Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Balozi Seif akabidhiwa nakala ya Taarifa ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Tanzania

$
0
0
Na Othman Khamis Ame, OMPR
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar  Balozi Seif Ali Iddi amewahakikishia wananchi wote kwamba Zanzibar chini ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar itabakia kuwa ya amani na utulivu ili kuwapa nafasi wananchi wake waendelee na harakati zao za kimaisha kama kawaida.
 
Alisema Serikali kupitia vyombo vyake vya ulinzi na usalama kamwe haitakubali kuona amani iliyopo anatokea mtu au kikundi kinachojaribu kuichezea amani hiyo na kuhatarisha maisha ya watu.
 
Balozi Seif Ali Iddi alisema hayo wakati akizungumza na Makamishna na watendaji wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Tanzania (NEC) mara baada ya kupokea nakala ya Taarifa ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi Tanzania kutoka kwa Mwenyekiti wa Tume hiyo  Jaji Staafu Mh. Daniel Lubuva.
 
Balozi Seif alisema uchaguzi wa Zanzibar kwa sasa umeshakamilika  kwa mujibu wa Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984 sura ya Tisa kifungu cha 118 iliyoipa mamlaka Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar kuendesha uchaguzi bila ya kuchukuwa amri au maelekezo kutoka kwa mtu ye yote.
 
Alisema kazi iliyopo mbele kwa Wazanzibari na Watanzania kwa ujumla ni  kufanya kazi kwa juhudi na maarifa huku wakijianda kwa uchaguzi mwengine ifikapo mwaka 2020.
 
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar aliupongeza Uongozi na Watendaji wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Tanzania { NEC } kwa kazi kubwa na nzito ya kusimamia uchaguzi wa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, Wabunge na Madiwani na kumalizika zoezi kwa salama na amani.
 
Mapema Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Tanzania Jaji Msaafu Mh. Daniel Lubuva alisema pamoja na jukumu la Tume hiyo kuendelea kusambaza Taarifa za Tume hiyo ya mwaka 2015 kwa Viongozi Wakuu lakini watendaji wake bado wana kazi ya kujiandaa na uchaguzi mwengine ujao wa Mwaka 2020.
 
Jaji Mstaafu Lubuva alisema sheria ya Kura ya Maoni nambari 11 ya Mwaka 2013 itaangaliwa upya kwa pamoja kati ya Watendaji wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Tanzania { NEC} na ile ya Uchaguzi ya Zanzibar { ZEC } ili kuona mapungufu yanayohitaji kufanyiwa marekebisho.
 
Alisema Kura ya Maoni itapigwa kama Katiba ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania ilivyofafanua baada ya pande hizo mbili kupitia  mapungufu hayo na baadaye kupendekeza mswaada wa marekebisho yatakayopelekwa Bungeni kwa hatua zaidi za kisheria.
 
Jaji Lubuva alifahamisha kwamba Kauli ya Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. John Pombe Magufuli ya kuendeleza Kura ya Maoni itaondoa shaka kwa Watanzania waliokuwa wakifikiria kwamba zoezi hilo limefifia.
 
Mwenyekiti huyo wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Tanzania ameelezea faraja yake kutokana na uhusiano wa karibu wa kikazi uliopo kwa muda mrefu kati ya Tume anayoiongoza na ile Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC),

Makonda Amtumbua Jipu Mhandisi wa Mkoa

$
0
0
MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda amemsimamisha kazi Mhandisi wa Mkoa, Josephat Shehemba kwa kushindwa kutimiza wajibu wake, ikiwemo usimamizi wa barabara na kusababisha kujengwa chini ya kiwango.

Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam, Makonda alisema amefikia uamuzi wa kumsimamisha kazi baada ya kuona injinia huyo ameshindwa kutekeleza majukumu yake ya usimamizi.

Alisema jukumu la usimamizi wa barabara, unapaswa kuwa chini ya Shehemba, lakini ameshindwa kufanya hivyo jambo lililosababisha usimamizi huo kufanya na wananchi na wakuu wa wilaya ambao sio kazi yao kufanya hivyo.

“Ni lazima alitakiwa kufanya kazi yake ya usimamizi na kuhakikisha barabara zinajengwa kwa kiwango kinachotakiwa lakini matokeo yake kazi yake ameiacha na kufanya na watu wengine ambao hawakupaswa kufanya hivyo,” alisema Makonda.

Aidha, Makonda alisema kukosekana kwa usimamizi mazuri wa kiongozi huyo kumesababisha barabara nyingi za mkoa huo kuwa chini ya kiwango na nyingine kuharibika muda mfupi baada tu ya kutengenezwa.

“Ameshindwa kusimamia lakini anakuwa mtu wa kwanza kudai fedha za kuwalipa wakandarasi ambao wamejenga barabara chini ya viwango angepaswa kusimamia atakapokwama au kumuona mkandarasi ameshindwa kufanya kazi yake kwa viwango basi angenieleza ili tuone tunafanya utaratibu gani,” alisisitiza.

Makonda pia alisema ni jukumu la kila kiongozi kutimiza wajibu wake, ikiwa ni pamoja na kuwa msimamizi mkuu katika idara yake.

“Hatutomvumilia kiongozi yeyote atakayekwenda kinyume na taratibu za kazi inavyomtaka kama ameshindwa bora ahame mkoa kwa sababu hapa kwangu sitamvumilia,” alisema.

Maandalizi ya Mahakama ya Mafisadi Yaanza....Jukwaa la Haki Jinai Lakutana Kufanya Tathmini

$
0
0
Wakati Bunge likiwa limepitisha sheria ya uanzishwaji wa Mahakama ya Mafisadi nchini, Jukwaa la Haki Jinai ambalo linajumuisha Taasisi za umma na serikali limekutana kujipanga namna zitakavyoweza kufanya kazi kwa ufanisi kwenye Mahakama hiyo.

Kauli hiyo ilitolewa jana na Waziri wa Katiba na Sheria, Dk. Harrison Mwakyembe alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari mjini Dodoma, mara baada ya kufungua kikao hicho cha kazi cha siku mbili cha jukwaa hilo.

Dk. Mwakyembe alisema jukwaa hilo limehudhuriwa na viongozi wote wa Taasisi ambazo zipo kwenye mfumo wa haki jinai ikiwemo Jeshi la Polisi, Usalama wa Taifa, Mahakama, Taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa(Takukuru).

Alisema kikao hicho kinafanyika kipindi muafaka kwa sababu jana Bunge lilipitisha muswada wa marekebisho ya sheria mbalimbali ambao unatoa mwanya wa kuanzisha mahakama ya mafisadi na makosa ya rushwa.

Alibainisha vyombo hivyo vinaangalia jinsi gani kimoja kimoja kwa ushirikiano vitakavyoweza kufanikisha uanzishaji wa Mahakama hiyo.

Kikao hicho kilihudhuriwa na idara ya polisi ambayo inatakiwa ipeleleze haraka, Takukuru ifanye uchunguzi kwa haraka, Timu ya DPP na waendesha mashtaka wake wote ifanye kazi kwa ufanisi sana kesi zisikae, Mahakama nayo kama kuna vitu vinakwamisha vitatuliwe.

Alisema chombo hicho kinatafakari namna vyombo hivyo vitakavyoshirikiana ili mahakama hiyo iweze kufanya kazi kwa ufanisi kama Rais alivyoahidi.
 
Hata hivyo alisema pamoja na hilo wanajadili changamoto mbalimbali zinazojitokeza katika usimamiaji wa haki jinai nchini.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Mashtaka nchini,Buswalo Mganga alisema changamoto zinazoikabili haki jinai nchini ni uhalifu ambao unafanywa na watanzania wenyewe na miongoni mwao wengine wanatoka nje na washirikiana na watanzania na vyombo vya habari.

Hukumu kesi ya Mauaji ya Mwangosi Inayomkabili Askari wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) Itatolewa Julai 21

$
0
0
Hukumu ya kesi ya mauaji ya mwandishi wa habari wa kituo cha televisheni cha Channel 10, Daudi Mwangosi itatolewa Julai 21 baada ya Mahakama Kuu kusikiliza majumuisho na maoni ya Baraza la Wazee. Kesi hiyo inamkabili askari wa kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) mkoani Iringa, Prisifius Simon.

Akitoa majumuisho ya kesi hiyo jana, Jaji Paul Kihwelo alisema ni wajibu wake kutoa majumuisho kwa kuangalia mazingira na ushahidi uliomgusa moja kwa moja mtuhumiwa.

Jaji Kihwelo alieleza mahakama kuwa askari huyo anatuhumiwa kufanya mauaji hayo kwa kukusudia Septemba 2, 2012.

Alieleza kuwa jukumu la kuthibitisha kosa kwa mtuhumiwa ni upande wa mashtaka na wanatakiwa wathibitishe bila kuacha wasiwasi wowote na si jukumu la upande wa pili kuthibitisha kuwa mtuhumiwa hakutenda kosa.

Alitaja vielelezo ambavyo vilitolewa mahakamani bila kupingwa kuwa ni pamoja na ramani ya tukio, taarifa ya uchunguzi ya kifo cha marehemu, ungamo la mtuhumiwa na kitabu cha kuchukilia silaha ofisi za FFU.

Akisoma majumuhisho kwenye upande wa ungamo, Jaji Kihwelo alisema maungamo yanayofanywa mbele ya mlinzi wa amani, yanaweza kutumika kutoa ushahidi.

Mtuhumiwa huyo alieleza mahakama wakati akitoa ushahidi wake kuwa kabla ya kufika kwa mlinzi wa amani, aliitwa kuhojiwa na RPC na RCO ndipo akaenda kufanya ungamo na kwamba hakufanya chochote zaidi ya kuambiwa asaini.

Akitoa maoni yake mmoja wa wazee wa mahakama, Khadija Husein alisema baada ya kusikiliza mashahidi wa pande zote kuanzia mwanzo hadi mwisho, wamegundua kuwa mtuhumiwa alienda kufanya ungamo kwa mlinzi wa amani akiwa huru na kusaini.

Khadija alisema si rahisi mtu kusaini kitu ambacho  hajakitolea maelezo, hivyo alichokisaini ndicho alichokitenda na alitoa ungamo akiwa huru bila kupigwa wala kutishiwa

Alisema endapo maelezo hayo yalikuwa si yake, yangepingwa mbele ya mahakama na wakili wake au yeye mwenyewe, lakini kwa kuwa yalipokelewa bila kupingwa hivyo ana hatia ya kutenda kosa bila kukusudia.

Mzee mwingine, Said Mbaga alipingana na maelezo hayo, akisema mtuhumiwa hana hatia kwa sababu shahidi wa kwanza hakuthibitisha kuwa alitenda kosa kwa sababu hakumuamuru kupiga bomu.

Mzee wa tatu, Sophia Ng’anguli alisema mtuhumiwa alitenda kosa bila kukusudia licha ya ushahidi wa upande wa mashtaka kuacha mashaka.

Alidai kitu cha msingi kinachomfunga mshitakiwa ni ungamo alilolitoa kwa mlinzi wa amani, ambalo aliandika na kusaini huku akikiri na kujutia kusababisha kifo cha Mwangosi.

Atakayempachika Mimba Mwanafunzi Kifungo cha Miaka 30 Jela

$
0
0
BUNGE limepitisha kwa kauli moja Sheria ya Marekebisho ya Sheria Mbalimbali Namba 2 ya mwaka 2016 ambayo pamoja na mambo mengine, imeongeza adhabu kwa watu wanaowapa mimba au kuoa ama kuolewa na mwanafunzi, sasa watafungwa jela miaka 30.

Sheria hiyo ilipitishwa jana bungeni mjini Dodoma baada ya Muswada kuwasilishwa Juni 24, mwaka huu na Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG) ambao baadhi ya wabunge walipata fursa ya kuuchangia.

Muswada huo ulilenga kufanya marekebisho katika sheria 21 kwa lengo la kuondoa mapungufu yaliyobainika wakati wa utekelezaji wa sheria hizo na umepitishwa kuwa sheria.

Sheria zilizopendekezwa kurekebishwa na sheria hiyo ni pamoja na ya Kudhibiti Utakatishaji wa Fedha Haramu; Kudhibiti Usafirishaji Haramu wa Binadamu; Kanuni za Madai; Usajili wa Makandarasi; Elimu; Ajira na Mahusiano Kazini na Sheria ya Taasisi za Kazi.

Muswada huo uliowasilishwa bungeni na Mwanasheria Mkuu wa Serikali, George Masaju unatamka adhabu ya kifungo cha miaka 30 jela katika marekebisho ya Sheria ya Elimu kwa watakaompa mimba, kumuoa au kuolewa mwanafunzi.

Awali adhabu iliyotamkwa katika sheria hiyo ya elimu ni mshitakiwa akibainika kuwa na kosa kutozwa faini ya Sh 500,000 na iwapo ni kosa la pili anatozwa faini ya Sh 500,000 au kifungo kisichozidi miaka mitatu.

Akiizungumzia sheria hiyo inayosubiriwa kusainiwa na Rais John Magufuli, Masaju alisema inawalinda watoto wote chini ya miaka 18 walioko na wasio shuleni na kuwa kosa hilo likifanywa na mtoto atahukumiwa kwa mujibu wa sheria ya mtoto.

Kifungu cha 60 A (i) kimeeleza kuwa itakuwa kinyume cha sheria katika mazingira yoyote yale kwa mtu yeyote kumuoa au kuolewa na mwanafunzi wa shule ya sekondari au ya msingi na atakayekiuka atafungwa jela miaka 30.

Katika Sheria ya Taasisi za Kazi inataka mwajiri anapokiuka masharti ya sheria ya kazi, ikiwa ni pamoja na kuchelewesha michango ya waajiriwa, kutoza faini na Ofisa wa Kazi ya papo kwa hapo isiyopungua Sh 100,000.

Wakichangia muswada huo, wabunge wameonesha furaha yao juu ya Sheria ya Elimu inayohusu adhabu ya miaka 30 jela. Hata hivyo, pamoja na furaha hiyo, baadhi ya wabunge wametoa angalizo la kutaka kupimwa kwanza DNA kabla ya kutoa hukumu huku wengine wakitaka kuwapo kwa nyongeza ya viboko.

Mbunge wa Geita Mjini, Constantine Kanyasu (CCM) alipongeza marekebisho hayo na kutaka adhabu ya miaka 30 iongezwe na kuchapwa viboko 12 kila mwezi mpaka aliyehukumiwa anamaliza kifungo kutokana na wahalifu hao kuwa na mazoea ya kuzoea gereza.

Naye Mbunge wa Viti Maalumu, Subira Mgalu (CCM) alisema pamoja na serikali kuja na marekebisho hayo pia waangalie namna ya kukabiliana na utoro shuleni ili kuwafanya wanafunzi kupata elimu.

Kwa upande wake, Mbunge wa Njombe Kusini, Edward Mwalongo (CCM) alitaka sheria imtake anayekutwa na kosa hilo kuacha fedha za fidia ambazo mama atazitumia wakati mwanaume akiwa jela.

Akijibu hoja ya kutumika kwa vipimo vya vinasaba (DNA), Masaju alisema kwa sasa utaratibu wa vipimo hivyo utatumika mahakamani na waendesha mashitaka kuhakikisha hawaachi shaka kwenye ushahidi kutokana na Tanzania kutokuwa na uwezo wa kumpima DNA mtoto akiwa tumboni.

Kuhusu Sheria ya Taasisi za Kazi, Mbunge wa Viti Maalumu, Hawa Chakoma (CCM), alitaka adhabu hiyo kuongezwa ili sheria kuleta tija na kutaka kazi ya kutoza faini hiyo isifanywe na Ofisa wa Kazi kama ilivyotamkwa katika sheria badala yake ifanywe na Mamlaka ya Usimamizi wa Mifuko ya Jamii (SSRA) kutokana na mifumo mizuri ya ufuatiliaji.

Akijibu hoja hiyo, Waziri wa Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu, Jenista Mhagama alisema serikali imekuja na sheria hiyo ili kuwabana waajiri wanaochelewesha michango ya waajiriwa na kuwa katika kutekeleza sheria waziri ataweka makundi na kuwa kampuni zenye kipato kikubwa adhabu yao itakuwa kubwa zaidi.

FFU Jela Miaka 30 kwa Kubaka Mwanafunzi........ Pia Atalipa Faini ya Milioni 15 na Viboko 12

$
0
0

ASKARI wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU), Raphael Makongojo (25) aliyembaka aliyekuwa mwanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Korogwe amehukumiwa kifungo cha miaka 30 jela.

Pia Makongojo amepewa adhabu kali, ikiwemo viboko 12 pamoja na kuamriwa kutoa faini ya Sh milioni 15 mara atakapomaliza kifungo chake.

Hukumu hiyo iliyotolewa na Mahakama ya Wilaya ya Arusha ndani ya chumba cha faragha (chemba) ambako waandishi hawakuruhusiwa kusikiliza hukumu, lakini baadaye waliambiwa kwa sharti la hakimu wala waendesha mashtaka kutajwa majina yao kwa sababu kesi hiyo iliendeshwa faragha.

Awali kesi hiyo ilianza kwa mshitakiwa kusomewa maelezo yake ya awali akituhumiwa kumbaka mwanafunzi wa Kidato cha Sita wa Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Korogwe ambaye hivi sasa amemaliza masomo.

Awali askari huyo alishushwa pamoja na mahabusu wenzake mahakamani hapo, lakini kwa kuwa kesi inayomkabili ni ya ubakaji hivyo inasikilizwa ndani ya chumba cha faragha (chemba) ambako hakuna ruhusa kwa wanahabari kuandika habari hiyo hadi hapo hukumu itakapotolewa.

Kwa mujibu wa Kifungu cha Sheria Namba 186 (3) cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai Sura ya 20 ya Mwenendo wa Makosa ya Kujamiiana ya Mwaka (1998) inayosema kuwa bila kujali masharti ya sheria nyingine yoyote inayohusisha makosa ya kujamiiana, ushahidi au mashahidi watakaohusika hawaruhusiwi kutolewa kwenye chombo chochote cha habari.

Awali, mshitakiwa huyo kwa mara ya kwanza alifikishwa mahakamani hapo na kusomewa shtaka lake kwa hakimu (jina linahifadhiwa) ambako Wakili wa Serikali (jina linahifadhiwa) alidai mahakamani hapo kuwa mtuhumiwa huyo alitenda kosa hilo Januari 16, mwaka huu katika eneo la Kwa Mrombo, FFU jijini Arusha.

Alidai kuwa mtuhumiwa huyo alitenda kosa hilo kinyume cha Kifungu cha 130(1 na 2 a) cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai, Sura ya 16.

Baada ya hukumu hiyo kutolewa, mama mzazi wa mtoto huyo ambaye hakupenda kutaja jina lake, aliiomba serikali kuingilia kwa makini sheria inayohusu makosa ya ubakaji ili adhabu itakayotolewa kwa mbakaji iwe kifungo cha maisha badala ya hakimu au mahakama kutoa kifungo cha miaka 30.

Aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga Aandaa Ibada ya Shukrani

$
0
0
Baada ya kimya cha muda mrefu, hatimaye aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga ameibuka na kukabidhi ofisi na akatoa ratiba ya shughuli zake katika Jimbo lake la Misungwi ikiwamo ibada ya shukrani. 

Kitwanga ambaye uteuzi wake ulitenguliwa May 20 na Rais John Magufuli baada ya kuingia bungeni na kujibu swali akiwa amelewa, alikabidhi ofisi jana kwa Mwigulu Nchemba ambaye amechukua nafasi yake.

Baada ya uteuzi wake kutenguliwa, Kitwanga alitoweka bungeni na baadaye ilielezwa kuwa alikwenda Israel kabla ya hivi karibuni kurejea nchini na kusema kuwa yote yaliyotokea anamwachia Mungu. 

Hivi karibuni, Rais Magufuli alimhamishia Mwigulu katika Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kutoka Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi huku Dk Charles Tizeba akimrithi Mwigulu. 

Akizungumza katika mahojiano baada ya kukabidhi ofisi, Kitwanga alisema kila Mtanzania anaweza kufanya kazi iwapo atapewa nafasi huku akinukuu kaulimbiu ya ‘Hapa Kazi Tu’ na kwamba amefanya makabidhiano hayo kwa wema na upendo wa hali ya juu. 

Alisema amekabidhi ofisi bila kinyongo kwa sababu Tanzania si nchi yake peke yake bali ni ya wananchi wote. 

Ratiba jimboni 
Akizungumzia ratiba jimboni mwake, Kitwanga alisema Agosti 6, atafanya ibada ya shukrani nyumbani kwake Misungwi kumshukuru Mungu akisema hiyo ni baada ya ziara yake ya wiki sita mfululizo kwa wapigakura wake. 

Ziara hiyo itaanza keshokutwa atakapokutana na kamati ya mipango na fedha kabla ya kufanya kikao na madiwani wote wa jimbo hilo Jumamosi ijayo. 

Alisema Jumatatu ijayo atakabidhi vifaa mbalimbali vikiwamo magodoro na vitanda kwa hospitali ya wilaya na zahanati, vyerahani na kompresa kwa vikundi za ujasiriamali katika hafla itakayofanyika kwenye Stendi ya Mabasi Misungwi: “Hapo nitatoa nafasi ya dakika 10 mpaka 20 kwa waandishi wa habari kuniuliza maswali... lakini nisingependa umbeya... kwangu mimi ni Tanzania kwanza, nawaambia kabisa.” 

Baada ya shughuli hiyo, alisema siku inayofuata atakutana na wenyeviti wa vijiji vyote vya jimbo hilo kupanga namna atakavyofanikisha ziara yake katika maeneo yao, kazi ambayo alisema ataifanya kwa wiki sita mfululizo; “nitafanya ziara siku tano kwa kila wiki mfululizo, zamani nilikuwa nikigawa muda wa kutembelea jimbo na kurudi Dar kufanya kazi sasa nitakuwa huko muda wote. Dar nitakuwa nakuja mara chache tu.” 

Tundu Lissu Ajisalimisha Mahakama Ya Kusutu Leo

$
0
0
Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu (CHADEMA), amepandishwa kizimbani baada ya kujisalimisha katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam, kujibu tuhuma za kuchapisha chapisho la uchochezi lenye kichwa cha habari' Machafuko yaja Zanzibar'.

Lissu alifika mahakamani hapo jana saa tano asubuhi, kwa ajili ya kuitikia wito wa kumtaka kwenda kujibu tuhuma za uchochezi zinazomkabili baada ya washitakiwa wenzake wawili akiwemo Mhariri wa Mawio ambalo lilifungiwa kwa muda usiojulikana, Simon Mkina kusomewa mashitaka.

Mbunge huyo na washitakiwa wenzake Mkina na mchapishaji wa Kampuni ya Jamana, Ismail Mehboob, walipanda kizimbani mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba.

Upande wa jamhuri ukiongozwa na Wakili wa Serikali, Paul Kadushi kwa kushirikiana na Salim Msemo, ulidai mahakamani hapo kuna washitakiwa Lissu, Mkina na Mehboob na mshitakiwa Jabir Idrisa bado hawajampata na wamepata taarifa anaumwa.

Kadushi aliomba kumsomea mashitaka Lissu, ambapo alimsomea mashitaka matatu ya kula njama kuchapisha chapisho la uchochezi, kuchapisha taarifa yya uchochezi na kosa la tano ambalo ni mbadala wa kosa la pili la kutishia.

Wakili huyo alidai Lissu na wenzake kati ya Januari 12 hadi 14, mwaka huu, Dar es Salaam, walikula njama ya kuchapisha chapisho la uchochezi katika gazeti la Mawio lenye kichwa cha habari kisemacho, ‘Machafuko yaja Zanzibar’.

Pia Lissu na wenzake walidaiwa Januari 14, mwaka huu, Dar es Salaam, kwa nia ya kuleta chuki na uchochezi kati ya wananchi na mamlaka halali ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, walichapisha chapisho hilo lenye uchochezi.

Aidha, Lissu alidaiwa siku hiyo kinyume cha sheria na bila ya mamlaka waliwatishia na kuwatia hofu wananchi wa Zanzibar wasiweze kuingia kwenye marudio ya Uchaguzi Mkuu.

Lissu alikana mashitaka hayo, ambapo Hakimu Simba alisema Juni 14, mwaka huu, shauri lilipokuja kwa mara ya kwanza upande wa utetezi ulileta pingamizi juu ya uhalali wa mashitaka wakiomba yafutwe.Kesi hiyo itatajwa Julai 14, mwaka huu

RIWAYA: Mwanafunzi Mchawi ( A Wizard Student ) - Sehemu ya Sita

$
0
0
Mtunzi:  Enea Faidy
 
Ilipoishia sehemu ya  Tano( kama hukuisoma bofya hapa).
Eddy alimwacha Dorice Solemba, akilia na moyo nje ya darasa. Na alipoingia darasani Eddy alifuatwa na Doreen kwenye kiti chake, na alitaka kumwambia kitu muhimu....

Endelea...
Doreen alizidi kujilegeza sana kwa Eddy ili amteke kimawazo na kiakili sawasawa. Alirembua macho kama aliyekula kungu huku akimtazama Eddy.. 

Hakika kwa urembo aliokuwa nao Doreen na vituko alivofanya alizidi kuziteka hisia za Eddy haswa. Mtoto wa kiume alijikuta anaishiwa pozi, uvumilivu ukamshinda akajikuta anakohoa kidogo ili asafishe koo na kuweza kusema la moyoni.
 
"Eddy!" Doreen aliita kwa sauti ya mvuto sana.
"Naam"
"niambie basi.."
"ah!.. Doreen kama nilivosema awali wewe in mzuri sana hivyo basi .... nataka uwe mpenzi wangu.. please! naomba unielewe!" Eddy aliongea kwa sauti ya chini ili majirani wasiweze kusikia.
"Eddy! we ni shemeji yangu siwezi kumsaliti rafiki yangu Dorice!" Doreen alijifanya kukataa ingawa moyoni mwake alifurahia ushindi wa kumpata Eddy ilhali warembo wore shuleni pale waliikosa nafasi ile isipokuwa Dorice.
"Doreen! plz naomba nikubalie nakupenda sana "
"Na Dorice je?"
"habari za Dorice achana nazo me nimeachana nae, nakupenda wewe"
"mi sitaki Eddy!" sauti aliyoitoa Doreen ilionesha kabisa alikuwa anataka Ila alivunga tu.
"Nikubalie Dori.. nakupenda Doreen.. usinitese!" Eddy alisema huku machozi yakimlengalenga kwani hakutaka kumkosa Doreen. Ama kweli dawa za Doreen alizotafuna kabla ya kumfuata Eddy zilifanya kazi vizuri sana.
"Okey! nakubali kuwa na wewe!"
"Oh my God kweli Doreen unanipenda? asante sana!" Eddy aliachia tabasamu mwanana na alitamani hata kumkumbatia Ila aliogopa kufanya vile kwani walikuwa darasani.
"Nakupenda Eddy Ila kuna sharti moja muhimu inabidi ufate ili uwe na Mimi..."
"sharti gani tena?" Eddy alishtuka
"upo tayari?"
"ehm.. ah ndio coz I love u.. ntafanya"
"good.. nafurahi sana"
"Niambie basi mpenzi.." alisema Eddy akitabasamu.
"usijali nitakuambia baadae..."
Alisema Doreen huku akiinuka kitini na kuondoka zake. Eddy alikuwa na furaha sana hakuweza hata kusoma zaidi ya kumfikiria Doreen na kila Mara aliachia tabasamu.

==>Endelea Nayo  <<Kwa Kubofya Hapa>>

Serikali Yakanusha Kupima UKIMWI Nyumba Kwa Nyumba

$
0
0

Kumekuwepo na taarifa mbalimbali zinazozagaa kwenye mitandao ya kijamii zinazotokana na habari iliyoandikwa na kuchapishwa kwenye gazeti la Jambo leo la tarehe 24 Juni, 2016, toleo namba 2482 yenye kichwa cha habari "Sasa ukimwi kupimwa nyumba kwa nyumba".

Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) inapenda kutoa ufafanuzi kwamba UKIMWI HAUTAPIMWA NYUMBA KWA NYUMBA bali itafanya utafiti wa Viashiria na Matokeo ya UKIMWI Tanzania kuanzia mwezi Septemba 2016 ambapo UKIMWI utapimwa kwenye kaya chache ambazo zimechaguliwa kitaalam nchi nzima ili ziweze kuwakilisha kaya nyingine nyingi ambazo hazitahusika moja kwa moja katika utafiti huu.

Utafiti huu utajumuisha kaya zipatazo 16,000 ambazo ni sampuli iliyochaguliwa kisayansi kutoka mikoa yote ya Tanzania Bara na Zanzibar na utahusisha watu wazima wasiopungua 40,000 wakiwemo watoto takribani 8,000. 

Aidha, katika utafiti huu kutakuwa na kupima homa ya ini, kupima wingi wa chembechembe za damu yaani CD4, kupima wingi wa virusi katika damu na kupima kiwango cha ufanisi wa dawa za kufubaza VVU kwa watu wanaotumia dawa hizo.

Ifahamike kwamba, utafiti huu wa Viashiria na Matokeo ya UKIMWI wa mwaka 2016 unafanyika nchini kwa mara ya 4 ambapo utafiti wa kwanza ulifanyika mwaka 2003, wa pili ulifanyika mwaka 2007 na wa tatu ulifanyika mwaka 2011.

Hivyo, Ofisi ya Taifa ya Takwimu inapenda kuwatoa hofu wananchi kwakuwa utafiti huu sio mpya katika nchi yetu na watanzania ambao wamekuwa wakipitiwa na utafiti huu, wamekuwa wakitoa ushirikiano kwa zaidi ya asilimia 90.

Utafiti huu wa Viashiria na Matokeo ya UKIMWI Tanzania utaendeshwa na Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) kwa kushirikiana na Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Tanzania Bara, Wizara ya Afya kwa Tanzania Zanzibar, Ofisi ya Mtakwimu Mkuu wa Serikali, Zanzibar (OCGS), Tume ya Taifa ya Kudhibiti UKIMWI (TACAIDS) na Tume ya UKIMWI Zanzibar (ZAC).
 
Imetolewa na:
Mkurugenzi Mkuu,
Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS),
Dar es Salaam,
28 Juni, 2016.

Makamu Wa Rais Mhe. Samia Akutana Na Rais Wa Comoro Pamoja Na Balozi Wa Japan Nchini Jijini Dar Es Salaam

$
0
0
Rais wa Comoro AzaliI Assouman amesema serikali yake itaendelea kudumisha uhusianona ushirikiano wa kihistoria  kati ya Tanzania  na Comoro katika sekta mbalimbali ikiwemo elimu,afya na biashara.

Rais huyo wa Comoro ametoa kauli hiyo katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam alipokutana na kufanya mazungumzo na Makamu wa Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa niaba ya Rais John Pombe Magufuli akiwa kwenye mapumziko mafupi kabla ya  kuendelea na safari yake ya Mecca – SaudiArabia kwa ajili ya ibada ya UMRAH.

Rais  Azali Assouman pia amepongeza jitihada zinazofanywa na serikali ya awamu ya Tanozinazolenga kuhakikisha wananchi wa Tanzania wanapata huduma bora za kijamii nakusisitiza kuwa serikali yake itaendelea kujifunza kutoka Tanzania ili kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili wananchi wa Komoro.

Akitoa ujumbe wa Rais JOHN MAGUFULI kwa Rais wa  Comoro Azali assouman, Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan amemhakikishia Rais wa Comoro kuwa Tanzania itadumisha uhusiano uliopo kati ya nchi hizo MBILI hasa kwenye sekta za elimu, afya na biashara kwa ajili ya manufaa ya nchi hizo MBILI.
 
Makamu wa Rais pia amemtakia Rais wa Comoro kheri katika safari yake ya Mecca– Saudi Arabia kwa ajili ya Ibada ya Umrah.
 
Wakati huo huo Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa JAPAN hapa nchini Masaharu Yoshida na kumweleza kuwa serikali itaendelea kuweka na kuboresha mazingira bora kwa ajili ya wawekezaji kutoka mataifa mbalimbali Duniani ikiwemo wawekezaji kutoka
nchini  JAPAN.
 
Makamu wa Rais amesema serikali ya JAPAN imekuwa mshirika mkubwa wa maendeleo kwa Tanzania katika kufadhili miradi mbalimbali ya maendeleo Tanzania Bara na Visiwa hasa kwenye sekta ya elimu, afya na maji na kusema jambo hilo ni zuri na lakuigwa na washirika wengine wa maendeleo.
 
Kwa upande wake Balozi wa Japan hapa nchini MASAHARU YOSHINDA amemhakikishia Makamu wa Rais SAMIA SULUHU HASSAN kuwa nchi yake itaendelea kufadhili  ipasavyo miradi ya maendeleo hapa nchini ili kuhakikisha wananchi wa Tanzania wanapata huduma bora za kijamii.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Balozi wa Japan nchini Mhe. Yoshida Masaharu Ikulu jijini Dar es Salaam ambapo Balozi wa Japan Nchini alisema nchi yake imeridhishwa na kasi ya Serikali ya Rais Mhe. Magufuli na kuahidi kuendelea kuisaidia Tanzania

Watano wafariki, 13 wajeruhiwa Jijini Mwanza

$
0
0

WATU watano wamefariki  dunia na wengine 13 kujeruhiwa katika ajali ya basi lenye namba za usajili T. 449 BCB mali ya kampuni ya Super Sami lililokuwa likitokea  Dar es Salaam kwenda Mwanza.

Ajali hiyo imetokea usiku wa kuamikia leo katika eneo la Bashini Kata ya Mabuki Wilaya ya Misungwi mkoani Mwanza, baada ya gari hilo kugonga jiwe lililokuwa barabarani na kusababisha William Elias, Dereva wa gari hilo kushindwa kulimdu.

Watu waliopoteza maisha katika ajali hiyo ni Valieth Odede, William Elias (Dereva) huku mwanaume mmoja na wanawake wawili wenye umri wa miaka 25- 30 majina yao bado yakiwa bado hayajafahamika mpaka hivi sasa.

Majeruhi katika ajali hiyo ni 13, ambao ni Sophia Miraji, Kibilo Mwacha, Boniphace Charles na Frank Kunyumi ambao wamelazwa katika Hospitali ya Wilaya ya Misungwi kwa ajili ya kupatiwa matibabu ya awali kutokana na kujeruhiwa vibaya.

Wengine ni Stanley Zacharia, Sia Dauson, Hellen Leheke, Michael Leonard, Kudra Ibrahim (mtoto wa miaka miwili), Zamda Issa, Marieth Christopher, Elizabeth Simon na Dickson Msamba ambao wamelazwa katika hospitali ya Rufaa ya Bugando (BMC) jijini hapa.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Ahmed Msangi, akizungumzia tukio hilo, amesema chanzo cha ajali hiyo ni dereva wa gari hilo kuwa katika mwendo kasi na kusababisha ashindwe kulimdu basi hilo na kusababisha kupinduka.

Msangi, amesema kuwa kutokana na ajali hiyo jeshi la Polisi mkoani hapa linaendelea kuchunguza gari hilo pamoja na kufanya uchunguzi juu ya ajali hiyo iliosababisha vifo vya watu watano kupoteza maisha na wengine 13 kujeruhiwa.

Lesotho Yakubali Kutekeleza Masharti Ya SADC

$
0
0
WAZIRI MKUU wa Lesotho, Dk. Pakalitha Mosisili amekubali kutekeleza masharti yaliyowekwa na Wakuu wa Nchi na Serikali na Kamati ya Siasa, Ulinzi na Usalama ya Jumuiya ya Uchumi na Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC Double Troika Summit), na kuridhia timu ya uchunguzi kwenda nchini humo kufanya uchunguzi wa hali ya kiusalama na kisiasa.

Dk. Mosisili ametoa uamuzi huo leo (Jumanne, 28 Juni, 2016) wakati wa kikao maalum cha Wakuu wa Nchi na Serikali (SADC Summit) na wakuu wa nchi wanaounda Kamati ya Siasa, Ulinzi na Usalama (SADC Organ on Politics, Defense and Security Cooperation) kilichofanyika kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa (GICC), jijini Gaborone, Botswana.

Pia amekubali viongozi waupinzani na baadhi ya maofisa wa kijeshi wanaoishi uhamishoni ambao walikimbia machafuko yaliyotokea nchini humo warejee nchini mwao na kuahidi kwamba atahakikisha wanapatiwa ulinziwa kutosha.

Januari mwaka huu, mkutano wa SADC Double Troika uliagizakwambaifikapo Februari Mosi, mwaka huuSerikali ya Lesotho iwe imetangaza matokeo ya Tume iliyoundwa kuchunguza matatizo ya kisiasa na kiusalama nchini humo hususan mazingira yaliyopelekea kifo cha marehemu Luteni Jenerali Maaparankoe Mahao ambaye alikuwa Mkuuwa Majeshi.

Kwaupande wake, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ambaye alikuwa akimwakilisha Rais Dk. John Pombe Magufuli katika kikao hicho amesema wamepitia ripoti iliyoundwa na timu ya SADC iliyochunguza kuhusu matatizo ya Lethoto ambayo iliwahoji Viongozi wa Serikali, Jeshi, Bunge na familia ya marehemu Luteni Jenerali Mahao.

“Lengo la hatuahiiza SADC ni kuhakikisha inarejesha hali ya amani na utulivu kwenye maeneo ya siasa, ulinzi na usalama katika nchi wanachama wa Jumuiya hiyo ili wananchi wake waweze kuishi vizuri,” amesema

Pia Waziri Mkuu amesema Tanzania inatarajiwa kukabidhiwa uenyekiti wa Wakuu wa Nchina Serikali na Kamati ya Siasa, Ulinzi na Usalama ya Jumuiya ya Uchumi na Maendeleo ya nchi za Kusini mwa Afrika (SADC Double Troika Summit), Agosti mwaka huu ambapo kitafanyika kikao kingine nchini  Tanzania.

Mkutano huo wa ulifunguliwa na Rais wa Botswana, Mhe. Lt. Jen. Seretse Khama Ian Khama na ulihudhuriwa na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ambaye alikuwa akimwakilisha Rais Dk. John Pombe Magufuli;  Rais wa Afrika Kusini, Bw. Jacob Zuma; Rais wa Msumbiji, Bw. Filipe Jacinto Nyusi; Rais wa Zimbabwe, Bw. Robert Mugabe, Mfalme Muswati wa III wa Swazland.

SADC Double Troika ni kikao maalum kinachojumuisha Wakuu wa Nchi na Serikali (SADC Summit) na wakuu wa nchi wanaounda Kamati ya Siasa, Ulinzi na Usalama (SADC Organ on Politics, Defense and Security Cooperation).

SADC Double Troika ni mkutano unaohusisha viongozi wakuu watatu wanaoongoza chombo cha ushirikiano wa siasa, ulinzi na usalama na wengine watatu kutoka kwenye Mkutano wa wakuu wa nchi wanachama wa SADC. Hawa wanawakilisha mwenyekiti aliyepo madarakani, mwenyekiti aliyemaliza muda wake na mwenyekiti ajaye ambaye huwa ni makamu mwenyekiti.

Chini ya muundo wa SADC, kuna mambo makuu mawili; la kwanza likiwa ni utangamano wa kikanda ambao unasimamiwa na mkutano wa wakuu wa nchi (SADC Summit) na la pili ni la siasa, ulinzi na usalama ambalo linasimamiwa na chombo maalum (SADC Organ).

Wajumbe wa mkutano wa SADC Organ ni Msumbiji (Mwenyekiti); Afrika Kusini (Mwenyekiti aliyemaliza muda wake) na Tanzania inayotarajia kuchukua uenyekiti wa chombo hiki ifikapo Agosti, 2016. Botswana, Zimbabwe na Swaziland ndizo zinaunda SADC Summit.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumatano ya June 29

Sheria ya Manunuzi Yaanza Kung’ata....Posho Zafyekwa, Vikao Vyapunguza Kutoka 12 Hadi 4

$
0
0

MAREKEBISHO ya Sheria mpya ya Manunuzi, yamewasilishwa bungeni yakitamka kufyeka posho za watendaji, wanaosimamia mchakato wa zabuni na kuondoa vikao vya bodi kutoka 12 kwa mwaka hadi vinne, ikisisitiza kuziba mianya ya rushwa na kuongeza uwazi.

Aidha, muswada wa marekebisho hayo, unataka kampuni au mshauri wa nje ili apewe zabuni katika shughuli zinazogharimiwa na fedha za umma, ahakikishe asilimia 60 ya wafanyakazi wa kampuni yake ni Watanzania.

Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango, aliyasema hayo jana mjini Dodoma wakati akiwasilisha Muswada wa Marekebisho ya Sheria ya Ununuzi wa Umma wa Mwaka 2016.

Kupungua kwa vikao vya bodi, kumeelezwa na Dk Mpango kuwa kutapunguza gharama zinazotokana na posho ya vikao vya bodi ya zabuni na ada zinazolipwa kwa kamati zinazohusika na mchakato ya zabuni.

Aidha, posho zinazotokana na utekelezaji wa majukumu ya kazi ya kila siku ya washiriki itafutwa. Hata hivyo, imeruhusu kuwapo kwa vikao vya dharura pale Mwenyekiti wa Bodi akiona ni lazima.

Pamoja na kupunguzwa vikao, muda wa zabuni nao umepunguzwa na pia taasisi nunuzi itaruhusiwa kufanya majadiliano ya bei wakati wa mchakato wa zabuni kwa lengo la kupunguza bei ya ununuzi na kuongeza bei ya kuuza mali za serikali.

Dk Mpango alisema sheria hiyo mpya, itaziba mianya ya rushwa, kuongeza kasi, uwazi, uwajibikaji na kuleta upendeleo maalumu kwa kampuni za Tanzania katika zabuni za ndani na za kimataifa.

Pia sheria hiyo itaongeza ufanisi na kupata thamani halisi ya fedha, inayotumika kwa kununua huduma na bidhaa.

Dk Mpango alisema pamoja na kuongeza uwajibikaji, sheria hiyo mpya itapunguza vikao vya bodi hadi kuwa kimoja kwa robo mwaka na vikao vya dharura, kufanyika pale ambapo mwenyekiti ataona inabidi.

Pamoja na maelekezo hayo mapya, serikali pia itaanza kununua bidhaa na huduma kwa bei inayoendana na bei ya soko, iwapo wabunge watapitisha marekebisho ya Sheria ya Ununuzi wa Umma.

Pamoja na ununuzi wa bei ya soko, sheria mpya imelenga kuweka sharti la kisheria kutoa upendeleo katika zabuni mbalimbali, hasa kwa makundi maalumu kama vile wanawake, vijana, wazee na watu wenye mahitaji maalumu.

Alieleza kuwa sheria mpya imelenga kuiwezesha serikali, kunufaika na matumizi ya viwango na kuweka sharti la kisheria la kutumia mifumo ya kuongeza uwazi katika ununuzi ili kuongeza uadilifu na uwajibikaji.

Kwa mujibu wa waziri, sheria mpya imelenga kurahisisha ununuzi wa umma na kuipa faida serikali baada ya kuwapo kwa changamoto nyingi kwa Sheria Namba 7 ya Mwaka 2011, ambayo ilianza kutekelezwa mwaka huo.

Changamoto hizo ni pamoja na bei ya juu ya bidhaa na huduma zinazonunuliwa na serikali kulinganisha na bei ya soko kutokana na zuio la majadiliano kuhusu bei kati ya taasisi nunuzi na mzabuni.

Pamoja na changamoto ya bei, kumekuwepo na muda mrefu wa mchakato, gharama kubwa zinazotokana na matangazo na vikao mbalimbali vya kupitia zabuni, kutozingatiwa kwa viwango na kutokuwepo kwa upendeleo katika ushiriki wa zabuni kwa makundi maalumu.

Mapendekezo ya muswada huo, pia yametaka pale kampuni au taasisi ya umma inapolazimika kufanya ununuzi kutoka nje ya nchi, hasa kama ni suala la ushauri linafanywa na kampuni ya nje ya nchi, ofisi hiyo ya serikali inalazimika kuhakikisha kuna wataalamu wa ndani ya nchi.

Aidha, kampuni au mshauri huyo wa nje ili apewe zabuni katika shughuli ambazo zinagharimiwa na fedha za umma, kuna kigezo cha kuhakikisha wafanyakazi wa kampuni yake, zaidi ya asilimia 60 ni Watanzania.

Mbali na kuwa na asilimia 60 ya wafanyakazi Watanzania, kampuni husika lazima ieleze kiwango cha bidhaa na huduma zinazozalishwa ndani ya nchi, ambazo itazinunua katika utekelezaji wa shughuli zake.

Nayo Kamati ya Bunge ya Bajeti imeitaka serikali kusimamia na kuhakikisha kwamba watumishi wa umma ambao hawastahili kupewa magari, watumie magari yao binafsi ; na wale ambao wanastahili wakopeshwe magari na serikali na kupewa posho kidogo kwa ajili ya mafuta na matengenezo.

Pia, imeitaka serikali iandae utaratibu wa kununua magari kwa pamoja yasiyo na gharama kubwa kulingana na bei ya soko.

Akisoma maoni ya Kamati ya Bunge ya Bajeti kuhusu Muswada wa Marekebisho ya Sheria ya Ununuzi wa Umma wa mwaka 2016, Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Hawa Ghasia alisema kamati imekubaliana na serikali kufanya manunuzi kwa kuzingatia thamani ya fedha kwa bidhaa, ikiwamo manunuzi ya magari 

Alisema muswada huo unaonesha kwamba inawezekana kupunguza gharama za serikali kwa kufuata thamani ya fedha.

Aidha kamati hiyo imeishauri serikali kuanzisha mfuko wa uwezeshaji wa makandarasi ili waweze kumudu utoaji wa huduma mbalimbali, zinazohuisha gharama kubwa, mfano ukandarasi wa barabara. 

Mfuko huo utakuwa ukitoa dhamana. Pia kamati hiyo inataka kujua mwanzo wa matumizi ya sheria mpya.

Wabunge waliochangia muswada huo, waliitaka serikali nayo kujiunga katika sheria hiyo kwa kuona kwamba inawalipa wazabuni mapema au inaeleza watakavyoweza kuwa wazabuni wanapochelewesha malipo, hasa kutokana na kampeni yake ya ununuzi kwa bei ya soko.

Wabunge hao walisema kwamba serikali inajua sababu za bei kubwa na hivyo inafaa ikajipanga kuondoa kasoro hiyo ili hiyo sheria iweze kutekelezeka.

Mbunge wa Mwibara, Kangi Ligora (CCM) alitoa tahadhari kwamba sheria inabadilishwa Ibara 40 ambayo ni sehemu kubwa na kusema kwamba lazima ijiandae kuondoa sababu za bei kubwa na pia kutofuta kipengele cha kamati ya mipango na fedha kwenye halmashauri kupitia zabuni kwa lengo la kujiridhisha.

Kauli ya kutofuta kipengele hicho katika muswada, pia ilizungumzwa na wabunge waliochangia jana.

Aidha wengine walitaka kuwapo na dirisha kwa ajili ya dharura na hasa dirisha kwa ajili ya bidhaa za afya na tiba. Wabunge wengine waliochangia ni Martha Mlata, Rita Kabati, Ali Hassan, Dk Diodorus Kamara, Japhet Asunga, Adadi Rajab, Jitu Son, John Kadutu na Amina Mollel.

Gesi ya Helium ya Futi za ujazo B ilioni 54 Yagundulika Tanzania

$
0
0

GESI ya helium ya takribani futi za ujazo bilioni 54 inayoelezwa kuwa adimu duniani, imegundulika nchini Tanzania na kuiweka nchi kuwa miongoni mwa mataifa machache yenye madini mengi na muhimu.

Wagunduzi wa gesi hiyo ni watafiti kutoka vyuo vikuu viwili nchini Uingereza vya Oxford na Durham kwa kushirikiana na wataalamu wa madini kutoka nchini Norway.

Watafiti hao wamegundua hifadhi kubwa zaidi duniani ya gesi hiyo ya barafu, kama inavyofahamika katika eneo la Bonde la Ufa nchini.

Taarifa za waandishi wa habari nchini Japan, zimeeleza kuwa watafiti hao wamesema kuwa uhaba wa gesi hiyo duniani ulikuwa umesababisha taharuki haswa kwa madaktari, ambao wanatumia gesi hiyo adimu kuendesha mashine za utabibu zijulikanazo kama ‘MRI scanners’.

Pia hutumia katika mitambo ya kinyuklia na katika sekta nyingine nyingi za kiteknolojia.

Wiki iliyopita, Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo wakati akijibu swali bungeni mjini Dodoma alisema madini yanayotumika kwa ajili ya mitambo ya Apollo na pia vifaa vya matibabu kama MRI na NMR, yamegundulika kuwepo nchini Tanzania.

Hata hivyo, hakufafanua zaidi kiasi cha madini hayo na namna nchi itakavyonufaika na ugunduzi huo. Hata alipotafutwa jana, simu yake ya mkononi ilipokewa na msaidizi wake na kueleza kuwa waziri yuko kikaoni. Madini aina ya helium yanatumika kwa ajili ya mitambo na pia kwenye vifaa vya matibabu kama MRI na NMR.

Kabla ugunduzi huo, watafiti walikuwa wamebashiri ukosefu wa gesi hiyo ifikapo mwaka wa 2035.

Mnamo mwaka 2010, mwanasayansi ambaye alikuwa mshindi ya Tuzo la Nobel, Robert Richardson alitabiri kumalizika kwa gesi hiyo katika kipindi kifupi. Ukosefu huo ulikuwa umesababisha wataalamu, kuhimiza kutungwa kwa sheria itakayopunguza matumizi yake katika bidhaa zisizo za dharura.

Mtaalamu kutoka Chuo Kikuu cha Oxford, Chris Ballentine alisema gesi hiyo iliyopatikana nchini inaweza kujaza silinda za gesi milioni 1.2 za mashine za MRI.

CCM Yawalima Barua Wabunge Wake.....Sasa Watakiwa Kujieleza Kamati Kuu

$
0
0

Kamati Kuu ya CCM imeagiza Kamati ya Wabunge wa chama hicho kuwapa barua za kujieleza wabunge wao wasiohudhuria, wanaochelewa na wanaondoka kabla ya vikao vya Bunge kuahirishwa. 

Tayari maagizo hayo yamefanyiwa kazi na Katibu wa Wabunge wa CCM, Jasson Rweikiza ambaye amewalima barua wabunge hao. 

Katika barua yenye kichwa cha habari “Maagizo ya Kamati Kuu ya CCM” aliyopewa mmoja wa wabunge wa CCM inaonyesha wametakiwa kujieleza kwa nini siku nyingine walifika wamechelewa na mara kadhaa walitoka mapema kabla kuahirishwa kwa Bunge. 

“Mwenendo huu ni kukiuka kanuni za Kamati ya Wabunge wote wa CCM hasa kanuni ya 41. Tafadhali andika maelezo kwa nini Kamati Kuu isichukue hatua? Maelezo yanifikie  kabla ya Juni 25 mwaka huu,” ilisema sehemu ya barua ya mmoja wa wabunge walioandikiwa. 

Alipoulizwa Rweikiza kuhusiana na barua hiyo alisema haitambui na kwamba imeghushiwa. 

“Kanuni zipo zinazoongoza vikao vya Bunge, zipo pia zinazoongoza wabunge wa CCM. 

"Wakitaka kuondoa wabunge wa CCM wanazijua sana, isipokuwa hatujafikia hatua ya kufundishana kwa kuanza kuandikiana barua,”alisema. 

“Wanajua mbunge hawezi kuondoka bila kwenda kwa Spika na kuomba ruhusa au kujulisha kwenye chama kwamba anatoka, wanajua,” alisema Rweikiza na kusisitiza kwamba hata taarifa zinazoonyesha kuna wabunge wanaotakiwa kujieleza kwake ni majungu tu. 

Japokuwa Rweikiza ameikana barua hiyo, wabunge kadhaa wa CCM walioomba majina yao yasitajwe wamekiri kwamba barua hizo zimetolewa na kwamba wanabanwa kwa kutakiwa kujisajili mara mbili; kitabu cha Bunge na cha CCM. 

Katika ukurasa wake wa Facebook uliosambazwa kwenye mitandao ya kijamii, Mbunge wa Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa (Chadema), alisema wabunge wa CCM wanalalamikia kulazimishwa kuingia bungeni kwa kuwa Bunge halina ladha. 

Pia, Msigwa alisema wabunge hao wa CCM wanadai Naibu Spika Dk Tulia Ackson hafuati kanuni na taratibu na kwamba wametakiwa kujieleza Kamati Kuu ya CCM. 

Aidha, baadhi ya wabunge wa CCM walionekana kukerwa na utaratibu wa kujisajili sehemu mbili yaani Bunge na CCM mara mbili kwa siku. 

“Kuna haja gani ya kutia dole (kusaini kwa utaratibu wa kieletroniki) halafu tena tuje tusaini kwenye makaratasi ya CCM?,” alihoji mmoja wa  wabunge. 

Alisema ili kusaini karatasi hizo inawapasa wabunge kwenda upande wa Kambi Rasmi ya Upinzani ambapo wabunge waliokabidhiwa kazi ya kuzitunza karatasi hizo hukaa kama kambi mbadala baada ya wabunge wa upinzani kususia vikao vinavyoendeshwa na Dk Tulia.

“Wengine tunaheshima zetu hatuwezi kwenda upande wa upinzani kufuata makaratasi ya kusaini. Kwanza Bunge lenyewe halina mvuto unakuja hapa watu wawili ndio wanapewa nafasi ya kuchangia mjadala na baada ya hapo wanapitisha,” alisema. 

Mbunge mwingine wa CCM alisema haoni haja ya kuwepo ndani ya Bunge kwa sababu hawapewi nafasi ya kutosha ya majadiliano na hivyo bora kutokuwepo ndani ya ukumbi muda wote. 

“Mimi saa hizi naingia ndani ya ukumbi wa Bunge nasaini natoka naenda zangu kantini (ya Bunge) kuangalia mpira maana hata nikikaa ndani sitopata nafasi ya kuchangia,” alisema mbunge huyo. 

Alisema haoni haja ya kusaini mara mbili kwa sababu CCM wanaweza kutumia usajili wa Bunge kufahamu wabunge waliopo na wasiohudhuria kwa wakati wanaouhitaji. 

Alisema orodha hiyo haina mashiko kwa sababu wanazo namba za wabunge wote kama kuna jambo ambalo wanahitaji basi wanaweza kuwataarifu. 

“Hata mimi nimepewa barua ya kujieleza lakini si kwamba ni mtoro bali tunakuwa na majukumu mengine ya kibunge nje ya Bunge,” alisema. 

Hatua hiyo inakuja wakati wabunge 118 wa vyama vinavyounda Ukawa, wakiwa wamesusia vikao vya Bunge vinavyoendeshwa na Naibu Spika, Dk Tulia Ackson kwa madai ya kuongoza vikao kibabe na kutofuata kanuni. 

Hii ni wiki ya nne tangu Dk Tulia aanze kuendesha vikao vya Bunge peke yake bila kupokewa na wenyekiti wa Bunge kama ilivyokuwa kabla hajatofautiana na kambi rasmi ya upinzani

Kujitoa EU: Uingereza Yawatoa hofu Watanzania

$
0
0
Siku chache baada ya Uingereza kuamua kujitoa katika Umoja wa Ulaya (EU), Balozi wa nchi hiyo nchini amesema wataendelea kuimarisha uhusiano na Tanzania ili kuhakikisha uwekezaji haupungui.

Akijibu swali kuhusu athari zozote zitakazojitokeza kwa Tanzania baada ya Uingereza kujitoa EU, Balozi wa Uingereza nchini, Dianna Melrose alisema jana kuwa haitapunguza uwekezaji, misaada wala vita dhidi ya rushwa na uhalifu wa kimtandao.

“Uhusiano wetu utaendelea kuwa imara kama ulivyokuwa awali,” alisema Melrose.

Balozi Melrose alisisitiza kuwa Uingereza itaendelea kuwa mwanachama katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa (UN), Umoja wa Kujihami wa Nchi za Magharibi (Nato), Umoja wa nchi saba zilizoendelea zaidi duniani (G7), umoja wa mawaziri wa fedha na magavana wa benki kuu kutoka nchi zenye uchumi mkubwa duniani (G20) na Jumuiya ya Madola na kushirikiana na Tanzania.

Tangu Juni 23 Uingereza ilipopiga kura ya maoni kujitoa EU, umetokea mtikisiko mkubwa kati ya England na washirika wake Wales, Scotland na Ireland Kaskazini.

Kura hiyo ya maoni imesababisha Waziri Mkuu, David Cameron kutangaza kujiuzulu kwa kushindwa kwake kushawishi nchi hiyo kubaki EU.

Mtikisiko mwingine mkubwa umejitokeza katika masoko ya hisa ambapo tangu Alhamisi iliyopita yameporomoka na kupoteza Dola za Marekani trilioni mbili.

Ofisa Mtendaji Mkuu wa Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE), Moremi Marwa alisema soko lake na mengine Uingereza ni miongoni mwa nchi nne zenye mchango mkubwa wa kifedha kwa EU.

Takwimu zinaonyesha kuwa kwa mwaka jana pekee ilichangia Pauni 12.9 bilioni (zaidi Sh37.5 trilioni).

Kiasi hicho ni kikubwa kwa Sh10 trilioni ya bajeti ya Tanzania kwa mwaka ujao wa fedha, 2016/2017.

“DSE haijaunganishwa sana na masoko ya nje lakini tunao wawekezaji wengi kutoka Uingereza,” alisema Moremi na kubainisha kuwa, mabadiliko yanaweza yakaonekana Soko la Hisa la Johanessburg (JSE), Afrika Kusini.

Alipoulizwa Katibu Mkuu wa Viwanda na Uwekezaji, Profesa Adolf Mkenda kwamba Serikali imejipanga vipi kukabiliana na athari zitakazojitokeza baada ya Uingereza kujitoa alisema ni mapema sana kwa wizara yake na Tanzania kwa ujumla kutetereka kwa namna yoyote kwa sasa kwa kuwa uhusiano mkubwa uliopo ni ule wa kiuwekezaji.

“Uwekezaji siyo suala la siku moja,” alisema na kufafanua kuwa mikataba ambayo ilishatiwa saini ni lazima itekelezwe kama makubaliano yalivyofanywa. “Masoko ya hisa ndiyo yanayoweza kuathirika kwa muda huu mfupi,” aliongeza.

Mkurugenzi wa Uhusiano na Sheria wa Shirikisho la Wenye Viwanda Tanzania (CTI), Hussein Kamote alisema muda huo wa utekelezaji wa maadhimio ya kujitoa ni mrefu na huenda hatua za haraka zikachukuliwa kabla athari za kiuchumi hazijasambaa duniani kote.

Taarifa ya Lugumi Yapigwa Kalenda Tena Bungeni

$
0
0

Ripoti ya sakata la mkataba wa kampuni ya Lugumi Enteprises na Jeshi la Polisi, ambayo ilikuwa iwasilishwe kwenye mkutano unaoendelea wa Bunge, sasa itawasilishwa kwenye mkutano ujao.

Makamu mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), Hilary Aeshi alisema ripoti hiyo itaunganishwa katika taarifa za kamati ambazo kwa utaratibu huwasilishwa kwenye mkutano huo.

Sakata hilo linahusisha utekelezaji mbovu wa mkataba wa kufunga mashine za kielektroniki za kuchukulia alama za vidole kwenye vituo 108 vya polisi.

Hadi wakati Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) akifanya ukaguzi wa mkataba huo wa Sh37 bilioni uliosainiwa mwaka 2013, ni vituo 14 tu vilivyokuwa vimefungwa mashine hizo, lakini mzabuni alishalipwa Sh36 bilioni.

Baada ya sakata hilo kuibuliwa, wabunge walitaka liwasilishwe kwenye mkutano unaoendelea mjini Dodoma, lakini PAC ikaunda kamati ndogo ambayo sasa inatakiwa iwasilishe ripoti ya uchunguzi wake.

Hadi jana asubuhi ripoti ya kamati hiyo ndogo, iliyoundwa na wajumbe tisa, ilikuwa bado haijawasilisha ripoti yao.

Hata hivyo, Aeshi ambaye pia ni mbunge wa Sumbawanga Mjini (CCM), alisema alitarajia kukabidhiwa ripoti hiyo na kamati ndogo jana na baada ya hapo kazi ya uchambuzi wa kamati nzima itaanza.

Serikali Yasisitiza Nchi iko Salama

$
0
0
SERIKALI imewatoa hofu Watanzania wote Bara na Visiwani kuwa nchi iko salama na inaendelea kuwa salama pamoja na kuwapo kwa vitisho kwa njia ya mtandao.

Kauli hiyo ilitolewa jana na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Hamad Yussuf Masauni, wakati wa kujibu swali la nyongeza la Mbunge wa Viti Maalumu, Tauhida Nyimbo (CCM) aliyetaka kauli ya serikali kutokana kuwapo kwa taarifa za vitisho zinazotolewa kwenye mtandao wakati huu wa maandalizi ya sikukuu ya Idd el Fitr.

Alisema pamoja na kuwapo kwa vitendo vya kiuhalifu vinavyotokea, nchi bado iko salama na itaendelea kuwa salama kutokana na serikali kuhakikisha inadhibiti uhalifu huo. 

Serikali imeendelea kusisitiza kuwa mikutano ya kisiasa itaendelea kuzuiwa hadi pale polisi watakapoona inafaa kufanyika.

Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images