Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Mwanasheria Mkuu Zanzibar Aapishwa Rasmi Leo

$
0
0
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein leo amemuapisha Bwana Said Hassan Said, kuwa Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar. 

Rais wa Zanzibar na Mwenyeikiti wa Baraza la Mapinduzi alimteua Bwana Said Hassan jana kushika wadhifa huo kwa mujibu wa uwezo aliopewa chini ya Kifungu cha 55 (1) cha Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984.
 
Hafla ya kumuapisha Mwanasheria Mkuu huyo ilifanyika Ikulu Mjini Zanzibar na kuhudhuriwa na viongozi mbali mbali wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar. 
 
Miongoni mwao ni Jaji Mkuu wa Zanzibar Mhe. Omar Othman Makungu, Katibu Mkuu Kiongozi na Katibu wa Baraza la Mapinduzi Dk. Abdulhamid Yahya Mzee, Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Mhe. Abdalla Mwinyi Khamis. 
 
Wengine ni Naibu Kadhi Mkuu wa Zanzibar Sheikh Hassan Othman Ngwali, Naibu Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh Mahmoud Mussa Wadi, Meya wa Manispaa ya Mji wa Zanzibar Khatib Abrahman Khatib,Washauri wa Rais wa Zanzibar na viongozi wengine wa Serikali. 
Viongozi mbali mbali na watendaji waliohudhuria katika hafla ya kuapishwa Said Hassan Said kuwa Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar katika ukumbi wa mikutano Ikulu Mjini Zanzibar leo asubuhi.

Watu Wawili Wauawa Na Majambazi Jijini Mwanza. Wengine Saba Wajeruhiwa.

$
0
0

Watu wawili wameuawa Jijini Mwanza kwa kupigwa risasi na Majambazi, huku Wengine saba wakijeruhiwa katika tukio la uvamizi wa duka lililokuwa likitoa huduma mbalimbali za kifedha.

Kamanda wa Polisi Mkoani Mwanza, Justus Kamugisha, amesema kuwa tukio hilo lilitokea jana majira ya saa mbili usiku katika eneo la Bugarika Sokoni, baada ya watu watatu wanaosadikika kuwa ni majambazi waliokuwa na bunduki aina ya SMG kuvamia katika duka la mfanyabiashara na mkazi wa eneo hilo aitwae Daniel Marwa (30).

Kamanda Kamugisha amewataja waliouawa kuwa ni Julius Wankaba (30) ambae ni dereva bodaboda, pamoja na mfanyabiashara mmoja mwenye duka katika eneo hilo aliefahamika kwa jina la Mama Yuni (35).

Amewataja waliojeruhiwa kuwa ni Magesa Mungari (38), Simioni Charles (26) ambao wamelazwa katika Hospitali ya Rufaa Bugando huku wengine wakiwa ni Mwita Ryoba (30), Frank Willium (19), Saumu Said (20), Masumbuko Kanduru (38) pamoja na Emmanuel Francis ambao wanapata matibabu katika Hospital ya Rufaa ya Mkoa wa Mwanza Sekour Toure.

Baadhi ya Mashuhuda wa tukio hilo, akiwemo mmiliki wa duka lililovamiwa, wanasema majambazi hao walipofika eneo la tukio walianza kufyatua risasi ovyo ili kuwatawanya wananchi waliokuwa wamekusanyika katika eneo hilo wakiangalia taarifa ya habari na wengine wakinywa kahawa,  na hivyo kusababisha wananchi kutawanyika jambo lililosababisha vifo na majeruhi hao.

Katika tukio hilo, Majambazi hao walifanikiwa kupora fedha taslimu kiasi cha Shilingi Milioni Mbili, Vocha za simu za mitandao mbalimbali zinazokadiliwa kuwa za shilingi Laki Nane pamoja na simu sita za wateja.

Kamanda Kamugisha amesema Jeshi la polisi Mkoani Mwanza limeanzisha msako mkali ili kuwakamata waliohusika na tukio hilo, huku likiahidi zawadi ya fedha kiasi cha shilingi Milioni Moja kwa yeyote atakaesaidia kufanikiwa kukamatwa kwa watuhumiwa hao.

Wakati huo huo, Jeshi la Polisi Mkoani Mwanza linaendelea kumsaka mtu aliehusika na wizi wa mtoto mwenye umri wa siku moja katika Hospitali ya Wilaya ya Magu, ambapo tukio hilo limetokea Machi 23 mwaka huu, majira ya saa nane mchana baada ya mtu mmoja asiefahamika mwenye jinsia ya kike, kufika katika wodi ya wazazi na kumuiba mtoto huyo wakati mama yake amelala.

Aidha katika katika kusherehekea Sikukuu ya Pasaka, Jeshi hilo limepiga marufuku watoto kwenda kuogelea katika fukweni (Beach) pamoja na uwepo wa disko toto Jijini Mwanza.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumapili Ya March 27

Serikali Ya Tanzania Haina Mpango Kwa Kuteketeza Meno Ya Tembo Yaliyohifadhiwa

$
0
0

Serikali ya Tanzania imetoa tamko kuwa kwa sasa haina mpango wowote wa kuteketeza meno ya tembo yaliyohifadhiwa ambayo yametokana na vitendo vya ujangili na vifo asilia vya tembo.

Tamko hilo limetolewa hivi karibuni na Waziri wa Maliasili na Utalii Prof. Jumanne Maghembe akizungumza na Balozi wa Marekani hapa nchini Bw. Mark Childress alipotembelewa na balozi huyo ofisini kwake kujadili maendeleo ya sekta ya Maliasili mchini.

Prof. Maghembe alisema hayo baada Balozi huyo wa Marekani hapa nchini kutoa pendekezo kwa Serikali ya Tanzania kuchoma sehemu meno ya tembo yaliyohifadhiwa ili kutoa ujumbe mzito duniani juu ya dhamira ya Serikali kukomesha biashara hiyo haramu.

"Naomba niweke wazi kuwa kwa sasa hatupo tayari kuteketeza meno haya, tunaweza kuyatumia kwenye tafiti za kisayansi au vielelezo kwa ajili ya kesi za ujangili ambazo zipo mahakamani na nyingine ambazo bado zinafanyiwa uchunguzi" Alisema Prof. Maghembe.

Zipo nchi mbalimbali duniani ambazo zimechukua hatua ya kuteketeza meno yake ya tembo yaliyohifadhiwa ikiwemo nchi jirani ya Kenya na Malawi ambapo inaaminika kuwa kufanya hivyo ni njia mojawapo ya kushawishi Ulimwengu kukomesha biashara hii haramu ya meno ya tembo.

Nchi nyingine ni Chad, Ubelgiji, Ufaransa, China, India, Marekani na Ureno. Kwa upande wa nchi ambazo zina msimamo sawa na Tanzania katika kuendelea kuhifadhi meno yake ya Tembo ni pamoja na Afrika ya Kusini, Botswana na Zimbabwe.

Akizungumzia kuhusu kuendeleza sekta ya Maliasili nchini, Prof.Maghembe amemuomba Balozi wa Marekani Bw. Mark Childress kushirikiana na Serikali ya Tanzania katika kukuza sekta hiyo kwa kuleta wawekezaji mbalimbali kutoka Marekani kuja kuwekeza Tanzania pamoja na kusaidia kwenye mapambano dhidi ya Ujangili.

Aliongeza kuwa Tanzania ina fursa nyingi ambazo zinahitaji uwekezaji mkubwa ikiwemo hoteli za kitalii, fukwe za kisasa na kuendeleza vivutio mbalimbali vilivyomo hapa nchini.

Prof. Maghembe amemshukuru balozi huyo kwa misaada mbalimbali kutoka Serikali ya Marekani ya kuendeleza sekta ya Maliasili nchini ukiwemo wa hivi karibuni wa mbwa maalum (Snifer Dogs) kwa ajili ya kusaidia utambuzi wa rasilimali za Maliasili zinazoweza kutoroshwa nje ya nchi kupitia bandari na viwanja vya ndege.

Katika taarifa iliyowasilishwa kwenye kikao baina ya Waziri wa Maliasili Prof. Jumanne Maghembe na Balozi wa Marekani hapa nchini Bw. Mark Childress imeonesha kuwa katika kipindi cha miaka mitano iliyopita Serikali ya Marekani imetoa misaada mbalimbali ambayo jumla yake ni dola za kimarekani Milioni 41.35 katika kusaidia eneo la uhifadhi hapa nchini.

Akizungumzia mahusiano baina ya Tanzania na Marekani Balozi Mark Childress alimueleza Prof. maghembe kuwa Serikali ya Marekani itaendeleza mahusiano mazuri yaliyopo baina ya nchi hizi mbili ambapo pia ofisi yake ya ubalozi imeshatafuta wadau mbalimbali ambao wapo tayari kusaidia fedha, vifaa na mafunzo kwa ajili ya kuimarisha uhifadhi na mapambano dhidi ya ujangili.

Ajali ya Lori Yaua watu 7 na Kujeruhi 10

$
0
0

WATU saba wamekufa na wengine 10  k u j e r u h i w a baada ya gari walilokuwa wanasafiri nalo aina ya Mitsubishi Fuso kupasuka tairi la mbele na kugonga kingo za barabara katika barabara kuu ya Igunga-Singida.

Wengi wao walikuwa wafanyabiashara ya samaki waliokuwa wakitokea Igunga kwenda kijiji cha Loya wilayani Uyui, Tabora.

Kutokea kwa ajali na vifo hivyo kumethibitishwa na Kamanda wa Polisi mkoa wa Tabora, Khamis Selemani Issah aliyesema ilitokea majira ya saa tatu usiku katika kijiji cha Nanga, kata ya Nanga wilaya ya Igunga.

Alisema lori hilo lenye namba za usajili T 124 ACS lilibeba abiria wengi kinyume na sheria za usafirishaji wa abiria na kuongeza kuwa hatua kali zitachukuliwa kwa watakaobanika kubeba abiria katika magari ya mizigo.

Mara baada ya ajali hiyo, dereva wake aliyetajwa kuwa ni Joseph Masali alitoweka eneo la tukio na jeshi la polisi linamtafuta aweze kujibu tuhumu zinazomkabili kuhusiana na ajali hiyo.

Kamanda huyo aliendelea kusema ajali hiyo imesababishwa na uzembe wa dereva kutokana na mwendo kasi pamoja na pia kwa kuvunja sheria ya kubeba abiria kwa gari la mizigo.

Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Wilaya ya Igunga, Abdallah Ombeni alipokea majeruhi 11 na miili 6 katika hospital hiyo huku majeruhi mmoja alisafirishwa katika Hospital ya Rufaa ya Nkinga kwa matibabu zaidi kutokana na hali yake kuwa mbaya, hata hivyo alifariki dunia akiwa njiani.

Amewataja waliokufa kuwa ni Masesa Sagalali, Omar Rajabu, Shaaban Ibrahim, Sagalali Maige, Selestine Lipande, Juma Iddi na mwingine aliyetambulika kwa jina mmoja la James. Juma Hassan, mmoja wa majeruhi wa ajali hiyo alisema chanzo cha ajali hiyo ni mwendokasi.

Mtoto wa Siku Moja Aibwa Hospitali ya Rufaa ya Bugando

$
0
0

Mtoto wa siku moja ameibwa katika mazingira ya kutatanisha katika Hospitali ya Rufaa ya Bugando, akiwa pembeni mwa mama yake aliyekuwa amelala, mwenye umri wa miaka 16.

Akizungumzia uporaji huo jana, Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mwanza, Justus Kamugisha, amesema aliyepora mtoto huyo aliingia ndani ya wodi ya wazazi ya Hospitali ya Rufaa ya Bugando, akiwa amejifunga ushungi.

“Alipoingia wodini alikuta mama wa mtoto amesinzia akiwa peke yake wodini, ndipo akamuiba mtoto wake wa kike mwenye umri wa siku moja na kuondoka naye kwenda kusikojulikana,” alisema.

Kwa mujibu wa Kamanda Kamugisha, Jeshi la Polisi limeanza uchunguzi wa tukio hilo kwa kuhoji wauguzi, walinzi na wazazi waliokuwa wamelazwa wodini hapo.

Katika hatua nyingine, Kamanda Kamugisha amesema Jeshi la Polisi mkoani humo, litaanza kufanya uhakiki wa silaha kuanzia Aprili mosi hadi Juni 30 mwaka huu, katika ofisi za makamanda wa Polisi wa wilaya zote za Mkoa wa Mwanza.

Amesema uhakiki wa silaha ni wa kitaifa na utahusu wamiliki binafsi, kampuni binafsi na taasisi mbalimbali za Serikali na zisizo za kiserikali zinazomiliki silaha.

“Lengo ni kupata kumbukumbu ya uhalali wa umiliki wa silaha. Watu wote wanaomiliki silaha watii agizo hili bila kulazimishwa, ili tufanikishe uhakiki kwa wakati na tuimarishe usalama katika mkoa wetu,” alisema.

Aliwataka watu wanaomiliki silaha isivyo halali, kusalimisha silaha hizo wenyewe kwenye ofisi za Serikali na kwa wakuu wa Polisi wa wilaya (OCD) kabla ya muda wa uhakiki wa silaha kumalizika.

“Baada ya hapo tutafanya msako kabambe wa watu waliokaidi kuhakiki silaha zao,” alisema.

Madereva Watatu wa Malori Wajeruhiwa Kwa Risasi na Mlinzi wa Hoteli

$
0
0

Madereva watatu wa malori yaendayo mikoani na wasaidizi wao watatu, wamenusurika kifo baada ya kupigwa risasi sehemu mbalimbali za mwilini na mlinzi wa nyumba moja ya wageni iliyopo Ubena, Chalinze mkoani Pwani.

Tukio hilo limetokea jana alfajiri saa 11.30 kwenye hoteli hiyo ambako madereva na wasaidizi hao walikuwa wamefikia kwa mapumziko kabla ya kuendelea na safari. 

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani, Boniventura Mushongi alisema tukio hilo lilitokea baada ya kuwapo kutokuelewana kati ya mmoja wa madereva na mlinzi wa nyumba hiyo.

Kamanda Mushongi alisema taarifa za awali zinasema baada ya mabishano hayo ambayo bado hayajajulikana chanzo chake, mlinzi huyo alikoki silaha yake aina ya Shortgun na kupiga risasi moja hewani kutuliza vurugu na kumjeruhi mmoja wa madereva hao.

Hata hivyo, mabishano yalizidi baada ya madereva wengine kujitokeza kuingilia ndipo mlinzi huyo akapiga risasi nyingine ambayo ilitoka na gololi zake kusambaa na kuwajeruhi wengine wanne ambao walipelekwa Kituo cha Afya Chalinze kwa matibabu.

Alisema mlinzi huyo amekimbia na anaendelea kutafutwa na chanzo cha tukio hilo kinachunguzwa.

Mganga Mkuu wa Hospitali ya Chalinze, Dk Victor Bamba alisema walipokea majeruhi watano ambao walipatiwa huduma ya kwanza na kutokana na hali zao kuwa mbaya walihamishiwa Hospitali ya Tumbi.

Akizungumza wodini Tumbi walikolazwa, mmoja wa madereva hao, Harun Adeli alisema walifika hapo juzi saa mbili usiku na kuamua kulala ndani ya magari yao ili jana waendelee na safari na ilipofika saa kumi na moja alfajiri walisikia makelele yanayoashiria ugomvi ndani ya hoteli hiyo.

“Wakati tunashangaa tulishtukia risasi zinarindima na ndipo zilipotufikia,” alisema.

Muuguzi wa zamu katika Hospitali ya Tumbi, Habibu Yahaya alisema aliwapokea majeruhi Stephen Fredy, Beno Henry, Akrey Dallu, Ramadhani Saidi, Amani Almasi na Adel wote wakazi wa Dar es Salaam.

Diwani wa Ubena, Nicolaus Muyunga alisema kwa mujibu wa majirani, yalitokea mabishano kati ya utingo na dereva ambao walikuwa wamekunywa na kulala kwenye meza muda mrefu, walipotakiwa kuchukua vyumba wakalale ndani au warudi katika magari yao walikataa na mlinzi alipotaka kuwaondoa kwa nguvu walimzidi nguvu, hivyo akajitetea kwa kupiga risasi hewani.

Rais Magufuli Ahudhuria Ibada Ya Pasaka Kanisa La Kkkt La Azania Front Jijini Dar Es Salaam Leo

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akilakiwa na Askofu Mkuu wa Dayosisi ya Mashariki na Pwani Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania Dkt. Alex Malasusa alipowasili kwa Ibada ya Pasaka katika Kanisa la KKKT la Azania Front jijini Dar es salaam leo Machi 27, 2016

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli na Mkewe Mama Magufuli wakishiriki na waumini wengine Ibada ya Pasaka katika Kanisa la KKKT la Azania Front jijini Dar es salaam leo Machi 27, 2016
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akisalimia waumini huku akisikilizwa na Askofu Mkuu wa Dayosisi ya Mashariki na Pwani Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania Dkt. Alex Malasusa na Mchungaji Chalres Mzinga baada ya Ibada ya Pasaka katika Kanisa la KKKT la Azania Front jijini Dar es salaam leo Machi 27, 2016
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli  na Mkewe Mama Janeth Magufuli pamoja na Mama Rebecca Malasusa na Askofu Mkuu wa Dayosisi ya Mashariki na Pwani Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania Dkt. Alex Malasusa baada ya Ibada ya Pasaka katika Kanisa la KKKT la Azania Front jijini Dar es salaam leo Machi 27, 2016
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli  akiwapungia waumini baada ya  Ibada ya Pasaka katika Kanisa la KKKT la Azania Front jijini Dar es salaam leo Machi 27, 2016
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli  akisalimiana na mtoto Javiera Lyimo (9) anayesoma darasa la tano shule ya Genesis jijini  baada ya  Ibada ya Pasaka katika Kanisa la KKKT la Azania Front jijini Dar es salaam leo Machi 27, 2016.

Rais Magufuli aitakia heri Taifa Stars dhidi ya Chad

$
0
0

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ameitakia heri timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) katika mchezo wake dhidi ya Timu ya Taifa ya Chad, utakaofanyika katika uwanja wa Taifa Jijini Dar es salaam, kesho tarehe 28 Machi, 2016. 

Taifa Stars itacheza mchezo huo wa marudiano, ikiwa ni wiki moja tangu ilipocheza mchezo wa kwanza, katika Jiji la N’Djamena nchini Chad ambapo Taifa Stars ilishinda bao 1–0. 

Katika salamu hizo Rais Magufuli amewataka wachezaji, benchi la ufundi na viongozi  wa Shirikisho la Soka hapa nchini (TFF), kutambua kuwa watanzania wana matumaini makubwa kuwa timu yao itafanya vizuri katika mchezo huo, ikiwa ni  juhudi za kutafuta tiketi ya kufuzu kucheza fainali za kombe la soka barani Afrika, zitakazofanyika Gabon hapo Mwaka ujao wa 2017.
 
“Watanzania wote tuiombee timu yetu ifanye vizuri ushindi wa Taifa Stars ni heshima kwa nchi yetu na sifa muhimu kimataifa mimi naamini kama tulishinda N’Djamena tunao uwezo wa kushinda hapo kesho” amesisitiza Rais Magufuli 

Gerson Msigwa 
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
Dar es salaam 
27 Machi, 2016

Rais Magufuli Awataka Watanzania kuwa Wamoja

$
0
0

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amewasihi watanzania kuendelea kuwa wamoja na kushirikiana kuijenga nchi yao, badala ya kubaguana.

Rais Magufuli ametoa wito huo leo katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Usharika wa Azania Front Jijini Dar es salaam, ambako amesali ibada ya Pasaka pamoja na waumini wa kanisa hilo.

Amesema Mwenyezi Mungu alimtoa mwanae wa pekee Yesu Kristo kuja kuikomboa dunia bila kuwabagua wanadamu, vivyo hivyo nasi binadamu tunapaswa kutobaguana, iwe kwa dini zetu, makabila yetu, mitazamo ya kisiasa na hata rangi zetu.

Aidha, Rais Magufuli amewakumbusha watanzania kufanya kazi kama ambavyo vitabu vitakatifu vinasisitiza umuhimu wa kufanya kazi, na amebainisha kuwa Tanzania yenye neema inawezekana endapo kila mtu atazingatia kufanya kazi.

“Tukifanya kazi hatuhitaji hata misaada kutoka nje, nchi hii ina neema nyingi. Kwa kweli tukifanya kazi kwa bidi nchi yetu inapaswa kuwa inatoa misaada kwa nchi nyingine na sio kuomba misaada kutoka nchi nyingine” Amesisitiza Dkt. Magufuli.

Rais Magufuli ambaye amesali kwenye kanisa hilo kwa mara ya kwanza tangu achaguliwe kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, lakini ikiwa ni mara yake ya nne kusali katika kanisa hilo hata kabla ya kuwa Rais, amewaomba watanzania kuendelea kuliombea Taifa lao na pia kumuombea yeye ili afanikiwe kutekeleza jukumu kubwa na zito la kuiongoza nchi.

Pamoja na kuongoza maombi ya kumuombea Rais Magufuli na Mkewe Mama Janeth Magufuli waliohudhuria ibada hiyo, Askofu Mkuu wa KKKT Dayosisi ya Mashariki na Pwani, Dkt. Alex Malasusa amempongeza Rais Magufuli kwa tabia yake ya kupenda kuhudhuria ibada na kuwasihi viongozi wengine kupenda ibada.

Askofu Malasusa ameuelezea ufufuo wa Yesu Kristo kuwa jambo la kuleta  matumaini, na hivyo amepongeza mwelekeo wa nchi kwa sasa, huku akisema Kanisa linaona matumaini kwa Taifa.

Serikali Yaanda Muongozo wa Ajira kwa Vijana

$
0
0

Kutokana na Tanzania kuwa na uchumi wa soko huria vijana wengi wameanza kushiriki katika sekta isiyo rasmi hivyo kunawafanya kuchangia nusu ya uchumi wa Taifa katika shughuli zao za kila siku.

Hayo yamesemwa na mkurugenzi msaidizi wa Taasisi ya Soko la Ajira Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu Ahmed Makbel wakati akizungumza kuhusu mikakati mbalimbali na hatua zilizoanza kuchukuliwa na serikali  ili kuhakikisha inawainua vijana kiuchumi.

Makble amezitaka taasisi zisizo za kiserikali kushirikiana na Serikali ili waweze kutekeleza maagizo ya Rais Dkt. John Pombe Magufuli na kuhakikisha vijana wanafanya kazi zenye staha na kipato kizuri pamoja na mazingira mazuri ya kazi.

Mkurugenzi huyo amesema serikali imeanza kufanyia kazi baadhi ya mapendekezo ya wadau wa maendeleo kuhusu kuwainua vijana kuanzia kwenye vipato vyao vya kila siku sambamba na kuhakikisha fedha mbalimbali zinazotolewa na serikali ziwafikie walengwa wa mifuko hiyo.

Makbel ameongeza kuwa wahusika wakuu wa serikali kuanzia ngazi ya mtaa watoe mazingira rafiki kwa vijana ili waone wao ni sehemu kubwa yakuchangia pato la taifa na serikali kuu wameanza vikao vya pamoja ili waone wanatekeleza vipi mipango ya kukuza uchumi wa vijana.

Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) Yatangaza Majina 22 ya Wajumbe wa Viti Maalumu CCM

$
0
0

Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) imetangaza majina 22 ya wajumbe wa viti maalumu wa Baraza la Wawakilishi, wote kutoka CCM.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Mwenyekiti wa Tume hiyo, Jecha Salim Jecha, wajumbe hao ni Salama Aboud Talib, Shadya Mohamed Suleiman, Bihindi Hamad Khamis, Salma Mussa Bilal, Mwanaidi Kassim Mussa, Panya Ali Abdalla, Mgeni Hassan Juma na Zaina Abdalla Salum.

Wengine ni Salha Mohammed Mwinyijuma, Zulfa Mmaka Omar, Lulu Msham Abdalla, Wanu Hafidh Ameir, Saada Ramadhani Mwenda, Tatu Mohamed Ussi na Amina Idd Mabrouk.

Jecha aliwatangaza wawakilishi wengine wa viti maalumu kuwa ni Choum Kombo Khamis, Mtumwa Suleiman Makame, Mwantatu Mbaraka Khamis, Riziki Pembe Juma, Viwe Khamis Abdalla, Hamida Abdalla Issa na Hidaya Ali Makame.

Makonda Aingilia kati Vurugu za makanisani.....Asema Muumini Atakayekimbilia Polisi Kulishitaki Kanisa Atamuweka Rumande

$
0
0

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda amesema mkoa wake hauko salama kama watu wanavyodhani kwa sababu silaha nyingi zinamilikiwa kiholela na mafunzo ya matumizi ya silaha hizo hutolewa hata kwa watoto.

Makonda alisema hayo jana wakati wa ibada ya Pasaka iliyofanyika katika Kanisa la Anglikana la Mtakatifu Albano na kuwataka wakazi wa Dar es Salaam kujitokeza kuhakiki silaha zao na kusalimisha zile zinazomilikiwa kinyume cha sheria.

Alisisitiza kwamba ifikapo Julai Mosi, operesheni maalumu ya kukamata silaha zinazomilikiwa kinyume cha sheria itaanza na yeye mwenyewe ndiye atakayeiongoza.

“Tumegundua kwamba kwenye bonde la mto unaotenganisha Mkoa wa Dar es Salaam na Pwani, kuna mafunzo yanatolewa kwa watoto. Wazazi wanadhani watoto wao wamekwenda shule  kumbe wamechukuliwa huko.Hatuwezi kukubali hali hiyo iendelee."Alisema

Mkuu huyo wa mkoa aliwataka waumini waendelee kumuombea ili afanye kazi yake vizuri kwa kutenda  haki pia aliwataka pia wamwombee Rais Magufuli  kwa sababu kazi anayoifanya ni kubwa.

Alisema Rais anapotumbua jipu moja,ndani yake kuna kundi la watu wanaoathirika na hatua aliyoichukua hivyo, alisema watu wa aina hiyo hawawezi kumpenda kwa sababu amevunja mtandao wa masilahi yao.

“Ninaomba kanisa pamoja na viongozi wote wa dini mnisaidie katika kuhimiza suala la ulinzi na usalama ili amani yetu iendelee kudumu. Ninaomba tushirikiane katika hilo, Dar es Salaam haiko salama kama mnavyodhani, mengine siwezi kusema kwa sababu sijaruhusiwa na Rais,” alisema. 

Migogoro kanisani 
Akizungumzia migogoro makanisani, Makonda alisema hataki kusikia kiongozi yeyote wa dini anakimbilia polisi au mahakamani kutaka suluhisho la matatizo yao ya ndani na kuwa atamweka ndani atakayejaribu kufanya hivyo.

Alisema ni aibu kubwa kwa kanisa kukimbilia kwenye vyombo vya dola badala ya polisi na Serikali kukimbilia kanisani kuomba ushauri. Alisema kanisa ndicho chombo cha usuluhishi wa matatizo mbalimbali ya jamii.

“Serikali inahitaji msaada wa kanisa na viongozi wa dini ili iweze kufanya kazi vizuri. Sitaki kusikia polisi wanakwenda kanisani (kukamata watu) katika mkoa wangu na wale wanaotoa taarifa kutaka polisi nitawaweka ndani,” alisema Makonda ambaye kabla ya kuwa mkuu wa mkoa, alikuwa mkuu wa Wilaya ya Kinondoni.

 Askofu Mokiwa 
Awali, Askofu Mkuu wa Kanisa la Anglikana, Dayosisi ya Dar es Salaam, Valentino Mokiwa alibainisha mambo mbalimbali aliyoyaita majipu ambayo yanafanya kanisa hilo lisiendelee katika kufundisha waumini wake yaliyo mema.

Mokiwa alitaja mambo hayo kuwa ni pamoja na mashindano ya kimadhehebu. Alisema madhehebu mbalimbali yanashindanishwa kupima kanisa lipi ni kubwa, lina waumini wangapi, linamilikiwa na nani na nguvu yake ni ipi.

Jambo jingine alisema ni maaskofu wenyewe kupigana vita. Alisema sasa ni kawaida kwa askofu mmoja kumchimba mwingine, askofu mmoja kupanga mapinduzi dhidi ya mwingine na baadhi ya maaskofu kutukanana waziwazi.

Mechi ya Taifa Stars na Chad Yaota Mbawa........Chad Wamejitoa Kwenye Mashindano Kwa Madai Kwamba Hawana Fedha

$
0
0

Shirikisho la Soka la Chad, limetangaza kuiondoa timu yake ya taifa katika mechi za kuwania kufuzu Fainali za Afrika zitakazofanyika nchini Gabon mwakani.

Tanzania na Chad zilikuwa zicheze leo, mechi ya marudiano ya kuwania kufuzu fainali hizo. Katika mchezo wa kwanza, Stars iliifunga Chad bao 1-0, mchezo uliofanyika kwenye mji wa N’Djamena.

Mtandao wa Twitter wa Shirikisho la Soka Afrika, CAF ulithibitisha jana kupokea taarifa ya Chad na tayari limetangaza adhabu ya kuisimamisha nchi hiyo.

“Shirikisho la Soka la Chad limeondolewa kushiriki mashindano yajayo ya Afcon na linatakiwa kulipa faini ya Dola 20,000,” ilisema taarifa hiyo ya CAF kwa kifupi.

Kujitoa kwa Chad kumevuruga msimamo wa Kundi G la michuano hiyo kwani kwa mujibu wa Kanuni za Mashindano ya CAF, Ibara ya 58 inasema: “Ikiwa timu itajitoa kwenye mashindano hatua za awa li za makundi, matokeo yote yatafutwa (pointi, mabao ya kufunga na kufungwa).

Ibara ya 59 ya kanuni hizo za mashindano inasema Kamati ya Maandalizi itatoa adhabu kali kulingana na uzito wa timu kujitoa.

Kwa hatua hiyo, Misri iliyoshinda mabao 5-1, Nigeria 2-0 na Tanzania 1-0 zitakuwa zimepoteza matokeo hayo.

Kwa mujibu wa kanuni, Misri sasa itakuwa na pointi nne ikifuatiwa na Nigeria pointi mbili na Tanzania itabakia na pointi moja.

Michezo itakayobakia ni ya Misri kuifunga Tanzania 3-0 na sare ya 1-1 dhidi ya Nigeria wakati Taifa Stars inabakiwa na pointi moja ya suluhu na Nigeria. Nigeria itabakia na pointi mbili za Tanzania na Misri kabla ya mchezo wao wa kesho kwenye mji wa Alexandria.

Mratibu wa timu ya Taifa, Msafiri Ahmed Mgoyi alikiri kuziona taarifa za Chad kutocheza mchezo na kusema:“Tumezipata taarifa hizo lakini bado tunaendelea kujiandaa kama kawaida mpaka pale tutakapopata taarifa rasmi kutoka TFF ambao wanapokea maelekezo kutoka Caf.”

Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania, TFF, Jamal Malinzi alisema jana kupitia ukurasa wake wa Twitter kuwa iwapo Chad itashindwa kucheza mchezo, uamuzi wa mwisho utatolewa na chombo husika kinachosimamia mashindano hayo.

“Hadi sasa timu ya Chad haijatua nchini kwa ajili ya mechi ya kesho. TFF itatoa taarifa kamili leo usiku (jana) baada ya kikao cha maandalizi ya mchezo. Kwa mujibu wa kanuni za CAF Kamati ya Maandalizi ya mashindano ya Caf ndiyo inatoa uamuzi,” alisema Malinzi.

Kocha Msaidizi wa Taifa Stars, Hemed Morocco alisema jana kuwa benchi la ufundi na wachezaji kama ilivyo kwa watu wengine nao wamezipata taarifa hizo ingawa haziwezi kuathiri saikolojia yao kwa namna yoyote ile.

“Sisi kwa upande wetu tunafahamu mechi ipo kama kawaida kwani hatujapewa taarifa yoyote kutoka kwa TFF, hivyo kama ni kweli au la haiwezi kuvuruga mipango na maandalizi yetu kama timu, ingawa ufafanuzi zaidi tunausubiri,” alisema Morocco.

Wakati hali hiyo ikitokea, mashabiki wa soka walikwishaanza kukata tiketi za mchezo kati ya Sh25,000 ikiwa ni kiingilio cha juu na Sh5,000.

Boko Haram Wateka Wanawake Wengine 16

$
0
0

Wapiganaji wa Kundi la Boko Haram wamewateka nyara wanawake 16 katika eneo la mashambani, Kaskazini Mashariki mwa Jimbo la Adamawa.

Vyanzo vya habari vilisema wanawake hao walitekwa msituni, walipokuwa wakitafuta kuni na wengine walikuwa wakivua samaki kando ya mto.

Wanawake hao hadi sasa hawafahamiki mahali walipohifadhiwa na watekaji.

Kundi hilo lililoenea nchini humo, limekuwa likijihusisha na vitendo vya utekaji wa mara kwa mara. Awali, liliwateka wasichana ambao ni wanafunzi zaidi ya 200 ambao mpaka sasa hawajapatikana.

Wakati huohuo, Jeshi la Nigeria limewakomboa zaidi ya watu 800, waliokuwa wakishikiliwa na kundi hilo katika vijiji kadhaa, kaskazini mashariki mwa nchi hiyo.

Mateka wengine walikombolewa katika Jimbo la Borno, huku 520 wakikombolewa katika Kijiji cha Kisuma, baada ya mapambano kati ya wanajeshi hao na wapiganaji wa kundi hilo, mateka wengine 309 waliokolewa katika vijiji vingine 11 vinavyodhibitiwa na kundi hilo.

Rais wa nchi hiyo, Muhammadu Buhari alipokuwa anaingia madarakani alisema atahakikisha anapambana na kundi hilo

Askofu Awataka Mafisadi na Wahujumu Uchumi Wajitumbue MAJIPU Wenyewe

$
0
0

Wahujumu uchumi, mafisadi na wote wanaokiuka viapo vyao wametakiwa kujitumbua majipu wenyewe badala ya kusubiri Rais John Magufuli, kwa kuungama kwa viongozi wao wa dini ili kusafisha nafsi zao.

Ushauri huo ulitolewa juzi na Paroko wa Kanisa Katoliki mjini Mugumu wilayani Serengeti, Alois Magabe wakati wa ibada ya mkesha wa Pasaka.

“Hawa watu wanapaswa kumpata Mungu kwa kuungama kwa sababu matendo yao siyo tu dhambi, bali yana madhara na udhalimu kwa umma kijamii, kiuchumi na hata kisiasa,” alisema Padri Magabe na kuongeza:

“Matendo ya uhujumu uchumi, ufisadi, wizi na ushirikina yanawatenga wanadamu na Mungu, wahusika lazima watubu na kurejea katika njia safi badala ya kusubiri kutumbuliwa na Rais,” alisema Padri Magabe.

Aliwataka waumini wa dini na madhehebu yote kutumia maadhimisho ya sikukuu za kidini kuhimiza matendo mema, kutimiza wajibu, haki, heshima kwa utu wa mwanadamu na usawa kwa wote bila kujali tofauti miongoni mwao.

Naye Askofu Naamon Kajeri wa Kanisa la Mennonite Tanzania (KMKT) Jimbo la Mara, aliwataka viongozi wa Serikali na siasa ngazi zote kuongoza kwa hofu ya Mungu, kutimiza kwa vitendo maandiko kuwa mamlaka zote duniani zinawekwa na Mungu.

Askofu Kajeri aliwata wote wenye dhamana kutenda haki na kuchukua hatua stahiki kwa wanaokiuka misingi, ili dhana ya usawa isimame na kuonekana miongoni mwa wananchi. 

Alisema kuendelea kuhubiri dhana hiyo bila kuisimamisha, haina maana yoyote.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumatatu Ya March 28

20 Watiwa Mbaroni Wakituhumiwa Kumpiga Mawe Ofisa wa JWTZ Aliyemgonga Mtembea Kwa Miguu

$
0
0

Polisi mkoani Ruvuma inawashikilia waendesha bodaboda 20 Manispaa ya Songea wanaodaiwa kumshambulia askari wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) Kikosi cha 411 KJ Ruhuwiko, kwa kupiga mawe gari alilokuwa akiendesha baada ya kumgonga mtembea kwa miguu.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma, Zubeir Mwombeji alisema tukio hilo lilitokea Machi 24 saa 3.00 usiku maeneo ya Shule ya Msingi Mfaranyaki, karibu na Kituo Kikuu cha Polisi Songea Mjini.

Mwombeji alimtaja mwanajeshi huyo aliyejeruhiwa kwa kushambuliwa na waendesha bodaboda kuwa ni Luten Samweli Nginila (32), ambaye amelazwa Hospitali ya Rufani Mkoa.

Alisema Luteni Nginila alijeruhiwa sehemu mbalimbali za mwili na kupoteza fahamu baada ya kushambuliwa na waendesha bodaboda, ambao walivunja kwa mawe vioo vya gari alilokuwa akiendesha.

Aliendelea kuwa chanzo cha tukio hilo, inadaiwa kutokea ajali maeneo ya majengo ambako askari huyo alikuwa akiendesha gari aina ya Nissan XTRAIL akitokea Bar ya Ramour .

Alisema alipofika eneo la majengo, Bahati Mbero alikatisha ghafla barabarani hivyo askari huyo kushindwa kumudu gari na kusababisha ajali.

Kufuatia hali hiyo, waendesha bodaboda waliokuwa karibu walikusanyika kwa lengo la kumshambulia, hali iliyomlazimu kuwasha gari kukimbia ili kuokoa maisha.

Hata hivyo, bodaboda hao walimkimbiza na alipofika Shule ya Msingi Mfaranyaki tairi la gari lake lilichomoka, hivyo walimzingira na kumshushia kipigo wakiwamo abiria watatu aliokuwa nao.

Mwombeji aliwataja waliokuwamo ndani ya gari hilo kuwa ni Kaumbya Kateka (24) mkazi wa Majengo, Joyce Edson (24) mkazi wa Mpambalyoto na Jackline Mwita (22) mwanafunzi wa Chuo cha Uuguzi Peramiho. Alisema katika vurugu hizo baadhi ya vitu vilipotea ambavyo ni mali ya askari huyo.

Vitu vilivyopotea ni simu mbili za mkononi, pochi ambayo ilikuwa imehifadhi vitambulisho mbalimbali na Sh120,00.

Alisema wanaendelea kuwabaini wengine waliohusika, taratibu za kuwafikisha mahakamani zitafuata.

Rais Magufuli Amuapisha Mkuu Wa Mkoa Mpya Wa Songwe Mhe. Chiku Gallawa Ikulu Dar Es Salaam

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akimuapisha Luteni Mstaafu Chiku Gallawa kuwa mkuu wa mkoa mpya wa Songwe Ikulu jijini Dar es salaam leo Machi 28, 2016

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akimshuhudia Luteni Mstaafu Chiku Gallawa akiweka sahihi katika hati ya kiapo mara baada ya kuapa kuwa mkuu wa mkoa mpya wa Songwe Ikulu jijini Dar es salaam leo Machi 28, 2016.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akisaini hati ya kiapo cha Luteni Mstaafu Chiku Gallawa  mara baada ya kumuapisha  kuwa mkuu wa mkoa mpya wa Songwe Ikulu jijini Dar es salaam leo Machi 28, 2016
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akimkabidhi nyenzo za kazi  Luteni Mstaafu Chiku Gallawa  mara baada ya kumuapisha  kuwa mkuu wa mkoa mpya wa Songwe Ikulu jijini Dar es salaam leo Machi 28, 2016
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli katika picha ya pamoja na Makamu wa Rais Mhe Samia suluhu Hassan, Waziri Mkuu Mhe Kassim  na  Luteni Mstaafu Chiku Gallawa  baada ya kumuapisha  kuwa mkuu wa mkoa mpya wa Songwe Ikulu jijini Dar es salaam leo Machi 28, 2016.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akipeana mikono na Luteni Mstaafu Chiku Gallawa  mara baada ya kumuapisha  kuwa mkuu wa mkoa mpya wa Songwe Ikulu jijini Dar es salaam leo Machi 28, 2016. Kulia ni mume wa mkuu huyo wa Mkoa Bw. Juma` Boma na kushoto ni bintiye.

PICHA NA IKULU

Dk Shein amteua Balozi Seif Ali Idd Kuwa Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar

$
0
0

Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Dk Ali Mohammed Shein amemteua Balozi Seif Ali Idd kuwa Makamu wa Pili wa Rais wa visiwa hivyo.

Kwa mujibu wa mamlaka aliyopewa chini ya kifungu cha 39 (2) cha Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984, Dk Shein amemteua Balozi Idd ambaye alikuwa na wadhifa huo hata kipindi kilichopita.

Uteuzi wa Balozi Idd aliyezaliwa Februari 23, mwaka 1942, ulianza jana ikiwa ni siku nne tangu kuapishwa kwa Shein kuwa Rais wa Zanzibar.

Balozi Idd anakuwa mtu wa pili kuteuliwa na Dk Shein baada ya kuteuliwa kwa mwanasheria mkuu wa Zanzibar Said Hassan Said mwishoni mwa wiki.

Dk Shein sasa atakuwa na wakati mgumu wa ama kumteua au kutomteua Makamu wa Kwanza wa Rais ili kukidhi matakwa ya Serikali ya Umoja wa Kitaifa (SUK) kwani hakuna chama cha upinzani kilichokidhi vigezo vya kushirikishwa katika kuunda Serikali.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images