanyia ukatili mtoto wake aitwaye Neema Sospeter miaka 10, mwanafunzi wa darasa la kwanza, wa kumpaka mavi ya mbuzi kwenye majeraha ya moto aliyoungua maeneo ya mapaja ya miguu yote miwili kwa muda wa wiki mbili na kupelekea majeruhi kuwa na hali mbaya kiafya, kitendo ambacho ni kinyume na sheria.

Inadaiwa kuwa tukio hilo la ajali ya moto dhidi ya mtoto lilitokea tarehe 04.08.2017 majira ya saa 19:45hrs usiku, katika mtaa wa Kitangiri wilayani Ilemela ambapo majeruhi alikuwa akiishi na mama yake kwani wazazi wake walitengana kwa muda mr

Inasemekana ajali hiyo ya moto ilitokea baada ya majeruhi kumwagikiwa na mafuta ya taa pindi alipokuwa akiweka kwenye taa ya kibatari ndipo alipowasha moto na njiti ya kibiriti moto ulilipuka na kumuunguza kwenye maeneo hayo.

Inasemekana kuwa baada ya mama wa mwenye mtoto kukosa fedha za matibabu aliamua kumpeleka mtoto kwa baba yake Mtaa wa Chakechake – Mkuyuni alipokua akiishi na mke mwingine ili amsaidie mtoto apate matibabu, lakini inadaiwa kuwa baada ya mtoto kufikishwa kwa baba yake hakupelekwa hospitali badala yake alikuwa akipakwa mavi ya mbuzi na kupelekea hali yake kuzidi kuwa mbaya.

Wananchi walitoa taarifa polisi kuhusiana na tukio hilo, ambapo askari walifanya ufuatiliaji wa haraka hadi maeneo hayo na kufanikiwa kumkuta mtoto  akiwa kwenye hali ngumu.  Askari kwa kushirikiana na wananchi walimchukua mtoto huyo na kumkimbiza Hospitali ya Mkoa ya Sekou Toure kupatiwa matibabu huku baba wa mtoto Sospeter Rajabu akitiwa nguvuni.

Polisi wapo kwenye upelelezi na mahojiano na mtuhumiwa dhidi ya ukatili aliyokuwa akimtendea mwanae, pindi uchunguzi ukikamilika mtuhumiwa atafikishwa mahakamani.

Majeruhi amelazwa Hospitali ya Mkoa ya Sekou Toure akiendelea kupatiwa matibabu na hali yake inaendelea vizuri.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza Naibu Kamishina wa Polisi Ahmed Msangi anatoa wito kwa wananchi wa Mkoa wa Mwanza, kuwa pale ambapo kunatokea mtoto au mtu yeyote anapata majeraha au kuungua ni vizuri wakawaone madaktari katika hospitali ambapo wanaweza kupata huduma bora na stahiki za matibabu kuliko kutumia njia za kienyeji zisizofaa ambazo hazina ubora/usahihi, kwani kufuata njia ambazo si sahihi na bora kunaweza kupelekea kifo kwa mgonjwa.

Imetolewa na;

DCP: Ahmed Msangi

Kamanda wa Polisi (M) Mwanza

Serikali Kukutana na Wawekezaji wa Viwanda ilivyotangaza nia ya Kuvitwaa sababu ya Kusuasua katika uzalishaji.

Makamanda Zimamoto wapanguliwa

$
0
0
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Tanzania Bara, Thobias Andengenye amefanya mabadiliko ya baadhi ya Makamanda wa Mikoa na Wakuu wa Vitengo wa Jeshi hilo.

Katika mabadiliko hayo, aliyekuwa Kamanda wa Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa Arusha Kamishna Msaidizi (ACF), Bakari Mrisho amekuwa Mkuu wa Chuo na Mafunzo, nafasi yake inachukuliwa na Mrakibu (SF) Kennedy Komba, ambaye alikuwa Kamanda wa Zimamoto Mkoa wa Iringa na nafasi yake inachukiliwa na Mrakibu Msaidizi (ASF), James John toka Makao Makuu.

Kamanda wa Mkoa wa Kilimanjaro Kamishna Msaidizi (ACF), Gilbert Mvungi, amekuwa Kamanda wa Zimamoto Mkoa wa Kigoma, nafasi yake inachukuliwa na Kamishna Msaidizi (ACF), Baraza Mvano ambaye alikuwa Kamanda wa Zimamoto Mkoa wa Kigoma.

Kamanda wa Viwanja vya Ndege Nchini, Kamishna Msaidizi (ACF), Juma Kwiyamba amehamishiwa Makao Makuu, nafasi yake inachukuliwa na Kamishna Msaidizi (ACF) Christom Manyologa.

Kamishna Msaidizi (ACF) Fikiri Salla amekuwa Kamanda wa Mkoa wa Mbeya, anajaza nafasi iliyokuwa wazi baada ya Kamanda wa Zimamoto Mkoa wa Mbeya kuteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama, Dkt. John Pombe Magufuli kuwa Kamishna wa Usalama dhidi ya Moto.

Kamanda wa Zimamoto Mkoa wa Pwani, Mratibu Msaidizi (ASF) Goodluck Zelote amekuwa Kamanda wa Zimamoto Mkoa wa Tanga, nafasi yake inachukuliwa na Mrakibu Msaidizi (ASF) Happy Shirima toka Makao Makuu.

Mratibu Msaidizi (ASF), Fatma Ngenya amekuwa Kamanda wa Zimamoto Mkoa wa Manyara, anachukua nafasi ya Mkaguzi Msaidizi (A/INSP) Heriel Kimaro ambaye amehamishiwa Makao Makuu.

Uhamisho huo ni Mabadiliko ya kawaida yanayotokea ndani ya Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, katika kuongeza ufanisi wa utendaji kazi.

Pata Tiba ya Tiba ya Tatizo la Nguvu Za Kiume........Inasaidia Kukufanya Urudie Mara 5 na kuchelewa kwa Dakika 20

$
0
0
TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO LINATIBIKA.Baada ya utafiti wa mda mrefu juu ya matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume na ukosaji wa hamu ya tendo la ndoa ama kushindwa kurudia tendo kwa haraka DR Magise imekuletea tiba ya matatizo hayo kwa kutumia dawa za: 
 
FUUl POWER:Ni dawa asili ya vidonge inayotibu tatizo la upungufu au ukosefu wa nguvu za kiume,dawa hii inamchanganyiko wakutosha wenyekuzalisha vichocheo vingi vya Hemone za Gestrogen vikiwemo vitamin B6&B1,vitamini E,pamoja na madini aina ya zinc vitakufanya kuwa na nguvu na mzunguko mzuri wa damu na kuongeza hamu na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya hatua nne au zaidi,na kuchelewa kufika kileleni zaidi dakka 20-30.
 
NYAMVA:Inarutubisha maumbile ya uume yani kurefusha na kunenepesha nchi 4-7 upana cm3-4 standard kiafya haijalishi umri wako hata kwa wazee ukiitumia maumbile yako yatabaki kuwa hivyo siku zote,Pia tunatibu Presha,kisukari siku7,ngiri,chango la tumbo tumbo kujaa gesi,kutopata choo vizuri

 TUPO TZ DAR ES SALAAM .HUDUMA HII UTALETEWA POPOTE ULIPO .WASILIANA NAMI 0783741788,0715741788 -DR MAGISE

Odinga kutinga mahakamani kupinga matokeo

$
0
0
Kiongozi wa Muungano wa Vyama vya Upinzani nchini Kenya, Raila Odinga ametangaza rasmi kuwa muungano wake wa National Super Alliance (NASA) utawasilisha kesi mahakamani kupinga ushindi wa Rais Uhuru Kenyatta katika uchaguzi mkuu uliofanyika Jumanne wiki iliyopita.

Ameyasema hayo jana alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari jijini Nairobi, ambapo alisema kuwa ingawa muungano huo ulikuwa umeapa kutowasilisha kesi mahakamani kwa kipindi hiki, lakini wameona kuwa ni heri kufanya hivyo ili kuweza kufichua maovu yaliyojitokeza wakati wa uchaguzi mkuu.

“Tumeamua kwenda mahakamani kufungua kesi ili tufichue jinsi kura zilivyokuwa zikichakachuliwa, tuwaonyeshe Wakenya uovu uliokuwa ukifanyika wakati wa upigaji kura,na kupelekea kumpa ushindi Uhuru Kenyatta,” alisema Odinga

Aidha, Odinga alisema kuwa mitambo ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi IEBC ilidukuliwa na matokeo kuvurugwa kwaajili ya kumnufaisha, Uhuru Kenyatta ambapo kulikuwa na pengo dogo kati yake na mpinzani wake.

Hata hivyo, aliongeza kuwa udukuzi huo una uhusiano mkubwa na mauaji ya meneja wa teknolojia katika tume hiyo Chris Msando ambaye aliuawa wiki moja kabla ya uchaguzi huo kufanyika.

Hakimu Ataka Upelezi Wa Kesi Ya Viongozi Wa Simba Ukamilishwe Haraka

$
0
0
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imeutaka upande wa mashtaka katika kesi inayomkabili   Rais wa Klabu ya Simba, Evans Aveva na makamu wake, Godfrey Nyange maarufu kama Kaburu kueleza upelelezi umefikia wapi.

Hakimu Mkazi Mkuu, Victoria Nongwa alieleza hayo baada ya Mwendesha Mashtaka Mwandamizi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Leonard Swai kudai upelelezi bado haujakamilika.

Swai aliomba apewe siku 14 kwa ajili ya kukamilisha ripoti ya polisi ya upelelezi ambayo wanasubiri.

Kwa upande wa wakili wa utetezi, Mutakyamirwa Philemon  aliomba mahakama itoe siku saba, lakini Swai alisisitiza kuomba siku 14 kama ilivyo kwenye kesi nyingine.

Kesi hiyo imeahirishwa hadi Agosti 30, 2017 kwa ajili ya kutajwa ili kuangalia kama upelelezi umekamilika ama la.

 Aveva na Kaburu wanakabiliwa na mashtaka matano ya kughushi, kuwasilisha nyaraka ya uongo na kutakatisha fedha za kigeni Dola300,000 za Marekani.

Wanafunzi 106 watoroka usiku, wavamia sherehe na kupiga watu vibaya

$
0
0
Jeshi la Polisi mkoani Tabora linawashikilia wanafunzi 106 wa shule ya Sekondari ya Milambo kwa madai ya kufanya vurugu na kujeruhi wananchi zaidi ya sita katika eneo la jirani na shule hiyo.

Wanafunzi hao wa kidato cha sita wamefanya vurugu hizo usiku baada ya kutoroka shuleni na kuvamia kwenye sherehe ya harusi ambapo walitaka sherehe hiyo iendelee hadi muda watakao amua wao.

Akizungumzia tukio hilo, Kamanda wa Polisi mkoani humo, SACP Wilbroad Mutafungwa amethibitisha kutokea kwa tukio hilo ambapo ameeleza kuwa wanafunzi hao 106 wanashikiliwa na jeshi la polisi kuhusiana na tukio hilo. 

==>Tazama  tukio hilo hapo chini

Mapacha walioungana Wafariki Dunia

$
0
0
Pacha walioungana ambao walikuwa wakitumia pamoja baadhi ya viungo vya ndani, wamefariki dunia juzi jioni katika Hospitali ya Taifa Muhimbili wakiwa na umri wa siku 26.

Daktari bingwa wa upasuaji wa watoto wa hospitali hiyo, Zaituni Bokhari alisema jana kuwa watoto hao wamefariki dunia baada ya kupata maambukizi ya kifua kwa muda mfupi.

Alisema kutokana na hali waliyokuwa nayo ilikuwa ni rahisi kwao kupata maambukizi mbalimbali hasa kwenye mapafu na katika baadhi ya viungo vyao.

“Walikuwa wanaendelea vizuri sana ila (juzi) jana ndiyo walibadilika ghafla, wakaanza kuonekana wanapata tatizo la kupumua, hata hivyo, mmoja alizaliwa na tatizo la kupumua,” alisema Dk Bokhari.

Watoto hao walizaliwa katika Hospitali ya Misheni ya Berega, Morogoro, Julai 21.

Kutokana na hali zao, Julai 24 walifikishwa Muhimbili ambako walichukuliwa vipimo mbalimbali vya kuchunguza afya zao na kuangalia uwezekano wa kuwatenganisha.

Baada ya kufanyiwa vipimo vya kimaabara kwa takribani wiki nzima, iligundulika kuwa wanatumia pamoja baadhi ya viungo vya ndani ikiwamo moyo na ini.

Majibu hayo yalikuja baada ya vipimo vya radiolojia vikiwamo CT Scan, MRI, X Ray, moyo (ECO) pamoja na vipimo vyote vya damu.

Mbali ya kugundulika kuwa wanatumia pamoja baadhi ya viungo vya ndani ikiwamo moyo na ini, Dk Bokhari alisema watoto hao wameungana sehemu ya kifua na tumbo na baada ya vipimo vya CT Scan, ikaonekana pia kwamba kuna baadhi ya ogani zimeshikana.

Pia alisema majibu hayo ya CT Scan ya tumbo na kifua yalionyesha kuwa kuna chemba nyingi za milango ambazo walikuwa wakishirikiana.

Pamoja na hali hiyo, Dk Bokhari alisema jopo la madaktari lilikuwa limejiandaa kuwatenganisha watoto hao na kwamba kazi hiyo ilikuwa ifanyike katika miezi sita ijayo.

Jinsi Punyeto Inavyo Sababisha Ukosefu Na Upungufu Wa Nguvu za Kiume

$
0
0

Ukosefu  na/ama  upungufu  wa  nguvu  za  kiume, ni  tatizo  linalo  wakabili  mamilioni  ya  wanaume  duniani.  Zipo  sababu  nyingi  zinazo  sababisha  tatizo  la  ukosefu  wa  nguvu  za  kiume.  

Miongoni  mwa  sababu  hizo  ni  pamoja  na  maradhi  kisukari, presha,shinikizo  la  damu, moyo, figo, matatizo  kwenye  mishipa  ya  ubongo  &  mishipa  ya  uti  wa mgongo, matatizo  kwenye  mishipa itumikayo  kusafrisha damu  mwilini, maradhi  ya  ngiri,  pamoja  na   upigaji  punyeto  kwa  muda  mrefu.

Katika  makala  yetu  ya  leo, tutaangalia  namna   suala  la  upigaji  punyeto linavyo  athiri  nguvu  za  kiume.

Kabla  hatujaangalia  namna  suala la upigaji  punyeto linavyo  maliza  nguvu  za  kiume, ni  vyema  tukafahamu  kwanza  kuhusu  SAYANSI  YA  MFUMO  WA  NGUVU  ZA  KIUME.

Kufahamu   kuhusu   SAYANSI  YA  MFUMO  WA  NGUVU  ZA  KIUME  tafadhali  tembelea :

Ukisoma  vizuri  kuhusu  mfumo  wa  nguvu  za  kiume, utagundua  kuwa   Suala  la  nguvu  za  kiume  ni  suala  la  kimfumo.  Ili  mwanaume  awe na nguvu  za  kiume, aendelee  kuwa  na  nguvu  za  kiume na  azilinde  nguvu  zake za  kiume, ni  lazima  ogani  zote zinazo  husika  na  mfumo  wa  nguvu  za  kiume  ziwe  na  afya  njema  na  ziwe  na  ushirikiano   thabiti  na  wenye  afya.

Vile  vile , utagundua  kuwa , mambo  makuu  muhimu  katika   mfumo  wa  nguvu  za  kiume  ni  kama  ifuatavyo:

i.Mishipa  imara  ya  ubongo  na  yenye  afya  njema

ii. Mishipa  imara  ya  uti  wa  mgongo  (  spinal  cords )

iii.Mishipa  imara  itumikayo  kusafirisha  damu  mwilini  (  Blood Vessels )

iv. Mfumo  imara  wa  usafirishaji  damu  mwilini

v. Mishipa  ya  uume  iliyo  imara  na  yenye  afya  njema

vi. Uhusiano  imara  na  wenye  afya  kati  ya  mishipa  ya  fahamu  iliyopo  katika  ubongo, mishipa  ya  kwenye  uti  wa  mgongo  pamoja  na  misuli & mishipa  ya  kwenye  uume.

Hivyo  basi, ili  mwanaume  aweze  kuwa  na  nguvu  imara  za  kiume, na  aendelee  kuwa  na  nguvu  hizo ni  lazima  mambo  yote  muhimu  katika  mfumo  wa  nguvu za  kiume  yawe  imara  pasi na  hitilafu  yoyote.

Hitilafu  yoyote  katika  mambo  hayo, itasababisha  ukosefu na/ama  upungufu wa  nguvu  za  kiume  kwa  mwanaume  huyo.  Pale inapotokea    hitilafu  ama  mapungufu  katika  ogani  zaidi  ya  moja  kati  ya  zilizo  tajwa hapo  juu, basi  tatizo  kwa  muhusika  huwa  kubwa  mara  dufu.

JINSI  PUNYETO  INAVYO  SABABISHA  TATIZO  LA  UKOSEFU &  UPUNGUFU  WA  NGUVU  ZA  KIUME.
Mwanaume   anapopatwa na  wazo  la  kufanya  tendo  la  ndoa, ubongo  hutoa  ishara  kwenye  mishipa  ya  uti  wa  mgongo  ambayo  nayo  husafirisha  taarifa  hadi  kwenye  mishipa &  misuli  ya  uume.

Mishipa  ya  uume inapopokea  taarifa  hiyo, hutanuka. Na  mishipa  ya  uume  inapotanuka, hufanya  mambo  mawili  muhimu  sana :

i.Husababisha  mishipa  ya  ateri  kupanuka  na  hivyo  kuruhusu  damu  kuingia kwa  kasi  sana   ndani  ya  mishipa  ya  uume  na  hivyo  kuufanya  uume  usimame  na  kuwa  imara  bara bara.

ii. Huibinya na  kuiziba  mishipa  ya  vena  na  hivyo  kuzuia  kunyonya  ama  kufyonza  damu  iliyo  ingia  ndani  ya  mishipa ya  uume.  (  KAZI  KUBWA  YA  MISHIPA  YA  VENA  ILIYO  KARIBU NA  MISHIPA  YA  UUME  NI KUHAKIKISHA  HAKUNA  DAMU NDANI YA  MISHIPA  YA  UUME. HIVYO  BASI  DAMU  INAPOINGIA  NDANI YA  MISHIPA  YA  UUME, MISHIPA  YA  VENA  HU “SENSE” JAMBO  HILO  KWA  HARAKA  NA HIVYO  KUIFYONZA  DAMU  HIYO  KUTOKA KWENYE MISHIPA  YA UUME  YA  KUITOA  NJE YA MISHIPA  YA  UUME.  NA  DAMU INAPOKOSEKANA  NDANI  YA  MISHIPA  YA  UUME, HUUFANYA  UUME  KUSINYAA  NA  KULEGEA )

Mtu  anayepiga  punyeto  husababisha  mambo  yafuatayo  katika  mwili  wake :

1. Huuwa  nguvu  ya  mishipa  & misuli ya  uume ambayo  ndio  inayo husika  na  kusimama  kwa  uume

2. Mishipa  ya   uume  inapo  sinyaa  na  kukosa  nguvu  yake  ya  asili, husababisha  mambo  yafuatayo :

i.Huondoa  uwezo  wa  mishipa  &  misuli  ya  uume  kutanuka, na  hii  ndio  sababu  inayo  wafanya  waathirika  wa  punyeto  kutumia  nguvu  nyingi  sana  katika  kuufanya  uume  usimame.

ii.Huondoa  uwezo  wa  mishipa &  misuli  ya  uume  kuibana  na  kuiziba  mishipa  ya  vena, na  hii ndio  sababu  inayo  fanya  waathirika  wa  punyeto  kufika  kileleni  haraka  sana, kwani damu  inayo  ingia  kwenye misuli  ya  uume   hufyonzwa  ndani ya  muda  mfupi sana. 
 
 Hii  hutokea  kwa  sababu  mishipa na  misuli  ya  uume inakuwa  imelegea,na  mishipa  ya  vena inakuwa  imepwaya, hivyo  msuguano wowote ule  hufanya  mishipa  ya  vena  kufunguka  na  kufyonza  damu  kutoka  kwenye mishipa  ya  uume  na hivyo  kuufanya  uume  kusinyaa  ndani ya dakika ama sekunde  chache sana.

3. Vile  vile  punyeto  hufanya  uume  kusinyaa na  kurudi ndani  na  kuufanya  uonekane kama  uume  wa  motto mdogo.

Kwa  ufupi  punyeto  husababisha  ukosefu  wa  nguvu  za  kiume  kwa  sababu  kuu  zifuatazo :

i.Kwanza   hudhoofisha  na  kuharibu  mishipa  ya  uume,  ambayo  ndio  hufanya  uume kusimama.

ii.Pili  hudhoofisha  utendaji  kazi  wa  mishipa  ya  ateri, ambayo  ndio  hutumika  kama  njia  ya  kusafirisha  damu kupeleka kwenye  misuli  ya  uume  na  ivyo  kuufanya  uume  usimame

iii. Tatu, punyeto  hupelekea  kuvuja  kwa  mishipa  ya  vena  na  hivyo  kusababisha  damu  kufyonzwa  kwa  haraka  sana  kila  iingiapo ndani  ya  misuli ya  uume  na  matokeo  yake  ni  uume   kusimama  kwa  muda  mfupi  sana  wakati wa  tendo  la  ndoa.

iv. Punyeto  huathiri  mtiririko  wa  damu  kwenda  kwenye  mishipa  ya  uume, kwa  sababu  hudhoofisha  misuli &  mishipa  ya  uume  pamoja  na mishipa ya  ateri  ambayo  ndio  hutumika  katika  kusafirisha  damu kwenda  kwenye  uume

DALILI  ZA  MTU  ALIYE  ATHIRIWA  NA  PUNYETO
Dalili  kuu  za  mtu  aliye athiriwa  na  punyeto  ni  kama  ifuatavyo:

i.           Uume  kusinyaa  na  kuwa  kama  wa  mtoto
ii.         Uume kurudi  ndani
iii.       Uume  kusimama  ukiwa  legelege
iv.       Kufika  kileleni  haraka  wakati  wa  tendo  la  ndoa.

TIBA   YA   NGUVU  ZA  KIUME  KWA MTU  ALIYE  ATHIRIKA  NA  PUNYETO.
Dawa   asilia  ya  nguvu  za  kiume iitwayo JIKO  ni tiba  bora  na  ya  uhakika  kabisa  kwa  mtu  aliye  athiriwa   na  punyeto.  Dawa  hii, pamoja  na  mambo  mengine  mengi, husaidia  kufanya  mambio  yafuatayo  katika  mwili  wa  mwanaume  aliye  athiriwa  na  punyeto :

i.Kuimarisha  mishipa  & misuli  ya  uume  ulio  legea na  hivyo  kuurejeshea  uwezo wake wa  asili

ii. Hutibu   tatizo  la  uume  kurudi  ndani

iii.Humaliza  tatizo  la  kusimama  kwa  uume  ukiwa  legelege

iv.Hutibu  na  kuponya  kabisa  tatizo  la  kufika  kieleleni  haraka.

BEI  YA  DAWA  :  Dawa  hii  inapatikana  kwa  gharama  ya  SHILINGI  ELFU  THEMANINI  TU (Tsh. 80,000/=)

MAHALI  INAPOPATIKANA :  Dawa  hii  inapatikana  katika  duka  la  dawa  asilia  liitwalo  NEEMA  HERBALIST  &  NUTRITIONAL  FOODS  CLINIC  lililopo  jijini  DAR  ES  SALAAM  katika  eneo  la  UBUNGO   nyuma  ya  jengo  la  UBUNGO  PLAZA   karibu  na SHULE  YA  MSINGI  UBUNGO  NATIONAL  HOUSING.

Kwa  wateja  wasio  weza  kufika  ofisini  kwetu. Watafikishiwa  dawa  mahali  popote  walipo  jijini  DAR  ES  SALAAM.

Kwa   wateja  waliopo  mikoani  watatumiwa  dawa  kwa  njia  ya  MABASI

Kwa  wateja  waliopo   Zanzibar  wata fikishiwa  dawa  kwa  njia  ya  usafiri  wa boti.

Na  kwa  wateja  waliopo  UGHAIBUNI  watatumiwa  dawa  kwa  njia  ya  POSTA  ama  DHL.

MAWASILIANO :  WASILIANA  NASI   KWA  SIMU  NAMBA  0766  53  83  84.

Kwa  taarifa  zaidi  kuhusu  huduma  zetu, tutembelee kila  siku  kwenye  blogu  yetu :

Mawakili wa Kizungu Wakwamisha Maonbi ya Dhamana ya Bilionea Wa Escrow

$
0
0
Mawakili kutoka nje ya nchi wanaomtetea bilionea wa kampuni ya kufua umeme ya Independent Power Tanzania Limited (IPTL), Harbinder Singh Sethi, kuhusu kupewa dhamana, jana walikwamisha usikilizwaji wa maombi hayo.

Bilionea huyo na mwenzake James Rugemalira, wanakabiliwa na kesi ya uhujumu uchumi wakidaiwa kuchota mabilioni ya fedha kutoka katika Akaunti ya Tegeta Escrow ndani ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT), isivyo halali.

Pia, wanakabiliwa na mashtaka ya utakatishaji fedha ambayo ni miongoni mwa mashtaka yasiyo na dhamana, lakini washtakiwa, kila mmoja kwa wakati wake wameamua kusaka dhamana katika Divisheni ya Makosa ya Uhujumu Uchumi na Rushwa, maarufu kama Mahakama ya Mafisadi.

Hata hivyo, Mkurugenzi wa Mashtaka amemuwekea pingamizi bilionea huyo katika maombi yake hayo, ambalo lilipangwa kusikilizwa jana na Jaji Winfrida Korosso, lakini usikilizwaji wa pingamizi hilo ulikwama baada ya bilionea huyo kuamua kuyaondoa mahakamani maombi hayo.

Seth aliamau kuyaondoa mahakamani maombi hayo kutokana na kuhusisha mawakili kutoka nchini Afrika Kusini, ambao aliwakodi kuongeza nguvu kwa kushirikiana na mawakili wazawa kumpigania katika dhamana yake hiyo.

Maombi ya kuyaondoa maombi hayo mahakamani yalitolewa na kiongozi wa jopo la mawakili wanaomtetea bilionea huyo, Melkizedeck Lutema, baada ya kubainika mawakili hao wa nje hawakuwa na sifa za kufanya kazi nchini.

Ingawa mawakili hao walikuwa hawajatambulishwa mahakamani, lakini katika nyaraka mbalimbali zinazohusiana na maombi hayo, wametajwa kuwa miongoni mwa mawakili wake.

Kutokana na kasoro hiyo Wakili Lutema aliiomba mahakama iyaondoe maombi hayo kwa lengo la kuanza upya mchakato wa kuyawasilisha mombi ambalo mahakama iliridhia.

Wakili wa Serikali Mkuu, Dk Zainabu Mango, alisema mawakili hao hawana cheti cha kufanya kazi katika mahakama za hapa nchini kutoka kwa Jaji Mkuu.

Wakili Mango alisema kuwa ili wakili kutoka nje ya nchi aruhusiwe kufanya kazi katika mahakama za ndani ni lazima aombe kibali kutoka kwa Jaji Mkuu ambacho analazimika pia kukilipia, jambo ambalo mawakili hao hawakuwa wamelifanya.

Seth na Rugemalira wanakabiliwa na kesi hiyo ya uhujumu uchumi yenye jumla ya mashtaka 12 katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, kwa mujibu wa sheria za Tanzania mashtaka hayo hayana dhamana na hadi sasa washtakiwa wanasota mahabusu.

Watanzania Tuunge Mkono Juhudi za Rais Magufuli kwa Vitendo.

$
0
0
Na Agness Moshi – MAELEZO.
 Tukielekea miaka miwili tangu kuapishwa kwa Rais John Pombe Magufuli kuwa Rais wa Awamu Ya Tano wa Jamhuri Ya Muungano wa Tanzania ni wajibu wa kila Mtanzania mwenye kiu ya maendeleo na mzalendo kwa nchi yake kuunga mkono juhudi za Rais ili kuifikia Tanzania ya uchumi wa kati ifikapo mwaka  2025.

 Nakumbuka hotuba yake ya kwanza baada ya kula kiapo cha kulitumikia Taifa hili  aliyoitoa katika shughuli za kuapishwa uwanja wa Uhuru jijini Dar Es Salaam, Novemba 5, mwaka  2015 ambayo ilibeba maneno yenye busara, hekima na yenye hamasa ya  kuleta maendeleo ya nchi yetu.

 “Nchi yetu ni kubwa kuliko vyama vyetu vya siasa, mapenzi yetu na matakwa yetu.Uchaguzi Mkuu sasa umekwisha sote tushikamane kama watu wa Taifa moja kuijenga nchi yetu kwa kuweka itikadi na vyama vyetu pembeni”,alisema Rais Magufuli.

 Ni wazi maendeleo ya nchi hayana dini, kabila, itikadi au chama bali yana undugu na uzalendo, ushirikiano, umoja, kufanya kazi kwa bidii na amani baina ya wananchi na serikali kwa ujumla.

 Hivyo basi, tunawajibu wa kushikamana kama watoto wa baba mmoja na kufanya kazi kwa bidii na kuunga mkono juhudi  za Rais  Magufuli kwa vitendo ili tuweze kuifikisha Nchi kwenye uchumi wa kati utakaotuwezesha kupambana na maadui wakubwa watatu ambao ni Maradhi, Ujinga na Umaskini badala ya kukaa vijiweni kujadili mambo yasiyo na tija kwa  maendeleo yetu.

 Aidha, hivi karibuni tumeshuhudia Taasisi, Mashirika,Viongozi mbalimbali wa dini na serikali  na watu mbalimbali wakituma salamu za pongezi kwa Rais Magufuli kwa juhudi na utendaji kazi wake. Lakini je?,tumewahi kujiuliza pongezi hizi na za maneno tu au wanashiriki kwa vitendo?

 Sina maana kuwa, kumpongeza Rais ni vibaya au uovu,ni jambo jema lakini ingekua vyema zaidi kama pongezi zingeambatana na vitendo  kwani  “maneno bila vitendo si kitu” ndio maana Serikali  Awamu Ya Tano inaongozwa na  kaulimbiu  ya “HAPA KAZI TU” kwa lengo la kuhamasisha Watanzania kufanyakazi kwa  bidiii badala ya kusubiri serikali kuwafanyia kila kitu.Kauli mbiu hii imekua ikitumika pia nchi mbalimbali duniani ili kuhamasishana katika kufanyakazi na kujiletea maendeleo.

 Maneno ya Rais Magufuli alipohutubia Bunge la Jamhuri Ya Muungano wa Tanzania kwa mara ya Kwanza yanaishi na kutekelezwa kwa vitendo katika Serikali ya Awamu ya Tano hadi  kwa wananchi wenye kupenda maendeleo .

 “Kila mmoja wetu afanye kazi, awe shambani, ofisini, kiwandani, sokoni, kwenye bustani na kadhalika badala ya kupoteza muda vijiweni”, alisema Rais Magufuli.

Ni wazi kuwa , Rais Magufuli amekuwa kiongozi  anayeisimamia na kutekeleza kauli mbiu ya Serikali yake kikamilifu tangu aingie  madarakani kwa  kuwajibika ipasavyo katika kuhakikisha utekelezaji wa  miradi mbalimbali ambayo imekua na manufaa makubwa kwa wananchi na Serikali kwa ujumla.

 Hivi karibuni,  tumeshudia Mradi  wa ujenzi wa bomba la mafuta kutoka Hoima nchini Uganda mpaka kwenye bandari ya Tanga kwasababu  ni  moja ya mradi mkubwa ambao nchi imetekeleza na utakaobadilisha maisha ya watanzania takribani elfu 30 kwa wakati mmoja. Pia, kuinufaisha Serikali kupitia kodi na utengenezaji wa ajira kwa wananchi wake.

 Ipo miradi midogo ambayo imetekelezwa na tumeona , ikiwa ni pamoja na ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami, mfano barabara ya Msata-Bagamoyo na  Kagoma-Biharamuro-Lusahunga na  mabadiliko kwenye sekta ya afya ambayo yamekua msaada mkubwa katika  kubadilisha maisha ya watanzania na kuifanikisha safari ya nchi kuelekea uchumi wa kati na ujenzi wa Tanzania ya viwanda.

 Kama Serikali iliahidi na imetekeleza, yatupasa kuhakikisha tunafanya kazi kwa biidi kwenye miradi hiyo na kuhakisha tunailinda ili isiharibike kwa namna yoyote badala ya kutoa pongezi za maneno matupu.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images

<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>
<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596344.js" async> </script>