Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Mali za Yusuf Manji Hatarini Kukamatwa, Kuuzwa

$
0
0

Siku moja baada ya mfanyabiashara Yusuf Manji kuhama kwenye jengo la Quality Plaza, uongozi wa kampuni ya udalali ya Yono umesema kinachosubiriwa ni mfanyabiashara huyo kulipa deni au kukamatwa kwa mali zake.

Akizungumza jana, Mwenyekiti wa Bodi ya kampuni hiyo, Stanley Kevela alisema Manji alipewa siku 14 zilizoanza kuhesabiwa tangu Jumamosi ili kulipa deni.

Alisema endapo siku hizo zitamalizika bila kulipwa, mali za mfanyabiashara huyo zitakamatwa ili kufidia deni la Dola 6.1 milioni za Marekani (zaidi ya Sh13 bilioni) anazodaiwa.

Kevela alisema fedha hizo ni gharama ya kupanga kwenye jengo hilo ambalo ni mali ya Mfuko wa Pensheni wa Watumishi wa Umma (PSPF).

Alisema baada ya kukamilika kwa mchakato huo, kampuni italikabidhi jengo hilo kwa PSPF kwa ajili ya shughuli nyingine.

Mfanyabiashara huyo alipotafutwa jana ili kuzungumzia suala hilo, simu yake ya mkononi haikupatikana.

Mkurugenzi wa kampuni ya Yono, Skolastika Kevela alisema kazi ya kuondoa mali za mpangaji kwenye jengo hilo ilikamilika juzi.

“Kampuni zote zimeshaondoa vifaa na milango ya jengo hilo imefungwa kwa kufuli za kampuni yetu. Tutalisimamia jengo hadi tutakapowakabidhi PSPF,” alisema.

Uamuzi wa Manji kuhamishwa kwenye jengo hilo ulitolewa na Mahakama kutokana na kushindwa kulipa kodi ya pango ambapo  alipewa masaa 24 ya kuondoa vitu  vyake.

Fundi Pancha Atupwa Jela Miaka 30 Kwa Kukutwa na Misokoto 601 ya Bangi

$
0
0

Fundi wa kuziba pancha, Harson Solomon (38), mkazi wa wilayani hapa amehukumiwa kifungo cha miaka 30 jela baada ya kutiwa hatiani kwa kupatikana na misokoto 601 ya bangi. 

Kifungo hicho kimeangukia sheria mpya ya udhibiti wa dawa za kulevya iliyosainiwa Mei 11, 2015 na aliyekuwa Rais wakati huo, Jakaya Kikwete. Imeelezwa Solomon ni miongoni mwa washtakiwa wa mwanzo kufungwa kwa sheria hiyo. 

Awali, sheria ilikuwa inatoa mwanya wa faini na mtu anaposhindwa kulipa ndipo hutumikia kifungo jela lakini hivi sasa anayepatikana na hatia ya kukutwa na kiwango kikubwa hutupwa jela. 

Kifungu cha 11(1) D cha sheria hiyo mpya, kinaeleza wazi mtu anayezalisha, kumiliki, kuuza, kununua au kusafirisha dawa za kulevya ikiwamo bangi, adhabu ya chini ni kifungo cha miaka 30 jela. 

Hukumu hiyo ilitolewa jana na Hakimu Mkazi Mfawidhi, Joachim Tiganga baada ya kuridhishwa bila kuacha shaka na ushahidi wa upande wa mashtaka. 

Wakili wa Serikali, Ignas Mwinuka alidai kortini kuwa Desemba 1, 2015 katika maeneo ya Mwika Kimangara, Moshi Vijijini mshitakiwa alipatikana na kiasi hicho cha bangi.

 Pia, anadaiwa kuruhusu eneo lake kutumika kuuza bangi na gongo. 

Akisoma hukumu, Hakimu Tiganga alisema matumizi ya dawa za kulevya yanazidi kuongezeka nchini na kuathiri jamii, hivyo Mahakama inatoa adhabu hiyo iwe fundisho kwa wengine. 

Katika kipindi chote tangu afikishwe kortini kwa mara ya kwanza Desemba 11 mwaka jana, mshtakiwa alikana mashtaka hadi alipotiwa hatiani na kuhukumiwa jana.

TANZIA: Aliyekuwa mbunge wa Rufiji na daktari bingwa wa moyo, Prof. Mtulia afariki dunia

$
0
0
Profesa Idris Mtulia aliyefariki dunia jana, ameacha pengo katika sekta ya afya huku wagonjwa zaidi ya 20 wakimsubiri awafanyie upasuaji. 

Daktari wa Hospitali ya Tumaini, Profesa Chalonde Yongolo (aliyewahi kufanya kazi na Profesa Mtulia) alisema licha ya kuwa mwalimu wake, alikuwa akishirikiana naye kufanya kazi hospitalini hapo.

 Profesa Mtulia (pichani) aliyefariki dunia ghafla nyumbani kwake Upanga jijini Dar es Salaam jana asubuhi imeelezwa alikuwa mchapakazi, mwenye maadili msaada mkubwa kwa jamii.

“Ni pigo kubwa, leo alikuwa na wagonjwa 20 ambao walitarajia kupata huduma ya upasuaji. Nimepokea taarifa za msiba huu saa sita mchana na kwa mujibu wa mke wa marehemu kifo chake ni cha ghafla kwa kuwa aliamka salama na alipata kifungua kinywa na akaenda kupumzika na kupitiwa na mauti.” 

Profesa Mtulia aliwahi kuwa mbunge wa Rufiji na Mwenyekiti wa Bodi ya Bohari Kuu ya Dawa (MSD). 

Mkurugenzi wa MSD, Laurean Bwanakunu alisema licha ya kuwa alikuwa amemaliza muda wake lakini Profesa Mtulia aliitumikia bodi hiyo kwa kipindi cha miaka mitatu. 

“Bado alikuwa mshauri katika mambo mbalimbali yahusuyo bodi.”
 
Bwanakunu alisema Profesa Mtulia alikuwa mchangamfu, mcheshi na huru kuzungumza na watu wote pasipo kujali rika. 

“Hakuwa mtu wa kawaida, alikuwa daktari hivyo alifanya majukumu yake kama mtu anayeelewa vizuri kitu anachokifanya na hata baada ya kumaliza muda wake mchango wake ulikuwa ni muhimu. 

"Alikuwa mtaalamu wa afya, msikivu na mpenda haki aliyehakikisha watu wanapata huduma kwa muda mwafaka."

PICHA: Ajali ya Lori na Hiace Yaua Watu 9 na Kujeruhi 18

$
0
0
Watu tisa wamefariki dunia na wengine 18 kujeruhiwa katika ajali ya gari iliyotokea eneo la Ifunda mkoani Iringa jana baada ya lori kugonga gari dogo la abiria aina ya Toyota Hiace. 

Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Amina Masenza alisema dereva wa lori hilo lililokuwa likitokea Mbeya kuelekea Dar es Salaam, alishindwa kufunga breki na kuigonga Hiace hiyo iliyokuwa imeegeshwa pembeni ya barabara. 

“Lori limeharibika kabisa na Hiace pia imeharibika kabisa,” alisema Kamanda Masenza. 

“Lori hilo liliposhindwa kufunga breki liliigonga Hiace ambalo lilikuwa na abiria na kwenda mbele na kisha kugonga watembea kwa miguu,,” 

Masenza alisema katika ajali hiyo iliyotokea jana jioni, madereva wa magari hayo wote wamejeruhiwa na wamelazwa Hospitali ya Mkoa wa Iringa pamoja na majeruhi wengine. 

“Dereva mmoja yupo chumba cha upasuaji kwa kuwa mguu wake umevunjika na mwingine yupo wodini,” alisema 

Mkuu wa Wilaya ya Mvomero Alia na 'Utapeli' Vyeti vya Ndoa

$
0
0

Mkuu wa Wilaya ya Mvomero, Mohamed Utali ametoa agizo kwa Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri hiyo, Florent Kyombo kutomhamisha mwalimu yeyote kwa kigezo cha cheti cha ndoa. 

Alisema baadhi wanaghushi vyeti hivyo na vya maradhi ili wapate nafasi ya kufundisha kwenye shule zilizopo kando mwa barabara kuu na mijini hivyo kusababisha shule zilizopo mbali kukosa walimu. Utali alisema hayo jana alipofungua baraza la madiwani. 

Alisema shule zilizofanya vibaya kwenye matokeo ya darasa la saba ni zilizopo mbali na barabara kuu na zenye upungufu wa walimu. 

Mkuu huyo wa wilaya ambaye kitaaluma ni mwalimu alisema anafahamu mbinu na ujanja wanaofanya baadhi ya walimu wanaotaka kufundisha shule za barabarani. 

“Mwalimu atakayekuja na kimemo cha kiongozi, ama cheti cha ndoa au ugonjwa na kuomba afundishe shule iliyopo kando mwa barabara kuu usikubali kumhamisha, tutumie madaktari tuwapime tujue hayo maradhi yao,” alisema Utali. 

Mwenyekiti wa halmashauri hiyo, Jonas Van Zeland alimtaka mkurugenzi kuwafuatilia walimu watoro na wanaoshindwa kukaa jirani na shule wanazofundisha kwa madai kuwa mazingira siyo rafiki. 

Mkurugenzi wa halmashauri hiyo, Kyomba alisema katika matokeo ya darasa la saba mwaka huu, Wilaya ya Mvomero imeshika nafasi ya sita kimkoa na shule zilizofanya vibaya ni zenye uhaba wa walimu. 

Alisema atahakikisha anafanya ukaguzi wa mara kwa mara kwenye shule hizo na kuwaomba wazazi, walezi na viongozi wengine wa kata na vijiji, pamoja na madiwani kumpa ushirikiano.

Lowassa Apongeza Mikutano ya Hadhara ya Kisiasa Kuzuiwa.....Asema Mikutano Yandani imekuwa Mitamu Zaidi na Imewaimarisha

$
0
0
Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Edward Lowassa, amesema anamshukuru  Rais Dk. John Magufuli kwa kuruhusu vikao vya ndani.

Amesema vikao hivo,  “ni vitamu zaidi kuliko vile ya nje.”

Hayo aliyasema   Dar es Salaam alipofungua mafunzo ya siku mbili kwa madiwani, wabunge na viongozi wa Chadema Mkoa wa Dar es Salaam yanayoendelea kutolewa na Shirika la Konrad Adenauer Stiftung (KAS) la   Ujerumani.

Akizungumzia   ziara za kanda zilizofanywa na viongozi wa chama hicho  hivi karibuni, Lowassa alisema vikao vya ndani vimewapa nafasi na muda mwingi wa kuzungumza na wanachama  kwa karibu zaidi.

“Tumefanya ziara, tumeona hali ya barabara ni nzuri lakini hali ni nzuri zaidi tulivyozungumza na wanachama wetu na tunamshukuru Rais.

“Aliona hakuna haja ya mikutano ya nje akatupatia vikao vya ndani, Loh! Ni vizuri, ni vitamu zaidi kuliko vile vya nje.

“Tunapata nafasi nzuri ya kuzungumza na wanachama ana kwa ana, kwa muda mrefu kwa mapenzi na mahaba.

“Nataka niwaambie Chadema ipo imara sana. Watu walidhani wamekata tamaa lakini wapo imara katika kuhakikisha chama kinapata ushindi  mwaka 2020,”alisema Lowassa.

Alisema yapo malalamiko madogo madogo likiwamo watu wengi kutaka uongozi wa chama.

Alipendekeza yawepo mabadiliko katika katiba ya nchi kuongeza nafasi za uongozi.

“Wana malalamiko madogo madogo lakini mengi ni ya uongozi, kila mtu anataka kuwa kiongozi hadi nikakumbuka kule Kenya walipobadilisha  Katiba wakaongeza nafasi za uongozi, magavana, mameya na nyingine ili zipatikane nafasi za siasa za kuongoza  na mimi nadhani tungepata muda tufafanue katiba ili ziongezwe nafasi za uteuzi.

“Au mnaonaje?” Lowassa aliwauliza wajumbe ambao kwa pamoja waliitikia: “Ndiyoo”

Alisema kuna kila dalili ya Chadema kushinda uchaguzi wa 2020.

Aliwataka  viongozi wa chama hicho kushikamana na kuepuka maneno ya kuwagawa akisisitiza kuwa  bila mshikamano hawataweza kushinda uchaguzi ujao.

“Dalili zote zinaonyesha tutashinda lakini kama tutakuwa wamoja.

“Bila umoja hatuwezi kushinda na CCM wanajua maana ya umoja ndiyo maana wanasema umoja ni ushindi, hivyo maneno ya kutugawa tusiyakubali, viongozi tushikamane,” alisema Lowassa.

Alitaja mbinu nyingine ya ushindi kuwa ni kwenda vijijini kutoa elimu kwa sababu utafiti unaonyesha kuwa CCM imekuwa ikishinda maeneo yaliyo nyuma katika elimu.

“Wakati tukiwa Dodoma kwenye ziara kuna vijiji mtu anakuambia mimi nampigia kura Nyerere (Hayati Baba wa Taifa Mwalimu  Nyerere), na akiona polisi anakimbia.

“Sasa kama mtu anakimbia akimwona polisi anawezaje kulinda kura?  Hivyo bila kwenda kutoa elimu vijijini hatuwezi kushinda,” alisisitiza Lowassa na kuongeza:

“ ‘There is no time left’ (Hatuna muda wa kupoteza),  muda uliobaki ni mdogo sana hatuna budi kuutumia vizuri kwa kuangalia wapi tulikosea na turekebishe vipi na tuongee kutoka moyoni tusiogopane.

“Tukosoane bila kusingiziana na tuone muda uliobaki tunafanya nini ili tushinde,” alisema Lowassa.

Magufuli Kuisuka Upya CCM.....Aitisha Vikao vya CC na NEC Disemba 13

$
0
0
Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (NEC), inatarajia kukutana Desemba 13, mwaka huu jijini Dar es Salaam, imefahamika.

Taarifa iliyotolewa Dar es Salaam jana na Kaimu Msemaji wa chama hicho, Seleman Mwenda, ilisema mkutano huo utatanguliwa na kikao cha Kamati Kuu (CC), kitakachofanyika Desemba 11 hadi 12, jijini Dar es Salaam.

Ingawa hadi sasa ajenda za vikao hivyo hazijajulikana, lakini wachambuzi wa masuala ya  siasa wanasema, kufanyika kwa vikao hivyo kunatajwa kuwa ni mkakati wa Mwenyekiti wa chama hicho, Rais Dk. John Magufuli  kutaka kuisuka upya CCM.

Baadhi ya wachambuzi hao wanasema uteuzi wa wajumbe watatu wa sekretarieti ya chama hicho kuwa mabalozi ni mwendelezo wa mkakati huo kuelekea uchaguzi mkuu wa ndani wa chama hicho mwakani.

Mbali na hao mjumbe mwingine wa sekretarieti, Dk Asha -Rose Migiro aliteuliwa kuwa Balozi wa Tanzania nchini Uingereza na nafasi yake ndani ya chama kuchukuliwa na Pindi Chana ambaye naye ameteuliwa kuwa balozi.

Katika Serikali ya awamu ya nne, Pindi Chana alikuwa Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto na baadae mwaka huu aliteuliwa kuwa Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa, Siasa na Uhusiano wa Kimataifa.

Mjumbe wa Kamati Kuu (CC), Dk. Emmanuel Nchimbi, kuteuliwa kuwa balozi kunathibitisha kuhusu uwapo wa mkakati wa Rais Magufuli kusuka upya chama hicho kwa kuweka sura mpya.

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye ambaye pia ni Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi wa chama hatarajiwi kuwapo katika safu hiyo mpya, kwani tayari yupo serikalini.

Mwingine ni Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho (Bara), Rajabu Luhwavi ambaye ameteuliwa kuwa balozi anazidi kutoa taswira kuhusu mkakati wa Rais Magufuli kusuka upya chama hicho.

Katika hotuba ya Rais Dk. Magufuli baada ya kukabidhiwa uenyekiti wa chama hicho alisema miongoni mwa mambo atakayoyatekeleza ni kuimarisha utendaji kazi wa chama, huku akimnukuu hayati Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere kwa kusema kuwa chama legelege huzaa serikali legelege.

“Nitashirikiana nanyi kujenga chama madhubuti chenye uwezo wa kuisimamia vizuri Serikali ili itekeleze ipasavyo majukumu yake, ikiwezekana tutapitia upya katiba na kanuni zetu ili kukidhi mazingira ya sasa na kuweza kuwatumikia wananchi ipasavyo.

“Tutahakikisha pia tunakuwa na safu bora ya uongozi katika ngazi zote kuanzia shina hadi taifa. Tutaangalia muundo (structure) wa chama chetu katika ngazi mbalimbali na kuondoa vyeo visivyokuwa na tija katika chama na hasa wakati huu wa mfumo wa vyama vingi” alisema Dk. Magufuli.

Dk. Magufuli alihoji kuhusu uhalali wa kuendelea kuwapo vijana wa chipukizi ndani ya chama hicho pamoja na baadhi ya safu za uongozi ndani ya chama hicho.

“WanaCCM ni lazima tujiulize je ni kweli katika zama hizi bado tunahitaji mtoto wa miaka 8 hadi 15 kuwa chipukizi kwa ajili ya kumtumia kwenye siasa badala ya kumwacha asome?  Kama akiwepo chipukizi wa CCM, chipukizi wa NCCR au Chadema ama TLP tutakuwa tunajenga nchi ya namna gani?

“Je bado kuna umuhimu wa kuwa na makamanda wa vijana ambao mara nyingi wenye kupewa vyeo hivyo ni wale wenye uwezo wa kifedha pekee?  Je walezi kwenye Umoja wa Wanawake (UWT) bado wanahitajika? Je washauri ndani ya Jumuiya ya Wazazi wanahitajika?" Alihoji Dk. Magufuli.

CUF Wakanusha Taarifa za Maalim Seif Kutaka Kukihama Chama Hicho

$
0
0

Chama cha Wananchi (CUF), kimesema taarifa zinazosambazwa katika vyombo vya habari na mitandao ya kijamii, kwamba Katibu Mkuu, Maalim Seif Sharif Hamad anataka kuhama chama hicho ni za kupuuzwa kwa kuwa hazina ukweli.

Naibu Katibu Mkuu wa CUF Zanzibar, Nassor Ahmed Mazrui alisema hayo jana  baada ya baadhi ya vyombo vya habari kuripoti kuwa Maalim anataka kuondoka ndani ya chama hicho cha upinzani.

Alisema tangu kuibuka kwa mgogoro ndani ya CUF na Mwenyekiti wao, Profesa Ibrahim Lipumba imekuwapo mikakati ya kuwakatisha tamaa jambo ambalo halitafanikiwa.

Mazrui alisema wanaopanga mikakati wamehangaika kila njia na wameonekana kukwama, hivyo kuibuka na mkakati wa kumzushia Katibu Mkuu kuhama chama.

“Hivi unafikiria Katibu Mkuu anaweza kuhama chama katika mazingira rahisi kiasi hicho? Hiki chama amekipigania vya kutosha wataondoka wao,” alisema.

Naibu Katibu Mkuu huyo aliwataka wana CUF kuendelea kutoa ushirikiano kwa Katibu Mkuu wao na kupuuza kauli za watu ambao wamepoteza mwelekeo kisiasa.

Alisema CUF si chama kinachotegemea mtu mmoja, na pia hakiko tayari kumpoteza Maalim kwa vibwagizo vya vibaraka wa chama tawala, ambao hawataki kupigania mabadiliko nchini.

Aidha, kuhusu chama kuwa kimya kuhusu madai yao ya ushindi katika uchaguzi wa Oktoba 25 mwaka jana, alisema bado wanaendelea na mchakato huo na watatoa taarifa hivi karibuni kuhusu hatua waliyofikia.

Mazrui alisema kila kitu kinakwenda vizuri na kutaka wana CUF kuwa na subira katika kipindi hiki, kwani mambo mazuri hayahitaji haraka.

Alisema ushirikiano wanaopata kutoka jumuiya ya kimataifa ni mzuri hali ambayo inawapa matumaini ya kuhakikisha kuwa haki inapatikana.

“Suala la madai ya ushindi wa uchaguzi linakwenda vizuri, na naamini hatima yake itapatikana kwa busara, ni vema wana CUF kuwa na subira,” alisema.

Jana katika baadhi ya magazeti ziliandikwa habari zikimhusisha Maalim na kuhama CUF na kutajwa kutarajia kuhamia vyama vya ADA-TADEA, AFP au ACT-Wazalendo, ambapo viongozi wa vyama hivyo walikanusha taarifa hizo.

Hali kadhalika Katibu Mkuu huyo alihusishwa na kutaka kujiunga na vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa).

Rais Dkt Magufuli aagiza Machinga wasiondolewa jijini Mwanza

$
0
0

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amemuagiza Waziri na Katibu Mkuu katika Ofisi ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) kusitisha mara moja utekelezaji wa zoezi la kuwaondoa wafanyabiashara wadogo maarufu kwa jina la Machinga katika Jiji la Mwanza mpaka hapo mamlaka husika itakapokamilisha maandalizi ya maeneo watakapohamishiwa na kwa kuwashirikisha wamachinga wenyewe.

Rais Magufuli akiwa na Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan ametoa agizo hilo leo tarehe 06 Desemba, 2016 Ikulu Jijini Dar es Salaam huku akionya kuwa kiongozi yeyote ambaye hayupo tayari kutekeleza agizo hilo aachie ngazi.

“Kumeibuka tabia ya Wakuu wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi kuwafukuza Wamachinga bila utaratibu wowote wa wapi wanawapeleka na wakati mwingine wanapelekwa maeneo ya mbali ambayo hayafai hata kwa kufanya biashara, hili jambo sio sawa hata kidogo.

“Sipendi Wamachinga wafanye biashara kwenye hifadhi ya barabara lakini hakuna sheria katika nchi hii inayosema mtu wa biashara ndogondogo au Mmachinga hatakiwi kukaa katikati ya mji, tukianza kwenda kwenye utaratibu wa namna hiyo maana yake tunaanza kutengeneza  madaraja ya Watanzania, kwamba kuna Watanzania fulani wa daraja fulani wanapaswa kukaa katikati ya mji na Watanzania wa daraja fulani hawatakiwi kukaa katikati ya mji, huo sio mwelekeo wetu na wala Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi ambayo mimi na wewe (Makamu wa Rais) tulipita kuinadi, haisemi tutengeneze madaraja ya watu wanaostahili kukaa mjini na wengine hawastahili kukaa mjini, sasa nimeona hili nilizungumze na nataka kulirudia kwa mara ya mwisho” amesema Rais Magufuli.

Dkt. Magufuli ameelekeza kuwa Wamachinga waliondolewa katika maeneo yao Jijini Mwanza waachwe waendelee na shughuli zao mpaka hapo Halmashauri ya Jiji la Mwanza itakapokamilisha maandalizi ya mahali watakapohamishiwa na kwa kuwashirikisha Wamachinga wenyewe.

“Narudia na hii ni mara ya mwisho, kawaambieni hata Wamachinga wa Mwanza warudi kwenye maeneo yao mpaka watakapowatengenezea utaratibu mzuri, Kigamboni hapa palikuwa na wamachinga eneo fulani wamehama vizuri kweli, wakatengenezewa miundo mbinu yao katika soko lao na sasa hivi wanafanya kazi vizuri, na waliwashirikisha viongozi wa Wamachinga, lakini Mwanza imekuwa ni amri tu na wengine wanatumia hata msemo wa Hapa Kazi Tu, mimi sikusema msemo wa Hapa Kazi Tu wa namna hiyo, nadhani mmenielewa” amesisitiza Rais Magufuli alipokuwa akiwaekeleza Naibu Waziri wa TAMISEMI Mhe. Suleiman Jafo na Katibu Mkuu TAMISEMI Mhandisi Mussa Iyombe.

Wakati huo huo, Rais Magufuli ameagiza Wizara ya Nishati na Madini kusitisha mara moja zoezi la kuwaondoa wachimbaji wadogo katika Kijiji cha Nyaligongo kilichopo katika Kata ya Mwakitolyo Mkoani Shinyanga na badala yake wachimbaji hao waachwe waendelee na shughuli zao, na leseni ya mwekezaji anayedai eneo hilo ni lake aondolewe.

“Wale waliofukuzwa Shinyanga wabaki palepale, kama ni leseni ya huyo mwekezaji ifutwe, Mhe. Makamu wa Rais fuatilia hili, mweleze Waziri wa Nishati na Madini, waache kufukuza wananchi hovyohovyo, wale wanapata riziki yao, wanasomesha watoto wao lakini wanafukuzwa tu.

“Na hizi ndio ajira zenyewe, tulisema tunatengeneza ajira, wewe mwekezaji ni mmoja unakwenda kuwafukuza watu 5,000? haiwezekani na wala haingii akilini” amesisitiza Rais Magufuli.

Rais Magufuli amekemea vitendo vya wawekezaji wakubwa kupewa maeneo ambayo wachimbaji wadogo wanaendesha shughuli zao tena kwa mtindo kwa kutengeneza nyaraka zinaonesha mwekezaji husika alipewa eneo hilo kabla ya wachimbaji wadogo na kusisitiza kuwa mchezo huo hautavumiliwa.

Hata hivyo Rais Magufuli amesema maagizo yake hayana maana kuwa Wamachinga na Wachimbaji wadogo waendeshe shughuli zao kwa kuvunja sheria bali wazingatie sheria na Mamlaka zisiwanyanyase watu wanyonge.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam

06 Desemba, 2016

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumatano ya Disemba 7

Maofisa 111 TASAF Watumbuliwa........Serikali Yabaini Mchecho Mchafu, Vigogo Wahusishwa

$
0
0
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Angellah Kairuki amemuagiza Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (Tasaf), kuwasimamisha kazi maofisa waandamizi watano wa mfuko.

Maofisa hao ni wanaosimamia mpango huo pamoja na Meneja wa Uratibu na Mkurugenzi wa Uratibu kutokana na kushindwa kusimamia mpango wa kunusuru kaya masikini.

Kairuki alisema maofisa hao ndio viongozi wasimamizi wakuu wa mpango huo katika Awamu ya Tatu ya Tasaf na wamesimamishwa kupisha uchunguzi wa jinsi walivyohusika kuvuruga utekelezaji wa mpango huo hadi kufikia kuandikisha kaya zisizo na sifa ufanyike.

Akizungumza na waandishi wa habari jana, Dar es Salaam, Kairuki alisema ameshauriana na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) na tayari ameshaelekeza waratibu wa Tasaf wa wilaya pia wasimamishwe kazi.

“Nimemwelekeza Mkurugenzi Mtendaji wa Tasaf awasimamishe kazi mara moja na kuendelea na hatua nyingine za kinidhamu dhidi ya maofisa washauri 106 walioko kwenye halmashauri walioshindwa kufuatilia na kusimamia mpango huu mpaka kusababisha kaya zisizostahili kuingizwa kwenye mpango na kuendelea kulipwa isivyostahili,” alisema Kairuki.

Aidha alisema ameagiza ufanyike uchunguzi wa kina kubaini ushiriki wa maofisa hao na kuchukua hatua stahiki kwa wale watakaothibitika kuhusika.

Aidha ametaka uchunguzi huo ukamilike ndani ya mwezi. Karuki alisema baada ya uhakiki kufanyika kaya 55,692 zimeondolewa kwenye mpango kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo vifo, kaya kuhama kijiji, kutojitokeza mara tatu mfululizo kupokea ruzuku, kuwa wajumbe wa kamati mbalimbali, wastaafu, viongozi na watumishi wa umma.

Alisema kuanzia Januari 2014 hadi Septemba 2016, Sh 6,427,110,309 zimeokolewa kwa kaya 42,035 zilizoondolewa kwa kipindi hicho na kwa kuwa kazi hiyo ni endelevu kuanzia Oktoba 2016 wakikamilisha kuziondoa kaya zisizostahili kiasi hicho cha fedha kinaweza kubadilika.

Hata hivyo amewaagiza Tasaf kuhakikisha wanaendelea kushirikiana na halmashauri kuongeza udhibiti wa fedha wakati wa malipo na kuhakikisha fedha zinalipwa kwa kaya zenye sifa peke yake.

Aidha, amewaagiza Tasaf kuendelea kushirikiana na halmashauri zote kukamilisha kazi ya uhakiki wa nyumba kwa nyumba katika halmashauri zote nchini kabla ya malipo yanayofuata ya Januari/ Februari 2017 kufanyika.

Mzee wa Miaka 75 Aweka Bango la Mke Anayemtaka

$
0
0
Katika  hali isiyo ya kawaida mzee mwenye umri wa miaka 75, Athuman Mchambua, mkazi wa Mtoni kwa Azizi Ally jijini Dar es Salaam amezua gumzo mtaani  baada ya kuamua kutafuta mke kwa kuweka bango barabarani.

Katika bango aliloliweka katikati ya barabara Mzee Mchambua alianisha sifa tano za mke anayemtaka pamoja na namba za simu za kuwasiliana naye.

Sifa hizo ni pamoja na awe mshika dini, uvumilivu wa ndoa, uwezo wa kilimo, apendo wa mume, watoto na wajukuu pamoja na usafi wa hali ya juu.

Mzee Mchambua ambaye alizungumza na Shirika la Utangazaji la Uingereza (BBC Swahili) hivi karibuni alisema alifanya uamuzi huo baada ya kufiwa na mke wake aliyezaa naye watoto 11 na kumwacha akiwa hana mtu wa kumsaidia kutunza familia na kufanya shughuli za shambani.

Katika mazungumzo na mwandishi wa BBC, alisema tayari wamejitokeza wanawake wanne waliotaka kuolewa naye lakini hakuna hata mmoja aliyekidhi vigezo alivyoainisha.

Alisema alilazimika kutumia njia ya tangazo kwa sababu anafiri kwa umri alionao hawezi kumpata mke kwa njia ya kawaida.

Alisema endapo njia hiyo itashindikana kumpata mke mwenye sifa anazotaka atalazimika kutumia madalali kumsaidia kumtafuta mke mwenye sifa.

BBC pia ilizungumza na mmoja wa watoto wa Mzee Mchambua, ambaye alisema anaona uamuzi wa baba yake ni sawa kwa sababu ameweka sifa za mwanamke anayemtaka.

Mtoto huyo alisema wapo tayari kumpokea mke mpya wa baba yao na watamheshimu kama mama yao mzazi.

Video: Dereva Atiwa Mbaroni Kwa Kucheza Muziki Huku Akiendesha Gari

$
0
0
POLISI mkoani Singida inamshikilia dereva wa gari dogo la abiria la Super Mamuu, kwa tuhuma za kuendesha kwa mwendo wa hatari.

Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida, Mayala Towo, alimtaja dereva anayeshikiliwa kuwa ni Saidi Juma (26) mkazi wa Dodoma ambaye inadaiwa siku ya tukio alikuwa anaendesha basi aina ya Nissan Civilian lenye namba za usajili T.360 DAY huku akicheza muziki.

Inaelezwa kuwa tukio hilo lilitokea Desemba 4, mwaka huu, saa 11: 00 jioni katika Mji Mdogo wa Itigi wilayani Manyoni wakati mtuhumiwa akiwa na wenzake watatu, alipoendesha gari hilo kwa mwendo wa hatari kwa kucheza muziki huku akiachiana usukani na wenzake hao wakati gari hilo likiwa kwenye mwendo.
Kamanda Towo aliwataja watuhumiwa wengine ambapo pia wanashikiliwa na Polisi kuwa ni Joseph Ramadhan (27), Ezekiel Joseph (24) na Sebastian Godfrey (23) wote wakazi wa Majengo, Itigi.

Hapa chini ni video ya dereva huyo akicheza wakati anaendesha gari.

Waziri Mkuu Majaliwa aibana NCAA, ataka nyaraka za Faru John ifikapo Desemba 8, 2016

$
0
0
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa ameugiza uongozi wa Mamlaka ya Hifadhi ya  Ngorongoro (NCAA), kumpelekea nyaraka zote zilizotumika katika kumhamisha faru maarufu kwa jina la John katika hifadhi hiyo ifikapo Desemba 8, 2016.

Majaliwa amesema ana taarifa kuwa walimhamisha Faru John Kreta kwa siri na kumpeleka  V I P Grumet  Serengeti Disemba 17, 2015 na waliahidiwa kupewa sh. milioni 200 ambapo  na wamepewa sh.  milioni 100 kwa ahadi ya kumaliziwa sh. milioni 100 nyingine baadaye.

Amesema hayo Desemba 6, 2016 alipotembelea Ofisi za makao makuu ya NCAA, zilizoko wilayani Ngorongoro mkoa Arusha  wakati akizungumza na watumishi wa mamlaka hiyo pamoja na Wajumbe wa  Baraza la Wafugaji ikiwa ni  sehemu ya ziara yake ya kikazi mkoani hapa.

“Naomba niletewe nyaraka zote zilizotumika kumuomba na kumuondoa faru huyo na barua zilizotumika kujadili suala la faru John. Nasikia amekufa naomba pembe ziletwe ofisini na iwapo itathibitika aliondoka bila ya kufuata taratibu wahusika wote watachukuliwa hatua kali za kisheria,”.

Aidha, Majaliwa amepiga marufuku tabia ya baadhi ya watumishi wa mamlaka hiyo ambao wanawakabidhi watoto kupeleka ng’ombe wao ndani ya kreta. “ Watumishi wa Ngorongoro ndiyo wanaopeleka ng’ombe ndani ya kreta na si wenyeji. Sasa marufuku na tutakayemkuta hatutakuwa na msamaha naye,”.

Amewataka watumishi hao kuhakikisha wanakuwa waadilifu na wanafanyakazi kwa kufuata misingi ya kiutumishi na kuacha tabia za kuendekeza rushwa na wizi.

Wakati huo huo Waziri Mkuu amemsimamisha kazi Mhasibu Mkuu wa NCAA, Sezzary Simfukwe kutokana na tuhuma za ubadhilifu wa fedha zinazomkabili na tayari  anahojiwa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU).

“Haiwezekani mtumishi  awe anachunguzwa  na TAKUKURU halafu aendelee kuwa ofisini si atavuruga uchunguzi. Asimamishwe kazi kuanzia leo mpaka hapo uchunguzi utakapokamilika na aikibainika kwamba hana hatia atarudi kazini,” alisema.

Isikilize Video ya Rais Magufuli Akiwapiga Marufuku Wakuu wa Mikoa Kuwasumbua Machinga

$
0
0

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amemuagiza Waziri na Katibu Mkuu katika Ofisi ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) kusitisha mara moja utekelezaji wa zoezi la kuwaondoa wafanyabiashara wadogo maarufu kwa jina la Machinga katika Jiji la Mwanza pamoja na mikoa mingine mpaka hapo mamlaka husika zitakapokamilisha maandalizi ya maeneo watakapohamishiwa na kwa kuwashirikisha wamachinga wenyewe.
 
Rais Magufuli akiwa na Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan ametoa agizo hilo  tarehe 06 Desemba, 2016 Ikulu Jijini Dar es Salaam huku akionya kuwa kiongozi yeyote ambaye hayupo tayari kutekeleza agizo hilo aachie ngazi.

Waziri Simbachawene 'ANYWEA' kuhusu Zoezi la Kuwaondoa Machinga

$
0
0
Waziri wa nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tamisemi Mhe. George Simbachawene ameitikia mara moja agizo lililotolewa na Rais Dkt John Pombe Magufuli la kusitisha zoezi la kuwaondoa machinga maeneo yasiyo rasmi

Mhe. Simbachawene, ameitikia agizo hilo kwa kuwataka  wakuu wa wilaya pamoja na halmashauri zote nchini kuangalia ufumbuzi na utaratibu mzuri wa kuwashirikisha wajasiriamali hao ili kupata ufumbuzi ulioshirikisha kuliko utaratibu wa sasa wakuwafukuza bila kusikiliza madai yao.

Mhe. Simbachawene amesema, Rais Magufuli anatambua mchango mkubwa na kazi nzuri inayofanywa na wakuu wa wilaya katika kuleta maendeleo hivyo kuweka maeneo sahihi kwaajili ya wafanyabiashara wadogo kutaleta maana kubwa ya uwajibikaji. 

 “Kwa kuanzia ni vema yakatengwa maeneo ya katikati ya mji yenye wateja wa bidhaa zinazouzwa, kwa kuangalia uwezekano wa kufunga mtaa japo mmoja ili utumike kwa kazi za kimachinga,” alisema jana Simbachawene wakati akiongea na waandishi wa habari.

Alisema usumbufu unaojitokeza maeneo mbalimbali unasababisha wananchi kupoteza mitaji yao ambayo wengine wamekopa kwenye vikundi vya vicoba na hivyo kuhatarisha mustakabali wa maisha yao na familia zao.

Hivi karibuni waziri huyu alitoa agizo kwa wakuu wa mikoa na wakuu wa wilaya nchi nzima kuhakikisha wanawaondoa wafanyabiashara hao katika maeneo yasiyo rasmi kwa sababu wanaleta usumbufu na uchafu, agizo ambalo lilianza kutekelezwa mara moja katika maeneo mbalimbali ikiwemo Mwanza na Dar es Salaam.
 

Ripoti ya Madaktari kuhusu chanzo cha kifo cha mchezaji wa Mbao FC

$
0
0

Ripoti iliyotolewa na Mganga Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Dk. Thoma Rutta na kusomwa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kagera, Augustine Ollomi inaeleza kuwa kusimama kwa moyo ghafla  ndio chanzo cha kifo chipukizi wa Mbao FC ya Mwanza, Ismail Khalfan Mrisho.

Taarifa hiyo ilitolewa jana na kamanda huyo alipokuwa akizungumza kuelezea chanzo cha kifo cha mchezaji huyo kilichotokea Jumapili wakati wa mchezo wa Mbao FC dhidi ya Mwadui FC ikiwa ni ligi ya vijana katika uwaja wa Kaitaba mkoani Kagera.

Daktari ametoa taarifa ya uchunguzi na kusema chanzo ni kusimama kwa moyo ghafla. Marehemu hakuwa na jeraha lolote, alisema Kamanda Ollomi.

Ismail Mrisho alizaliwa Mei 22, 1997 akiwa ni mtoto wa kwanza katika familia yao. Amesoma Shule ya Msingi Nyakabungo kuanzia mwaka 2006 hadi 2012. Mwana 2013 alijiunga na Sekondari ya Mwanza ambapo alihitimu mwaka 2016. Ismail alikuwa amepata ufadhili wa kwenda kusoma Chuo Kikuu cha Louisiana State nchini Marekani kuanzia mwakani.

Ismail lifikwa na mauti muda mfupi baada ya kugongana na mchezaji wa Mwadui, alipojaribu kusimama baada ya hapo alianguka tena ndipo alipokimbizwa hospitali mjini Bukoba lakini akafariki. 

Kabla ya kukumbwa na mauti hayo, aliifungia timu yake ya Mbao goli la kuongoza ambapo mchezo ulimalizika kwa Mbao kupata ushindi wa 2-0.

Ugomvi wa CUF Wachukua Sura Mpya......Upande wa Lipumba na Maalim Seif Watangaza Kusimamisha Wagombea Kivyao

$
0
0
Mgogoro wa uongozi unaoendelea ndani ya chama cha CUF huenda ukaathiri ushiriki wake kwenye uchaguzi mdogo unaotarajiwa kufanyika Januari 27 baada ya pande zote mbili zinazosigana kujiandaa kuteua wagombea.

Mbali ya mgogoro huo kuhofiwa kukiathiri chama pengine hadi kusababisha wagombea wake kuzuiwa, pia unaweza kuudhoofisha Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa).

Habari kutoka ndani ya chama hicho zinasema upande wa Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba anayetambuliwa na Msajili wa vyama vya siasa uko kwenye maandalizi ilhali ule wa Katibu Mkuu, Seif Sharrif Hamad unatarajiwa kukutana na watendaji wa chama kujadili ushiriki wao.

Profesa Lipumba aliyeiongoza CUF tangu mwaka 1995, alijiuzulu kwa hiari uenyekiti wake Agosti 2015 lakini siku chache kabla ya CUF kuitisha mkutano Agosti mwaka huu wa kujadili barua yake, aliandika barua ya kutengua kujiuzulu na akarejea kazini.

Siku ya mkutano mkuu uliofanyika Ubungo Plaza, wajumbe waliridhia kujiuzulu kwake lakini walipoingia kuchagua mrithi wake, wafuasi wa Profesa Lipumba walivamia mkutano na kuuvuruga hali iliyosababisha baadaye kusimamishwa kwake.

Alipoulizwa jana namna CUF yenye mgogoro itakavyoshiriki uchaguzi wa madiwani katika kata 22 Bara na ubunge wa Jimbo la Dimani, Zanzibar, Kaimu Mwenyekiti wa Kamati ya Uongozi CUF, Julius Mtatiro alisema wapo katika mikakati kuhakikisha wanashiriki kikamilifu.

Mtatiro alisema muda wowote kuanzia sasa Katibu Mkuu, Maalim Seif atakutana na watendaji wa chama kujadili kwa kina suala hilo na kutoa maelekezo.

“Tutashiriki vizuri na niwaweke wazi Watanzania kuwa shughuli za chama zinaendelea kama kawaida hivyo kamati za utendaji zitatimiza wajibu wake wa kuwapitisha wagombea watakaojitosa kwenye kinyang’anyiro,” alisema.

Kuhusu Profesa Lipumba, Mtatiro alisema, “Hatuwezi kufanya kazi na mtu wa CCM kumsogeza karibu yetu ni kumleta atuharibie chama jambo ambalo hatuwezi kuliruhusu. Ingekuwa lile suala la kujiuzulu aliteleza tungemwelewa na kumsamehe lakini inavyoonekana yupo kwenye mipango yake katu hatuwezi kumuweka karibu.”

Lakini Naibu Mkurugenzi wa Habari na Uenezi wa CUF anayemuunga mkono Lipumba, Abdul Kambaya alisema, “Tuna kikao leo (jana) upande wa Bara chini ya Mwenyekiti Profesa Lipumba kujadili suala hilo la uchaguzi, kuhusu upande wa Zanzibar sifahamu chochote.”

Akizungumzia uchaguzi huo mdogo, Naibu Katibu Mkuu wa Chadema upande wa Zanzibar, Salum Mwalimu alisema Ukawa utakuwa bega kwa bega na CUF katika uchaguzi huo kwani wanaitambua kuwa iko moja si mbili kama inavyotengenezwa na watu wasiopenda maendeleo ya chama hicho.

“Tunatambua na kuheshimu uamuzi wa wanachama na viongozi halali wa chama, CUF iko moja, kama kuna mtu anatengeneza propaganda alifanya hivyo akiamini anakwenda kukiua chama ajue bado kinaendelea kusimama,” alisema.

“Pale atakaposimamishwa mgombea kutoka chama hicho Ukawa tutamuunga mkono na kumpigania kuhakikisha anashinda. Tunaamini pia nao watafanya hivyo akisimamishwa mgombea wa Chadema, ”alisema Mwalimu

Katibu Mkuu wa NCCR-Mageuzi Juju Danda alisema mgogoro wa CUF hautaleta changamoto yoyote kwenye Ukawa kwa kuwa wanamtambua katibu mkuu. Alisema Ukawa unamtambua Maalim Seif na ndiye mtendaji mkuu wa chama hivyo watakuwa tayari kushirikiana naye katika kila jambo.

Kuhusu mpasuko unaoendelea ndani ya chama hicho, Danda alisema suala hilo waachiwe CUF wenyewe ndiyo watakaoamua. “Mtendaji Mkuu wa chama ni katibu si Mwenyekiti, na kwa kuwa tupo pamoja na Maalim hatuoni changamoto yoyote yeye ndiye anayesimamia uteuzi na tunategemea mambo yatakwenda sawa,” alisema.

Katika hatua nyingine hatima ya Jaji Sekieti Kihiyo anayesikilkiza kesi ya CUF kujitoa sasa itajulikana Desemba 14 atakapotoa uamuzi wa maombi ya wadai kumtaka ajiondoe.

Jaji Kihiyo alipanga kutoa uamuzi wa maombi hayo dhidi yake jana baada ya kumaliza kusikiliza hoja za pande zote katika kesi hiyo, ambazo zilizua mvutano mkali baina ya mawakili wa wadai kwa upande mmoja na mawakili wa wadaiwa pamoja na Jaji Kihiyo kwa upande mwingine.

Kesi hiyo imefunguliwa na baadhi ya wajumbe wa Bodi ya Wadhamnini wa CUF, dhidi ya Profesa Lipumba, Naibu Katibu Mkuu wa chana hicho Bara, Magdalena Sakaya pamoja na wanachama wengine tisa waliosimamishwa uanachama wa chama hicho.

Wengine ni Msajili wa Vyama vya Siasa, Jaji Francis Mutungi, ambaye ndiye mdaiwa wa kwanza katika kesi hiyo na Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), ambaye ni mdaiwa wa pili.

Kesi hiyo ilitarajiwa kusikilizwa jana lakini kabla ya kuendelea, kiongozi wa jopo la mawakili wa wadai, Juma Nassoro aliieleza mahakama kuwa wadai wameandika barua wakimtaka jaji ajiondoe kuendelea na kesi hiyo kwa maelezo hawana imani naye.

Rais Magufuli awapandisha vyeo Maafisa Wakuu wawili wa JWTZ kuwa Meja Jenerali

$
0
0

ais na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Tanzania Mh. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli amewapandisha vyeo Maafisa Wakuu wawili wa JWTZ kuwa Meja Jenerali kuanzia tarehe 03 Disemba 2016. Maafisa Wakuu hao ni;

Brigedia Jenerali George William Ingram ambaye ni Mkuu wa Kamandi ya Jeshi la Anga, na  Brigedia Jenerali Michael Wambura Isamuhyo ambaye ni Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa.

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Davis Adolf Mwamunyange kwa niaba ya Rais na Amiri Jeshi Mkuu anawapongeza na kuwatakia kheri katika vyeo vyao vipya.
 

Imetolewa  na  Kurugenzi  ya  Habari  na
Uhusiano Makao Makuu ya Jeshi, Upanga
S.L.P  9203,   

Dar es Salaam,  Tanzania.

Kwa Mawasiliano zaidi: 0784-477638/0756-716085
R5
Brigedia Jenerali George William Ingram ambaye ni Mkuu wa Kamandi ya Jeshi la Anga
Brigedia Jenerali Michael Wambura Isamuhyo ambaye ni Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa.

RIWAYA: She is My Wife- Sehemu ya 49 & 50 (Mwisho)

$
0
0
Mwandishi: EDDAZARIA G.MSULWA

ILIPOISHIA  
“Tumekupata”
Alipokea jibu mmoja kutoka, makao makuu. Wakaendelea kujibu mashambulizi ya watu hao ambao wamewavamia na hawakujua niwatu wangapi. Hali katika eneo la mto ikazidi kuwa mbaya zaidi milio ya bunduki, ilizidi kurindima kila kona.
“Helcoptar…..!!!”
Anna alishangaa baada ya kuona helcoptar zipatazo sita za jeshi la marekani zikifika katika eneo hilo, huku wajeshi wengi wakishuka kwenye helcoptar hizo zilizopo hewani, kwa kutumia kamba ndefu hadi chini.
‘Tunakufa leo’
Halima alijisemea kimoyo moyo huku akiendelea kuftyatua risasi nyingi kuelekea walipo wanajeshi hao.

ENDELEA
“Sister nguvu yetu imesha anza kuwa ndogo tunafanyaje”
Jamaa mmoja alizungumza huku akibadili magazine ya mwisho katika bunduki yake na endapo risasi zitakwisha kwenye magazine hiyo, basi hatokuwa na msaada wowote.
“Endelea kupambana hatuwezi kurudi nyuma”

Fetty alizungumza huku akizendelea kufyatua risasi kuelekea walipo wanajeshi hao
“Fetty eheee omba msaada kwa mkuu, lasivyo tutakufa humu”
Halima alilalamika kama kawaida yake, Fetty kutazama idadi ya wanajeshi wanao shuka kwenye helecoptar hizo kubwa za kijeshi, ikambidi awasilianen na bwana Rusev.
“Muheshimiwa wanajeshi wa Marekani wametuvamia”
“Endeleni kupambana”
“Sawa muheshimiwa ila tunahitaji msaada wa vijana wengine”

“Msaada….. Masaada wa nini pambaneni”
Majibu ya bwana Rusev, yakamtia hasira Fetty aliye jibanza kwenye mti huku akisikilizia jinsi risasi hizo zinavyo  zidi kupigwa kwenye sehemu walipo.
“Muheshimiwa nakuheshimu, ila narudia tena nahitaji msaada wako”
“Kama hamjampata Agnes basi, hakuna cha msaada wowote kutoka kwangu”
Mawasiliano yakakatwa, Fetry akabaki aking’ata meno yake kwa hasira. Kumbukumbu ya tukio hili likamrudisha miaka ya nyuma, jinsi siku wanajeshi wa Tanzania walivyo vamia kwenye kambi yao, na kuwashambulia sana kisha wakaingia mikononi mwao wanajeshi hao, hapo ndipo ulipo kuwa mwisho wa maisha yao ya furaha na amani na wakajikuta wakiwa wanaishi kama wakimbizi na kukubali kufanya kazi na watu ambao ni magaidi wa kidunia, ili mradi waweze kuendelea kuishi kwenye maisha haya.

Fetty akiwa katika mawazo hayo, akamshuhudia kijana mmoja wa bwana Rusev akianguka chini, baada ya kupigwa risasi ya kichwa, akiwa anashangaa tukio hilo, kijana mwengine akajitokea kwa hasira kwenye mti alio kuwa amejificha huku akiwa na bastola mbili mkononi mwake, akifyatua risasi zisizo na idadi, ila alicho weza kukutana nacho, ni mvua ya risasi zizizo toka kwenye jeshi lilio wazidi nguvu.
“Fetty amesemaje”
Halima alizungumza huku machozi yakimlenga lenga.
“Mmmmmm…….”
“Amesemaje mkuuuuuu…..”
“Hana msaada na sisi, tupambane kama kufa tufe ila si kukamatwa”

“Mungu weeeee, nini sasa hichi”
Halima alizungumza huku machozi yakimwagika, akachomo magazine kwenye bunduki yake na kukuta ikiwa na risasi chache, akajipapasa hana tena magazine. Akageuza kichwa sehemu alipo Anna, akamkuta akiendelea kufyatua risasi pasipo kuangalia wezake wapo katika hali gani. Vijana wawili wa bwana Rusev walio bakia, wanazidi kuyapigania maisha yao kwani ni heri kufa kuliko kukamatwa na jeshi hilo.
“Nakupenda Anna, Fetty”
Halima alizungumza kwa sauti ya unyonge, akairudishia Magazine yake kwenye bunduki, akapiga goti mmoja chini, akawatazama jinsi wanajeshi wa wanavyo zivurumisha risasi katika eneo walipo.
“One one one bullet”(Mtu mmoja, risasi moja)
Halima alizungumza huku akiendelea kufyatatua risasi kwa kila aliye weza kumuona kwa wakati huo. Ila zilipo fika risasi kumi na mbili, bunduki yake ikagoma kutoa risasi, ikiashiria kwamba hakuna risasi nyingine ndani ya bunduki hiyo aina ya AK47, zinazo tumika sana nchini Russia.
                                                                                                 ***  
     Asubuhi na mapema, raisi Praygod akakurupuka kitandani, akaka kitako huku akionekana kuwa na wasiwasi mwingi sana. Rahabu taratibu akajinyanyua na kumtazama jinsi anavyo tokwa na jasho jingi mwilini.
“Una tatizo gani mume wangu?”
“Naota mandoto mabaya mabaya tu”
“Ohoo pole mume wangu”

Rahab alizungumza huku akimkumbatia raisi Praygod, taratibu akaanza kumpapasa kifuani mwake, hisia za mapenzi zikaanza kuusisimua mwili wa raisi Praygod, taratibu akajikuta akianza kumnyonya mke wake mdomo, baada ya muda wakajikuta wakizama kwenye dimbwi zito la kupena haki ya wanandoa.
Baada ya kumaliza wakaingia bafuni kuoga, Rahab akamuandalia mume wake nguo za kuvaa kwenye kikao anacho kwenda kukifanya na wakuu wote wa kitengo cha usalama wa taifa.
“Leo nitapendeza sana mke wangu”
“Kwa nini?”
“Umenichagulia nguo wewe”
“Ahaaa si kawaida”
“Sawa ila utapendeza sana, siku zote nimezoea kujichagulia nguo mwenyewe”

“Ila si una wafanyakazi wenye jukumu hili?”
“Ndio ila mke wangu upo kwa nini nichaguliwe na mfanyakazi”
“Hapa utakuwa poa sana”
Rahab alizungumza baada ya kumfunga tai raisi Praygod, akampiga busu la mdomoni
“Twende tukapate kifungua kinywa pamoja”
Wakatoka na kwenda kwenye sebla yao, ambapo wakakuta chakula tayari kimesha andaliwa na kukaguliwa na daktari maalumu anaye weza kukagua chakula cha raisi kabla hajakila. Wakapata chakula baada ya kumaliza akaomba kuweza kuitiwa wafanyakazi wote wa ikulu, ikawa kama alivyo agiza.
“Nimewaita hapa kutokana nahitaji kuwatambulisha mama yenu, so mukimuona huko nje misije mukamdharau.”
“Muheshimuni kama munavyo niheshimu mimi, mpendeni kama munavyo nipenda mimi. Nisinge penda mtu yoyote kuweza kuona mtu ana….ana anaa mkosea adabu”
“Mumenielewa”

Ndio muheshimiwa”
Baada ya utambulisho huo, raisi Praygod akawaamuru wafanyakazi wake kuweza kuondoka, akabaki na mke wake. Akamtuma mmoja wa walinzi wake kwenda kumuita Samson kwenye chumba chake. Samson akafika katika sehemu walipo.
“Umeamkaje muheshimiwa”
Samson alisalimia kwa heshima
“Salama tu kaa”
“Madam Rahab je wewe umeakaje?”
“Nipo salama”
Kwa nguvu aliyo weza kumuwekea Samson. Rahab anamamlaka makubwa ya kuweza kumuamrisha Samson, akafanya kile alicho weza kumuambia.
“Jiandaeni kwani nitawahitaji kwenye kikao baada ya muda fulani hivi”
“Baby kwa nini sisi?”
“Nahitaji tusaidiane katika kuirudisha heshima ya nchi, pia kesho tutakwenda kwenye misiba ya wanajeshi wali fariki walipo kuwa wakimsafirisha makamu wa raisi”
“Kwani hawakuzikwa?”

“Ndio, hawajazikwa, nimeagiza kwamba iwe siku ya maombolezi kwani pia wale wananchi walio poteza maisha uwanja wataifa inabdidi kuzikwa kesho”
“Sawa”
Raisi Praygod akawaaga, akaongozana na walinzi wake wawili hadi chumba cha mkutano.
“Hivi umempataje pataje raisi?”
Samson alizungumza huku akiachia tabasamu pana usoni mwake
“Ni story ndefu sana, tangu tuachane pale kwenye ndege basi ikawa ndio siku ya mimi kuweza kuonana na raisi Pray”
“Ahaaa maisha haya bwana, adui yako amekuwa mume wako”
“Usiongee kwa sauti kubwa, tusije kuhisiwa vibaya. Ila kusema kweli ninampenda mume wangu”
Samson hakuwa na chakuzungumza zaidi ya kuanza kupata kifungua kinywa, Rahab akaondoka na kuelekea chumbani kwao kujiandaa na kikao ambacho mume wake alimuhitaji kuweza kufika.
                                                                                      ***
“Kila mmoja ninaamini ameyaona yaliyo jitokeza.”
“Nchi imepata fedheha mbele ya wageni, walio huzuria msiba ulio kuwa wangu pamoja na wahanga wengine. Kiongozi mkubwa wa nchi kuweza kufanya mambo ambayo yangefanywa na wagaidi ameweza kuyafanya yeye.”
“Inaonekana ni jinsi gani, kitengo chenu, kilivyo jisahau kwa asiliimia nyingi tuu kwani hadi inafikia hatua ya matukio ya ajabu kama kushambuliwa kwa wanajeshi na makamu wa raisi kutoroshwa, yote ni uzembe na inavyo onekana anamiliki kundi kubwa la vijana anao weza kuwatumia katika kuleta machafuko kwenye nchi hii.”

Raisi Praygod alizungumza kwa saut iliyo jaa msisitizo mkubwa huku akiwatazama viongozi hao wapatao kumi na mbili walio izunguka meza kubwa katika eneo hilo.
“Yote yaliyo weza kujitokeza, hayaweze kubadilika, ila tunaweza kuyafanya wananchi wakaweza kutuamini na kuishi kwa amani. Kwani inavyo onekana hali ya amni imekuwa tata kwa wananchi.”
“Hivyo basi, nitahakikisha kwamba tunafanya kazi, iliyo wafanya kila mmoja wenu kuwa katika kitengo alicho kuwepo. Hata mimi mwenyewe nitahakikisha kwamba ninafanya kazi zote zakijeshi kama ni kuua basi tuue yule anaye stahili kuuliwa.”
“Sinto kuwa na msamaha kwa mtu ambaye ukimpa nafasi moja, anakuua wewe. Kuanzia sasa nahitaji kusikia ni wapi alipo makamu wa raisi wangu, yeye na kundi lake tuweze kuwatia nguvuni kwa pamoja. Nakaribisha maoni”

Raisi  Praygod akazima maiki yake aliyo kuwa akitumia kuzungumzia. Kiongozi mmoja akanyoosha kidole na raisi Praygod akampa nafasi ya kuzungumza
“Muheshimiwa, kwanza tuombe radhi ya yale yaliyo jitokeza. Pili tumeweza kupata sehemu ambayo makamu wako amejificha na kundi lake”
“Ni hapa ndani ya nchi?”
Raisi Praygod alizungumza huku akimtumbulia macho kiongozi huyo.
“Hapana si ndani ya nchi hii, ila yupo nchini Kenya, na taarifa hizi tulizipata kwa wana usalama wa nchi ya Kenya”
“Eheee mu..mu muu mumejipangaje?”
“Tulimesha andaa taskforce kuweza kuvamia katika sehemu hiyo, huku tukishirikiana na interpol”
“Fanyeni mawasiliano na raisi wa Kenya sasa hivi nizungumze naye”
                                                                                    ***
“Kwa nini memenisaidia?”
Agnes aliuliza swali baada ya kumaliza kupata kifungua kinywa akiwa na Jackline pamoja na Monk
“Kwani inatubidi kurudi nchini kwetu kuimarisha ulinzi na si kuendelea kutumika katika vikosi vya ajabu”
“Umejuaje kama ni vikosi vya ajabu na umenifamu fahamu vipi mimi?”
Agnes aliendelea kumuuliza maswali Jackline ili kuweza kumfahamu vizuri
“Kipindi nyinyi munakuja kwenye ngome ya bwana Rusev, mimi nilikuwa ni miongoni mwa walinzi wake wakaribu. Wiki moja baada ya nyinyi kufika pale mimi nilipewa kazi ya kwenda kumuangamiza raisi wa Korea kaskazini.”

Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images