MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA
ILIPOISHIA
"Yes mpango umekwenda vizuri kama nilivyo panga"
John alionekana akiwa amefurahi sana kwa habari hiyo. Iliyo onyeshwa kwenye kituo hichi cha habari. Hii ni baada ya muandishi huyo kudai kwamba ndege hiyo ilikuwa ikitokea nchini Brazili, kwenda bara la Afrika. Abiria wote waliomo ndani ya ndege hiyo wamekufa kwenye mlipuko huo wa ndege ulio tokea majira ya mida hii ya mchana, jambo lililo nipa wasiwasi mwingi, hadi nikajihisi mwili mzima kuishiwa na nguvu.
ENDELEA
Pretty akamtazama John kwa umakini huku akionekana kuwa na mshangao mkubwa.
"Unafurahia nini?"
"Kuna mpango niliupanga na vijana wangu, kuhusiana hiyo ndege"
"Unataka kusema wewe umehusika kwenye mpango wa hiyo ndege kulipuka?"
Pretty alimuuliza John huku akimkodolea macho ya wasiwasi. Mimi hata nguvu ya kunyanyuka kwenye kochi sikuwa nayo hii yote ni kwakuiwazia familia yangu.
"Ndio"
"Kwanini?"
Kuna mjinga nilimuua, sasa ulikua muda wakuiteketeza famia yake"
Nikastukia kumuona Pretty akinyanyuka kwa hasira na kumrukia John, hadi sofa alilo likalia wakaaanguka nalo. Sheila akasimama kwa haraka na kumchomoa Pretty aliyekuwa akimshambulia mumewe kwa kumpiga kwa makofi mfululizo.
"Wewe ni gaidi"
Pretty alizungumza kwa hasira, huku mimi nikiwa nimepigwa na bumbuazi lililo nifanya nishindwe kufanya kitu cha aina yoyote.
"No no nakudanganya Pretty"
John alizungumza huku akicheka.
"Muongo wewe"
"Kweli Pretty siwezi kufanya kitu kama hicho. Kwanza nitaanzia wapi. Eti Henry kweli ninaweza kufanya jambo hili?"
Nilitabasamu tu, hata kinywa changu kikashindwa kufunguka. Tangu nizaliwe sijawahi kukumbana na hali ya mshangao kama hii, iliyo nimaliza nguvu zote.
Pretty akafungua mlango na kutoka huku akiubamiza kwanguvu. Jambo lililo nistua na kurudi kwenye hali yangu yakawaida. Nikanyanyuka kwa haraka na kumfwata Pretty ndani kwake
"Nilazima nimpeleke polisi nikamstaki"
Pretty alizungumza kwa hasira huku akiingia chumbani kwake. Nikamfwata na kumkuta akiwa amekaa kwenye kitanda huku akilia.
"Pretty nisikilize, kitu kimoja"
"Nahitaji zile video mbili kama una flash zihifadhi sawa"
Pretty alibaki akiwa amenikodolea macho. Nikatoa simu mfukoni na kuingiza namba za Blanka. Ikaita kwa muda mrefu, kisha ilapokelewa.
"Blanka wamefika?"
"Hawajafika"
Jibu la Blanka likanifanya nizidi kuchanganyiliwa, hadi mwili ukawa unanitetemeka kwa woga kwani swala la akufiwa nafamilia tena kwa wakati mmoja, sikuliwazia kichwani mwangu.
"Hawajakupigia?"
"Hapana hawajanipigia"
Nikakata simu nakushusha pumzi kubwa, nikabaki nimesimma pasipo kuzungumza kitu chochote na Pretty. Nikamshika mkono Pretty na kumnyanyua juu.
"Twende kwangu"
"Kufanya nini?"
"Twende tu"
Tukatoka sebleni, Petty akaziingiza video zote mbili kwenye flash, kisha akachukua begi lake lenye laptop.
Tukaondo hadi nyumbani mwangu. Kitu cha kwanza nikaifwata simu ya chumbani kwangu. Nikamiinya kitufe cha kusikiliza ujumbe wa sauti, ili kutambua kama kuna ujumbe wowote wa suti ulio ingia nikiwa sipo.
"Eddy mume wangu, mbona hupokei simu?"
Ilikuwa nisauti ya Phidaya, kwenye ujumbe wa kwanza wasauti
"Tumeamua kubadilisha safari, tupo Marekani kwa sasa. Shamsa ndio alitoa pendekezo la sisi kubadilisha safari. Ukipata ujumbe huu usiwe na wasiwasi, tupo salama na kesho tunakwenda Tanzania. Nakuupenda mume wangu"
Ujumbe wasauti, ukawa umekwisha. Nikashusha pumzi nyingi, huku tabasamu pana likiwa usoni mwangu. Nikatoka sebleni na kumkuta Pretty akiwa anaminya minya batani za laptop yake.
"Unafanya nini?"
"Nachapisha habari za kumchafua John kwenye mtandao na kuituma hii video ya mauaji"
"Hapana usifanye hivyo"
"Kwanini?"
"Nataka kumuua John taratibu"
"Kumuua taratibu!?"
"Ndio"
Nikaanza kumuadisia historia nzima ya maisha yangu. Kuanzia nilivyokua shule na John hadi leo ni adui yangu.
"Sasa kwanini hutaki tumuue sasa hivi?"
"Pretty mpango wangu ni mrahisi sana. Nataka kumuua kwa kifo chakumzalilisha na kumtesa sana."
"Ila familia yangu ipo salama"
"Kweli?"
"Ndio"
Pretty akanikumbatia kwa furaha, huku machozi yakimwagika kwani historia yangu ilimuuzunisha sana.
Siku ya pili, tukakutana na John na Sheila wakiwa kwenye maandalizi. Ikamlazimu Pretty kuwaomba msamaha kwa kile kilicho jitokeza jana mchana. Hii ikiwa ni moja ya mpango wetu wa kumteketeza John na Sheila, pasipo wao kujua chochote.
"Nilijua tu nihasira, mimi nimemsamehe"
John alizungumza huku akimpa mkono Pretty.
Ikawa ni furaha kubwa sana kwa John, na Sheila wake. Wakiamini urafiki wetu utaendelea kama kawaida na laiti wangejua wasinge ruhusu kujipendekeza kwetu.
***
Siku ya harusi ya John ikawadia, mimi na Pretty tukawa nimiongoni mwa waalikwa kwenye sherehe hii ndani ya kanisa hili kubwa la Roman katolic.
"Kila kitu umekipanga sawa?"
Nilimuuliza Pretty mara baada ya kufika kanisani, tukishuka kwenye gari yetu aina ya BMW, tulilo linunua jana kwa kazi moja tu iliyopo mbele yetu.
"Kila kitu kipo powa mpenzi"
Kabla sijazunguza chochote simu yangu ikaita kwa namba ya Blanka, ndio inayo nipigia.
"Nipigie bwana"
Blanka alizungumza kwa furaha, ikanibidi nikate simu na kumpigia.
"Ndio kaka Eddy. Kweli wewe nikiboko"
"Kwanin?"
"Yaaani toto lako nikopi na wewe yaani umefanya kazi kubwa kulitafuta"
"Kwani wamefika?"
"Ahaaa ndio nipo hapa uwanja wa ndege nimewapokea yaani weee acha tuu. Ninafuraha yakufa mtu"
"Hembu mpe Junio simu nizungumze naye"
"Dady tumefika Tanzania"
"Umemuona antie?"
"Ndio, ila kuna joto kali"
"Poleni mwanangu, mpe mama simu"
Nikasikia sauti ya Junio ikimuita Phidaya, furaha ikazidi kuongezeka moyoni mwangu, nakujiamini zaidi kwamba kazi yangu inazidi kuwa nyepesi zaidi.
"Mume"
"Niambie mke wangu"
"Safi, tumesha fika Tz yaani hapa nijoto"
"Sasa hivi nisangapi?"
"Saa.....saa tano inakwenda saa sita usiku"
"Poleni kwa uchovu"
"Yàani wee acha tu, yaani tumetoka Marekani jana alfajiri, tunashukuru Mungu ndege tuliyo panda haikupita kwenye nchi nyingi"
"Ilikuwaje mukaenda Marekani?"
"Hilo swali muulize mwanao Shamsa"
"Mpe simu"
"Vipi wewe"
"Ahaaa safi baba"
"Hembu sogea pembeni uniambie nini kilitokea?"
"Wee acha baba, kipindi tupo uwanja wa ndege kuna jamaa nilikua ninamtilia mashaka, sasa tulipo maliza kukaguliwa. Kipindi sasa tunaelekea kupanda basi lile linalo wapeleka watu kwenye ndege"