Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Kutana na Mtaalamu wa NYOTA Akusaidie.....Huzuia Chuma Ulete, Anatoa Pete za Bahati Nasibu, Anatafsri Nyota na Atakupa Jini la Mali

$
0
0
Kutana  na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH Maalim HUSSEIN Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika..

JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na  Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na Maalim Hussein Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO NDANI YA SAA 12 TU. 

Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine? Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao Endapo utafata Atakacho kuelekeza.Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.
 
Maalim Hussein Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..
Anatibu kwa Kutumia  Vitabu vya QUR-AN Dawa za Asili za Africa,Dawa za Kiarabu na Majini.

Anatafsiri Ndoto. Kushinda BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA,Hutoa  PETE ZA BAHATI inayoendana na NYOTA YAKO. Mvuto wa Mwili na BIASHARA, Kinga ya Mwili,ZINDIKO za Nyumba.HUZUIA CHUMA ULETE NA KUKUPA DAWA YA KUONGEZA FAIDA KWENYE BIASHARA. HURUDISHA MALI ZILIZOPOTEA AU KUDHULUMIWA.MIGUU Kufa GANZI.Kufungua KIZAZI kwa wale walio fungwa kwa njia za KISHIRIKINA. Anakupa Jini la Mali kwa yule anaehitaji Utajiri BILA MASHARTI. PIA ANATOA POCHI YA MAAJABU ISIO ISHA HELA( Magic Wallet)..Nguvu za KIUME,HUMALIZA KESI YA AINA YOYOTE NDANI YA SIKU 14. na mengi zaidiWhatsapp +255 674 835107 -calls +255746757102
 
Pia Anatibu kwa Njia ya simu popote Pale Ulipo..

PICHA: Hospitali Marekani yafanikisha upasuaji mkubwa wa wanafunzi Walionusurika katika Ajali

$
0
0
Watoto watatu wa shule ya msingi ya Lucky Vicent walionusurika katika ajali ya basi, wamefanyiwa upasuaji na sasa wapo wodini wakiendelea na mazoeazi, ila Doreen, jana alipewa MAPUMZIKO maalumu akiwa anaandaliwa tayari kwa UPASUAJI wa uti wa mgongo 'spine'  unaofanyika leo.

Mbunge wa Singida Kaskazini, Lazaro Nyalandu aliyeshiriki katika kuwasafirisha watoto hao, ameandika katika ukurasa wake wa facebook akisema  watoto hao kwa sasa wamewekwa kwenye vyumba vya peke yao.

 Upasuaji huo umefanyika katika Hospitali ya Mercy, Sioux City, Marekani.

 Amefafanua upasuaji waliofanyiwa na kusema mtoto Saidia alifanyiwa upasuaji wa mfupa wa kulia wa nyonga, mkono wa kulia na kuwekewa ngao kwenye shingo atakayotakiwa kukaa nayo kwa wiki sita.

“Kwa upande wa mtoto Wilson, yeye amefanyiwa upasuaji wa nyonga ya kulia, kiwiko cha kulia kilichokuwa kimevunjika mara tatu na kiwiko cha kushoto,” amesema

Amesema Doreen yeye amefanyiwa upasuaji wa nyonga, taya katika upasuaji uliochukua saa nne. Leo Doreen atafanyiwa upasuaji wa uti wa mgongo. 

Uamuzi wa Rais Magufuli kuhusu wafanyakazi 9 wa TBC waliotangaza habari ya UONGO Kuwa amepongezwa na Rais Trump

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt John Pombe Magufuli amewasamehe wafanyakazi tisa wa Shirika la Utangazaji la Taifa (TBC) waliokuwa wamesimamishwa kazi kwa kosa la kurusha habari ya uongo kumhusu kiongozi huyo wa nchi.

Wafanyakazi hao walisamishwa kazi mwezi Machi kwa kuhusika katika makosa ya kiweledi na kiuhariri yaliyosababisha kutangazwa kwa taarifa ambayo haikuwa sahihi Machi 03, 2017.

Wafanyakazi hao walirusha hewani taarifa ya uongo iliyosambazwa na mtandao wa Fox Channel.com kuwa Rais wa Marekani, Donald Trump amesifu utendaji kazi wa Rais John Pombe Magufuli na kwamba ni mfano mzuri wa kuigwa Afrika.

Taarifa iliyosainiwa na Mkurugenzi Mkuu wa TBC, Dk. Ayub Rioba, ilieleza kuwa makosa hayo yalileta usumbufu kwa umma na yasingefanyika endapo taratibu zote za kitaalamu zingefuatwa kuthibitisha ukweli wa taarifa yenyewe.

Watangazaji waliotangaziwa msahama huo ni Rais Dkt Magufu ni pamoja na Gabriel Zackaria, Elizabeth Mramba, Prudence Constantine, Dorothy Mmari, Ramadhani Mpenda, Leya Mushi, Alpha Wawa, Chunga Ruza na Judica Losai. 

Rais Dkt Magufuli alitoa msamaha huo alipofanya ziara katika kituo hicho jana ili kuangalia utendaji kazi pamoja na kuzungumza na wafanyakazi kuweza kutambua changamoto zinazowakabili.

Mmiliki wa shule ya Lucky, Waandishi 10 na Meya wa Jiji la Arusha Watiwa Mbaroni

$
0
0

Mmiliki wa Shule, Meya wa jiji la Arusha pamoja na waandishi wa habari 10 wamefikishwa kituo cha polisi (Central) kwa kufanya mkusanyiko bila kibali ndani ya shule ya Lucky Vicent.

Kutoka Arusha taarifa zinasema kuwa Mkuu wa upelelezi Wilaya ya Arusha (jina lake halijafahamika) amedai kuwa kosa ambalo wamelifanya waandishi pamoja Wamiliki ni kufanya mkusanyiko bila kibali ambao ni kinyume cha sheria.

Vyanzo vya habari vinadai kuwa chanzo cha kukamatwa ni baada Wamiliki wa shule binafsi kwenda shuleni Lucky Vicent kutoa michango ya Rambirambi shuleni Lucky Vicent

Habari zinasema kuwa kwa sasa Watu wote waliokamatwa tayari wamefikisha kituo cha kati kilichopo mjini Arusha (Central)
 
Waliokamatwa kwenye msafara huo wanatajwa ni wanahabari 10, Mmiliki wa shule ya Lucky Vicent na Meya Kalist Lazaro.

Waandishi waliokamatwa ni pamoja na  1 .Godfrey Thomas ayo tv 2.Alphonce kusaga Triple A 3.Filbert Rweyemamu mwananchi 4.Husein Tuta Itv 5.Joseph Ngilisho Sunrise radio 6.Geofrey Steven Radio 5 7.Janeth Mushi Mtanzania 8.Zephania Ubwani The Citizen 9.Elihuruma Yohani mwakilishi wa Tanzania Daima 10.Idd uwesu Azam Tv

Majibu ya Waziri Mwigulu kuhusu utoaji wa fomu za PF3

$
0
0
Waziri wa mambo ya ndani ya nchi, Mwigulu Lameck Nchemba amesema kuanzia sasa mtu yoyote atayeweza kupata majeraha yasiyokuwa na utata wapewe matibabu kwanza hospitali bila ya kuwa na kibali kutoka kwa Jeshi la Polisi (PF3) kama ilivyozoeleka.

Mwigulu ametoa kauli hiyo kupitia ukurasa wake wa kijamii Facebook kwa kusema utaratibu huo unajicho la karibu kutoka kwenye vyombo vya usalama ili kubaini ukweli wa jeraha la muhusika.

"Tumeamua majeruhi, mahututi asiyeweza kutoroka na mtu mwenye majeraha yasiyo na utata wapewe matibabu kwanza bila PF3..Hatua za kufuata PF3 zianze mara moja wakati akiendelea kupewa matibabu, hii tunalengea kuokoa maisha yao kwanza, utaratibu huu unajicho la karibu kutoka kwenye vyombo vyetu vya usalama ili kubaini ukweli jeraha la mhusika". Ameandika Mwigulu

Mwigulu amesema hayo baada ya Jeshi la Polisi kutupiwa lawama nyingi kutoka kwa wananchi walipatwa na matatizo kushindwa kupewa huduma hospitali kwa haraka mpaka wapitie kituo cha Polisi kupatiwa cheti cha PF3 ili aende kupata huduma.

Serikali Yatolea Ufafanuzi Kazi Ya Ofisi Ya Mdhibiti Na Mkaguzi Wa Hesabu Za Serikali

$
0
0
Na Benny Mwaipaja, WFM-Dodoma
Serikali imeeleza kuwa Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania haijawahi kumuhusisha Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika ukaguzi wa Balozi au ukaguzi wowote ule kama Umoja wa Mataifa kwa sababu hakuna ulazima wa kufanya hivyo Kikatiba na Kisheria.

Hayo yameelezwa Bungeni mjini Dodoma na Naibu Waziri wa Fedha na Mipango (MB), Dkt. Ashatu Kijaji, alipokuwa akijibu swali la msingi la Mbunge wa Kiwengwa Khamisi Mtwana Ally (CCM), aliyetaka kujua ni mara ngapi Ofisi hiyo ya Bara imeishirikisha Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali ya Zanzibar.

Akijibu swali hilo Dkt. Kijaji alisema kuwa, Ofisi hizo kila moja ina mipaka yake ya kufanya ukaguzi na kwamba jukumu la ukaguzi wa Taasisi za Muungano lipo kwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

“Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi wa Hesabu za Serikali imeanzishwa kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 na kwamba majukumu ya Ofisi hiyo yameainishwa katika ibara ya 143(2) ya katiba hiyo”. Alisema Dkt. Kijaji

Dkt Kijaji aliongeza kuwa, eneo hilo linamtaka Mdhibiti na Makguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kufanya ukaguzi angalau mara moja kila mwaka na kutoa taarifa kuhusu ukaguzi wa Hesabu za Serikali, Bunge na Mahakama.

Aidha, Dkt. Kijaji alisema kuwa majukumu hayo yameainishwa katika kifungu cha 10 cha Sheria ya Ukaguzi wa Umma ya mwaka 2008 na kanuni zake za mwaka 2009.

Dkt. Kijaji alifafanua kuwa, ukaguzi wa Balozi unafanyika chini ya fungu 34, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa kuwa Ofisi zote za Ubalozi ni sehemu ya fungu 34.

“Hivyo basi, ukaguzi wa Balozi kama ilivyo kwa Taasisi nyingine za Muungano unafanywa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania .”alisema Dkt. Kijaji

Aliongeza kuwa, Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali wa Zanzibar, majukumu yake yameainishwa kwenye ibara ya 112 ya Katiba (3) ya katiba ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ya mwaka 1984.

Akiongeza majibu ya swali hilo, Waziri wa Mazingira na Muungano, Januari Makamba alisema kuwa wakaguzi wa pande zote kutoka Tanzania Bara na Visiwani hufanya kazi kwa kushirikiana katika mambo ya ukaguzi wa hesabu za serikali.

Katika swali la nyongeza Mbunge wa Mkwajuni, Ally Zubeir Ngwali (CUF), alihoji ni kwanini fedha za mfuko wa Jimbo hazijawahi kukaguliwa na zitakaguliwa kwa utaratibu upi.

Akijibu swali hilo, Naibu Waziri, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Selemani Jaffo alisema upo utaratibu maalum wa kushughulikia mambo hayo.

Rais Magufuli kumkabidhi Museveni uenyekiti EAC Jumamosi hii

$
0
0
Na Regina Mkonde
Rais John Magufuli Jumamosi ya Mei 20, 2017 katika mkutano wa 18 wa Wakuu wa Nchi mwanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC)anatarajiwa kumkabidhi kijiti cha uenyekiti wa jumuiya hiyo Rais wa Uganda, Yoweli Museveni baada ya Tanzania kuingoza EAC kwa vipindi viwili mfululizo.

Hayo yamesemwa jana Mei, 18 na Waziri wa Mambo ya Nje, Balozi Augustine Mahiga katika Mkutano wa 34 wa Baraza la Mawaziri la EAC, ambapo alieleza mafanikio yaliyopatikana katika kipindi ambacho Tanzania iliiongoza jumuiya hiyo, ikiwemo kuridhia maombi ya muda mrefu ya uanachama, ya nchi ya Jamhuri ya Sudan Kusini na kuipatia uanachama kamili wa jumuiya hiyo.

“Tanzania tumemaliza muda wetu baada ya kuiongoza vipindi viwili mfululizo, Rais Magufuli Jumamosi atamkabidhi uenyekiti Rais Museveni wa Uganda,” alisema.

Alieleza kuwa, pamoja na Rais Magufuli kukabidhi kijiti hicho kwa Museveni, Rais Mstaafu Benjamin Mkapa anatarajiwa pia katika mkutano huo kuwasilisha ripoti ya mazungumzo ya pamoja ya kuleta amani, ikiwa ni utekelezaji wa agizo la wakuu wa nchi wa EAC lililotolewa mwezi Januari,2017.  

Kuhusu mkutano wa Baraza la Mawaziri wa EAC uliofanyika jana Mei 18, 2017, alisema wajumbe wa baraza hilo watajadili ushirikiano wa masuala mbalimbali yanayohusu jumuiya hiyo, ikiwemo ushirikiano kibiashara, uwekezaji, elimu pamoja na huduma mbalimbali za kuendesha nchi wanachama hasa ujenzi wa miundombinu na uchukuzi.

“Kwanza Tanzania itatoa ripoti ya ushirikiano kwa kipindi cha miaka miwili iliyoiongoza EAC ikiwemo ya ushirikiano kibiashara, kielimu na huduma za kuendesha nchi,” alisema.

Alisema wajumbe hao watajadili namna ya kuondoa na au kupunguza vikwazo visivyo vya kisheria hasa vinavyokwamisha biashara ikiwemo ushuru wa forodha, vizuizi vya magari, aina za biashara, na kwamba watajadili namna ya kuanzisha soko imara la pamoja.

“Kuna vikwazo visivyo vya lazima vinavyokwamisha biashara kwa nchi wananchama, mfano Tanzania tuna vyombo viwili vinavyopima ubora wa bidhaa, TBS na TFDA ambapo wenzetu wanasema ngazi hizi mbili zinazuia biashara zao, kwa hiyo tutazungumzia suala hili. Pia tutajadili namna ya kutekeleza lengo letu la kuzuia uingizwaji wa nguo za mitumba kutoka nchi za nje ya jumuiya hii,” alisema.

Kwa upande wa elimu, Balozi Mahiga alisema wajumbe hao watajadili namna ya kuanzisha mfumo wa elimu ambao utasaidia kuondoa tofauti ya upatikanaji elimu katika vyuo vya EAC ikiwemo wanafunzi wa jumuiya hiyo kupata elimu kwa malipo na vigezo vinavyo fanana na kwamba kusiwepo na vikwazo.

“Tulikuwa na chuo kimoja tu cha jumuiya, lakini sasa tuna vyuo tanzu katika nchi ya Tanzania, Kenya na Uganda kwa hiyo kuna umuhimu wa kuwa na mfumo wa elimu kwa wanafunzi kupata elimu kwa malipo na vigezo vinavyofanana. Mwanafunzi wa Tanzania akienda Kenya asome kwa vigezo na gharama ileile anayolipa mwanafunzi wa Kenya,” alisema.

Waziri Mwijage awatangazia vita watumishi wa umma

$
0
0
Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Charles Mwijage ametangaza vita kwa watumishi wanaoruhusu uingizwaji wa bidhaa bandia nchini, na kutoa onyo kwamba watakao fanya hivyo wajiandae kuondoka.   

Mwijage ametoa onyo hilo juzi Bungeni mjini Dodoma, wakati akisoma bajeti ya wizara yake, ambapo pia alipiga marufuku bidhaa bandia kuingia nchini kutoka nje ya nchi kuanzia Julai mosi mwaka huu.

“Ikifika mwezi Julai mwaka huu, kama bidhaa feki zikipita kuingia nchini mtakuwa hamnitakii mema, na walio chini yangu mkae kabisa mkao wa kuondoka kama bidhaa zisizokidhi viwango zitapia na kuja kuumiza viwanda vyetu nchini,” alisema.

Habari Mpya kuhusu Majeruhi Doreen wa ajali ya Wanafunzi Arusha Aliyefanyiwa Oparesheni Jana

$
0
0
Taarifa mpya za usiku huu kuhusu hali ya  Mtoto Doreen ( kwa mujibu wa mbunge Lazaro Nyarandu)   ni kuwa amemaliza kufanyiwa upasuaji wa uti wa mgongo na Madaktari wamesema wamefanikiwa kwa ufanisi mkubwa kupita matarajio.

Doreen alikuwa afanyiwe upasuaji kwa makadrio ya masaa matano na dakika 30 lakini zoezi hilo lilikamilika kwa masaa manne huku timu ya “Surgical Support” IKIWA na watu 6 na wakiongozwa na Madaktari bingwa wawili, Dr. Meyer na Dr. Durward.

Mtoto Doreen amehamishwa kutoka chumba cha upasuaji na kupekewa ICU na Madaktari wamesema kwasababu hali yake imeridhisha sana, baadae leo watamtoa ICU ambako wamempumzisha baada ya upasuaji na kumrudisha wodi ya watoto

Jeshi la Polisi Lajibu tuhuma za vyeti feki

$
0
0
Jeshi la Polisi nchini limekanusha taarifa zinazosambazwa kwenye mitandao ya kijamii zikiwahusisha askari wake kuwepo katika majina ya vyeti feki na kusema taarifa hizo ni za uongo na wala hazijatolewa na Jeshi hilo.

Hayo yamebainishwa na taarifa iliyotolewa na Msemaji wa Jeshi la Polisi, ACP Advera Bulimba na kusema wanaendelea kumtafuta mtu aliyesambaza taarifa hiyo kwa lengo la kupotosha umma ili hatua kali za kisheria zichukuliwe dhidi yake na kuwa fundisho kwa watu wengine wenye tabia kama hiyo.

"Jeshi la Polisi nchini, linaujulisha umma kwamba, orodha ya majina ambayo yamekuwa yakisambazwa kwenye mitandao ya kijamii yakidai kuwa ni majina ya askari wa jeshi la polisi wenye vyeti feki ni ya uongo na wala taarifa hiyo haijatolewa na jeshi la polisi". Ilisema taarifa hiyo

Nape Nnauye afunguka kuhusu ukimya wa Kinana, Mwenendo wa shughuli za Bunge pamoja Polisi Kutumia Nguvu Kubwa

$
0
0
Na Regina Mkonde 
 Mbunge wa Jimbo la Mtama, Nape Nnauye amefunguka kuhusu masuala mbalimbali ikiwemo, ukimya wa Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana, muenendo wa shughuli za Bunge pamoja na tukio lililotokea hivi karibuni la Askari Polisi mmoja wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) kufyatua risasi hewani mbele ya aliyekuwa Naibu Waziri wa Fedha, Adam Malima baada ya kutokea majibizano yaliyosababishwa na dereva wa Malima kuegesha gari vibaya.

Nape amefunguka hayo jana  jijini Dar es Salaam, wakati akizungumza na wanahabari ambapo alisema, Kinana ambaye baadhi ya watu wanadai kuwa ukimya wake umetokana na kujiuzulu, yuko katika wadhifa wake wa ukatibu mkuu na anaendelea kufanya kazi za chama.

“Mimi sio msemaji wa chama, lakini Katibu Mkuu yupo na anafanya kazi yake kama kawaida…., mimi bado ni mwanachama na muumini mzuri wa CCM inayopenda haki, na nina amini hiki ndicho chama pekee bora kitakachoweza kuwakomboa watanzania pamoja na kuamiwa ikiwa kitatekeleza mkataba wake na wananchi ambao ni wa kutimiza ahadi zake ilizo ziahidi,” alisema.

Kuhusu tukio la Askari Polisi kufyatua risasi hewani, ambalo Kamishna wa Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Kamanda Simon Sirro alisema ulikuwa uamuzi wa busara wa kuondoa taharuki katika tukio hilo, na mbinu ya kuwatia nguvuni watuhumiwa.

Nape alishauri vyombo vya dola kutotumia nguvu kwani kitendo hicho kitajenga hofu na chuki baina ya serikali na wananchi na hata kwa chama tawala CCM, huku akiisihi serikali kuondoa vitendo vinavyotia hofu wananchi.

“Ni vizuri vyombo vya dola vikatimiza majukumu yake kwa kuwa ni vyombo vya wananchi, si vizuri vikitumia nguvu kubwa pale isipostahili. Ifikie hatua raia asiye na silaha Polisi wasitumie nguvu kushughulika naye kwa kutumia silaha. Nimeona ile video ikionyesha Malima alikuwa anauliza chanzo cha tatizo,” alisema na kuongeza.

“Kuna nchi tamaduni zake ni kutumia mabavu na nyingine zinatumia demokrasia, nchi yetu utamaduni wake si wa kutumia nguvu, tumezoea kuelewana kwa mazungumzo. Vyombo vya dola visitumie nguvu kwa kuwa tunajenga usugu usio na maana. Na kama kuna mazingira hatarishi basi nguvu itumike.”

Kuhusu mienendo ya shughuli za Wabunge Bungeni, aliwataka wabunge kutekeleza majukumu yao ikiwemo kuwawakilisha na kusimamia vema masilahi ya wananchi wanaowawakilisha, pamoja na kuisimamia serikali kutekeleza vizuri majukumu yake.

“Bunge ni mkutano wa wananchi, na wabunge wapo kwa niaba ya wananchi katika kupitisha na kushauri mipango ya serikali. Ni vizuri wasimame katika maeneo yao, wasiwe wapiga makofi, pale serikali inapofanya vizuri ipongezwe na inapofanya vibaya ikosolewe,” alisema.

Kuhusu Uhuru wa Vyombo vya Habari, alisema ifikie hatua wananasiasa wawe na ngozi ngumu ya kuvumilia kukosolewa  na watu kupitia vyombo vya habari. Pia ameshauri wananchi wanaotaka maonesho ya vikao vya bunge moja kwa moja, kuuomba mhimili huo kubadilisha sheria zake ambazo zimeipa mamlaka ya kuamua namna ya kuendesha shughuli zake.

“Naamini uamuzi wa siku ile wa kuzuia shughuli za bunge live ulikuwa sahihi sababu sheria zinasema Bunge litaendeshwa kwa sheria zake. Wananchi wanaozungumzia Bunge live, waliombe libadilishe sheria zake ili lianze kuonyeshwa live,” alisema

CCM Wampa 'Makavu' Lowassa

$
0
0
Chama cha Mapinduzi mkoa wa Arusha kimeishangaa kauli ya aliyekuwa Waziri Mkuu Edward Lowassa kusema kuwa Rais John Magufuli amemtuma ‘mtoto mdogo’ kwenda kuiwakilisha serikali kwenye mazishi ya wanafunzi wa  shule ya Lucky Vicent

 Akizungumza  na waandishi wa habari jana, Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Arusha Michael Lekule ,alisema kauli ya Waziri huyo mstaafu ameitoa kwa kudanganya wananchi na kuonesha serikali ya Magufuli haishirikiani na wananchi ,wakati serikali iliubeba msiba huo mzito wa taifa.

 Alisema jitihada za serikali ya Magufuli zimeonekana kupitia kwa wawakilishi wake Makamu wa Rais Samia Suluhu pamoja na Mrisho Gambo pamoja na wanachama wa CCM ambao walijitokeza kwa wingi kwenye msiba huo mzito

 "Serikali ilijitoa kwa hali na mali kuwezesha  familia 35 kwenda kupumzisha wapendwa wao,na ilihakikisha kila mwili unapumzika mahala popote familia inapopata,tunajiuliza walitaka nini kama kote nafasi ilijazwa na serikali ya Magufuli," alisema Michael

 "CCM inakanusha kwanguvu upotoshaji huo,hata ukiangalia siku ile uwanja wa shekh Amri Abeid wanaccm walijaa uwanjani ,kikubwa CCM imeguswa na msiba uliotokea na Rais wetu amekuwa bega kwa bega juu ya tukio lililotokea,"alisema

 Pia alisema wamemshangaa kwa kusema Rais alimtuma mtoto mdogo wakati yeye mwaka 2007 ajali mbaya iliyotokea Monduli duka bovu na kuua watu 20 ambao 11 walikuwa ni askari wa JKT,rais Kikwete alimtuma aje kuiwakilisha serikali.

 Hata hivyo alimtaka kiongozi huyo, ajiulize kama yeye kipindi akiwa Waziri Mkuu aliweza kutumwa na Rais, amuwakilishe kwenye msiba wa watu 20, je yeye na Makamu wa Rais ni nani mdogo?

 "Tena ajali hiyo ilikuwa ya kitaifa,askari 11 walifariki kwenye ajali,mbona hajayasema ya kwake?," alisema Lekule

Jeshi la Polisi latofautiana na agizo la Waziri wa Mambo ya Ndani Kuhusu PF3

$
0
0
Baada ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba kutoa taarifa kupitia ukurasa wake wa Facebook kuwa kuanzia sasa majeruhi, mahutiti asiyeweza kutoroka atatibiwa kwanza ndipo ashughulikie fomu ya polisi namba 3 (PF3), Jeshi la Polisi limetolea ufafanuzi  zaidi  wa taarifa hiyo.

Katika taarifa ya Waziri Nchemba alisema, “Tumeamua, majeruhi, mahututi asiyeweza kutoroka,na mtu mwenye majeraha yasiyo na utata wapewe matibabu kwanza bila PF3.”

Aliendelea kueleza zaidi kwamba, “Hatua za kufuata PF3 zianze mara moja wakati akiendelea kupewa matibabu, hii tunalenga kuokoa maisha yao kwanza. Utaratibu huu unajicho la karibu kutoka kwenye vyombo vyetu vya usalama ili kubaini ukweli jeraha la mhusika.”

Kwa upande wa Jeshi la Polisi kupitia kwa msemaji wake, Msemaji wa Jeshi la Polisi, Advera Bulimba-ACP ameeleza umma wa Watazania kwamba, fomu hiyo ni ya lazima kwa mtu yeyote aliyepata majereha kabla ya kutibiwa na itaendelea kutumika kwa mujibu wa sheria.

“Fomu ya Polisi namba 3 ijulikanayo kama PF.3 hutolewa kwa mtu baada ya Polisi kupata taarifa kutoka kwa mlalamikaji au muathirika kwa matukio yenye madhara mwilini, ajali au matukio yenye kuleta mashaka kuhusu vyanzo vyake kama vile kipigo, kujeruhi, ubakaji, kulawiti,  kunywa sumu na mengineyo.

“Ieleweke wazi kwamba matumizi ya PF3 ni ya lazima na yanaendelea kama kawaida  kwa mujibu wa sheria. Fomu hiyo inapaswa kutumika katika kila aina ya tukio tajwa hapo juu ili muathirika aweze kupata matibabu katika vitu vya afya na hatua za kiupelelezi kwa Jeshi la Polisi ziweze kuendelea.”

Aidha, ACP Bulimba aliongeza kuwa,“Katika mazingira mengine hali ya muathirika yaweza kuwa mbaya, hivyo huduma za kuokoa maisha (huduma ya kwanza) inaweza kuendelea kutolewa wakati watoa huduma wakiijulisha Polisi ili kuharakisha upatikanaji wa PF.3”

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya May 19

OFA: Jipatie Riwaya Kalii Iitwayo My Mom's Friend Toka Kwa Mtunzi Makini Eddazaria

$
0
0
OFA YA WEEKEND. PATA KITABU CHA MY MOM'S FRIEND KWA SH 7000 TU KUPITIA WHATSAPP 0657072588 au EMAIL eddazariaM@gmail.com  

"Rafiki wa mama anaweza kuwa kama mama kwako kwani heshima ambayo unampatia mama yako ndio hiyo unayo stahili kumpatia na yeye. Ila hali imekuwa tofauti kwa mama Caro, uchu wa mapenzi unamfanya afanye juhudi ya kumpeleka mbele za haki rafiki yake kwa ajili ya kuhakikisha kwamba ana nasa kwenye penzi la mtoto wa rafiki, yake kitu kinacho pelekea kuharibika kwa maisha kwa kijana huyo, chuku, uhasama na uadui mkubwa unatawala katikati yao."
 
Ungana nami kwenye kisa hichi cha kusisimua kilicho andaliwa nami Eddazaria G.Msulwa
 
NAOMBA MUZIDI KU SUPPORT KAZI YANGU YA UANDISHI KWA KUNUNUA KITABU HICHI NA VINGINE VINGI. Wasiliana nami 0768516188 au 0657072588
KARIBUNI SANA

SORRY MADAM -Sehemu ya 63 & 64 (Destination of my enemies)

$
0
0
 MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWAILIPOISHIA

ILIPOISHIA
“Ankooo”
Soroo akamkumbatia Lee Si, wakatoka nje ya ofisi hizo wakiwa wanatembea kuelekea kwenye moja ya bustani wakaka kwenye moja ya viti.
“Unajua ni sehemu gani alipo Black Shadow?”
Lee Si alimuuliza Soroo, mara baada ya kutoa noti ya dola mia na kumkabidhi, Sa Yon a Shamsa waliweza kumuona Lee Si akiwa na mtoto mmoja, Shamsa alipo jaribu kumkazia macho mtoto huyo akagundua ni Junio, jambo lililo mfanya ashuke kwenye gari na kuanza kukimbia kuelekea kule walipo kaa Soroo na Lee Si

ENDELEA
Shamsa akazidisha kasi, hadi karibu na bustani akasita kidogo kukimbia huku macho yake yote akiwa amemtupia Soroo, Lee Si, alipo muona Shamsa akatamani asimame na akimbie, ila akashindwa na kujikuta akiachia tabasamu pana la kinafki ili mradi asistukiwe mpango wake. Shamsa akaanza kutembea hatua za taratibu hadi sehemu walipo Soroo na Lee Si.Kufanana kwa Soroo na Junio ambaye kwa sasa ni Marehemu, kukamfanya Shamsa kulengwa lengwa na machozi.

Saroo akabaki akimshangaa Shamsa aliye piga magoti mbele yake, hakumjua ni nani aliye kuja. Soroo akamtazama Lee Si kisha akamtazama Shamsa, aliye anza kumshika mkono wake wa kulia. Shamsa akashindwa kujizuia na kujikuta akiangua kilio huku akimkumbatia Soroo, uchungu wa kifo cha Junio ukamrejea upya.
“Wewe nani?”
Soroo alimuuliza Shamsa huku ajijitoa mikononi mwake, Shamsa hakumjibu chochote zaidi ya kulia kwani hadi sauti wamefanana, Sa Yoo alisimama kwa mbali akishuhudia hali nzima inavyo endelea.

“Akooo Lee Si eti huyu ni nani?”
“Ahaa ahaa hu…..uuyu…..”
Lee Si alijing’ata ng’ata, hakujua ajibu nini japo swali alilo ulizwa ni rahisi sana kwake.
“Unaitwa nani mtoto mzuri?”
Shamsa alizungumza huku akijipangusa machozi yake kwa kiganja chake cha mkono wa kushoto.
“Soroo, wewe unaitwa nani?”
“Shamsa”
“Mbona sasa unalia?”
Shamsa akajitahidi kuachia tabasamu pana, kisha viganja vyake taratibu vikaanza kupapasa mashavu yote mawali ya Soroo.

“Nimetokea kukupenda”
“Akoo Lee Si, Shamsa ananipenda kama anti Phidaya”
Lee Si alitingisha kichwa tu, mdomo wake alijikuta ukiwa mzito gafla, hata maneno ambayo alipanga kumshawishi mtoto huyo yote yaliparanganyuka kichwani.
“Unamjua anti Phidaya?”
“Eheee alikuja siku ile kutuletea vyakula na hele hapa, akaniambia amenipenda”
“Ahaa basi mimi pia nianakupenda kutokana anti Phidaya ni mama yangu”
“Ahahaa kweliii?”
“Ndio”
Soroo akajikuta akifurahi sana kusikia maneno ya Shamsa, akamkumbatia tena na kumuomba asimame. Mlezi mmoja wa choa baada ya kuona ujio wa Shamsa, ikamlazimu kufika kwenye bustani hiyo kuuliza ni kitu gani kinacho endelea. Ikabidi Lee Si kuchukua jukumu la kumuelezea Shamsa kwamba ni mtoto wa bosi wake ambaye alikuja naye siku chache zilizo pita.

Mlezi huyo baada ya kusikia habari hiyo, akafurahi sana na kuomba kwenye na Shamsa ofisini kumtambulishwa kwa baadhi ya walezi wa chuo hicho ambao wanamuheshimu sana Phidaya kama mwanamke shujjaa aliye jitolea kuwalea watoto hao. Walezi hao hawakusita kumpa pole Shamsa kwa mama yake kutekwa, kila mmoja alisikitika sana kwa taarifa hiyo kwani wameondokewa mtu muhimu sana kwenye maisha yake.

“Nina imani kwamba atakuwa salama, nahisi watu hao wanahitaji pesa tu”
Shamsa aliwafariji walezi hao, ambao tukio la Phidaya kutekwa liliwagusa kwa kiasi kikubwa sana. Ila mlezi mmoja aakashindwa kustahimili kuuliza kitu amchacho kinamsumbua moyoni mwake.

“Mbona weewe na mama yako mumetokea sana kumpenda Soroo, kuliko watoto wengine?”
“Kusema kweli Soroo amefanana sana na mdogo wangu, mtoto wa mama, alifariki mwaka jana akiwa na miaka sita, ndio maana nilipo muona Soroo kwa mara ya kwanza nilijisikia uchungu sana”
MManeno ya Shamsa yakwafanya baadhi ya wamama walezi kumwagikwa na machozi, japo ni maneno machache ila kila mmoja alitambua uchungu wa kufiwa na mtoto,  wakamuangalia Soroo, mbaye muda wote alijiegemeza mapajani mwa Shamsa.

   Kitendo cha Shamsa kuingia na Soroo ofisini kwa walezi wa kituo cha kulele watoto, kilimkera sana Lee Si akanyanyuka kwa hasira kwenye benchi alillo kuwa amekalia na kwenda kwenye gari lake huku akimpita Sa Yoo pasipo kumsemesha neon la aina yoyote. Sa Yoo kama kawaida yake akamkata Lee Si jicho moja kali, kisha akatabasamu nakuegemea gari la Phidaya ambalo kwa sasa yeye ndio analitumia. Lee Si aliweza kuona kitendo ambacho Sa Yoo amekifanya, hakuhitaji kujibizana na Sa Yoo, akawasha gari na kuondoka kwa kasi huku akitimua vumbi kuingia barabarani.
                                                                                               ***
   Majira ya saa mbili usiku, ndege ya dokta Ranjiti ikatua wanja wa ndege jijini Cairo nchini Misri. Phidaya akiongozana na wahudhumu wawili wa ndege wakashuka na kumkuta dokta Ranjiti akiwa anawasubiri pembeni yake akiwa Kim pamona na walinzi wengine wapya watatu.
“Karibu mke wangu”
Dokta Rnjito alizungumza huku akiachia tabasamu pana, akajaribu kumkumbatia Phidaya, ila akamzuia na kuongoza moja kwa moja hadi kwenye gari aina Ranger rover Sport, akaingia na kumsubiria mume wake amfwate. Dokta Ranjiti akaingia kwenye gari akiwa amekasirika.

“Kwa nini umeniaibisha mbele ya wafanyakazi wangu?”
Dokta Ranjiti alizungumza kwa kufoka akiwa amekazia macho Phidaya, ambaye hakujali ukali huo wa dokta Ranjiti
“Umekuwa jeusi sio?”
“Ehee babuee usinipigi……”
Kofi zito likatua shavuni mwa Phidaya, hadi Kim aliye kaa siti ya mbele ahageuka kungalia kinacho endelea, akamkuta Phidaya akiwa amejikunyata huku mikono yake miwili akiiweka kweye shavu alilo tandikwa kofi zito

“Endesha gari”
Dokta Kim alizungumza huku akijiweka vizuri kwenye siti, Kim bila pingamizi akawasha gari na safari ya kueleka kwenye hoteli moja ya kifahari, ambayo dokta Kim, amepangishwa kwa miezi sita ikaanza. Ukimya ndani ya gari ulitawala kwa asilimia mia moja, hapakuwa na mtu aliye zungumza kitu cha aina yoyote hadi wanafika hotelini. Taratibu Phidaya akashuka kwenye gari, baada ya kufunguliwa mlango na Kim, dokta Ranjiti akamshika mkono na kunaza kutembea naye kuelekea ndani.
“Hichi ndio chumba chetu tutakacho kaa hapa kwa miezi sita hadi mambo yatulie ndani ya Japani sawa mama”
Phidaya hakuzungumza kitu cha aina yoyote zaidi ya kutafuta sofa na kukaa, moyoni mwake akazidi kumchukia Ranjiti, hakumpenda kama asivyo mpenda Sheteni.

Taratibu dokta Ranjiti, akaanza kuvua nguo zake moja baada ya nyingine mbele ya Phidaya hadi akabakiwa na bukta ya ndani tu.
“Nimekumisi mke wangu”
Dokta Ranjiti alizungumza huku akipanua mikono yake na kumkumbatia Phidaya aliye jikalia kwenye kochi, akimtazama kwa macho makali kuanzia juu hadi chini. Dokta Ranjiti, akaanza kunyonya shingo ya Phidaya, kuanzia upande wa kulie kwenda kushoto, juu kwenda chini.

Phidaya hakutikisika wala kuhisi kitu cha ania yoyote, mawazo yake yote yapo Japani kwa mwanaye Shamsa hakujua yupo kwenye hali gani kwa sasa. Hadi dokta Ranjiti anammalizia kumvua nguondipo Phidya akastuka, kutoka katika dibwi zito la mawazo.
“Unataka kufanya nini?”
“Phidaya alimuuliza kwa sauti ya ukali kiasi cha kumstua dokta Ranjiti aliye katika hisia kali za kimapenzi
“Ninahamu mke wangu”
Dokta Ranjiti alizungumza kwa sauti ya mahaba, mazito
“Hembu niondolee upuuzi wako, nahitaji kwenda kuoga”
Phidaya alizungumza huku akitaka kunyanyuka kwenda bafuni, ila dokta Ranjiti akamzuia.

“Usitake nitumie nguvu”
Dokta Ranjiti alibadilika dakika hiyo hiyo na kuzungumza kwa sauti ya ukali, Phidaya hakuwa na jinsi zaidi ya kukubali, mumewe kumfanya chochote ajisikiacho. Dokta Ranjiti akaanza kulifaidi tunda la Phidaya, kila alivyo zidi kufanya kitendo hicho ndivyo jinsi kumbukumbu za Phidaya zilivyo anza kumrejea kichwani mwake, akaanza kukumbuka jinsi mwanume wake wa zamani aliye jengeka kifua, alivyo kuwa akilala juu yake na kumkumbatia, mihemo yakimapenzi ya mwanaume huyo ilizidi kumfanya Phidaya kumbukumbu kurejea na kuiona sura ya mwanaume huyo, hakuiona sura ya dokta Ranjiti bali aliona sura ya mwanaume anaye kumbuka kwamba alimpenda sana kupita maelezo

“Mke wangu unanipenda…….”
Dokta Ranjiti alizungumza huku akihema akijitajidi kukipandisha kiliama kirefu kwa kasi
“Ohooo yesssss nakupenda sana mume wangu EDDY”
Jina la Eddy likamfanya dokta Ranjiti, kasi, mashamsham yakupandisha mlima mrefu kukatika gafla, macho yakamtoka hakuamini kwamba kumbukumbu za Phidaya zimerejea.
                                                                                                       ***
   Raisi mstaafu Praygod, baada ya kukabidhi nyaraka zote za serikali, kwa Mzee Godwion, hakuona haja ya kuendelea kukaaa nchini, kwa kutumia ndege yake binafsi aliyo kabidiwa na rafiki yake kipenzi Frennando ,yeye na mke wake, Rahab, wakiwa na walinzi wawili Pricsa na mllinzi wa kiume Emily wakaianza safari kwenda nchini Misri kwa ajili ya mapumziko kabla ya kwenda Mexco kuishi.

“Muheshimiwa kwa nini umeamua kuondoka mapema kiasi hichi nchini?”
Emily alimuuliza raisI mstafu bwana Praygod.
“Kwa sababu ya vitisho vya Godwin”
“Alikuambiaje?”
“Alinipa masaa ya kukaa nchini, sikuhitaji kulizungumza hilo mapema kwani lingezaa mtafaruku. Kwa sasa ninahitaji kuituliza akili yangu, nione kama miaka mingine mitano ijayo kama nitaweza kushinda uchaguzi”

“KKwa hiyo huto rudi tena Tanzania siku hizi za usoni?”
“Sijafikiria, au unashauri nini mke wangu?”
“Tuangalie upepo mume wangu”
Rahab alizungumza na kuendelea kucheza game kwenye simu yake, Priscar hakuzungumza chochote zaidi ya kuyasikiliza mazungumzo hayo.
“Ila ninawaonea sana huruma Watanzania, watanikumbuka”
“Kwa nini muheshimiwa?”
“Ahaa matokeo ya kura zao watayaona, tupo sisi tusikilizie itakuwaje”
 Safari yao ilizidi kusonga mbele, wakiendelea kuzungumza wakijadili mstakabali wa nchi ya Tanzania unapo elekea, akazidi kuwafumbua masikio walinzi wake mambo ambayo yalifanywa na mzee Godwin akiwa jeshini hadi hapo alipo kuwa, kila mmoja akaonyesha wasiwasi wake juu ya hali itakavyo kutwa siku chache zijazo.

Wakafika nchini Misri majira ya saa nane usiku, balozi wa Tanzania nchini hapo akawapokea akiwa na ulinzi wa kutosha, moja kwa moja wakaelekea kwenye hoteli kubwa ya kifarahi, iliyo andaliwa kwa ajili yake apumzike hapo kwa kipindi chote atakacho yeye na mke wake pamoja na walinzi wao.
                                                                                                 ***
   Mawazo mengi yakazidi kumuweka Eddy katika hali ya unyonge, hakutambua ni wapi alipo Phidaya. Siku zikazidi kuyoyoma, hapakuwa na matumaini yoyote ya kumuona Phidaya.

“Black Shadow”
Soroo alimuita Eddy mara baada ya kuingia kwenye pango hilo na kumkuta akifanya mazoezi ya viongo akiwa amevalia kinyago chake kichwani.
“Naam”
“Umesikia kwamba madam Phidaya ametekwa nyara?”
“Hapana kwani Phidaya ni nani?”
Eddy alijifanya hajui chochote ili azidi kupata habari kutoka kwa mtoto huyo aliye anza kumuamini sana kutokana na upeo wake wa akili kuwa mkubwa sana.
“Madam Phidaya ni mmoja wa wazamini wa kituo chetu, anatupatia misaada sana”

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumamosi ya May 20

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumamosi ya May 20

Tamko la TEF baada ya Star Tv kutangaza kufanya mahojiano na Makonda

Watuishi 72 Wasimamishwa Kazi Misungwi Jijini Mwanza

$
0
0
Watumishi zaidi ya sabini wamesimamishwa kazi wilayani Misungwi Mwanza kwa kukutwa na vyeti feki, ubadhilifu wa mali za Umma na utovu wa nidhamu.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Misungwi Bw. Athon Masele amesema kuwa watumishi 68 wamekutwa na vyeti feki, wawili walikuwa ni wabadhilifu wa mali za Umma huku wengine wawili walikuwa ni watovu wa nidhamu, jambo ambali limepelekea idara ya elimu na afya kuathirika kwa kiwango kikubwa zaidi.

Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Misungwi Mh. Charles Kitwanga amesema mwaka jana walisimamishwa kazi watumishi wawili kwa tuhuma za ubadhilifu wa mali za umma ambapo katika kipindi cha mwezi mmoja mapato yameongezeka kwa kiwango kikubwa kutoka kiasi cha shilingi milioni 24 hadi shilingi milioni 120 kwa mwezi hali iliyosaidia kupata hati safi baada ya CAG kuridhishwa na utendaji kazi wa halmashauri
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images