Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Mahakama Kuu Yamwamuru Msajili wa Vyama vya Siasa kutotoa ruzuku kwa Prof. Lipumba na kundi lake mpaka shauri litakapoamuliw

0
0
Mahakama Kuu imemuamuru Msajili wa Vyama vya Siasa nchini kutotoa ruzuku kwa Prof. Ibrahim Lipumba wa Chama cha Wananchi, CUF, na kundi lake.

Zuio hilo ni mpaka shauri dhidi ya Msajili na Mwanasheria Mkuu wa Serikali kuhusu kutoa fedha za ruzuku shilingi milioni 369 kwa njia za wizi na udanganyifu litakaposikilizwa na kutolewa maamuzi.

Uamuzi huo umefikiwa na Jaji Dyansobela baada ya kukubaliana na hoja zilizowasilishwa kwa hati ya dharura.

Jopo la Mawakili wa CUF, liliiomba Mahakama Kuu kutoa amri hiyo kwa kuwa fedha zilizotolewa awali shilingi milioni 369 hazijulikani zimetumika vipi, na hazikuwa katika mikono salama wala hakuna udhibiti wowote wa chama kuhusu fedha hizo ikizingatiwa kwamba, Prof. Lipumba alishavuliwa uanachama.

Mawakili hao akiwemo Juma Nassor , wamesisitiza kwamba, mazingira yaliyopo ni vyema na busara kwa fedha za umma zilizopaswa kutolewa kama ruzuku kwa chama cha CUF kwa sasa ziendelee kubakia serikalini.

Aidha, wameiomba Mahakama Kuu kwamba amri hiyo pia ifungamane na kesi ya msingi namba 23/2016 ya kuhoji maamuzi ya msajili kumtambua Prof Lipumba kwa nafasi ya uenyekiti iliyopo mbele ya Jaji Kihijo ambayo kwa sasa imekatiwa rufani ya kufanyiwa marejeo mbele ya Mahakama ya Rufani Tanzania.

Meneja wa Diamond Platinumz, Babu Tale na Erick Shigongo Ndani ya Bifu Zito

0
0
Mgogoro ulioanza kufukuta kwenye mitandao ya kijamii kati ya mmiliki wa makampuni ya Global Publishers, Erick Shigongo na meneja wa Diamond Platinumz, Babu Tale umechukua sura mpya  baada ya meneja huyo kudai ametishiwa.

Mtafaruku kati ya wawili hao ulianza baada ya Shigongo kuandika katika ukurasa wake wa Instagram ushauri wake kwa Diamond akidai kuwa kitendo cha kujikita katika matamasha ya kimataifa na kuyaweka kando ya ndani huku akitaka kulipwa zaidi ya shilingi milioni 100 pia ndani ya nchi kutamgharimu hususan kupoteza mashabiki wa ndani siku za usoni.

Akifunguka jana kupitia ‘Shilawadu’ ya Clouds TV, Babu Tale ambaye alimtaja Shigongo kuwa ni mtani wake kikabila, alimlalamikia kwa kudai kuwa alimpigia simu na kumweleza maneno ambayo aliyatafsiri kama vitisho.

Alidai kuwa baada ya kumpigia simu na mwandishi huyo nguli wa vitabu vya uhamasishaji wa kiuchumi na masimulizi alimuuliza ‘kama anataka vita’ kati yao baada ya maelezo.

“Nikipata matatizo leo,  ina maana aliyeniambia ‘ninataka vita’ ina maana amenisababishia matatizo. Lakini sitaishia hapa nitafuata vyombo vya sheria ili vinilinde,” alisema Babu Tale.

Meneja huyo wa WCB alionesha kushangazwa na kitendo cha Shigongo kumshauri Diamond kupitia Instagram, akidai kuwa kama angekuwa na nia njema kweli angemuita na kumshauri hata akiwa ofisini kwake.

Tale alienda mbali na kueleza kuwa Shigongo anampango wa kumuangusha katika biashara zake baada ya wawili hao kushindwana katika mambo yao ya kibiashara. Alimlaumu Shigongo pia kwa kuweka hadharani ujumbe aliomtumia kwenye simu.

Bado haijajulikana uhalisia wa chanzo cha mgogoro huo, lakini dalili zote zinaonesha huenda kukawa na msuguano wa kibiashara au kutoelewana katika hoja dhidi ya Diamond Platinumz ambaye ni bidhaa kubwa Afrika iliyo kwenye mikono ya Babu Tale na Salaam.

UVCCM yavishukia vyama vya upinzani Kwa Ubinafsi na Udikteta

0
0
Tunawashukurukwa kupokea wito wetu na kuja, karibuni sana tunawaahidi kwamba tutaendelea kushirikiana nanyi katika kila hatua.

Aidha Umoja wa Vijana wa CCM unavipongeza sana vyombo vyote vya habari nchini kwa juhudi zenu za kuhabarisha, kuelimisha, kuwaasa, kuwaelekeza na kuihabarisha jamiii katika masuala kadhaa yanayohusiana na mipango ya maendeleo, mikakati, sera na malengo ya Serikali na mipango ya vyama vya siasa.

Ndugu Waandishi wa habari.

Tumewaita leo kuzungumzia mambo 2 makubwa, na suala zima la mtikisiko wa demokrasia katika mchakato wa uteuzi wa wagombea Ubunge katika Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) ulivyoendeshwa ndani ya vyama vya upinzani nchini.

Bunge la Afrika Mashariki kama mjuavyo ni chombo kikubwa na chenye heshima ya pekee katika kanda yetu. Kuwepo kwake kunaashiria muendelezo wa kufufua dhana, dhamira, mikakati, fikra na malengo ambayo yaliasisiwa na waasisi wa Mataifa yote yaliyomo katika Kanda yetu ili hatimaye siku moja ishuhudiwe Kanda hii na Bara zima la Afrika likiunda dola moja.

Ni jambo la heri na faraja kuona EAC ya sasa ikiwa ni yenye kufikia malengo ya utengamano na mafanikio hususan katika nyanja za kiuchumi na kiusalama kama vile kuwa na Pasi moja ya kusafria, miingiliano ya wananchi wake katika ufanyaji wa biashara pia mkakati kuelekea kupata viwango sawia vya ushuru wa Forodha.

Masuala mengine ni kuona maeneo ya mipaka yetu kukiendelea kuwa na ustawi wa hali ya utulivu na usalama, wakati huo EAC ikifanya kila linalowezekana kumaliza migogoro yake ya kisiasa ambapo mazungumzo ya upatanishi huko Burundi yamekuwa yakiendelea chini ya mpatanishi mkuu Rais mstaafu Benjamin Mkapa sambamba na wananchi wa pande zote za nchi wanachama tukishuhudia wakiishi kwa maelewano, umoja, udugu na mafahamiano.

Ni katika jumla ya mambo yanayofurahisha na pengine yakiwasuta na kuwaaibisha maadui na vibaraka ambao aghalab hutumiwa kwa malipo yenye ujira wa dhambi toka kwa mabeberu katika kuhakikisha mipango batili ya kutaka kudhoofisha, kuigawa na kukwamisha juhudi za EAC isiimarike..

Aidha kuibuliwa na kupokewa kwa mpango uitwao ” One Stop Boarder” yaani (OSB) sasa umefanikiwa huko mipakani baina ya nchi wanachama. Pia kuanzishwa miradi mikubwa ya kiuchumi mfano bomba la mafuta toka Kampala (Uganda) hadi Tanga (Tanzania) ujenzi wa reli toka kigali hadi Uganda huku EAC ikielekea kuwa na sarafu moja kabla ya kufikiwa azimio la uundwaji wa Shirikisho moja.

Umoja wa Vijana wa CCM tumelazimika kuyataja na kuyaainisha maeneo hayo yaliopata mafanikio kwa uchache lengo likiwa ni kuonyesha uwepo na ustawi wa EAC pamoja na umuhimu wa bunge lake kama ni jambo nyeti na wala si suala dogo au la mchezo mchezo kama ambavyo baadhi ya vyama vya siasa nchini vimeonyesha udhaifu.

Ndugu Waandishi wa Habari,

Baadhi ya vyama vya siasa nchini vimeshindwa hata kuteua wagombea ubunge wengi ili kuwania nafasi katika bunge hilo la Jumuiya ya Afrika Mashariki kwa sababu zinazotokana aidha na ubinafsi, umimi na udikteta.

Tunachukua fursa hii kwanza kukipongeza Chama Cha Mapinduzi na wanachama wake wote 450 ambao kwa ujasiri, uwezo na kujiamini kwao wamethubutu kujitokeza na kuchukua fomu za kuwania nafasi za ubunge wa EAC.

Kitendo cha wanachama hao wa CCM kujitokeza kwa wingi kimsingi kimeidhihirishia dunia kwamba chama chetu bado ni cha kidemokrasia kinachoungwa mkono na kuaminiwa na wananchi wengi wakiwemo Vijana, wanawake na wana taaluma mbali mbali wakitambua ndicho chama pekee imara chenye kujali, kuthamini na kufuata misingi ya usawa na demokrasia ya kweli.

Wanachama 450 wa CCM walichukua fomu kwa kufuata taratibu baada ya mchujo wa kidemokrasia kufanyika ndani ya CCM, wanachama 12 wamebahatika kuteuliwa na vikao vya kikatiba ambapo sasa wagombea hao watasimama mbele ya wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kusaka ridhaa kwa kujieleza na kuomba kura.

Ndugu Waandishi wa habari,

Umoja wa Vijana CCM kwa tunasikitishwa sana na mwenendo wa demokrasia ndani ya vyama vya upinzani katika uteuzi wa kuwapata wagombea wa ubunge wa bunge la Afrika Mashariki (EALA) Chadema, CUF na NCCR Mageuzi kwa jinsi walivyowasilisha uwakilishi haba na finyu lakini pia kujitokeza kwa wagombea wachache hali inayoonyesha uminyaji wa demokrasia ndani ya vyama vyao.

Chadema na washirika wao mara kadhaa hujigamba vichochoroni na kujionyesha kuwa wao ni watetezi wa demokrasia lakini unapofikia wakati wa utekelezaji wa jambo hilo kwa vitendo, ndani ya chama hicho humea ukandamizaji wa haki na kujitokeza upendeleo, ukanda, kubebana aidha kwa asili, ujamaa na urafiki au kulipana fadhila.

Katu huu si mwenendo mwema ulioonyeshwa na vyama vya upinzani. Vimejipaka matope ya fedheha kwa kushindwa kuonyesha kama ni waumini wa kweli wa demokrasia badala yake havikujali wala kuheshimu dhana ya demokrasia na kujikuta vimejianika na kuuthibitishia umma wa watanzania kuwa vyama hivyo ni vya watu maalum vya kibwanyenye na vya kiimla .

Kufanya uteuzi wa wanachama wanaogombea nafasi za kidemokrasia kwa kumtazama asili yake, anatoka kanda ipi, kabila, imani yake au nasaba licha ya kwenda kinyume na misingi ya Taifa letu lakini pia ni kinyume na matakwa ya katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

UVCCM kwa kauli moja tunawaamsha na kuwatumia ujumbe watanzania wenzetu hususan Vijana mahali popote walipo wavikatae na kuvikwepa vyama vya aina hiyo, wasikubali kugawanywa kwa asili zao, imani au rangi na nasaba.

Taifa letu ni alama pana ya kuenzi na kudumisha demokrasia si tu barani Afrika lakini vile vile duniani kote, hivyo kwa umoja wetu, kwa nguvu zetu, akili na maarifa tulionayo, abadan tusijaribu kuichezea amani yetu, umoja na mshikamano wetu uliojengwa na waasisi wa Taifa letu na kukubali kuvishabikia vyama na viongozi wasaka madaraka kwa hila ambao ni wafujaji na wakandamizaji wa misingi ya demokrasia ndani ya vyama kama ilivyojionyesha kwa vyama vya upinzani vya Tanzania katika uteuzi wa wabunge EAC.

Mchakato wa Uchaguzi ndani ya UVCCM.

Uchaguzi Mkuu wa CCM wa mwaka 2017, unafanyika wakati ambapo CCM inatimiza miaka 40 tokea kuasisiwa kwake tarehe 5 Februari, 1977 na ni wakati ambapo nchi yetu inatimiza miaka 25 ya Mfumo wa Vyama Vingi ulioridhiwa na Mkutano Mkuu wa CCM kutokana na busara za Viongozi wake.

Ratiba ya Uchaguzi Mkuu wa Chama na Jumuiya zake inaonesha mchakato wa Uchaguzi wa Jumuiya za CCM kuwa unaanza kabla ya ule wa CCM. Utaratibu huu unalenga kuwawezesha wanachama wa Jumuiya za CCM ambao watakuwa ni wagombea wa nafasi mbalimbali za uongozi katika CCM, au wale waliochaguliwa kuwakilisha Jumuiya zao katika Vikao vya CCM ili waweze kuhudhuria mikutano ya Chama inayowahusu.

Umoja wa Vijana wa CCM umekamilisha maandalizi yote ya msingi ya awali kwa ajili ya Uchaguzi unaotarajia kuanza tarehe 1 April, 2017 ikiwemo kusambaza vifaa katika Mikoa na Wilaya zote nchini wa ajili ya kufanikisha uchaguzi kwa wakati.

Aidha Sekretarieti ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama Cha Mapinduzi imekamilisha mapitio na uteuzi wa Makatibu wa Mikoa na Wilaya katika Jumuiya ambao watakuwa ndio wakurugenzi wa Uchaguzi katika maeneo yao.

Tunaendelea kuwakumbusha Watendaji wetu muda wote kusimamia haki, ukweli na usawa lazima vijana wa CCM muda wote tuishi katika maneno na maagizo ya Mwenyekiti wetu wa CCM Dkt. John Pombe Magufuli.

Hatutamvumilia mtendaji yeyote atakayekiuka Kanuni, Taratibu na miongozo kwa makusudi ili kufurahisha kikundi au watu fulani. Uchaguzi huu 2017 UVCCM tunataka kuidhihirishia dunia na Vyama vya Upinzani kuwa CCM ni Chuo Cha Demokrasia ulimwenguni.

Mwisho niendelee kuwahamasisha vyema wote nchini yenye sifa kujitokeza kwa wingi kugombea nafasi mbali za uongozi ndani ya CCM na Jumuiya zake kuanzia ngazi ya Shina, Tawi, Kata, Wilaya, Mikoa na Taifa.

KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI
Shaka Hamdu Shaka (MNEC)

KAIMU KATIBU MKUU

Zitto Kabwe, CHADEMA Watofautiana Tena

0
0
Ikiwa ni takribani miaka mitano tangu Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe, avurugane na Chadema ambacho kilikuwa chama chake, sasa hali hiyo inaonekana kurudi tena kupitia uchaguzi wa ubunge wa Afrika Mashariki (EALA).

Tofauti na awali ambapo alikosana na Chadema na kufukuzwa uanachama kutokana na kile kilichodaiwa ni kuandaa waraka wa mabadiliko ya 2013, sasa hivi ubunge wa EALA unaonekana kumvuruga tena mwanasiasa huyo na Chadema, baada ya kuandika barua kwa Spika wa Bunge akitaka utaratibu uliotangazwa wa namna ya kupata wabunge ubadilishwe.

Utaratibu huo mpya uliotangazwa, unatoa nafasi kwa wabunge wa EALA kwa mwaka 2017 kulingana na idadi ya wabunge wa kila chama kwenye Bunge la Jamhuri ya Muungano.

Kwa mujibu wa Mwongozo huo, kutokana na idadi ya wabunge wa vyama kwa kila chama, CCM imepata nafasi za wabunge sita kwenda EALA, Chadema mbili, CUF moja, huku ACT Wazalendo  pamoja na NCCR Mageuzi, vikiwa havina nafasi hata moja kwenye Bunge hilo la Afrika Mashariki, kutokana na kuwa na mbunge mmoja kila kimoja, hivyo kutokidhi vigezo.

Kutokana na hali hiyo, Zitto ameliandikia Bunge barua kutaka Kamati ya Kanuni za Bunge ikutane kujadili uchaguzi wa wajumbe wa Tanzania kwenye Bunge la Afrika Mashariki.

Barua hiyo, ambayo baadhi ya wachambuzi wa siasa wanadai inalenga kutaka utaratibu wa awali ubadilishwe ili chama cha Zitto (ACT Wazalendo), kimwingize mwanachama wake, Profesa Kitila Mkumbo kugombea ubunge huo, inasema mwongozo uliotolewa na Bunge umekwenda kinyume cha Mkataba wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Wanasema endapo hoja ya Zitto ikikubaliwa, ni rahisi zaidi wagombea wa Chadema wakakosa nafasi hizo na badala yake nafasi za upinzani kuiwakilisha Tanzania kwenye Bunge la Afrika Mashariki zikachukuliwa na wagombea wa ACT na wale wa CUF.

Hali hiyo inaelezwa kuchangiwa na wabunge wengi kwenye Bunge la Jamhuri wa Muungano wa Tanzania kuwa ni wa CCM, hivyo ni rahisi kuweka msimamo wa kuwapigia kura wale wagombea wa ACT Wazalendo na wale wa CUF, badala ya wale wa Chadema kutokana na hali ya kisiasa iliyopo nchini kwa sasa.

Barua ya Zitto ya Machi 28 iliyoandikwa kutokana na Tangazo la Bunge kwenye gazeti namba 11 la Machi 17, lililotangaza uchaguzi huo na masharti yake, ilisema mwongozo wa uchaguzi huo unavunja kanuni mbalimbali na kwamba kitakachofanyika sasa kitakuwa ni uteuzi na siyo uchaguzi.

Alisema pia mwongozo huo, mbali na kuvunja Mkataba wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, unataka suala la jinsi lizingatiwe kwenye wabunge wanaokwenda kuiwakilisha nchi katika Bunge hilo.

Baada ya Zitto kuandika malalamiko hayo, Mwanasheria wa Chadema, John Malya, naye aliyajibu akirejea hukumu mbili za kesi ya Anthon Komu (kwenye Divisheni ya Mwanzo na Divisheni ya Rufani).

Malya aliandika kwamba, mwongozo wa Ofisi ya Spika wa Bunge wa kugawa idadi ya viti kwa vyama ni sahihi, kwa sababu Divisheni zote mbili za Mahakama ya Haki ya Afrika Mashariki ziliamua.

Katika sehemu ya barua yake, alisema: “Mwenye kupaswa kubeba mzigo wa makundi ya Zanzibar, Bara na Wanawake (ukiachilia mbali kundi la vyama vya upinzani) ni chama chenye wabunge wengi (CCM)”.

Hoja hiyo ya Malya inachambuliwa na Ado Shaibu, ambaye aliandika ujumbe unaogusa hoja za kisheria ambazo alitumia Malya kukosoa malalamiko ya Zitto.

Shaibu alisema ni kosa kutumia kesi ya Antony Komu ambayo iliamuliwa na Divisheni ya Mwanzo ya Mahakama ya Afrika Mashariki, lakini baadaye Divisheni ya Rufani ya Mahakama ya Haki ya Afrika Mashariki ikatengua hukumu hiyo kwa hoja ya kwamba Divisheni ya Mwanzo ya Mahakama haikuwa na mamlaka ya kuamua suala husika.

Kairuki: Serikali Haitamvumilia Mtumishi Mwenye Cheti Feki

0
0
Inakadiliwa kuwa watumishi 4,300 wapya wanataajiriwa kuajiriwa katika kada ya elimu na wasanifu wa maabara ambapo ajira hizo mpya zinakuja bada ya kukamilika kwa zoezi zima la kuhakiki watumishi hewa.

Hayo yamebainishwa mkoani Tabora na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma Mh. Angela Kairuki, wakati akizungumza na watumishi na wanachuo, ambapo amesema kuwa, kwa muda mwingi taifa limekuwa likikabiliwa na changamoto ya watumishi hewa huku likipoteza fedha nyingi.

Aidha Mhe. Kairuki amesema kuwa kamwe serikali haitamvumilia mtumishi ambaye atabainika kuwa na vyeti feki, huku akiwataka watanzania kutambua madhara ya vyeti hivyo kuwa ni kutopatikana kwa huduma stahiki huku akiwataka wahitimu katika kada mbali mbali kutowaonea haya watu ambao wanataka kupora ajira za wenzao.

Rais Magufuli aiapisha kamati kuchunguza mchanga unaoshikiliwa kwenye makontena

0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 01 Aprili, 2017 amewaapisha wajumbe wa kamati maalum ya kuchunguza kiwango na aina ya madini yaliyomo kwenye mchanga wenye madini ulio ndani ya makontena yaliyopo katika maeneo mbalimbali hapa nchini.
 
Hafla ya kiapo kwa wajumbe wa kamati hiyo imefanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wakiwemo Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe. George Mcheche Masaju, Katibu Mkuu Kiongozi Mhe. Balozi John Kijazi, Kamishna wa Maadili Mhe. Jaji Harold Nsekela na viongozi wa vyombo vya ulinzi na usalama.
 
Kamati hiyo ya wanasayansi 8 walioteuliwa na Mhe. Rais Magufuli tarehe 29 Machi, 2017 inaongozwa na Mwenyekiti wake Prof. Abdulkarim Hamis Mruma na itafanya kazi ya uchunguzi kwa siku 20 kisha kuwasilisha ripoti yake kwa Mhe. Rais.
 
Akizungumza baada ya kuwaapisha, Mhe. Rais Magufuli amesema ameamua kuunda kamati hiyo yenye wasomi waliobobea katika masuala ya jiolojia, kemikali na uchambuzi wa kisayansi ili wawawakilishe Watanzania zaidi ya Milioni 50 ambao wanataka kujua ukweli kuhusu rasilimali yao ya madini.
 
“Hivi sasa duniani kuna vita nyingi na vita mojawapo ni vita ya uchumi, kwa hiyo tunawatuma nyinyi mwende mkapigane vita hii katika sekta hii ya madini, mkawawakilishe Watanzania zaidi ya Milioni 50, mkapate ukweli wote na wala msikubali kuyumbishwa na mtu yeyote, tumieni utaalamu wenu, busara zenu, uzalendo wenu kwa Taifa na upendo wenu kwa Watanzania hasa masikini wenye shida nyingi” amesema Mhe. Rais Magufuli.
 
Mhe. Dkt. Magufuli amewahakikishia kuwa Serikali itatoa kila aina ya ushirikiano kufanikisha kazi hiyo na ametaka wawe huru kutumia vitendea kazi vyovyote vinavyohitajika zikiwemo maabara mbalimbali za taasisi za Serikali na nyinginezo.
 
“Nendeni popote mnapohitaji kufanya kazi tutawapa ushirikiano, fungueni makontena popote yalipo, chukueni sampuli na mkazipime mjue kilichomo na naviagiza vyombo vya dola vihakikishe hakuna mtu atakayewakwamisha” amesisitiza Mhe. Rais Magufuli
 
Aidha, Mhe. Dkt. Magufuli amesema baada ya kuunda kamati hii ya wanasayansi ataunda kamati nyingine ya wachumi na wanasheria kwa ajili ya kufanya tathmini na kuiangalia sera na sheria ya madini kwa lengo la kupata taarifa zaidi juu ya biashara ya madini hapa nchini.
 
Wakati huo huo, Mhe. Rais Magufuli amekutana na kufanya mazungumzo na Kiongozi Mkuu wa Jumuiya ya Kihindu ya BAPS Swaminarayan Sanstha Duniani Mtukufu Mahant Swami Maharaj ambaye yupo nchini kwa ziara ya siku 7.
 
Pamoja na kumshukuru kwa ujio wake hapa nchini, Mhe. Rais Magufuli amemhakikishia kuwa Serikali ya Tanzania itaendeleza na kuimarisha zaidi uhusiano na ushirikiano wake na Jumuiya hiyo na amewaalika wafanyabiashara walio chini ya Jumuiya hiyo kuja nchini Tanzania kuwekeza katika viwanda, kilimo na shughuli nyingine za biashara na uwekezaji.
 
“Nimefurahishwa sana na ujio wako Mtukufu Mahant Swami Maharaj, sisi Tanzania tumekuwa tukishirikiana na Jumuiya ya Hindu tangu miaka mingi, nitafurahi kama mtaungana na juhudi za Serikali ya Tanzania kujenga viwanda, njooni mjenge viwanda na Serikali itawapa ushirikiano wowote mtakaohitaji” amesema Mhe. Rais Magufuli.
 
Mtukufu Mahant Swami Maharaj ambaye amefanya dua ya kuliombea Taifa na Rais, amemshukuru Mhe. Rais Magufuli kwa kukutana nae na amemhakikishia kuwa uhusiano na ushirikiano kati ya Jumuiya hiyo na Tanzania ulioanzishwa tangu enzi za utawala wa Awamu ya Kwanza ya Tanzania unaendelezwa na kukuzwa zaidi.
 
Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam
01 Aprili, 2017

Waziri Mkuu wa Ethiopia, Hailemariam Dessalegn ahitimisha ziara yake ya kikazi ya siku mbili nchini

0
0
Waziri Mkuu wa Shirikisho la Jamhuri ya Kidemokrasi ya Ethiopia Mhe. Hailemariam Dessalegn ameondoka nchini leo kurejea nchini mwake Ethiopia baada ya kumaliza ziara yake rasmi ya kiserikali hapa nchini aliyoifanya kwa mwaliko wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli.

Katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam, Mhe. Hailemariam Dessalegn ameagwa na mwenyeji wake Mhe. Rais Magufuli aliyeongozana na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa.

Akiwa nchini Mhe. Hailemariam Dessalegn amefanya mazungumzo na mwenyeji wake Mhe. Rais Magufuli Ikulu Jijini Dar es Salaam, amehudhuria dhifa ya kitaifa iliyoandaliwa na Mhe. Dkt. Magufuli kwa heshima yake na leo asubuhi ametembelea bandari ya Dar es Salaam ambapo amesema nchi yake ipo tayari kuitumia bandari hiyo sambamba na kuanzisha kituo cha huduma za usafirishaji wa mizigo kwa ndege (Cargo Hub) katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere kupitia shirika lake la ndege la Ethiopia Airline.


Emmanuel Buhohela
Kaimu Mwandishi wa Habari wa Rais Msaidizi
Dar es Salaam

01 Aprili, 2017

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumapili ya April 2


SORRY MADAM -Sehemu ya 45 & 46 (Destination of my enemies)

0
0
MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWAILIPOISHIA
ILIPOISHIA
Makachero wanao uongoza msafara huo wakashuka kwenye magari yao kila mmoja akiwa na bastola iliyo jaa risasi mkononi mwake. Wakatembea kwa tahafhari kubwa wakijaribu kuchunguza kila sehemu ya msitu huo kwa umakini wa hali ya juu. Umakini wao ulizidi kuongezeka kwani wana kiongozi wao mkubwa wa nchi. Wakafika hadi eneo la handaki. Makachero wawili wakaingia ndani ya handaki hilo. Gafla milio mingi ya risasi ikasikika ndani ya handaki hilo jambo lililo wachanganya raisi na watu wake walio baki nje ya handaki.

ENDELEA
   Milio hiyo ya risasi ikawafanya makachero wengine kumzunguka raisi Praygod Makuya kuzuia hata kama kuna tatizo baya litatokea waweze kumlinda. Ikawalazimu makachero wawili kuingia katika handaki bastola zao zikiwa mikononi mwao. Cha kushangaza wakawakuta wezao wakiwa wamesimaa huku wanatetemeka mithili ya watu walio mwagiwa maji ya baridi  na kusimamishwa kwenye kilele cha mlima Kilimanjaro.

Wakajaribu kuwauliza kwa ishara ni kitu gani kimepelekea hadi wakawa wanafyatua risasi ovyo ovyo. Ila hakuna aliye weza kutoa jibu kati yao zaidi ya wao kuendelea kutetemeka.  Ikawalazimu wezao hao wawili kuanza kutembea taratibu ndani ya handaki hilo kuchunguza ni nini ambacho kimetokea.

Wakaingia kwenye moja ya chumba ambapo cha kwanza kukutana nacho chini ni damu nyingi za mwanadamu. Katika kupitisha pitisha macho yao huku na huku. Wakamkuta mke wa raisi akiwa amelala juu ya kitanda huku damu nyingi zikiwa zinamwagika mwilini mwake, akikaribia kuiaga dunia.

 ***
 Kitu kisicho onekana kikazidi kuwateketeza makachero walio mshambulia Priscar hadi wote wakafa.
Katika hali ya kumshangaza Priscar akajikuta akivutwa nje ya gari na kulazwa pembeni pasipo kumuona mtu anaye mfanyia mambo yote hayo. Jeraha la risasi iliyo mpiga ndani ya dakika moja likawa limekauka na mwili wake ukarudi katika hali yake ya kawaida.
“Wewe ni nani unaye nifanyia haya yote”
Ilimbidi Priscar kuuliza kwani hisia za kusnikwa na mtu huyo asiye oenekana kwenye mwili wake mara kadhaa, anazihisi ila tatizo ni mboni zake za macho haziwezi kumuona mtu huyo.

Hakuna ambacho aliweza kuambulia kujibiwa. Gari lake ambalo limeingia kwa nyuma ndani ya mtaro akashangaa likisitolewa taratibu na kusimamishwa barabarani. Kisha akajikuta akishikwa mkono wa kulia akikokotwa hadi kwenye mlango wa kuingilia ndani ya gari hilo. Mlango ukafunguliwa bila hata ya kupenda akajikuta akinyanyuliwa na kuingizwa kwenye gari na kukalishwa kwenye siti ya dereva.

Akafungwa mkanda, gari ikawashwa na mikono yake ikashikishwa kwenye mskani wa gari hiyo na mlango ukafungwa. Ikiashiria aondoke katika eneo hilo haraka iwezekanavyo kwani kuna gari baadhi za polisi zinakuja kuwapa nguvu makachero wanao pambana na mtu aliye hitaji kuuvamia msafara wa raisi.

 ***
Dokta akamuachia simu Shamsa kisha yeye akazidi kusonga mbele. Kulifwata gari lililo kosa kosa kuwagonga.  Shamsa kabla hajafika hatua nyingi simu hiyo ikaita kuangalia vizuri akakuta ni jina la baba yake, hakuona haja ya kuelekea anapo kwenda dokta wake. Akaipokea na kuiweka sikioni mwake.

“Baba habari”
“Ohoo Salama binti yangu, mumefika salama”
“Ndio baba hapa tumefika hospitalini”
“Mbona unazungumza kwa furaha sana?”
“Hpana baba kidogo nimebadilisha mazingira, kidogo ninafurahi sana”
Shamsa akiendelea kuzungumza na simu tayari dokta wale alisha fika kwenye  gari na kukutana na binti anaye mfahamu akitokea ndani ya gari hilo huku akimwagikwa na machozi.
“Sa Yoo unatatizo gani?”
Daktari alimuuliza huku  hasira yake ikiwa imebubujika kifuani mwake mithili ya barafu la maji liwekwapo juani
“Bibi yangu hali yake ni mbaya”

Dokta baada ya kusikia hiyo na kutokana anamfahamu vizuri binti huyo pamoja na bibi yake ambaye pia alisha wahi kumuhudumia katika maswala ya saikolojia, hakuwa na budi zaidi ya kuondoka na Sa Yoo wakielekea ndani. Wakaungana na Shamsa kuingia ndani ya hospoitali hiyo pasipo Eddy kumjua binti wa tatu anaye ingia na kina Sa Yoo ni nani, kwani binti huyo ameziachia nywele zake ndefu kwa nyuma nakuizuia sura yake kuweza kuonekana vizuri kwa mbele

Kutokana na uhalifu alio ufanya Eddy, ikamuwia ugumu kushuka ndani ya gari kuhofia kuingia mikononi mwa polisi, moja ni lazima astakiwe kwa kusa la kuwapiga polisi, mbili ni lazima atakabidhiwa katika ubalozi wa Tanzania aweze kurudishwa Tanzania, jambo ambalo hakuhitaji kuweza kulisikia kwa wakati huo.
Sa Yoo na daktari wakakimbilia kwenye  chumba cha wagonjwa mahututi huku wakimuacha Shamsa akiwa amekaa sehemu maalumu ya mapokezi akimsubiria mwenyeji wake afike. Shamsa akaitumia nafasi hiyo kuweza kumfikiria ni wapi ambapo anaweza kumpata Eddy.

Mwanaume anaye muheshimu kama baba yake, wazo la kurudi kwenye familia ya magaidi wa Al-Shabab likaanza kumpotea taratibu kichwani mwake, akaanza kufikiria kuungana tena na Eddy ambaye aliamini kwamba amekufa na hilo ndio jambo ambalo lilimfanya akubali kurudi katika familia ya Al-Shabab watu walio muulia wazazi wake baba na mama akiwa mdogo kisha akachukuliwa mateka na kuwa miongoni mwa askari wakikosi  hicho akiwa mdogo sana.
“Nilazima niwaue Al-Shabab wote”
Shamsa alizungumza huku picha ya askari wa kikosi hicho ikiwajia jia kichwani mwake. Hasira dhidi ya kikosi hicho ikazidi kumpanda moyoni mwake hadi mwili mzima ukaanza kumtetemeka.

Kwa kupitia kioo cha pembeni cha gari alilomo Eddy, akaona gari mbili za polisi zikija katia maeneo ya maegesho ya hospitalini hapo. Wasiwasi mwingi ukazidi kumpanda, akataka kushuka na kukimbia akaoona itakuwa ni hatari sana kwake na itakuwa ni rahisi kwa yeye kuweza kukamatwa na askari hao. Gari hizo zikazidi kulisogelea gari ambalo Eddy yupo, kwa haraka ikamlazimu kuweza kuinama ndani gari hilo ili asiweze kuonekana.
Gari hizo za polisi zikasimama karibu kabisa na gari alilopo. Wakashuka askari wanne walio valia nguo nyeusi huku viunoni mwao wakiwa wamening’iniza pingu pamoja na kuchomeka bastola zao zilizomo kwenye vifuko maalumu vya kuchomekea bastola.

   Askari hao wakatizama tizama kila sehemu ya maegesho ya magari hayo wakionekana kwamba kuna gari wanaitafuta, mmoja wao akaanza kupiga hatua za kulifwata gari hilo taratibu huku akijaribu kutazama namba ya usajili ya gari hilo kwani ni gari lililo mbebea muhalifu anayetafutwa ndani ya Japan nzima.
                                                                                              ***
  Miliyo ya risasi ilipo kata ndani ya handaki makachero wote walio nje ya handaki wakiongozwa na raisi Praygod wakaingia ndani huku wakionekana kuwa na shauku kubwa ya kujua ni kitu gani kinacho endelea ndani ya handaki. Wakawakuta makachero wa kwanza wakiwa hai huku wamesimama, hata kabla hawajawauliza wakawaona makachero wengine  wakitoka ndani ya chumba kimoja huku wakiwa wamembeba Rahab anaye endelea kuvujwa na damu nyingi.
Ikabaki nusu Raisi Praygod kuchanganyikiwa baada ya kumuona Rahab akiwa katika hali hiyo.

“Ah…aaa aahme faafaanyaa nini mke wangu”
Raisi Praygod aliuliza huku mwili ukimtetemeka, makachero walio tangulia kuingia ndani ya handaki hilo wakakosa jibu la kuzungumza na fika wanatambu kwamba wao ndio wameusika katika kumpiga risasi Rahab baada ya Rahab kuanza kufanya jaribio la kuwashambulia makachero hao ila akashindwa na kujikuta akipigwa risasi kadhaa zilizo mfanya kuingia ndani ya chumba huku hali yake ikiwa mbaya sana.
Kutokana hapakuwa na jibu kwa makachero hao, raisi Praygod akatoa amri ya mke wake awaishwe mara moja kwenye gari wampeleke hospitali.

Safari ya kurudi jijini Dar es Salaam ikaanza huku gari hizo zikiendeshwa kwa mwendo kasi. Ndani ya dakika arobaini na tano wakawa wameingia ndani  ya hospitali ya taifa muhimbili huku hali ya raabu kizidi kuwa mbaya kila jinsi dakika zilivyo zidi kwenda.
Madaktari wakaanza kazi ya kumuhudumia mke wa raisi, raisi Praygod akashindwa kuyazuai machozi yake.kumwagika. Hakujali kama ni kiongozi wa nchi alicho kihitaji kwa wakati huo ni kusikia mke wake anaendelea vizuri.

Madaktari ndani ya chumba cha upasuaji wakafanikiwa kutoa risasi zote sita zilizo ingia ndani ya mwili wa Rahab.
“Dokta…….”
Nesi mmoja alimuita daktari kiongozi wa opereshini hiyo, macho yao wote yakatua kwenye mwili wa Rahab, hapakuwa na mtu aliye weza kuamini kitu walicho kiona, woga kati yao ukazidi kutawala madaktari wote sita pamoja na nesi mmoja waliomo ndani ya chumba hicho.  Vidonda vilivyo kuwa kwenye mwili wa Rahab vilijiziba na kurudi katika hali ya kawaida.

Kitendo cha Rahab kuyafumbua macho yake yaliyo mekundu mithili ya damu kikawafanya madaktari wpte waliomo ndani ya chumba kuanza kukimbilia mlangoni, kila mmoja akijaribu kuyaokoa maisha yake. Hadi wanafika mlangoni tayari Rahab alisha simama wima na kuchomo sindano zote za madripu zilizo kuwa zimechomwa mwilini mwake. Kila walipo jaribu kuufungua mlango haukufunguka na taa zilizomo ndani ya chumba hicho zikaanza kufifia na kigiza cha mbali kikaanza kutawala ndani ya chumba.

***
   Njia nzima Priscar akajikuta akijiuliza maswali ni kitui gani kilicho weza kutoke katika muda mchache uliopita.

“Au naota?”
Swali hilo alilipatia jibu akilini mwake kwamba kila kitu kinacho tokea kwa wakati huo si ndoto bali ni hali alisi inayo jitokeza.
“Madam”
Priscar aliwaza sehemu alipo mucha Rahab, ikamlazimu kuongeza mwendo kasi wa gari lake kuelekea nje ya jiji la Dar es Salaam. Hadi anafika katika maeneo ya hamdaki ikamlazimu kusimaisha gari lake mbali kidogo na sehemu na lilipo hamdaki, akashuka na kuanza kukimbia kuelekea sehemu ya handaki, kabla hajalifikia akasikia milio kadhaa ya risasi ikirindima ndani ya handaki hilo.

Alipo chunguza vizuri akaziona gari za ikulu zikiwa zimesimama nje ya handaki hilo, huku Raisi Praygod akiwa wamezungukwa na walinzi wake. Baada ya milio ya risasi kunyamaza akawashuhudia walinzi hao wakiongozana na raisi wakiingi ndani ya handaki hilo. Baada ya dakika tano mbeleni akawaona wakitoka wakiwa wamembeba Rahab akionekana akiwa katika hali mbaya.
Priscar akataka kujitokeza ili  akasaidiane nao ila akaona itakuwa ni hatari kwake, akaendelea kujibanza kwenye mti huo hadi wakaondoka kwa kasi katika eneo hilo.
Kudhibitisha ni kitu gani kilicho weza kutokea ndani ya handaki hilo, kwa haraka akakimbia nje ya handaki hilo kutazama ni nini kilicho tokea.

Hakuamini macho yake baada ya kukuta damu nyingi zikiwa chini ya sakafu zikitokea katika chumba alipo ingia akazidikuta zikiwa nyingi jkuu ya kitanda. Jasho likaanza kumtirirka akifikiria ni kitu gani ambacho kimetokea bosi wake.
 
Kwa haraka akatoka ndani ya handaki na kurudi alipo liacha gari lake. Akaingia ndani ya gari na kuanza kuelekea Dar es Salaam akiamini kwamba ni lazima Rahab atakuwa amepelekwa kwenye moja ya hospitali iliyopo jijini Dar es Salaam.

Maalim Seif: Lipumba Hana Uwezo wa Kunivua Ukatibu Mkuu CUF

0
0
Sarakasi za kisiasa zinaendelea kutawala ndani ya chama cha CUF baada ya Katibu Mkuu wake, Maalim Seif Sharif Hamad, kudai kuwa Profesa Ibrahim Lipumba anatumiwa kukihujumu chama hicho.

Maalim Seif alimtuhumu Profesa Lipumba ambaye ni Mwenyekiti wa CUF, anayetambuliwa na ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa nchini kuwa anakihujumu chama ili kishindwe kudai haki waliyoipata katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 25 mwaka juzi.

Aliyasema hayo jana katika kijiji cha Tumbatu Mkoa wa Kaskazini Unguja alipozungumza na wanachama wa chama hicho, ikiwa ni ziara maalumu ya uimarishaji wa chama katika mikoa yote ya Kisiwa cha Unguja.

Maalim Seif alisema pamoja na Profesa Lipumba kupata nguvu kutoka vyombo vya dola na Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa katika kukihujumu chama hicho, lakini hawataweza kufikia malengo hayo.

Alisema taasisi hizo kwa pamoja zimekuwa zikimuunga mkono Lipumba kwa kumpa kila nguvu anayohitaji ili kuona anafanikisha malengo ya CCM ya kuitawala nchi bila ya kuwepo kwa chama kikuu pinzani, ila nguvu zao hizo zitagonga mwamba.

“Nashangaa sana kuona Lipumba amekubali kutumika na CCM kwa kukihujumu chama kwa masilahi binafsi, lakini nataka muelewe wananchi kuwa pamoja na nguvu zao zote hizo katu hawataweza kuwakatisha tamaa Wazanzibari ya kudai haki yao waliyoipata katika uchaguzi uliopita,” alisema.

Alishangazwa kuona Ofisi ya Msajili kwa kushirikiana na vyombo vya dola badala ya kufuata Katiba na sheria za nchi, wao wamekuwa wakikihujumu chama hicho.

“Pamoja na hujuma hizi zinazofanywa na Lipumba katika chama chetu, lakini nashangaa Rais (John) Magufuli anatumbua watendaji wabovu, lakini humu mrajisi (Msajili) wa Vyama vya Siasa anamuachia,” alisema.

Kuhusu kuondolewa kwenye nafasi yake, Maalim Seif alisema kwa mujibu wa katiba ya CUF, Lipumba hana uwezo wa kumvua nyadhifa hiyo hata kama angekuwa ni mwenyekiti halali.

Alisema kwa mujibu wa katiba yao ili Katibu avuliwe wadhifa wake lazima mkutano mkuu uhudhuriwe na zaidi ya nusu ya idadi wajumbe.

Alisema kikao kilichofanyika chini ya Profesa Lipumba kilihudhuriwa na wajumbe wasiokuwa na ujumbe kihalali, ambao walipandikizwa kuonesha kama kikao hicho kilikuwa halali.

“Ikiwa mimi nimefukuzwa chama kutokana na madai kuwa sihudhurii vikao vinavyofanywa na ofisi za chama hicho jijini Dar es Salaam, mbona yeye Lipumba tangu mwaka 2015 hawajawahi kuja ofisi kuu ya chama ambayo ni mtendeni hadi leo, kwa hiyo naye alitakiwa kufukuzwa,” alihoji.

Maalim Seif alisema kuwa kinachosikitisha ni kuona Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa nayo kuidhinisha kuwa wamekubaliana na mageuzi hayo yaliyofanywa na Lipumba kwa kushirikiana na wajumbe wake.

“Ninachokifahamu mimi ndani ya katiba yetu inasema kuwa ili uamuzi wa kuvuliwa nafasi ya uongozi ni lazima anayedaiwa kufanya kosa aitwe na uongozi kujieleza, lakini mimi sijaitwa kujieleza,” alihoji Maalim Seif.

Akizungumzia madai ya kushinda Uchaguzi Mkuu uliopita, Maalim Seif alisema waliwataka wananchi wa Zanzibar kutokata tamaa na haki yao, huku akidai hivi karibuni dola ya Zanzibar itakuwa chini ya CUF.

Naibu Katibu Mkuu wa CUF Zanzibar, Nassor Ahmed Mazrui, alisema uongozi wa CUF unasikitika kuona vyombo vya dola vikiingilia mamlaka ya chama hicho na kusahau wajibu wao.

Alisema kuwa wajibu wa vyombo hivyo ni kusimamia amani ya wanachama na viongozi wake, lakini ni jambo la kushangaza kwa viongozi wa vyombo hivyo kuwa ni miongoni mwa wanaongoza kuonesha chuki dhidi ya CUF.

Alisema pamoja na hujuma hizo, lakini viongozi wakuu wa chama hicho chini ya Maalim Seif, hawatosita kudai haki yao hadi kieleweke.

Akijibu tuhuma hizo, Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho bara na anayemuunga mkono Profesa Lipumba, Magdalena Sakaya alimtuhumu Maalim Seif kuwa ndiye anakula njama za kukidhoofisha chama.

Alisema Seif amekataza ruzuku zisifike kwenye wilaya, hakuna mikutano na hakuna hata pikipiki huku wenzao Chadema waliokuja juzi wamekuwa chama kikuu cha upinzani kutokana na kuwa wamoja.

“Malalamiko anayotoa ajikite kwenye katiba, aichambue kifungu kwa kifungu atabaini anakosea wapi.

“Hii ni taasisi  ya chama, siyo kampuni ya mtu, lazima tufuate katiba tuliyojiwekea ambayo ipo wazi inatoa maelekezo ya kila kitu, anayekengeuka anafanya makusudi na sisi hatuwezi kukaa kimya bila kuchukua hatua ikiwa ni pamoja na kuteua watakaofanya kazi alizotakiwa kufanya yeye,” alisema Sakaya.

Alieleza kuwa badala ya kujenga chama, ameamua kukidhoofisha na anatumiwa kufanya hivyo akijificha kwenye mwamvuli wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa).

“Amekuwa bwana kesi, kila kukicha anafungua mpya, mimi nina kesi, Lipumba ana kesi, Msajili wa Vyama ana kesi, mwanasheria ana kesi, akae kimya asubiri ziishe, ”alisema Naibu katibu mkuu huyo.

Waziri Mkuu Majaliwa amtaka Mkuu wa Mkoa wa Pwani Evarist Ndikilo kuwasaka wafugaji wanaodaiwa kuwapiga wakulima Bagamoyo

0
0
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amemuagiza Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Evarist Ndikilo kupiga kambi katika Kata ya Miono wilayani Bagamoyo na kuwasaka wafugaji wanaopiga wakulima.

Waziri mkuu alitoa agizo hilo alipozungumza na wakazi wa kata hiyo hivi karibuni alipokwenda kukagua miundombinu ya Hifadhi ya Taifa ya Saadani iliyopo wilayani Bagamoyo mkoani Pwani.

Taarifa ya Ofisi ya Waziri Mkuu ilisema diwani wa Miono, Juma Mpwimbwi akiwasilisha kero zao kwa kiongozi huyo alisema wanakabiliwa na tatizo la wakulima kupigwa na wafugaji na wakipelekwa kituo cha polisi hawachukuliwi hatua.

“Wafugaji wanatupiga lakini wenzetu hawachukuliwi hatua na hata ukienda kushtaki polisi hawakai kwa sababu wanadai wao wana fedha,” alisema diwani huyo.

Pia, alisema waliahidiwa barabara ya lami tangu miaka saba iliyopita, lakini hadi sasa hawana hata kipande kidogo tu cha barabara hiyo.

Mkazi wa kata hiyo, Shabani Mkwimbi akizungumza kwa niaba ya wananchi wenzake alisema wana kituo cha polisi na mahakama, lakini utendaji kazi wa viongozi waliopo unatia shaka.

Alimlalamikia mkuu wa kituo cha polisi na hakimu akidai wafugaji pekee ndiyo wanaoshinda kesi.

Waziri Mkuu Majaliwa aliwahakikishia wakazi hao kwamba hakuna hata mtu mmoja ambaye yuko juu ya sheria. Alisema suala la polisi litashughulikiwa na kamanda wa mkoa.

Majaliwa alisema msimamo wa Serikali ni kuwaona wakulima na wafugaji wanafanya kazi zao kwa uhuru.

“Hakuna mfugaji anayeruhusiwa kupeleka ng’ombe kwenye mashamba yenye chakula. Mkuu wa mkoa hili ni agizo, njoo upige kambi hapa na watu wako, na usake wahusika hadi wabainike. Ni lazima tuwajue ni kina nani wamehusika na hili,” alisema.

Je, Umeathiriwa na Punyeto Kiasi cha Kushindwa Kurudia Tendo la Ndoa???.....Bofya Hapa Kupata Tiba, Pia Tuna Handsome Up ya Kuongeza Maumbile

0
0
NATURAL BEAUTY COSMETIC ni kampuni inayotoa bidhaa ORIGINAL zenye matokeo mazuri bila kemiko wala madhara yoyote. Pata punguzo la bei kwa bidhaa hizi. 
 
1.HANDSOME UP ni kifaa kinachoongeza maumbile ya kiume  kwa 99% kwa size uipendayo wewe na kuimarisha misuli ya uume kwa @170,000/= tuu. 
 
2.MEN GELY kupaka. Hii inaongeza kwa wastani wa inch 6.5 na inapatikana kwa @120,000/=.  
 
3. MAX MAN 2. Ni vidonge kwa ajili ya nguvu ambavyo vinasaidia sana hata kwa watu wenye kisukari na waliokua wakifanya sana masturbation. Pia huongeza hamu ya tendo la ndoa kwa @130,000/=tu.     
 
Tupo DAR ES SALAAM  kariakoo na kinondoni kanisani.

Kwa mawasiliano zaidi piga  0759029968 au 0659618585.
Popote ulipo utapata huduma zetu.
 
Follow us
@natural2162
@natural2162
@natural2162
@natural2162
 
     Bidhaa zetu zote ni garantii na unapewa risiti
              Karibu

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya lEo Jumatatu ya April 3

Mwenge wa Uhuru kukimbizwa katika mikoa yote 31 kwa siku 195

0
0
Mbio za Mwenge wa Uhuru kwa mwaka 2017 zimezinduliwa rasmi jana katika uwanja wa Kumbukumbu Mjini Mpanda mkoani Katavi na unatarajiwa kuzunguka katika mikoa yote 31, ukipita kwenye halmashauri 195 kwa muda wa siku 195.

Katika sherehe hizo za uzinduzi, kiongozi wa mbio hizo kwa mwaka huu pia ametangazwa rasmi, ambapo atakuwa ni Amour Amad Amour kutoka mkoa wa Kaskazini Unguja visiwani Zanzibar.

Kiongozi huyo atasaidiana na wenzake watano katika kukimbiza mwenge huo ambao ni pamoja na Bahati Mwaniguta Lugodisha (Geita), Bi Fatima Yunus Hassan (Kusini Pemba), Fredrick Joseph (Singida), Salome Obadia Mwakitalima (Katavi) na Shukran Islam Msumi (Mjini Magharibi).

Kauli mbiu ya mbio hizo kwa mwaka huu inasema "SHIRIKI KUKUZA UCHUMI WA VIWANDA KWA MAENDELEO YA NCHI YETU'

Mgeni rasmi katika uzinduzi huo alikuwa ni makamu wa pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Balozi Seif Ali Idd kwa niaba ya Rais wa serikali hiyo Dkt. Ali Mohamed Shein, ambapo katika ujumbe wake amesisitiza umuhimu wa watanzania wote kuweka nguvu zao katika kujenga taifa la viwanda

Alisema hadi sasa tangu serikali yake iingie madarakani kwa muhula wa pili tayari viwanda vitatu vya watu binafsi vimekwishajengwa visiwani Zanzibar

Balozi Seif alisema mbali na kaulimbiu ya mwaka huu kusisitiza umuhimu wa viwanda, pia mbio hizo zitakuwa zikieneza ujumbe kuhusu mapambano dhidi ya Malira, UKIMWI, Dawa za Kulevya pamoja na rushwa.

Mbio hizo zimeanzia katika wilaya ya Mpanda, na kilele chake kitakuwa ni Oktoba 14 katika mkoa wa Mjini Magharibi.

Aliyetumbuliwa na Rais Magufuli Dk Mwele Malecela Ateuliwa Kuwa Mkurugenzi Shirika la Afya Duniani (WHO)

0
0
Salamu za pongezi zimeendelea kumiminika kwa aliyekuwa Mkurugenzi wa Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (Nimr), Dk Mwele Malecela baada ya kuteuliwa kuwa Mkurugenzi wa Vituo vya Kudhibiti na Kuzuia Magonjwa Afrika vya Shirika la Afya Duniani (WHO), Kanda ya Afrika.

Pia, Dk Mwele  aliteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Mpango wa Maalumu wa WHO wa kutokomeza magonjwa yasiyopewa kipaumbele (Espen) na sasa atahamia kituo chake cha kazi Congo-Brazaville. 

Mradi wa Espen ulianza kutekelezwa mwaka 2016 hadi 2020, una lengo la kumaliza magonjwa yasiyopewa kipaumbele kwa kutoa vifaa tiba, elimu na dawa. 

Magonjwa yasiyopewa kipaumbele ni pamoja na matende, mabusha, kichocho, minyoo ya tumbo na usubi. 

Miongoni mwa waliomtumia pongezi ni Mkurugenzi wa Taasisi ya Afya ya Sikika, Irenei Kiria ambaye aliandika katika ukurasa wake wa Twitter: “Hongera Mwele kwa kupata nafasi hiyo ina maana ulipangwa kulisaidia Taifa letu ukiwa nje.”

 Mwingine ni Mhadhiri wa Saikolojia wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Profesa Kitila Mkumbo aliyeandika katika ukurasa wake wa twitter akisema: “Nina furaha kwa uteuzi wa Dk Mwele kuwa Mkurugenzi wa WHO.Nahisi kusamehewa kwa kuikosoa Serikali baada ya kumuondoa Nimr.” 

Mbunge wa Kigamboni, Dk Faustine Ndugulile yeye aliandika katika ukurasa wake akimpongeza Dk Mwele na kusema, “Nimezidiwa na furaha baada ya kupata taarifa kuwa umepata kazi kubwa katika ogani ya kimataifa. Mlango mmoja ukifungwa mwingine hufunguliwa. Katumikie vyema.” 

Dk Mwele aliondolewa kuwa Mkurugenzi wa Nimr na Rais John Magufuli Desemba 17 mwaka jana. 

Kuondolewa kwake katika nafasi hiyo kulifanyika siku moja baada ya kutoa ripoti ya utafiti wa magonjwa, ndani yake ikiwamo taarifa ya virusi vya ugonjwa wa Zika katika maeneo ya Morogoro, Geita na Magharibi mwa Tanzania. 

Taarifa ya Dk Mwele, ilieleza kuwa kati ya watu 533 waliopimwa, asilimia 15.6 walibainika kuwa na virusi hivyo. 

Siku moja baada ya kutoa takwimu hizo, Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu akiwa na Dk Mwele aliitisha mkutano na waandishi wa habari kukanusha taarifa hizo kwamba ugonjwa huo bado haujaingia nchini.


Zitto Kabwe Agonga Mwamba Ubunge ELA....... Spika Ndugai Agomea Maombi Yake

0
0
Mbunge  wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe (ACT-Wazalendo),  amegonga mwamba baada ya Kamati ya Kanuni ya Bunge kutoa msimamo wake kuhusu uchaguzi wa wabunge wa Bunge la Afrika Mashariki (EALA).

Hatua hiyo inatokana na Zitto kuwasilisha barua kwa Spika wa Bunge, Job Ndugai, Machi 28, mwaka huu akitaka kamati hiyo kutoa ufafanuzi wa mgombe wa kundi C ili kila chama kiweze kushiriki uchaguzi, badala ya kupewa kwa vyama vilivyokuwa na idadi kubwa ya wabunge.

Kutokana na Tangazo la Bunge kwenye gazeti namba 11 la Machi 17, lililotangaza uchaguzi huo na masharti yake, Zitto, alisema mwongozo wa uchaguzi huo unavunja kanuni mbalimbali na kwamba kitakachofanyika sasa kitakuwa ni uteuzi na si uchaguzi.

Alisema pia mwongozo huo, mbali na kuvunja mkataba wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, unaotaka suala la jinsi lizingatiwe kwenye wabunge wanaokwenda kuiwakilisha nchi katika Bunge hilo, lakini pia inavinyima vyama vingine vyenye uwakilishi bungeni haki ya kuchaguliwa.

Chanzo cha kuaminika kimeema  kuwa uamuzi huo ulifikiwa katika kikao cha Kamati ya Kanuni, kilichokutana juzi mjini Dodoma chini ya Spika wa Bunge, Job Ndugai, huku Naibu Spika, Dk. Tulia Ackson akihudhuria.

Viongozi wengine waliohudhuria kikao hicho ni Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe, Waziri wa Katiba na Sheria, Profesa Palamagamba Kabudi na  Mbunge wa Kawe, Halima Mdee.

Wengine ni Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe pamoja na wajumbe kadhaa, ambapo baada ya kufunguliwa kwa kikao hicho kilichomalizika usiku wa juzi, Spika Ndugai, alihoji uhalali wa Zitto kuandika barua ya kuhoji mgawanyo huo wa wabunge wa EALA.

“Kifupi ni kwamba Zitto amekwama na hana tena namna maana Spika alimsema sana kutokana na mgawanyo lakini kabla ya kuendelea zaidi kwamba alimuuliza Waziri wa Katiba na Sheria, Profesa Kabudi kama kuna tatizo naye akasema hakuna na Spika hajakosea.

“… ila ni kikao ambacho Spika kwa kweli amesimamia sheria na ni kiongozi asiyeyumba katika kusimamia sheria, sasa tunakwenda kwenye uchaguzi huku ukweli ukiwa umeshajulikana, CCM watakuwa na viti sita, Chadema viwili na CUF kimoja,” alisema mtoa habari huyo

Baaada ya majadiliano ya kina na ufafanuzi wa kisheria kuhusu mgawanyo huo wajumbe wa Kamati ya Kanuni walikubaliana na Spika Ndugai kwa kauli moja, huku hoja ya Zitto ikitupwa na uchaguzi huo wa EALA  utafanyika kwa kuzingatia uwiano wa idadi ya wabunge wa vyama vyenye uwakilishi bungeni.

Hata hivyo kanuni ya 5(5) ya nyongeza ya tatu ya kanuni za Bunge inaeleza “Chama  chochote cha siasa chenye haki ya kusimamisha mgombea wa EALA kinaweza kuweka wagombea watatu katika  ya wagombea ubunge”.

Kutokana na hilo msingi huo wa kikanuni inaonesha kuwa vyama vingine tofauti na Chadema , CUF na CCM, haviwezi kusimamisha wagombea kwa sababu havikidhi kigezo cha kanuni ya 12 za Kudumu za Bunge.

Jinsi Punyeto Inavyo Sababisha Ukosefu Na Upungufu Wa Nguvu za Kiume

0
0

Ukosefu  na/ama  upungufu  wa  nguvu  za  kiume, ni  tatizo  linalo  wakabili  mamilioni  ya  wanaume  duniani.  Zipo  sababu  nyingi  zinazo  sababisha  tatizo  la  ukosefu  wa  nguvu  za  kiume.  

Miongoni  mwa  sababu  hizo  ni  pamoja  na  maradhi  kisukari, presha,shinikizo  la  damu, moyo, figo, matatizo  kwenye  mishipa  ya  ubongo  &  mishipa  ya  uti  wa mgongo, matatizo  kwenye  mishipa itumikayo  kusafrisha damu  mwilini, maradhi  ya  ngiri,  pamoja  na   upigaji  punyeto  kwa  muda  mrefu.

Katika  makala  yetu  ya  leo, tutaangalia  namna   suala  la  upigaji  punyeto linavyo  athiri  nguvu  za  kiume.

Kabla  hatujaangalia  namna  suala la upigaji  punyeto linavyo  maliza  nguvu  za  kiume, ni  vyema  tukafahamu  kwanza  kuhusu  SAYANSI  YA  MFUMO  WA  NGUVU  ZA  KIUME.

Kufahamu   kuhusu   SAYANSI  YA  MFUMO  WA  NGUVU  ZA  KIUME  tafadhali  tembelea :

Ukisoma  vizuri  kuhusu  mfumo  wa  nguvu  za  kiume, utagundua  kuwa   Suala  la  nguvu  za  kiume  ni  suala  la  kimfumo.  Ili  mwanaume  awe na nguvu  za  kiume, aendelee  kuwa  na  nguvu  za  kiume na  azilinde  nguvu  zake za  kiume, ni  lazima  ogani  zote zinazo  husika  na  mfumo  wa  nguvu  za  kiume  ziwe  na  afya  njema  na  ziwe  na  ushirikiano   thabiti  na  wenye  afya.

Vile  vile , utagundua  kuwa , mambo  makuu  muhimu  katika   mfumo  wa  nguvu  za  kiume  ni  kama  ifuatavyo:

i.Mishipa  imara  ya  ubongo  na  yenye  afya  njema

ii. Mishipa  imara  ya  uti  wa  mgongo  (  spinal  cords )

iii.Mishipa  imara  itumikayo  kusafirisha  damu  mwilini  (  Blood Vessels )

iv. Mfumo  imara  wa  usafirishaji  damu  mwilini

v. Mishipa  ya  uume  iliyo  imara  na  yenye  afya  njema

vi. Uhusiano  imara  na  wenye  afya  kati  ya  mishipa  ya  fahamu  iliyopo  katika  ubongo, mishipa  ya  kwenye  uti  wa  mgongo  pamoja  na  misuli & mishipa  ya  kwenye  uume.

Hivyo  basi, ili  mwanaume  aweze  kuwa  na  nguvu  imara  za  kiume, na  aendelee  kuwa  na  nguvu  hizo ni  lazima  mambo  yote  muhimu  katika  mfumo  wa  nguvu za  kiume  yawe  imara  pasi na  hitilafu  yoyote.

Hitilafu  yoyote  katika  mambo  hayo, itasababisha  ukosefu na/ama  upungufu wa  nguvu  za  kiume  kwa  mwanaume  huyo.  Pale inapotokea    hitilafu  ama  mapungufu  katika  ogani  zaidi  ya  moja  kati  ya  zilizo  tajwa hapo  juu, basi  tatizo  kwa  muhusika  huwa  kubwa  mara  dufu.

JINSI  PUNYETO  INAVYO  SABABISHA  TATIZO  LA  UKOSEFU &  UPUNGUFU  WA  NGUVU  ZA  KIUME.
Mwanaume   anapopatwa na  wazo  la  kufanya  tendo  la  ndoa, ubongo  hutoa  ishara  kwenye  mishipa  ya  uti  wa  mgongo  ambayo  nayo  husafirisha  taarifa  hadi  kwenye  mishipa &  misuli  ya  uume.

Mishipa  ya  uume inapopokea  taarifa  hiyo, hutanuka. Na  mishipa  ya  uume  inapotanuka, hufanya  mambo  mawili  muhimu  sana :

i.Husababisha  mishipa  ya  ateri  kupanuka  na  hivyo  kuruhusu  damu  kuingia kwa  kasi  sana   ndani  ya  mishipa  ya  uume  na  hivyo  kuufanya  uume  usimame  na  kuwa  imara  bara bara.

ii. Huibinya na  kuiziba  mishipa  ya  vena  na  hivyo  kuzuia  kunyonya  ama  kufyonza  damu  iliyo  ingia  ndani  ya  mishipa ya  uume.  (  KAZI  KUBWA  YA  MISHIPA  YA  VENA  ILIYO  KARIBU NA  MISHIPA  YA  UUME  NI KUHAKIKISHA  HAKUNA  DAMU NDANI YA  MISHIPA  YA  UUME. HIVYO  BASI  DAMU  INAPOINGIA  NDANI YA  MISHIPA  YA  UUME, MISHIPA  YA  VENA  HU “SENSE” JAMBO  HILO  KWA  HARAKA  NA HIVYO  KUIFYONZA  DAMU  HIYO  KUTOKA KWENYE MISHIPA  YA UUME  YA  KUITOA  NJE YA MISHIPA  YA  UUME.  NA  DAMU INAPOKOSEKANA  NDANI  YA  MISHIPA  YA  UUME, HUUFANYA  UUME  KUSINYAA  NA  KULEGEA )

Mtu  anayepiga  punyeto  husababisha  mambo  yafuatayo  katika  mwili  wake :

1. Huuwa  nguvu  ya  mishipa  & misuli ya  uume ambayo  ndio  inayo husika  na  kusimama  kwa  uume

2. Mishipa  ya   uume  inapo  sinyaa  na  kukosa  nguvu  yake  ya  asili, husababisha  mambo  yafuatayo :

i.Huondoa  uwezo  wa  mishipa  &  misuli  ya  uume  kutanuka, na  hii  ndio  sababu  inayo  wafanya  waathirika  wa  punyeto  kutumia  nguvu  nyingi  sana  katika  kuufanya  uume  usimame.

ii.Huondoa  uwezo  wa  mishipa &  misuli  ya  uume  kuibana  na  kuiziba  mishipa  ya  vena, na  hii ndio  sababu  inayo  fanya  waathirika  wa  punyeto  kufika  kileleni  haraka  sana, kwani damu  inayo  ingia  kwenye misuli  ya  uume   hufyonzwa  ndani ya  muda  mfupi sana. 
 
 Hii  hutokea  kwa  sababu  mishipa na  misuli  ya  uume inakuwa  imelegea,na  mishipa  ya  vena inakuwa  imepwaya, hivyo  msuguano wowote ule  hufanya  mishipa  ya  vena  kufunguka  na  kufyonza  damu  kutoka  kwenye mishipa  ya  uume  na hivyo  kuufanya  uume  kusinyaa  ndani ya dakika ama sekunde  chache sana.

3. Vile  vile  punyeto  hufanya  uume  kusinyaa na  kurudi ndani  na  kuufanya  uonekane kama  uume  wa  motto mdogo.

Kwa  ufupi  punyeto  husababisha  ukosefu  wa  nguvu  za  kiume  kwa  sababu  kuu  zifuatazo :

i.Kwanza   hudhoofisha  na  kuharibu  mishipa  ya  uume,  ambayo  ndio  hufanya  uume kusimama.

ii.Pili  hudhoofisha  utendaji  kazi  wa  mishipa  ya  ateri, ambayo  ndio  hutumika  kama  njia  ya  kusafirisha  damu kupeleka kwenye  misuli  ya  uume  na  ivyo  kuufanya  uume  usimame

iii. Tatu, punyeto  hupelekea  kuvuja  kwa  mishipa  ya  vena  na  hivyo  kusababisha  damu  kufyonzwa  kwa  haraka  sana  kila  iingiapo ndani  ya  misuli ya  uume  na  matokeo  yake  ni  uume   kusimama  kwa  muda  mfupi  sana  wakati wa  tendo  la  ndoa.

iv. Punyeto  huathiri  mtiririko  wa  damu  kwenda  kwenye  mishipa  ya  uume, kwa  sababu  hudhoofisha  misuli &  mishipa  ya  uume  pamoja  na mishipa ya  ateri  ambayo  ndio  hutumika  katika  kusafirisha  damu kwenda  kwenye  uume

DALILI  ZA  MTU  ALIYE  ATHIRIWA  NA  PUNYETO
Dalili  kuu  za  mtu  aliye athiriwa  na  punyeto  ni  kama  ifuatavyo:

i.           Uume  kusinyaa  na  kuwa  kama  wa  mtoto
ii.         Uume kurudi  ndani
iii.       Uume  kusimama  ukiwa  legelege
iv.       Kufika  kileleni  haraka  wakati  wa  tendo  la  ndoa.

TIBA   YA   NGUVU  ZA  KIUME  KWA MTU  ALIYE  ATHIRIKA  NA  PUNYETO.
Dawa   asilia  ya  nguvu  za  kiume iitwayo JIKO  ni tiba  bora  na  ya  uhakika  kabisa  kwa  mtu  aliye  athiriwa   na  punyeto.  Dawa  hii, pamoja  na  mambo  mengine  mengi, husaidia  kufanya  mambio  yafuatayo  katika  mwili  wa  mwanaume  aliye  athiriwa  na  punyeto :

i.Kuimarisha  mishipa  & misuli  ya  uume  ulio  legea na  hivyo  kuurejeshea  uwezo wake wa  asili

ii. Hutibu   tatizo  la  uume  kurudi  ndani

iii.Humaliza  tatizo  la  kusimama  kwa  uume  ukiwa  legelege

iv.Hutibu  na  kuponya  kabisa  tatizo  la  kufika  kieleleni  haraka.

BEI  YA  DAWA  :  Dawa  hii  inapatikana  kwa  gharama  ya  SHILINGI  ELFU  THEMANINI  TU (Tsh. 80,000/=)

MAHALI  INAPOPATIKANA :  Dawa  hii  inapatikana  katika  duka  la  dawa  asilia  liitwalo  NEEMA  HERBALIST  &  NUTRITIONAL  FOODS  CLINIC  lililopo  jijini  DAR  ES  SALAAM  katika  eneo  la  UBUNGO   nyuma  ya  jengo  la  UBUNGO  PLAZA   karibu  na SHULE  YA  MSINGI  UBUNGO  NATIONAL  HOUSING.

Kwa  wateja  wasio  weza  kufika  ofisini  kwetu. Watafikishiwa  dawa  mahali  popote  walipo  jijini  DAR  ES  SALAAM.

Kwa   wateja  waliopo  mikoani  watatumiwa  dawa  kwa  njia  ya  MABASI

Kwa  wateja  waliopo   Zanzibar  wata fikishiwa  dawa  kwa  njia  ya  usafiri  wa boti.

Na  kwa  wateja  waliopo  UGHAIBUNI  watatumiwa  dawa  kwa  njia  ya  POSTA  ama  DHL.

MAWASILIANO :  WASILIANA  NASI   KWA  SIMU  NAMBA  0766  53  83  84.

Kwa  taarifa  zaidi  kuhusu  huduma  zetu, tutembelee kila  siku  kwenye  blogu  yetu :

Nay wa Mitego ahofia usalama wa maisha yake

0
0
Rapa Nay wa Mitego anayetamba na wimbo wa  'Wapo'  uliojipatia umaarufu mkubwa hadi serikalini amedai kuwa usalama wa maisha yake upo hatarini na kwamba kuna watu wanaopanga kumpoteza ili asiwepo duniani.

Katika ukurasa wake wa Instagram Nay 'amerusha jiwe gizani' pasipo kumtaja mtu ambaye anataka kumuangamiza huku  akisisistiza kuwa yupo tayari kufanyiwa chochote na kwamba hajajipanga kupambana na watu wao.

"Usalama wa maisha yangu umekuwa mdogo kwasasa, wanapanga kunipoteza ikibidi nisiwepo kabisa kwenye hii dunia. Nipo tayari kwa chochote wanacho panga kufanya coz sijajipanga kupambana nao"  Ameandika Nay.

Nay ameongeza "Mimi ni Mwanamuziki si vingine. Kwa chochote kitachotokea familia yangu itakuwa na cha kuongea. Siwezi kuhama nchi wala kukimbia nitafia hapa hapa. Na siko tayari kupindisha chochote.! Nyie Ndo mtanilinda. Sina mlinzi na sitarajii kuwa na mlinzi. OnlyGod"

Nay ametoa taarifa hizo ikiwa ni siku chache baada ya kuachia wimbo huo na kukamatwa na polisi lakini baadaye akaachiwa kwa amri ya Rais na kujipatia nafasi ya kuonana na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo.

Hiki ndicho alichoandika.

Kamishna Jenerali wa Uhamiaji afanya Mabadiliko Makubwa ya viongozi wa Mikoa nchini na baadhi ya viwanja vya ndege

0
0
Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Nchini Dr. Anna Peter Makakala amefanya mabadiliko makubwa ya Viongozi wa Uhamiaji wa Mikoa mbalimbali hapa nchini pamoja na kuwateua Wakuu Wapya wa mikoa kushika nyadhifa hizo katika Mikoa iliyopo Tanzania Bara na Visiwani Zanzibar.

Katika Mabadiliko haya Naibu Kamishna wa Uhamiaji Sixstus Faustine Nyaki aliyekuwa Mkuu wa Uhamiaji Mkoa wa Mwanza amehamishiwa  mkoa wa  Simiyu wakati aliyekuwa Mkuu wa Uhamiaji Mkoa wa Rukwa Naibu Kamishna  wa Uhamiaji Selemani  Bandiho  Kameya amehamishiwa Mkoa wa Tabora.

Mkuu wa Uhamiaji Mkoa wa Mbeya, Naibu Kamishna wa Uhamiaji Asumsio  Paulus Achacha amehamishiwa Mkoa wa Kaskazini Pemba, Mkuu wa Uhamiaji Mkoa wa  Manyara  Naibu Kamishna  Peter Jerome Kundy amehamishiwa Mkoa wa Dodoma kuchukua nafasi ya  Kamishna Msaidizi  Ali Mohamed ambaye amehamishiwa   kuwa Mkuu wa Uhamiaji mkoa wa  Arusha.

Naibu Kamishna wa Uhamiaji  Mkemi Mhina Seif  ameteuliwa kuwa Mkuu wa Uhamiaji Mkoa wa Kusini Unguja, Naibu Kamishna wa Uhamiaji  Muhsin Abdallah Muhsin ameteuliwa kuwa Mkuu wa Uhamiaji Mkoa wa Kaskazini Unguja,  Naibu Kamishna wa Uhamiaji  Said Omary Hamdani ameteuliwa kuwa Mkuu wa Uhamiaji  Mkoa wa Mjini Magharibi na  Naibu Kamishna wa Uhamiaji Othman Khamis Salum  ameteuliwa kuwa Mkuu wa Uhamiaji Mjini Magharibi Unguja.

Katika mabadiliko hayo baadhi ya Wakuu wa Uhamiaji wa Mikoa wamebaki katika Vituo vyao vya kazi vya awali akiwemo aliyekuwa Mkuu wa Uhamiaji Mkoa wa Morogoro Naibu Kamishna wa Uhamiaji  Safina Muhindi, Mkuu wa Uhamiaji Mkoa wa Lindi Naibu Kamishna wa Uhamiaji George Kombe, Mkuu wa Uhamiaji Mkoa wa Ruvuma  Naibu Kamishna wa Uhamiaji Hilgaty Laurent  Shauri, Mkuu wa Uhamiaji Mkoa wa Singida Naibu Kamishna wa Uhamiaji Faith Alexander Ihano  na Mkuu wa Uhamiaji Mkoa wa Mara  Naibu Kamishna  Fredrick Eustace  Kiondo.

 Wengine waliobaki kwenye vituo vyao vya awali ni pamoja na  Naibu Kamishna wa Uhamiaji  Abdallah  Ramadhani Towo  mkoa wa Kagera na  Naibu Kamishna wa Uhamiaji  Anastazia  Gasper Ngatunga mkoa wa Shinyanga.

Katika mabadiliko hayo Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Dr. Makakala pia amewateua  Viongozi wa Uhamiaji wa Mikoa wapya katika baadhi ya mikoa hapa nchini ambapo Naibu Kamishna wa Uhamiaji Mary Francis Palmer   kuwa Mkuu wa Uhamiaji Mkoa wa Dar es Salaam,  Naibu Kamishna wa Uhamiaji  Plasid  Mazengo,  Mkuu wa Uhamiaji Mkoa wa  Pwani, Mrakibu Mwandamizi wa Uhamiaji  James Andrew Mwanjotile, Mkuu wa Uhamiaji  Mkoa wa  Mtwara,  Kamishna Msaidizi Mwandamizi  Hope Jaffer Kawawa Mkuu wa Uhamiaji Mkoa wa  Iringa,  na  Kamishna Msaidizi wa Uhamiaji  Hosea Alphonce Kagimbo  Mkoa wa Njombe.

Wengine ni Naibu Kamishna wa Uhamiaji  Rashid Salum Magetta  Mkuu wa Uhamiaji  Mkoa wa Songwe,  Naibu Kamishna wa Uhamiaji Carlos John Haule,  Mkuu wa Uhamiaji Mkoa wa Rukwa,  Naibu Kamishna wa Uhamiaji  Julieth Deodatus Sagamiko Mkuu wa Uhamiaji Mkoa wa  Manyara,  Naibu Kamishna wa Uhamiaji  Albert Joseph Rwelamila, Mkuu wa Uhamiaji  Mkoa wa Kilimanjaro na  Naibu Kamishna wa Uhamiaji  Paul Laurent Eranga,  Mkuu wa Uhamiaji Mkoa wa  Mwanza.

Naibu Kamishna wa Uhamiaji Crispin Crispin Ngonyani ameteuliwa kuwa Mkuu wa Uhamiaji Mkoa wa  Tanga,  Naibu Kamishna wa Uhamiaji  Shaban Omar Hatibu  Mkuu wa Uhamiaji Mkoa wa  Katavi,  Naibu Kamishna wa Uhamiaji   Remigius Ibrahimu Pesambili Mkuu  wa Uhamiaji  Mkoa wa Kigoma na Mrakibu Mwandamizi wa Uhamiaji Novaita Edmund Mrosso ameteuliwa kuwa  Mkuu wa Uhamiaji Mkoa wa Mbeya.

Aidha Mrakibu Mwandamizi wa Uhamiaji Bakari Mohamed Ameir ameteuliwa kuwa Mkuu wa Kituo cha Uhamiaji cha Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume [AAKIA] na Kamishna Msaidizi  Mwandamizi wa Uhamiaji Fulgence Andrew Mutarasha  kuwa  Mkuu wa Uhamiaji Kituo cha Uwanja wa Ndege wa Kimataifa Julius Nyerere[JNIA].

Imetolewa na
Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Nchini
Dr. A. P. Makakala

3 Machi 2017

Mgomo wa Mabsi na Daladala Wasitishwa

0
0
Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri na Nchi Kavu na Majini, Sumatra, pamoja na wadau wa sekta ya usafirishaji wamekubaliana kusitisha mgomo wa usafirishaji wa abiria na mizigo uliopangwa kuanza kesho.

Akizungumza leo jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mkuu wa Sumatra, Gilliard Ngewe amesema kusitishwa huko kunatokana na kikao na Waziri wa Mawasiliano Uchukuzi na Ujenzi, Prof. Makame Mbarawa, kuhusu kuandika kwa kutenganisha makosa ya dereva na wamiliki wa mabasi

Bw. Ngewe amesema, kanuni hizo zitaandikwa ndani ya siku 14 katika rasimu hiyo na wadau wa usafirishaji kuendelea na shughuli za usafirishaji na kwamba, baada ya kufanya marekebisho ya rasimu ya kanuni itarudishwa kwa wadau kuweza kujadiliwa kwa ajili ya kuwasilishwa Bungeni .

Naye Makamu Mwenyekiti wa Wamiliki wa Mabasi, Taboa, Abdallah Mohamed, amesema wamekubaliana na Sumatra kurekebishwa kwa baadhi ya kanuni za makosa kati ya wamiliki na madereva wa mabasi.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images