Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Ufafanuzi wa TRA kuhusu ongezeko la thamani kwenye huduma za kifedha

$
0
0

UPOTOSHAJI kuhusu makato ya Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) katika miamala ya benki na simu za mikononi, uliotangazwa na baadhi ya benki, umeilazimu Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kutoa ufafanuzi na  kuzuia benki hizo kutoza kodi kwa wateja wao.

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Kamishna Mkuu wa TRA, Alphayo Kidata, alihoji kwa nini mabenki yametoa matangazo ya kuanza kutoza kodi hiyo, wakati hata kanuni za utekelezaji wa sheria hiyo hazijatolewa.

Kidata alisema pamoja na kupitishwa kwa sheria hiyo bungeni, lakini muongozo unaotokana na kanuni bado haujatolewa, ndio maana TRA imeshindwa kuelewa kwanini taasisi hizo zimetoa taarifa zao kwa wananchi.

Kutokana na hali hiyo ya kutoa matangazo ya kutekeleza sheria hiyo, wakati kanuni za kutekeleza sheria yenyewe hazijatolewa, Kidata alisema kumeonekana dalili za nia ovu.

“Tangu lini mmeona benki au taasisi ya fedha inaanza kutoa matangazo ya utekelezaji wa sheria za serikali? Hii ni kwa sababu ya nia ovu. 

“Kuna taarifa ambazo si za kweli zinazoenezwa kupitia mitandao ya kijamii kuwa VAT itatozwa kwenye amana ya mwenye fedha kwenye benki. Hii si kweli,” alisema Kidata.

Usahihi wa kodi
“Juzi Bunge la Tanzania lilipitisha marekebisho ya sheria hiyo ya mwaka 2014 kuanzia Julai mosi mwaka huu kwenye huduma za kifedha kwa kurekebisha kifungu cha 13 cha jedwali la msamaha wa kodi, lakini taasisi hizo zimekuwa zikipotosha umma,” alisema.

Alisema kutokana na upotoshaji huo, TRA imeamua kueleza ukweli kuhusu utekelezaji wa sheria hiyo, ili kuondoa utata na upotoshaji unaohusu utekelezaji wa sheria hiyo.

Kidata alisema sheria hiyo inalenga kutoza VAT kwa kiwango cha asilimia 18, kwenye ada ambazo benki zinatoza wateja wake katika huduma mbalimbali zitolewazo na benki au taasisi za fedha.

“Ukweli ni kuwa kiasi cha VAT kitakachotozwa ni asilimia 18 ya kiasi cha gharama ya huduma iliyotolewa na benki au taasisi yoyote ya fedha na si kwa mteja,” alisema.

Akitolea mfano suala hilo, Kidata alisema kama ada ya huduma ya benki ambayo mteja ametozwa ni Sh 1,000, VAT itakayotozwa kwenye kiasi hicho ni Sh 152.50 tu na benki kubaki na Sh 847.50 na si kuwaongezea wananchi mzigo.

“Kiwango hiki cha Sh 152.50 ndicho kitakachorejeshwa serikalini na benki au taasisi ya fedha baada ya kupunguza VAT iliyolipwa kwenye manunuzi ambayo yamefanywa kwa benki au taasisi ya fedha husika. Kwa mujibu wa sheria hii, VAT haitatozwa kwenye riba inayotozwa na benki kwenye mikopo,” alisema.

Alisema kuna maelezo yametolewa na moja ya benki hapa nchini kuwa mtumiaji wa huduma za kifedha, atatakiwa kulipia kwa fedha taslimu kama muamala husika haukupitia kwenye akaunti na kuongeza kuwa taarifa hiyo siyo sahihi, kwa kuwa ukusanyaji wa VAT husika, utafanywa kwa njia ile ile ambayo gharama za huduma za kifedha zinakusanywa sasa.

Kidata alisema TRA itatoa maelekezo ya namna utoaji wa risiti za kielektroniki utakavyofanyika, ili kuwezesha mabenki au taasisi za kifedha kutimiza matakwa ya kisheria ya VAT ya mwaka 2014 kama ilivyorekebishwa mwaka 2016.

“Hivyo tunazitaka benki na taasisi za fedha zilizoamua kwa makusudi kutoa taarifa zisizo sahihi kwa umma, kuacha mara moja vinginevyo hatua kali za kisheria zitachukuliwa.

 “Kimsingi benki na taasisi za fedha zinazohusika zinaagizwa kurekebisha mara moja taarifa walizokwishazisambaza ili zibebe maudhui sahihi ya marekebisho ya sheria hii,” alisema.

Barua BoT
Alisema katika hatua za awali, tayari wamewapa maelekezo Benki Kuu (BoT) ambayo ni msimamizi wao mkuu, ihakikishe hicho kinachofanyika kinasitishwa na hatua mbalimbali za kisheria zitachukuliwa.

“Mwanzo benki na taasisi hizo za fedha zilikuwa zikichukua tozo yote wanayotoza, hivyo sasa tumewataka katika hiyo hiyo waliyokuwa wakichukua, ndiyo watoe kodi na si kumuongezea mwananchi mzigo kwa sababu kila kodi ina msingi wake na si kila kodi inapopanda, imlenge mwananchi. Sisi tumelenga hiyo hiyo wanayotoza,” alisema.

Alitoa mwito kwa mtu yeyote mwenye uhakika kuwa ameongezewa makato na benki au taasisi za fedha kwa madai ya utekelezaji wa sheria hiyo, atoe taarifa ili hatua zaidi za kisheria zichukuliwe.

Majengo Ya Mahakama ya Mafisadi Kukabidhiwa Jumatatu

$
0
0
WAKATI Mahakama Maalumu ya Ufisadi na Uhujumu Uchumi ikitarajiwa kuanza wakati wowote, majengo ya mahakama hiyo yanatarajiwa kukabidhiwa keshokutwa jumatatu.

Jaji Mkuu, Mohamed Othman Chande, alisema jana kuwa mkandarasi aliyekabidhiwa kazi ya kukarabati majengo hayo yaliyopo katika Shule Kuu ya Sheria, pembeni mwa kituo cha mabasi cha Simu 2000, Ubungo Dar es Salaam, yako katika hatua za mwisho za ukarabati.

Akizungumza katika viwanja vya Karimjee baada ya kuapisha mawakili wapya 623 wa Mahakama Kuu, Jaji Chande alisema tayari Bunge limeshapitisha muswada wa sheria ya uanzishwaji wa mahakama hiyo.

Alisema kwa sasa muswada huo utawasilishwa kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa ajili ya kuusaini ili uwe sheria, kisha sheria hiyo itatangazwa katika gazeti la Serikali ili kuruhusu shughuli za mahakama hiyo kuanza.

Kwa mujibu wa Jaji Mkuu, Mahakama iko tayari kuendesha Divisheni hiyo ya Mahakama na baada ya kukabidhiwa majengo hayo, wataanza kutoa semina kwa majaji na watumishi wengine wa mahakama hiyo, kuhusu divisheni hiyo itakavyoendesha shughuli zake.

Aliweka wazi kuwa mpaka sasa hakuna kesi hata moja iliyokwishatambuliwa kwamba itashughulikiwa na mahakama hiyo.

Askofu Gwajima ni Mgonjwa.....Ashindwa Kutokea Mahakamani Kwenye Kesi Inayomkabili

$
0
0
PETER Kibatala wakili wa Josephati Gwajima Askofu wa Kanisa la ufufuo na uzima jana aliiomba mahakama kuahirisha tarehe ya kusikiliza kesi inayomkabili askofu huyo sababu anaumwa.
 
Kibatala alidai mahakamani Kisutu kuwa kutotokea kwa mteja wake jana kulitokana na yeye kuwa nje ya nchi kwa ajili ya matibabu.

Wakili huyo  aliwasilisha madai hayo jana katika Mahakaama ya Hakimu Mkazi Kisutu mbele ya Hakimu Syprian Mkeha Hakimu Mfawidhi anayesikiliza kesi hiyo inayomkabili Gwajima

Mahakama ilikubali ombi hilo na kwamba kesi hiyo itatajwa tena 2 Agosti mwaka huu.

Katika kesi hiyo Gwajima anadaiwa kutoa lugha ya matusi dhidi ya Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo, Askofu wa Mkuu wa Kanisa Katoliki Jimbo la Dar es Salaam.

Gwajima anadaiwa kufanya tukio hilo kati ya 16 na 25 Machi, mwaka 2015 katika Viwanja vya Tanganyika Packers Wilaya ya Kinondoni, Dar es Salaam.

TRA Yaifungia Kampuni ya Mkono kwa Kudaiwa kodi Sh. Bilioni 1.1

$
0
0
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kupitia kampuni ya udalali ya Yono Auction Mart & Co imeifungia kampuni ya Mkono & Company Advocate kwa kushindwa kulipa malimbikizo ya kodi inayofikia Sh1 bilioni. 

Kampuni hiyo inahusishwa na Mbunge wa Musoma Vijijini, Nimrod Mkono (CCM) ambaye pia ni wakili maarufu nchini. 

Hata hivyo, Mkono hakupatikana mara moja kuzungumzia suala hilo. Hati ya TRA iliyosainiwa na Kamishna wa TRA, Neema Mrema imesema Yono imepewa mamlaka na Kamishina Mkuu wa mamlaka hiyo chini ya kifungu cha 64 cha Sheria ya Kodi ya mwaka 2015 ya kushika mali za mdaiwa anayeshindwa kulipa kodi. 

“Naomba kupata usaidizi wa Yono Auction Mart &Company Ltd na Polisi kutaifisha na kuhamisha bidhaa na mali popote zilipo ili kwa njia yoyote zikiuzwa zilipe deni jumla ya Sh1,101,432,045.99 pamoja na gharama za wito uliotolewa chini ya Kamishna….” ilisema sehemu ya hati hiyo.

Akizungumzia suala hilo, Mkurugenzi wa Yono Auction Mart Co. Ltd, Stanley Yono alikiri kuifungia kampuni hiyo mpaka itakapolipa deni hilo. 

“Ni kweli tumeifungia kampuni ya uwakili ya Mkono na hapa tuko kwenye eneo la tukio. Anadaiwa zaidi ya Sh1 bilioni ikiwa ni malimbikizo ya VAT (Kodi ya Ongezeko la Thamani), kodi za mishahara na nyinginezo kwa mwaka mzima. Amegoma kutia saini hii hati lakini haitasaidia kitu kwani tumeshamfungia,” alisema Yono. 
 
Mkurugenzi wa Elimu na Huduma kwa Mlipa kodi wa TRA, Richard Kayombo alikiri kuifungia kampuni hiyo. 

Tamko la RC Makonda kuhusu mashoga waliopo jijini Dar es Salaam

$
0
0

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda ametangaza vita na makaka poa (mashoga) na madada poa (makahaba) walioko jijini Dar es Salaam kuwa utaendeshwa msako mkali wa kuwaondoa.

Mkuu wa Mkoa huyo aliyasema hayo kufuatia hali ya vitendo hivyo visiyokubalika na jamii kuzidi kushamiri na kuwa kuna hatari kubwa ya watoto wadogo kuiga vitendo hivyo vinavyoleta picha mbaya kwani ni kinyume na maadili ya mtanzania.

Aidha alisema hawezi kuifumbia macho hali hii kwani inamomonyoa maadali ya jamii na kuwa yuko tayari kulivalia njuga suala hili ili kuhakikisha anawamaliza wote mkoani

Sakati hili la ushoga na ukahaba limeibuka siku za hivi karibuni baada ya kituo cha televisheni cha Clouds Tv kumhoji shoga mmoja ambapo jamii ilipinga kitendo hicho na kuona kama walikuwa wakiuhalalisha ushoga na kuaminisha jamii kuwa ni kitu kizuri.

Rufani ya Sheikh Ponda Yakwama Mahakama Kuu

$
0
0
RUFANI ya Jamhuri kupinga hukumu ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Morogoro kumwachia huru Sheikh Ponda Issa Ponda, dhidi ya kosa la kushawishi wakazi wa mkoa huo kufanya kosa, ilikwama kuendelea jana na kuahirishwa kwa wiki tatu baada ya mawakili wa utetezi kuomba muda wa kujadili na mteja wao.

Jana kesi hiyo ilitajwa na Jaji Edson Mkasimongwa katika Mahakama Kuu Tanzania, Kanda ya Dar es Salaam.
 
Wakili wa Serikali Malangwe Mchungahela alidai kuwa kesi hiyo ilipangwa kutajwa jana kwa ajili ya kupanga tarehe ya kuanza kusikiliza.
 
Hata hivyo, mawakili wa utetezi, Abubakar Mohammed na Juma Nassoro, kwa nyakati tofauti waliomba mahakama kuwapa muda wa kuzungumza na Sheikh Ponda, kama wataendelea kutoa huduma kwake ama la.
 
Nassoro alidai kuwa makubaliano yao ya awali ya kumtetea katika mahakama ya chini yalishamalizika, na hakuna maelekezo yoyote ili kuweza kumuwakilisha mahakamani hapo. Jaji Mkasimongwa alisema kesi hiyo itasikilizwa Julai 23.
 
Katika rufani hiyo, upande wa Jamhuri uliwasilisha hoja nne ikiwemo, mahakama ya chini ilikosea kwa kutokuzingatia uzito wa ushahidi wa kielektroniki katika kutoka uamuzi wake.
 
Sababu ya pili na ya tatu, Jamhuri inadai, Hakimu wa Mary Moyo alikosea aliposema hati ya mashtaka ilikuwa na mapungufu ya kisheria na Sheikh Ponda hakuwa na nia ya kushawishi umma wa mkoa huo kufanya kosa siku ya tukio.
 
Sababu ya mwisho ya Jamhuri katika kupinga kuachiwa huru kwa Sheikh Ponda ni kwamba hakimu alikosea kusema kuwa ilishindwa kuthibitisha kosa bila kuacha shaka.

RIWAYA: Mwanafunzi Mchawi ( A Wizard Student ) - Sehemu ya Nane

$
0
0
Mtunzi: Enea Faidy

Ilipoishia sehemu ya Saba ( kama hukuisoma bofya hapa)...
....Mwalimu John alidhaniwa kufariki, hivyo harakati za mazishi ziliandaliwa.. Je John alikufa kweli?
Dorice alikuwa kwenye harakati za kutoroka, lakini kuna kitu kilimshtua..

Eddy alipewa sharti la kutofanya mapenzi na Doreen lakini tayari hamu ya mapenzi ilimvaa kwa kasi ya ajabu. Je atafanya mapenzi na Doreen?..

ENDELEA...

... MIPANGO YA MAZISHI kumzika mwalimu John ilikuwa tayari imekamilika, ndugu walikuwa tayari wamewasili kwa majonzi. Huzuni iliwatawala sana kwani mwalimu John alikuwa ndiye tegemezi la familia yote kwa ujumla. Kelele za vilio zilitawala mtaa mzima aliokuwa akiishi mwalimu John, kila MTU alisema lake juu ya msiba ule lakini ukweli haukujulikana.

Make wa mwalimu John alipoteza fahamu kila Mara huku akijutia tendon alilomfanyia mumewe kwa kumpiga na upawa kichwani .Lakini alijiahidi kutomwambia mtu yoyote akihofia kukamatwa kwa kosa la mauaji. Nyuso za watu wote zilitia huruma sana kwa kuondokewa na mwalimu John kipenzi cha watu wengi.

Walimu kutoka shule ya sekondari Mabango walikuwepo pale msibani wakimuaga mwalimu mwenzao.

Jeneza la gharama lilitengenezwa, mwili wa mwalimu John ukawekwa ndani ya jeneza. Make wa mwalimu John alikuwa haamini kama mume wake ndo anapelekwa kuzikwa.. Aliachia yowe Kali lililowashtua wote pale msibani "Rudi mume wangu.. Rudi mpenzi wangu usife..." Alilia mke wa John.

Wazazi wake walikuwa wakigalagala chini kama wehu,hawakujali vumbi lililokuwa limetapakaa ardhini kutokana jua Kali la kiangazi.

Hatimaye Jeneza lililokuwa limebeba mwili wa marehemu John likaingizwa kwenye gari kwaajili ya kupelekwa makaburini huku likisindikizwa na nyimbo za huzuni zinazopigwa misibani. Watu wote wakaelekea makaburini kwani magari ya kutosha yalikuwa yamekodiwa.

Mwalimu John alikuwa ndani ya Jeneza akilia kwa sauti ili Atolewe kwani alikuwa hajafa. Lakini hakuna MTU yeyote aliyesikia kilio cha Mwalimu John wala kuhisi, " Inamaana wananizika mzimamzima?" Alijiuliza mwalimu John huku moyo wake ukiwa umezimia kwa mile akionacho.

"Haiwezekani nizikwe mzima mzima! Hapana" alisema Mwalimu John huku akijaribu kujiinua lakini mwili wake ulikuwa bado mzito kama vile umegandishwa na barafu. Akiwa ndani ya jeneza hilo akasikia kicheko kikali sana kutoka kwa Doreen.

"Doreen nisamehe tafadhali" alijitetea Mwalimu John.
Machozi yalizidi kumtoka kwa kasi sana , ndipo alipokumbuka kosa lake kwa Doreen.

Zilikuwa ni wiki mbili tangu Doreen ahamie shule ya Mabango, kutokana na uzuri na utanashati wa mwalimu John. doreen alivutiwa nae sana hivyo akaamua kumwambia ukweli mwalimu wake kuwa anampenda na anahitaji kuwa naye kimapenzi. Mwalimu John alimtazama binti yule kwa jeuri na dharau kisha akamjibu " We mtoto ni mpumbavu sana! Umezunguka kote huko ukaona uniletee umalaya wako hapa? Mbwa koko wewe hebu niondokee hapa!"
 
"Mwalimu John hunitaki? Unanitusi? Sasa nitakuonyesha kazi!" Alisema Doreen kwa kujiamini sana kisha akaondoka zake
.
Wakati Mwalimu John akiendelea na kumbukumbu hizo ghafla akahisi jeneza lake linanyanyuliwa Tayari kwa kumuweka kaburini...

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumapili ya July 3


CHADEMA Waapa Kutibua Mkutano wa CCM .....Vijana 2000 Kupelekwa Dodoma Kwa Ajili ya Kazi Hiyo

$
0
0
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimepanga kulisaidia Jeshi la Polisi kuzuia Mkutano Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Hivi karibuni Jeshi la Polisi lilitoa zuio la mikutano ya siasa ya wazi na ya ndani nchini kote, hata hivyo CCM imepanga kufanya Mkutano Mkuu tarehe 23 Julai mwaka huu mjini Dodoma.

Kwenye mkutano huo, Dk. Jakaya Kikwete, Mwenyekiti wa CCM atakabidhi mamlaka hayo kwa Dk. John Magufuli ikiwa ni utaratibu wa kawaida wa chama hicho.

Baraza la Vijana wa Chadema (Bavicha) limepanga kuzuia mkutano huo kwa madai ya kulisaidia Jeshi la Polisi kusimamia agizo lake kwa vyama vya siasa nchini.

Wakizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Slaam viongozi wa Bavicha walisema, hatua hiyo ni katika kuhakikisha wanalisaidia jeshi kutekeleza amri iliyotolewa na Rais Magufuli ya kuzuia mikutano ya vyama vya siasa hadi mwaka 2020.

“Tumeandaa vijana takribani 2000 kutoka mikoa yote nchini watakaokwenda Dodoma kusaidiana na Jeshi la Polisi kutawanya mkutano usio halali wa CCM.  Kwa sababau Jeshi la Polisi limezuia mikutano yote ya siasa kwa sasa.

“Pia ni katika kuunga mkono kauli ya Rais Magufuli kwamba, hakuna mikutano ya vyama vya siasa mpaka mwaka 2020. Huu ndio msiamamo wa baraza.

“Mikutano yetu sisi kama Chadema tunazuiwa lakini CCM wanafanya. Mahafari ya chama cha mapinduzi yanafanyika. Ni jana CHASO (Jumuiya ya Wanafunzi wa Vyuo Vikuu Chadema) Morogoro tumezuiwa lakini UVCCM (Umoja wa Vijana wa CCM) Mkoa wa Morogogo wamefanya na picha zipo. Hii sio haki, kama mbwai na iwe mbwai,” alisema Patrick ole Sosopi, Makamu Mwenyekiti wa baraza hilo.

George Tito, Mwenyekiti wa Bavicha Mkoa wa Mbeya alisema “… ni kwamba, huko mikoani vijana wameshajipanga. Wana ari kubwa ya kwenda Dodoma.

“Tumeamua kufikia hatua hii kwa sababu tumekuwa tunaona hakuna haki katika nchi hii. Kuna mahafali yanafanyika vyuo vikuu, wenzetu CCM wanaruhusiwa sisi Chadema tunakatazwa.Vijana wa Chadema wamekuwa wakikamatwa bila sababu za msingi,” alisema Tito.

Rais Magufuli Atuma salamu za Rambirambi Ajali Morogoro Iliyoua Watu 12

$
0
0
 TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amezitumia salamu za pole familia, ndugu, jamaa na marafiki wa watu 12 waliopoteza maisha kufuatia ajali mbili zilizotokea katika eneo moja la VETA Dakawa, Tarafa ya Dumila, Wilaya ya Kilosa Mkoani Morogoro.

Ajali ya kwanza imetokea majira ya saa 11:30 jioni ya tarehe 30 Juni, 2016 ambapo watu 5 wamefariki dunia kufuatia malori mawili, mojawapo likiwa na shehena ya mafuta kugongana na kisha kuwaka moto, na ajali ya pili ikatokea hapohapo majira ya saa 10:00 alfajiri ya tarehe 01 Julai, 2016 baada ya basi la kampuni ya Otta High Class kuligonga lori la mafuta lililokuwa likiungua moto na kusababisha vifo vya watu 7 mpaka sasa.

Katika salamu zake kupitia kwa Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dkt. Steven Kebwe, Rais Magufuli amesema amepokea kwa mshituko na masikitiko taarifa za vifo vya watu hao ambao licha ya taifa kupoteza nguvu kazi muhimu, ndugu, jamaa na marafiki wamepoteza watu waliowategemea na wapendwa wao.

“Ndugu Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dkt. Steven Kebwe naomba unifikishie salamu zangu za pole kwa wote waliopatwa na msiba na uwaambie naunga nao katika kipindi hiki kigumu cha majonzi.

“Pia nawaombea wawe na moyo wa uvumilivu na ustahimilivu na Mwenyezi awapumzishe marehemu wote mahali pema peponi, Amina” amesema Rais Magufuli.

Rais Magufuli pia amewaombea majeruhi wote waliolazwa hospitali na wale wanaoendelea kupata matibabu wakiwa majumbani, kupona haraka ili waendelee na kazi zao za kila siku.

Gerson Msigwa
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
Dar es salaam
02 Julai, 2016

Makamu wa Rais Samia Aviagiza viwanda Vyote nchini Kutumia Msibomilia (BARCODES)

$
0
0
 TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania SAMIA SULUHU HASSAN ameviagiza viwanda vyote nchini kutumia msibomilia (BARCODES) za Tanzania kama hatua ya kuimarisha masoko na utambulisho wa bidhaa za Tanzania katika masoko ya ndani na ya nje ya nchini.

Makamu wa Rais ametoa agizo hilo kwenye uzinduzi wa kampeni ya “NUNUA 620 Nunua Bidhaa za Tanzania” pamoja na Kusherekea miaka MITANO ya Taasisi ya Global Standard One –GSI-kwenye Viwanja wa Mwalimu Nyerere katika Maonyesho ya  40 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es salaam (SABASABA) mara baada ya kutembelea mabanda mbalimbali ya maonyesho.

Makamu wa Rais amesema matumizi ya BARCODES ni muhimu na ni ya lazima kwa sababu yanajumuisha taarifa nyingi ikiwemo asili ya bidhaa,jina la kampuni, kumbukumbu za uzalishaji,utunzaji,usafirishaji na usambazaji wa bidhaa.

Ameleeza kwamba itakuwa ni aibu kubwa kama katika masoko ya ndani ya nchi bado kutakuwa na bidhaa zinazotumia msibomilia (BARCODES) za nje na  kusisitiza kuwa matumizi ya Barcodes za Tanzania zitazuia na kupungua upotevu wa ajira kwa wataalamu wa ndani ya nchi.

Makamu wa Rais SAMIA SULUHU HASSAN amesema kuwa serikali ya awamu ya TANO ipo Tayari kufanya kazi na sekta binafsi katika kuleta mapinduzi makubwa yatakayosaidia kukuza uchumi wa taifa.

Kuhusu uanzishwaji wa Majukwa ya kumwezesha wanawake Kiuchumi  nchini, Makamu wa Rais amesema kuwa atahakikisha majukwaa hayo yanaleta matokeo chanya na yenye tija kwa wanawake Wakitanzania mijini na viijijini kwa kuwezeshwa kupata kupata elimu ya ujasiriamali,fursa za masoko,upatikanaji wa mikopo nafuu pamoja na elimu ya kukabiliana na changamoto mbalimbali zinazowakwaza wanawake kiuchumi.

Makamu wa Rais pia ametoa wito maalum kwa wanawake kote nchini kujiunga na majukwaa hayo pindi yatakapoanzishwa kwenye maeneo yao kwa sababu yatakuwa na faida kubwa kwao kwa kuunganisha nguvukazi zao na kuzalisha bidhaa zenye ubora wa hali ya juu.

Imetolewa na
Ofisi ya Makumu wa Rais
2-Jul-16

Makonda Apiga Marufuku Kuvuta Sigara Hadharani......Pia Kapiga Marufuku Kuvuta Shisha

$
0
0
Baada ya kutangaza vita dhidi ya mashoga juzi, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda jana alitangaza vita nyingine; hataki uvutaji shisha akisema inachanganywa na vilevi vinavyoharibu vijana. 

Makonda, ambaye alikuwa akihutubia Tamasha la Vijana lililoandaliwa na Upendo Media Group kwenye Uwanja wa Taifa aliagiza wavuta shisha hadharani, sigara na mashoga wakamatwe ndani ya siku saba. 

“Ni marufuku biashara ya shisha kwenye mkoa wangu. Wanaofanya bishara hiyo wote nitawakamata. Mimi ndiye mbabe wa vita,” alisema Makonda na kuongeza: “Nina imani watakuwa wamefungasha virago vyao iwe ni kwenye klabu au baa maana humo wanachanganya vitu vingi; bangi na vilevi ambavyo vina madhara.” 

Alisema vijana wa vyuo na sekondari ndiyo waathirika wakubwa wa kilevi hicho, ambacho huvutwa kwa njia ya bomba la mpira linalotoka kwenye jiko maalumu ambalo tumbaku huunguzwa na kutoa moshi. 

“Baada ya siku saba tutakutana (Gereza la Segerea),” alisema. 

“Kwa utafiti nilioufanya chini ya TFDA, shisha ina madhara makubwa kwa wanaoivuta na wasiovuta. Inasababisha kansa ya mapafu na koo. 

“Na pia inasababisha utegemezi ambapo mtu bila kuvuta hawezi kuona maisha, lakini pia inapunguza uwezo wa kufikiri na inamaliza nguvu kazi katika taifa,” aliongeza. 

Kwa mujibu wa Shirika la Afya Duniani (WHO), kiwango cha shisha inayovutwa kwa saa moja, ni sawa na kuvuta sigara kati ya 100 na 200. 

Utafiti wa shirika hilo unaonyesha kuwa mvuta sigara wa kawaida huingiza nusu lita ya moshi kwa kila sigara, lakini mvuta shisha ni zaidi ya hivyo. 

Kuhusu uvutaji wa sigara, Makonda alisema ndani ya siku saba zijazo ni marufuku kuvuta sigara hadharani na kila anayehitaji kufanya hivyo atapaswa kutafuta sehemu iliyojitenga ili akate kiu yake. 

“Kila anayevuta sigara, atapaswa kuvuta sehemu ambayo hatawabughudhi wenzake. 

"Tumechoka kupanda magari na watu wanaovuta sigara, kukaa hoteli na watu wa aina hiyo. Sasa mvutaji anapaswa kuvuta sehemu ya peke yake, na sio kwenye jumuiko la watu. Madhara ni makubwa kwa tusiovuta kuliko wanaovuta,” alisema. 

Maagizo ya Makonda yanakuja ikiwa ni wiki moja tangu apige marufuku abiria na dereva wa bodaboda kusafiria chombo hicho bila ya kuvaa kofia ngumu. 

Alisema kupanda pikipiki bila kofia hiyo ni dhamira ya kutaka kujiua kwa sababu dereva na abiria wakipata ajali ni rahisi zaidi kupoteza maisha iwapo kichwa kitajipiga ardhini. 

“Nimewasiliana na kamati yangu ya usalama barabarani ya mkoa. Hili nitalisimamia kikamilifu lazima wote wavae helmet na wakikamatwa wote watashtakiwa,” alisema. 

Mapema mwaka huu, mara baada ya kuteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa, Makonda alitoa maagizo matatu yanayohusu ombaomba wa barabarani kuondoka na kubomolewa kwa majengo makubwa yaliyojengwa kinyume na taratibu na yasiyo na maegesho.

Agizo la tatu la Makonda lilikuwa ni wamiliki wa baa kutopiga muziki nje ya utaratibu wa vibali vyao. 

Makonda pia alirudia wito wake wa kutaka watu wanaojishughulisha na biashara ya ushoga wakamatwe mara moja. 

Alisema miaka michache iliyopita Taifa lilikataa msaada wenye sharti la ushoga, lakini inashangaza kuwa bado zipo taasisi zisizo za kiserikali zilizoundwa kwa ajili ya kutoa misaada kwa watu wanaojihusisha na vitendo hivyo.

 “Nimefanya mazungumzo na  Waziri wa Katiba na Sheria. Hatutaki hili liendelee kwa sababu hiyo naiagiza TCRA kuwa wapo watu wanaojitangaza kwenye instagram na vyombo vya habari kwamba wao ni mashoga, wakamatwe haraka iwezekanavyo na kama kuna shoga ana akaunti kwenye mitandao ya kijamii na wale wafuasi wake wote ni watuhumiwa sawasawa na mhusika,” alisema. 

Ushoga, ambao ni uhusiano wa mapenzi wa watu wa jinsia moja, ni marufuku nchini, kwa mujibu wa Sheria ya Adhabu. 

Kwa mujibu wa Sura ya 16, sehemu ya 154, mtu anayejihusisha na ngono na mtu mwingine kinyume na maumbile au anayemruhusu mtu mwingine kufanya naye ngono kinyume na maumbile, atakuwa amefanya kosa la jinai na kustahili kifungo cha miaka 14 jela.

Mkuu wa Wilaya Mteule wa Mbozi, Ally Masoud Maswanya ajiuzulu

$
0
0
Kada aliyeteuliwa kuwa mkuu wa Wilaya ya Mbozi, Ally Muswanya ameachia wadhifa huo hata kabla ya kuapishwa.

Wakati uteuzi wa makada watatu wa kwanza ulisahihishwa na Ikulu, Maswanya hajaibuka kwenye hafla ya kiapo na tayari mtu mwingine amekwenda kuziba nafasi yake. 

Maswanya, ambaye alikuwa aapishwe juzi na mkuu wa Mkoa wa Songwe, Chiku Galawa, hakuapishwa na badala yake aliapishwa John Palingo ambaye katika uteuzi uliotangazwa na Ikulu alikuwa aongoze Wilaya ya Kongwa. 

Taarifa za Maswanya kuachia nafasi hiyo zilianza kusambaa kwenye mitandao ya kijamii juzi usiku zikieleza kuwa amejiuzulu nafasi hiyo, lakini haikuelezwa sababu za kuchukua uamuzi huo wa kukataa kumwakilisha Rais wilayani. 

Hata hivyo, Maswanya, ambaye ni meneja wa kampuni ya huduma za simu ya Tigo, Kanda ya Ziwa, hakutaka kuzungumzia kwa kina sakata hilo. 

“Kama ambavyo inajulikana, mimi ni meneja wa Kanda wa Tigo,” alisema Maswanya alipozungumza na Mwandishi

“Hayo ndiyo yako kwenye mamlaka yangu kuzungumzia. Kama ni suala la Tigo, karibu tuzungumze yote kuhusu mipango na mikakati yetu.” 

Maswanya alisema kwa sasa, nguvu akili na uwezo wake wote anaelekeza katika kutimiza wajibu kwenye nafasi hiyo yake Kanda ya Ziwa. 

Hata baada ya kuulizwa kama ndiye aliyekataa uteuzi, Maswanya alisisitiza “Hayo yatazungumziwa na mamlaka husika ambazo naamini kwa nafasi yako unazijua.” 

Alipoulizwa kama Maswanya alihudhuria hafla ya kula kiapo ya wakuu wa wilaya katikati ya wiki, kaimu mkurugenzi wa Idara ya Mawasiliano ya Rais, Gerson Msigwa alisema hafahamu kama alikuwapo au la kwa kuwa wengi ni wakuu wapya hivyo haikuwa rahisi kwake kujua nani hakuwapo.

Sarakasi ya meneja huyo kutochukua madaraka aliyopewa na Rais inafanya idadi ya watu walioteuliwa na kushindwa kuanza kazi kutokana na sababu tofauti kufikia wanne. 

Kabla ya wakuu wateule kula kiapo cha maadili Ikulu jijini Dar es Salaam, Rais Magufuli alieleza kuwa uteuzi wa wakuu hao ulifanywa kwa makini na kwamba anafahamu kwa majina watu wote aliowateua, akisema alizingatia umri, elimu na uzoefu. 

Tukio la kwanza lilikuwa la uteuzi wa Fikiri Said kuwa mkuu wa Wilaya ya Ikungi, lakini akabadilishwa kwa maelezo kuwa jina lake liliwekwa kimakosa. Badala yake aliyekuwa katibu wa CCM wa Mkoa wa Mwanza, Miraji Mtaturu akateuliwa kuchukua nafasi hiyo. 

Pia aliyeteuliwa kuongoza Wilaya ya Rombo, Fatma Toufiq alibadilishwa kwa maelezo kuwa tayari alishakuwa na wadhifa mwingine wa ubunge wa viti maalum na nafasi yake akapewa Agness Hokororo. 

Rais John Magufuli alisema wakati akielezea suala hilo kuwa hakutaka mtu ashike nafasi mbili kwa wakati mmoja na kwamba hiyo ndiyo tafsiri ya falsafa ya “Hapa Kazi Tu”. 

Tukio lililokuwa la aina yake katika uteuzi huo ni la kubatilisha uteuzi wa Emile Ntakamulenga aliyetangazwa kuwa mkuu wa Wilaya ya Serengeti. 

Hakukuwa na taarifa za awali za kubatilisha uteuzi huo na Ntakamulenga alienda Ikulu kama makada wengine, akaruhusiwa kujisajili na kuingia kwenye viwanja vya makazi hayo makuu ya nchi. 

Lakini wakati akisubiri kula kiapo cha maadili, Jaji Salome Kaganda akatoa maelezo kuwa kulifanyika makosa katika kutangaza jina lake na kwamba aliyekusudiwa alikuwa Nurdin Babu ambaye naye alikuwa ameitwa Ikulu siku hiyo.

Kutokana na makosa hayo, Jaji Kaganda alisema: “Naomba utupishe” na ndipo Ntakamulenga akanyanyuka na kuanza kuondoka kutoka viunga vya Ikulu akiacha maswali. 

Akizungumzia kutoapishwa kwa Maswanya kuwa mkuu wa Wilaya ya Mbozi na badala yake kumwapisha Palingo, Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Chiku Galawa alisema alipokea ujumbe mfupi kwa njia ya simu kutoka kwa Katibu Mkuu Kiongozi akijulishwa kwamba mtu aliyekuwa amepangiwa wilaya hiyo, John Ernest Palingo amebadilishwa kituo cha kazi, hivyo ataongoza Mbozi. 

Galawa alisema alipokea maelekezo ya ujumbe huo kutoka kwa Katibu Mkuu Kiongozi kwamba ampokee na kumuapisha ili aanze kazi mara moja, lakini akaongeza kuwa hana taarifa za mtu aliyeteuliwa awali kuwa bosi wa Mbozi. 

“Nilichofanya ni kutekeleza maagizo ya mkuu wangu,” alisema Galawa. 

“Pia mimi nilichokuwa nahitaji ni kukamilishiwa ma-DC wangu kwa wilaya zote, hivyo jana (juzi) asubuhi nilifanya mawasiliano na DC aliyeelekezwa na Katibu Mkuu Kiongozi, tukamtumia tiketi ya ndege na jana (juzi) mchana alifika na nikamuapisha kwa kuwa ni DC wa Mbozi pekee aliyekuwa amebaki.” 

Alisema siku ya Alhamisi alimuapisha mkuu wa Wilaya ya Ileje, na kwamba wengine wa wilaya za Momba na Songwe hawakutumiwa tiketi mapema, lakini walifika na juzi asubuhi aliwaapisha wakati wakimsubiri Palingo. 

Alisema kazi ya kwanza kuwapangia ni mbio za Mwenge wa Uhuru ambao uliingia jana asubuhi mkoani kwake ukitokea Mbeya. Alisema mwenge huo utawawezesha kufahamu vyema jiografia ya wilaya zao. 

Mkoani Dodoma, Jordan Rugimbana aliwaapisha wakuu wapya sita kati ya saba wa wilaya za mkoa huo baada ya Rais Magufuli kufanya mabadiliko madogo. 

Baada ya kuwaapisha wakuu hao wa wilaya, Rugimbana alielezea mabadiliko hayo ya Rais yaliyofanya akosekane mteule wa wilaya moja. 

“Aliyeteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Kongwa sasa atakwenda kuwa Mkuu wa Wilaya ya Mbozi baada ya aliyeteuliwa kujiuzulu,” alisema.

Alisema kutokana na mabadiliko hayo, Wilaya ya Kongwa inasubiri uteuzi mwingine utakaofanyika wakati wowote kuanzia sasa. 

Wakuu wa wilaya walioapishwa Dodoma ni Elizabeth Kitundu (Bahi), Vumilia Nyamoga (Chamwino), Simon Odunga (Chemba), Christina Mdeme (Dodoma Mjini), Veneranda Makota (Kondoa) na Jabir Shekimweri (Mpwapwa). 

Mwarobaini Wizi wa Bodaboda Wapatikana....VETA Wabuni Kifaa Cha Kudhibiti Wizi Huo Kwa Kutumia Simu

$
0
0

MAMLAKA ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (Veta), imebuni kifaa cha kudhibiti wizi wa magari na pikipiki za abiria maarufu bodaboda, kwa kutumia simu.

Kwa kutumia kifaa hicho, dereva atakuwa na uwezo wa kuzima pikipiki au gari kwa kutumia simu ya mkononi, ambayo namba yake itakuwa imefungwa katika chombo hicho cha usafiri.

Akizungumzia kifaa hicho, Mwalimu wa Teknolojia ya Mawasiliano wa Veta, Valerian Sanga alisema alishirikiana na mwalimu mwenzake wa chuo hicho anayefundisha masuala ya umeme, Christian Brighton kubuni kifaa hicho kilichowachukua miaka miwili kukamilika.

“Wiki tatu zilizopita ndio tumekamilisha kifaa hiki na kuanza kufanya kazi, tukafunga kwenye pikipiki hii (akionesha) kupima na kuonesha watu namna ya kuweka ulinzi kwenye vifaa vyao kwa kuwa mifumo kama hii, inauzwa katika kampuni za nje lakini ni gharama sana,” alisema.

Mwalimu huyo anatoka Kituo cha Veta Kipawa jijini Dar es Salaam, ambacho kilibuni mfumo huo ili kudhibiti wizi wa pikipiki.

Ubunifu huo ulichangia mamlaka hiyo, kupata tuzo ya mshindi wa jumla wa Maonesho ya Kimataifa ya 40 Dar es Salaam, yanayoendelea katika viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere. 

Sanga alisema kifaa hicho kina GPS na kinatumia mawasiliano ya simu kwa kutumia GSM, itakayo saidia kujua sehemu pikipiki au gari lilipo, lakini pia kikimwezesha mmiliki kuzima nakuwasha usafiri wake popote ulipo.

“Unatumia simu ya mkononi ambayo namba zako zinakuwa zimefungwa katika chombo cha usafiri, ili zikuwezeshe kuzima kama kimeibiwa ambapo baada ya dakika tano kitazima na hakitawaka mpaka utume tena ujumbe wa kutaka iwake,” alisema.

Sanga alisema kwa sasa wanafunga kifaa hicho kwa gharama ya Sh 400,000, lakini anatarajia baadaye watakapopata oda nyingi, watapunguza bei kwani kwa siku nne tangu kuanza maonesho hayo wameshapata watu wengi wanaohitaji.

“Tunategemea kupata watu wengi wanohitaji na tayari watu wawili; mmoja ana pikipiki ishirini na mwingine kumi, wametaka tuwafungie huku tukiamini mpaka maonesho yaishe tutapata wengi zaidi,”alisema.

Alisema ili kukidhi mahitaji hayo, wamekuwa wakifundisha wanafunzi wa chuo hicho ili washirikiane katika kutengeneza vifaa hivyo kwa wingi ikiwa watajitokeza wengi wanaozihitaji.

Baadhi ya watu waliotembelea kuona pikipiki hiyo, walishangazwa na utaalamu huo kufanyika nchini na kutaka serikali kusaidia, hususani wakati huu wa taifa linapojiandaa kwa uchumi wa viwanda.

Mmoja wa wananchi hao, Godwin Mlulu alisema kifaa hicho kimekuja wakati muafaka kutokana na kukithiri kwa wizi wa pikipiki. Lakini alipendekeza bei ipunguzwe, kwa kuwa wamiliki wengi wa pikipiki za biashara, ni wenye kipato cha chini.

Mwigulu Nchemba Aahidi Makubwa kwa Askari Jeshi la Polisi

$
0
0
WAZIRI wa mambo ya ndani ya nchi Mwigulu Nchemba, amesema kuwa Serikali itahakikisha inakabiliana kwa nguvu zote na tatizo la makazi ya askari polisi nchini ili kulipa hadhi jeshi hilo ambalo linakabiliwa na changamoto mbalimbali.

Nchemba aliyasema hayo jana wakati alipokuwa akizungumza na maafisa wa jeshi hilo pamoja na askari wa kawaida wa mkoa wa Dodoma katika kikao kazi kilichofanyika kwenye bwalo la jeshi hilo mjini Dodoma.
 
Mwigulu alisema kuwa mojawapo ya suala ambalo wizara yake italipa kipaumbele ni makazi ya askari wa jeshi hilo ambayo mengi hivi sasa yamechoka na kukosa hadhi ya kutumiwa na askari wa jeshi hilo.
 
“Suala la makazi tutalipa kipaumbele kikubwa sana na tutaanza hatua kwa hatua kulifanyia kazi suala hili ili askari wetu waondokana na adha hii wanayoipata kwa muda mrefu sasa,” alisema Mwigulu.
 
Alisema kero nyingine watakayoifanyia kazi ni kuhakikisha kuwa mazingira ya kufanyia kazi kwa askari polisi yanaboreshwa kuanzia kazini kwao na pia kwenye makazi yao.
 
“Kumekuwapo na tatizo la mafuta kwa jili ya magari mnayoyatumia … hata tukio likitokea mnashindwa kufika kwa kukosa mafuta. 
 
"Pia kuna maslahi duni, umeme maofisini pamoja na nyumbani mnapoishi imekuwa ni kero kubwa kwenu hivyo sisi kama wizara tutahakikisha haya yote tunayaondoa,” alisema Mwigulu.
 
Katika hatua nyingine, Mwigulu alitoa rai kwa askari polisi nchini kuhakikisha kuwa wanazingatia miiko ya kazi yao kwa kufanya kazi kwa kuzingatia maadili kama ambavyo walivyofundishwa katika mafunzo yao.
 
“Mimi uwepo wangu hapa sijaja kuwafundisha kazi kwakuwa tayari kazi yenu mnaijua… ambayo mmefundishwa mkiwa chuoni. Hivyo sisi kama wizara jukumu letu ni kuweka mazingira wezeshi ili mfanye kazi zenu katika mazingira mazuri,” alisema.
 
Aidha alilitaka jeshi hilo kutumia nguvu katika mahali panastahili tu kufanya hivyo ili hata mwanachi akisikia utendaji wao ajivunie uwapo wa jeshi hilo.
 
“Tumieni nguvu mahali mbapo Mtanzania wa kawaida akisikia ajivunie uwapo wenu kama ambavyo mmejitahidi katika suala la madawa ya kulevya. Kama tutaweza kuubaini mnyororo huo na kuukata, mwanchi wa kawaida atajivunia,” alisema.
 
Aidha alisema kuwa jeshi hilo bado lina kazi kubwa ya kufanya ili kukomesha mtandao wa watu wanaojihusisha na madawa ya kulevya nchini na pia akalitaka jeshi hilo kuhakikisha linakuwa mtetezi wa wanyonge.
 
Kamanda wa polisi mkoa wa Dodoma, Lazaro Mambosasa, awali akimkaribisha Waziri Mwigulu alisema kuwa jeshi hilo limejipanga vilivyo katika kuhakisha uhalifu unakomeshwa mkoani hapa.
 
“Mweshimiwa waziri mwenye utakuwa ni shahidi ukiwa katika vikao vya bunge uliona namna ambavyo amani na usalama ulikuwepo wa kutosha. Hii yote ni kutokana na kujipanga vizuri kwa jeshi la polisi mkoani hapa,” alisema Mambosasa.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumatatu Ya July 4

Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu (HESLB) yakanusha Taarifa kuwa Haina Fedha za kulipa wanafunzi

$
0
0

TAARIFA KWA UMMA
KUKANUSHA TAARIFA KWAMBA BODI HAINA FEDHA

Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu inapenda kukanusha taarifa za upotoshaji zinazoenezwa kwa sasa kwamba haina fedha.

Si kweli kwamba Bodi haina fedha, ila ni kweli kwamba kumekuwa na ucheleweshaji wa kufikisha fedha za wanafunzi vyuoni kutokana na zoezi la kuhakiki wanafunzi wanaonufaika na mikopo linaloendelea vyuoni hivi sasa.

Hata hivyo, maandalizi ya malipo hayo yameshafanyika na ‘pay sheets’ zimeshapelekwa vyuoni tayari kwa wanafunzi wanaonufaika na mikopo kusaini.

Bodi inatarajia wakati wowote wiki ijayo baada ya zoezi la uhakiki kukamilika; itapeleka fedha hizo vyuoni.

IMETOLEWA NA:
KITENGO CHA HABARI, ELIMU NA MAWASILIANO
BODI YA MIKOPO YA WANAFUNZI WA ELIMU YA JUU
TAREHE 2 JULAI 2016

Chadema: Maandalizi ya Kuuzuia Mkutano wa CCM Yameanza

$
0
0

KATIKA kutekeleza tamko la Baraza la Vijana wa Chadema (Bavicha) la kufika Dodoma kusaidiana na Jeshi la Polisi kuzuia Mkutano Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Bavicha Dodoma wameanza maandalizi ya kupokea vijana zaidi ya 2000.

Akizungumza na waandishi wa habari mjini Dodoma jana Malambaya Manyanya, Mwenyekiti wa Bavicha Mkoa wa Dodoma alisema, kwa sasa viongozi wa mkoa wameanza maadalizi ya kuwapokea wageni wao ambao wanatarajiwa kuanza kuwasili tarehe 21 na 22 Julai mwaka huu.

Alisema, maadalizi hayo ni ya kuwapokea vijana ambao watatoka katika mikoa yote ya Tanzania kwa lengo la kutimiza tamko la Bavicha taifa la kushirikiana na Jeshi la Polisi Mkoa wa Dodoma kuzuia mikutano na vikao vya CCM.

Alisema, kwa sasa mkoa tayari umeunda kikosi cha kufanya kazi ya maadalizi ya ugeni huo ambapo kwa nia njema utafika mjini Dodoma kutekeleza kauli ya Rais John Magufuli ya kuzuia vikao vyote na mikutano ya vyama vya siasa.

Alisema, maadalizi hayo ya kuwapokea vijana hao ni pamoja na viongozi wa kitaifa wa Bavicha kwa maana ya kutafuta mahali pa kulala na maandalizi ya chakula.

“Wapo watu ambao wanadhani Bavicha wana mpango wa kufanya fujo, sisi tunataka kurejesha Demokrasia nchini na kutekeleza kauli ya mkuu wa nchi.

“Tumekuwa tukiona jinsi mikutano ya Chadema inavyozuiliwa, na sasa msimamo wa Bavicha ni  kuzuia mkutano ya CCM unaotarajiwa kufanyika Julai 23 kwa lengo la kubadilishana uongozi kati ya mwenyekiti wa sasa wa CCM na rais msitaafu wa awamu ya nne Jakaya Kikwete na Rais John Magufuli.

“Tumeandaa vijana takribani 2000 kutoka mikoa yote nchini watakaokuja Dodoma kusaidiana na Jeshi la Polisi kutawanya mkutano usio halali wa CCM.

“Kwa sababau mkuu wa nchi ametoa tamko la kuzuia mikutano yote ya siasa ikiwa ni pamoja na vikao vya ndani na mikutano ya hadhara hadi 2020.” Alisema Malambaya.

Alisema, Jeshi la Polisi lilizuia mikutano ya vyama vya siasa vya upinzani na mahafali ya Jumuiya ya Wanafunzi wa Vyuo Vikuu Chadema (CHASO) na kuwa, sasa wanashirikiana na polisi kuhakikisha mikutano ya CCM haitafanyika.

Siku 72 za Vita ya UKAWA na Naibu Spika, Dk Tulia Ackson

$
0
0
Kukamilika kwa siku 72 za mkutano wa Bunge la Bajeti kumeacha rekodi mpya ya wabunge wa upinzani kususia vikao vya Bunge kwa muda mrefu zaidi kutokana na madai ya kutoridhishwa na utendaji wa Naibu Spika, Dk Tulia Ackson katika chombo hicho cha uwakilishi nchini.

Wapinzani chini ya mwavuli wao wa Ukawa, wamejikuta kwa mara ya kwanza, 12 kati yao wakisimamishwa kuhudhuria vikao vya Bunge kwa nyakati tofauti baada ya kutiwa hatiani na Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge inayoongozwa na Mbunge wa Newala (CCM), George Mkuchika kwa kukiuka maadili. Wachambuzi wa siasa wameeleza kuwa hali hiyo imefanya Bunge kuongozwa kwa mgogoro ulioathiri mijadala na mikakati ya ndani na nje ya bajeti hiyo.

Hata hivyo, uamuzi wa Ukawa kususia vikao vinavyoongozwa na Dk Tulia kuliwafanya wabunge wa CCM kupoteza wastani wa dakika tatu kati ya 10 ambazo hupatiwa kujadili hoja, kwani walikuta wakitumia dakika za mwanzo kwenye mizaha, kebehi na vioja dhidi ya wapinzani badala ya mijadala.

Baadhi ya wabunge ambao walioongoza kumwaga vijembe ni Livingstone Lusinde (Mtera), Goodluck Mlinga (Ulanga Mashariki), Juliana Shonza (Viti Maalumu) na Abdallah Ulega (Mkuranga).

Ulega katika moja ya michango yake alifikia uamuzi wa kumpatia mtoto wake mchanga jina la Tulia kama ishara ya “kumuenzi Dk Tulia kwa uendeshaji wa Bunge unaofuata kanuni.”

“Dk Tulia umekuwa mvumilivu licha ya wabunge wa upinzani kususia vikao vinavyoendeshwa na wewe. Mke wangu naye amekuwa mvumilivu kama wewe na nitampatia mtoto wangu jina la Tulia,”alisema Ulega kabla ya siku chache Dk Tulia kutembela Hospitali ya Taifa Muhimbili kumuona mtoto huyo.

Mlinga alijikuta akiingia kwenye orodha ya wabunge waliotoa vioja bungeni wakati akichangia bajeti ya Wizara ya Katiba na Sheria aliposema wanawake wa vyama vya upinzani ni lazima waitwe ‘baby’ ili wapate ubunge wa viti maalumu.

Kauli nyingine iliyoibua mjadala ni ile aliyoitoa kwenye mjadala wa bajeti ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa kutaka Sanamu ya Askari iliyopo Mtaa wa Samora Jijini Dar es Salaam ibadilishwe na kuwekwa ya mwanamuziki wa kizazi kipya, Diamond Platinumz kutokana na kuipaisha nchi kimataifa.

Wabunge 12 wasimamishwa 
Katika adhabu za awali, kambi ya upinzani ilishuhudia wabunge saba wakisimamishwa kushiriki vikao vya Bunge baada ya kutiwa hatiani na Kamati ya Maadili kuhusika na vurugu zilizotokea bungeni Januari 27, mwaka huu wakati wakipinga kusitisha matangazo ya moja kwa moja ya Bunge.

Wabunge wawili wa Chadema Esther Bulaya (Bunda Mjini) na Tundu Lissu wa Singida Mashariki, walisimamishwa kuhudhuria vikao vyote vya Bunge la Bajeti lililomalizika wiki iliyopita na mkutano utakaoanza Septemba.

Wengine wa Chadema Pauline Gekul (Babati Mjini), Godbless Lema (Arusha Mjini), Halima Mdee (Kawe) na Kabwe Zitto, Mbunge wa Kigoma Mjini kupitia ACT–Wazalendo walisimamishwa kuhudhuria vikao vyote vya bajeti.

Mbunge wa Tarime Vijijini, John Heche (Chadema) alipigwa marufuku kuhudhuria vikao 10 mfululizo. Juni 17 mwaka huu wabunge wawili wa viti maalumu pia kutoka Chadema, Suzan Lyimo na Anatropia Theonest walisimamishwa kwa kudaiwa kusema uongo bungeni.

Suzan alisimamishwa vikao vitano wakati Anatropia alisimamishwa vikao vitatu na kukatwa nusu mshahara na posho.

Kama hiyo haitoshi, wabunge wengine watatu, Joseph Mbilinyi (Mbeya Mjini), James Ole Millya (Simanjiro) na Saed Kubenea wa Ubungo walisimamishwa vikao vya Bunge kuanzia siku hiyo na kumalizia adhabu vikao vya Septemba.

Mbilinyi alisimamishwa vikao 10 kwa kudharau mamlaka ya spika kwa kuonyesha kidole cha kati juu cha mkono wa kulia, ishara ambayo inatafsiriwa ni matusi.

Kubenea na Ole Millya walisimamishwa vikao vitano kwa kudaiwa kusema uongo baada ya kushindwa kuthibitisha madai yao. 

Upinzani wasusa 
Ukilinganisha na mabunge yaliyopita, ukiacha Bunge la Katiba, wabunge wa upinzani walikuwa wakipinga jambo bungeni bila kutoka katika mkutano, lakini safari hii walikuja na staili mpya ya kususia vikao vyote vinavyoendeshwa na Dk Tulia na kusababisha kutochangia bajeti kuu.

Wabunge hao walisusa pia kushirikiana na wabunge wa CCM katika kutumia kantini ya Bunge, michezo na mitandao ya kijamii, mbaya zaidi wamekuwa hawawasalimu.

“Wao wameamua kuanza kututenga wenyewe, Dk Tulia anaona kiongozi wa upinzani anatukanwa, anacheza tu, lakini mbunge wa upinzani anapelekwa kwenye Kamati ya Maadili. Ngoja na sisi tujitenge,” alisema Mwenyekiti Mwenza wa Ukawa, James Mbatia.

Ingawa kuna wenyeviti wanne ambao kwa kawaida Spika hupokezana nao, katika mikutano yote iliyotangulia kiongozi huyo aliacha kiti mara moja tu kwa Andrew Chenge, lakini siku nyingine alikaa mwenyewe na kufanya wabunge wa Ukawa kuondoka ukumbini kila anapoongoza. 

Mbunge CCM akerwa
Hata hivyo, Mbunge wa Kasulu Mjini, Daniel Nsanzugwako (CCM), ingawa alipingwa na wabunge wengi wa CCM, alisema bado anaamini katika kukaa kwa pamoja kati ya wabunge wa upinzani na Dk Tulia ili kumaliza tofauti zao.

Dk Tulia aliwataka wabunge hao kufuata utaratibu wa kikanuni wa kufikisha malalamiko yao kuhusu kiti cha Spika, licha ya kwamba hata yale yaliyofikishwa dhidi yake hayakutolewa maamuzi yoyote. 

Hoja zilizosisimua 
Unapozungumza hoja zilizosisimua katika mkutano huo wa tatu, huwezi kuacha suala la kiinua mgongo cha wabunge kukatwa kodi kwani wabunge karibu wote waliopata nafasi ya kuchangia bajeti kuu waliibuka na hoja hiyo kuipinga, lakini waliambulia patupu.

Hoja hiyo ilihitimishwa baada ya Rais Dk John Magufuli kukubali kukatwa kodi katika kiinua mgongo chake pamoja na Makamu wa Rais, Waziri Mkuu, mawaziri, wakuu wa mikoa na wilaya.

Wabunge wa CCM walimshukia Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango wakidai kuwa kitendo cha kukata kodi za kiinua mgongo cha wabunge ni mtego wa kuwachonganisha na wananchi.

“Kwanini muwaache Rais, mawaziri, wakuu wa mikoa, wakuu wa wilaya na majaji?” alihoji mbunge wa Nzega Mjini, Hussein Bashe wakati akichangia mjadala huo kabla ya viongozi hao kujumuishwa.

Mbunge wa viti maalumu (CCM), Jacqueline Msongozi alisema Dk Mpango amegusa pabaya kwa kukata kiinua mgongo kwa kuwa tayari kila mwezi hukatwa Sh1.3 milioni ya kodi na kwa miaka mitano watakayokaa bungeni watakuwa wamekatwa Sh50 milioni.

Hoja nyingine iliyojadiliwa kwa kila wizara ni bajeti iliyopitishwa na Bunge kutopelekwa yote ambapo Mbunge wa Tarime Mjini, Easter Matiko (Chadema), alisema katika miaka yote aliyokuwa bungeni hajawahi kuona Serikali ikileta bajeti bungeni inayotekelezeka.

Hata hivyo, Mbunge wa Lulindi Jerome Bwanausi (CCM) alisema usimamizi wa karibu wa Bunge katika kuhakikisha wanachopanga Serikali inatekeleza unaanza mwaka huu kwa kamati ya Bajeti kukutana kila baada ya miezi mitatu ili kujadili utekelezaji wa bajeti na kutoa ushauri.

Kubana matumizi 
Miongoni mwa mambo yalitajwa sana ni kubana matumizi kukidhi sera ya Rais Magufuli, ambapo Mbunge wa Sengerema-CCM, William Ngeleja alisema ni moja ya mambo mema yaliyo kwenye mkutano huo.

“Uchungu wa bajeti hii ni mafisadi na wala rushwa. Walizoea kufanya kazi kwa mazoea wataumia sana. Fedha za matumizi ya kawaida zimepunguzwa kwa kiasi kikubwa, uadilifu ndio utatawala matendo ya watumishi,” alisema Ngeleja.

Katika wizara mbalimbali matumizi ya kawaida ikiwemo bajeti zilizokuwa zikitolewa kwa ajili ya viburudisho imepunguzwa kwa kiasi kikubwa huku ofisi na wizara zikiagizwa kutumia kumbi za Serikali wakati wanapofanya mikutano, makongamano na warsha.

Kesi za Mafisadi Kutozidi miezi 9

$
0
0
JAJI Mkuu, Mohammed Chande Othman, amesema Mahakama Maalumu ya Uhujumu Uchumi na Ufisadi itaamua kesi kwa muda usiozidi miezi tisa na kwamba itaanza na majaji 14.

Aidha, wameandaa kozi maalumu kwa majaji 14 watakaofanya kazi katika mahakama hiyo itakayoanza Julai 11 hadi 15, mwaka huu, kwenye Chuo cha Mahakama Lushoto mkoani Tanga, ili kupeana mwongozo juu ya uendeshaji wa mahakama hiyo.

Jaji Mkuu alisema, kesi zitakazoendeshwa katika mahakama hiyo ni zile ambazo upelelezi wake umekamilika ili uamuzi utolewe mapema. Kwa mujibu wa Jaji Mkuu, dhamira ya Serikali ya Awamu ya Tano ni kupambana na uhalifu huo.

Aliyasema hayo jana wakati alipotembelea Maonesho ya 40 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam yanayoendelea kwenye Viwanja vya Mwalimu Nyerere vilivyopo katika Barabara ya Kilwa, ambayo alisema yamezidi kuwa bora kuliko miaka mingine. 

Alisema baada ya sheria hiyo ya uhujumu uchumi kupitishwa na Bunge, imekuwa na marekebisho mengi na kuboreshwa kwa kiasi kikubwa.

Jaji Mkuu alisema pia, hatua inayofuata ni Rais kutoa idhini ya sheria hiyo na baadaye kupitishwa kwa kutangazwa katika Gazeti la Serikali ili ianze kutumika.

Alieleza kuwa baada ya kutangazwa katika Gazeti hilo la Serikali, Jaji anatakiwa kutunga kanuni mbalimbali, mojawapo ikiwa ya kulinda mashahidi kutokana na kuwa sheria hiyo inahusu makosa makubwa na hatari ya ugaidi, rushwa na uhujumu uchumi.

“Tuko mbioni kutunga kanuni hizo na kuhakikisha mashahidi wanalindwa. Jengo la mahakama hii litakuwa katika Chuo cha Sheria karibu na Mlimani City na tayari tumepeleka wasajili watendaji,” alisema.

Mwishoni mwa wiki, Jaji Mkuu huyo alisema kuwa majengo ya mahakama hiyo yatakabidhiwa leo. Kutokana na maelezo yake, Mahakama iko tayari kuendesha divisheni hiyo, baada ya kukabidhiwa majengo hayo.

Alisema wataanza kutoa semina kwa majaji na watumishi wengine wa mahakama hiyo juu ya namna divisheni hiyo itakavyoendesha shughuli zake. 

Aidha, aliweka wazi kuwa hadi sasa hakuna kesi hata moja iliyokwishatambuliwa kwamba itashughulikiwa na mahakama hiyo.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images