Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Alhamisi ya Octoba 20


RC Mrisho Gambo apigiwa simu Rais Magufuli. Soma walichozungumza

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Arusha amesema kuwa Rais Dkt John Pombe Magufuli amempigia simu  na kumwambia kuwa ana imani naye na kuwa hajafikiria kutengua uteuzi wake labda kumpandisha cheo.

Hayo yamesemwa jana na Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari  baada ya taarifa kuhusu Rais kutengua uteuzi wake kusambaa kwenye mitandao ya kijamii.

Mkuu wa mkoa alisema kuwa alipigiwa simu nyingi na watu wengi lakini kabla hajawajibu Rais Magufuli akampigia simu na kumueleza kuwa ana imani naye na kuwa ahakikishe anawatumikia wananchi wa Arusha kwani yeye sio bosi wao bali ni mtumishi wao.

Pia mkuu wa mkoa alieleza kuwa Rais amempa maagizo ya kuhakikisha anasimamia wananchi wa mkoa wa Arusha walipe kodi kwa ajili ya maendeleo ya mkoa huo na nchi kwa ujumla.

Aidha, ili kuthibitisha kuwa ni Rais Magufuli ndiye aliyempigia simu, Rais aliomba kuongea na yeyote aliyekuwa karibu ndipo mkuu wa mkoa akampa mmoja wa waliokuwa katika mkutano huo kuthibitisha kuwa ni Rais Magufuli.

Habari ya kutenguliwa kwa mkuu wa mkoa wa Arusha imekuja ikiwa ni siku moja baada ya kuibuka mvutano mkali kati ya mkuu huyo wa mkoa na Mbunge wa Arusha Mjini Godbless Lema kuhusu mradi wa ujenzi wa hospitali itakayotoa huduma kwa mama na mtoto mkoani humo.

Kamati ya Bunge Yakataa faini ya 500,000/- Kwa Kila Kosa Barabarani

$
0
0
Kamati  ya Bunge ya Katiba, Sheria na Utawala imekataa mapendekezo ya kufanyia marekebisho Sheria ya Leseni za Uchukuzi ya mwaka 1973 yenye lengo la kuongeza kiwango cha adhabu ya faini hadi kufikia asilimia 500 kwa watakaokiuka masharti ya leseni hizo.

Mapendekezo hayo yaliwasilishwa mbele ya kamati hiyo mjini Dodoma jana na Mamlaka ya Usafiri wa Majini na Nchi Kavu (Sumatra).

Baada ya kuyakataa mapendekezo hayo, kamati hiyo imetoa muda wa siku mbili kwa Sumatra kuhakikisha inawasilisha mbele ya kamati hiyo mapendekezo yanayokubalika.

Sumatra inapendekeza kuongeza kiwango cha adhabu ya faini kutoka kati ya Sh 10,000 na Sh 50,000 hadi Sh 200,000 na 500,000 kwa watoa huduma za uchukuzi, watakaokiuka masharti ya leseni zao.

Mwenyekiti wa kamati hiyo, Mohammed Mchengerwa alisema mapendekezo hayo, yatazidi kuwaongezea mzigo Watanzania badala ya kuwasaidia. 

Alisema kiwango hicho cha faini kubwa, kamwe hakitazuia tatizo la ajali za barabarani, zaidi ya kuongeza ukubwa wa tatizo la rushwa.

“Serikali ya Awamu ya Tano imejipanga kuwasaidia wananchi, lakini mapendekezo haya yatazidi kuwaongezea mzigo kwa sababu kiwango cha faini hizi kama kitapitishwa, watoa huduma za uchukuzi watahamishia hasara yao kwa wananchi,” alisisitiza.

Aliitaka mamlaka hiyo, kwenda kuyafanyia kazi tena mapendekezo hayo kwa kuwasiliana na Mwanasheria Mkuu wa Serikali na kuwasilisha viwango vya faini vinavyokubalika. 

Mmoja wa wajumbe wa kamati hiyo, Joseph Mhagama ambaye pia ni mbunge wa Madaba, alisema mapendekezo hayo hayana nyongeza yoyote, itakayoisaidia serikali katika kudhibiti tatizo la ajali barabarani.

“Kwa sasa serikali imeweka nguvu zake katika kupunguza ajali za barabarani, lakini kiwango cha faini hizi hakina uhusiano wowote na jitihada hizi zaidi ya kuiongezea Sumatra mapato na kuwapa mzigo walipa kodi,” alisema.

Akiwasilisha mapendekezo ya mamlaka hiyo mbele ya Kamati hiyo, Mkurugenzi Mkuu wa Sumatra, Gilliard Ngewe alisema mapendekezo ya marekebisho ya sheria hiyo, yamelenga  kuiboresha zaidi sheria hiyo ya leseni za uchukuzi.

Alisema marekebisho hayo, pia yatasaidia mamlaka hizo kuendana na mahitaji ya sasa hasa katika eneo la adhabu ya faini, hali itakayopunguza kiwango kikubwa cha kukiukwa kwa masharti ya leseni hizo za uchukuzi.

Waziri Mkuu Amsimamisha Kazi Mhandisi Wa Maji Lindi

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amemsimamisha kazi Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Lindi (LUWASA), Mhandisi Adam Alexander (pichani mwenye mafaili) kwa kosa la matumizi mabaya ya ofisi pamoja na kushindwa kusimamia ujenzi wa kituo cha kuzalisha maji katika Manispaa ya Lindi.

Waziri Mkuu amemkabidhi Mhandisi huyo kwa Kamanda wa TAKUKURU Mkoa wa Lindi, Bw. Stephen Chami na kumuelekeza afanye uchunguzi zaidi juu ya suala hilo.

Waziri Mkuu ametoa agizo hilo jana Jumatano, Oktoba 19, 2016  wakati alipotembelea mradi wa maji wa Ng'apa ambapo aliagiza nafasi hiyo ikaimiwe na Mkurugenzi Msaidizi wa mamlaka hiyo, Mhandisi Idrisa Sengulo.

"Kamanda wa TAKUKURU fanya mapitio ya kina ya mshahara wake. Yeye anasema analipwa Wizarani, mimi najua analipwa na LUWASA. Angalia kazi aliyokwenda kuifanya Dar es Salaam kama inalingana na siku alizokaa,” alisisitiza Waziri Mkuu.

Mhandisi hiyo anakabiliwa na tuhuma mbalimbali ikiwemo matumizi mabaya ya fedha za ofisi pamoja na kupokea mshahara bila la kulipa kodi ya mapato ya mshahara (PAYE), kujilipa kiwango kikubwa cha posho pamoja na kusafiri kwa muda mrefu.

Waziri Mkuu alisema Serikali haiwezi kuvumilia kuona wananchi wanapata shida huku watendaji waliopewa dhamana ya kuwatumikia hawaonekani kwenye vituo vyao vya kazi. "Huyu nimemuita mimi aje huku, hadi jana alikuwa Dar es Salaam."

Alipoulizwa sababu za kutokuwepo ofisini kwake kwa muda mrefu, Mkurugenzi huyo alisema kwamba alikuwa Dar es Salaam akiandika maombi ya fedha kwa ajili ya kutatulia changamoto mbalimbali zinazoikabili mamlaka hiyo.

"Unatumia siku ngapi kuandika proposal, msomi unatumia mwezi mzima kuandika proposal na unakaa Dar es Salaam hata Katibu Mkuu wako hajui na huko unajilipa posho tu! Tena badala ya kulipwa sh.120,000 kwa siku wewe unajilipa sh.150,000. Hatuwezi kuvumilia hali hii,” amesema.

Waziri Mkuu amemaliza ziara yake siku tatu mkoani Lindi na amerejea jijini Dar es Salaam.
                        
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU

Jeshi la Polisi Dar laua majambazi Hatari 6

$
0
0
Watu sita wanaotuhumiwa kuwa majambazi hatari, wameuawa katika majibizano ya risasi na Polisi katika eneo la Mbezi kwa Yusuf Makondeni katika Manispaa ya Kinondoni, Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa Kaimu Kamanda wa Kanda Maalumu, Naibu Kamishna wa Polisi, Lucas Mkondya, watuhumiwa hao waliuawa katika majibizano ya risasi na Kikosi Maalumu cha Kupambana na Ujambazi wa Kutumia Silaha.

Mkondya alisema wamepata taarifa kutoka kwa raia mwema kuwa kuna kikundi cha watu wenye silaha, wamejipanga kufanya tukio la ujambazi kwa kutumia silaha kwa mfanyabiashara aliyekuwa akitoka Benki ya Diamond Trust Bank (DTB), tawi la Barabara ya Nyerere, ambaye angepita katika barabara hiyo kwenda mkoani Morogoro.

Alisema baada ya kupata taarifa hizo, polisi waliweka mtego na majambazi hao wakitumia gari aina ya Toyota Carina lenye namba za usajili T970 DGZ rangi ya fedha, walionekana wakilifukuza gari la mfanyabiashara huyo, kisha kulipita na kumsimamisha kwa nguvu.

“Majambazi wawili wakiwa na bastola walishuka katika gari hilo. Baada ya kugundua kuwa wameingia kwenye mtego wa polisi, walianza kufyatua risasi kwa askari wakitumia bastola na wenzao waliokuwa wamejaa kwenye gari yao walianza kushuka huku wakifyatua risasi kuelekea kwa askari,” alisema Kaimu Kamanda Mkondya.

Alisema kutokana na hali hiyo, askari walianza kujibu mashambulizi na kuwaua majambazi hao na baada ya upekuzi, zilipatikana bastola mbili, moja ya kijeshi aina ya Chinese ikiwa na risasi moja ndani ya kasha la risasi; na nyingine aina ya Browning ikiwa imefutwa namba zake na maganda sita ya risasi yaliyookotwa katika eneo la tukio.

Miili ya watuhumiwa hao imehifadhiwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) na upelelezi unaendelea ili kubaini mtandao mzima wa ujambazi.

Katika tukio lingine la Oktoba 17, mwaka huu saa 2:00 usiku katika maeneo ya Tegeta Masaiti, watuhumiwa watatu wa ujambazi wakiwa wamepakizana kwenye pikipiki aina ya Fekon yenye namba MC370 BEY, wakiwa na bunduki aina ya shotgun iliyokatwa mtutu na kitako, walivamia duka la Abdallah Juma (46), mkazi wa Tegeta na kupora fedha za mauzo na kuiba vocha za mitandao mbalimbali, ambazo thamani yake haijafahamika.

“Polisi baada ya kupata taarifa waliwafukuza majambazi hao, walipoona wanakaribiwa na askari, walitupa chini begi walilokuwa nalo na kutelekeza pikipiki yao kisha kukimbia, begi lilipopekuliwa lilipatikana na silaha hiyo,” alisema.

Aidha, wananchi wenye hasira waliendelea kuwakimbiza majambazi hao na kumuua mmoja huku wengine wakikimbilia kusikojulikana. 

Katika hatua nyingine, Mkondya alisema wamekamata watuhumiwa wawili wa unyang’anyi kwa kutumia nguvu wakiwa na pikipiki moja na funguo bandia 75.

Alisema watuhumiwa hao, Ally Makwega (53) mkazi wa Tandika na Fabian Greyson (39) mkazi wa Yombo walikamatwa Oktoba 4, mwaka huu saa 6:00 usiku.

Watuhumiwa hao walikamatwa wakiwa na pikipiki yenye namba MC292 AMD aina ya Boxer rangi nyekundu, wanayoitumia kufanya uhalifu, wakiwa na funguo bandia 75 ambazo huzitumia katika kuvunja nyumba mbalimbali ya biashara za kulala wageni, maghala ya kuhifadhia bidhaa na maduka.

Baada ya watuhumiwa hao kuhojiwa, walikiri kuhusika na matukio mbalimbali ya uvunjaji wa maghala na kuiba katika mikoa ya Dar es Salaam, Morogoro na Dodoma.

Watuhumiwa hao watafikishwa mahakamani baada ya upelelezi kukamilika.

Wawili mbaroni kwa wizi wa miundombinu ya TANESCO Yenye Thamani ya Milioni 61

$
0
0
Wakazi wawili wa Manispaa ya Kinondoni wanashikiliwa na Polisi wakituhumiwa kukutwa na miundombinu ya Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) yenye thamani ya Sh milioni 61.

Walikutwa na miundombinu ya shirika hilo ikiwemo vifaa kwa ajili ya kuunganishia umeme.

Akizungumza Dar es Salaam jana, Kaimu Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Lucas Mkondya, alisema watuhumiwa hao walikamatwa juzi saa 10 jioni katika maeneo tofauti ya manispaa hiyo.

Alisema katika tukio la kwanza, maeneo ya Makumbusho, polisi wakishirikiana na kikosi kazi cha kuzuia uharibifu wa miundombinu ya Tanesco, walipata taarifa kutoka kwa raia wema kuhusu kuwepo kwa watu wanaohujumu miundombinu ya shirika hilo.

“Kikosi kazi walifika eneo hilo katika nyumba ya Wilfred Baruti (45) mkazi wa Makumbusho na kufanya upekuzi katika nyumba hiyo na vilipatikana vifaa mbalimbali vinavyotumika kuunganisha umeme vya Tanesco,” alisema Mkondya.

Aidha, alisema pia polisi walikwenda katika nyumba nyingine ya Beatrice Emmanuel (42) mkazi wa Salasala Mabanda Mengi walikofanya upekuzi na kufanikiwa kukamata vifaa ambavyo ni nyaya aina ya drums mbili, rola ya nyaya aina ya AICC ya umeme wa milimeta 50 ambazo hutumiwa na Tanesco kituo cha Kilimahewa cha Kawe, wilayani Kinondoni.

Alisema upelelezi ukikamilika watafikishwa mahakamani.
Mkuu wa kitengo cha mawasiliano Leila Muhaji akizungumza na waandishi wa kuhusu wizi huo wa vifaa vya umeme vyenye thamani ya milioni 61,Kulia ni Kaimu Kamishna wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam,Lucas Mkondya.

RIWAYA: She is My Wife- Sehemu ya 27 & 28

$
0
0
MUANDISHI : EDDAZARIA
ILIPOISHIA
“Si unataka kuniua? Niue sasa”
Halima alizungumza kwa hasira huku ameyang’ata meno yake, akimtazama Fetty anaye tetemeka kwa hasira kali, iliyo pelekea sura yake kukunjana na kutisha mithili ya chui jike, aliye uliwa watoto wake
akishuhudia.Gafla mlio wa risasi ukasikika huku kishindo kikubwa cha mtu kuanguka chini kikisikika
ndani ya chumba walichomo.

ENDELEA
Wote macho yao wakayapeleka sehemu alipo angukia mtu huyo, aliye pigwa risasi na kukuta ni yule nahodha msaidizi akiwa chini amelala huku, damu zikimtoka kifuani mwake na kwenye mkono wake wakulia akiwa ameshika bastola ikiashiria kwamba alitaka kuwashambulia wote waliomo ndani ya chumba ila Anna alimuwahi.

Halima akatoka na kuwaacha wezake kwenye chumba walichopo, akatoka nje ya manohari na kupanda juu kabisa, akawasha sigara yake taratibu na kuanza kuvuta, huku  akijaribu kuishusha hasira yake iliyo tokana na wezake kumuamini Samson, ambaye hataki hata kumuona kwenye macho yake.
                                                                                           *********
Rahab na raisi Praygod Makuya walipo malizwa kufunguliwa kamba zao kwa ajili ya kudumbukizwa kwenye jungu kubwa lenye maji yaliyo chemshwa kwa ajili yao. Rahab akamkonyeza muheshimiwa raisi na hapo hapo, wakaanza kupambana na vijeba hivyo vipatavyo sita, na kuwafanya watu wengine walio kusanyika katika eneo la uwanja kushuhudia kuuawa kwao, ili wawale wakaanza kuchanganyikiwa kwani kwa mapigo aliyo kuwa akiyapiga Rahab, yalimshangaza hadi chifu wao, hakuamini kuona mtoto wa kike akipambana kwa kiasi cha kuwaangusha vijeba wenye miraba miine.
“Twende muheshimiwa”

Rahab alizungumza baada ya kupata kijinafasi cha kukimbia kutoka kwenye kundi kubwa la watu hawa. Wakaanza kukimbia kuiingia msituni huku wakifwatwa kwa nyuma na kundi la askari wa kijiji hichi ambao wanatumia mishale na upendi katika kuwashumbulia. Kila walivyo kimbia ndivyo kundi la askari hao lilvyo zidi kuwafukuzia, na mbaya zaidi, mwanga wa mbalamwezi ulimulika kila upende wa anga na kuwafanya washinde kujificha kwenye vichaka kuhofia kuonekana na kukamatwa tena.
“Nimechoka…..”

Raisi alizungumza huku akionekana kukatishwa tamaa na kukimbia huko, Rahab akamshika mkono raisi na kuendelea kukimbia, kwa bahati nzuri wakakuta moja ya pango, wakaingia pasipo kuchunguza ndani ya pango hili kutakuwa na kitu gani. Askari hao waliokuwa wanawakimbiza wakapita kwa spidi katika pango hilo pasipo kuchunguza sana kama watu wanao wakimbiza watakuwa wameingia ndani ya pango hilo.
“Asante tena binti”

Rahisi alizungumza huku akiendelea kuhema kwa fujo, akionekana dhahiri kwamba hakuwa ni mtu wa mazoezi. Hawakuwa na sababu ya kuendelea kukaa tena ndani ya pango hilo baada ya kikundi hicho cha askari kupita kwa kasi katika eneo hilo. Wakabadilisha muelekeo na kupita katika njia tofauti na walio kwenda askari hao, ambao laiti wakitiwa mikononi basi hukumu yao ni ile ile ya kwenda kutafunwa nyama. Usiku mzima wakautumia kukimbia, na kutembea pale ilipo walazimu kufanya hivyo, hadi kunapambazuka bado wapo kwenye msitu huu ambao hawaelewi wanaweza kujitoa.
“Tunaweza kupumzika sasa”

Rahab alimuambia muheshimiwa Raisi, baada ya kupata eneo lililo tulia na lina maficho ya wao kupumzika. Raisi Praygod hakuwa na kipingamizi zaidi ya kutafuta sehemu na akajibwaga kama mzigo, miguu yake yote ikawa inawaka moto kwa jinsi alivyo kimbia na kutembea kwa muda mrefu, akavivua viatu vyake na kuviweka pembeni kisha akajilaza.

Rahab akasimama na kuanza kulichunguza eneo zima, kuhakikisha kama wanaweza hata kujilaza kidogo katika sehemu hiyo pasipo buguzi. Akiwa katika kuchunguza chunguza sehemu akabahatika kupata kuona mti wenye matunda mengi makubwa na mazuri, akausogelea na kulichuma tunda moja, akalipasua na kulilamba. Akapata laza tamu ya tunda hilo ambalo hakujua ni tunda la aina gani. Akaanza kulitafuna taratibu kusikilizia kama kuna madhara yoyote atakayo yapata, ila haikuwa hivyo kadri jinsi alivyo zidi kulila ndivyo jinsi alivyo zidi kunogewa na tunda hilo, na wala hakusikia mabadiliko yoyote katika mwili wake. Akachuma mengi kidogo na kurudi sehemu alipo lala muheshimiwa raisi Praygog.

“Muheshimiwa amka”
Rais akajinyanyua kivivu na kukaa kitako, huku akipiga miyayo, akiashiria kwamba yupo katika hali ya uchovu mkubwa. Rahab akampa tunda moja muheshimiwa kwa ajili ya kupunguza njaa ambayo inaendelea kukwangua matumbo yao, muheshimiwa raisi akaanza kula matunda hayo.
“Matunda gani haya?”

RIWAYA: Sorry Madam - Sehemu ya 71 & 72 (Riwaya inawafaa kuanzia miaka 18 na kuendelea )

$
0
0
MUANDISHI : EDDAZARIA

ILIPOISHIA
John akanisogelea hadi sehemu tuliyo jilaza, akanitazama kwa muda, mimi pamoja na mwanangu aliye anza kulia
“Mwanao ni mzuri sana”
John alizungumza huku akimtazama mwanangu pamoja na mama yake aliye jilaza, akiwa ameishiwa nguvu za mwilini mwake
“Goodbye my friend”(Kwaheri rafiki yangu)
John alizungumza kwa sauti ya upole nikastukia risasi kadha zikitua kifuani mwangu na kuninyamazisha kimya katika sehemu niliyo lala

ENDELEA
Sauti ya milio ya ndege nikaanza kuisikia kwa mbali kwenye masikio yangu, taratibu nikajaribu kuyafumbua macho yangu kuweza kuona n kitu gani kinacho endelea ila, ukungu mwingi umawa umetawala kwenye mboni yamacho yangu, jamvo lililo nifanya nisione kitu cha aina yoyote, nikajaribu kupapasa katika sehemu niliyo lala, nikagundua kwamba nimelalia kitanda cha kamba, ila sikuweza kutambua ni sehemu gani niliyopo.Muda jinsi ulivyo yoyoma ndivyo nilivyo weza kugundua kwamba eneo nililopo, kuna watu wanao zungumza lugha nisiyo ijua
"Nipo wapi?"

Nilijarivu kuzungumza huku nikijitahidi kunyanyuka kutoka katika kitanda nilicho lala ila milono ya watu si chini ya wanne wakanirudusha kulala tena kwebye kitanda.Sauti za wanaume pamoja na wanawake zikaendelea kupenya kwenye masikio yangu, nilipo anza kusikia milio ya watoto wadogo wakicheza na wengine kulia ndipo nilipo amini kwamba eneo hili ni salama kwa maisha yangu

 Nikawasikia wakiendelea kunong'oneza, mara sauti ya kike ikasikika, ambayo sikuweza kuisikia tangu wàlipo anza kuzungumza watu hawa, ambao hadi sasa hivi siwezi kuwaona vizuri zaidi ya vivuli vyenye giza, vilivyo simana pembeni ya kitanda nilicho kilalia.Nkasikia wakiyazungumza maneno niliyo yasema dakila kadhaa za nyuma nikiwauliza kwamba hapa nilipo ni wapi
"Hei"
Sauti ya msichana hiyo ilinisemesha, ila sikujua anataka kusema kitu gani
"Nipo wapi, dada?"

Nliyarudia maneno yangu niliyo yazungumza hapo awali
"Unazungumza kiswahili wewe?"
Msichslana huyo aliniuliza, kwa lugha ya kiswahili jamvo lililo nifanya nizidi kufarijika moyoni mwangu na kuamini kwamva nimepata mwokozi katika wakahi huu mgunu nilio nao katika yangu maisha
"Ndio, ndio dada"
Niliitikia kwa haraka ila hata ninaye zungumza naye asibadili mawazo ya kunisaidia mimi
"Unaitwa nani?"
"Eddy, Eddy dada yangu"
Nikamsikia msichana huyo akizungumza na wezake huubakilitaja jina langu, kwa wezake ambao ninaamini hawaijui lugha ya kiswahili tunayo zungumza
"Umetokea wapi?"
"Tanzania dada yangu"
"Ulikuja huku kufanyaje?"
"Wapi, kwani hapa ni wapi?"

Kabla sijajibiwa nilicho kiuliza nikasikia sauti za watu waliomo ndani ya chumba wakisalimia kwa pamoja kwa kutumia lugha wanayo izungumza, sauti nzito ya mwanaume ikaitikia na kuwafanya watu wote kukaa kimya ndani ya chumba tulichopo
"Mumesema, ameamka?"
Mwanaume huyo alizungumza kiswahili cha kuvuta maneo, akionekana kwamba hakifahamu vizuri
"Ndio baba, na anazungumza kiswahili"
"Amesema ametokea wapi?"
"Tanzania, ila hajanitaji ni sehemu gani"
Mwanaume huyo akaendelea kuzungumza kilugha chao, baada ya muda akatoka ndani ya chumba tulichopo
"Eddy baba amrsema tukuache upumzike"
"Ndoja kwanza, unaitwa nani?"
Msichana huyo akakaa kimya kwa sekunde kadhaa kisha akajikoholesha kidogo kuliweka koo lake vizuri kisha akanijibu kwa upole
"Nitakujibu, ukiwa vizuri"

Nikamsikia akitoka ndani ya chumba nilichopo, nikajipapasa kifuani mwangu, na kukuta kitambaa kigumu kikiwa kimefungwa kuzunguka usawa wa kifua changu chote
"Ehee Mungu warehema, nisaidie mimi mja wako"
Nilizumgumza kwa sauti ya chini, huku nkihisi machozi yakinitiririka pembezoni mwa macho yangu.Kumbukumbu za maisha yangu ya nyuma nilipo kua bado mdogo zikaanza kunijia kichwani mwangu, picha ya sura ya mana yangu ikaanza kunijia kichwani na iukumbuka baadhinya matukio ya furaha aliyo kua akinifanyia

'Eddy mwanangu jaribu kuishinda hasira yako'
Nimaneno ya mama, niliyo anza kuyakumbuka vizuei na hili tukio lilitokea kipindi nilipo mpiga mwenzangu nilipo kua chekechea hadi akapoteza maisha akiwa anakimbizwa kupelekwa hospitalini
'Usiwe mjinga na wewe utakubali vipi kupigwa na mwanaumwe mwenzio'
Nimanenoya mzee Godwin, alipo kua akinifundisha mbinu za kupigana baada ya kupugwa sana na wezangu nilipo kua darasa la kwanza
'Mwanaume halisi, hupambana hadi dakika ya mwisho ya uhai wake'
'Hata ikiwezekana kutoa roho ya mtu wewe toa tu, ili mradi uwe msindi'

Nimaneno menfine ya mzee Godwin alipokua akinifundisha kadei siku zilivyokua zikienda jambo ambalo alinifanya na mimi ka katili na roho ya kinyama tangu nilipo kua mdogo.
'Uwe unasamehe saba mara sabini, kwani Mungu anawasamehe wale wote walio mkosea'
Nimaneno mengine ya mama, alipokua akinifundisha kusoma biblia kabla ya kulala, kwani alipenda kunikuza katika mazingira ya kidini na kumujua Mungu
'Mimi baba yako, nihodari sana wa kuua pale ninapo kua kwenye uwanya wa vita, risasi yangy moja inapo toka kwenye mdomo wa hii bastola yangu, hua nilazima imuangamize mtu'


Dk Slaa Aingilia Kati Ugomvi wa Godbless Lema na RC Gambo.......Huu Hapa ni Ujumbe Wake

$
0
0
Ugomvi wa maneno kati ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo na Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema limemuibua katibu Mkuu wa zamani wa Chadema, Dk Wilbroad Slaa aliyeandika ujumbe mrefu akimkingia kifua mbunge huyo.

Gambo na Lema walirushiana maneno juzi mbele ya wafadhili kwenye hafla ya kuweka jiwe la msingi kwenye mradi wa maendeleo wa ujenzi wa hospitali itakayohudumia bure wanawake na watoto uliogharimu shilingi bilioni 9.

Kupitia ujumbe huo uliosambazwa kwenye mitandao ya kijamii ambao alithibitisha kuwa ni wa kwake, Dk Slaa amemrushia lawama Mkuu huyo wa Mkoa akidai kuwa anaijua vizuri historia ya ardhi na mradi huo.

==> Usome Hapo Chini 
 
 Mrisho Gambo,
Naamini hii ID ni ya kwako na hasa kwakuwa kwenye post unaonekana ukizungumza, napata uhakika kuwa ni wewe.

1) Mkuu wa Mkoa, nakuheshimu kwa kuwa cheo chako ni kikubwa sana. Hata hivyo, ulichokifanya leo na " propaganda unazopiga zimenifanya nikudharau na kukupuuza. Ningeliweza kuishia katika kukudharau na kukupuuza, lakini

2) Aibu uliyoiletea Taifa letu leo, inanifanya " nipige kelele" kuwa " siasa za maji taka siyo wakati wake huu.

a). Mhe.Mrisho Gambo, wewe kama Mkuu wa Mkoa unayo au mamlaka au vyombo vya dola kukusaidia kufanya utafiti wa maana kuliko aibu kubwa uliyoiletea Taifa letu mbele ya Wahisani/ Wafadhili wetu kupitia Maternity Africa. Hukufanya hivyo, umeamini propaganda kuliko busara na hekima. Kwa hilo siwezi kukusamehe wala kukuheshimu pamoja na cheo au vyeo vyote ulivyonavyo.

b). Mrisho Gambo, ungelikuwa wa busara iwapo ungelimwomba kiongozi au mwakilishi wa ADF (ulikuwa na uwezo wa kujua ADF ni nani na historiaya yake ni ipi- kwa kupenda propaganda hukufanya hivyo) au Mwakilishi wa Maternity Africa hasa Happy (ambaye alisaini pia barua ya kukualika kuwa mgeni rasmi, au hata Mhe.Mbunge Lema ambaye kimsingi ndiye chimbuko la upatikanaji wa Ardhi hiyo kutoka kwa Marehemu Advocate Mawala (Mwenyezi Mungu amlaze mahala pema peponi), na pia chimbuko la Upatikanaji mradi kutoka kwa wafadhili wetu.

Kutokupenda kushauriwa na hao wenye kujua mradi imekufanya "kuonekana juha" na " mwongo" kwa kuwa historia haifutwi kwa " propaganda za jukwaani". Lakini kwa bahati mbaya athari ya propaganda imeenda mpaka kuichafua Taifa letu kwa wahisani. Ujenzi ndiyo kwanza unaanza. Umeombwa kufanya "Ground Breaking ceremony", unadhani wawakilishi wa wahisani na hasa kule kwenye chimbuko la fedha wanapata picha gani ya Taifa letu.

c). Mrisho Gambo, busara na hekima ya kawaida ingelikuwezesha kuelewa barua ya mwaliko ambayo imesisitiza mara mbili hivi, kuwa wahusika ni taasisi isiyojihusisha na siasa. Wakasema mradi kwa muda sasa umekumbwa na matatizo yenye sura ya kisiasa. Ulipaswa kutafakari, kutafiti na kutafiti njia makini zaidi ya kuona wakina mama wajawazito, wenye fistula na watoto wachanga hawakosei au hata hawacheleweshewi kupata huduma hiyo kwa sababu za kipuuzi tu. Eti unasoma historia! Unaijua historia au unaota ndoto!

Nimepiga kelele kwa kuwa ninaijua vizuri hiyo historia A to Z. Sikuambii ungeliniuliza, lakini wapo kwenye kikao hicho ambao wasingelihitaji kuisoma bali kuitoa kichwani historia hiyo, tangu kupatikana kwa Ardhi, mchakato wa kuchora ramani, kuisajili na kupata vibali vyote vya Kituo hicho cha Afya (japo kwa kweli ni hospitali, inaitwa kituo cha Afya tu kwa. Sababu za kisheria).

3) Mrisho Gambo, kwa hili Watanzania wa Arusha na wote wenye kujua ukweli hatutakusamehe kwa aibu uliyotupatia, na kujenga misingi ya kutufungia miradi mingine kwa wahisani wetu.

Kama una chembe dogo la busara:
a). Utakaa chini na kutafakari umekosea wapi.

b). Uwe na unyenyekevu uwaite wahusika wote ofisini kwako waombe wakupe " historia kamili" na wakupe mchakato mzima mpaka kufikia siku hii muhimu ya "Ground Breaking ceremony (uzinduzi wa Kazi ya ujenzi).

c). Ukipata Taarifa kamili, uwe na unyenyekevu, acha kiburi. Kiburi hakikusaidii wala haitasaidia jamii unayopaswa kuwatumikia (unless una malengo tofauti). Kwa unyenyekevu mkubwa Waombe msamaha Wahisani wetu kwa kuwaingiza katika " siasa ya Arusha" ambayo hawahusiki nayo; awaombe msamaha wakina mama, watoto na jamii ya Wananchi wa Arusha wapenda maendeleo kwa kuwachafua na kuwaletea vurugu kiasi cha kuifanya Arusha ionekane kila leo ni mahali pa vurugu, kumbuka vurugu husababishwa na viongozi wasiotumia busara na hekima. Uongozi ni busara na hekima siyo mabavu wala nguvu ya mamlaka.

Nimeyasema haya kwa uchungu mkubwa. Mimi siko kwenye siasa, na wala sina interest na siasa. Siangalii uso wa mtu. Kama ambavyo niliaga kuwa " Nastaafu Party Politics, lakini nitapiga kelele pale maslahi ya Taifa langu yanavyokanyagwa" nitakuwa mwendawazimu kunyamaza wakati mradi wa Tshs Takriban 9 Billioni unahatarishwa na upuuzi na uzembe wa kiongozi mmoja mwenye kuendekeza propaganda zisizo na msingi.

Nawaomba sana Radhi wahisani wetu. Mtuvumilie siyo kwa ajili yetu bali kwa ajili ya kina mama na watoto walengwa wa huduma itakayotolewa na " Kituo cha Mama na Mtoto" (propaganda kwamba Hospitali ni ya mke wa Lema zipuuzeni).

Happy, umevumilia mengi katika miradi mingi uliyofadhili na kuisimamia. Usirudi nyuma. Timiza ndoto yako iliyoanza katika umri mdogo sana. Matunda yanaonekana pamoja na vikwazo vya mara kwa mara vya wapinga maendeleo. Viongozi, " Tenganisheni siasa na Maendeleo" Watumikieni Watanzania bila kuangalia nyuso zao, mrengo wao. Siasa ni sayansi na siasa ni utumishi.

Dr.Wilbroad Peter Slaa 

Serikali Yapunguza Deni La Mifuko Ya Hifadhi Ya Jamii

$
0
0

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Serikali tayari imeshalipa sh. bilioni 722.7 kati ya sh. bilioni 964.2 za madeni ya michango ya jumla ambayo Serikali inadaiwa na mifuko ya hifadhi ya jamii nchini.

Ametoa kauli hiyo leo (Alhamisi, Oktoba 20, 2016) wakati akifungua Mkutano wa Sita wa wadau wa NSSF ulioanza leo kwenye Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha (AICC), Arusha na kuhudhuriwa na washiriki zaidi ya 600.

Amesema sekta hiyo imekua kwa asilimia 15 kutoka sh. trilioni 8.9 mwaka 2015 hadi kufikia sh. trilioni 10.2 mwaka 2016. “Hadi kufikia Juni 2016, takwimu zinaonesha idadi ya wanachama imeongezeka na kufikia milioni 2.1. Rasilmali za mifuko zimefikia shilingi trilioni 10.28 na mafao yaliyolipwa kwa kipindi cha mwaka kinachoishia Juni 2016 ni shillingi trilioni 2.93. Michango ya wanachama kwa mwaka ni shilingi trilioni 2.15 uwekezaji katika nyanja mbalimbali umefikia kiasi cha shilingi trilioni 9.29,” ameongeza.

Waziri Mkuu pia amemuagiza Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Prof. Godius Kahyarara awaandikie barua waajiri wote wanaodaiwa na shirika hilo na kuwataka wawasilishe fedha wanayodaiwa mara moja na wale ambao hawatalipa ndani muda utakaowekwa wafikishwe mahakamani na yeye apewe taarifa.

“Kumekuwepo na changamoto ya muda mrefu ya baadhi ya waajiri kutolipa michango kwa wakati hali inayoleta usumbufu mkubwa kwa wanachama hasa wanapofikia muda wa kustaafu. Suala hili halikubaliki, hivyo natoa maelekezo kwa waajiri wote nchini waheshimu sheria na wawasilishe michango yao kwa wakati,” amesisitiza.

Mbali ya kuwabana waajiri, Waziri Mkuu pia amewataka wanunuzi wa nyumba za shirika hilo na wapangaji wote wanaodaiwa wakamilishe malipo yao na wasipofanya hivyo ndani ya muda uliopangwa wafikishwe mahakamani.

“Nimeambiwa pia lipo tatizo la wadaiwa wa nyumba yaani wanunuzi na wapangaji. Suala hili lilitolewa maelekezo na Waziri wa Nchi, Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na wenye Ulemavu. Nataka nisisitize kuwa watu wote walionunua nyumba za NSSF na bado hawajakamilisha malipo na wale waliopanga lakini hawalipi kodi wanatakiwa kulipa haraka au wakabidhi nyumba hizo kwa NSSF ziuzwe kwa watu wengine, vinginevyo nao wafikishwe mahakamani.”

Akizungumzia utendaji wa shirika hilo, Waziri Mkuu amewapongeza viongozi wa shirika hilo na Bodi ya Wadhamini kwa uamuzi wake wa kuwekeza kwenye uzalishaji wa sukari nchini. Amesema kiwanda kitakachojengwa, kinatarajiwa kutoa ajira zaidi ya 100,000 kwa Watanzania na hivyo kuongeza wanachama katika mfuko wa NSSF.

“Nimefurahishwa na uamuzi wa NSSF na PPF kuungana ili kukabiliana na tatizo la sukari nchini. Tumeelezwa hapa kuwa mashirika haya yatashirikiana kujenga Kiwanda cha Sukari kitakachozalisha tani 200,000 kwa mwaka. Kiwanda hicho kitajengwa katika eneo la Mkulazi lililopo mkoani Morogoro,” amesema.

Mapema, akielezea utendaji wa shirika hilo, Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, Prof. Godius Kahyarara alisema limeboresha mafao ya wanachama wake kutoka sh. 80,000 hadi sh. 100,000 kwa mwezi.

Alisema limeanza kufanya upembuzi yakinifu wa kujenga nyumba za watumishi Dodoma ili kuendana na uamuzi wa serikali kuhamia Dodoma. “Upembuzi bado unaendelea lakini tumeshabaini kuna uwezekano wa kujenga nyumba 200 hadi 300 mkoani Dodoma,” alisema.

Kuhusu uwekezaji kwenye ujenzi wa Daraja la Mwalimu Nyerere lililopo Kigamboni, Dar es Salaam, Prof. Kahyarara alisema uwekezaji huo unalipa kwa sababu makusanyo ya tozo kwa watumiaji yamefikia asilimia 109. “Tuna uhakika kwamba fedha tulizowekeza zitarudi,” amesisitiza.

Wakati huohuo, Waziri Mkuu amepokea msaada wa tani 45 za saruji ambazo ni sawa na mifuko 900 yenye thamani ya sh. milioni 15 kwa ajili ya waathirika wa tetememo la ardhi mkoani Kagera. Amepokea msaada huo kutoka kwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya NSSF, Prof. Samuel Wangwe.

Akiwasilisha msaada huo, Prof. Wangwe alisema wameguswa na tatizo lilitokea mkoani Kagera na wameamua kutoa mchango ili kusaidia juhudi za Serikali kukabiliana na maafa hayo. Pia alisema wamekamilisha ahadi yao ya madawati 6,000 yenye thamani ya sh. milioni 400 ambayo waliitoa awali.

Waziri Mkuu aliwashukuru kwa misaada hiyo na kuwahakikishia kwamba itafikishwa kwa walengwa.

TSNP kutinga kwa Dk. Ndalichako, wapanga kutoa tamko la kupinga vigezo vya kupewa mkopo

$
0
0

Mtandao wa Wanafunzi wa Vyuo Vikuu Tanzania ( TSNP) umepanga kuunda kamati ya viongozi wa serikali za vyuo vikuu ili kukutana kwa dharura na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Dk. Joyce Ndalichako.

Pia imepanga kuandaa tamko la kupinga tamko la mabadiliko ya vigezo vitakavyozingatiwa katika utoaji mikopo kwa wanafunzi wa vyuo vikuu, lililotolewa hivi karibuni na Naibu Waziri wa Elimu Mhandisi Stella Manyanya.

Mtandao huo umedai kuwa, mabadiliko hayo ya vigezo yamesababisha wanafunzi wengi kukosa mikopo huku baadhi yao kupunguziwa fedha za kujikimu.

Mkurugenzi wa Haki za Wanafunzi TSNP, Venancy Shitindi janaalisema kuwa TSNP kwa sasa inakusanya taarifa za changamoto zinazo wakabili wanafunzi waliokosa mikopo ili kuandaa tamko la kupinga mabadiliko hayo, litakalo pelekwa katika Ofisi ya Rais, Waziri Mkuu na Wizara ya Elimu.

“Tumepanga kutengeneza kamati ndogo ya viongozi kwa ajili ya kukutana kwa dharura na waziri mwenye dhamana ya elimu ili kutoa malalamiko ya wanafunzi juu ya vigezo vipya vilivyotolewa na wizara yake, pia tunakusanya taarifa na kuandaa tamko tutakalolisambaza katika ofisi ya rais, wizara ya elimu na ofisi ya waziri mkuu,” alisema.

Alidai kuwa, mtandao huo umefanya utafiti wa vigezo vipya vilivyotajwa na kubaini kuwa haviendani na sera ya elimu ya mwaka 2014, wala ilani ya Chama cha Mapinduzi (CCM) pamoja na mpango mkakati wa kitaifa wa maendeleo kama alivyosema Mhandisi Manyanya katika taarifa yake aliyoitoa kwa vyombo vya habari.

“Baada ya kusoma taarifa ya Naibu Waziri Manyanya tulikwenda kuangalia sera ya elimu ya mwaka 2014, tukakuta hakuna sehemu iliyoainisha kundi linalostahili kupata mkopo bali imeeleza elimu itolewe bure na mikopo itolewe kwa kila mwanafunzi. Na kwamba elimu imepewa kipaumbele cha kuleta maendeleo katika nyanja zote haijasema kwa wanaosomea masomo ya sayansi pekee,” alisema na kuongeza.

“Hata mpango wa maendeleo wa miaka 5 yaani 2025, unaeleza kuwa Tanzania inatakiwa kuwa na uchumi wa kati na kwamba imetoa kipaumbele elimu kutolewa bure kwa nyanja zote ili wapatikane wataalamu wa fani mbalimbali na wa kutosha.”

Hata hivyo, taarifa iliyotolewa na Mhandisi Manyanya ilisema kuwa serikali kupitia Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu, huandaa sifa na vigezo vya utoaji Mikopo kila mwaka ili kuendana na malengo na matarajio yaliyopo katika mipango na mikakati ya kitaifa kama ilivyoainishwa katika Dira ya Taifa 2025.

Na kwamba Serikali imetoa vipaumbele katika utoaji mikopo kwa wanafunzi wa mafunzo ya Fani za Sayansi za Tiba na Afya,Ualimu wa Sayansi na Hisabati, Uhandisi wa Viwanda, Kilimo, Mifugo, Mafuta na Gesi Asilia, Sayansi Asilia na Mabadiliko ya Tabianchi, Sayansi za Ardhi, Usanifu Majengo na Miundombinu.

Wadau wa haki za binadamu nchini waendelea kusisitiza adhabu ya kifo ifutwe

$
0
0
Licha ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutotekeleza adhabu ya kifo kwa zaidi ya miaka 20. Imeendelea kusisitizwa kuifuta sheria ya adhabu ya kifo kwa watuhumiwa wa makosa ya mauaji kwa kuwa haisaidii kupunguza makosa hayo na kwamba iangalie chanzo cha tatizo hilo kwa lengo la kufanyia marekebisho.

Ushauri huo umetolewa jana na wadau mbalimbali wa haki za binadamu katika kongamano la kuijadili adhabu ya kifo nchini, lililoandaliwa na Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) kwa kushirikiana na Shirika la Umoja wa Mataifa (UN).

Wadau hao walisema kuwa, falsafa ya ukuaji wa adhabu huzingatia vigezo viwili ambavyo ni kutoa funzo kwa jamii pamoja ma kumrekebisha mkosaji. Wadau hao waliitumia hoja hiyo kuisisitiza serikali kufuta adhabu ya kifo kwa kuwa endapo mtuhumiwa akiuawa hatopata fundisho na pia kifo chake kinatafsiriwa sawa na kosa hilo kujirudia.

Mkurugenzi Mtendaji wa LHRC Hellen Kijo-Bisimba alisema kituo hicho hakitaacha kuishauri serikali kuifuta adhabu hiyo kwa kuwa haisaidii kutokomeza matukio ya mauaji na pia huenda ikaathiri watu wasio na hatia.

“Inabidi serikali iangalie chimbuko la matukio ya mauaji ili litokomezwe na si kuhukumu watu kwa adhabu ya kifo, hatumaanishi wasihukumiwe bali watafutiwe adhabu nyingine kwa kuwa tangu kuanza kutumika adhabu hii matendo ya mauaji hayajapungua,” alisema.

Aliongeza kuwa ” Kumuua mtu si suluhisho bali kosa hilo linazidi kufanyika na si sahihi. LHRC tunaendelea kuipinga adhabu hii sababu haisaidii kupunguza mauaji,”

Bisimba alidai kuwa, asilimia kubwa ya wanaohukumiwa adhabu ya kifo ni watu wasio na kipato na kwamba hali hii huonyesha adhabu hiyo hutekelezwa kitabaka zaidi.

Mwakilishi wa UN, Roeland Van de Geev alisema kuwa shirika hilo halitailazimisha serikali kuifuta sheria hiyo bali litawezesha mashirika yasiyo ya kiserikali (NGO’s) yanayohusika na haki za binadamu nchini kuishauri serikali kufuta adhabu hiyo.

“Nchi zaidi ya 140 duniani zimefuta adhabu hiyo, na hakuna matukio ya kutisha ya mauaji katika nchi husika, mfano Marekani inatekeleza adhabu ya kifo lakini matukio ya mauaji bado yanaendelea. Hii inamaanisha kwamba suluhu pekee ni kutibu au kuzuia vyanzo vya matukio hayo,” alisema.

Alishauri kuwa “Adhabu hii hafai kutekelezwa sababu inaondoa utu wa mtu. Tanzania pamoja na nchi za Ukanda wa Afrika Mashariki zifute sheria hiyo.”

Bahame Tom Nyanduga kutoka Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora alisema adhabu hiyo haistahili kuendelea kutekelezwa nchini kutokana kwamba ilianzishwa na wakoloni kwa lengo la kulinda utawala wao.

“Haki ya binadamu ya kuishi ndiyo msingi wa haki nyingine, katiba ya 1977 inatambua haki ya kuishi. Mahakama haiwezi futa adhabu hii bali serikali ndiyo yenye wajibu wa kuifuta sheria hiyo hivyo ni vyema ikafanya hivyo,” alisema.

Alisema ingawa serikali haijatekeleza adhabu hiyo kwa zaidi ya miaka 20 lakini inawajibu wa kuifuta sababu watu wanazidi kuhukumiwa.

“Nchi zaidi ya 20 Afrika zimefuta adhabu hii na hatusikii kama kuna kukithiri kwa matukio ya mauaji.Ni vigumu kuhusisha adhabu ya kifo kama suluhisho pekee la kutokomeza mauaji,” alisema.

Sheikh Ally Hemko kutoka Baraza Kuu la Waisilamu Tanzania (Bakwata) alishauri jamii kuepukana na vitendo vya mauaji kwa kuwa dini hairuhusu.

“Dini yetu hufundisha kuwa mtu anayeua nae aue ingawa pia inasisitiza kuua ni dhambi hivyo ili kuondokana na utata huo, jamii inawajibu wa kuacha vitendo hivyo sababu hata kama sheria hiyo ikifutwa watu wasio wema watazidi kuua,” alisema.

Kikosi Kazi Cha Jeshi La Wananchi (JWTZ) Cha Wasili Kagera Kwa Ajili Ya Kujenga Miundombinu Iliyoathiriwa Na Tetemeko La Ardhi

$
0
0
Kikosi kazi cha jeshi la wananchi wa Tanzania (JWTZ)kutoka makao makuu ya Jeshi kimewasili Mkoani Kagera kwaajili ya ujenzi wa miundombinu ya serekali iliyoathiriwa vibaya na tetemeko la ardhi lililotokea Mkoana Kagera septemba 10 mwaka huu.

Akiongea wakati wa uzinduzi wa ujenzi wa kituo cha afya katika kijiji cha Kabambyaile Kata ya Ishozi Wilaya ya Missenyi, Mkuu wa Mkoa wa Kagera Meja Jenerali mstaafu Salum Kijuu alisema kuwa kikosi hicho kinawataalamu wa fani zote za ujenzi na wamekuja na vifaa vyote vya ujenzi.

"Hiki kikosi kitafanya kazi kwa masaa 24 yaani watajenga usiku na mchana taasisi zote za umma zilizoathiriwa na tetemeko ikiwa ni pamoja na mashule na zahanati ili watoto waende shule na wagonjwa waendelee kupata matibabu"alisema.

Alisema mpaka kufikia july mwakani ujenzi wa miundombinu utakuwa umekamilika kwa robo tatu na aliwataka wananchi wawape ushirikiano maeneo yote watakayopita kujenga miundombinu ya umma.

Kiongozi wa kikosi hicho Meja Buchadi Kakura alisema kuwa kikosi hicho kimekuja Kagera kusaidia serekali ya Mkoa kurudisha miundombinu yote ya umma iliyoathiriwa na tetemeko la ardhi katika hali yake ya kawaida.

"Ni vigumu kusema lini tutakamilisha ujenzi ila sisi tutafanya kazi usiku na mchana ili ujenzi huu ukamilike ndani ya muda mfupi"Alisema Meja Kakura.
Mkuu wa Mkoa wa Kagera Meja Jenerali mstaafu Salimu Kijuu(mwenye Suti)akisikiliza maelezo juu ya kikosi kazi cha askari waliokuja kujenga miundo mbinu ya umma iliyoathiriwa na tetemeko la ardhi

Shirika la Viwango Tanzania (TBS) Kufumuliwa.....Waziri Mwijage Asema Litaundwa Upya, Vijana 136 Kuajiriwa

$
0
0

WAZIRI wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage amesema atalifumua na kuliunda upya Shirika la Viwango Tanzania (TBS) na kwamba wameshaanza kutafuta vijana 136 watakaoajiriwa katika shirika hilo kwa lengo la kudhibiti bidhaa, zinazoingizwa nchini chini ya viwango.

Aidha, wataweka kitengo maalumu kwa vijana hao, watakaokuwa na uwezo wa kuchunguza mipaka ya nchi, kunusanusa katika bandari bubu, kukamata, kuwasiliana na Polisi na kusimama mahakamani kutoa ushahidi.

Mwijage aliyasema hayo Dar es Salaam jana wakati wa utoaji wa tuzo kwa washiriki wa Programu ya Kaizen iliyo chini ya Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Japan (JICA) kwa kushirikiana na Serikali ya Tanzania.

 Alisema lengo la kuiunda upya TBS ni kuhakikisha kwamba kazi zinafanyika ipasavyo ili kulinda viwanda vya ndani, vinavyozalisha bidhaa mbalimbali.

“Tutahakikisha kwamba hakuna bidhaa zitakazoingia bandarini bila ya kuwa na viwango vinavyotakiwa. Lengo ni kuwalinda walaji na viwanda vyetu, kwa nini tuagize vitu nje wakati viwanda vyetu vinazalisha bidhaa,’’ alisema Mwijage.

Hatua yake hiyo imekuja siku chache, baada ya makontena 100 kutoroshwa katika bandari kavu za Dar es Salaam bila ya kukaguliwa na hivyo kuikosesha mapato serikali na pia kuwa na hatari ya kuingiza bidhaa zilizo chini ya kiwango.

Akizungumza utekelezaji wa agizo la Mwijage na hadi Jumanne wiki hii kwa waliotorosha makontena hayo kujisalimisha, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TBS, Dk Egid Mubofu alisema jana kuwa waziri ameongeza siku za utekelezaji wa agizo lake la kuwataka wafanyabiashara walioingiza maontena 100 bandarini bila kukaguliwa na TBS, watoe taarifa.

Dk Mubofu alisema baada ya agizo la awali, lililokuwa linamalizika Jumanne Oktoba 18, waziri aliongeza hadi leo ndipo hatua stahiki zichukuliwe.

Hata hivyo, alisema mwitikio umekuwa mkubwa na baada ya majumuisho ya leo, atakuwa katika nafasi nzuri ya kutoa taarifa kuhusu suala hilo. 

Septemba 13, Mwijage alitoa siku nne kwa wafanyabiashara waliopitisha makontena 100 bandarini bila kukaguliwa na TBS, wakatoe taarifa katika shirika hilo.

Mwijage alisema wafanyabiashara ambao hawatajisalimisha baada ya kumalizika kwa siku hizo, hatua stahiki zitachukuliwa ikiwemo kulipa faini ya asilimia 15.

Akizungumzia Programu ya Kaizen, Waziri Mwijage alisema jambo linalotakiwa kwa sasa ni kuhakikisha kwamba viwanda vingi, vinakuwa na mfumo huo wa Kaizen, kwani utasaidia kuzalisha bidhaa bora na zenye viwango vya hali ya juu.

Alisisitiza lazima wafanyabiashara waboreshe bidhaa zao na kwamba wasitengeneze bidhaa kumtosheleza mteja bali kumridhisha mteja.

“Hatutaki kuingiziwa bidhaa ‘midabwada’ wala mataputapu, tunachotaka ni bidhaa zenye viwango vinavyotakiwa na tunataka wazalishaji wetu mzalishe bidhaa zenye viwango na viwango vya kimataifa kwa ajili ya kuuza nje ya nchi,’’ alifafanua.

Hata hivyo, alisema sababu ya viwanda kufa ni baada ya kufunguliwa milango ya bidhaa kutoka nje kuingia nchini, ambazo hazikukidhi viwango na kwamba wafanyabiashara kutoka nje walikuwa wanashindana na wafanyabiashara waliopo, ambao waliwekeza fedha nyingi katika miradi yao.

Kwa mujibu wa Mwijage, mpango huo wa Kaizen umefanywa katika mikoa mitatu ya Dar es Salaam, Morogoro na Dodoma ambapo umesaidia kuongeza tija katika uzalishaji na kupunguza upotevu wa malighafi.

Aidha, aliwataka Watanzania kupenda vitu vya nyumbani kwani wanahakikishiwa ubora na endapo vitakuwa na tatizo ni rahisi kuwabana wafanyabiashara wa ndani kuliko wa nje.

Kwa upande wake, Mwakilishi wa JICA nchini, Toshio Nagase alisema mpango huo umesaidia kufundisha wakufunzi kwenye kampuni na viwanda zaidi ya 50 vilivyopo nchini.

Nagase alisema Kaizen imeleta matokeo kwa vitendo kwenye maeneo ya biashara kwa njia ya kusafisha eneo, kupunguza malighafi, kuhakikisha ubora wa bidhaa na kubadilisha tabia au motisha kwa wafanyakazi.

‘’Tunaamini kwamba Kaizen ni jambo muhimu katika kutengeneza viwanda vyenye ushindani kibiashara na kufanikisha lengo la kukuza viwanda kuelekea mwaka 2025,’’ alisema.

Alisisitiza kuwa mradi huo wa miaka mitatu, ulianza mwaka 2013 na kwamba ulianza Japan na nchi za Afrika unatekelezwa katika nchi za Ethiopia, Tunisia, Misri, Ghana, Zambia na Tanzania.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Ijumaa ya Octoba 21


Watu 6 wanaswa na silaha kwa mganga wa kienyeji Mwanza

$
0
0
Taarifa Ya Jeshi La Polisi Mkoa Wa Mwanza Kwa Vyombo

Kwamba Tarehe 18.10.2016 Majira Ya Saa 13:00hrs Katika Eneo La Buswelu Kata Ya Buswelu Wilaya Ya Ilemela Jiji Na Mkoa Wa Mwanza, Askari Wakiwa Katika Misako Na Doria Walifanikiwa Kuwakamata Watu Sita Wakiwa Na Silaha Mbili Zilizotengenezwa Kienyeji Pamoja Na Risasi Ishirini Na Tatu, Ambazo Walikuwa Wakizitumia Katika Matukio Ya Unyang’anyi Wa Mali Na Uporaji Hapa Jijini Mwanza Na Mikoa Mingine.

Aidha Tukio Hilo Limefanikiwa Baada Ya Kupokea Taarifa Kutoka Kwa Raia Wema Kuhusu Uwepo Wa Wahalifu Hao, Ndipo Askari Walifanikiwa Kumkamata Kwanza Jeremiah Maligia @ Mkumbo Miaka 25, Mnyiramba, Fundi Seremala Mkazi Wa Malega – Singida Ambaye Alipohojiwa Alikiri Kuhusika Na Kutaja Wenzake Waliokuwa Wakishirikiana, Na Kuwa Silaha Wamezificha Kwa Mganga Wa Kienyeji Aitwaye Leornad Litta @ Makai Anayeishi Mtaa Wa Kagida – Buswelu.

Askari Walikwenda Mahali Hapo Na Kufanikiwa Kumkamata Mganga Huyo Wa Kienyeji Bwana Leornad Litta Miaka 39, Akiwa Na  Silaha Hizo Mbili Zilizotengenezwa Kienyeji Hapo Nyumbani Kwake Na Risasi Ishirini Na Mbili Zinazotumiwa Na Bunduki Ya Aina Ya Short Gun Na Risasi Moja Ya Rifle Aina Ya Mark Iv.

Aidha Katika Kuhojiwa Zaidi  Na Askari Watuhumiwa Tajwa Hapo Juu Waliwataja Washirika Wao Wanne Ambao Walikuwa Wakishirikiana Katika Kufanya Uhalifu Ambapo Askari Walifanikiwa Kuwakamata, Ambao Ni 1. Kamgisha Jovini Kamhambwa Miaka 40, Mlinzi Na Mkazi Wa Iloganzala, 2. Juma Yusuph @ Jimi Miaka 35, Mkazi Wa Bwani Kinondoni, 3. Samweli Peter Miaka 36, Mkazi Wa Busweli Na 4. Shabani Hussein Miaka 26, Fundi Viatu Na Mkazi Wa Nyasaka Msumbiji.

Watuhumiwa Wote Walipofanyiwa Mahojiano Walikiri Kwamba Silaha Hizo Walizitumia Katika Unyang’anyi Wa Mali Na Uporaji Katika Maeneo Ya Jiji Na Mkoa Wa Mwanza, Aidha Jeshi La Polisi Kwa Sasa Linaendelea Na Uchunguzi Kuhusiana Na Tukio Hilo Na Matukio Waliyokuwa Wameyafanya, Pindi Uchunguzi Ukikamilika Watuhumiwa Wote Watafikishwa Mahakamani.

Kamanda Wa Polisi Mkoa Wa Mwanza Naibu Kamishina Wa Polisi Ahmed Msangi Anatoa Wito Kwa Wakazi Wa Jiji Na Mkoa Wa Mwanza Akiwataka Kuendelea Na Tabia Ya Kutoa Ushirikiano Kwa Jeshi Lao La Polisi, Ili Tuweze Kudhibiti Uhalifu Katika Mkoa Wetu., Lakini Pia Anatoa Angalizo Kwa Wananchi Haswa Vijana Akiwataka Kuacha

Tabia Ya Kujihusisha Na Uhalifu Bali Wajikite Katika Kufanya Shughuli Halali Za Maendeleo, Kwani Jeshi La Polisi Lipo Vizuri

Kuhakikisha Ulinzi Na Usalama Upo Kwa Raia Wote Wa Jiji Na Mkoa Wa Mwanza.

Katika Tukio La Pili

Mnamo Tarehe 18.10.2016 Majira Ya Saa 14:00hrs Mchana Katika Eneo La Ilemela Wilaya Ya Ilemela Jiji Na Mkoa Wa Mwanza, Askari Walifanikiwa Kuwakamata Watu Wawili Ambao Ni 1. Rahim Feka Miaka 28, Mkazi Wa Ilala – Dar Es Salaam, 2.  Ally Kawalale Miaka 32, Mkazi Wa Jetrumo – Arport Dar Es Salaam, Wakiwa Wanataka Kuuza Gari Lenye Namba T.778 Azv Aina Ya Toyota Land Cruiser Lililokuwa Wameliiba Huko Ilala Jijini Dar Es Salaam.

Aidha Watuhumiwa Hao Walikamatwa  Baada Ya Kupokelewa Taarifa Ya Kuibiwa Kwa Gari Hilo Huko Dar Es Salaam Na Kwamba Kuna Uwezekano Kuwepo Eneo La Kanda Ya Ziwa, Ndipo Ulifanyika Upelelzi Kuhusiana Na Taarifa Hiyo, Na Kufanikiwa Kuwakamata Watuhumiwa Tajwa Hapo Juu Wakiwa Na Gari Hilo.

Watuhumiwa Wote Wapo Chini Ya Ulinzi Wa Jeshi La Polisi Wakiendelea Na Mahojiano , Huku Taratibu Za Kuwasafirisha Kwenda Dar Es Salaam Wakiwa Chini Ya Ulinzi  Wa Askari Polisi Zikiwa Bado Zinaendelea.

Kamanda Wa Polisi Mkoa Wa Mwanza Naibu Kamishina Wa Polisi Ahmed Msangi Anatoa Rai Kwa Wakazi Wa Jiji Na Mkoa Wa Mwanza Akiwataka Kuacha Tabia Ya Kununua Vitu Vya Wizi, Bali Pindi Wanapoona Biashara Za Wizi Zinataka Kufanyika Au Zinafanyika Watoe Taarifa Polisi Ili Watuhumiwa Waweze Kukamatwa Na Kufikishwa Mahakamani.

Katika Tukio La Tatu

Kwamba Tarehe 18.10.2016 Majira Ya Saa 23:00hrs Katika Kitongoji Cha Ibungiro Kijiji Cha Sagani Kata Ya Kandawe Wilaya Ya Magu Mkoa Wa Mwanza, Mtu Mmoja Msichana Aliyejulikana Kwa Jina La Dema Charles @ Bulayi Miaka 20, Mkazi Wa Kandawe, Ameuawa Kwa Kukatwa Na Vitu Vyenye Ncha Kali Sehemu Za Kichwani Na Kiunoni

Akiwa Amelalala Na Watu Wasiojulikana, Huku Wenzake Wa Wili Wakijeruhiwa Sehemu Mbalimbali Za Miili Yao.

Majeruhi Waliojeruhiwa Katika Tukio Hilo Ni 1.mariam Lucas @ Kapele Miaka 26, Mkazi Wa  Kijiji Cha Sagani Aliyejeruhiwa  Shingoni Na Kwenye Kiganja Cha Mkono Wa Kulia, 2. Kapelele Makubi @ Salulo Miaka 90, Ambaye Ni Baba Mwenye Nyumba/ Mji, Aliyejeruhiwa Mgongoni, Kichwani Na Kiunoni.

Inadaiwa Kuwa Wauaji Hao Walifika Katika Nyumba Hiyo Majira Tajwa Hapo Juu Na Kuwakuta Wenye Mji  Wakiwa Wamelala, Ndipo Waliingia Ndani Na Kufanya Mauaji Hayo, Hadi Sasa Hakuna Mtu Yeyote Aliyekamatwa Kuhusiana Na Tukio Hilo.

Aidha Uchunguzi Wa Awali Umebainisha Kuwa Mauji Hayo Yametokana Na Kulipiza Kisasi, Jeshi La Polisi Kwa Sasa Lipo Katika Upelezi Pamoja Na Uchunguzi Kuhusiana Na Tukio Hilo, Majeruhi Wapo Katika Hospitali Ya Wilaya Ya Magu Wakiendelea Kupatiwa Matibabu Na Hali Zao Zinaendelea Vizuri.

Kamanda Wa Polisi Mkoa Wa Mwanza Naibu Kamishina Wa Polisi Ahmed Msangi Anatoa Wito Kwa Wakazi Wa Jiji Na Mkoa Wa Mwanza Akiwataka Kutoa Ushirikiano Kwa Jeshi La Polisi Ili Watuhumiwa Wa Mauaji Hayo Wawezwe Kukamatwa Na Kufikishwa Katika Vyombo Vya Sheria.

Imetolewa Na:

Dcp: Ahmed Msangi

Kamanda Wa Polisi (M) Mwanza

Waziri Kairuki Afanya Ziara Dar, Kinondoni Kukagua Mradi Wa TASAF.......Asisitiza Waliotafuna Fedha Hizo Watatumbuliwa

$
0
0
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Angella Kairuki amesema atahakikisha anawachukulia hatua watendaji wote, walioshiriki katika udanganyifu wa kuingiza kaya zisizostahili katika Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini unaosimamiwa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (Tasaf).

Aidha, aliiagiza Tasaf kuhakikisha inafuatilia kaya zote ambazo ziliingizwa katika mpango huo bila kuwa na sifa zinazostahili, kwa kuziorodhesha kwa majina, wanapoishi na kiasi cha fedha walichopokea ili ripoti hiyo iwasilishwe kwa Rais John Magufuli.

Kairuki aliyasema hayo jana wakati akizungumza baada ya kupokea ripoti ya utekelezaji wa Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini (Tasaf III) ya Mkoa wa Dar es Salaam, sambamba na kuzungumza na wananchi katika mitaa ya Kigogo Kati na Mikoroshoni, Manispaa ya Kinondoni.

“Kaya ambazo hazistahili hawafanyi peke yao wanashirikiana na watu, kama ni viongozi katika ngazi za mitaa na kata mitaa tunataka majina, na katika kila jina tujue nani alishiriki kumuingiza nani alikuwa akimchukulia na kama yupo mtumishi wetu wa umma tujue ni nani na hatua gani za kinidhamu zimechukuliwa.”

 “...Msije mkashangaa nikaja kuelekeza polisi kukamata hawa na hawa kwa sababu hizi hela ni lazima zirudi,” alisema Kairuki.

Alisema ameshapokea taarifa za mikoa mbalimbali, lakini Dar es Salaam na wilaya zake bado na mwisho ilikuwa ni Oktoba 6, mwaka huu, lakini aliwaongeza wiki moja ambayo tayari imeisha na orodha hiyo inatakiwa ipelekwe kwa Rais Magufuli.

Kairuki aliongeza kuwa pamoja na mkoa kusema umeondoa kaya 789 ambazo hazina sifa, lakini kuna kaya 5,457 ambazo zinapaswa kuondolewa katika mpango huo kwa kuwa hazina sifa za kupokea ruzuku hiyo. 

“...baada ya kuelekeza uhakiki wa nyumba kwa nyumba, sisi kwa taarifa tulizonazo tutaondoa kaya 5,457. Sasa ujiulize nyinyi ndio mlikuwa katika zoezi na mkapata idadi hiyo, hapa inaonesha kuna kitu hakipo sawa,” alisema.

Alisema katika kaya hizo zitakazoondolewa, 1,867 hazina vigezo vya umasikini, 563 zipo kwenye orodha lakini zilikuwa hazijitokezi kuchukua ruzuku na hazijulikani zilipo na kaya nyingine 2,114 hazikupatikana wala kujulikana zilipo wakati wa ukaguzi.

Alisema kaya hizi ni nyingi na hasa ikizingatiwa asilimia 76 hazijaingizwa katika mpango huo, hivyo kaya hizo ambazo ziliandikishwa zinapaswa kwenda kukaguliwa ili ziweze kuingizwa katika mpango huo ili katika awamu ya nane ya uhawilishaji fedha waweze kupata.

Kairuki alisema kiasi kikubwa cha fedha kimepotea, ambacho kingeweza kuwasaidia watu wanaostahili kuwa katika mpango huo. 

Alisema wilaya za Kinondoni na Temeke zimeshapokea malipo ya awamu saba ambayo ni Sh bilioni 6.7. Alisema hadi sasa kuna kaya 32,456 zilizoondolewa kwenye mpango huo.

Kwa wastani kaya moja hulipwa kati ya Sh 20,000 hadi 60,000 kwa kutegemea idadi ya watu katika kaya.

Akizungumza katika mkutano huo, Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Ali Hapi ambaye pia ni Kaimu Mkuu wa Mkoa alisema mpango huo ni muhimu kwa maendeleo ya taifa, lakini kuna watu wanaoharibu taswira ya Tasaf.

Alisema kuna fedha nyingi ambazo zinaishia kwenye mikono ya wajanja na haziwafikii walengwa wa mpango huo.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Tasaf, Ladislaus Mwamanga alisema mpango huo umeandaliwa kitaalamu na utaendelea kuwa endelevu na kwamba mradi huo unategemea zaidi serikali na wafadhili, lakini hadi sasa kiasi kikubwa kimekuwa kikitoka kwa wafadhili.
 Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa umma na Utawala bora Mh. Angela Kairukia akiwa sambamba na Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni,akiendelea na ziara katika Mkoa wa Dar es salaam kukagua maendeleo ya mradi wa kusaidia kaya masikini TASAF

Nyota ya Godbless Lema Inavyomng'arisha RC Gambo Mbele ya Rais Magufuli

$
0
0
Kama mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema anapambana na Mrisho Gambo ili kujijenga kwa wananchi wake, basi mkuu huyo wa mkoa ananufaika na vita hiyo na anatarajia makubwa zaidi baada ya mzozo wa mwanzoni mwa wiki.

Wakati Gambo akitarajia kupandishwa cheo na Rais John Magufuli, madiwani wa jiji hilo wametangaza kususia vikao vyote hadi viongozi wa juu wa Serikali watakapoingilia kati mgogoro uliopo.

Wawili hao waliingia kwenye mzozo mwingine mapema wiki hii wakati Gambo alipoalikwa kuzindua ujenzi wa hospitali ya mama na mtoto, itakayojengwa kwa ufad kwa ufadhili wa taasisi ya Martenity Africa alipojaribu kueleza historia ya kiwanja cha jengo hilo, maelezo ambayo Lema aliyapinga kwa sauti kubwa na kusababisha shughuli hiyo kuvurugika.

Baada ya mzozo huo, Gambo amedokeza kuwa kuna makubwa yanafuata.

“Baada ya hilo, simu zilikuja kibao, lakini bahati nzuri kabla sijauliza kokote, na Mheshimiwa Rais ndio akawa ananipigia akaniambia nina full confidence (nina imani) na wewe. Labda wafikirie promotion (kupandisha cheo), lakini hayo mengine hayapo,” alisema Gambo akiwaeleza wafanyabiashara wa mjini hapa kuhusu barua iliyosambaa juzi kwenye mitandao ya kijamii kuwa Rais ametengua uteuzi wake.

“Baadaye (Rais) akaniambia kwamba sasa ili (wafanyabiashara) wajue kwamba kweli nimekupigia simu, niitie mmoja uliye naye karibu ili niongee naye. Ndio (mwenyekiti wa wafanyabiashara wa Arusha) akapata previledge (bahati) naye ya kuongea na Mheshimiwa Rais.”

Iwapo Gambo atapandishwa cheo, ambacho kwa mukhtadha wa utumishi wa umma chaweza kuwa ni kuteuliwa kuwa mbunge na baadaye waziri, itakuwa ni mara ya pili kupanda cheo siku chache baada ya kuzozana na Lema.

Gambo, ambaye aliteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Arusha Juni 26, alilumbana na Lema Agosti Mosi mbele na Naibu Waziri wa Tamisemi, Suleiman Jafo.

Katika tukio hilo, Lema alisema Gambo haheshimu mipaka ya kazi zake, akimtuhumu kuingilia maamuzi ambayo tayari yameshajadiliwa kwenye vikao halali vya halmashauri na kupitishwa na ofisi ya mkuu wa mkoa katika kikao cha wakuu wa idara, maofisa tarafa, waratibu wa elimu kata watumishi wa Mamlaka ya Maji Safi na Mazingira (Auwsa) jijini hapa.

“Nimeona nizungumze hapahapa ili naibu waziri ufahamu hali ilivyo hapa. Kwa mfano Baraza la Madiwani la mwaka 2008, ndilo lililopitisha kiwango cha posho kwa madiwani kutoka Sh100,000 hadi 120,000. Jambo la kushangaza DC ameandika barua Tamisemi na nakala kwa Takukuru ili wachunguze jambo ambalo limeshapata baraka za Tamisemi,” alisema Lema.

Hali hiyo ilimfanya naibu waziri kuingilia kati na kuahidi kuzishughulikia changamoto hizo na kumpa nafasi Gambo, ambaye wakati huo alikuwa mkuu wa wilaya, kujibu hoja hizo. 

“Mheshimiwa mbunge nataka ujue mimi ndiyo mkuu wa shughuli za Serikali hapa wilayani. Muda wowote nina uwezo wa kuingilia kati mambo ambayo naona hayaendi sawa, hata kama yupo katibu tawala na viongozi wengine,” alisema Gambo.

“Rais aliona ninafaa ndiyo maana akaniteua na sihitaji kujifunza namna ya kuwa mkuu wa wilaya  kwa kuwa huu ni mwaka tano.”

Malumbano hayo yaliendelea na kumuhusisha pia Meya wa Jiji la Arusha, Calist Lazaro ambaye aliungana na Lema na madiwani wengine kupinga jambo hilo.

Baada ya vuta nikuvute hiyo mbele ya waziri, Agosti 18 Gambo aliteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha kuchukua nafasi ya Felix Ntibenda.

Siku chache baada ya uteuzi huo, Gambo aliagiza halmashauri ya jiji kutafuta fedha za kupunguza deni la walimu ambalo ni Sh154 milioni. 

Mkurugenzi wa jiji hilo, Athuman Kilamia alitangaza posho za madiwani ambazo zilikuwa zinalipwa kinyume cha taratibu, zitumike kupunguza deni la walimu na zikatolewa.

Mgogoro ukaibuka kati ya madiwani wa jiji hilo ambao wengi ni kutoka Chadema.

Sakata la Jumanne wiki hii linaweza kumpa cheo kikubwa zaidi kutokana na Rais Magufuli kumpigia simu kwa lengo la kumthibitishia kuwa yuko pamoja naye siku ambayo barua ya kughushi ilisambaa kwenye mitandao ya kijamii kuwa mkuu huyo wa nchi ametengua uteuzi wa Gambo.

Sakata hilo lilitokea katika uwekaji wa jiwe la msingi la ujenzi wa hospitali ya mama na mtoto jijini Arusha ambao utagharimu Sh9 bilioni, sehemu kubwa ya fedha hizo zikitoka taasisi ya Martenity Africa.

Mvutano huo ulianza baada ya Gambo kusema kuwa ardhi kwa ajili ya ujenzi wa hospitali imetolewa na Taasisi ya Mawalla Fund kwa kuwa muasisi wake, Nyaga Mawalla alikuwa na maono ya kusaidia afya ya mama na mtoto.

Kauli yake ilikuwa ikimaanisha kuwa Mfuko wa Maendeleo wa Arusha (ArDF) haikutoa kiwanja hicho kwa Martenity Africa wala kutafuta mfadhili.

Jambo hilo liliwakera viongozi wa ArDF, ambayo imeanzishwa na Lema na Elifuraha Mlowe, ambaye ni mwenyekiti. 

Lema alimtaka ndugu wa wakili huyo amsahihishe Gambo, lakini hakuna kilichofanyika, ndipo aliposimama na kuanza kupinga kwa sauti maelezo ya Gambo.

Lema alikuwa akisema mkuu huyo wa mkoa anapotosha ukweli kwa misingi ya kisiasa, kwa kuwa Mawalla Fund ilitoa kiwanja hicho kwa ArDF, ambayo ilitafuta wafadhili na kusaini nao mkataba wa ujenzi wa hospitali.

Wageni kwenye hafla hiyo iliyofanyika Bulka walijaribu kuwatuliza wawili hao, hawakufanikiwa kutokana na Lema kuendelea kueleza kwa sauti kuwa Gambo anapotosha, huku mkuu huyo wa mkoa akizungumza kwenye kipaza sauti kumtaka mbunge huyo atulie.

Shughuli hiyo ilimalizika kiutata na hivyo waandaaji wakashindwa kuendesha harambee iliyopangwa kufanyika baada ya uzinduzi.

Majambazi Hatari Wauawa.....Bunduki 9 Zakamatwa

$
0
0
Jeshi la polisi limedai kwamba limeua majambazi wawili hatari na kukamata bunduki tisa, kati ya hizo SMG saba, shotgun moja na riffle moja, risasi 473 na magazini 16 baada ya majibizano ya risasi katika misitu ya Milima ya Usambara, Kijiji cha Magamba wilayani Lushoto. 

Katika majibizano hayo, pia polisi walidai kukamata bendera zenye maandishi ya lugha ya Kiarabu, redio saba za upepo na soksi za kuficha nyuso.
 
Kamishna wa Operesheni na Mafunzo wa Polisi, Nsato Marijani alisema jana kuwa hiyo ilikuwa operesheni ya kuwasaka majambazi waliovamia Chuo Kikuu cha Sekomu, wilayani humo hivi karibuni.

Alisema katika tukio hilo, askari wawili walijeruhiwa kwa risasi. Marijani ambaye alikuwa katika milima hiyo inayodaiwa kuwa ngome ya majambazi hao, aliwataja waliouawa kuwa ni Mudrick Abdi (24) maarufu kwa jina la Osama, mkazi wa Mbagala Majimatitu Dar es Salaam na Sultan Abdallah (24) mkazi wa Kiembesamaki, Zanzibar. 

Alisema askari waliojeruhiwa wanaendelea na matibabu na kwamba hawakupata madhara makubwa kwa kuwa walikuwa wamevaa majaketi ya kuzuia kupenya risasi . 

Vita ya Kukabili Njaa Yatangazwa......Mikoa Yote Yatakiwa Kuimarisha Mifumo ya Kuhifadhi Chakula

$
0
0

Mwezi mmoja tangu Serikali iseme usalama wa chakula ni kwa asilimia 123, jana Ofisi ya Waziri Mkuu imezitaka wizara, mikoa na halmashauri kuchukua hatua za kukabiliana na tishio la njaa ikiwamo kuzuia matumizi ya nafaka kutengeneza pombe. 

Pia, ofisi hiyo ya Waziri Mkuu imewataka wananchi kuhifadhi chakula baada ya Mamlaka ya Hali ya Hewa (TMA), kutabiri kuwa kuanzia Oktoba hadi Desemba mwaka huu, maeneo mengi ya nchi yatakuwa na mvua zitakazonyesha chini ya kiwango huku maeneo mengine yakikumbwa na ukame. 

Akizungumza jana, Mkurugenzi wa Idara ya Maafa, Ofisi ya Waziri Mkuu, Brigedia Mbaazi Msuya alisema hali hiyo itasababisha ukame na tishio la njaa katika baadhi ya maeneo ambayo hutegemea mvua katika kilimo. 

Msuya alisema kutokana na utabiri wa TMA, wananchi wanashauriwa kulima mazao ya muda mfupi na yanayostahimili ukame. 

“Maofisa ugani wanatakiwa kutoa ushauri kwa wananchi kuhusu mazao wanayotakiwa kupanda kwenye maeneo yao,” alisema. 

Aliwataka wananchi kuweka akiba ya chakula cha kutosha hasa kwenye maeneo ambayo yanapata mvua chini ya kiwango. 

Kaimu Mkurugenzi, Idara ya Usalama wa Chakula wa Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi, MaryStela Mtalo alisema idara hiyo itafanya kazi ya uratibu, ufuatiliaji na ukusanyaji na kutoa taarifa za chakula kwa wakati. 

 “Wakala wa Taifa Hifadhi ya Chakula wanaelekezwa kununua na kuhifadhi akiba ya chakula cha kutosha ili kukabiliana na upungufu unaotarajiwa katika baadhi ya maeneo,” alisema. 

“Mikoa na Halmashauri zake zisimamie na kuimarisha mifumo ya kuhifadhi chakula baada ya mavuno ili kupunguza upotevu wa chakula na kuhakikisha chakula kinapatikana.” 

Taarifa hii ya tishio la njaa inapingana na ile iliyotolewa Septemba 8 na Naibu Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi William Tate Ole Nasha kwamba Watanzania wasiwe na wasiwasi kuhusu hali ya chakula nchini kwa maelezo kuwa kuna ziada ya chakula zaidi ya asilimia 123 ikilichozalishwa msimu uliopita. 

Akizindua tovuti ya Wakala wa Taifa Hifadhi ya Chakula (NFRA) mjini Dodoma, Naibu Waziri Ole Nasha alisema hali ya chakula inaridhisha kutokana na ukweli kuwa uzalishaji wa chakula ni kwa asilimia 100 hali ya utoshelevu wa chakula ni asilimia 101 hadi 120 hali inayotafsiriwa kuwa kuna chakula cha kutosha kwa miaka mitatu hadi minne. 

“Nawasihi Watanzania kutunza chakula kilichopo ili kitumike sasa na baadaye, hali ya uwepo wa  chakula ndani ya nchi itaonyesha kuwa kuna usalama kwa wananchi na wanaweza kuendelea na  shughuli zao za kila siku,” alisema.

 Pia ni tofauti na taarifa iliyotolewa Jumanne iliyopita na Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Chakula na Mifugo Dk Florence Turuka kwamba wilaya 42 nchini zinakabiliwa na uhaba wa chakula huku Mkoa wa Kagera ukikumbwa na baa la njaa na ukame. 

Kutokana na ukame huo, ng’ombe waliokuwa wanauzwa kwa Sh 600,000 wilayani Karagwe sasa wanauzwa kwa Sh 20,000. 

“Licha ya kwamba ripoti ya dunia inaonyesha hali ya chakula duniani ni mbaya, Tanzania kipo chakula na kinatosheleza kwa kiwango cha juu cha asilimia 123,”alisema Turuka wakati akizindua ripoti ya Shirika la Chakula na Kilimo Duniani (FAO) kwa mwaka 2016 inayoonyesha kuwa dunia inakabiliwa na balaa la njaa kutokana na mabadiliko ya tabianchi.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images