Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Mchungaji Ajibu Tuhuma Za Kukutwa Na Mafuta Ya Mchekanambingu

0
0
VERA  SIDIKA: Miongoni  mwa  wakenya  maarufu  wanao daiwa  kutumia  mafuta  ya  mchekanambingu  kwa  ajili  ya  kungarisha  nyota  zao
*****

Mchungaji   Lewis  Njoroge  wa  kanisa  la  New  Tongue  Faith  lililopo  jijini  Nairobi  hapa Kenya, ameibuka  na  kujibu  tuhuma  zinazo  mkabili  za  kukutwa  na  mafuta  ya  MCHEKANAMBINGU.

Pastor   Njoroge  ambae  kwa  muda  mrefu  sasa  amekuwa  akiwatahadharisha  waumini  wake  na  wakenya  kwa  ujumla  kuhusu  kutotumia   MAFUTA  YA  MCHEKANAMBINGU  kwa  madai  kuwa  ni  MAFUTA  YA  KUZIMU  , wiki  iliyopita  aliripotiwa  na  vyombo  mbalimbali  vya  habari  nchini  Kenya, akidaiwa  kujipata  matatani  baada  ya  Mafuta  ya  MCHEKANAMBINGU  kukutwa  ofisini kwake.

Mara kadhaa  Pastor  Njoroge  maarufu  kama  Pastor  Njoroo,. Amekuwa  akiwakemea  waumini  wake  pamoja  na  wakenya  kwa  ujumla, kutothubutu  kutumia  MAFUTA  YA  MCHEKANAMBINGU  kwa  sababu   ni mafuta  kutoka  kuzimu,  yanayo  tolewa  na  mganga  wa  jadi  kutoka  Tanzania, ajulikanae  kama  mungu  wa  kabili, ambae  kwa  mujibu wa  PASTOR  Njoroge , ni  wakala  wa  kuzimu.

Pia  Pastor Njoroge  amekuwa akiwatuhumu  baadhi  ya  wachungaji, wasanii  wakubwa  na wafanyabiashara  maarufu  kujihusisha  na  matumizi  ya   mafuta  ya  mchekanambingu.

Aidha Pastor  Njoroge  amewahi  kunukuliwa  akitoa shutuma  zake  kwa  baadhi  ya  magazeti  ya  Kenya,  akivitumuhu  ku wahamasisha  vijana  kutumia mafuta  ya  mchekanambingu.

“ Sasa  hivi, kila  mtu  akiwa  maarufu  na  kupata  mafanikio  hapa  Kenya, magazeti  yana  muhusisha  mtu  huyo  na  mafuta  ya  mchekanambingu.  Matokeo yake  sasa  hivi  kila  kijana, anafikiri  hawezi kufanikiwa  katika  jambo  lake  bila  kutumia  mafuta  ya  mchekanambingu “….

Pastor  Njoroge  aliongeza  kwa  kusema  kuwa  mafuta  ya  mchekanambingu  ni mafuta  kutoka  kuzimu, na  yoyote  atake  jipaka  mafuta  hayo  anakuwa  amejiunganisha  moja  kwa  moja  na  utawala  wa  kuzimu. Mafanikio  atakayo  yapata  yatakuwa  ya  muda  mfupi  tu na  malipo  yake  yatakuwa  makubwa  kuliko  mafanikio  aliyo  yapata.

Wiki mbili  zilizopita  vyombo  mbalimbali  vya  habari  nchini  Kenya, viliripoti kuhusu  tuhuma  za  kukutwa  kwa  mafuta  ya   mchekanambingu  kwenye  ofisi  za  Pastor Njoroge, jambo  ambalo lilizua  mtafaruku  mkubwa  kati  ya  Pastor  Njoroge  na  waumini wake.

Inaelezwa kuwa, mmoja  kati  ya  wazee  wa  kanisa  la  New Tongue  Faith, aliingia  ofisini  kwa  Pastor Njoroge  kwa  ajili  ya  kuchukua  documents. Sasa  wakati  anapekua  makabrasha  katika  ofisi  hiyo  alishangaa  kukuta  kibox  chenye  vichupa  vinne kikiwa  sambamba  na  karatasi  yenye  maelekezo  ya  jinsi  ya  kutumia  mafuta  ya  mchekanambingu.

Ikadaiwa  kuwa, baada  ya  kuulizwa  kuhusu  mafuta hayo  yamefikaje  ofisini  kwake, Pastor Njoroge  hakuwa  na majibu  yenye  kueleweka.

Suala  hili  lilifika  kwa wazee  na  viongozi  wa  kanisa  kwa  ajili  ya  kulijadili  na  baadae  likavuja  kwa  waumini.

Akifanya  mahojiano na  kituo  kimoja  cha  redio  nchini  Kenya, Pastor  Njoroge  alisema “  Mafuta  hayo  yalipandikizwa  ofisini  kwake,  kwa  lengo  la  kumchafulia  jina  lake “.

“ Ndugu  mwandishi, vita  vyetu  si  kwa  jinsi  ya  mwili. Vita tunavyopigana wakristo  ni  vya  rohoni. Nina  wapinzani  wengi  sana  ambao  wanajaribu  kunikwamisha, lakini  ninasema  watashindana  lakini  hawatashinda “.

Tulimpigia  simu  dokta  mungu  wa  kabili  kupitia  namba  yake  0744 000 473  ili  atueleze  kama  anamfahamu  Pastor  Njoroge, alijibu  kwa  ufupi  “ Simfahamu “

Mafuta  ya  mchekanambingu, yamekuwa  maarufu  sana  hapa  nchini  Kenya, ambapo  inasemekana  kuwa  yanatumika  kwa  kazi  mbalimbali  kama  vile kusafisha  nyota, kusafisha  mwili, kumkinga  mtu  dhidi ya  maadui,  kuimarisha  mahusiano  ya  kimapenzi, kuharakisha  ndoa, kumvuta mpenzi, kuwakinga  watoto,  kukuza  biashara,  uongozi  nakadhalika, huku  wateja  wake  wakubwa  wakitajwa  kuwa  wanasiasa  wakubwa, viongozi, wafanya  biashara, wasanii  wa  muziki, nakadhalika.

SOURCE : VYOMBO  MBALIMBALI  VYA  HABARI  NCHINI  KENYA.

Jinsi Punyeto Inavyo Sababisha Ukosefu Na Upungufu Wa Nguvu za Kiume

0
0

Ukosefu  na/ama  upungufu  wa  nguvu  za  kiume, ni  tatizo  linalo  wakabili  mamilioni  ya  wanaume  duniani.  Zipo  sababu  nyingi  zinazo  sababisha  tatizo  la  ukosefu  wa  nguvu  za  kiume.  

Miongoni  mwa  sababu  hizo  ni  pamoja  na  maradhi  kisukari, presha,shinikizo  la  damu, moyo, figo, matatizo  kwenye  mishipa  ya  ubongo  &  mishipa  ya  uti  wa mgongo, matatizo  kwenye  mishipa itumikayo  kusafrisha damu  mwilini, maradhi  ya  ngiri,  pamoja  na   upigaji  punyeto  kwa  muda  mrefu.

Katika  makala  yetu  ya  leo, tutaangalia  namna   suala  la  upigaji  punyeto linavyo  athiri  nguvu  za  kiume.

Kabla  hatujaangalia  namna  suala la upigaji  punyeto linavyo  maliza  nguvu  za  kiume, ni  vyema  tukafahamu  kwanza  kuhusu  SAYANSI  YA  MFUMO  WA  NGUVU  ZA  KIUME.

Kufahamu   kuhusu   SAYANSI  YA  MFUMO  WA  NGUVU  ZA  KIUME  tafadhali  tembelea :

Ukisoma  vizuri  kuhusu  mfumo  wa  nguvu  za  kiume, utagundua  kuwa   Suala  la  nguvu  za  kiume  ni  suala  la  kimfumo.  Ili  mwanaume  awe na nguvu  za  kiume, aendelee  kuwa  na  nguvu  za  kiume na  azilinde  nguvu  zake za  kiume, ni  lazima  ogani  zote zinazo  husika  na  mfumo  wa  nguvu  za  kiume  ziwe  na  afya  njema  na  ziwe  na  ushirikiano   thabiti  na  wenye  afya.

Vile  vile , utagundua  kuwa , mambo  makuu  muhimu  katika   mfumo  wa  nguvu  za  kiume  ni  kama  ifuatavyo:

i.Mishipa  imara  ya  ubongo  na  yenye  afya  njema

ii. Mishipa  imara  ya  uti  wa  mgongo  (  spinal  cords )

iii.Mishipa  imara  itumikayo  kusafirisha  damu  mwilini  (  Blood Vessels )

iv. Mfumo  imara  wa  usafirishaji  damu  mwilini

v. Mishipa  ya  uume  iliyo  imara  na  yenye  afya  njema

vi. Uhusiano  imara  na  wenye  afya  kati  ya  mishipa  ya  fahamu  iliyopo  katika  ubongo, mishipa  ya  kwenye  uti  wa  mgongo  pamoja  na  misuli & mishipa  ya  kwenye  uume.

Hivyo  basi, ili  mwanaume  aweze  kuwa  na  nguvu  imara  za  kiume, na  aendelee  kuwa  na  nguvu  hizo ni  lazima  mambo  yote  muhimu  katika  mfumo  wa  nguvu za  kiume  yawe  imara  pasi na  hitilafu  yoyote.

Hitilafu  yoyote  katika  mambo  hayo, itasababisha  ukosefu na/ama  upungufu wa  nguvu  za  kiume  kwa  mwanaume  huyo.  Pale inapotokea    hitilafu  ama  mapungufu  katika  ogani  zaidi  ya  moja  kati  ya  zilizo  tajwa hapo  juu, basi  tatizo  kwa  muhusika  huwa  kubwa  mara  dufu.

JINSI  PUNYETO  INAVYO  SABABISHA  TATIZO  LA  UKOSEFU &  UPUNGUFU  WA  NGUVU  ZA  KIUME.
Mwanaume   anapopatwa na  wazo  la  kufanya  tendo  la  ndoa, ubongo  hutoa  ishara  kwenye  mishipa  ya  uti  wa  mgongo  ambayo  nayo  husafirisha  taarifa  hadi  kwenye  mishipa &  misuli  ya  uume.

Mishipa  ya  uume inapopokea  taarifa  hiyo, hutanuka. Na  mishipa  ya  uume  inapotanuka, hufanya  mambo  mawili  muhimu  sana :

i.Husababisha  mishipa  ya  ateri  kupanuka  na  hivyo  kuruhusu  damu  kuingia kwa  kasi  sana   ndani  ya  mishipa  ya  uume  na  hivyo  kuufanya  uume  usimame  na  kuwa  imara  bara bara.

ii. Huibinya na  kuiziba  mishipa  ya  vena  na  hivyo  kuzuia  kunyonya  ama  kufyonza  damu  iliyo  ingia  ndani  ya  mishipa ya  uume.  (  KAZI  KUBWA  YA  MISHIPA  YA  VENA  ILIYO  KARIBU NA  MISHIPA  YA  UUME  NI KUHAKIKISHA  HAKUNA  DAMU NDANI YA  MISHIPA  YA  UUME. HIVYO  BASI  DAMU  INAPOINGIA  NDANI YA  MISHIPA  YA  UUME, MISHIPA  YA  VENA  HU “SENSE” JAMBO  HILO  KWA  HARAKA  NA HIVYO  KUIFYONZA  DAMU  HIYO  KUTOKA KWENYE MISHIPA  YA UUME  YA  KUITOA  NJE YA MISHIPA  YA  UUME.  NA  DAMU INAPOKOSEKANA  NDANI  YA  MISHIPA  YA  UUME, HUUFANYA  UUME  KUSINYAA  NA  KULEGEA )

Mtu  anayepiga  punyeto  husababisha  mambo  yafuatayo  katika  mwili  wake :

1. Huuwa  nguvu  ya  mishipa  & misuli ya  uume ambayo  ndio  inayo husika  na  kusimama  kwa  uume

2. Mishipa  ya   uume  inapo  sinyaa  na  kukosa  nguvu  yake  ya  asili, husababisha  mambo  yafuatayo :

i.Huondoa  uwezo  wa  mishipa  &  misuli  ya  uume  kutanuka, na  hii  ndio  sababu  inayo  wafanya  waathirika  wa  punyeto  kutumia  nguvu  nyingi  sana  katika  kuufanya  uume  usimame.

ii.Huondoa  uwezo  wa  mishipa &  misuli  ya  uume  kuibana  na  kuiziba  mishipa  ya  vena, na  hii ndio  sababu  inayo  fanya  waathirika  wa  punyeto  kufika  kileleni  haraka  sana, kwani damu  inayo  ingia  kwenye misuli  ya  uume   hufyonzwa  ndani ya  muda  mfupi sana. 
 
 Hii  hutokea  kwa  sababu  mishipa na  misuli  ya  uume inakuwa  imelegea,na  mishipa  ya  vena inakuwa  imepwaya, hivyo  msuguano wowote ule  hufanya  mishipa  ya  vena  kufunguka  na  kufyonza  damu  kutoka  kwenye mishipa  ya  uume  na hivyo  kuufanya  uume  kusinyaa  ndani ya dakika ama sekunde  chache sana.

3. Vile  vile  punyeto  hufanya  uume  kusinyaa na  kurudi ndani  na  kuufanya  uonekane kama  uume  wa  motto mdogo.

Kwa  ufupi  punyeto  husababisha  ukosefu  wa  nguvu  za  kiume  kwa  sababu  kuu  zifuatazo :

i.Kwanza   hudhoofisha  na  kuharibu  mishipa  ya  uume,  ambayo  ndio  hufanya  uume kusimama.

ii.Pili  hudhoofisha  utendaji  kazi  wa  mishipa  ya  ateri, ambayo  ndio  hutumika  kama  njia  ya  kusafirisha  damu kupeleka kwenye  misuli  ya  uume  na  ivyo  kuufanya  uume  usimame

iii. Tatu, punyeto  hupelekea  kuvuja  kwa  mishipa  ya  vena  na  hivyo  kusababisha  damu  kufyonzwa  kwa  haraka  sana  kila  iingiapo ndani  ya  misuli ya  uume  na  matokeo  yake  ni  uume   kusimama  kwa  muda  mfupi  sana  wakati wa  tendo  la  ndoa.

iv. Punyeto  huathiri  mtiririko  wa  damu  kwenda  kwenye  mishipa  ya  uume, kwa  sababu  hudhoofisha  misuli &  mishipa  ya  uume  pamoja  na mishipa ya  ateri  ambayo  ndio  hutumika  katika  kusafirisha  damu kwenda  kwenye  uume

DALILI  ZA  MTU  ALIYE  ATHIRIWA  NA  PUNYETO
Dalili  kuu  za  mtu  aliye athiriwa  na  punyeto  ni  kama  ifuatavyo:

i.           Uume  kusinyaa  na  kuwa  kama  wa  mtoto
ii.         Uume kurudi  ndani
iii.       Uume  kusimama  ukiwa  legelege
iv.       Kufika  kileleni  haraka  wakati  wa  tendo  la  ndoa.

TIBA   YA   NGUVU  ZA  KIUME  KWA MTU  ALIYE  ATHIRIKA  NA  PUNYETO.
Dawa   asilia  ya  nguvu  za  kiume iitwayo JIKO  ni tiba  bora  na  ya  uhakika  kabisa  kwa  mtu  aliye  athiriwa   na  punyeto.  Dawa  hii, pamoja  na  mambo  mengine  mengi, husaidia  kufanya  mambio  yafuatayo  katika  mwili  wa  mwanaume  aliye  athiriwa  na  punyeto :

i.Kuimarisha  mishipa  & misuli  ya  uume  ulio  legea na  hivyo  kuurejeshea  uwezo wake wa  asili

ii. Hutibu   tatizo  la  uume  kurudi  ndani

iii.Humaliza  tatizo  la  kusimama  kwa  uume  ukiwa  legelege

iv.Hutibu  na  kuponya  kabisa  tatizo  la  kufika  kieleleni  haraka.

BEI  YA  DAWA  :  Dawa  hii  inapatikana  kwa  gharama  ya  SHILINGI  ELFU  THEMANINI  TU (Tsh. 80,000/=)

MAHALI  INAPOPATIKANA :  Dawa  hii  inapatikana  katika  duka  la  dawa  asilia  liitwalo  NEEMA  HERBALIST  &  NUTRITIONAL  FOODS  CLINIC  lililopo  jijini  DAR  ES  SALAAM  katika  eneo  la  UBUNGO   nyuma  ya  jengo  la  UBUNGO  PLAZA   karibu  na SHULE  YA  MSINGI  UBUNGO  NATIONAL  HOUSING.

Kwa  wateja  wasio  weza  kufika  ofisini  kwetu. Watafikishiwa  dawa  mahali  popote  walipo  jijini  DAR  ES  SALAAM.

Kwa   wateja  waliopo  mikoani  watatumiwa  dawa  kwa  njia  ya  MABASI

Kwa  wateja  waliopo   Zanzibar  wata fikishiwa  dawa  kwa  njia  ya  usafiri  wa boti.

Na  kwa  wateja  waliopo  UGHAIBUNI  watatumiwa  dawa  kwa  njia  ya  POSTA  ama  DHL.

MAWASILIANO :  WASILIANA  NASI   KWA  SIMU  NAMBA  0766  53  83  84.

Kwa  taarifa  zaidi  kuhusu  huduma  zetu, tutembelee kila  siku  kwenye  blogu  yetu :

Rais Magufuli aongoza mamia Ya Wananchi kumuaga Dk Masaburi

0
0

Rais John Magufuli leo ameongoza mamia ya wakazi wa jiji la Dar es Salaam kuuga mwili wa aliyekuwa meya wa jiji hilo, Dk Didas Masaburi aliyefariki Jumatano iliyopita na kusema Masaburi ana wake wanne au watano na watoto zaidi ya 20.

Kauli ya Dk Magufuli ameitoa muda mfupi baada ya msomaji wa wasifu wa Dk Masaburi kusema kuwa ameacha mke mmoja waliyefunga naye ndoa Jannet Masaburi na wajane wawili kauli ambayo ilizua miguno kutoka kwa waombolezaji.

Alipopewa nafasi ya kuzungumza Dk Magufuli alisema anamfahamu Dk Masaburi kuwa alikuwa  na wake wanne au watano hivi.

Alisema hata watoto anafahamu kuwa anao zaidi ya 20.Rais Magufuli alisema Masaburi alikuwa rafiki yake,ndugu yake na mpiganaji mwenzake ndani ya CCM.

Baadhi ya Viongozi mbalimbali wa Kiserikali na Kichama wakiongozwa na Rais Dkt John Pombe Magufuli (wa tano kulia) wakiwa katika viwanja vya Karimjee mapema leo asubuhi kutoa heshima ya mwisho na kuaga mwili wa Marehemu Dkt Didas Masaburi,aliyefariki wiki iliopita katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili,wakishiriki 
Baadhi ya waombolezaji wakisubiri kuaga mwili wa mpendwa wao Dkt Didas Masaburi 

Watumishi TBS na TRA Waliohusika n a Upotevu wa Makontena 100 Bandarini Watakiwa Kujisalimisha Haraka kabla Hawatumbuliwa

0
0

Serikali imewataka baadhi ya wafanyakazi wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS) walioshirikiana na wenzao wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kupitisha  makontena zaidi ya 100 bila kukaguliwa na shirika hilo katika Bandari ya Dar es Salaam kujisalimisha haraka.

Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage alitoa agizo hilo jana wakati akizindua baraza la wafanyakazi wa TBS.

“Nimeanza kukusanya orodha ya majina ya watu waliosaidia kupitisha makontena haya na nikija nayo hawatapona,” alisema.

Aliwataka wote wanaojijua kuhusika kujisalimisha mapema na kutubu ili wasamehewe kabla ya hatua hiyo.

Makontena hayo yalipitishwa katika Bandari ya Dar es Salaam hivi karibuni bila ya kuthibitishwa na TBS.

Pia, aliitaka TRA kuacha kutoa makontena bila ya shirika hilo kuthibitisha au kukagua ubora wa bidhaa zinazoingizwa nchini kwa sababu ndilo lenye mamlaka hayo.

Alisema watakaotubu watapaswa kusema walishiriki vipi na lini, walishirikiana na nani na kutaja sehemu yalikopelekwa ili Serikali iweze kusaidia kukomesha hali hiyo.

Mwijage alisema anaamini waliofanya hivyo katika mamlaka hiyo walifanya kwa utashi wao bila ya ushiriki wa viongozi wao na kwamba sasa wakati umefika wa kukomesha tabia hiyo.

Alilitaka baraza hilo jipya la wafanyakazi kushirikiana na menejimenti kuhakikisha matatizo yanayojitokeza yanapatiwa ufumbuzi kwa masilahi ya nchi na kwamba Serikali itahakikisha inaongeza vitendea kazi na watumishi ili kufikia malengo ya shirika.

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TBS, Dk Egid Mubofu alisema baraza hilo lina wajumbe 48 wanaotoka katika vitengo mbalimbali na litakaa kwa muda wa miaka mitano.

“Baraza hili linaundwa kutokana na mkataba wa menejimenti na Chama cha Wafanyakazi (Raawu),” alisema Dk Mubofu.

Alisema wafanyakazi wanatakiwa kufanya kazi kwa weledi na uadilifu katika majukumu yao ya kila siku.

Mwenyekiti wa bodi ya wakurugenzi TBS, Profesa Mekanya Maboko alilitaka baraza hilo kufanya kazi kwa kushirikiana na menejimenti na bodi kuhakikisha shughuli za udhibiti wa ubora zinafanyika kwa ufanisi.

“Bodi itaendelea kuisimamia menejimenti na kuishauri ifanye kazi kwa kuzingatia sera na sheria,” alisema.

Riwaya ya Kusisimua: AM NOT A DOCTOR....Bofya Hapa Ujipatie Nakala Yako Kwa Bei Nzuri!

0
0

Mwandishi makini wa Riwaya za kusisimua,  EDDAZARIA G.MSULWA anawakaribisha kununua kitabu chake cha AM NOT A DOCTOR kupitia WhatsApp 0657072588.
 
Kitabu hiki kinapatikana kwa sh 10000 tu kwa watu kumi wa kwanza kukinunua watapa ofa ya kitabu cha HARD DAY bureeeee.
 
Wasiliana nami 0657072588 au 0768516188

ATCL Yatoa Ofa Ya Mwezi Mmoja Kwa Safari Za Mwanza.

0
0
Na Daudi Manongi-MAELEZO
Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL) imetoa ofa ya mwezi mmoja kwa abira wanaosafiri kutoka Dar es salaam kwenda Mwanza kulipa nauli ya shilingi 160,000/- kwa safari moja.

Kauli hiyo imetolewa leo jijini Dar es salaam na na Kaimu Afisa Mawasiliano wa Kampuni Bi.Lily Fungamtama wakati akiongea na Idara ya Habari.

Amesema Ndege za Kampuni zimeanza kutoa huduma kuanzia Jumamosi ya wiki iliyopita ya tarehe 15 ya mwezi huu kama ilivyobainisha kupitia vyombo vya Habari.

Safari hizo zilianza kwa kutoa huduma ya kusafirisha abiria kuelekea nchini Comoro na hapa nchini itoa safari katika mikoa ya Mwanza, Arusha na Kigoma.

Bi.Fungamtama amesema kwa kuanzia walianza na mazoezi ya vitendo kwa marubani na wafanyakazi wa ndani ya Ndege ambapo hatimaye walianza safari za biashara ya kusafirisha abiria mnamo tarehe 15 Oktoba kama ilivyopangwa.

Ameongeza kuwa ATCL imeboresha huduma zake kwa kiasi kikubwa kwa kuwapatia wateja wake ofa ya kubeba kilo 20 za mizigo na kilo 7 za mzigo wa mkononi bure   pamoja na kutoa vinywaji na ubadilishaji wa tiketi ni bure ndani ya mwezi.

Aidha, Kaimu Afisa Mawasiliano wa Kampuni Bi.Lily amekanusha taarifa potofu kuwa zimekwama kuanza safari zilizopangwa.

Amesema kuwa habari hizo sio za kweli kwani hivi sasa wameshaanza huduma katika mikoa hiyo mitatu.

Kampuni ya Ndege ya ATCL kwa sasa ina ndege tatu,zikiwemo mbili aina ya Dash8-Q400 zenye uwezo wa kubeba abiria 76 kila moja na Dash8-Q300 moja yenye uwezo wa kubeba  abiria 50.

Masharti Ya Leseni Kwa Wazalishaji Wa Bidhaa Zinazotozwa Ushuru Wa Bidhaa (Excise Goods)

0
0

Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) inapenda kuutaarifu umma kuwa, kwa mujibu wa vifungu vya 8 na 16 vya Sheria ya Ushuru wa Bidhaa Sura ya 147, wazalishaji wote wa bidhaa zinazotozwa Ushuru wa Bidhaa na wazalishaji wa malighafi ya kutengenezea spiriti wanatakiwa kusajiliwa na kupewa leseni na Kamishna Mkuu wa TRA kabla ya kuanza uzalishaji. 

Bidhaa zinazotozwa Ushuru wa Bidhaa zimeainishwa katika jedwali la nne la Sheria husika. Baadhi ya bidhaa hizo ni kama Bia, Sigara, Spiriti, Mvinyo na Vinywaji baridi.

Masharti ya Leseni

Maombi yote yatumwe kwa Kamishna Mkuu kwa kutumia fomu ya maombi ya leseni inayopatikana katika ofisi za TRA au tovuti: www.tra.go.tz

    Maombi tofauti yafanywe kama ifuatavyo:
  1. Kwa kila kiwanda ambacho kitatumika kuzalisha bidhaa.  Leseni itatumika kwa kiwanda kilichopewa leseni pekee
  2. Kwa kila aina ya bidhaa itakayozalishwa na leseni itatumika kuzalisha bidhaa husika pekee.
  3. Mmiliki wa leseni hataruhusiwa kuhamisha umiliki wa leseni husika, kubadili kiwanda au kuzalisha bidhaa tofauti katika kiwanda kilichopewa leseni bila kufanya maombi na kuruhusiwa na Kamishna Mkuu.
  4. Baada ya kupewa leseni, mzalishaji anatakiwa kumjulisha Kamishna Mkuu juu ya tarehe ya kuanza uzalishaji ndani ya siku 21 tangu uzalishaji huo kuanza.
  5. Pindi bidhaa yoyote inapoamuliwa kwa mujibu wa Sheria ya Bunge kuanza kutozwa Ushuru wa Bidhaa, mzalishaji wake anapaswa kumjulisha Kamishna Mkuu na kuomba leseni ya uzalishaji ndani ya siku 21 baada ya bidhaa husika kuanza kutozwa Ushuru wa Bidhaa.
  6. Leseni ya uzalishaji itakwisha muda wake kila tarehe 31 Disemba ya mwaka ambapo mmiliki atatakiwa kuomba leseni mpya.
  7. Wazalishaji wa spiriti yenye vionjo na isiyo na vionjo (Denatured and Undenatured Spirit) pia wanatakiwa kuomba leseni za uzalishaji kwa Kamishna Mkuu.
Uzalishaji wa bidhaa zinazotozwa Ushuru wa Bidhaa bila ya leseni ni kosa linalopelekea adhabu ya faini au kifungo au faini na kifungo ikiwa ni pamoja na kutaifishwa kwa mitambo na bidhaa zote zilizohusika katika utendaji wa kosa hili. Wazalishaji wote wanaaswa kumiliki leseni halali katika wakati wote wa uzalishaji na TRA kwa kushirikiana na wadau wengine wataendesha ukaguzi endelevu kuhakiki matakwa haya ya sheria.

Waombaji wanatakiwa kufanya maombi katika ofisi yoyote ya TRA ambako viwanda husika vinapatikana ili kuepuka adhabu kali zinazotokana na ukiukwaji wa matakwa haya ya sheria.

“Pamoja Tunajenga Taifa Letu”

Limetolewa na:
Idara ya Huduma na Elimu kwa Mlipakodi
TRA-Makao Makuu
Dar es Salaam

Waziri Mkuu Achoshwa Na Madudu Bodi Ya Korosho.....Aagiza ifanyiwe marekebisho makubwa, Aishangaa kung’ang’ania minada

0
0

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amemuagiza Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi, Dk Charles Tizeba kuifanyia marekebisho makubwa Bodi ya Korosho na menejimenti yake  baada ya kushindwa kusimamia zao hilo ipasavyo.

Amesema Serikali itafanya mapitio ya bodi zote za mazao ya biashara na imeanza na zao la korosho kisha zao la pamba, tumbaku, kahawa, katani na chai. Katika tathmini na mapitio hayo , bodi itakayobainika kushindwa kutekeleza majukumu yake itavunjwa.

Waziri Mkuu alitoa agizo hilo jana jioni (Jumapili, Oktoba 16, 2016) wakati akihutubia wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye uwanja cha Sokoine wilayani Nachingwea mkoani Lindi.

Alisema anaishangaa bodi hiyo kuacha kutekeleza majukumu yake na kuingilia minada ya korosho na kuzuia baadhi ya wafanyabiashara wasiweze kununua zao hilo hali inayoashiria kuwepo kwa watu waliopangwa kununua bila ya kufuata utaratibu.

“Bodi leo wamejipa jukumu la kusimamia minada ! sio kazi yao ni kazi ya chama kikuu, zao la korosho linalimwa kutoka mkoani Ruvuma hadi Tanga, mtasimamia minada mingapi viachieni vyama vikuu. Vyama vikuu vikiharibu walalamikaji waje kwenu kama sehemu ya rufaa. Sasa nyinyi mnasimamia minada mnaharibu walalamikaji watakwenda kwa nani  ?  kwa nini mng’ang’anie kwenda kwenye minada,” alihoji Waziri Mkuu.

Waziri Mkuu alisema Ijumaa (Oktoba 14,2016) bodi hiyo  ilisitisha mnada wa korosho Lindi kwa sababu wanunuzi hawakuweka bondi (dhamana ya mauzo) na alishatoa maagizo ya kuwataka wanunuzi wasiruhusiwe kununua hadi waweke asilimia 25 ya malipo.

Alisema maagizo hayo aliyatoa tangu mwezi Aprili ila  watendaji wa bodi hiyo hawakuyafanyia kazi kwa wakati na badala yake waliwazuia wafanyabiashara waliotaka kununua korosho Lindi kwa madai ya kutokuwa na bondi huku wakiwaruhusu wa Mtwara.

“Kama kule walinunua bila bondi kwa nini wasiwaruhusu na Lindi wakanunua bila  bondi ili nijue kwamba mliamua kugoma kuteleza maelekezo ya Serikali? Au hamkumtaka aliyeshinda  nyie  mlikuwa mnamtaka nani nitashughulika na nyie,” alisisitiza.

Aliongeza kuwa “Nimesema tukitoa maelekezo lazima yatekelezwe na atakayeshindwa hatufai, Mheshimiwa mbunge umelalamika juu ya bodi hawa ndio wabeba maelekezo hatujawahi kuona bodi ya korosho ikienda vijijini kuzungumza na vyama vikuu hata mara moja,”.

Akizungumzia kuhusu suala la wakulima kulazimishwa kufungua akaunti  za kupitishia malipo yao alisema wasiwalazimishe.“Waelimisheni wakulima umuhimu wa kufungua akaunti lakini si kwa kuwalazimisha wote wawe na akaunti hadi yule mwenye kilo tano…na akaunti yenyewe inafunguliwa kwa sh. 100,000,” alisema.

Alisema “’wanashindwa kutekeleza niliyowaagiza, halafu wanasingizia utendaji wao mbovu kuwa ndio maagizo yangu,’ niliwaagiza wapi,” alihoji na kuongeza kuwa  “yapo makundi yanafanya mambo yanavyotaka alafu yakiwazidi mambo wanasingizia viongozi wajuu na ndio wale wanaosema kila kitu nimeagizwa kutoka juu, juu wapi?

“Lazima tuendelee kudhibiti nidhamu ya vyombo vya tunavyoviunda kwa ajili ya kuwahudumia wananchi. Tutaendelea kusimamia nidhamu kwa taasisi zinazowahudumia wakulima nchi nzima,” alisisitiza.

Wakati huo huo Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Bw. Godfrey Zambi alimkabidhi Waziri Mkuu msaada wa sh. milioni 16.3 pamoja na nguo kwa ajili ya kusaidia  wananchi walioathirika na tetemeko la ardhi lililotokea mkoani Kagera Jumamosi, Septemba 10, mwaka huu na kusababisha vifo vya watu 17 na wengine 440 walijeruhiwa.

Maamuzi ya Umoja wa Ulaya Baada ya Burundi kujitoa Mahakama ya ICC

0
0

Siku chache baada ya Burundi kutangaza maamuzi ya kujitoa kwenye Mahakama ya makosa ya uhalifu ICC, Umoja wa Ulaya umetangaza kuitenga serikali ya Burundi kwenye masuala ya fedha za kikosi chake kilichotumwa nchini Somalia kujiunga na kikosi cha Umoja wa Afrika kusimamia amani nchini humo (AMISOM).

Umoja wa Ulaya, ambaye ni mfadhili mkuu wa Burundi unachangia 20% ya bajeti ya taifa hilo, umeamua kuchukua vikwazo dhidi ya serikali ya Burundi, inayotuhumiwa kwa ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu na kukataa mpaka sasa kuketi kwenye meza ya mazungumzo na upinzani wake. 

Serikali ya Burundi imeendelea kutengwa katika ngazi za kimataifa, na kutuhumiwa uhalifu mbaya dhidi ya binadamu, Umoja wa Ulaya unataka kuzuia moja ya sehemu kuu zinazoipatia serikali ya Burundi fedha za kigeni.

Umoja wa Ulaya umechukua uamuzi wa kutopitisha tena mishahara ya askari wa nchi hiyo wanaosimamia amani nchini Somalia kwenye akaunti ya serikali. 

Uamuzi wa EU unakuja wakati ambao uchumi wa Burundi umeendelea kudorora, hata baadhi ya shughuli zinazoingiza mapato kwa serikali zimekwama kutokana na hali mbaya ya kiuchumi

Ni wiki tatu sasa tangu Umoja wa Ulaya kutuma fedha kwenye akaunti ya Umoja wa Afrika ili kulipa mishahara askari wa kikosi cha Umoja wa Afrika nchini Somalia (AMISOM).

Ripoti kutoka Brussels Ubelgiji zinasema Umoja wa Ulaya umelipa tu malimbikizo ya kipindi kinachoishia hadi Machi 16, 2016, tarehe ambayo Umoja wa Ulaya uliiwekea vikwazo serikali ya Burundi, kwa mujibu wa Ibara ya 96 ya Mkataba wa Cotonou.

Tangu wakati huo, Umoja wa Ulaya ulisimamisha misaada yake ya moja kwa moja kwa serikal ya Burundi. Ni Euro milioni 5 tu za mishahara ya askari 5,500 wa Burundi wa kikosi cha AMISOM zimekua zikipitishwa kwenye hazina ya serikali ya Burundi.

Masauni Ashauri Kifungu Cha Umoja Wa Kitaifa Kifutwe Katika Katiba Ya Zanzibar Ya Mwaka 1984

0
0

Na Is-haka Omar, Zanzibar.
WAJUMBE wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar wameshauriwa kuondosha mfumo wa Serikali ya Umoja wa Kitaifa (SUK) katika Katiba ya Zanzibar ya Mwaka mwaka 1984.

Ushauri huo umetolewa na Katibu  wa Idara ya Siasa na Uhusiano wa kimataifa wa Kamati Maalum ya NEC, CCM Zanzibar,  Hamad Yussuf Masauni katika Majumuisho ya ziara yake ya kuimarisha uhai wa Chama huko katika Ukumbi wa Amani Mkoa wa Mjini, Unguja.

Alisema huu ndio wakati mwafaka wa kuondosha mfumo huo kwani hauna tija katika maendeleo ya nchi badala yake ukiachwa itakuwa ni fursa kwa wapinzani kurudi tena katika serikali baada ya kufanyika Uchaguzi Mkuu ujao wa mwaka 2020.

Alieleza kwamba nia ya CCM kukubali kuingia katika mfumo wa Serikali ya Umoja wa kitaifa (SUK) ni kushirikiana na vyama vya upinzani katika mipango ya maendeleo ya nchi pamoja na kumaliza siasa za chuki, hali ambayo CUF haikutaka kubadilika hivyo hakuna haja ya kubakisha mfumo huo katika Katiba ya Zanzibar.

Masauni aliwasihi Wawakilishi wa CCM kuhakikisha wanalinda kwa vitendo  maslahi ya Chama kwa kuandaa taratibu zote za kisheria kwa kufuta kipengele ndani ya Katiba kinachoeleza uwepo wa mfumo huo.

Alisema hatua ya mwisho itakuwa kurudi kwa wananchi kupiga kura ya maoni ya kukubali ama kukataa kuendelea na SUK, jambo ambalo kwa sasa ni rahisi kwani wananchi wengi hasa wafuasi wa CCM hawataki kuendelea na serikali hiyo.

“ Huu ni wakati mwafaka wa kuifuta CUF katika siasa za Zanzibar kwani hatuwezi kuendelea kuwa na ushirikiano na Chama kinachojali maslahi binafsi pamoja sera za utengano badala ya kuwaunganisha wananchi.

Hakuna haja ya kuendelea na SUK kwani katika miaka mitano ya mfumo huo wenzetu walionyesha udhaifu mkubwa na kupelekea nchi kuanza kuyumba kwani hata viongozi wao wa majimbo hawakufanya chochote kwa wananchi na mzigo wote waliwasukumia viongozi wa CCM.”, alisema Masauni na kuongeza kuwa serikali iliyopo sasa inaendelea kuwatumikia wananchi wote bila ya ubaguzi.

Aliwapongeza Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi kwa juhudi zao za kufanya mabadiliko ya baadhi ya sheria ndani ya Katiba ya Zanzibar zilizokuwa zikiwajengea ngome ya kujiamini chama cha CUF katika Baraza hilo.

Akizungumzia Uchaguzi wa ndani ya CCM unaotarajiwa kufanyika mwaka 2017, Masauni alikemea tabia na vitendo vya kuendekeza siasa za makundi ndani ya CCM kwani  hali hiyo aliitaja kuwa  inasababisha kupatikana kwa viongozi wasiokuwa waadilifu ndani ya chama hicho.

Alisema baadhi ya viongozi wa CCM wanatakiwa kuwakataa watu watakaoingia ndani ya Chama hicho kuwania nafasi za uongozi kupitia nguvu za fedha na umaarufu kwani watu hao ndiyo chanzo cha kujengeka makundi yasiyokuwa na lazima ndani ya chama chetu.

“ Sote tunakumbuka athari mbaya ya makundi iliyojitokeza katika chaguzi zilizopita na kuendelea kutusumbua mpaka sasa kwani kuna baadhi ya wanachama waliweka mbele maslahi ya watu binafsi badala ya CCM.”, alifafanua Masauni.

Masauni ambaye pia ni Waziri wa Mambo ya ndani ya Nchi, alieleza kwamba serikali haitovumilia kuona vitendo vya uhalifu vinaendelea katika maeneo mbali mbali ya Zanzibar, na wanaofanya vitendo hivyo waache kabla hawajachukuliwa hatua za kisheria.

Aliwataka wananchi kuendelea kutoa ushirikiano kwa vyombo vya ulinzi na usalama ili kupunguza kesi za uhalifu unaotokea katika maeneo mbali mbali nchini kwani kuna baadhi ya wananchi wanakataa kutoa ushahidi kwa watu wanaojihusisha na vitendo vya uhalifu.

Mapema akizungumza Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mjini, Bora afya Silima Juma aliwapongeza baadhi ya viongozi wa Majimbo wanaotekeleza vizuri Ilani ya CCM ya mwaka 2015/2020 kwa wananchi.

Alisema tokea kumalizika kwa Uchaguzi wa Marudio hali ya kisiasa ndani ya Mkoa huo imeimarika kwani kila mwanachama na wananchi kwa ujumla wamekuwa wakifanya kazi za kujitafutia kipato bila ya usumbufu.

Nao wanachama wa Chama hicho, waliahidi kutoa ushirikiano kwa mambo mbali mbali yatakayoiwezesha CCM kurudi madarakani katika uchaguzi Mkuu ujao.

Walipongeza juhudi zinazofanywa na Rais wa Zanzibar, Dkt. Ali Mohamed Shein na Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania John Pombe Magufuli kwa kutekeleza ahadi mbali mbali walizoahidi wananchi katika kampeni za Uchaguzi uliopita.

Masaburi Atajwa kama mtu aliyelianya jiji la Dar kuwa maarufu duniani

0
0

Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam, Isaya Mwita leo amekiri kuwa mtangulizi wake ambaye amefariki dunia, Didas Masaburi alifanya kazi kubwa ya kuboresha miundombinu ya jiji hilo pamoja na kulitambulisha katika anga za kimataifa.

Meya Mwita ameyasema hayo leo Jijini Dar es Salaam katika safari ya mwisho ya kuuaga mwili wa Marehemu Masaburi aliyefariki dunia usiku wa kuamkia Alhamisi katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.

“Binadamu anapokuwa ameondoka huwa tunazungumza mema aliyoyafanya katika jamii yetu. Mimi Sikuwahi kufanya nae kazi lakini nimekuta kazi ambazo amefanya katika halmashauri ya jiji,” amesema.

Ameongeza kuwa “Moja ya mambo ambayo sitasahau niliyoyakuta aliyoyafanya katika utawala wake ni kuuleta mradi wa DMDP uliolenga kusukuma na kutaka kuboresha maeneo ya miundombinu ya DSM, ukiona kazi aliyoacha mimi ndio naendelea nayo sasa.”

Amesema jambo lingine alilofanya Marehemu Masaburi enzi za utawala wake ni kuleta miji mikubwa duniani kuja kuwekeza na kutoa misaada ya kimaendeleo nchini.

Miongoni mwa majiji aliyoyataja Mwita ni jiji la Hamburg, Shanghai na Torotonto.

“Aliileta hapa miji mikubwa duniani, mimi napata mialiko sasa katika nchi mbalimbali na hii ni matunda ya jitihada zake katika kulitangaza jiji la Dar es Salaam na Tanzania kwa ujumla.” amesema.

Pia Meya Mwita amesema kuwa, Masaburi alifanikiwa kutoa mamlaka na madaraka ya kiutendaji kutoka serikali kuu hadi serikali za mitaa.

“Alipokuwa akiongolea dhana kubwa ya kutoa madaraka kutoka serikali kuu kuja serikali za mitaahili, alikuwa anamaanisha. Jambo hili si jepesi kwa kuwa, halmashauri za mitaa bila ya kuwa na nguvu kubwa haziwezi leta maendeleo mfano Kenya na Uganda halmashauri zake zinauwezo na mamlaka ya kupanga maendeleo,” amesema.

Amesisitiza kuwa “Japo hakufanikiwa kwa kiwango hicho mawazo yake yataishi na mimi kama mrithi wake nitaendelea kuyaenzi.”

Marehemu Didas Masaburi enzi za uhai wake aliwahi kuwa Diwani wa Kata ya Kivukoni, Mwenyekiti wa Jumuiya ya Tawala za Serikali za Mitaa (ALAT).

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumanne ya Octoba 18

Waziri Wa Fedha Aitaka Benki Ya Maendeleo Tib Kujikita Katika Uwekezaji Wa Viwanda

0
0

Waziri wa Fedha na Mipango Dk. Philip Mpango amezindua rasmi bodi ya wakurugenzi ya Benki ya Maendeleo TIB kwa kuiagaiza iweke mikakati yakutaua changamoto mbalimbali zitakozoiwezesha kushiriki kikamilifu katika utelezaji wa Mpango wa pili wa maendeleo wa miaka mitano.

Bodi hiyo imeundwa kufuatia uteuzi wa Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Magufuli uliofanyika mwezi  Julai 2016.

Akizindua bodi hiyo, Dkt. Mpango aliwakumbusha wajumbe kufanya kazi kwa ufanisi na weledi ili kuweza kufanikisha azma ya Rais ya kujenga Tanzania ya Viwanda.
 
“Serikali ya awamu ya tano imejikita kwenye kuhakikisha kuwa uchumi wetu unakuwa ni uchumi wa viwanda. Benki hii ikiwa ni benki ya kisera inawajibu wa kuhakikisha hili linatekelezwa. Kwa mantiki hiyo ni matarajio ya serikali kuona kuwa benki inachochea maendeleo katika nyanja zote muhimu za uendelezaji wa viwanda  vya kuzalisha umeme na miundombinu yake, maji, barabara/usafirishaji na mawasiliano ili  kufikia malengo tarajiwa hususan kuhakikisha kuwa Tanzania inakuwa ni nchi ya uchumi wa kati unaotegemea viwanda ” alisema Dkt. Mpango.

Kwenye maelezo yake ya awali, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Maendeleo TIB, Charles Singili mbali na kuainisha juhudi zinazofanywa na benki hiyo katika kutekeleza mipango ya maendeleo ya Taifa alielezea changamoto mbalimbali zinazoikabili benki hiyo. Changamoto hizo ni pamoja na udogo wa mtaji, uhitaji wa kuwepo kwa fedha za kuandaa miradi, taratibu ndefu za upatikanaji wa vibali vya kukopa kwa taasisi za Serikali na uwepo wa mikopo chechefu.
 
Waziri Mpango pia aliongelea changamoto zinazo ikabili benki hiyo ikiwemo suala la mtaji ambapo alisema, “Serikali ya awamu ya tano inalifanyia kazi suala hili ili kuleta suluhisho endelevu na kuiwezesha benki hii kutimiza malengo ya kuundwa kwake”.

Pia aliisisitizia bodi kuweka mikakati madhubuti katika  kukusanya madeni, kusimamia mikopo inayotolewa  na kuhakikisha kuwa mikopo inayoidhinishwa ni kwa miradi inayo stahili na yenye uwezo wa kurejesha mikopo hiyo.

 Aidha, aliitaka benki hiyo kutokufanya kazi kwa mashinikizo yoyote kutoka kwa watu, wanasiasa, idara au taasisi yoyote; bali wazingatie sheria, kanuni na taratibu zinazoongoza tasnia ya mabenki kama zinavyoelekezwa na Benki Kuu ya Tanzania.
 
Kwa upande wake, Mwenyekiti mpya ya bodi hiyo ilioteuliwa Profesa Palamagamba John Kabudi alimuahidi Waziri kuwa watafanya kazi kwa weledi wa hali ya juu na kutekekeleza maelekezo aliyoyatoa ili kutimiza matarajio ya Serikali na waliowateua.

 Aidha, Mwenyekiti Profesa Kabudi alisema “Tutafanya jitihada ya kutafuta ufumbuzi wa changamoto mbalimbali zinazo ikabili benki yetu, Kwa yale yanayohitaji maelekezo ya ofisi yako hatutasita kuwasiliana na ofisi yako na yale yaliyoko ndani ya mamlaka yetu tutayashughulikia kulingana na taratibu za kiutendaji katika sekta husika.”

Bodi hiyo iliyozinduliwa rasmi mjini Dodoma sasa itaanza kazi zake rasmi kuhakikisha inaiendeleza na kuiimarisha Benki hiyo ya Maendeleo TIB.
 

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Asikitishwa Na Mwekezaji Kubadili Matumizi Ya Kiwanda Na Kukitelekeza

0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amemuagiza Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Bw. Godfrey Zambi kuhakikisha anadhibiti wafanyabiashara wanaonunua korosho kwa njia ya magendo na atakayekamatwa achukuliwe hatua.

Pia amewataka wananchi wa mkoa huo kutouza korosho zao kwa walanguzi maarufu kangomba na badala yake wazipeleke kwenye masoko rasmi ili waweze kupata tija.

Biashara ya kangomba ni mwiko atakayekamatwa amebeba korosho za kangomba atachukuliwa hatua za kisheria na chombo chake cha usafiri kitataifishwa” alisema.

Waziri Mkuu alitoa agizo hilo jana Jumatatu, Oktoba 17, 2016 wakati akizungumza kwa nyakati tofauti na wananchi wa wilaya ya Ruangwa katika mikutano iliyofanyika kwenye vijiji vya Mibure, Namakuku, Ng’imbwa, Chienjele, Mkata, Mitope na Kitandi

“Marufuku kuuza korosho kwa kangomba kwani mnapata hasara kipimo kinachotumika si rasmi. Mkoa kamateni na taifisheni korosho na chombo cha usafiri kitakachotumika kubeba korosho za magendo,” alisema.

Alisema ni vema wakulima wakaachana na biashara ya kangomba kwa sababu haina tija na badala yake wasubiri na kwenda kuuza korosho zao katika minada kwa bei nzuri.

“Mwaka huu korosho itauzika kwa bei ya juu zaidi isiyopungua sh.3500, msikubali kuuza korosho mlizizitolea jasho kwa walanguzi wanaotumia kangomba kwa sh. 1000 huu ni wizi, kwani kile kipimo cha wanachotumia ni sawa na kilo mbili, hivyo unapoteza zaidi ya sh. 6000”. alisema

Katika hatua nyingine Waziri Mkuu aliwasisitiza wananchi hao kuongeza idadi ya mazao ya biashara na kuanza kulima alizeti ambapo wataweza kupata faida ya zaidi ya sh. milioni moja kwenye shamba la ukubwa wa ekari moja. 

Wakati huo huo Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Bw. Godfrey Zambi ametoa miezi miwili kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Ruangwa, Bw. Andrea Chezue kuhakikisha ujenzi wa zahanati ya kijiji cha Mibure unakamilika. “Ndani ya miezi miwili Zahanati iwe imekamilika, tuache kuzungumza sasa ni vitendo tu”amesema.

Awali Waziri Mkuu alitembelea kiwanda cha kukamua mafuta ya ufuta na karanga cha Ilulu kilichoko wilayani Nachingwea na kukuta kimetelekezwa. 

Aliagiza uongozi wa kiwanda kumpelekea nyaraka zote za umiliki. Kiwanda hicho kilibinafsishwa kwa marehemu Abbas Gulamali na sasa kinasimamiwa na familia yake. 

“Nawahitaji Dodoma Oktoba 22 waje na nyaraka zao ili nijue walipokabidhiwa kiwanda hiki walitaka kufanya nini,” alimuagiza Msimamizi wa Kiwanda hicho Dinna Mavumbi kuwajulisha wahusika.

Waziri Mkuu alisema haiwezekani kiwanda hicho kilichojengwa kwa fedha za umma kikatelekezwa bila ya kuendelezwa. 

Alisema baada ya kupitia nyaraka zao ataangalia namna ya kurudisha majengo hayo ya kiwanda kwa Serikali. “Hatuwezi kuacha raslimali hii ikiwa imetelekezwa msituni inaharibika.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
JUMATATU, OKTOBA 17, 2016
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa na Mkewe Mary Majaliwa wakiangalia kiwanda  cha ILULU kilichokuwa kinatengeneza mafuta ambacho muekezaji amekifanya kuwa Ghala nakukitelekeza na watu kuiba vifaa na kufanya uharibifu mkubwa .Kiwanda hicho kipo wilaya ya Rungwe Mkoani Lindi .Waziri Mkuu yupo katika ziara ya kikazi katika wilaya ya Nachingwea na Rungwe Mkoani Lindi(Picha na Chris Mfinanga)

Safari ya Tanzania ya viwanda yaanza......NBS Waagizwa kushirikiana na UNIDO na CTI kuvifanyia utafiti viwanda vidogo nchini

0
0
Serikali imeitaka Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo nchini ikiwemo Shirika la Maendeleo ya Viwanda Duniani (UNIDO) na Shirikisho la Viwanda Nchini (CTI) kuendelea kufanya utafiti ili kubaini idadi na maendeleo ya viwanda vidogo vilivyopo nchini.

Hayo yamesemwa jana  Jijini na Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Dkt Charles Mwijage wakati wa uzinduzi wa matokeo ya Sensa ya Uzalishaji bidhaa Viwandani mwaka 2013.

Dkt Mwijage alisema kuwa katika mataifa yanayoendelea duniani ikiwemo Korea Kusini, Malaysia na Singapore uchumi wa nchi hizo umeweza kukua kwa kiwango kwa juu zaidi kutokana na kuweka mkazo katika kuendeleza viwanda vidogo na vya kati.

Alisema katika kuharakisha kasi ya maendeleo ya viwanda vidogo  nchini, Wizara yake imekusudia kuwajengea hamasa Watanzania kupendelea kujenga viwanda vidogo vidogo na vya kati, kwani kukua kwa sekta ya viwanda nchini kutaisaidia kuinua uchumi wanchi.

“Asilimia 25- 40 ya mazao ya kilimo yanayovunwa huharibika kabla ya kufikishwa kiwandani, katika kukabiliana na hali hiyo Serikali imekusudia kujenga viwanda vidogo vidogo ili kuwawezesha wakulima wapate sehemu nzuri zaidi za kuhifadhi mazao yao” alisema Mwijage.

Aidha, Dkt Mwijage alisema, sekta ya viwanda vidogo vidogo nchini imeendelea kukua kwa kasi nchini ambapo hadi sasa kuna jumla ya viwanda 3800 vilivyoanzishwa nchini kuanzia Novemba 2015 hadi oktoba, 2016.

Katika hatua hiyo Dkt Mwijage alisema kuwa Wizara yake inaendelea kuhamasisha Sekta binafsi kuwekeza katika Sekta ya viwanda vidogo, vya kati na vikubwa ikiwa jukumu kuu la Serikali ni kuhakikisha nchi inakuwa salama na inajenga mazingira wezeshi kwenye sekta binafsi kuzalisha na kufanya biashara.

Naye Mkurugenzi Mkuu Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) Dkt. Albina Chuwa alisema kuwa matokeo hayo yanaonyesha mafanikio katika sekta ya viwanda ikiwemo kuongezeka kwa ajira zipatazo 264,223 nchini na kuchangia uchumi kwa takribani Shilingi bilioni 8.0 kwa mwaka 2013.

Alisema kuwa Takwimu za matokeo ya sensa ya uzalishaji viwandani ni rasmi na kuwataka watunga sera, wanasiasa, viongozi, sekta binafsi na watu binafsi kutumia  matokeo hayo kwa lengo la kuboresha Sekta ya viwanda nchini.

Na Beatrice Lyimo, MAELEZO

Serikali Yatenga Bilioni 70 kumaliza tatizo la ukosefu wa dawa nchini.

0
0
Serikali  imesema imetenga jumla ya shilingi bilioni 70 kwa ajili ya kununua dawa na vifaa tiba ili kumaliza tatizo la ukosefu wa dawa nchini.

Aidha imetenga jumla ya shilingi bilioni 85 kwa ajili ya kupunguza deni linalodaiwa na bohari ya dawa MSD lengo likiwa ni kuhakikisha wananchi wanapata huduma za afya zenye ubora.

Akifungua mkutano mkuu wa waganga wakuu wa mikoa na wilaya zote nchini jana mjini Dodoma makamu wa rais mama Samia Suluhu Hassan alisema dawa hizo zitakazonunuliwa zitaenda moja kwa moja katika vituo vya afya vilivyopo hapa Nchini.

Alisema lengo la serikali ni kupunguza changamoto zilizopo katika sekta ya afya huku akiweka bayana dhamira ya serikali ya kujenga kiwanda cha Dawa katika mkoa wa Simiyu.

Mbali na hilo alizungumzia suala la tiba asili na tiba mbadala na kuitaka Wizara ya Afya maendeleo ya jamii,jinsia,Wazee na Watoto kuhakikisha wanazipa umuhimu kwa kuzitambua na kuzisajili.

Kwa upande wake mwenyekiti wa Waganga hao dokta Sudi Leonard  aliiomba serikali kutatua tatizo la dawa na vifaa tiba lililopo nchini ambalo limekuwa likisababisha malalamiko na manung`uniko kwa wananchi hasa kwa makundi maalum kama wajawazito,watoto,wazee na wenye magonjwa sugu.

Mkutano huo ni wa siku nne wenye lengo la kujadili kwa pamoja masuala mbalimbali yahususyo afya na ustawi wa jamii,kubadilishana uzoefu na kujadili namna ya kutatua changamoto zilizopo ukibeba kauli mbiu isemayo mfumo na huduma bora za afya ni nguzo muhimu kuelekea Tanzania yenye viwanda na uchumi wa kati.

Serikali imeyasainisha mikataba ya kujiendesha kwa faida Mashirika 12 ya Umma.......Yatakayojiendesha kihasara kuchukuliwa hatua.

0
0
Taasisi na Mashirika ya Umma nchini yametakiwa kujiendesha kwa faida huku yakiwa na mtazamo wa kiushindani na makampuni yaliyo chini ya sekta binafsi na kwamba hakuna sababu yoyote kwa mashirika hayo kuendeshwa kwa hasara na kugeuka mzigo kwa serikal

Msajili wa Hazina nchini Bw. Lawrence Mafuru ametoa agizo hilo jana jijini Dar es Salaam wakati akisaini makubaliano ya kiutendaji na taasisi 12 za umma, mkataba unaohusisha malengo ya uendeshaji, namna ya kuhudumia wananchi sambamba na usimamizi bora wa rasilimali za umma zilizopo ndani ya mashirika hayo.

Zoezi hilo la linafanya idadi ya taasisi ambazo msajili wa hazina amesaini nazo makubaliano kufikia thelathini tangu aanze utaratibu huo unaoendana na falsafa ya serikali ya awamu ya tano ya kuhakikisha kunakuwa na uwajibikaji katika taasisi na mashirika ya umma.

Katika maelezo yake Bw. Mafuru amesema haikubaliki kuona makampuni na taasisi za umma zikiendelea kupata hasara kwa kutekeleza majukumu yale yale ambayo taasisi na makampuni binafsi yanapata ufanisi na faida pasipo visingizio vyovyote.

Mauzo ya hisa katika Soko la Hisa Dar (DSE) yaporomoka kwa asilimia 94

0
0
Mauzo ya Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE) yameshuka katika kipindi cha wiki iliyopita kwa 91% kutoka Tsh 32.5 Bilioni na kufikia Tsh 3 Billion. Pia Idadi ya hisa zilizouzwa na kununuliwa zimeshuka kwa 94% kutoka 9 millioni hadi laki 5.

Afisa Masoko Mwandamizi wa DSE, Marry Kinabo, wakati akisungumza na waandishi wa habari jana, alisema kilichochangia kushuka kwa idadi ya mauzo ya hisa ni kutokana na wiki husika kuwa na siku pungufu za kazi na kwamba mauzo ya hisa hizo yalifanyika kuanzia Jumatatu hadi Alhamisi ya tarehe 13 ambapo siku iliyofuata (Ijumaa) ilikuwa siku kuu ya kumbukumbu ya Kifo cha Baba wa Taifa Mwl. Julias Kambarage Nyerere.

Vile vile, Kinabo alisema kuwa, kutokana na idadi ya mauzo ya hisa kushuka, kumepelekea ukubwa wa mtaji wa soko hilo kushuka kwa 3% kutoka Trilioni 21.49 hadi Trilioni 20.8

Aidha, alitaja kampuni zinazoongoza kwa idadi ya hisa zilizouzwa na kununuliwa kuwa ni CRDB kwa 53%, TCC 41% na TBL 4%.

Hata hivyo, alisema mtaji wa makampuni ya ndani umebaki kwenye kiwango kile kile cha Trilioni 8.13 wakati viashiria katika Sekta ya viwanda (IA), Sekta ya huduma za kibenki na kifedha (BI) na Sekta ya huduma za kibiashara (CS) wiki hii umebaki kama awali.

Watu 13 Kizimbani Kwa Mauaji ya Watafiti Dodoma

0
0

Wanawake wanne na wanaume tisa wamefikishwa mahakamani mjini Dodoma na kusomewa mashtaka ya mauaji ya watafiti wa Chuo cha Utafiti wa Udongo na Maendeleo ya Ardhi kilichopo Selian mkoani Arusha. 

Mbele ya Hakimu Mkazi, Joseph Fovo washtakiwa hawakutakiwa kujibu chochote kwa kuwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Dodoma haina mamlaka kisheria kusikiliza kesi hiyo isipokuwa Mahakama Kuu. 

Wanadaiwa kuwaua Nicas Mag- azine, Theresia Nguma na Faraji Mafuru, Oktoba Mosi kwenye Kijiji cha Iringa Mvumi wilayani Chamwino. 

Wakili wa Serikali, Beatrice Nsana aliwasomea mashtaka hayo jana akidai walitenda kosa hilo la jinai kinyume na kifungu cha 196 na 197 cha Sheria ya Kanuni ya Adhabu na marekebisho yake ya mwaka 2002. 

Washtakiwa hao ni Cecilia Mwalu, Dorca Mbehu, Edna Nuno, Grace Masaulwa, Juma Madeha, Albert Chimanga, Sosteness Mseche, Julius Chimanga, David Chimanga, Lazaro Kwanga, Yoramu Samamba, Edward Lungwa na Simon Samamba, wote wakazi wa Kijiji cha Iringa Mvumi.

Kesi hiyo namba 36/2016 iliahirishwa hadi Oktoba 31. Nsana alidai upelelezi haujakamilika. 

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkinga Afikishwa Mahakamani Kwa Kosa La Kumtishia Bastola Askari wa Usalama Barabarani (Trafiki)

0
0
Ilikuwa kama mchezo wa kuigiza kwenye Mahakama ya Hakimu Mkazi Morogoro baada ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkinga mkoani Tanga, Emmanuel Mkumbo kufikishwa ili apandishwe kizimbani kujibu mashtaka sita, likiwamo la kutishia kuua. 

Tukio zima la kumpeleka mahakamani, kumpandisha kizimbani na kumsomea mashtaka kwa muda wa dakika 30 hivi lilitawaliwa na vituko. Kwanza, ni jaribio la kuwaficha wanahabari. 

Kabla ya kufikishwa mahakamani, Polisi mkoani Morogoro iliwaarifu wanahabari kuwa ingetoa taarifa kuhusu mkurugenzi huyo lakini saa 4:30 asubuhi wakati Kamanda wa Polisi mkoani Morogoro, Ulrich Matei akijiandaa kuzungumza nao, alipigiwa simu akatoka nje ya ukumbi na aliporejea alisema hawezi kutoa taarifa tena na akaondoka. 

Waandishi walipofika mahakamani saa 5:00 asubuhi walikuta Kamanda Matei akishuka kwenye gari na alipanda tena akasogea kando kuzungumza na baadhi ya askari wake. 

Pili, baada ya hakimu kumaliza kusikiliza kesi hiyo, Mkumbo hakurudishwa mahabusu mahakamani hapo kama ilivyo ada ili kusubiri utaratibu mwingine badala yake mshtakiwa huyo alihamishiwa chumba cha hakimu ambacho hakikuwa na kesi inayoendelea. 

Humo ndugu zake walimpelekea koti kubwa jeusi na kofia aina ya pama, hivyo alitoka akiwa tofauti na alivyoingia akiwa na fulana yenye rangi nyeupe, bluu na nyeusi. Baada ya kuvaa alitoka akiwa amezingirwa na polisi, huku ndugu wakiwazuia wanahabari kumpiga picha. 

Mashtaka dhidi yake
Mkumbo ambaye ni mkazi wa Tegeta jijini Dar es Salaam alipandishwa kizimbani kujibu mashtaka sita, la kwanza likiwa la kutishia kuua kwa bastola na la pili ni la usalama barabarani lenye makosa matano.

Alisomewa mashtaka hayo na mawakili wa Serikali Sunday Hyera na Edgar Bantulaki. Katika shtaka la kwanza, mbele ya hakimu Agripina Kimaze anadaiwa Oktoba 15, saa 10:30 jioni alitenda kosa la kutishia kuua eneo la Mkambarani, Manispaa ya Morogoro.

Anadaiwa katika shtaka hilo la jinai namba 226 la mwaka 2016, alitishia kumuua kwa bastola askari namba 5057, Koplo Tuti Ndaga wa Kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Morogoro, kinyume na kifungu namba 89 (1),(2),(a) cha Sheria ya Kanuni ya Adhabu namba16. 

Katika shtaka la pili la ukiukwaji wa sheria za usalama barabarani lenye makosa matano, ilidaiwa kuwa; kwanza, siku na muda huo eneo la Mbuyuni Mkambalani, mshtakiwa alikuwa akiendesha gari aina ya Toyota Prado lenye rangi ya kijivu bila kuwa na leseni. 

Pili, ilidaiwa alikuwa akiendesha gari hilo ambalo halikuwa na bima; tatu, alikutwa akiendesha kwa mwendo kasi; na nne, alikataa kupeleka gari Kituo cha Polisi cha Kingoluwira kama alivyoamriwa na askari, WP namba 5392 Sajenti Anna. 

Ilidaiwa katika shtaka la tano kwamba, wakati akiendesha alisimamisha gari katikati ya barabara kuu ya Morogoro-Dar es Salaam kwa uzembe, bila uangalifu wala kuzingatia watumiaji wengine wa barabara. Mkurugenzi huyo alikana mashtaka yote yanayomkabili.

Hakimu Kimaze alitoa masharti ya dhamana kwa mshtakiwa kwamba awe na mdhamini mmoja kwa kila shtaka, yaani shtaka la jinai na la usalama barabarani lenye makosa matano, wote wawe wakazi wa Morogoro na mmoja akitakiwa kuweka dhamana ya Sh500,000 kwa kosa la kwanza na Sh1 milioni kwa kosa la pili. 

Mshtakiwa alikidhi masharti ya dhamana na kuachiwa huru, huku gari likiendelea kushikiliwa kwenye Kituo Kikuu cha Polisi Mkoa wa Morogoro.

Hakimu Kimaze aliahirisha shauri hilo hadi Oktoba 31, usikilizwaji wa awali utakapoanza baada ya upande wa mashtaka kudai upelelezi umekamilika.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images