Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Uteuzi: Rais Dkt Magufuli ateua Wenyeviti 7 wa Bodi za Taasisi za Serikali

0
0

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, amefanya uteuzi wa Wenyeviti 7 wa Bodi za Taasisi za Serikali, na pia ameteua Mwenyekiti wa Baraza la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi Tanzania na Mjumbe mmoja wa Baraza la Taifa la Biashara.

Taarifa iliyotolewa leo tarehe 19 Desemba, 2016 na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi imewataja walioteuliwa kama ifuatavyo;
 
1. Rais Magufuli amemteua Bw. Ali Mufuruki kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Mfuko wa Taifa wa Dhamana ya Hifadhi ya Mazingira.
 
Ali Mufuruki ni Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni za Infotech Investment na Mwenyekiti wa Taasisi ya Afrika inayojihusisha na uendelezaji wa vipaji vya uongozi katika ukanda wa Afrika Mashariki.
 
2. Rais Magufuli amemteua Mhandisi Christopher Kajolo Chiza kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TanTrade)
Mhandisi Christopher Kajolo Chiza anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Sabetha Mwambenja ambaye amemaliza muda wake.
 
3. Rais Magufuli amemteua Bw. Peter M. Maduki kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA)
 
Peter M. Maduki anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Prof. Idrissa Mshoro ambaye amemaliza muda wake.
 
4. Rais Magufuli amemteua Dkt. Yamungu Kayandabila kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania (TIRA).
 
Dkt. Yamungu Kayandabila ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi na anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Bw. Peter Ilomo ambaye amemaliza muda wake.
 
5. Rais Magufuli amemteua Prof. Godwin Daniel Mjema kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Kampuni ya Huduma za Fedha na Mikopo (UTT-MFI)
 
Prof. Godwin Daniel Mjema ni Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Balozi Fadhili D. Mbaga ambaye amemaliza muda wake.
 
6. Rais Magufuli amemteua Kepteni Ernest Mihayo Bupamba kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri ya Chuo cha Bahari (DMI)
 
Kepteni Ernest Mihayo Bupamba ni Mwendesha Meli Mkuu (Principal Captain) Katika Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi.
 
7. Rais Magufuli amemteua Dkt. Aloyce S. Hepelwa kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Taasisi ya Miradi ya Maendeleo ya Miundombinu (UTT-PID)
 
Dkt. Aloyce S. Hepewa ni Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
 
Aidha, Rais Magufuli amemteua Dkt. John Jingu kuwa Mwenyekiti wa Baraza la Uwezeshaji wananchi Kiuchumi Tanzania.
 
Dkt. John Jingu ni Mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
 
Halikadhalika, Rais Magufuli amemteua Dkt. Rashid Adam Tamatama kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Utafiti wa Uvuvi (TAFIRI).
 
 Dkt. Rashid Adam Tamatama ni Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
 
Pia, Rais Magufuli amemteua Bibi. Zuhura Muro kuwa Mjumbe wa Baraza la Taifa la Biashara (Tanzania National Business Council– TNBC).
 
Bibi. Zuhura Muro ni Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi inayojihusisha na huduma za ushauri wa ubora na mafunzo (Service Limited) katika ofisi zake za Dar es Salaam.
 
 Wateule wote waliotajwa hapo juu, uteuzi wao umeanza tarehe 17 Desemba, 2016
 
 Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam
19 Desemba, 2016

Wananchi 21 wafikishwa mahakamani kwa kuvamia na kufanya vurugu katika kituo cha polisi.

0
0
Jumla ya watuhumiwa 21 akiwemo mwanamke mmoja wamefikishwa katika mahakama ya Wilaya ya Chunya kwa kuhusika na vurugu zilizotokana na wananchi wilayani humo kuvamia kituo cha polisi kwa lengo la kuwatoa watuhumiwa wa mauaji ili kuwaadhibu.

Watu hao waliofikishwa mahakamani ni sehemu ya watuhumiwa 41 waliokamatwa, kati yao wanaume wakiwa 34 na wanaweke 7 baada ya vurugu zilizotokea jana na kusabababisha jumla ya watu 7 kujeruhiwa wakiwemo askari polisi wanne, na wananchi watatu huku mwananchi mmoja aliyefahamika kwa jina la AMOKE MBILINYI (25) akifariki dunia.

Taarifa ya Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya imeeleza kuwa tukio hilo limetokea mnamo tarehe 18.12.2016 majira ya saa 11:45 asubuhi katika Kituo cha Polisi Makongolosi kilichopo Kata ya Makongolisi, Wilayani Chunya ambapo kundi la wananchi walioamua kujichukulia sheria mkononi walivamia kituo hicho cha Polisi na kufanya fujo kwa kuwarushia  mawe hovyo askari.

Kwa mujibu wa jeshi hilo, lengo la uvamizi huo ilikuwa ni kuwatoa watuhumiwa wawili waliofahamika kwa majina ya 1. ERASTO ROBERT, mkazi wa Kilombero na 2. BASI LINUS mkazi wa Makongolosi waliokuwa wanakabiliwa na kosa la mauaji kwa lengo la kuwatoa nje na kuwauawa kwa kuwachoma moto. 

Aidha wananchi hao walifunga barabara ya Chunya/Makongolosi kwa kuweka mawe makubwa na magogo hali iliyosababisha usumbufu mkubwa wa watumiaji wengine wa barabara hiyo.

Jeshi hilo limesema thamani ya uharibifu bado kufahamika na hali imerejea kuwa shwari

Awali mnamo tarehe 11.12.2016 majira ya saa 23:20 katika Kitongoji cha Manyanya, mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la JACOB BROWN Mkazi wa Manyanya alivamiwa na watu wasiojulikana akiwa peke yake shambani kwake na kuuawa ambapo Polisi walifanya msako na kuwakamata watu hao wawili kwa mahojiano zaidi kuhusiana na tukio hilo.

Rais Magufuli Afanya Uteuzi Wa Wakuu Wa Wilaya Wawili Na Wakurugenzi Watatu .........Nafasi ya Humphrey Polepole yachukuliwa na Kisare Makori

0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, leo tarehe 19 Desemba, 2016 amefanya uteuzi wa Wakuu wa Wilaya 2 na Wakurugenzi 3 wa Mamlaka za Serikali za Mitaa.

Taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi imeeleza kuwa Mhe. Rais Magufuli amemteua Bw. Kisare M. Makori kuwa Mkuu wa Wilaya ya Ubungo katika Mkoa wa Dar es Salaam.

Bw. Kisare M. Makori anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Bw. Humphrey Polepole ambaye hivi karibuni ameteuliwa kuwa Katibu wa Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi (NEC), Itikadi na Uenezi.

Halikadhalika, Mhe. Rais Magufuli amemteua Bw. Avod Mmanda Herman kuwa Mkuu wa Wilaya ya Mtwara iliyopo katika Mkoa wa Mtwara.

Bw. Avod Mmanda Herman anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Dkt. Khatib M. Kazungu ambaye hivi karibuni ameteuliwa kuwa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango.

Aidha, Mhe. Rais Magufuli amemteua Bw. Ramadhan Geodrey Mwangulumbi kuwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga iliyopo Mkoani Shinyanga.

Bw. Ramadhan Geodrey Mwangulumbi anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Bw. Lewis Kalinjuna ambaye anastaafu kwa mujibu wa Sheria.

Mhe. Rais Magufuli amemteua Bw Rojas John Romuli kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda iliyopo katika Mkoa wa Katavi.

Bw. Rojas John Romuli anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Ngalinda Hawamu Ahmada aliyefariki dunia hivi karibuni.

Mhe. Rais Magufuli amemteua Bw. Rashid K. Gembe kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkinga iliyopo katika Mkoa wa Tanga.

Bw. Rashid K. Gembe anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Bw. Mkumbo Emmanuel Barnabas ambaye uteuzi wake ulitenguliwa hivi karibuni.

Uteuzi wa huu unaanza mara moja na wateule wote wanatakiwa kuripoti Makao Makuu ya Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) mara wapatapo taarifa hii.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam

19 Desemba, 2016

Makatibu tawala wapya 27 wateuliwa......Orodha kamili iko hapa

0
0
Serikali kupitia Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa umma imetangaza Makatibu Tawala wa Wilaya walioteuliwa kujaza nafasi zilizokuwa wazi za Makatibu Tawala wa Wilaya katika Wilaya nyingine mbalimbali.

Orodha kamili ya Makatibu Tawala wa Wilaya 27 walioteuliwa pamoja na vituo vyao vya kazi ni kama ifuatavyo ;-

Shibuda Ashinda Uenyekiti Baraza la Vyama vya Siasa......Aahidi Kuimarisha Uhusiano kati ya UKAWA na Rais Magufuli

0
0

Mwenyekiti mpya wa Baraza la Vyama vya Siasa nchini, John Shibuda ametamba kuwa ataimarisha uhusiano wa kisiasa kati ya Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) na Rais John Magufuli ambaye ni Mwenyekiti wa CCM. 

Shibuda ambaye ni Katibu Mkuu wa Chama cha Ada Tadea, alitoa tambo hizo jana, ikiwa ni dakika chache baada ya kuchaguliwa kuongoza baraza hilo kwa kipindi cha miaka miwili katika uchaguzi uliofanyika jijini Dar  akichukua nafasi ya Peter Kuga Mziray wa APPTMaendeleo kilichofutwa na Msajili wa Vyama vya Siasa. 

Shibuda alisema atatumia fursa, uzoefu na uwezo alionao kuhakikisha vyama vyote vinakuwa na matumaini ya ushiriki wa kisiasa kupitia heshima ya baraza hilo. 

“Nimepokea kwa furaha matokeo haya lakini najua nina mzigo mbele yangu. Hilo la mahusiano ninamtanguliza Mungu anisaidie ili kuhakikisha naotesha matumaini mapya katika baraza hili. Nitakunjua vizibo vyote vilivyoziba katika mahusiano haya, ushirikiano wa siasa zetu uwe kwa masilahi ya Watanzania na utaifa wetu,” alisema mbunge huyo wa zamani wa CCM na Chadema. 

Shibuda aliibuka mshindi baada ya kupata kura 20 dhidi ya mpinzani wake, Mwenyekiti wa CCK, Constantine Akitanda aliyefuata kwa kura 14. 

Jumla ya kura 36 zilipigwa huku mbili zikiharibika. Katibu wa CCK, Renatus Muabhi alipongeza ushindi wa Shibuda huku akitoa angalizo kuwa asikubali kutumika kulinda masilahi ya kundi la chama kilichopo madarakani. 

 “Namwamini kwa uzoefu wake atasaidia kurejesha heshima ya baraza hilo ila kama atayumbishwa, sisi tuko tayari kushawishi kura ya kumwondoa madarakani,” alisema. 

Wengine waliogombea kiti hicho ni Hashim Rungwe (Chaumma), Anna Mghwira (ACT), Fahmy Dovutwa (UPDP), Hassan Kisavya (NRA), na John Cheyo wa UDP ambaye alijitoa. 

Baadhi ya vyama vilivyoshiriki katika uchaguzi huo ni Sauti ya Umma (Sau), CUF, CCM, DP, Demokrasia Makini, Jahazi Asilia, Ada-Tadea, CCK na Chadema. 

Baraza la Vyama vya Siasa ni chombo kilichoundwa kwa mujibu wa Sheria ya Vyama vya Siasa kwa lengo la kuweka jukwaa la kujadiliana masuala yenye masilahi kwa Taifa na uimarishaji wa mfumo wa vyama vingi nchini.

Baba Mzazi Wa Ben Saanane Kukagua Maiti Iliyowekwa Kwenye Kiroba

0
0
Wakati polisi wakisema kuwa wanaufanyia mchakato wa vipimo vya vinasaba (DNA), mwili wa mtu anayedaiwa kuuawa nje kidogo ya mji wa Moshi na kuwekwa kwenye kiroba na kuchomwa moto, familia ya Ben Saanane, msaidizi wa Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe ambaye hajulikani aliko imesema inaenda kuuangalia mwili huo. 

Hatua hiyo ya polisi kupima DNA ilielezwa na Kamanda wa Polisi Mkoa Kilimanjaro, Wilbroad Mutafungwa baada ya hadi jana, mwili huo kutotambuliwa. 

Mauaji hayo yaligunduliwa Ijumaa iliyopita, baada ya watu waliokuwa na gari ndogo ambao hawajafahamika, kumchoma moto mtu huyo katika Kijiji cha Ongoma na kisha kutoweka kusikojulikana. 

Kamanda Mutafungwa aliwaambia waandishi wa habari jana kuwa mtu huyo hajafahamika na wala hakuna mtu aliyejitokeza kuutambua mwili huo hivyo kulilazimu jeshi kufanya uchunguzi huo wa kisayansi. 

Kamanda Mutafungwa alitoa wito kwa ndugu, jamaa na marafiki waliopotelewa na ndugu, wafike katika Hospitali ya Rufaa ya KCMC kuutambua mwili huo. 

Kuhusu madai ya marehemu kwamba alikuwa amevaa suruali inayofanana na sare za wafungwa, Kamanda Mutafungwa alisema si kweli kwani nguo iliyoonekana ni blanketi jepesi la rangi ya chungwa. 

Mzazi wa Saanane 
Wakati polisi ikijiandaa kwa mchakato huo, baba wa Saanane, Focus Saanane, jana alikuwa anajiandaa kwenda KCMC kuangalia mwili huo. 

Akizungumza jana mjini Moshi, Saanane alisema japokuwa mtoto wake alipotelea Dar es Salaam, watakwenda kuuangalia mwili huo ili kujiridhisha. 

Juzi Saanane alikaririwa akiiomba Serikali kufanya uchunguzi wa kupotea kwa mwanaye akisema ndiyo pekee yenye vyombo vya kiuchunguzi. 

Kuokotwa kwa mwili huo kunashabihiana na tukio la kupatikana kwa miili mingine saba katika Mto Ruvu mkoani Pwani ikiwa imefungwa katika viroba na kuwekewa mawe ili izame. 

Miili hiyo ilizikwa na wananchi wanaoishi jirani na mto huo bila kufanyika kwa vipimo vya DNA wala kutoa tangazo la watu waliopotolewa na ndugu zao kujitokeza kutambua maiti hizo hali iliyoibua utata. 

Tayari Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, alishaagiza kufanyika kwa uchunguzi wa miili hiyo na kutaka wale wote waliohusika na mauaji hayo watafutwe na kukamatwa.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumanne ya Disemba 20

Kiwango cha Pesa Kesi za Mafisadi Kushushwa Chini ili Kuwabana Wengi

0
0
WAZIRI wa Katiba na Sheria, Dk Harrison Mwakyembe amesema serikali inatarajia kujadili kushusha kiwango cha fedha kinachohusika katika makosa ya rushwa na uhujumu uchumi kwenye mahakama ya mafisadi ili kukomesha vitendo vya rushwa.

Mwakyembe alitoa kauli hiyo jana mara baada ya kufanya mazungumzo na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda.

“Nimeulizwa sana na waandishi wa habari tangu Julai hadi sasa walitegemea kungekuwa na kesi nyingi lakini kuna kesi moja katika Mahakama ya Mafisadi tumekuja kubaini kwamba uchache wa kesi ndiyo mafanikio makubwa ya hatua ya kisheria tuliyochukua,”amesema.

Aliongeza kwa sasa waliozoea kupora mabilioni wamerudi nyuma ambapo wezi hao wameonekana wakiiba fedha chini ya Sh bilioni moja iliyopo kisheria hivyo wanategemea kujadili sheria hiyo ili iwalenge hata wanaochukua kiasi kidogo.

“Sisi kama serikali tukiona wizi sasa umenza kupungua na kuenea katika viwango vya Sh milioni 400, 500, 700 tumeanza kujadiliana kuangalia uwezekano wa kushusha kiwango cha fedha ili tuweze kukomesha kabisa udokozi, ubadhilifu, wizi wa fedha au mali ya umma,”alisema.

Aidha alifafanua uamuzi wa Mkuu wa Mkoa huo, Paul Makonda kutafuta vijana wanaojua sheria ili kusaidia wananchi kabla ya kwenda mahakamani ni mzuri.

Aliongeza kuwa tayari wamepeleka mswada wa msaada wa kisheria ambao utasaidia wananchi hasa wa vijijini na wanawake ambao ndiyo wanaumizwa na desturi zilizopitwa na muda ili kuwasaidia kupata haki na itakuwa na wasaidizi wa kisheria nchi nzima wapatao 4,900.

Makonda alisema wamejadili utoaji na upatikanaji wa haki kwa wakati kwani kuna changamoto ya watu kuwa wengi na kuchelewa kupata haki zao.

Alisema kwa kuona adha hiyo mkoa huo kwa kushirikiana na Wakuu wa wilaya watajenga Mahakama za Mwanzo 20 ili kuongeza kasi za utoaji na upatikanaji wa haki kwa wananchi endapo wanapopelekwa vituo vya polisi.

Benki ya AfDB yaikopesha Tanzania Bilioni 360 kwa ajili ya bajeti ya 2016/2017

0
0
Na Benny Mwaipaja-WFM, Dar es salaam
Benki ya Maendeleo ya Afrika-AfDB, imeipatia Tanzania mkopo wenye masharti nafuu wa dola Milioni 164, karibu Shilingi Bilioni 360, kwaajili ya kuchangia Bajeti kuu ya Serikali katika kipindi cha Mwaka wa Fedha 2016/2017 pamoja na kuongeza mtaji wa Benki ya Maendeleo ya Kilimo nchini-TADB.

Mikataba miwili imesainiwa jana Jijini Dar es salaam kati ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Doto James kwa niaba ya Serikali na Mwakilishi Mkazi wa Benki ya Maendeleo ya Afrika anayeondoka Dkt. Tonia Kandielo.

Mkataba wa kwanza uliosainiwa ni kwa ajili ya kutunisha Mfuko Mkuu wa Serikali ambapo Benki hiyo imetoa dola za kimarekani milioni 70 sawa na tsh 154 bilioni ambazo zitaelekezwa kuongeza ufanisi wa utendaji kazi wa Shirika la Ugavi wa Umeme nchini-TANESCO.

Mkataba wa pili ni kwaajili ya kuongezea mtaji wa Benki ya Maendeleo ya Kilimo nchini-TADB wenye thamani ya dola Milioni 94 sawa na shilingi Bilioni 204 kwa ajili ya kuiongezea uwezo Benki hiyo kutoa mikopo yenye riba nafuu kwa wakulima ili kuongeza mnyonyoro wa thamani kuanzia uzalishaji, uongezaji thamani na upatikanaji wa masoko ya uhakika ya mazao ya wakulima.

Uhai wa mikopo yote miwili utakuwa ni miaka 40 ambapo serikali itaanza kuilipa baada ya miaka kumi tangu kutolewa kwake, huku riba yake ikiwa chini ya asilimia 1.

Akizungumza baada ya kusainiwa kwa mkopo huo, Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Doto James, amesema mkopo huo umekuja wakati muafaka na utasaidia kukuza na kuimarisha TANESCO na kuendeleza kilimo nchini.

“Tanzania ni nchi iliyonufaika zaidi na mikopo yenye masharti nafuu kutoka Benki ya Maendeleo ya Afrika-AFDB ikilinganishwa na nchi nyingine yoyote iliyoko katika Ukanda wa Kusini mwa Afrika,” alisema Bw. James.

Kwa upande wake, Mwakilishi Mkazi wa AFDB anayeondoka Dkt. Tonia Kandielo amesema kuwa hadi sasa Benki yake imeipatia Tanzania mkopo wenye thamani ya zaidi ya dola za Marekani bilioni 2, ambazo zimewekezwa kwenye miradi mbalimbali ikiwemo ujenzi wa miundombinu ya barabara, maji, nishati ya umeme, elimu na kilimo.

“Ninaamini kuwa hatua ya kuongeza mtaji katika Benki ya Maendeleo ya Kilimo-TADB itachochea maendeleo ya kilimo nchini, na tunaahidi kuwa tutaendelea kuiwezesha zaidi siku zijazo,” alisema Dkt. Kandielo.

Kuhusu Sekta ya Nishati, Dkt. Kandielo amesema kuwa Benki yake imeona umuhimu wa kuliwezesha shirika hilo ili liweze kutoa huduma kwa ufanisi zaidi ili kuchochea uchumi wa Taifa.

“Mikopo hii inahusiana na vipaumbele tulivyoviweka kama Benki ambavyo viko katika malengo matano ambapo tunataka kuwekeza katika sekta ya nishati, uzalishaji wa chakula, kuendeleza viwanda, kuiunganisha Afrika na kuboresha maisha ya waafrika kwa ujumla,” aliongeza Dkt. Kandielo

Wakati huo huo, Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango, amemuaga rasmi Dkt. Tonio Kandielo ambaye amehamishiwa nchini Afrika Kusini kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Benki hiyo atakaye simamia Kanda ya Kusini mwa Afrika.

Dkt. Mpango, amesifu jitihada kubwa zilizofanywa na mwana mama huyo katika kipindi cha miaka 6 aliyokuwepo hapa nchini ambapo ameweza kusimamia vizuri maslahi ya Tanzania katika Benki hiyo.

Amesema kuwa katika kipindi hicho Tanzania imeshuhudia maendeleo makubwa katika sekta za ujenzi wa miundombinu ya barabara, kilimo, maji na umeme, ambapo benki hiyo ilihakikisha kuwa miradi inatekelezwa kwa viwango vinavyotakiwa.

Amemwomba Mkurugenzi Mkuu huyo kuwezesha upatikanaji wa fedha kwaajili ya ujenzi wa Reli ya Kati kwa kiwango cha kimataifa (Standard gauge) inayohitaji fedha nyingi, kusimamia utekelezaji wa mradi wa umeme wa kikanda unaoanzia nchini Zambia, uboreshaji wa Bandari ya Itungi na Mbambabay.

Akijibu hoja za Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango, Dkt. Tonia Kandielo amesema kuwa anaamini mrithi wake ataendeleza mazuri aliyoyafanya na kwamba yeye binafsi atahakikisha anafuatilia kwa karibu miradi ambayo mikataba yake imesainiwa katika nyanja za maboresho ya sekta ya umeme na kilimo.


Taasisi zinazohamasisha ushoga kufutwa

0
0

WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba ametaka apewe taarifa kuhusu taasisi na mashirika yasiyo ya kiserikali (NGO) wanaohamasisha au kutangaza ndoa za jinsia moja nchini ili azifutie usajili mara moja.

Aidha ametaka kutajwa kwa watu wanaojihusisha na vitendo hivyo ili wachukuliwe hatua za kisheria kwa kujihusisha na vitendo hivyo ambavyo vinapigwa vita dunia nzima.

Nchemba aliyasema hayo jana mjini Kibaha alipokuwa akizungumza na taasisi za Kijeshi za mkoa huo zikiwemo Uhamiaji, Polisi, Magereza na Zimamoto juu ya kujua changamoto mbalimbali zinazowakabili.

Alisema kuwa taasisi hizo hazifai kwani zinafanya kazi ya laana ambayo ni kinyume cha maadili ya Kitanzania na hazistahili kuendelea kufanya kazi kwa upotoshaji huo.

“Leteni majina ya taasisi hizo ili tuzifute kwani hazistahili kuendelea kufanya jambo hilo ambalo ni laana na halipaswi kufumbiwa macho ndani ya jamii,” alisema Nchemba.

Kamanda wa polisi mkoani Pwani Bonaventura Mushongi alisema kuwa jeshi hilo linakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwa ni pamoja na upungufu wa vitendea kazi, ikiwa ni pamoja na magari.

Mushongi alisema kuwa licha ya kukabiliwa na changamoto hizo wamekuwa wakikabiliana na uhalifu kwenye mkoa huo ambao umekuwa kimbilio la wahalifu kutoka mikoa jirani ya Dar es Salaam.

Polepole atangaza 'vua gamba' ya CCM kivingine

0
0
Mabadiliko yaliyofanywa ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) yamekuja na mkakati mpya wa kuwavua ‘gamba’ makada wa chama hicho wenye ukwasi waliovuna kinyume na taratibu.

Katibu wa Halmashauri Kuu (NEC) Itikadi na Uenezi wa chama hicho, Humphrey Polepole amesema kuwa wako katika mkakati wa kukisafisha zaidi chama hicho, akiwataka matajiri wenye ‘makandokando’ wajiondoe mapema.

“Kuwa tajiri si dhambi na si kwamba CCM inafukuza matajiri, hapana. Tatizo letu kama CCM katika mwelekeo mpya, mtazamo mpya na maegeuzi yanayofanyika, hatuhitaji kuwa na aina ya matariji wanaojipatia utajiri wao kwa hila, kwa rushwa na kwa dhuluma,” alisema Polepole katika mahojiano na kituo kimoja cha runinga nchini.

“Ukijiona wewe ni tajiri na mikono yako ni michafu kwa maana ya kuwa na makando ya kukosa uaminifu, hulipi kodi, ukae mbali na CCM,” aliongeza.

Alisema watawachukulia hatua za kuwaondoa ndani ya chama hicho na kuwakabidhi kwa vyombo vya dola ili wachukuliwe hatua za kisheria.

Tangu alipochaguliwa, Polepole amekuwa akisisitiza kuwa chama hicho kitajikita katika msingi wake wa kuwatumikia wanyonge.

Mkakati huo wa kuwang’oa matajiri wasiowaaminifu ndani ya chama hicho unafanana na oparesheni iliyobatizwa jina la ‘Vua Gamba’ ndani ya chama hicho miaka kadhaa iliyopita, iliyolenga kuwang’oa viongozi na vigogo ambao walibainishwa kujipatia mali kinyume cha utaratibu na mafisadi.

Mahakama Kuu Yakubali Ombi la Godbless Lema Kuongezewa Muda wa Rufaa ya Dhamana Yake

0
0
Mahakama Kuu Kanda ya Arusha, imelikubali ombi la  Mbunge wa Arusha Mjini Godbless Lema,  la kuongezewa muda wa kuwasilisha Notisi ya nia ya kukata rufaa ya dhamana yake.

Akitoa uamuzi wake kuanzia saa 12:26 hadi saa saba mchana, Jaji Dk. Modesta Opiyo wa Mahakama hiyo, alisema Mahakama hiyo imeruhusu maombi ya kuwasilisha Notisi ya kuomba kuongezewa muda wa kuwasilisha notisi ya nia ya kukata rufaa ya dhamana yake.

Jaji Opiyo amesema hoja za Upande wa serikali zilizowasilishwa na Wakili Hashim Ngole za kudai waleta maombi hayo walikuwa wazembe na walichelewa siku nne kuwasilisha Notisi baada ya rufaa yao kuondolewa na Jaji Fatuma Masengi Desemba 2 hazina mashiko.

Alisema kuondoa kesi mahakamani haimaanishi kuwanyima fursa ya kupigania nia ya kukata rufaaa, bali milango inakuwa wazi haijafungwa.

Aidha amesema siku nne zinazolalamikiwa kuwa walichelewa kutoa maombi hayo, mahakama inaona hoja hizo hazina mashiko sababu siku mbili kati ya hizo zilikuwa siku za mapumziko Jumamosi na Jumapili, hivyo walitumia siku mbili kuandaa nyaraka na kuleta maombi hayo.

Pia alisema katika maombi hayo wametoa pia sababu za nia ya kutaka kukata rufaa na sababu hizo ziko wazi. 

“Katika hili hakuna uvunjifu wowote wa sheria uliofanywa na kutokana na hilo Mahakama hii inatumia busara zake kuruhusu maombi haya ya kutoa Notisi ya kuomba kuongezewa muda wa kukata rufaa juu ya dhamana yake Mbunge huyu,” alisema Jaji Opiyo.

Amesema Mahakama inatoa siku kumi pekee kuanzia uamuzi huo utolewa mleta maombi (Lema) kuwasilisha Notisi yake ya kuomba kuongezewa muda wa kukata rufaa.

Baada ya kutolewa kwa maamuzi hayo, tayari Wakili Sheck Mfinanga ameshakata Notisi Mahakama Kuu Kanda ya Arusha na kupokelewa.

Mfinganga amesema wanasubiri mahakama ili wapangiwe Jaji waendelee na kesi hiyo ya hatma ya dhamana ya Lema.

Polisi yamnasa mtuhumiwa Sugu wa utapeli Tanzania

0
0
Jeshi la Polisi nchini limefanikiwa  kumkamata mtuhumiwa wa utapeli anayejulikana kwa jina la  Wilfred Masawe (36) ,  mkazi wa  Buza, Temeke jijini Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Msemaji wa Jeshi Mtuhumiwa huyo alikuwa akitumia mbinu mbalimbali kutapeli zikiwemo kujitambulisha kama kiongozi wa serikali kwa kutumia mtandao wa Whatsapp,  huku akieleza kuwa yupo nje ya nchi na kuna tatizo la msiba ambao umetokea nchini na unamuhusu na hivyo alikua akitoa maelekezo kwa watendaji wa serikali waweze kusaidia gharama za matibabu hospitalini, gharama za kusafirisha mwili wa marehemu na gharama za mazishi.

Taarifa hiyo pia imesema mtuhumiwa huyo alikuwa akitumia mbinu ya kujifanya kiongozi mkubwa wa dini ya kikristo (Askofu) na kuwaambia waumini na viongozi mbalimbali kuhusu maandalizi ya makongamano ya kidini kwa lengo la kuwaomba michango kuweza kufanikisha makongamano hayo.

Baadhi ya matukio aliyofanikiwa kutapeli ni pamoja na kuwatapeli viongozi wa serikali, wafanyabiashara, mameneja na wakurugenzi wa taasisi za umma, wanasiasa pamoja na waumini wa madhehebu ya dini.

Aidha, matukio yote hayo alikuwa akiyafanya peke yake na alikuwa akiyaendesha kwa mawasiliano ya njia ya ujumbe mfupi (SMS) bila kuzungumza kwa simu.

Jeshi la Polisi linakamilisha taratibu za kisheria ili mtuhumiwa huyo afikishwe mahakamani ili sheria ichukue mkondo wake.
***
 

Mwenyekiti Wa CCM Taifa Rais Magufuli Akutana Na Viongozi Wapya Wa Chama Aliowateua Hivi Karibuni Na Dc Mteule Wa Ubungo

0
0
Mwenyekiti wa CCM Taifa Rais Dkt John Pombe Magufuli akisalimiana na Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Mteule Mhe. Kisare Makori akishuhudiwa na viongozi wapya wa CCM aliowateua hivi karibuni. Kutoka kulia ni Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM Humphrey Polepole, Katibu NEC Siasa na Uhusiano wa Kimataifa Kanali Ngemela Eslom Lubinga na Naibu Katibu Mkuu wa CCM Bara Ndg. Rodrick Mpogolo walipoenda kujitambulisha Ikulu jijini Dar es salaam leo Desemba 20, 2016.


Mwenyekiti wa CCM Taifa Rais Dkt John Pombe Magufuli akiwa na Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Mteule Mhe. Kisare Makori (kushoto) pamoja na viongozi wapya wa CCM aliowateua hivi karibuni. Kutoka kulia ni Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM Humphrey Polepole, Katibu NEC Siasa na Uhusiano wa Kimataifa Kanali Ngemela Eslom Lubinga na Naibu Katibu Mkuu wa CCM Bara Ndg. Rodrick Mpogolo walipoenda kujitambulisha Ikulu jijini Dar es salaam leo Desemba 20, 2016.
Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Mteule Mhe. Kisare Makori (kushoto) akibadilishana mawasiliano na na viongozi wapya wa CCM walioteuliwa hivi karibuni. Kutoka kulia ni Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM Humphrey Polepole, Naibu Katibu Mkuu wa CCM Bara Ndg. Rodrick Mpogolo na Katibu NEC Siasa na Uhusiano wa Kimataifa Kanali Ngemela Eslom Lubinga walipoenda kujitambulisha kwa Mwenyekiti wa CCM Rais Dkt John Pombe Magufuli Ikulu jijini Dar es salaam leo Desemba 20, 2016. PICHA NA IKULU

Serikali Haijazuia Watumishi Wa Umma Kukopa Benki

0
0
Kumekuwa na taarifa inasambazwa katika mitandao ya kijamii, makundi ya ‘WhatsApp’, ‘Facebook’ na majukwaa mbalimbali ikieleza kuwa Serikali imepiga marufuku watumishi wa umma kukopa Benki,SACCOS,VICOBA na Taasisi mbalimbali za kifedha.

Taarifa iliyotolewa leo tarehe 20 Desemba 2016 na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali imeeleza kuwa taarifa inayosambazwa, ambayo imetafsiri mawasiliano ya Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali ni ya kupotosha, hivyo watumishi wote wa umma wanaombwa kuipuuza.

Vilevile watumishi wa umma wametakiwa kuzingatia kuwa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali HAINA mamlaka ya kuzuia wala kuruhusu mtumishi yeyote wa Serikali kukopa au kutokopa katika Taasisi yoyote ya Fedha nchini.

Watumishi wa umma pia wamekumbushwa kuwa mikopo yote ya watumishi wa umma katika Taasisi za Fedha hutolewa kwa kuzingatia Sheria, Kanuni na taratibu zilizopo ili mradi mtumishi awe ametimiza vigezo.

Aidha, watumishi wa umma wameaswa kuacha tabia ya kusambaza taarifa zisizo za kweli na ambazo zina mamlaka husika ya kuzitoa ikiwa ni pamoja na kuzingatia maadili ya utumishi wa umma.
***
 

Ajali yaua Watu Wanne wakiwemo Polisi Wawili

0
0
Watu wanne wakiwamo polisi wawili, wamefariki dunia baada ya gari walilokuwa wakisafiria kuacha njia na kupindua katika kijiji cha Seruka kata ya Chipogoro tarafa ya Rudi wilayani Mpwapwa mkoa wa Dodoma.

Ajali hiyo ilitokea Desemba 19, mwaka huu, saa 11:30 jioni katika kijiji hicho baada ya gari walilokuwa wakisafiria T517 CDL Toyota Alphat katika barabara kuu ya Dodoma- Iringa, kuacha njia na kupinduka na kusababisha vifo vya watu wanne na majeruhi tisa.

Kaimu Kamanda wa Polisi mkoani humo, Ernest Kimola, amesema gari hiyo iliyokuwa ikiendeshwa na Aggrey Lucas, baada ya kufika katika kijiji hicho, liliacha njia na kupinduka na kusababisha vifo vya askari Konstebo Mahende na Konstebo Sasi Mwita ambaye ni askari mkoa wa Songwe.

Kamanda Kimola amewataja wengine waliofariki katika ajali hiyo ni mke wa Konstebo Mwita, Pendo Mwita na Emaculata Nyangi.

Amewataja majeruhi wa ajali hiyo ni Neema Mwita (8), Jenifa Mwita (4), Nyangi Wambura (23), Konstebo Nashon (23) ambaye ni polisi kituo cha Tunduma na Baraka Chacha (9).

Wengine ni Juli Mwita (6), Pc Enock ambaye ni mmiliki wa gari lililopata ajali, Makongoro Charles na Elizabeth Cosmas ambao wote wamelazwa katika hospitali ya mkoa wa Dodoma.

Aidha, kamanda Kimola amesema miili ya marehemu hao waliofariki katika ajali hiyo, imehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhia maiti katika hospitali ya mkoa wa Dodoma.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatano ya Disemba 21

Rais Magufuli Akataa Shule Kuitwa Jina Lake

0
0

Rais John Magufuli amekataa shule ya msingi iliyojengwa hivi karibuni eneo la Bunju, Wilaya ya Kinondoni kuitwa kwa jina lake badala yake ameagiza iitwe kwa jina la Mkuu wa wilaya hiyo, Ally Hapi. 

Taarifa ya badiliko la jina haikutolewa na Idara ya Kurugenzi ya Mawasiliano ya Ikulu kama ilivyozoeleka bali na mkuu wa wilaya hiyo wakati wa hafla ya kukabidhi vifaa mbalimbali vya usafi kwa uongozi wa shule hiyo. 

“Shule hii imejengwa kwa fedha zilizopatikana baada ya Serikali Kuu kubana matumizi. Tukaamua iitwe John Magufuli lakini yeye akatoa agizo shule ipewe jina la mkuu wa wilaya sina budi kukubaliana na hilo,” alisema Hapi. 

Shule hiyo mpya iliyopo Bunju jijini imejengwa kwa lengo la kupunguza msongamano wa wanafunzi katika Shule ya Msingi Bunju A ambayo ilikuwa na wanafunzi 3,224.

Mwalimu mkuu wa shule hiyo mpya, Ali Mwakapalila alisema ingawa inatarajiwa kuanza kupokea wanafunzi Januari 9 mwakani inakabiliwa na changamoto mbalimbali. 

“Hakuna umeme wala maji, hii inaweza kuleta madhara kwa wanafunzi hasa linapokuja suala la matumizi ya vyoo,” alisema. 

Baada ya hafla hiyo, Hapi alikwenda kwenye kiwanda cha saruji cha Twiga Cement ambako alipokea msaada wa mifuko 600 ya saruji kwa ajili ya kufanikisha ujenzi wa madarasa na majengo mengine. 

Akipokea msaada huo, Hapi alisema msaada kutoka Twiga Cement unaunga mkono juhudi za Serikali ya Awamu ya Tano inayoipa sekta ya elimu kipaumbele ili kuhakikisha inatolewa katika mazingira bora. 

“Msaada huu umekuja muda muafaka. Tumeshajenga shule ila tunataka kuongeza madarasa, maabara, ofisi ya elimu na kuzungushia uzio ili watoto wawe katika mazingira salama. Lengo ni kuifanya shule hii iwe ya kisasa na itakuwa mfano kwa shule zote za Wilaya ya Kinondoni,” alieleza. 

Pia, Hapi alisema wilaya hiyo ipo kwenye mipango ya kujenga maktaba ya kisasa kwa kushirikiana na kampuni hiyo ya saruji. 

Mkurugenzi Mtendaji wa Twiga Cement, Alfonso Velez alisema kuchangia katika shughuli za kijamii ni moja ya mambo ambayo wamekuwa wakiyapa kipaumbele zaidi. 

“Kushiriki shughuli za maendeleo katika jamii ni jambo ambalo tunalipenda zaidi. Yalipo maendeleo Twiga Cement ipo pia,” alisema Velez.

Ahukumiwa Miaka 25 Jela Au Faini Bilioni 3.7 Kwa Kujihusisha na Biashara ya Meno ya Tembo

0
0
Mahakama  ya Hakimu Mkazi Tanga, imemtia hatiani na kumuhukumu kwenda jela miaka 25 au kulipa faini ya Sh bilioni 3.7 mfanyabiashara Charles Kijangwa kwa kujihusisha na biashara ya meno ya tembo.

Kijangwa alihukumiwa jana mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi, Cresencia Kisongo, baada ya kuruka dhamana kwa miaka sita. Alishindwa kulipa faini.

Mshtakiwa huyo alikabidhiwa mahakamani hapo baada ya kukamatwa na askari wa kikosi cha kuzuia ujangili Kanda ya Mashariki na Pwani kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi Wilaya ya Lushoto.

Wakili wa Serikali Mwandamizi, Saraji Iboru, alidai mahakamani kuwa mshtakiwa Kijangwa alikuwa akitafutwa na Serikali kwa muda mrefu tangu mwaka 2010 baada ya kuruka dhamana katika shauri la uhujumu uchumi namba 6/2007.

Mshtakiwa alishtakiwa na wenzake Michael Msuya na Nyaisa Makori ambao walitiwa hatiani na mahakama, wakahukumiwa kwenda jela miaka mitano kwa kosa la kumiliki kilo 5,000 za meno ya tembo kwa shtaka la kwanza.

Katika shtaka la pili la kula njama, washtakiwa wote walihukumiwa kwenda jela miaka mitano au kulipa faini ya Sh 10,950,000 baada ya kupatikana na hatia ya kusafirisha kilo 5,000 za meno ya tembo kwenda nchini Taiwan mwaka 2006.

Iboru aliiambia mahakama kuwa washtakiwa watatu, Kijangwa na wenzake walihukumiwa kwenda jela miaka mitano au faini ya Sh 50,000 katika shtaka la kujihusisha na biashara ya nyara za Serikali kinyume cha sheria.

Alidai mshtakiwa hakufika mwenyewe mahakamani hapo bali aliletwa baada ya kukamatwa Desemba 11, mwaka huu wilayani Lushoto.

Aliiomba mahakama kumtia hatiani mshtakiwa na kuhakiksha anatumikia adhabu iliyotolewa dhidi yake akiwa hayupo.

Hakimu Kisongo baada ya kusikiliza maombi hayo, alimtia hatiani mshtakiwa na kumuhukumu kwenda jela miaka 25 au kulipa faini ya Sh bilioni 3.7.

Mshtakiwa Kijangwa alitenda kosa hilo Novemba 2005 na Aprili 2006 kwa kusafirisha makontena mawili ya meno ya tembo yenye ujazo wa tani 5,000 yaliyokamatwa katika bandari ndogo ya Konshugi nchini Taiwan.

Makontena hayo ambayo yalitokea katika Bandari ya Tanga yakiwa na shehena ya kamba za katani na meno ya tembo ndani yake, yalikuwa yanapelekwa Manila nchini Philipine.

Mapya Yaibuka Sakata la Bwana harusi Aliyemkimbia Bi Harusi Siku ya Ndoa

0
0
Mapya  yameibuka sakata la kukwama kufungwa kwa ndoa ya Samwel Mwakalobo na Ginen Mgaya, baada ya kubainika kuwa moja ya sababu ni Bibi harusi mtarajiwa kuendeleza uhusiano na mzazi mwenzake.

Bwana harusi, Samuel Mwakalobo alitoweka muda mfupi kabla ya kufunga ndoa na Ginen Mgaya  katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Usharika wa Isanga jijini Mbeya.

Mwakalobo (26) alizua taharuki hiyo  Ijumaa ya Desemba 16, baada ya kutoonekana kanisani kufunga ndoa mbele ya Mchungaji Andagile Mwakijungu.

Habari zimedai kuwa kabla ya mpango wa kufunga ndoa hiyo, Mgaya tayari alishapata mtoto kabla hajaolewa, na Bwana harusi kubaini dakika za mwisho kuwa wawili hao walikuwa bado wana uhusiano wa karibu.

Habari hizo za ndani kutoka familia ya Bibi harusi, zilidai kuwa kilichofanya Bwana harusi amtelekeze Bibi harusi ni wasiwasi aliokuwa nao juu ya uhakika wa ujauzito wa mkewe huyo mtarajiwa, kuwa ni wake kweli au wa mpenzi wake huyo wa zamani.

“Hofu hiyo ilijengeka kutokana na taarifa alizoziamini Bwana harusi kuwa Bibi harusi anaendeleza uhusiano na mzazi mwenziwe. Ni hofu tu ambayo angeifanyia kazi na angegundua kuwa haina ukweli wowote,” kilidai chanzo hicho.

Chanzo hicho kiliendelea kudai:“Unajua muda mwingine binadamu tunahitaji kufanya uamuzi kwa kutafakari … maana shemeji yetu (Bwana harusi) alipigiwa simu na mzazi mwenza wa Bibi harusi na kuelezwa maneno ya ‘shombo’ na yeye bila kufanyia utafiti, akaamua kususa harusi.”

Wakati taarifa hizo zikibainisha hayo, familia ya Bwana harusi imeendelea kufanya jitihada za kuhakikisha suala hilo linamalizika kistaarabu.

Anayeelezwa kufuatilia suala hilo kwa karibuni ni kaka yake, ambaye hadi jana jitihada za kumtafuta mdogo wake zilikuwa zimeshindikana kutokana na kutopokea simu yake ya mkononi mara zote.

“Anayeongoza familia ya Bwana harusi ni kaka yake. Inasemekana pia kuwa wawili hao waliingia kwenye mgogoro dakika za mwisho kabla ya harusi na ndiyo maana baada ya kutoweka hataki hata kupokea simu,” kilieleza chanzo kingine.

Awali, mpambe wa Bibi harusi alieleza kuwa siku mbili kabla ya harusi hiyo, Bwana harusi alikuwa kwenye migogoro ya kifamilia na ndugu zake kuhusu fedha za sherehe na mpaka siku ya sherehe, suala hilo walikuwa hawajalitatua.

“Lakini tunashukuru kaka yake ni mstaarabu, aliamua kuonesha upendo kwa mdogo wake na amekuwa akilifuatilia suala hilo ili limalizike kwa amani, lakini mdogo mtu hapatikani,” alisema mpambe huyo.

Alisema jitihada za Bibi harusi kumtafuta Bwana harusi hazijazaa matunda, kwani hadi juzi alikuwa hapatikani hata nyumbani kwake, ingawa redio ilikuwa inasikika ndani ya chumba hicho kilichofungwa kufuli kwa nje.

Simu ya Bwana harusi ilikuwa ikiita muda mwingi bila kupokewa, lakini hatua zingine zilidai kuwa Bwana huyo ambaye ni mfanyabiashara kwenye kituo cha mabasi yaendayo Chunya eneo la Isanga jijini Mbeya hajafungua duka lake.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images