Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Katibu Mkuu Chadema Ziarani Ghana

$
0
0

Katibu Mkuu wa Chadema Dk Vincent Mashinji ameanza ziara ya kikazi ya siku tano nchini Ghana ambako pamoja na shughuli nyingine, atashiriki mkutano wa kimkakati kuhusu masuala ya uchaguzi.

Katika ziara hiyo, Mashinji anatarajiwa kukutana na mgombea urais wa chama rafiki na Chadema, New Patriotic Party (NPP), Nana Akufo Addo kwa ajili ya kushauriana, kubadilishana uzoefu wa kisiasa na kupeana mikakati ya ushindi katika uchaguzi.

Dk Vincent Mashinji pia atakutana na Dk Klaus Schuler ambaye ni meneja wa kampeni wa Kansela wa Ujerumani, Angela Merkel. Dk Schuler pia ni Meneja Mkuu wa chama tawala Ujerumani cha CDU.

Katika ziara hiyo, Dk Mashinji ameambatana na Mkurugenzi wa Bunge na Halmashauri, John Mrema ambaye katika Uchaguzi Mkuu uliopita alikuwa meneja wa kampeni wa mgombea urais wa Chadema aliyewakilisha Ukawa, Edward Lowassa.

 Mbali ya Tanzania, nchi nyingine 15 zinazotarajiwa kushiriki mkutano huo ni pamoja na Kenya, Uganda, Zimbabwe, DRC, Angola, Namibia, Nigeria, Senegal, Ivory Coast, Togo, Burkina Faso, Benin, Afrika Kusini, Ghana na Ujerumani.

Bodaboda Wagongana Jijini Mwanza, mmoja afariki

$
0
0
Mwendesha pikipiki ambaye hajafahamika amefariki dunia baada kugongana uso kwa uso na mwenzake, eneo la Mabatini jijini Mwanza.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Ahmed Msangi alisema bodaboda mwingine Stanley Maimu (24), alijeruhiwa katika tukio hilo lililotokea Mei 15.

Msangi alisema ajali hiyo ilisababishwa na mwendokasi wa wahusika, hivyo bodaboda wote walishindwa kumudu pikipiki zao na kugongana uso kwa uso.

Katika tukio jingine, Polisi inawashikilia watu wawili; Chacha Mwita (34) na Rashid Mohamed (34) wakazi wa Kata ya Kitangiri wilayani Ilemela kwa kosa la kukutwa na misokoto sita ya bangi kinyume na sheria.

Kamanda msangi alisema Mei 14 saa 14.00 mchana, polisi waliokuwa doria walifanikiwa kupata taarifa kutoka kwa wasamaria wema kuwapo kwa watu hao wanaojihusisha na biashara hiyo haramu ya kuuza dawa za kulevya.

Aliwataka wananchi kuendelea kutoa ushirikiano wanapobaini vitendo vya uhalifu.

Mtu Mwingine Auawa Kwa Kukatwa Mapanga Usiku Sengerema Mkoani Mwanza

$
0
0

Wakati upelelezi wa tukio la watu saba wa familia moja kuuawa kwa kukatwa mapanga na watu wasiojulikana ukiendelea, mauaji mengine ya aina hiyo yametokea wilayani Sengerema.

Safari hii, mkazi wa Kijiji cha Bilulumo, Kata ya Kafunzo, James Mgambo (71) aliuawa kwa kukatwa mapanga na watu wasiojulikana usiku wa kuamkia jana.

Kwa mujibu wa Diwani wa Kata ya Kafunzo, Dotto Bulunda, mke wa Mgambo aliyetajwa kwa jjina la Nyangalo Masisa (65) alijeruhiwa katika tukio hilo na amelazwa Hospitali ya Wilaya ya Sengerema.

“Chanzo cha mauaji hayo hakijajulikana na polisi wamefika kwa ajili ya uchunguzi,” alisema Bulunda. 

Ofisa Mtendaji wa Kijiji cha Bilulumo, Said Makelemo alisema mapanga mawili yanayoaminika kutumika yalikutwa eneo la tukio.

Mmoja wa majirani wa familia hiyo, Lameck Kasabulilo alisema hawakusikia kelele za kuomba msaada.

Kwa mujibu wa msemaji wa familia, Hakimu Elisha, mazishi ya Mgambo yanatarajiwa kufanyika leo katika makaburi ya ukoo yaliyopo kijijni hapo.

Mgaga Mkuu wa Hospitali Teule Wilaya ya Sengerema, Dk Mary Jose alisema mwili wa marehemu umehifadhiwa chumba cha kuhifadhi maiti, huku hali ya majeruhi ikiendelea vizuri.

Mkuu wa Wilaya Sengerema, Zainab Telack alisema tayari uchunguzi wa kina kuhusu tukio hilo umeanza na kuapa wahusika watasakwa na kutiwa mbaroni.

Mabasi ya Mwendo Kasi ( Dart ) Yaanza kwa Changamoto Lukuki....... Mfumo wa Kukatia Tiketi Walalamikiwa, Walimu nao Walalamika Kutotambuliwa

$
0
0
Huduma  ya usafiri wa mabasi yaendayo haraka imeanza rasmi jana jijini Dar es Salaam huku yakilalamikiwa na watumiaji wakiwemo baadhi ya watu waliokuwa na msamaha wa kusafiri bila kutoa nauli, ambao sasa hawatambuliwi na mfumo mpya.

Utaratibu uliokuwa umezoeleka awali wa askari wa polisi, jeshi, magereza na walimu kutolipa nauli kwenye usafiri wa daladala, umeonekana kugonga mwamba chini ya mabasi hayo. 

Jana  mwalimu ambaye hakufahamika jina lake alisikika akitaka mwongozo wa kutolipa nauli kwa kuwa yeye ni mwalimu.

“ Mama mfumo huu haumtambui mwalimu, askari,” alimjibu mmoja wa wahudumu wa UDA-RT aliyekuwa akihakiki tiketi za abiria kabla ya kupanda basi.

Akijibu hoja hiyo, Mkurugenzi Mtendaji wa UDA-RT, David Mgwasa alisema mwongozo uliotolewa na Sumatra, unamtambua mwanafunzi pekee ambaye anatakiwa kulipa Sh 200, wengine wote wanatakiwa kulipa nauli.

Mbali na walimu, askari, pia watu wenye ulemavu ambao walikuwa hawalipi nauli kwenye daladala, kwenye mfumo wa mabasi yaendayo haraka wanatakiwa kulipa.

Mambo mengine yaliyolalamikiwa ni mfumo wa ukataji tiketi, ambao unadaiwa kusababisha foleni ndefu huku wahudumu wakiwa hawana chenji, jambo lililosababisha baadhi ya watu kulipa kiasi kikubwa cha fedha.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti, baadhi ya abiria walisema walilazimika kukaa zaidi ya dakika 20 vituoni kutokana na kusubiri chenji na wengine kuamua kuacha fedha zao.

“Nimetoa Sh 1,000, nimepewa tiketi na kurudishiwa Sh 200 na kuwa hana Sh 150. Hapa inaonesha nimesafiri kwa Sh 800. Nauli hii ningeitumia kupanda daladala na kuzunguka nalo ili nipate kiti, ningepandia upande wa pili ningetumia Sh 500,” alisema Kasum Swakala, mkazi wa Ubungo Bonyokwa. 

“Nina haraka na siwezi kuipata hiyo 150 ambayo hawajanipa katika chenji yangu, inabidi tu kuondoka ili kuwapisha wengine lakini hali hii inatuumiza sana na siyo sawa kwa sababu kesho siwezi kurudi kuwadai chenji yangu,” alisema.

“Nimetoka Mbezi na kulipa 400, nimefika hapa wanasema hawana cheji kama nataka nilipe 800, siwezi kulipa kiasi hicho naenda kupanda daladala.”

Meneja Uhusiano wa UDA-RT, Deus Bugaywa alikiri kuwapo changamoto ya chenji na kusema asubuhi walikuwa na chenji nyingi ambazo ziliisha haraka hivyo kuleta usumbufu kwa baadhi ya abiria.

Mkazi wa Mbezi, Laurence Msuya alilalamikia hatua ya kukata tiketi mara mbili na kusema imesababisha usumbufu kwao kwa kupoteza muda. Wakala wa kukatisha tiketi katika kituo cha Mbezi alilalamikiwa kuchelewa kufika  jambo lililozidisha msongamano.

Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya UDA-RT, David Mgwasa alisema hali hiyo itaondoka pale mfumo wa kadi utakapoanza kufanya kazi.

“ Wananchi tuliwafundisha namna ya kutumia kadi, na siku moja kabla Serikali ikazuia matumizi yake, sasa tunasubiri maamuzi ili tuanze kuuza. Tulijua wananchi wangekuwa na kadi na wale wachache ambao ni wanafunzi na wale wanatumia mara moja moja ndio wangetumia tiketi za karatasi,” alisema Mkurugenzi wa Uendeshaji na Usimamizi wa Miundombinu wa Wakala wa Mradi wa Mabasi Yaendayo Haraka (Dart), John Shauri 

Alisema mfumo wa tiketi za kadi uko katika hatua za mwisho na mazungumzo.“ Ilikuwa ni lazima tuanze tiketi za karatasi, kwani tutakuwa na mifumo miwili inayofanya kazi hii ya tiketi za karatasi na kadi, mambo yakiwekwa sawa kadi zitaanza kutumika,” alisema.

Changamoto nyingine katika huduma hiyo iliyofanywa na baadhi ya wakala wa kukatisha tiketi kuzongwa au kutakiwa kutoa ufafanuzi ni pamoja na abiria kupewa tiketi za wanafunzi wakati wamelipa nauli ya watu wazima. 

Baadhi ya abiria walijikuta wakikata tiketi nyingine kutokana na za awali kuisha muda wake. Hali hiyo ilitokana na wakazi hao kukata tiketi na kwenda kwenye shughuli zao nyingine na walipofika kituoni na kukuta muda wake umeisha walilazimika kukata nyingine.

“Awali walisema hizi tiketi unaweza kupandia basi wakati wowote lakini nashangaa leo nimekata tiketi nikaamua kwenda kwenye shughuli nyingine. Nimerudi hapa wakati tiketi inakaguliwa ikagoma kusoma kwa madai kuwa muda wake wa matumizi umeisha,” alisema mmoja wa wakazi wa Kimara Mwisho.

Akijibu hoja hiyo, Mgwasa alisema tiketi za karatasi zinatakiwa kutumika kwa safari moja na kuwa zinadumu kwa saa mbili kabla ya kuisha muda wa matumizi na ametumia fursa hiyo kuwasihi wananchi kukata tiketi pale tu wanapotaka kusafiri.

Tiketi zilizokuwa zikitolewa na mawakala wanaohusika zilikuwa hazina maelezo ya nauli waliyolipa abiria zaidi ya kuonesha tarehe, muda uliokata, kituo ulichokatia jambo ambalo liliwafanya abiria kuhoji na kuona ni ujanja wa kupoteza mapato ya serikali.

Walimu 35,411 Kuajiriwa Mwezi wa 7 Mwaka Huu

$
0
0

Walimu 35,411 nchini wataajiriwa katika shule za msingi na sekondari katika mwaka wa fedha 2016/2017.

Watakaokaidi kwenda kuripoti katika mikoa ya pembezoni, hawataajiriwa na serikali.

Hatua hiyo imeelezwa kwamba imetokana na serikali kupokea maombi mengi ya kazi kwa walimu, ambao mwaka jana hawakuripoti katika vituo walivyopangiwa pembezoni mwa miji kwa kutegemea kuajiriwa na shule binafsi, lakini hawakufanikiwa.

Naibu Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Selemani Jaffo alisema hayo alipokuwa akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Mchinga, Hamidu Bobali (CUF) aliyetaka kufahamu serikali inafanya nini kwa walimu waliopangiwa kwenda mikoa ya pembezoni, ikiwemo Lindi na kwingineko, lakini hawakuripoti.

Jaffo alisema ni kweli kuna walimu wengi ambao hawakuripoti katika mikoa ya pembezoni. Alisema si Lindi peke yake, bali na mikoa mingine, ikiwemo Katavi na Kigoma.

Alisema kwa mwaka huu, wataajiri walimu 35,411, lakini ambaye hataripoti katika mikoa hiyo na kuishia mijini tu, hawataajiriwa tena serikalini, kama wanavyoomba tena baada ya kukosa katika shule binafsi.

Mjane Aliyemwaga Machozi Mbele ya Rais Magufuli Akabidhiwa Nyumba Yake

$
0
0

Hatimaye mjane aliyemwaga machozi mbele ya Rais John Magufuli akidai kudhulumiwa mali ya urithi, amepewa nyumba na shamba baada ya Mkuu wa Wilaya ya Babati mkoani Manyara, Crispin Meela kusuluhisha mgogoro wa umiliki wa mali hizo.

Hivi karibuni akiwa mjini Babati, Rais Magufuli alimuagiza Meela ahakikishe mjane huyo, Mwanaidi Mussa anapewa mali zake ikiwamo nyumba na shamba zilizokuwa zinadaiwa kuchukuliwa na mke mdogo kinyume cha sheria.

Meela alimkabidhi nyumba na shamba la ekari 2.5 mjane huyo juzi na kuagiza mke mdogo kama hakuridhika na uamuzi, akakate rufaa mahakamani.

Meela pia aliwataka wananchi kuacha kurubuniwa na watu wachache wenye maslahi binafsi na badala yake wafuate maelekezo yanayotolewa na vyombo vya sheria.

“Migogoro ya mirathi imeendelea kukithiri katika maeneo mengi nchini kutokana na watu kutofuata sheria za mirathi na wengine wakitaka kunufaika na mali zinazoachwa na marehemu,” alisema Meela.

Mwanaidi ambaye amezeeka, alidai kwa muda mrefu amewaomba viongozi wa Serikali ya mtaa anaoishi wamsaidie, kutatua tatizo lake lakini walimpuuza.

Mke mdogo, Asia Musa alidai kuwa nyumba hiyo aliyokabidhiwa Mwanaidi, aliijenga na mumewe kauli ambayo ilikinzana na ya mke mkubwa aliyedai kuwa wakati Asia anaoelewa alikuta nyumba ameshaijenga na mumewe.

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Akutana Na Balozi Wa Tanzania Nchini Uingereza, Dkt. Asha- Rose Migiro

$
0
0

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana  na Balozi wa Tanzania  nchini Uingereza, Dkt. Asha – Rose  Migiro kabla ya mazungumzo yao  Ofisini kwake jijini Dar es salaam  Mei 17, 2016.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza  na Balozi wa Tanzania nchini Uingereza, Dkt. Asha – Rose Migiro  ofisini kwake jijini Dar es salaam Mei 17, 2016.

(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

David Kafulila ashindwa kesi yake dhidi ya Hasna Mwilima mahakama kuu kanda ya Tabora

$
0
0

Mbunge wa zamani wa   Kigoma kusini (NCCR-MAGEUZI), David Kafulila ameshindwa kwenye kesi yake iliyokuwa ikisikilizwa mahakama kuu kanda ya Tabora kuhusu kupinga matokeo yaliyompa ushindi mbunge wa CCM, Hasna Mwilima
 
Kesi hii ilifunguliwa katika mahakama kuu kanda ya Tabora na kuendeshwa  chini ya Jaji Ferdinand Wambari.
 
Katika kesi hiyo upande wa mlalamikaji (Kafulila) uliongozwa na mawakili Prof. Abdallah Safari, Tundu Lissu na Daniel Lumenyera, Ili hali upande wa mlalamikiwa (Husna) uliongozwa na wakili Kenedy Fungamtama pamoja na mawakili wa serikali upande wa mwanasheria mkuu.

Bunge laitaka Serikali kuharakisha ujenzi wa reli ya kati kwa kiwango cha standard gauge.

$
0
0
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu imeshauri Serikali kuharakisha ujenzi wa reli ya kati kwa kiwango cha standard gauge ili kuisaidia Bandari ya Dar es salaam kukabiliana na ushindani kutoka bandari ya nchi jirani.

Hatua hii itasaidia kuleta maendeleo ya haraka hapa nchini kupitia upokeaji na usafirishaji wa  mizigo mingi ya nchini na nje ya nchi.

Kauli hiyo imetolewa leo mjini Dodoma na Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu Profesa Norman Sigala wakati akiwasilisha taarifa kuhusu utekelezaji wa bajeti ya Wizara ya Ujenzi ,Uchukuzi na Mawasiliano ya mwaka ujao wa fedha.

Amesema kuwa nchi nyingine za wanachama wa Afrika Mashariki zinaendelea kujenga reli kwa kiwango cha standard gauge kutoka Mombasa kupitia Nairobi , Kampala hadi Kigali kwa kasi kubwa.

Mhe. Profesa Norman alisema kuwa ili Bandari za Tanzania ziweze kushindana na Bandari za Kenya katika kupokea mizigo ya nchi za Uganda na Rwanda ni vema reli ya kati ikajengwa kwa kiwango cha standard gauge ili iziunganishe nchi hizo na reli inawezesha kusafirisha mizigo bila vikwazo.

Aliongeza kuwa kukamilika kwa reli kwa kiwango hicho itasaidia kuwanufaisha mikoa 15 ya Tanzania bara.

Profesa Norman alisema kuwa ni vema Serikali ikaharakisha ujenzi wa reli ya kati na matawi yake yote ambayo ni kutoka Dar salaam kwenda kigoma, Uvinza hadi Msongati kwa ajili ya mizigo ya Burundi.

Alisema kuwa tawi jingine ni lile la kutoka Tabora hadi Kalemi kwa ajili ya mizigo ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo(DRC) na ile ya kutoka Tabora kupitia Shinyanga hadi Mwanza kwa ajili ya Ukanda wa ziwa.

Kwa upande wa Msemaji wa Kambi Rasmi  ya Upinzani Bungeni Mhe. James Mbatia akiwalisha maoni ya Kambi hiyo alisema kuwa reli ya kati ikiboreshwa itasaidia kutawala soko la usafirishaji wa abiria na mizigo ya ndani na nje ya nchi kama vile DRC, Burundi , Uganda na Rwanda.

Alisema kuwa hivi sasa watanzania wanatakiwa kuwa na reli ambayo itaendana na hali  ya sasa inayowezesha usafirishaji wa mizigo kwa kasi na uwezo mkubwa wa kubeba mzigo mzito.

Mhe. Mbatia alishauri kuwa ili kufupisha ujenzi wa reli hiyo ni vema kukawa na wakandarasi ambao watapewa vipande vidogo vidogo vya takribani kilometa 200 ambavyo vitajengwa kwa wakati.

Naye Waziri wa Ujenzi ,Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa alisema kuwa Serikali kupitia Kampuni Hodhi ya Rasilimali za Reli(RAHACO) inaendelea na uboreshaji wa miundo mbinu ya reli ili kuongeza uwezo wa njia zilizopo za reli ya kati za kubeba mizigo mizito zaidi.

Alisema kuwa mara baada ya kukakamilisha uboreshaji wa reli hiyo kutasaidia uhimilivu wa  mwendo kasi wa juu na kupunguza ajali za treni.

Wizara hiyo imeliomba Bunge kuidhinisha shilingi 4,895,279,317,500.00 kwa ajili ya utekelezaji wa majukumu mbalimbali katika mwaka wa fedha ujao.

Kati ya fedha hizo shilingi 2,212,141,496,500.00 ni kwa ajili ya sekta ya ujenzi, shilingi 2,587,333,762,000.00 ni kwa ajili ya sekta ya uchukuzi na shilingi 95, 804,059,000.00 ni kwa ajili ya sekta ya mawasiliano.

Tiketi Za Treni Kununuliwa Kwa Njia Ya Mfumo Wa Kielektroniki

$
0
0
Kampuni ya Reli Tanzania (TRL) inatarajia kuanza kutoa huduma ya uuzaji wa tiketi kwa abiria wanaotumia usafiri wa treni kwa mfumo wa kielektroniki lengo likiwa ni kuwawezesha wananchi kuweza kurahisha ununuaji wa tiketi hizo na kupunguza usumbufu.

Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhe. Profesa Makame Mbarawa wakati akijibu swali la nyongeza lililoihusu Wizara yake ambapo ametaja maeneo ambayo mfumo huo utaanza kufanya kazi ni pamoja na Mpanda mpaka Tabora, Kigoma mpaka Tabora.

Kwa upande wake Naibu Waziri wa Wizara hiyo, Mhe. Mhandisi Edwin Ngonyani akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum, Mhe. Sabreen Hamza lililotaka kujua kwanini TRL isianzishe mfumo wa uwakala wa tiketi ili kupunguza adha wanayoipata wakazi alisema kuwa kutokana na mahitaji makubwa ya usafiri wa treni katika Mikoa ya Kigoma, uuzaji wa tiketi katika Stesheni ya Reli Kigoma umekuwa na changamoto kubwa kutokana na ulanguzi wa tiketi.

Amefafanua kuwa, ili kudhibiti ulanguzi huo, Kampuni ya Reli Tanzania iliamua kubadilisha utaratibu kwa kuuza tiketi siku za safari na kwa kutumia vitambulisho jambo ambalo limesaidia kwa kiasi kikubwa kudhibiti ulanguzi wa tiketi hizo.

Ameongeza kuwa, utaratibu huo umekuwa na changamoto zake kwa kusababisha wasafiri kulala stesheni au kuwalazimu kuamka alfajiri ili kuwahi tiketi hizo.

"Ufumbuzi wa kudumu wa tatizo hili si kuanzisha mfumo wa uwakala ambao utaiongezea TRL gharama za uendeshaji, tatizo kubwa lililopo ni idadi ndogo ya safari za treni ambapo huduma inayotolewa hivi sasa haikidhi mahitaji halisi ya wananchi na hivyo kuwa na uhaba wa tiketi kwa abiria", alisema Mhe. Ngonyani.

Aliongeza kuwa ili kukabiliana na changamoto hiyo, Serikali inatarajia kuongeza idadi ya treni za abiria kwa njia ya Kigoma ili kukidhi mahitaji ya wananchi wa Mkoa huo.

Mkenya Auawa na Polisi Kwa Kipigo .....Walikuwa Katika Maandamano Kutaka Tume ya Uchaguzi Iundwe Upya

$
0
0
Kijana mfuasi wa muungano wa upinzani nchini Kenya(CORD), Ben Ngari aliyeshambuliwa kinyama na polisi jana amefariki dunia kwa sababu ya majeraha yaliyompata
 
Wafuasi wa CORD jana waliandamana kushinikiza kuundwa upya kwa Tume ya Uchaguzi (IEBC)

==> Tazama video ya Kipigo

Kesi ya aliyemtukana Rais Magufuli Facebook imeendelea leo Mahakamani

$
0
0

Kesi inayomkabili Isaac Abakuk ambaye anatuhumiwa kumtukana Rais John Magufuli kwenye ukurasa wake wa facebook imeendelea leo May 17 2016 kwenye Mahakama Kuu kanda ya Arusha ambapo ushahidi umekamilika na kesi itaanza kusiklizwa mfululizo kuanzia June 7 mwaka huu.

Hakimu mfawidhi wa mahakama hiyo Augustino Rwezire anayesikiliza kesi hiyo amesema upande wa mashtaka umekamilisha ushahidi wake na mtuhumiwa ataendelea na dhamana hadi kesi hiyo  itakapoanza kusikilizwa

Kitendo Cha Kuchapisha Ramani ya Tanzania Isiyo Rasmi Ni Kosa Kwa Mujibu Wa Mamlaka.....Hii ndo Ramani Sahihi ya Tanzania

$
0
0

WIZARA ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi imebaini kuwepo kwa ongezeko la matumizi ya ramani ya Tanzania ambayo mipaka yake imepotoshwa.

Upotoshwaji huu umefanywa kwenye “diary” (vitabu vya kumbukumbu na matukio), Kalenda, mabango, matangazo ya kwenye vyombo vya habari na sehemu nyinginezo. Jambo hilo la kupotosha mipaka ni hatari kwa usalama wa nchi.
 
Ili kuepusha upotoshaji wa mipaka ya nchi yetu tunashauri ramani sahihi zitumike.

Ramani sahihi ya Tanzania inatakiwa kuonesha mpaka kwa sehemu ya maziwa ya Victoria, Tanganyika na Nyasa ukipita katikati ya maziwa hayo. 

Hivi karibuni tumebaini matumizi ya ramani ya Tanzania  kwenye majarida, magazeti na hata Luninga inayopotosha mpaka kwa sehemu ya ziwa Nyasa ikionesha mpaka kupita pembezoni mwa ziwa.

Kitendo cha kuchapisha ramani yenye makosa kwa kutumia vyanzo visivyo rasmi ni kosa kwa mujibu wa mamlaka (Instrument) ya Mhe. Waziri aliyepewa dhamana ya kusimamia sekta ya ardhi ikiwemo masuala ya upimaji na ramani.

Idara ya Upimaji na Ramani ambayo ndiyo yenye mamlaka ya kuandaa, kuchapisha, kutunza na kusambaza ramani zote nchini ipo tayari kutoa ramani kwa matumizi yaliyokusudiwa ikiwa ni pamoja na kutoa elimu na ushauri kuhusu usahihi wa ramani kabla ya kuitumia.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumatano ya May 18

Polisi Akamatwa na Noti Bandia Zenye Thamani ya Sh. 870,000

$
0
0

ASKARI Polisi Ezekiel Dinoso (32) mkazi wa tarafa ya Mgeta, wilayani Mvomero mkoani Morogoro amekutwa na noti bandia za Sh 10,000 zenye thamani ya Sh 870,000, akijiandaa kuzitumbukiza katika akaunti ya mtandao wa Tigo Pesa katika duka mojawapo eneo la Mawenzi, Manispaa ya Morogoro.

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro, Ulrich Matei, alisema jana kuwa tukio hilo ni la Mei 14, mwaka huu saa 1:00 usiku katika eneo la Mawezi , Manispaa ya Morogoro.

Mtuhumiwa alikutwa katika duka la Hadija Hamis (35) mkazi wa Chamwino, wakati alipohitaji kuwekewa fedha hizo, mwenye duka alimtilia shaka hivyo kuarifu Polisi. 

Mtuhumiwa alipokamatwa na askari baada ya kutolewa taarifa Kituo cha Polisi, alikutwa akiwa na noti bandia 87 za Sh 10,000.

Alitaja namba za noti hizo ni BX 7287490 zikiwa noti 22 , BX 728792 zikiwa noti 20, BX 728791 noti 19 na BX7287487 zikiwa noti 15 na kufanya jumla ya thamani ya Sh 870,000 ambazo ni bandia.

Kamanda Matei alisema mtuhumiwa huyo anaendelea kuhojiwa na baada ya uchunguzi kukamilika atafikishwa mahakamani.

Katika tukio jingine, Rashidi Shabani (30) na Michael Lukasa (39), wote wakazi wa Ngerengere wanashikiliwa na Polisi kwa kuwakuta na nyama ya nyati kilo 300 na silaha aina ya gobole iliyotumika kumuulia mnyama huyo.

Kamanda wa Polisi wa Morogoro, Matei, alisema walikamatwa Mei 14, mwaka huu saa 2:00 usiku katika kijiji cha Kinonko, kata ya Gwata, wilaya ya Morogoro. 

Matei alisema, kukamatwa kwa watuhumiwa hao kumetokana na jitihada zinazofanywa na polisi kwa kushirikiana na wananchi katika kukomesha vitendo vya uhalifu.

Mtoto wa Chacha Wangwe Abadili Msimamo Mahakamani

$
0
0

Mtoto wa aliyekuwa mwanasiasa machachari na Mbunge wa Tarime, Chacha Wangwe, amebadili msimamo mahakamani katika kesi ya kuchapisha taarifa za uongo kupitia mtandao wa kijamii, kuwa Zanzibar inakandamizwa na Tanzania Bara na kwamba ni koloni lake.

Mtoto huyo, Bob Chacha Wangwe (24), ambaye ni mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, alibadili msimamo jana aliposomewa shtaka hilo kwa mara ya pili, katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.

Wangwe alipandishwa kizimbani kwa mara ya kwanza Mei 11, na alisomewa shtaka linalomkabili na alikiri kutenda kosa hilo.

Mshtakiwa anapokiri kosa, kwa kawaida Mahakama inaweza kumtia hatiani na kumpa adhabu kwa mujibu wa sheria, kulingana na kosa siku hiyo hiyo au siku nyingine yoyote.

Baada ya kusomewa shtaka na kukiri, Hakimu Mkazi Mkuu, Waria lwande Lema, aliamuru mshtakiwa huyo apelekwe rumande hadi jana, Mei 17, kwa kuwa hakimu aliyepangwa kusikiliza kesi hiyo hakuwapo.

Hata hivyo, jana mshtakiwa huyo alipopandishwa kizimbani na kusomewa shtaka hilo, ili kusomewa maelezo ya awali kabla ya Mahakama kumtia hatiani na kumhukumu, tofauti na siku ya kwanza, alikana kutenda kosa hilo.

Kutoka na mshtakiwa huyo kukana kosa, Wakili wa Serikali, Salim Msemo, aliieleza Mahakama kuwa upelelezi bado haujakamilika, hivyo aliiomba ipange tarehe nyingine ya kutajwa kwa kesi hiyo.

Wakili wa mshtakiwa huyo Peter Kibatala aliiomba Mahakama impe dhamana kwa kuwa shtaka linalomkabili linadhaminika, maombi ambayo yalikubaliwa na aliachiwa kwa dhamana na kesi iliahirishwa hadi Juni 15.

Wangwe ambaye baba yake kwa sasa ni marehemu, anadaiwa Machi 15, jijini Dar es Salaam, alisambaza taarifa za uongo kupitia mtandao wa kijamii wa Facebook.

Samia: Sijawahi Kupinga Utumbuaji Majipu, Lakini Nilishauri Wakuu wa Mikoa Wazingatie Sheria Kabla ya Kumfukuza Mtu

$
0
0
Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan amewataka wakuu wa mikoa na wilaya kuzingatia sheria na kanuni za utumishi wa umma wanapotaka kuwafukuza watumishi wasio waadilifu.

Alisema hajapinga kauli ya Rais John Magufuli ya kutumbua majipu kama alivyonukuliwa na baadhi ya vyombo vya habari, hivi karibuni kwenye Maadhimisho ya Siku ya Wauguzi Duniani.

Samia aliyasema hayo juzi wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Arusha, wakati akisisitiza zoezi la kuhamisha mifugo iliyopo ndani ya Mamlaka ya Hifadhi za Taifa (Tanapa).

Alisema wakuu wa mikoa na wilaya nchini, wanapaswa kuhakikisha wanapotaka kuwawajibisha watumishi wa umma wanafuata sheria, kanuni na taratibu za utumishi wa umma.

Aliongeza kuwa mwenye mamlaka ya kutumbua majipu ni Rais pekee, kwa sababu anateua, anaajiri na kufukuza kwa hiyo viongozi wengine wakiwamo wakuu wa mikoa na wa wilaya wafuate taratibu.

“Rais pekee ndiye mwenye mamlaka ya kuteua, kutengua na kuajiri lakini sijapinga utumbuaji majipu, bali nasisitiza kila mkuu wa mkoa na DC (mkuu wa wilaya) afuate sheria, kanuni na taratibu za utumishi wa umma,” alisema Samia.

Makamu wa Rais, aliwataka wakuu wa mikoa kuhakikisha mifugo ya nje ya nchi iliyopo hifadhini inaondolewa ifikapo Juni 30.

Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Martine Shigela alishukuru Tanapa kwa kuwapa msaada madawati ili kupunguza kero ya wanafunzi kukaa chini.

Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Dk Joel Bendera alisisitiza kuwa atahakikisha mkoa wake unapunguza migogoro ya ardhi ili hifadhi za Taifa ziweze kulindwa, huku wananchi wakiheshimu na kulinda mipaka ya hifadhi na rasilimali za Taifa.

Mganga mbaroni akidaiwa kugoma kumhudumia mjamzito

$
0
0

Polisi mkoani Mara inamshikilia mganga wa zahanati katika Kijiji cha Rwamchanga wilayani Serengeti kwa madai ya kushindwa kumhudumia mjamzito aliyejifungua pacha na kusababisha kifo cha mtoto mmoja.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mara, Ramadhan Ng’anzi alisema tukio hilo lilitokea Mei 15.

“Tunamshikilia kwa makosa matatu, likiwamo la uzembe, kufanya makusudi na kushindwa kuwajibika sawa na kiapo cha kazi yake, tunaendelea na mahojiano yatakapokamilika atafikishwa mahakamani,” alisema Ng’anzi.

Akisimulia chanzo cha mwanae kupoteza maisha, Shida Mugesi akiwa katika Hospitali ya Nyerere alisema alifika zahanati saa 12 asubuhi na kumuomba mganga amuhudumie, lakini alikataa.

“Nilikaa kwa muda wa saa mbili bila kupatiwa huduma, ghafla nilihisi uchungu wa kusukuma mtoto tukamuita mganga wa zamu ili anisaidie aligoma na kudai nimsubiri anakwenda kuoga na wakati huo alikuwa anazungumza kwa simu bila kuonyesha ushirikiano. Nilianza kujifungua mwenyewe,” alisema.

Muuguzi ambaye hakutaka jina lake litajwe alisema walipopima uzito wa watoto kwa mjamzito huyo walibaini kuwa aliyefariki alikuwa na kilo 2.5 na mwingine 2.3.

Muuguzi wa zahanati hiyo, Frida Kasonga alisema aliposikia taarifa ya kuwapo kwa mgonjwa huyo alilazimika kurudi kituoni kumsaidia lakini alikuta mtoto mmoja ameshafariki dunia.

“Haikuwa zamu yangu ila nililazimika kurudi baada ya kusikia mganga aliyekuwa zamu kagoma kuwasaidia,” alisema Frida.

Ofisa mtendaji kata, Fadhila Nyamburapi na Mwenyekiti wa kitogoji cha Kazi, Samwel Nyakande walilaani kitendo hicho na kutaka sheria ichukue mkondo wake.

Bavicha Walaani Hotuba ya Godbless Lema Kuzuiwa Bungeni........Wataka Waziri Kitwanga Ajiuzulu na Akigoma Awajibishwe

$
0
0

Wakati uchunguzi wa kampuni ya Lugumi inayodaiwa kushindwa kutekeleza mradi wa utambuzi wa vidole kwenye vituo vya polisi ukiendelea, Baraza la Vijana la Chadema (Bavicha) limemtaka Waziri wa Mambo ya Ndani ya nchi, Charles Kitwanga kujiuzulu wadhifa wake kupisha uchunguzi huo.

Limesema haiwezekani waziri anayetajwa kuhusika katika sakata hilo kuendelea na kazi huku Jeshi la Polisi linalodaiwa kutapeliwa na kampuni hiyo likiwa chini ya wizara yake.

Hata hivyo, waziri huyo amewajibu vijana hao wa upinzani kwa kusema hawezi kubishana na watoto na hayo waliyoyatoa ni mawazo yao binafsi wana haki ya kuyasema.

“Nimeshasema mara nyingi, siwezi kuzungumza tena kuhusu haya mambo. Wao kama wamesema waache waseme,” alisema.

Baraza hilo lililoibuka na hoja tatu jana, limesema kama waziri huyo atagoma kujiuzulu kupisha uchunguzi unaofanywa na kamati ndogo ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), Rais John Magufuli anapaswa kumwajibisha ingawa suala hilo ni gumu kutokana na uswahiba uliopo kati ya kiongozi huyo mkuu wa nchi na Kitwanga.

Kampuni ya Lugumi ilibainika kutotimiza matakwa ya mkataba wake baada ya kufunga mashine 14 tu kati ya 108 zilizotakiwa kufungwa, licha ya kulipwa zaidi ya asilimia 90 ya fedha kwa mujibu wa mkataba ambazo ni Sh37 bilioni.

Ripoti ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) ya mwaka 2013/14 ndiyo iliyofichua udhaifu huo na baadaye Bunge kuanza uchunguzi baada ya kutoridhishwa na maelezo ya Wizara ya Mambo ya Ndani na polisi kuhusu mkataba huo.

Kitwanga anahusishwa na Lugumi kupitia kampuni ya Infosys anayodaiwa kuwa ni mmoja wa wanahisa. Infosys ambayo imekanusha kuhusika katika sakata hilo, imedaiwa kuwa iliisaidia kampuni ya Lugumi kupata vifaa kutoka kampuni ya Dell ya Marekani ili viweze kufungwa kwenye vituo vya polisi.

Akizungumza na waandishi wa habari, Katibu Mkuu wa Bavicha, Julius Mwita alisema: “Hotuba ya upinzani inaeleza kuwa Lugumi inamilikiwa na Kitwanga na ana ubia hilo siyo siri. Kilichoelezwa kama kingesomwa bungeni kingemfanya apoteze uhalali wa kuwa waziri na tunajua Magufuli hawezi kumfanya chochote maana ni maswahiba.

“Hotuba ile pia ilimtaja Rais ila cha ajabu upinzani wakaambiwa wafute maneno ‘rais’. Rais Magufuli ameshindwa kuitumbua Lugumi na kwa kilichotokea bungeni suala hilo haliguswi.”

Alisema Rais anapaswa kujibu hoja zilizotolewa na wapinzani kuhusu Lugumi na kubainisha kuwa kamati ndogo iliyoundwa kuchunguza kampuni hiyo haiwezi kutenda haki wakati Kitwanga akiendelea kuwa waziri.

Katibu mwenezi wa baraza hilo, Edward Sembeye alisema: “Katika ripoti ya CAG ameeleza juu ya ununuzi wa ile feri kuwa ni mbovu na haifanyi kazi hivi hili siyo jipu?

Kuhusu suala la Jaji Mkuu, Mwita alisema kitendo cha kuisifia Sheria ya Mtandao alipokuwa London, Uingereza hivi karibuni si kizuri kwa maelezo kuwa kazi ya majaji ni kutafsiri misingi ya kikatiba: “Tunamtaka afute kauli hii na aseme sheria hiyo imetungwa itumike lakini uzuri na ubaya wake hapaswi kuusema maana ni kama anatoa hukumu kabla watuhumiwa hawajafikishwa mahakamani.”

Upinzani Wamtega Rais Magufuli....Watumia Njia Mbadala Bungeni Kukumbushia Uuzwaji wa Nyumba za Serikali, Wadai MV Dar es Salaam Ni Jipu Lililoiva

$
0
0
Kambi ya Upinzani imelizidi maarifa  Bunge na kurejesha sakata la kuuzwa nyumba za Serikali ambalo juzi lilisababisha kiti cha Spika kuagiza yaondolewe maneno yanayomtaja Rais katika hotuba ya maoni mbadala.

Juzi, Kamati ya Kanuni za Bunge ilihariri hotuba ya msemaji wa kambi ya upinzani wa Wizara ya Mambo ya Ndani, ikiondoa maneno yanayomtaja Rais John Magufuli na badala yake kuweka neno Serikali kwenye sakata la uuzwaji nyumba za Serikali.

Kamati hiyo pia iliondoa suala la mkataba wa Jeshi la Polisi na kampuni ya Lugumi Enterprises, rushwa, mauaji ya wanasiasa, mwenendo wa Rais na Bunge kulinda wahalifu, jambo lililomfanya msemaji wa kambi hiyo, Godbless Lema kukataa kusoma hotuba yake.

Lakini jana katika hotuba ya kambi ya upinzani kwa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, mbunge wa Vunjo, James Mbatia alilirejesha sakata hilo akieleza kuwa ni muda sahihi kwa Rais John Magufuli kurekebisha kasoro zilizojitokeza wakati akiwa waziri ili kurejesha imani katika jamii.

Mbali na sakata hilo, pia Mbatia alizungumzia sakata la kivuko cha Mv Dar es Salaam ambacho kinatakiwa kifanye safari kati ya Dar es Salaam na Bagamoyo, akikielezea kuwa “ni jipu ambalo limeiva kwa viwango vyote na sasa linatakiwa litumbuliwe mara moja”.

Suala la Mv Dar es Salaam liliungwa mkono na Mbunge wa Kigoma Mjini (ACT-Wazalendo), Zitto Kabwe wakati akichangia hotuba ya bajeti ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano.

Zitto alisema kuwa hoja ya kivuko hicho lazima ichukuliwe hatua ili iaminike kuwa kuna nia ya dhati ya kupambana na ufisadi nchini.

“Naona suala hili linakwepwakwepwa, hivyo litolewe maamuzi,” alisema Zitto.

Pia mbunge wa Rombo (Chadema), Joseph Selasini alisema suala la Mv Dar es Salaam kuwa iko chini ya kiwango, liliwahi kusemwa na mbunge wa upinzani lakini Serikali ikakataa.

Hata hivyo, Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Serikali (CAG) amesema ukweli katika ripoti yake. “Hili suala inabidi liangaliwe kwa kuwa kuna watu wanahitaji kutumbuliwa hivyo hao watu waangaliwe,” alisema Selasini.

Akisoma hotuba ya maoni mbadala ya kambi ya upinzani, Mbatia alisema wakala wa majengo nchini ndiye muhusika mkuu katika kuhakikisha nyumba za Serikali zinakuwa katika hali nzuri kwa watumishi wa Serikali kuishi.

“Katika muktadha huo, kambi ya upinzania inalikumbusha Bunge kwamba kati ya mwaka 2002 mpaka 2004 Serikali iliuza nyumba 7,921 na mpaka mwaka 2008 ilikuwa imejenga nyumba 650 tu,” alisema Mbatia.

Alisema katika biashara hiyo ya kuuza nyumba zilizokuwa mali ya Tamisemi, Serikali ilipata Sh252 milioni lakini sasa inahitaji kusaka zaidi ya mara mbili ya kiasi hicho kujenga nyumba za fidia.

Mbatia alisema Serikali ingetumia Sh677.6 milioni kujenga nyumba mpya ili zirejeshwe Tamisemi.

“Kwa vile hata wale waliouziwa nyumba hizo, kuna taarifa kati yao wapo walioziuza na kujipatia faida kubwa kinyume na mikataba ya mauzo hayo, kambi ya upinzani inapendekeza wanyang’anywe nyumba hizo kwa kukiuka mikataba na malengo ya mauzo.”

Mbatia alisema kumbukumbu rasmi za Bunge zinaonyesha Serikali ilitoa taarifa kuwa kamati iliundwa kuchunguza mchakato wa mauzo ya nyumba hizo na ilitarajiwa kumaliza kazi Februari 2007, lakini hadi leo hakuna taarifa iliyotolewa na Serikali na kuitaka Serikali ya Awamu ya Tano izirejeshe.

Akinukuu kumbukumbu rasmi za Bunge za Aprili 25, 2008 wakati wa kikao cha 18 cha Mkutano wa 11, Mbatia alisema baada ya mjadala mkubwa wa hoja binafsi iliyowasilishwa na mbunge wa Vunjo, Aloyce Kimaro, Bunge kwa kauli moja lilipitisha azimio kuwa nyumba hizo zirejeshwe serikalini.

“Bunge linaazimia kwamba Serikali ifanye yafuatayo: Itekeleze mara moja bila kusita, agizo la Rais kurejesha nyumba zilizouzwa kinyume cha utaratibu na kwa watu ambao hawakuwa watumishi wa Serikali wakati huo na vilevile nyumba ambazo hazikupaswa kuuzwa kama zile zilizopo kwenye maeneo ya utawala wa Serikali,” alisema akinukuu azimio hilo.

Mbatia aliitaka Serikali itafsiri kaulimbiu ya “hapa kazi tu” kwa kuelekeza azimio hilo, akisema Kikwete alikosa uthubutu wa kusimamia msimamo wake.

“Tunajua uuzwaji huo ulisimamiwa na wizara aliyokuwa akiiongoza yeye (Rais Magufuli) na kuna uwezekano mkubwa kwamba alisimamia maamuzi ambayo hakuwa na uwezo wa kuyakiuka,” alisema Mbatia.

“Sasa ni muda sahihi Rais Magufuli kurekebisha kasoro alizozisimamia katika mchakato huo ili kurejesha imani katika jamii.”

Kivuko cha Bagamoyo
Kuhusu kivuko cha Bagamoyo, Mbatia alisema kilinunuliwa na Temesa chini ya uongozi wa Waziri wa Ujenzi wa Serikali ya Awamu ya Nne ambaye ndiye Rais wa sasa.

Mbatia alisema kwa mujibu wa ripoti ya CAG katika hesabu za Serikali Kuu za mwaka ulioishia Juni 30, 2015 iliyotolewa Machi 2016, alibaini ununuzi wa boti ‘feki’ na mbovu uliofanywa na Temesa na kugharimu dola 4,980,000 za Marekani (sawa na Sh7.9 bilioni).

Alisema CAG alibaini masuala makuu mawili ambayo ni kasi ya kivuko hicho ni tofauti na kasi iliyotakiwa kuwapo na pia cheti cha kukikubali kivuko hicho kilikuwa kinyume na Kanuni ya 247 ya Sheria ya Manunuzi ya Umma.

“Tabibu wa kutumbua jipu hili yuko wapi? Au msemo usemao kuwa ‘mganga hajigangi’ unatumika hapa?” alihoji.

Juzi jioni hali kama hiyo ya kuzungumza masuala yaliyozuiwa na Kamati ya Kanuni za Bunge, ilijitokeza wakati wabunge wakijadili Hotuba ya Makadirio na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Ndani.

Akichangia mjadala huo, Lema alianza tena kuzungumzia suala la Lugumi, akisema kabla ya kuandika hotuba hiyo alikaa pamoja na Waziri Charles Kitwanga wakila ugali nyumbani kwake na kumtaka amwambie ni mambo gani ayajumuishe kwenye hotuba yake ambayo yangeisaidia nchi.

“Haya mambo ambayo mimi nimeyaandika, nimeyajadili nyumbani kwake tukiwa tunakula ugali. Na nakwambia mimi ni mara ya pili kuingia bungeni. Ninazijua siasa za Bunge.

"Ninakuomba mheshimiwa uniambie mimi kama kambi ya upinzani ninaweza kuzungumza mambo gani ambayo Serikali haiwezi kuja nayo direct. Usiponiambia mimi nitakunyookea na nitataka majibu.

“Waheshimiwa wabunge, nimeuliza swali ambalo nimeambiwa na kamati niliondoe, kwamba hivi kamati ya Bunge inapotembelea kote huko kutafuta sakata hili la Lugumi, CAG anashindwa kutwambiwa kama mkataba ule ulikuwa thamani yake ya fedha na vifaa ni OK au ni no, anashindwa kujua?” alihoji Lema huku akishangiliwa.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images