Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Bunge Lakataa majina ya wagombea wa CHADEMA na CUF kwenda kugombea nafasi ya Ubunge wa Afrika Mashariki (EALA)

$
0
0

Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania limekataa majina ya wagombea wa CHADEMA na CUF kwenda kugombea nafasi ya Ubunge wa Afrika Mashariki (EALA) baada ya kukutwa na mapungufu katika fomu zao.

Hatua hiyo imekuja baada ya wagombea hao kuonekana na mapungufu mbalimbali yaliyobainika kwenye nyaraka zao a uteuzi yakiwa yamekiuka masharti ya Ibara ya 50 ya Mkataba wa Kuanzishwa kwa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Ibara ya 67 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Kifungu cha 4(4) cha Sheria ya Uchaguzi wa wajumbe wa Bunge la Afrika Mashariki ya Mwaka 2011 iliyotungwa na Bunge la Afrika Mashariki.

Aidha taarifa hiyo imesema CHADEMA uteuzi wao haukuzingatia jinsia, lakini pia hawajaambatanisha fomu za maombi ya wagombea, orodha ya waombaji pamoja na fomu ya matokeo ya kura.

Huku CUF wakiwa wametuma fomu za uteuzi wa wagombea zikiwa zimewasilishwa na mamlaka mbili tofauti, wagombea wawili hawana uthibitisho wa uraia wao, fomu za uthibitisho wa hiari ya kugombea haikuwepo kwa wagombea wote, orodha ya waombaji haipo kwa mgombea mmoja, fomu ya matokeo ya kura kwa wagombea haikuwepo pamoja na fomu ya mahudhurio kwa mgombea mmoja kutotimia.

Kutokana na mapungufu hayo msimamizi wa Uchaguzi Dr. Thomas D. Kashililah amesema ameshindwa kufanya uteuzi huo huku akiwataka kurekebisha mapungufu yaliyobainishwa kabla ya saa 7 mchana, Aprili 4 ofisini kwake mjini Dodoma.

Kwa upande mwingine amewashukuru wadau wote hususani vyama vyote vya siasa nchini kwa ushirikiano mzuri waliyompa katika zoezi zima la mchakato wa uteuzi wagombea pamoja na vyombo vya habari kwa ujumla.

SADC Yalipongeza Baraza La Usalama La UN Kwa Kuongeza Muda Kwa Misheni Ya Ulinzi DRC

$
0
0
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Mawaziri ya Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama ya Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC), Mhe. Dkt. Augustine Mahiga amelipongeza Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa (UNSC) kwa kuridhia na kupitisha azimio namba 2348 (2017) la kuongeza muda kwa Misheni ya Ulinzi wa Amani chini ya MONUSCO iliyopo Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) hadi tarehe 31 Machi, 2018.

Mhe. Mahiga ametoa pongezi hizo wakati akihutubia Baraza hilo kwenye Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa Jijini New York, Marekani hivi karibuni.

Mhe. Mahiga ambaye aliwakilisha nchi 15 za SADC alisema kuwa anaupongeza Umoja wa Mataifa kwa ujumla chini ya uongozi wa Katibu Mkuu, Bw. Antonio Guterres kwa kufikia uamuzi wa kuongeza muda kwa MONUSCO na jitihada nyingine nyingi za kutafuta suluhu ya kudumu kwa changamoto mbalimbali zinazoikabili DRC kwa muda mrefu ikiwemo ukosefu wa amani na usalama.

Mhe. Mahiga alisema kuwa, kupitishwa kwa azimio hilo kunatoa matumaini mapya kwa wananchi wa DRC na dunia kwa ujumla kwamba Umoja wa Mataifa una nia ya dhati kuhakikisha amani ya kudumu inapatikana nchini humo.

Aidha, Mhe. Waziri Mahiga alitumia nafasi hiyo kuuomba Umoja wa Mataifa kutambua mchango mkubwa unaotolewa na Kikosi Maalum cha Force Brigade Intervention-FIB kilichoundwa na SADC ambacho kinashirikiana na MONUSCO katika ulinzi wa amani nchini DRC.

Alieleza kuwa katika kipindi cha miaka minne tangu kuanzishwa kwa FIB kimeonesha uwezo mkubwa kwa kufanya operesheni ngumu za kukabiliana na vikundi vya waasi na kuvidhibiti, hali iliyopelekea MONUSCO kuaminika zaidi. FIB ina mchango wa vikosi vya ulinzi wa amani kutoka nchi tatu za SADC ambazo ni Tanzania, Afrika Kusini na Malawi.

“Kuanzishwa kwa FIB miaka minne iliyopita ulikuwa ni uamuzi wa pekee kwa Baraza la Usalama na SADC katika masuala ya ulinzi wa amani hususan kwenye maeneo yenye changamoto kubwa za usalama na amani. Hivyo naamini pamoja na kwamba FIB ni Chombo cha muda bado kinahitaji kutambuliwa na kupongezwa” alisema Waziri Mahiga.

Kuhusu changamoto mbalimbali ambazo MONUSCO inakabiliana nazo ikiwemo matishio mapya ya usalama katika maeneo ya Kivu, mbinu mpya za mashambulizi za waasi, ukatili kwa raia na ukiukwaji wa haki za binadamu Waziri Mahiga alisema masuala haya yanailazimu pia MONUSCO kubadilisha mbinu za operesheni ikiwemo kuongezewa vifaa na bajeti ili kuweza kukabiliana kikamilifu na changamoto hizo.

Pia aliliomba Baraza la Usalama, SADC, Umoja wa Afrika, ICGLR na Nchi zinazoongea Kifaransa kushirikiana katika kutafuta suluhu ya kudumu kwa changamoto zinazoikabili DRC kwa sasa.

Vile vile, Mhe. Waziri Mahiga alitumia nafasi hiyo kwa niaba ya SADC kuiomba na kuialika Jumuiya za Kimataifa kuisaidia Tume ya Uchaguzi ya DRC ili iweze kuandikisha wapiga kura na kuandaa uchaguzi nchi nzima. Pia aliwaomba wanasiasa wa nchini DRC kukabiliana na vurugu za kisiasa zinazoendelea nchini humo kwa sasa na kukwamisha utekelezaji wa Mkataba uliofikiwa mwezi Desemba 2016 chini ya Baraza la Maaskofu (SENCO) la DRC.

Mhe. Mahiga aliongeza kusema kuwa SADC itatuma Misheni Maalum ya Mawaziri nchini DRC katika kipindi cha majuma mawili kuanzia sasa kwa ajili ya kwenda kuzungumza na kushauriana na wadau mbalimbali wa masuala ya siasa nchini DRC ili kutafuta suluhu.”Sisi , nchi wanachama wa SADC hatupo tayari kuona Mkataba wa Desemba unakwama” alisisitiza Waziri Mahiga.

Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki
Dar es Salaam, 03 Aprili, 2017.

Umoja Wa Ulaya Waipatia Serikali Ya Tanzania Msaada Wa Bilioni 490

$
0
0
Na Daudi Manongi - MAELEZO
Serikali kupitia Wizara ya Fedha na Mipango imesaini msaada wa shilingi Bilioni 490 usiokuwa na masharti yeyote kutoka Umoja wa Ulaya ikiwa ni msaada wa kibajeti kwa kipindi cha miaka minne kuanzia mwaka wa bajeti wa 2017/18.
 
Mkataba huo umesainiwa na Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango Bw. Dotto James kwa niaba ya Serikali na Balozi wa Umoja wa Ulaya (EU) nchini Bw.Roeland van de Geer kwa niaba ya Umoja wa Ulaya.
 
Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kusaini mkataba huo Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango Dotto James amesema Umoja wa Ulaya umetoa msaada huo kutokana na kuvutiwa na juhudi za Serikali ya Awamu ya Tano katika maeneo mbalimbali ikiwemo kupambana na rushwa na ubadhirifu wa mali za umma.
 
“Nadhani mmeshuhudia utiaji saini huu ulioisha hivi punde na Umoja wa Ulaya wametuhakikishia kuendelea kutusaidia katika masuala ya misaada ya kibajeti pamoja na kuwa bega kwa bega na Serikali katika masuala mbalimbali ya maendeleo”, aliongeza Katibu Mkuu huyo.
 
Pamoja na hayo mpango wa pili wa maendeleo wa Taifa wa Bajeti ya mwaka 2017/18 pia utapewa msaada na umoja huo kwani wameuona mpango huo una tija na kuweka mkazo katika viwanda na kilimo.
 
Kwa upande wake Balozi wa Umoja wa Ulaya (EU) nchini Roeland Van de Geer amesema kuwa wameliangalia zaidi suala la utawala kama eneo kuu katika mpango wa ushirikiano na Tanzania na vilevile wanatazamia maendeleo zaidi katika maeneo ya kilimo,ujenzi wa barabara za vijijini na nishati.
 
“Mkataba ambao tumeusaini utaiwezesha Wizara ya Fedha na Mipango katika ukusanyaji wa mapato,zitaboresha uwajibikaji na utumiaji mzuri wa mali za Serikali, na Umoja wa Ulaya unasapoti azma ya viwanda ya Serikali ya Awamu ya Tano,”Aliongeza Roeland Van de Geer.
 
Amesema kuwa ushirikiano uliopo katika ya Tanzia na Umoja wa Ulaya ni mpana sana na utaendelea kuimarika zaidi katika kipindi hiki ambacho mageuzi ya sera yanahitajika.

Maalim Seif: Simtambui Lipumba na Hana Uwezo wa Kunitoa......Mi ndo Katibu Mkuu halali wa CUF

$
0
0
Jana  Katibu mkuu wa chama cha wananchi CUF Maalim Seif alifanya mahojiano na kituo cha Television cha Azam two na kusema hamtambui mwenyekiti wa chama hicho Pro. Ibrahim Lipumba pamoja na uwamuzi aliochukuwa wakumuweka kando na nafasi yake kukaimiwa na Magdalena Sakaya.

Malim Seif alisema  hawezi kwenda ofisi za Buguruni kwa kuwa makao makuu ya chama hicho yapo Zanzibar na sio Dar es Salaam

==>Msikilize hapo chini akiongea

Ratiba ya Mkutano wa Saba wa Bunge Linaloanza Leo Jumanne April 4

$
0
0
Waziri wa Fedha na Uchumi Dkt Philip Mpango anatarajiwa kusoma Bajeti ya serikali kwa mwaka wa fedha 2017/18 siku ya Alhamisi, Juni 15 mwaka huu.

Tarehe hiyo ni kwa mujibu wa ratiba ya Mkutano wa Saba wa Bunge unaoanza leo  Jumanne (Aprili 4) katika ukumbi wa Bunge mjini Dodoma, mkutano ambao ni maalum kwa ajili ya bajeti.

Ratiba hiyo inaonesha shughuli ya kwanza kuwa ni uchaguzi wa wabunge wa Bunge la Afrika Mashariki siku ya Jumanne, na Bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu itasomwa siku ya Alhamisi, Aprili 6 na kujadiliwa kwa siku nne, ikifuatiwa na bajeti ya Rais (siku 4) na Bajeti ya Ofisi ya Makamu wa Rais (Siku 1) kabla ya bajeti ya Wizara ya Sheria na Katiba Aprili 25.

Mbali na bajeti za wizara, mkutano huo pia utajadili na kupitisha miswada kadhaa ya sheria ukiwemo Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria Mbalimbali wa Mwaka, 2017

==>Itazame hapa ratiba kamili ya mkutano huu, ambao utamalizika siku ya tarehe 30, Juni, 2017

Polisi Yaua Majambazi Yakiume Yaliyokuwa Yamevaa Hijabu

$
0
0
Watu watatu wanaodhaniwa kuwa ni majambazi  wameuwa kwa kupigwa risasi na polisi baada ya kukaidi amri ya kutakiwa kusimama eneo la kizuizi cha Mwembe Muhoro wilayani Rufiji, mkoani Pwani.

Watu hao walikuwa wamepakiana kwenye pikipiki moja huku wakiwa wamevaa hijabu.

Akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na tukio hilo, kamanda wa Polisi mkoani Pwani ,Onesmo Lyanga alisema pikipiki nyingine mbili zilifanikiwa kukimbia.

Akielezea juu ya tukio hilo alifafanua,lilitokea Aprili 2 mwaka huu majira ya mchana ,Muhoro ,Rufiji barabara kuu ya Dar es Salaam Lindi.

“Siku ya tukio askari walipata taarifa kuwa kulikuwa na pikipiki tatu zikitokea Kibiti kwenda mikoa ya Kusini zikiwa zimebeba watu watatu kila moja “

“Miongoni mwa pikipiki hizo kati yake mbili wamebebwa watu waliovaa hijabu,” alisema Lyanga.

Alisema askari wa barabarani walipewa taarifa katika kizuizi cha Mparange na kuwasimamisha ili wawahoji lakini walikataa na kupita ambapo waliwajulisha wenzao kwenye kizuizi cha Ikwiriri lakini walikaidi kusimama.

“Baada ya hapo walifika kizuizi cha Ikwiriri lakini bado walikaidi kusimama na kuendelea kukimbia ndipo walipofika kituo cha Muhoro “

“Hata hivyo hawakusimama na askari waliokuwa doria wakiwa kwenye gari waliwafuatilia na wakavuka daraja la Mkapa na waliwapa onyo kwa kupiga risasi hewani,” alisema Lyanga.

Aidha alibainisha baada ya hapo watu hao waliruka kwenye pikipiki na kuanza kukimbilia msituni na ndipo askari walipowapiga risasi za miguu na kiunoni na kufanikiwa kuwakamata.

“Majeruhi hao walijulikana ni wanaume hata hivyo majina yao hayakuweza kufahamika na walikuwa kwenye pikipiki yenye namba za usajili MC 272 BLW aina ya Boxer yenye rangi nyeusi”

“Watu hao wanaodhaniwa kuwa ni majambazi  kwa mwonekano wao walijaribu kuwawahisha hospitali ya Misheni ya Mchukwi,” alisema Lyanga.

Lyanga alisema walipofikishwa hospitali daktari alithibitisha kuwa watu hao wamefariki dunia .

Hata hivyo majina yao hayakuweza kufahamika huku pikipiki nyingine mbili zilitoroka na kuelekea mkoa wa Lindi na taarifa zimetolewa polisi ili wawakamate.

Aliwataka wananchi kuwa watulivu pale wanaposimamishwa na askari polisi badala ya kujaribu kutoroka na kwa sasa jeshi hilo limeimarisha doria katika kukabiliana na uhalifu.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumanne ya April 4

VIDEO: Swali la kwanza la Mbunge Salma Kikwete (Mke wa Rais Mstaafu ) bungeni Leo

$
0
0
Baada ya kuapishwa, Mbunge Salma Kikwete ameuliza swali kwa mara ya kwanza na kulielekeza OR-Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Mkutano wa saba wa bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania umeanza leo Dodoma. Leo asubuhi kabla ya kuanza kwa kipindi cha maswali na majibu mbunge wa kuteuliwa Mama Salma Kikwete aliapishwa

VIDEO: Wabunge Wakishangilia Baada ya Rais Mstaafu Jakaya Kikwete Kutambulishwa Leo Bungeni

$
0
0
Mkutano wa saba wa bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania umeanza leo Dodoma. Mkutano huu ni kwa ajili kupitisha bajeti ya Serikali itakayowasilishwa bungeni June 15 mwaka huu.

Hapa chini kuna video fupi ya Wabunge wakishangilia baada ya Spika Ndugai kutambulisha uwepo wa Rais Mstaafu, Dkt Jakaya Kikwete  bungeni.

Rais Magufuli afanya mabadiliko madogo katika safu ya Makatibu Wakuu wa Wizara.....Profesa Kitila Mkumbo Kateuliwa Kuwa Katibu Mkuu Wizara ya Maji na Umwagiliaji

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 04 Aprili, 2017 amefanya mabadiliko madogo katika safu ya Makatibu Wakuu.

Taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi imeeleza kuwa Mhe. Rais Magufuli amemteua Prof. Kitila Alexander Mkumbo kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji na Umwagiliaji.

Prof. Kitila Alexander Mkumbo anachukua nafasi ya Mhandisi Mbogo Futakamba ambaye amestaafu.

Kabla ya Uteuzi huu Prof. Kitila Alexander Mkumbo alikuwa Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM).

Mhe. Rais Magufuli amemteua Dkt. Leonard Akwilapo kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia.
Kabla ya Uteuzi huo Dkt. Leonard Akwilapo alikuwa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia.

Kufuatia uteuzi huo aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Bi. Maimuna Tarishi amehamishwa na kuwa Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Bunge).

Bi. Maimuna Tarishi anachukua nafasi iliyoachwa na Mussa Uledi ambaye uteuzi wake ulitenguliwa.

Mhe. Rais Magufuli amemteua Dkt. Ave Maria Semakafu kuwa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia ambako anajaza nafasi iliyoachwa na Dkt. Leonard Akwilapo ambaye ameteuliwa kuwa Katibu Mkuu wa Wizara hiyo.

Kabla ya Uteuzi huo Dkt. Ave Maria Semakafu alikuwa Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS).

Wateule hao wataapishwa kesho tarehe 05 Aprili, 2017 saa 3:00 Ikulu Jijini Dar es Salaam.

Kikwete: Ni zamu ya kumuunga mkono mke wangu

$
0
0
Baada ya kupokelewa kwa shangwe katika ukumbi wa bunge leo hii, Rais wa awamu ya nne, Jakaya Kikwete amesema ni zamu yake kwa sasa kumuunga mkono mkewe Mama Salma Kikwete.

Kikwete aliyekuwa ameambatana na familia yake, ameshuhudia mkewe akila kiapo cha ubunge katika kikao cha kwanza cha bunge lililoanza leo mjini Dodoma.

Salma Kikwete ambaye ni mwenyekiti wa WAMA, alionekana kuwa mstari wa mbele kumuunga mkono mumewe wakati wa utekelezaji wa majukumu yake ya kulitumikia taifa.

“Leo asubuhi nmeshuhudia kiapo cha mke wangu, mheshimiwa Salma Rashd Kikwete kuwa mbunge wa kuteuliwa bungeni Dodoma. Ni zamu yangu kumuunga mkono,”alinukuliwa Kikwete katika akaunti yake ya twiter.

Kikwete aliingia ndani ya bunge hilo huku akishangiliwa na idadi kubwa ya wabunge wa bunge hilo.

Polisi Dar watumia silaha kuwatawanya wafanyabiashara Mwenge

$
0
0
Jeshi la Polisi limetumia silaha za moto kuwatawanya wafanyabiashara katika eneo la Mwenge, wilayani Kinondoni leo.

Taharuki iliwakumba wakazi wa eneo hilo mara baada ya polisi hao kuanza kuwatanya wafanyabiashara hao waliofunga barabara wakishinikiza magari yaruhusiwe kupaki katika eneo hilo.

Inaelezwa kuwa polisi wamezuia watu  kupaki magari katika eneo hilo  hali iliyosababisha wafanyabiashara hao kutofungua biashara zao leo.

Mmoja wa wafanyabiashara na shuhuda wa tukio hilo, Musa Godwin alisema polisi walifika sokoni hapo saa12 asubuhi na kutawanya wafanyabiashara waliofunga barabara kuzuia polisi magari yasiegeshwe eneo hilo.

"Walifika hapa sokoni saa 12 asubuhi na baadhi ya watu walifunga njia ikasababisha polisi wapige risasi hewani, hadi sasa wanazunguka hapa kuzuia magari ambao ni wanunuaji wetu," alisema Godwin.

EWURA Yatangaza bei Mpya Za Mafuta........ Petroli Yashuka, Diseli Yapanda

$
0
0
Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) imetangaza mabadiliko ya bei za mafuta nchini zitakazoanza kutumika kuanzia kesho, huku mafuta ya petroli yakionekana kushuka.

Bei za jumla na rejareja kwa mafuta ya petroli, dizeli na ya taa zimebadilika ikilinganishwa na beo za Machi Mosi mwaka huu.

Akizungumza na waandishi wa Habari leo katika Makao Makuu ya ofisi za EWURA, Meneja Mawasiliano ma Uhusiano wa EWURA, Titus Kaguo amesema, bei ya reja reja ya petroli imepungua kwa Shilingi tatu kwa lita ambayo ni sawa na asilimia 0.13, pianbei ya jumla imepungua kwa Shilingi 5.65 kwa lita sawa na asilimia 0.29.

Aidha Kaguo amesema bei ya rejareja ya Dizeli imepanda kwa Shilingi saba kwa lita sawa na asilimia 0.36 wakati bei ya jumla ikiwa imepanda kwa Shilingi 3.68 kwa lita sawa asilimia 0.21.

"Hii shilingi tatu inaweza kuonekana ni ndogo lakini ina impact () kubwa sana kwa jamii, kwa kiasi kikubwa mabadiliko haya yametokana na mabadiliko ya bei za mafuta katika soko la dunia, mfumuko wa bei, pia gharama za usafirishaji ikilinganishwa na mwezi uliopita," amesema Kaguo.

==>Bei zota ziko hapo chini.....Tazama jedwali hili

EFM yakanusha kurusha habari ya Prof. Kitila Mkumbo kukataa uteuzi wa Rais Magufuli

Kitila Mkumbo Amshukuru Rais Magufuli Kwa Kumteua Kuwa Katibu Mkuu Wizara ya Maji na Umwagiliaji

$
0
0
Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Prof. Kitila Mkumbo amemshukuru Rais Magufuli kwa kumteua kuwa Katibu Mkuu Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo akichukua nafasi ya Mhandisi Mbogo Futakamba ambaye amestaafu.

Prof. Mkumbo ambaye pia ni kada na mshauri wa Chama cha ACT Wazalendo kinachoongozwa na Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe, amesema Rais amempa heshima kubwa kwa nafasi hiyo, na yeye kama mtumishi wa umma hawezi kuikataa kwa kuwa ni kazi aliyotumwa na mkuu wa nchi.

"Ukishapewa kazi na mkuu wa nchi, unaipokea na unaifanya kwa bidii kama yalivyo matarajio, kwahiyo nimepokea uteuzi, nimekubali, mkuu wa nchi akikupa kazi utaikataa vipi, mkuu wa nchi akikupa kazi unaifanya, kumbuka mimi ni mtumishi wa umma" Amesema Prof Kitila 

==>Msikilize hapo chini

Kauli ya ACT Wazalendo kuhusu Rais Magufuli kumteua Mwanachama wao , Prof. Kitila Mkumbo Kuwa Katibu Mkuu Wizara ya Maji na Umwagiliaji

$
0
0
Leo asubuhi Rais John Pombe Magufuli amemteua Mshauri wa Chama chetu Prof. Kitila Mkumbo kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji na Umwagiliaji. 

Chama cha ACT Wazalendo kimepokea kwa mikono miwili taarifa juu ya uteuzi wa mshauri wa chama chetu Kwa sababu imeonyesha kuwa Rais ameona kuwa hata Watanzania walio kwenye Vyama vya Upinzani wana uwezo, weledi na uzalendo wa kutumikia nchi yetu.

Kwa nafasi hii ya Ukatibu Mkuu wa Wizara, ndugu Kitila hawezi kuendelea kuwa Mshauri wa Chama nafasi ambayo inamfanya kuhudhuria vikao vyote vya Chama ikiwemo Kamati Kuu. 

Ndugu Mkumbo ameandika barua ya kujiuzulu nafasi yake ya mshauri wa Chama na kubaki kuwa mwanachama wa kawaida tu. Nimeipokea barua yake na kumkubalia Kwa maslahi mapana ya nchi yetu.

ACT Wazalendo tunamshukuru ndugu Kitila Mkumbo kwa mchango wake katika uongozi wa Chama chetu kwa wakati wote ambao alikitumikia Chama chetu kama mshauri wa chama. 

Msimamo wa chama chetu ni utumishi wa kizalendo kwa Taifa utokanao na kila mwananchi, ndio msingi wa kaulimbiu yetu ya ‘Taifa Kwanza, Leo na Kesho’, hivyo basi tunamtakia kila la kheri ndugu Kitila katika utumishi wake kwa Taifa letu katika nafasi yake hii mpya. 

Wizara Hii ni kubwa na muhimu Sana kwa nchi yetu. Maji ni tatizo moja kubwa ambalo wananchi wetu wanakumbana nalo na Kama Taifa hatujaweza kulimaliza. 

Tunamtakia kila la kheri ndugu Mkumbo katika kuongeza nguvu kumaliza kero ya maji na kuhakikisha tunaimarisha Kilimo cha Umwagiliaji nchi nzima. Tunamsihi aanze na ajenda ya Mfuko wa Maji Vijijini na kuanzishwa Kwa Wakala wa Maji Vijijini utakaosimamia upatikanaji wa Maji Kwa wananchi wetu.

Kwa hatua hii, tunaona Rais ameamua kuunganisha nchi yetu Kwa kufanya kazi na watu wote bila kuwabagua Kwa itikadi zao za vyama.

 Watanzania ni wamoja na kauli za kuwagawa zinaumiza zaidi Taifa kuliko kuliweka pamoja. Tunaamini kuwa Rais Ana nia njema katika uteuzi huu na sisi tumempa baraka zote Mwanachama wetu mwanzilishi wa Chama kwenda kwenye nafasi ya juu zaidi ya utumishi wa umma. Tunaamini hatamwangusha Rais na muhimu zaidi hatawaangusha Watanzania.

Kabwe Z. Ruyagwa Zitto
Kiongozi wa Chama – ACT Wazalendo
Aprili 4, 2017
Dodoma

TRA yatangaza kukusanya Tsh 10.87 trilioni kuanzia June 2016 mpaka March 2017

$
0
0
Mamlaka ya Mapato Tanzania imekusanya kodi ya jumla ya Sh. Trilioni 10.87 katika kipindi cha miezi tisa ya mwaka wa fedha 2016/17 ambapo makusanyo hayo ni sawa na ukuaji wa makusanyo ya asilimia 9.99

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi wa Elimu ya Mlipa Kodi, Richard Kayombo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari, amesema kuwa Mamlaka ya Mapato Tanzania inawashukuru walipakodi wote ambao wameitikia wito.

“TRA inatoa wito kwa kila mlipakodi kuwajibika kulipa kwa wakati pamoja na kufichua wale wasiotimiza wao kikamilifu,”amesema Kayombo.

Aidha, pamoja na mafanikio hayo kwa kipindi cha miezi tisa Mamlaka hiyo itaelekeza juhudi zake katika kukusanya kodi mbali mbali ili kuhakikisha lengo la mwaka la kukusanya Trilioni 15.1 linafikiwa.

Hata hivyo, amesema kuwa TRA inazidi kusisitiza matumizi mashine za EFD pamoja na zoezi la uhakiki wa TIN katika mikoa ya Arusha, Kilimanjaro, Dodoma, Mbeya, Morogoro, Tanga na Pwani linaendelea hivyo wananchi wanatakiwa kuhakikisha wanatumia mashine za EFD.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatano ya April 5

Ijue Sayansi ya Kusimama na Kusinyaa kwa UUme ( Sayansi ya Nguvu za Kiume)

$
0
0

Ukosefu  na/ama  upungufu wa  nguvu  za  kiume, ni tatizo linalo  wakabili  mamilioni  ya  wanaume duniani.

Tatizo  la  ukosefu/upungufu  wa  nguvu  za  kiume ni  nini  ?

Ukosefu  ama  upungufu  wa  nguvu za  kiume  ni  ile  hali  ya  mwanaume  kutokuwa  na  uwezo  wa kufanya  tendo  la  ndoa  kwa  ukamilifu

HATUA  MBILI  MUHIMU  KATIKA  KUSIMAMA  KWA  UUME
Ili  mwanaume   aweze  kufanya  tendo  la  ndoa  na  andelee  kufanya  tendo  la  ndoa, ni  lazima  uume wake  upitie  hatua  kuu  mbili  kama  ifuatavyo :

Hatua  ya  kwanza, ni  lazima  uume  wake  uweze  kusimama  barabara  na  kuwa  mgumu  kama  msumari.

Na  hatua  ya  pili  ni  lazima, uume  wake  uendelee  kusimama  kwa  muda  mrefu  wakati  wa  tendo  la  ndoa.  Hatua  zote  mbili  zinapo  kamilika, ndipo  tunapo  pata  kitu  kinaitwa STRONGER  AND  LONGER  ERECTION

JINSI  HATUA  ZA  KUSIMAMA  KWA  UUME  ZINAVYO  TOKEA.

1. HATUA   YA  KWANZA:

DAMU  KUTIRIRIKA  KWA  KASI KUINGIA  NDANI  YA  MISHIPA  YA  UUME  NA  KUUFANYA  UUME  KUSIMAMA  NA  KUWA  MGUMU.

Unapopata  wazo  la  kufanya  tendo  la  ndoa, mishipa  ya  fahamu iliyopo  kwenye  ubongo,  hupeleka  ishara  kwenye  mishipa  ya  uti  wa  mgongo, ambayo  nayo  hupeleka  taarifa  hadi  kwenye  mishipa  ya  uume. Taarifa  inapofika  kwenye  mishipa  ya  uume  huifanya  mishipa hiyo  ku-relax  na  hatimaye   kufanya  mishipa  ya  ateri  kufunguka  na  kutanuka. Mishipa  ya  ateri  inapo  tanuka  na  kufunguka, huruhusu  damu  kuingia  kwa  kasi  ndani  ya  mishipa  ya  uume  na  hivyo  kuufanya  huume  kusimama.

Ni  muhimu  kujua  kuwa, mishipa  ya  uume  inapo relax  hupelekea  kuisukuma na  hatimaye  kuiziba  mishipa  ya  vena  iliyo  karibu  na  mishipa  ya  uume  na  hivyo  kuiondolea  uwezo  wa  kunyonya  damu  iliyomo  ndani  ya  mishipa  ya  uume  na  kuipeleka  sehemu  nyingine  za  mwili.

N.B: Kazi  kubwa  ya  mishipa  ya  vena  ni  kunyonya  damu  iliyomo  ndani  ya  mishipa  ya  uume  na  kuipeleka  katika  sehemu  nyingine  za  mwili.  Au  kwa  lugha  nyingine  unaweza  kusema, kazi  kubwa  ya  mishipa  ya  vena  ni  kuhakikisha  hakuna  damu  kwenye  mishipa  ya  uume.
 
2. HATUA  YA  PILI  :
DAMU  KUENDELEA  KUHIFADHIWA  KATIKA  UUME  WAKATI  UUME  UKIWA  UMESIMAMA  NA  HIVYO  KUUFANYA  UUME  UENDELEE  KUDUMU  KATIKA TENDO LA NDOA   KWA  MUDA  MREFU.

Uume  ulio  simama, ili  uendelee  kusimama, ni  lazima  mishipa  ya  vena  isiwe  na  uwezo   wa  kunyonya  damu  kutoka  katika  mishipa  ya  uume  na  kuipeleka  katika  sehemu  nyinginezo  za  mwili. .

Mishipa  ya  Vena  ndio  inayo  husika  na  kunyonya  damu  kutoka  kwenye  mishipa  ya  uume na  kupeleka  sehemu  nyingine  za  mwili.  Ili  uume  uendelee  kusimama  lazima  mishipa  hii  ya  vena  iwe imezibwa. Ili  iweze  kuzibwa   ni  lazima  misuli  laini  ya  kwenye  uume  iwe - ime  relax na  hivyo  kuifanya  mishipa  ya  vena  kushindwa  ku  nyonya damu  kutoka  kwenye  uume.

Endapo  mishipa  ya  vena  itazibuka , basi  itanyonya  na  kutoa  damu yote  kutoka  kwenye  mishipa  ya  uume uliosimama  na  kuipeleka  sehemu  nyinginezo  za  mwili  na  hatimaye  uume  huo ulio simama  na  utasinyaa  mara  moja.

JINSI  UUME  UNAVYO  SIMAMA  NA  KUSISIMKA.
Tumeisha  zifahamu  hatua  mbili  muhimu  katika  kusimama  kwa  uume

Jinsi  Uume  unavyo  simama: Katika  uume  kuna chemba  yenye  mishipa  laini  sana, ambayo  ndio  huufanya  uume  kusimama.

Mishipa  hii  ipo kama  sponji  hivyo  huweza  kunyauka  na  kutanuka.

Damu  inapoingia  ndani  ya  mishipa  hii  huufanya  uume  kusimama  na  kuwa  mgumu  kama  msumari.

Damu  inapoendelea  kuhifadhiwa  ndani  ya  mishipa  hii  wakati  wa  tendo  la  ndoa, huufanya  uume  uendelee  kusimama.

Mwanaume  unapo  patwa  na  wazo la  kufanya  tendo  la  ndoa, mishipa  ya  fahamu  iliyo  kwenye  ubongo  hupeleka  ishara  kwenye  uti  wa mgongo, ambao  nao  hufikisha   taarifa  kwenye  mishipa  ya  uume.

Taarifa  ikisha  fika  kwenye  mishipa  ya  uume, huifanya  mishipa  ya  uume  ku-relax  na  mishipa  ya  uume  inapo  relax, hufanya  mambo  makuu  mawili;

i. Kwanza  hufanya  mishipa  ya  ateri  kufunguka na  hivyo  damu  kutiririka  kwa  kasi  sana  kuingia  kwenye  mishipa  ya  uume

( Mishipa  ya  ateri  ndio  inayo  tumika  kama  njia  ya  kuingiza  damu  kwenye  uume. Bila  mishipa  ya  ateri  imara  na  yenye  afya, damu  haiwezi kuingia  kwenye  mishipa  ya  uume, na  damu  isipoweza kuingia  kwenye  mishipa  ya  uume, basi  uume  hauwezi  kusimama )

ii.Pili huibana  mishipa  ya  vena  na  hivyo  kuizuia    kunyonya  damu  kutoka  kwenye  uume  na  kuipeleka  kwenye  sehemu nyingine  za  mwili. Matokeo  yake  kuufanya  uume  uendelee  kusimama  kwa  muda  mrefu  wakati  wa  tendo  la  ndoa.

Kumbuka ,kazi  kubwa  ya  mishipa  ya  neva  iliyo  karibu  na  mishipa ya  uume, ni kunyonya  damu kutoka  ndani  ya  mishipa  ya  uume  na  kuipeleka  kwenye  sehemu  nyingine  za  mwili. Kwa  lugha  nyingine, kazi  kubwa  ya  mishipa  ya  vena  ni  kuhakikisha  hakuna  damu  kwenye  mishipa  ya  uume ulio simama.

Kadri  damu  inavyo  zidi  kuingia  ndani  ya mishipa  ya  uume, ndivyo  uume  unavyo  zidi  kuwa  mgumu  na  kukakamaa.

Na  kadri  damu  inavyo  hifadhiwa  ndani  ya  mishipa  ya  uume, ndivyo  uume  unavyo endelea  kusimama  wakati  wa  tendo  la  ndoa kwa  muda mrefu.

Baada  ya  kumaliza  kufanya  tendo  la  ndoa,mishipa  ya  uume inarudi  katika  hali  yake  ya  kawaida (inanyauka ), ikisha  nyauka, mishipa  ya  ateri  inanyauka  pia, vena  zinafunguka  na  kunyonya  damu  katika  mishipa  ya  uume  na  kuirejesha  katika  sehemu nyinginezo  za  mwili  na  hatimaye  uume  kurudi  katika  hali  ya  kawaida  ( Flaccid ).

Hali  hii  itaendelea  kujirudia  kwa  kadri  utakavyo  kuwa  ukiendelea kufanya  tendo  la  ndoa.

Mambo  Muhimu  Katika  Kuufanya Uume  Usimame na  Kuendelea  kudumu  katika  kusimama  kwa  muda  mrefu wakati  wa  tendo  la  ndoa.

Ili  uume  uweze  kusimama  imara  kama  msumari na  uendelee  kusimama  imara  na  kwa  muda  mrefu  wakati  wa  tendo la  ndoa, ni  lazima  mambo  yafuatayo yawepo.

1. Mishipa ya   uume iliyo  imara  na  yenye  afya  njema.

2. Mfumo   mzuri  wa damu  katika   mwili  mzima.

3.Mtiririko  imara  wa  damu kuingia  na  kutoka  ndani  ya  mishipa  ya  uume.

4. Ushirikiano  wenye  afya  kati  ya  mishipa  ya  fahamu  ya  kwenye  ubongo  (nerves), mishipa  ya  kwenye  uti  wa  mgongo  pamoja  na  mishipa  ya  kwenye  uume.

Ili  mwanaume  aweze  kuwa  imara  katika  tendo  la  ndoa, ni  lazima  mambo  manne  niliyo yataja  hapo  juu  yawe  sawa  sawa  bila  hitilafu  yoyote. Kinyume  chake, mwanaume  hawezi  kuwa  na  nguvu  za  kiume.

MAMBO   YANAYO SABABISHA   UKOSEFU/UPUNGUFU  WA  NGUVU  ZA  KIUME.
Tumeshajua   nguvu za  kiume  ni  nini, jinsi  uume  unavyo  simama, hatua  za  kusimama  kwa  uume, pamoja  na  mambo  yanayo  fanya  uume  uweze  kusimama  na  kuwa  na  uwezo  wa  kuendelea  kusimama  wakati  wa  tendo  la  ndoa.

Ni  vyema  tukajua  mambo  yanayo  sababisha  kushindwa  kusimama  kwa  uume, mambo  yanayo  sababisha  uume  ushindwe kuendelea  kusimama  kwa  muda  mrefu  wakati  wa  tendo  la  ndoa   pamoja  na  mambo  yanayo  fanya  mtu  ashindwe  kurudia  tendo  la  ndoa.

Yafuatayo  ni  mambo  yanayo  sababisha  ukosefu wa  nguvu  za  kiume.

1. MAGONJWA  YANAYO  SHAMBULIA  MFUMO  WA  DAMU  PAMOJA  NA  MISHIPA  YA  DAMU.

Damu  ndio  nishati  inayo wezesha  kusimama  kwa  uume  na kuufanya  kuwa  mgumu na  imara  kama  msumari.

Damu  ndio  nishati  inayo weza   kuufanya  uume uendelee kusimama  wakati  wa  tendo  la  ndoa.

Damu  ndio  nishati  inayo  upa  uume  uimara  na  uwezo  wa  kurudia  tendo  la  ndoa  zaidi  ya  mara  moja.

Hivyo  basi  ili  uume  uweze  kuwa  imara na  wenye  nguvu, pamoja  na  kuwa  na  uwezo  wa  kumudu  na  kustahimili   tendo  la  ndoa  wakati  wowote , basi  ni  lazima   mwanaume  awe  na mfumo  imara  wa  damu  utakao  ruhusu  kutiririka  kwa  damu  kwenda  katika  sehemu mbalimbali  za  mwili  ikiwamo  uume.

Ili  mfumo  uweze  kuwa  imara  ni  lazima  mhusika  awe  na  damu  ya  kutosha, na  pili  awe  na  mishipa  ya  damu  yenye  afya.

Katika  mwili  wa  mwanadamu,kuna  mishipa  inayo  tumika  kusafirisha  damu  kutoka  katika  sehemu moja  ya  mwili kwenda  katika  sehemu  nyingine  ya  mwili  ikiwemo  uume. Mishipa  hiyo  ni  kama  vile  vena (veins), atery ( ateri) na  capillary  ( kapilari )

Mishipa  hii  ya  damu  inapaswa  kuwa  imara  na  yenye  afya  njema  wakati  wote.   Mishipa  hii  ikipatwa  na  hitilifu, basi  itazuia  kusafirishwa  kwa  damu  katika  sehemu  mbalimbali za  mwili  wa  mwanadamu  na  hatimaye  kufanya  suala  la  kuwa  na  nguvu  za  kiume  kwa  mhusika  kuwa  ugumu  kwa  sababu   ya  kushindwa  kupeleka  damu  kwenye  mishipa  ya  uume.

Magonjwa  kwenye  mishipa  ya  damu  huzuia   kutirika  kwa  damu kwenye  ogani  muhimu   kama  vile  moyo, ubongo na  figo.

VIASHIRIA  VYA  MAGONJWA  KWENYE  MISHIPA  YA  DAMU.
Utajuaje  kwamba  una  magonjwa  kwenye  mishipa  yako  ya  damu ?

Ukiwa  una  matatizo  yafuatayo ya  kiafya, ni  ishara  kwamba, una  magonjwa  kwenye  mishipa  yako  ya  damu:

1.  Kolestrol ( Ama  lehemu  kwenye  damu )
Kolestrol  nyingi  kwenye  damu, huzuia  kutiririka  kwa  damu. Kolestrol  ikizidi  kwenye  damu,  hupelekea  kuziba   mishipa  ya  ateri  ambayo  kazi  yake  ni  kupeleka  damu  kwenye  uume. Matokeo  yake  ni  mhusika  kutokuwa  na  uwezo  wa  kusimamisha  uume  wake barabara  kwa  sababu uume  hauwezi  kusimama  bila  damu  kuingia  ndani  ya  mishipa  ya  uume. 
 
 Hivyo  basi pamoja  na  dawa  ya  nguvu  za  kiume, yakupasa  kutibu  kolestrol. Unaweza  kuondoa  kolestrol  kwenye  damu  kwa  kutumia  dawa  mbali  za  asili  kama  vile mdalasini,uwatu, habbat sodah  etc.  Jinsi  ya  kujitibu  kolestrol  kwa  kutumia dawa asilia  tafadhali  tembelea


2.      Shinikizo  Kubwa  la  Damu
Shinikizo  Kuu la  Damu husababisha  mishipa  ya  ateri  ambayo  hutiririsha  damu  iingiayo  kwenye  uume  kuziba  na  kushindwa kutanuka  kwa  kiwango  inachotakiwa  kutanuka.

Pia  huifanya  mishipa  laini  katika  uume   kushindwa  ku-relax  na  hivyo  kushindwa  kuizuia  mishipa  ya  vena  ya  kunyonya  damu  kutoka  kwenye  mishipa  ya  uume  na  kuipeleka  kwenye  maeneo  mengineyo  ya  mwilini.

Matokeo  yake  kunakuwa hakuna  kiasi  cha  kutosha  cha  damu  iingiayo  kwenye  uume  na  hivyo  kufanya  uume  ushindwe  kusimama.

Vile  vile  hata  kiasi  kidogo  cha  damu  kinacho  ingia  kwenye  uume, kinashindwa  kuendelea  kuhifadhiwa  ndani  ya  uume  wakati uume  ukiwa  umesimama, na  matokeo yake  ni  uume  kusinyaa  ndani  ya  kipindi kifupi  sana  tangu  usimame.

Pamoja  na kutumia  dawa  ya  nguvu  za  kiume, unapaswa   pia  kutumia  dawa  asilia  kujitibu  tatizo  la  shinikizo  kuu  la  damu.

Kufahamu  jinsi  ya  kujitibu  tatizo  la shinikizo  la  damu  kwa  njia  ya  asilia, tembelea :


3.  Ugonjwa  wa  kisukari :
 Ugonjwa  wa  kisukari  ni  miongoni  mwa  vyanzo  vikuu  vya  tatizo  la  ukosefu wa  nguvu  za  kiume.  Kusimama  kwa  uume  kunategemeana  na  kutiririka  kwa  damu  mwilini. Kisukari  huathiri  mishipa  ya  damu pamoja  na  usambazaji  wa  damu  kwenye  ogani  muhimu  mwilini  kama  vile  moyo, ubongo, figo  na  uume.

Kiukweli, mwanaume  mwenye  kisukari  yupo  katika  risk  kubwa  ya  kupatwa  na  tatizo  la  ukosefu  wa  nguvu  za  kiume,m tena  katika  kiwango  kikubwa  sana.

Unashauriwa pamoja  na kutumia  dawa  ya  nguvu  za  kiume, tumia  pamoja  na  dawa  mbalimbali  za  asili  kwa  ajili  ya  kubalance  sukari  yako mwilini. 
 
Zipo  dawa  mbalimbali  za  asili  zinazo  saidia  kubalance  kiwango  cha  sukari  mwilini. Dwa  hizo  ni  pamoja na mdalasini, unga  wa  uwatu, mbegu  za  uwatu, manjano, majani  ya  manjano,mbegu  za  katani, nakadhalika. Namna  ya  kutumia  dawa  hizo  kujitibu  tatizo  la  sukari, tafadhali  tembelea :http://neemaherbalist.blogspot.com/2015/07/jitibu-kisukari-presha-shinikizo-la.html

4. Magonjwa  ya  figo
Tatizo  la  ugonjwa  wa  figo  huathiri  vitu vingi  ambavyo  ni  muhimu  sana  katika  kuufanya  uume  uweze  kusimama  na  kuendelea  kudumu  katika  kusimama.

Tatizo  la  figo, huathiri  homoni, huathiri kutiririka   kwa  damu  kwenda  kwenye  mishipa  ya  uume. Huathiri  mfumo  wa mishipa  ya  neva  pamoja  na  nishati  ya  mwili mzima.

Pamoja  na  dawa  ya  kutibu  tatizo  la  nguvu za  kiume, unapaswa  pia, kutibu  tatizo  la  figo. Kufahamu  jinsi  ya  kujitibu  magonjwa mbalimbali  ya  figo  kwa  kutumia  dawa mbalimbali  asilia, tembelea :http://neemaherbalist.blogspot.com/2015/07/jitibu-kisukari-presha-shinikizo-la.html

5.        Ugonjwa  wa  moyo
Moyo  ndio  supplier  mkubwa  wa  damu  katika  sehemu  mbalimbali  za  mwili.  Ugonjwa  wa  moyo  hupunguza  uwezo  wa  moyo  kusambaza  damu  kwenye  mishipa  mbalimbali  ya  damu  na  hivyo  kuathiri  utendaji  kazi  wa  mishipa ya  damu  kama  vile  ateri  na  vena. Matokeo  yake  ni  mishipa  hiyo  kushindwa  kupeleka  damu  ya  kutosha  katika  uume  pamoja  na  kushindwa  kuifanya  mishipa  ya  uume  kurelax na  matokeo  yake,. Ukosefu  wa nguvu  za  kiume. Hivyo  basi, pamoja  na  dawa  ya  nguvu  za  kiume, unapaswa  pia   kutibu  tatizo  la  moyo. Kufahamu  jinsi  unavyo  weza  kutibu ugonjwa  wa  moyo  kwa  dawa  asilia, tembelea :


6.  Kupwaya  kwa  mishipa  ya  vena.
Kazi  kubwa  ya  mishipa  ya  vena  kwenye  uume   kunyonya  damu  iliyomo  ndani  ya mishipa  ya  uume  na  kuipeleka  katika sehemu  nyingine  za  mwili.  Mishipa  ya  vena iliyopo  karibu  na  uume  kazi  yake  kubwa  ni kuhakikisha  hakuna  damu  yoyote  kwenye mishipa  ya  uume. ( KUMBUKA  KUWA  DAMU NDIO  HUFANYA  UUMU  USIMAME, HIVYO CHOCHOTE  KILE  KITAKACHO  FANYA  DAMU ISIKAE  NDANI  YA  MISHIPA  YA  UUME , KITAFANYA  UUME  USINYAE  )

Ili  uume  uendelee  kusimama  ni  lazima, mishipa  ya  vena  isiwe  na  uwezo  wa kunyonya  damu  kutoka  kwenye  mishipa  ya uume  kupeleka  nje  ya  mishipa  ya  uume.

Na  ili  mishipa  ya  vena  isiwe  na  uwezo  wa   kunyonya  damu  kutoka  kwenye   mishipa ya  uume  ulio  simama  na  kuipeleka  kwenye sehemu  nyingine  za  mwili,  ni  lazima mishipa  ya  uume  iwe  imara  na  thabiti  isiyo na  hitilafu  yoyote  ile.

Mishipa  ya  vena  ikipwaya, mwanaume hutokuwa  na  uwezo  wa  kusimamisha  uume wako, na  ikitokea  umefanikiwa kuusimamisha  basi  utasimama  ukiwa legelege  sana  na  utasinyaa  ndani  ya  muda mfupi  sana, kwa  sababu  damu  iliyo  ingia ndani  ya  uume  wako  na  kuufanya  usimame, itanyonywa  ndani  ya  muda  mfupi  sana  na kutolewa  nje  ya  mishipa  ya  uume  na  hivyo kuufanya  uume  wako  usimame.

 Tatizo  la  kupwaya  kwa  mishipa  ya  vena linasababishwa  na  kupiga  punyeto  kwa muda  mrefu  pamoja  na  ugonjwa  wa kisukari.

KUPIGA  PUNYETO  KWA  MUDA  MREFU: Kupiga  punyeto  kwa  muda  mrefu  ni  moja kati  ya  vyanzo  vikuu  vya  tatizo  la  la ukosefu  wa  nguvu  za  kiume.  Asilimia kubwa  ya  vijana  wenye  tatizo  la  ukosefu wa  nguvu  za  kiume, linasababishwa  na upigaji  wa  punyeto  kwa  muda  mrefu.

JINSI  PUNYETO  INAVYO  SABABISHA UKOSEFU  WA  NGUVU  ZA  KIUME.

Unapopiga  punyeto  unakuwa  unaiminya mishipa  ya  uume   ambayo  ndio  inaufanya uume  usimame.

Matokeo  yake  unaifanya  mishipa  hiyo  ilegee na  kutokuwa  na  uwezo  wa  kusimama  tena.

Mishipa  ya  uume  iliyo  legea  kutokana  na upigaji  punyeto, huleta  madhara  yafuatayo  :

i.           Huondoa  uwezo  wa  mishipa  ya  uume kurelax.

( Unapopata  wazo  la  kufanya  tendo  la ndoa, mishipa  ya  uume  ina relax  , mishipa  iki  relax  husababisha  mishipa ya  ateri  kupanuka  na  kuruhusu  damu kingie  ndani  ya  mishipa  ya  uume  na hatimaye  kuufanya  uume  usimame  na kuwa  mgumu)
 
ii.Mishipa   ya  kiume  ikishindwa  ku relax husababisha  mishipa  ya  ateri  kuziba

iii. Mishipa  ya  ateri  ikiziba, damu  haiwezi kutiririka  kuingia  kwenye  mishipa  ya uume, na  hata  ikitokea  damu  imeingia ndani  ya  mishipa  ya  uume  basi huingia  kiasi  kidogo sana   tena  kwa presha  ndogo  sana  hivyo  basi  hata kama  uume  utasimama   basi utasimama  ukiwa  legelege  sana

iv. Mishipa  ya  uume  ikishindwa  kurelax basi  haitakuwa  na  uwezo  wa  kuipush na  kuiziba  mishipa  ya  vena  ambayo ndio  hunyonya  damu  kutoka  kwenye mishipa  ya  uume  ulio  simama. 
 
Matokeo  yake  basi, damu  kidogo  iliyo ingia  ndani  ya  mishipa  ya  uume  na kuufanya  uume  kusimama, hunyonywa na  kutolewa  nje  ya  mishipa  ya  uume ndani  ya  sekunde  chache  sana  na hivyo  kuufanya  uume usinyae  ndani ya  muda  mfupi  sana.

v. Mishipa  ya  uume  kulegea

vi. Uume  kurudi ndani  na  kusinyaa  na kuwa  kama  uume  wa  mtoto

6. Tatizo  la  unene  kupita  kiasi : Tatizo  la unene  na  uzito  kupita  kiasi  ni  miongoni mwa  mambo  yanayo  sababisha  upungufu wa  nguvu  za  kiume. Unene  kupita  kiasi humuweka  mtu  katika  hatari  ya  kupatwa na  magonjwa  kama  vile  kisukari, presha, moyo  na  shinikizo  kuu  la  damu. 
 
Na magonjwa  ya  kisukari, moyo,presha  na shinikizo  la  damu  husababisha  upungufu na ukosefu  wa  nguvu  za  kiume, na  hivyo kumuweka  muhusika  katika  hatari  kuu  ya kupatwa  na  tatizo  la  ukosefu/upungufu  wa nguvu  za  kiume.

Hivyo  basi  kwa  wewe  mwenye  tatizo  la unene  na  uzito  kupita  kiasi , pamoja  na kutumia  tiba  ya  nguvu  za  kiume,  ni  vyema ukafanya  na  mpango  wa  kupunguza  unene na  uzito  wako.

JINSI  YA  KUPUNGUZA  UZITO  NA  UNENE KWA  KUTUMIA  TIBA  ASILIA, TAFADHALI TEMBELEA:


7.   Matatizo  Katika  mfumo  wa  Ubongo

Uume  hauwezi  kusimama   bila  ya  kuwa  na ushirikiano  na  ubongo.  Ili mtu  uume  uweze kusimama, mtu  lazima  apate  wazo  la kufanya  tendo  la  ndoa  (UBONGO  UNA HUSIKA  HAPO ), akishapata  wazo, ubungo hupeleka  ishara  kwenye  mishipa  ya  fahamu iliyopo  katika  uti  wa  mgongo  ambayo  nayo hupeleka  taarifa  kwenye  mishipa  ya  uume then  uume  usimama.   
 
Hivyo  basi  ili  mtu  aweze  kuwa  na uwezo  wa kusimamisha  uume  wake  ni lazima  kuwa  na  mawasiliano  mazuri  na  imara  kati  ya mishipa  ya  fahamu ( ubongo ), mishipa  ya  kwenye  uti  wa  mgongo   na  mishipa  ya  kwenye    uume.  Bila ushirikiano  kati  ya  vitu  hivyo  vitatu, uume hauwezi  kusimama.

Magonjwa  yanayoweza  kuathiri  ushirikiano  kati  ya  mishipa  ya  ubongo  na  mishipa  ya  uume, yanaweza  kusababisha  kushindwa  kusimama  kwa  uume.

Magonjwa  hayo  ni  pamoja  na  kiharusi,kupoteza  kumbukumbu  (  Alzheimer ), multiple  sclerosis pamoja  na  ugonjwa  wa  Parkinson.

Ni  vyema  mgonjwa  akatibiwa  kwanza magonjwa  hayo  kabla  ya  kuanza  kutumia dawa  ya  nguvu  za  kiume.  Kufahamu  jinsi ya  kujitibu  magonjwa  tajwa  hapo  juu  kwa njia  asilia,tafadhali  tembelea

Mambo   mengine  yanayo  sababisha  ukosefu na  upungufu  wa  nguvu  za  kiume, ni pamoja  na  maumivu & majeraha  kwenye  uti wa  mgongo,  chango  la  kiume , ngiri  na matatizo  katika  homoni.

 VIASHRIA  VYA  MTU  MWENYE  TATIZO  LA UKOSEFU/UPUNGUFU  WA  NGUVU  ZA KIUME.

Mtu  mwenye  tatizo  la  ukosefu  wa  nguvu  za kiume  huwa  na  dalili  zifuatazo ;

1. Kushindwa  kabisa  kusimamisha  uume wake

2. Uume  kusimama  ukiwa  legelege

3. Kuwahi  kumaliza  tendo  la  ndoa

4. Mwanaume  kutokuwa  na uwezo  wa kufanya  tendo  la  ndoa  katika  baadhi ya  staili  ( Mara  nyingi   mwanaume huyu huwa  na  uwezo  wa  kufanya tendo  la  ndoa    staili  moja  tu ).  Hapa mwanaume  anakuwa  na  uwezo  wa kufanya  tendo  la  ndoa  kwa  staili  ya   “ missionary” pekee.  Ikibadilishwa   staili, mwanaume  anakuwa hana  tena  uwezo wa  kusimamisha  uume  wake  japo katika  hali  ya  u lege  lege

5. Uume  kutokuwa  na  uwezo  wa kusimama  wenyewe   bila kushikwashikwa  ama  kutomaswa kwa muda  mrefu.

6. Uume  kusinyaa  ukiwa  ndani  ya mwanamke.

7. Uume  kusinyaa, pindi  inapotokea activity  yoyote  ya  kiungo  ama  ogani nyingine  ya  mwanaume  wakati  wa tendo  la  ndoa. Kwa  mfano, wakati  wa tendo  la  ndoa, ikitokea  mwanaume amekohoa  au  kupiga  chafya, uume  nao unasinyaa.

8. Uume  kusinyaa  mara  tu  baada  ya kutolewa  ndani  ya  uke ( Kwa  mfano kama  unafanya  tendo  la  ndoa, halafu uume  ukatoka  nje, kitendo  cha kuushika  kuurudisha ndani, tayari  una sinyaa )

9. Kutokuwa  na  uwezo  wa  kurudia  tendo la  ndoa.

10.  Kupatwa  na  maumivu  wakati  wa tendo  la  ndoa.

VIASHIRIA  VYA  MWANAUME  ASIYE  NA TATIZO  LA UKOSEFU  WA  NGUVU  ZA KIUME.

Mwanaume  asiye  na  tatizo  la  ukosefu  wa nguvu  za  kiume, huonyesha  ishara  zifuatazo ;

i.Uume  husimama  ukiwa  imara  kama msumari.

ii.Hukaa  kifuani  kwa  muda  mrefu  ( Wastani  ni  kati  ya  dakika  20  hadi  45 )

iii.Huweza  kurudia  tendo  la  ndoa  zaidi ya  mara  tatu  bila  misuli  ya  uume kuchoka.

iv.Huweza  kufanya  tendo  la  ndoa  kwa staili  yoyote  ile

v.Uume  husimama  wenyewe  bila kushikwa  shikwa  wala  kuwa stimulated  kwa  namna  yoyote  ile

vi.Kwa  ufupi  anakuwa  na  uwezo  wa kufanya na  kukamilisha  tendo  la  ndoa kwa  uukamilifu  mkubwa.

TIBA  ASILIA  YA  TATIZO  LA UKOSEFU/UPUNGUFU  WA  NGUVU  ZA KIUME.

Dawa  asilia  ya  JIKO   ni  dawa  asilia  inayo tibu  na  kuponyesha  kabisa  tatizo  la ukosefu  wa  nguvu  za  kiume.

                              MFUMO   WA  DAWA
Dozi  ya  dawa  ya  JIKO ni  mkusanyiko  wa dawa  nne  asilia  zenye  uwezo  mkubwa  sana katika kutibu  na  kuponyesha  kabisa  tatizo la  ukosefu/upungufu  wa  nguvu  za  kiume.

Dawa  hizi  zipo  katika  mfumo  wa  MIZIZI  na UNGA  UNGA.

JINSI   DOZI  YA  DAWA  YA  JIKO  INAVYO FANYA  KAZI.
Dozi  ya  dawa  ya  JIKO  inafanya  kazi zifuatazo  katika  mwili  wa  mwanadamu.

KAZI  INAYO  FANYWA  NA  DAWA  YA  JIKO .
Dawa  ya  JIKO  inasadia  katika  mambo makuu yafuatayo:
1.  Inasaidia   kuimarisha  mishipa  ya  uume  ulio legea  na  hivyo  kuufanya  uume  uwe  na uwezo  wa  kusimama  barabara  kama msumari  wakati  wa  tendo  la  ndoa.

2. Inasaidia  kusafisha  mishipa  ya  kwenye uume  na  hivyo  kusaidia  katika  kuongeza kasi  ya  msukumo  wa  damu  kwenye mishipa  ya  kwenye  uume.

3. Huongeza  damu  mwilini

4. Husaidia  kuongeza  msukumo (pressure)  wa damu  kwenye  mishipa  ya  uume  na  hivyo kuufanya  uume  kuwa  na  nguvu  za  ajabu.

5. Huipa  misuli  ya  uume  uwezo  wa  kuziba  wa kuizuia  mishipa  ya  vena   kunyonya  damu kwenye  mishipa  ya  uume  wakati  wa  tendo la  ndoa  na  matokeo  yake  kukupa  uwezo wa  kufanya  tendo  la  ndoa  kwa  muda  mrefu

               ( Kuzuia  hali  ya  kufika  kileleni haraka  )

6. Husaidia  kurelax  mind  na  hivyo  kumfanya mtu  awe  na  uwezo  wa  kuconcentrate  wakati wa  tendo la  ndoa   bila  kuathiriwa  na msongo  wa  mawazo

7.  Hurejesha, kuimarisha  na  kuboresha ushirikiano  kati  ya  mishipa  ya  fahamu  ya  kwenye  ubongo  (nerves), mishipa  ya  kwenye  uti  wa  mgongo  pamoja  na  mishipa  ya  kwenye  uume
8. Humfanya  mwanaume  awe  na  uwezo  wa kurudia  tendo  la  ndoa  mara  nyingi  zaidi bila  kuchoka.
9. Husaidia  kuongeza  hamu  ya  tendo  la  ndoa.10. Husaidia  kuurudisha  nje  uume  ulio ingia ndani.
11. Husaidia  kutibu  side effects  za  punyeto na  matumizi  ya  muda  mrefu  ya dawa  kali za  (za  kizungu ) za  kuongeza  nguvu  za kiume.

12. Husaidia  kutibu  chango  la  kiume.

13.Dawa  hii  huwasaidia  hata  wanawake wanao sumbuliwa  na  tatizo  la  ukosefu  wa hamu ya  tendo  la  ndoa.

BEI  YA  DAWA:  Dozi  ya  dawa  ya  JIKO inapatikana  kwa  gharama  ya  SHILINGI ELFU  THEMANINI  TU  (Tshs.80,000/=)

MAHALI  TUNAPOPATIKANA :
Dozi  ya  dawa  ya  JIKO, inatolewa  na  duka  la dawa  asilia  la  NEEMA 

HERBALIST  &   NUTRITIONAL  FOODS  CLINIC. Tunapatikana jijini  DAR ES  SALAAM, katika  eneo  la UBUNGO     karibu  na  SHULE  YA MSINGI  UNGUNGO  NATIONAL  HOUSING  NYUMA  YA  JENGO  LA  UBUNGO  PLAZA.

Kwa  wasio  weza  kufika  ofisini  kwetu, tunatoa huduma  ya kuwapelekea  dawa  mahali  walipo ( DELIVERY )

Kwa  wateja  waliopo  nje  ya  DAR  ES  SALAAM, watatumiwa  dawa  kwa  njia  ya  mabasi, wateja  waliopo  Zanzibar, watatumiwa  dawa kwa   njia  ya  boti  na  kwa  wateja  waliopo Ulaya, America  na  Arabuni, watatumiwa dawa  kwa  njia  ya  DHL  au POSTA.

WASILIANA  NASI  KWA  SIMU  NAMBA

0766  53  83  84.
Na  kwa  maelezo  zaidi  kuhusu  huduma  zetu, endelea  kutembelea:

Matokeo ya uchaguzi wa Wabunge wa Bunge la Afrika Mashariki......Wabunge Wote wa CHADEMA Wapingwa

$
0
0
Jana Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania lilipiga kura kuchagua wabunge watakaoiwakilisha nchi katika Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki (EALA) kwa kipindi cha miaka mitano.

Baada ya mvutano wa muda mrefu kuhusu uchaguzi huo, ulifanyika na Spika wa Bunge, Job Ndugai kutangaza orodha ya washindi waliochaguliwa kuiwakilisha nchi.

Tanzania inatakiwa kutoa wabunge 9 kwenda EALA, lakini matokeo ya jana yalitangaza washindi saba tu baada ya wagombea wawili kupigiwa kura nyingi za hapana, na hivyo kuonekana kuwa wabunge hawakuwataka.

Kati ya wabunge 7 waliotangazwa, 6 ni wa Chama cha Mapinduzi (CCM) na mmoja na wa Chama cha Wananchi (CUF).

Wagombea wa CHADEMA, Lawrence Masha na Ezekiah Wenje walipingwa kwa kupigiwa kura nyingi za hapana.
  1.      Fancy Nkuhi (CCM)
  2.     Happiness Legiko (CCM)
  3.     Maryam Ussi Yahya (CCM)
  4.     Dkt Abdullah Makame (CCM)
  5.     Dkt Ngwaru Maghembe (CCM)
  6.     Alhaj Adam Kimbisa (CCM)
  7.     Habib Mnyaa (CUF)
Baada ya matokeo hayo kutangazwa, Mwenyekiti wa CHADEMA na Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe akizungumza na waandishi wa habari nje ya ukumbi wa Bunge alisema kuwa, hawayakubali matokeo hayo na kuwa watakwenda mahakamani.

Mbowe pia amemtuhumu Rais Dkt Magufuli na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa kuhusika katika mchakato wa kuwakataa wagombea wa CHADEMA na kusema kuwa, wao hawatakubaliana na hilo kwa sababu Spika wa Bunge amekiuka kanuni za bunge, na uchaguzi wote ulikuwa na kasoro.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images