Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Jeshi la Polisi Lasema Linaendelea kuchunguza alipo msaidizi wa Mbowe, Ben Saanane.......Latoa ufafanuzi kuhusu maiti saba

$
0
0
Ukiwa umetimia mwezi mmoja, baada ya Msaidizi wa Freeman Mbowe ambaye ni Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Benard Saanane (pichani) kupotea, Jeshi la Polisi limesema linachunguza taarifa za kupotea kwake ambazo ilizopokea kutoka kwa mtu aliyejitambulisha kama rafiki wa Saanane Desemba, 5, 2016.

Wakati akizungumza na waandishi wa habari, Desemba 21, 2016 Kaimu Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai, CP Robert Boaz amesema Jeshi la polisi limefungua jalada la uchunguzi na kwamba taratibu za kiupelelezi za mtu aliyepotea zilifuatwa na bado upelelezi wa suala hilo unaendelea.

“Tuanashukuru wananchi wanaotupatia taarifa kuhusu tukio hilo, tunaahidi kwamba taarifa hizo tutazifanyia kazi. Tunazidi kuwaomba wananchi wenye taarifa za kupotea Saanane waziwasilishe katika kituo chochote cha polisi,” amesema.

Sambamba na hilo, Kamishna Boaz amefafanua tukio la uzikwaji wa maiti saba zilizokufa maji katika mto Ruvu, pasipo kufanyiwa uchunguzi wa kutambua waliokufa na chanzo cha vifo vyao.

“Mtakumbuka kati ya tarehe 6 hadi 12, 1016 huko mto Ruvu jeshi la polisi lilipata taarifa ya kuonekana maiti saba zikiwa zinaelea mtoni kwa nyakati na maeneo mbalimbali, baada ya taarifa hizo kupatikana askari na daktari walifika eneo la tukio na kufanya uchunguzi wa kitaalamu,” amesema na kuongeza.

“Kutokana na ukweli kwamba baadhi ya maiti zilikuwa zimeharibika, maiti 6 ziliamuliwa kuzikwa katika eneo la tukio na moja yenye unafuu ilipelekwa hospitali ya wilaya ya Bagamoyo kwenye chumba cha maiti hadi pale ilipozikwa na halmashauri baada ya maiti hiyo kutotambuliwa na mtu yeyote.”

CP Boaz amesema hatua zote za kitaalam zilifuatwa na kwamba upelelezi unaendelea kufanywa ikiwemo wa kuwatambua marehemu hao na kujua chanzo cha vifo vyao

Wizara yalaani Ukeketaji wa Watoto maeneo ya Kivule, Dar es Salaam

$
0
0
Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto inakemea vikali vitendo vya ukeketaji vinavyotaarifiwa kufanyika katika Kata ya Kivule, Manispaa ya Ilala jijini Dar es salaam, na mikoa mengine ambayo imekaririwa na vyombo vya habari.

Wizara inaagiza wazazi na walezi kuacha mara moja vitendo vya ukeketaji kwani ni ukatili, husababisha madhara kwa watoto wa kike na wasichana ni kosa la jinai.

Athari za ukeketaji kwa wahanga ni pamoja na kusababisha majeraha kwa watoto, vifo, vilema, maradhi kama fistula na mengineyo. Watoto wa kike na wanawake wamekuwa wakifanyiwa ukatili wa vitendo vya ukeketaji bila ridhaa yao na wakati mwingine ridhaa hiyo huwa imepatikana kwa hila, jambo ambalo ni ukiukwaji wa haki za binadamu.

Wizara inatoa rai kwa vyombo vya dola kuwakamata wazazi, walezi, mangariba, na wote wanaoendeleza vitendo vya ukeketaji dhidi ya watoto wa kike na wasichana katika kata ya Kivule na maeneo mengine nchini, na kuwafikisha mahakamani ili sheria iwezekuchukua mkondo wake.

Wizara itaendelea kupambana na vitendo vya ukeketaji vinavyotaarifiwa katika jamii zetu, na itaongeza juhudi ya utoaji elimu kwa jamii sambamba na kuwachukulia hatua wote wanaojihusisha na mila potofu ya ukeketaji.

Wito unatolewa kwa kila mwananchi kushiriki katika kuzuia vitendo vya ukeketaji na hasa kufichua matukio ya ukeketaji, na kutoa ushahidi mahakamani ili wahusika waweze kuchukuliwa hatua stahiki.

Wizara inatoa rai kwa Maafisa Maendeleo ya Jamii na Maafisa Ustawi wa Jamii katika Mikoa, Halmashauri na Kata katika maeneo ambako kunaarifiwa kuwepo vitendo vya ukeketaji kuhakikisha kuwa wanashirikiana na mamlaka husika kuzuia ukatili huo katika nchi yetu.

Erasto T. Ching’oro

Msemaji wa Wizara-Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na watoto

21/12/2016

Maoni Sheria ya Huduma za Habari mwisho Januari 10

Majambazi Wawili Wauawa Jijini Mbeya Katika Mapambano Makali Kati Yao Na Jeshi La Polisi

$
0
0
Askari wa Jeshi la Polisi Mkoani Mbeya wamefanikiwa kuzuia tukio la ujambazi katika mapambano ya kurushiana risasi na watu waliosadikiwa kuwa ni majambazi na kuua wawili kati yao.

Taarifa iliyotolewa leo na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Dhahiri Kidavashari imesema kuwa mnamo tarehe 19.12.2016 majira ya saa 1:45 jioni katika Kijiji cha Busisya, Wilaya ya Rungwe, Askari Polisi walipata taarifa za siri za kuwepo kwa majambazi wenye silaha ambao walikuwa na lengo la kufanya uvamizi katika Duka la Mfanyabiashara wa soda na bia za jumla ambaye pia ni wakala wa kutuma na kupokea pesa kwa njia ya mtandao.

Askari hao walianza kuwafuatilia majambazi hao na muda wa saa 1:45 jioni askari walikutana na majambazi hao wakiwa wamepakiana katika pikipiki ambapo baada ya majambazi hao kugundua kuwa wanafuatiliwa na askari walianza kuwarushia risasi askari na ndipo yalitokea majibizano ya risasi kati ya askari na majambazi hao.

Askari walifanikiwa kuwapiga risasi majambazi wawili ambao walifariki papo hapo na mmoja wao aliweza kutupa silaha aliyokuwa akiitumia na kukimbia.

Aidha katika tukio hilo silaha bunduki tatu pamoja na risasi tisa ziliweza kupatikana zilizokuwa zinatumiwa na majambazi hayo. Silaha hizo ni Mark IV yenye namba 38482 na risasi mbili, Short Gun Greener yenye namba G.73878 na risasi 01 na Gobole lililotengenezwa kienyeji ambalo halina namba na risasi 06.

Pia baada ya kupekuliwa majambazi hao walikutwa na vitu vingine ambavyo ni Rungu moja, Praizi moja, Bisibisi moja, mafuta ya cherehani, koti la ngozi rangi ya brown pamoja na begi dogo rangi nyeusi ambalo lilitumika kuhifadhi vitu hivyo.

Miili ya marehemu imehifadhiwa katika Hospitali ya Serikali Makandana Wilaya ya Rungwe kwa uchunguzi wa kitabibu na bado haijatambulika. Msako unaendelea. Katika tukio hilo hakuna mali iliyoporwa wala askari kupata madhara. Jitihada za kumtafuta jambazi aliyekimbia zinaendelea, Upelelezi unaendelea.

Rais wa Gambia: Hakuna wa kunitoa Madarakani, labda Mungu Pekee

$
0
0
Rais wa Gambia Yahya Jammeh amesema kuwa atakataa jaribio lolote la viongozi wa eneo la magharibi mwa Afrika la kumlazimisha kuondoka madarakani licha ya kushindwa katika uchaguzi na mpinzani wake, Adama Barrow.

Akihutubia Wanachama wa Muungano nchini humo Bw. Jammeh amesema: ”Waje wajaribu kuniondoa wanasubiri nini? mimi ni mtu mpenda amani lakini haimaanishi kwamba sitalitetea taifa langu, kwa ujasiri na uzalendo na kuibuka mshindi”.

“Mimi sio muasi, haki yangu haiwezi kuvurugwa. Hii ni nafasi yangu, hakuna mtu anayeweza kuniondoa labda Mungu,” amesema.

Amesema kuwa alikataa wito wa Muungano wa Viongozi wa Mataifa ya Magharibi ECOWAS akiwemo Rais Muhammadu Buhari wa Nigeria na Ellen Johnson Sirleaf wa Liberia kuondoka nchini Gambia.

“’Wao ni kina nani wa kuniambia mimi niondoke nchini mwangu,” amesema na kuwashutumu viongozi hao kwa kuingilia mambo ya ndani ya Gambia.

ECOWAS tayari imesema kuwa inamtambua Bw. Barrow kama Rais wa taifa hilo na kwamba litachukua hatua zozote kuhakikisha kuwa matokeo ya uchaguzi yanaheshimiwa.

Viongozi wa eneo hilo watahudhuria kuapishwa kwa Bw. Barrow mnamo mwezi Januari 18 kulingana na taarifa ya Ecowas.

Rais Jammeh awali alikuwa amekubali matokeo ya uchaguzi huo mnamo Desemba 1, 2016 lakini baadaye akaitisha uchaguzi mpya utakaoandaliwa na tume ya uchaguzi inayomcha Mungu kwa madai kuwa matokeo hayo uchaguzi yaligubikwa na dosari.

Uteuzi: Mhandisi Boniface Gissima ateuliwa kuwa Mkurugenzi Mkuu wa REA

$
0
0

Bodi ya Nishati Vijijini (REB) imemteua Mhandisi Boniface Gissima NyamoHanga kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kuziba nafasi iliyoachwa wazi na aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu wa Wakala Dk.Lutengano Mwakahesya aliyestaafu mwezi Juni 2016.

Kwa mujibu wa Taarifa iliyotolewa kwa Vyombo vya Habari na Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini Dk.Gideon Kaunda inaeleza kuwa uteuzi huo umefanyika kwa mujibu wa Sheria namba 8 ya mwaka 2005 ya Nishati Vijijini katika kikao kilichofanyika Tarehe 17 Desemba 2016.

Aidha taarifa hiyo inaeleza kuwa kabla ya uteuzi huu Mhandisi Gissima Nyamo­Hanga alikuwa Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA).

Imeongeza kuwa Mhandisi Gissima ana uzoefu wa miaka 20 katika Sekta ya Nishati na pia ameshika nyadhifa mbalimbali tangu mwaka 2008 alipoajiriwa REA.

Mbali na hayo Mhandisi huyu amehitimu Shahada ya Uhandisi katika fani ya Umeme, Shahada ya Uzamili katika Menejimenti ya Uhandisi,Shahada ya Uzamili ya Usimamizi wa Biashara (MBA) zote kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Stashahada ya Juu ya Sheria na Upatanishi na Usuluhishi ya Chuo cha Ustawi wa Jamii Dar es Salaam.

Bodi ya Wakala wa Nishati ya Umeme Vijijini (REA) inaomba sekta mbalimbali kumpatia ushirikiano Mhandisi Boniface Gissima Nyamo­Hanga ili kumuwezesha kutekeleza majukumu na malengo yake.

Uhamiaji Yazipiga Marufuku Simba, Yanga na Azam Kutumia Wachezaji wa Kigeni

$
0
0


Serikali imevipiga marufuku Klabu za ligi kuu Tanzania hususani Simba, Yanga na Azam kuwatumia wachezaji wa kigeni mpaka watakapokamilisha taratibu zao za uhamiaji.

Uamuzi huo umekuja siku chache baada ya klabu ya Ndanda FC kutuma malalamiko TFF kwamba Simba iliwatumia wachezaji wake wawili wa kigeni Daniel Agyei na James Kotei kwa madai kwamba hawana vibali vya kufanya kazi nchini.

Klabu hizo zimepewa maagizo kwamba wachezaji na makocha wote wa kigeni ambao hawajakamilisha taratibu za uhamiaji hawatoruhusiwa kuzihudumia klabu zao hadi hapo watakapokamilisha taratibu hizo.

Idara ya uhamiaji kupitia kwa afisa uhamiaji John Msumule leo alitoa tamko kwa klabu zote za Ligi Kuu Tanzania bara kutoendelea kuwatumia wachezaji wake wa kigeni hadi watakapotimiza masharti ya uwepo wao nchini kisheria na uhamiaji wamezitaka klabu za Simba, Yanga na Azam FC kuhakikisha wachezaji wake na makocha wao wa kigeni wanapata vibali vya kufanyia kazi nchini pamoja na kuishi.

Hata hivyo kwa upande wa Yanga wao wachezaji wao wana vibali vya kazi na vya kuishi nchini isipokuwa makocha wao ndio wana vibali vya kazi pekee.

Kwa upande wa watani zao wa jadi Simba wao hawajatimiza vigezo hivyo kwa wachezaji wao wa kigeni na makocha wao, hivyo hawaruhusiwi kuendelea kuwatumia wachezaji wao ambao hawana vibali mpaka watakapo vipata vibali ingawa uongozi wa klabu ya Simba ulisema kuwa wachezaji hao wamekamilika kila kitu.

Habari zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Alhamisi ya Disemba 22


Aliyekufa muda mfupi baada ya kubatizwa azikwa kiislam

$
0
0

Kijana Issa Juma aliyeripotiwa kufariki dunia Jumapili iliyopita, muda mfupi baada ya kubadili dini na kubatizwa katika mto mmoja kwa imani ya Kikristo akijiunga na kanisa la Efatha kwa jina la Paulo, amezikwa kwa imani ya Kiislam.

Uamuzi huo umefikiwa baada ya kuwepo mvutano kati ya Kanisa la Efatha na viongozi wa dini ya Kiislam wakitaka kijana huyo azikwe kwa imani yao, lakini mwisho kauli ya wazazi wa marehemu ilikuwa na nguvu zaidi na hivyo kuzikwa kwa imani ya Kiislam.

Akizungumzia uamuzi huo, mama mdogo wa marehemu ambaye jina lake halikupatikana alizungumza kwa niaba ya mama mzazi, Rehema Juma alithibitisha kuwa walimzika ndugu yao Jumanne wiki hii kwa imani ya Kiislam.

Kifo cha kijana huyo kiliibua sintofahamu ikiwa ni saa chache baada ya kuzaliwa kwa mara pili kwa imani ya Kikristo na haikufahamika mara moja chanzo chake kama alikuwa na ugonjwa ama ni masuala ya kiimani.

Shahidi wa pili atoa ushahidi Kesi ya Tundu Lissu.......Neno ‘dikteta uchwara’ Latikisa

$
0
0
Kesi ya uchochezi dhidi ya Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu jana imeendelea katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam ambapo upande wa Mashtaka umetoa ushahidi wa pili.

Lissu anakabiliwa na mashtaka ya kutoa kauli za kichochezi na maudhi dhidi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Magufuli.

Shahidi huyo wa pili aliyetambulishwa kama ASP Kimweri, alisema kauli ya Lissu aliyoitoa June 28 mwaka huu kuhusu ‘Dikteta uchwara’, ililenga katika kufanya uchochezi na ilikuwa ya maudhi dhidi ya Rais na ililenga kuchochea wananchi kuipinga na kuichukia Serikali.

Akizungumza mbele ya Hakimu Mkazi, Godfrey Mwampamba, shahidi huyo aliongeza kuwa kauli hiyo ya Lissu pia ililenga katika kuhatarisha usalama wa taifa kama ingesambazwa sehemu kubwa.

Naye Wakili wa Lissu, Peter Kibatala alimtaka shahidi huyo kuieleza mahakama ni nani ambaye mteja wake alikuwa anamtaja kama ‘dikteta uchwara’ na taifa analolizungumzia kwenye madai yake.

Akijibu maswali ya Wakili Kibatala, ASP Kimweli alisema kuwa hakufahamu kiuhalisia ni nani ambaye Mbunge huyo alikuwa akimrejea katika matamko yake na pia hakufahamu ni taifa gani alilokuwa akilimaanisha.

Kesi hiyo imeahirishwa hadi Januari 18 mwakani itakaposikilizwa tena mahakamani hapo. Lissu yuko nje kwa dhamana.

Godbless Lema augua ghafla gerezani......ashindwa kufika mahakamani Kusikiliza Kesi Zinazomkabili

$
0
0

Kesi iliyokuwa isikilizwe 21 Disemba 2016 inayomkabili Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema pamoja na mkewe, Neema Lema wakituhumiwa kumtukana Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo imeahirishwa kutokana na hali ya Godbless Lema kuwa mbaya gerezani.

Taarifa za Godbless Lema kushindwa kufika mahakamani zimetolewa na wakili wa serikali Elizabeth Swai kwa Hakimu Mfawidhi katika Mahakama ya Hakimu Mkazi, Augustino Rwezile ambapo alisema kuwa alipata taarifa kutoka kwa Afisa Magereza zikieleza kuwa mbunge huyo anaumwa na amepewa mapumziko hivyo asingeweza kufika mahakamani.

Aidha, taarifa kutoka kwa kiongozi huyo wa magereza hazikueleza wazi kuwa mbunge huyo anaugua ugonjwa gani.

Kuhusu kesi hiyo inayowakabili wanandoa hao wawili jana  walikuwa wasomewe hoja za awali ambapo pia shahidi wa kwanza kutoka upande wa Jamhuri, George Katabazi alikuwa atoe ushahidi.

Godbless Lema na Neema Lema wanakabiliwa na kesi ya kumtukana Mkuu wa Mkoa wa Arusha kitendo wananchodaiwa kuwa walikitenda kupitia ujumbe mfupi wa simu mara baada ya Rais Magufuli kumteua Mrisho Gambo kuuongoza mkoa huo.

Kesi hiyo imeahirishwa hadi tarehe 18 Januari 2017.

Mkuu wa Wilaya aagiza kukamatwa mwandishi wa habari wa ITV

$
0
0

Mwandishi wa habari wa Kituo cha ITV mkoani Arusha, Khalfan Lihundi, anashikiliwa na polisi katika Kituo cha Polisi Usa River, wilayani Arumeru kwa tuhuma za kuandika habari zinazodaiwa kuwa ni za uchochezi.

Lihundi alikamatwa jana jijini hapa majira ya saa nane mchana na askari anayedaiwa kutumwa na Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, Alexander Mnyeti.

Mmoja wa waandishi wa habari walioshuhudia tukio hilo, Basil Elias, alisema kuwa, walipokuwa ofisini, alifika ofisa wa polisi akidai ametumwa kumfuata Lihundi kwa ajili ya mahojiano.

Kwa mujibu wa Elias ambaye alimnukuu ofisa huyo wa polisi, Lihundi anadaiwa kuandika habari ya uchochezi kuhusu mgogoro wa maji bila kumhoji mkuu huyo wa wilaya.

“Habari hiyo inayodaiwa kuwa ni ya uchochezi, ilikuwa ni malalamiko ya wananchi juu ya tatizo la maji katika wilaya hiyo,” alisema Elias.

Akizungumzia tukio hilo, Mwenyekiti wa Chama  cha Waandishi wa Habari, Mkoa wa  Arusha (APC), Claud Gwandu, pamoja na kulaani  tukio hilo, alisema hatua hiyo haikubaliki kwani  haikufuata taratibu za kuadhibu mwandishi wa habari.

“Hili ni tukio la kulaani na halikubaliki kwani kama mwandishi amekosea, zinapaswa kufuatwa taratibu na siyo kukamatwa kama mhalifu.

“Kilichofanyika ni matumizi mabaya ya madaraka, hivyo viongozi wa kuteuliwa hasa wakuu wa wilaya, wawe na utaratibu wa kufuata taratibu kwani mwandishi akikosea, kuna taratibu za kufuata, tunachotaka apewe dhamana,”alisema Gwandu.

Naye Kamanda wa Polisi, Mkoa wa Arusha, Charles Mkumbo, alisema amesikia kuna mwandishi amekamatwa kwa kosa la uchochezi.

“Mkuu wa wilaya ametumia mamlaka yake ya sheria inayomruhusu kumweka ndani mtu hadi saa 48. Kwa hiyo, siwezi kuingilia kati suala hilo,” alisema Kamanda  Mkumbo.

Tundu Lissu akamatwa na Jeshi la Polisi

$
0
0

TUNDU Lissu, Mbunge wa Singida Mashariki kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) anashikiliwa na Jeshi la Polisi katika Kituo Kikuu cha Kanda Maalumu ya Dar es Salaam

“Nashikiliwa na polisi hapa Kituo Kikuu kutokana na ile press conference (mkutano na waandishi wa habari) kuhusu kupotea kwa Ben Saanane,” alimweleza mwandishi wa habari hii kupitia simu leo.

Mwandishi alimtafuta Lissu kutaka kujua baadhi ya mambo, ndipo alipopokea simu na kueleza hivyo. Hakuna taarifa zaidi mpaka sasa.

Saanane ambaye ni Msaidizi wa Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa-Freeman Mbowe alipotea ghafla takribani mwezi mmoja sasa na hajulikani alipo.

Wafuasi wa CHADEMA wamekuwa wakimsaka kiongozi huyo bila mafanikio yoyote jambo ambalo limeendelea kuzua hofu kama yu hai ama ameuawa.

Tarehe 14 Desemba mwaka huu, Lissu alizungumza na waandishi wa habari katika Makao Makuu ya chama hicho, Kinondoni jijini Dar es Salaam akiomba vyombo vya ulinzi kusaidia kupatikana kwa kiongozi huyo.

Chanzo: Mwanahalisi

Serikali ya Nigeria Yakamata magunia 102 ya 'Mchele wa Plastiki'

$
0
0

Mara nyingi tumekuwa tukisikia juu ya vipodozi bandia au dawa bandia lakini masuala yanayohusu chakula bandia hayakuwa yakigonga vichwa vya habari sana hadi hivi karibuni dunia ilipopata mshtuko juu ya uwepo wa mchele wa bandia.

Mchele huu wa bandia ambao umekuwa ukihatarisha afya za watu wengi hufanana sana na mchele wa kawaida kiasi kwamba ukiiangalia kwa macho huwezi kuutofautisha. 

Mchele huu unaosambaa kwa kasi duniani hutengenezwa kwa plastiki na utofauti wake na mchele wa asili huonekana mara baada ya kuupika.

Jana, mamlaka katika mji wa Lagos nchini Nigeria ilikamata magunia 102 ya mchele wa plastiki yaliyokuwa yanaingizwa nchini humo na wafanyabiashara haramu ambao walitaka kuuza katika msimu huu wa sikukuu ili kujipatia fedha nyingi zaidi.

Nigeria inaendelea na uchunguzi  kutambua ni kiwango gani cha mchele huo kimekuwa kikiuzwa na ni vipi unaweza kuondolewa sokoni ili kulinda afya za raia wa Nigeria waliokwisha utumia na kuwapeleka wahusika wa biashara hiyo haramu mbele ya sheria

Mchele huu umeelezwa kuwa ni hatari sana kwa afya ya binadamu kwani ni sawa na kumlisha mtu plastiki lakini pia wingi wa kemikali zinazotumika katika utengenezaji wa mchele huo.

China imedaiwa kuwa ndiyo nchini inayoongoza kwa utengenezaji wa mchele huu.

SORRY MADAM -Sehemu ya 1 & 2 (Destination of my enemies)

$
0
0
MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA

Televishen pamoja na Tv zote nchini Tanzania, zipo hewani, kuweza kuyanyakua mazungumzo ya moja kwa moja ya Raisi Praygod Makuya, kwenye uteuzi wa mawaziri wapya, hii ni kutokana na waziri mkuu kuweza kujiudhulu, kwa kusumbuliwa na matatizo ya kiafya yaliyo mchukua kipindi kirefu kukaa nje ya ofisi pasipo uwepo wake. Kama kanuni na taratibu za nchi ya Tanzania, inamlazimu raisi kuweza kufanya hivyo punde tu waziri mkuu anapokuwa ameachia kiti hicho kinacho tamaniwa na kila kiongozi aliyopo serikalini.

Raisi akaanza kutaja majina ya mawaziri wapya watakao chukua nafasi za mawaziri walio punguzwa kwenye wizara mbalimbali. Masikio ya wananchi wengi wa Tanzania, ni kwenye wizara ya ulinzi, ambayo katika siku za hivi karibuni imetokea kuyumba, hadi wananchi kuanza kupoteza imani na serikali yao pamoja na jeshi zima la polisi. Majina kadhalika ya mawaziri wapya na wazamani walio badilishwa wizara ya kaendelea kutajwa, ikafikia kwenye wizara ya ulinzi ulinzi, hapa raisi akanyamaza kidogo na kumeza fumba la mate huku akizikodolea kamera zilizopo mita chache kutoka katika sehemu aliyo simama.

“Katika wizara ya ulinzi, nimeweza kufanya mabadiliko makubwa sana, ambayo ninaamini yatakwenda kufurahiwa na wananchi walio wengi. Kwa maana katika kipindi changu cha utawala nimeweza kupokea malalamiko mengi sana kuhusiana na uhalifu katika jamii inayo tuzunguka.”
“Wizara hii nimeweza kuweka watu hodari, wanao weza kuhakikisha wanafuta hofu yote iliyo jengeka katika mioyo mingi ya wananchi”

“Basi hapa waziri wa wizara hii, anaitwa Eddy Godwin, makamu wake atakuwa Bernad Ngoswe”
Wananchi wengi wakabaki wakiwa wameshangazwa na jina hilo kwani, hawajawahi kulisikia kwenye serikali tangu raisi Praygod kuingia madarakani.
“Hivi huyo Eddy Godwin ni nani?”
Mchaga mmoja alisikika akiwauliza wezake walio kusanyika katika duka lake la kuuza tv, redio na vitu vingine vya majumbani, lililopo maeneo ya Kariakoo.
“Hata mimi simfahamu”
“Hawa watakuwa wanagawiana, kwanini wasimpe yule….yule nani….”
“Chande?”
“Hapana yule, ambaye wamekwenda kumtupia kwenye kilimo”

“Ahaaaa Masele”
“Ehee huyo huyo, yule jamaa anaonekana yupo fiti sana”
“Yaani wee acha. Ila baadaye si wanaapishwa, tutakuja kumcheki huyo jamaa mwenyewe”
“Etieee”
“Naye asije akatuletea ufala kama huyu mwenzie aliye pita Haki ya Mungu, naye tutamuombea mabaya”
“Hahaaa maswawe punguza munkari bwana”
“Sio munkarti chalii yangu, yaani waziri akiwa ovyo hata hawa watendaji wake huku chini wote wanakuwa mambumbu,  hembu nenda pale sentral kaseme unatatizo uone kama hawata taka rushwa”

Nazungumzo ya watu mbalimbali katika mitaa tofauti ndani na nje ya jiji la Dar es Salaam, yalikuwa ni kuhusiana na huyo waziri mpya waliye msikia jina lake likitajwa. Wengi wao hawakuonyesha imani yoyote kwa waziri huyo, wanaamini naye atafanya madudu kama aliyo yafanya waziri aliye pita, kwa kuweza kuwapa polisi, uhuru ulio ptiliza, hadi inafikia hatua kwamba wananchi wa maisha ya chini wananyimwa haki zao za msingi, na wenye pesa ndio waliweza kupata haki zao na kuwakandamiza wale wasio kuwa nacho.
                                                                                            ***
“Mume wangu utaweza, au ndio majukumu mazito uliyo kabidhiwa?”
Phidaya alimuulimuuliza mumewe, huku akimfunga tai vizuri kwenda kwenye sherehe ya wao kuapishwa inayo fanyikia kwenye viwanja vya ikulu muda wa jioni ya siku hii,waliyo tangazwa kama mawaziri wapya.

“Mungu ni mwema nitaweza tu”
“Eddy mume wangu usije ukaenda ukaboronga huko ikawa ni mamatizo, mengine. Napenda tuishi kwa amani”
“Baby wewe ndio mtu wa kunipa mimi moyo, ila si mtu wa kunikatisha tamaa”
“Sio kama nakukatisha tamaa mume wangu, kumbuka kwamba tumepitia shida nyingi sana, hadi leo tumepata hii amani, ninaona kwamba tutaipoteza amani hii”
“Never, nitahakikisha amani ya familia yangu kwanza, haiyumbi kisha nitahakikisha imani ya wananchi wangu, pia inapatikana”
“Sawa mume wangu mimi ninakuombea kila laheri, ila usisahau kwamba ninakupenda sana Eddy wangu, kupota maelezo”
“Nakupenda pia mke wangu”
Taratibu Phidaya akambusu mume wake mdomoni, akamuweka vizuri koti la suti aliyo ivaa. Wakatoka nje ya chumba chao na kuanza kushusha ngazi za gorofani hadi wakafika sebleni, walipo wakuta Shamsa na Junio wakitazama tv.

“Badilisheni chaneli muda si mrefu mutaniona nikiwa nimetokelezea kwenye kideo, nitaringaje”
Eddy alizungumza huku akizunguka zunguka na kuwafanya watoto wake wote kucheka.
“Mungu wangu…!! Hapa hawajapata waziri”
Phidaya alizungumza huku akicheka kicheko, kilicho mfanya hadi machozi ya furaha kumwagika.
“Weee, waziri wameupata, yaani varangati nitakalo kwenda kulianzisha ni kama shehe aliye lishwa nguruwe pasipo kujua, sasa akagundua, hiyo movie yake nitawaadisia nikirudi”
“Hembu nenda huko muda ujue unakwenda, ngoja uvuliwe huo uwaziri wako uone kama utazunguka zunguka tena”
“Nani anivue, subutuu nitampiga ngumii moja tuu, hadi aimbe haleluya”

“Dady usisahaku kuniletea zawadi?”
“Mwanangu, huko ikulu kuna zawadi gani”
“Eddy nenda bwana unachelewa, weee jizungushe zungushe kama tiara”
Eddy akambusu mke wake, akafungua mlango na kutoka nje na kumkuta dereva wa gari la serikali akiwa anamsubiria kwa ajili ya kumpeleka ikulu kwenye sherehe hiyo.
“Shikamoo muheshimiwa?”
Eddy hakuitikia salamu hiyo zaidi ya kuingia ndani ya gari na dereva huyo naye akaingia ndani ya gari, akawasha gari taratibu wakatoka kwenye geti kubwa la jumbu hili la Eddy alilo linunua siku chache baada ya kutoka katika mapumziko ya harusi yao yeye na mke wake Phidaya.


Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Apokea Msaada Wa Maafa Ya Tetemeko La Ardhi Kagera

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amepokea fedha taslimu sh. milioni 10 kutoka Kanisa la Evangelistic Assemblies of God Tanzania (EAGT) zikiwa ni msaada kwa ajili ya watu waliopatwa na maafa kutokana na tetemeko la ardhi mkoani Kagera.

Makabidhiano ya mchango huo yamefanyika leo mchana (Alhamisi, Oktoba 22, 2016) kwenye Makazi ya Waziri Mkuu, Oysterbay, jijini Dar es Salaam.

Akikabidhi mchango huo, Askofu Mkuu wa Kanisa la EAGT, Dk. Brown Mwakipesile amesema kanisa hilo limeona lina wajibu wa kuisadia Serikali kuwapunguzia machungu watu waliopatwa na maafa kutokana na tetemeko la ardhi lililotokea mkoani Kagera, Septemba 10, mwaka huu na kusababisha vifo vya watu 17.

“Tumeona ni vema kanisa la EAGT lishiriki kuisadia Serikali kuwafariji wananchi waliopata maafa kutokana na tetemeko hilo. Tumeona ni wajibu wetu kwa sababu waliopatwa na maafa ni watu wetu wote. Tunawaombea wote waliopatwa na shida waweze kupata nafuu mapema zaidi,” amesema.

Askofu Mkuu Dk. Brown ametumia fursa hiyo kuipongeza Serikali kwa kusimamia vema suala hilo tangu lilipotokea hadi sasa na kuongeza kuwa wanamuomba Mwenyezi Mungu awape nguvu viongozi wa Serikali ya awamu ya tano ili waweze kutimiza majukumu yao ipasavyo.

“Ukiacha hili la tetemeko, tumeona jinsi Serikali ilivyosimamia vizuri suala la madawati hadi sasa kuna baadhi ya maeneo wamevuka hadi malengo. Tunamshukuru Mheshimiwa Rais Magufuli na Serikali nzima kwa kusimamia jambo hilo vizuri,” amesema.

Amesema kanisa hilo linatoa shukrani nyingi kwa Mheshimiwa Rais Dk. John Pombe Magufuli kwa jitihada zinazofanywa na Serikali yake kukabili mambo mbalimbali yanayowagusa wananchi walio wengi.

Akitoa shukrani kwa Baba Askofu Mwakipesile na viongozi wa kanisa hilo aliombatana nao, Waziri Mkuu ameahidi kuwa Serikali itahakikisha michango hiyo inafikishwa Kagera kwa walengwa. “Nawashukuru sana kwa jinsi mlivyoguswa na kuamua kuwachangia wenzetu waliopatwa na maafa, tutahakikisha inawafikia walengwa,” amesema.

Waziri Mkuu amesema anawashukuru sana viongozi wa dini zote kwa jinsi wanavyoisadia Serikali kuwahudumia wananchi kupitia sekta mbalimbali. “Tunatambua juhudi zinazofanywa na taasisi za dini zote kuunga mkono juhudi za Serikali, tunafarijika mno na tunawashukuru sana,” ameongeza.

Amemuomba Askofu huyo pamoja na viongozi wengine wa dini wawaombee kwa Mungu viongozi waliopo madarakani ili awape hekima na busara na awawezeshe kuwaongoza vema Watanzania.

Tetemeko hilo la ardhi liliharibu miundombinu ya barabara, shule, zahanati na kujeruhi watu 440. Pia lilisababisha nyumba 2,063 kuanguka huku nyingine 14,081 zikiwa katika hali hatarishi na 9,471 zikipata uharibifu mdogo huku wananchi 126,315 wakihitaji misaada mbalimbali.
                           

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,

Rais Magufuli Amteua Jaji Semistocles Kaijage kuwa Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi (NEC) Kuchukua Nafasi ya Damiani Lubuva

Mwandishi wa ITV Aliyekamatwa Kwa Amri ya Mkuu wa Wilaya Aachiwa Kwa Dhamana

$
0
0
Mwandishi  wa kujitegemea wa kituo cha televisheni cha ITV, Halfani Lihundi ameachiwa kwa dhamana kutoka katika kituo cha Polisi cha Changamoto, Usa River wilayani Arumeru mkoani Arusha alikokuwa anashikiliwa tangu juzi, na kutakiwa kuripoti kituoni hapo Desemba 27, mwaka huu.

Alikuwa anashikiliwa kwa amri ya Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, Alexander Mnyeti, baada ya kuripoti habari inayoelezwa na mkuu huyo wa wilaya kuwa haikuwa sawa na kuamuru kukamatwa kisha, kulala mahabusu na hatimaye kufanikiwa kutoka jana saa tisa alasiri.

Awali, waandishi wa habari wa Arusha walikusanyika kituoni hapo ili kujua hatma ya mwenzao na baadaye kuamua kwenda kumuona Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi ili kumweleza kuwa mwenzao amekamatwa kwa sababu ya migogoro ya wananchi.

Wakati Lukuvi anatoka kwenye kikao cha kujadili migogoro ya ardhi kilichofanyika ukumbi wa Mkuu wa Mkoa wa Arusha, waandishi waliimba wimbo wenye lengo la kufikisha ujumbe kuwa, wanataka wenzao aachiwe huru. Waliimba; “Solidarity Forever, Bring Back Halfani Lihundi.”

Lukuvi alisema hahusiki na suala hilo na kuwasihi wanahabari kwenda naye Usa River kwenye mkutano ambapo Mnyeti atatoa tamko juu ya suala hilo.

Lakini Mnyeti alipokuwa akitoka kikaoni hapo aliulizwa na waandishi kuhusu suala hilo na kosa lipi limefanya Lihundi kushikiliwa Polisi, lakini hakuzungumza chochote na kuelekea kwenye gari lake kusubiri msafara wa Lukuvi. 

Awali, ilidaiwa kuwa Mnyeti ndiye aliyeamuru Lihundi akamatwe kwa madai ya kuandika habari za uchochezi za kijiji cha Leguruki, Arumeru.

Alisema alipotaka kujua kosa analoshitakiwa nalo Lihundi, alijibiwa hana kosa ila yupo kwa amri ya Mkuu wa Wilaya. Hata hivyo, RB ya Polisi Usa River 4763/2016 inaonesha ana kosa la uchochezi.

Aliyenajisi binti wa miaka 9 Ahukumiwa Miaka 30 Jela

$
0
0
Mahakama  ya Wilaya ya Ilala, imemhukumu Shabani Huseni (29), kifungo cha miaka 30 jela, baada ya kupatikana na hatia ya kunajisi mtoto wa miaka tisa.

Akisoma hukumu hiyo jana Hakimu Mkazi Catherine Kihoja alisema upande wa mashitaka ulipeleka mashahidi watano ambao wameweza kuthibitisha mashitaka bila kuacha shaka yoyote.

“Kutokana na ushahidi uliotolewa mahakamani hapa umeweza kuthibitisha mashitaka hivyo, mshitakiwa ninamtia hatiani kama alivyoshitakiwa,’’alisema Hakimu Kioja.

Kabla ya kutolewa kwa adhabu hiyo Wakili wa Serikali, Neema Moshi, aliomba mahakama kutoa adhabu kali kwa mujibu wa sheria kwa kuwa mtoto aliyefanyiwa kitendo hicho ameathirika kisaikolojia na kupata madhara kiafya kutokana na kutokwa na harufu mbaya sehemu zake za siri.

Aidha, mshitakiwa aliomba mahakama impunguzie adhabu kwa kile alichodai kwamba hana ndugu, ombi ambalo lilitupiliwa mbali.

Inadaiwa kuwa mshitakiwa alitenda kosa hilo tarehe isiyofahamika Julai mwaka jana eneo la Kipunguni B, Moshi Baa wilayani Ilala ambapo alimbaka mtoto wa miaka tisa.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Ijumaa ya Disemba 23

Viewing all 45270 articles
Browse latest View live


Latest Images