Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Saida Karoli Adai Kutishiwa Kuuawa......Aahirisha Show zake Kujinusuru

$
0
0
Ikiwa imepita miezi miwili toka msanii wa nyimbo za asili Tanzania Said Karoli arudi rasmi kwenye muziki na kuachia kazi zake mbili zilizopata mafanikio na kuwafikia watu wengi zaidi ameibuka na kudai watu wameanza kumpiga vita kishirikina na wanataka kumuua

Said Karoli ambaye sasa anafanya vyema na wimbo wake 'Orugambo' amedai kuwa ushirikina upo na watu wanampiga vita ili aweze kupotea tena kwenye muziki kama ilivyotokea kipindi cha nyuma na kudai kuna mtu amelipwa pesa ili amuuwe kabisa jambo lililopelekea kuahirisha baadhi ya show zake.

"Huyo mtu alinielekeza watu kadhaa ambao wamepanga mpango wa kuniua aliniambia, sasa mimi nimeshalipwa nikuuwe nikuondoe duniani kabisa yaani kabla ya kufika Mwanza, Geita tena bora hata hizi show zingine uvunje, kweli ramani aliyonipa nilichoka ikabidi show zingine za Bukoba tumezivunja tukasema ngoja tutulie kwanza tuone nini kitaendelea" alisema Said Karoli

Saida Karoli anakiri wazi kuwa suala la ushirikiana lipo na kwake si jambo la ajabu kumtokea kwani tayari ameshakutana na mambo ya namna hiyo sana na kudai yeye anamtegemea Mungu na kumuomba Mungu.

Lipumba Amwangukia Maalim Seifu.......Amtaka Arudi Ofisini, Wakutane na Kumaliza Tofauti Zao

$
0
0
Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF) anayetambuliwa na msajili wa Vyama Vya Siasa nchini Profesa Ibrahim Lipumba amemtaka Katibu Mkuu wa CUF Mhe. Maalim Seif Sharif Hamad kurudi wafanye mazungumzo na kumaliza tofauti.

Profesa Lipumba amesema hayo leo wakati akizungumza na waandishi wa habari katika Makao Makuu ya ofisi za Chama Cha Wananchi (CUF) zilizopo Buguruni.

 Lipumba amemtaka Katibu Mkuu huyo kurudi wafanye mazungumzo na atambue kuwa yeye ndiye Mwenyekiti wa CUF na ndiye boss wake.

"Maalim analalamika lakini malalamiko yake hayana msingi, yeye ni Katibu Mkuu anapaswa kufuata misingi ya Mwenyekiti, anatambua kuwa Mwenyekiti ni boss kwa mujibu wa Katiba ya CUF, Mwenyekiti nipo yeye aje kufanya kazi hapa. Maalim ni mkongwe wa siasa tunataka kuwa na maelewano, nampigia simu hapokei, nasikia saizi akija Dar es Salaam anakwenda uchochoroni huko Magomeni wakati tuna ofisi hapa nzuri, Katibu Mkuu unauzoefu wa kisiasa tufanye majadiliano ofisi zetu ziko hapa njoo tuzungumze" alisisitiza Lipumba

Aidha Lipumba amesema kama Katibu Mkuu wa CUF hatakuja ofisini kwa ajili ya majadiliano na mazungumzo kwa lengo la kumaliza migogoro yao basi Naibu Katibu Mkuu ataendelea kukaimu nafasi hiyo kwa mujibu wa Katiba yao ya CUF.

"Katibu Mkuu akishindwa kutekeleza majukumu yake Naibu Katibu Mkuu anafanya kazi kwa kufuata maelekezo ya Mwenyekiti ataendelea Kukaimu nafasi hiyo mpaka pale Katibu Mkuu atakapokuwa tayari kuja hapa ataruhusiwa kufanya kazi na ofisi yake ipo hapa, akiwa anakuja ofsini anafuata utaratibu na kufuata maelekezo yangu mimi sina shida ila kama hatakuja basi Naibu Katibu Mkuu ataendelea kufanya kazi" alisema Lipumba

Mbali na hilo Lipumba amesema kuwa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) toka kimempokea Mhe. Edward Lowassa wameacha ajenda ya ufisadi na wameiweka kando ajenda hiyo na kusema sasa hivi wao ndiyo ajenda yao hiyo.

Serikali yalipongeza Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC)

$
0
0
Serikali imelipongeza shirika la utangazaji la Tanzania(TBC) kwa kuendelea kurusha matangazo mubashara katika ziara  mbalimbali za viongozi hapa nchini ikiwemo ziara ya Rais wa Jamhuri Misri hapa nchini.

Pongezi hizo zimetolewa mapema hii leo jijini Dar es salaam na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan muda mfupi mara baada ya kuagana na Rais wa Misri katika uwanja wa Ndege wa kimataifa wa Julius Kambarage Nyerere.

Amesema kuwa shirika hilo la utangazaji linafanya vizuri ambapo limekuwa likihakikisha kuwa kila tukio kubwa limekuwa likirushwa mubashara hivyo kuwafikia wananchi moja kwa moja kwa wakati muafaka.

“Niwapongeze sana TBC, kwani tangu jana tumekuwa pamoja kwenye mapokezi mpaka leo hii tena wakati wa kumuaga, hivyo hongereni sana na nampongeza mkurugenzi wa TBC kwa kazi nzuri anayoifanya,”amesema Samia Suluhu.

Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) limekuwa likihakikisha linarusha matangazo mubashara ili kuweza kuifikia jamii moja kwa moja, hivyo kufikisha ujumbe kwa muda muafaka

Shamsha Ampongeza Rais Magufuli kwa Kuinyoosha Nchi

$
0
0
Malikia wa filamu bongo 'Shamsa Ford' amefunguka kwa kumshukuru Rais Magufuli kwa namna anavyoendesha nchi kwa sasa huku akidai ameweza kuwasaidia vijana kuwa wabunifu katika maisha yao tofauti na awali.

Shamsa ameeleza hayo kupitia ukurasa wake wa Instagram, baada ya kuwepo maneno ya muda mrefu kwa jamii hasa vijana kulalamika maisha yamekuwa magumu kwa kuwa Rais Magufuli amebana baadhi ya mirija ambayo vijana hao walikuwa wanaitumia kupata mahitaji yao ya kuendesha familia zao kila leo.

"Tunalalamika maisha ni magumu sana labda kwa kuwa hatujazoea hii hali, ila mimi nakupongeza sana Rais wangu Magufuli kwa kazi unayoifanya. Kwanza umetusaidia vijana kuwa wabunifu kila siku", ameandika Shamsa.

Pamoja na hayo, Shamsa ameendelea kwa kusema "walikuwa wamezoea kupewa tu pesa na kazi hawafanyi ila kwa sasa anaona kila kijana anafanya kazi kwa bidii na kuheshimu pesa vizuri. Hivyo suala hilo limeweza kusaidia hata kwa uchumi wa nchi kukua kutokana na kwamba kila kijana anafanya kazi kwa bidii".

Kwa upande mwingine, Shamsa amemuombea Rais Magufuli Mungu Amlinde amlinde na mabaya anayoombewa na baadhi ya watu ambao wanatamani yamfikie ili asiweze kutimiza yale aliyokusudia kuyatekeleza kwa wananchi wa Tanzania.

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Gazi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0
Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Tupo Mbagala

Atiwa Mbaroni Kwa Kujifanya ni Mkurugenzi wa Habari IKULU

$
0
0
Mfanyabiasha Ramadhani Athumani Juma maarufu kama Elias Jeremiah Mazimbaka amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu wakikabiliwa na shtaka la kujitambulisha   kuwa yeye ni Mkurugenzi wa Habari wa Ikulu, Gerson Msigwa.

Amesema hati ya mashtaka jana wakili wa Serikali, Jacqline Nyantori alidai kuwa kati ya Juni 28 na Julai 4,2017 Dar es Salaam kwa nia ya kudanganya alijitambulisha kama Gerson Msigwa ambaye ni Mkurugenzi wa Habari wa Ikulu kwa Ladslaus Matindi.

Amedai  kuwa mshtakiwa huyo alifanya kosa hilo katika kipindi hicho kwa lengo la kujaribu kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu

Mshtakiwa alikana shtaka upande wa mashtaka ulidai upelezi bado haujakamilika, Mshtakiwa ametakiwa kuwa na wadhamini wawili wanaoaminika ambao watasaini bondi ya sh 1 milioni.Kesi imeahirishwa 23,8,2017 na mtuhumiwa  hajakamilisha masharti hayo.

Wema Sepetu Mahakamani tena leo.........Uamuzi vielelezo kesi ya Wema kutolewa Agosti 18

$
0
0
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Agosti 18, 2017 itatoa uamuzi kuhusiana na kielelezo cha msokoto mmoja wa bangi na vipisi viwili vya bangi vipokelewe kama kielelezo ama la.

Uamuzi huo unatarajiwa kutolewa na Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba katika kesi inayomkabili  Mlimbwende wa Tanzania wa mwaka 2006, Wema Sepetu na wenzake wawili.

Ni baada ya Wakili wa Serikali, Costantine  Kakula kumuongoza ushahidi wa kwanza wa upande wa mashtaka,  Mkemia kutoka ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali, Elias Mulima kuendelea kutoa ushahidi wake.

Ambapo alidai kuwa alipima msokoto mmoja na vipisi viwili vinavyodaiwa kukutwa nyumbani kwa Wema na kugundua ni bangi.

Hata hivyo, Mulima kupitia Kakula aliomba kuitoa bahasha iliyofungwa juu yenye muhuri, saini ya shahidi huyo na namba ya maabara 291 ya 2017 mahakamani hapo kama kielelezo cha ushahidi.

Kakula alimuuliza ushahidi huyo baada ya Mahakama kuipokea bahasha hiyo, anakumbuka kuna vitu gani ndani ya bahasha hiyo?

Mulima alidai ndani ya bahasha kulikuwa na msokoto mmoja, vipisi viwili ndani yake vina majani ya bangi na akaomba shahidi huyo aifungue bahasha hiyo.

Shahidi aliifungua bahasha hiyo na kuomba kutoa msokoto mmoja na vipisi viwili vya bangi mahakamani kama kielelezo cha ushahidi.

Wakili Tundu Lissu alipinga kisipokelewe kama kielelezo cha ushahidi kwa sababu ndani ya bahasha hiyo kuna vitu zaidi ya msokoto mmoja na vipisi viwili vinavyodaiwa kuwa ni bangi.

Alidai Lissu vipisi viwili vyenye majani  ukiviangalia kwa makini ni vipisi vya sigara za kienyeji ambayo imetumika kwa sababu vina alama ya kuungua ambavyo kwao vinaitwa twagooso.

Lissu alibainisha kuwa kitu kinachoitwa msokoto wa bangi hakijulikani.

“Haiwezekani vitu vilivyotolewa kwenye bahasha kuwa ndiyo vitu shahidi alivielezea, mahakama isikubali kuvipokea kama kielelezo,” alieleza Lissu.

Kwa upande wa Wakili Kakula alidai kuwa amesikia mapingamizi ya upande wa utetezi na kwamba hayana msingi wowote kisheria.

Alidai kuwa wakati Shahidi wake anatoa ushahidi alieleza vitu vilivyokuwamo ndani ya bahasha msokoto mmoja na vipisi viwili vya bangi, hakuna kitu ambacho shahidi huyo kakisema kimekutwa hakipo.

Alibainisha kuwa huwezi kuongelea kila kitu bali vitu vya msingi na akaomba mahakama kupokea msokoto mmoja na vipisi viwili vya bangi kama kielelezo.

Lissu alisisitiza kuwa kila kilichomo kwenye bahasha hiyo iliyofungwa kilipaswa kutajwa na kwamba wateja wao wanakabiliwa na shtaka ambalo wakibainika wanahatia watafungwa.

Kutokana na hoja hizo Hakimu Simba alisema Agosti 18, 2017 atatoa uamuzi juu ya hoja hizo na kesi hiyo pia inaendelea kusikilizwa kwa ushahidi wa mashahidi wa upande wa mashtaka.

Awali katika ushahidi wa Mkemia huyo, Mulima alidai kuwa Februari 8, 2017 akipokea sampuli ya mkojo wa Wema.

Mwingine kafikishwa Mahakamani leo kwa Kukutwa na Sare za JWTZ

$
0
0
Mfanyabiashara wa Kariakoo, Casto Onyomolile Ngogo (35) amepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kujibu shtaka la uhujumu uchumi kwa kukutwa akiwa na suruali 5,000 za Jeshi la Wananchi (JWTZ), tisheti na vitu.

Akisoma hati ya mashtaka, Wakili wa Serikali, Wankyo Simon  kwa Hakimu Mkazi Mkuu,Thomas Simba  alidai kuwa Ngogo ambaye ni mkazi wa Tabata Segerea, Juni 15, 2017 alikutwa na vifaa hivyo katika maeneo ya bandari kavu ya Galco Inland Container (ICD) iliyopo Sokota Chang'ombe.

Wakili wa Serikali, Simon alidai kuwa siku hiyo, mshtakiwa huyo alikutwa  na suruali 5,000 za JWTZ zenye thamani ya Sh50 milioni ambazo zimepatikana kwa njia isiyo halali.

Ngogo anadaiwa kuwa Juni 15, 2017 katika eneo hilo alikutwa na maofisa wa Jeshi la Polisi akiwa na tisheti 50 za JWTZ zenye thamani ya Sh500, 000.

Aliendelea kudaiwa kuwa Juni 17, 2017 mshtakiwa huyo katika eneo la African Inland Container Deport alikutwa na polisi akiwa na pea 20 za viatu vya JWTZ bila ya kuwa na uhalali.

Mshtakiwa huyo hakuruhusiwa kuongea chochote kwa sababu shtaka linalomkabili Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu haina mamlaka ya kuisikiliza hadi Mahakama Kuu.

Hata hivyo, Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) amewasilisha hati ya kuzuia dhamana chini ya kifungu cha 36 (2) cha sheria ya uhujumu uchumi.

Kesi imeahirishwa hadi Agosti 29, 2017 kwa ajili ya kutajwa upelelezi bado.

Wafuasi 13 Watoka Nduki Mahakamani Baada ya Kesi Yao Kufutwa.....Polisi Wapambana Kuwanasa Tena

$
0
0
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imewaachia huru wafuasi 22 wa Chama cha CUF waliokuwa wakikabiliwa na mashtaka manne, likiwemo la kukutwa na mabomu ya machozi 10, ambayo yanatumiwa na Jeshi la Polisi.

Hakimu Mkazi Mwandamizi, Godfrey Mwambapa leo Jumanne, Agosti 15 amewaachia huru wafuasi hao chini ya kifungu cha 225 c ha mwenendo wa mashauri ya Jinai (CPA).

Kesi hiyo ilikuwa katika hatua ya washtakiwa hao kusomewa maelezo ya awali (PH) na leo washtakiwa hao walipaswa kusomewa, lakini Wakili wa Serikali, Nassoro Katuga amedai kuwa walikuwa bado hawajayaandaa  na akaomba iahirishwe.

Hata hivyo, wakili wa washtakiwa hao, Hashimu Mziray hakuwa na pingamizi lakini  Hakimu Mwambapa  kutokana na kesi hiyo kuahirishwa  mara kwa mara takribani mara sita aliifuta kesi hiyo na kuwaachia huru washtakiwa.

Baada ya washtakiwa hao kuachiwa huru askari polisi walianza kuwakamata kitendo ambacho kilizua purukushani kwa sababu washtakiwa hao walikuwa wakijikwamua mikononi mwa askari hao na kukimbia.

Hata hivyo, wengi wao walifanikiwa kukimbia na baadhi yao walikamatwa na kuwekwa chini ya ulinzi wa askari hao.

Pia, washitakiwa hao wanaodaiwa kutenda makosa hayo kati ya Zanzibar na Dar es Salaam wanatuhumiwa kuwa wanachama wa kikundi cha ‘Blue Guard’, kinachojitwika mamlaka ya polisi.

Washitakiwa hao waliokuwa wakikabiliwa na kesi hiyo  ni Hamis Omary Hamis, Said Mohamed Zaharani, Hamid Nassoro au Hemed, Nassoro Humudi Ally, Othuman Humud au Abdallah, Swalehe Ally Swalehe na Hamis Hamis Haji.

Wengine ni Majid Juma, Mohamed Khamis Ally, Ramadhan Juma, Juma Hamad Seif, Masoud Asa Fumu, Jecha Faki Juma, Mbaruku Bakari, Muhsin Ally Juma, Juma Omary Hamis na Haji Rashid Juma.

Pia, wamo  Ally Nassoro au Haji, Ally Juma Salum, Juma Haji au Mmanga, Mohamed Amir Mohamed na Mohamed Zuberi.

Kwa pamoja walikuwa wakidaiwa kuwa Septemba 20 na 25, mwaka 2016, katika maeneo mbalimbali ya Zanzibar na Dar es Salaam na wenzao, ambao hawapo mahakamani, walikula njama ya kutenda kosa kwa kuunda kikosi cha brigadi, ambacho kinafanya kazi kama polisi kinyume cha sheria.

Washtakiwa hao pia wanadaiwa katika tarehe hizo na maeneo hayo, wakiwa wanachama wa kikundi cha ‘Blue Guard’, kwa madhumuni ya kujiingiza katika ajira, walikuwa wakifanya majukumu ya polisi.

Wanadaiwa  kuwa Septemba 25, mwaka2016, maeneo ya Mwananyamala ‘A’, wilayani Kinondoni, Dar es Salaam, walikutwa wakimiliki visu vitano na mabomu 10 ya machozi.

Pia, wanadaiwa kuwa siku hiyo walikutwa wakimiliki mabomu hayo 10 ya machozi kinyume cha sheria, kwa kuwa kimsingi humilikiwa na Jeshi la Polisi.Walikana mashtaka hayo na walikuwa  wapo nje baada ya kukamilisha masharti ya dhamana waliyopewa.

Washtakiwa hao wanatetewa na wakili Hashimu Mziray ambaye alilaani kitendo cha askari hao wa polisi kuwakamata wateja wake bila ya kufuata utaratibu.

Chid Benz Akamatwa tena na dawa za kulevya

$
0
0

Jeshi la polisi  Mkoa wa Ilala, limewakamata watu saba akiwemo msanii wa muziki wa kizazi kipya, Rashid Makwiro maarufu kama ‘Chid Benz’ kwa tuhuma za kukutwa na dawa za kulevya aina ya Heroine.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala, Salum Hamduni amesema watuhumiwa hao walikamatwa Agosti 12 mwaka huu  saa 11.50 jioni wakijihusisha na uuzaji wa dawa za kulevya.

Amesema jeshi la polisi limefanya msako wake na kuwakamata    watuhumiwa hao wakiwa katika eneo ambalo linajihusisha na uuzaji wa dawa hizo.

“Chid Benz na wenzake  wapo kituo cha Polisi cha msimbazi ambapo tunaendelea na upelelezi ukikamilika tutawafikisha mahakamani na kiasi cha dawa zilizokamatwa zimepelekwa kwa mkemia mkuu na itajulikana ni kiasi gani za dawa za kulevya zilizokamatwa,”amesema  Hamduni.

Hamduni amesema jeshi hilo linafanya msako liweze kubaini mtandao mzima unaojihusisha na biashara ya dawa za kulevya na watumiaji ili kuhakikisha wote wanachukuliwa hatua na kufikishwa kwenye vyombo vya sheria.

Itakumbukwa kuwa , Oktoba 24,2014, Chid alikamatwa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere(JNIA) jiji la Dar es Salaam akiwa na dawa za kulevya, akijaribu kuvuka nazo kwenda mkoani Mbeya kushiriki onyesho la Instagram Party wakati akijua kuwa ni kinyume cha sheria .

Msanii huyo wa kizazi kipya alikiri shtaka hilo na ndipo , Februari 26 mwaka 2015,  Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu ilipomhukumu kifungo cha miaka miwili jela au kulipa faini ya Sh900,000 baada ya kupatikana na hatia ya katika makosa matatu likiwemo la  kukutwa na dawa za kulevya aina ya bangi na Heroine yenye thamani ya Sh 40,358.

Hata hivyo msanii huyo alifanikiwa kulipa faini na kukwepa kifungo hicho.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatano ya August 16

Japan yaahidi kuboresha miundombinu ya Dar ili kumaliza changamoto ya foleni

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli jana tarehe 15 Agosti, 2017 amekutana na kufanya mazungumzo na Mbunge na aliyewahi kuwa Waziri wa Mambo ya Nje wa Japan Mhe. Ichiro Aisawa Ikulu Jijini Dar es Salaam.

Katika Mazungumzo hayo Mhe. Ichiro Aisawa amempongeza Mhe. Rais Magufuli kwa uongozi mzuri, kupambana na rushwa na msukumo mkubwa anaoutoa katika maendeleo, juhudi ambazo zinasaidia kuimarisha uchumi na kuboresha huduma za kijamii.

Mhe. Ichiro Aisawa ambaye ametembelea baadhi ya miradi inayojengwa hapa nchini na kampuni za Japan ukiwemo mradi wa ujenzi wa barabara za juu (Flyover) wa TAZARA na Mradi wa kuzalishaji umeme kwa gesi wa Kinyerezi amemhakikishia Mhe. Rais Magufuli kuwa kampuni hizo zitafanya kazi nzuri na zitakamilisha kazi kama ilivyopangwa.

Pia Mhe. Ichiro Aisawa amesema baada ya kuona changamoto ya foleni katika Jiji la Dar es Salaam amebaini kuwa nchi yake bado inahitaji kuendelea kushirikiana na Tanzania katika kuboresha miundombinu ya Jiji la Dar es Salaam na ameahidi kufikisha ujumbe huo kwa Waziri Mkuu wa Japan Mhe. Shinzo Abe.

Kwa upande wake Mhe. Rais Magufuli amemshukuru Mhe. Ichiro Aisawa kwa kuja Tanzania na amemhakikishia kuwa Tanzania inatambua mchango mkubwa ambao Japan inautoa katika maendeleo, na itaendeleza na kukuza zaidi uhusiano na ushirikiano wake na Japan katika masuala mbalimbali.

Mhe. Rais Magufuli ameishukuru Japan kwa kutoa fedha kwa ajili ya kutekeleza miradi mikubwa ya ujenzi Jijini Dar es Salaam ikiwemo upanuzi wa barabara ya Mwenge – Morocco utakaoiwezesha barabara hiyo kuwa na zaidi ya njia nane, ujenzi wa barabara ya TAZARA, ujenzi wa Daraja la Gerezani njia nne, na barabara ya Bendera tatu hadi Kamata.

Aidha, Mhe. Rais Magufuli amemuomba Mhe. Ichiro Aisawa ambaye ni mwakilishi wa wabunge wa Japan wanaoshughulikia masuala ya Afrika kuwahamasisha wawekezaji na wafanyabiashara kutoka Japan kuja kuwekeza hapa nchini na ameahidi kuwa Serikali itahakikisha uwekezaji wao unalindwa kama itakavyofanya kwa kampuni ya kutengeneza rangi ya Kansai Plascon ambayo awali ilijulikana kama Sadolin, na kampuni inayozalisha Betri za Panasonic hapa nchini, ili uwekezaji huo ulete manufaa hapa nchini.

“Naomba unifikishie ujumbe kwa Waziri Mkuu Shinzo Abe kuwa Tanzania inamshukuru kwa ushirikiano huu mkubwa, tunamkaribisha sana Tanzania na kwa kuwa Serikali yetu imehamia Dodoma tutafurahi sana kama Japan itaweka alamu ya urafiki wetu kwa kutujengea barabara za Dodoma mjini, iwe ni flyover au kilometa 20 za barabara, sawa tu” amesema Mhe. Rais Magufuli.

Mazungumzo hayo yamehudhuriwa na Balozi wa Japan hapa nchini Mhe. Masaharu Yoshida.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam

Uhamiaji Yawataka Vigogo Wastaafu Warejeshe Paspoti za Kidipolamsia

$
0
0
Idara ya Uhamiaji inapenda kuufahamisha Umma kwamba, utolewaji wa pasipoti zenye hadhi ya Kidiplomasia (Diplomatic Passport) na Kiutumishi (Service Passport) upo kwa mujibu wa Sheria ya Pasipoti na Hati za Kusafiria Sura ya 42 ya mwaka 2002 pamoja na Kanuni zake.

Katika Vifungu Namba 10(2) na (3) na Jedwali la Pili na la Tatu la Sheria hiyo, makundi mbalimbali ya watu wanaostahiki kupewa pasipoti hizo yameainishwa.

Hivyo, Idara ya Uhamiaji inawataka wale wote ambao wamefikia ukomo wa Utumishi wa nyadhifa na hadhi hizo, warejeshe pasipoti hizo kwenye Ofisi za Uhamiaji ndani ya kipindi cha mwezi mmoja tangu tarehe ya kutolewa kwa taarifa hii, kama yalivyo matakwa ya Kifungu cha 8(2) cha Sheria tajwa hapo juu; isipokuwa wale ambao kwa mujibu wa nyadhifa zao wanaruhusiwa kisheria kuendelea kutumia Pasipoti hizo hata baada ya kustaafu kwao wakiwemo Viongozi Wakuu wa Nchi wastaafu, Wakuu wa Mihimili ya dola Wastaafu na Wakuu wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama Wastaafu kama ilivyoainishwa katika Jedwali la Tatu kwenye Sheria hiyo.

Baada ya kuisha kwa kipindi tajwa yaani mwezi mmoja baada ya kutolewa kwa taarifa hii, wasiostahiki kuwa nazo watazuiliwa safari zao mara watakapopita katika vituo vya kuingia na kutoka nchini ikiwa ni pamoja na Viwanja vya Ndege. Aidha, ieleweke kwamba, kuendelea kuwa na Pasipoti hizo kwa wasiostahiki ni kosa kisheria chini ya kifungu cha 19(2)(k) cha Sheria tajwa.

Imetolewa na
KITENGO CHA UHUSIANO,
IDARA YA UHAMIAJI,
MAKAO MAKUU.

15 AGOSTI, 2017.

Vigogo 6 Jijini Mbeya Kortini kwa Kutafuna Bilioni 5

$
0
0
Vigogo 6 kati ya 12 wanaotuhumiwa kuhusika kwenye kashifa ya ufisadi wa soko la Kimataifa la Mwanjelwa jijini Mbeya wamepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi mkoani Mbeya na kusomewa mashtaka matatu ya uhujumu uchumi.

Waliopandishwa kizimbani Mahakamani hapo ni aliyekuwa Meya wa jiji hilo, Athanas Kapunga (70)  aliyekuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Jiji hilo, Elizabeth Munuo (65) na aliyekuwa Kaimu Mkurugenzi wa Jiji hilo Dk. Samwel Lazaro ambaye kwa sasa ni Mganga Mkuu wa Mkoa wa Songwe.
 
Wengine ni aliyekuwa Mtunza Hazina wa Jiji hilo, James Jorojik (62), aliyekuwa Mwasibu wa jiji hilo, Tumaini Msigwa (47) na Mhandisi wa jiji hilo, Emily Maganga (42). 

Mwendesha mashtaka wa serikali, Shadrack Martin, akisaidiwa na Hebel Kihaka pamoja na Baraka Mgaya wakati akiwasomea mashtaka yanayowakabili vigogo hao alisema wote kwa pamoja walitenda makosa ya uhujumi uchumi kati ya mwaka 2008 na 2013 hivyo kuisababishia serikali hasara kubwa.

Katika Shtaka la kwanza mwendesha mashtaka huyo alisema linawahusu watuhumiwa waili ambao ni Athanas Kapunga ambaye alikuwa Meya wa Jiji la Mbeya na Elizabeth Munuo ambaye alikuwa Mkurugenzi wa Jiji ambao wanadaiwa kuisababishia halmashauri hiyo hasara ya Shilingi Bilioni 3.3, ambapo wanadaiwa kusaini mkopo wa kiasi hicho cha fedha kutoka katika Benki ya CRDB ambao ulianza kulipiwa riba kabla ya kuanza kujengwa kwa Soko hilo la Mwanjelwa kinyume cha vifungu vya sheria namba 57 (1) na 60 (1)  na (2)  vya Sheria za uhujumu uchumi Sura ya 200 ya mwaka 2002.

Martini alisema shtaka la pili linawahusu Dk.Samwel Lazaro, James Jorojik, tumain Msigwa na Emily Maganga ambao kwa pamoja wanadaiwa kushindwa kutekeleza majukumu yao kwa kuidhinisha malipo ya shilingi milioni 304,470,500 kwa Mkandarasi aliyekuwa anajenga soko hilo, Nandhra Engineering and Constaction ltd wakati kazi hiyo ilikuwa tayari imefanywa na Kampuni ya Tanzania Building Works ltd.

Aidha  Washtakiwa wa Shataka namba mbili pia wanashtakiwa kwa kosa la tatu la kuisababishia Halmashauri ya Jiji hasara ya shilingi 1,140,228,750 kwa kuidhinisha malipo ya fedha hizo kwa wakandarasi Tanzania Building Works na Nadhra Engineering kwa ajili ya ujenzi wa Soko hilo wakati kazi iliyotajwa haikuwemo kwenye Mkataba.

Washtakiwa hao kwa pamoja walikuwa wakitetewa na Mawakili watatu wakiongozwa na James Kyando, Baraka Mbwilo na Secilia Luhanga ambao waliiomba Mahakama hiyo kutoa maelezo kuhusu uwezekano wa wateja wao kupata dhamana. H

ata hivyo Mwendesha Mashtaka wa serikali alisema upelelezi wa shauri hilo bado haujakamilika hivyo akaiomba mahakama kupanga siku nyingine kwa ajili ya kutajwa tena.

Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi mkoa wa Mbeya, Michael Mteite alisema Mahakama haina uwezo wa kusikiliza kesi ya uhujumu uchumi hivyo washtakiwa wataendelea kukaa mahabusu hadi Agosti 29, Mwaka huu kesi hiyo itakapotajwa tena.

Kufikishwa Mahakamani kwa vigogo hao kunatokana na agizo la Waziri mkuu alilotoa Julai 31 mwaka huu wakati wa ziara ya kikazi jijini hapa alipozungumza na Watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbeya na Jiji na kuwataja wahusika 13 waliotajwa kwenye Ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali  (CAG) na kupendekeza wachukuliwe hatua.

Wananchi Wamwaga Machozi Moto Ukiteketeza Soko Kuu SIDO Jijini Mbeya

$
0
0
Soko kuu la Jijini Mbeya maarufu kama SIDO limeungua moto usiku wa kuamkia leo .Moto huo ulianza majira ya saa 3 usiku ambapo mali za wafanyabiashara mbalimbali katika soko hilo zimeteketea.

Kwa upande mwingine wananchi wamesikika wakimwaga machozi ya lawama kwa Jeshi la Polisi wakilaumu kutoruhusiwa  kusogea eneo la tukio kuokoa mali zao kwa kuwafyatulia risasi hewani.
Hii ni mara ya tatu sasa ambapo soko hili liliisha ungua mara mbili mfululizo kabla ya  kuungua tena kwa mara nyingine  usiku wa kuamkia leo.

==> Tazama video ya tuki hilo hapo chini

Wanafunzi wa fani za afya na Sayansi Kupewa Asilimia 40 ya Mkopo Wote Elimu ya Juu (HESLB) 2017/2018

$
0
0
Zaidi  ya wanafunzi 30,000 wa vyuo vya elimu ya juu nchini kwa mwaka mpya wa masomo 2017/18, watanufaika na Sh bilioni 427 kutoka Bodi Mikopo ya Elimu ya Juu (HESLB), huku wanufaika hao wakiwekwa kwenye mikondo mitatu.

Jana Mkurugenzi Mtendaji wa HESLB, Abdul –Razaq Badru alisema kwa mwaka huu wanufaika wasiopungua 30,000 watapata mikopo ya elimu kulingana na fani walizochagua kusoma.

Akifafanua idadi na kiwango cha mkopo kitakachotolewa kwa kila mkondo kulingana na fani watakazosoma, Badru alisema bodi imepanga mikondo mitatu ya mikopo. 

Mkondo wa kwanza unawahusu wanafunzi wa fani za afya, sayansi ya elimu na hesabu, ambapo kundi hilo litapata asilimia 40 ya mkopo huo ambao ni sawa na Sh bilioni 170.8.

Badru alisema kundi hilo ndilo litapata mkopo mkubwa kuliko makundi mengine kutokana na fani hizo kuwa adimu na zina mahitaji makubwa ya soko nchini hasa kwa kuwapata wataalamu watakaosaidia taifa kwenye sekta za afya, sayansi na elimu.

Mkondo wa pili umepangwa kupata asilimia 35 ya mkopo wote ambao ni sawa na Sh bilioni 149.45 na wanafunzi watakaonufaika ni wale wa fani za uhandisi, kilimo, misitu, sayansi ya ardhi, usafirishaji na fani kama hizo.

Mkondo wa tatu umepangwa kupata asilimia 25 ya mkopo wote ambao ni sawa na Sh blioni 106.75 na wanufaika wa mkopo huo ni wanafunzi wote watakaosoma fani za lugha, sanaa, jamii na fani nyingine kama hizo.

Badru alisema pamoja na bodi kuweka mikondo hiyo, lakini pia suala la jinsia litazingatiwa ili kuepusha jinsi moja kuwa na idadi kubwa ya wanufaika wa mikopo hiyo. 

Katika hatua nyingine kwa mwezi mmoja uliopita, bodi hiyo imekusanya marejesho ya mkopo ya Sh bilioni 31.1 huku ikiweka mikakati ya mwaka huu ya kukusanya kila mwezi zaidi ya Sh bilioni 14.

Mtendaji huyo wa HELSB alisema lengo lao ni kuhakikisha wanufaika wote wanafikiwa na kurejesha madeni yao ili yasaidie wengine kupata elimu. 

Alisema mikakati yaliyojiwekea kuanzia mwaka huu ni kukusanya zaidi ya Sh bilioni 14 kila mwezi na kwamba tangu mwaka huu wa fedha uanze, kwa mwezi Julai pekee wamekusanya Sh bilioni 31.1 huku sekta ya umma ikiongoza kwa wanufaika wake kurejesha madeni yao.

“Tunakwenda vizuri na tumejiwekea mikakati ya kuhakikisha madeni ya mikopo hiyo yanarejeshwa ili yaweze kunufaisha wengine, kwa sekta ya umma tumefanikiwa kuwafikia asilimia 82 ya wadaiwa wote na sekta binafsi tumefanikiwa kwa asilimia arobaini,” alisema Badru.

Aliongeza kuwa hivi sasa wameweka nguvu kwenye sekta binafsi, kwa kuwa imekuwa vigumu kuwafikia wadaiwa wote kutokana na sekta hiyo waajiriwa wake kuhamahama kila wakati au kuacha kazi.

Akizungumzia mikakati ya kukusanya madeni ya mikopo hiyo, Badru alisema wapo mbioni kuanzisha kampeni ya ‘’Kurejesha mkopo ni uzalendo uliotukuka’’, itakayofanywa nchi nzima kuhamasisha wanufaika wa bodi hiyo kujenga tabia ya kurejesha kwa hiari madeni yao.

Alitaja mkakati mwingine ni bodi hiyo hivi sasa iko kwenye hatua za awali za mazungumzo na taasisi za fedha nchini ili kuona jinsi ya wao kununua mikopo hiyo ya wadaiwa kupitia waajiri wao.

Awali operesheni ya utafutaji, ufuatiliaji na ukaguzi wa wadaiwa sugu wa bodi hiyo mahala pa kazi yaliyoendesha mapema mwaka huu kwa kipindi cha mwaka mmoja uliopita, ilifanikiwa kwa kukusanya Sh bilioni 116 ikiwa ni kiwango cha marejesho cha asilimia 46, huku awali walilenga kukusanya Sh bilioni 76.

Hata hivyo, aliwakumbusha waajiri wote nchini kuhakikisha wanatoa taarifa za waajiri wanaodaiwa na bodi hiyo na kuhakikisha wanakata asilimia 15 ya mshahara yao na kuipeleka bodi ili kulipa madeni yao

Credit:Habari leo

Kutana na Mtaalamu wa Kusafisha Nyota........Anatoa Mvuto wa Biashara, Kupandishwa Cheo, Kurudishiwa Mali Uliyoibiwa na Mengne

$
0
0
Kutana na Mtaalamu wa Kusafisha Nyota........Anatoa Mvuto wa Biashara, Kupandishwa Cheo, Kurudishiwa Mali Uliyoibiwa na Mengne
 
Kutana Maajabu ya Mtabibu MAALIM MOHAMEDI MASUDI Mganga wa Waganga Sasa Yupo Mikoa Yote Tanzania
Pia anatoa Tiba kwa Njia ya Simu ukiwa popote Pale Tanzania au Nje ya Tanzania..
MAALIM MOHAMEDI MASUDI ni Mtabibu na Mtafiti wa Dawa za Asili ya Africa, na Duniani Katika utoaji wa Tiba za Asili..
 
Je unasumbulia na Mapenzi..?
(Umeachwa na Umpendae awe Mume/ Mke au mpenzi na Anaishi na Mtu Mwingine na Bado Unampenda?) Umejaribu sehemu Nyingi bila Mafanikio?Wasiliana na MAALIM MOHAMEDI MASUDI Akusaidie Kumshika Umpendae Asikusaliti(LIMBWATA) Kumtawala Mpenzi wako kwa sababu Maalum..Anauwezo wa Kusambalatisha Mahusiano yao ndani ya siku Moja tu.
Je Unasumbuliwa na Madeni?
Biashara yako Haina wateja?
Unatatizo la kutokushika Mimba na umehangaika sehemu nyingi bila mafanikio?
Wasiliana na MAALIM MOHAMEDI MASUDI Kwa Majibu ya Maswali yako..

Anasafisha NYOTA na Kutoa PETE za BAHATI kuendana na NYOTA yako. UTAJIRI USIO NA MASHARTI.(Magic Wallet_Pochi ya Maajabu Isio Isha Hela)
KUWA MAARUFU na KUJULIKANA
Kupandishwa CHEO na HESHIMA Mahala pa KAZI.
Utapewa Nguvu ya Kujilinda na MALI ZAKO zako na Mwili wako.. Huzuia Chuma Ulete katika Biashara.. Hurudisha MALI zilizo Potea au KUDHULUMIWA.

Mvuto wa Biashara na Mwili wako.
Hutibu kabisa Nguvu za Kiume na Kurefusha Uume kwa saizi Unayotaka.
Magonjwa Sugu(Miguu Kufa Ganzi, kisukari, Presha, Pumu nk.
Wasiliana nae kwa namba
0655516982
0688856265
0621898709(Whatsapp)

Kwa Nini Wanaume Wengi Wanaupungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo?

$
0
0
Asilimia 45 ya wanaume wapo tofauti na wengine kwa kuwatimizia vyema wake au wapenzi Wao na kuwasababishia kutoka nje ya ndoa zao.

NINI CHANZO CHA HAYO?Kupiga punyeto,Ngiri,Vidonda vya tumbo,Magonjwa ya moyo,Presha,Kisukari,Korodani moja kuvimba,Msongo wa mwazo,Kufanyiwa tohara ukiwa mtu mzima n.k.DOKTA MANYANDA sasa kapata tiba sahihi ya tatizo la NGUVU ZA KIUME.

MUHAMA:Hii hutibu na kuponyesha kabisa tatizo la nguvu za kiume,utakuwa na uwezo wa kurudia tendo zaidi ya mara tatu bila kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dakika 15-20.DAWA hii imechanganywa miti 12.Hata wazee wenye umri mkubwa wanapona kabisa.OKO NDOA YAKO SASA. 

MANGUNGU MIX: Ndio tiba tosha kwa sasa ambayo hurefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo inch 1-8 na unene sentimita 1-5,dawa hii ipo ya kupaka na kunywa na haina madhara yoyote kwa mtumiaji.

NITOFAUTI NA ULIZO WAHI KUZITUMIA.Pia tuna dawa za kupatanisha mke,mme,mpenzi au bosi wako kwa mda mfupi sana,Uzazi,Kusafisha nyota,

Je unamali yako unauza hupati wateja?Wasiliana nami 0716-263605 

DOKTA MANYANDA ANAPATIKANA KASULU KIGOMA,Kwa wale wa mikoani huduma hii utaipata popote pale.

Pata Tiba ya Tiba ya Tatizo la Nguvu Za Kiume........Inasaidia Kukufanya Urudie Mara 5 na kuchelewa kwa Dakika 20

$
0
0
TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO LINATIBIKA.Baada ya utafiti wa mda mrefu juu ya matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume na ukosaji wa hamu ya tendo la ndoa ama kushindwa kurudia tendo kwa haraka DR Magise imekuletea tiba ya matatizo hayo kwa kutumia dawa za: 
 
FUUl POWER:Ni dawa asili ya vidonge inayotibu tatizo la upungufu au ukosefu wa nguvu za kiume,dawa hii inamchanganyiko wakutosha wenyekuzalisha vichocheo vingi vya Hemone za Gestrogen vikiwemo vitamin B6&B1,vitamini E,pamoja na madini aina ya zinc vitakufanya kuwa na nguvu na mzunguko mzuri wa damu na kuongeza hamu na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya hatua nne au zaidi,na kuchelewa kufika kileleni zaidi dakka 20-30.
 
NYAMVA:Inarutubisha maumbile ya uume yani kurefusha na kunenepesha nchi 4-7 upana cm3-4 standard kiafya haijalishi umri wako hata kwa wazee ukiitumia maumbile yako yatabaki kuwa hivyo siku zote,Pia tunatibu Presha,kisukari siku7,ngiri,chango la tumbo tumbo kujaa gesi,kutopata choo vizuri

 TUPO TZ DAR ES SALAAM .HUDUMA HII UTALETEWA POPOTE ULIPO .WASILIANA NAMI 0783741788,0715741788 -DR MAGISE

Zambia: Kuanzia Sasa Kila Mwananchi ni Lazima Apimwe UKIMWI, Sio Hiari Tena

$
0
0
Rais wa Zambia, Edgar Lungu, ametangaza kwamba wananchi wote wanaofika katika vituo vya afya vya serikali wapimwe virusi vya Ukimwi kwa lazima, wapatiwe ushauri nasaha na tiba.

Rais Lungu amesema, sera hiyo mpya inaenda sawia na agenda ya serikali ya kutokomeza virusi vya HIV nchini humo ifikapo mwaka 2030.

Katika tangazo hilo, kiongozi huyo amesisitiza umuhimu wa kulinda maisha ya wale walioathirika na wale ambao wako hatarini kuambukizwa virusi hivyo.

Amesema, licha ya sera hiyo kukiuka haki ya mtu kupima kwa hiari lakini akasisitiza kuwa hakuna mtu mwenye haki ya kuweka rehani maisha ya binadamu mwenzake.

Sera hiyo inakiuka muongozo wa Shirika la Afya Duniani, WHO, na Shirika la Ukimwi la Umoja wa Mataifa, UNAIDS, unaohamasisha watu kupima Vvu na kupata ushauri nasaha kwa hiari.

Zambia ni miongoni mwa nchi zenye kiwango cha juu cha maambukizi ya ugonjwa huo kusini mwa bara la Afrika ikiwa na asilimia 11.6 huku watu walio na umri wa miaka kuanzia 15 mpaka 49 wakiishi na virusi vya ukimwi.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live


Latest Images