Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Jinsi Wachawi Wanavyo Tumia Maji Ya Kisima Kutengeneza “UKIMWI WA KICHAWI ”.

$
0
0
IMESIMULIWA  NA  DOKTA. MUNGWA  KABILI………….0744  000  473

Wachawi  wana  uwezo  wa  kutengeneza  magonjwa  mbalimbali kama  vile  ugumba, udhaifu  wa  nguvu  za  kiume, kifafa, upofu, ukichaa, kiharusi, ukimwi nakadhalika.

Hapa  mgonjwa  akienda  kupimwa  hospitali  anakutwa  hana  tatizo  wala  ugonjwa  wowote  lakini  anakuwa  anaonyesha  dalili  zote  za  ugonjwa  husika.  Ukiona  hali  hiyo  basi  ujue  ugonjwa  wako  umetengenezwa   na  wachawi.

Mara  nyingi,ingawa  si  mara  zote, kabla  wachawi  hawajamtupia  mtu  ugonjwa  husika, hujidhihirisha  kwanza  kwa  kutumia  njia  zao  za  kichawi  kama  muhusika  hana  maradhi  wanayo  taka  kumsababishia.

Kama  wakigundua  mhusika  tayari anaugua  maradhi wanayo  taka  kumsababishia, basi  humtengenezea  ugonjwa  mwengine, na  ndumba  ambazo  zingetumika  kumsababishia  maradhi  mhusika, huelekezwa   kwa  mtu  mwingine (  Katika  ulimwengu  wa  wachawi, ndumba  zina  gharama  kubwa  sana,  hivyo  huwa  hazitumiki  bila  sababu  wala  faida )

Kwa  mfano  huko  vijijini, kama  wachawi  wanataka  kumtengenezea  mtu  ugonjwa  wa  kisukari, watataka  kwanza  wajue  kama  mtu  huyo tayari  ana  maradhi  ya  kisukari  au  bado  hajaanza  kushambuliwa  na  kisukari.

WACHAWI  WANAJUAJE  KAMA  MTU  FULANI  ANA  MARADHI  YA  KISUKARI

Kujua  kama  mtu  Fulani  ana  maradhi  ya  kisukari,  wachawi  watafuatilia  mienendo  ya  mtu  huyo kwa  lengo la  kupata  sehemu  atakayo  kojoa.  Siku  wakibahatisha  kumuona  mhusika amekojoa  mahali, basi  watakwenda  hadi  kwenye  eneo  alipokojoa na  kusubiri  kwa  muda  wa  kuanzia  dakika  arobaini  hadi  lisaa  limoja.  Ndani  ya  muda  huo,  KAMA  WATATOKEA  SISIMIZI, basi  ujue  mtu  huyo  ANA  KISUKARI  lakini  KAMA  SISIMIZI  HAWATATOKEA  basi  ujue  mtu  huyo  HANA  MARADHI  YA  KISUKARI. Baada  ya  kipimo  hicho  ndipo  watachukua  hatua  stahiki, za  ama  kumsababishia  maradhi  ya  kisukari  ama  vinginevyo (  KUHUSU  NAMNA  WACHAWI  WANAVYO  TENGENEZA  “KISUKARI  CHA  KICHAWI”  NITAELEZEA  SIKU  ZIJAZO.)

Ukimwi  wa  Kichawi : Katika  ulimwengu wa  kitabibu, “ ukimwi  wa  kichawi” ni  pale  mtu  anapo  onyesha  dalili  zote  za  muathirika  wa  ukimwi, lakini  vipimo  vya  hospitali  vinaonyesha  mtu  huyo  yupo   ( HIV-NEGATIVE)  yaani  bado  hajaathirika .

Hapa  mgonjwa  husika, atapimwa  vipimo  vyote  vya  hospitali  na  vyoote  vitaonyesha  hajaathirika, lakini  ataendelea  kuonyesha  dalili zote  za  mgonjwa  wa  ukimwi . Mgonjwa  huyu  ataendelea  kuugua  na  kuteseka  bila  kupata  nafuu  yoyote  licha  kutumia  dawa  mbalimbali, na  mwisho  wa  siku  atapoteza  maisha  yake.

Zipo  njia  kuu  mbili  wanazo  tumia  wachawi  kusababisha  maradhi  ya  aina  mbalimbali  kwa  watu  mbalimbali. Njia  ya  kwanza, ni  kwa  njia  ya  kuwalisha  dawa  mbalimbali  za  kichawi, ambazo  husababisha  maradhi  ya  aina  mbalimbali ( WACHAWI  WANA  MAARIFA  MAKUBWA  SANA  JUU  YA  MITI  MBALIMBALI  INAYO  SABABISHA  MARADHI NA  MATATIZO  MBALIMBALI )

Njia  ya  pili  ni  kwa  njia ya  majini. Hapa mgonjwa  husika, atasababishiwa  maradhi  ya  aina  Fulani  kwa  kutumiwa  majini  majini  ambayo  yameapishwa  kwenda  kufanya  makazi  yao  kwenye  damu  ya  mtu  aliekusudiwa  na  kusababisha  maradhi  Fulani  kwa  mtu  huyo, hadi   pale  umauti  utakapo  mkuta.

Katika  kutengeneza “ ukimwi  wa  kichawi “ pia  zipo  njia  kuu  mbili  zinazo  tumiwa  na  wachawi.  Njia  ya  kumlisha  mkusudiwa ndumba za  kichawi  ambazo  husababisha  mtu kuugua  maradhi  yanayo  fanana  dalili  zake  na  maradhi  ya  ukimwi  na  njia  ya  pili  ni  kumtupia  majini  ambayo  yatamfanya  augue  maradhi  yanayo  fanana  na  ukimwi.

Leo  tutaangalia  njia  ya kwanza, yaani  njia  ya  kumlisha  ndumba  za  kichawi  mtu  aliye  kusudiwa. Tutaangalia  njia  wachawi  wanavyo  weza  kumlisha  mtu  uchawi, utakao  msababishia  maradhi  ya  ukimwi  na  jinsi  unavyo weza  kujikinga  dhidi  ya  husda  hiyo, na  kwa  wale  ambao tayari  wameshalishwa  uchawi  huo, jinsi wanavyo  weza  kusaidiwa  kupata  tiba  ya  kuondoa  maradhi  hayo  ya  kichawi  mwilini.

Zipo njia  zaidi  ya  arobaini  ambazo  wachawi  wanaweza  kuzitumia, kutengeneza  uchawi  na  kumlisha  mtu, ambao  utamsababishia  kuugua  maradhi  ambayo  dalili  zake  zinafanana  na  ukimwi. Leo  tutaingalia  njia  moja  wapo  kama  ifuatavyo

JINSI  WACHAWI  WANAVYO  TUMIA  MAJI  YA  KISIMA  KUTENGENEZA  “ UKIMWI  WA  KICHAWI “

Awali  ya  yote, wote  tunapaswa  kufahamu  kwamba  katika  ulimwengu  wa  tiba  za  jadi “ MAJI”  yanaweza  kutumika  kama  TIBA  na  wakati  huo  huo, yanaweza  kutumika  kama  “ UCHAWI  WENYE KUDHURU”

Maji  yenyewe  kama  yenyewe, bila  kuchanganya  na  kitu  chochote  kile, yanaweza  kutumika   kama  tiba  ya  magonjwa  karibu  yoote  unayo  yafahamu,  kuanzia  kisukari, kifafa, ugumba, udhaifu  katika  nguvu  za  kiume, kuongeza  urefu  wa  maumbile  ya  kiume ( HAPA  HUTUMIKA  MAJI YAITWAYO  MAJI  YA  FATIRU ), fangasi  za  sehemu za  siri, magonjwa  ya  ngozi,  nakadhalika. 

Sio  tu katika  kutibu  magonjwa  na  maradhi  mbalimbali, maji  pia hutumika  kama  tiba  dhidi  ya  matatizo  mbalimbali  ya  kimaisha kama  vile kuondoa  nuksi, mikosi  nakadhalika.

Vile  vile  maji  yanaweza  kutumika  katika  kutengeneza  uchawi  wenye  kudhuru, wa  aina  mbalimbali.

( KATIKA  SIKU  ZINAZO  KUJA, NITAWEKA  SOMO  KUHUSU  TIBA  MBALIMBALI  ZA  JADI  KWA  NJIA  YA  MAJI  BILA  KUSAHAU,  JINSI  WACHAWI  WANAVYO  TUMIA  MAJI  KUTENGENEZA  UCHAWI  WENYE  KUDHURU  WA AINA   MBALIMBALI )

Katika  ulimwengu  wa  tiba  za  jadi, maji  ya  mtoni, baharini, ziwani, kisimani, kwenye  dimbwi  nakadhalika, huweza  kutumika  eidha  kama  tiba  ya  magonjwa  mbalimbali au  kama  uchawi wa  aina  mbalimbali.

Kinacho  yapa  maji  hayo  kuwa  na  nguvu  ya  kitabibu, ni njia  zilizo  tumika  kuyachukua  maji  hayo. Kila  maji  yanatumika  katika  tiba  yake  na  uchawi  wake. Maji  ya  mtoni  yana tiba  zake  na  uchawi  wake, maji  ya  ziwani, maji  ya  baharini, kisimani  nakadhalika. 

Mfano mdogo, maji  ya  mtoni  yanaweza  kutumika  katika  kutengeneza  uchawi  unaoitwa  “ NSUNKWA”  ambao ni  maalumu  kwa ajili  ya  kumuhamisha  adui yako, aende  kuishi  mbali  na  wewe.

Kila aina  ya  maji  yana  taratibu  yake  namna  ya  kuyachukua  na  kuyatumia  katika  eidha  tiba  au  uchawi.

Leo  tutaona  jinsi  wachawi  wanavyo  tumia  maji  ya  kisima, katika  kutengeneza  maradhi  ya  ukimwi.

Katika  kutengeneza  ukimwi  wa  kichawi, wachawi  hufanya  kama  ifuatavyo :

Kwanza  wanachukua  maji  ya  kisima  kisicho  kauka .Pili  wanachukua  kitovu  cha  mtoto mchanga  kilichodondoka  chenyewe ( Kuweni  makini  sana  na  vitovu  vya  watoto  wenu )  

Tatu  wanachukua  “ Tegelo” ; Kwa  wale  wasio  fahamu Tegelo  ni  mfuko wa  chakula  cha  kuku  na  chakula  chake.  Tegelo  na  kitovu  cha  mtoto, vinachanganywa  na dawa  zingine za  aina  kumi  na  tatu ( sitazitaja  zote  kwa  sababu  za  kimiiko  ya  kazi  yangu: kuna  watu wabaya  wanaweza  kujifunza  kitu  hapo na  kwenda  kuwaumiza  watu )

Vikishachanganywa  vinachomwa  vyote  kwa  pamoja, kisha  vinaenda  kupikwa  njia  panda usiku wa  manane  kwenye  hayo  maji  ya  kisima, pamoja  na  mafuta  ya  usiku.  Baada  ya  hapo  linafanyika  tambiko  maalumu  kisha  vitu  hivyo  vinaenda  kuzikwa  kaburini  kwa  muda  wa  siku  saba.  Baada  ya  hapo uchawi  huo  utakuwa  umekamilika.

 JINSI  WANAVYO  TEGA  UCHAWI  HUO :  Uchawi  huo  hupitia  kwenye  chakula ( sana  sana  “ mboga  yenye  mchuzi “), au  kinywaji.

Mtu  atakae  lishwa  uchawi  huu  ataanza  kuonyesha  dalili  za  ugonjwa  wa  ukimwi, kulingana  na  muda  alio nuiziwa, kama  amenuiziwa  aanze  kuugua  baada  ya  miezi  sita, basi  baada  ya  miezi  sita  kweli  ataanza  kuugua  maradhi hayo, kama  ni  mwezi mmoja  ni mwezi  mmoja.

Mkilishwa  mke  na  mume, basi  mke  na  mume  wote mtaugua  maradhi  hayo. Mkilishwa  familia nzima, basi familia  yote  mtaugua  maradhi  hayo  mmoja  baada  ya  mwingine. Ndio maana  baadhi  ya  familia  unakuta  watu wote   ni waathirika.

Na  kama  mtalishwa  kwenye  sherehe , au msiba, basi  watu  wote  mtaugua  maradhi  ya  ukimwi, isipokuwa  tu  wale  wenye  kinga  zao.

                                   TIBA   YAKE.
Zipo  tiba  za  aina  nyingi  ambazo  zinatibu  maradhi  haya  ya  kutengenezwa. Leo  tutaangazia  tiba  moja  wapo.

Kama una muuguza  mgonjwa  ameugua  maradhi  haya  kwa  muda  mrefu,  bila nafuu  yoyote. Ameenda  kupima  hospitali  akaambiwa  hajaathirika lakini  bado  anaendelea  kuonyesha  dalili  za  mtu  aliye  athirika, basi  fanya  kama  ifuatavyo:

 ==>Moja  chukua  dawa  inaitwa  Mlali, pili chukua  dawa  inaitwa  Hangachalo,. Tatu  chukua  dawa  inaitwa  Tarigula, Nne  chukua  dawa  inaitwa  Mwinula, Tano; chukua  dawa  inaitwa  Mzima

==>Dawa  hizi  zitachemshwa  pamoja na  kisu  kikiwa  kimesimama ndani, kisha  unampa mgonjwa  wako  anakuwa  anakunywa mara  tatu  kwa  siku  asubuhi  mchana  na  jioni  kwa  siku  thelathini., Na  nyingine  unakuwa  unampiga  nayo mgongoni  kila  anapokuwa  anakunywa.

Atatapika  uchawi  wote,na  ndani  ya  siku  arobaini, inshaalah  uchawi  na  sumu  yote  itakuwa  imetoka  mwilini  na  atarejea  katika  hali  yake  ya  kawaida.

KINGA :  Kinga  ni bora, kuliko  tiba. Kujiepusha  na  shari  kama  hii, unatakiwa  uwe  na  kinga  bora.

Zipo  kinga  nyingi  bora, ila leo  nitaelezea  kuhusu  kinga  moja. Kinga  hii  inatengenezwa  kwa mchanganyiko  wa    miti na  vizimba  zaidi  ya  mia  moja  na  ishirini . Moja  kati  ya  vizimba  vilivyopo  katika  kinga  hii, ni mti mmoja  ambao  haupatikani  popote  pale  duniani  isipokuwa  mkoa  wa Kigoma  tu.

Ukiwa  na  kinga  hiyo, na  ikatokea  umelishwa  uchawi  wa aina  yoyote  ile  utautapika, na  aliye  kuwekea  uchawi  huo, atapata  madhara  makubwa.

IMESIMULIWA  NA  Dokta.MUNGWA  KABILI.. 0744- 000 473
 

Alichokisema Leo RC Paul Makonda Akiwa Polisi Kuhusu Madawa ya Kulevya

$
0
0
Leo  mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda amezungumza akiwa kituo cha kati cha Polisi Dar es salaam pembeni ya Kamishna Simon Sirro kuhusu ishu ya dawa za kulevya inayoendelea kwenye headlines.

Mambo  aliyoyasema mkuu wa mkoa Paul Makonda leo ni kutoa siku kumi kuanzia kesho February 7 2017 kwa Wenyeviti wa mtaa, Wazazi na Watumiaji na Wafanyabiashara.

==>Natoa siku 10 kwa kila Mwenyekiti wa Mtaa kwenye mitaa yote Dar es salaam kutoa taarifa za mtaa wake juu ya dawa za kulevya.
 
==>Natoa siku 10 kuanzia kesho kwa Wazazi, kama wewe ni mzazi unaishi na mtoto anatumia dawa za kulevya na unaishi nae, njoo utoe taarifa….. tukikukamata baada ya siku kumi na mwanao anahusika tutaamini na wewe ulikua sehemu ya kumfanya mtoto wako atumie dawa za kulevya.
 
==>Natoa siku 10 kwa Wafanyabiashara na Watumiaji wa dawa za kulevya, waje wenyewe Polisi kwa kamishna, kama umekua ukifanya biashara ya dawa za kulevya na umeacha njoo Polisi, nguvu tunayo, uwezo tunao…. hakuna kiunga tutashindwa kufika, hizi kelele nyingine zinatupa hamasa

VIDEO: Msikilize Rais Magufuli Akiongelea Swala la Madawa ya Kulevya

$
0
0
Rais Magufuli ameviagiza vyombo vya ulinzi na usalama kuwakamata wanaohusika na Dawa za Kulevya bila kuangalia umaarufu au cheo cha mtu.

Magufuli ameyasema hayo leo alipokuwa akizungumza  mara  baada ya kuwaapisha viongozi mbalimbali akiwemo Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Vanance Mabeyo pamoja na viongozi wengine wa majeshi, na mabalozi.

==> Msikilize hapo chini akiongea

Rais Magufuli Aagiza Majeshi Yajenge Viwanda

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli ameyataka majeshi yote hapa nchini yajipange kuendana na sera ya ujenzi wa viwanda kwa kuhakikisha viwanda vya kutengeneza mahitaji yanayoweza kupatikana hapa nchini

Rais Magufuli ametoa agizo hilo leo mara baada ya kumuapisha Jenerali Venance Salvatory Mabeyo kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania katika hafla iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam.

Ametoa wito kwa uongozi mpya wa Jeshi hilo chini ya Jenerali Venance Mabeyo kuendeleza juhudi za kuilinda nchi na kuhakikisha viwanda vya kuzalisha bidhaa mbalimbali kwa ajili ya majeshi kama vile sare na vifaa, vinajengwa.

Rais Magufuli amempongeza Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Mstaafu Jenerali Davis Mwamunyange kwa kuliongoza jeshi hilo kwa kipindi chote alichokuwa madarakani na kueleza kuwa watanzania wana imani kubwa na JWTZ.

Kabla ya kuapishwa kushika wadhifa wa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania Rais Magufuli amemvalisha Jenerali Venance Salvatory Mabeyo cheo kipya cha Jenerali alichopandishwa kutoka Luteni Jenerali.

Aidha, Mhe. Rais Magufuli amemuapisha Luteni Jenerali James Alois Mwakibolwa kuwa Mnadhimu Mkuu wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ).

Luteni Jenerali James Alois Mwakibolwa amechukua nafasi iliyoachwa wazi na Jenerali Venance Salvatory Mabeyo ambaye sasa ni Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania.

Wakati huo huo, Mhe. Rais Magufuli amemuapisha Kamishna Juma Ali Malewa kuwa Kamishna Jenerali wa Magereza.

Kabla ya kuapishwa kushika wadhifa huo, Mhe. Rais Magufuli amevalisha Kamishna Juma Ali Malewa cheo kipya cha Kamishna Jenerali.

Kamishna Jenerali Juma Ali Malewa amechukua nafasi iliyoachwa wazi na Kamishna John Casmir Minja ambaye amestaafu.

Halikadhalika, Mhe. Rais Magufuli amemuapisha Mhe. Balozi. Luteni Jenerali Mstaafu Paul Meela kuwa Balozi wa Tanzania katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC).

Mhe. Balozi Luteni Jenerali Mstaafu Paul Meela anachukua nafasi ya Mhe. Balozi Antony Ngereza Cheche ambaye amestaafu.

Pia, Mhe. Rais Magufuli amemuapisha Mhe. Balozi Samuel Shelukindo kuwa Balozi wa Tanzania nchini Ufaransa.

Mhe. Balozi Samuel Shelukindo anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Mhe. Balozi Begum Taj ambaye amestaafu.

Mhe. Rais Magufuli amemuapisha Bw. Nyakimura Mathias Muhoji kuwa Katibu wa Tume ya Utumishi wa Umma.

Bw. Nyakimura Mathias Muhoji anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Claudia Mpangala ambaye amestaafu.

Katika hatua nyingine, Mhe. Rais Magufuli ameshuhudia tukio la kuapishwa kwa Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai Kamishna Robert Boazi Mikomangwa.

Kamishna Robert Boaz Mikomangwa ameapishwa na Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini Inspekta Jenerali wa Polisi - Ernest Mangu.

hafla hiyo imehudhuriwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Ali Mohamed Shein, Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa, Kaimu Jaji Mkuu Mhe. Prof. Ibrahim Khamis Juma na Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli.

==> Msikilize Hapo Chini Akiongea.......

Ester Bulaya Apinga Kitendo cha Kuwakamata Waathirika wa Madawa ya Kulevya na Kuwatupa Selo........Ataka Rais Magufuli Ashauriwe Vizuri

$
0
0
Mbunge wa Bunda Mjini Mh. Ester Bulaya amefunguka na kutaka siasa isiingizwe kwenye vita ya madawa ya kulevya na kusema viongozi wasimdanganye Rais Magufuli ili kujihakikishia vyeo vyao au nafasi zao katika uongozi.

Ester Bulaya ametoa rai hiyo leo bungeni alipokuwa akichangia mjadala wa taarifa za kamati na kusema Rais anapaswa kuambiwa ukweli ili waweze kumsaidia kupambambana vyema na madawa ya kulevya.

"Tusifanye siasa kwenye vita hii ya madawa ya kulevya, tusimuongopee Rais kwa kutaka kuhakikisha vyeo vyetu tumwambie ukweli, ili kumsaidia Rais anapaswa kumteua kamishina wa hii tume maana tangu tulipopitisha sheria hiki chombo hakina kamishna, tutakapo hakikisha hicho chombo kinapata kamishna kwa kumsaidia Mhe. Rais tutakamata wale wanaoingiza dawa za kulevya wale mapapa na si hao wanaokamatwa sasa hivi" alisema Bulaya

Mbali na hilo Mbunge Ester Bulaya amesema kuwa hawa watu wanaokamatwa saizi wanapaswa kupelekwa mahospitali kupata matibabu na si vinginevyo kwani hao ni waathirika wa dawa.

"Mdogo wangu Makonda akitaka kupambana na dawa za kulevya aende magerezani akakutana na kina mama Reyla watamwambia mapapa wa madawa ya kulevya, ili tuungane pamoja na tunamkaribisha katika hili lindi kuhakikisha nchi yetu inapambana vikali dhidi ya madawa ya kulevya, kwa sababu mimi mwenyewe nina mdogo wangu anayenifuata yupo Mwananyamala anakunywa dawa methadone, hivyo ninachokisema nina uchungu nacho kwa kuwa nimekifanyia utafiti wa kina" Ester Bulaya 

==>Msikilize Hapo chini Akiongea

Vita ya dawa za kulevya: Watuhumiwa 12 kati ya 112 Wapandishwa Mahakamani akiwemo Wema Sepetu

$
0
0
Sakata la Madawa ya kulevya limeendelea kugonga vichwa vya habari wiki hii ambapo Jumatatu hii Jeshi la polisi limedai toka lianze operesheni hiyo tayari limewakamata watuhumiwa 112 na kati ya hao 12 wamepandishwa mahakamani Jumatatu hii kwajili ya kiapo cha kutorudia matumizi ya Madawa ya kulevya baada ya kukiri kutumia.

Kati ya watu hao 12 ni pamoja na Wema Sepetu, Romy Jones, Petit Man, TID pamoja na wengine.

Aidha Wema Sepetu baada ya kiapo hicho atarudishwa polisi kwajili ya kuandaliwa shtaka jipya linalomkabili la kukutwa na msokoto wa bangi nyumbani kwake.

Akiongea na waandishi wa habari leo, Kamanda wa Polisi wa Kanda maalumu ya Dar es Salaam, Simon Sirro amesema watuhumiwa wengi waliohojiwa walikiri kutumia Madawa ya kulevya na kati ya hao walieleza watu ambao wanawauzia.

“Tumewakamata watuhumiwa jumla 112 na tumekamata kete 299 zinazodhaniwa ni za Madawa ya kulevya na kwa kawaida haya Madawa Mkemia Mkuu wa serikali yeye ndiye atakayetuambia ni Madawa ya aina gani,” alisema Kamanda.

Aliongeza, “Katika watuhumiwa 112, kuna watuhumiwa 12 tumewapeleka leo mahakamani, tumewapeleka mahakamani kwa sababu sheria ya mwenendo wa mashtaka iko wazi kifungu cha 73 na 74, huwa tunaweza kuomba kwa mweshimiwa hakimu kuwaombea watuhumiwa kwa kiapo, kwamba hawa watuhumiwa tunataka wabadilishe tabia zao. Tunawapeleka mahakamani ili wakae chini ya uangalizi wa jeshi la polisi na mahakama kwa muda wa miaka 2 wasifanye makosa tena,”

“Kwa sababu tulichokibaini kwa wote tuliowakamata wengine wanakiri na wamekwenda kuonyesha hayo Madawa ya kulevya. Kwa hiyo kusudio la kwanza wawe chini ya uangalizi wetu, na kusudio la pili la kiapo chetu waache hiyo tabia ili wabadilike wawe raia wema, lakini la tatu tumeomba wale wanakuja kuripoti kituoni angalau mara mbili kwa mwezi na lengo letu ni kuona hawa ndugu zetu ambao walikuwa wanavuta madawa ya kulevya wamecha kabisa,”

Gigy Money Ampiga Chini Mo J.......Ahamishia Penzi Lake kwa Joti

$
0
0
U heard ya CloudsFM Leo, chini ya mtangazaji Soudy Brown imeleta hii  habari inayowahusu Watangazaji wa ChoiceFM, Gigy Money na Mo J ambapo inadaiwa wameachana baada ya Mo J kushtukia.

Inasemekana Mo J ameshtukia mawasiliano ambayo mwenzake alikuwa akiyafanya na mtu mwingine ambayo ikapelekea ugomvi hata mmoja kubeba nguo zake, sasa leo Soudy Brown ameongea na wote wawili.

"Mbali na mimi kuwa naye kwenye mahusiano yeye ana mambo yake anayafanya na alikuwa anayafanya labda amejisikia kumpost Joti au ni mshikaji wake" Amesema Mo J

"Nimeamua tu kumpunguza instagram……..kwani Joti hafai kupendwa na Gigy Money na ninakuambia pale sichomoki na nimefika dada yako, Mo J tushamwagana kipindi kitaenda tu" Amesema Gigy Money

==> Sikiliza habari kamili hapo chini

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumanne ya February 7


CUF Wakataa Suluhu na Profesa Lipumba

$
0
0
Chama cha Wananchi (CUF) kimesema hakitafanya mazungumzo kusaka suluhu na mwenyekiti wake, Profesa Ibrahim Lipumba anayetambuliwa na Msajili wa Vyama vya Siasa na kwamba, kipo tayari kwa lolote hata kama kitafutiwa usajili.
 
Aidha, chama hicho kimesema hakijutii kumkaribisha na kumuunga mkono Edward Lowassa, ambaye aliteuliwa kugombea urais mwaka 2015 kwa tiketi ya Chadema na kuwakilisha Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa).
 
Hayo yamesemwa na Naibu Mkurugenzi wa Habari na Uenezi wa CUF,  Mbarala Maharagande kujibu madai yaliyotolewa na Profesa Lipumba alipokuwa akifanya mahojiano na kituo kimoja cha televisheni hapa nchini.
 
Katika mahojiano hayo, Profesa Lipumba alidai kuwa mgogoro uliopo ndani ya chama hicho kwa sasa hautamalizwa na mahakama pekee bali viongozi wa pande zote mbili wanatakiwa kuzungumza, lakini Maharagande amesema haiwezekani kwa vile Lipumba alishakwisha kukivuruga chama na hafai tena kuendelea kuwa kiongozi.
 
“Lipumba anasema tukae tulimalize suala hili kwa kuongea sisi wenyewe. Jambo hilo haliwezekani kwa kuwa kama kupandikiza chuki, uhasama, uharibifu wa chama miongoni mwa wanachama na viongozi ameshafanya na kufanikiwa hilo kwa baadhi ya wanachama na viongozi wake na kuharibu taswira ya chama kwa jamii,” amesema Maharagande.

Wabunge wazidi kupinga Wizara kuhamia Udom

$
0
0
Siku chache baada ya wabunge kueleza kutoridhishwa na Serikali kuhamia kwenye majengo ya Chuo Kikuu Dodoma (Udom), Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii nayo imepinga hatua hiyo.
 
Kamati hiyo pia imeshauri Tume ya Vyuo Vikuu (TCU), kuachana na utaratibu wa kupangia wanafunzi vyuo na ijikite kusimamia ubora wa elimu inayotolewa na vyuo vikuu nchini.
 
Mapendekezo hayo yametolewa bungeni mjini Dodoma na Mwenyekiti wa kamati hiyo, Peter Serukamba alipokuwa akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa shughuli za kamati hiyo kwa mwaka 2016.
 
Serukamba amesema kamati hiyo ya Bunge inaunga mkono Serikali kuhamia Dodoma, lakini utaratibu wa Wizara kuhamishia ofisi zao Udom siyo sawa.
 
Wizara ambazo zimehamishia ofisi zake Udom kutoka Dar es Salaam ni Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora; Katiba na Sheria; Kilimo, Mifugo na Uvuvi; Mambo ya Ndani ya Nchi na Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi.

Dk.Kigwangalla aagiza kukamatwa kwa mtu anayejiita James Delicious kwa kujitangaza shoga

$
0
0
Naibu Waziri wa Afya, Ustawi wa jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dk. Hamis Kigwangala, ametoa maagizo mazito kwa Vyombo vya Usalama nchini kuhakikisha vinamkamata mtu anayejulikana kwenye mitandao ya kijamii kama James Delicious kufuatia  kujitangaza kwake  kama shoga kinyume cha sheria ya Tanzania.

Dk. Kigwangalla ametoa kauli hiyo jana jioni mjini Dodoma Bungeni wakati akijibu hoja za wabunge juu ya hatua kwa mtu anayefanya vitendo hivyo ambapo ameviagiza vyombo vya usalama kumtafuta mtu huyo na iwe fundisho  kwani ni kinyume  na sheria za nchi  kwa kuendesha biashara ya kuuza ngono ya kinyume cha maumbile.

Mbali na James Delicious, wengine ambao ameagiza wajisalimishe wenyewe kituo cha Polisi Central Dar es Salaam ni pamoja na  Kaoge Mvuto na Dani Mtoto wa Mama ambao wamekuwa wakijinadai kufanya vitendo hivyo hapa nchini ambavyo ni kinyume na sheria.
 
KIGWANGALLA: Serikali kupiga Marufuku Matumizi ya Pombe za VIROBA Kufikia Mwezi wa Sita mwaka 2017.

Wakati huo huo, akiendelea kujibu maswali amebainisha kuwa Serikali itazuia viroba kutengenezwa nchini na kufuta kabisa matumizi ya pombe za aina ya viroba hapa nchini wakati akijibu hoja za wabunge kufuatia michango mbalimbali ya wabunge juu ya hoja za Kamati za UKIMWI na Madawa ya Kulevya na Kamati ya Huduma na Maendeleo ya jamii.

Dk. Kigwangalla alisema, ‘haitopita mwezi wa sita Serikali itakuwa imepiga total ban (marufuku) matumizi ya madawa ya kulevya nchini….’

Miezi kadhaa iliyopita Dk. Kigwangalla aliongoza kikosi kazi cha Serikali kilichokuwa kinashughulikia suala la viroba ili kutathmini ukubwa wa tatizo na kupendekeza hatua za kuchukua.

Kikosi kazi kilibaini changamoto nyingi ikiwemo ya uwepo wa viwanda bubu na pombe zinazochanganywa na spirit ya viwandani.

Tundu Lissu akamatwa na polisi....Asafirishwa Usiku kutoka Dodoma hadi Dar

$
0
0
Mwanasheria Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Tundu Lissu amekamatwa na Jeshi la Polisi wakati akitoka bungeni  mkoani Dodoma na kusafirishwa usiku kwenda Jijini Dar es salaam.

Lissu ambaye pia ni Mbunge wa Singida Mashariki(Chadema) na Mnazimu wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni ametiwa nguvuni kama ilivyokuwa kwa Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema.

Kamanda wa Mkoa wa Dodoma, Lazaro Mambosasa, amesema kuwa wamemkamata Tundu Lissu kutokana na makosa aliyoyafanya Dar es salaam.

”Sisi tunawajibu wa kumkamata na kumpeleka sehemu husika, tumemkamata kwa maagizo tuliyopewa kutoka Dar es salaam na kama unataka kujua muulize kamanda wa Dar es salaam,”alisema jana Kamanda Mambosasa.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo Freeman Mbowe, alisema kuwa hafahamu sababu za kukamatwa na kusafirishwa kwa Mwanasheria Mkuu wa chama hicho.

“Ni kweli wamemkamata lakini mpaka sasa hatujui  lengo lake ni nini na wanampeleka wapi kwa ajili ya nini na kwa lengo lipi,”amesema Mbowe.

Sakata la masheikh wa Uamsho laibuka tena.......Mbunge ataka kujua sababu za kuendelea kushikiliwa ilhali ushahidi ulishakosekana

$
0
0
Sakata la masheikh wa Uamusho walioshtakiwa kwa tuhuma za ugaidi, limeibuka bungeni jana baada ya Mbunge wa Konde, Khatib Said Haji (CUF) kuhoji ni nchi gani ambayo haina tishio la kigaidi inaweza kuwa na mlundukano wa watu wenye makosa hayo kwenye magereza.

“Hapa katika jibu nimeambiwa siku 60 zinatosha kutoa ushahidi na kwamba, kama ushahidi haukupatikana, watuhumiwa waachiwe. Lakini masheikh wa Uamsho wana miaka minne sasa wapo katika magereza na ushahidi umeshindwa kupatikana,” alisema Khatib. 

Alihoji iwapo watuhumiwa hao wanawekwa mahabusu kwa
kuwa wana kesi ya kujibu, au kwa amri ya viongozi wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ). 

“Waziri wa vikosi vya SMZ Zanzibar na Makamu wa Rais Zanzibar wamewahi kunukuliwa wakisema kwamba waliwaleta masheikh Tanzania ili wanyee ndoo katika magereza ya Tanzania Bara.”Alisema Khatib Said Haji

Akijibu swali hilo, Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani, Hamad Yusuph Masauni alisema kesi za watuhumiwa hao zipo mahakamani na kwa taratibu hawaruhusiwi kujibu hoja kortini. 

Hali hiyo ilisababisha baadhi ya wabunge kuguna bungeni hali iliyomfanya Waziri wa Katiba na Sheria, Dk Harrison Mwakyembe kuongezea majibu ya swali hilo.

Dk Mwakyembe alisema ni kweli kwamba sheria inataka mahakama kama upelelezi haujakamilika ndani ya siku 60, mtuhumiwa kuachiwa huru, lakini Mkuu wa Upelelezi wa Mkoa (RCO) anaweza kupeleka maombi mahakamani ya kuongezwa siku. 

Alisema baada ya hapo suala linakuwa chini ya Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) na kwamba, kulingana na uzito wa shtaka anaweza kuomba kuongeza muda. 

“Suala la ugaidi si dogo ni la kimtandao na kuutambua huo mtandao si suala dogo,” alisema Dk Mwakyembe

Alichokisema Zitto Kabwe Bungeni Kuhusu Sakata la Wema Sepetu Kukamatwa na Madawa ya Kulevya

$
0
0
Mbunge wa Kigoma mjini, Zitto Kabwe (ACT-Wazalendo) amesema Serikali imeshindwa vita dhidi ya madawa ya kulevya kwa kutokiwezesha chombo kilichoundwa na sheria ili kupambana nayo.

“Kamati (ya Bunge) imelalamika kuwa Mamlaka ya Kudhibiti Madawa ya Kulevya ina bajeti finyu na hata hiyo bajeti haitolewi na hivyo kusababisha Mamlaka kukosa vitendea kazi, kushindwa kutoa elimu kwa umma, kushindwa kufanya operesheni za ukamataji wa wafanyabiashara wa dawa za kulevya na kushindwa kutoa ushauri nasaha kwa waathirika,” alisema Zitto.

Zitto alikuwa akizungumzia taarifa ya Kamati ya Bunge ya masuala ya Ukimwi imebaini dosari nyingi katika sera ya dawa za kulevya ya mwaka 2004 ambayo imepitwa na wakati.

Wakichangia katika taarifa ya shughuli za kamati kwa mwaka 2016/17, wabunge, akiwemo Zitto, walisema dawa za kulevya ni janga la taifa na linahitaji mikakati ya kupambana na siyo kuwaweka rumande waathirika ambao wanahitaji kupatiwa matibabu.

Zitto alibainisha kuwa watuhumiwa waliokamatwa katika vita inayoendelea jijini Dar es Salaam  wamelazwa ndani kwa zaidi ya siku tatu bila kufikishwa mahakamani.

“Baadhi ya watuhumiwa wameelezwa kuteswa na kupigwa na polisi na kulazimishwa kutoa maelezo kwa Polisi," alisema Zitto. "Umma haujaelezwa kama watu hawa wamekamatwa na madawa hayo ama wamehisiwa kuwa ni watumiaji tu.”

==>Msikilize Hapo Chini Akiongea

Mbunge Adai yuko tayari kutaja Wabunge Wanaouza Madawa ya Kulevya

$
0
0
Kuanzia wiki iliyopita, vita dhidi ya Madawa ya kulevya iliyoibuliwa na mkuu wa mkoa wa Dar es salaam, inazidi kuchukua sura mpya kila kukicha huku wengine wakitega masikio kwenye vyombo vya habari kutaka kujua kitu gani kinaendelea huko Mahakamani.

Vita hiyo juu ya madawa ya kulevya imefika mpaka bungeni na baadhi ya wabunge walikuwa wakitoa hoja mbalimbali huko mjini Dodoma. 

Mbunge wa Ulanga, Goodluck Mlinga jana alisema yeye yupo tayari kuwataja baadhi ya wabunge wanaohusika na biashara hiyo.

Mbunge huyo awali alizungumzia mambo mbalimbali yakiwemo masuala ya elimu lakini la mwisho aliweza kuzungumzia suala hilo ambalo kwa sasa kila mtu anataka kutambua nini kinaendelea.

” Suala ninalotaka ni hili suala linashika headline ni suala la madawa ya kulevya, naomba niwaambie sisi viongozi naomba niquote, ‘nitasema ukweli uongo kwangu mwiko.’ Kwahiyo nitakachotaka kukisema mtu yeyote akitaka anihukumu akihukumu chama changu kwanza, na kama wewe ni mwana CCM utanichukia rudisha kadi ndo unichukie.

"Wafanya biashara wa madawa ya kulevya hakuna asiowajua, tunawajua humu ndani wapo, nje ya bunge wapo, kwanini hatuwataji?" alihoji.

Aliongeza, “Kwanini hatuwataji tunakaa kimya? Mheshimiwa mwenyekiti kama kwa ridhaa yako unaniruhusu mimi nitawataja hata humu ndani. Madawa ya kulevya ni pamoja na bangi, kuna mbunge alisimama humu alisema bangi hazina madhara alijuaje kama hazina madhara kama hatumii? tungeanza na huyu. 

"Viongozi wenzangu naomba niwahakikishie kama tutakuwa wanafiki mbinguni sisi ndiyo tutakaokuwa kuni, tutakuwa kuni mbinguni tunawafumbia macho watumiaji wa madawa ya kulevya tunakula nao. 

"Nimpongeze ndugu yangu Paul Makonda kwa kuthubutu kutaja neno madawa ya kulevya lakini nimhakikishie kila marafiki watano wanaomzunguka watatu ni wafanyabiashara wa madawa ya kulevya, aanze na hao.”

==>Msikilize Hapo chini akiongea

TID, Tunda Na Wasanii Wengine Wanaotuhumiwa Kwa Madawa ya Kulevya wafikishwa Mahakamani

$
0
0
Takriban watuhumiwa 10 wa dawa za kulevya ambao ni miongoni mwa watu waliotajwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu asubuhi hii.

Miongoni mwa waliofikishwa mahakamani sasa ni wasanii Rommy Jones, TID, Babuu wa Kitaa, Petit Man, Tunda (model wa kike), Lulu Diva, Recho, Joan, na wengine.

Watuhumiwa wote wamesomewa kiapo cha Mahakama ambapo upande wa Jamuhuri umeomba watuhumiwa hao waamrishwe kuwekwa chini ya uangalizi kwa kuripoti polisi mara 2 kwa mwezi kwa kipindi cha miaka 2 ili kuangaliwa kama wameacha tabia ya kutumia dawa hizo hususani bangi

               
Wakili wa upande wa utetezi amedai taarifa hizo hazijakamilika kwani hazioneshi wanaojiusisha na dawa za kulevya na walikamatwa lini na wapi na hakuna ushahidi wa kujitosheleza wa madai hayo kiasi cha wao kupata dhamana ya kuangaliwa tabia zao bila polisi kutoa ufafanuzi wa kina wa kwanini wanahitaji kupata dhamana ya uangalizi wa nidhamu.

Maamuzi ya mahakama kuhusu wasanii wanaoshtakiwa kwa dawa za kulevya

$
0
0
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam leo imetoa maamuzi kwa baadhi ya wasanii waliokuwa wanashikiliwa na Jeshi la Polisi kwa tuhuma za kujihusisha na biashara ya dawa za kulevya.

Mahakama hiyo imekubali maombi ya Jamhuri kuhusu tuhuma zinazomkabili Petitman na wenzake wanne kwamba watakuwa nje kwa dhamana ya shilingi milioni 20 na watatakiwa kuripoti kituo cha polisi mara mbili kwa mwezi kwa muda wa miaka mitatu na kila mmoja anatakiwa kuwa na mdhamini mmoja mwaminifu.

Aidha kwa TID, Tunda, Recho, Rommy Jones, Babu wa Kitaa na Nyandu Tozi  watakuwa chini ya uangalizi kwa mwaka mmoja na dhamana ya Tsh milioni 10, wakivunja masharti watarudi Mahakamani

Wabunge wa upinzani Walivyosusa na kutoka nje kisa kukamatwa kwa Tundu Lissu

$
0
0
Wabunge wote wa vyama vya upinzani waliokuwa bungeni katika kikao kinachoendelea jioni hii wametoka nje ya Bunge, wakipinga wenzao kufukuzwa bungeni pamoja na kitendo cha Mbunge Tundu Lissu kukamatwa.

Wabunge waliokuwa wameamuliwa kutoka nje ya ukumbi wa Bunge na Naibu Spika Dkt Tulia Ackson ni pamoja na mbunge wa Kawe Halima Mdee, Mbunge wa Bunda Mjini Ester Bulaya na Mbunge wa Serengeti Marwa Ryoba.

Wabunge hao watatu wamedaiwa kupinga uamuzi wa Naibu Spika kuhusu muongozo ulioombwa na mbunge wa Kigoma Mjini Zitto Kabwe, kuhusu utaratibu uliotumika kumkamata mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu.

Mara baada ya Naibu Spika kutoa maamuzi ya kuwaondoa wabunge hao watatu bungeni, ndipo wabunge wengine wa upinzani pia wakaamua kutoka kama ishara ya kupinga maamuzi hayo, pia ikiwa ni ishara ya kupinga utaratibu wa kukamatwa kwa mbunge Tundu Lissu.

Nje ya ukumbi wa Bunge, Mbunge wa Kigoma Mjini Zitto Kabwe , amesema wamefikia hatua hiyo kuonesha kuwa uataratibu unaotumiwa kukamata wabunge wakiwa bungeni siyo sahihi, na kwamba kesho wataendelea na vikao vya bunge lakini mapambano yataendelea.

"Kesho tunarudi bungeni, lakini mapambano yataendelea, tunataka kuonesha kuwa utaratibu huu wa kuvizia wabunge kwenye milango ya bunge bila taarifa rasmi ya Spika na bila kuwaeleza wabunge sababu za kukamatwa kwao siyo sawa. Tukilifumbia macho litakuja kumtokea mbunge yoyote hata wa CCM" Amesema Zitto.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatano ya February 8

Askofu amfananisha Rais Magufuli na Yesu Kristo......Asema Hata Yesu Alisisitiza Juu ya Ulipaji wa Kodi na Usshuru

$
0
0
Na Nathaniel Limu, Singida
Askofu mstaafu wa kanisa la Pentekoste (FPCT)  Singida mjini Dk. Paul Samweli, amesema suala la serikali ya Dk.  John Magufuli kusisitiza ulipaji wa kodi na ushuru ni utekelezaji wa maagizo ya Yesu Kristo,  hivyo waumini na Watanzania kwa ujumla, wanatakiwa kutii na kuzingatia wajibu wao huo.

Akiijengea nguvu hoja yake hiyo, amesema kwa mujibu wa kitabu kitakatifu cha Mungu  cha biblia Warumi 13  (msitari 1-14), inaonesha wazi Yesu kristo alipigia debe Mamlaka ya mapato Tanzania (TRA).

Askofu Paul alisema katika Warumi 13  kimeainisha kuwa watoza kodi na ushuru, ni wahudumu wa Mungu kuwa wapeni haki zao, mtu wa kodi, kodi, mtu wa ushuru, ushuru.

Dk. Paul amesema hayo juzi wakati akihubiri kwenye ibada ya kawaida ambayo pia ilihudhuriwa na kamanda wa jeshi la polisi  mkoa mkoani  hapa ACP Debora Daudi Magiligimba.

Akisisitiza, alisema kwa vile ulipaji   kodi umepewa baraka zote na Mwenyezi Mungu, waumini wa madhehebu mbalimbali ya dini, wanapaswa kuwa mstari wa mbele katika kutii agizo la Mungu la kulipa kodi uliowekwa kisheria bila shurti.

“Serikali ya Rais Magufuli katika hili la uhimizaji wa ulipaji kodi na ushuru, inafanya vizuri kazi iliyopo mbele yetu waumini wa dini na Watanzania kwa ujumla, ni kulipa kodi na ushuru kwa wakati, ili nchi yetu iweze kusonga mbele kimaendeleo. Haya mambo ya  kukwepa kulipa kodi au ushuru, yakomeshwe,” alisema.

Kuhusu watoza kodi na ushuru Dk.Paul, alisema kuwa katika Biblia (Luka Mtakatifu 3 -12-17)  inasema  watoza kodi/ushuru waliagizwa wasitoze kubwa ambayo itakuwa kinyume na sheria inavyoagiza.

Akifafanua, alisema wafanyakazi wa TRA, katika utekelezaji wa majukumu yao, wanatakiwa kutoza kodi na ushuru kwa mujibu na sheria, kanuni na taratibu zilizowekwa na si vinginevyo.

“Wakitoza kodi au ushuru mkubwa ambao upo  kinyume na sheria, watakuwa wanamudhulumu mlipaji, kitendo hicho sio tu binadamu mwenye maadili mema hakipendi, lakini pia, nacho hakitampendeza Mwenyezi Mungu,” alisema.

Kwaupande wa jeshi la polisi, Dk. Paul amesema kwamba katika kitabu cha Warumi 3 mstari wa 14, kimewataka askari polisi katika kutekeleza majukumu yao, wasidhulumu mtu wala wasiwababikizie watu kesi za uongo. Pia watosheke na mshahara wanaolipwa.

“Kamanda maneno yaliyotamkwa  na mtumishi wa Mungu Yohana, yanamtaka  kila askari polisi, aridhike na mshahara wake. Ina maana asiwe na tamaa ya kuomba rushwa na vile vile asibabikie  mwananchi kesi, bali atatekeleza wajibu wake kwa mujibu wa mkataba wake wa kazi,” alisema.

Dk. Paul alitumia  fursa hiyo kulipongeza jeshi la polisi mkoa wa Singida kwa juhudi zake za kudhibiti vitendo vya kihalifu ambavyo vinaweza kuhatalisha amani na utulivu ulipo.

“Nikupongeze kipekee kamanda Magiligimba kwa kuazisha utamaduni mpya wa kuongea na waumini wa madhehebu ya dini kwenye nyumba zao ibada. Pia kwa uamuzi wako wa kudhibiti uhalifu kabla haujatokea. Kwa kifupi unataka dalili za kutokea uhalifu, zishughulikiwe mapema kabla hazijaleta madhara. Sisi kanisa tunakuunga mkono katika hili. Mungu akutangulie,” alisema Dk.Paul.


Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images