Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Kenya waomba kuwaajiri madaktari kutoka Tanzania

$
0
0
Serikali ya Kenya imeiomba Tanzania kuiruhusu kuajiri madaktari kutoka nchini humo ili kujaza nafasi ya madaktari walioingia kwenye mgomo kwa zaidi ya siku 90 hadi sasa.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu amethibitisha kupokea ombi hilo la Serikali ya Kenya. Hata hivyo, hakutaka kutoa ufafanuzi zaidi.

“Ndio… lakini tafadhali usiniulize maswali zaidi,” Waziri Ummy anakaririwa na The Citizen.

Hivi karibuni, Serikali ya Kenya ilitangaza mpango wa kuwaajiri madaktari kutoka Tanzania, Ethiopia na Cuba kwa lengo la kuziba pengo la madaktari walioingia katika mgomo nchini humo.

Hata hivyo, Jumuiya ya Madaktari Tanzania (MAT) kupitia kwa Mwenyekiti wake mteule, Dkt. Elisha Osati jana kilieleza kuwa hakiungi mkono ombi la Serikali ya Kenya katika kipindi hiki ambacho madaktari wa nchi hiyo wako kwenye mgomo.

“MAT haiungi mkono mpango wa Serikali ya Kenya kuwaajili madaktari wa Tanzania. Labda kama ombi hili litafanyika baada ya mgomo kuisha,” Dkt. Osati aliandika kupitia mtandao wa Twitter.

Ombi hilo limekuja ikiwa ni siku chache baada ya MAT kuiomba Serikali kuwaajiri madaktari kwani kuna zaidi ya madaktari 1500 wapya waliopewa leseni lakini bado hawajaajiriwa.

Madaktari wa Kenya wameingia kwenye mgomo wakidai ongezeko la mshahara wa kima cha chini hadi shilingi milioni 9,700,000 za Tanzania, kiasi ambacho Serikali ya nchi hiyo imesema haiwezi kumudu.

Kafulila Amtaka Makonda Aoneshe Vyeti Hadharani au Kama Hana Ajiuzulu ili Watu Waendeleee na Mambo Mengine

$
0
0
Aliyekuwa Mbunge wa Kigoma Kusini, David Kafulila ameibuka na kuongea mambo matano kuhusiana na sakata la vyeti feki linalomuandamana Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda. Kafulila amesema yafuatayo;

"Kwanza ni ushauri wangu kwamba Makonda amsaidie Rais ama kwa kuonesha vyeti vyake vyote kuondoa utata au ajizulu ili serikali iendelee na mambo mengine. 

"Obama alipotuhumiwa kuhusu uraia wake USA alifanya kazi ndogo tu ya kuweka vyeti vyake vyote hadharani na akawa amefunga utata wa uraia wake. hivyo ni vema Makonda afanye hivyo kama anavyo au akae pembeni kwani nchi ni muhimu kuliko mahusiano yake na Rais.

"Rais anapaswa kujua kuwa hoja ya jinai ya kughushi vyeti inayopigiwa kelele inahusu pia umakini wa mamlaka yake kama mteuzi wa Makonda kwamba kuna shida ya vetting. hivyo kuondoa hilo ni kuchukua hatua stahiki. hakuna namna Rais atamlinda Makonda na akabaki na sifa ya kuwa Rais anaesimamia haki na Usawa. Itafanya aonekane kama waliomizwa na ukali wake katika kusimamia sheria ni kwasababu hawakuwa na ukaribu nae na zaidi itafanya aonekane Rais wa kawaida sana kwa kulinda uovu kwa sababu za binafsi.Hivyo ukimya wa Rais unafanya dhamira yake ya uzalendo ihojike kwani sio kawaida yake.

"Mamlaka kama Sekretariet ya Maadili ya Uongozi ilipaswa kuwa imeshachukua hatua kuondoa wingu hili kwani kinachojadiliwa hapa mbali zaidi ya jinai pia kinahusu uadilifu wa Kiongozi(intergrity). ukimya wa taasisi hii ni mfano mbaya wa namna taasisi zinavopigwa ganzi pindi haki inapotakiwa kutendeka lakini inagusa maslahi ya Rais. huu ni uzoefu niliopata kuona hata kwenye sakata la Escrow.likitokea jambo ambalo Rais ana maslahi taasisi zetu zimekuwa nzito na kigugumizi kuchukua hatua ipasavyo.

"Chuo cha Uvuvi walichomsajili kwa cheti cha form4 ambacho anatuhumiwa kuwa sio chake pamoja na Chuo Kikuu ni taasisi ambazo mjadala huu unahusu heshima ya taasisi hizo. hivyo ilipaswa zijitokeze kuthibitisha au kukanusha. ukimya wao unaashiria hofu yao kwasababu kaguswa mtoto wa mfalme! Huu ni mfano mbaya kabisa kwa taasisi za taaluma kwamba zinaweza kuwa za hovyo kiasi hiki.

"Kibaya zaidi ni ukimya wa NECTA ambao ni mamlaka ya kutoa vyeti. sasa cheti kinachosumbua hapa ni cha form4 ambacho ni mali yao. lakn kwa woga wamekaa kimya kuficha ukweli na kuacha mjadala wa cheti uwe kati ya Askofu na RC na watanzania wakati wao ambao ni mamlaka sahihi kuondoa utata wamekaa kimya kwa hofu ya kugusa mtoto wa mfalme.. Hili ni fundisho la kwani nchi hii haiendelei kwasababu taasisi hizi haziko imara kutimiza majukumu yake kisheria bali zinafanya majukumu yake kwa kadiri ya mapenzi ya mteule wao."

Nay Wa Mitege 'Amlilia' Vanessa Mdee

$
0
0
Msanii wa muziki wa hip hop Nay wa Mitego amefunguka kwa kumpa pole mwanadada Vanessa Mdee ambaye anashikiliwa na jeshi la polisi kwa tuhuma za kutumia na kusambaza dawa za kulevya.

Muimbaji huyo alijisalimisha kwa jeshi la polisi siku 5 zilizopita baada ya kutajwa kwenye list ya RC Makonda ya watu wanaojihusisha na biashara ya dawa za kulevya na kutakiwa kujisalimisha polisi central kwajili ya mahojiano.

Rapper huyo ameonyesha kuguswa na tukio hilo lililomtokea muimbaji huyo wa wimbo Cash Madame huku akimtaka kuvumilia kwa yote yanayoendelea.

“Vanessamdee Sijui ulipo anzia, but mpaka apa ulipofikia umepambana sana. Nina imani mungu ndo aliye kufanyia wepesi mpaka kua #BrandKubwa na kupata hatua Ulizo nazo. Naamini Mungu Huyu Huyu ndiye atakae kufanyia Wepesi Kwenye yanayo kukabili ivi sasa. Amini izi ni Changa moto tu na ni Mapito ambayo Binadamu tunapitia kwenye Safari ya kuelekea kutimiza Ndoto zetu,” aliandika Nay Instagram.

Aliongeza, “I pray for you my friend Vanessa, naamini brand yako haiwezi haribika kirahisi kwa sababu umepambana sana ni wasichana wachache wenye kuweza ku-fight kama wewe. Mungu ata kusimamia uzidi kusonga mbele, Haya yata pita nina imani utakua strongZaidi. #CashMadame KeepItUp. Napenda kuona Wasichana wakifanikiwa kwa kufanya kazi kwa bidii #VannesaTheBrand wewe ni mwanamke wa shoka. Usiyumbishwe kuwa Mfano. Najivunia uwepo wako kwenye Game,”

Kimenuka CCM: Sophia Simba, Madabida wavuliwa uanachama........Emmanuel Nchimbi Kapewa Onyo Kali

$
0
0
Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake wa CCM taifa ambaye pia ni mbunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Sophia Simba na wenyeviti wa CCM wa mikoa minne wamefukuzwa uanachama wa chama hicho kwa madai ya ukiukwaji wa maadili ya chama

Mbali na maamuzi hayo, chama hicho pia kimewafukuza uanachama wenyeviti wanne wa mikoa ambao ni pamoja na Ramadhan Madabida (Dar es Salaam), Jesca Msambatavangu (Iringa), Erasto Kwilasa na Christopher Sanya (Mara).

Pia chama hicho kimetangaza kuwavua uanachama wenyeviti wake katika wilaya za Gairo, Babati Mjini, Kinondoni na Longido huku wengine wakipewa onyo kali huku.

Panga hilo pia limefika katika wajumbe wa NEC ambapo ndugu Ali Hera Sumaye kutoka Babati Mjini naye akifukuzwa uanachama na wengine kupewa onyo kali.

Maamuzi hayo yamefanywa katika kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa ya chama hicho (NEC) kilichokaa leo mjini Dodoma kuelekea mkutano mkuu maalum wa chama hicho utakaofanyika kesho JUmapili ya Machi 12, 2017.

Akizungumza na wanahabari mjini humo, Katibu wa Itikadi na Uenezi wa chama hicho, Humphrey Polepole ametaja maamuzi mengine kuwa ni kutoa onyo kali kwa mjumbe wake wa Kamati Kuu, Dkt. Emmanuel Nchimbi ambaye ni balozi wa Tanzania nchini Brazil, huku Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Dodoma, Adam Kimbisa akisamehewa

"Ndugu Kimbisa amesamehewa makosa baada ya kuomba radhi, kujirekebisha na kuwaongoza vyema wana CCM mkoa wa Dodoma kupata ushindi wa uchaguzi mkuu, Ndugu. Emmanuel Nchimbi amepewa onyo kali na anatakiwa kuomba radhi wanachama na uongozi wa CCM, tunajua huyu ni Balozi wetu Brazil, lakini ametakiwa afanye hivyo mara moja akiwa huko huko Brazil, na taarifa yetu ataipata" Amesema Polepole

Polepole amesema maamuzi hayo ni ya mwisho, na hayatakuwa na nafasi ya kukatiwa rufaa katika ngazi yoyote ya chama hicho.
Wajumbe wa Kamati Kuu ya CCM, Dkt. Emmanuel Nchimbi, Sophia Simba na Adam Kimbisa walipotoka nje ya kikao cha kamati hiyo wakati wa mchakato wa kumtafuta mgombea urais wa CCM katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2015

Bashe, Musukuma, Malima Watiwa mbaroni Kwa Kufanya Vurugu Katika Mkutano wa CCM

$
0
0
Wabunge Hussein Bashe wa Nzega Mjini na Joseph Kasheku wa Geita wakiwa na aliyewahi kuwa mbunge wa Kisarawe, Adam Malima wamehojiwa polisi na kisha kuachiwa baada ya kukamatwa kwa tuhuma za kupanga njama za kuvuruga mkutano mkuu wa CCM

Inaelezwa kuwa, wabunge hao ambao ni wajumbe wa mkutano mkuu maalum wa CCM, ambao unatarajiwa kufanyika kesho, Machi 12 mjini Dodoma walikuwa wakipanga njama za kuvuruga mkutano huo kwa kugawa pesa kwa baadhi ya wajumbe.

Kamanda wa Polisi mkoani Dodoma amethibitisha kukamatwa kwa wabunge hao, kwa ajili ya mahojiano, lakini amesema kuwa baada ya mahojiano, wabunge hao wameachiwa kwa dhamana baada ya kujidhamini wao wenyewe.

"Walikuwa wanahojiwa tu lakini kwa sasa wameshaachiwa, kulikuwa na tuhuma kwamba wanagawa hela wanapanga kuvuruga mkutano wa CCM, wamejidhamini wenyewe, na upelelezi bado unaendelea ili kubaini kama ni kweli" Amesema Kamanda Mambosasa

Kuhusu endapo watu hao walikutwa na pesa, Kamanda amesema mmoja kati yao amekutwa na pesa lakini akadai kuwa ni pesa zake kwa ajili ya matumizi binafsi.


Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumapili ya March 12

SORRY MADAM -Sehemu ya 39 & 40 (Destination of my enemies)

$
0
0
MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWAILIPOISHIA

ILIPOISHIA
“Moja, hakikisha kwamba unaurudisha uhai wa Eddy Godwin”
“Mbili ndani ya masaa 48, Eddy awe amerudi madarakani la sivyo bomu hili litaisambaratisha ikulu yako”
Simu hiyo ikakata, huku video iliyo kuwa inaonekana kwenye tv hiyo ikapotea na kubakisha mwanga wa bluu wa tv hiyo kubwa, watu wote waliomo ndani ya ofisi
hiyo wakabaki wakimtazama raisi Praygod azungumze kitu juu ya hilo.

ENDELEA
Jasho jingi likazidi kumwagika raisi Praygod, hakuwa na jambo la kuweza kuzungunza na wala hakuweza kutambua ni wapi alipo Eddy.
"Muheshimiwa Eddy si amesha kufa sasa itakuwaje?"
Mmoja wa wafanyakazi wake walinuuliza
"Yupo hai"
Kila mmoja akabaki akiduwaa, baada ya kulisikia hilo swala, raisi alipo ligundua hilo akakohoa kidogo.

"Endeleeni na kazi"
Akatoka ndani ya ofisi yake na kuelekea katika eneo lake la kulala, kichwani mwake akazidi kujiuliza ni nani aliye weza kuufanya mchezo huo kwani wataalamu wake walipo jaribu kutafuta ni eneo gani simu hiyo ya vitisho ni wapi ilipo tokea hawakuweza kuipata. Kitu kilicho zidi kumuumiza zaidi ni wapi alipo kuwepo mke wake kipenzi Shamsa, kwani inasadikika tangu atoke jana majira ya asubuhi kutokana na taarifa aliyo pewa, hakuweza kurejea kabisa hadi majira haya ya asubuhi.

Akafungua moja ya droo yake na kutoa vidonge viwili na kuvimeza pasipo hata kunywa maji, akavisukumiza kwa mafumba kazaa ya mate kisha akasimama mbele ya kioo kikubwa kilichopo mbele ya chumba chake na kujitazama uso wake ulio jaa wasiwask, iliyo changanyikana na hasira kali sana.

"EDDY, EDDY, EDDY"
Raisi Praygod alizungumza huku jazba ikizidi kuongezeka kifuani mwake. Taratibu akakisogelea kitanda na kujilaza, huku akihema taratibu taratibu.

***
Mwanga mkali wa jua ukaanza kupenya kwenye macho ya mtubaliye lala kitandani huku mwilini mwake akiwa amebakiwa na boksa tu. Akajaribu kunyanyuka kitandani ila maumivu makali ya paja yakamfanya kurudi tena kitandani. Kwa sekunde kadhaa akatumia kuchunguza kufahanu ni wapi alipo, ila ikawa ni swali gumu sana Kwakwe kuweza kufahamu alipo, kwani chumba hicho kimetawaliwa na mitambo mingi ya kushangza.

Kitanda alicho lalia pembeni yake kuna bomba lililo ning'inizwa dripu ya maji iliyo peleka mrija wake moja kwa moja hadi kwenye mkono wake wa kulia na kisindano kidogo kilicho weza kuunganishwa na mrja huo, kimeingia moja kwa moja kwenye mshipa wake wa damu.

"Hapa ni wapi?"
Alizungunza huku akijaribu kujikaza kunyanyuka, mguh wake ulio fungwa bandeji zilizo badikika rangi kutokana na dawa akiyo pakwa, ukazidi kumuuma.

Akiwa katika kutazama tazama mlango wa chumba hicho kikubwa kinacho onekana kwamba kipo juu ya gorofa kubwa, ukafunguliwa. Akaingia mwanaume aliye valia koti jeupe pamoja na miwani kubwa kiasi. Katika kumtazama kwa haraka haraka ni lazima utagundua kwamba mtu huyo ni daktari.
"Karibu tena duniani Mr Eddy Godwin"
Mtu huyo mwenye asili ya kizungu izungumza kiswahili sahihi kilicho mshangaza hata Eddy mwenyewe.

"Wewe ni nani?"
Lilikuwa ni swali la kwanza la Eddy huku akimkazia macho daktari huyo aliye zidi kupiga hatua kumfwata katika kitanda alicho lala.
"Kuna hofu ya kuhofia, mimi ni rafiki yako wa karibu. Naitwa dokta William"
Alizungumza huku akigeuza geuza dripu linalo endelea kushusha maji kwenye miishipa ya Eddy.

"Unajisikiaje?"
"Nina maumivu kwenye mguu. Kwanza hapa ni wapi?"
"Hapa upo Mosscow Russia"
"Nilifikaje hapa?"
Eddy aliiza huku akizidi kumkazia macho daktari huyo kwani jibu lake tayari lilianza kumpa wasiwasi mkubwa.
"Nilikutoa Tanzania siju chache za nyuma. Niweza kukufwatilia wewe kwa ukaribu mkubwa hadi nikafanikiwa kukupata"

"Ulinijuaje mimi?"
"Nilikujua kupitia mama yako, alikuwa ni rafiki yangu wa karibu sana. Kiufupi mama yako alikuwa ni mwema sana kipindi nilipo kuwa nikiifanya kazi ya kuwafundisha madktari wa jeshi nchini Tanzania.
"Usiwe na shaka kwani Tanzania ni moja ya nchi niliyo ipenda sana na ni nchi ambayo viongozi wake baadhi ni wakatili sana wakiongozwa na raisi Praygod"

Eddy akastuka kusikia jina jilo, katika kumchunguza chunguza dokta William kwa haraka haraka akatambua kwamba ni mtu ambaye hakuwa na nia mbaya sana kwake japo hakuhitaji kuliamini hilo kwa asilimia mia moja.
"Nil stori ndefu sana mimi na Tanzania pamoja na viongozi wake na sasa nipo katika mpango wa kuhakikisha kwamba nina lipa kisasi kwa nchi hiyo."

"Kwa nini unahitaji kulipa kisasi?"
Dokta William akaivua miwani yake taratibu, kwa mbali machozi yakawa yanamlenga lenga, hakuhitaji kuzungumza kitu cha aina yoyote. Akaondoka na kusimama kwenye moja ya mashine inayo ongozwa na kompyuta aina ya Laptop. Akaanza kuiminya minya batani zake kwa mwendo wa kasi akionekana kuseti baadhi ya vitu katika mtambo huo. Kila alivyo zidi kuminya batani za kumpyuta hiyo asira dhidi ya Tanzania hususani raisi Praygod zikazidi kumpanda mara dufu.
***

Kwa mwendo wa boti waliyo kuwa nayo, haikuwasaidia sana kuweza kupasua mawimba makubwa ambayo yanaendelea kuikumba bahari ya hindi mara mwa mara. Upepe mkali na wenye nguvu wa kuyumbisha hata meli kubwa ulizidi kuirusha boti hiyo waliyo panda Shamsa na Briton kutoka upande mmoja kwenda mwengine.

Halo hiyo kikaifanya boti hiyo kuzima gafla, hofu ya kufa ndani ya maji ikaanza kumtawala Shamsa ambaye kwa Mara kadhaa alionekana kumkumbatia Briton huku akilia sana. Alihisi hakuwa na bahati ya kuishi jwani familia yake aliyo kuwa akiitegemea tayari ilisha fariki kuanzia Eddy hadi mtoto wake Junio.

"Bray tunakufa mpenzi wangu"
"No hatuwezi kufa, tusonge Mbele"
Briton alizungumza huku akiendelea kujitahidi kuhakikisha kwamba boti huyo inasonga Mbele. Bahari ikazidi kuchafuka, hats akari ambao walikuwa doria katika maji waka waliamriwa kughairisha msako huyo kwank hali ilitisha sana. Mvua taratibu ikaanza kunyesha jambo lililio zidi kuwachanganya Briton na Shamsa. Radi zikaanza kutawala kila kona. Gafla boti yao ikabenuliwa na kuzamishwa ndani ya maji, kila mmoja akaangukia upande wake. Hali ikazidi kuwa mbaya kwani radio, mawimbi Na upepeo vikazidi kuongezeka kadri ya muda ulivyo zidi kwenda ndivyo ikawa afadhali ya dakika moja nyuma.

Kila mmoja alijikuta akiwa katika upande wake, baridi kali ikazidi kuunynyasa mwili wa Shamsa, maumivu makali ya tumbo yakarejea gafla mwilini mwa Shamsa na kumfanya aanze kuishi wa nguvu, dakika kadhaa mbeleni akapoteza fahamu.
***
Hali ya usalama ikazidi kuimarishwa maeneo mbali mbaali ndanj na nje ya jiji la Dar es Salaam. Wanaanchi kupitia katika vyombo vya habari. Video, redio na magazetini raisi Praygod akatangaza hali ya usalama katika maeneo yote yanchi, akiendelea kuwahakikishia kwamba hakuto kuwa na jambo lolote bays litakalo weza kujitokeza. Wanaanchi pamoja na wafanya biashara wakarudi katika maeneo yao ya kazi.

Kitu kilicho zidi kimchanganya raisi Praygod ni wapi alipo mke wake kipenzi Rahab. Msako wa kuhakikisha kwamba mke wa raisi anapatikana ukazidi kuendelea.

Kwa siku ya pili mfululizo hapakuwa na askari akiye weza kulaza kichwa chake kwenye kitanda chake kama ilivyo siku za nyuma. Kuanzia wakuu wa majeshi hadi waliopo ngazi za chini, kazi ikawa ni kuhakikisha kwamva mke wa raisi anapatikana. Hapakuwa na mtu mwenye wazo la kujua kwamba mke wa raisi yupo kwenye pango ambalo lilitumiwa Na waasi wanawake ambao kwa sasa baadhi yao wapo katika mikono ya wamarekani.
"Madam tutaendelea kukaa humu hadi lini?"
"Hadi siku ambayo nitaamua mimi kutoka ndani ya handaki hili"

"Ika utakuwa unampa wasiwasi muheshimiwa raisi"."Nalitambua hilo ila sinto hitaji kurudi ikulu hadi nihakikishe ninampata Eddy, iwe kwa kuua au kufanya lolote ni kuhakikisha kwamba tunampata Eddy"
Priscar hakuwa na kitu chochote cha kuzungumza zaidi ya kuyasikiliza matakwa ya bosi wake.
"Ila kuna kitu kimoja nahitaji tuweze kukifanya kwa pamoja"
"Kitu gani madam"
"Nilazima kuhakikisha kwamba tunapata pesa tena pesa ya kutosha"

Bashe: Sina Hofu Ya Kutimuliwa CCM

$
0
0

Mbunge wa Nzega Mjini Hussein Bashe amefunga mazito leo asubuhi kuhusiana na sakata la timua timua linaloendelea dhidi ya wanachama wasaliti ndani ya CCM huko Jijini Dodoma katika Mkutano Mkuu Maalum wa CCM.

Mbunge huyo amesema hawezi kuwa na hofu ya aina yeyote kwa kuwa hana jambo baya alilolifanya ndani ya chama hicho hivyo hawezi kuteteleka na wanaotimuliwa wanachama.

“Sina hofu na timua timua ya wanachama wasaliti kwasababau naamini wamefanya maamuzi kwa kupitia mchakato ndani ya chama, kwa hiyo sina hofu kwasababu chama chetu kinaongozwa na katiba pamoja  na kanuni zilizopo unakuwa na hofu pale unahisi kuna jambo umelifanya kinyume na taratibu”-Alisema Bashe

Kwa upande mwingine Mbunge huyo amegoma kuzungumzia sakata la yeye kushikiliwa na Jeshi la Polisi hapo jana na kusema suala hilo kamuachia Katibu Mkuu wa chama hicho ndugu Abdurahaman Kinana.

Umoja wa Mataifa waingilia kati sakata la kupotea kwa Ben Saanane

$
0
0
Sakata la kupotea kwa mkuu wa Idara ya Sera na Utafiti wa Chadema, Ben Saanane limechukua sura nyingine baada ya Umoja wa Mataifa (UN) kusema upo tayari kutuma watu nchini kwa ajili ya uchunguzi.

Saanane, ambaye pia ni msaidizi wa mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, alipotea katika mazingira ya kutatanisha Novemba 18 mwaka jana na hadi sasa haijaeleweka kuwa alitekwa au kuuawa, ingawa Chadema imehusisha kutoweka kwake na taarifa ambayo Saanane aliitoa kwenye mitandao ya kijamii kuhusu utata wa elimu ya baadhi ya viongozi.

Siku chache baada ya kupotea kwa Saanane, Mwanasheria Mkuu wa Chadema, Tundu Lissu aliitaka Serikali kueleza kama inamshikilia kada huyo au ifanye uchunguzi wa kina kuhusu kupotea kwake.

Sanjari na hilo, Lissu aliitaka Serikali kufuatilia ujumbe wa vitisho ambao Saanane aliwahi kutumiwa kwenye simu yake ya mkononi na mtu ambaye bado hajafahamika.

Akisisitiza msimamo wa chama chake, Lissu alizitaka mamlaka zote husika na usalama wa raia ziseme hali halisi inayozingira sintofahamu ya mahali alipo, ikiwa yuko ndani ya nchi au nje, au hata kama amefariki na kuzikwa kwa kutotambuliwa.

Wakati utata huo ukiendelea, ofisi ya kamishna mkuu wa haki za binadamu duniani ya UN yenye makao yake makuu jijini Geneva, Uswisi, imesema iko tayari kutuma timu ya uchunguzi.

Uamuzi huo ulifikiwa katika mkutano uliotishwa na ofisi hiyo, Kanda ya Afrika uliohusisha nchi za Sudan, Rwanda, Burundi, Kenya, Uganda, Ethiopia, Djibouti na Tanzania.

Jana, mkurugenzi wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Dk Hellen Kijo- Bisimba alisema suala hilo liliibuka baada ya wajumbe wa mkutano huo kutaka kujua undani wa sakata hilo, lakini hakukuwa na taarifa za kina.

“Wajumbe walionyesha kuguswa na suala la mtu kupotea katika mazingira ya utata na kutaka tuelezee kwa undani ilivyokuwa. Hatukuwa na taarifa za kina hivyo wakasema wako tayari kulifanyia kazi endapo tutatuma urgent alert,” taarifa ya dharura.

“Taarifa tutakayotuma ndiyo itakayowawezesha wao kutuma timu ya uchunguzi ije hapa baada ya hapo watajua ni kitu gani waseme kwa Serikali.”

Dk Bisimba alieleza kuwa bado taarifa hiyo haijaandikwa kutokana na kuwasubiri ndugu wa Saanane ambao wanatakiwa kutoa maelezo kwa kina.

“Tuliwaambia ndugu zake waje tupate maelezo yatakayotuwezesha kuandika hiyo urgent alert,  lakini bado hawajaja. Watakapofika tutaandika na kuituma ili uchunguzi ufanyike.”

Alipotafutwa kuhusu maendeleo ya uchunguzi wa suala hilo, Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai(DCI), Kamishna Robert Boaz alisema: “Nitafute Jumatatu kwa sasa nipo kwenye kikao.”

Magufuli: Hatuna Muda wa Kumbembeleza Mtu Kukichangia Chama Chetu

$
0
0
Mwenyekiti wa CCM, Rais Dk John Magufuli amesema chama hicho hakitambembeleza mtu kukichangia katika shughuli mbalimbali.
 
Akihutubia mkutano Mkuu wa CCM unaofanyika leo Dodoma, Dk Magufuli amewaambia wajumbe wa mkutano huo kuwa kwa miaka yote CCM kimekuwa kikiomba hata kwa watu ambao hawastahili.
 
“Matokeo yake wamekuwa wakitumia nafasi hiyo kudhalilisha. Hakuna tena omba omba hatutaki kumbembeleza mtu akitaka kutuchangia atuchangie,”amesema.
 
Amesema kuwa chama hicho kina utajiri unaokiwezesha kujitegemea na kwamba mwanachama atakayetumia mali za chama kwa maslahi binafsi atachukuliwa hatua kali.

Ukumbi mpya wa CCM wapewa jina la Kikwete

$
0
0
Wajumbe wa Mkutano Mkuu Maalum wa CCM wamekubaliana kuita ukumbi mpya uliopo eneo la Dodoma Makulu ‘Kikwete Hall’.
 
Makubaliano hayo yametokana na Mwenyekiti wa Taifa wa CCM Rais Dk John Magufuli kupendekeza kwa wajumbe hao ukumbi huo uitwe Kikwete.
 
“Leo tumekaa katika ukumbi huu mzuri kuna watu wamefanya kazi na miongoni mwao atakuwa ni Mzee wetu Jakaya Kikwete (Rais Mstaafu wa awamu ya nne). Mtakumbuka kabla ya hapa tulikuwa tukikaa kule yanatolewa magunia tunakaa,”amesema.
 
Wajumbe hao walikubaliana na wazo hilo na baadaye Rais Magufuli walishikana mkono na Rais Kikwete.

Wajumbe wa CCM wapitisha mabadiliko ya Katiba ya CCM

$
0
0
Wajumbe 2,356 wa Mkutano Mkuu Maalum wa CCM leo wamepitisha mabadiliko ya Katiba ya CCM kwa kauli moja chini ya Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dkt. John Pombe Magufuli

Mabadiliko hayo ya CCM yamelenga katika maeneo matatu makuu ikiwa ni pamoja na Katiba ya Chama Cha Mapinduzi, Kanuni za Uchaguzi za CCM pamoja na Kanuni za Jumuiya (UWT, UVCCM na Wazazi)

Kwa upande wa Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi amedai kuwa kumekuwa na upotoshaji mkubwa ukiendelea kuwa mabadiliko hayo yanafanywa kwa kumlenga mtu au kundi fulani la watu na kusema huo si kweli bali wanafanya mabadiliko hayo kwa lengo la kukijenga chama.

Mbali na hilo Mwenyekiti wa CCM Dkt. John Pombe Magufuli aliweka wazi lengo kuu la mabadiliko hayo ni pamoja na kuimarisha chama chao na kukufanya kiendelee kutawala na kufanya vyema siku hadi siku.

“Mabadiliko yanalenga kuboresha mfumo na muunda wa chama chetu, wa sasa una mapungufu mengi utakuta watendaji wanafanya majukumu yanayofanana na kugongana kimaamuzi, pia kuliibuka vyeo vilivyo na nguvu, watu walivitumia kwa maslahi yao binafsi japokuwa kikatiba havipo”. Alisema Magufuli

Aidha Mwenyekiti huyo alitoa onyo kali kwa mamluki yeyote atakajitokeza kuharibu mchakato huo kwa namna moja ama nyingine na kusema adhabu kali dhidi yake itachukuliwa.

Askofu Gwajima amshambulia tena Makonda

$
0
0
Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima ametaja makosa ya kisheria yaliyomfanya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,Paul Makonda kukimbilia Afrika Kusini.

Akizungumza leo kanisani kwake, Ubungo, jijini hapa, Gwajima alidai  kosa la kwanza la Makonda ni kughushi cheti ambacho kinaonyesha yeye ni Paul Makonda wakati akifahamu kuwa yeye ni Daudi Bashite.

“Kosa hilo kwa mujibu wa Gwajima ni kifungo cha miaka saba.Kosa jingine ni kula kiapo cha ukuu wa wilaya na ukuu wa mkoa akisema yeye ni Makonda wakati akijua yeye ni Bashite,” alisema

Gwajima alisema  kosa la hilo la kula kiapo na cheti feki  ni kifungo cha miaka mitatu.

Kosa jingine  alisema ni kupokea mshahara na posho kwa jina la Makonda wakati akifahamu si yeye   na kuongeza kuwa kosa hilo likithibitika atatakiwa kurudisha mishahara na posho zote alizochukua.

==>Tazama Video ya Mahubiri yake hapo chini

Vigogo wa CHADEMA watimkia CCM. Yumo pia msaidizi wa Mbowe

$
0
0
Wakati Mkutano Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) ulipokuwa ukiendelea mkoani Dodoma, baadhi ya waliokuwa wachama na viongozi wa ngazi za juu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) pamoja na ACT-Wazalendo wamepokelewa rasmi na CCM baada ya kutangaza kujiunga na chama hicho.

Viongozi hao waliojiunga na CCM leo wamesema sababu kubwa iliyopelekea na kufikia uamuzi huo ni utendaji kazi wa Rais na Mwenyekiti wa CCM, Dkt John Pombe Magufuli.

Miongoni mwa wengi waliopokelewa leo ni pamoja na, Moses Machali Mbunge wa zamani wa Kasulu Mjini kwa tiketi ya NCCR- Mageuzi na baadae kuahimia ACT Wazalendo. Alitangaza kujiunga CCM Novemba mwaka jana ambapo leo amepokelewa rasmi. Dkt Yared Fubusa, Aliyekuwa Mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA Mkoa wa Kigoma na Mgombea Ubunge jimbo Kigoma Kaskazini (CHADEMA).

Mwingine ni aliyetangaza kujiunga na CCM na kupokelewa na Mkutano Mkuu leo ni, aliyekuwa Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Said Arfi.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatatu ya March 13


Jinsi Ya Kuandaa Na Kutayarisha Lishe Maalumu Kwa Wanaume Wenye Tatizo La Ukosefu Na Upungufu Wa Nguvu Za Kiume

$
0
0
 Ukosefu  na/au   upungufu  wa  nguvu  za  kiume  ni  tatizo  linalo wakabili  mamilioni  ya  wanaume  duniani. 

Kufahamu  mambo  yanayo  sababisha  tatizo  la  ukosefu/ upungufu  wa  nguvu  za  kiume, dalili  za  mwanaume  mwenye  tatizo  la  ukosefu na/ama  upungufu  wa  nguvu  za  kiume, viashiria  vya  tatizo  la  ukosefu/upungufu  wa  nguvu  za  kiume, athari za  tatizo  la  ukosefu  na  upungufu  wa  nguvu  za  kiume, tafadhali  tembelea : http://neemaherbalist.blogspot.com/2015/07/uhusiano-kati-ya-damu-na-tatizo-la.html

LISHE  MAALUMU  KWA WANAUME  WENYE  TATIZO  LA  UKOSEFU NA/AMA  UPUNGUFU  WA  NGUVU  ZA  KIUME
Hii ni  Tiba-Lishe  maalumu  kwa  wanaume  wenye  kusumbuliwa  na  tatizo  la  ukosefu na  upungufu  wa  nguvu  za kiume. Tiba –lishe  hii  inajumuisha  vyakula,matunda, mimea mbalimbali, pamoja  na  dawa  ya  asili  iitwayo  Jiko.
 
JINSI  YA  KUANDAA  NA  KUTAYARISHA  LISHE  MAALUMU  KWA  WANAUME  WENYE  TATIZO  LA  UKOSEFU NA /AMA  UPUNGUFU  WA  NGUVU  ZA  KIUME
 
Mahitaji
1.     Dawa  asilia  ya  Jiko
2.     Juice  ya msafisha  tumbo
3.     Supu  ya  nyanya  chungu
4.     Vitunguu  swaumu/vitunguu maji
5.     Juice  ya  rozera
6.      Vumbi la Kongo ( Congo Dust )
7.     Pink salt   ( Chumvi  ya pinki ) au  Himalayan Salt
8.     Pilipili manga

MAANDALIZI , MATAYARISHO  NA  MATUMIZI
Jinsi  Ya  Kuandaa, Kutayarisha  na  Kutumia  dawa asilia ya  Jiko.

Chukua  vijiko  vidogo   viwili  vyenye  dawa  ya jiko, kisha  tia  kwenye  kikombe chenye  maji  ya  moto  ambacho  ujazo  wake  ni  milimita  mia  mbili  hamsini ( 250mills ). Iache  kwa  kama  dakika  kumi, kisha  koroga  halafu  tumia  kunywa pamoja  na  machicha  yake. Utafanya  hivyo  mara  mbili kwa  siku, asubuhi  na  jioni  kwa  muda  wa   siku  thelathini. 
 
AU  Chukua  vijiko  vidogo  viwili  vyenye  dawa  yako  halafu chemsha  pamoja  na  maji  robo  lita  hadi itokote kabisa, kisha  ipua  halafu  tumia  kunywa  dawa  pamoja  na  machicha  yake. Utafanya  hivyo  mara  mbili  kwa  siku, asubuhi  na  jioni  kwa muda  wa  siku  thelathini

VUMBI  LA  CONGO ( CONGO DUST ) :   Katika  kipindi  cha  siku  thelathini  za  matumizi  ya  tiba  asilia  ya  Jiko. Unashauriwa  kutumia  vumbi  la  congo  walau  mara  moja  kwa  wiki  kwa  muda  wa  wiki nne. Yani  wiki ya  kwanza, utumie  mara  moja, wiki ya  pili  utumie  maara  moja, wiki  ya tatu  utumie  mara  moja, na  wiki  ya  nne  utumie  mara  moja.

MATAYARISHO   NA   MATUMIZI  YA  VUMBI  LA  CONGO
Chukua  dawa  yako  kiasi  cha kujaa  kwenye  kidole, kisha changanya  kwenye  mafuta  ya  kujipaka  halafu  tumia  kupaka  kwenye  kichwa  cha  uume  wako.  Utafanya  hivyo, nusu  saa  kabla  ya  kushiriki  tendo  la  ndoa.

LISHE   MAALUMU   YA   KUTUMIA   PAMOJA   NA   DAWA   YA   JIKO
Pamoja  na  dawa  ya  Jiko, unashauriwa  kutumia  lishe  maalumu  kama  ifuatavyo:

1.     SUPU   YA  NYANYA  CHUNGU  AMA  NGOGWE : Unashauriwa  kutumia  supu  ya  nyanya  chungu  mara  mbili  kwa  siku  asubuhi  na  jioni kwa  siku thelathini.

Mahitaji :    
·Robo  kilo  ya  nyanya  chungu  (  Tumia nyanya chungu  zenye  rangi  ya  kijani kwani  ndio  zenye  virutubisho  vinavyo hitajika.
·Nusu  kijiko  kidogo  cha  chumvi  ya  pinki  (  Pink  Salt), au  Himalayan  salt  pamoja  na  maji  lita  mbili.  (  Kama  utakosa  hizo  chumvi  utatumia   nyanya  chungu  peke  yake  bila kuongeza  chochote  )

Matayarisho :  Baada  ya  kuziosha  nyanya  zako  bila  kutoa  vikonyo vyake, ziweke  kwenye  maji  kiasi  cha  lita  mbili, ndani  ya  maji  hayo ongeza  nusu  kijiko  kidogo  cha  chumvi  ya  pink, au  Himalayan Salt  ( Kama  hauna  hizo  chumvi   chemsha nyanya  zako  peke  yake  bila  kuchanganya  na  chochote), kisha  chemsha hadi  itoe  supu. Baada  ya  hapo, ipua kisha  tumia  kula  supu  yako  pamoja  na  kutafuna  nyanya  chungu  zote   ulizo  chemsha.  

Utafanya  hivi  mara   mbili   kwa  siku,asubuhi  na  jioni  kwa  muda  wa  siku thelathini.  Asubuhi  utatumia  muda  wwowote  kati  ya  saa  kumi na  mbili  alfajiri  na  saa nne  asubuhi  na  usiku  utatumia  muda  wowote  kati  ya  saa  moja  usiku hadi  saa  nne  usiku. )

N.B :KABLA  YA  KUTUMIA  SUPU  YA NYANYA  CHUNGU,  WEKA  TOFAUTI  AMA  INTERVAL  YA DAKIKA  KUMI   HADI  KUMI  NA  TANO TANGU UMETUMIA  DAWA  YA  JIKO. KWA MFANO  KAMA  UMETUMIA  DAWA  YA  JIKO  SAA  MBILI  KAMILI,ASUBUHI,  BASI  SUPU  YA  NYANYA  CHUNGU  ITUMIE  SAA  MBILI  NA  DAKIKA  KUMI AU  NA  DAKIKA  KUMI  NA  TANO . UTAFANYA VIVYO   HIVYO   WAKATI WA  USIKU.

Pia  kama, utakosa  nafasi  ya   kuchemsha  nyanya  chungu, basi unashauriwa  kutafuna  nyanya  chungu  zikiwa  mbichi  pamoja  na  maji  ya  uvugu  vugu  lita  moja  na  nusu, mara  mbili  kwa  siku  asubuhi na  jioni  kwa  muda  wa  siku  thelathini.

3. JUICE  YA  ROZERA :  Unashauriwa  kutumia  juice  ya Rozera  mara kwa  mara, kila  upatapo  nafasi.. Unashauriwa  kutumia  lita  moja  hadi  mbili  ya juice  ya  Rozera kila  siku  kwa  muda  wa  siku  thelathini  mfululizo. Unatakiwa kutumia  lita  hiyo  moja  ya  juice  ya   Rozera  kwa  wakati  mmoja. Kama  ni mchana  utakunywa  lita nzima  ya  juisi  ya  Rozera, na  kama  ni  jioni, utakunywa  lita  nzima  ya  juisi ya  Rozera. Unatakiwa  kuinywa  bila  ya  kuchanganya na  kitu  chochote  kile. Na  muda  mzuri  wa  kuinywa, ni  kati  ya  saa  sita mchana     hadi  saa  saa  2   kamili  usiku.

Matayaraisho  Ya  Juice  Ya  Rozera :  Chukua  vijiko  vikubwa  vinne  vya  rozera  iliyo kaushwa, kisha  loweka  kwenye  maji  lita  mbili, iache  kwa  muda wa  dakika  thelathini, kisha  chemsha  hadi  itokote.  Itakapo tokota, ipua, chuja, makapi  weka  pembeni, baki  na  juisi  yako ambayo  utaitumia  kwa  kunywa  yote . Utafanya  hivyo  mara  moja  kwa  siku  kwa  muda  wa  siku  thelathini. Unaweza  kuinywa  ikiwa  ya  moto, ama  ikiwa  imepoa. Ila vizuri zaidi  uinywe  ikiwa ya  moto.

4.  JUICE  YA  MSAFISHA TUMBO : Unashauriwa  kunywa  walau  lita  moja ya  juisi  ya  dawa  asilia  ya  MSAFISHA TUMBO mara  moja  kwawiki  katika  kipindi  cha  wiki  nne utakazo  kuwa  unatumia  dozi ya  dawa  ya  Jiko.   Hii  ina  maana  kuwa  ndani  ya  wiki  nne  za  dozi  ya  Jiko,  utatumia  lita  nne  za  juisi  ya  Msafisha  Tumbo, lita  moja  kila wiki, kwa  muda  muda  wa  wiki  nne.

Matayarisho  Ya  Juisi  Ya  Msafisha  Tumbo:  Chukua  vijiko  vitatu  vidogo  vyenye  dawa  ya msafisha  tumbo,,  kisha  weka  kwenye  lita  moja  ya  maji, halafu chemsha  hadi  itokote, ikisha  tokota, ipua  chuja, makapi  weka  pembeni, ubaki  na  juisi  yako  ambayo  utaitumia  kwa  kunywa  yote. Unatakiwa  kuinywa  ikiwa  ya  moto  na  muda  mzuri  wa  kuinywa  ni  saa  kumi  na  mbili  jioni.

5.  VITUNGUU  MAJI  NA  VITUNGUU  SWAUMU:  Katika  kipindi  chote  utakacho  kuwa  unatumia  dozi  ya  dawa  ya  Jiko, unashauriwa  kutumia  kwa  wingi sana, vitunguu  maji  na  vitunguu  swaumu.

NJIA  ZA  KUTUMIA  VITUNGUU  MAJI  NA  VITUNGUU  SWAUMU
Zipo njia  kuu tatu  za  kutumia  kitunguu  maji  na  kitunguu  swaumu  kama lishe  maalumu  kwa  mwanaume  anaye  tumia  tiba  ya  ukosefu  na  upungufu  wa  nguvu  za  kiume.

A. MCHANGANYIKO   WA   JUICE  YA  KITUNGUU  MAJI  NA  KITUNGUU  SWAUMU
Unashauriwa  kutumia  mchanganyiko  huu, walau  mara  moja  kwa  wiki.Lakini  kama  utaweza  kutumia  mara  mbili  au  tatu  kwa  wiki, sio mbaya  pia.
 
Mahitaji :   Kitunguu  swaumu  kiasi  ha  robo  kilo, kitunguu
maji  robo  kilo.
Matayarisho :  Blend au  saga  robo  kilo  ya  kitunguu  swaumu kupata  juisi  yake. Ukisha  saga, weka  juisi  yako  kwenye  sufuria
safi.  

Kisha  saga  robo  kilo  ya  kitunguu  maji  kupata  juisi
yake, ukisha  pata  juisi  ya  kitunguu  maji, changanya  pamoja  na ile  juisi  ya  kitunguu  swaumu  halafu  chemsha  hadi  itokote.
 
Ikisha  tokota, ipua  iache  ipoe.  Ikisha  poa  tumia  kunywa
mchanganyiko  wako  wote. Utakunywa  mara  moja  tu  kwa  siku.
 
Kama  utapenda, unaweza  kuchanga  na  asali  robo  lita  na  kuchemsha pamoja, kisha  ikisha  tokota, ipua  iache  ipoe  na  utumie  kunywa.

B.  KACHUMBARI   YA   KITUNGUU  MAJI  NA  KITUNGUU  SWAUMU
Chukua    vitunguu  maji  vikubwa vinne, kisha  vimenye  na  kuvikata  kata, kama  vitunguu  vya kachumbari. Halafu  chukua  punje  kumi  na  sita  za  vituu  swaumu, vikate  kate  na  uvichanganye  pamoja  na  vitunguu  maji  ulivyo vikatakata.   

Tumia  kula  mchanganyiko  wako  wote. Utafanya  hivyo mara  moja  tu  kwa  siku. Unaweza  kuongeza na  chumvi  ya  kawaidakidogo  kama  utapenda.  Tumia kachumbari hii  mara  nyingi  kadri  utakavyo  weza.
MENGINEYO

  Kama  ni  mtumiaji  wa  chai, penda  sana  kutumia  chai  iliyo ungwa  kwa  pilipili  manga  na  tangawizi.  Na  kama  unaatumia  uji, penda  sana  kutumia  uji  ulioungwa  kwa  pilipili  manga

 Jenga  mazoea  ya  kutumia  nyanya  chungu  katika  kila  mlo  wako. Kwa  mfano, kamaunakulala  ugali  na  nyama, basi  nyanya   chungu  pia  ziwepo  pembeni ( NYANYA  CHUNGU  ZINAZO HITAJIKA  HAPA  NI  ZILE  ZENYE  RANGI  YA  KIJANI KIBICHI )
 
vi.  Jenga  mazoea  ya  kuwa  unajumuisha  kitunguu  swaumu  kwenye  mlo  wako. Nyanya  chungu  iwe  kiungo  kisicho  kosa  katika  mlo  wako. Mfano, kama  unakula  ugali  na  nyama, basi  katika  mchuzi  ya  mboga  yako, kitunguu  swaumu  kiwe miongoni  mwa  viungo.

Kwa mahitaji  yako ya  dawa  ya  JIKO  pamoja  na  vumbi  la  kongo, wasiliana  na NEEMA  HERBALIST, duka  la  kuuza  dawa  mbalimbali  za  asili. Tunapatikana  Ubungo  jijini  Dar  Es  Salaam, jirani  na  SHULE  YA  MSINGI  UBUNGO   NATIONAL  HOUSING, nyuma  ya  jengo  la  UBUNGO  PLAZA.
 
Kwa  wateja  waliopo  jijini  Dar  Es  Salaam, wasio na  muda  au  nafasi  ya  kuja  ofisini  kwetu  Ubungo, tunayo  huduma  ya  kuwafikishia  dawa  mahali  walipo ( HOME & OFFICE  DELIVERY)
 
Kwa wateja  waliopo  nje  ya  mkoa  wa  Dar  Es  Salaam, watatumiwa  dawa  kwa  njia  ya usafiri  wa  mabasi mbalimbali. Wateja  waliopo  Zanzibar  watatumiwa  dawa  kwa  njia  ya  usafiri wa  boti, wateja waliopo  Nairobi  watatumiwa  dawa  kwa  mabasi  ya  DAR EX PRESS, wateja  waliopo  MOMBASA  watatumiwa  dawa  kwa  mabasi  ya  TAHMEED, na  wale  wa ughaibuni  watatumiwa  dawa  kwa  njia  ya  POSTA  au  DHL.

WASILIANA  NASI  KWA  SIMU NAMBA  0766 53 83 84.

Na  kwa  taarifa  zaiddi  kuhusu  huduma  zetu, tutembelee  kila  siku kwenye  blogu yetu:

www.neemaherbalist.com

Lowassa Akawaribisha UKAWA Kina Sophia Simba Waliovuliwa Uanachama CCM

$
0
0
Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa, amekaribisha waliokuwa wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), akiwamo aliyekuwa Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake (UWT), Sophia Simba kujiunga na Vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa).

Lowassa ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), aliyasema hayo jana katika taarifa yake.

Alisema  wanachama hao walikuwa  mashujaa wa kutetea haki, demokrasia na taratibu kwa kupinga dhuluma ndani ya chama chao cha CCM.

“Nafsi yangu imenisukuma kushika kalamu na kuandika haya kutokana na kile kilichotokea Dodoma katika vikao vya CCM.

“Ni takriban miezi 20 sasa toka nilipojitoa  CCM, lakini nasikia bado naendelea kutajwatajwa huko katika vikao vyao.

“Wamewatimua wanachama na viongozi wao ambao wengi wao walitumia demokasia yao kupinga upindishwaji wa kanuni na sheria za chama chao.

“Nataka kuwaambia kuwa wakati wakifanya hivyo walikuwa mashujaa wa haki na demokrasia na misingi ya utawala bora nchini,” alisema Lowassa katika taarifa yake

Mjumbe huyo wa Kamati Kuu alisema   wanachama hao wa CCM walisimamia kile walichokiamini bila ya kuvunja sheria, wamekata minyororo ya unyonge na uonevu.

“Mbegu ile waliyoipanda itamea na kuzaa matunda demokrasia ya kweli nchini kwetu.

“Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere aliwahi kusema kwamba upinzani wa kweli utatokea CCM, naamini usemi huo sasa unatimia kwa kasi kubwa.

“Nawakaribisha Chadema na Ukawa kwa jumla huku kuna maisha mazuri sana, hakuna minyororo ya utumwa wa siasa. Kilichowapata ni sawa na kumpiga chura teke unamuongezea kasi tu.

“…waje wajiunge nasi katika safari ya kuleta demokrasia ya kweli na siasa zenye ukomavu, safari hii inahitaji umoja na mshikamano kufikia malengo,” alisema.

Lowassa alisema anashangazwa na namna hatua ya CCM kujinasibu kuwa CCM ikiyumba.

Alisema nchi itayumba lakini anaamini  kinachotokea  na jinsi CCM inavyoyumba  ndivyo wananchi wanavyozidi kukomaa katika siasa na kuimarika katika harakati za kutafuta mabadiliko ya kweli.

Alisema Watanzania wa sasa hawawezi tena kuvumilia ukandamizaji wa haki zao za msingi unaofanywa na watawala.

“Nidhamu ya woga haina tena nafasi katika kujenga nchi yenye  kuheshimu misingi ya haki demokasia na utawala bora,” alisema.

Juzi, CCM kilitangaza kuwafukuza wanachama wake 12, akiwamo Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake (UWT), Sophia Simba, ambaye wiki iliyopita alitangaza kutogombea tena nafasi hiyo.

Wengine waliofukuzwa ni wenyeviti mikoa ambao ni Jesca Msambatavangu (Iringa), Erasto Kwilasa (Shinyanga), Ramadhan Madabiba (Dar es Salaam) na Christopher Sanya (Mara).

Waliofukuzwa wengine  ni Willfred ole Mollel ambaye ni Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Arusha Mjini, mjumbe wa NEC wa Wilaya ya Babati Mjini, Ally Sumaye na Mathias Manga wa Wilaya ya Arumeru.

Katika orodha hiyo pia wamo wenyeviti wa wilaya wa chama hicho ambao ni Omari Awadhi (Gairo), Ally Msuya (Babati Mjini), Makolo Laizer (Longido) na Salumu Madenge (Kinondoni-Dar es Salaam).

Wanachama wengine waliochukuliwa hatua baada ya kufanya makosa kama hayo kuwa ni Balozi Dk. Emmanuel Nchimbi ambaye amepewa onyo kali na anatakiwa kuomba radhi.

Wakati Nchimbi akipewa onyo, Adam Kimbisa ambaye ni Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Dodoma na Mbunge wa Afrika Mashariki   amesamehewa.

Kutokana na uamuzi huo Sophia atalazimika kupoteza ubunge.  Ilielezwa kuwa amefukuzwa baada ya kupatikana na makosa ya maadili kinyume na Katiba na kanuni za chama hicho.

Rais Magufuli Atuma Salamu Za Rambi Rambi Kufuatia Kifo Cha Balozi Sir George Kahama ( mmoja wa Waasisi wa Taifa)

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli, ametuma salamu za rambirambi kwa familia ya mmoja wa Waasisi wa Taifa na Waziri Mstaafu Bw. George Kahama kufuatia kifo cha kiongozi huyo kilichotokea  tarehe 12 Machi, 2017.

Bw. George Kahama amefariki dunia akiwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili Jijini Dar es Salaam alikokuwa akipatiwa matibabu.

Katika Salamu zake Mhe. Rais Magufuli amesema Taifa limempoteza mmoja wa watu waliotoa mchango mkubwa katika kupigania uhuru, maendeleo na ustawi wa jamii ya watanzania akiwa katika nyadhifa mbalimbali za uongozi hususani kuwa miongoni mwa Mawaziri katika Baraza la kwanza la Mawaziri ambapo alishika wadhifa huo kwa awamu tatu za uongozi wa Tanzania.

“Sir George Kahama alikuwa kiongozi shupavu, mzalendo, mwanasiasa mahiri, aliyewapenda Watanzania na aliyejitoa kushirikiana na viongozi wenzake akiwemo Baba wa Taifa Hayati Mwl. Julius Kambarage Nyerere kupigania uhuru, kujenga misingi ya Taifa likiwemo Azimio la Arusha, kujenga misingi ya uchumi wa ujamaa na kujitegemea na mengine mengi, kwa hakika hatutamsahau”

“Japo kuwa Sir. George Kahama ametangulia mbele za haki, sisi viongozi tuliopo tutamuenzi kwa kuhakikisha tunaendeleza juhudi za kuipigania Tanzania aliyoshiriki kuijenga, na pia tunamuombea kwa Mwenyezi Mungu aipumzishe roho yake mahali pema peponi, Amina” amesema Mhe. Rais Magufuli katika salamu hizo.

Pamoja na familia ya Marehemu Bw. George Kahama, Mhe. Dkt. Magufuli amewapa pole nyingi wanachama wote wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Wabunge, Ndugu, Jamaa na Marafiki wote walioguswa na msiba huo.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dodoma

Gwajima Ajitosa Sakata La Vanessa Mdee...

$
0
0
Askofu Gwajima bado hajamsameha Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda.Akizungumza jana mbele ya waumini wa kanisa lake, Gwajima alisema:

"Sasa hapo ndio najiuliza, polisi na uhamiaji waseme kwanini wanasuasua na kuna makosa niliyoyataja angalau saba ya jinai wakati wengine wamelala ndani kwa kuhisiwa tu wakiwemo wanamuziki kwa mfano Vanessa Mdee.

"Amelala ndani tu alikuwa nje wakati sisi ametajwa naye ametajwa amerudi ndani leo siku ya tatu Vanessa Mdee leo yuko ndani kwa kuhisiwa tu.

"Lakini huyu mpaka tumetaja Daudi Bashite yupo katorokaje? Huyu kakimbiaje? Vanessa Mdee simfahamu wala simjui lakini alikuwa ana performing zake nje ya nchi kashikwa pale yuko ndani leo, huyu katorokaje? Kwanini wengine wako ndani na wengine wanazunguka mitaa ya South Africa wakati walitakiwa wawe hapa na wao, mbona mimi nilienda kulala tu?"

==>Msikilize Hapo Chini

Jinsi Ya Kuandaa Na Kutayarisha Lishe Maalumu Ya Kuongeza Na Kunenepesha Mwili

$
0
0
Kama umekonda  na  kudhoofika  mwili  kutokana  na  sababu  mbalimbali  kama  vile kuugua  magonjwa  na  maradhi  mbalimbali  au  kupatwa  na  msongo  mawazo, basi  fuata  maelekezo  yafuatayo  ili  upate  kujua  namna  ya  kuandaa  na  kutayarishe  lishe  maalumu  ya  asili  itakayo  kusaidia kunenepa  na  kurejesha  afya  ya  mwili  wako  katika  hali  yake  ya  kawaida.

MAHITAJI:
1.    Dawa  Lishe  ya  kuongeza  na  kunenepesha  mwili

2.   Asali  ya  tende

3.   Ufuta

4.     Ukwaju

5.    Kitunguu  swaumu

6.   Giligiliani

7.    Juisi  ya  Komamanga na  Asali

MATAYARISHO  NA  MATUMIZI
Matumizi  ya  lishe  hii, yame  gawanyika  katika  awamu  kuu  mbili. Awamu  ya  kwanza, itachukua  siku thelathini  na  awamu  ya  pili  itachukua  siku  thelathini pia.

Katika  awamu  ya  kwanza , mgonjwa  atatumia  DAWA  LISHE  YA  KUNENEPESHA  MWILI, ASALI  YA  TENDE  NA  UFUTA  na  awamu  ya  pili, mgonjwa  atatumia   UKWAJU, KITUNGUU  SWAUMU, GILIGILIANI  na  JUISI  YA  KOMAMANGA  & ASALI  kwa  kufuata  utaratibu  utakao  elezwa  hapo  chini.

AWAMU   YA   KWANZA
SIKU   THELATHINI  ZA  KWANZA

Mahitaji

1.   Dawa  lishe  ya  kuongeza  na  kunenepesha  mwili

2.   Ufuta

3.   Asali  ya  Tende  (   Dates  Syrup )

MATAYARISHO  , MAELEKEZO  NA  MATUMIZI
1.   Dawa –Lishe  ya  Kunenepesha  Mwili

Chukua  vijiko   vitatu vikubwa  vyenye  dawa  yako, kisha  changanya  na  maji  nusu  lita halafu chemsha  hadi  itokote, Ikiisha  tokota, ipua  acha  ipoe  kidogo kisha  tumia  kunywa  pamoja  na  machicha  yake.  Utafanya  hivyo  mara  mbili  kwa  siku  asubuhi  na  jioni  kwa  muda wa  siku  thelathini.

2.   Ufuta : Matayarisho : Chukua  vijiko  vikubwa  vinane  vyenye  ufuta, kisha  changanya  na  lita  moja  na  nusu  ya  maji. Kama  hauna  tatizo  na  sukari, unaweza  kuongeza  na  sukari  kiasi ili  kuipa  ladha.  Ikisha  tokota, ipua iache  ipoe  kiasi  kisha  tumia  kula  ufuta wote  pamoja  na  supu  yake  ama  juisi  yake. Utafanya  hivyo mara  mbili  kwa siku  asubuhi  na  jioni  kwa  muda  wa  siku  thelathini.

(N.B:   KAMA  UNA  NAFASI,  BADALA  YA  KUTUMIA  VIJIKO  VINANE  TU VYA  UFUTA  KWENYE LITA  MOJA  NA  NUSU  YA  MAJI, WEWE  TUMIA  ROBO KILO  YA  UFUTA  KWENYE  LITA  TATU  YA  MAJI, CHEMSHA  HADI  ITOKOTE,  IACHE  IPOE, KISHA  TUMIA  KULA . FANYA  HIVYO  MARA  MBILI  KWA  SIKU  ASUBUHI NA  JIONI  KWA  MUDA  WA SIKU  THELATHINI )

2.   ASALI  YA  TENDE
3.   Tumia  kula  vijiko vikubwa  vinne  vya  tende  mara  mbili  kwa siku  asubuhi  na  usiku   kwa  muda  wa  siku  thelathini. Yaani  asubuhi  kula  vijiko  vikubwa vinne  na  usiku  kula  vijiko  vikubwa vinne  vya  asali  ya  tende.

( HABARI  NJEMA  KWA  WATEJA  WETU  NI  KWAMBA, ASALI  YA  TENDE  SASA  INAPATIKANA  MOJA  KWA  MOJA  DUKANI   KWETU . UTAPATIWA  DAWA  LISHE  PAMOJA  NA  ASALI  YA  TENDE  UTAKAYO  ITUMIA  KWA  MUDA  WA  SIKU  THELATHINI  KWA  UTARATIBU  WA  MAELEKEZO  HAYO  HAPO  JUU )
AWAMU   YA  PILI
Awamu  ya  pili  ya  lishe  hii, itaanza  baada  ya  kukamilika  kwa  siku  thelathini  za  kutumia  dawa  lishe, ufuta  pamoja  na  asali  ya  tende. Kama  ilivyo  kuwa  kwa  awamu  ya  kwanza, awamu  ya  pili  pia  itachukua  muda  wa  siku  thelathini

MAHITAJI, MATAYARISHO   NA  MATUMIZI

1.  UKWAJU
Matayarisho na  Maandalizi
Chukua ukwaju  kiasi  cha  robo kilo , weka  kwenye  maji  kiasi  cha  lita  moja, ongeza pilipili  manga kiasi cha  kijiko kimoja kidogo  ( tea spoon ) halafu ongeza sukari  vijiko  vitatu vikubwa, ongeza karafuu  ya unga  kijiko kimoja kidogo, pamoja  na hiriki vijiko  vikubwa  viwili.

Ukisha  fanya  hivyo, chemsha  hadi  mchanganyiko  wako  utokote. Ukisha  tokota, ipua  na  kuchuja  kisha  weka  kwenye  chombo  kisafi.

MATUMIZI :
Tumia  kunywa  mchanganyiko  huu kila  siku  asubuhi  baada  ya  kunywa  chai. Utafanya  hivyo  kwa  muda  wa  siku  thelathini  mfululizo.

2.   JUISI   YA  KOMAMANGA  NA  ASALI
Matayarisho  na  Matumizi

Tayarisha  juisi  ya  komamanga  kiasi  cha  nusu  lita, changanya  na asali ya  kawaida  vijiko vikubwa    vinane, kisha  ongeza  chumvi kijiko kidogo( tea spoon)

Koroga  mchanganyiko  wako  halafu  tumia  kunywa. Utafanya  hivyo  mara  moja   kwa  siku kwa  muda  wa  siku thelathini.

Matunda  ya  makomamanga  yanapatikana  masokoni, ingawa  mara  nyingi  hupatikana  kwa  uchache. Kama  utabahatika  kupata matunda  mengi, basi  unashauriwa  kuyachukua  kwa  wingi  na  kuyahifadhi, sehemu  salama ili usipate  usumbufu  wakati  wa  kutumia  tiba  yako.

Mbali  na  kutumika  katika lishe  ya  kuongeza  na  kunenepesha  mwili, tunda  la  komamanga, linasaidia  kuondoa  harufu  mbaya  ya  kinywa. Kwa  kuondoa  harufu  mbaya  ya  kinywa, kula  walau  tunda  moja  la  komamanga  kwa  siku  kwa  muda  wa  siku  thelathini  mfululizo. Utapata  matokeo  mazuri . ( HII  ITAWASAIDIA  ZAIDI  WALE  AMBAO  TATIZO  LAO  LA  KUTOKWA  NA  HARUFU  MBAYA  YA  KINYWA  LIMEANZIA  KINYWANI  NA  SIO  TUMBONI

ALTERNATIVE (MBADALA )  WA JUISI  YA  KOMAMANGA  ILIYO  UNGWA  NA  ASALI.

Kama  utashindwa  kupata makoma manga, basi  utafanya  kama  ifuatavyo :

KITUNGUU  SWAUMU
Chukua punje  nne  za  vitunguu  swaumu, zitwange kisha  tia  kwenye  maji nusu lita halafu ongeza  juisi  ya  ndimu  moja  au  limao  moja kisha  chemsha hadi mchanganyiko  wako  uchemke.

Matumizi :  Tumia  hivyo kila  siku  usiku baada  ya  kula  chakula cha  usiku. Utafanya  hivyo  kwa  muda  wa  siku  thelathini mfululizo.

AU
Vile vile , mbadala  mwingine wa  kutumia  juisi  ya komamanga  iliyo  changanywa  na  asali, unaweza  kutumia  JUISI  YA  GILIGILIANI  kwa  kufuata  utaratibu  ufuatao :

JUISI   YA   GILIGILIANI
MATAYARISHO   NA   MATUMIZI YA  JUISI  YA  GILI GILIANI

Chukua giligiliani  fresh, kisha zi -blend ( ZISAGE ) ili  kupata  juice  yake  kiasi  cha  robo  lita.

 Ndani  ya  juisi  yako  ya  giligiliani, kamuliamo ndimu fresh moja, halafu  ongeza  chumvi  kiasi robo  kijiko  kidogo ( tea spoon), koroga  kisha  tumia  kunywa.  Utakunywa  usiku  baada  ya  kula  chakula  cha  usiku. Utafanya  hivyo mara   moja  kwa  siku  kwa  muda  wa  siku  thelathini  mfululizo.

PIA : Jenga  utaratibu  wa  kuwa  unakula    giligiliani kwa wingi. Hakikisha  katika  kila  mlo  wako, inakuwepo  mboga  ya  giligiliani  pembeni.

VITU   VINGINE VYA   KUZINGATIA..
Pamoja na kutumia  lishe  hii  ya  asili  kwa  kufuata  utaratibu  huo  hapo  juu, unashauriwa  kuzingatia  matumizi  ya  vyakula  vifuatavyo:

TANGAWIZI
Jenga  tabia  ya  kuwa  una tumia  tangawizi, kila  mara  upatapo  nafasi.  Utaratibu  wa  jinsi  ya  kutayarisha  tangawizi ni  kama  ifuatavyo :

Chukua kipande  kimoja  cha  tangawizi, kisha  kitwange  halafu ongeza  vikombe  viwili vya  maji  vyenye  ujazo  wa  milimita  mia  mbili  na  hamsini ( 250 mills). Chemsha pamoja  kisha ongeza  maziwa  kiasi cha  robo lita  na  sukari ili kupata  ladha.  Fanya  hivi  kila  mara  uapatapo  nafasi. Ukiweza kufanya  hivyo walau  mara  mbili  kwa  siku, itakuwa  vizuri  zaidi.

  AU  chukua  kipande  kimoja  cha  tangawizi, kitwange kisha  chemsha pamoja  na  chumvi nusu  kijiko  kidogo  kwenye  maji kiasi  cha  nusu   lita  halafu tumia  kunywa  kikombe  kimoja  nusu  saa  kabla  ya  kula  chakula chako  cha  asubuhi, mchana  na usiku.

HIRIKI
Jenga utaratibu  wa  kuwa  unakunywa  mara  kwa  mara  chai  iliyo  changanywa  na  hiriki.

MACHUNGWA
Jenga utaratibu  wa  kuwa  unakula  machungwa kwa  wingi,  kwa  kadri utakavyo  weza. Unashauriwa  kuwa  unachanganya na  chumvi  kidogo  pamoja  na  pilipili  manga.

KWA  MAHITAJI  YAKO  YA  DAWA-LISHE  YA  KUNENEPESHA  & KUONGEZA  MWILI  PAMOJA  NA  ASALI  YA  TENDE.

Kwa  mahitaji  yako  ya  DAWA-LISHE ya  kuongeza & kunenepesha  mwili, pamoja  na  asali  ya  tende, fika  katika  duka  la  NEEMA  HERBALIST.

Tunapatikana  UBUNGO  jijini  DAR  ES  SALAAM, jirani  na  SHULE  YA  MSINGI   UBUNGO  NATIONAL  HOUSING  nyuma  ya  jengo  la  UBUNGO  PLAZA.

WASILIANA  NASI  KWA  SIMU  NAMBA  0766 53 83 84.

Kwa wateja  wetu  waliopo  jijini  Dar  Es  Salaam, ambao  hawana  nafasi  ya  kufika  dukani  kwetu  Ubungo, tunayo  huduma  ya  kuwapelekea  dawa  mahali  walipo ( HOME & OFFICE  DELIVERY  )

Kwa wateja  waliopo  nje  ya  mkoa   wa  Dar  Es  Salaam,  watatumiwa  dawa  kwa  kutumia  mabasi  mbalimbali.

Kwa  wateja  waliopo  Zanzibar, watatumiwa  dawa  kwa  njia  ya  usafiri  wa  boti.

Kwa  wateja  waliopo  ughaibuni, watatumiwa  dawa  kwa  njia  ya  POSTA  au  DHL.

Na kwa  taarifa  zaidi  kuhusu  huduma  zetu, tutembelee  kila  siku  katika  blogu  yetu :

Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images