MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWAILIPOISHIA
ILIPOISHIA
Kwa bahati nzuri, Shamsa akamkuta Eddy akiwa tayari amemaliza kuoga na kuvaa nguo zake pamoja na kinyago chake. Eddy katika kumduwaa, Shamsa aliye mjia kwa kasi, ndani ya bafu hilo akiongozana na waandhishi wa habari. Akastukia Shamsa akimkumbatia kwa nguvu bila hata kusita Shamsa akaanza kumnyonye denda black shadow, huku waandishi wakifyatua kamera zao kupiga picha za kuweka kwenye magazeti yao.
ENDELEA
Kitendo hicho kikampa Eddy kigugumizi, akataka kumuita Shamsa ila sauti haikutoka akajikuta akiugulia tu huku akijaribu kumtoa Shamsa mwilini mwake.
Mabaunsa na wapambe wa Sabogo wakawa tayari wamesha ingia ndani ya bafu. Mabaunsa wakambeba juu juu Shamsa aliye anza kupiga kelele za furaha.
“I love you black shadow”(Nakupenda black shadow)
Waandishi wa habari nao wakatolewa ndani ya bafu hilo. Akabaki Eddy na Sabogo.
“Hao ndio mashabiki kiongozi inabidi uwavumilie tu”
Eddy hakujibu kitu zaidi ya kubaki kimya, akimfikiria Shamsa.
‘Huyu mtoto amepatwa na nini?’
Alijiuliza swahi hilo kichwani mwake.
“Kiongozi?”
“Mmmmmmm”
Eddy alistuka kutoka katika dibwi la mawazo mengi
“Huyu binti amekuumiza nini, tumchukulie hatua za kisheria?”
“Hapana muacheni, na kama inawezekana kesho nahitaji akae meza ya VIP”
“VIP tena! Au umesha mzimikia tukamlete upate naye burudani usiku mzima. Kwa maana anaonekana kama changudoa”
“Fanya kama nilivyo kuagiza kufanya”
Eddy alizungumza kwa sauti nzito hadi Sabogo mwenyewe akabaki kimya na kutingisha kichwa akimaanisha kwamba amemuelewa.
Shamsa akamkuta Sa Yoo nje ya ukumbi, akamkimbilia na kumkumbatia kwa nguvu rafiki yake huyo huku akishangilia kama ameokota kipande cha dhahabu barabarani.
“Vipi nieleze umefanikiwa?”
“Ndio yaani ninafuraha achaa. NAKUPENDA BLACKKKK SHADOOOOOOWWWWWWWWW”
Shamsa alizungumza kwa sauti kubwa kama mwenda wazimu. Hata baadhi ya watui wakabaki wakimshangaa. Kutokana yupo nje ya ukumbi amboa mpiganaji huyo ametoka kuzichapa ulingoni muda mfupi ulio pita. Kila mtu akaamini kwamba binti huyo amechanganyikiwa kwa upendo kama wanachanganyikiwavyo wasichana wengine wanapo waonaga watu maarufu duniani.
Njia nzima ndani ya gari Shamsa, aliendelea kumzungumzia black Shadow. Kumbukumbu ya jinsi alivyo mrukia black shadow na kumnyonya denda, zikawa zinamrudia rudia. Hadi ikafikia kipindi akaanza kuutathini mwili wa mpiganaji huyo, akiwa hana nguo.
“Huli chakula?”
“Nimeshiba”
Shamsa alijibu huku akielekea chumbani kwake mara baada ya kufika katika nyuma wanayo ishi na Sa Yoo. Akaingia ndani kwake na kuufunga mlango kwa funguo. Haraka haraka akazivua nguo zake zote na kubaki kama alivyo zaliwa. Akasimama mbele ya kioo kikubwa cha kabati na kuanza kujichunguza huku akigeuka geuka akiliangalia umbo lake lililo jengeka vizuri.
“Mimi mzuri, kesho nawahi mapemaa ukumbini nimuone black shadow”
***
Ndani ya ndege ya kifahari aina ya Jet, Mzee Gdowin na John, pamoja na walinzi wao wawili. Waliendelea kuzungumza mambo mengi kuendelea kikundi chao ambacho kina watu wengi sana dunia. Ndege iliendelea kupasua mawingu kuelekea bara la Asia, ikitokea Amerika ya kaskazini. Ni safari ambayo imewachukua masaa mengi kadhaa, ila lengo na zumuni lao ni kwenda kuishuhudia fainali ya mapambano inayo endelea ndani ya Japani.
Wametokea kujikuta wakimpenda black shadow, mpiganaji mwenye ujuzi mkubwa sana katika maswala ya kupigana, wameona ni vyema wamchukue huyo ili awe miongoni mwa washirika wao ili kuzidi kujitanua kwenye kikuni chao.
Mara kadhaa wakajikuta wakitazama baadhi ya video za mapambano manne ya black Shadow. Ujuzi wao wa kupigana ulizidi kuwachanganya, na kutamani ndege hiyo iweze kufika katika muda mchache. Kwani wanahofia matajiri wengine duniani wanaweza kujitokeza na kumchukua black shadow katika mambo mbalimbali, ikiwemo uigizaji wa filamu.
“Mzee usiwe na hofu tutampata tuu. Nguvu ya kila kitu tunayo”
John alizungumza huku akimtazama Mzee Godwin anaye onekana kuwa na wasiwasi mwingi sana.
“Hawa marubani sijui wanaiendeshaje hii ndege, naona tunachelewa”
“Tutafika tu”
Masaa manne mbele teyeri wakawa wamefika nchini Japani, majira ya saa nne asubuhi. Wakapokelewa na mwenyeji wao ambaye moja kwa moja akawapeleka hadi kwenye hoteli moja ya kifahari.
“Pambano linaanza saa ngapi?”
Aliuliza mzee Godwin baada ya kupumzika kwa dakika kadhaa baada ya kufika hotelini.
“Saa nne usiku”
“Ahaa, hatuwezi kuonana na huyo black shadow muda huu kabla ya pambano?”
Mzee Godwin alimuuliza mwenyeji wao bwana Jackson Lee.
“Kusema kweli itakuwa ni ngumu kutokana black shadow yupo kwenye maandalizi ya pambano la usiku”
“Sawa kila kitu kiwekeni sawa, hata kesho muutaarifu uongozi wake kwamba ninahitaji kufanya naye kikao”
“Sawa mueheshimiwa”
***
Kengele ya mlangoni ndio iliyo mkurupusha Sa Yoo. Akajizoa zoa kitandani kwake na kuiangalia saa yake ya ukutani na kukuta ni saa tano na dakika tano asubuhi. Akasimama na kujinyoosha mara kadhaa huku akipiga miyayo. Taratibu kwa wenge la usingizi akaanza kutembea kuelekea mlangoni. Akafika mlangoni na kuminya moja ya batani ambayo pembeni yake kuna kitivii kidogo cha ukutani kinacho muonyesha mtu aliyopo nje ya mlango. Akamuona kijana mmoja aliye valia tisheni yekundu na kofia nyekundu akiwa amesimama, huku mkononi mwake akiwa ameshika boksi.
Uvaaji wa kijana huyo ukamuashiria Sa Yoo kwamba huyo ni mlete mizigo kutoka katika kampuni moja kubwa ya kutuma mizigo ndani ya Japani. Akafungua mlango na kumtazama kijana huyo.
“Wewe ndio Ms Shamsa?”
“Hapana ila unaweza kusema shida yako”
“Kuna mzigo wake hapa nimeagizwa kuuleta kama yupo basi nahitaji kuweza kumuona”
“Umetokea wapi?”
“Madam kama wewe si muhusika basi, siwezi kukuambia kwamba unatokea wapi?”
“Mmmmmm”
Sa Yoo aliguna kisha akaanza kumuita Shamsa kwa sauti kubwa. Shamsa aliitikia baada ya muda akatoka akiwa amejifunga taulo akiashiria kwamba naye ndio kwanza anaamka.
“Kuna mzigo wako hapa”
Sa Yoo alizungumza huku akiondoka mlangoni na kwenda kujibwaga kwenye sofa na kujilaza kumalizia malizia usingizi wake.
“Naamini wewe ndio ms Shamsa?”
“Ndio”
“Kuna mzigo wako hapa kutoka kwa Mr Sabogo”
“Mr Sabogo ndio nani?”
Sa Yoo baada ya kusikia hilo jina akakurupuka na kukimbilia mlangoni akiwa katika sura ya furahja
“Humjui wewe Mr Sabogo, si yule mzamini wa black shadow”
Shamsa kusikia hivyo akawa kama mtu aliye changanyikiwa kwa haraka, akasaini kwenye karatasi maalumu ya kijana huyo kisha wakaagana naye kijana huyo na kuufunga mlango. Akaanza kulifungu boksi hilo. Macho yao wote yakatua kwenye ua zuri jekundu, linalo nukia vizuri, Sa Yoo akalitoa ndipo wakaziona tiketi mbili zilizo kuwa chini ndani ya boksi.
“VIP TIKETIIIIIII UUUUUUUUU”
Shamsa alizungumza huku akiruka juu kwa furaha, Sa Yoon aye akampokonya moja wote wakajikuta wakiruka ruka kwa kushangilia kupata mualiko huo kutoka kwa black shadow.
Kila mmoja akawa anaombea muda na masaa yaweze kukimbia kwa haraka ili wafike ukumbini kushuhudia pambano ambalo si kwasababu watu wanalipenda, ila Shamsa anampenda mpiganaji wa pambano huyo ambaye ni black Shadow
Majira ya saa mbili usiku Sa Yoo na Shamsa wakawa wamefika katika ukumbi wa mapambano. Kwa siku hiyo hawakupita katika lango wanalo pita watu wa kawaidia ila walipita katika lango la kuingilia katika viti maalumu vya watu wenye hadhi ya juu. Kila sehemu Shamsa alipo pita alitazamwa na watu kwani habari za yeye kumbusu black shadow, zilienea kwenye magazeti mengi. Kwa msaada wa muhudumu katika sehemu hiyo maalumu wakaonyeshwa viti vyao vya kukaa, ambavyo mbele yake kuna kioo kikubwa na kigumu kinacho onyesha pambano hilo kwa ukaribu zaidi kutokana na lensi ya mvutano iliyo tengenezwa kwenye kioo hicho.
“Munatumia kinywaji gani?”
Dada muhudumu aliwauliza, kila mtu akaseme kinywaji anachho kihitaji. Watu walizidi kumiminika katika ukumbi, kila mtu aliitafuta siti yake na kuweza kukaa kusubiria muda muafaka wa pambano hilo liweze kufika.
Ulinzi mkali ukaimarishwa katika sehemu ya VIP, mzee Godwin na John ambaye muda wote maisha yake ni yakusukumwa kwenye kiti maalumu cha matairi. Wakaingi katika sehemu hiyo. Wakakaribishwa katika sehemu waliyo andaliwa, ambapo kuna wadada sita walio valia chupi aina ya bikini na sidiria wakiwa wamesimama, kwa ajili ya kuwapa huduma ya kuwachua chua miili yao pale watakapo kuwa wakiendelea kuliangalia pambano hilo.
Vipaza sauti vilivyomo ndani ya uwanja vilianza kutoa sauti ya kike ya mtangazaji wa pambano wa siku ya leo. Kelele zilizidi kurindima kila mahali, watu walikuwa kama wameingiwa na pepo la kushangilia kila walipo sikia jina la black shadow.
Wadada wengi walishika mabango yaliyo andikwa ujumbe tofauti tofauti wakionyesha hisia zao za kumpenda mpiganaji huyo, aliye jizolea umaarufu katika kipindi kifupi tu.
Macho ya Shamsa yakaendelea kutazama huku na kule, mara kadhaa alijaribu kuyapitia mabango ya wasichana waliyo yashika, akajikuta akiingiwa na woga pamoja na wivu wa kumkosa mpiganaji huyo katika swala zima la mapenzi.
“Anaye kuja kwenu kwa sasa ni BLACK SHADOWWW”
Uwanja mzima ukasimama huku watu wakimshangilia. Eddy hakuamini kupata idadi kubwa ya watu wanao mshangilia, kila alipo pitisha macho yake huku na kule aliona baadhi ya watu wakiwa wamevaa mavazi kama yake. Akaanza kutembea kwa kujiamini kuelekea uwanjani. Hakusita kupita karibu na washabiki walio kaa karibu na njia ya kuelekea ulingoni. Akawapa mikono kuashiria kwamba anawapenda kama wanavyo mpenda.
Akaingia ulingoni na kuendelea kuzunguka huku mkono wake mmoja wa kulia akiwa ameunyoosha juu, kwa ishara ya kuwasalimia watu. Muendesha shuhuli akamkaribisha Yong Po. Mashabiki wake nao wakasimama na kumshangilia mpiganaji huyo anaye sifika kwa kuweka rekodi ya kuwavunja vunja wapiganaji anao kutana nao. Hakuwa mwenye mwili mkubwa wa kutisha, ila sura yake iliyo komaa na yenye upara ulio kolezwa mafuta hadi unameta meta, ndivyo vilivyo mfanya Eddy ahofie kidogo. Ili kupoteza hofu hiyo ikambidi Eddy ashushe pumzi nyingi na kujiweka sawa huku akinyoosha nyoosha viungo vyake.
Muendesha shuhuli akatoka uwanjani na kuwaacha Eddy na mjapani huyo aliye komaa sana akionekana ni mpambanaji wa kipindi kirefu cha nyuma. Refarii akasimama katikati yao, akawapa sheria zinazo takiwa kufwatwa, alipo hakikisha kila mmoja ameelewa sheria hizo. Akaanzisha mpambano.
Young Po akaanza kuruka ruka huku akiichezesha miguu yake kwa kasi, jambo lililo mfanya Eddy kutazama miguu hiyo inavyo kwenda, kwani hakujua ni muda gani, mpinzani wake huyo atarusha teke. Kufumba na kufumbua Eddy akajikuta akiwa ameanguka chini, hakuelewa hata teke hilo la kifuani amepigwa muda gani.
Eddy akanyanyuka kwa haraka na kupanga mashambulizi, akarusha ngumi kadhaa baadhi zikampata Young Po ila baadhi alizikwepa. Yoong Po hakuwa nyuma, na yeye akaendelea kutupa mashambulizi ya kustukia kwani tayari alisha weza kumsoma Eddy kupitia mikanda ya video aliyo cheza jana. Alimgundua kwamba black Shadow ni mwepesi sana katika kukwepa, kurusha ngumi na mateke.
Pambano likazidi kufaana, watu walizidi kushangilia kila pale mmoja kati ya wapiganaji alivyorusha makonde kwa mwenzake.
Kila mmoja wa mashabiki hadi inatimu robo saa, hakuweza kujua mshindi ni nani kwani wapiganaji hao walijitahidi kila mmoja kufanya awezalo kuhakikisha kwamba anajibu makonde ya mwenzake.
Jasho likazidi kuwatirika wapiganaji, hata Shamsa mwenyewe, japo amekaakatika sehemu ambayo ina kiyoyozi cha kutosha ila naye jasho lilimwagika kila alipo shuhudia black shadow anapigwa.
Shamsa akajikuta akiaanza kuingiwa na furaha moyoni mwake baada ya kuanza kuona black shadow anamzidi Young Po. Si Shamsa pekee bali hata mashabiki wa black shadow nao walianza kumshangilia. Mzee Godwin na John nao hawakuwa nyuma kumshangilia mpiganaji huyo waliye muhitaji kwa udi na uvumba. Yong Po alipigwa ngumi moja takatifu ya shingoni iliyo muangusha chini na kulala kifudi fudi.
Uwanja mzima ukanyanyuka kwa kushangilia, refarii akamsogelea Yong Po. Akainama na kumuuliza kama ana weza kuendelea na pambano.
“Nipatie”