Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Rais Magufuli Atishia kumfukuza kazi mtoto wa dada yake

$
0
0
Rais Dkt John Pombe Magufuli ametishia kufukuza kazi mtoto wa dada yake kutokana na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) kutopeleka umeme katika kiwanda kipya cha kusindika matunda cha Bakhresa.

Rais Magufuli alisema jana alipokuwa akifungua rasmi kiwanda cha kusindika matunda cha Bakhresa kilichopo Mwandege, Mkuranga mkoani Pwani.

Wakati wa hafla hiyo ya ufunguzi, kiongozi mmoja wa kiwanda hicho akieleza changamoto wanazokumbana nazo alisema kuwa tatizo linalowakabili ni la umeme ambapo wameongea na TANESCO lakini hadi leo umeme haijafikishwa kiwandani hapo hivyo kuwalazimu kutumia jenereta kuendesha mitambo kitu kinachopelekea kuongezeka kwa gharama za uzalishaji.

Aliposimama kuhutubia Rais Magufuli aliuliza kama kuna kiongozi yeyote wa TANESCO mkoa wa Pwani ndipo akasimama mtoto wa dada yake. Rais Magufuli akamwambia anafahamu kuwa amefanya kazi nzuri alipokuwa Kagera na Tanga na kuwa anataka ahakikishe umeme unafika katika kiwanda hicho la si hivyo ataanza kumtumbua yeye ambaye ni mtoto wa dada yake.

Rais Magufuli alielekeza maswali mawili kwa TANESCO wakati wa hotuba yake, kwanza, kama TANESCO wanania ya kufanya biashara, kwanini hawapeleki umeme kiwandani hapo kwa sababu ni fursa ya kibiashara, pili aliuliza kama TANESCO wanania ya kuona Tanzania inakuwa ya viwanda, kama wanania, kwanini hawapeleki umeme kiwandani hapo.

Rais Magufuli ametoa miezi miwili kwa TANESCO kuhakikisha kuwa wanafikisha umeme kiwandani hapo kama wanataka kuendelea na kazi zao.

Kuhusu ombi la uongozi wa kiwanda hicho kutumia  gesi asilia inayopita jirani na kiwanda hicho, Rais Magufuli alisema kuwa watakaa na Wizara ni Nishati na Madini na Wizara ya Viwanda na Biashara kuona namna wanaweza kulishughulikia hilo.

CUF Hatarini Kufutiwa Usajili

$
0
0
Mgogoro unaoiandama CUF huenda ukailetea balaa zaidi, baada ya kuwapo kwa taarifa kuwa huenda ikafutwa kama itazidi kukomalia msimamo ilionao wa kutotaka ushauri.

Mgogoro huo umekipasua chama hicho na kuwa makundi mawili, moja likiongozwa na Profesa Ibrahim Lipumba na jingine likiwa chini ya Katibu Mkuu, Maalim Seif Sharif Hamad.

Profesa Lipumba aliyevuliwa uanachama na Baraza Kuu la Uongozi amejitwalia ofisi kuu za chama hicho zilizopo Buguruni jijini Dar es Salaam, wakati Maalim Seif na wanaomuunga mkono wako makao makuu ya chama hicho Vuga visiwani Zanzibar.

Msajili Msaidizi Sisty Nyahoza kupitia mahojiano yake na kituo cha Channel Ten, ametumia nafasi hiyo kumtambua Profesa Lipumba kuwa bado ni mwenyekiti halali wa CUF na kwamba ofisi hiyo inayo mamlaka ya kukifuta chama chochote.

Alipoulizwa kuwa migogoro hii inayoendelea haiwezi kusababisha chama kikafutwa, Nyahoza amesema vipo vyama viwili vilivyowahi kufutwa usajili wake kwa sababu ya migogoro ya uongozi na kuvitaja vyama hivyo kuwa ni chama cha Pona kilichofutwa Mei 2001.

“Kilikuwa na mgogoro wa uongozi, ambao ulifanya washindwe kufanya uchaguzi wa viongozi wa kitaifa, kingine ni chama cha TPP, vilifutwa kwa hivyo migogoro inaweza ikavunja chama na kikafutwa,” amesema.

RIWAYA: Sorry Madam - Sehemu ya 65 & 66 (Riwaya inawafaa kuanzia miaka 18 na kuendelea )

$
0
0
Mtunzi : Eddazaria g.Msulwa

Ilioishia
Nilimuuliza dorecy na kumfanya phidaya kunitazama kwa jicho kali lililo jaa hasira
“ndio, ila kuna ishu khalid alitaka kukufanyia wewe na phidaya akaiingilia kati na kuwa adui mwengine wa khalid”
“jambo gani hilo?”
Hata kabla dorecy hajanijibu tukasikia milio mingi ya risasi kwenye kordo yetu huku kelele za watu wagonjwa na manesi wakike zikisikia jambo lililo tushtua sote ndani ya chumba

Endelea
Milio ya risasi ikaendelea kurindima nje ya chumba tulichopo na kuzidi kutupagawisha sote tuliopo ndani ya chumb hichi, wasiwasi mwingi ukawa kwa dorecy ambaye fika anaoenekana kuchanganyikiwa
“eddy hao ni watu wa mume wangu”
Dorecy alizungumza huku mwili mzima ukimtetemeka, nikapiga hatua za haraka hadi dirishani na kuchungulia chini ambapo kuna umbali wa ghorofa mbili kwenda chini.
“hatuwezi kutoka humu ndani”
Nilizungumza huku nikiwatazama dorery na phidaya
“itakuwaje sasa?”

Phidaya alizungumza huku machozi yakimwagika kwa wingi.Nikapiga hatua hadi mlangoni, nikachungulia kwenye sehemu ya kuingizia funguo, nikamshuhudia jamaa mmoja akitandika risasi ya kichwa mzee mmoja aliye ambiwa alale chini ila akaleta kiherehe cha kujinyanyua, ndipo akakutana na maafa hayo ambayo ni yakinyama sana.

Gafla simu ya phidaya ikaita na kutufanya sote kumgeukia na kumtazama kwa macho ya mshangao, kwa kiwewe alicho nacho akashindwa hata kuikata na kujikuta akiiachia na kuanguka chini, nikachungulia tena kwenye tobo la kuingizia funguo na kumuona jamaa aliye muua mzee, akiutazama mlango wetu kwa umakini.
“ingieni bafuni”

Nilizungumza kwa sauti ya chinichini, dorecy akamshika mkono phidaya na kukimbilia kwenye bafu liilopo humu ndani ya chumba changu.Jamaa akapiga hatua hadi ulipo mlango uku bunduki yake aina ya ‘short gun’ ikiwa mkononi mwake.

Nikajibanza nyuma ya mlango, huku mapigo ya moyo yakinienda mbio kiasi kwani bado sijaiamini afya yangu kwa kiasi kikubwa kutokana na majeraha ya risasi yaliyopo mwilini mwangu.Mlango taratibu ukafunguliwa, nikaanza kuona kiatu cheusi kikitangulia mbele, jamaa akasimama kwa muda, gafla simu ya phidaya iliyo anguka chini ikaanza kuita tena na kumfanya jamaa kupiga hatua za taratibu hadi sehemu ilipo anguka simu na kuiokota.Mapigo ya moyo yakazidi kunienda mbio, kwani endapo jamaa atageuka nyuma nilazima ataniona.Akaitazama simu ya phidaya kwa muda na kuitupa chini na kuchanguka, akatazama mlango wa kuingilia bafuni ambapo ndani yake yupo phidaya na dorecy

Simu ya jamaa ikaita, akaitoa kwenye koti lake, akaipokea nakuiweka sikioni mwake, akazungumza kwa lugha ya kiarabu, nikastukia kumuona jamaa akichomoka kwa kasi, ndani ya chumba pasipo kuniona nyuma ya mlango, ving’ora vya gari za polisi, nikaanza kuvisikia na kunifanya nishushe pumzi nyingi, na kujikalia chini, huku jasho jingi likimwagika.Ndani ya dakika kadaa askari kadhaa wakawa wameingia katika sehemu tulipo, dorecy na phidaya wakatoka bafuni, askari na madaktari walio salimika katika vamizi la majambazi hawa
                                                                                                  ***
Wagonjwa tulio salimika tukahamishwa kwenye hospitali moja, inayo milikiwa na jeshi la nchi ya philipines, matiibabu yangu hayakuchukua muda mrefu sana, nikaruhusiwa kutoka hospitalini na kuhamia kwenye hoteli ambayo phidaya anaishi kwa siri sana, na amelipiwa gharama zote na dorecy ambaye tayari amerudi kwa mume wake.
“phidaya,itatubidi turudi tanzania”

Nilizungumza huku macho yangu yakimtazama phidaya aliye jilalia kiuvivu kwenye kitanda, huku akiwa tumbo wazi akilichezea chezea kwa kiganja chake tumbo lake lenye kiumbe ndani
“si usubiri niweze kujifungua kwanza”
“hatuwezi kuishi hapa, pasipo sisi kuwa na kazi, unadhani tutayamudu vipi haya maisha?”
“sawa mume wangu, je tukirudi huko tanzania, tutafikia wapi wakati umesha sema kwamba mama yako alitekwa na baba yako mkubwa”

Nikamtazama phidaya kwa muda, kwani kitu alicho kizungumza kinamaana kubwa sana kwangu, isitoshe sijajua ni hali gani inayo endela kati ya mzee godwin na mama yangu.Nikanyanyuka taratibu na kuisogelea computer iliyopo kwenye meza humu chumbani kwetu, ambayo imeunganishwa na huduma ya internet.Nikaiwasha taratibu, baada ya muda nikafungua mtandao wa google
“unataka kufanya nini?” phidaya alizungumza huku akipiga hatua na kuja kukaa kwenye kiti nilicho kikalia mimi
“kuna mtu nataka kumtafuta”
“nani?”
“baba yangu mzazi, anaishi afrika kusini”
“mmmm sawa”

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumamosi ya Octoba 8

Agizo la Rais Magufuli kwa Mabalozi wanaoiwakilisha Tanzania katika nchi nyingine

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, jana tarehe 07 Oktoba, 2016 amekutana na Mabalozi wanaoiwakilisha Tanzania katika nchi mbalimbali duniani ambapo pamoja na mambo mengine ametaka utekelezaji wa diplomasia ya uchumi utiliwe mkazo katika uwekezaji kwenye sekta ya viwanda.

Katika Mkutano huo uliofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa na Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan na Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa, Rais Magufuli aliyehutubia na kuongoza majadiliano juu ya masuala mbalimbali ya shughuli za mabalozi, alisema Tanzania imeweka dhamira ya kuikuza sekta ya viwanda kutoka ukuaji wa asilimia 7.3 hadi kufikia asilimia 15 ifikapo mwaka 2021 na kuzalisha ajira kwa asilimia 40.

“Sasa nimeona niwaite waheshimiwa Mabalozi ili tuelewane, mjue mwelekeo tunaoutaka na mjue ni namna gani mtakavyoshiriki kuhamasisha uwekezaji wa viwanda.

“Nataka badala ya kubaki mmejifungia ofisini, mtoke mwende mkawatafute wawekezaji waje wawekeze katika viwanda ili nchi yetu inufaike kwa watu wetu kupata ajira, Serikali kukusanya kodi na tuinue maendeleo yetu” alisema Rais Magufuli.

Maeneo mengine ambayo Rais Magufuli ametaka Mabalozi wayafanyie kazi ni kutangaza na kuwavutia watalii kuja hapa nchini, kufanyia kazi fursa zote zenye manufaa kwa Tanzania katika nchi wanakowakilisha, kulinda mali za nchi zilizopo katika nchi hizo na kufuatilia utekelezaji wa mikataba ya biashara na uwekezaji inayofanywa kati ya Tanzania na nchi wanakowakilisha.

Pia Rais Magufuli aliwataka waheshimiwa Mabalozi wote kufanya kazi kwa juhudi, kuondoa kasoro za utendaji kazi ambazo zimekuwa zikilalamikiwa katika ofisi zao na kubana matumizi ya fedha yasiyokuwa ya lazima.

Dkt. Magufuli aliitaka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kujipanga na kudhibiti mianya yote ya matumizi mabaya ya fedha za umma ambazo zimekuwa zikitumika katika safari za nje ya nchi na matumizi mengine yasiyo ya lazima, pamoja na kuhakikisha watumishi wote ambao wapo katika ofisi za ubalozi kwenye nchi mbalimbali bila sababu za msingi wanarejeshwa nchini ili kupunguza mzigo wa gharama kwa Serikali.

“Kuna wafanyakazi wapo kwenye Balozi zetu wakati hata sifa za kuwa katika nafasi wanazoshikilia hawana, ilifika mahali mtu akiharibu hapa nyumbani anapangiwa ubalozini.

“Wakati mwingine unakuta ubalozi wa Tanzania kwenye nchi fulani una idadi kubwa ya wafanyakazi kuliko mahitaji ya ubalozi huo, haiwezekani” alisisitiza Rais Magufuli.

Hata hivyo Dkt. Magufuli aliwapongeza Mabalozi wote wa Tanzania kwa kazi wanazozifanya kwenye nchi wanazowakilisha na amewahakikishia kuwa Serikali ina matumaini nao na inawategemea kuwa wataendelea kuiwakilisha na kuitangaza vizuri Tanzania.

Mkutano huo pia ulihuduriwa na Viongozi mbalimbali wakiwemo Mawaziri, Naibu Mawaziri, Makatibu Wakuu, Naibu Makatibu Wakuu, Wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama, Viongozi wa Taasisi mbalimbali na Wakurugenzi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam

Majibu ya Daktari: Kijana Said Ally Aliyetobolewa Macho Na Scorpion Hawezi Kuona Tena

$
0
0
Na Dotto Mwaibale
MAJONZI na vilio vilitawala ofisini kwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda wakati Kijna Said Mrisho anayedaiwa kujeruhiwa na kutobolewa macho na Salumu Henjelewe maarufu kama Scorpion Buguruni Sheli alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari mbele ya mkuu wa mkoa Dar es Salaam jana asubuhi kuwa hata ona tena katika maisha yake kufuatia kujeruhiwa vibaya kwenye mishipa ya macho na mtuhumiwa huyo na kupoteza uwezekano wa kuona.

"Nilijua ipo siku moja nitakufa lakini sikutegemea kuwa nitakuja kutolewa macho yangu kikatili kiasi hiki sijui mungu anampango gani na mimi wala sijui nini  hatima ya maisha yangu" alisema Mrisho ambapo ukumbi mzima uligubikwa na ukimya sanjari  na simanzi huku mke wake Stara Soud akishindwa kujizuia kulia.

Mrisho alisema anamshukuru sana Rais John Magufuli na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda kwa jitihada walizofanya za kumsaidia kupata matibabu lakini imeshindikana kwa kuwa mishipa yote yenye uwezo wa kumfanya aweze kuona imeharibiwa vibaya na mtuhumiwa huyo hivyo hataweza kuona tena katika maisha yake.
 
"Kama mishipa isingeharibiwa kwa visu mama yangu kipenzi Halima Lwiza Abdallah alikuwa yupo tayari kutoa jicho lake moja kwa ajili ya kunisaidia niweze kuona lakini kwa bahati mbaya hilo halitawezekana baada ya madaktari kunieleza kuwa mishipa ya macho yangu imeharibiwa" alisema Mrisho kwa huzuni na kuanza kulia.
 
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda alisema wamepokea kwa huzuni taarifa hiyo ya madaktari na kumuomba Mrisho asikate tamaa kwani serikali itaangalia jinsi ya kumsaidia.
 
Makonda alisema serikali itatoa sh.milioni 10 kama mtaji ili ziweze  kumsaidia wakati wakiangalia namna ya kuwashirikisha watu wengine kwa ajili ya kumsaidia.

Makonda alisema serikali itamsaidia kufanyiwa upasuaji wa kuwekewa macho ya bandia ili awe katika mwonekano wa kawaida ingawa atakuwa haoni.

"Pamoja na kumpatia kiasi hicho cha fedha katika kipindi hiki cha mpito ambacho atakuwa akihitaji kwenda katika matibabu na sehemu zingine tutakuwa tukimsaidia usafari wa kwenda maeneo hayo" alisema Makonda.
Kijana Said Mrisho anayedaiwa kujeruhiwa na kutobolewa macho na Salumu Henjelewe maarufu kama Scorpion (kulia), akilia kwa uchungu wakati akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda jana. Kushoto ni mke wake, Stara Soud
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam akiwa ameinama kwa uchungu wakati kijana huyo alipokuwa akizungumza na wanahabari.
 Mganga Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Grace Magembe (kushoto), akimfariji kijana Said Mrisho.

Bodi ya Mikopo (HESLB ) Yasitisha Mikopo Ya Walimu Wanafunzi Waliompiga Mwanafunzi Mbeya

$
0
0

Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) inautaarifu umma kuwa imesitisha mikopo ya elimu ya juu iliyokuwa ikitolewa kwa walimu-wanafunzi wanne waliosimamishwa masomo kwa kuhusika katika tukio la kumshambulia na kumuumiza mwanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Kutwa ya Mbeya. Walimu hao walikuwa katika mafunzo ya vitendo.

1. Frank Msigwa - Chuo Kikuu Kishiriki cha Dar es Salaam (DUCE)

2. John Deo- Chuo Kikuu Kishiriki cha Dar es Salaam (DUCE)

3. Evance Sanga - Chuo Kikuu Kishiriki cha Dar es Salaam (DUCE)

4. Sante Gwamaka - Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere (MNMA)

Kwa utovu huo wa nidhamu, wanafunzi hao wamesimamishwa masomo na mamlaka husika kwa hiyo wamepoteza sifa za kuendelea kupokea mikopo. 

Mikataba inayosainiwa na wanufaika wa mikopo inawataka wanufaika kuzingatia masharti kadhaa ikiwa ni pamoja na nidhamu na kufuata sheria na taratibu za vyuo na mamlaka halali.

Aidha, kwa mujibu wa taratibu za kukopeshwa, wanafunzi hawa watatakiwa kuanza kurejesha kiasi walichokopeshwa mara moja.

Bodi ya Mikopo inawakumbusha wanufaika wanaoendelea masomo kuzingatia masharti ya ukopeshwaji na kuheshimu sheria, kanuni taratibu na kuwa mfano mwema katika jamii. Mikopo na ruzuku zinazotolewa na Serikali ni kwa ajili ya kuwaandaa kuwa raia wema, waadilifu, na wachapa kazi ili kujenga uchumi imara na ustawi kwa wote.

Imetolewa na:
Abdul-Razaq Badru
Mkurugenzi Mtendaji

Ijumaa, Oktoba 7, 2016

Ahukumiwa Kifungo cha Maisha Jela kwa KUMLAWITI Mgoni Wake Aliyemfumania na Mkewe

$
0
0
Mahakama ya Wilaya ya Ilala imemhukumu kifungo cha maisha jela, Erick Kasila (39) baada ya kupatikana na hatia katika mashtaka matatu likiwamo la kumlawiti mwanamume kwa madai kuwa alimfumania gesti na akiwa na mke wake.

Kasila anadaiwa kumlawiti Idd Kambi katika nyumba ya kulala Wageni ya Maembe, Yombo Kiwalani, Wilaya ya Ilala na kumpiga picha za utupu na kutisha kunitumia katika mitandao ya kijamiina kumnyang’anya nguo alizovaa, fedha, laptop na viatu.

Mshtakiwa wa pili katika kesi hiyo, Juma Richard (31) alihukumiwa kifungo cha miaka 14 jela baada ya kupatikana na hatia ya kumlazimisha mlalamikaji kumnyonya uume wake na kumtaka kusaini karatasi ya ahadi ya Sh1 milioni ili asisambaze picha walizompiga wakati wakimlawiti, ambazo hata hivyo, walizisambaza katika mitandao ya kijamii.

Akisoma hukumu hiyo jana, Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama hiyo, Said Mkasiwa alisema ameridhishwa na ushahidi wa mashahidi watano dhidi ya washtakiwa na vielelezo vya picha zinazoonyesha mlalamikaji alikuwa analawitiwa, nyingine zikionyesha mshtakiwa akimlazimisha mlalamikaji amnyonye sehemu zake za siri.

Akipitia baadhi ya ushahidi uliotolewa mahakamani hapo, Hakimu Mkasiwa alisema kulawitiwa kwa mwanamume huyo ni baada ya kukutwa na Sanifa Bakari ambaye ni mke wa Kasila.

Kabla ya hukumu hiyo, upande wa mashtaka ukiongozwa na Wakili wa Serikali, Silvia Mitanto uliiomba Mahakama kutoa adhabu kali dhidi ya washtakiwa hao kwa kitendo walichokifanya ambacho kimemuathiri mlalamikaji kisaikolojia.

Washtakiwa walipopewa nafasi ya kujitetea kwa nini wasipewe adhabu kali, walishindwa na badala yake waliomba nakala ya hukumu.

Ofisi Ya Makao Makuu Ya Hifadhi Ya Serengeti Yateketea Kwa Moto Leo Jumamosi.

Rais Magufuli Mgeni Rasmi Kwenye Sherehe Za Mabohora Kuadhimisha Mwaka Mpya Wa Kiislamu 1438 Msikiti Wa Bohota Upanda, Dar Es Salaam, Leo

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 08 Oktoba, 2016 amehutubia katika tamasha la madhehebu ya Bohora ambayo yanafanya maadhimisho ya dunia ya sikukuu ya mwaka mpya wa Kiislam Jijini Dar es Salaam.

Maadhimisho hayo yamewaleta nchini wafuasi zaidi ya 30,000 kutoka nchi mbalimbali duniani na kuongozwa na Kiongozi Mkuu wa Madhehebu ya Bohora Duniani Mtukufu Dkt. Syedna Mufaddal Saifuddin Saheb (TUS).

Akihutubia wafuasi wa Bohora katika Msikiti wa Hakimi uliopo Upanga Jijini Dar es Salaam, Rais Magufuli amemshukuru Kiongozi Mkuu wa Bohora kwa kukubali kufanya maadhimisho ya mwaka mpya wa madhehebu hayo hapa nchini na amewashukuru na kuwapongeza wafuasi wa madhehebu hayo kwa kukubali kuja hapa nchini na kukaa kwa siku zote za maadhimisho yaani kuanzia tarehe 02 Oktoba, 2016 walipoanza hadi tarehe 11 Oktoba, 2016 watakapomaliza.

Rais Magufuli, amewapongeza viongozi na wafuasi wa madhehebu ya Bohora kwa kutumia maadhimisho haya kuhimiza amani, upendo na mshikamano na pia amewashukuru kwa kushiriki katika maendeleo ya kijamii na kiuchumi ikiwemo mchango Dola za Marekani 53,000 zilizotolewa na Kiongozi Mkuu wa Bohora kwa Serikali kwa ajili ya kuchangia kampeni ya utengenezaji wa madawati, na kuwaleta madaktari kutoka Hospitali ya Saifee ya India waliotoa matibabu bure kwa wananchi wa Arusha.

Aidha, Rais Magufuli amewakaribisha wafuasi wa Bohora duniani kuja kuwekeza hapa nchini katika sekta mbalimbali zikiwemo Kilimo, Uvuvi, Misitu, Mifugo, Madini na Gesi kwani soko la uhakika lipo ndani ya nchi, katika Jumuiya ya Afrika Mashariki na Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) yenye watu takribani milioni 400.

Kwa upande wake Kiongozi Mkuu wa Madhehebu ya Bohora Dkt. Syedna Mufaddal Saifuddin Saheb (TUS) amemshukuru Rais Magufuli kwa kuungana na wafuasi wa madhehebu ya Bohora katika maadhimisho hayo na amesema wafuasi wote wa Bohora wanahimizwa kushirikiana na mamlaka zilizopo katika nchi wanazoishi, kuwa raia wema na kufuata sheria.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John pombe Magufuli akiagana  na Kiongozi wa Jumuiya ya Mabohora Duniani, Dk Seydna Mufaddal Saifuddin kwenye msikiti wa Bohora ulioko Upanga jijini Dar es salaam ambako alikuwa mgeni rasmi kwenye sherehe za Mabohora kuadhimisha Mwaka Mpya wa Kiislamu wa 1438 leo Oktoba 8, 2016
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John pombe Magufuli akisalimiana na Kiongozi wa Jumuiya ya  Mabohora Duniani, Dk Seydna Mufaddal Saifuddin mara alipowasili kwenye msikiti wa Bohora ulioko Upanga jijini Dar es salaam  ambako alikuwa mgeni rasmi kwenye sherehe za Mabohora kuadhimisha Mwaka Mpya wa Kiislamu wa 1438 leo Oktoba 8, 2016
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John pombe Magufuli akiwasili  kwenye msikiti wa Bohora ulioko Upanga  jijini Dar es salaam ambako alikuwa mgeni rasmi kwenye sherehe za Mabohora kuadhimisha Mwaka Mpya wa Kiislamu wa 1438 leo Oktoba 8, 2016

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumapili ya Octoba 9

Shule Nyingine 12 Zafutwa

$
0
0
Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi imezifuta shule nyingine za awali na msingi nchini ambazo hazijasajiliwa zaidi ya 10 kuanzia Desemba mwaka jana. Aidha, shule tano kati ya 40 zilizokuwa zimefutiwa usajili zimekamilisha taratibu na kurejeshewa usajili wake.

Kaimu Mkurugenzi wa Usajili wa Shule katika wizara hiyo, Khadija Mcheka amesema mpaka sasa bado wanaendelea na ukaguzi kubaini shule ambazo hazijasajiliwa.

Alizitaja shule ambazo zimefutwa kwa kutosajiliwa kuwa ni Mwandai Junior Academy, shule ya msingi DACETE, shule za msingi Malaika na Fares Kisingo (FK) za wilaya ya Kinondoni. Nyingine ni shule ya msingi The Unity, shule ya sekondari Jotac iliyopo eneo la Kipunguni, Verena iliyopo eneo la Pugu zote wilaya ya Ilala, Exodus iliyopo Kigamboni na Havard Junior ya wilaya ya Temeke.

Alisema shule nyingine zilizofutwa kabisa ni shule ya sekondari ya Kahe ambayo imefutwa kutokana na wamiliki kushindwa kuiendesha na pia majengo yake yamebadilishiwa matumizi. 

Alisema shule nyingine za Deogrolius International School iliyopo Kitunda, Desinity na Almustakim zote za jijini Dar es Salaam nazo zimefutiwa usajili. Alisema awali yalitolewa majina ya wamiliki.

Mcheka alisema pia shule mbili hazitakiwi kuwa za bweni ambazo ni Heritage iliyopo Banana Ukonga na Hellens iliyopo Kinondoni.

Akizungumzia shule zilizorejeshewa usajili, alisema ni Gisera, Rose Land, Conerstone na Grace za jijini Dar es Salaam na Must Lead na Qunu zilizopo mkoani Pwani huku shule ya Fountain Gate ikifutiwa usajili wa kuendesha shughuli za bweni.

Akifafanua kuhusu shule ya Coner Stone alisema baada ya ukaguzi na kufutiwa usajili kuanzia mwezi Julai zipo shule ambazo zilikamilisha utaratibu na kurejeshewa usajili, na kwamba hakuna shule iliyoelezwa kufutiwa usajili kwa uongo.

“Kuhusu shule zinazolalamika kutangazwa kimakosa si kweli isipokuwa jambo lililofanyika baada ya kuwapelekea barua kuwataka kutawanya wanafunzi baada ya kufutiwa usajili walikamilisha utaratibu ndipo wakasajiliwa,“ alisisitiza.

Alisema ukaguzi huo wa shule unaendelea katika mikoa yote nchini kwa kuwatumia wakaguzi wa Kanda na watakaobainika watafutwa mpaka watakapokidhi vigezo vinavyotakiwa. 

Hivi karibuni Mcheka alisema kuanzia Julai hadi Desemba mwaka jana, waligundua kuwepo kwa shule 35 zisizosajiliwa na kuzifuta na baadaye walizifungia shule nyingine 12. 

Mcheka alisema shule zinaweza kufutwa kwa sababu mbili zikiwamo zilizosajiliwa, lakini zikakiuka vigezo ambapo zikitimiza vigezo zinaweza kuomba upya usajili na kupewa.

“Lakini aina ya pili ni zile ambazo hazijasajiliwa na zinaendeshwa kinyume cha sheria ambazo nazo zikifuata taratibu zikatimiza vigezo zinaweza kupewa usajili,” alifafanua Kaimu Mkurugenzi huyo wa Usajili wa Shule.

Alisema katika kipindi hicho mpaka Agosti mwaka huu baada ya tangazo la kuwataka kusajiliwa shule za awali nne, zile za awali na msingi 105 na sekondari 19, walifika wizarani kwa ajili ya kupata taratibu za usajili ambapo zipo zilizosajiliwa na nyingine kupewa vibali.

Alisema katika usajili, wapo waliokidhi viwango na wengine walipatiwa maelekezo na kupatiwa vibali vya kutumia majengo yaliyopo huku wengine wakipewa vibali vya kujenga majengo ya shule kabla ya kupata usajili. 

Alisema kwa shule walizozifungia, waliwaandikia barua za kuwafungia na kuwataka kuhakikisha wanawatawanya wanafunzi katika shule zilizosajiliwa kwa gharama zao bila kuwaathiri wanafunzi.

Alitaja shule zilizofungiwa kwa kuendesha shughuli zake bila usajili kuwa ni shule ya awali na msingi Must Lead ya mkoa wa Pwani, kwa upande wa mkoa wa Dar es Salaam ni Brainstorm, Pax, Lassana, Grace, Rose Land, Julius Raymod, St Thomas, Mary Mother of Mercy, Noble Sinkonde, Immaculate Heart of Mary, St Columba, Corner Stone, Dancraig, Mwalimu Edward Kalunga, Edson Mwidunda, Gisela, Kingstar, St Columba, Bilal Muslim, Thado, Hocet , Elishadai, Lawrance Citizen, Comrade, Dar Elite Preparatory, Golden Hill Academy na Hekima.

Nyingine ni Pwani Islamic, St Kizito na Rwazi Encysloped za Kagera, Dancraig na Qunu za Pwani, Hellen’s ya Njombe, Joseph ya Arusha, Samandito na Maguzu za Geita. Alizitaja shule za sekondari zilizofungiwa kwa sababu hiyo kuwa ni Hananasif, Elu, Hocet, Safina za Dar es Salaam na Namnyaki ya Iringa.

Sababu kifo cha Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wanawake Tanzania (UWT) Dodoma

$
0
0

Mashuhuda  wa ajali iliyosababisha kifo cha Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wanawake Tanzania (UWT) Mkoa wa Dodoma, Salome Kiwaya wamesema alikufa kutokana na kushindwa kupewa msaada kwa haraka.

Walisema baada ya ajali walisikia sauti za watu wakilia kuomba msaada lakini ilichukua muda wa sasa tatu ndipo walipopata msaada wa kuokolewa kutokana na ukosefu wa vifaa vya uokoaji.

Juzi katika eneo la Emmaus mkoani hapa ilitokea ajali ya gari la Toyota Noah na lori ambayo ilichukua maisha ya Mwenyekiti huyo na watu wengine watatu kujeruhiwa. 

Mmoja wa mashuhuda hao Amri Juma alisema alisikia sauti za wanawake wakiomba msaada ili waweze kuokolewa.

“Ni jambo la kusikitisha kuona zaidi ya saa tatu hakuna vifaa vya uokoaji vilivyokuwa vimefika kwa ajili ya uokoaji, ajali ilitokea saa nane mchana lakini mpaka saa 11 jioni ndio watu wanakuja kutolewa.

‘’‘Breakdown moja ilipofika ilishindwa kunyanyua lori, ilipofika ya pili ilishindwa, hali inayoonesha kuna uhaba wa vifaa hivyo mamlaka husika zijipange kuwa na vifaa vya uokoaji."

 Juma alisema Dodoma imeanza kuandaliwa kuwa makao makuu ya nchi hivyo wakati umefika wa kuanza kujengewa uwezo wa kuwa na vifaa vya kisasa vya uokoaji. 

Katibu wa UWT Mkoa wa Dodoma, Kaundime Kasase, akizungumzia kifo hicho alisema;

“imeniuma sana na bado inaniuma, sina hata la kusema kwani nimefanya naye kazi kwa ukaribu, alikuwa mtu anayependa viongozi wake wote."

Mtoto aliyekuwa ndani ya gari hilo, Dearest Mabuba (8) alisema; “Tulikuwa tumetoka kwenye birthday (siku ya kuzaliwa) yangu ndipo gari likapata ajali, mama yangu Annastazia Amandus ambaye alikuwa akiendesha gari hilo akaumia kichwani na dada akachanika kwenye kiwiko,” alisema.

Meya wa Manispaa ya Dodoma, Jaffari Mwanyemba alisema wamempoteza mtu muhimu.

“Alikuwa akijichanganya kila mahali, tumepoteza mtu muhimu tuige mazuri yake”. 

Mbunge wa Viti Maalumu na Mwenyekiti mstaafu wa UWT Mkoa wa Dodoma, Fatma Tawfiq alisema;

“Mwenyezi Mungu ndiye alikuwa akifahamu siri hii. “Ni jambo la kushtukiza sana tumuombee Mungu amuweke mahali pema peponi,” alisema.

Hata hivyo kwa upande wake, Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani mkoa wa Dodoma, Marson Mwakyoma alisema walifika eneo la tukio dakika 10 baada ya ajali hiyo kutokea.

“Si lazima askari avae sare tulifika mapema na vikosi vingine vya uokoaji vilikuja kwa wakati, nadhani kitu muhimu kinachotakiwa kufanyika ni kuimarisha vifaa vya uokoaji,” alisema.

Mbunge wa Budalang’i nchini Kenya Asimulia Jinsi Rais Magufuli alivyoiteka Kenya

$
0
0

Mbunge wa Budalang’i nchini Kenya, Ababu Namwamba amesema Rais John Magufuli anavuma kwa umashuhuri nchini humo akitajwa kwa namna anavyopambana na ufisadi na kubana matumizi ya Serikali, lakini akasema sifa hizo zitapendeza iwapo huduma muhimu kwa wananchi zitaboreshwa na kuthibitika kwenye tafiti zitakazofanywa.

Akizungumza na waandishi wa habari wakati alipohudhuria mkutano wa demokrasia ulioandaliwa na ACT – Wazalendo jana, Namwamba ambaye pia ni kiongozi wa chama cha Labour of Kenya (LPK), alisema Rais Magufuli ana mtandao Kenya unaomshabikia kwa uongozi wake, ikiwamo harakati zake za kupambana na ufisadi

“Lakini swali kuu katika fikra za  Wakenya wengi ni sasa je, mambo yote tunayoona kwenye vyombo vya habari ni porojo tu ama ile inaitwa propaganda au ni masuala kweli yanayobadili maisha ya Watanzania wengi? Hivyo ingawa sifa za Magufuli zinaenea huku na kule, tungependa kuona mabadiliko halisi hapa Tanzania,” alisema.

“Tungependa kuona kwa mfano takwimu za ufisadi zimepungua. Takwimu za kuonyesha hali ya maisha ya Mtanzania wa kawaida imebadilika huduma kama vile maji, elimu na afya kwamba kweli zimebadilika hilo ndilo la muhimu zaidi, kinyume cha hapo hatutapata sababu ya kuamini au kuona kwamba mabadiliko hayo ni halisi.”

Namwamba, ambaye Julai 7 mwaka huu alijiuzulu ukatibu mkuu wa chama cha ODM kinachoongozwa na Waziri Mkuu mstaafu, Raila Odinga baada ya kutoelewana, alisema siasa za nchi hizo mbili zinakaribiana kwa kuwa mashindano ya wanasiasa yaliyopo nchini ni kama yalivyo Kenya.

 “Kila mara mnapokuwa na uchaguzi hapa sisi hutazama kwa makini sana kwa sababu kuna mengi ya kujifunza.
"
 Hata hivyo, Namwamba alionya kuwa suala la ukabila nchini ni la kutiliwa maanani kwa kuwa kufanya siasa kwa misingi hiyo kumesababisha maafa makubwa ikiwamo mgawanyiko kwa wananchi.

 Alisema siasa nzuri zinazopaswa kuendelezwa nchini ni zile za kuwaleta wananchi pamoja na kama ni mashindano, yawe ya sera, dhana, huduma bora kuliko kumtazama kiongozi wa chama au mgombea kwa kabila lake.

Alisema amekuja nchini kushirikiana na Kiongozi wa ACT – Wazalendo, Zitto Kabwe kupanda mbegu ya ushirikiano na kwamba atashiriki kuhamasisha vijana kutambua viongozi walioweka historia wakiwamo Mwalimu Julius Nyerere na Nelson Mandela.

 Zitto akizungumza katika mkutano huo alieleza kuwa chama chake kinaunga mkono juhudi zinazofanywa na Rais Magufuli katika kurejesha nidhamu ya kazi kwa watumishi wa umma na kupambana na ufisadi.

 “Lakini tungependa kuona hatua zinachukuliwa zaidi ikiwa ni pamoja na kuwafikisha kwenye vyombo vinavyohusika watumishi 154 wachukuliwe hatua zinazostahili.Pia suala la Escrow nalo linapaswa kuchukuliwa hatua na mengine mengi.” 

Mshauri wa ACT, Profesa Kitila Mkumbo aliwasilisha mada ya; “Sisi ni kina nani?” akilenga kuwaelimisha wanachama wake kujihusisha na maisha ya watu, kwa kuwa kushughulikia changamoto na matatizo ni mchakato unaoendelea iwe ndani au nje ya Serikali.

“Chama chetu siyo cha kuvizia makosa ya Serikali ndipo tufanye siasa, tunajipanga kushindanisha ubora wa sera, kina itikadi yake kamili, ni jukumu letu kukosoa Serikali lakini jambo la muhimu ni kuonyesha tuna vitu gani bora kwa wananchi.”

 Mwenyekiti wa Jukwaa la Katiba, Deus Kibamba ambaye alitoa mada iliyohusu masuala ya Katiba alisema mchakato wa Katiba hauna budi kurudishwa nyuma kwa hatua moja hadi kwenye rasimu.

“Kuna mambo mengi yamejitokeza ambayo yamewachanganya wananchi, hivi sasa wengi wanatofautiana hawajui uliishia kwenye hatua gani. Pia, hali iliyojitokeza kule Zanzibar ambapo wakati unajadiliwa awali kulikuwa na Serikali ya umoja ambayo sasa haipo. Kuna mambo mengi ambayo tumekuwa tunarudi nyuma hatua tano kisha kwenda mbele hatua mbili.”

NECTA Kupigilia Panga la Mwisho Kwa Wenye Vyeti FEKI Kuanzia Kesho.....Watumishi Wote Kufuatwa Vituoni Kukaguliwa

$
0
0

Hatua ya Baraza la Mitihani nchini (Necta) kutoa ratiba ya kufanya uhakiki wa vyeti vya kidato cha nne, sita na ualimu kwa watumishi wote wa umma sasa ni wazi imezidi kupandisha joto kwa vigogo na watumishi mbalimbali ambao hawana sifa za kielimu kushika nafasi walizo nazo.

Katika taarifa yake ya sasa Baraza la Mitihani nchini, limetangaza kuwafuata katika maeneo yao ya kazi watumishi wote walioko katika mamlaka za mikoa, halmashauri na manispaa kwa ajili ya kufanya uhakiki wa vyeti vyao hivyo vya kitaaluma.

Kwa mujibu wa barua iliyosainiwa na  Edga Kasuga kwa niaba ya Katibu Mtendaji wa Baraza hilo kwenda kwa Makatibu tawala wa Mikoa, uhakiki utafanyika katika ofisi za Makatibu Tawala wa mikoa kuanzia Oktoba 10 hadi 14 mwaka huu, ingawa ratiba nyingine ya uhakiki imeonyesha zoezi hilo litafikia tamati Novemba 7 mwaka huu.

“Ili kufanikisha zoezi hilo Baraza limetaka kupata orodha (nakala- laini ya soft copy) ya watumishi wote wa umma waliopo katika Mkoa, Halmashauri na Manispaa.

“Nakala za vyeti vya kidato cha nne, cha sita na ualimu vya watumishi wote walioandikishwa na chumba cha kufanyia uhakiki,” inaeleza taarifa hiyo ya Baraza la Mitihani.

Kwa mujibu wa ratiba iliyotolewa na Baraza la Mitihani, uhakiki huo utafanywa katika makundi matano katika mikoa tofauti tofauti.

Oktoba 10, mwaka huu kundi la kwanza litafanya uhakiki katika Mkoa wa Mtwara, kundi la pili Singida, kundi la tatu Rukwa, kundi la nne Katavi na kundi la tano litakuwa Geita.

Oktoba 17 mwaka huu, kundi la kwanza litakuwa Lindi, la pili Manyara la tatu Songwe, la nne Kigoma na la tano litakuwa Mwanza.

Oktoba 24 mwaka huu, kundi la kwanza litakuwa Morogoro, la pili Arusha, la tatu Mbeya, la nne Tabora na la tano Mara.

Oktoba 31 mwaka huu, kundi la kwanza litakuwa Pwani, la pili Kilimanjaro, tatu Ruvuma, la nne Shinyanga na la tano Simiyu.

Novemba 7 mwaka huu, kundi la kwanza litakuwa Dar es Salaam, la pili Tanga, la tatu Njombe, la nne Dodoma na la tano Iringa.
==


Sumaye: Kuwa mpinzani yataka moyo

$
0
0
WAZIRI Mkuu mstaafu, Fredrick Sumaye, amekiri kuwapo na ugumu wa kufanya siasa nje ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) na kuwataka wanachama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kujitoa na kufanya kazi kwa moyo.

Sumaye ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema alitoa kauli hiyo Wilaya ya Mkuranga, mkoani Pwani jana wakati wa shughuli ya kuchangia ujenzi wa Ofisi ya Chadema iliyopo wilayani humo.

Alisema wanachama wa chama hicho kuanzia ngazi ya chini wanapaswa kujitoa katika shughuli za ujenzi wa chama ili kuweza kufikia lengo la kushika dola ifikapo mwaka 2020.

“Ninaamini wote tuliopo tutajitoa kwa moyo mmoja, najua ni kazi ngumu kuwa na chama tofauti na chama tawala lakini tunapaswa kupambana kufikia malengo,” alisema.

Sumaye ambaye kabla ya kampeni za Uchaguzi Mkuu uliofanyika Oktoba 25, mwaka jana hazijaanza alijitoa CCM na kuhamia Chadema kwenda kumwongezea nguvu aliyekuwa mgombea urais wa Chadema chini ya mwavuli wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa, alisema kwa sasa hata CCM inajua kuwa Chadema itashika dola hivyo vijana wakijenge kuanzia ngazi ya matawi.

“Lazima tujitolee, dola haipatikani kiurahisi, tunapaswa tuwaeleze wananchi tutawafanyia nini, hatuwezi kufanya kazi za chama kwenye nyumba ya mtu au ofisi za vichochoroni kuanzia mwaka 1992,” alisema Sumaye.

Naye Katibu Mkuu Taifa wa Chadema, Vicent Mashinji, alisema kwa sasa ni wakati wa kudai Katiba Pendekezwa iliyokuwa ikisimamiwa na Jaji mstaafu Joseph Warioba, ili kupunguza madaraka ya rais.

“Tunahitaji Katiba ya wananchi, tunapaswa kufanya hii kampeni kwa ngazi ya msingi, tunahitaji rais hatuitaji Mungu, rais asiseme mimi sichezewi kwa sababu yeye si Mungu, ambaye hachezewi ni Mungu tu binadamu wote kuna aina ya kuchezeana,” alisema Mashinji.

Pia alisema Katiba mpya itasaidia kupata tume huru ya uchaguzi huku akirejea uchaguzi wa marudio uliofanyika Zanzibar Machi 21, mwaka huu na kudai kuwa Serikali imekuwa ikifanya mambo kwa kukurupuka bila kufuata sheria za nchi.

“Siamini kama miaka yote tutavumilia, uvumilivu una kikomo, tunalalamika lakini inawezekana safari ijayo wakalalamika wao, kila siku mnasema hatushindi tutashinda tu,” alisema Mashinji.

Alisema kwa mwenendo wa Serikali iliyopo bila Katiba mpya nchi inaweza ikaingia katika machafuko bila sababu za msingi.

Mashinji alisema Taifa linabomoka kuanzia juu kwenda chini na itakuwa ngumu kuliokoa.

Alisema katika uongozi demokrasia ni suala la msingi na si kuongoza nchi kwa matamko na amri.

Katika hafla hiyo, jumla ya Sh milioni 9.9 zilipatikana ikiwamo ahadi na kati ya hizo Sh milioni tatu zilitolewa na Dk. Mashinji.

Aliyetaka Mwamunyage apindue nchi ashinda kesi

$
0
0
Mwanafunzi  wa mwaka wa tatu wa  Chuo cha Maendeleo ya Jamii (CDTI) cha mkoani Arusha, Allan Mbando, ameibwaga Serikali katika kesi ya kudaiwa kusambaza ujumbe kupitia Mtandao wa Facebook akimtaka Mwamunyange apindue nchi.

Katika mtandao huo wa kijamii, Mbando, anadaiwa kutuma ujumbe uliosomeka kwamba: “Mwamunyange pindua nchi haiwezekani wote wawe nje, halafu hakuna aliyepewa mamlaka ya kukalia kile kiti.”

Kutokana na madai hayo, Jeshi la Polisi mkoani Arusha lilimfungulia mashtaka Mbando ya kudaiwa kusambaza ujumbe huo uliokusudia kueneza na kufanya uchochezi.

Akisoma hukumu ya kesi hiyo mjini hapa juzi, Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi wa Mkoa wa Arusha, Augustine Rwizile, alisema mahakama hiyo imepitia kwa kina hoja na ushahidi wa pande zote mbili katika kesi hiyo.

Hakimu Rwizile alisema baada ya kupitia ushahidi katika kesi hiyo, mahakama imejiridhisha kuwa upande wa Jamhuri katika kesi hiyo haukuweza kuwasilisha ushahidi unaoweza kumtia hatiani mshtakiwa.

Alisema mbali na ushahidi huo kutojitosheleza, pia hapakuwapo na jambo lolote lenye nia ovu ya kusababisha au kufanya uchochezi katika ujumbe uliosambazwa na mshtakiwa.

“Sasa mahakama hii inamwachia huru mshtakiwa baada ya upande wa Jamhuri kushindwa kuthibitisha mashtaka yake pasipo kuacha shaka yoyote.

“Lakini pia kama kutakuwa na upande ambao haujaridhika katika hukumu hii unaweza kukata rufaa,” alisema Rwizile.

Akisoma hukumu hiyo, alisema ujumbe uliosambazwa haukuwa na umuhimu wowote kwa kuwa haukumwelezea Mwamunyange ni nani katika nchi anayotakiwa kuipindua huku pia ujumbe huo ukiwa haukutaja nchi iliyolengwa kupinduliwa.

“Ujumbe ulioandikwa katika Facebook haumtambulishi Mwamunyange ni nani. Lakini ujumbe hauonyeshi jambo la msingi lenye uhusiano wa kisiasa katika Taifa linalodaiwa,” alisema Rwizile.

Kutokana na sababu hizo ikiwamo ushahidi uliowasilishwa mahakamani hapo kushindwa kuthibitisha ujumbe uliosambazwa na mshtakiwa, mahakama ililazimika kumwachia mshtakiwa.

Mshtakiwa huyo katika kesi hiyo alikuwa akitetewa na Wakili Moses Mahuna.

Mbando anaongeza idadi ya watu walioshtakiwa mahakamani kutokana na makosa ya mtandaoni baada ya Aprili, mwaka huu mkazi mwingine wa Arusha, Isack Habakuki (40), kufikishwa mahakamani na kusomewa mashtaka ya kusambaza lugha ya matusi na dhihaka kwa Rais Dk. John Magufuli. 

Baada ya kesi hiyo kuendelea kusomwa mahakamani hapo, Isack alihukumiwa kifungo cha miaka mitatu jela au kulipa faini ya Sh milioni saba na yeye alikubali kuzilipa kwa awamu.

Mtu mwingine aliyeshtakiwa Aprili, mwaka huu kwa makosa ya mtandaoni ni kondakta wa daladala, Hamimu Seif (42), aliyepandishwa kizimbani kwa kosa analodaiwa kulifanya Machi 10, mwaka huu alipotishia kumuua Rais Magufuli kwa maneno akiwa katika Baa ya Soweto iliyopo Makumbusho, Wilaya ya Kinondoni jijini Dar es Salaam.

Majina ya waliochaguliwa kujiunga na vyuo mbali mbali kwa awamu ya pili

$
0
0

 Majina ya waliochaguliwa kujiunga na vyuo mbali mbali kwa awamu ya pili

==>Chuo Kikuu Eckern Ford  (2nd Round)  <<bonyeza Hapa>>

==>Chuo Kikuu Ruaha-iringa 2nd Round)  <<bonyeza Hapa>>

==>Chuo Kikuu Mwl. nyerere Dar (2nd Round) <<bonyeza Hapa>>

==>Chuo Kikuu Tumaini-dar  (2nd Round)  <<bonyeza Hapa>>

==>Chuo Kikuu St.john (2nd Round) <<bonyeza Hapa>>

==>Chuo Kikuu Mwenge (2nd Round)  <<bonyeza Hapa>>

==>Chuo Kikuu Zanzbar (2nd Round)  <<bonyeza Hapa>>

==>Chuo Kikuu Iringa (2nd Round)    <<bonyeza Hapa>>

==>Chuo Cha Mipango Dodoma(2nd Round) <<bonyeza Hapa>>

==>Chuo Cha Ifm  (2nd Round) <<bonyeza Hapa>>

==>Chuo Cha Udsm,muce&duce(2nd Round) <<bonyeza Hapa>>

==>Chuo Cha Makumira-arusha (Second Round)<<bonyeza Hapa>>

==>Chuo Cha Arusha University(2nd Round)<<bonyeza Hapa>>

==>Chuo Cha Stefano Moshi(1st &2nd Round)<<bonyeza Hapa>>

==>Chuo Cha Marian (Second Round)  <<bonyeza Hapa>>

==>Chuo Cha Saut-mwanza (Second Round) <<bonyeza Hapa>>

==>Chuo Cha Teku(Second Round) <<bonyeza Hapa>>

==>Chuo Cha Muccobs/mocu(Second Round)<<bonyeza Hapa>>

==>Chuo Cha Bugando(Second Round) <<bonyeza Hapa>>

==>Chuo Cha Jordan (Second Round)   <<bonyeza Hapa>>

==>Chuo Cha Amucta(Second Round)  <<bonyeza Hapa>>

==>Chuo Cha Kiu(Second Round) <<bonyeza Hapa>>

==>Chuo Cha Mum(Second Round)  <<bonyeza Hapa>>

==>Chuo Cha Mweka Second Round)  <<bonyeza Hapa>>

==>Chuo Cha Ajuco Songea( 2nd Round) <<bonyeza Hapa>>

Taarifa kutoka Ikulu: Rais Magufuli afanya uteuzi wa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA)

$
0
0

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, amemteua Mhandisi James Mitayakingi Kilaba kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA).

Taarifa iliyotolewa leo na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi imeeleza kuwa uteuzi wa Mhandisi James Mitayakingi Kilaba umeanza jana Jumamosi tarehe 08 Oktoba, 2016.

Kabla ya uteuzi huo, Mhandisi James Mitayakingi Kilaba alikuwa akikaimu nafasi hiyo, baada ya uteuzi wa aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu wa TCRA Dkt. Ally Yahaya Simba kutenguliwa.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam

09 Oktoba, 2016

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatatu ya Octoba 10

Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images