Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Jeshi la Polisi Latoa Tahadhari Msimu Huu wa Sikukuu

$
0
0

Jeshi la Polisi kupitia msemaji wake, Kamishna Msaidizi wa Polisi na Msemaji wa Jeshi hilo, Advera John Bulimba, lilitoa tahadhari za kiusalama kuhusiana na sikukuu hizo mbele ya waandishi wa habari jana huku pia wazoefu wa masuala ya biashara na wakuu wa dini wakitoa usia wao kuhusiana na mambo muhimu ya kuzingatia ili sikukuu isiharibiwe kwa habari mbaya za misiba na majanga.

Katika taarifa yao kwa umma, polisi walichimba mkwara mzito kwa kuahidi kuchukua hatua za kisheria kwa wote watakaofurahia sikukuu hizo kwa namna inayokiuka sheria na kuhatarisha usalama, huku Askofu Mkuu wa Jimbo la Mahenge, Agapiti Ndorobo, akionya kuwa kila mmoja anapaswa kuhakikisha kuwa hatendi mambo ya ovyo na kumchukiza Mungu.

Mhadhiri wa Uchumi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dk. Joel Silas, aliwashauri Watanzania kutumia vyema rasilimali zao katika kipindi hiki ili sikukuu zikimalizika wasibaki bila kitu mikononi mwao.

Keshokutwa, Watanzania wataungana na watu wengine duniani kote kusherehekea Krismasi kabla ya kufuatiwa na siku ya kupeana zawadi (Boxing Day) katika siku inayofuata na mwaka mpya ifikapo mwisho wa mwezi huu.

TAHADHARI YA POLISI

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Kamishna Bulimba alisema baadhi ya wahalifu hutumia vipindi vya sikukuu kufanya vitendo vya kihalifu, lakini akaonya kuwa yeyote atakayejaribu kufanya hivyo atachukuliwa hatua kali kwa sababu wamejipanga kuhakikisha kuwa amani na utulivu vinaendelea kudumishwa wakati wote.

“Tumejipanga vya kutosha, siwezi kuweka mbinu hadharani hapa kwa sababu za kiusalama, lakini itoshe tu kuwaambia kwamba Jeshi la Polisi liko vizuri na asithubutu mtu yeyote kufanya uhalifu mahali popote maana tuna mkono mrefu… tutamkamata,” alisema Bulimba.

Aliwataka wananchi kutoa ushirikiano kwa kufikisha taarifa haraka wanapobaini kuwa kuna mtu, kundi au watu wanaowatilia shaka, huku kila mmoja akiwa mlinzi wa jirani yake katika biashara, makazi na mahali pengine. “Ukiona kuna mtu anaingia kwa jirani yako halafu humfahamu au unamtilia shaka, mpigie simu au piga simu polisi kupitia namba 111 na 112,” alisema.

Aliongeza kuwa jeshi hilo limejipanga pia kwa kuimarisha ulinzi katika maeneo ya kuabudia, sehemu za fukwe za bahari, sehemu za starehe na maeneo mengine ambayo yatakuwa na mikusanyiko mikubwa ya watu. Bulimba aliwataka waendeshaji wa kumbi za starehe kuzingatia uhalali wa matumizi ya kumbi zao na kuepuka kuzidisha idadi ya watu tofauti na uwezo wa kumbi zao na kwamba kwa yeyote atakayebainika kufanya hivyo atachukuliwa hatua kali.

Kuhusu ulinzi katika barabara, Bulimba alisema jeshi hilo pia limejipanga kudhibiti matukio ya kizembe ikiwamo madereva walevi na kwamba wameandaa vituo vya polisi vya kuhamishika ambavyo vitawekwa katika maeneo tofauti ili kuwarahisishia wananchi kuripoti moja kwa moja matukio yanayotishia usalama wa raia na mali.

Aidha, Bulimba alikumbushia vilevile kuwa ni marufuku kusherehekea sikukuu hizi kwa kupiga fataki, kuchoma matairi barabarani na kuandaa ‘disco toto’ kwa sababu matendo yote hayo ni uhalifu na wahusika watachukuliwa hatua za kisheria.

Yafuatayo ni kati ya mambo mengi ya kuzingatia, yapo takribani tisa ya msingi kuyakumbuka katika kipindi hiki cha sikukuu za mwisho wa mwaka.

1. TUMIA FEDHA KWA MPANGO

Kati ya mambo muhimu ya kuzingatia kuelekea sikukuu ya Krismasi na pia zile za ‘Boxing Day” na Mwaka Mpya ni kutumia fedha kwa umakini.

Tahadhari hii inatolewa kutokana na ukweli kuwa baada ya kumalizika kwa sikukuu hizo, hali huwa ngumu. Isitoshe, Januari ni mwezi unaombatana na changamoto nyingi. “Kuna masuala ya kodi za pango, ada za watoto shuleni na majukumu mengine mbalimbali.

Yeyote yule asipokuwa makini, dunia yote ataiona chungu na Januari ataiona ndefu. Ni muhimu kukumbuka kuwa kuna maisha baada ya sikukuu hizi,” mmoja wa wafuatiliaji wa masuala ya kiuchumi aliiambia Nipashe jana.

Akizungumzia hilo, Dk. Silas alisema ni lazima Watanzania wabadilishe muundo wa maisha kwa kuelekeza matumizi ya fedha katika mambo ya msingi kwa kuepuka kuishi kwa mazoea.

2. ZINGATIA SHERIA BARABARANI

Hili ni eneo jingine la kuchunga sana, hasa kwa madereva na watu wengine watakaosafiri kutoka eneo moja hadi jingine kwa nia ya kufurahia sikukuu. 

Kwa mujibu wa Polisi, ajali nyingi zinazotokea katika kipindi cha kuelekea mwisho wa mwaka husababishwa na watu wanaopuuza sheria za usalama barabarani, hasa kwa kuendesha vyombo vya moto kwa kasi kubwa na pia kujazana kwenye vyombo hivyo kupita kiasi. 

Wapo pia wanaotembea kwa miguu barabarani bila ya uangalifu. Ili kutimiza ndoto ya kuuona mwaka mpya, kila mmoja anapaswa kuzingatia sheria awapo barabarani.

3. ULEVI KUPITILIZA NI KUITA KIFO

Ulevi wa pombe kupitiliza kwa baadhi ya madereva ni chanzo kimojawapo kikubwa cha ajali za mwisho wa mwaka. Baadhi ya ajali hizi zilisababishwa na ulevi na hivyo, ni muhimu kujua kuwa unywaji holela ni sawa na kujiweka karibu na kifo au ulemavu wa kudumu.

4. ACHA MICHEPUKO, IPE RAHA FAMILIA

Viongozi wa dini, akiwamo Askofu Ndorobo, wanasisitiza juu ya upendo kwa familia, na hasa katika kipindi kama hiki cha kuelekea sikukuu. Kwa sababu hiyo, inashauriwa kuwa ni vizuri kwa kila mmoja kuachana na wapenzi wa nje ya ndoa na badala yake kufurahi na familia. Madhara ya kutenda kinyume chake ni pamoja na kuyumbisha ndoa baada ya sikukuu hizi kumalizika.

Askofu Ndorobo alisema ni vyema Watanzania wakajenga utaratibu wa kufurahi kwa pamoja kwenye matukio ya kifamilia kama kumbukumbu za siku za kuzaliwa, maisha ya ndoa miaka mitano na zaidi na sherehe nyinginezo, na kwamba kwa kufanya hivyo yatapunguza maovu mengi kwenye jamii.

5. USILE BATA PEKE YAKO, WAKUMBUKE YATIMA

Inashauriwa kwa kila mmoja kuwakumbuka yatima, masikini, walemavu na watu wengine wenye mahitaji maalumu na siyo kufaidi sikukuu na watu wachache wa familia peke yake. Lengo kubwa katika hili ni pamoja na kusambaza upendo, kuleta furaha kwa kila mmoja walau katika sikukuu hizi.

6. UMAKINI UNUNUZI WA ZAWADI ZISIWE ‘FEKI’

Mama au baba wa familia anapokwenda dukani kununulia bidhaa za zawadi kwa ajili ya sikukuu anapaswa kuwa makini wakati wote kutokana na mrundikano wa bidhaa bandia katika baadhi ya maeneo. Kwenda kufanya manunuzi holela kunaweza kuwasababishia kero wapendwa wako badala ya kuwaletea furaha iliyokusudiwa. Umakini huu uwe maradufu.

7. USIACHE WATOTO PEKE YAO KUOGELEA, DISCO

Kati ya makosa makubwa hufanyika katika siku za sikukuu ni pamoja na kuwaachia watoto waende kusherehekea siku hiyo kwenye maeneo mbalimbali bila ya uangalizi makini. Kwa mfano, ni hatari kuwaachia waogelee peke yao na pia siyo busara pia kuwaacha warundikane kwenye kumbi za disco, maarufu kama ‘disco toto’ wakiwa peke yao.

Kutozingatia maelekezo hayo yaliyosisitizwa jana na Jeshi la Polisi ni sawa na kujiweka tayari kwa kulia na kusaga meno kutokana na taarifa mbaya kuhusiana na usalama wa watoto. “Kuna uzembe ambao huwa unafanywa na wazazi wa kuwaachia watoto kuzurula ovyo na wakati mwingine kuhatarisha maisha yao.

Sasa nataka ieleweke hivi, mzazi akibainika amezembea kumlinda mtoto wake na akaletwa kituoni, lazima atakuwa na kitu cha kujibu na tutamwajibisha,” alisema Bulimba na kuongeza: “Kwa suala la disco toto, tulishalipiga marufuku. Halipo kabisa.”

8. EPUKA UCHOMAJI MATAIRI, ULIPUAJI FATAKI

Kusherehekea sikukuu kwa kuchoma matairi barabarani au kulipua mafataki kiholela ni miongoni mwa makosa makubwa yanayoweza kuharibu furaha na kuwa kilio kwa wahusika baada ya kukamatwa na kwenda kuwekwa mahabusu. Bulimba alilikumbushia hilo jana na kuonya kuwa wakiukaji wa maelekezo hayo wajiandae kukamatwa na kuwekwa mbaroni.

9. KUMUOGOPA MUNGU

Jambo lingine muhimu ni kuendeleza amani kwa kufanya matendo yanayozingatia uwapo wa Mungu. Askofu Ndorobo alisema wapo watu waliozoea uhalifu kwa kutomhofia Mungu na hilo ni tatizo kubwa linalopaswa kufanyiwa kazi sasa na hata baada ya kipindi hiki.

“Kinachopungua kwa (baadhi ya) Watanzania ni hali ya kutomuogopa Mungu kwa dhambi. Kila Mtanzania ni mlinzi wa mwenzake na pia ni mtunza uhai wa mwenzake. Ndiyo maana kila mmoja akiheshimu uhai wa mtu… matukio mabaya hayatatokea,” alisema Askofu Ndorobo.

Mahakama Yafuta Kesi ya Mtuhumiwa wa Escrow

$
0
0

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam imemwachia huru Mhandisi Mkuu wa Mradi wa Umeme Vijijini (REA), Theophillo Bwekea, baada ya Jamhuri kuonyesha haina nia ya kuendelea na kesi hiyo.

Bwekea alikuwa akituhumiwa kupokea rushwa ya Sh milioni 161.7 kutoka kwa Mkurugenzi wa Kampuni ya VIP Engineering, James Rugemalira.

Wakili wa Serikali, Odossa Olombe, alidai mahakamani hapo mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Respiciou Mwijage kwamba upelelezi wa kesi hiyo haujakamilika.

Hivyo aliomba kuondoa kesi hiyo chini ya kifungu cha sheria namba 98(a) cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai (CPA) aya ya 20 iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2002.

Hakimu Mwijage aliyakubali maombi ya upande wa Jamhuri na kuamuru mshtakiwa kuachiwa huru chini ya kifungu cha sheria namba 98(a) cha CPA.

Mshtakiwa huyo alifikishwa mahakamani kwa mara ya kwanza na kusomewa mashtaka Januari 20, 2015.

Wakili wa Serikali kutoka Takukuru, Leonard Swai, awali akisoma mashtaka alidai kuwa mshtakiwa anatuhumiwa kupokea rushwa ya Sh 161,700,000 kutoka kwa Mkurugenzi wa Kampuni ya VIP Engineering, James Rugemalira, ambazo ni sehemu ya fedha zilizokuwamo kwenye Akaunti ya Tegeta Escrow.

Kabla ya kufanya kazi REA, Theophillo alikuwa Wizara ya Nishati na Madini, kitengo cha kusimamia umeme, ambako anadaiwa alishiriki kutunga sera ya kampuni binafsi kuuza umeme Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) na ilipoanza kutumika, Kampuni ya kufua umeme ya IPTL ilikuwa ya kwanza kupata zabuni.

Wakili Swai, alidai Februari 12, 2014 katika Benki ya Mkombozi, mshtakiwa akiwa Mhandisi Mkuu wa REA, kwa rushwa alijipatia Sh milioni 161.7 kupitia akaunti namba 00410102643901 fedha ambazo ni sehemu ya zilizokuwapo katika Akaunti ya Tegeta Escrow.

Alidai fedha hizo aliingiziwa katika akaunti yake na Rugemalira ambaye ni mshauri binafsi wa kimataifa, Mkurugenzi wa VIP Engineering na alikuwa Mkurugenzi wa IPTL.

Fedha hizo zinadaiwa alipewa zawadi kwa kuwa alikuwa mmoja wa wajumbe walioandaa sera zilizoruhusu sekta binafsi kuuza umeme Tanesco.

Mshtakiwa huyo alikuwa nje kwa dhamana baada ya kutimiza masharti ya kuwa na wadhamini wawili ambao ni watumishi wa Serikali ama kutoka taasisi inayotambulika waliotakiwa kuwa na barua za utambulisho na kila mmoja kusaini dhamana ya maandishi ya Sh milioni 25.

Serikali yapiga marufuku Kuagiza nyama ya kuku kutoka nje ya Nchi

$
0
0

Serikali imepiga marufuku kuagiza na kuingiza nyama za kuku waliochinjwa kutoka nje ya nchi ili kulinda afya za walaji wa bidhaa hiyo ya nyama nchini.

Katazo hilo limetolewa na Naibu Waziri wa Kilimo Mifugo na Uvuvi, Mhe. William Tate Ole Nasha kwenye mahojiano maalum na EATV ilipotaka kupata ufafanuzi wa serikali kuwa inahakikisha vipi nyama na vitoweo kutoka nje ya nchi zinaingizwa nchini zikiwa na ubora unaokidhi viwango vya afya kwa walaji.

Ole Nasha amesema hairuhusiwi kuagiza wala kuuza kuku waliochinjwa kutoka nje ya nchi kwakuwa kwa sasa nchi inajitosheleza na inajitegemea kwa kiwango kikubwa cha nyama.

Amewataka wafugaji na wafanyabiashara kutumia fursa za kuzalisha nyama kwa tija na ubora zaidi ili nchi ianze kuuza vitoweo vya nyama hasa kuku nje ya nchi.

Ameongeza kuwa tayari serikali inaendelea kuchukua hatua za kisheria kwa viongozi wanaoshirikiana na wafanyabiashara wasio waaminifu kuingiza nyama hizo za kuku wa nje nchini.

chama cha Kutetea Abiria Taifa (CHAKUA) Chapigwa Marufuku Mikoani

$
0
0
Kamanda wa Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani nchini DCP Mohamed Mpinga amesitisha utendaji wa chama cha Kutetea Abiria Taifa (CHAKUA) kuendelea na shuguli zake katika mikoa yote nchini isipokuwa kwa mkoa wa Dar es Salaam pekee

Akitaja sababu za kusitisha utendaji wa chama hicho jana  jijini Dar es Salaam wakati akitoa ripoti ya namna walivyojipanga kuzuia ajali za Barabarani DCP Mpinga alisema, utendaji mbaya na kukiuka maadili na kujikita katika usimamizi wa sheria badala ya kutoa elimu unaofanywa na chama hicho ndiyo sababu ya kusitishwa kwa utendaji wao na kwamba kuanzia sasa shughuli zao zitafanywa na Mabalozi wa Usalama Barabarani.

Muda mfupi baada ya kutolewa kwa tamko hilo, Mwenyekiti Taifa wa Chama cha Kutetea Abiria Taifa, Bwana Hassan Mchanjama  alikanusha tuhuma hizo huku akisema kuwa, kuzuia utendaji wa chama cha abiria kwa kile alichokiita ni maslahi binafsi ni kuwanyima wananchi mahala pa kuwasilisha kero zao ambapo amebainisha kuwa chama hicho hakijawahi kukiuka taratibu zake za utendaji kama ilivyoelezwa.

Mbali na suala hilo DCP Mohamed Mpinga amewataka wamiliki wa magari kote nchini kuondoa na kuacha mara moja kutumia taa zenye mwanga mkali maarufu kwa jina la 'Sportlights' katika vyombo vyao vya moto kwani taa hizo ziimekuwa kero kwa madereva wengine na kuchangia ajali za barabarani nchini.

Madereva Wazembe Kuwekwa Selo Badala ya Kulipa Faini

$
0
0

JESHI la Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani nchini limesema litachukua hatua kali kwa kuweka mahabusu madereva watakaokiuka sheria za usalama barabarani katika kipindi hiki cha sikukuu badala ya kulipa faini kama ilivyozoeleka.

Kauli hiyo ilitolewa jana Dar es Salaam na Kamanda wa Polisi wa Kikosi hicho, Mohammed Mpinga, alipozungumza na vyombo vya habari akisema kutoza faini kumekuwa hakuwafanyi madereva kuacha kuvunja sheria.

“Kitendo cha kutoza faini, kimekuwa kikiwafanya madereva kuvunja sheria kwa makusudi, wakijua wakikamatwa watalipa faini na kuachwa,” alisema Mpinga.

Mpinga alisema katika kipindi hiki, watu wengi hupenda kusafiri kwenda maeneo mbalimbali na hivyo kuongeza matumizi ya vyombo vya moto barabarani ambapo pia huambatana na starehe nyingi ikiwa ni pamoja na ulevi kwa madereva.

Alieleza kutokana na hali hiyo ya starehe na ulevi, madereva wengi hupoteza umakini na kushindwa kuzingatia sheria za usalama barabarani na hatimaye kusababisha ajali ambazo hugharimu maisha ya watu wengi.

Alifafanua, kwamba kipindi hiki madereva huwa na haraka na huendesha kwa mwendo kasi, hunywa pombe, hupenda kupita magari ambayo ya mbele yao bila hadhari na hufanya makosa ya kizembe yanayohatarisha maisha.

Kamanda Mpinga alisema kwa kutambua hilo, wamejipanga ili kuwatia mbaroni madereva hao na kuwachukulia hatua kwa mujibu wa sheria.

Aidha, alisema katika kipindi cha kuelekea mwishoni na mwanzoni mwa mwaka mpya, wamekuwa wakifanya operesheni katika barabara zote, stendi za mabasi ili kukagua ubora wa mabasi, mikanda, kupima ulevi madereva, uzidishaji abiria na nauli.

Alisema katika operesheni hii inayoendelea mikoani kwa kipindi kifupi madereva wa mabasi ya abiria wamekamatwa kwa mwendo kasi wa zaidi ya kilometa 90 kwa saa, ambapo katika mikoa tofauti jumla ya madereva 277 walifikishwa mahakamani wakitokea mahabusu na kulipa faini ya kati ya Sh. 300,000 na Sh 600,000

Mpigapicha maarufu Mpoki Bukuku afariki dunia

$
0
0
Mpiga picha maarufu Mpoki Bukuku amefariki dunia leo katika Taasisi ya Mifupa (MOI), alikokuwa amelazwa akipatiwa matibabu.

Taarifa zinasema Mpoki amefariki dunia mchana huu na alipokelewa jana usiku baada ya kupata ajali ya gari maeneo la Mwenge ITV.

Mpoki Bukuku amewahi kufanya kazi kama Mpiga Picha Mkuu katika gazeti la Mwananchi pia amewahi kufanya kazi magazeti kadhaa likiwemo Majira na Nipashe.

Rais Magufuli Afanya Uapisho Wa Mwenyekiti NEC , Kamishna Wa Maadili Na Majaji Wa Mahakama Ya Rufani

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, leo tarehe 23 Desemba, 2016 amewaapisha viongozi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma na Majaji wa Mahakama ya Rufani aliowateua jana tarehe 22 Desemba, 2016.

Hafla ya kuwaapisha viongozi hao imehudhuriwa na Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa, Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Mohamed Chande Othman, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Utumishi na Utawala Bora Mhe. Anjellah Kairuki, Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe. George Mcheche Masaju na Viongozi wengine mbalimbali.

Walioapishwa ni Mhe. Mhe. Jaji Semistocles Simon Kaijage aliyeapishwa kuwa Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Mhe. Jaji Mstaafu Hamid Mahmoud Hamid aliyeapishwa kuwa Makamu Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) na Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufaa, Mhe. Jaji Harold Reginald Nsekela aliyeapishwa kuwa Kamishna wa Maadili katika Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma. Viongozi hawa watashika nyadhifa hizo kwa kipindi cha miaka mitano.

Kwa upande wa Majaji walioapishwa kuwa Majaji wa Mahakama ya Rufani ni Mhe. Jaji Rehema Kiwanga Mkuye, Mhe. Jaji Sivangilwa Sikalalilwa Mwangesi na Mhe. Jaji Dkt. Gerald Alex Mbonimpa Ndika, Mhe. Jaji Jackobs Casthom Mwatebela Mwambegele.

Wakati huo huo, Mhe. Rais Magufuli amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Uturuki hapa nchini Mhe. Yesamin Eralp ambapo viongozi hao wamezungumzia uhusiano na ushirikiano kati ya Tanzania na Uturuki hususani katika masuala ya ushirikiano wa kiuchumi na maendeleo.

Katika hatua nyingine, Mhe. Rais Magufuli na Mkewe Mhe. Mama Janeth Magufuli wamemtembelea na kumpa pole Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo kufuatia kifo cha Dada yake aitwaye Efrazia Pengo aliyefariki dunia jana tarehe 22 Desemba, 2016 katika Kijiji cha Mwazye, Wilaya ya Sumbawanga Mkoani Rukwa akiwa na umri wa miaka 79.

Mhe. Rais Magufuli na Mhe. Mama Janeth Magufuli wamemtembelea Kardinali Pengo katika makazi yake yaliyopo Kurasini Jijini Dar es Salaam.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam
23 Desemba, 2016
.

 Mhe. Jaji Semistocles Kaijage akisaini hati ya kiapo mbele ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli wakati wa kiapo cha kuwa Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Ikulu Jijini Dar es Salaam.


 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha Mhe. Jaji Mstaafu Hamid Mohamed Hamid kuwa Makamu kuwa Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Ikulu Jijini Dar es Salaam.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimuapishaJaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufani Mhe. Jaji Harold Nsekela kuwa Kamishna wa Maadili katika Sekretariat ya Maadili ya Viongozi wa Umma, Ikulu Jijini Dar es Salaam.


  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha Mhe. Jaji Rehema Kiwanga Mkuye kuwa Jaji wa Mahakama ya Rufani.


 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha Mhe. Jaji Sivangilwe Sikalaliwa Mwangesi kuwa Jaji wa Mahakama ya Rufani.


 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimkabidhi vitendea kazi Mhe. Jaji Dkt. Gerald Ndika kuwa Jaji wa Mahakama ya Rufani.


 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha Mhe. Jaji Jackobs Mwambegele kuwa Jaji wa Mahakama ya Rufani.

Rais Magufuli Akutana Na Waziri Mkuu Majaliwa Ikulu Jijini Dar

$
0
0
Rais John Magufuli  akisalimiana na  Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa Ikulu jijini Dar es salaam Desemba 23, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)


 Rais John Magufuli akiteta na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, Ikulu jijini Dar es salaam, Desemba 23, 2016.
  Rais John Magufuli akiteta na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, Ikulu jijini Dar es salaam, Desemba 23, 2016.
Rais John Magufuli akizungumza na mtoto  Doreen Ndika ambaye aliambatana na baba yake, Jaji Dkt. Gerald Ndika  aliyeapishwa na Rais `Ikulu jijini Dar es salaam Desemba 23, 2016 kuwa Jaji wa Mahakama ya Rufani Tanzania. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Picha: Mwenyekiti Mpya Wa NEC Jaji Semistocles Kaijage Aanza Kazi Rasmi.

$
0
0
Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Bw. Kailima Ramadhan (kushoto) akimkaribisha Mwenyekiti mpya wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Jaji wa Mahakama ya Rufaa, Mhe. Jaji Semistocles Kaijage (kulia) kwenye Ofisi za Tume zilizoko Posta jijini Dar es salaam. Mhe. Jaji Semistocles Kaijage ameapishwa leo Ikulu jijini  Dar es salaam kuiongoza Tume hiyo kwa kipindi cha miaka 5.
Baadhi ya Watumishi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) wakimpokea Mwenyekiti mpya wa Tume hiyo mara baada ya kuwasili katika Ofisi za Tume ya Taifa ya Uchaguzi Posta, jijini Dar es salaam.
Baadhi ya Watumishi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) wakimpokea Mwenyekiti mpya wa Tume hiyo mara baada ya kuwasili katika Ofisi za Tume ya Taifa ya Uchaguzi Posta, jijini Dar es salaam.
 Mwenyekiti mpya wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Jaji wa Mahakama ya Rufaa, Mhe. Jaji Semistocles Kaijage (kulia) akiwa Ofisini kwake kwa mara ya kwanza mara baada ya kuapishwa leo. Mhe. Jaji Semistocles Kaijage ameteuliwa kuongoza Tume hiyo kwa kipindi cha miaka mitano kuanzia tarehe 20 Desemba, 2016.
Mwenyekiti mpya wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Jaji wa Mahakama ya Rufaa, Mhe. Jaji Semistocles Kaijage (kushoto) akizungumza na Wajumbe wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi ofisini kwake leo.
Mwenyekiti mpya wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Jaji wa Mahakama ya Rufaa, Mhe. Jaji Semistocles Kaijage (kushoto) akizungumza na Wajumbe wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi ofisini kwake leo.

SORRY MADAM -Sehemu ya 3 & 4 (Destination of my enemies)

$
0
0
MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA
ILIPOISHIA
“Yule mshenzi amepewa uwaziri wa ulinzi Tanzania?”
“Mungu wangu………ana sifa gani za yeye kuwa waziri?”
“Ndio hivyo. Yaani laiti ningejua huyu mchenzi ningemuua tangu tukiwa ndani ya ndege ninaamini kwamba tusinge kuwa tunazungumza mazungumuzo ya kumuuhusu huyu kibwengo mtu”
“Kwa nini usimuue?”
“Mazingira hayakuruhusu, alipelekea kunipa shida ya kutafutwa hapo bendeni kwa hayati Mzee Madiba”
“Ulitokaje tokaje ndani ya ndege?”
Swali la Madam Mery likamfanya Mzee Godwin kurudisha kumbukumbu zake nyuma kwa haraka hadi siku aliyo toka kupambana na Eddy ndani ya ndege na taratibu akaanza kusimulia.

ENDELEA
“Nilipo onekanana sura yangu, iliniazimu mimi kuondoka na kuachana na Edddy kwani endepo ningeendelea kupambana naye ningeingia mikononi mwa askari na ingekuwa ni swala jengine.”
“Nilijichanganya katikati ya askari ambao walikuwa wakikagua watu basi, nikafanikiwa kutoka pasipo wao kugundua kwamba mimi ndio niliye kuwa nimesababisha maafa hayo”

“Sasa uliingiaje ndani ya ndege?”
“Ahaa, nilimtumia njia ya kujificha kwenye mizigo, baada ya kumuona Eddy akiwa anahangaikia usafiri wa kuja nchini Tanzania”
“Aiseee una hatari kweli kweli wewe”
“Weee acha tu, sasa lengo na thumuni la kukuita hapa ninahitaji kuweza kumpoteza Eddy mara moja kwenye huu uso wa dunia. Ila tahadhari ni moja, dogo amekuwa waziri, tena waziri wa ulinzi”

“Kama nilishindwa kumuua kipindi akiwa mtu wa kawaida, basi ujue kazi ya kumuangamiza yeye ni kubwa sana”
Madam Mery akashusha pumzi nyingi huku akimtazama Mzee Godwin anaye onekana kuwa na mawazo mengi kichwani mwake. Mzee Gowin kabla hajaendelea kuzungumza ujumbe mfupi ukaingia kwenye simu yake, taratibu akaanza kuusoma, na tabasamu pana likajijenga usoni mwake ikiwa ni ishara ya furaha
                                                                                         ***
    Kukamatwa kwa mchungaji Mandingo na Madam Glory watu maarufu katika nchi ya Tanzania kukaana kuwashangaza wananchi wengi, vyombo vingi vya habari vilidai kwamba watu hao wamekamatwa na waziri mpya wa ulinzi. Waandishi wengi walifunga foleni kwenye jengo la waziri wa ulinzi wakihitaji kufanya mkotano na waziri huyo ambaye hadi sasa hivi hawamuelewi nini ni maana ya kuwakamata watumishi hao wenye kumsaidia kila mwenye shida mbele ya macho yao
“Muhesimiwa, muheshimiwaa”
Waandishi baadhi walimuuita Eddy alipo kuwa akishuka kwenye gari lake.

“Ni kwa nini umeamua kuwakamata watumishi wa bwana Mchungaji Mandingo na Madam Grory?”
Muandishi mmoja wa gazeti la Habari Sasa alimuuliza waziri Eddy Godwin
“Siwezi kuzungumza lolote kwa sasa, ila huo ni mwanzo tu waujibikaji wangu, ila kazi inaendelea”
Eddy alijibu na kuomba kupishwa kukiwahi kikao cha wakuu wa jeshi la polisi ambao tayari wamesha wasili kwenye ukumbi wa mikutano tangu saa mbili asubuhi. Eddy hakuwa na haja ya kwenda ofisisni kwake moja kwa moja akaelekea katika ukumbi wa mkutano, Akawakuta wakuu wote wa jeshi la polisi, kutoka mikoani mwote wakiwa wanamngojea.
“Wakubwa zangu shikamoni”

Waziri Eddy alisalimia kwani watu wote waliomo ndani ya ofisi yake wamempita umri mkubwa sana na wengine ni sawa na baba zake. Kila mmoja akaitikia salamu hiyo
“Samahani kwa kuchelewa kuweza kuwahi kwenye kikao, ila hakuna kilicho haribika.”
“Lengo la kuwaita hapa ninahitaji kujadiliana nanyi, kuhusiana na watendaji wenu katika mikoa yenu.”
“Napenda kujua ni nini kilicho pungua kwenye idara yenu kuanzia madai munayo idaia serikali ili yaweze kulipwa haraka iwezekanavyo”
Eddy alizungumza na kuwatazama wakuu wote walio fika kwenye kikao hichi. Mmoja akanyoosha kidole na kuzungumza.

“Mkuu hapo kinacho tusumbua kwanza ni ufinyu wa mishahara kwa vijana wetu, mishahara kupungua na mazingira mabaya ya nyumba wanazo ishi kambini. Magari ni machakavu, piklikipi za doria ni chache kwahiyo inapelekea vitendo vingi vya uhalifu kufanyika katika nchi yetu”
“Asante nitalishuhulikia, mwengine”
“Muheshimiwa sisi tunahitaji sihasa isiingizwe kwenye majeshi kama hawa wezako walio pita kwa maana walikuwa wakituletea siaaa kwenye kazi zetu na kujikuta vijana wetu wakishindwa kufanya kazi kwa amani, jambo linalo pelekea uhalifu kuzidi kuongezeka”

“Asante baba yangu, ngoja niwatoe hofu kwenye hili. Mimi si mwana siasa na wala sina chama ila ninanchi. Labda nitoe rai moja kwenu. Musidanganyike na mwanasiasa yoyote. Yoyote ambaye ataingia kwenye jeshi la polisi, kama muhalifu hakikisheni munamuua na si kumuacha hai”
Wazo la waziri Eddy Godwin likawafanya wakuu wengi wa jeshi kushangaa kwani hawakutegemea kupata wazo kama hilo kwenye kikao hicho.
“Muheshimiwa kumbuka kwamba sisi ni jeshi la polisi kazi yetu ni kulinda wananchi na mali zao. Sasa unapo sema tuwaue inakuwa ni kazi kidogo kwetu huoni kwamba tutakuwa na sifa mbaya?”

“Samahani baba yangu kwa majibu haya nitakayo kupa, ila kiukweli hadi sasa hivi nyinyi muna sifa mbaya mbaya mbaya zaidi ya shetani na ubaya wake. Wahalifu wengi tupo nao huku juu serikalini. Wanawatumikisha vijana wadogo wanakamatwa na kufungwa, ila muzizi ipo inaendelea kuzalisha matatizo mengine mengi kwenye ngi hii. Sasa hii ni amri wala sio ombi, na lolote litakalo fanyika basi mimi nitakuwa muwajibikaji katika kuyajibu hayo ICC”
Baadhi ya wakuu wa polisi wakapiga makofi kwa ujasiri anao uonyesha kijana mdogo mwenye mamlaka makubwa kwenye nchi hii.
“Tumekuelewa muheshimiwa”
“Asanteni kwa kunielelewa, ila wapeni tahathari vijana wenu. Nitakuwa nikizunguka zunguka kwenye kila mkoa na vituo vyote kisiri pasipo wao kujua, endapo nitaumdua kuna ubadhilifu wowote kwa wananchi basi, kijana huyo au hao watawajibika katika hilo. Asanteni kwa muda wenu” 

***
“Mbona unatabasamu?”
Madam Mery alimuuliza mzee Godwin
“Kijana wangu, niliye potezana naye muda yupo hai”
“Ni nani?”
“John”
“John yupi?”
“Yule aliye kua mwanafunzi wako”
Furaha ya mzee Godwin na Madam Mery ikazidi kuongezeka kwani mtu waliye kuwa wanamtegemea kwenye mipango yao wamepata ujumbe wake kwa njia ya simu.
“Sasa yupo wapi?”
“Yeye mwenyewe hakuniambia kwamba yupo wapi ila atanijulisha kwamba yupo wapi”
“Sawa”
“Ila itabidi kuunda kikosi chenye nguvu na safari hii, Eddy nilazima afee”
Mzee Godwin alizungumza huku akiachia tabasamu pana usoni mwake, macho yake akiwa amemtazama Madam Mery.

Wizara ya Elimu yatoa ufafanuzi kuhusu ajira za Walimu

$
0
0
Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi imesema haihusiki na utoaji wa ajira za walimu nchini, isipokuwa inachokifanya ni uhakiki wa taarifa za walimu wenye sifa za kuajiriwa serikalini.

Akizungumza nakituo cha  EATV leo, Naibu Waziri wa Elimu, Mhandisi Stella Manyanya amesema kuwa kwa sasa wizara hiyo inapitia taarifa (CV) za walimu waliohitimu ngazi ya Stashada na Stashahada, na baada ya hapo itazituma taarifa hizo katika Wizara ya Utumishi ambao ndiyo wanaohusika na kuajiri.

Akizungumzia sababu za kuwatenga wahitimu wa ngazi ya cheti, Manyanya amesema uhitaji mkubwa uliopo kwa sasa ni kwa walimu wa sekondari hususani wa masomo ya Phisics, Hisabati, Chemistry na Biolojia, hivyo inawahitaji kwa haraka zaidi walimu hao huku akisema wahitimu wengine ambao siyo wa masomo hayo na ambao siyo kwa ajili ya kufundisha sekondari, wasubiri utaratibu wa wizara inayohusika na utumishi.

"Siyo kwamba hatuhitaji walimu wa shule za msingi, lakini uhitaji mkubwa tulionao kwa sasa ni walimu wa sekondari, sisi hatuajiri, sisi tunafanya uhakiki, na sasa tunapitia CV za wahitimu waliotuma taarifa zao, tukishajiridhisha na wale ambao taarifa zao ni sahihi na wana sifa tunazohitaji, tunazipeleka Utumishi, hao ndiyo wataajiri, halafu majina yatapelekwa TAMISEMI kwa ajili ya kupangiwa maeneo ya kazi" Amesema Manyanya

Kuhusu idadi ya walimu wanaohitajika haraka, Manyanya amesema, wanahitajika walimu wengi kuliko idadi waliyoitoa mwanzo, na kuwataka wote waliotuma taarifa zao wawe na subira kwa kuwa mchako wa uhakiki bado unaendelea na majina yatatangazwa muda mfupi ujao ambao hautazidi kipindi cha miezi mitatu.

Rais Magufuli Na Mkewe Mama Janeth Magufuli Wamtembelea Askofu Mkuu Polycarp Kardinali Pengo

$
0
0
Rais wa Tanzania Dkt. John Magufuli na Mkewe Mhe. Mama Janeth Magufuli wamemtembelea na kumpa pole Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo.

Hatua hiyo ni kufuatia kifo cha Dada yake aitwaye Efrazia Pengo aliyefariki dunia jana tarehe 22 Desemba, 2016 katika Kijiji cha Mwazye, Wilaya ya Sumbawanga Mkoani Rukwa akiwa na umri wa miaka 79.

Mhe. Rais Magufuli na Mhe. Mama Janeth Magufuli wamemtembelea Kardinali Pengo katika makazi yake yaliyopo Kurasini Jijini Dar es Salaam.

Dereva bodaboda akatwa sikio kwa tuhuma ya kufumaniwa na mke wa dereva teksi

$
0
0
Dereva bodaboda wa Mji Mdogo wa Qatesh wilayani Hanang’ Mkoa wa Manyara, amekatwa sikio kwa kisu kwa tuhuma za kufumaniwa akiwa na mke wa dereva wa teksi.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Manyara, Kamishna Msaidizi, Francis Massawe alisema tukio hilo lilitokea Desemba 21 saa 6:10 usiku kwenye Kitongoji cha Qendangonyi, Kata ya Ganana wilayani Hanang’.

Kamanda Massawe alisema chanzo cha tukio hilo ni wivu wa mapenzi na majeruhi amepata kilema cha maisha baada ya sikio kutolewa.

Alisema wanamshikilia dereva teksi kwa uchunguzi wa tukio hilo kabla ya kumfikisha mahakamani.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumamosi Ya Disemba 24

Polisi Yanasa 200 Kwa Ujambazi Dar

$
0
0
JESHI la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam linawashikilia watuhumiwa 200 wanaohusishwa na makosa mbalimbali.

Wanne kati ya hao, wanatuhumiwa kukutwa na gari lililoibwa hivi karibuni katika eneo la ofisi za Mamlaka ya Udhibiti wa Bima Tanzania (TIRA) zilizopo Manispaa ya Ilala.

Mkuu wa Operesheni Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Lucas Mkondya, alitaja watu hao wanne wanaotuhumiwa kukutwa na gari hilo kuwa ni Leonard Said, Omary Said, Shomaly Kilobo na Adam Unemba.

Alisema katika uchunguzi wa awali, watuhumiwa wote wamekiri kuhusika katika wizi wa gari hilo, aina ya Toyota Spacio lenye namba za usajili T 398 CAE, boksi la chuma la kutunzia fedha na televisheni ya ukubwa wa inchi 32.

Alisema Desemba 5, mwaka huu alipokea taarifa kutoka kwa Mhasibu Mkuu wa TIRA, Egnance Edward (53) kuwa wamekuta ofisi za mamlaka hiyo, zimevunjwa na kuibwa baadhi ya vifaa ikiwemo gari hilo.

Jaji Magimbi kusikiliza rufaa ya Godbless Lema Desemba 28

$
0
0
JAJI Salma Magimbi wa Mahakama Kuu Kanda ya Arusha ndiye atakayesikiliza rufaa ya kutaka dhamana ya Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema, Desemba 28 mwaka huu katika Mahakama Kuu Kanda ya Arusha.

Akizungumza na waandishi wa habari jana, Wakili wa Lema, Sheck Mfinanga alisema rufaa hiyo namba 126 ya mwaka 2016, imepangiwa kusikilizwa na Jaji huyo. Alisema kimsingi wanalalamikia uamuzi wa Mahakama kutomwachia huru, licha ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha kumpatia dhamana.

Awali, uamuzi uliotolewa Novemba 11 mwaka huu katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha na Hakimu Desderi Kamugisha, ambapo Lema anakabiliwa na kesi namba 440 na 441 za uchochezi dhidi ya Rais John Magufuli, uliweka wazi dhamana.

Hakimu Kamugisha alikubali kutoa dhamana kwa madai kuwa sheria haizuii kumpa dhamana mtu kwa kesi ya uchochezi, ila kabla ya kutoa masharti ya dhamana licha ya kutamka dhamana ipo wazi, mawakili wa serikali walipinga kumpatia dhamana Lema, kwa madai wameonesha nia ya kukata rufaa.

Kutokana na mawakili hao kusema hivyo, Hakimu aliamua kesi hiyo ibaki kama ilivyo na mtuhumiwa asubiri maamuzi ya Mahakama Kuu.

Lema alilazimika kwenda mahabusu hadi sasa katika Gereza Kuu la Kisongo. Baada ya hatua hiyo, mawakili wa Lema wakiongozwa na Sheck Mfinanga, walianza kutafuta suluhisho la mteja wao kupata dhamana na walianza na kuandika maombi na kuitaka Mahakama Kuu kufanya marejeo kwa kuitisha faili la kesi hiyo kutoka Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha.

Lakini, ombi lilitupwa na Kaimu Jaji Mfawidhi, Sekela Moshi, Novemba 11 mwaka huu kwa madai kuwa walikosea, badala ya kufanya marejeo walitakiwa kukata rufaa. Mawakili hao walilazimika kukata rufaa siku hiyo hiyo na Desemba 2 mwaka huu, ilitupwa na Jaji Fatuma Masengi kwa madai kuwa ilikuwa nje ya muda.

Baada ya hatua hiyo, mawakili hao walipeleka ombi Mahakama Kuu, kuomba kuongezewa muda wa kupeleka notisi ya kukata rufaa yao juu ya dhamana na hatimaye Desemba 20, Jaji Dk Modesta Opiyo, alikubali na kumwongezea muda Lema wa siku 10.

Siku hiyo ya kuongezewa muda, mawakili wa Lema walifanikiwa kukata rufaa hiyo. Lema anashikiliwa kwa zaidi ya mwezi katika mahabusu ya Gereza Kuu Kisongo.

Alikamatwa Novemba 2 mwaka huu nje ya viwanja vya Bunge mjini Dodoma na alifikishwa mahakamani Novemba nane mwaka huu, akikabiliwa na mashitaka ya uchochezi dhidi ya Rais John Magufuli.

Makamu wa Rais ataka wazazi na walezi kuacha kuwaoza watoto wakiwa wadogo

$
0
0
MAKAMU wa Rais, Samia Suluhu Hassan amewataka wazazi na walezi wa visiwani Zanzibar, kuacha tabia ya kuwaoza wasichana wakiwa na umri mdogo, bali wawasomeshe kwa ajili ya manufaa yao ya jamii kwa ujumla.

Samia alisema hayo kwa nyakati tofauti, wakati akizindua madarasa ya kisasa iliyojengwa kwenye eneo la Kilimani na kukagua ujenzi wa vyumba vya madarasa na ujenzi wa msikiti mkubwa kuliko yote nchini Tanzania unaojengwa katika eneo la Ijitimai Kidoti mkoani Kaskazini Unguja.

Ujenzi huo unafanywa kwa michango ya wananchi. Alisema hayo katika siku yake ya kwanza ya ziara ya Kikazi Unguja.

Taarifa iliyotolewa na Ofisi ya Makamu wa Rais, Zanzibar, ilieleza kuwa makamu huyo wa Rais yupo katika ziara visiwani Zanzibar.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, Samia alisema kama wazazi na walezi watasomesha watoto wa kike, elimu watakayopata itasaidia kwa kiasi kikubwa wasichana hao, kufanya maamuzi sahihi na yenye tija katika jamii.

Alisisitiza kuwa elimu ni haki ya msingi kwa mtoto wa kike, hivyo ni muhimu kwa jamii ya Zanzibar ihakikishe watoto wa kike wote wanapata elimu, kwani watakuwa na uwezo wa kuchagua na kuandaa mustakbali wa maisha yao ya baadaye, ikilinganishwa na hali ilivyo sasa kwenye baadhi ya maeneo.

Kuhusu elimu ya dini, aliwahimiza wazazi na walezi, kuwalea watoto katika maadili mema kwa kuzingatia maandiko matakatifu ya Mtume Mohammad (S.A.W).

Penzi la Bibi wa Miaka 60 Laua Kijana wa Miaka 23

$
0
0
KIJANA mwenye umri wa 23 na mpenzi wake, bibi mwenye umri wa miaka 60 , wakazi wa kijiji cha Tentula, Kata ya Ikozi wilayani Sumbawanga, wanashikiliwa na polisi wakihutumiwa kumshambulia na kumuua kikatili jirani yao aitwae Desder Justino (23) kwa kile kinachoelezwa kuwa ni wivu wa mapenzi.

Inaelezwa kuwa, Justino pia alikuwa na mahusiano ya kimapenzi na bibi huyo.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Rukwa, George Kyando alithibitisha tukio hilo na kueleza kuwa mauaji hayo yalitokea Desemba 21 mwaka huu saa nne asubuhi katika nyumba ya mwanamke huyo iliyopo kijijini Tentula.

Taarifa kutoka kijijini humo zinadai kuwa, mwanamke huyo licha ya umri wake kuwa mkubwa, alikuwa na uhusiano wa kimapenzi na vijana hao wawili wa rika moja.

Kamanda Kyando hakuwa tayari kutaja majina ya wapenzi hao ambao ni watuhumiwa wa mauaji kwa sababu za uchunguzi.

Lakini alisema mwanaume ana umri wa miaka 23 huku mpenzi wake ana umri wa miaka 60. Akielezea zaidi, Kamanda Kyando alisema siku ya tukio Justino alikwenda nyumbani kwa mwanamke huyo ambaye anadaiwa kuwa na uhusiano naye wa kimapenzi na kumkuta kijana mwingine (mtuhumiwa), na hapo ndipo ugomvi ukaibuka baina ya vijana hao.Alisema Justino alijeruwa kichwani.

“Wawili hao yaani wapenzi hao (mwanamke na mwanaume) walimshambulia Justino (Desder) kwa kumpiga kichwani na kitu chenye ncha kali na kumjeruhi vibaya na alikufa akiwa anatibiwa hospitalini,” alisema Kamanda Kyando na kuongeza  kuwa, watuhumiwa hao wanashikiliwa na watafikishwa mahakamani uchunguzi wa awali utakapokamilika.

Kingunge Asema Bila tume huru Wapinzani Wasahau Kuingia Ikulu .......Lowassa Akubali Yaliyopita Si Ndwele

$
0
0
Mwanasiasa mkongwe nchini, Kingunge Ngombale Mwiru amesema bila ya kuwa na tume huru ya uchaguzi na Katiba Mpya, vyama vya upinzani visahau kushinda urais katika Uchaguzi Mkuu ujao.

Kauli ya Kingunge imekuja siku moja baada Rais John Magufuli kumteua Jaji Themistocles Kaijage kuwa mwenyekiti mpya wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) baada ya Jaji Damian Lubuva kufikia muda wake wa kustaafu.

Kwa muda mrefu, NEC imekuwa ikilalamikiwa na vyama vya upinzani kwa kutokuwa huru kwa sababu ya uongozi wake wote huteuliwa na Rais ambaye pia ni mwenyekiti wa CCM, huku sheria zikikataza matokeo ya nafasi ya urais kupingwa mahakamani.

Mbali na mwenyekiti kuteuliwa na Rais, wasimamizi wa uchaguzi wa majimbo ni wakurugenzi wa wilaya ambao pia huteuliwa na Rais kwa kuwa NEC haina wafanyakazi wake kote nchini.

Akizungumza katika mkutano wa kuwafariji vijana waliokamatwa na Jeshi la Polisi na kushtakiwa kwa makosa yaliyohusu Uchaguzi Mkuu uliopita, uliofanyika jijini Dar es Salaam jana, Kingunge aliwatia moyo vijana hao, akisema hakuna ushindi unaopatikana bila kupambana.

Kingunge, aliyetumia muda mrefu kueleza historia ya maisha yake katika siasa na jinsi alivyopambana katika harakati za kudai uhuru, alisema hali ya sasa ni mbaya kuliko wakati wa wakoloni wa Kiingereza ambao walikujwa wakali, kwa sababu CCM haifuati Katiba wala sheria.

“Yako mambo ambayo itabidi tujitahidi yaamuliwe sasa kabla ya 2020. Mambo hayo makubwa kwanza ni tume huru (ya uchaguzi). Suala hilo lazima lizungumzwe sasa, hatuwezi kwenda 2020 na tume ya sasa na Katiba ya mwaka 1977. Tukienda hivyo sahau habari ya upinzani kushinda uchaguzi,” alisema.

Kingunge ambaye aliwahi kushika nyadhifa mbalimbali serikalini ikiwamo ya waziri anayeshughulikia Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) na mkuu wa mkoa alisema, “(Pia) Sheria inayohusu matokeo ya uchaguzi wa Rais kuhojiwa. Hivi sasa sheria inasema matokeo ya uchaguzi wa Rais hayahojiwi mahakamani. Lazima hilo suala lipate jibu sasa. Kwa hiyo Katiba na sheria iseme, matokeo ya uchaguzi wa Rais yanaweza kuhojiwa mahakamani. Tusipokuwa na hilo, tutakuwa na matatizo makubwa sana.”

Alisema pamoja na kwamba Chadema inapendwa na wananchi wengi na Edward Lowasa aliyegombea urais kwa tiketi chama hicho, anapendwa, bado ni vigumu kushinda kwa sababu mfumo uliopo sasa.

“Tufanye yoyote, lakini tuhakikishe, ama tunapata Katiba Mpya au vipengele hivi vya sheria vinafanyiwa marekebisho. Kwa maoni yangu, kundi hili lililo madarakani bila shinikizo kubwa kutoka kwa wananchi, halitataka mabadiliko,” alisema.

Alisema enzi zao walifanikiwa kupata uhuru kwa sababu walijitolea kwa nguvu na wengine, na yeye akiwamo, waliacha kazi za mishahara mikubwa na kujiunga na Tanu kupigania uhuru.

“Tulifanikiwa kupata uhuru kwa sababu walijitoa mhanga. Wengi tu waliacha kazi, mtu anamaliza chuo kikuu anasema sitaki kazi anaingia Tanu kusaidia. Kwa hiyo tukawa na jeshi kubwa la vijana waliohakikisha nchi inapata uhuru,” alisema.

“Ninyi mnapambana katika mazingira magumu na wazee wenzenu walipambana katika mazingira hayo. Haikuwa rahisi. Wapo wengi walitusaliti, wengine hawakufanya lolote. Baba yangu tuligombana, nilipoacha kazi kwenda kuitumikia Tanu. Miezi sita hatukuzungumza.”

Akizungumza mkutano huo, Lowassa, ambaye ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema, aliwatia moyo vijana walioshtakiwa wakati wa Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015, akisema bado jeshi kubwa la vijana linahitajika.

“Yaliyopita si ndwele, tugange yaliyopo na yajayo. Si haki kusema unakwenda mahali pengine, mwenzako amepasafisha, safisha pa kwako. Nimefurahia moyo huo. Kama alivyosema Ngombale, tunataka jeshi kubwa zaidi, watu wengi zaidi,” alisema Lowassa. 

Mbowe Aeleza kwa nini Amekuwa Kimya Kupotea kwa Ben Saanane

$
0
0
Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe amesema amekuwa kimya muda mrefu kuhusiana na kupotea katika mazingira ya kutatanisha, msaidizi wake Ben Saanane kwa kuwa suala hilo lipo kwenye uchunguzi. 

Mbowe alisema hayo jana alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari jijini Mbeya wakati wa uchaguzi wa viongozi wa chama hicho Kanda ya Nyasa inayojumuisha mikoa ya Iringa, Mbeya, Songwe, Njombe na Rukwa. 

Alisema yeye pia ameathiriwa na tukio hilo kama ilivyo kwa wazazi wake na ndugu wengine kwa kuwa ni mtu muhimu kwake katika kutekeleza majukumu yake. 

“Ndugu zangu Watanzania msione nipo kimya, nimefanya hivi kutokana na kuwa suala hili lipo kwenye uchunguzi kwani tukizidisha kuongea ongea wale ambao wamemteka wanaweza kupoteza uhai wake kisa maneno,” alisema Mbowe. 

Alisema, “Chadema ni taasisi ambayo ina vyombo vya ulinzi na usalama ambavyo vinaendelea kuchunguza tukio hili la aina yake.” 

Katika hatua nyingine, Mbowe aliishitumu Serikali akidai kwamba imeendelea kuwafunga wanachama wake na kwamba mpaka sasa 180 wapo mahabusu. Alisema hizo ni jitihada za kuua nguvu za upinzani. 

Akijibu madai hayo, Kamishna wa Polisi (Operesheni na Mafunzo), Nsato Marijani alisema jeshi hilo linawashikilia watu wengi kwa makosa mbalimbali vituoni na wengine mahabusu katika magereza. Alisema polisi haimkamati mfuasi wa chama cha siasa bali mtu anayekwenda kinyume cha sheria. 

“Hayo yanayosemwa siyo ya kweli, waache kulipaka tope jeshi la polisi. Tutaendelea kuwakamata watu wote wanaovunja sheria. Hata kama akiwa mjomba wangu tutamkamata.” 

Msigwa kidedea 
Katika uchaguzi huo, Mbunge wa Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa aliibuka kidedea baada ya kushinda kwa kupata kura za ndiyo 62 sawa na asilimia 58.49 kati ya kura 106 zilizopigwa. 

Akitangaza matokeo hayo, msimamizi wa uchaguzi huo Naibu Katibu Mkuu wa Chadema (Bara), John Mnyika alisema nafasi ya makamu mwenyekiti imechukuliwa na Sadrick Malila ambaye alipata kura za ndiyo 93 sawa na asilimia 88 ya kura zilizopigwa 106 huku kura tatu zikiharibika. 

Mnyika alisema kuwa nafasi ya  mweka hazina imechukuliwa na Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Mbeya, Sophia Mwakagenda ambaye alishinda kwa kupata kura 91 ambayo ni sawa na asilimia 86 kura zote 106 zilizopigwa. 

Mnyika alisema katika uchaguzi huo wajumbe walipiga kura za ndiyo au hapana kwa lengo la kufanya uchaguzi wa maridhiano kwani uchaguzi wa kuweka wagombea wawili husababisha makundi na kuleta migogoro ndani ya chama. 

“Hivyo Kamati Kuu Taifa baada ya kuliona hilo tukaamua kuwaita wagombea wote na kuwaeleza nia yetu ya kufanya hivyo na hatujafanya huku tu, hata kanda nyingine tulizopita tumefanya hivyo" Alisema Mnyika
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images