Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Sakata la UDA Laitikisa Serikali

$
0
0

Wakati Serikali ikiendelea kuchunguza mikataba kati ya Shirika la Usafiri Dar es Salaam (Uda) na Wakala wa Mabasi Yaendayo Haraka Dar es Salaam (Dart) kuhusu Mradi wa Mabasi Yaendayo Haraka (BRT), Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) ametia pilipili kidonda kwa kuibua udanganyifu unaolizunguka shirika hilo.

Kwenye ripoti yake ya mwaka wa fedha 2014/2015 aliyoitoa bungeni Jumatatu, CAG Profesa Mussa Assad amebainisha kwamba Dart ilifanya makubaliano na msimamizi wa uendeshaji, Uda-RT kutoa huduma ya mpito ya usafiri kwa kutumia mabasi 76 yenye vigezo vilivyoainishwa kwenye mkataba.

Tofauti na makubaliano hayo, Uda ilinunua mabasi 140 ambayo yalikuwa na nembo ya Uda-RT badala ya Dart kinyume na vigezo vilivyoainishwa kwenye mkataba.

Meneja wa Miundombinu wa Dart, Mhandisi Mohamed Kuganda alisema wenye taarifa sahihi ni Uda-RT.

Hata hivyo, alikiri kufahamu ununuzi wa mabasi hayo na kusema waliwauliza Uda-RT na wakajibiwa kuwa, “barabara za kutumika mabasi hayo zipo nyingi.”

Mwenyekiti Mtendaji wa Kampuni ya Simon Group na Uda-RT, Robert Kisena alisema hawezi kuzungumzia suala hilo kwa kuwa limeelekezwa serikalini: “Hoja za CAG zinaihusu Serikali hivyo siwezi kujibu.”

Akizungumza  ofisini kwake, Msajili wa Hazina Lawrence Mafuru alisema Serikali hairidhishwi na uendeshwaji wa Uda, lakini haina la kufanya.

Alifafanua kuwa Serikali haijawahi kujitoa katika umiliki wa shirika hilo na kwamba bado inazo asilimia 49 ya hisa zote na Simon Group ina asilimia 51 zilizobaki.

Alieleza kuwa uendeshaji wa shirika hilo: “Hauna utawala bora.”

Hata hivyo, alisema ni vigumu kwa sasa kumiliki shirika hilo kwa asilimia 100 kwa sababu wenye hisa nyingi ndiyo wenye uamuzi.

“Tulichukuaje hilo shirika? Labda kama wenzetu watakubali kutuuzia hisa, vinginevyo hatuwezi kuwanyang’anya,” alisema. 

Uchunguzi wa CAG 
Akikumbusha juu ya ufuatiliaji baada ya ubinafsishaji, CAG ameiambia Serikali kuwa hisa za Uda ambazo hazikugawiwa, ziliuzwa kwa kampuni ya Simon Group kwa Sh1,142,643,935.

Alisema kampuni hiyo ililipa asilimia 24.9 tu ya makubaliano ya bei ya mwanzo, Sh285 milioni kwenye akaunti ya Uda yenye namba 01J1021393700 iliyopo Benki ya CRDB.

Ripoti inasema hakuna ushahidi wa malipo ya asilimia 75.1 ambazo ni sawa na Sh858 milioni zilizobakia.

CAG amebainisha pia kuwa aliyekuwa mwenyekiti wa Uda, Idd Simba alipokea Sh320 milioni alizowekewa katika akaunti yake binafsi kwa ajili ya huduma ya ushauri wa kitaalamu kutoka Simon Group Limited.

Utata uliopo ni kwamba Simon Group inadai kuwa kiasi hicho: “Ni sehemu ya malipo ya mauzo ya hisa za Uda.”

Akizungumzia suala hilo hivi karibuni, CAG mstaafu Ludovick Utouh alisema anashangaa kuona Uda ikiuzwa na fedha zake kuwekwa kwenye akaunti ya mtu binafsi kitendo ambacho ni kosa la jinai lakini kesi hiyo ilifunguliwa na kisha kufutwa.

Ingawa mwaka 2013 aliyekuwa Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP), Dk Eliezer Feleshi aliwasilisha hati ya kutokuwa na nia ya kuendelea kuwashtaki Idd Simba na wenzake, CAG ameendelea kuishauri Serikali kupitia Msajili wa Hazina kufuatilia kwa karibu juu ya ubia wake ndani ya Uda ili kuhakikisha: “Maslahi ya umma hayapotei.”

Hata hivyo, Mafuru alisema kwa kuwa kesi iliyokuwa mahakamani imekwisha na uamuzi umeshatolewa, itakuwa vigumu kulirejesha serikalini shirika hilo.

 “Kesi zilizokuwa mahakamani zimekwisha ndiyo maana ninaweza kuzungumzia… Uda inaendelea kufanya kazi.”

Simba, aliyewahi kuwa Waziri wa Viwanda na Biashara katika awamu ya tatu, alishtakiwa pamoja na aliyekuwa mkurugenzi wa shirika hilo, Salim Mwaking’inda na Meneja Mkuu, Victor Milanzi na Mkurugenzi wa Simon Group Limited, Simon Kisena, kwa kosa la uhujumu uchumi.

CAG alisema alitoa mapendekezo ya kukiukwa kwa kanuni za uuzaji wa hisa hizo tangu mwaka 2011/2012 lakini yalipuuzwa. 

Alisena Uda iliuzwa bila kibali cha Serikali na hisa zilithaminishwa kwa Sh744.79 kwa kila moja Oktoba 2009, lakini Novemba 2010, zikashushwa mpaka Sh656.15.

Hata hivyo, katika uuzaji, Bodi ya Wakurugenzi ya Uda ilitoa punguzo la asilimia 60 kwa kila hisa kwa mwekezaji huyo. Bodi ilizingatia tathmini ya Oktoba 2009 bila kuwapo na sababu za kufanya hivyo.

CAG alisema: “Kwa mujibu wa majibu ya Mlipaji Mkuu wa Serikali, Serikali haitambui uuzwaji wa hisa hizo.”

Uda ni moja ya mashirika 158 yaliyokaguliwa na CAG kwa mwaka wa fedha uliopita kati ya 185 yanayostahili. 

Licha ya tahadhari iliyotolewa mwaka jana na wabunge wa upinzani juu ya uharamu wa kuuzwa kwa hisa za Uda, ripoti ya CAG imeweka wazi kilichokuwa kinaelezwa.

Kwa nyakati tofauti, Mbunge wa Kawe, Halima Mdee na wa Kibamba, John Mnyika walisema shirika hilo liliuzwa kwa: “Bei ya kutupwa.”

Watakaolipa mishahara HEWA kuburuzwa Mahakamani

$
0
0
Serikali imesema vigogo wa juu katika utumishi wa umma, watakaobainika kuhusika kwa namna moja au nyingine katika kufanikisha ulipaji wa mishahara hewa, watafunguliwa kesi ya jinai.

Aidha, imesema ifikapo Julai mosi, mwaka huu Halmashauri zote nchini ziwe zimefunga na kutumia mifumo ya kielektroniki katika kukusanya mapato yake ya ndani na zimetakiwa kusitisha ukusanyaji kwa njia ya mawakala.

Katika hatua nyingine imesema hadi kufikia Machi, 2016, watumishi 90 wamechukuliwa hatua mbalimbali za kinidhamu na wengine kufikishwa mahakamani kwa kukiuka taratibu na sheria za kazi wakiwemo wakurugenzi watendaji (DED) wa halmashauri watano ambao wamevuliwa madaraka.

Hayo yalisemwa kwa wakati tofauti na mawaziri wawili katika Ofisi ya Rais, walipowasilisha hotuba za bajeti kwa ofisi zao kwa mwaka ujao wa fedha bungeni mjini Dodoma jana. 

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Utumishi na Utawala Bora, Angela Kairuki akiwasilisha hotuba ya ofisi hiyo, alisema kuanzia sasa kiongozi wa serikali wakiwemo wa ngazi za juu watakaobainika kuhusika kwa njia moja au nyingine katika kufanikisha ulipaji wa mishahara hewa watafunguliwa kesi za jinai.

Waziri huyo alisema uchumi imara na endelevu katika nchi yoyote unahitaji uwepo wa utumishi wa umma uliotukuka unaozingatia utawala bora, utawala wa sheria, maadili na mifumo thabiti ya usimamizi na utekelezaji.

Alisema mipango na bajeti ya mwaka ujao wa fedha kwa ofisi hiyo imezingatia dhamana hiyo ambayo imebeba dhamira ya Serikali ya Awamu ya Tano ya kuleta mabadiliko makubwa katika utumishi wa umma kwa kuimarisha uwajibikaji na uadilifu.

Alisema utekelezaji wa dhamira hiyo utasaidia kujenga utumishi wa umma uliotukuka kwa kuondokana na matumizi mabaya ya madaraka, kuondokana na ukiukwaji wa maadili ya uongozi na utumishi wa umma, kuondokana na ucheleweshaji wa maamuzi, kutosimamiwa kwa uwazi na kutowajibika kwa viongozi na watumishi.

“Ni lazima tuwe na viongozi wa umma wanaozingatia maadili yao ya kazi na ndio maana tunasisitiza kuwa viongozi wote watakaobainika kuhusika na ulipaji au kusaidia kulipa watumishi hewa mishahara, tutawafungulia kesi za jinai,” alisema Kairuki.

Kwa upande wake, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), George Simbachawene akiwasilisha hotuba ya bajeti yake, alisema katika mwaka wa fedha unaomalizika, watumishi 78 wa Mamlaka za Serikali za Mitaa walichukuliwa hatua za kinidhamu na kijinai.

Alisema kati ya watumishi hao, ma-DED watano wamevuliwa madaraka na kupangiwa kazi nyingine na wakurugenzi watatu wamefunguliwa kesi mahakamani na kesi hizo bado zinaendelea.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Alhamisi ya April 28

Msajili wa Vyama Avikaba Koo Vyama 21 Vya Siasa Ambavyo Havijakaguliwa......Kwa Mujibu wa CAG, ni Chama cha CUF Pekee ndo Kimekaguliwa

$
0
0

Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, Jaji Francis Mutungi ametoa miezi mitatu kwa vyama 21 ambavyo havijakaguliwa kuwasilisha hesabu zake.

Kauli ya Jaji Mutungi imekuja siku nne baada ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Profesa Mussa Juma Assad kutoa taarifa juu ya ukaguzi wa hesabu katika vyama vya siasa 22 vyenye usajili wa kudumu, CAG alieleza kati ya vyama hivyo, chama cha CUF pekee ndicho kilikuwa kimepeleka hesabu zake kwa kipindi cha miezi sita, kati ya Januari hadi Juni 2015.

Alisema vyama vingine 21 havikuwasilisha vitabu vya hesabu kwa ajili ya ukaguzi kinyume na kifungu cha 14 cha Sheria ya vya ma vya siasa namba 5 ya mwaka 1992.

Akizungumza jana nje ya viwanja vya Bunge, Jaji Mutungi alisema ukaguzi wa fedha katika vyama ni suala la kisheria na lina mchakato wake, akisisitiza kuwa ofisi yake imeisoma taarifa ya CAG na inaifanyia kazi kwa kuvipa vyama hivyo miezi mitatu.

“Kwa mujibu wa sheria tunatakiwa kuvikumbusha vyama kufanya ukaguzi na tulifanya hivyo mwanzoni mwa mwezi huu (Aprili).

"Tuliviandikia barua vyama vyote. Ila kutokana na kuibuliwa kwa suala hili tumeviandikia barua na kuvipa miezi mitatu kukamilisha hesabu zao,” alisema.

Alisema ofisi yake haiwezi kuweka shinikizo kuhusu suala hilo kwa maelezo kuwa jambo hilo  linafanyika kwa matakwa ya kisheria.

Bandari Ya Dar es Salaam Kuunganisha Singapore Na Afrika Mashariki

$
0
0

Waziri wa Biashara na Viwanda wa Singapore, Dk. Koh Poh Koon, amesema wamepanga kutumia bandari ya Dar es Salaam kuwa kiunganishi cha biashara kati ya nchi hiyo na mataifa mengine ya Afrika Mashariki.

Dk. Koon ameyasema hayo jana(Jumatano, Aprili 27, 2016), wakati alipomtembelea Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa ofisini kwake mjini Dodoma, na kwamba  Singapore ipo tayari kutoa fursa kwa wataalam wa Tanzania kwenda kufanya kazi katika Bandari ya Singapore ili kupata uzoefu utakaosaidia uendeshaji wa bandari za Tanzania.

Dk. Koon ambaye ameambatana na wafanyabiashara wakubwa wapatao 40, amemweleza Waziri Mkuu kwamba kampuni ya Hyflux ya Singapore imeanza kuwekeza nchini kwa kujenga eneo maalum la uchumi (Special Economic Zone) mkoani Morogoro ambapo ndani ya kipindi cha miaka mitano wanatarajia kujenga miundombinu wezeshi ya kuweka viwanda vya kati (light industries), maeneo ya biashara na nyumba za makazi zipatazo 37,000.

“Jiwe la msingi la mradi huo litawekwa tarehe 29 Aprili 2016 na Waziri wa Biashara,Viwanda na Uwekezaji, Charles Mwijage,” alisema.

Mbali na ushirikiano katika sekta ya biashara na uwekezaji, Dk Koon amweleza Waziri Mkuu kwamba nchi yake itaisaidia Tanzania kujenga uwezo wa kiufundi katika maeneo mbalimbali ya menejimenti na uendeshaji wa bandari na ufundi katika sekta ya gesi na mafuta.

“Hadi sasa makampuni ya Singapore yaliyowekeza nchini ni pamoja na Pavillion Energy ambayo imewekeza kiasi cha Dola za Kimarekani bilioni 1.2 katika sekta ya gesi na inatarajia kuwekeza zaidi dola za kimarekani bilioni 3 kwa ajili ya ujenzi wa kinu cha kuchakata gesi (LNG plant) kitakachojengwa mikoa ya Kusini kwa ubia na makampuni ya gesi kutoka Ulaya na Marekani”.

Amesema kampuni ya PIL ya Singapore inatarajia kuwekeza Dola za Kimarekani milioni 400 kwa ajili ya kuanzisha kituo cha kutoa huduma kwa makampuni ya gesi.

Amesema lengo la ziara hiyo ni kuimarisha ushirikiano baina ya mataifa hayo pamoja na kuweka mikakati ya kuinua uchumi na kupanua wigo wa biashara.

Kwa upande wake, Waziri Mkuu Majaliwa ameishukuru Serikali ya Singapore kwa uwekezaji unaofanywa na makampuni yake nchini na kwa misaada ya kiufundi ambayo wameitoa kwa Tanzania katika nyanja mbalimbali.

Ili kusaidia juhudi za Serikali ya Awamu ya Tano za kukuza uchumi, Waziri Mkuu ameyakaribisha makampuni mengine ya Singapore kuja nchini kufanya uwekezaji katika maeneo mbalimbali ikiwa ni pamoja na  kuanzisha viwanda, mahoteli, kilimo na nishati.

Amemuahidi Dk. Koon kwamba Tanzania ipo tayari kukamilisha mazungumzo ya kusaini Mkataba wa Kuvutia na kulinda uwekezaji baina ya nchi mbili (Bilateral Investment Protection and Promotion Agreement) na Mkataba wa Kuepuka kutoza ushuru mara mbili (Double Taxation Avoidance Agreement) ili kuvutia uwekezaji zaidi kutoka Singapore. 

Waziri Mkuu, Majaliwa amewataka Watanzania kutumia fursa ya ushirikiano kati ya Singapore na Tanzania kuanzisha biashara mpya zitakazowanufaisha wote.

Waziri Mkuu amesema Singapore ina uwezo mkubwa kibiashara pamoja na uzoefu wa siku nyingi kwenye uendeshaji wa bandari hivyo Tanzania itapata nafasi ya kujifunza namna ya uendeshaji katika sekta hizo.

Amesema Tanzania imefungua milango ya uwekezaji kwa wafanyabiashara wa Singapore kuja kuwekeza katika sekta za viwanda, usafiri wa anga na kwenye Maeneo ya Uzalishaji kwa Mauzo Nje (EPZ).

Wafanyakazi 8,000 Hawajawasilishiwa Michango ya NSSF

$
0
0
Wafanyakazi takriban 8,000 ambao ni wanachama wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) hawajawasilishiwa michango kutoka kwa waajiri wao yenye thamani ya Sh bilioni 21.4.

Kutokana na hali hiyo, NSSF imetoa muda wa miezi miwili kwa waajiri wote nchini ambao hawajawasilisha fedha za michango hiyo kwa shirika hilo, kuwasilisha mara michango hiyo kabla ya Julai mosi, mwaka huu.

Kwa mujibu wa shirika hilo, endapo muajiri yeyote atashindwa kutekeleza agizo hilo katika muda huo uliotolewa, NSSF haitakuwa na njia nyingine zaidi ya kuwaburuza waajiri hao mahakamani kwa mujibu wa sheria.

Aidha shirika hilo, lilibainisha wazi kati ya waajiri sugu wasiowasilisha kwa wakati michango ya wafanyakazi wao kwa shirika hilo, ni Shirika la Reli la Tanzania na Zambia (Tazara) na baadhi ya kampuni za ulinzi.

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Kaimu Mkurugenzi wa Uwezeshaji wa NSSF, James Aigo alisema ni kosa la jinai kwa mujibu wa Sheria ya NSSF kwa mwajiri kutowasilisha michango ya mfanyakazi wake.

Aigo alisema kwa mujibu wa sheria hiyo waajiri wote wanatakiwa wawasilishe michango ya wafanyakazi wao ndani ya siku 30 kutoka tarehe ya mwisho wa mwezi husika.

 “Lakini kuna baadhi ya waajiri kwa sababu wanazozijua wenyewe, wanashindwa kutekeleza hitaji hili la kisheria kikamilifu kwa kushindwa kuwasilisha michango ya wafanyakazi kwa wakati,” alisisitiza Aigo.

Alisema kwa mwaka huu wa fedha unaoisha Julai mosi, mwaka huu, takribani wafanyakazi 8,000 ambao ni wanachama wa shirika hilo hawajawasilishiwa michango kutoka kwa waajiriwa wao.

Alisema kati ya hao wafanyakazi 3,234 wanatokea Dar es Salaam, ambao ni sawa na asilimia 60 ya wafanyakazi wote ambao hawajawasilishiwa michango na waajiri wao yenye thamani ya Sh bilioni 21.4.

Kaimu Mkurugenzi wa Uwekezaji na Miradi, Mseli Abdallah aliwataka wateja waliopangisha na kununua nyumba kwa mkopo kupitia nyumba za NSSF, kukamilisha malipo yao kabla ya kutolewa kwenye nyumba hizo.
Baadhi ya waandishi wa habari wakifuatilia taarifa hiyo wakati Bw James Oigo Kaimu Mkurugenzi wa Uendeshaji Shirika la Taifa la  Hifadhi ya Jamii NSSF akizungumza nao katika mkutano huo.
Baadhi ya maofisa wa shirika hilo wakiwa katika mkutano huo.

Korea Kuleta Walimu wa Sayansi na Hisabati ili Kupunguza Uhaba wa Walimu Nchini

$
0
0

SerikaliI ya Korea imepanga kuleta nchini walimu wa masomo ya hisabati na sayansi kwa shule za sekondari, kusaidia kupunguza uhaba wa walimu wa masomo hayo.

Itatekeleza azma hiyo kupitia Mpango wake wa Kusambaza Walimu wa Kikorea katika nchi Zinazoendelea (KTDP).

Akizungumza jana alipotembelea Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Rais wa Taasisi ya Elimu ya Kimataifa (NIIED), Kim Kwangho, alisema nchi yake imekuwa ikisambaza walimu.

Alisema mpaka sasa wamesambaza walimu 61 katika nchi mbalimbali zinazoendelea; na mwaka huu watasambaza walimu 140 kwa nchi 15.

“Tumeona katika kuunga mkono juhudi za serikali kuongeza walimu wa masomo ya sayansi na kwa mara ya kwanza mwaka huu taasisi yetu itasambaza walimu 10 hapa Tanzania kati yao watano watahusika katika masomo ya hisabati na wengine watano watahusika na masomo ya Sayansi,” alisema Kwang-ho.

Aidha alisema licha ya kusambaza walimu hao, Serikali ya Korea inatoa ufadhili kwa wanafunzi wenye vipaji kimataifa ili kuendeleza masomo yao katika taasisi za elimu ya juu nchini kwao, lengo likiwa ni kusaidia kukuza viongozi wa baadae wenye elimu.

Kwang-ho alisema waombaji wa ufadhili huo ni wale waliosoma tu Shahada ya kwanza na shahada ya Uzamili nchini; na haitawahusu wale wote ambao wamewahi kusoma Korea.

Katika hatua nyingine, Kwang-ho alisema Korea ina mpango wa kufungua kituo cha kutoa kozi ya lugha ya Kikorea katika chuo kikuu hapa nchini, lengo likiwa ni kupanua wigo wa fursa kwa wanafunzi wa Kitanzania kujifunza lugha hiyo.

Kwa upande wake, Kaimu Mkurugenzi wa Masuala ya Mahusiano Kimataifa, Opportuna Kweka alisema tayari rais huyo ameshakutana na Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Profesa Rwekaza Mukandala na kujadili uwezekano wa kuanzisha kituo hicho.

Urusi Kuwekeza Hapa Nchini

$
0
0

Tanzania imewapokea wafanyabiashara 50 kutoka Urusi kuja kuwekeza kwenye sekta mbalimbali nchini.

Akieleza ujio wa wafanyabiashara hao, Katibu Mkuu wa Biashara na Uwekezaji wa Wizara ya Viwanda na Biashara, Adolf Mkenda alisema baada ya kushirikiana kisiasa kwa muda mrefu, Urusi imeamua kuisaidia Tanzania kuimarisha uchumi wake.

Wafanyabiashara hao wanatarajia kukutana leo katika kongamano litakalobainisha fursa zilizopo kwa wageni hao kuwekeza hasa kwenye kilimo, nishati, usafiri, viwanda na madini.

Urusi ni miongoni mwa mataifa 10 makubwa kiuchumi duniani na imeendelea kisayansi na kiteknolojia huku ikiwa na idadi kubwa ya watu.

Rais mstaafu, Jakaya Kikwete wakati akiwaaga mabalozi 36 wa Tanzania, aliwaagiza kulitangaza Taifa huko waliko ili kuvutia wawekezaji na kuwaongezea masoko Watanzania.

Balozi wa Tanzania nchini Urusi, Wynjones Kisamba ameanza kuonyesha njia kwa ugeni huo unaotarajia kuongeza biashara za Taifa hilo.

Mkurugenzi wa Kituo cha Uwekezaji nchini (TIC), Julieth Kairuki alisema Watanzania wana uhakika na soko la mbogamboga, matunda, asali na bidhaa nyingine nchini humo na kwamba kinachotakiwa ni kuongeza ubora ili kukidhi viwango vya kimataifa.

Halmashauri ya Rombo Hatarini Kufutwa

$
0
0

Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Saidi Meck Sadiki amesema Halmashauri Wilaya ya Rombo iko hatarini kufutwa kutokana na kushindwa kufikia lengo la Serikali la kukusanya mapato kutoka kwenye vyanzo vyake.

Sadiki alisema hayo jana wakati akizungumza na madiwani, wenyeviti wa vijiji na wakuu wa idara wa halmashauri hiyo.

Alisema wilaya hiyo inatumia asilimia 93 ya ruzuku kutoka serikalini hali inayosababisha kuwa hatarini kufutwa kwa kushindwa kukusanya mapato.

Mkuu wa wilaya hiyo, Lembris Kipuyo aliitaka halmashauri hiyo kubuni vyanzo vipya vya ukusanyaji wa mapato ili kufikia lengo iliyojiwekea.

Alisema Serikali imetangaza halmashauri ambazo zitashindwa kukusanya mapato na kufikia asilimia 80 ifikapo Juni mwaka huu zitafutwa. 

“Serikali haina lelemama ikifika hiyo tarehe kama mmeshindwa kufikia lengo itafutwa, taarifa nilizonazo mko asilimia 43 hali ambayo ni hatari kwa halmashauri ambayo iko mipakani mwa nchi nyingine,” alisema Sadiki.

Serikali Kununua Magari Mengi Zaidi ya Polisi

$
0
0

Serikali imepanga mwaka ujao wa fedha kununua magari  mengi kwa ajili ya kuyasambaza kwenye vituo tofauti vya Polisi nchini vyenye uhaba.

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga alisema mpango huo utatekelezwa katika bajeti ya mwaka 2016/17.

Alisema hayo wakati akijibu swali la Mbunge wa Igalula, Musa Ntimizi (CCM), aliyehoji kama wizara haioni umuhimu wa kuvipatia magari vituo vya polisi ambavyo havina magari katika jimbo hilo ili kurahisisha utendaji kazi.

Mbunge huyo pia alitaka wizara kumalizia ujenzi wa kituo cha polisi kikubwa kilichojengwa katika kata ya Loya halmashauri ya Tabora (Uyui) ambapo kwa sasa wananchi wameishiwa nguvu ya kuendeleza ujenzi huo.

Waziri alisema, serikali inatambua kazi kubwa inayofanywa na wananchi katika kuchangia maendeleo, alimtaka mbunge huyo kuwasiliana na wizara yake ili waweze kuona namna ya kusaidia kumalizia ujenzi wa kituo hicho ili kianze kufanya kazi.

Katika swali la msingi, mbunge huyo alitaka kufahamu ni lini kituo cha Loya kitafunguliwa hasa ikizingatiwa kuwa Loya ni zaidi ya kilomita 120 kutoka makao makuu ya Wilaya Isikizye ambapo ndiko kwenye kituo cha polisi.

Pia alihoji serikali ina mpango gani wa kuwaongezea bajeti ya mafuta kuwarahisishia watendaji kazi, maana maeneo ya jimbo ni makubwa na yote yanahitaji huduma za kipolisi.

Akijibu swali hilo, Kitwanga alisema pamoja na mwitikio wa wananchi na wadau kujenga kituo hicho, bado hakijakamilika sehemu ya kuhifadhi silaha, huduma ya choo na makazi ya askari.

Waziri huyo alisema, pindi hivyo vitu vitakapokamilika kituo hicho kitafunguliwa na askari watapelekwa.

Alisema, serikali ina mpango wa kuongeza bajeti ya mafuta katika maeneo mbalimbali kulingana na upatikanaji wa fedha, ili kukidhi mahitaji ya doria, misako na operesheni mbalimbali katika kutoa huduma ya ulinzi na usalama kwa wananchi.

Hatifungani "BOND" Ya Benki ya NMB Kuwainua Wananchi Kiuchumi

$
0
0

NMB imeanza kupita kila kona kutoa elimu kwa wananchi na wafanyabiashara kuhusu uwekezaji wa fedha kupitia BOND “Hati fungani”. 

Hati Fungani ni namna moja wapo ya kumpa mwananchi njia mbadala ya kuwekeza pesa zake na kuachana na “vibubu”.
 
Akiongea na waandishi wa habari, Meneja Mawasiliano Mwandamizi wa NMB Bi. Joseline Kamuhanda alisema Hati Fungani ni njia moja wapo ya kuwasaidia wananchi kuachana na tabia ya kuweka pesa zao ndani  bila faida yoyote.
 
“Hati Fungani inampa mwananchi njia mbadala ya uwekezaji wa pesa, fedha utayoiwekeza itakupa faida zaidi kulingana na kiasi cha hati fungani zilizonunuliwa.” alisema.
 
Ili kuweza kuwekeza pesa zako kupitia hati fungani unahitaji kuwa na Central Depository System (CDS account) ambayo inatolewa na Soko la Hisa la Dar es Salaam. Namba hii hutunza kumbukumbu za mteja katika Soko la Hisa na pia hutumika katika kununua na kuuza hisa. 
 
Meneja wa mahusiano ya wawekezaji Bi. Anna Mwasha, akizungumza na waandishi wa habari alisema uwekezaji kupitia hati fungani utawanufaisha wananchi wote ambao  licha ya kutumia nguvu na rasilimali nyingi, hawapati faida wanayostahili kutokana na tabia ya kuwekeza pesa zao kwenye vitegauchumi visivyo na faida ya uhakika.
 
“Ni kitu kizuri kwa kuwa ukiwekeza kwenye hati fungani,  hata utapokuwa unataka pesa yako kabla ya muda wa ukomavu, unaweza kuuza hati fungani hiyo kwenye Soko la Hisa na badala yake, mwananchi mwingine ataendelea kupokea riba mpaka muda wa ukomavu wa hati fungani, hivyo ni kitu ambacho ni kizuri kwa kila mtu”. Alisema Meneja wa mahusiano ya wawekezaji

Madiwani wa Chadema Wilayani Hai Wasusa Kuhudhuria Kikao cha Mkuu wa Mkoa Said Meck Sadiki

$
0
0
Madiwani  wa Halmashauri ya Wilaya ya Hai wakiongozwa na Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo, Helga Mchomvu, wamesusa kuhudhuria kikao cha Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Said Meck Sadiki wakati akizungumza na viongozi wa vitongoji, vijiji, kata, viongozi wa taasisi za serikali na dini.

Sadiki alifika wilayani Hai jana, ikiwa ni moja ya ziara zake katika wilaya zote za Mkoa wa Kilimanjaro kwa ajili ya kujitambulisha pamoja na kuzungumza na viongozi mbalimbali wanaowakilisha wananchi, pamoja na kusikiliza kero zinazozikabili wilaya hizo.

Katika kikao hicho kilichofanyika katika ukumbi wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri, Usharika wa Hai Mjini, madiwani hao ambao wote ni wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) hawakuonekana hata mmoja huku eneo walilokuwa wameandaliwa likibaki na viti vilivyo wazi.

Awali, Mkuu wa Mkoa alipowasili ofisini kwa Mkuu wa Wilaya kwa lengo la kupokea taarifa ya wilaya, Mwenyekiti wa Halmashauri, Mchomvu aliwasili kwa kuchelewa na muda ulipofika wa kuelekea ukumbini, alitokomea kusikojulikana.

Hali hiyo ilimshangaza Mkuu wa Wilaya ya Hai, Gelasius Byakanwa ambaye alisema siasa ziliisha baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 25, mwaka jana, lakini inashangaza kwenye masuala ya maendeleo ya wananchi bado viongozi wanaendelea kuziendekeza.

Byakanwa alisema, licha ya madiwani wote 17 wanaounda Baraza la Madiwani Wilaya ya Hai kuwa ni wa Chadema, bado wanasimamia na kutekeleza Ilani ya Chama Cha Mapinduzi ambacho ndicho chama kilichopewa ridhaa na Watanzania kuongoza kwa awamu nyingine ya tano.

“Ni jambo la kushangaza kuona viongozi waliochaguliwa na wananchi wanashindwa kuwakilisha wananchi wao katika kupeleka na kuzisemea kero zao mbalimbali zinazowakabili, na badala yake wamekuwa wakisusa vikao vya kupanga maendeleo. Kwa siasa hizi wananchi hawawezi kupata maendeleo,” alisema Byakanwa.

Akiwasilisha taarifa za kutofika kwa madiwani hao, Katibu wa Mbunge wa Jimbo la Hai, Rosemary Kuringe alisema, amewasiliana na madiwani wake na kuelezwa kuwa hawakupata taarifa za ziara hiyo ya Mkuu wa Mkoa.

Akijibu baadhi ya maswali yaliyoulizwa na viongozi mbalimbali, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Hai, Saidi Mderu alikiri kutoa taarifa kwa madiwani wote katika kikao cha Baraza Maalumu la Madiwani kilichofanyika Aprili 22, mwaka huu.

“Kwa suala hili la viongozi hawa kususa, namwachia Mungu, niliwapa taarifa madiwani wote tena nilisisitiza, cha kushangaza wakati Mkuu wa Mkoa amewasili kwenye Ofisi ya Mkuu wa Wilaya, Mwenyekiti wa Halmashauri alifika akiwa amechelewa lakini wakati tumekuja kwenye ukumbi hatukumuona,” alisema Mderu.
Mkuu wa Wilaya ya Hai ,Gelasius Byakanwa akizungumza katika kikao hicho.
Mkurugenzi wa Halmshauri ya wilaya ya Hai,Said Mderu akijibu hoja mbalimbali zilizoibuliwa katika kikao hicho.

Wabunge MABUBU Kubanwa Bungeni......Ni Wale Wanaoshiriki Vikao vya Bunge Lakini Hawachangii Chochote

$
0
0

Kiti cha Spika wa Bunge kimesema ipo haja ya kufanya marekebisho ya Sheria pamoja na Kanuni ili kila mbunge apate posho kulingana na kazi aliyofanya bungeni, badala ya utaratibu wa sasa wa kuangalia mahudhurio pekee. 

Aidha, kimewataka wabunge kubadilika na kuacha tabia ya kuchukua posho za vikao vya Bunge bila kuzitolea jasho.

Kauli hiyo imekuja kutokana na Mwongozo ulioombwa Aprili 25, mwaka huu na Mbunge wa Nzega Mjini, Hussein Bashe (CCM) ambaye alikitaka kiti cha Spika kutoa Mwongozo kuhusu usahihi wa wabunge wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni kulipwa posho na mishahara wakati hawashiriki na kutimiza wajibu wao wa kuchangia kwenye mjadala wa Bunge la Bajeti linaloendelea katika Mkutano wa Tatu wa Bunge la 11.

Bashe alisema mbunge huyo alitumia Kanuni ya 68(7) ya Kanuni za Kudumu za Bunge akiomba Mwongozo wa Spika kutokana na Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, kuamua kutoshiriki mjadala unaoendelea bungeni, lakini wabunge hao wanasaini na kulipwa mishahara na posho.

Hivyo akaomba Mwongozo endapo ni haki kwa wabunge hao kupokea posho wakati hawashiriki wala kutimiza wajibu wao wa kisheria. 

Katika kujenga hoja hiyo, Bashe alitumia Ibara ya 63(3) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania isemayo, “Kwa madhumuni ya utekelezaji wa madaraka yake Bunge laweza kujadili utekelezaji wa kila Wizara wakati wa Mkutano wa Bunge wa kila mwaka wa bajeti.”

Aidha, Bashe alitumia Ibara ya 73 ya Katiba ya Tanzania kufafanua kuhusu malipo ya mshahara, posho na malipo mengine kwa wabunge. 

Akitoa Mwongozo wa Spika, Naibu Spika wa Bunge, Dk Tulia Ackson alisema kwa mujibu wa Katiba ya Tanzania, Ibara ya 73 imeainisha masharti ya kazi ya wabunge.

Alisema mbunge anastahili kulipwa mshahara kwa kila mwezi, na kufafanua kuwa mbunge anapohudhuria vikao bungeni na kamati atalipwa posho ya vikao kwa kiwango kitakachowekwa na Serikali na Kanuni za Bunge. 

Alisema malipo ya mshahara ni suala la Kikatiba na Sheria hulipwa kwa mbunge kutokana na kazi yake ya ubunge.

Hivyo malipo ya posho kwa wabunge yanatokana na mahudhurio yao bungeni na siyo kwa kuchangia kama ambavyo wengi wao wanapenda iwe hivyo. 

“Kimsingi kuhudhuria bungeni pekee siyo njia inayopendeza kwa kuwa mbunge anapofika bungeni anatarajiwa atekeleze majukumu yake yalivyoainishwa katika Ibara ya 63.

“…Tabia hii ya kutochangia mijadala na kuzunguka zunguka bungeni haikubaliki na haitakiwi kuendelea, kila mbunge atekeleze wajibu wake na sio anahudhuria ili alipwe posho,” alisema Dk Ackson.

Wakati huo huo, Spika wa Bunge, Job Ndugai amefanya mabadiliko katika Kamati mbalimbali za Bunge, kwa kubadilisha wabunge 16 wa Kamati za Awali kwenda nyingine. 

Aidha, Spika amewapangia Kamati wabunge wapya wanne, walioapishwa mwanzoni mwa Mkutano huu wa Bunge, ambao ni Shamsi Vuai Nahodha, Rita Kabati, Oliver Semuguruka na Lucy Owenya.

Jinsi Punyeto Inavyo Sababisha Ukosefu Na Upungufu Wa Nguvu za Kiume

$
0
0

Ukosefu  na/ama  upungufu  wa  nguvu  za  kiume, ni  tatizo  linalo  wakabili  mamilioni  ya  wanaume  duniani.  Zipo  sababu  nyingi  zinazo  sababisha  tatizo  la  ukosefu  wa  nguvu  za  kiume.  

Miongoni  mwa  sababu  hizo  ni  pamoja  na  maradhi  kisukari, presha,shinikizo  la  damu, moyo, figo, matatizo  kwenye  mishipa  ya  ubongo  &  mishipa  ya  uti  wa mgongo, matatizo  kwenye  mishipa itumikayo  kusafrisha damu  mwilini, maradhi  ya  ngiri,  pamoja  na   upigaji  punyeto  kwa  muda  mrefu.

Katika  makala  yetu  ya  leo, tutaangalia  namna   suala  la  upigaji  punyeto linavyo  athiri  nguvu  za  kiume.

Kabla  hatujaangalia  namna  suala la upigaji  punyeto linavyo  maliza  nguvu  za  kiume, ni  vyema  tukafahamu  kwanza  kuhusu  SAYANSI  YA  MFUMO  WA  NGUVU  ZA  KIUME.

Kufahamu   kuhusu   SAYANSI  YA  MFUMO  WA  NGUVU  ZA  KIUME  tafadhali  tembelea :

Ukisoma  vizuri  kuhusu  mfumo  wa  nguvu  za  kiume, utagundua  kuwa   Suala  la  nguvu  za  kiume  ni  suala  la  kimfumo.  Ili  mwanaume  awe na nguvu  za  kiume, aendelee  kuwa  na  nguvu  za  kiume na  azilinde  nguvu  zake za  kiume, ni  lazima  ogani  zote zinazo  husika  na  mfumo  wa  nguvu  za  kiume  ziwe  na  afya  njema  na  ziwe  na  ushirikiano   thabiti  na  wenye  afya.

Vile  vile , utagundua  kuwa , mambo  makuu  muhimu  katika   mfumo  wa  nguvu  za  kiume  ni  kama  ifuatavyo:

i.Mishipa  imara  ya  ubongo  na  yenye  afya  njema

ii. Mishipa  imara  ya  uti  wa  mgongo  (  spinal  cords )

iii.Mishipa  imara  itumikayo  kusafirisha  damu  mwilini  (  Blood Vessels )

iv. Mfumo  imara  wa  usafirishaji  damu  mwilini

v. Mishipa  ya  uume  iliyo  imara  na  yenye  afya  njema

vi. Uhusiano  imara  na  wenye  afya  kati  ya  mishipa  ya  fahamu  iliyopo  katika  ubongo, mishipa  ya  kwenye  uti  wa  mgongo  pamoja  na  misuli & mishipa  ya  kwenye  uume.

Hivyo  basi, ili  mwanaume  aweze  kuwa  na  nguvu  imara  za  kiume, na  aendelee  kuwa  na  nguvu  hizo ni  lazima  mambo  yote  muhimu  katika  mfumo  wa  nguvu za  kiume  yawe  imara  pasi na  hitilafu  yoyote.

Hitilafu  yoyote  katika  mambo  hayo, itasababisha  ukosefu na/ama  upungufu wa  nguvu  za  kiume  kwa  mwanaume  huyo.  Pale inapotokea    hitilafu  ama  mapungufu  katika  ogani  zaidi  ya  moja  kati  ya  zilizo  tajwa hapo  juu, basi  tatizo  kwa  muhusika  huwa  kubwa  mara  dufu.

JINSI  PUNYETO  INAVYO  SABABISHA  TATIZO  LA  UKOSEFU &  UPUNGUFU  WA  NGUVU  ZA  KIUME.
Mwanaume   anapopatwa na  wazo  la  kufanya  tendo  la  ndoa, ubongo  hutoa  ishara  kwenye  mishipa  ya  uti  wa  mgongo  ambayo  nayo  husafirisha  taarifa  hadi  kwenye  mishipa &  misuli  ya  uume.

Mishipa  ya  uume inapopokea  taarifa  hiyo, hutanuka. Na  mishipa  ya  uume  inapotanuka, hufanya  mambo  mawili  muhimu  sana :

i.Husababisha  mishipa  ya  ateri  kupanuka  na  hivyo  kuruhusu  damu  kuingia kwa  kasi  sana   ndani  ya  mishipa  ya  uume  na  hivyo  kuufanya  uume  usimame  na  kuwa  imara  bara bara.

ii. Huibinya na  kuiziba  mishipa  ya  vena  na  hivyo  kuzuia  kunyonya  ama  kufyonza  damu  iliyo  ingia  ndani  ya  mishipa ya  uume.  (  KAZI  KUBWA  YA  MISHIPA  YA  VENA  ILIYO  KARIBU NA  MISHIPA  YA  UUME  NI KUHAKIKISHA  HAKUNA  DAMU NDANI YA  MISHIPA  YA  UUME. HIVYO  BASI  DAMU  INAPOINGIA  NDANI YA  MISHIPA  YA  UUME, MISHIPA  YA  VENA  HU “SENSE” JAMBO  HILO  KWA  HARAKA  NA HIVYO  KUIFYONZA  DAMU  HIYO  KUTOKA KWENYE MISHIPA  YA UUME  YA  KUITOA  NJE YA MISHIPA  YA  UUME.  NA  DAMU INAPOKOSEKANA  NDANI  YA  MISHIPA  YA  UUME, HUUFANYA  UUME  KUSINYAA  NA  KULEGEA )

Mtu  anayepiga  punyeto  husababisha  mambo  yafuatayo  katika  mwili  wake :

1. Huuwa  nguvu  ya  mishipa  & misuli ya  uume ambayo  ndio  inayo husika  na  kusimama  kwa  uume

2. Mishipa  ya   uume  inapo  sinyaa  na  kukosa  nguvu  yake  ya  asili, husababisha  mambo  yafuatayo :

i.Huondoa  uwezo  wa  mishipa  &  misuli  ya  uume  kutanuka, na  hii  ndio  sababu  inayo  wafanya  waathirika  wa  punyeto  kutumia  nguvu  nyingi  sana  katika  kuufanya  uume  usimame.

ii.Huondoa  uwezo  wa  mishipa &  misuli  ya  uume  kuibana  na  kuiziba  mishipa  ya  vena, na  hii ndio  sababu  inayo  fanya  waathirika  wa  punyeto  kufika  kileleni  haraka  sana, kwani damu  inayo  ingia  kwenye misuli  ya  uume   hufyonzwa  ndani ya  muda  mfupi sana. 
 
 Hii  hutokea  kwa  sababu  mishipa na  misuli  ya  uume inakuwa  imelegea,na  mishipa  ya  vena inakuwa  imepwaya, hivyo  msuguano wowote ule  hufanya  mishipa  ya  vena  kufunguka  na  kufyonza  damu  kutoka  kwenye mishipa  ya  uume  na hivyo  kuufanya  uume  kusinyaa  ndani ya dakika ama sekunde  chache sana.

3. Vile  vile  punyeto  hufanya  uume  kusinyaa na  kurudi ndani  na  kuufanya  uonekane kama  uume  wa  motto mdogo.

Kwa  ufupi  punyeto  husababisha  ukosefu  wa  nguvu  za  kiume  kwa  sababu  kuu  zifuatazo :

i.Kwanza   hudhoofisha  na  kuharibu  mishipa  ya  uume,  ambayo  ndio  hufanya  uume kusimama.

ii.Pili  hudhoofisha  utendaji  kazi  wa  mishipa  ya  ateri, ambayo  ndio  hutumika  kama  njia  ya  kusafirisha  damu kupeleka kwenye  misuli  ya  uume  na  ivyo  kuufanya  uume  usimame

iii. Tatu, punyeto  hupelekea  kuvuja  kwa  mishipa  ya  vena  na  hivyo  kusababisha  damu  kufyonzwa  kwa  haraka  sana  kila  iingiapo ndani  ya  misuli ya  uume  na  matokeo  yake  ni  uume   kusimama  kwa  muda  mfupi  sana  wakati wa  tendo  la  ndoa.

iv. Punyeto  huathiri  mtiririko  wa  damu  kwenda  kwenye  mishipa  ya  uume, kwa  sababu  hudhoofisha  misuli &  mishipa  ya  uume  pamoja  na mishipa ya  ateri  ambayo  ndio  hutumika  katika  kusafirisha  damu kwenda  kwenye  uume

DALILI  ZA  MTU  ALIYE  ATHIRIWA  NA  PUNYETO
Dalili  kuu  za  mtu  aliye athiriwa  na  punyeto  ni  kama  ifuatavyo:

i.           Uume  kusinyaa  na  kuwa  kama  wa  mtoto
ii.         Uume kurudi  ndani
iii.       Uume  kusimama  ukiwa  legelege
iv.       Kufika  kileleni  haraka  wakati  wa  tendo  la  ndoa.

TIBA   YA   NGUVU  ZA  KIUME  KWA MTU  ALIYE  ATHIRIKA  NA  PUNYETO.
Dawa   asilia  ya  nguvu  za  kiume iitwayo JIKO  ni tiba  bora  na  ya  uhakika  kabisa  kwa  mtu  aliye  athiriwa   na  punyeto.  Dawa  hii, pamoja  na  mambo  mengine  mengi, husaidia  kufanya  mambio  yafuatayo  katika  mwili  wa  mwanaume  aliye  athiriwa  na  punyeto :

i.Kuimarisha  mishipa  & misuli  ya  uume  ulio  legea na  hivyo  kuurejeshea  uwezo wake wa  asili

ii. Hutibu   tatizo  la  uume  kurudi  ndani

iii.Humaliza  tatizo  la  kusimama  kwa  uume  ukiwa  legelege

iv.Hutibu  na  kuponya  kabisa  tatizo  la  kufika  kieleleni  haraka.

BEI  YA  DAWA  :  Dawa  hii  inapatikana  kwa  gharama  ya  SHILINGI  ELFU  THEMANINI  TU (Tsh. 80,000/=)

MAHALI  INAPOPATIKANA :  Dawa  hii  inapatikana  katika  duka  la  dawa  asilia  liitwalo  NEEMA  HERBALIST  &  NUTRITIONAL  FOODS  CLINIC  lililopo  jijini  DAR  ES  SALAAM  katika  eneo  la  UBUNGO   nyuma  ya  jengo  la  UBUNGO  PLAZA   karibu  na SHULE  YA  MSINGI  UBUNGO  NATIONAL  HOUSING.

Kwa  wateja  wasio  weza  kufika  ofisini  kwetu. Watafikishiwa  dawa  mahali  popote  walipo  jijini  DAR  ES  SALAAM.

Kwa   wateja  waliopo  mikoani  watatumiwa  dawa  kwa  njia  ya  MABASI

Kwa  wateja  waliopo   Zanzibar  wata fikishiwa  dawa  kwa  njia  ya  usafiri  wa boti.

Na  kwa  wateja  waliopo  UGHAIBUNI  watatumiwa  dawa  kwa  njia  ya  POSTA  ama  DHL.

MAWASILIANO :  WASILIANA  NASI   KWA  SIMU  NAMBA  0766  53  83  84.

Kwa  taarifa  zaidi  kuhusu  huduma  zetu, tutembelee kila  siku  kwenye  blogu  yetu :

Serikali Kuwasilisha Mswada wa Sheria ya Ndoa

$
0
0

Serikali   imejiandaa kuleta Muswada wa Sheria bungeni kutoa haki ya kusoma kwa watoto wote wa kike na kiume wa shule za msingi, sekondari na kutoruhusiwa kuoa au kuolewa.

Aidha, Waziri wa Katiba na Sheria, Dk Harrison Mwakyembe amesema serikali inaendelea kukamilisha utaratibu wa kupata maoni ya wananchi kuhusu marekebisho ya Sheria ya Ndoa na kutungwa kwa Sheria mpya ya Mirathi na Urithi kuondokana na mkanganyiko uliopo kuhusu sheria hiyo.

Bunge lilielezwa hayo jana mjini Dodoma wakati waziri huyo akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Ileje, Janeth Mbene (CCM) aliyehoji ni lini serikali itaanza maandalizi ya kuchukua maoni juu ya kufanya marekebisho sheria ya ndoa ya mwaka 1971.

Akijibu swali hilo, Dk Mwakyembe alisema hatua za awali zimeshaanza kuchukuliwa na wizara hiyo ili kupata maoni ya wananchi juu ya marekebisho ya sheria hiyo ya ndoa ya mwaka 1971 na kutungwa kwa sheria mpya ya mirathi na urithi.

Alisema serikali ina nia ya dhati ya kufanyia marekebisho sheria ya ndoa na kwamba mchakato huo ulisitishwa kwa kuwa Tume ya mabadiliko ya Katiba ilikuwa ikikusanya maoni kuhusu mabadiliko ya katiba , hivyo walidhani wananchi wangetoa pia maoni juu ya sheria hiyo.

Rais Magufuli Atengua Uteuzi wa Mkurugenzi Mtendaji wa TIC

$
0
0

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, ametengua uteuzi wa Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji nchini (TIC), Bi. Juliet Kairuki kuanzia tarehe 24 Aprili mwaka huu.

Taarifa iliyotolewa na kwa vyombo vya habari na Katibu Mkuu wa Biashara na Uwekezaji, Prof. Adolf Mkenda, imesema kuwa hatua hiyo imekuja baada ya rais Dkt. Magufuli kupata taarifa kuwa Mkurugenzi huyo alikua hachukui mshahara wa serikali tangu alipoajiriwa mwaka 2013 jambo ambalo linazua maswali mengi.

Aidha, taarifa hiyo iliyosainiwa na Katibu Mkuu huyo imeongeza kuwa endapo Bi. Kairuki atakuwa tayari kuendelea kufanyakazi na Serikali ya Awamu ya Tano atapangiwa kazi nyingine. Mchakato wa kumpata Mkuregenzi mpya umeanza mara moja.

Kwa mujibu wa Prof. Mkenda kwenye taarifa yake hiyo amesema Bw. Clifford Katondo Tandali, atakaimu nafasi ya Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo hicho cha Uwekezaji nchini TIC.

Vipaza Sauti Vya Bunge Vyaharibika, Bunge Lasimama kwa Dakika 30

$
0
0
Shughuli za Bunge la Muungano leo zilisimama kwa dakika 36 kabla ya kuendelea tena, baada ya vipasa sauti vya ukumbini kushindwa kufanya kazi.

Spika wa Bunge, Job Ndugai amelazimika kuahirisha shughuli mara baada ya kipindi cha maswali ya papo kwa hapo kwa Waziri Mkuu ambacho hata hivyo wabunge walichukua muda mrefu kuuliza maswali kutokana na kuhama hama wakitafuta mahali pa kusikika.

Awali, wabunge waliokuwa na nafasi ya kuuliza maswali  walilazimka kuhama maeneo yao na kuzua minong’ono ndani ya ukumbi, huku Mbunge wa Mkuranga (CCM), Abdallah Ulega na Mbunge wa Manonga (CCM), Seif Gulamali wakilazimika kuuliza maswali yao wakiwa uso kwa uso na Waziri Mkuu mbele ya ukumbi.

Hata hivyo, kuna hali ya sintofahamu, kwani vipaza sauti vimeharibika ikiwa ukumbi huo umefanya kazi kwa siku sita tu tangu ulipokabidhiwa baada ya ukarabati mkubwa.

April 18, Naibu Spika wa Bunge, Dk Tulia Ackson alikabidhiwa ukumbi huo ikielezwa kuwa ulikuwa umefanyiwa matengenezo makubwa katika maeneo mbalimbali kwa lengo la kuuboresha.

Watu Watatu Wanaosadikiwa Kuwa Majambazi Wauawa Katika Jaribio La Uhalifu Wilayani Chunya Mkoani Mbeya

$
0
0
JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA.
Mnamo tarehe 27.04.2016 majira ya saa 20:00 usiku huko katika Kijiji na Kata ya Matundasi, Tarafa ya Kiwanja, Wilaya ya Chunya, Mkoa wa Mbeya, watu watatu wanaosadikiwa kuwa majambazi waliuawa katika majibizano ya risasi na askari polisi wakiwa katika harakati za kufanya uhalifu kwenye duka bia la jumla mali ya bwana HAMIS mkazi wa Matundasi.

Inadaiwa kuwa majambazi hao wapatao watano walikuwa wakitumia pikipiki mbili huku pikipiki moja ikibeba majambazi watatu na nyingine majambazi wawili huku wakiwa na silaha aina ya SMG yenye namba 1996 AFU 1120 na risasi 26 kwenye magazine walitaka kufanya uhalifu kwenye duka la jumla la kuuza bia mali ya HAMISI.

Kutokana na taarifa za siri/intelejensia, Jeshi la Polisi lilijipanga kukabiliana na majambazi hao na katika majibizano ya risasi, jambazi mmoja ambaye alikuwa na silaha aina ya SMG yenye namba 1996 AFU 1120, risasi 26 kwenye magazine aliuawa baada ya kujeruhiwa kwa kupigwa risasi tumboni na mguuni na aliweza kufahamika kwa jina moja BARAKA, anayekadiliwa kuwa na umri kati ya 35 hadi 38, fundi ujenzi mkazi wa Makongolosi.

Aidha majambazi wengine wanne walifanikiwa kukimbia kuelekea kijiji cha Matondo na ndipo askari polisi waliendesha msako mkali kuelekea kijiji hicho na majambazi hao baada ya kuwaona Polisi waliwasha pikipiki zao kwa nia ya kukimbia huku wakirusha risasi ovyo ndipo Polisi walijibu mapigo na kufanikiwa kuwaua majambazi wengine wawili na kukamata Pikipiki moja yenye namba ya usajili MC 761 AFS aina ya Sanlg iliyokuwa ikitumiwa na majambazi hao.

Majambazi wengine wawili walikimbia na msako mkali unaendelea ili kuwakamata. Miili ya marehemu imehifadhi katika Hospitali ya Wilaya Chunya.

Wito:
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Mrakibu Mwandamizi wa Polisi Butusyo A. Mwambelo anatoa wito kwa wananchi kuendelea kushirikiana na Jeshi la Polisi kwa kutoa taarifa za siri ili kuzuia vitendo vya kihalifu mapema kabla ya kutokea.

Imesainiwa na:
 [BUTUSYO A. MWAMBELO – SSP]
KAIMU KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA. 

Appointment To The Chairman, Vice Chairman And Board Members Of The Tanzania Communication Regulatory Authority (TCRA)

Mwili wa Papa Wemba wawasili DRC

$
0
0
Mamia ya watu wamekusanyika leo nje ya uwanja wa ndege wa Kinshasa kuupokea mwili wa mwanamuziki Papa Wemba uliowasili nchini humo kutoka Abidjan

Mwanamuziki huyo ambaye ametajwa kuwa mmoja ya waanzilishi wa muziki wa kizazi kipya cha Soukous  alifariki dunia April 24 baada ya kuanguka jukwaani akiwa anatumbuiza huko Ivory Coast  

Papa Wemba anatarajiwa kuzikwa  siku ya Jumanne  ya wiki ijayo

Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images