Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Jinsi Kitambi Kinavyopatikana na Jinsi Kinavyoondolewa na Dawa ya Mkataa Kitambi

$
0
0

Kitambi  ni  ile  hali  ya  tumbo  kuwa kubwa  na  kuchomoza  kwa  mbele  na  wakati mwingine  kufikia  hatua  ya  kunin’ginia.
JINSI  KITAMBI  KINAVYO  PATIKANA
Kwa  mujibu  wa  tafiti  mbalimbali  za  kitaalamu, mwili wa binadamu una seli kati  ya bilioni 50  hadi 200 za mafuta zilizogawanyika katika  sehemu  mbalimbali  za  mwili wa binadamu.

 Kwa wanawake  seli hizo  zipo sana katika maeneo ya matiti, kwenye  nyonga, kiunoni na kwenye makalio.

Kwa upande  wa  wanaume seli  hizo zinapatikana  sana kwenye kifua, tumboni na kwenye makalio pia.

Mafuta ya tumbo yanayofanya kitambi hukusanywa kwa njia kuu mbili:

i.Njia  ya kwanza ni mafuta kutoka kwenye tishu zilizo chini ya ngozi

ii.Na  njia  ya pili ni kutoka kwenye ogani za ndani kama moyo, kongosho n.k

SABABU ZA KUPATA KITAMBI
Sababu kubwa ya kitambi ni kukosekana ulingano wa nguvu(kalori) katika  mwili  wa  mwanadamu, hali  inayo  sababishwa  na  mtu  kula vyakula vinavyotia nguvu sana kuliko jinsi anavyoweza kutumia na kutoa kama taka mwili.

VYAKULA  VINAVYO  CHANGIA KULETA  KITAMBI

Vyakula vinavyochangia  kuleta  kitambi ni  pamoja  na :
i.Vyakula  vyenye  mafuta  mengi  kama  vile  nyama nyekundu  (iwe ni ya kuchemsha, kukaanga au kuchoma), nyama  ya  kuku  wa  kizungu  ( iwe  ya  kuchemsha, kukaanga  ama  kuchoma ), mafuta ya kupikia, (hasa yale yatokanayo na bidhaa za wanyama, kama siagi, na jibini), viazi ya kukaanga kwa  mafuta  (chips) pamoja  na  pizza.

ii.Vyakula vyenye wanga mwingi kama  vile ugali wa mahindi, mihogo, wali, mkate  mweupe.

iii. Vyakula  na  vinywaji  vyenye  sukari  nyingi  iliyo  ongezwa( added  sugar ), kama  vile  soda  na  keki.

iv. Vyakula  vilivyo  tengenezwa  kwa  ngano  na  sukari kama  vile  keki, skonzi, chapatti, maandazi, mkate  mweupe  nakadhalika

v. Pamoja  na  vinywaji  vilivyo  tengenezwa  kwa  kutumia  ngano  kama  vile  bia  za  aina  mbalimbali  na  kadhalika.

Vyakula  vilivyo  tajwa  hapo  juu, vikitumiwa  bila  kuzingatia  kanuni  za  mlo  kamili, huchangia  kuleta  tatizo  la  kitambi.

vi. Sababu nyingine ni  kutofanya  mazoezi  ya  mwili  na  viungo(  physical  exercises  )  kwa  muda  mrefu.

JINSI YA KUJUA KAMA UNA KITAMBI
Kitambi kinaweza kuonekana kirahisi kwa macho. Ila kujua ni kwa kiwango gani kitambi chako kipo inabidi kufanya vipimo vya kiuno(waist) na nyonga (hips).

Mzingo wa kiuno ukiwa >102 cm au 40  kwa wanaume na >88 cm au 35  kwa wanawake, na uwiano wa kiuno na hips(Waist-Hip Ratio) ikiwa >0.9 kwa wanaume na >0.85 kwa wanawake.

BMI ya 30 au zaidi inaashiria 'Obese' uzito kuzidi kiasi. Kuwa na mzingo uliozidi kawaida ni kiashiria hatari cha matatizo ya kimetaboliki, kuliko hata cha BMI.

Kipimo kingine cha kitambi ambacho kimeonyesha uwezo zaidi kuliko BMI katika kutabiri uwezekano mkubwa wa magonjwa ya moyo ni Index Of Central Obesity(Waist-To-Height Ratio-WHtR) ambapo uwiano ukiwa sawa na 0.5 au zaidi, hii ikimaanisha mzingo wa kiuno angalau ni nusu ya kimo cha mtu.

Kipimo kingine ni Body Volume Index, kinachopima kitambi kwa kupima umbo la mtu na mgawanyo wa uzito wake.

MAMBO  YANAYO  MUWEKA  MTU  KATIKA  HATARI  YA  KUPATWA  NA  KITAMBI
Tumekwisha  ona  hapo  juu jinsi  kitambi  kinavyo  patikana  na  vyakula  pamoja  na  sababu  nyinginezo  zinazo  sababisha  kutokea  kwa  kitambi, sasa  tutazame  mambo  yatakayo  kufanya  uwe  katika  hatari  ya  kupatwa  na  kitambi.

Kwa  mujibu  wa  tafiti  mbalimbali  za kitaalamu, mambo  yafuatayo  huwaweka  watu  katika  hatari  kubwa   ya  kupatwa  na  kitambi :

1. Ulaji  mbovu  wa  chakula; Ulaji  mbovu  wa  chakula  ni  ulaji  usio  zingatia  kanuni  za  mlo  kamili. Hapa  mtu  hufululiza  kutumia  chakula  cha  aina  fulani  pekee  bila  kuzingatia  aina  nyinginezo  za  chakula.  Mfano; mtu  anaweza  kuwa  anakula  mlo  ufuatao :

Asubuhi :  Mchemsho  ama    supu  ya  ng’ombe , chapatti  tatu  na  soda  moja.  Mchana :   Ugali  nyama  choma anashushia  kwa  maji  na  soda.

Jioni :  Mchemsho  wa  kuku  na  bia  mbili  nakuendelea.

Usiku  :  Chips  mayai  au  chips  kuku  au  chips  mishikaki  na  bia.

Mtu  huyu  akiendelea  na  utaratibu  huu  kwa  muda  mrefu, ni  lazima  atapatwa  na  kitambi.

2. Ulaji  mfululizo  wa  vyakula  vyenye  mafuta  mengi

3. Ulaji  mfululizo  wa  vyakula  vyenye wanga  mwingi  

4.Ulaji  mfululizo  wa  vyakula  vyenye  sukari  iliyo  ongezwa ( added  sugar  ).

5.Ulaji  mfululizo  wa  vyakula  vya  ngano.

6.Ulaji  mfululizo  wa   vinywaji  vyenye ngano  na  sukari.

7.Kutofanya  mazoezi  ya  mwili  na viungo  ( physical  exercises  ).

Mhusika  anapokuwa  katika  makundi  yote  yali yotajwa  hapo  juu, hali  huwa  mbaya  zaidi. 

NJIA ZA KUONDOA KITAMBI
Kuwa  na  kitambi  ni  lugha  ya  mwili  ( body-language )  inayo  leta  ujumbe  kwako  kwamba  “ Mwili    wako  haupo  salama  tena “

Kama  una  kitambi   maana  yake  una  mafuta  yasiyo  hitajika  mwilini, mwili  wako  unatumika  kuhifadhi  mafuta  usiyo  yahitaji.

Hali  hii  kitabibu  imaanisha  kwamba, ogani  nyinginezo  zilizomo  ndani  ya  mwili  wako  zinao gelea  kwenye  mafuta( fats  )  yasihotika  yaliyomo ndani  ya  mwili  wako,  jambo  linalo  kuweka  katika  hatari  kubwa  sana  ya  kushambuliwa  na  magonjwa  hatari  kama  vile  shinikizo  kubwa  la  damu, kiharusi  na kisukari  na  kwa kutaja  machache.

Hivyo  basi  ili  kuondokana  na  hatari  hiyo, yakupasa   kupambana  kuondoa  hayo  mafuta  yasiyo  hitajika  mwilini  mwako.

NJIA  ZA  KUONDOA  KITAMBI.
Unaweza  kuondokana  na  kitambi  kwa  kufanya  diet  pamoja  na  mazoezi ya  mwili  na  viungo.

Vilevile  unaweza  kuondoa  kitambi  na  kupunguza  mafuta  mwilini  kwa  kutumia  dawa  asilia  ya  kuondoa  kitambi  na  kuondoa  mafuta  yasiyo  hitajika  mwilini.

DAWA   ASILIA  YA  KUONDOA  KIAMBI  NA  MAFUTA  MWILINI.
Hii  ni  njia  ya  uhakika  kabisa  ya  kuondoa  tatizo  la  kitambi  pamoja  na  mafuta  yasiyo  hitajika  mwilini.

 Unaweza  kuondoa  tatizo  la  kitambi  pamoja  na  kupunguza  mafuta  mwilini  kwa  kutumia  DAWA  ASILIA   IITWAYO YA  MKATAA  KITAMBI.

 Dawa   hii  ni  ya asili  kabisa
“  Pure  Herbal “, ambayo  haijachanganywa  na  kemikali  yoyote, haina  side  effect kwa  mtumiaji  na  inaondoa  kabisa  tatizo  la  kitambi  ndani  ya  siku  kumi  na  nne.

JINSI  DAWA  YA  MKATAA  KITAMBI  INAVYO  FANYA  KAZI.
1.Huyeyusha  mafuta  yasiyo  hitajika  mwilini.

2.Husaidia  kupunguza  hamu  ya  chakula.

3.Inazuia  kutengenezwa  kwa  seli  za  mafuta  ( fat cells  ) katika  mwili  wa  mwanadamu. Unapokula  chakula  chenye  mafuta  mengi, dawa  hii asilia  hupambana  kuyafanya  mafuta  hayo  yasitengeneze  seli  za  mafuta  mwilini  mwako. Hali  hii  huuepusha  mwili  wako  kuhifadhi  mafuta   yasiyo  hitajika  mwilini.

4. Husaidia  kupunguza  uzito wa mwili  kwa  haraka  sana  endapo  itatumika  pamoja  na  diet  ya  kabechi.

UFANISI  WA  DAWA.
Ufanisi  wa  dawa  hii  ni  wa  asilimia  mia  moja. Dozi  ya  dawa  hii  hutumika  kwa  muda  wa  siki  ishirini  na  moja.

MATOKEO  YA  DAWA:
Dawa  hii  huondoa  kabisa  kitambi  ndani  ya  siku  kumi  na  nne.

BEI  YA  DAWA :
Dawa  hii  inaoatikana  kwa  kiasi  cha  SHILINGI  ELFU  HAMSINI  TU  (Tshs. 50,000/=)

MAHALI  TUNAPO  PATIKANA.
Tunapatikana  jijini  DAR  ES  SALAAM, katika  eneo  la  UBUNGO  karibu  na  SHULE  MSINGI  UBUNGO  NATIONAL  HOUSING  nyuma  ya  jengo  la  UBUNGO  PLAZA.

KWA  WATEJA  WASIO  WEZA  KUFIKA  OFISINI  KWETU.
Kwa  wateja  wasio  weza  kufika  ofisini  kwetu  Tabata, tunao  utaratibu  wa  kuwafikishia  dawa  mahali  popote  walipo  ndani  ya  jiji  la  Dar  Es  salaam.

KWA  WATEJA  WA  NJE  YA  DAR  ES  SALAAM.
Kwa  wateja  waliopo  nje  ya  Dar  Es  salaam, tunawatumia  dawa  kwa  njia  ya  MABASI.

Kwa  wateja  wa  ZANZIBAR  tunawatumia  dawa  kwa njia  ya  boti.

KWA  WATEJA  WA  NJE  YA  NCHI:
Kwa  wateja  wa  nje  ya  nchi, tunatumia  dawa  kwa  njia  ya  POSTA  au  DHL.

WASILIANA  NASI  KWA  SIMU  NAMBA : 0766  53 83 84

TUTEMBELEE:

Dk. Slaa azungumza kwa njia ya simu kuhusu madai ya kujiunga CUF

$
0
0
Wakati mgogoro ndani ya Chama cha Wananchi (CUF) ukizidi kutokota, Mwenyekiti anayetambuliwa na Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa, Profesa Ibrahimu Lipumba anadaiwa kutaka kumvuta aliyekuwa Katibu Mkuu wa chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Dk. Wilbroad Slaa, kujiunga na CUF.

Madai hayo yameibuka baada ya kuwepo kwa mawasiliano ya karibu kati ya Prof. Lipumba na Dk. Slaa ambao kwa nyakati tofauti mwaka 2015, walijiondoa kwenye vyama vyao kipindi cha mchakato wa kusaka mgombea urais wa vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya wananchi (Ukawa).

Ingawa Dk. Slaa kaika mahojiano alikanusha habari za yeye kutaka kujiunga na CUF, lakini habari zinasema kuwa mawasiliano kati ya Prof. Lipumba amekuwa akihaha kumshawishi Dk. Slaa pindi atakaporejea nchini ajiunge na CUF na kushika moja ya nafasi za juu za uongozi.

Taarifa za kuaminika zilieleza kuwa mawasiliano kati ya Prof. Lipumba  na DK. Slaa yanalenga kuboresha safu ya uongozi wa chama hicho kwa kumpa wadhifa wa Ukatibu Mkuu au Umakamu Mwenyekiti licha ya kudaiwa kwenda kinyume cha Katiba iliyoanzisha CUF.

Kwa mujibu wa katiba hiyo, nafasi za juu za uongozi wa chama hicho zinatakiwa kuzingatia uwiano wa pande mbili za Muungano. Endapo mwenyekiti anatoka Bara, Katibu Mkuu atatoka upande wa pili wa Muungano.

Baadhi ya wana CUF wanaomuunga mkono Prof Lipumba wamekiri kuwa kumekuwa na mawasiliano ya wawili hao, huku wakisema hakuna anayejua kiini cha kuimarika kwa mawasiliano hayo wakati huu ambapo CUF imepasuka katika makundi mawili, moja likiongozwa na Katibu Mkuu Maalim Seif na jingine lipo chini ya Lipumba.

Msemaji wa CUF inayoongozwa na Maalim Seif, Mbarala Maharagande, amesema kuwa taarifa za kurudi kwa Dk. Slaa amezisikia  japo hajui atajiunga na chama gani.

“Labda wale watu wa Lipumba ukiwauliza wanaweza kukuhakikishia hilo. Kwa nafasi ya katibu itakuwa ngumu kwa sababu katiba yetu hairuhusu, lakini kuwa mwanachama anaweza. Nguvu ya Lipumba ilishapungua sana na wenye chama chao (wananchi) watakwenda kukichukua na kumtoa ofisini kwa hiyo kama anarudi Dk. Slaa kuja kuongezea nguvu upande huo inawezekana”. alisema Maharagande.

Akizungumza kwa njia ya simu, Dk Slaa aliyekuwa Mbunge wa Karatu alisema taarifa hizo si sahihi kwani alishaahidi kwamba hatarudi kwenye siasa za vyama.

Alisema hawezi kuyumba kwenye uamuzi wake licha ya kukataa kuweka wazi kwamba ni lini atarejeea nchini, alisisitiza kuwa msimamo wake wa kuachana na siasa za vyama uko palepale.

“Maneno yangu hayayumbi, sitafanya siasa za vyama, nimeachana nazo. Naomba msiniingize kwenye siasa uchwara, sizifanyi hizo… Saisa ni ajenda. Hizo siasa za kishabiki zifanyeni nyinyi huko Tanzania, mimi sifanyi ushabiki, hakuna mtu anayekula ushabiki, ndiyo maana siasa zangu siku zote ni ajenda, Watu wanataka maji, wanataka chakula, wanataka elimu bora, si ushabiki”

“Kwa miaka 20 niliyokuwa kwenye siasa sijawahi kufanya  ushabiki, nilitafuta ajenda na kuipanga mikakati kwa ajili ya wananchi” alisema Dk Slaa alipozungumza na mwandishi wa habari hizi.

Alisema atasimama kupiga kelele kwa ajili ya Tanzania pale atakapoona mambo yanakwenda kombo na atafanya hivyo kwa mustakabali wa Taifa si siasa.

Septemba 25, 2015 akizungumza na wandishi wa habari kwa zaidi ya saa 2 kisha kutangaza kujitoa Chadema, alisema ni afadhali apotee kwenye ulimwengu wa siasa duniani kuliko kumuunga mkono Lowassa.

Credit: TanzaniaDaima

Kamanda Sirro awataka wananchi kutojichukulia sheria mikononi

$
0
0
Kamanda wa Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam, Kamishna Simon Sirro amewataka wananchi kuacha kujichukulia sheria mikononi badala yake waviachie vyombo husika ili viweze kufanya kazi yake.

Ameyasema hayo Jijini Dar es salaam wakati akizungumza na waandishi wa habari. Amesema kuwa wananchi kujichukulia sheria mikononi pindi wawakamatapo watuhumiwa ni kinyume cha sheria hivyo wanatakiwa kuacha mara moja tabia hiyo.

“Ni vyema wananchi wakaacha  tabia ya kujichukulia sheria mikononi ili vyombo usika vifanye kazi yake,”amesema Sirro.

Aidha, amesema kuwa wananchi kuwauwa watuhumiwa ni kosa kisheria kwani watakao bainika kufanya hivyo sheria kali dhidi yao zitachukuliwa.

Hata hivyo, ameongeza kuwa ni bora wananchi waache tabia hiyo ya kujichukulia sheria mikononi kwani vyombo husika kama Polisi na Mahakama vipo kwa ajili ya shughuli hiyo.

LIVE: Yanayojiri Bungeni Dodoma muda huu ( April 19)

$
0
0
Fuatilia hapa moja kwa moja kutoka Bungeni Dodoma, kuona yote yanayojiri katika Bunge la 11, Mkutano wa saba. 

Mkutano huu ni mahususi kwa ajili ya Bunge la bajeti ambapo Wizara mbali mbali zitawasilisha makadirio ya mapato na matumizi kwa mwaka wa fedha 2017/18 kabla ya kupitishwa na Bunge.

==> Bofya hapo chini  kutazama

Huu ndo Uwezo wa Korea Kaskazini Kivita......Ana Makombora Zaidi ya 1000 Yanayoweza Kurushwa Toka Bara Moja Hadi Jingine

$
0
0
Korea kaskazini inaaminika kumiliki zaidi ya silaha 1000 zenye uwezo tofauti ikiwemo kombora la maasafa marefu ambalo linaweza kuishambulia Marekani.

Mpango wa Pyongyang umeendelea katika miongo kadhaa ya hivi karibuni kutoka mizinga mikubwa katika miaka ya tisini na sabini hadi makombora ya masafa mafupi mbali na yale ya masafa marefu katika miaka 80 na 90.

Mifumo ilio na uwezo mkubwa inadaiwa kufanyiwa utafiti.

Hivi karibuni, Korea Kaskazini ilitangaza kwamba inaunda makombora ya masafa marefu yanayoweza kurushwa kutoka bara moja hadi jingine ambayo yanaweza kushambulia mataifa ya magharibi.

Taifa la Korea Kaskazini linaaminika kutengeza kombora la masafa marefu zaidi ambalo wachunguzi wamelitaja kuwa KN-08 ama Hwasong-13.
Makombora ya Hwasong yakiwa katika maonyesho

Ishara za kwanza kuhusu utengenezaji huo ulifanyika Septemba 2016 ambapo taifa hilo lilifanyia majaribio mashine mpya ya roketi ambayo baadhi ya watu wanasema inaweza kurusha kombora kutoka bara moja hadi jingine.

Idara ya ulinzi nchini Marekani Pentagon inaamini kwamba Korea Kaskazini inamiliki makombora 6 aina ya KN-08, ambalo lina uwezo wa kufika hadi Marekani.

Korea kaskazini inaaminika kutengeza toleo jipya la kombora hilo linalojulikana kama KN-14. Haahivyo makombora hayo hayajafanyiwa majaribio.

Lakini mnamo mwezi Januari 2017, kulikuwa na ishara ya jaribio, muda mfupi baada ya kiongozi Kim Jong un kudai kwamba taifa hilo lilikuwa katika awamu ya mwisho ya kutengeza kombora la masafa marefu linaloweza kurushwa kutoka bara moja hadi jingine.

Mpango wa kisasa wa kutengeza makombora yaa Korea Kasakzini ulianza kwa kutengeza makombora ya scud ambapo yalipitia Misri mwaka 1976.

Kufikia 1984, taifa hilo lilikuwa likitengeza makombora yake kwa jina Hwasong.

Inaaminika kuwa na makombora tofauti tofauti ya masafa mafupi ambayo yanaweza kulenga taifa jirani la Korea Kusini.

Uhusiano kati ya mataifa hayo mawili ya Korea umeharibika na yamekuwa yakijiandaa kukabiliana kivita.

Kombora la Hwasong 5 na Hwasong 6 ambayo pia hujulikana kama Scud B na Scud C yana uwezo wa kwenda kilomita 300 na 500 mtawalia kulingana na kituo cha Marekani kinachofanya utafiti wa kuzuia kuenea kwa nuklia.

Makombora hayo yanaweza kubeba makombora ya kemikali na nyuklia.

Silaha hizo zimejaribiwa na kupelekwa katika maeneo yanayohitajika na kombora la Hwasong-6 limeuzwa nchini Iran.

Ramani ya Korea Kaskazini na majirani zake wa Korea Kusini

Korea Kaskazini ilianza mpango huo mapema miaka ya 80 kutengeza kombora la masafa ya kadri kwa jina Nodong likiwa na uwezo wa kusafiri urefu wa kilomita 1000.

Kombora hilo limetengezwa kwa muundo wa Scud ,lakini ni asilimia 50 kwa ukubwa na lina mashine yenye uwezo mkubwa.

Uchanganuzi wa mwezi Aprili 2016 wa taassii ya kimataifa kuhusu utafiti wa mikakati ,unasema kuwa makombora hayo yalithibtishwa yanaweza kupiga maeneo yote ya Korea Kusini na Japan.

Imeongezea kuwa maonyesho ya Oktoba 2010 yalithibitisha kuwa kombora hilo linaweza kufika urefu wa kilomita 1,600 ikimaanisha kwamba linaweza kupiga kambi kadhaa za Marekani zilizopo katika eneo la Okinawa.

Makombora hayo ya Nodong yanadaiwa kujaribiwa 2006, 2009, 2014 na 2016.

Kombora la Musudan

Korea Kaskazni imekuwa ikitengeza makombora ya Musudan kwa miaka kadhaa, na hivi karibuni ilifanya majaribio 2016.

Makadirio yanatofautiana kuhusu viwango vyake, huku ujasusi wa Israel ukitaja uwezo wake kuwa kilomita 2,500 nacho kitengo cha ulinzi wa makombora nchini Marekani kikikadiria kuwa na uwezo wa kufika kilomita 3,200.

Duru nyingine zinasema kuwa kombora hilo lina uwezo wa kwenda kilomita 4,000.

Kombora la masafa mafupi la Musudan ambalo pia linajulikana kama Nodong B ama Taepodong-x linaweza kulishambulia taifa lote la Korea Kusini na Japan.

Kombora hilo linaweza kushambulia kambi za kijeshi za Marekani katika eneo la Guam.
Kombora la masafa marefu la Taepodong linaloweza kurushwa kutoka bara moja hadi jingine

Korea Kaskazini inasema kuwa imefanyia majaribio kombora la masafa ya kadri, kwa jina Pukguksong, mnamo mwezi Agosti 2016 likirushwa kutoka kwa manuwari.

Kombora la pili lilirushwa kutoka ardhini mnamo mwezi Februari 2017.

Pyongyang ilisema kuwa ilitumia mafuta ,na kufanya kuwa rahisi kuliwasilisha na kurusha. Hatahivyo maelezo kuhusu uwezo wake hayajulikani.

Credit: BBC

Rais Magufuli aamuru Madaktari walioomba kufanyakazi Kenya waajiriwe Tanzania

$
0
0
Madaktari 258 ambao walikidhi vigezo vya kwenda kufanya kazi nchini Kenya, sasa wataajiriwa na serikali ya Tanzania kutokana na kuwepo na zuio la Mahakama ya Kenya la kuwaajiri.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu, amesema uamuzi huo umefikiwa baada ya Rais Magufuli kumwelekeza jana kuwa awaajiri madaktari hao pamoja na wataalam wengine wa afya 11.

Madakatari hao walioomba hizo nafasi za kwenda Kenya walikuwa 496 kati ya 500 waliotakiwa, 258 ndio wakakidhi vigezo.

Mkataba wa Tanzania na Kenya ilikuwa mpaka Aprili 6 wawe wamepatikana hao madaktari na kati ya Aprili 6 mpaka 10 wasafirishwe kwenda Kenya, sasa baada ya kuajiriwa na serikali, Kenya wakiwa tayari na kuhitaji tena madaktari  watatafutiwa wengine.

Taarifa ya ajali ya treni na daladala ya kutoka Gongo la Mboto Alfajri leo Aprili 19, 2017.

$
0
0
Mtu mmoja amefariki dunia baada ya kutokea ajali ya basi la abiria/daladala (T 435 DGG) kutoka Gongo la Mboto kwenda Mnazi Mmoja kuigonga treni ya Pugu leo Aprili 19, 2017 saa 11 alfajiri katika makutano ya reli na barabara ya Nkurumah jijini Dar es Salaam.

Majeruhi wa ajali ni 23 , wanane wapo hospitali ya Amana na waliobakia 15 wapo Hospitali ya Taifa Muhimbili MOI watatu kati yao ni mahututi. Taarifa zaidi itatolewa kuhusu ajali hiyo.

Hata hivyo treni ya Pugu inaendelea na huduma zake kwa kufuata ratiba.

Imetolewa na Afisi ya Uhusiano kwa niaba ya Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TRL

Nd. Focus Sahani,
Dar es Salaam,
Aprili 19, 2017.

Sakata la Watumishi we Vyeti FEKI Lachukua Sura Mpya

$
0
0
Sakata la watumishi wa umma kushughi vyeti vya elimu limezidi kuchukua sura mpya na sasa wamefikia zaidi ya 10,000.

Hatua hiyo, inatokana na uhakiki uliofanywa na Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma ambayo imebaini waombaji kazi 39,511 kati yao, 1,951 wana vyeti vya kughushi.

Kuongezeka kwa idadi hiyo, kunatokana na kauli ya Rais Dk. John Magufuli, wiki iliyopita, kwamba anasubiri ripoti ya wafanyakazi wa Serikali ambao wamebainika kuwa na vyeti feki.

Kauli hiyo aliitoa Dar es Salaam, wakati akizindua mabweni mapya ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM).

Alisema anafahamu idadi ya watumishi wenye vyeti feki ni zaidi ya 9,000 na anaisubiri ripoti hiyo kuifanyia kazi.

“Kwa hiyo mnaweza mkaona shida zilizopo katika nchi hii, huku wafanyakazi hewa karibu 19,000, wanafunzi hewa ni zaidi ya 56,000, kila mahali unapokwenda ni matatizo, lakini ni lazima niyatatue matatizo kwa sababu mlinichagua kwa ajili hiyo,” alisema Rais Magufuli.

Akiwasilisha hotuba ya bajeti ya mwaka 2017/18 kwa ofisi yake jana bungeni mjini hapa, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Angella Kairuki, alisema baada ya kubainika kwa hali hiyo, wahusika waliondolewa kwenye mchakato, huku vyeti hivyo vikiwasilishwa katika mamlaka husika kwa hatua za kisheria.

“Wahusika waliondolewa katika mchakato pamoja na vyeti hivyo kuchukuliwa na kuwasilishwa kwa mamlaka husika kwa ajili ya hatua zaidi,” alisema Kairuki.

Hata hivyo, zipo taarifa zinazodai kuwa orodha ya watumishi wa umma ambao wamebainika kuwa na vyeti feki itawekwa hadharani Aprili 30.

Zaidi inaelezwa kuwa sakata hilo la vyeti feki linawagusa pia mabalozi ambao ni wawakilishi wa Watanzania katika mataifa mbalimbali, wakuu wa wilaya na mikoa.

Wizara yatenga Sh18.1 bil kujenga mahakama

$
0
0
Serikali kupitia Wizara ya Katiba na Sheria kwa Mwaka 2017/18 imetenga Sh18.1 bilioni kwa ajili ya kujenga na kukarabati mahakama mbalimbali nchini.
 
Kauli hiyo ilitolewa jana bungeni na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Angela Kairuki alipokuwa akijibu swali la nyongeza lililoulizwa na Mbunge wa Mlalo, Rashid Shangazi(CCM).
 
Shangazi alihoji ni lini Serikali itakarabati majengo machakavu ya Mahakama ya Mwanzo Mtahe iliyopo kwenye Jimbo la Mlalo mkoani Tanga.
 
Kairuki alisema azma ya Serikali ni kusogeza huduma za mahakama karibu na wananchi na kwamba katika mwaka wa fedha 2016/17 zilitengwa Sh 46.5 bilioni ambazo zimefanya kazi kubwa.
 
Alisema mahakama ambazo zipo kwenye utaratibu wa kukarabatiwa ni Mahakama Kuu ya Tanga na Dar es salaam na kuanza ujenzi katika Mahakama Kuu ya Mara na Kigoma.
 
Katika swali la msingi la Mbunge wa Njombe Mjini (CCM), Edward Mwalongo alitaka kujua kama Serikali itakuwa tayari kukarabati Mahakama za Mwanzo za Mahenye na Igomonyi ili wananchi waweze kupata huduma hiyo karibu.
 
Akijibu swali hilo Kairuki alisema moja ya changamoto kubwa zinazoikabili Mahakama ni uchakavu wa miundombinu na ukosefu wa majengo ya kutosha.
 
Alisema mpango uliopo ni kujenga majengo mapya na siyo kukarabati yaliyopo hasa ikizingatiwa kuwa majengo yaliyoombewa na mbunge yapo kwenye hifadhi za barabara na pia ujenzi wa Mahakama ya Mwanzo Njombe ni miongoni mwa miradi ya kipaumbele.
 
Kuhusu Mahakama ya Mahenye alisema imeshapata nafasi katika Ofisi ya Kijiji cha Uwemba kwa ajili ya kuendesha shughuli za Mahakama ya Mwanzo Mahenye ili huduma iendelee kutolewa wakati mipango ya ujenzi inaendelea.

Imebainika: Kumbe Marekani haikutuma meli za kivita Korea Kaskazini........Vilikuwa ni Vitisho Kwa Korea Kaskazini

$
0
0
Marekani na Korea Kaskazini zimeendelea kujibizana vikali, ambapo safari ya meli za kivita za Marekani ikiwemo meli yenye uwezo wa kubeba ndege za kivita ya Carl Vinson imeibua hisia kubwa na uwezekano wa Marekani kufanya shambulio la mapema kujaribu kulemaza mfumo wa kijeshi wa Korea Kaskazini.

Wakati taarifa hizo zikienea, imebainika kwamba meli hizo za kivita za Marekani hazikuwa zinaelekea upande wa Korea Kaskazini kama ilivyoripotiwa awali, bali zilikuwa zinaelekea eneo tofauti.

Awali iliripotiwa kuwa, Jeshi la wanamaji la Marekani lilikuwa likielekea Korea kama hatua ya kuionya Korea Kaskazini, ambapo Rais Trump pia alitangaza kwamba kundi kubwa la meli za kivita lilikuwa likitumwa eneo hilo, hivyo imebainika kuwa si kweli.

Hadi kufikia mwishoni mwa wiki, meli hizo zilikuwa zimesafiri mbali sana na rasi ya Korea na zilikuwa zinapitia mlango wa bahari wa Sunda kuingia katika Bahari ya Hindi.

Wakuu wa jeshi la wanamaji la Marekani katika Bahari ya Pasifiki walisema Jumanne kwamba walikuwa wamefutilia mbali safari ya meli hizo katika bandari ya Perth.

Kundi hilo la meli sasa "linaelekea Magharibi mwa Pasiki kama lilivyoamrishwa".

Bado haijabainika iwapo kulitokea sintofahamu katika mawasiliano au labla Marekani ilipotosha watu makusudi kujaribu kumtia wasiwasi kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong-un.

Aidha, Marekani imesema Korea Kaskazini ilipotekeleza jaribio la kombora ambalo lilifeli mwishoni mwa wiki ilikuwa na nia fulani ya kiuchokozi.

Waziri wa Ulinzi wa Marekani, James Mattis amesema Marekani inafanya kazi kwa karibu na China kukabiliana na Korea Kaskazini. Amesema kuwa jaribio hilo lililofanywa na Korea Kaskazini lilikuwa la kutojali na ilifanya hivyo kwa kuichokoza Marekani.

Aidha, Korea Kaskazini wamesema kuwa itafanya majaribio ya makombora kila wiki na pia ikaonya kwamba kutatokea vita kamili iwapo Marekani itaichukulia hatua za kijeshi.

“Iwapo Marekani wanapanga kutushambulia, tutajibu kwa shambulio la nyuklia kwa mtindo na njia yetu wenyewe,” amesema Naibu waziri wa mambo ya nje wa Korea Kaskazini, Han Song-ryol

Pande zote mbili zimekuwa zikijibizana vikali baada ya Korea Kaskazini kufanya jaribio hilo la makombora.

Bw Mattis alisema kwamba jaribio hilo la Jumapili halikuhusisha kombora linaloweza kuruka kutoka bara moja hadi jingine lakini bado lilikuwa ishara ya kutojali.

“Inadhihirisha ni kwa nini tunafanya kazi kwa karibu kwa sasa na Wachina…tunajaribu kudhibiti hali hii na lengo letu ni kumaliza silaha za nyuklia katika rasi ya Korea,” alisema.

Credit:BBC

Rais Magufuli, Makomandoo Kupamba Sherehe Za Miaka 53 ya Muungano Dodoma

$
0
0
Na: Lilian Lundo - MAELEZO.
Maonesho ya ukakamavu na mbinu za medani katika kupambana na adui hasa kulinda amani ya nchi yetu kutoka Kikosi Maalum cha Makomandoo wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ), itakuwa ni sehemu ya shamrasha zitakazopamba maadhimisho ya miaka 53 ya Muungano yatakayofanyika kwa mara ya kwanza mjini Dodoma Aprili 26 mwaka huu.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Ajira, Kazi, Vijana na Watu Wenye Ulemavu, Jenista Mhagama maadhimisho hayo yanatarajiwa kuhudhuriwa na Rais Dkt. John Pombe Magufuli, pia yatapambwa na burudani nyingine kutoka vikundi mbalimbali.

Taarifa ya Waziri Mhagama ametaja shughuli nyingine zinazotarajiwa kufanyika siku ya Muungano kuwa ni gwaride la heshima lililoandaliwa na vikosi vya ulinzi na usalama (JWTZ,JKT, Polisi na Magereza) na onesho la mbwa na farasi waliofunzwa.

Aidha, Waziri Mhagama aliongeza kuwa mambo mengine yatakayofanyika ni gwaride la uzalendo la wanafunzi wa shule za sekondari za Dodoma, burudani za vikundi vya ngoma za asili kutoka Dodoma na Zanzibar, Yamoto Band, vikundi vya muziki wa kizazi kipya kutoka kwa wasanii Mchungaji Zayumba, Jacob Beats, Mwenge Jazz Band na Mgosi Maturumbeta.

“Kauli mbiu ya sherehe za kutimiza miaka 53 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ni Miaka 53 ya Muungano; Tuulinde na Kuumarisha, Tupige Vita Dawa za Kulevya na Kufanya Kazi kwa Bidii,” alifafanua Waziri Jenista Mhagama.

Ametoa wito kwa wananchi wote nchini kusherehekea siku hiyo muhimu kwa kudumisha amani, upendo, umoja na mshikamano kwa maendeleo ya nchi.

“Ninaomba kuchukua nafasi ya pekee kuwaomba wananchi wote waliopo Dodoma kujitokeza kwa wingi uwanja wa Jamhuri siku hiyo ya Jumatano tarehe 26 Aprili 2017 kuanzia saa 12:00 asubuhi ili kusherehekea kwa pamoja maadhimisho hayo muhimu kwa nchi yetu,” alisema Jenista Mhagama.

Maadhimisho ya Muungano yanafanyika kwa mara ya kwanza Dodoma ikiwa ni siku kadhaa tangu Serikali ya Awamu ya Tano ianze kutumiza azma ya kuhamia katika makao makuu hayo mapya

Hahari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Alhamisi ya April 20

Agness Masogange Mahakamani Tena Leo

$
0
0
Msanii Agnes Waya, maarufu Masogange anatarajiwa kupandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam leo wakati kesi yake ya tuhuma za kutumia dawa za kulevya inapokuja kwa kutajwa na kuangalia kama upelelezi umekamilika au la.

Masogange anatarajiwa kufikishwa mbele ya Hakimu Mkazi, Wilbard Mashauri wa mahakama hiyo, ambaye ndiye anasikiliza kesi hiyo.

Mara ya mwisho kesi hiyo ilipotajwa mahakamani hapo hakimu huyo alimpa onyo mshtakiwa huyo baada ya kuchelewa kufika katika chumba cha mahakama, hatua iliyofikiwa baada ya Wakili wa Masogange, Nictogen Itege kuieleza mahakama kuwa mteja wake yuko njiani anakuja.

Taarifa hiyo ilisababisha, Hakimu Mashauri kumuhoji kuwa mbona yeye yupo mahakamani? Akadai kuwa walipita njia tofauti ndiyo sababu ikatokea kuwa mmoja kafika mwingine bado.

Hakimu Mashauri alisema mteja wake anatakiwa afuate masharti ya dhamana na mamlaka. Hata hivyo, baada ya muda kidogo Masogange alionekana katika viwanja vya Mahakama wakati kesi yake tayari ilikuwa imeahirishwa.

Awali, akisoma hati ya mashtaka, Wakili wa Serikali Constantine Kakula alidai kuwa kati ya Februari 7 na 14, 2017 katika maeneo yasiyojulikana ndani ya Jiji la Dar es Salaam Masogange alitumia dawa za kulevya aina ya Heroin (Diacety Imophine).

Katika shtaka la pili, Kakula alidai kuwa kati ya Februari 7 na 14, 2017 mtuhumiwa huyo alitumia dawa za kulevya aina ya Oxazepam na kwamba alifanya makosa hayo chini ya kifungu cha 18 (a) cha Sharia ya Kupambana na Dawa za Kulevya namba 5 ya mwaka 2015.

Baada ya kusomewa mashtaka hayo, Masogange alikana na yuko nje kwa dhamana ya wadhamini wawili waliosaini bondi ya Sh. milioni 10.

Raia wa kigeni nchini wapewa siku 90

Mwakyembe, Nassari Wavurugana Bungeni

$
0
0
Mbunge wa Arumeru Mashariki (Chadema), Joshua Nasari na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk Harrison Mwakyembe jana walichafua hali ya hewa bungeni na kusababisha mzozo mkubwa katika mjadala uliokuwa ukiendelea.

Wawili hao walihamisha mjadala wa hotuba ya bajeti ya Ofisi ya Rais Tamisemi na kurudisha suala la Richmond lililotokea mwaka 2008, huku Nasari akimtuhumu Dk Mwakyembe kuwa hakutenda haki katika ripoti yake na kumuondoa bila kumpa nafasi ya kujitetea aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa.

“Huyu Mwakyembe ndiye aliyeongoza ripoti ya Richmond na hakumpa nafasi mheshimiwa Lowasa ajitetee, leo tena kapewa dhamana ya kuongoza Wizara ya Habari, Nape (Nnauye) ameondolewa lakini hakuna nafasi ya kumhoji Mkuu wa Mkoa... hakuna haki hapo,” alisema.

Kauli za Nasari zilimfanya Dk Mwakyembe kuomba mwongozo na aliposimama alisema: “Nilikuwa naongoza kamati na utaratibu mzuri wa kisheria ni kuwa, kama utaona kuna ushahidi wa kutosha hakuna sababu ya kumuita mtu, unaleta taarifa bungeni halafu Bunge linakuja kuamua.”

Dk Mwakyembe alisema katika taarifa yao, waliona hakuna sababu ya kumuita Lowassa kuhojiwa kwani ushahidi ulikuwa wazi na ndiyo maana hakutakiwa kuitwa mbele ya kamati badala yake walikuja kumshtaki bungeni.

“Huyu mtu wanayekuwa na mahaba naye kwa sasa, nasema wamlete hata leo waone kama hatutamnyoa kwa chupa, kanuni za kibunge zinaruhusu anaweza kuirudisha tena taarifa ya Richmond na ikaanza upya,” alisema Dk Mwakyembe.

Live: Maswali ya papo kwa hapo kwa Waziri Mkuu Bungeni leo April 20, 2017

$
0
0
Fuatilia hapa yanayojiri Bungeni Dodoma muda huu, ambapo leo Aprili 20, 2017 Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa anajibu maswali ya moja kwa moja ya Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania..

==Hapo chini kuna Live Video toka bungeni

Hoja ya kutaja wabunge 11 watakaotekwa yazimwa.....Usalama wa Taifa Wapigwa Marufuku Bungeni

$
0
0
Mazoea ya baadhi ya wabunge kuomba mwongozo wa kiti cha spika kuzima hoja za wabunge wenzao, jana uliibuka tena baada ya Mbunge wa Makambako, Deo Sanga kuomba mwongozo uliozima hoja ya kutaja majina ya wabunge 11 wanaodaiwa kutaka kutekwa.
 
Sanga aliomba mwongozo wa Spika kwa kutumia Kanuni 68 (7) pamoja na 64 A,B,C, alisema ndani ya Bunge yameongelewa mambo yanayohusu mahakama, usalama, mauaji na kutekwa.
 
“Nilikuwa nadhani kupitia kanuni hizi naomba mwongozo wako nini kazi ya Bunge mheshimiwa naibu spika,” alisema.
 
Mwongozo huo uliibuka baada ya Mbunge wa Viti Maalum CCM, Angelina Malembeka kuwataka wabunge waliosema kuna orodha ya wabunge 11 wanaotakiwa kutekwa kuwataja majina yao.
 
Hoja ya Malembeka ilimlenga Mbunge wa Nzega Mjini (CCM), Hussein Bashe ambaye siku za karibuni aliliambia Bunge kwamba ameambiwa na mmoja wa mawaziri kuwa kuna wabunge 11 watatekwa na Usalama wa Taifa.
 
Malembeka alitoa hoja hiyo wakati akichangia mjadala wa hotuba ya bajeti ya Ofisi ya Rais, Tamisemi na Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kwa mwaka wa fedha 2017/18.
 
Hata hivyo, mwongozo wa spika ulioombwa na Sanga ulizima kiu ya Malembeka aliyetaka kumbana Bashe ataje majina ya wabunge hao 11, badala ya kutaja idadi pekee.
 
Akijibu mwongozo wa Sanga, Naibu Spika wa Bunge, Dk Tulia Ackson aliamua kupiga marufuku masuala ya Usalama wa Taifa kujadiliwa bungeni. 

Dk Tulia alisema wanaotaka kufanya hivyo wawasilishe hoja mahsusi kwa kufuata Kanuni za Kudumu za Bunge.
 
Awali, Malembeka alisema ni vizuri Usalama wa Taifa wakaongezwa fedha, mbinu mpya na vifaa ili kurahisisha utendaji wao wa kazi.
 
“Kutwa mtu anatuma ujumbe kwenye simu kwa rafiki yake eti nimetekwa nyara, waulizeni waliotekwa hiyo simu wamepata wapi ya kutumia huo ujumbe kuwa wametekwa?
 
“Kutekwa nyara si mchezo, waulizeni wenzenu waliotekwa
watawaambia si mchezo. Na hao wanaojifanya usalama feki naomba mheshimiwa waziri uwashughulikie kwa sababu sasa mtu akishakata ‘panki’ lake akavaa kaunda suti yake anatoa kitambulisho anasema mimi Usalama wa Taifa.
 
“Usalama wa Taifa mchezo! Mtu anajizungusha zungusha
anawatisha watu mtaani unasema Usalama wa Taifa sasa wale wanaojifanya Usalama wa Taifa na kuogopesha watu mtaani washughulikiwe,” alisema.

Majibu ya Harmorappa Baada ya Kuulizwa Kuhusu Jinsia Yake

$
0
0
Rapa Harmorapa jana aliwaacha mdomo wazi baadhi ya mashabiki wake baada ya kutoa jibu tofauti kuhusu jinsia yake.

Akichat na mashabiki katika mtandao wa facebook wa EATV ndani ya kipindi cha  Kikaangoni, rapa huyo aliulizwa swali kuhusu jinsi yake "Wewe ni mwanaume wa aina gani?' na rapa huyo kujibu "Mimi ni strong woman".
Jibu hilo limewashangaza mashabiki wengi wa rapa huyo kwa kuwa wanajua yeye ni mwanaume huku wengine wakidhani huenda hakuelewa swali kutokana na lugha ya kingereza iliyotumiwa.

Akiongea kuhusu uwezo wake wa kuongea na kuandika lugha ya kingereza alisema:“Lugha ya Kiingereza naifahamu vizuri lakini ile kuongea ongea ndiyo siwezi”

Rapa huyo kwa sasa anafanya vizuri na wimbo wake ‘Kiboko ya Mabishoo’.

Rais Magufuli Kufungua Kongamano La Maadili

$
0
0
RAIS Dk. John Magufuli anatarajiwa kufungua kongamano la maadili  lililoandaliwa na Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (Bakwata).

Akizungumza kwa niaba ya Mufti wa Tanzania, Sheikh Mkuu Aboubakar Zuberi Mwenyekiti wa Halmashauri Kuu ya Bakwata, Sheikh Khamis Mataka, alisema kongamano hilo litafanyika Aprili 24.

Alisema lengo la kongamano hilo ni kujadili mmomonyoko wa maadili uliopo ndani ya jamii hivi sasa.

“Kongamano hili limeandaliwa na Bakwata ambapo litahudhuriwa na masheikh mbalimbali pamoja na viongozi wa kidini kutoka mikoa mbalimbali, lengo likiwa ni kuangalia jinsi maadili yalivyoporomoka na kutafuta mbinu ya kuijenga jamii iliyo bora,” alisema Sheikh Mataka.

Alisema kongamano hilo la siku moja litafungwa na Rais wa Zanzibar, Dk. Ali Mohamed Shein.

Alisema wengine watakaohudhuria kongamano hilo ni wajumbe wa Ulamaa Taifa, masheikh kutoka taasisi mbalimbali, viongozi wa kidini kanda, mabalozi, wakuu wa vyombo vya usalama na wananchi walioalikwa.

Sheikh Mataka alisisitiza kuwa maadili ni muhimu ndani ya jamii na kwamba kwa sasa nchi inakabiliwa na mmomonyoko wa maadili.

“Ukiona jamii inazungukwa na walevi, watumiaji dawa za kulevya, binadamu wengine wanafurahia wenzao wakiuawa au kupata ajali, ni hali ya kupoteza mwelekeo wa maadili,” alisema Sheikh Mataka.

Harmorappa Ampa Ushauri Rais Magufuli

$
0
0
Msanii Harmorapa ambaye sasa anafanya vyema na wimbo wake 'Kiboko ya mabishoo' amefunguka na kutoa ushauri kwa Rais Magufuli juu ya mambo ambayo angependa kuona Rais anayafanyia kazi.

Harmorapa akiwa kwenye kipindi cha Kikaangoni kinachofanyika kupitia ukurasa wa Facebook wa EATV kila siku ya Jumatano  ameshauri Rais Magufuli kuboresha zaidi miundombinu ambayo inaweza kuleta tija na maendeleo kwa nchi lakini pia amemuomba awaangalie pia wasanii ili waweze kunufaika na kazi zao.

"Rais Magufuli unajua yeye ndiye mwenye nchi sasa, hivyo mimi namuomba aboreshe zaidi suala la miundombinu natambua amefanya mambo mengi na makubwa kwenye sekta hiyo ila aboreshe zaidi, lakini pia namuomba Rais Magufuli aendelee kuwafinya wale wajanja wajanja kama ambavyo anafanya saizi na kingine atuangalie na sisi wasanii na kazi zetu" alisema Harmorapa

Mbali na hilo Harmorapa amegusia suala la yeye kuonekana ni mtu wa kiki amesema kuwa yeye si mtu wa kiki bali hizo kiki zinamfuata yeye.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images