Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Jambazi Awajeruhi Kwa Bomu Askari na Raia Wanne Kigoma

$
0
0
Polisi na raia wanne wamejeruhiwa kwa bomu la kutupwa kwa mkono walipokuwa wakimkamata mtuhumiwa wa ujambazi kwenye Kijiji cha Uvinza mkoani Kigoma. Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kigoma, Ferdinand Mtui alisema jana kuwa tukio hilo lilitokea Oktoba 14. 

Alimtaja mtuhumiwa huyo kuwa ni Yahya Kamuhanda (49) mkazi wa kijiji hicho. Mtui aliwataja majeruhi hao kuwa ni askari polisi F.3187 Koplo Isaya na raia Saidi Mohamed, Seleman Kashali, Joseph Daudi na Hassan Nasibu, wote wakazi wa Kijiji cha Uvinza. 

Alisema askari walipata taarifa kutoka kwa raia wema kwamba Kamuhanda anajiandaa kufanya uhalifu hivyo waliweka mtego eneo la Uvinza Madukani alikokwenda kununua mahitaji. 

Alidai kuwa alipotambua anafuatiliwa alitupa bomu ndipo polisi walimpiga risasi mguuni na wananchi walimvamia na kumshambulia kabla ya askari kutumia nguvu kumwokoa asiuawe kwa kipigo. 

Mtui alisema mtuhumiwa alipohojiwa alisema alificha bunduki kijijini kwao Lukole wilayani Ngara mkoani Kagera, ambako askari walikamata SMG yenye namba 78GA5062 ikiwa imefukiwa ardhini.

 Pia, walikamata magazini saba, moja ilikuwa na risasi 40, nne (risasi 30 kila moja) na mbili (risasi 20 kila moja) na risasi 75 zilikuwa kwenye mfuko wa sandarusi. Pingu moja na funguo zake, maski tisa na laini 20 za mtandao wa Halotel ambazo hazijasajiliwa. 

Mtui alisema mtuhumiwa huyo alifariki dunia juzi akipatiwa matibabu kwenye Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Kigoma (Maweni). Alisema majeruhi wote watano walipata matibabu hospitalini hapo na waliruhusiwa kurudi nyumbani. 


Basi la Barcelona Lapata Ajali na Kuua Watu 10 Mkoani Lindi

$
0
0
Watu 10 wamefariki dunia na wengine 44 wamejeruhiwa baada ya basi la kampuni ya Barcelona walilokuwa wakisafiria kutoka jijini Dar es Salaam kwenda mkoani Lindi  kupata ajali eneo na Miteja mkoani Lindi.

Taarifa iliyotolewa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Lindi, Renata Mzinga imesema kuwa chanzo cha ajali hiyo kimetokana na tairi ya gari ya upande wa kushoto kupasuka na kutokana na mwendo wa kasi wa basi hilo, dereva alipoteza uelekeo ndipo likapinduka.

Pia Kamanda Mzinga amesema kuwa wamechunguza na kugundua kua licha ya kuwa basi hilo lilikuwa na uwezo wa kubeba abiria 48, wakati basi hilo linapata ajali kulikuwa na abiria 54 kitu ambacho ni kosa kisheria.

Aidha, Kamanda Mzinga amesema kuwa bado wanaendelea na uchunguzi kuweza kubaini alipo dereva ili kuweza kufahamu ni kipi hasa kilichotokea. Hadi sasa wanamshikilia kondakta wa basi hilo lakini bado hajaweza kuelezea tukio halisi.

Lowassa na Kikwete Wakutana Uso Kwa Uoso Dar

$
0
0
Hatimaye mazishi ya kuuaga mwili wa Meya wa zamani wa Jiji la Dar es Salaam, Dk. Didas Masaburi, yamewakutanisha Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa na Rais mstaafu wa awamu ya nne, Jakaya Kikwete kwa kusalimiana na kushikana mikono.

Tukio hilo la aina yake liliwafanya watu mbalimbali waliokuwa katika msiba huo kubaki wakishangaa, hasa baada ya Rais mstaafu Kikwete kumfuata Lowassa na kumwuliza hali rafiki yake huyo wa zamani waliokulia wote CCM.

Tangu wakati huo viongozi hao ambao walikuwa marafiki wa karibu tangu ujana wao walikuwa wakirushiana vijembe ambapo jana walikutana ana kwa ana katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam wakati wa kuuaga mwili wa Dk. Masaburi kabla ya kwenda kuzikwa nyumbani kwake Chanika Manispaa ya Ilala.

Akiwa katika viwanja hivyo, Kikwete alipomwona Lowassa akiingia viwanjani hapo alinyanyuka na kumfuta Lowassa katika kiti chake kisha kusalimiana naye kwa kupeana mikoni huku wakizungumza.

Lowassa aliyekuwa ameketi jirani na Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana pamoja na mkewe Regina Lowassa, alisimama na kumjibu salamu.

Kwa muda mrefu wanasiasa hao ambao wamewahi kuwa marafiki hadi kupewa jina la utani ‘Boys II Men’, waliingia katika uhasama kwa kile kinachodaiwa ni kusalitiana kisiasa.

Urafiki wa wawili hao ulianza kuingia doa mwaka 2008 wakati wa kashfa ya Richmond iliyosababisha Lowassa kujiuzulu uwaziri mkuu kwa kile alichoeleza ni kunyimwa haki ya kusikilizwa baada ya kuibuka kwa kashfa hiyo kwa kile alichodai ilikuwa ni vita ya kutaka ‘uwaziri mkuu’.

Ukaribu wa Lowassa na Kikwete uliendelea kupungua na kuwa shakani zaidi wakati wa Uchaguzi Mkuu wa mwaka jana baada ya Lowassa kukatwa jina lake katika kinyang’ anyiro cha kuwania nafasi ya kugombea urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) na kuamua kuhamia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).

Kwa takribani mwaka mmoja sasa tangu mchakato wa ndani wa CCM wa kumpata mgombea wake wa urais Julai 10, mwaka jana umalizike wawili hao hawajawahi kukutana hadharani na kupeana mikono.

Katika mchakato huo Kamati Kuu ya CCM iliyokutana hadi usiku wa manane iliibuka na jibu kwamba, jina la Edward Lowassa limekatwa katika watu wanaowania urais kupitia chama hicho.

Waliopitishwa na kuingia tano bora na Kamati Kuu walikuwa ni Bernard Membe, Dk John Magufuli, Dk Asha Rose Migiro, January Makamba na Amina Salum Ali, huku makada wengine 33 wakitupwa akiwamo Lowassa.

Kutokana na hali hiyo Lowassa alichukua aumuzi mzito wa kuihama CCM, Julai 28, mwaka jana na kujiunga na Chadema na hatimaye kuteuliwa kuwa mgombea urais kupitia chama hicho cha upinzani akiungwa mkoano na vyama vinaunda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa).

Mahakama Yaitupilia Mbali Kesi Ya Mbowe Hotels Dhidi Ya Shirika La Nyumba La Taifa (NHC )

$
0
0
Mahakama kuu kitengo cha Ardhi imetupilia mbali kesi ya maombi ya kurejea katika jengo iliyokuwa ofisi ya Tanzania Daima pamoja na ukumbi wa bilcanas.

Hukumu hiyo imetolewa leo na Jaji mfawidhi wa mahakama hiyo, Sivangilwa Mwangezi ambaye amesema kuwa taratibu zote zilifuatwa kuondoa vitu katika jengo hilo.

Amesema katika hukumu hiyo hakuna mtu aliyevunjiwa haki yake ya msingi kutokana na kufuatwa kwa Sheria dhidi ya madai ya Shirika la Nyumba NHC, kwa Mbowe HotelS.

Wakili wa upande wa NHC, Aliko Mwamnenge amesema kutokana na hukumu hiyo Mbowe hotelS wanadaiwa sh. Bilioni 1.7 na NHC.Amesema vitu haviwezi kurudishwa mpaka pale mlalamikiwa atakapolipa deni lake kwa NHC.

Nae Wakili upande Mbowe Hotel, John Malya amesema wamepokea hukumu na kuomba nakala ili kuweza kuifanyia kazi.Amesema kuwa nakala wakiipata wanaweza kuamua katika kukata rufaa.

Rais Magufuli Atengua Uteuzi wa Mkurugenzi Aliyewatishia Bastola Trafiki

RIWAYA: Sorry Madam - Sehemu ya 71 & 72 (Riwaya inawafaa kuanzia miaka 18 na kuendelea )

$
0
0
Mtunzi : Eddazaria g.Msulwa

ILIPOISHIA
“Nafanya hii, kwa ajili yakulipiza kisasi cha mume wangu”
“Ngoja kwanza, nipo tayari kufa, ila ninakuomba usimuue mke wangu”
Nilizungumza kwa ujasiri, nikiwa nipo tayari kwa kufa, Madam Mery akalinyanyua panga lake juu, akalishusha kwa kasi kwenye mkono wangu wa kulia

ENDELEA
Nikatoa ukulele mkali, ulio mfanya madam Mery kusitisha zoezi lake kuukata mkono wangu, panga lake likiwa limesimama sentimita chache kutoka ulipo mkono wangu
“Madam, ninakuomba unisamee”

Nilizungumza huku machozi yakiendelea kunimwagika usoni mwangu, madam Mery akanitazama kwa macho ya hasira yaliyo jaa
ukatili mkubwa, akawatazama Victoria na John ambao macho yao yote yalikuwa kwetu

“Natambua kwamba mimi nimkosaji sana kwako, ninastahili kufa mbele yako, ila si mbele ya macho ya mke wangu.Mtazame jinsi alivyo katika hali yake.Mule ndani amebeba kiumbe kama ulicho kuwa umekibeba wewe, miezi tisa, na Derick akakiangamiza mbele yetu.Yule ni mwanamke mwenzako ambaye anauchungu kama wewe”

Nilizungumza huku machozi yakiendelea kunimwagilka usoni mwangu, madam Mery kwa mbali machozi yakaanza kumlenga lenga, macho yake yamebadilika rangi na kuwa mekundu kiasi huku sura yake ikiwa imejaa mikunjo kwenye paji lake la uso akinitazama kwa uchungu sana
“Mery mimi pia ni binadamu, kumbuka ni mambo mangapi tuliyafanya tukiwa pamoja, vuta kumbukumbu ni vitu vingapi tulishiriki tukiwa pamoja, Eheeee, leo hii unataka kuimwaga damu yangu, leo hii unataka kunisulubu kikatili, le……..”

“Eddy STOP TALKING”(Eddy nyamazakuzungumza)
Madam Merry alizungumza kwa sauti ya juu, yenye uchungu ndani yake.Akalitupa chini panga lake alilokuwa amelishika.Machozi mengi yakaanza kumbubujika usoni mwake, John na Vivtoria wakabaki wakimtazama madam Mery, ambaye taratibu alianza kupiga hatua za kuelekea kwenye gari lake alilo kuja nalo

“Madam Vipi?”
John alizungumza huku akimwafwata madam Mery kwa nyuma
“John ninakuomba uniache”
Madam Mery aluzungumza huku akiunyanyua mkono wake mmoja akimzuia John asimfwae anapo elekea
“Ila madam haya sio makubaliano yetu”
“John sipo sawa nimekuambia usinifwate”

Madam Mery alizungumza kwa sauti ya ukali, huku machozi yakiendelea kumchuruzika usoni mwake.
“Sasa Madam tumfanye nini Eddy?”
Madam Mery akageuka kwa hasira, hadi John akastuka kidogo, akanitazama jinsi machozi yanavyo nimwagika, akayafumba macho yake kwa sekunde kadhaa, akionekana akifikiria kitu cha kufanya juu yangu.
“Kesho nimkute akiwa hai”

Madam Mery alizungumza kwa sauti ya upole, kisha akaelekea lilipo gari lake, akafunguliwa mlango na mlinzi wake, akaingia ndani ya gari na wakaondoka zao.John akalisindikiza magari ya Madam Merry yanayotoka kwenye geti kubwa la Godauni, lilipo fungwa taratibu John akanigeukia, akanitazama kwa macho ya dharau huku Victoria akiwa amejichokea, kwani ninaamini mipango yao waliyo kuwa wameipanga dhidi yangu imeharibika.John akamfwata Victoria sehemu alipo simama, wakanong’onezana kwa muda kasha wakamtama Phidaya ambaye muda wote, amejilaza chini huku machozi yakimwagika kwa uchungu.

“Mchukueni huyo Malaya mumrudishe mulipo mtoa”
John aliwaamrisha watu wake, wakamnyanyua Phidaya na kumbeba juu juu, japo anajitahidi kujitoa mikononi mwa watu walio mbeba, huku aikiliita jina langu kwa sauyti ya juu, ila hakuifanikiwa kujitoa mikononi mwao John akapiga hatua hadi katika sehemu nilipo fungwa, akanitazama kwa muda, huku macho yake yakiwa yamejaa dharau kubwa, akanitemea mate ya usoni, akiyasindikiza kwa kofi zito lililo tua kwenye shavu langu la kushoto

“Mmmmmm Eddy, unajisikiaje?”
John alizungumza huku akivifikisha viganja vyake, na kuvipuliza taratibu taratibu.Akanishika sikio langu la upande wakulia, akaanza kulivuta kwa nguvu zake zote, nikaendelea kuugulia maumivu ndani kwa ndani, sikutoa sauti yoyote kwenye kinjwa changu
“Waooo, unajifanya komandoo usikii maumivu eheeee?”
John alizungumza, huku akiliachia sikio langu.Akaanza kunitandika vibao mfululizo kwenye mashavu yangu, hasira ikazidi kumiliki nafisi yangu.

“John, tumpeleke kisimani, hapo unajisumbua bure”
Victori alitoa wazo ambalo John alilikubali, wafanyakazi wao wakanishusha kwenye meza, majamaa wawili wakanibeba kwenye mabega yao. kama wawindaji walio beba swala waliye muua kwenye mawindo yao.

Tukaingia kwenye moja ya ukumbi mkubwa wenye mwanga hafifu, unao pita kwa kutumia madirisha machache yaliyopo juu yake.Wakanibwaga chini, na kunifanya nitoe mguno wa maumivu kutokana na kujiumiza sehemu ya paja langu, nililo pigwa risasi Taa kubwa zenye rangi nyeupe zikawaka na kulifanya eneo zima la ikumbu kuponekana vizuri, kuna mashimo makubwa mawili, kwa haraka nikatabua ndio hivyo visima wanavyo vizungumzia, mabaunsa walio kuwa wamenibeba, wakaufunga mwili wangu kwa kamba ngumu aina ya manila.

“Eddy utakufa kifo kibaya sana”
John alizungumza huku akiwa ameniinamia
“Usiombe nikatoka, kwenye mikono yeno, utajuta”
Nilizungumza kwa kujiamini sana, John akaanza kucheka kwa dharau, huku akinipiga piga mashavuni mwangu
“Eddy huwezi kutoka mikononi mwangu, nakujua wewe vizuri sana.Huwezi fanya chochote dhidi yangu.Muda wako umekwisha kaka”

“Angalia wakwako ndio utakuwa umekwisha”
John akaanza kunipiga mateke mfululizo kwenye mbavu zangu, nikaendelea kutoa sauti ya maumivu ila John hakunionea huruma zaidi ya kuendelea kunipiga kwa nguvu zake zote
“Mchukueni na mukamdumbukize kwenye kisima”
John aliwaamrisha watu wake, wakanibeba, kabla hawajaondoka na mimi, Victoria akawazuia.Akapi ga hatua hadi sehemu tulipo simama

“Eddy nakupenda kaka yangu, kwaheri”
Victoria alizungumza huku akinibusu shavuni mwangu, akawarusuhu watu kuonipeleka kwenye kisima kilichopo kwenye huu ukumbi, kwa jinsi walivyo nifunga kamba mwili wangu sikuweza kufanya kitu cha aina yoyote zaidia ya mwili wangu kunyooka moja kwa moja, mithili ya mtu aliye fariki dunia.

Rais Magufuli Atuma Salamu za Rambirambi Kufuatia vifo vya Watu 11 Ajali ya basi la Barcelona

$
0
0

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amemtumia salamu za rambirambi Mkuu wa Mkoa wa Lindi Bw. Godfrey Zambi kufuatia vifo vya watu 11 vilivyosababishwa na ajali ya basi la kampuni ya Barcelona iliyotokea jana tarehe 17 Oktoba, 2016 katika eneo la Miteja Wilaya ya Kilwa Mkoani Lindi.

Basi hilo lenye namba T 101 CUU lililokuwa likisafiri kutoka Dar es Salaam kwenda Kijiji cha Mahuta katika Wilaya ya Newala Mkoani Lindi, lilipinduka baada ya gurudumu lake la kushoto kupasuka na kusababisha vifo vya watu 10 papo hapo na mwingine 1 kufariki dunia baadaye akiwa anapatiwa matibabu katika hospitali ya Wilaya ya Lindi, huku watu wengine 43 wakiwa wamejeruhiwa.

Katika salamu zake, Rais Magufuli amesema amepokea taarifa za vifo vya watu hao kwa mshituko na huzuni kwa kuwa kwa mara nyingine Taifa limepoteza watu wake na familia zimepoteza wapendwa wao na watu ambao ziliwapenda na kuwategemea.

"Ndugu Mkuu wa Mkoa wa Lindi Bw. Godfrey Zambi naomba unifikishie salamu nyingi za pole kwa wote waliopoteza jamaa na ndugu zao katika ajali hii, kwa hakika nimeguswa sana na vifo hivi na naungana na familia za marehemu wote katika maombolezo na sala" amesema Rais Magufuli.

Dkt. Magufuli amewasihi wote walioguswa na vifo hivyo kuwa na moyo wa subira na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu cha huzuni na majonzi na amewaombea Marehemu wote wapumzishwe mahali pema peponi, Amina.

Pia Rais Magufuli amewaombea majeruhi wote wapone haraka ili waungane na familia zao na kurejea katika shughuli za ujenzi wa Taifa,
 
Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam
18 Oktoba, 2016.

Taarifa Muhimu: Serikali Yatangaza UHAKIKI wa Wanafunzi Wote Walioko Vyuo Vikuu Ambao Wanasoma Shahada

$
0
0

Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia inawatangazia Viongozi wa vyuo vyote vinavyotoa shahada nchini vya umma na vya binafsi kuwa kutakuwa na uhakiki wa ubora wa vyuo hivyo.   

Uhakiki huo utaanza siku ya Jumatano Oktoba 19, 2016, hivyo, vyuo vyote vinatakiwa kutoa ushirikiano kwa timu za wataalamu zitakazofika kwa ajili ya kufanya uhakiki huo.

Aidha, katika ukaguzi wa sifa za wanafunzi wanaoendelea na masomo vyuo vyote, Tume ya Vyuo Vikuu nchini (TCU), itatoa majina ya wanafunzi wanaotambuliwa na kwamba walidahiliwa kupitia TCU katika Programu zao za Shahada katika vyuo mbalimbali vinavyotoa shahada nchini siku ya Jumanne Oktoba 18, 2016.

Hivyo, wanafunzi wote wanatakiwa kuangalia majina yao katika Tovuti ya TCU na kwa yeyote ambaye hataona jina lake awasiliane na Uongozi wa TCU haraka iwezekanavyo ili kupata maelezo Zaidi. Mwanafunzi ambaye hatazingatia haya ndani ya wiki mbili atapoteza sifa za kuendelea na masomo.

Imetolewa na:

Katibu Mkuu
Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatano ya Octoba 19

Wizara ya Mambo ya Nje yakanusha Tanzania kujitoa katika matumizi ya Viza ya Pamoja ya Utalii katika Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.

$
0
0


Mchakato wa kuanzisha Viza ya Pamoja ya Utalii katika Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Ndugu wanahabari:
Wiki iliyopita baadhi ya vyombo vya habari na mitandao ya jamii ya hapa nchini na nje ya nchi iliandika taarifa kuhusu Tanzania kujitoa au kugomea utaratibu wa visa ya pamoja ya utalii (Single Tourist Visa) wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Kufuatia taarifa hiyo, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki imekuwa ikipokea simu nyingi kutoka kwa watu mbalimbali wakiwemo waandishi wa habari kutaka kufahamu ukweli wa jambo hilo. 


Hivyo, Wizara imeona itoe taarifa rasmi kufafanua namna ya mchakato wa uanzishwaji wa viza ya pamoja ya utalii ndani ya nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki unavyoendelea.

Suala la Uanzishwaji wa Viza ya Pamoja ya Utalii kwa Nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki bado liko katika majadiliano ya Nchi Wanachama kupitia Vikao vya Sekta ya Utalii na Wanyamapori. 

Katika kufanikisha azma hii,  Baraza la Kisekta la Mawaziri wa  Maliasili na Usimamizi wa Wanyamapori uliofanyika  tarehe 1 Novemba 2008 liliunda Kikosi Kazi kwa ajili ya kufanya  utafiti kwa lengo la kubainisha mahitaji na utayari wa Nchi wanachama juu ya kuanzisha  Viza ya Pamoja ya Utalii.  Utafiti uliofanyika mwaka 2010, ulibainisha masuala muhimu yafuatayo ya kuzingatiwa kabla ya kuanzishwa kwa Viza ya Pamoja ya Utalii:

a)Kurazinisha  (harmonization) sheria za Viza za Nchi Wanachama;
b)Idara ya Uhamiaji  kuanzisha Mfumo  wa  kudhibiti Usalama;
c)Utoaji wa Viza kuwa wa kielektroniki;
d)Kuwepo kwa mfumo wa ukusanyaji na ugawanyaji wa mapato pamoja na namna ya kulipa;
e)Kuwepo kwa maafisa uhamiaji katika kila ofisi za ubalozi;
f)Kujenga uwezo wa watumishi kwenye suala la  mfumo wa kieletroniki  wa utoaji wa viza ya pamoja ya Utalii.

Kufuatia matokeo ya utafiti huo, Mkutano wa 5 wa Baraza  la Kisekta la Mawaziri wa Utalii na Usimamizi wa Wanyamapori  uliofanyika  mwezi Julai 2013  jijini Bujumbura, Burundi pamoja na mambo mengine uliagiza kuundwa kwa kikosi kazi ambacho kitajumuisha wataalamu kutoka Taasisi za Uhamiaji, Utalii, Fedha, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Tehama, Usalama, na Sheria katika nchi wanachama ili  kuandaa mpango kazi  na  kushughulikia masuala yote ambayo  yatajitokeza kuhusiana  na uanzishwaji wa  Viza ya Pamoja ya Utalii. Hata hivyo, kabla ya utekelezaji wa maagizo hayo, Nchi za Uganda, Kenya na Rwanda zilianzisha  Viza ya Pamoja ya Utalii baina yao nje ya vikao vya Jumuiya.

Ni vema ikaeleweka kwa umma wa Watanzania na Afrika Mashariki kwa Ujumla kuwa kwa kuzingatia Mfumo wa Maamuzi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, ambao ni wa kukubaliana kwa pamoja (consensus) hakuna Mfumo wowote wa uanzishwaji wa Visa ya Pamoja ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ulioanzishwa.
 
Hii inamaanisha kuwa hakuna Visa ya Pamoja ya Utalii katika Jumuiya ya Afrika Mashariki iliyokubalika. Kwa mantiki hiyo, taarifa zilizotolewa na vyombo vya habari hazina ukweli wowote na zilikuwa na lengo la kuichafua Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayoongozwa na Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli.

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inawawahakikishia umma wa Tanzania kuwa itaendelea kuheshimu maamuzi ya vikao halali vya Jumuiya na kushiriki katika majadiliano ya kuanzisha visa ya pamoja ya utalii ndani ya Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki
Dar es Salaam, 18 Oktoba  2016.

Majaliwa: Waharibifu Wa Mazingira Wakamatwe

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameuagiza uongozi wa mkoa wa Lindi kuhakikisha wanawakamata na kuwachukulia hatua watu wote wanaoharibu mazingira kwa kufyeka na kuchoma moto misitu kwa sababu wanaharibu mazingira na kusababisha ukame.

Amesema mkoa huo upo hatarini kugeuka jangwa na tayari vyanzo vingi vya maji vimeanza kukauka kwa sababu ya uharibifu wa mazingira unaotokana na watu kufanya shughuli za kijamii kwenye vyanzo vya maji.

Waziri Mkuu ametoa agizo hilo jana Jumanne, Oktoba 18, 2016 wakati akizungumza kwa nyakati tofauti na wananchi wa wilaya ya Ruangwa katika mikutano iliyofanyika kwenye vijiji vya Nanjaru, Nachinyimba, Nambiranje, Mkaranga, Nandenje, Nachinyimba na Mandarawe.

Alisema wakulima wa ufuta wanatakiwa kuendelea kutumia mashamba yao ya zamani na kuacha tabia ya kufyeka misitu kila mwaka na badala yake waanzishe mpango wa upandaji miti ili kuepusha taifa kugeuka kuwa jangwa.

“Vyanzo vya maji vimekauka kwa sababu tumekata miti mingi. Mito yote iliyokuwa inatiririsha maji imekauka. Viongozi wa mkoa hakikisheni misitu inalindwa na atakayekutwa analima kwenye vyanzo vya maji akamatwe,” alisema.

Waziri mkuu aliongeza kuwa “Ukataji miti huu unaoendelea katika maeneo yetu  hakutosababisha kukosekana kwa maji tu, bali  hata mazao yatapungua. Jambo hili  itasababisha njaa katika vijiji vyetu, hivyo tuache kukata miti.

Waziri Mkuu alisema kwa sasa Serikari inatumia gharama kubwa kuchimba visima virefu kutafuta maji. Amesema zamani walikuwa wanachimba mita 20 au 30 wanakuta maji na gharama yake ilikuwa sh. milioni 35, ambako kwa sasa wanalazimika kuchimba mita zaidi ya 150 kwa gharama y ash milioni 75 kwa kisima kimoja.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Bw. Godfrey Zambi,aliwataka watendaji wa kata na vijiji kuimalisha ulinzi wa maeneo ya misitu na maji, na atakayeshindwa atachukuliwa hatua kali za kisheria.

“Hatuko tayari kutengeneza jangwa hivyo tutapamba na wale wote wenye tabia za kuchoma moto misitu au kulima kwenye vyanzo vya maji,” alisema.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
JUMNNE, OKTOBA 18, 2016

Mwigulu Nchemba Afafanua kuhusu tuhuma za kughushi vyeti vya kitaaluma na kutumia jina la mtu mwingine.

$
0
0
Wakati Serikali ikitangaza msako kwa watu walioghushi vyeti na kutumia majina ya watu wengine, Waziri wa mambo ya ndani ya Nchi, Mwigilu Nchemba, ameibuka na kutoa ufafanuzi wa utata wa majina yake.

Hatua hiyo imekuja baada ya kuibuka kwa mjadala wa usahihi wa majina yake pamoja na kuhusishwa kughushi vyeti ya elimu.

Katika andiko lake aliloliweka jana katika mitandao ya kijamii ambalo baadaye lilithibitishwa na mmoja wa wasaidizi wake, Mwigulu alisema watu wanaoandika historia yake hawamjui kwani uhalisia alikuwa akiitwa Lameck Madelu Mkumbo, sasa Lameck si jina la Kinyiramba na Madelu si jina halisi la baba yake bali la utani.

“Ni vema kuweka rekodi sawa, kwanza anasema (aliyeandika) nilikuwa naitwa Lameck Madelu Mkumbo, sasa moja Lameck sio jina la kinyiramba, na Madelu sio jina halisi la baba bali ni utani kuwa ana ndevu nyingi, yaani ni mandevu. Ndiyo maana hata kwenye ubunge nililiongeza tu kama a.k.a ili watu, hasa wazee wanifahamu, hili haliko kwenye vyeti.

“Hili la Lameck siyo jina la Kinyiramba ni jina la daktari aliyenipokea zahanati iliyopo Kijiji cha Mukulu, daktari tunaita hivyo, lakini ni nesi ndiye aliyekuwa anaitwa Mwigulu na jina la kizungu Lameck.

“Mimi nilipelekwa hospitali nikiitwa Mugulo na jina la ukoo kwa watoto wote wa kiume ni Shumbi, ambalo hata hivyo wanatumia wazee tu, wanaojua Kinyiramba hilo ndio jina la Kinyiramba,” alisema Mwigulu na kuongeza:

“Mama yangu aliulizwa jina akanitaja kwa muuguzi (nesi) akamwambia mama unamwitaje jina hilo hakuna lingine, mama akamwambia hakuna labda mtaje wewe, basi jamaa akajitaja,” alisema.

Alisema suala hilo ni jambo la kawadai hasa kwa kijijini kwani familia inakuwa na watoto wengi hadi majina inakuwa si jambo la kujali.

“Hata pale kijijini kuna wengine waliotajwa majina ya waganga wa kienyeji wazee walikopewa dawa, majina ya manesi, matabibu kama mimi, majina ya walimu,” alisema.

Akizungumzia maisha yake ya elimu, alisema aliacha shule kwa mara ya kwanza mwaka 1984 baada ya kuanza na kaka yake aliyemtaja kwa jina la Jugulu.

Mbunge  huyo wa Iramba alisema kutokana na hali hiyo, baba yao aliwataka wapeane zamu ya kwenda shule hali iliyomfanya aache shule.

“Mwaka 1985, nikaachia darasa la tano nikaenda kuchunga miaka kama miwili. Nikarudi tena baada ya mifugo kuanza kufa sana, mzee akashauriwa awekeze kwenye elimu. Walimu walikuwa wanashinda nyumbani kumsihi anirudishe shule, ndiyo nikarudi na nikachukua majina ya daktari.

“Mtu asichanganye kuona ni udanganyifu, mimi sijachukua vyeti vya mtu. Nimefanya mitihani tena kwa kupiga na picha za passport ili mtu asitumie haki ya mtu mwingine aliyefaulu na mpaka sasa naona ni struggle (kupambana) za mfano, kuwa nilisoma kwa mazingira ya kutoka kuchunga na kurudishwa shule na kufaulu mwenyewe,” alisema Mwigulu.

Waziri huyo alisema kwa anayetaka kuthibitisha maelezo aliyotoa, anaweza kuwauliza aliosoma nao shule ya msingi.

“Comrades kwa mawazo yangu kosa ni mtu kuchukua nafasi ya mtu aliyefaulu na kwenda yeye, hapo ni kuiba haki ya mtu. Najua hii ilikuwa ikitokea baadhi ya maeneo, mtu anafaulu ila anakuwa hataki kwenda shule au amefariki then anakwenda mwingine. Mimi sijawahi chukua nafasi ya mtu.

“Halafu watu wanasema jina la mtu, labda kama wanamaanisha tofauti na wizi wa jina kwani kila mmoja hapo alipo ana jina la mtu, yaani atakuwa John wa Biblia, Mohamed wa Quran, litakuwa la babu, bibi la mganga, daktari, rafiki, kiongozi au hata la tukio.

“Nijuavyo jina unakula kiapo tu kama sio la kwako kisheria na unatumia, na hata sasa nikitamani jina jipya nakula kiapo na kutangaza katika Gazeti la Serikali na lisipopingwa ndiyo linakuwa jina langu jipya.

“Hoja ni kama mtu kapora cheti cha mtu, kapora nafasi ya mtu mwingine aliyefaulu akaenda kuisomea yeye. But, things do change pia kutokana na nyakati na mazingira,” alisema Mwigulu.

Panya Road Apewa Kipigo Kizito na Wananchi .....Azinduka Akiwa Mochwari

$
0
0

Mtoto Isack Ernest (16) anayetuhumiwa kuwa ni mhalifu, maarufu Panya Road, amezinduka akiwa chumba cha kuhifadhia maiti (mochwari) katika Hospitali ya Temeke, Dar es Salaam.

Isack ni miongoni mwa vijana watano waliopigwa na wananchi wenye hasira kwa madai ya kuiba mali zao hali iliyosabisha apoteze fahamu na kudhaniwa amefariki dunia.

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Kamanda wa Polisi Mkoa wa kipolisi Temeke, Kamishna Msaidizi Mwandamizi, Gilles Muroto, alisema baada ya polisi kupigiwa simu na raia wema kuwa kuna vijana watatu wamefariki dunia, walikwenda eneo la tukio na kuwakuta wakiwa na hali mbaya.

“Mmoja wao anayeitwa Kelvin Nyambocha (14) alifariki dunia baada ya kupigwa na kuchomwa moto na wananchi.
 
“Kabla ya kufariki, Kelvin alifuatana na wenzake kwa lengo la kwenda kuangalia tamasha la kuibua vipaji vya muziki wa singeli lililoandaliwa na Radio Clouds Fm lililofanyika Mbagala Zakhem,” alisema Kamishna Muroto.

Alisema wakati wanarudi nyumbani, kundi la vijana hao wanaojiita Panya Road waliokuwa na silaha za jadi (mapanga), waliwavamia watembea kwa miguu na kuwaibia mali zao na ndipo wananchi walipofanikiwa kuwakamata watano. 

Alisema Isack alipigwa hadi akazimia kiasi ambacho walijua amefariki dunia na ndipo alipopelekwa chumba cha kuhifadhia maiti na kufanyiwa taratibu zote, ikiwa ni pamoja na kuvuliwa nguo na kuwekewa namba tayari kwa kuingizwa kwenye jokofu.

“Wakati amewekwa chini kwa ajili ya kuingizwa kwenye jokofu, alizinduka kwa kupumua na kuonekana bado yupo hai, hali iliyosababisha kupelekwa chumba cha uangalizi maalumu (ICU),” alisema Kamishna Muroto.

Alisema baada ya kupata fahamu na afya yake kutengemaa, alihojiwa na Jeshi la Polisi, akawataja wenzake 10 waliokuwa kikundi kimoja. Vijana hao ni Menso Somba (16), Adam Jumanne (16), Bakari Amir (14), Ally Said (17), Abdillah Yusuf (16), Brown Mathias (15), Jafari Salum (13), Hamisi Mwanda (16), Siraji Hamisi (16) na Jeremia Gaudence (13).

Wakati vijana hao wakipewa mapanga yao mbele ya ofisi ya Kamanda wa Polisi wa Temeke huku wazazi wao wakishuhudia, walianza kuyagombea wengine wakidai kuwa yao yamebadilishwa na kupewa wenzao.

Kamishna Muroto alisema kikundi hicho kina bendera inayoonyesha michoro mbalimbali ikiwamo askari mwenye silaha anakimbia huku anatiririka damu, mtu ameanguka chini akiwa amekatwa mkono, nyumba na vijana wawili wakiwa wameshika panga.

Alisema kundi hilo la vijana ambalo linazunguka maeneo mbalimbali, limekuwa likijiita ‘Taifa Jipya’.

Kamishna Muroto alisema kijana mwingine, Faraji Suleiman (19) ambaye pia hali yake ni mbaya, amelazwa Hopitali ya Taifa Muhimbili (MNH) kwa matibabu zaidi.

Kamanda Muroto alisema vijana wawili aliowataja kuwa Hamisi Mponda (18) na Abdallah Omari (15) walitibiwa hospitali ya Temeke na kuruhusiwa.

Alisema jeshi hilo kupitia Sheria ya Watoto ya mwaka 2009 kifungu 7-9, linakusudia kuwafikisha mahakamani wazazi wa watoto 16 ambao walitajwa na kuthibitisha kufanya uhalifu huo, kwa kushindwa kuwaangalia watoto wao.

Kamishna Muroto alisema wazazi wana wajibu wa kuhakikisha mtoto anakuwa chini ya uangalizi ambao hauwezi kumsababishia madhara ya kimwili na kisaikolojia.

“Hii ina maana kila mzazi ahakikishe mtoto wake ana ulinzi, yuko salama muda wote dhidi ya udhalilishaji na hatari zote ili watoto hawa wakue vizuri,” alisema Kamishna Muroto.

Alisema jukumu la mzazi ni kuhakikisha mtoto anakuwa kwenye malezi bora na si kumwacha akilelewa na walimwengu.

“Mzazi atakayeshindwa kumsimamia vyema mtoto wake na kukiuka sheria ya mtoto ya mwaka 2009 katika kifungu cha 14, atafikishwa mahakamani na akitiwa hatiani atafungwa miezi 6 au kulipa faini ya Sh milioni 5,” alisema Kamanda Muroto.

Alisema kutokana na mazingira waliyokutwa watoto hao, wazazi wao wanatuhumiwa kwa kukiuka sheria hiyo ya watoto.

Akisimulia mkasa huo, Isack Ernest alisema yeye ni mwanafunzi wa kidato cha tatu katika Shule ya Sekondari Lumo na hajawahi kufanya vitendo vya kihalifu.

Alisema wakati yupo kwao, wenzake walimfuata na kumwambia waende kwenye tamasha la singeli Mbagala.
 
“Tulienda na baada ya kumaliza tamasha, wenzangu wakasema twende tukale (walimaanisha wakapore), mimi nikajibu sina pesa, ndipo waliposema wakienda kula hawatanigawia kwa kuwa aliyekula kala, ndipo walipokwenda kuvamia watembea kwa miguu na kuiba.

“Wakati nikiwa ng’ambo ya pili, nikasikia sauti ya watu wanasema mwizi mwizi, mwizi,” alisema Isack.
 
Alisema baada ya kupigiwa kelele za wezi, walikimbia na kumfuata alipo ndipo kipigo kilipomwangukia yeye hadi kupoteza fahamu.

“Nilikuja kushtuka nipo ICU, huku nikiwa sijui niko wapi, nimekoma kujihusisha na makundi kwa sababu sijawahi kuiba katika maisha yangu,” alisema Isack.

Baba mzazi wa kijana huyo, Ernest Chalo, alisema mtoto wake alimuaga anakwenda kuangalia mpira Mbagala Oktoba 15, mwaka huu.

Alisema wakati yeye anafuatilia mchezo wa timu ya Simba na Kagera Sugar, alipigiwa simu na mtu asiyemfahamu akimpa taarifa ya kuwa mtoto wake amefariki dunia.
“Kiukweli nilichanganyikiwa kwa sababu nimetoka kumzika mke wangu wiki moja iliyopita, tena napokea taarifa ya mtoto kufariki, nilitoka mpaka kwa mwenyekiti wangu wa mtaa na kumpa taarifa, nikachukua usafiri wa pikipiki kwenda Hospitali ya Temeke,” alisema Chalo.

Alisema alipofika hospitalini hapo, aliambiwa mtoto wake yupo chumba cha kuhifadhia maiti, lakini alipoletewa mwili kuutambua haukuwa wa mtoto wake, ndipo akatokea msamaria mwema akamwambia mtoto wake alizinduka.

“Kutokana na baridi kali ya chumba cha kuhifadhia maiti, mtoto wangu alipoingizwa mle ndani alipumua na hivyo kuhamishiwa ICU,” alisema Chalo.

Godbless Lema, Mkuu wa Mkoa Arusha Watibuana Mbele ya Wafadhili

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo, jana alikuwa katika wakati mgumu baada ya  kuzomewa na wananchi wakati wa uzinduzi wa Hospitali ya Mama na Mtoto   mjini Arusha.

Tukio hilo lilitokea wakati kiongozi huyo alipozungumzia mradi wa ujenzi wa hospitali hiyo na kudaiwa kupotosha ukweli wa mradi huo.

Katika maelezo yake, Gambo alisema eneo la hospitali hiyo lilitolewa na familia ya Nyaga Mawalla, jambo ambalo   wananchi walilipinga wakishirikiana na Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema (Chadema).

Hospitali hiyo itakayogharimu Sh bilioni tisa, inajengwa kwa wafadhili ambao ni Taasisi ya Maternity Afrika, Taasisi ya Maendeleo Arusha (ArDF)  na Mbunge   Lema.

Kabla mkuu huyo wa mkoa hajazomewa, alipewa nafasi ya kuzungumza na ndipo alipoeleza jinsi familia ya Mawalla ilivyotoa eneo hilo.

Wakati akitoa kauli hiyo, Lema ambaye alikuwapo mahali hapo, alisimama na kupaza sauti akisema, “mkuu wa mkoa anapotosha ukweli wa mradi huu”.

Hatua hiyo ya Lema  kulalamika kwa sauti, iliwafanya wananchi nao  kumzoea Gambo huku baadhi yao wakimtuhumu kuingiza siasa katika shughuli za maendeleo.

Kutokana na zomeazomea hiyo,  polisi waliokuwapo mahali hapo  wakiwa na silaha za moto na mabomu ya machozi, walilazimika kusogea eneo la meza kuu huku wengine wakimzunguka Gambo aliyekuwa akiendelea kubishana na Lema kuhusu ukweli wa mradi wa hospitali hiyo.

“Huyoo, acha kupotosha ukweli wewee, usilete siasa kwenye maendeleo, huyooooo,” zilisikika sauti za wananchi kutoka upande wa pili wa meza kuu huku Lema naye akisikika akihoji kwa nini mkuu huyo wa mkoa alikuwa akisema uongo.

Katika hotuba yake ambayo pia ilikatishwa baada ya kutokea kelele hizo, Gambo aliishukuru familia ya marehemu Mawalla kwa kile alichosema ilitoa eneo hilo na kuwatafuta wafadhili wa kujenga hospitali hiyo.

“Hili wazo lilikuwa ni la familia ya Mawalla kwa sababu  ardhi ni mali yao na walikuwa na maono ya kujenga hospitali hii.

“Kwa hiyo, Serikali itakuwa pamoja nanyi bega kwa bega kuhakikisha mnafanikiwa,” alisema Gambo huku akizomewa na wananchi.

Wafadhili kutoka Ulaya waliokuwa kwenye uzinduzi huo, walijikusanya makundi na kumkumbatia Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Maternity Afrika, Andrew Brown, wakimpa pole kwa kile kilichotokea.

Hata hivyo, baadhi ya wafadhili hao walianza kulia wakionyesha ni kwa kiasi gani hawakuridhishwa na mvutano kati ya mkuu wa mkoa, mbunge na wananchi.

Akizungumza na waandishi wa habari baada ya uzinduzi huo, Lema alisema mkuu huyo wa mkoa alifanya makosa kuupotosha umma kuhusu mradi huo.
“Mkuu wa mkoa alitakiwa kufika saa 4.00 asubuhi lakini hakuonekana kwa madai kwamba asingeweza kuja kama mimi nipo.

“Ilipofika saa saba kasoro bila kumuona, nikampigia simu Katibu Mkuu Kiongozi, John Kijazi kumweleza suala hili, naye akampigia simu Katibu Mkuu Tamisemi.

“Inavyoonekana Tamisemi walimpigia simu mkuu wa mkoa ndipo akaamua kuja akiwa amechelewa.

“Kwa hiyo, kilichofanyika hapa kinaonyesha aina ya viongozi walioaminiwa na Rais John Magufuli wamsaidie kuongoza nchi.

“Wafadhili walimualika kuipa heshima Serikali, lakini hakuonekana hadi alipopewa maagizo.

“Kwa faida ya wasiofahamu ni kwamba mimi kupitia ArDF ndiyo tuliotafuta ardhi kwa marehemu Nyanga Mawalla.

“Kibaya zaidi, alipofika hapa akaagiza ratiba ibadilishwe mimi nisizungumze kwa sababu anazozijua yeye.

“Ushahidi wa ratiba hiyo ni kwamba, ilipangwa azungumze mtendaji mkuu wa Maternity Afrika, kisha mkurugenzi wa ArDF, baadaye mimi mbunge pamoja na Mawalla kutoa historia ya mradi na mwisho mkuu wa mkoa.

“Lakini, ratiba hiyo haikufuatwa na badala yake alifanya anavyojua yeye  mradi tu nisizungumze.

“Sasa, hivi unawezaje kuwalazimisha  Maternity Afrika wasinilete mimi wakati kwenye mkataba wa hili eneo mimi na ArDF ndiyo wasimamizi wa mradi?” alihoji Lema.

Mwenyekiti wa ArDF, Elifuraha Mtoi, alisema Taasisi ya ArDF kwa kushirikiana na Lema ndiyo waliofanikisha mradi huo.

“Hizi ni jitihada binafsi za ArDF kwa sababu  baada ya kupata wafadhili, tuliwaunganisha na Mawalla Trust ambao ndiyo wamiliki wa maeneo haya.

“Kwa hiyo, kilichofanywa na mkuu wa mkoa kimetufedhehesha mbele ya wafadhili,” alisema Mtoi.

Awali, Mtendaji Mkuu wa Maternity Afrika (Brown), alisema fedha za ujenzi wa hospitali hiyo zitatokana na michango mbalimbali ya wafadhili na sadaka kutoka makanisani.

Mwenyekiti wa Chadema Mkoa wa Arusha, Amani Golugwa ambaye pia ni mmoja wa waaanzilishi wa Taasisi ya ArDF, alimtangaza Gambo kama adui wa maendeleo mkoani Arusha.

NMB Kuendelea Kusherehekea Huduma Kwa Mteja Kwa Mwezi Mzima

$
0
0
Wiki ya kwanza ya mwezi Oktoba hujulikana kama wiki ya huduma kwa mteja na huadhimishwa duniani kote. Benki ya NMB imeamua kuendelea kusherehekea huduma kwa mteja kwa mwezi mzima ili kuonyesha jinsi inavyomjali mteja kibiashara, kimaendeleo pamoja na amani kwa ujumla. NMB imejikita kwenye kutoa huduma bora zinazofikia malengo ya wateja wa ndani na nje.
 
Kutana na Meneja Mwandamizi  wa huduma kwa wateja wa NMB, Amanda Feruzi anayetuelezea maoni binafsi na ya kampuni kuhusu huduma kwa mteja na kwanini ni muhimu kuadhimisha huduma kwa mteja.

Mimi: Karibu sana Amanda, tuanze kwa kufahamu jukumu lako ni nini?
Amanda: Jukumu langu ni kutengeneza, kuratibu, kufuatilia na kupima ubora wa huduma kwenye benki

Mimi: Huduma kwa mteja inamaanisha nini kwako na kwenye benki kwa ujumla?
Amanda: Binafsi, naamini kwamba huduma kwa mteja ni kuwaheshimu na kuwajali wateja kwa kutumia weledi kufanikisha mahitaji yao. Kama shirika – huduma kwa wateja ni jambo la msingi sana hapa NMB na ndio maana kila siku tunaboresha huduma na bidhaa zetu ili kufanikisha malendo ya wateja wetu.

Mimi: Kwanini ni muhimu kuwa na wiki ya huduma kwa mteja?
Amanda: Wateja wetu (wa ndani na nje) ndiyo sababu ya sisi kuwa na mafanikio. Kwahiyo, tunasherehekea mchango wao na kuwaahidi kwamba TUNAWAJALI kwa kuwa sehemu ya mafanikio yetu.

Mimi: Ni kitu gani cha muhimu sana cha kufuata unapokuwa unamhudumia mteja?
Amanda: Kitu cha msingi sana wakati wa kumhudumia mteja ni kuhakikisha mahitaji na matarajio yake yanafikiwa. Inapotokea kwamba kwa namna moja au nyingine hatujafikia matarajio ya mteja wetu, tunachukua mrejesho na kulifanyia kazi suala hilo.

Mimi: Msemo wa “mteja ni mfalme” una ukweli kiasi gani?
Amanda: Tunaposema mteja ni mfalme, tunarudi palepale kwenye kutilia msisitizo wa kusherehekea wiki ya huduma kwa mteja. Mteja ni mfalme kwa sababu ndiye sababu ya sisi kufanikiwa na kuongeza jitihada ili kufanikisha malengo yake. Mteja anahitaji huduma bora kwenye pesa zake hivyo, ni wajibu wetu kumsikiliza kwa makini, kumwelewa na kufanikisha mahitaji yake.

Mimi: Kama huduma kwa mteja ingekuwa ni mnyama, unafikiri angekuwa ni mnyama gani na kwanini?
Amanda: Hilo ni swali zuri lakini gumu pia. Mi nafikiri ningefananisha wiki ya mteja na tembo. Tembo ni wapole na viongozi wasiotumia mabavu. Hiyo ndio sababu tembo wenzao huwaheshimu kutokana na uwezo wao wa kutatua matatizo. Hiyo ni sawa na hhuduma kwa mteja.

Mimi: Ahsante sana kwa kuzungumza nasi kuhusu huduma kwa mteja na namna mlivyojipanga kuhakikisha kwamba mnatimiza matarajio ya wateja wenu.
Amanda: Shukrani sana.

Zitto Atoa Neno Ugomvi wa RC Arusha na Godbless Lema

$
0
0
Jana October  18 2016 kulifanyika hafla ya uwekaji wa jiwe la msingi katika hospitali ya mama na mtoto inayojengwa eneo ya Burka nje kidogo ya jiji la Arusha, lakini shughuli hiyo ilisimama baada  mbunge wa jimbo la Arusha mjini Godbless Lema kusimama kupinga maelezo yaliyokuwa yakitolewa na mkuu wa mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo.

Maelezo ya RC Gambo yalisema kwamba eneo la mradi ule limetokana na maono aliyokuwa nayo Marehemu Advocate Nyaga Mawala, maelezo ambayo mbunge Lema alikuwa akiyapinga na kudai yeye amehusika kutafuta ardhi na wafadhili, Lema alidai maelezo hayo yamejaa upotoshwaji na siasa ndani. Unaweza kuangalia video hii hapa chini.

Leo October 19 2016, mbunge wa kigoma mjini na kiongozi mkuu wa chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe kupitia ukurasa wake wa facebook ametoa ushauri kwa RC Gambo na Mbunge Lema, Zitto amesema…..…

"Nakasirishwa sana kuona viongozi vijana wanafanya mambo ya hovyo. Mkuu wa mkoa wa Arusha mdogo wangu Mrisho Gambo una dhamana zaidi Kwa vijana. Mnapofanya mambo ya kijinga mnaharibu nafasi ya vijana kuaminiwa zaidi. 

"Kaa Na Mbunge Godbless Lema mnywe kahawa pale New Arusha Na muanze upya. Ndugu yangu Lema nashauri punguza munkari. Juhudi zako Arusha haziwezi kufutika kirahisi. 

"Nakushauri kaa chini Na Mkuu wa Mkoa wako mpige mstari muanze Kazi upya Kwa pamoja. Viongozi jiepusheni kuonyesha hasira zenu hadharani. Sio hekima."-Zitto Kabwe

Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais IKULU Asema Taarifa Hii Inayosambazwa Mitandaoni ni ya UONGO, Ipuuzwe

$
0
0

Hii  Taarifa (katika picha)  inasambazwa  mitandaoni  kwamba  Imetoka  IKULU. Mkurugenzi  wa  Mawasiliano ya  Rais ,Gerson Msigwa  kasema  ni  ya  uongo, imetengenezwa  na  watu  wenye  nia  ovu  hivyo  ipuuzwe

Scorpion afunguliwa mashtaka upya

$
0
0

Mahakama ya Wilaya ya Ilala, imemfungulia mashtaka mapya Salum Njwete (Scorpion).Amefunguliwa mashtaka mengine yanayofanana na ya awali ya unyang’anyanyi wa kutumia silaha.

Hata hivyo Njwete amekana shtaka na kurudishwa rumande,huku Hakimu Flora Haule anayesimamia kesi hiyo akizuia dhamana.

Awali Mahakama hiyo ilimfutia mashtaka yanayomkabili Scorpion baada ya upande wa mashtaka kuomba shtaka hilo liondolewe mahakamani kwa sababu hawana nia ya kuendelea na kesi hiyo na kutokana na maombi hayo, Hakimu Adelf Sachore alikubaliana na ombi hilo kwa kuzingatia kifungu namba 91 kifungu kidogo cha kwanza cha sheria ambacho kinampa Mamlaka Mkurugenzi Wa Mashtaka nchini (DPP) kuondoa shtaka mahakamani muda wowote ili mradi kama kesi hiyo haijatolewa hukumu.

Njwete anakabiliwa na shtaka la unyang'anyi wa kutumia silaha na kumjeruhi Saidi Mrisho.

BAVICHA: Nini hatma ya Vijana waliokosa mikopo ya Elimu ya Juu?

$
0
0
Baraza la Vijana wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) tumepokea kwa mshtuko mkubwa taarifa kuwa utawala huu wa Serikali ya CCM, chini ya Rais John Magufuli zaidi ya nusu ya wanafunzi waliodahiliwa kwa ajili ya masomo ya elimu ya juu mwaka wa masomo 2016/2017, wako katika hatari ya kukosa fursa ya kupata elimu hiyo kwa sababu ambazo hazieleweki hadi sasa.

Kwa mujibu wa taarifa za vyombo vya habari na vyanzo vingine, Tume ya Vyuo Vikuu Nchini (TCU) imeweza kudahili takriban wanafunzi wapya 58,000 kwa ajili ya elimu ya juu katika vyuo vikuu mbalimbali nchini kwa mwaka huu wa masomo.

Lakini katika hali ambayo tunajua itaumiza vijana wengi na kuwasikitisha Watanzania, taarifa ambazo zimethibitishwa na Serikali ya Rais Magufuli kupitia kwa Mkurugenzi wa Bodi ya Mikopo, ni kwamba zaidi ya nusu ya idadi hiyo ya waliodahiliwa na TCU kusoma elimu ya juu, hawatapata mikopo!

Hivyo ndoto za kutafuta mafanikio yao, kwa ajili ya jamii zao na taifa letu kwa ujumla zinaelekea kukatiliwa. Hili ni jambo kubwa na zito kwa sababu linagusa moja ya misingi muhimu ya taifa lolote lenye ndoto ya kutaka kuendelea, achilia mbali kuwa taifa lenye uchumi wa kati unaotegemea viwanda.

Kwa mujibu wa Gazeti la The Guardian la Oktoba 18, mwaka huu, Serikali ya CCM, chini ya Rais Magufuli imesema itawakopesha wanafunzi wapatao 24,000, idadi ambayo haifiki hata nusu ya wanafunzi wote waliodahiliwa na TCU.

Hata hivyo kauli hiyo ya Mkurugenzi wa Bodi, tumeichukulia kuwa si ya kweli hata kidogo, bali ya mtu anayejaribu kuficha mambo kwa ajili ya “nusu shari kuliko shari kamili”.

Tunasema hivyo kwa sababu hadi sasa Bodi hiyo hiyo, imeshatoa mikopo kwa wanafunzi 3,966 tu. Idadi hiyo ni sawa na asilimia 6 tu kati ya wanafunzi wote waliopata udahili wa kusoma elimu ya juu kwa mwaka huu.

Maana yake ni kwamba kuwakopesha vijana wapatao 24,000 ili wasome elimu ya juu bado nayo ni ahadi tu ya maneno, lakini uhalisia uliopo kwa vitendo hadi sasa ni kwamba Serikali ina uwezo wa kuwakopesha vijana wake 3,966 pekee nchi nzima.

Idadi hiyo ambayo serikali imeweza kuwakopesha mikopo, haifiki hata nusu ya jumla ya wanafunzi wanaopaswa kudahiliwa na mojawapo ya vyuo vikuu vikubwa nchini, mathalani Chuo Kikuu Dar es Salaam.

WAMEKOPESHWA CHAKULA NA KULALA, SI KUSOMA!
Aidha, kwa muda mrefu sasa, walau tangu kuanza kwa utaratibu wa serikali kuwakopesha wanafunzi kwa ajili ya elimu ya juu, inaeleweka kuwa HESLB imekuwa ikitoa mikopo kwa ajili ya vitu vitatu; ada, malazi na chakula.

Katika hali ambayo inazidi kushangaza na kuibua maswali kuwa kuna jambo kubwa ambalo linafichwa, BAVICHA tunazo taarifa kuwa hata hao wanafunzi asilimia 6 ambao bodi inadai imeshawapatia mkopo, katika vyuo vingi wamepata fedha kwa ajili ya CHAKULA NA KULALA tu.

Hawajalipiwa fedha ya ada (tuition fees hadi sasa).
Kwa mantiki hiyo ni kwamba, Serikali ya CCM, chini ya Rais Magufuli hadi sasa wiki ya tatu tangu vyuo vifunguliwe si tu kwamba imeshindwa kuwakopesha wanafunzi wote wanaostahili kupata mkopo kwa ajili ya elimu ya juu, bali hata imeshindwa hata kulipa fedha za ada kwa wanafunzi ambao tayari imeshawakopesha. Hali hii ikiendelea tutegemee kuona vyuo vikuu na taasisi zingine za elimu ya juu vikifungwa kwa sababu vitakuwa haviwezi kujiendesha.

Taarifa hizi za Bodi ya Mikopo zinapaswa kulishtua taifa letu na kila Mtanzania aone jinsi ambavyo Serikali ya CCM chini ya Rais John Magufuli haijajipanga na wala haijui inachokifanya katika kuhakikisha inatoa elimu bora kwa Vijana wetu.

Lakini pia zinathibitisha kuwa Serikali ya Rais Magufuli iko katika hali mbaya ya kifedha na hivyo inahitaji msaada wa fikra mpya nje ya CCM kuikwamua vinginevyo tujiandae kwa mwendelezo wa janga kubwa zaidi katika sekta ya elimu.

Tunamtaka Rais John Magufuli kujitokeza hadharani, na kuueleza umma wa Watanzania hatma ya Vijana waliokosa mikopo, na kama ahadi zake alizozitoa wakati wa Kampeni zilikuwa ni ulaghai au ghiliba za kutafuta kura?
 
Pia Rais Magufuli anapaswa kuwaeleza watanzania ikiwa ameshindwa utekelezaji wa ahadi zake ikiwemo Elimu bora, au akubali kuwa yeye ni Muongo kwa sababu wakati wa kampeni alisema nanukuu; “ETI NIWE RAIS HALAFU NISIKIE WANACHUO WAMEKOSA AU WAMECHELWESHEWA MIKOPO YAO, WATANIJUA MIMI NI NANI, KITU CHENYEWE KINAITWA MIKOPO HALAFU UNACHELEWESHA” Mwisho wa kunukuu.

Tunawataka Viongozi wa serikali za wanafunzi katika Vyuo Vikuu vyote nchini, kuungana pamoja ili kudai haki ya wanafunzi wenzao, tukitambua kuwa, baadhi ya Viongozi wa shirikisho la serikali za wanafunzi wa elimu ya Juu (TAHILISO) wamekuwa wakitumika kwa ajili ya CCM badala ya maslahi mahsusi ya wanafunzi na hivyo kuidhoofisha taasisi hii muhimu ya wasomi, hivyo umoja wao ni muhimu katika kuipata haki hii.

Tunatoa wito kwa taasisi mbalimbali za kutetea haki za vijana, asasi za vijana pamoja na mtandao wa wanafunzi Tanzania, kujitokeza hadharani na kuwapigania vijana hawa katika kuhakikisha wanapata haki yao ya msingi ya elimu.

Imetolewa leo Jumatano,19.10.2016
Patrobas Katambi
Mwenyekiti wa BAVICHA Taifa

Bodi ya Wadhamini CUF yafungua kesi dhidi ya Jaji Mutungi na Mwanasheria Mkuu wa Serikali

$
0
0
BODI ya Baraza la Wadhamini la Chama cha Wananchi (CUF), imefungua kesi dhidi ya Jaji Francis Mutungi, George Masaju, Profesa Ibrahimu Lipumba na wafuasi 12 waliotimuliwa na chama hicho katika Mahakama Kuu ya Tanzania.

Jaji Mutungi ni Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, Masaju ni Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG) na Prof. Lipumba ni Mwenyekiti wa CUF anayetambuliwa na Msajili wa Vyama vya Siasa.

Bodi hiyo imefungua kesi hiyo ikiwa ni wiki chache baada ya mahakama hiyo kutoa kibali cha kufungua kesi dhidi yao.

Kibali hicho kilitolewa mbele ya Jaji Ama Isario Munisi ambapo alisema, mahakama ilijiridhisha kwamba, maombi ya bodi hiyo yaliyokuwa na hati ya kiapo cha Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad zipo sahihi, hivyo wanapaswa kufungua kesi hiyo ndani ya siku 14.

Hatua ya bodi kukimbilia mahakamani inatokana na kuibuka kwa mgogoro ndani ya chama hicho baada ya Prof. Lipumba kutangaza kujiuzulu nafasi ya Uenyekiti Agosti 6, mwaka jana na Juni mwaka huu, kutangaza kutengua barua yake na kisha kurejea kwenye wadhifa wake.

Bodi hiyo inayowakilishwa na mawakili zaidi ya 10 akiwemo Juma Nassoro, Hashimu Mziray na Twaha Taslima leo wamefanikiwa kufungua kesi iliyopokelewa na kupatiwa namba 23 ya mwaka 2016 chini ya hati ya dharura.

Akizungumza na waandishi wa habari baada ya kufungua kesi hiyo, Wakili Mziray amesema msingi wa kesi yao umejengwa katika hoja kubwa tatu ambazo;

Bodi imeiomba Mahakama Kuu kutengua barua ya Jaji Mutungi ya Septemba 23, mwaka huu iliyotengua uamuzi halali wa CUF, kumfuta uanachama Prof. Lipumba.

Pia bodi inaiomba mahakama hiyo kumzuia Jaji Mutungi kuendelea kufuatilia suala la CUF baada ya kupitishwa kwa uamuzi wa kumfuta uanachama Prof. Lipumba kwa kuwa, suala lake limefanyika kihalali.

Aidha katika hoja ya tatu, wanaiomba mahakama kumzuia rasmi Jaji Mutungi kutoingilia masuala yanayoihusu CUF, badala yake afanye kazi zinazomuhusu kisheria.

Badaa ya kueleza hayo, Wakili Mziray amesema sababu ya kufungua kesi hiyo chini ya hati ya dharura inatokana na hatari iliyopo ndani ya chama hicho.

“Licha ya kuwa kuna mambo yaliyotokea ndani ya chama, lakini kuna sababu ya kufungua kesi chini ya hati ya dharura kutokana na Ofisi Kuu ya chama pale Buguruni imekaliwa na watu ambao sio wanachama,”anasema na kuongeza;

“Lengo la chama ni kudhibiti ofisi zake zote katika hali ya usalama ikiwemo Makao Makuu, kwani Kaimu Katibu Mkuu anahitaji kusimamia kazi na shughuli za chama akiwa huru.”

Mbarara Maharagande, aliyeteuliwa kushika nafasi ya Unaibu Mkurugenzi wa Habari, Uenezi na Mahusiano wa CUF amesema kuwa, chama hicho kinasikitishwa na utendaji kazi wa Jeshi la Polisi kwa kuwalinda na kuwaachia wahalifu wanaoivuruga CUF, badala yake inawakamata wasiohusika.

“Tunashangaa kuona polisi wanaharakisha kuwafikisha mahakamani wafuasi 23 waliokuja kuongeza nguvu ya kukilinda chama wakitokea Zanzibar, huku wakishindwa kuwachukuliwa hatua waliofanya tukio la utekaji ambalo ndio la kwanza kutokea,” anasema.

Maharagande anasema kutokana na hatua hiyo, asubuhi ya leo viongozi wa chama hicho wamekwenda Ofisi za Mkurugenzi wa Mashtaka nchini (DPP), Biswaro Mganga kuulizia hatma ya wafuasi waliohusika na tukio la utekaji iwapo wamechukuliwa hatua.

“Licha ya kufika ofisi hapo tumeshangazwa kuona hata kwenye orodha ya jalada la kesi za leo hakuna majina ya washtakiwa hao, licha ya kuwa wamekamatwa muda mrefu lakini wameshindwa kuchukuliwa hatua,” amesema
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images