Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Idara ya Uhamiaji Yatoa Ufafanuzi Kuhusu Kukamatwa na Kuhojiwa kwa Kigogo wa Kampuni ya ACACIA Akiwa Uwanja wa Ndege


TANZIA: Mmiliki wa Hoteli za Ngurdoto, Impala na Naura Springs za Arusha, Afariki dunia

$
0
0
Mfanyabiashara maarufu nchini anayemiliki hoteli za kifahari jijini Arusha, Maleu Mrema amefariki dunia  nchini Afrika Kusini alipokuwa akipatiwa matababu.
 
Kwa mujibu wa familia ya marehemu, Maleu ambaye anamiliki Hoteli za Impala, Naura, Ngurdoto zilizopo jijini Arusha, wamesema ndugu yao alifia Afrika Kusini na kwamba taarifa zaidi kuhusu msiba huo zitatolewa leo.
 
Familia wamesema hadi sasa hawajapata taarifa rasmi kutoka hospitalini hapo kuelezea chanzo cha kifo cha mpendwa wao.
 
Mrema alipelekwa Afrika Kusini mwezi Juni mwaka huu baada ya kusumbuliwa na matatizo ya kiafya.

The Impala Group of Hotels inajumuisha:
1) Impala hotel (Arusha)
2) Impala hotel (Moshi)
3) Ngurdoto Mountain Lodge (Arusha)
4) Naura Springs Hotel (Arusha)
5) Impala shuttle Services (Arusha)
6) The Classic Tours & Travels

Ufafanuzi wa serikali kuhusu kuzuiwa kwa uzinduzi wa filamu ya Mangwangala mkoani Geita.

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Gazi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0
Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Tupo Mbagala

Kwa Nini Wanaume Wengi Wanaupungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo?

$
0
0
Asilimia 45 ya wanaume wapo tofauti na wengine kwa kuwatimizia vyema wake au wapenzi Wao na kuwasababishia kutoka nje ya ndoa zao.

NINI CHANZO CHA HAYO?Kupiga punyeto,Ngiri,Vidonda vya tumbo,Magonjwa ya moyo,Presha,Kisukari,Korodani moja kuvimba,Msongo wa mwazo,Kufanyiwa tohara ukiwa mtu mzima n.k.DOKTA MANYANDA sasa kapata tiba sahihi ya tatizo la NGUVU ZA KIUME.

MUHAMA:Hii hutibu na kuponyesha kabisa tatizo la nguvu za kiume,utakuwa na uwezo wa kurudia tendo zaidi ya mara tatu bila kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dakika 15-20.DAWA hii imechanganywa miti 12.Hata wazee wenye umri mkubwa wanapona kabisa.OKO NDOA YAKO SASA. 

MANGUNGU MIX: Ndio tiba tosha kwa sasa ambayo hurefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo inch 1-8 na unene sentimita 1-5,dawa hii ipo ya kupaka na kunywa na haina madhara yoyote kwa mtumiaji.

NITOFAUTI NA ULIZO WAHI KUZITUMIA.Pia tuna dawa za kupatanisha mke,mme,mpenzi au bosi wako kwa mda mfupi sana,Uzazi,Kusafisha nyota,

Je unamali yako unauza hupati wateja?Wasiliana nami 0716-263605 

DOKTA MANYANDA ANAPATIKANA KASULU KIGOMA,Kwa wale wa mikoani huduma hii utaipata popote pale.

Pata Tiba ya Tiba ya Tatizo la Nguvu Za Kiume........Inasaidia Kukufanya Urudie Mara 5 na kuchelewa kwa Dakika 20

$
0
0
TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO LINATIBIKA.Baada ya utafiti wa mda mrefu juu ya matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume na ukosaji wa hamu ya tendo la ndoa ama kushindwa kurudia tendo kwa haraka DR Magise imekuletea tiba ya matatizo hayo kwa kutumia dawa za: 
 
FUUl POWER:Ni dawa asili ya vidonge inayotibu tatizo la upungufu au ukosefu wa nguvu za kiume,dawa hii inamchanganyiko wakutosha wenyekuzalisha vichocheo vingi vya Hemone za Gestrogen vikiwemo vitamin B6&B1,vitamini E,pamoja na madini aina ya zinc vitakufanya kuwa na nguvu na mzunguko mzuri wa damu na kuongeza hamu na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya hatua nne au zaidi,na kuchelewa kufika kileleni zaidi dakka 20-30.
 
NYAMVA:Inarutubisha maumbile ya uume yani kurefusha na kunenepesha nchi 4-7 upana cm3-4 standard kiafya haijalishi umri wako hata kwa wazee ukiitumia maumbile yako yatabaki kuwa hivyo siku zote,Pia tunatibu Presha,kisukari siku7,ngiri,chango la tumbo tumbo kujaa gesi,kutopata choo vizuri

 TUPO TZ DAR ES SALAAM .HUDUMA HII UTALETEWA POPOTE ULIPO .WASILIANA NAMI 0783741788,0715741788 -DR MAGISE

Mazoezi ya Kijeshi ya Kihistoria Kufanyika Nchini......Yanahusisha Majeshi ya Nchi 7 za SADC

$
0
0
Vikosi maalumu vya majeshi ya nchi za Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) vimepiga kambi kwenye eneo la mapango ya Amboni, Tanga kwa ajili ya mazoez ya kijeshi.

Katika mapango hayo, mwaka jana yalitokea mauaji yaliyofanywa na watu wasiojulikana na kuzua hofu kwa wakazi wa eneo hilo ambao mwishowe walihamishwa na Serikali.

Akizungumza na waandishi wa habari   jana, Mkuu wa mpango huo, Meja Jenerali Harrison Msebo, alisema vikosi hivyo vitakuwa vikifanya mazoezi katika eneo hilo kama sehemu ya kupambana na ugaidi na uharamia baharini.

Kwa mujibu wa Meja Jenerali Msebo, mazoezi hayo yajulikanayo kwa jina la EX Matumbawe, yanatarajia kuanza Agosti 2 hadi Septemba mosi mwaka huu.

“Mazoezi hayo yanafanyika kwa mara ya kwanza  Tanzania baada ya vikosi vya majeshi ya nchi washirika kuanza kufanya mazoezi ya pamoja kwa ajili ya kujihami dhidi ya matukio mbalimbali ya uhalifu tangu mwaka 2015.

“Pamoja na mambo mengine, lengo letu ni kuhakikisha vikosi vya majeshi katika nchi washirika vinajengewa uwezo wa kupanga na kutekeleza operesheni za vikosi maalumu  na kujifunza mbinu na weledi katika kupambana na matukio ya uvamizi yanayoweza kufanywa na maharamia na magaidi.

“Mazoezi hayo yanatokana na mbinu za kupigana vita pamoja na matishio ya ugaidi kubadilika mara kwa mara.

“Hivyo kupitia mazoezi hayo, tutaweza kuvitayarisha vikosi vyetu dhidi ya mapambano ya aina yoyote yanayoweza kutokea,” alisema Meja Jenerali Msebo.

Alizitaja nchi zenye majeshi yatakayoshiriki mazoezi hayo  kuwa ni Afrika Kusini, Botswana, Lesotho, Malawi, Zambia, Zimbabwe   na wenyeji Tanzania.

Naye  Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Martine Shigela, alisema mazoezi hayo yataimarisha uhusiano wa kijeshi baina ya nchi wanachama wa SADC na yatawasaidia wanajeshi hao kubadilishana uzoefu katika utendaji kazi wao.

“Kwa hiyo napenda kuwaomba wananchi, kwamba watoe ushirikiano wakati wote wa mazoezi hayo ingawa pia nawaomba wananchi wasipende kuokota vitu ambavyo wana hofu navyo.

“Kama wananchi wakiona kitu wasichokielewa, basi watoe taarifa wahusika waje kuvitambua badala ya kuviokota kwa ajili ya matumizi yao,” alisema Shigela.

Wakati mazoezi hayo yakitarajia kuanza mwaka jana hali ilikuwa tete na ilizua taharuki jijini Tanga baada ya watu wasiojulikana, kuua idadi kadhaa ya watu katika eneo la mapango hayo.

Serikali ililazimika kupeleka vikosi vya Jeshi la Polisi na askari wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) kwa ajili ya kukabiliana na wahalifu hao.

Wakati vikosi hivyo vya ulinzi na usalama vikifanya kazi, vilikuwa vikiendesha operesheni maalumu ya upekuzi ndani ya mapango hayo kwa lengo la kukabiliana na wahalifu hao.

Kutokana na hali ya usalama kuwa tete katika eneo hilo, baadhi ya watu walilazimika kuhama makazi yao kuokoa maisha yao.

Askofu Josephat Gwajima Kashindwa Kufika Mahakamani Leo Kusikiliza Hukumu ya Kesi Yake

$
0
0

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Agosti 30, 2017 itatoa hukumu katika kesi ya kushindwa kuhifadhi silaha na risasi inayomkabili Askofu wa Kanisa la ufufuo na uzima, Josephat Gwajima na wenzake watatu.

Hukumu hiyo ilipaswa kutolewa leo Jumatatu, Julai 31 kwa Hakimu Mfawidhi, Cyprian Mkeha lakini ilishindikana kwa sababu hakimu huyo alikuwa na udhuru.

Hata hivyo, Wakili Peter Kibatala amemueleza Hakimu Mkazi Mkuu, Godfrey Mwambapa wakati kesi ilipoitwa mbele yake kuwa Askofu Gwajima ni mgonjwa na mahakamani hapo amewakilishwa na mdhamini wake.

Hayo yametokea baada wakili wa Serikali, Shedrack Kimaro kuiambia mahakama kuwa washtakiwa George Mzava, Msaidizi wa Askofu Gwajima, Yekonia Bihagaze (39) na Georgey Milulu wapo mahakamani lakini Askofu Gwajima hayupo.

Pia, amedai kesi ilipangwa kwa ajili ya washtakiwa hao kusomewa hukumu lakini wamepata taarifa Hakimu Mfawidhi, Mkeha anayeisikiliza kesi hiyo anaudhuru.

Baada ya kutolewa kwa maelezo hayo kesi imeahirishwa hadi Agosti 30, 2017 ambapo watasomewa hukumu.

Mzava, Bihagaze na Milulu wao wanakabiliwa na mashtaka mawili ya kukutwa wakimiliki bastola aina ya berretta pamoja na risasi 20 kinyume cha sheria.

Hukumu hiyo inatarajiwa kutolewa siku hiyo na Hakimu Mfawidhi wa mahakama hiyo, Cyprian Mkeha mara baada ya mashahidi wa upande wa mashtaka na utetezi kutoa ushahidi wao na kuufunga.

Katika kesi hiyo, upande wa mashtaka uliwakilishwa na Mawakili wa Serikali, Shedrack Kimaro na Joseph Maugo.

Huku upande wa utetezi uliwakilishwa na Wakili Peter Kibatala ambapo washtakiwa walijitetea pamoja na mashahidi wao wawili akiwamo Nesi wa hospitali ya TMJ, Devotha Bayona na Mchungaji wa Kanisa la Ufufuo na Uzima George Kiwia.

Katika ushahidi wa upande wa utetezi wa shahidi, Devotha alidai kuwa yeye ni afisa muugizi daraja la pili katika Hospitali ya TMJ na yupo kitengo cha ICU.

Machi 29, 2015 aliingia zamu usiku akipokea zamu toka kwa Nesi Rebecca ambaye aliacha kazi 2016 wakati huo Askofu alikuwa amelazwa katika hospitali hiyo kwa siku ya tatu.

Anakumbuka siku hiyo walikwenda askari wawili na mtu mwingine Bihagaze wakagonga mlango wa ICU wakahitaji begi la mgonjwa, walivyojitambulisha alitaka kuhakikisha ni kweli akamfuata Gwajima na kumuuliza. Alieleza ushahidi.

Amedai Gwajima alimueleza ni kweli Bihagaze ni msaidizi wake na kwamba Bihagaze alimwambia yupo pamoja na askari hao wanataka begi la mgonjwa.

Muuguzi huyo amesema Gwajima alisema hawezi kutoa begi hadi wapewe maelezo maalumu na kwamba begi hilo lilikuwepo pembeni ya kitanda cha Gwajima.

Baada ya kupewa majibu hayo na Gwajima, aliwaambia polisi amesema hawezi kulitoa hadi polisi waandike maelezo, wakamueleza wanachohitaji ni begi na maelezo wataandika kesho.

Wakati wanajibizana Gwajima alisikia na akamwambia nesi atawapa hilo begi kwa sababu ndani Lina silaha yake.

“Polisi walitaka kuingia kinguvu nikawaambia hapa ni ICU hamuwezi kuingia kinguvu, " alieleza nesi huyo na kwamba Gwajima alimwambia kama wanalihitaji kinguvu chukua begi mpe Bihagaze awape polisi.

Amedai kabla hajampatia begi hilo Bihagaze polisi walimpokonya, akafunga mlango akaendelea na mgonjwa wake lakini alimuona mgonjwa anamawazo.

Washtakiwa wengine mbali na Gwajima wao wanadaiwa kuwa Machi 29, 2015 katika Hospitali ya TMJ iliyopo Mikocheni A walikutwa wakimiliki Bastola aina ya Berretta yenye namba ya siri CAT 5802 bila ya kuwa na kibali toka kwa mamlaka inayohusika na silaha na milipuko.

Imeendelea kudaiwa kuwa washtakiwa hao walifanya kosa hilo kinyume na kifungu cha 32 (1) na cha 34 (1) (2) na(3) cha sheria ya Silaha na Milipuko sura ya 223 iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2010.

Pia, wanadaiwa kuwa siku hiyo ya tukio washtakiwa hao pia walikutwa wakimiliki isivyo halali risasi tatu za bastola pamoja na risasi 17 za bunduki aina ya Shotgun.

Washtakiwa hao wapo nje kwa dhamana baada ya kukamilisha masharti waliyopewa ya kuwa kila mshtakiwa awe na mdhamini mmoja anayeaminika ambaye alisaini hati ya maneno ya dhamana yenye thamani ya Sh1 milioni.

Malinzi na Mwesigwa Mambo Magumu.....Warudishwa Tena Rumande

$
0
0
Kesi inayomkabili Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania, TFF, Jamali Malinzi na wenzake imeendelea leo July 31, 2017 katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu na kusogezwa tena mbele hadi August 11, 2017 kwa sababu upelelezi haujakamilika.

Wakili wa Serikali Mwandamizi, Nassoro Katuga amedai mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Wilbard Mashauri kuwa kesi hiyo ilikuja kwa ajili ya kutajwa na kwamba upelelezi haujakamilika ambapo hata hivyo, Mawakili wa washtakiwa, James Bwana na Abraham Senguji hawakuwa na pingamizi na suala la upelelezi.

Hakimu Mkazi Mkuu, Wilbard Mashauri ameahirisha kesi hiyo hadi August 11, 2017.

Waziri Mkuu Aagiza kukamatwa kwa viongozi 12 wa Jiji la Mbeya kwa kusabaisha hasara ya Bilioni 63

$
0
0
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, ameitaka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) iwakamate watendaji 12 wa Halmashauri ya Jiji la Mbeya wakiwamo aliyekuwa mstahiki meya Athanas Kapuga.

Amesema pia wakamatwe, wakurugenzi watatu, kaimu mkurugenzi, wahasibu wawili na wajumbe wa bodi wanne kwa kuisababishia hasara jiji hilo kiasi cha Sh63 bilioni katika ujenzi wa Soko la Mwanjelwa.

Amewataka makamanda wa Takukuru kuanzia leo wawakamate watuhumiwa hao na kwamba anatuma timu kutoka ofisi ya waziri mkuu kwa ajili ya kuandaa mashtaka hayo ambapo itatua Mbeya  Jumatano.

Rais wa Simba SC, Evans Aveva na Makamu wake Geofrey Nyange ‘Kaburu’ Wapigwa Kalenda na Kurudi Rumande

$
0
0
Mahakama  ya Hakimu Mkazi Kisutu leo July 31, 2017 imetoa siku saba kwa upande wa mashtaka ufanye jitihada za kukamilisha upelelezi wa kesi inayowakabili Rais wa Simba SC, Evans Aveva na Makamu wake Geofrey Nyange ‘Kaburu’.

Hatua hiyo imekuja baada ya Mwendesha Mashitaka wa TAKUKURU, Leonard Swai  kudai mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Victoria Nongwa kuwa upelelezi wa shauri hilo haujakamilika.

Upande wa utetezi ukiongozwa na Wakili Mtakyamirwa Philemon ulidai mara ya nne sasa upande wa mashitaka unadai upelelezi haujakamilika na kudai wanatakiwa kuhakikisha wanakuwa makini na shauri hilo ili wakamilishe upelelezi kwani washitakiwa wako ndani kwa kosa lisilo na dhamana.

Hata hivyo, Swai alidai kuwa mashitaka ya kughushi wanahitaji upelelezi wa kina hivyo anaomba Mahakama kuwapa siku 14.

Hakimu Nongwa alisema Mahakama imezingatia hoja za pande zote mbili kwamba mashitaka ya kughushi yanachukua muda mrefu kukamilika na kusisitiza kuwa licha ya sheria kutaka kuahirishwa kwa kesi kusizidi siku 14 ombi la upande wa utetezi lina maana hivyo kutoa muda huo ili kama washitakiwa wana kosa watiwe hatiani.

Hakimu Nongwa aliahirisha kesi hiyo hadi August 7, 2017 kwa ajili ya kutajwa.

Unasumbuliwa na Kiharusi,Ngiri au Kifafa?......Unatatizo la Nguvu za Kiume, Kuachika au Tatizo la Uzazi? . Kutana na Mtalaamu Huyu Akusaidie

$
0
0
SASA YUPO DAR; Anauwezo wa kutabiri nyota yako na kukuletea mafanikio makubwa katia biashara yako, kazini na malengo yako ya maisha.Pia anatoa pete ya bahati yenye uwezo wa kukuletea mafanikio makubwa na kutimiza ndoto zako.

Je, Umedhurumiwa? unamdai na hakulipi?...Njoo upatiwe dawa ulipwe haraka. Anadawa ya kumvuta mpenzi wako popote alipo kwa masaa 6 tu na kumtuliza asitoke kwako

Je, unaugomvi usioisha na mpenzi wako na unaachwa mara kwa mara? Njoo upate dawa ufurahie penzi tulivu la umpendae.

Anadawa za nguvu za kiume, kuimarisha mishipa iliyolegea, kuongeza homoni na kukufanya udumu katika tendo hadi dakika 45 na unaweza kurudia tendo hata mara 4 bila kuchoka.

Anatibu Busha bila kupasua,uzazi, mshipa wa ngiri,kiharusi,kifafa,kuondoa majini machafu nakadhalika.

Mpigie kwa simu: 0755505099

Rais wa Urusi, Vladimir Putin Kawafukuza wanadiplomasia 755 wa Marekani

$
0
0
Rais wa Urusi, Vladimir Putin ameagiza kuondolewa wanadiplomasia na wafanyakazi 755 wa Marekani waliopo nchini humo na anafikiria kuchukua hatua za nyongeza kulipiza kisasi kwa vikwazo vya uchumi ilivyowekewa nchini hiyo.

Putin alisema jana katika mahojiano ya moja kwa moja kwenye televisheni ya taifa kwamba aliagiza hatua hizo kwa sababu “alifikiri ulikuwa wakati wa kuonyesha kwamba hawawezi kubaki bila kujibu mapigo."

Utekelezwaji wa agizo la usitishwaji shughuli za wafanyakazi hao wa ubalozi wa Marekani nchini Urusi unatarajiwa kuwa Septemba Mosi mwaka huu. Watabaki wafanyakazi 455.

Desemba 2016, aliyekuwa rais wa Marekani, Barack Obama aliamuru kutimuliwa wanadiplomaisa 35 wa Urusi kutokana na tuhuma za Urusi kuingilia uchaguzi wa Marekani kupitia njia ya mtandao.

Jumanne iliyopita mabunge yote mawili ya Congress ya Marekani yaliidhinisha kwa wingi wa kura vikwazo vya kiuchumi dhidi ya Urusi.

Mashirika ya ujasusi nchini Marekani yanaamini kuwa Urusi ilijaribu kuingilia uchaguzi wa urais wa mwaka 2016 kwa lengo la kumsaidia Donald Trump kupata ushindi.

Urusi imekuwa ikikanusha kuingilia kwa vyovyote uchaguzi huo.

CHADEMA Yapinga Wawekezaji Kunyang'anywa Viwanda Walivyobinafsishiwa

$
0
0

Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe amesema Serikali haiwezi kujenga viwanda peke yake bila kuihusisha sekta binafsi ambayo ndiyo mdau mkuu katika uwekezaji nchini.

Mbowe amepinga kusudio la Rais John Magufuli kuwanyang'anya wawekezaji viwanda walivyobinafsishiwa kwa madai kwamba Serikali ilitakiwa kutafuta chanzo cha kufungwa kwa viwanda hivyo kabla ya kufikia uamuzi wake.

Mwenyekiti huyo amebainisha sababu mbalimbali zilizofanya viwanda hivyo visifanye kazi kuwa ni pamoja na kutopatiwa ruzuku na Serikali, teknolojia ya zamani ya viwanda hivyo na wakati viwanda hivyo vinajengwa kulikuwa na mfumo hodhi wa soko.

"Hakuna mfanyabiashara duniani àmbaye atapewa kitega uchumi kinachozalisha halafu akakifunga. Hayupo!" amesema Mbowe.

Amesema Rais Magufuli hana mapenzi na sekta binafsi kwa kuwa anaamini kwamba kila mtu aliye kwenye sekta binafsi ni "mpiga dili."

"Viwanda vingi vimefungwa kwa sababu ya kodi mbaya hazilipiki, gharama ya kufanya biashara Tanzania ni maumivu makubwa sana.

"Takwimu za benki kuu zinasema kuwa kwenye benki za biashara Viwanda vimekopa 0%

"Viwanda vingi vilishindwa kuendeshwa kwa sababu vingi vilikuwa na teknolojia ya zamani"  Amesema Mbowe

Mbowe Aitaka Serikali Iweke Hadharani ripoti zote mbili za madini ili Kila Mtu Azisome

$
0
0
Serikali imetakiwa kuweka hadharani ripoti zote mbili za madini zilizoandaliwa na kamati zilizoundwa na Rais John Magufuli kuchunguza uendeshaji wa sekta ya madini nchini.

Hayo yamesemwa jijini dar es Salaam leo na Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, katika mkutano na vyombo vya habari ambao ulijikita kuelezea masuala ya uchumi.

Mbowe amesema Tanzania imegeuka kituko baada Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kuipatia kampuni ya Acacia ankara ya malimbikizi ya kodi yanayozidi Sh400 trilioni.

"Serikali iziweke hadharani ripoti zote za madini ili kila mtu asome na kujua kuna nini kwenye ripoti hizo. Kiasi cha kodi wanachodaiwa Acacia ni bajeti ya Tanzania kwa zaidi ya miaka 20. Hiki ni kituko," amesema.

Mbowe amesisitiza kwanza chama chake ndicho kilikuwa cha kwanza kudai mabadiliko katika sekta ya madini lakini kile kilichofanywa na serikali hakilingani na mabadiliko ambayo waliyapendekeza.

Akifafanua, amebainisha kuwa mabadiliko yaliyofanyika bungeni yamefanyika kwa papara na hayatalinufaisha taifa.

CHADEMA Yalia na Ugumu wa Maisha kwa Wananchi.....Yadai Serikali Imewatupa Wakulima

$
0
0
Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe amesema Serikali imeshindwa kusimamia mfumuko wa bei ya chakula nchini kwa sababu haitambui umuhimu wa Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA).

Mbowe amesema mwakà 2015, NFRA ilihifadhi tani 446,000 za chakula lakini kufikia mwaka huu wakala huyo amehifadhi tani 74,826 za chakula.

Mbowe amesema chakula kinapanda bei kwa sababu hakuna mkakati wowote wa Serikali kuwainua wakulima kwa kuwapatia pembejeo za kilimo.

"Usalama wa taifa ni usalama wa chakula, kama hakuna usalama wa chakula hakuna usalama wa Taifa.

"Mtakubaliana na mimi kuwa kwa miaka hii miwili vitu vimepanda bei lakini kipato cha wananchi hakijaongezeka

"Bei ya mahindi kwa mwakà 2015 ilikuwa ndogo lakini mwaka huu imefika zaidi ya 90,000. Wananchi wanapata shida kwa sababu Serikali yao imewatupa wakulima." Amesema Mbowe

Majadiliano kati ya Tanzania na kampuni ya Barrick Gold yaanza

$
0
0
Majadiliano kati ya kamati maalumu iliyoundwa na Rais John Magufuli na wawakilishi kutoka kampuni ya Barrick Gold Corporation juu ya biashara ya madini yanayochimbwa na migodi ya kampuni hiyo nchini yameanza leo, Julai 31 jijini Dar es Salaam.

Taarifa ya Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu, Gerson Msigwa imesema kamati ya Tanzania inaongozwa na Waziri wa Katiba na Sheria, Profesa Palamagamba Kabudi.

Imesema kamati kutoka Barrick inaongozwa na Ofisa Mwendeshaji Mkuu, Richard Williams.

Profesa Kabudi amekaririwa katika taarifa hiyo akisema wamejipanga vizuri kujadiliana na Barrick juu ya madai ya Tanzania katika biashara ya madini ya kampuni hiyo nchini na itahakikisha inasimamia masilahi ya nchi ipasavyo.

Williams imeelezwa ameshukuru uwepo wa majadiliano hayo, akisema Barrick imepokea madai ya Tanzania kwa mtazamo chanya na ipo tayari kujadiliana na kufikia makubaliano yenye masilahi kwa pande zote mbili.

Rais aliunda kamati hiyo baada ya kupokea ripoti za kamati zingine mbili, moja ilichunguza mchanga wa madini (makinikia) na nyingine ya kitaalamu iliyochunguza masuala ya kisheria na kiuchumi kuhusu mchanga huo unaosafirishwa nje ya nchi.

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Gazi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0
Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Tupo Mbagala

MALAWI: Polisi Watoa kibali cha kukamatwa kwa Rais Mstaafu Joyce Banda

$
0
0
Jeshi la polisi nchini Malawi limesema kuwa limepewa kibali maalum cha kumkamata Rais wa zamani wa nchi hiyo, Joyce Banda kwa tuhuma za matumizi mabaya ya ofisi na utakatishaji fedha.

Jeshi hilo limeeleza kuwa limekusanya vielelezo vya kutosha vinavyoonesha kuwa Rais huyo wa zamani ni mhusika katika kashfa kubwa ya rushwa na utakatishaji fedha kiasi cha dola za kimarekani milioni mia mbili na hamsini ($250m), katika kashfa inayofahamika kwa jina la ‘cashgate scandal’.

“Jeshi la polisi la Malawi linapenda kuwafahamisha wananchi kuwa kitengo chake cha kupambana na rushwa na udanganyifu kimefanya uchunguzi kuhusu tuhuma dhidi ya Rais Mstaafu, Joyce Banda na kimepata vielelezo vya kuaminika,” imeeleza sehemu ya taarifa ya polisi kwa umma.

“Vielelezo vilivyokusanywa vinaweza kuonesha kuwa Rais Mstaafu alifanya makosa yanayohusu matumizi mabaya ya ofisi na utakatishaji fedha,” aliongeza.

Mama Banda yuko nje ya nchi hiyo lakini polisi wamesema kuwa watatumia mfumo wa polisi wa kimataifa (Interpol) kusaidia kumrejesha nyumbani ili ajibu tuhuma hizo dhidi yake.

‘cashgate scandal’ ni kashfa kubwa ya rushwa kuwahi kutokea katika historia ya Malawi inayohusisha vigogo wa serikali.

KENYA: Mkurugenzi Tume ya Uchaguzi aliyepotea apatikana akiwa amefariki

$
0
0
Taharuki imetanda nchini Kenya baada ya Kaimu Mkurugenzi wa teknolojia wa Tume Huru ya Uchaguzi nchini humo (IEBC), Christopher Musando aliyepotea hivi karibuni kupatikana akiwa amefariki katika eneo la Kikuyu jijini Nairobi.

Kwa mujibu wa vyombo vya usalama nchini humo, Musando alifanya mawasiliano ya mwisho Jumamosi majira ya saa tisa alfajiri ambapo alituma ujumbe mfupi kwa mmoja kati ya wafanyakazi wake.

Jeshi la polisi nchini humo limesema kuwa mwili wa Musando ulipatikana pamoja na mwili wa mwanamke mwingine ambaye hakutambulika mapema na kisha kupelekwa katika chumba cha kuhifadhia maiti jijini humo.

Marehemu alikuwa na jukumu la kusambaza vifaa vya kielektroniki ambavyo vitatumika kuwatambua wapiga kura na kusambaza matokeo ya uchaguzi mkuu kutoka katika vituo vya kupigia kura.

Hata hivyo, hakuna taarifa rasmi kutoka kwa vyombo vya usalama kuhusu upelelezi wa tukio hilo na yaliyomkuta Musando.

Kenya inatarajia kufanya uchaguzi mkuu Agosti 8 mwaka huu, uchaguzi unaotajwa kuwa wa ushindani zaidi katika historia ya nchi hiyo.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images