MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWAILIPOISHIA
ILIPOISHIA
“Ankooo”
Soroo akamkumbatia Lee Si, wakatoka nje ya ofisi hizo wakiwa wanatembea kuelekea kwenye moja ya bustani wakaka kwenye moja ya viti.
“Unajua ni sehemu gani alipo Black Shadow?”
Lee Si alimuuliza Soroo, mara baada ya kutoa noti ya dola mia na kumkabidhi, Sa Yon a Shamsa waliweza kumuona Lee Si akiwa na mtoto mmoja, Shamsa alipo jaribu kumkazia macho mtoto huyo akagundua ni Junio, jambo lililo mfanya ashuke kwenye gari na kuanza kukimbia kuelekea kule walipo kaa Soroo na Lee Si
ENDELEA
Shamsa akazidisha kasi, hadi karibu na bustani akasita kidogo kukimbia huku macho yake yote akiwa amemtupia Soroo, Lee Si, alipo muona Shamsa akatamani asimame na akimbie, ila akashindwa na kujikuta akiachia tabasamu pana la kinafki ili mradi asistukiwe mpango wake. Shamsa akaanza kutembea hatua za taratibu hadi sehemu walipo Soroo na Lee Si.Kufanana kwa Soroo na Junio ambaye kwa sasa ni Marehemu, kukamfanya Shamsa kulengwa lengwa na machozi.
Saroo akabaki akimshangaa Shamsa aliye piga magoti mbele yake, hakumjua ni nani aliye kuja. Soroo akamtazama Lee Si kisha akamtazama Shamsa, aliye anza kumshika mkono wake wa kulia. Shamsa akashindwa kujizuia na kujikuta akiangua kilio huku akimkumbatia Soroo, uchungu wa kifo cha Junio ukamrejea upya.
“Wewe nani?”
Soroo alimuuliza Shamsa huku ajijitoa mikononi mwake, Shamsa hakumjibu chochote zaidi ya kulia kwani hadi sauti wamefanana, Sa Yoo alisimama kwa mbali akishuhudia hali nzima inavyo endelea.
“Akooo Lee Si eti huyu ni nani?”
“Ahaa ahaa hu…..uuyu…..”
Lee Si alijing’ata ng’ata, hakujua ajibu nini japo swali alilo ulizwa ni rahisi sana kwake.
“Unaitwa nani mtoto mzuri?”
Shamsa alizungumza huku akijipangusa machozi yake kwa kiganja chake cha mkono wa kushoto.
“Soroo, wewe unaitwa nani?”
“Shamsa”
“Mbona sasa unalia?”
Shamsa akajitahidi kuachia tabasamu pana, kisha viganja vyake taratibu vikaanza kupapasa mashavu yote mawali ya Soroo.
“Nimetokea kukupenda”
“Akoo Lee Si, Shamsa ananipenda kama anti Phidaya”
Lee Si alitingisha kichwa tu, mdomo wake alijikuta ukiwa mzito gafla, hata maneno ambayo alipanga kumshawishi mtoto huyo yote yaliparanganyuka kichwani.
“Unamjua anti Phidaya?”
“Eheee alikuja siku ile kutuletea vyakula na hele hapa, akaniambia amenipenda”
“Ahaa basi mimi pia nianakupenda kutokana anti Phidaya ni mama yangu”
“Ahahaa kweliii?”
“Ndio”
Soroo akajikuta akifurahi sana kusikia maneno ya Shamsa, akamkumbatia tena na kumuomba asimame. Mlezi mmoja wa choa baada ya kuona ujio wa Shamsa, ikamlazimu kufika kwenye bustani hiyo kuuliza ni kitu gani kinacho endelea. Ikabidi Lee Si kuchukua jukumu la kumuelezea Shamsa kwamba ni mtoto wa bosi wake ambaye alikuja naye siku chache zilizo pita.
Mlezi huyo baada ya kusikia habari hiyo, akafurahi sana na kuomba kwenye na Shamsa ofisini kumtambulishwa kwa baadhi ya walezi wa chuo hicho ambao wanamuheshimu sana Phidaya kama mwanamke shujjaa aliye jitolea kuwalea watoto hao. Walezi hao hawakusita kumpa pole Shamsa kwa mama yake kutekwa, kila mmoja alisikitika sana kwa taarifa hiyo kwani wameondokewa mtu muhimu sana kwenye maisha yake.
“Nina imani kwamba atakuwa salama, nahisi watu hao wanahitaji pesa tu”
Shamsa aliwafariji walezi hao, ambao tukio la Phidaya kutekwa liliwagusa kwa kiasi kikubwa sana. Ila mlezi mmoja aakashindwa kustahimili kuuliza kitu amchacho kinamsumbua moyoni mwake.
“Mbona weewe na mama yako mumetokea sana kumpenda Soroo, kuliko watoto wengine?”
“Kusema kweli Soroo amefanana sana na mdogo wangu, mtoto wa mama, alifariki mwaka jana akiwa na miaka sita, ndio maana nilipo muona Soroo kwa mara ya kwanza nilijisikia uchungu sana”
MManeno ya Shamsa yakwafanya baadhi ya wamama walezi kumwagikwa na machozi, japo ni maneno machache ila kila mmoja alitambua uchungu wa kufiwa na mtoto, wakamuangalia Soroo, mbaye muda wote alijiegemeza mapajani mwa Shamsa.
Kitendo cha Shamsa kuingia na Soroo ofisini kwa walezi wa kituo cha kulele watoto, kilimkera sana Lee Si akanyanyuka kwa hasira kwenye benchi alillo kuwa amekalia na kwenda kwenye gari lake huku akimpita Sa Yoo pasipo kumsemesha neon la aina yoyote. Sa Yoo kama kawaida yake akamkata Lee Si jicho moja kali, kisha akatabasamu nakuegemea gari la Phidaya ambalo kwa sasa yeye ndio analitumia. Lee Si aliweza kuona kitendo ambacho Sa Yoo amekifanya, hakuhitaji kujibizana na Sa Yoo, akawasha gari na kuondoka kwa kasi huku akitimua vumbi kuingia barabarani.
***
Majira ya saa mbili usiku, ndege ya dokta Ranjiti ikatua wanja wa ndege jijini Cairo nchini Misri. Phidaya akiongozana na wahudhumu wawili wa ndege wakashuka na kumkuta dokta Ranjiti akiwa anawasubiri pembeni yake akiwa Kim pamona na walinzi wengine wapya watatu.
“Karibu mke wangu”
Dokta Rnjito alizungumza huku akiachia tabasamu pana, akajaribu kumkumbatia Phidaya, ila akamzuia na kuongoza moja kwa moja hadi kwenye gari aina Ranger rover Sport, akaingia na kumsubiria mume wake amfwate. Dokta Ranjiti akaingia kwenye gari akiwa amekasirika.
“Kwa nini umeniaibisha mbele ya wafanyakazi wangu?”
Dokta Ranjiti alizungumza kwa kufoka akiwa amekazia macho Phidaya, ambaye hakujali ukali huo wa dokta Ranjiti
“Umekuwa jeusi sio?”
“Ehee babuee usinipigi……”
Kofi zito likatua shavuni mwa Phidaya, hadi Kim aliye kaa siti ya mbele ahageuka kungalia kinacho endelea, akamkuta Phidaya akiwa amejikunyata huku mikono yake miwili akiiweka kweye shavu alilo tandikwa kofi zito
“Endesha gari”
Dokta Kim alizungumza huku akijiweka vizuri kwenye siti, Kim bila pingamizi akawasha gari na safari ya kueleka kwenye hoteli moja ya kifahari, ambayo dokta Kim, amepangishwa kwa miezi sita ikaanza. Ukimya ndani ya gari ulitawala kwa asilimia mia moja, hapakuwa na mtu aliye zungumza kitu cha aina yoyote hadi wanafika hotelini. Taratibu Phidaya akashuka kwenye gari, baada ya kufunguliwa mlango na Kim, dokta Ranjiti akamshika mkono na kunaza kutembea naye kuelekea ndani.
“Hichi ndio chumba chetu tutakacho kaa hapa kwa miezi sita hadi mambo yatulie ndani ya Japani sawa mama”
Phidaya hakuzungumza kitu cha aina yoyote zaidi ya kutafuta sofa na kukaa, moyoni mwake akazidi kumchukia Ranjiti, hakumpenda kama asivyo mpenda Sheteni.
Taratibu dokta Ranjiti, akaanza kuvua nguo zake moja baada ya nyingine mbele ya Phidaya hadi akabakiwa na bukta ya ndani tu.
“Nimekumisi mke wangu”
Dokta Ranjiti alizungumza huku akipanua mikono yake na kumkumbatia Phidaya aliye jikalia kwenye kochi, akimtazama kwa macho makali kuanzia juu hadi chini. Dokta Ranjiti, akaanza kunyonya shingo ya Phidaya, kuanzia upande wa kulie kwenda kushoto, juu kwenda chini.
Phidaya hakutikisika wala kuhisi kitu cha ania yoyote, mawazo yake yote yapo Japani kwa mwanaye Shamsa hakujua yupo kwenye hali gani kwa sasa. Hadi dokta Ranjiti anammalizia kumvua nguondipo Phidya akastuka, kutoka katika dibwi zito la mawazo.
“Unataka kufanya nini?”
“Phidaya alimuuliza kwa sauti ya ukali kiasi cha kumstua dokta Ranjiti aliye katika hisia kali za kimapenzi
“Ninahamu mke wangu”
Dokta Ranjiti alizungumza kwa sauti ya mahaba, mazito
“Hembu niondolee upuuzi wako, nahitaji kwenda kuoga”
Phidaya alizungumza huku akitaka kunyanyuka kwenda bafuni, ila dokta Ranjiti akamzuia.
“Usitake nitumie nguvu”
Dokta Ranjiti alibadilika dakika hiyo hiyo na kuzungumza kwa sauti ya ukali, Phidaya hakuwa na jinsi zaidi ya kukubali, mumewe kumfanya chochote ajisikiacho. Dokta Ranjiti akaanza kulifaidi tunda la Phidaya, kila alivyo zidi kufanya kitendo hicho ndivyo jinsi kumbukumbu za Phidaya zilivyo anza kumrejea kichwani mwake, akaanza kukumbuka jinsi mwanume wake wa zamani aliye jengeka kifua, alivyo kuwa akilala juu yake na kumkumbatia, mihemo yakimapenzi ya mwanaume huyo ilizidi kumfanya Phidaya kumbukumbu kurejea na kuiona sura ya mwanaume huyo, hakuiona sura ya dokta Ranjiti bali aliona sura ya mwanaume anaye kumbuka kwamba alimpenda sana kupita maelezo
“Mke wangu unanipenda…….”
Dokta Ranjiti alizungumza huku akihema akijitajidi kukipandisha kiliama kirefu kwa kasi
“Ohooo yesssss nakupenda sana mume wangu EDDY”
Jina la Eddy likamfanya dokta Ranjiti, kasi, mashamsham yakupandisha mlima mrefu kukatika gafla, macho yakamtoka hakuamini kwamba kumbukumbu za Phidaya zimerejea.
***
Raisi mstaafu Praygod, baada ya kukabidhi nyaraka zote za serikali, kwa Mzee Godwion, hakuona haja ya kuendelea kukaaa nchini, kwa kutumia ndege yake binafsi aliyo kabidiwa na rafiki yake kipenzi Frennando ,yeye na mke wake, Rahab, wakiwa na walinzi wawili Pricsa na mllinzi wa kiume Emily wakaianza safari kwenda nchini Misri kwa ajili ya mapumziko kabla ya kwenda Mexco kuishi.
“Muheshimiwa kwa nini umeamua kuondoka mapema kiasi hichi nchini?”
Emily alimuuliza raisI mstafu bwana Praygod.
“Kwa sababu ya vitisho vya Godwin”
“Alikuambiaje?”
“Alinipa masaa ya kukaa nchini, sikuhitaji kulizungumza hilo mapema kwani lingezaa mtafaruku. Kwa sasa ninahitaji kuituliza akili yangu, nione kama miaka mingine mitano ijayo kama nitaweza kushinda uchaguzi”
“KKwa hiyo huto rudi tena Tanzania siku hizi za usoni?”
“Sijafikiria, au unashauri nini mke wangu?”
“Tuangalie upepo mume wangu”
Rahab alizungumza na kuendelea kucheza game kwenye simu yake, Priscar hakuzungumza chochote zaidi ya kuyasikiliza mazungumzo hayo.
“Ila ninawaonea sana huruma Watanzania, watanikumbuka”
“Kwa nini muheshimiwa?”
“Ahaa matokeo ya kura zao watayaona, tupo sisi tusikilizie itakuwaje”
Safari yao ilizidi kusonga mbele, wakiendelea kuzungumza wakijadili mstakabali wa nchi ya Tanzania unapo elekea, akazidi kuwafumbua masikio walinzi wake mambo ambayo yalifanywa na mzee Godwin akiwa jeshini hadi hapo alipo kuwa, kila mmoja akaonyesha wasiwasi wake juu ya hali itakavyo kutwa siku chache zijazo.
Wakafika nchini Misri majira ya saa nane usiku, balozi wa Tanzania nchini hapo akawapokea akiwa na ulinzi wa kutosha, moja kwa moja wakaelekea kwenye hoteli kubwa ya kifarahi, iliyo andaliwa kwa ajili yake apumzike hapo kwa kipindi chote atakacho yeye na mke wake pamoja na walinzi wao.
***
Mawazo mengi yakazidi kumuweka Eddy katika hali ya unyonge, hakutambua ni wapi alipo Phidaya. Siku zikazidi kuyoyoma, hapakuwa na matumaini yoyote ya kumuona Phidaya.
“Black Shadow”
Soroo alimuita Eddy mara baada ya kuingia kwenye pango hilo na kumkuta akifanya mazoezi ya viongo akiwa amevalia kinyago chake kichwani.
“Naam”
“Umesikia kwamba madam Phidaya ametekwa nyara?”
“Hapana kwani Phidaya ni nani?”
Eddy alijifanya hajui chochote ili azidi kupata habari kutoka kwa mtoto huyo aliye anza kumuamini sana kutokana na upeo wake wa akili kuwa mkubwa sana.
“Madam Phidaya ni mmoja wa wazamini wa kituo chetu, anatupatia misaada sana”