Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Bodi ya Wadhamni CUF Yawashitaki Mahakamani Profesa Ibrahm Lipumba na Msajili wa Vyama Jaji Francis Mutungi

0
0
Mgogoro  ndani ya Chama cha Wananchi (CUF) umeingia hatua ya pili baada ya Bodi ya Wadhamini kufungua kesi wakimtuhumu Prof. Ibrahim Lipumba, Jaji Francis Mutungi na watu 12 kwambwa, wanahujumu chama hicho.
 
Bodi hiyo jana imewasilisha maombi ya kufungua kesi katika Mahakama Kuu Tanzania, Kanda ya Dar es Salaam ya kuomba kibali cha kumzuia Jaji Mutungi, Msajili wa Vyama vya Siasas nchini kutofanya shughuli zake kinyume cha sheria.

Katika kesi hiyo, watuhumiwa ni pamoja na Prof. Ibrahim Lipumba, mwenyekiti wa chama hicho aliyerejeshwa kwa barua ya Jaji Mutungi na  watu 12 waliokuwa  wanachama  wa chama hicho.

Akizungumza na vyombo vya habari Juma Nassoro, wakili wa chama hicho alisema kuwa, wamewasilisha maombi hayo yaliyopelekwa kwa Eva Nkya, Msajili wa Mahakama hiyo ambapo ni ombi namba 75.

Wakili Nassoro alieleza kuwa, katika maombi ya awali waliyowasilisha kabla ya kesi ya msingi kuanza kusikilizwa  ni pamoja na mahakama kumuamuru Jaji Mutungi kutengua kauli yake ya uteuzi wa  Prof. Lipumba.

Alidai kuwa, mahakama hiyo iliwahi kubainisha kazi za msajili wa vyama ambapo sio kuingilia uamuzi wa ndani ya vyama vya siasa.

Wakili Nassoro alidai  kuwa, Jaji Mtungi hana mamlaka ya kutengua uamuzi wa Kamati Kuu ya chama hicho .

Prof. Lipumba aliandika barua ya kujiuzulu uenyekiti wa chama hicho Agosti mwaka jana kwa madai ya kutoridhishwa na ujio wa Edward Lowassa ambaye baadaye aliteuliwa kuwa mgombea urais wa Chadema katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka jana na kuungwa mkono na vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa).

Hata hivyo, mwaka huu aliaeleza kuandika barua ya kutengua barua yake ya wali ya kujiuzulu kwa madai ya kutaka kujenga chama jambo ambalo limesababisha chama hicho kupasuka.

Wiki iliyopita, Baraza Kuu la Uongozi la CUF, katika kikao cha dharura kilichofanyika Makao Makuu ya CUF, mjini Zanzibar lilimfukuza uanachama wa chama hicho Prof. Lipumba.

“Baraza Kuu linaweka bayana kwa wanachama wa CUF, Watanzania na mamlaka zote nchini kwamba kuanzia leo, Prof. Ibrahim Lipumba hana haki ya kujihusisha kwa namna yoyote ile na shughuli zozote za chama,” ilieleza taarifa ya CUF.

Aidha taarifa hiyo ilidokeza kuwa, uamuzi huo umechukuliwa baada ya baraza hilo kuridhika na mashtaka dhidi ya Prof. Lipumba kuongoza na kusimamia kikundi cha wahuni kuvamia Ofisi Kuu ya Chama, Buguruni, Dar es Salaam tarehe 24 Septemba, 2016 mwaka huu.

“Baraza kuu limetumia uwezo wake, kwa mujibu wa Ibara ya 10 (1) (c) na kwa kura zote 43 za wajumbe wake waliohudhuria kumfukuza uanachama Prof. Ibrahim Lipumba,” ilieleza taarifa hiyo.

Muswada wa kuweka masharti ya ualimu waja

0
0

Serikali  inakamilisha Muswada wa Sheria utakaoweka wazi sifa za walimu wakiwamo wa vyuo vikuu, msingi na sekondari nchini.

Hayo yalisemwa jana na Waziri wa Elimu, Sayansi , Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi, Profesa Joyce Ndalichako katika kongamano la kujadili hali halisi ya elimu nchini lililoandaliwa na walimu wastaafu.

Profesa Ndalichako alisema   serikali pia inaandaa  mpango wa kuanzisha chombo maalum cha kitaaluma kitakachosimamia walimu kwa mujibu wa sheria.

Alisema muswada huo utakapokuwa tayari utawasilishwa bungeni.

Alisema  pamoja na mambo mengine, utataja sifa za mwalimu mkuu na mkuu wa chuo  kuondoa dhana kwamba ualimu ni kazi ya walimu mazoea.

“Ni lazima kuwe na sheria inayoweka wazi sifa ya mwalimu mkuu wa chuo kikuu na sifa za kuweza kujiunga na chuo cha ualimu.

“Siyo kuweka tu sheria zisizojieleza hali ambayo imesababisha taifa kuwa na wasomi wasiokuwa na sifa.

“Ili tuweze kufikia katika mpango wa kutoa elimu bora ni lazima tuchukue hatua zinazostahiki kwa manufaa ya taifa ingawa unapochukua hatua Watanzania wengi wanalalamikia suala hili ila ukweli utabaki kuwa ukweli.

“Nchi haiwezi kuendeshwa na walimu wasiokuwa na sifa kwa sababu kitakachozalishwa pia kitakuwa ni mtihani na aibu kwa nchi.

“Kama kuna mwalimu yeyote ambaye anajijua hana sifa na amekalia kiti hicho kwa zaidi ya miaka 10 atambue kuwa hicho kiti atakiacha.

“Serikali hii ya awamu ya tano hatutaki kuwa na walimu wasiokuwa na sifa, bora kujiengua mwenyewe,”alisema Profesa Ndalichako.

Waziri   alisema changamoto kubwa inayoikabili wizara yake ni utekelezaji wa mipango endelevu ya wizara ambayo ni mizuri lakini utekelezaji wake ni mdogo kutokana na kuingiliana kwa mipango ya maendeleo endelevu.

Serikali Yatangaza kiama kwa Madalali wa Ardhi na Nyumba

0
0
WAZIRI wa Ardhi, Nyumba na  Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi ametishia kuwafutia usajili baadhi ya madalali wa ardhi na nyumba, kutokana na utendaji wao unaokiuka sheria wakati wa uuzwaji wa nyumba.

Kwa mujibu wa Lukuvi, nyumba nyingi zimekuwa zikiuzwa bila kufanyiwa tathmini ya gharama zake halisi na hata zilizofanyiwa wahusika wamekuwa hawashirikishwi.

Lukuvi alitoa kauli hiyo jana jijini Dar es Salaam alipokutana na madalali wa kampuni mbalimbali, ambapo aliwaeleza malalamiko anayoyapata kutoka kwa wananchi ambao nyumba zao ziliuzwa kwa utaratibu usioeleweka.

“Madalali mmekuwa mkiuza nyumba bila kujali thamani ya mali husika na wengine mnauza kwa bei ya chini, wengine mnauza kwa bei ya deni lile lile, huo ni uonevu wa hali ya juu huku mkitambua mnaowafanyia ni maskini,”alisema.

Alisema asilimia kubwa wanaokumbwa na uonevu huo ni wanawake wajane kutokana na kutojua kama mali walizoachiwa na waume zao kama ziliandikishwa katika mkopo wa benki.

Waziri Lukuvi aliongeza kuwa madalali wengi wamekuwa wakikiuka sheria za uuzaji wa nyumba pamoja na mali za masikini kwa bei ya chini, huku wengine wakifanya mnada katika siku za mwisho wa wiki.

“Madalali wengi wamekuwa wakiuza mali za watu kwa kisingizio cha amri ya mahakama tena kwa bei ya asilimia 25 badala ya 75 kama sheria inavyotaka huku mkijua kufanya hivyo ni uonevu na wizi.

“Ninazo taarifa zenu na hata majina yenu nayajua, nitawafutia usajili na majina yenu kutangazwa katika gazeti la Serikali,”alisema.

Waziri Lukuvi alisema madalali wengi wamekuwa wakifanya mnada wa kuuza mali wakati tayari wakiwa wameshapata wanunuzi na wengine wakiwa wameshatoa fedha za awali.

Alisema amepata malalamiko ya watu 84 kutoka sehemu mbalimbali nchini ambao wameonewa kwa namna moja au nyingine na madalali wanaoshirikiana na baadhi ya maofisa wa benki kwa kuwauzia au kuwabomolea nyumba zao kinyume cha utaratibu.

Katika hatua nyingine Waziri Lukuvi aliwataka madalali hao kupeleka taarifa zote za mali husika kabla ya kupigwa mnada kwa msajili wa ardhi na nyumba.

Picha: Waziri Mkuu alipotembelea wafanyabiashara wa Soko la Sabasaba mkoani Dodoma

0
0
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ameahidi kukutana na wafanyabiashara wa soko la Sabasaba mkoani Dodoma ili kuzungumzia namna ya kulikarabati na kulifanya liwe la kisasa.

Amesema miongoni mwa mambo watakayoyajadili katika kikao hicho ambacho hakutaja siku ni pamoja na kuboresha mazingira ya kufanyia biashara hasa kwa wanaouza bidhaa nje ya maduka.
 
Waziri Mkuu ametoa agizo hilo Jumatano, Oktoba 5, 2016wakati alipotembelea maduka hayo yaliyoko katika barabara ya One Way inayopita katikati ya barabara ya sita hadi ya 11 pamoja na soko la Sabasaba akiwa kwenye ziara ya kukagua maeneo ya kutolea huduma za jamii mjini Dodoma.
 
Alisema Serikali tayari imeshahamia Dodoma hivyo wafanyabiashara wanatakiwa kutumia fursa hiyo kwa kuboresha biashara zao ili waweze kumudu ushindani wa soko.
 
“Wafanyabiashara lazima mboreshe biashara zenu, muongeze usafi zaidi na ikiwezekana muimarishe majengo yenu yawe ya kisasa zaidi kwani haiwezekani maduka ya Makao Makuu ya Nchi yawe katika hali hii,” alisema.
 
Pia Waziri Mkuu aliwataka wafanyabiashara hao wasiogope kwenda kukopa katika taasisi mbalimbali za kifedha kwa lengo la kujiongeza mitaji na kupanua biashara.
 
Alisema tayari alishatoa maagizo kwa wamiliki wa benki kuhakikisha wanawawezesha wajasiriamali wadogo kwa kuwapa mikopo, hivyo aliwataka wasiogope na badala yake wachangamkie fursa hiyo.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU
Picha: Ofisi ya Waziri Mkuu
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akitembelea eneo maarufu la biashara mjini Dodoma la Sabsaba Oktoba 5, 2016. 
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akitembelea eneo maarufu la biashara mjini Dodoma la Sabasaba Oktoba 5, 2016. 
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akitembelea eneo maarufu la biashara mjini Dodoma la Sabsaba Oktoba 5, 2016.
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akitembelea eneo maarufu la biashara mjini Dodoma la Sabsaba Oktoba 5, 2016.

Mkuu wa Magereza Mkoa wa Dodoma matatani.....Waziri Mkuu Majaliwa aagiza achunguzwe

0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amemuagiza Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Bw. Jordan Rugimbana kuchunguza ni kwa nini Mkuu wa Magereza Mkoa wa Dodoma Bw Antonino Kilumbi amekwenda kutengeneza madawati kwa watu binafsi badala ya karakana ya Magereza kama ilivyokusudiwa na Serikali.

Magereza mkoa wa Dodoma ilipewa sh. milioni 24 na Serikali ili kutengeneza madawati 480 na kila moja lilitakiwa kugharimu sh. 50,000. Uongozi wa gereza hilo ulitengeneza madawati hayo kwa watu binafsi ambapo dawa moja limegharimu sh. 70,000.

Waziri Mkuu ametoa kauli hiyo Jumatano, Oktoba 5, 2016 wakati alipotembelea Gereza la Isanga mkoani Dodoma akiwa kwenye ziara ya kukagua maeneo yanayotoa huduma za jamii mjini hapa.

Alisema kama gereza hilo halikuwa na uwezo wa kutengeneza madawati hayo kwa nini kazi hiyo wasingeipeleka kwenye taasisi nyingine ya umma, hivyo amemtaka Mkuu wa Mkoa Bw. Rugimbana kufuatilia ziada ya sh. 20,000 kwenye utengenezaji wa kila dawati inatoka wapi na inakwenda kwa nani.

“Nimesikia kwamba mnawachangisha askari kiasi kilichoongezeka kwenye utengenezaji wa madawati hayo. Ni marufuku askari kutoa fedha mifukoni mwao kulipia shughuli za Serikali,” alisisitiza.

Serikali imeandaa utaratibu wa kuwezesha taasisi zake zikiwemo za kijeshi kwa kuzipa kazi ya kutengeneza bidhaa na miundombinu mbalimbali ikiwemo madawati ili kuyaongezea tija aliongeza

Kwa upande wake Mkuu wa Magereza Mkoa wa Dodoma Bw. Kilumbi alisema waliamua kupeleka kazi hiyo kwa watu binafsi kwa sababu hawana vifaa.

Aidha, Waziri Mkuu alimtaka mkuu huyo wa magereza mkoa kuimarisha kitengo cha ufundi seremala na kuhakikisha anatumia vizuri nguvu kazi aliyonayo katika kuzalisha bidhaa mbalimbali.

Kuhusu changamoto ya makazi kwa askari Waziri Mkuu alisema Serikali inatambua na imeweka mkakati wa wa ujenzi na kwa upande wa askari Magereza wataanzia kwa mkoa wa Dodoma.

Wakati huo huo Waziri Mkuu alitembelea maduka ya kuuzia bidhaa mbalimbali zikiwemo nguo katika maeneo ya soko la Sabasaba na Majengo.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU

Video: Walimu Warekodiwa Wakimfanyia Ukatili Wa Kutisha Mwanafunzi

0
0

Video hii ambayo imesambaa kwenye mitandao ya kijamii kuanzia leo alfajiri inawaonyesha walimu wakichangia kumpiga mwanafunzi mmoja ndani ya ofisi.

Walimu hawa wanaonekana si tu wanampiga mwanafunzi huyo kwa viboko, bali wengine wanampiga makofi ya uso, huku walimu wengine wakiwasihi wamuache mwanafunzi huyo kwani wanaweza kumuumiza.

Inadawa shule hii ni Mbeya Day, iliyopo jijini Mbeya

Waziri Mwigulu Nchemba Aliagiza Jeshi la Polisi Mkoani Mbeya kuwakamata Walimu wanaoonekana katika picha ya video wakimuadhibu Mwanafunzi kikatili.

0
0
Waziri wa Mambo ya Ndani, Mwigulu Nchemba ameagiza Jeshi la Polisi mkoani Mbeya kuwakamata walimu walioonekana kwenye video wakimwadhibu mwanafunzi vibaya. Tukio hilo lilitokea 28. September.

==>Taarifa rasmi za Waziri wa Mambo ya Ndani

Mnamo Tarehe 28.9.2016, mwanafunzi aitwaye Sebastian Chinguku wa form 3A mbeya day sec school aishie Uyole alipigwa na walimu watatu, Mwl Frank Msigwa, John Deo UDSM na Sanke Gwamaka wa Nyerere Memorial, wote wakiwa mafunzo. 


Mwl Frank alitoa assignment ya Kingereza na baadhi ya wanafunzi hawakufanya akiwepo Sebastian , darasani mwl alimpiga kofi kijana na kijana akahoji kwanini anampiga wakashikana koo, ndipo walimu wakamchukua na kumpeleka staff room na kuanza kumpiga .

Tangu tar 29. September mwanafunzi hakuonekana shuleni. Na mwl E.H wa Iringa University ndio aliyekuwa akisema mwacheni mtamuumiza  na ndiye  aliyechukua video.

Hao walimu wote hawapo wameondoka kwenda kwenye vyuo vyao. POLISI wanaendelea kuwahoji uongozi wa Mbeya Day Sec School na Mwanafunzi aliyeumizwa ikiwepo kumpeleka hospitali.

Nimeelekeza vyombo vya dola Dar wawatafute chuoni kwao hao walimu kuhusiana na shambulio hilo kwa mwanafunzi huyo. 

MWIGULU Nchemba, W MNN 

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Ijumaa ya Octoba 7


RIWAYA: She is My Wife- Sehemu ya 21 & 22

0
0
MWANDISHI : EDDAZARIA G.MSULWA

ILIPOISHIA...
“TATU, MBILI, MOJA”
Mlipuko mkubwa ulio ambatana na moto ukasikika machoni masikioni na watazamaji wa Tv walio kuwa wakilifwatilia tukio zima, na Tv zao zote, ndani ya sekunde mbili zikabadilika na kuwa chenga jambo lililo waacha midomo wazi Watanzania wengine na wengine kushindwa kustamihili ujasiri na kujikuta wakiangua vilio hadharani

ENDELEA...
Ukimya ukatawala miongoni mwa watu wengi walio kuwa wakitazama taarifa ya hivi punde, juu ya Raisi Praygod Makuya kutekwa na kulipuliwa kwenye ndege yake na watu ambao hadi sasa hivi hawajajulikana ni kina nani.Kila mmoja akaanza kuhisi kwamba ni ndoto ya asubuhi ila ndio ukweli halisi kwao, Tv zao zote zikaendelea kuonyesha chenga, jambo ambalo kwa kipindi hicho cha nchi ya Tanzania kutumiamfumo wa ‘Digital’ ni ngumu sana, kuziona chenga za namna hii kama ilivyo kuwa kipindi cha ‘Analogia’

Viongozi wote walio kuwa wamejikusanya kwenye chumba cha mikutano wakifanya wawasiliano namkuu wa jeshi la anga nchini Marekanani, wanabaki midomo wazi huku wengine wenye mioyo myepesi wakijikuta wakimwagikwa na machozi pasipo wao kutarajia.

“Mmmm”
Makamu wa raisi bwana Gift Kalunde anaguna nia yake ni kuwastua ambao bado wamepigwa na bumbuwazi.
“Jamani, kila mmoja amejionea kilicho tokea.Ila niawaomba muendelee na kazi”

Muheshimiwa Gift alizungumza kwa sauti ya unyonge yenye simanzi ndani yake, akajizoa kimya kimya na kutoka ndani ya ukumbi na kuingia kwenye moja ya chumba akajifungia na kuanza kushangilia hadi jasho la mwili likaanza kumwagika.Furaha yake si kuwa raisi wa muda ila furaha yake ni kuona adui yake namba moja ameondoka kwenye hii dunia.
                                                                                                   Anna baada ya kuvuta pumzi ya kutosha akajinyanyua na kushuka kitandani, akapiga hatua hadi mlangoni, akaufunga mlango kwa ndani kisha akarudi kwenye meza yenye computer kadhaa, akazitumbulia mimacho na kuwaona wezake wakiwa kwenye moja ya chumba, akaaendelea kuchunguza chunguza kwenye kila computer, akagundua wapo kwenye Nyambizi ya kijeshi(Submarine)
“Tutatokaje humu?”

Anna alijiuliza swali, huku akitazama kila sehemu ya chumba alichopo, akapiga hatua hadi kwenye moja ya kabati kubwa, akalifungua na kukuta shehena kubwa ya silaha zilizo pangwa vzuri, akachukua moja ya bastola aina ya ‘browning SFS’ na kuichomoa magazine akakuta risasi za kutosha, bila ya kupoteza muda akaanza kukusanya bastola ambazo anaweza kuzibeba kwa wakati mmoja, ambazo zote ni zaaina moja, akaiokota nguo yake na kukuta ikiwa imechanika sana kiasi cha kutowezekana kuvaliwa, Akayazungusha macho yake kwenye kila pande ya chumba na kukuta nguo za Mathias ambazo ni za jeshi zikiwa zimening’inizwa kwenye moja ya msumari, akachukua shati moja, na kulivaa, ambalo ukubwa wake kwake ukawa kama gauni,
“Ni nzuri”

Anna alijisemea mwenyewe kimoyo moyo huku akijitazama kwenye kioo kikubwa cha kabati.Akachukua mkanda wa suruali wa Mathias na kujifunga kiunoni, kutokana na wembamba ikamlazimu kutoboa tobo jipya katika mkanda huo, ili umbane vizuri.Akazichomeka bastola nane kiunoni mwake zote zikiwa zimeajaa lisaha za kutosha, kisha yeye mwenyewe akashika bastola mbili mkononi mwake ambazo zimefungwa viwambo vya kuzuia mlio.
“Bye muheshimiwa tumbo”

Anna alizungumza huku akifyatua risasi kadhaa zilizo tua kwenye tumbo la Mathias Reymond ambaye hadi tayari amesha fariki dunia, alipo ridhika, akashusha pumzi nyingi na kuanza kupiga hatua za haraka kuelekea ulipo mlango, akakishika taratibu kitasa cha mlango na kuanza kuuvuta polepole, akachungulia na kumkuta askari mmoja mwenye mwili mkubwa akiwa amesimama nje ya mlango huku mikono yake akiwa aimeweka kwa nyuma, kama sheria mojawapo ya kijeshi.
“Huyu ndio aliye nileta humu”

Anna alijisemea kimoyo moyo, bila hata ya kupoteza muda akafyatua risasi mbili zilizo ingia kwa nyuma kwenye kichwa askari huyo, na akaanguka kama gunia la chumvi huku kichwa chake kikichanguka kwa nyuma.Anna akaanza kutembea kwa umakini akiifwata njia iliyo nyooka yenye vyumba huku na huku, akiwa katikati ya kordo ndefu gafla mlio mkali wa sauti ya king’ora cha hatari, ikaanza kulia kwa nguvu akaanza kukimbia kabla hajafika mbali.

Gafla akakutana na askari wanne wakiwa na bunduki mikononi mwao na kumuamrisha Anna kunyoosha mikono juu, wazo la haraka likamjia Anna kichwani mwake, akapandishia shati lake juu, na kuziacha sehemu zake za siri wazi na kuwafanya askari hao kubaki wakishangaa, huku baadhi wakimeza mafumba ya mate kwa uchu mkali wa kuto kukutana na mwanamke kimwili katika kipindi kirefu cha wao kushinda ndani ya maji baharini kwenye nyambizi yao.

Sauti ya king’ora cha hatari kikaanza kuwastua Fetty na wezake wawili ambao hadi sasa hivi wapo ndani ya chumba ambacho hawajui ni wapi, walipo
“Nini hicho?” Halima aliuliza
“King’ora cha hatari hicho”

 Fetty alijibu huku akiandelea kusimama katikati ya chumba, huku kichwa chake kikiwa bado kimefunikwa na kofia jeusi, ambalo hadi muda huu wameshindwa kujivua kutokana na mikono yao kufungwa kwa nyuma na pingu.
Askari mmmoja akafungua ndani ya chumba walipo Fetty na wezake kuangalia kama wapo,
“Wewe mpumbavu rudi ukae chini”

Askari alizungumza huku akimfwata Fetty kwenye sehemu aliyo simama, kitendo cha kumsogelea Fetty ikawa ni koso lake kubwa, kwa kutumia hisia kali Fetty aliweza kujirusha na kumtandika askari kichwa kimoja kikali cha pua na kumfanya aanguke chini, kwa hasira askari akampiga mtama Fetty na kumuangusha chini, akamkalia Fetty tumboni na kunza kumshambulia kwa  kumtandika vibao mfululizo vya kichwani.

Watoto 22 na Mwalimu wao wa Madrasa Watiwa Mbaroni Kwa Madai ya Kujifunza UGAIDI

0
0
JESHI la polisi mkoani Pwani ,limewakamata watoto 22 wa madrasa ya Arahma pamoja na mwalimu wa madrasa hiyo Ashura Said(47) ambae alikuwa akiendesha mafunzo ya kigaidi kwa watoto hao,huko Kimarang’ombe ,kata ya Nianjema ,Bagamoyo.

Aidha jeshi hilo limefanikiwa kukuta bomu moja la moshi lenye namba G2020c.SS-STCS katika makazi anayoishi mwalimu huyo .

Akizungumzia tukio hilo,kamanda wa polisi mkoani Pwani,Boniventure Mushongi,alisema Ashura anashikiliwa na polisi kwa mahojiano zaidi kuhusiana na kuhusika kuendesha mafunzo ya kigaidi kinyume na sheria.

Alieleza kuwa taarifa hiyo ilitolewa na raia wema juu ya mwenendo wa mwalimu huyo wa madrasa na baada ya kumfanyia upekuzi polisi walifanikiwa kukuta na bomu moja la moshi.

Kamanda Mushongi,alisema uchunguzi wa awali ulibaini makazi hayo yanamilikiwa na taasisi ya kiislamu iitwayo Akha Laagul Islam,iliyosajiliwa kwa lengo la utoaji huduma kwa watoto yatima kutoka maeneo mbalimbali ikiwemo Dar es saalam ,Tanga,Handeni,Mlandizi na Bagamoyo kwa mkoa wa Pwani.

“Badala yake watoto hao wamekuwa wakitumika kwa mafunzo yasiyofaa kwa watoto wa kituo hicho”alisema kamanda Mushongi.

Hata hivyo alisema jeshi la polisi limewamakata watoto 22 ambao walikuwa wakijaribu kukimbia ambao kati yao 16 ni wakike na 6 ni wa kiume kwa ajili ya uchunguzi wa tukio.

Katika tukio jingine ,Bakari Saidi (45)mkazi wa Kimanzichana Kusini ,wilayani Mkuranga, ameuwawa kwa kupigwa risasi kifuani upande wa kulia na kutokea chini ya bega la kushoto ,mgongoni na watu wasiofahamika.

Katika tukio hilo,Omar Ally (55)ambae ni afisa mtendaji wa kijiji cha Kimanzichana Kusini,alijeruhiwa kwa kupigwa risasi kwenye mkono wake wa kushoto na amelazwa katika hospitali ya wilaya hiyo kwa matibabu.

Kadhalika katika eneo la tukio kumekutwa maganda mawili ya risasi yanayotumika kwenye silaha ya SAR/SMG .

Kamanda Mushongi alisema watu hao walivamia katika ofisi ya serikali ya kijiji cha Kimanzichana Kusini na kufanya mauaji hayo ambapo  mtu huyo alifariki dunia  na mwingine mmoja kujeruhiwa.

Anasema tukio hilo limetokea octaba 5 mwaka huu katika kitongoji cha Ukwama kata ya Kimanzichana tarafa ya Mkamba wilayani hapo.

“Wakati marehemu akiwa anajaza fomu za mkopo wa benki ya  akiba  Commerce bank(ACB),ghafla walitokea watu wawili wakiwa na silaha mbili na kuanza kuwafyatulia risasi na kutoweka kusikojulika wakitumia usafiri wa pikipiki"alisema kamanda Mushongi.

Kamanda huyo alifafanua kuwa mwili wake umehifadhiwa katika hospitali ya wilaya ya Mkuranga na utakabidhiwa kwa ndugu zake kwa ajili ya mazishi mara baada ya uchunguzi kukamilika.

Jeshi hilo limewahakikishia wananachi wote usalama wao na kwamba linapambana kwa nguvu na wale wenye nia ya kuwatia hofu wananchi,kwani hawataweza kufanikiwa katika mipango yao .

Limewaasa wananchi kuwafichua wahalifu ambao ni sehemu ya jamii wanapoishi badala ya kuoneana muhali pamoja na kutoa taarifa pale wanapobaini kuna watu ama raia asiyemwema

Serikali Yachachamaa....Walimu Waliomfanyia Ukatili Mwanafunzi Watimuliwa Chuoni, Mkuu wa Shule Apoteza Kibarua

0
0
Walimu  wanne wa Chuo Kikuu cha Elimu Dar es Salaam (Duce) na cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere waliohusika kumpiga vibaya mwanafunzi wa Shule ya Sekondari Mbeya wamefukuzwa chuo huku Jeshi la Polisi mkoani Mbeya likiwashikilia kwa mahojiano walimu wengine watano wa shule hiyo kutokana na tukio hilo.

Aidha, serikali imemvua madaraka Mkuu wa shule hiyo, Magreth Haule kwa kutochukua hatua baada ya kitendo hicho kufanyika shuleni hapo Septemba 28, mwaka huu.

Hatua hizo zimechukuliwa baada ya jana katika mitandao ya kijamii kusambaa kipande cha video kikionesha walimu zaidi ya watatu wakiwa eneo la ofisi wakimshambulia kwa kumpiga makofi, mateke na fimbo sehemu mbalimbali za mwili hasa kichwani mwanafunzi Sebastian Chinguku.

Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi, Profesa Joyce Ndalichako ametangaza kuwafukuza chuo walimu wanafunzi hao walioshiriki kitendo cha kumpiga mwanafunzi huyo wa kidato cha tatu wa Shule ya kutwa ya Sekondari ya Mbeya.

Walimu hao ni Frank Msigwa (anayedaiwa kumpiga zaidi mwanafunzi huyo kwa makofi kichwani), John Deo na Sante Gwamaka wote wa Duce na Evans Sanga wa Chuo Kikuu cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere.

Akizungumza na vyombo vya habari jijini Dar es Salaam jana, Profesa Ndalichako alisema kitendo hicho ni cha kikatili, jinai na kuwa walimu hao wanafunzi hawafai kuendelea na taaluma hiyo ya ualimu na kuwa hatua zaidi za kisheria zinaendelea kuchukuliwa dhidi yao.

Profesa Ndalichako alisema kwa mujibu wa taratibu za vyuo vikuu kitendo kilichofanywa na walimu wanafunzi hao ni kosa la jinai na kuwa hakiwezi kufumbiwa macho.

Alitoa onyo kali kwa wanafunzi wanaokwenda kwenye mafunzo kwa vitendo na kwenda kinyume cha taaluma yao kuwa wanapoteza sifa hivyo amewataka kuzingatia maadili ya fani na taaluma wanazosomea.

Mkoani Mbeya, Kamanda wa Polisi wa Mkoa, Dhahiri Kidavashari alisema wanawashikilia walimu wa shule hiyo watano kwa mahojiano kuhusu tukio hilo. Hata hivyo, alisema si kwamba walimu hao wanaohojiwa ndio waliohusika na tukio hilo bali wameanza na wale waliopo ili kupata taarifa zaidi.

“Hatuwezi kusema sasa hivi kama wale walimu ndio walioonekana katika kipande cha video kinachosambaa mitandaoni kwa kuwa hili ni suala la mahojiano, tunaamini hawa tulionao wanaweza wakatupa mwanga,” alisema.

Akieleza sababu ya adhabu hiyo, Kamanda alisema katika mahojiano ya awali imebainika kuwa mwalimu wa Kiingereza alitoa kazi, lakini baadhi ya wanafunzi hawakufanya baadaye mwalimu huyo aliwapa adhabu ya kupiga magoti, lakini mwanafunzi huyo alionekana kupinga kwa kueleza ana tatizo la goti hatoweza kufanya adhabu hiyo na mwalimu aliamua kumpeleka ofisini na kumpiga kwa kumchangia.

“Mwalimu aliwaadhibu wanafunzi darasani na alipotaka kumuadhibu mwanafunzi huyo mbele ya darasa, alionesha kupinga kupigwa mbele ya wanafunzi wenzake ndipo alipoamua kumpeleka ofisini na kutokea tukio linalosambaa,” aliongeza Kidavashari.

Katika taarifa yake, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba, alisema Septemba 28 mwaka huu, mwanafunzi Chinguku wa kidato cha tatu wa Shule ya Sekondari Mbeya, mkazi wa Uyole, alipigwa na walimu watatu.

“Nimeelekeza vyombo vya dola Dar es Salaam wawatafute chuoni kwao hao walimu kuhusiana na shambulio hilo kwa mwanafunzi huyo,” ilisema Mwigulu.

Naye Waziri katika Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), George Simbachawene ameagiza mamlaka za nidhamu kumvua madaraka Mkuu wa Shule hiyo, Haule kwa kushindwa kuchukua hatua na kutoa taarifa mara baada ya tukio hilo kufanywa na walimu hao shuleni hapo.

"Kwa kuwa waliotenda kosa hili wametoweka tangu Septemba 29, 2016 na hawajulikani walipo, nimesikitishwa kwa kitendo cha mwalimu mkuu wa shule hiyo, Magreth Haule kutochukua hatua. Hii inaonesha kulikuwa na dalili za kutaka kulificha tukio hili baya.

“Na kwa sababu hiyo, pamoja na kwamba wanaendelea kuhojiwa na Polisi, naagiza mamlaka yake ya nidhamu kumvua madaraka mkuu huyo wa shule," alisema Simbachawene katika taarifa yake kwa umma jana.

 Katika hatua nyingine, Rais wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT), Gratian Mukoba amelaani kitendo kilichofanywa na walimu hao na kukieleza kuwa ni cha mwituni na cha kinyama kwa kuwa hakuna adhabu kama hiyo katika utumishi wa ualimu.

"Nami nimeona hiyo video katika mitandao ya kijamii, kuna sheria za adhabu za viboko lakini si hii walioifanya hao walimu vijana maana walikuwa wakipiga makofi, ngumi, mateke, ngwara. Hizi hazipo kwenye ualimu, lazima wafuate sheria zinazosimamia utumishi wa walimu," alisema Mukoba.

Alishauri vyuo vya ualimu viweke mkazo katika kufundisha walimu vijana namna ya kuwa zaidi ya walimu, kuwa na uvumilivu, subira na kuzingatia sheria. Wafunzwe kisaikolojia kukubali kuwa hawaishii kuwa walimu bali wanaingia kwenye kundi la malezi.

Alisema kwa tukio hilo, ni lazima sheria ichukue mkondo wake ili iwe fundisho kwa wengine wenye tabia hizo hasa walimu vijana kwa kuwa kitaaluma ni tukio la kinyama lisilokubalika.

“Hata kama mwanafunzi ana makosa, amevuta bangi, huwezi kumuadhibu vile, maana pale hujui nani kavuta bangi nani mzima,” alisema Mukoba.

Awali, Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Amos Makalla alisema serikali inalifuatilia kwa karibu tukio la kupigwa kama mwizi mwanafunzi huyo wa shule hiyo ya jijini Mbeya na kusema tayari baadhi ya walimu akiwemo mkuu wa shule, wanashikiliwa na Polisi.

Makalla alibainisha hayo jana kwenye Maadhimisho ya Siku ya Fimbo Nyeupe Duniani yaliyofanyika kitaifa mkoani Mbeya na kusisitiza kuwa walimu waliohusika na tukio la kumpiga mwanafunzi wao kama mwizi wanasakwa na lazima watapatikana.

Alisema Septemba 26, mwaka huu, mwalimu aliyekuwa katika mafunzo kwa vitendo katika shule ya Sekondari ya Mbeya Day aliyemtaja kwa jina la Frank Msigwa alitoa kazi kwa wanafunzi darasani na Septemba 28 alipokuwa akisahihisha kazi zilizofanyika alibaini baadhi ya wanafunzi hawakufanya.

Makalla alifafanua kuwa miongoni mwa wanafunzi aliobaini hawakufanya kazi yake ni pamoja na Chinguku na ndipo aliwatoa nje ya darasa na kuwapa adhabu ya kupiga 'push up' lakini mwanafunzi huyo akagoma akidai kuwa na matatizo ya kiafya katika mbavu zake.

Alisema baada ya kugomea adhabu hiyo mwalimu aliwaamuru wapige magoti lakini pia mwanafunzi huyo aligoma akisema ana matatizo ya goti katika moja ya miguu yake ndipo mwalimu alilazimika kutoa adhabu ya kuwachapa viboko viwili kila mmoja na aliwapiga wote isipokuwa Chunguku ambaye kama alivyofanya kwenye adhabu za kwanza hii pia alikataa.

Alisema baada ya hapo mwalimu huyo alilazimika kwenda kuwaita wenzake wawili ambao nao walikuwa kwenye mafunzo ya ualimu kwa vitendo shuleni hapo na wakambeba mwanafunzi huyo hadi ofisini kwao ambako huko ndiko walianza kumchapa kwa kumchangia kama inavyooneshwa kwenye kipande cha video kilichosambazwa kwenye mitandao ya kijamii.

Kwa mujibu wa Makalla, walimu waliotenda kitendo hicho walitoroka na hawajulikani walipo. Alisema serikali inaendelea kuwasaka huku walimu wengine wakihojiwa Polisi.

Rais Magufuli Atangaza Kiama ....Ni cha Kuwanyang'anya Watu Wote Walioshindwa Kuendeleza Mashamba, Asisitiza Hatojali Hadhi ya Mtu

0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Magufuli amewataka watu wote nchini wanaohodhi mashamba makubwa na kutoyaendeleza wafanye hivyo ndani ya mwezi mmoja kabla hayawanyang’aya mashamba hayo kwa mujibu wa sheria na mamlaka aliyonayo.

Akizungumza jana na wananchi mkoani Pwani wakati wa zoezi la kuzindua kiwanda cha kusindika matunda, Rais Dkt. Magufuli alitumia fursa hiyo kuwataka wawekezaji wanaotaka kuja nchini kuwekeza wafanye hivyo kwa kuwa ardhi ipo ya kutosha.

“Nataka watu wote wanaotaka kuja nchini kuwekeza waje, kwa kuwa ardhi ya kutosha tunayo na nawataka watu wote waliohodhi ardhi hata kama walikuwa viongozi huko nyuma nataka wayalime ndani ya mwezi mmoja na kama wasipofanya hivyo nitabatilisha hati zao za umiliki na kuwapa watu wengine ambao wapo tayari kuendeleza ardhi hiyo" Alisema Rais Dkt. John Magufuli.

Aidha Rais Magufuli alisema baadhi ya wafanyabiashara wa sukari nchini wamekuwa siyo waaminifu kwa kuagiza sukari kwa ajili ya matumizi ya viwandani kutoka nje ya nchi sukari ambayo ikifika nchini huiweka kwenye mifuko na kuiuza kwa matumizi ya kawaida ya nyumbani jambo linaloweza kuathiri afya za watumiaji.

“Tatizo la sukari liliingia baada ya kuanza kuifuatilia sukari ili sukari inayopakiwa kwa matumizi ya binadamu iwe hivyo ndipo wafanyabiashara wakaanza kuficha sukari, ndiyo maana ninataka wawekezaji waje hapa kuwekeza katika kilimo cha sukari ili sukari izalishwe hapa nchini” Alisema Rais Dkt. Magufuli.

Pamoja na hayo Rais Magufuli alikemea tabia ya watu kuficha pesa na wengine kuzigeuza katika mfumo wa dolla na kuzificha chini ya ardhi na kusisitiza wanaofanya hivyo mwisho wake watakuta pesa hizo zimeharibika huku akiwataka wazitumie kuwekeza katika viwanda.

Zitto Kabwe Awamwagia Sifa UKAWA ......Atia Neno Kuhusu Mgogoro wa CUF

0
0

Kiongozi Mkuu wa Chama Cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe ameisifia nguvu ya vyama vya siasa vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) kwa kile walichokifanya hasa katika uchaguzi wa mwaka jana.
 
Akizungumza jana katika mahojiano maalum na kituo cha runinga cha Clouds TV, Zitto alisema kuwa chama chake hakiwezi kubeza nguvu kubwa iliyooneshwa na umoja huo na kwamba uliweka historia katika chaguzi zote zilizowahi kufanyika nchini.
 
“Ukawa umeweka historia Kubwa zaidi katika chaguzi za nchi yetu japo kuwa kuna madhaifu ila hatuwezi kupuuza nguvu ile,” alisema Zitto ambaye pia ni Mbunge wa Kigoma Mjini.
 
Hata hivyo, pamoja na kusifu nguvu ya muungano huo wa hivyo vya siasa ambavyo ni Chadema, Chama Cha Wananchi (CUF), NCCR-Mageuzi na NLD, Zitto alisisitiza kuwa chama chake hakitajiunga na umoja huo kutokana na maazimio na miiko waliyoiweka katika Azimio la Tabora la chama chake.
 
“Hatukuweza kujiunga na Ukawa kwasababu tuliweka kanuni zetu wazi  tulizozitangaza katika azimio la Tabora,” Zitto anakaririwa.
 
Katika hatua nyingine, Zitto alizungumzia mgogoro wa uenyekiti wa CUF unaoendelea ndani ya chama hicho na kutoa rai kwa vyama vingine vya siasa kutowafarakanisha.
 
Alisema kuwa CUF inapaswa kuachiwa suala hilo walimalize wenyewe katika vikao vyao vya ndani ya chama na sio vinginevyo. 

Aliongeza kuwa kutokana na mgogoro unaoendelea ndani ya CUF, hivi sasa ajenda yao kubwa [kupinga kufutwa kwa matokeo ya uchaguzi mkuu wa Oktoba]imewekwa kando bali sasa wanatafuta uhalali wa kiongozi wa chama hicho.
 
“Rai yangu tusichochee kabisa mgogoro huu bali ni tuwe kama madaraja ya kufanikisha mgogoro huu kumalizimika kwa amani,” alisema.
 
Hata hivyo, mapema wiki hii Baraza Kuu la Uongozi wa CUF lilifungua shauri mahakamani kuhusu mgogoro wa uongozi ndani ya chama hicho, wakimshataki Msajili vya Vyama vya Siasa nchini pamoja na Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

 Katika shauri hilo, wanapinga uamuzi wa Msajili kuandika barua ya kumtambua Profesa Ibrahim Lipumba kuwa Mwenyekiti halali wa chama hicho huku wakidai kuwa alijiuzulu na taarifa za kujiuzulu kwake waliziwasilisha kwa Msajili.
 
Baraza hilo limedai katika shauri hilo kuwa katiba na sheria ya vyama vya siasa haimpi mamlaka Msajili kuingilia maamuzi ya ndani ya vyama vya siasa. Shauri hilo bado halijaanza kusikilizwa.

Waziri Mkuu Akutana na Madudu Mamlaka ya Ustawishaji Makao Makuu Dodoma (CDA)

0
0
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amemuagiza Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera na Bunge), Bw. Uledi Mussa afuatilie malipo ya kiwanja kilichouzwa na CDA kwa sh. milioni 240 lakini fedha iliyoingia ofisini ni sh. milioni 6 tu.

“Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu, ninataka ufuatilie mauzo ya kiwanja namba 26 block AA eneo la Kikuyu East ambacho kimeuzwa kwa sh. milioni 240 lakini fedha iliyoingia CDA ni sh. milioni 6 tu. Nataka kujua nani ameingiza milioni 6 na nani kachukua hizo sh. milioni 234,” alisema.

Waziri Mkuu ametoa agizo hilo jana mchana Alhamisi, Oktoba 6, 2016 wakati akizungumza na watumishi na viongozi wa Mamlaka ya Ustawishaji Makao Makuu Dodoma (CDA) kwenye ukumbi wa Hazina ndogo mjini Dodoma.

Bila kutoa ufafanuzi zaidi, Waziri Mkuu alisema eneo hilo lilipaswa kuwa na kituo cha mafuta na akataka apatiwe taarifa mapema iwezekanavyo.

Pia alimwagiza Katibu Mkuu huyo afuatilie mkataba wa upangishaji wa jengo la CDA ambalo wamepangishwa taasisi ya Tunakopesha Limited kwa madai kuwa mhusika alipewa bure na sasa anataka kulipangisha tena ili apate cha juu.

Waziri Mkuu aliwaonya watumishi hao pamoja na viongozi wao waache tabia ya kushirikiana na madalali kuuza viwanja na akawataka wachape kazi wakijielekeza na kasi ya Serikali ya kuhamia Dodoma.

“Tabia ya watumishi kushirikiana na madalali kuuza ardhi sasa basi. Hata hivyo, nimefarijika kukuta mmeanza kuweka mfumo wa kielektoniki katika baadhi ya huduma. Ni lazima mauzo ya viwanja sasa hivi yafanyike kwa njia ya kieletroniki, madalali hawana nafasi,” alisisitiza.

Aliutaka uongozi wa CDA uongeze kasi ya upimaji viwanja kwa sababu mahitaji ni makubwa lakini akaonya kuwa wakati zoezi hilo likifanyika, wananchi walionunua viwanja na bado hawajamalizia kuvilipia, wasinyang’anywe kwa kigezo cha kutaka kuwauzia wengine.

“Mimi nataka idadi ya viwanja vilivyopimwa iongezeke. Lakini pia msitumie fursa hii kuwanyang’anya watu wenye umiliki halali eti kwa sababu Serikali inataka idadi ya viwanja vilivyopimwa iongezeke,” alisema.

“Kama mtu amepewa offer au hati yake asinyang’anywe hata kama amelipia nusu asinyang’anywe. Ahimizwe kumalizia hilo deni na ninyi kazi yenu ni kupima viwanja vingine,” alisisitiza.

“Natambua mnayo benki ya viwanja, lakini inabidi muongeze idadi ya viwanja vingi zaidi. Tumeita wawekezaji waje kujenga nyumba za kuishi watumishi, mahoteli na viwanda na maeneo yote haya inabidi yatengwe rasmi,” alisema.

Alisema jumla ya viwanja 70,000 vimepimwa tangu CDA ianzishwe mwaka 1973. Amesema kama wataendelea na kasi hiyo wakati mahitaji yameongezeka, itawachukua zaidi ya miaka 40 kukamilisha mahitaji ya viwanja 100,000 ambavyo vinatarajiwa kuanza kupimwa hivi karibuni.

Mapema, akitoa taarifa mbele ya Waziri Mkuu, Mkurugenzi Mkuu wa CDA, Eng. Paskasi Muragili alisema usanifu wa upimaji viwanja 20,000 umekamilika na kwamba wana lengo la kupima viwanja vingine 100,000 ifikapo Juni 2017.

Waziri Mkuu alitembelea Ofisi ya CDA na kukagua mfumo wa utunzaji mafaili wa zamani pamoja na uhamishaji wa taarifa za wenye viwanja kwenye mfumo wa kompyuta. Pia alikagua mifumo ya uuzaji viwanja kwa njia ya mtandao ambayo hata hivyo bado haijakamilika.

Wakati huo huo, Waziri Mkuu alipokea mchango wa zaidi ya sh. milioni moja kutoka kwa Mkuu wa Wilaya wa Kongwa, Bw. Deogratius Ndejembi zikiwa ni kwa ajili ya wakazi wa mkoa wa Kagera walioathirika kwa tetemeko la ardhi lilitokea Septemba 10, mwaka huu.

Pia Waziri Mkuu alipokea mchango mwingine wa zaidi ya sh. milioni tano kutoka kwa makundi mbalimbali ya wafanyabiasha wa Manispaa ya Dodoma wakiwemo wamiliki wa hoteli, nyumba za kulala wageni, waendesha bodaboda na madereva wa daladala.

Akipokea msaada huo, Waziri Mkuu aliwashukuru wafanyabiashara hao na kuwahakikishia kwamba fedha hizo zitapelekwa mkoani Kagera na kuwafikia walengwa kama ilivyokusudiwa.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU

Rais Magufuli atimiza ahadi yake kwa Balozi Omben Sefue.......... Amteua kuwa Mwenyekiti wa Bodi Chuo cha Diplomasia

0
0

Hatimaye Rais John Magufuli ametimiza ahadi yake kwa aliyekuwa Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue baada ya kumteua kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Chuo Cha Diplomasia.

Balozi Sefue amepata uteuzi huo jana ikiwa ni miezi kumi tangu Rais Magufuli atengue uteuzi wake [kama Katibu Mkuu Kiongozi]kwa sababu ambazo hazikutajwa huku akiahidi kumpangia kazi nyingine na nafasi yake ikajazwa na Balozi John Kijazi, .

Aidha, kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Waziri wa wizara hiyo, Balozi Augustine Mahiga amewateua wajumbe sita wa Bodi ya chuo hicho cha Diplomasia.

Wajumbe hao ni Balozi Begum Taj, Balozi John Haule, Juma Salum, Profesa Mohamed Bakari, Profesa Innocent Zilihona na Mathias Abias.

Taarifa hiyo imeeleza kuwa uteuzi huo umeanza rasmi Oktoba 6 mwaka huu.


Ofisi ya Taifa ya Takwimu yatoa vigezo kwa yeyote anayetaka kuwa Mdadisi au Mkusanyaji taarifa za kitakwimu.

Jinsi ya Kuandaa na Kutayarisha Dawa Lishe ya Kunenepesha,Kurutubisha na Kuongeza Mwili

0
0

Dawa-lishe  ya  kuongeza, kurutubisha  na  kunenepesha  mwili, ni  dawa  maalumu  kwa  watu  wenye  uzito  wa  chini  (  Under weight ) ambao  wanataka  kuongeza  mwili  na  uzito.


Dawa  hii  huwasaidia  watu  ambao  miili  yao  imedhoofu  kutokana  na  sababu  mbalimbali  kama  vile  kuugua  magonjwa  na  maradhi  mbalimbali.

Na  kwa  wale  watu  wembamba  ambao  wanataka  kuongeza  miili  yao, dawa  hii  huwasaidia  vizuri  sana.

FAHAMU  JINSI NA  NAMNA  YA  KUANDAA NA  KUTAYARISHA   DAWA-LISHE  MAALUMU   YA  KUONGEZA, KURUTUBISHA  NA  KUNENEPESHA  MWILI.

MAHITAJI   YA  DAWA –LISHE

i.           Dawa –lishe vijiko  viwili vikubwa.

ii.         Asali  ya  tende  vijiko  vitano  vikubwa.

iii.       Tangawizi  ya  unga  vijiko  vikubwa  viwili

iv.       Unga  wa ufuta

v.         Maziwa  fresh nusu  lita

vi.       Maji  ya  moto  kiasi  cha  milimita  mia  mbili  na  hamsini  ( 250 mills  )


MATAYARISHO
i. Chukua  vijiko  vinne  vyenye  dawa  lishe  yako  kisha  chemsha  na  nusu  lita  ya  maji  hadi  mchanganyiko  wako  utokote  halafu  ipua, chuja , makapi  weka  pembeni  kisha  hifadhi  juisi  yako.

ii.Tayarisha  uji kwa  kutumia  unga  wa  ufuta  na maziwa  fresh

iii.Chukua  vijiko  viwili  vikubwa  vya tangawizi  ya  unga  kisha  changanya  kwenye  kikombe  cha  maji  ya  moto  chenye  ujazo  wa  milimita  mia  mbili  hamsini  (  250  mills )

MATUMIZI:
i. Tumia  kunywa  nusu  lita  ya  dawa –lishe  yako  kisha

ii.Tumia kula  vijiko  vinne  vikubwa  vya  asali  ya  tende

iii.Kisha tumia  kunywa  vikombe  vinne  vya  uji  wa  ufuta  ulio changanywa  na  maziwa  fresh

iv.Halafu  kunywa  glasi  moja  ya  moto  iliyo  changanywa  na  vijiko  viwili  vikubwa vya tangawizi  ya  unga.

UTAFANYA  HIVYO  MARA  MBILI  KWA  SIKU  KWA  MUDA  WA  SIKU  THELATHINI  MFULULIZO.

Baada  ya  siku  thelathini, utaangalia  na  kujitathmini  kiasi  ulicho  ongezeka. Kama  utataka  kuendelea  kuongezeka  zaidi, utaendelea  kutumia  dozi  hii  hadi hapo utakapo fikia kiwango  utakacho  rizika  nacho.

BEI  YA  DAWA-LISHE : Bei  ya  Dawa-Lishe  ni  SHILINGI  ELFU  HAMSINI  TU (TSHS.50,000/=)

JINSI  YA  KUIPATA  DAWA  LISHE:
Dawa  hii  inapatikana  katiuka  duka  la dawa  asilia  la  NEEMA  HERBALIST  &  NUTRITIONAL  FOODS  CLINIC  lililopo  jijini  DAR  ES  SALAAN  katika  eneo  la  TABATA  MAKOKA  karibu  na  SHULE  YA  SEKONDARI  YA  MT. ANNUARITE.

Unaweza  kufika  moja  kwa  moja  katika  ofisi  zetu  AU  unaweza  kuletewa  mahali popote  ulipo  jijini  Dar   Es  salaam.

Kwa  wakaazi  wa  ZANZIBAR  watatumiwa dawa  kwa  njia  ya  usafiri  wa  boti  na  kwa  wateja  wetu  wa  ughaibuni watatumiwa  dawa  kwa  njia  ya  POSTA  au  DHL.

Kwa  mawasiliano  zaidi  wasiliana  nasi  kwa  simu

0766  53  83   84

Vile  vile  tunayo  dawa  ya  asili  iitwayo  JIKO  ambayo  inatibu  na  kuponyesha  kabisa  TATIZO  LA  UKOSEFU  WA  NGUVU  ZA  KIUME.

Kufahamu  kuhusu  SAYANSI  YA  NGUVU  ZA  KIUME  pamoja  na  jinsi  dwa  ya  JIKO  inavyo  fanya  kazi  tafadhali  tembelea:

Mamlaka ya Mapato (TRA): Makusanyo ya Kodi mwezi Septemba 2016

0
0
Mkurugenzi wa Elimu na huduma kwa mlipa kodi wa TRA, Bw. Richard Kayombo amesema mwenendo wa ukusanyaji mapato ya Serikali kwa sasa ni wa kuridhisha katika  kufikia  lengo la kukusanya kiasi cha shilingi trioni 15.1 kwa mwaka fedha wa 2016/2017.

Mamlaka ya Mapato nchini (TRA) imekusanya Mapato ya shilingi trilioni 1.37 kwa Mwezi September kati ya lengo la kukusanya shilingi trilioni 1.4 mwezi huo

Kuhusu zoezi la uboreshaji wa taarifa ya namba za utambulisho wa mlipa kodi linaloendelea jijini Dar es Salaam, Bw. Richard Kayombo amesema mpaka sasa TRA imetoa vyeti vipya vya TIN  kwa watu 15, 467 na zimebaki siku tisa kukamilisha zoezi hilo.

==> Tazama video hapo chini

Rais Magufuli Amfagilia Bakheresa....Amzawadia Eneo la Ardhi la Hekari 10,000, Ataka Sukari yake Iliyozuiwa Bandarini Apewe

0
0

RAIS Dk. John Magufuli, amemwagiza Waziri wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara, Charles Mwijage kumrudishia mfanyabiashara maarufu nchini, Said Salim Bakhresa sukari yake iliyozuiwa bandarini kwa sababu biashara yake ina tija kwa taifa.

Mbali na hayo, Rais pia amelipa Shirika la Umeme (Tanesco) miezi miwili kufikisha huduma ya umeme katika kiwanda cha kusindika matunda na kuzalisha juisi cha Bakhresa Food Products Ltd kilichopo Mwandege wilayani Mkuranga, mkoani Pwani.

Rais alitoa maagizo hayo jana  wakati wa hafla ya uzinduzi wa kiwanda hicho ambapo alisema ameridhishwa na uwekezaji wa kampuni hiyo.

Sukari hiyo ya Bakhresa ilizuiwa katika Bandari ya Dar es Salaam pamoja na wafanyabiashara wengine miezi michache iliyopita wakati Rais Magufuli alipotangaza kusitisha vibali vya kuagiza sukari kutoka nje kwa madai ya kulinda viwanda vya ndani.

Agizo hilo lilisababisha uhaba mkubwa wa sukari ambapo ilipanda na kufikia wastani wa Sh 4,500 hadi 6,000 katika baadhi ya mikoa nchini.

“Tena ndugu  yangu, nitakupa eneo ulime miwa ili upate sukari ya viwandani na ya majumbani, tena nitakupa bure, wewe Bakhresa umenifurahisha sana kwa uwekezaji wako na sukari yako niliyoizuia bandarini leo namwagiza Waziri Mwijage itoke na upatiwe,”alisema  Rais Magufuli bila kufafanua kiasi gani cha sukari kilichozuiwa.

Aidha Rais alisema kutokana na uhaba wa sukari unaoikumba Tanzania kwa miaka mingi ni vyema kushirikiana na wawekekzaji ili kuondokana na tatizo hilo.

Katika tamko lake Rais aliagiza Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kuipatia kampuni hiyo ya Azam  eneo la ekari 10,000 kwa ajili ya kilimo cha miwa.

“Kupitia kilimo hicho Watanzania wengi watapata ajira na pia kiwanda kitatumia sukari ambayo ni salama kwa afya zetu na pia kuongeza upatikanaji wa sukari hapahapa nchini,” alisema.

Kuhusu Tanesco, Rais Magufuli alisema suala hilo hawezi kulifumbia macho kwakuwa Tanzania ya viwanda inategemea zaidi upatikanaji wa umeme wa uhakika.

“Saa nyingine  inashangaza kweli, kiwanda kinaanza kujengwa, watu wapo, kinakamilika, watu wapo, kinaanza kufanya kazi watu wapo, kinaajiri watu wote hawa, wanafunga jenereta lao, tena makao makuu ya Wizara ya Nishati na Madini ipo kilomita chache  kutoka hapa,”alisema Rais Magufuli.

Rais pia alisema Serikali yake inaangalia namna ya kukutana na wataalamu kuangalia mfumo mzuri wa  kuwatoza kodi wawekezaji bila usumbufu.

Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Bakhresa, Aboubakari Salim alisema kuna urasimu mwingi katika upatikananji wa maeneo mapya ya kuanzisha viwanda.

“Tasisi za utozaji kodi zimekuwa nyingi ambapo utendaji wake ni ule ule hivyo zinatupa usumbufu katika utendaji wetu, tungeomba zipungue ili tufanye kazi kwa ufanisi zaidi,”alisema Salim.

Naye Meneja Mawasiliano wa Kampuni ya Azam, Hussein Ally, alisema kiwanda hicho kimeweza kutoa ajira 600 kwa Watanzania,  ambapo kati ya hizo wenye ajira za kudumu ni  380.

Kampuni ya Azam ina jumla ya viwanda 13 ambapo viwanda 11 vipo  Dar es Salaam na vingine viwili vipo Pwani.

Kwa upande wake Waziri wa Viwanda Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage alisema kuwa uwekezaji uliofanywa na makampuni ya Bakhresa unasaidia kuchochea kilimo cha matunda na kutoa fursa ya soko la uhakika kwa wakulima.

Simba yamwomba msamaha Rais Magufuli kwa mashabiki wake kuvunja viti vya Uwanja wa Taifa

0
0
Baada ya kujitokeza tukio la mashabiki wa Simba kuvunja viti vya Uwanja wa Taifa katika mchezo wa Yanga na Simba kisha Rais John Magufuli kuelezea masikitiko yake kwa kile kilichojitokeza katika mchezo huo, klabu ya Simba imejitokeza na kumuomba rais msamaha.

Akizungumza na waandishi wa habari, Msemaji wa Simba, Haji Manara amesema klabu inakubali kufanya kosa hilo na kwa pamoja kuanzia rais hadi mashabiki wanaomba msamaha kwa Rais Magufuli na kuahidi jambo hilo halitajitokeza tena.

“Rais wa klabu ya Simba, kamati ya utendaji, sekretarieti, benchi la ufundi na wachezaji, wanachama na mashabiki wa Simba wanaomba radhi kwa Rais wa Tanzania, Dk. John Pombe Magufuli kupitia kwa waziri mwenye dhamana ya michezo, Nape Nnauye kwa kitendo kisicho cha kiungwana kilichofanywa na mashabiki wetu katika mchezo wa Yanga,

“Tumeona twende mbali na tumwombe radhi rais wetu, hizi ni rasirimali zetu, zinajengwa na kodi zetu, serikali inatumia gharama  kubwa kuziendeleza rasirimali hizi, ni upuuzi wa hali ya juu kabisa kufanyika kitendo kama kile,” alisema Manara.

Aidha Manara amesema klabu ya Simba inaamini serikali itawaruhusu tena kuendelea kutumia uwanja wa taifa na kwa wanachama wote ambao watabainika kufanya uharibifu ule watachukuliwa hatua za kisheria.

“Tunaamini serikali itarudi nyuma na kuturuhusu kutumia uwanja wa taifa na katika hili tunaahidi tukio kama lile halitajitokeza tena, na kama klabu itabaini kuwa kuna wanachama wetu walishiriki kufanya tukio lile watachukuliwa hatua,

“Na tunaiomba serikali ifunge zile kamera za CCTV pale uwanjani ili tukio kama lile likijitokeza iwe rahisi kuwabaini waharifu waliohusika, ule ni uharifu wa makusudi, leo klabu inapata hasara, tunahangaika kufanya vikao mara wizara mara shirikisho kwa ajili ya watu wachache,” alisema Manara.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images