Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Waliotapeli Bilioni 62 Uingereza Waanza Kusakwa Jijini Dar es Salaam

$
0
0
Shirika la Kimataifa la Polisi linawasaka raia wawili wa Scotland wanaodaiwa kukimbilia Tanzania baada ya kufanya udanganyifu na kujipatia Paundi 20 milioni za Uingereza (sawa na Sh62 bilioni). 

Wawili hao, Gareth Johnson (48) na Geoffrey Johnson (72) walikuwa sehemu ya kundi la watu 18, lililohusishwa na uhalifu huo wa uchakachuaji ongezeko la kodi ya simu za mkononi nchini Uingereza.

Kutokana na kosa hilo, Mahakama Maalumu ya Mapato na Forodha ya Uingereza (HMRC) iliamuru wanafamilia hao, ambao ni baba na mwanae, walipe fidia ya Paundi 109 milioni (sawa na Sh337 bilioni).

Lakini hukumu hiyo ilitoka bila ya wawili hao kuwapo baada ya kutoroka kabla ya shauri hilo kuanza kusikilizwa na inasemekana walikimbilia Tanzania.

Akizumgumzia suala hilo, Mkuu wa Interpol Tanzania, Gustavus Babile alisema kibali cha kimataifa cha kukamatwa kwa wawili hao kipo kwenye tovuti yao.

Alisema walipokea taarifa kutoka Uingereza hivyo hatua inayofuata ni kukipeleka kibali hicho mahakamani kwa ajili kupata nguvu za kisheria za nchi.

Balile alisema baada ya hatua hiyo, utafanyika uchunguzi ili kubaini kama watuhumiwa hao wapo nchini. “Kama wapo watakamatwa,” alisema.

Picha na majina ya raia hao wa Scotland zimebandikwa kwenye tovuti ya Interpol kwa kuwekewa bendera nyekundu, ikiwa ni alama ya kusakwa na polisi hao wa kimataifa.

Awali, alipoulizwa kuhusu hilo, msemaji wa Jeshi la Polisi, Advera Bulimba alisema litashughulikiwa baada ya Uingereza kutoa taarifa ya watuhumiwa hao.

Hadi sasa inadaiwa kuwa Geoffrey na kijana wake wamekuwa “mafichoni” Tanzania kwa takriban miaka mitatu sasa. 

Mapema Aprili mwaka huu, Gazeti The Mirror la Uingereza liliripoti kuwa wawili hao, ambao wametakiwa kulipa fedha hizo mara moja au waongezewe adhabu ya kifungo cha miaka 14 jela, wamebainika kuwapo nchini.

Kwa mujibu wa gazeti hilo, uchunguzi wa awali ulibaini kuwa makazi yao mara baada ya kufika nchini yalikuwa jijini Dar es Salaam.

Hata hivyo, wakati uchuguzi huo ukibaini hilo, mienendo yao inaonyesha kuwa kwa sasa wapo mkoani Iringa.

Inadaiwa kuwa Geoffrey, ambaye Mahakama iliamuru afungwe jela miaka 10 katika hukumu ya mwaka 2014, ni wamiliki wa kampuni ya Johnson International Group ambayo makazi yake ni Kipawa jijini Dar.

Kampuni ya Johnson, ambayo inasimamiwa na kijana wake ambaye pia alihukumiwa kifungo cha miaka 10 jela, imeajiri wafanyakazi 125.

Lakini, taarifa ya gazeti hilo kwenye mtandao wake, inaeleza kuwa kampuni hiyo haina uhusiano mzuri na wafanyakazi wake kwa sababu haijawalipa mshahara kwa muda mrefu. 

Kutokana na mvutano uliokuwapo kati wa wafanyakazi hao na waajiri wao, wafanyakazi 40 walipeleka madai yao kwa mkuu wa mkoa mwaka 2014.

Pia, wafanyakazi hao walidai kunyanyaswa hasa pale walipoomba kuongezwa mshahara huku mwajiri wao akiwatishia kuondoa michango yao ya pensheni.

Mmoja wa wasimamizi wa kampuni ya Johnson, Leonard Lukule alisema hali hiyo imesababishwa na hali mbaya ya kiuchumi ndani ya kampuni.

“…Kuna wakati tulilazimika kutoa likizo za lazima kwa wafanyakazi,” alisema Lukule.

UVCCM Wafikishana Polisi

$
0
0
Sakata la uuzwaji kinyemela wa zaidi ya hekari 200 za shamba la Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM), Mkoa wa Iringa limechukua sura mpya baada ya aliyekuwa katibu wa mkoa huo, Ally Nyawenga kukamatwa na polisi.

Shamba hilo lililopo eneo la Igumbiro, nje kidogo ya mji wa Iringa, linadaiwa kuuzwa mwaka jana kwa zaidi ya Sh800 milioni baada ya baadhi ya viongozi kubadili matumizi yake na kuwa viwanja.

Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa, John Kauga alisema jana kuwa kiongozi huyo alikamatwa Morogoro siku chache zilizopita.

“Tulituma askari wetu na leo hii wanamleta. Taarifa za kumkamata ni hizo za uuzwaji wa shamba hilo kwa hivyo tutafanya naye mahojiano zaidi, lakini kwa sasa sina taarifa zaidi ya hapo labda tuwasiliane kesho (leo),” alisema.

Nyawenga alisimamishwa kazi mwishoni mwa mwaka  jana, akituhumiwa kusimamia uuzwaji wa shamba hilo kinyume cha utaratibu wa jumuiya hiyo. 

Mali zote za jumuiya hiyo zipo chini ya Baraza la Wadhamini, linaloongozwa na Mwenyekiti, Dk Emmanuel Nchimbi.

UVCCM ilianza kumiliki shamba hilo miaka ya 1970 likitumika kwa ajili ya kilimo kwa kukodisha vijana kwa bei nafuu ili kuwasaidia kujiendeleza kiuchumi.

Ally Simba aliyedaiwa kuwa msimamizi wa shamba hilo alikana nafasi hiyo huku akisema hakuhusishwa katika mipango hiyo.

“Sikuwa msimamizi, bali mjumbe tu wa kamati ya utekelezaji, msimamizi alikuwa Katibu wa UVCCM,” alisema Simba ambaye kwa sasa ni Katibu wa UVCCM Wilaya ya Mbinga.

Alisema kabla ya kuondoka Iringa mwaka 2014, hakuwahi kusikia vikao wala mipango ya uuzaji wa shamba hilo na kwamba hahusiki.

Akizungumzia kukamatwa kwa Nyawenga, Katibu wa UVCCM Mkoa wa Iringa, Abdulkarim Halamga alisema: “Kwa sababu ni mali ya vijana na katibu aliyekuwapo anahusika, hivyo kwa kushirikiana na polisi, tumemkamata baada ya waliouziwa viwanja kuanza kutudai huku vijana wakipinga kuuzwa kwa eneo lao. Kwa sababu hakuwa peke yake, taratibu nyingine zitafuatwa akishafikishwa Iringa.”

Mjumbe wa kamati ya utekelezaji ya UVCCM mkoani hapo, Thom Muyinga alisema kuuzwa kwa shamba hilo kumesababisha mpasuko ndani ya umoja huo.“Vijana wanataka mali yao, haiwezekani mali hiyo iuzwe kinyemela na kunufaisha kundi la watu wachache,” alisema.

Mmoja wa vijana hao, Katula Kalinga alisema japo tayari tume ya UVCCM ya kuchunguza mgogoro huo ilishakwenda Iringa, hakuna kinachoendelea.

Alimuomba Rais John Magufuli kufuta hati za viwanja hivyo ili shamba hilo, lirejeshwe kwa UVCCM.

Pia, walimuomba Mwenyekiti wa CCM, Jakaya Kikwete kutumbua majipu yanayokitafuna chama kwenye mkoa huo, ili vijana waendelee kunufaika na mali yao.

Walitaka kamati ya utekelezaji jumuiya hiyo Mkoa wa Iringa isimamishwe wakati uchunguzi ukiendelea.

12 Wakamatwa Wakituhumiwa Kuhusika na Mauaji ya Watu 7 Jijini Mwanza

$
0
0
Siku chache baada ya watu saba wa familia moja kuuawa kwa mapanga wilayani Sengerema mkoani Mwanza, polisi wamefanikiwa kuwatia mbaroni watu 12 kwa tuhuma za mauaji hayo huku mmojawapo akikamatwa kwa mganga wa kienyeji alikokuwa akijitibu.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Ahmed Msangi alisema hadi jana upelelezi wa tukio hilo lililozua hofu kwa wakazi wa Kijiji cha Sima unaendelea na tayari watuhumiwa 12 wamekamatwa.

“Hakuna jiwe litakalobaki bila kugeuzwa katika upelelezi wa jambo hili, tutawasaka na kuwakamata wote waliohusika kwa njia moja au nyingine na mauaji haya ya kinyama,” alisema Msangi.

Habari zilizopatikana kutoka kwa mtu wa karibu na familia ya marehemu Zakaria Mbata iliyopoteza mama na watoto watatu katika tukio hilo, zinaeleza kuwa wauaji walilenga kupora fedha zilizohifadhiwa kwenye mtandao wa simu.

Pia, chanzo kimoja cha habari kilisema kuwa polisi walimkamata mmoja wa watuhumiwa hao akiwa kwa mganga wa kienyeji alikokuwa akijitibu jeraha alilopata siku ya tukio.

“Katika purukushani za mauaji hayo, huyo mhalifu alijeruhiwa usoni, inaonekana alipigwa na kitu kizito, akakutwa kwa mganga wa kienyeji na amekamatwa kwa mahojiano,” kilisema chanzo hicho
 
Tukio Lenyewe
Usiku wa kuamkia Mei 11, watu wasiojulikana walivamia familia ya Zakaria Mbata na kuua watu saba kwa kuwakata mapanga sehemu mbalimbali za mwili.

Waliouawa katika tukio hilo ni mama wa familia hiyo, Augenia Philipo (62), mdogo wake Maria Philipo (56) na watoto wake; Yohana Mabula (20), Regina Aloyce (12) na Mkiwa Philipo (13).

Wageni wawili wa familia hiyo, waliojulikana kwa jina mojamoja ya Donald na Samson nao pia waliuawa katika tukio hilo.

Kiwanda Cha Bia Serengeti Breweries Limited (SBL) Chapigwa Faini

$
0
0
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira na Muungano), Luhaga Mpina amekiamuru Kiwanda cha Serengeti Breweries Limited (SBL), kulipa faini ya Sh16 milioni kwa kosa la kutiririsha maji yasiyo salama kwenye makazi ya watu.

Uamuzi huo ulichukuliwa mwishoni mwa wiki iliyopita mbele ya baadhi ya viongozi wa SBL kilichopo Chang’ombe Manispaa ya Temeke na Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (Nemc), baada ya kujiridhisha kuwa kilikiuka taratibu za utunzaji mazingira na kutotekeleza amri halali kwa zaidi ya miaka miwili.

Mpina aliigiza kiwanda hicho, kulipa faini ndani ya siku saba na kwamba asieleweke vibaya kuhusu uamuzi huo, bali anasimamia sheria.

“Nasimamia sheria wala sina nia mbaya na kiwanda chenu, naomba nieleweke hivyo na faini hii mlipe kwa wakati,” alisema Mpina.

Mkurugenzi Mkuu wa Nemc, Bonaventure Baya alisema baraza hilo limejijengea utaratibu wa mara kwa mara kufuatilia kanuni za afya za kiwanda hicho hasa majitaka yanayotiririka kuelekea kwenye makazi ya watu.

Meneja Mhandisi Biashara wa SBL, Peter Mkongwa alikanusha tuhuma hizo na kwamba, maji hutibiwa kwa dawa kabla ya kutiririshwa katika makazi ya watu. Alisema: “Tunasubiri mashine maalumu ya kuvuta maji hayo ili yaingie katika bomba.”

Tanesco Mkoa Wa Pwani Yamakamata Mmiliki Wa Yadi Ya Magari Kwa Wizi Wa Umeme

$
0
0

Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) Mkoa wa Pwani limemkamata mmoja wa wamiliki wa eneo la maegesho ya magari la White Star, Munira Mbowe akidaiwa kujiunganishia umeme kinyume cha sheria.

Mbowe ambaye ni mmiliki wa eneo hilo lililopo Kiluvya kwa Komba nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam, alikamatwa jana baada ya kufanyika msako wa kushtukiza kwa watu wanaodaiwa kujiunganishia umeme kinyume cha sheria.

Inadaiwa kuwa Mbowe amelisababishia shirika hilo hasara ya Sh50 milioni.

Akizungumza kwenye eneo hilo, Ofisa Usalama wa Tanesco Mkoa wa Pwani, Henry Byarugaba alidai kuwa baada ya kufanya ukaguzi waligundua umeme uliokuwa ukitumika katika eneo hilo haukuunganishwa na Tanesco.

“Tumekuwa tukibuni mbinu mpya kila kukicha ya kuwatia mbaroni wateja wetu wanaotuhujumu na leo (jana), tumembana huyu anayedaiwa ni mmiliki wa yard hii ya White Star baada ya kukuta anatumia umeme wa wizi uliounganishwa katika njia tatu,” alidai Byarugaba.

Alisema tayari wameshamfikisha Kituo cha Polisi Kibaha na hatua zingine za kisheria zinaendelea kuchukuliwa.

Hata hivyo, alidai kuwa hiyo siyo mara ya kwanza kwa Mbowe kukamatwa kwa kosa hilo. Alidai mwaka jana Tanesco ilipofanya msako, ilimkamata akiwa amejiunganishia umeme na alichukuliwa hatua za kisheria.

Alipoulizwa  kama tuhuma hizo zina ukweli, Mbowe alijitetea kuwa hajui ni nani aliyemuunganishia njia hizo tatu za umeme kwa sababu mara nyingi hufanya shughuli zake jijini Dar es Salaam, mara chache hufika kwenye yard hiyo kufanya kazi zingine ambazo ni chache.

“Ni kweli tumekutwa na kosa la kuiba umeme, lakini jamani nataka niwaeleze kuwa mimi sihusiki na kingine, nawaomba msinitoe kwenye vyombo vya habari, haya ni maisha tu, sio vizuri kunitoa jamani mimi sihusiki kabisa katika wizi huu,” alijitetea Mbowe.

Kaimu Meneja wa Taneso Mkoa wa Pwani, Selemani Mgwila alisema kitendo alichokifanya mteja wao huyo ni kosa kwani umeme waliokuwa wanautumia umesababisha upotevu wa mapato makubwa ya shirika.

“Tunalalamika kila siku mpaka shirika linaonekana halifanyi kazi kwa sababu ya hawa watu wachache, safari hii lazima sheria ichukue mkondo wake,” alisema.

Auawa Kwa Kuchomwa Visu Akituhumiwa Kutoka Kimapenzi na Mtalaka Wake

$
0
0

Mkazi wa Kijiji cha Chala B, Tarafa ya Chala wilayani Nkasi, Mkoa wa Rukwa, Moses Nambasita (48) ameuawa kwa kuchomwa visu kutokana na kinachodaiwa kuwa ni wivu wa mapenzi.

Akisimulia mkasa huo mwishoni mwa wiki iliyopita, Mwenyekiti wa Kitongoji hicho, Vincent Mwanambuu alisema tukio hilo lilitokea juzi saa 10 jioni baada ya kuvamiwa na kijana mmoja alipokuwa akitoka nyumbani kwake kwenda nyumba jirani, alishambuliwa kwa kuchomwa visu.

Mwanambuu alisema baada ya kupata taarifa hizo alitoa taarifa Kituo kidogo cha Polisi Chala, askari walifika na kuchukua mwili kwa ajili ya uchunguzi na kuanza msako dhidi ya mtuhumiwa.

Akielezea chanzo cha mauaji hayo, Mwanambuu alisema mtuhumiwa alipata taarifa kuwa Nambasita ana uhusiano na mtalaka wake, ambaye walikuwa wameachana kipindi kirefu.

Alidai kuwa kutokana na taarifa hizo, mtuhumiwa alipeleka shauri la ugoni katika Mahakama ya Mwanzo Chala.

“Lakini kabla hata shauri hilo halijamalizika, tunashangaa kuona mtuhumiwa ameamua kujichukulia sheria mikononi, baada ya kutekeleza unyama huo alikimbia na kutokomea kusikojulikana,” alisema.

Mtendaji wa Kijiji cha Chala, Godfrey Mwanakatwe alisema kutokana na mazingira hayo polisi wanawashikilia watu wanne kwa kosa la kushiriki mauaji hayo.

Hatua hiyo inatokana na baada ya wao kutoa taarifa kwa muuaji kuwa Nambasita ana uhusiano wa kimapenzi na mtalaka wake, ambaye mpaka sasa haijulikani alipo.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Rukwa, Jacob Mwaruanda alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kwamba, baada ya uchunguzi wa polisi ndugu wa marehemu waliruhusiwa kuuzika mwili huo.

Mwaruanda alisema chanzo cha kifo hicho ni wivu wa mapenzi na kuongeza kuwa mtuhumiwa alianza vizuri kwa kufuata sheria, lakini haijulikani kilichosababisha kuchukua uamuzi huo wa kinyama.

Alisema wanawashikilia watu watatu wakituhumiwa kushiriki mauaji hayo, kwa kutoa taarifa kwa mtuhumiwa kwamba Nambasita alikuwa na uhusiano na mtalaka wake.

Kamanda Mwaruanda aliwataka wananchi kuacha kujichukulia sheria mikononi, hivyo wafuate taratibu kupata haki zao.

Mbarawa ‘Kuvaa Viatu’ vya Magufuli Kesho Bungeni

$
0
0
Waziri  wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa wiki hii anatarajiwa kuanza kuvaa viatu vya Rais John Magufuli bungeni.

Kesho Profesa Mbarawa anatarajiwa kuwasilisha Makadirio ya Mapato na Matumizi ya wizara yake kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Mbunge huyo wa kuteuliwa atakuwa na jukumu kubwa la kuwasilisha bajeti hiyo ambayo kwa takriban miaka 10 ilikuwa jukumu la Dk Magufuli.

Magufuli alikuwa Waziri wa Ujenzi kwa miaka mingi kabla ya kujitosa kuwania urais kupitia CCM ambako aliteuliwa na kushinda Uchaguzi Mkuu, Oktoba mwaka jana.

Sekta tatu alizopewa Profesa Mbarawa ni nyeti na ngumu, hivyo Watanzania wanasubiri kuona atakavyoanza bajeti yake ya kwanza kesho tangu kuteuliwa na Dk Magufuli kushika nafasi hiyo.

Ujenzi bado ni sekta inayotegemewa na Taifa katika kuingiza mapato na pia kusaidia huduma za jamii. Masuala ya ujenzi wa barabara, madaraja, mawasiliano na uchukuzi vyote ni muhimu kwa uchumi. Hayo yanatiwa nguvu na jitihada za Rais Magufuli za kukusanya mapato tangu aingie madarakani.

Suala la bandari ni eneo mojawapo litakalogusa bajeti ya Profesa Mbarawa. Kuliibuka masuala mengi ya ufisadi katika bandari ya Dar es Salaam, mambo yanayotegemewa kuligusa Bunge.

Mbali ya hayo, masuala ya mawasiliano yatakuwa pia na nafasi katika bajeti ya Profesa Mbarawa. 

Atiwa Mbaroni Kwa Kudandia Helkopta

$
0
0

Polisi wa Kenya wanamshikilia mtu mmoja mjini Bungoma baada ya kuning’inia kwenye helikopta iliyoubeba mwili wa aliyekuwa mfanyabiashara Jacob Juma.

Mtu huyo, Saleh Wanjala ambaye hakutoa sababu za kufanya hivyo, alishikiliwa na polisi huku akipata matibabu kwenye Hospitali ya Rufaa Bungoma.

Wanjala alionekana akining’inia kwenye helikopta iliyobeba mwili wa mfanyabiashara huyo wakati ikipaa kutoka kwenye Uwanja wa Posta mjini Bungoma baada ya wananchi kutoa heshima za mwisho.

Wanjala aliamua kuidandia helikopta hiyo wakati ikiondoka kupeleka mwili wa Juma nyumbani kwake katika Kijiji cha Mungore.

Akisimulia mkasa huo, Wanjala alisema alikuwa karibu na helikopta hiyo wakati ikianza kupaa na kwamba aliumia baada ya mguu wake kukwama.

“Nilikuwa nimeketi chini ya helikopta na wakati ilipokuwa inaanza kupaa, mguu wangu ulikwama hapo ikabidi nijishikilie vizuri ili nisianguke,” alisema Wanjala.

Rubani wa helikopta hiyo alilazimika kumpeleka hadi uwanja wa ndege wa Bungoma mita 700 kutoka kwenye uwanja huo lakini Wanjala aliamua kuruka na kuumia vibaya miguu na mikono. Muuguzi wa Hospitali ya Bungoma, Leah Atsewa alisema bado wanamfanyia uchunguzi. 

Maalim Seif Awasha Moto Upya Zanzibar.....Awataka Wananchi Wasilipe Kodi na Waandae Siku ya Mgomo

$
0
0
Katibu  Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Maalim Seif Sharif Hamad, amewasha moto upya visiwani Zanzibar kwa kuwahimiza wananchi kufanya vitendo vinavyoonyesha kuikataa serikali inyoongozwa na Rais wa Zanzibar Dr. Ali Mohamed Shein

Maalim aliyasema hayo jana alipokuwa akizungumza na watendaji na viongozi wa CUF kutoka Wilaya ya Micheweni katika Mkoa wa Kaskazini Pemba ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya siku tano hapa.
 
‘Tukikazana, serikali hii itaondoka, ikiwa mnangoja Maalim Seif au Marekani kuiondoa, kwa sheria ya kimataifa haitawezekana kwani Marekani haiwezi kuingilia mambo ya ndani ya Zanzibar,” aliongeza Maalim Seif, ambaye alijitoa kwenye uchaguzi wa marudio wa Zanzibar uliofanyika Machi 20, mwaka huu na Dk Ali Mohamed Shein kuibuka mshindi.
 
Uchaguzi wa marudio wa Zanzibar ulifanyika baada ya Tume ya Uchaguzi ya huko kufuta matokeo ya uchaguzi uliofanyika Oktoba 25, mwaka jana.
 
Hata hivyo, Maalim Seif alisema Serikali ya CCM imeanza kutikisika kutokana na vikwazo vinavyoendelea kuwekwa na wahisani pamoja na hatua ya chama chake CUF kutowatambua viongozi wake pamoja na serikali.
 
“CCM wajue wamekalia kuti kavu, siku yoyote wataanguka...tufanye kazi mpaka haki yetu tuhakikishe imerudi na wenzetu hawana safari ya kudumu,” alisema Maalim Seif.
 
Aidha, aliwataka wanachama wa CUF kutumia mshikamano wao wa kuhakikisha wanafanikisha mpango wa kutoitambua Serikali ya CCM badala ya kuendelea kumsubiri yeye (Maalim Seif) au Marekani kuleta mabadiliko ya kiutawala visiwani humu.
 
Hata hivyo, Maalim Seif ameendelea kumshtumu Rais mstaafu Jakaya Kikwete, kwamba ndiye chimbuko la kufutwa matokeo ya Uchaguzi Mkuu wa Zanzibar.
 
"Baada ya Kikwete kupokea taarifa za CCM kushindwa Zanzibar, ndipo mipango ya kuvuruga matokeo ilipoanza kutekelezwa kwa kushirikiana na vyombo vya ulinzi na usalama," alidai.
 
Maalim Seif ambaye ni Makamu wa Kwanza wa Rais mstaafu wa Zanzibar, alisema Kikwete alichukua hatua za kumtaka Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) kusitisha mara moja kazi ya kutangaza matokeo ya uchaguzi huo.
 
Alisema wakati wajumbe wa ZEC wanaendelea kumsubiri ukumbini Mwenyekiti Jecha Salim Jecha, kuendelea kutangaza, alitoweka na baadaye kuibuka kutangaza kufuta matokeo ya uchaguzi wa Oktoba, mwaka jana bila kuwashirikisha viongozi wenzake wa Zec kinyume cha Katiba na sheria.
 
Maalim Seif alisema katika mkasa huo, Makamu Mwenyekiti wa ZEC, Jaji Abdulhakim Ameir Issa, alikamatwa na kushindwa kuendelea kutangaza matokeo ya wagombea urais katika uchaguzi huo.
 
Alisema kitendo alichofanya Kikwete hakikubaliki katika misingi ya demokrasia na utawala bora ni sawa na kufanya mapinduzi ya utawala.
 
Maalim Seif alisema kwa mujibu wa Katiba na Sheria ya Uchaguzi ya Zanzibar, hakuna kifungu kinachompa uwezo Mwenyekiti wa ZEC kufuta matokeo ya uchaguzi ambao tayari umeaisha kamilika.
 
Alisema Sheria ya Uchaguzi na Katiba ya Zanzibar imewapa haki wabunge, wawakilishi pamoja na madiwani kwenda mahakamani kama hawakuridhika na mchakato wa uchaguzi. 

“Zanzibar hakuna kifungu cha Katiba au sheria kinachoruhusu kurudiwa uchaguzi na uchaguzi wa Oktoba 25, mwaka jana ulikuwa huru na wa haki kwa mujibu wa ripoti za waangalizi wa uchaguzi wakiwamo Umoja wa Ulaya Marekani na Uingereza,” alisema Maalim Seif.
 
Aidha, alisema Mataifa ya Ulaya zikiwamo Marekani, Uingereza, Norway pamoja na Umoja wa Ulaya, yameanza kuchukua hatua za kuinyima misaada ya maendeleo Tanzania ikiwamo Zanzibar kutokana na mgogoro wa Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 25, mwaka jana.
 
Alisema wahisani hao pamoja na Shirika la Changamoto la Milenia (MCC) wamesema hawatotoa msaada mpaka suala la uchaguzi la Zanzibar likae sawa na kupatiwa muafaka wake.
 
Maalim Seif aliwataka wanachama wake kuonyesha kwa vitendo vya kweli vya kutoitambua serikali ikiwamo kukataa kulipishwa kodi za ovyo vyo pamoja na kujitenga na viongozi wa serikali katika utekelezaji wa majukumu yao.

"Mfano tunaweza kuamua siku flani kuanzia saa sita, tunasimamisha vyombo vyote vya usafiri na siku nyingine tunaamua kupiga honi Zanzibar nzima kuonyesha hatuitaki serikali ya CCM" Alisema Maalim Seif huku akishangiliwa na umati uliofurika katika ofisi za chama hicho.

"Wanasema ukitaka kumshinda adui unampiga akiwa dhaifu na udhaifu wao hawana fedha, na ili kuwadhibiti ni kuwanyima fedha na kuwachokoza kwa kuwaita majina mabaya kama dikteta, Nduli," alisema. 
 
Kuhusu suala la wakulima kuuzia serikali karafuu au kutoiuzia, alisema wananchi wenyewe ndiyo watakaoamua, lakini lengo la CUF ni kuona Serikali ya CCM inashindwa kuongoza Zanzibar kabla ya kumalizika miaka mitano.
 
Kwa mujibu wa Maalim Seif, tayari hali mbaya ya kiuchumi imeanza kujitokeza Zanzibar kutokana na bajeti ya mwaka huu kupoteza miradi mingi ya maendeleo kwa ufinyu wa fedha.
 
Kuhusu vitendo vya uvunjaji wa haki za binadamu, Maalim Seif alisema tayari yupo mwanasheria mzalendo ambaye ameanza kukusanya vielelezo mbalimbali kabla ya kufungua kesi katika Mahakama ya Kimataifa dhidi ya viongozi wenye dhamana ya kusimamia vyombo vya ulinzi na usalama wa raia.
 
Alisema tayari Waziri wa Mambo ya Ndani, Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP) na Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Muungano, wamepewa notisi ya kuarifiwa kufunguliwa mashtaka katika Mahakama ya Kimataifa kutokana na vitendo vya uvunjwaji wa haki za binadamu uliofanyika Zanzibar.
 
Alisema kwa sasa wanasheria wanapitia sheria kwa umakini za kuanzishwa kwa mahakama hiyo ya kimataifa ili kuangalia uwezekano wa serikali ya Zanzibar kufunguliwa mashtaka katika mahakama hiyo. 

Wakati wa ziara hiyo, Maalim Seif alipata wakati mgumu kutokana na barabara kufungwa na wafuasi wake wakimtaka atoe kauli juu ya hali ya kisiasa ya Zanzibar.

Jinsi Punyeto Inavyo Sababisha Ukosefu Na Upungufu Wa Nguvu za Kiume

$
0
0

Ukosefu  na/ama  upungufu  wa  nguvu  za  kiume, ni  tatizo  linalo  wakabili  mamilioni  ya  wanaume  duniani.  Zipo  sababu  nyingi  zinazo  sababisha  tatizo  la  ukosefu  wa  nguvu  za  kiume.  

Miongoni  mwa  sababu  hizo  ni  pamoja  na  maradhi  kisukari, presha,shinikizo  la  damu, moyo, figo, matatizo  kwenye  mishipa  ya  ubongo  &  mishipa  ya  uti  wa mgongo, matatizo  kwenye  mishipa itumikayo  kusafrisha damu  mwilini, maradhi  ya  ngiri,  pamoja  na   upigaji  punyeto  kwa  muda  mrefu.

Katika  makala  yetu  ya  leo, tutaangalia  namna   suala  la  upigaji  punyeto linavyo  athiri  nguvu  za  kiume.

Kabla  hatujaangalia  namna  suala la upigaji  punyeto linavyo  maliza  nguvu  za  kiume, ni  vyema  tukafahamu  kwanza  kuhusu  SAYANSI  YA  MFUMO  WA  NGUVU  ZA  KIUME.

Kufahamu   kuhusu   SAYANSI  YA  MFUMO  WA  NGUVU  ZA  KIUME  tafadhali  tembelea :

Ukisoma  vizuri  kuhusu  mfumo  wa  nguvu  za  kiume, utagundua  kuwa   Suala  la  nguvu  za  kiume  ni  suala  la  kimfumo.  Ili  mwanaume  awe na nguvu  za  kiume, aendelee  kuwa  na  nguvu  za  kiume na  azilinde  nguvu  zake za  kiume, ni  lazima  ogani  zote zinazo  husika  na  mfumo  wa  nguvu  za  kiume  ziwe  na  afya  njema  na  ziwe  na  ushirikiano   thabiti  na  wenye  afya.

Vile  vile , utagundua  kuwa , mambo  makuu  muhimu  katika   mfumo  wa  nguvu  za  kiume  ni  kama  ifuatavyo:

i.Mishipa  imara  ya  ubongo  na  yenye  afya  njema

ii. Mishipa  imara  ya  uti  wa  mgongo  (  spinal  cords )

iii.Mishipa  imara  itumikayo  kusafirisha  damu  mwilini  (  Blood Vessels )

iv. Mfumo  imara  wa  usafirishaji  damu  mwilini

v. Mishipa  ya  uume  iliyo  imara  na  yenye  afya  njema

vi. Uhusiano  imara  na  wenye  afya  kati  ya  mishipa  ya  fahamu  iliyopo  katika  ubongo, mishipa  ya  kwenye  uti  wa  mgongo  pamoja  na  misuli & mishipa  ya  kwenye  uume.

Hivyo  basi, ili  mwanaume  aweze  kuwa  na  nguvu  imara  za  kiume, na  aendelee  kuwa  na  nguvu  hizo ni  lazima  mambo  yote  muhimu  katika  mfumo  wa  nguvu za  kiume  yawe  imara  pasi na  hitilafu  yoyote.

Hitilafu  yoyote  katika  mambo  hayo, itasababisha  ukosefu na/ama  upungufu wa  nguvu  za  kiume  kwa  mwanaume  huyo.  Pale inapotokea    hitilafu  ama  mapungufu  katika  ogani  zaidi  ya  moja  kati  ya  zilizo  tajwa hapo  juu, basi  tatizo  kwa  muhusika  huwa  kubwa  mara  dufu.

JINSI  PUNYETO  INAVYO  SABABISHA  TATIZO  LA  UKOSEFU &  UPUNGUFU  WA  NGUVU  ZA  KIUME.
Mwanaume   anapopatwa na  wazo  la  kufanya  tendo  la  ndoa, ubongo  hutoa  ishara  kwenye  mishipa  ya  uti  wa  mgongo  ambayo  nayo  husafirisha  taarifa  hadi  kwenye  mishipa &  misuli  ya  uume.

Mishipa  ya  uume inapopokea  taarifa  hiyo, hutanuka. Na  mishipa  ya  uume  inapotanuka, hufanya  mambo  mawili  muhimu  sana :

i.Husababisha  mishipa  ya  ateri  kupanuka  na  hivyo  kuruhusu  damu  kuingia kwa  kasi  sana   ndani  ya  mishipa  ya  uume  na  hivyo  kuufanya  uume  usimame  na  kuwa  imara  bara bara.

ii. Huibinya na  kuiziba  mishipa  ya  vena  na  hivyo  kuzuia  kunyonya  ama  kufyonza  damu  iliyo  ingia  ndani  ya  mishipa ya  uume.  (  KAZI  KUBWA  YA  MISHIPA  YA  VENA  ILIYO  KARIBU NA  MISHIPA  YA  UUME  NI KUHAKIKISHA  HAKUNA  DAMU NDANI YA  MISHIPA  YA  UUME. HIVYO  BASI  DAMU  INAPOINGIA  NDANI YA  MISHIPA  YA  UUME, MISHIPA  YA  VENA  HU “SENSE” JAMBO  HILO  KWA  HARAKA  NA HIVYO  KUIFYONZA  DAMU  HIYO  KUTOKA KWENYE MISHIPA  YA UUME  YA  KUITOA  NJE YA MISHIPA  YA  UUME.  NA  DAMU INAPOKOSEKANA  NDANI  YA  MISHIPA  YA  UUME, HUUFANYA  UUME  KUSINYAA  NA  KULEGEA )

Mtu  anayepiga  punyeto  husababisha  mambo  yafuatayo  katika  mwili  wake :

1. Huuwa  nguvu  ya  mishipa  & misuli ya  uume ambayo  ndio  inayo husika  na  kusimama  kwa  uume

2. Mishipa  ya   uume  inapo  sinyaa  na  kukosa  nguvu  yake  ya  asili, husababisha  mambo  yafuatayo :

i.Huondoa  uwezo  wa  mishipa  &  misuli  ya  uume  kutanuka, na  hii  ndio  sababu  inayo  wafanya  waathirika  wa  punyeto  kutumia  nguvu  nyingi  sana  katika  kuufanya  uume  usimame.

ii.Huondoa  uwezo  wa  mishipa &  misuli  ya  uume  kuibana  na  kuiziba  mishipa  ya  vena, na  hii ndio  sababu  inayo  fanya  waathirika  wa  punyeto  kufika  kileleni  haraka  sana, kwani damu  inayo  ingia  kwenye misuli  ya  uume   hufyonzwa  ndani ya  muda  mfupi sana. 
 
 Hii  hutokea  kwa  sababu  mishipa na  misuli  ya  uume inakuwa  imelegea,na  mishipa  ya  vena inakuwa  imepwaya, hivyo  msuguano wowote ule  hufanya  mishipa  ya  vena  kufunguka  na  kufyonza  damu  kutoka  kwenye mishipa  ya  uume  na hivyo  kuufanya  uume  kusinyaa  ndani ya dakika ama sekunde  chache sana.

3. Vile  vile  punyeto  hufanya  uume  kusinyaa na  kurudi ndani  na  kuufanya  uonekane kama  uume  wa  motto mdogo.

Kwa  ufupi  punyeto  husababisha  ukosefu  wa  nguvu  za  kiume  kwa  sababu  kuu  zifuatazo :

i.Kwanza   hudhoofisha  na  kuharibu  mishipa  ya  uume,  ambayo  ndio  hufanya  uume kusimama.

ii.Pili  hudhoofisha  utendaji  kazi  wa  mishipa  ya  ateri, ambayo  ndio  hutumika  kama  njia  ya  kusafirisha  damu kupeleka kwenye  misuli  ya  uume  na  ivyo  kuufanya  uume  usimame

iii. Tatu, punyeto  hupelekea  kuvuja  kwa  mishipa  ya  vena  na  hivyo  kusababisha  damu  kufyonzwa  kwa  haraka  sana  kila  iingiapo ndani  ya  misuli ya  uume  na  matokeo  yake  ni  uume   kusimama  kwa  muda  mfupi  sana  wakati wa  tendo  la  ndoa.

iv. Punyeto  huathiri  mtiririko  wa  damu  kwenda  kwenye  mishipa  ya  uume, kwa  sababu  hudhoofisha  misuli &  mishipa  ya  uume  pamoja  na mishipa ya  ateri  ambayo  ndio  hutumika  katika  kusafirisha  damu kwenda  kwenye  uume

DALILI  ZA  MTU  ALIYE  ATHIRIWA  NA  PUNYETO
Dalili  kuu  za  mtu  aliye athiriwa  na  punyeto  ni  kama  ifuatavyo:

i.           Uume  kusinyaa  na  kuwa  kama  wa  mtoto
ii.         Uume kurudi  ndani
iii.       Uume  kusimama  ukiwa  legelege
iv.       Kufika  kileleni  haraka  wakati  wa  tendo  la  ndoa.

TIBA   YA   NGUVU  ZA  KIUME  KWA MTU  ALIYE  ATHIRIKA  NA  PUNYETO.
Dawa   asilia  ya  nguvu  za  kiume iitwayo JIKO  ni tiba  bora  na  ya  uhakika  kabisa  kwa  mtu  aliye  athiriwa   na  punyeto.  Dawa  hii, pamoja  na  mambo  mengine  mengi, husaidia  kufanya  mambio  yafuatayo  katika  mwili  wa  mwanaume  aliye  athiriwa  na  punyeto :

i.Kuimarisha  mishipa  & misuli  ya  uume  ulio  legea na  hivyo  kuurejeshea  uwezo wake wa  asili

ii. Hutibu   tatizo  la  uume  kurudi  ndani

iii.Humaliza  tatizo  la  kusimama  kwa  uume  ukiwa  legelege

iv.Hutibu  na  kuponya  kabisa  tatizo  la  kufika  kieleleni  haraka.

BEI  YA  DAWA  :  Dawa  hii  inapatikana  kwa  gharama  ya  SHILINGI  ELFU  THEMANINI  TU (Tsh. 80,000/=)

MAHALI  INAPOPATIKANA :  Dawa  hii  inapatikana  katika  duka  la  dawa  asilia  liitwalo  NEEMA  HERBALIST  &  NUTRITIONAL  FOODS  CLINIC  lililopo  jijini  DAR  ES  SALAAM  katika  eneo  la  UBUNGO   nyuma  ya  jengo  la  UBUNGO  PLAZA   karibu  na SHULE  YA  MSINGI  UBUNGO  NATIONAL  HOUSING.

Kwa  wateja  wasio  weza  kufika  ofisini  kwetu. Watafikishiwa  dawa  mahali  popote  walipo  jijini  DAR  ES  SALAAM.

Kwa   wateja  waliopo  mikoani  watatumiwa  dawa  kwa  njia  ya  MABASI

Kwa  wateja  waliopo   Zanzibar  wata fikishiwa  dawa  kwa  njia  ya  usafiri  wa boti.

Na  kwa  wateja  waliopo  UGHAIBUNI  watatumiwa  dawa  kwa  njia  ya  POSTA  ama  DHL.

MAWASILIANO :  WASILIANA  NASI   KWA  SIMU  NAMBA  0766  53  83  84.

Kwa  taarifa  zaidi  kuhusu  huduma  zetu, tutembelee kila  siku  kwenye  blogu  yetu :

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Aondoka London Kurejea Nchini

$
0
0
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiagana na wafanyakazi wa Ofisi ya Ubalozi wa Tanzania nchini Uingereza uliopo London wakati alipoondoka kwenye hoteli ya Intercontinental kurejea Dae es salaam Mei 15, 2016  Kushoto ni Jaji Mkuu wa Tanzania, Mohamed Othman. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Serikali Yasema Kusitishwa kwa Baadhi ya Misaada ya Wahisani Hakujaathiri Sekta ya Nishati

$
0
0
Waziri wa Nishati na Madini Prof Sospeter Muhongo ameliambia Bunge Mjini Dodoma kwamba miradi ya umeme vijijini (REA) haijaathirika chochote kwa Bodi ya Shirika la Changamoto za Milenia (MCC) kuondoa misada yake Tanzania.

Muhongo ameyasema hayo alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Iringa Mjini Mchungaji Peter Msigwa aliyetaka kujua serikali imepata hasara kiasi gani kwa MCC kuondoa fedha zake katika miradi ya umeme nchini.

Akijibu swali hilo Prof Muhongo amesema fedha za MCC zilikuwa haziendi kwenye miradi ya maendeleo ya umeme vijijini hivyo miradi hiyo itaendelea kama ilivyopangwa.

''Hakuna dola hata moja ya MCC iliyokuwa inaenda kwenye umeme vijijini fedha zilikuwa zikienda kwenye miradi ya maji, barabara na nishati lakini siyo umeme wa vijijini na fedha za kwenye nishati zilikuwa hazivuki theluthi moja hivyo kama umejiandaa kulima hekari 8 akakuongezea mtu 2 ili zifike 10 siku akiondoa za kwake utandelea na zako 8 kama kawaida''- Amesisitiza Prof. Muhongo.

Bodi ya Shirika la Changamoto za Milenia (MCC) ilisema Tanzania haijatimiza viwango vinavyohitajika ili kunufaika na ufadhili kutoka kwa shirika hilo, na hivyo basi haitapokea msaada wa awamu ya pili ambao ulikuwa wa jumla ya Dola 472.8 milioni ambazo ni sawa na shilingi trilioni moja za Tanzania.

Kwa awamu ya kwanza Tanzania ilipokea Dola 698 milioni na moja kati ya mambo yaliyosababisha MCC kuondoa fedha zao ni pamoja na kurudiwa kwa uchaguzi wa Zanzibar.

Waziri Nape Alivyofafanua Suala La Kurusha Live Bunge Mjini Dodoma

$
0
0
Sehemu ya Majumuisho ya Hotuba ya Bajeti ya Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye akitolea ufafanuzi suala la Bunge  kurushwa Live na studio za Bunge.

Bunge Liliahirishwa Leo Asubuhi Kupisha Kamati ya Kanuni ipitie Hotuba ya Upinzani Iliyozuiliwa

$
0
0
Hotuba ya Godbless Lema, Msemaji wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni katika Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi ilizuiliwa leo asubuhi  kusomwa Bungeni hadi ipitiwe  upya na kamati ya kanuni.

Bunge liliahirishwa  leo asubuhi hadi saa 10 jioni baada ya kuzuia kusomwa kwa hotuba hiyo kwa madai kwamba, ina maneno yanayohitajika kuondolewa ili ikidhi matakwa baada ya kupitiwa na Kamati ya Kanuni.

Ndani ya Hotuba ya Lema  kipo kipengelea kinachoelezea sakata la makataba tata wa Kampuni ya Lugumi ambapo Kamati ya Mambo ya Ndani ilielezwa suala hilo kutojadiliwa bungeni kwa madai tayari lilikuwa limeanza kuchunguzwa na Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC).

Kipengele kinachohusu mkataba wa Kampuni ya Lugumu kipo kwenye sehemu ya tano inayoeleza Mikataba Tata ya Jeshi la Polisi.

Kwa muda mrefu mkataba huo uliotolewa na Jeshi la Polisi nchini kwa Kampuni ya Lugumi Enterprises Ltd wenye thamani ya Sh 37 bilioni umedaiwa kuwa na harufu ya ufisadi.

Mwaka 2011, kampuni hiyo ilipewa zabuni ya kufunga mashine za alama za vidole katika vituo vya polisi 108 nchini na kulipwa Sh 34 bilioni kati ya Sh 37 bilioni sawa na asilimia 99 ya malipo yote.

Mambo mengine yaliyosababisha hotuba hiyo izuiliwe ni  Uuzwaji wa nyumba uliomtaja Rais John Magufuli moja kwa moja, Rushwa na bunge kutumika kuwalinda watuhumiwa , tabia ya Rais na usalama wa nchi na mwisho ni kuwataja viongozi wa juu wa serikali kwa maneno ya dhihaka.
 

Watu 11 Wakamatwa Mkoani Morogoro Kwa Tuhuma za Kumbaka na Kumdhalilisha Binti wa Miaka 21

$
0
0

Watuhumiwa wawili Zuberi Thabiti (30) na Iddy Adamu (32) wanaodaiwa kushirikiana kufanikisha tukio la kumbaka na kumdhalilisha binti wa miaka 21, mkulima (jina limehifadhiwa), mkazi wa Kata ya Dakawa, wilayani Mvomero, mkoani Morogoro, wamekamatwa na kohojiwa na jeshi la polisi mkoani humo.

Watuhumiwa hao wanadaiwa kufanya tukio hilo la kinyama usiku wa Mei 4, mwaka huu katika nyumba ya kulala wageni iitwayo Titii iliyoko Dakawa ambapo Zuberi ambaye ni dereva, mkazi wa Mbarali Mbeya anadaiwa kumbaka binti huyo huku Iddy ambaye ni mkulima, mkazi wa Makambako akirekodi picha za video kwa kutumia simu yake ya mkononi.

Kwa mujibu wa taarifa ya polisi, baada ya kurekodi katika simu yake, baadaye Iddy alizituma picha hizo kwa mtu aliyefahamika kwa jina la Rajabu Salehe (26), mkazi wa Dakawa ambaye naye alizisambaza picha hizo katika mitandao mbalimbali ya kijamii kwa watu mbalimbali.

Taarifa ya polisi imeeleza kuwa, chanzo cha tukio hilo ni kwamba, binti huyo alikuwa na uhusiano wa kimapenzi na Zuberi ambapo siku hiyo mtuhumiwa alimpigia simu binti huyo na kumwambia aende katika nyumba hiyo ya wageni.

Taarifa hiyo ya polisi imezidi kueleza kuwa, baada ya kufika katika chumba husika ndipo Iddy alipoingia kisha kumtaka binti huyo afanye atakachomuelekeza huku akimshikia kisu ili asipige kelele na baada ya kutekeleza ukatili huo (ubakaji), walimtaka asitoe siri hiyo vinginevyo atauawa.

Aidha, baada ya tukio hilo kuripotiwa kituo cha Polisi Dakawa Apliri 5, mwaka huu, polisi walianza uchunguzi mara moja ambapo walifanikiwa kuwakamata jumla ya watuhumiwa 11 wakiwemo Zuberi na Iddy pamoja na walioshiriki kuzisambaza picha hizo za udhalilishaji ambao ni;

Rajabu Salehe (26), Saidi Athumani (26),  Musini Ngai (36), Saidi Mohamedi (24), John Peter (24), Hassani Ramadhani (27), Ramadhani Ally (26), Lulu Peter (38) na Magreth Njonjome (30), wote wakazi wa Dakawa ambapo kwa pamoja wamefunguliwa shitaka la PICHA ZA UTUPU (P.O.N.O.GRAFIA) chini ya kifungu cha 14 (1) (a) cha sheria ya makosa ya mtandao.

Taarifa hiyo ya polisi pia imeeleza kuwa jeshi hilo linaendelea kuwatafuta watuhumiwa wengine huku jeshi hilo likitoa onyo kwa wananchi wote kuwa makini na matumizi ya mitandao ya kijamii kwa kutoshiriki makosa ya uhalifu wa kimtandao kwani sheria itachukua mkondo wake.

Katika hatua nyingine, Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Ummy Mwalimu leo alikemea suala hilo bungeni na kueleza masikitiko yake makubwa kwa watu hao kutekeleza unyama huo na kusisitiza kuwa watuhumiwa hao wafikishwe mahakamani haraka.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumanne ya May 17

Serikali: Hatuna Msamaha na Wauza Madawa ya Kulevya

$
0
0
Serikali  imesema haitakuwa na msamaha wala suluhu kwa wahusika wote wa biashara haramu ya dawa za kulevya. 

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga alitoa rai kwa watu wote kutojihusisha na uuzaji, utumiaji na usafirishaji wa dawa hizo.

Kitwanga aliyasema hayo jana bungeni mjini hapa wakati akiwasilisha Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara yake, kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Alisema, tatizo la biashara haramu na matumizi ya dawa za kulevya limeendelea kuwepo nchini na katika kipindi cha Julai, 2015 hadi Machi, 2016, kilogramu 141.7 za dawa za kulevya za viwandani ambazo ni heroin, cocaine, cannabis resin, morphine na mandrax zilikamatwa na watuhumiwa 719 (wanaume 644 na wanawake 75) walikamatwa na kufikishwa mahakamani.

“Aidha, kilo 18,513 na gramu 415 za bangi na kilo 15,402 za mirungi zilikamatwa ambapo watuhumiwa wanaume 9,935 na wanawake 1,020 walikamatwa na kufikishwa mahakamani,” alisema.

Alisema, katika mwaka 2016/17 Jeshi la Polisi litaendeleza mapambano dhidi ya biashara haramu ya dawa za kulevya kwa kubaini mtandao wa wahalifu wa ndani na nje ya nchi unaojihusisha na uingizaji na usambazaji wa dawa za kulevya nchini.

Akizungumzia vita dhidi ya biashara haramu ya usafirishaji wa binadamu, alisema wizara ilianzisha Sekretarieti ya Kupambana na Kudhibiti Biashara Haramu ya Usafirishaji wa Binadamu kwa lengo la kudhibiti biashara hiyo.

Kitwanga alisema hilo lilifanyika baada ya ripoti mbalimbali za kitaifa na kimataifa kuitaja Tanzania kama chanzo, njia ya kupitishia na kituo cha mwisho kwa biashara haramu ya kusafirisha binadamu.

Alisema katika mwaka 2015/16 sekretarieti hiyo ilizuia hati na nyaraka za kusafiria za wasichana 31 wa Tanzania kwa lengo la kufanya uchunguzi kubaini mtandao wa wasafirishaji haramu wa binadamu. 

Alisema katika mwaka wa fedha 2016/17 Sekretarieti imejipanga kufanya ufuatiliaji na uchunguzi wa wazi juu ya biashara hiyo.

Jeshi La Polisi Lanasa Mahausigeli 15 Waliokuwa Wakipelekwa Oman

$
0
0
Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam limewakamata wasichana 15 katika nyumba iliyopo maeneo ya Ukonga, waliokuwa tayari kusafirishwa kwenda Oman kufanya kazi za ndani.

Akizungumza na waandishi wa habari jana, Dar es Salaam, Kamishna wa Polisi wa kanda hiyo, Simon Sirro, alisema wasichana hao walikamatwa baada ya Polisi kupata taarifa toka kwa msiri kuwa kuna mtu amewaweka wasichana kwa ajili ya kuwasafirisha.

Sirro alisema Polisi walifuatilia na kufika katika eneo hilo na kufanikiwa kuwakuta katika nyumba ya Hadija Mohamed (40) wakiwa wamegawanywa katika vyumba viwili.

Alisema uchunguzi wa awali, umebaini kuwa mwanamke huyo anashirikiana na mwenzake Salma Habibu (43) mkazi wa Temeke kuwatafutia masoko nchini Oman na wao ni mawakala wanaoletewa kutoka mikoani na kuwapokea kwa ajili ya kuwasafirisha.

Aidha alisema watuhumiwa hao watapelekwa mahakamani ili sheria ichukue mkondo wake.

Pia ametoa onyo kwa watu wenye tabia hiyo kuacha, kwani wasichana hao wakifikishwa nje ya nchi hufanyiwa vitendo vya kikatili na unyanyasaji.

Katika tukio jingine, Polisi kanda hiyo imewakamata vijana 75, ikiwa ni muendelezo wa msako wa vijana wanaofanya matukio ya wizi wa majumbani nyakati za usiku.

Makamu wa Rais Atema Cheche.........Wakuu wa Mikoa na Wilaya Watakaopuuza Agiza Lake Watatumbuliwa!!

$
0
0
Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan ameagiza wakuu wa mikoa ya Geita, Arusha na Kagera kuhakikisha wanaondoa mifugo itokayo nje ya nchi pamoja na kuwaondoa wanachi waliovamia maeneo ya hifadhi za taifa (Tanapa) ifikapo Juni 30 mwaka huu.

Aidha ameagiza wakuu wa mikoa na wakuu wa wilaya kuhakikisha wanatenga maeneo maalumu kwa ajili ya mifugo inayotolewa ndani ya hifadhi na kupunguza mgogoro kwa wananchi wengine.

Samia alitoa maagizo hayo jana jijini Arusha, wakati alipokuwa akikabidhi hundi ya thamani ya Sh bilioni moja kwa wakuu wa mikoa 19 inayozunguka hifadhi za taifa (Tanapa) kwa ajili ya kununua madawati. 

Alisema, wakuu wa mikoa wakizembea kutekeleza uondoaji mifugo ndani ya hifadhi za taifa serikali itawawajibisha.

Alisema waliohifadhi mifugo ndani ya hifadhi hiyo waondoke na mifugo yao hadi Juni 30 mwaka huu kwani mkoa wa Kagera una ng’ombe milioni mbili wanaotoka nje ya nchi, na mikoa ya Arusha na Geita ina ng’ombe milioni tatu kutoka nje ya nchi.

Akizungumzia kuhusu kukabidhi madawati 16,500 katika wilaya zote 55 zilizopo kwenye mikoa 19 nchini, Samia aliipongeza Tanapa kwa kusaidia elimu nchini kwani baada ya serikali ilipotangaza kuwa elimu bure wanafunzi wengi wamejitokeza huku kukiwa na changamoto ya madawati

Samia alisema, kutokana na msaada huo wanafunzi wataondokana na adha ya kukaa chini na kuumia migongo kwani kila wilaya itapata madawati 300 huku wanafunzi 49,500 wakiwa wanakaa kwenye madawati na kuongeza usikivu zaidi.

Naye Waziri wa Maliasili na Utalii, Profesa Jumanne Maghembe alisema Tanapa wanatambua mchango wa elimu ndio maana wametoa msaada huo kwa mikoa 19 inayopakana na hifadhi za taifa.

Mkurugenzi wa Tanapa, Allan Kijazi alisema Tanapa itaendelea kushirikiana na serikali katika sekta ya elimu kwa lengo la kuhakikisha wanafunzi wanasoma kwa bidii pamoja na kujua jinsi ya kuhifadhi maliasili za Taifa.

Akitoa salamu za shukrani kwa Makamu wa Rais, Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Said Meck Sadiki aliishukuru Tanapa kwa kutoa madawati kwa wakuu wa mikoa na kusema kuwa, mkoa wa Kilimanjaro umepiga marufuku usafirishaji wanyama pori kupitia Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) kuanzia jana.

Serikali Kuajiri Askari Wapya 3700....... Askari 7000 na Wakaguzi 1300 Watapandishwa Vyeo

$
0
0
Serikali  inatarajia kumwaga ajira kwa askari  katika mwaka ujao wa fedha.Taarifa juu ya ajira hizo, zilitolewa jana bungeni  na  waziri  mwenye dhamana.

Akiwasilisha Makadirio ya Mapato ya Matumizi ya Wizara yake kwa mwaka 2016/17 kuhusu ajira za askari, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga alisema wataajiriwa askari wapya 3,700 katika mwaka wa fedha 2016/17.

Waziri Kitwanga alisema mbali ya kuajiri askari hao, pia watawapandisha vyeo askari 7,140, wakaguzi 1,325 na maofisa 991.

Alisema katika mwaka 2015/16, jumla ya askari polisi wapya 3,882 waliajiriwa, na askari wakaguzi na maofisa 4,065 wa vyeo mbalimbali walipandishwa vyeo kwa kufuata utaratibu wa ajira.

“Aidha, serikali imeendelea kuhuisha viwango vya mishahara na posho mbalimbali, ikiwemo posho ya chakula ambayo iliongezwa kutoka Sh 180,000 hadi kufikia Sh 300,000 kwa mwezi,” alieleza Waziri Kitwanga.

Alisema katika mwaka ujao wa fedha, Jeshi la Polisi litaongeza umakini katika kusimamia nidhamu kwa askari wake kwa kufanya uchambuzi wa kina (vetting) kwa kuchukua vijana waliomaliza mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), wanaoomba kujiunga na Jeshi la Polisi ili kuwa na askari wenye nidhamu na moyo wa dhati wa kulitumikia Taifa kwa ujumla.

Kwa upande wa Jeshi la Magereza, alisema linatarajia kutoa mafunzo kwa maofisa na askari 4,975 katika ngazi mbalimbali, ikiwa ni pamoja na yale ya Taaluma ya Urekebishaji.

Alisema ili kukabiliana na changamoto ya uchache wa miundombinu ya makazi kwa askari Polisi, serikali kupitia mkopo kutoka Serikali ya China inakusudia kujenga nyumba 4,136 chini ya usimamizi wa Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Polisi.

Akizungumzia Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, alisema jeshi hilo linahitaji vituo 152 Tanzania Bara, lakini kwa sasa lina vituo 57 na kati ya hivyo, 38 vipo katika miji na 19 katika viwanja vya ndege. 

Alisema huo ni upungufu wa vituo 95 hali inayosababisha maeneo mengi kukosa huduma za zimamoto na uokoaji.

Inategemea kujenga kituo kimoja cha zimamoto na uokoaji katika eneo la Kigamboni katika Jiji la Dar es Salaam na kuendelea na ujenzi wa Jengo la Makao Makuu Tazara - Mchicha, Dar es Salaam.

Aidha, alisema Jeshi la Polisi litaendelea kupambana na makosa yanayovuka mipaka hususani ugaidi, uharamia, biashara ya dawa za kulevya, biashara haramu ya kusafirisha binadamu, wizi wa vyombo vya moto hususani magari, wizi wa kutumia mitandao ya Tehama, bidhaa bandia, na biashara haramu ya silaha na uchafuzi wa mazingira.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images