Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Majaliwa Amtumbua JIPU Mhandisi wa Maji Nyumbani Kwa Rais Magufuli

$
0
0

Rungu lakuwatumbua majipuwatumishi wa ummawasiowajibika limetua kwaMhandisi wa Maji Wilaya yaChato, Peter Ngolemi baadaya Waziri Mkuu, KassimuMajaliwa kuagiza kusimamishwa na kuamuru Takukurukumchunguza kutokana nakumdanganya. 

Ngolemi, anadaiwa kumdanganya Majaliwa kuhusumradi wa maji katika Kijijicha Kalebezo ambao umesababisha wananchi kutembea umbali mrefu kutafutahuduma hiyo.
 
Mradi huo umesimama tangu mwaka 2011, kutokana nakukosa usimamizi baada yamashine mbili kutofanya kazi.Licha ya kumsimamisha,Waziri Mkuu aliagiza Takukuru kumchunguza na kumchukulia hatua za kisheria. 

“Hatuwezi kuwa na kiongozi muongo, naondoka naye. Mtumishi huyu atakaa pembeni Takukuru wamchunguze,” alisema.

Kabla ya kuchukua uamuzi huo, Majaliwa alimwita jukwaani na kumtaka ajibu madai ya wananchi kukosa maji muda mrefu.

“Mheshimiwa Waziri Mkuu, kuna mashine mbili na hili suala lipo kwa Mamlaka ya Maji Bukoba, lakini zile pampu mbili zipo,” alijibu Ngolemi huku akitetemeka na wananchi wakimzomea.

Hatua hiyo ilisababisha Majaliwa kusema: “Huwezi kumdanganya Waziri Mkuu anayetegemewa na wananchi wengi, nimepita pale wananchi wana mabango wanadai mashine ziling’olewa na kupelekwa Morogoro, halafu leo unaniambia zipo!

“Sasa naondoka na wewe, kaa pembeni kuanzia sasa hakuna kazi, Takukuru mchunguze na kumchukulia hatua.”

Baada ya agizo hilo, maofisa wa usalama walimchukua mhandisi huyo na kuondoka naye kwenye Uwanja wa Chato.

Katika hatua nyingine, Majaliwa ameagiza kufutwa kwa umiliki wa mashamba makubwa 11 yakiwamo ya Kanisa Katoliki Jimbo la Rulenge yenye ukubwa wa ekari 7,700 kwenye vijiji vya Kasharazi na Rwakalemera, Wilaya ya Ngara mkoani Kagera, kutokana na kutokuwa na hati na kutelekezwa kwa muda mrefu.

Pia, Majaliwa ameagiza kusimamishwa kazi kwa aliyekuwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ngara, Colnel Ngudungi na kutaka arejeshwe wilayani hapa kujibu tuhuma za kuhusika na upotevu wa fedha za mauzo ya mbao kwenye Msitu wa Rumasi.

Ngudungi alihamishwa kwenda Sekretarieti ya Mkoa wa Shinyanga Agosti 2015, kwa kile kilichoelezwa kuwa anakwenda kwa kazi maalumu.

Majaliwa ambaye alikuwa njiani kuelekea Geita akitokea Kagera, alitoa maagizo hayo jana alipozungumza na wakazi wa vijiji vya Kasulo na Rwakalemera, baada ya kusimamishwa na wananchi wakiwa na mabango wakiomba kurejeshewa ardhi ya kijiji huku baadhi yao wakidai wanatishiwa kwa bunduki wanaposogelea mashamba hayo.

Waliendelea kuwa uongozi wa kijiji umekithiri kwa ubadhirifu kwani licha ya Msitu wa Rumasi kuuzwa na mapato kutoonekana, kijiji kina minada ya ng’ombe ambayo sheria inataka asilimia 20 ya mapato ibaki eneo hilo.

Awali, Waziri mkuu alimuita kwenye mkutano huo Ofisa Ardhi na Maliasili wa Wilaya, Betty Munuo ili aeleze chanzo cha mgogoro wa ardhi katika vijiji hivyo.

Akitoa ufafanuzi huo, Munuo ambaye amehamishiwa wilayani hapo Agosti mwaka jana, alisema malalamiko hayo ameyarithi kwa mtangulizi wake na amefanya uchambuzi wa majina ya wamiliki wote wa mashamba na kwamba, uongozi wa wilaya ulikuwa unapanga kuwapatia notisi ya kujieleza.

Munuo alisema kati ya wamiliki 18 wa mashamba makubwa, saba ndiyo wenye hati huku matatu pekee ndiyo yameendelezwa.

Kwa mujibu wa Munuo, mashamba yaliyoendelezwa yanatumika kwa kilimo, ufugaji na shule na kwamba Shamba namba 606 lenye ukubwa wa ekari 161 linamilikiwa na Kanisa Katoliki Dayosisi ya Rulenge, Dario Zakaria shamba ana ekari 282 na Masista wa Mtakatifu Fransisco wanamiliki ekari 759.

“Mashamba manne ndiyo yenye hati lakini yametelekezwa, yaliyotelekezwa yote yapo Kijiji cha Rwakalemera nayo ni ya Abdallah Sadalla (ekari 521); Mahsen Saidi (458); Mshengezi Nyambele (3,88) na Mushengezi Nyambele (497).

Majaliwa aliwataja wamiliki wa mashamba yasiyo na hati kuwa ni Joseph Rugumyamheto (505) lipo Rwakalemera, Nicholaus Kidenke, Gwasa Angas Sababili (236) lipo Kasharazi na Makumi Rufyega (500) lipo Rwakalemera.

Wamiliki wengine ambao mashamba yao yapo kijiji cha Rwakalemera na ukubwa wake kwenye mabano ni Paulo Shikiri (250), Frank Derila (750), Godfrey Kitanga (800), Phillemon Mpanju (200), Issa Sama (500), Hekizayo Mtalitinya (225) na Joel Nkinga (1,250).

Majaliwa aliagiza kurejeshwa mara moja aliyekuwa Ofisa Ardhi wa Wilaya hiyo, Enock Mponzi ambaye amehamishiwa Halmashauri ya Wilaya ya Rorya mkoani Mara ili aende kusaidia uchunguzi.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Alhamisi Ya March 17

Jukwaa la Wakristo Tanzania (TCF) Latoa Tamko Zito Kuhusiana Na Hali Ilivyo Kwa Sasa Zanzibar

$
0
0

Jukwaa la Wakristo Tanzania (TCF) limetoa tamko kuhusiana na hali ilivyo sasa Zanzibar likisema linafadhaishwa na kusikitishwa nayo na kwamba linaamini isingefikia hapo endapo Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ingechukua hatua katika kutatua mgogoro huo. 

Katika tamko hilo lililosambazwa kwenye vyombo vya habari jana baada ya kikao cha TCF juzi, yamo mapendekezo manne likiwamo la kuitaka Serikali kurejesha mchakato wa Katiba kwa kuzingatia maudhui yaliyomo katika Rasimu ya Tume ya Mabadiliko ya Katiba ili kuondoa utata wa Serikali kushiriki masuala ya Zanzibar. 

“Sisi viongozi wa dini tuliokutana leo tarehe 15.03.2016, tunafadhaishwa na kusikitishwa na hali ya Zanzibar kwa sasa.

"Hali ya Zanzibar isingefika hapo ilipo iwapo Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ingechukua hatua ya kutatua mgogoro huu.

"Hali hii ya Zanzibar na udhaifu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano vinapelekea kushindwa kwa Serikali ya Muungano kuchukua hatua ya kusaidia hali ya Zanzibar. Hata hivyo, udhaifu huu wa Katiba hauondoi wajibu wa Serikali ya Muungano kuhakikisha haki na amani vinatawala Zanzibar,” ilisema sehemu ta tamko hilo lililotiwa saini na Askofu Mkuu wa Dayosisi ya Mwanza, Jude Ruwa’ichi.

Jukwaa halikufafanua hali ya Zanzibar kwa sasa inay- osababisha maaskofu hao kufadhaika lakini huenda limekusudia kueleza hofu iliyotanda katika visiwa hivyo tangu Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) ilipofuta uchaguzi na matokeo yote ya uchaguzi wa Zanzibar, na baadaye kutangaza kuwa utarudiwa Machi 20. 

Vyama tisa kikiwamo Chama cha Wananchi (CUF) vilitangaza kujitoa lakini ZEC imesisitiza vyama vyote vitashiriki. 

Hali imeendelea kuwa tete na hivi karibuni yamekuwapo matukio ya uchomaji moto makazi ya watu katika visiwa hivyo yanayoonyesha uvunjifu wa amani kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi wa marudio Jumapili ijayo. 

Baadhi ya matukio hayo ni kuchomwa moto maskani za CCM na CUF, nyumba 11 za watu ikiwamo ya Kamishna wa Polisi Zanzibar, Hamdan Omar Makame iliyoko Kijichi, Mkoa wa Mjini Magharibi. 

Baada ya kutathimini hali hiyo, TCF imesema pamoja na udhaifu wa Katiba, Serikali ya Muungano bado ina wajibu wa kuhakikisha uhuru, haki na amani vinatawala Zanzibar kuelekea uchaguzi huo wa marudio.

 “Hata hivyo, Serikali ya Muungano pamoja na taasisi zinazosimamia mchakato wa uchaguzi, zinao wajibu wa kuhakikisha kuwa suala la uhuru, haki na amani Zanzibar vinalindwa na kuheshimiwa. Suala la uhuru, haki ni wajibu wetu sisi viongozi wa dini na Watanzania wote na halina mbadala,” ilisema sehemu ya tamko hilo. 

Jukwaa limesisitiza kwamba ni jukumu la kila mmoja kutimiza wajibu wake kulinda uhuru, haki na amani na kuweka uzalendo kwanza kuliko kutanguliza maslahi binafsi au ya vyama vya siasa. 

Mbali ya pendekezo la kuitaka Serikali kurejesha mchakato wa Katiba, pia limewataka viongozi wa dini kuwahimiza Watanzania wote kuendelea kuiombea Tanzania (Bara na Zanzibar) ibaki kuwa Taifa lililojengwa katika msingi ya uhuru, haki na amani. 

Pili, limelitaka Jeshi la Polisi, vikosi vya ulinzi na usalama na Jeshi la Wananchi wa Tanzania, kwa wakati huu kuendelea kutimiza wajibu wa kusimamia amani na taratibu kwa haki bila upendeleo.

 Mwisho limesisitiza kwamba viongozi wa dini wabaki kuwa sauti ya kinabii na wahubiri wa uhuru, haki na amani wakati huu, wakati wa uchaguzi na haada ya uchaguzi.

Watu 42 Watiwa Mbaroni Zanzibar Wakituhumiwa Kulipua Nyumba ya Kamishna wa Polisi

$
0
0

Jeshi la Polisi Zanzibar linawashikilia watu 42 wakituhumiwa kuhusika na mlipuko uliotokea juzi usiku katika nyumba ya Kamishna wa Polisi, Hamdan Omar Makame.

Akizungumza na waandishi wa habari katika ofisi za makao makuu ya polisi Ziwani, Kamanda wa Polisi wa mkoa wa Mjini Magharibi, Mkadam Khamis Mkadam alisema hadi jana mchana watu 42 walikuwa ndani kwa ajili ya kuhojiwa na jeshi hilo.

Alisema uchunguzi unaendelea na bado watu wengine wanatafutwa kuhusiana na tukio hilo.

“Bado tunaendelea na uchunguzi wa jambo hili na tukishakamilisha tutatoa taarifa rasmi,” alisema Kamanda Mkadam.

Waziri Kitwanga Afanya Mazungumzo Na Wakuu Wa Vyombo Vya Ulinzi Na Usalama Zanzibar....Akanusha Wazanzibar Kukimbilia Nchi Jirani Kwa Kuogopa Vurugu

$
0
0

WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga amewataka wananchi wa visiwani Zanzibar kujitokeza kwa wingi Machi 20, 2016 ili waweze kupiga kura kwa amani na utulivu bila kubughudhiwa na mtu yeyote.
 
Kitwanga amesema kuwa ulinzi umeimarishwa na kuwataka wananchi visiwani humo kujitokeza kwa wingi kuja kumchagua kiongozi wanaompenda siku ya uchaguzi huo na watarejea nyumbani kwao salama mara baada ya kumaliza kupiga kura.
 
Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kumaliza mazungumzo na Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Polisi Makao Makuu ya Polisi Zanzibar na baadaye kuzungumza na Wakuu wa vyombo vya Ulinzi na Usalama, Waziri Kitwanga alisisitiza kuwa, vyombo vya ulinzi na usalama vimejiandaa vizuri na wananchi waondoe shaka kwani hawatakubali vurugu ya aina yoyote itokee.
 
“Jitokezeni kupiga kura siku ya uchaguzi kwani ni haki yenu, nawahakikishia usalama upo na wa hali ya juu, asijitokeze mtu yeyote akawatisha kutokuja kupiga kura, tumejipanga vizuri na lengo letu kubwa kabisa ni kuwalinda wananchi,” alisema Kitwanga.
 
Hata hivyo Waziri Kitwanga alisema hakuna mwananchi yeyote anayehama kwakuogopa vurugu siku ya uchaguzi bali watu wanasafiri kwasababu mbalimbali ikiwemo hiki ni kipindi cha maandalizi ya Sikukuu ya Pasaka.

“Hali ya Pemba ni shwari na pia nataka kusisitiza nikiwa Waziri wa Mambo ya Ndani sijapata taarifa yoyote rasmi kama kuna watu wanakimbilia nchi jirani. Lakini hata hilo la watu kukimbilia msituni inabidi tujiulize Pemba kuna msitu mkubwa wa watu kwenda kujificha? Haya mambo ni ya kuzusha, watu waende wakajionee wenyewe,” alisema Kitwanga. 

 Alisema hakuna dalili yoyote ya  watu wanaokimbia kutoka Zanzibar kukimbilia Tanzania Bara kutokana na idadi ya wasafiri kati ya Bara na Zanzibar kuwa ya kawaida.

 Alisema kama kuna ongezeko lolote basi ni kutokana na sherehe za Pasaka kukaribia na si suala la kuogopa uchaguzi kama inavyoelezwa. 

Waziri Kitwanga alisema yupo hapa Zanzibar ili kuhakikisha maandalizi yote ya uchaguzi wa marudio Jumapili unafanyika kama ulivyopangwa. 

 “Vitisho vinavyoendelea tulivitegemea, tunajua kama kuna watu hawataki uchaguzi na wanatumia mbinu mbalimbali ikiwamo ya milipuko kutisha watu. Wito wangu kwa watu wanaotaka kupiga kura wajitokeze kwa wingi na usalama wao upo,” alisema waziri huyo.

Rais Magufuli Akerwa Na Mikataba Mibovu Ya Kampuni ya Kufua Umeme ya IPTL....Aeleza Kilichomfanya Amrudishe Profesa Muhongo Wizara ya Nishati

$
0
0

Rais John Magufuli jana aliitaja kampuni ya kuzalisha umeme ya IPTL wakati akizungumzia matatizo yanayosababishwa na kununua umeme unaozalishwa na mitambo ya kukodi na kupiga marufuku mikataba hiyo. 

Rais pia alipuuzia shutuma zinazorushwa dhidi ya Profesa Sospeter Muhongo, ambaye alijiuzulu wadhifa wa Waziri wa Nishati na Madini kutokana na sakata la IPTL, akisema “wakati mwingine vitu vizuri hupigwa vita” na hivyo amemrejesha mbunge huyo wa Musoma Vijijini kwenye wizara hiyo kwa sababu ya uchapakazi na si siasa.

 Tangu aingie madarakani, Rais Magufuli amekuwa akifichua kashfa za ufisadi ambazo hazikuwahi kujadiliwa vikali katika utawala uliopita, lakini jana alitoa mfano wa IPTL kama moja ya mikataba iliyoisababishia Serikali matatizo. 

Kashfa zilizoikumba sekta hiyo ni pamoja na mkataba wa uzalishaji umeme na kampuni ya Richmond Development iliyodhihirika baadaye kuwa haikuwa na uwezo, uchotwaji wa zaidi ya Sh300 bilioni kutoka kwenye Akaunti ya Tegeta Escrow iliyohusisha IPTL, mikataba ya ununuzi umeme kwa bei kubwa kutoka kampuni binafsi na ununuzi wa umeme kutoka mitambo ya kukodi.

“Ni matumani yangu kuwa sitasikia tena mnaleta mapendekezo kwamba tunataka kuongeza mkataba huu au tunataka kukodi mtambo huu.Suala la kukodi likalegee, lizimie na life kabisa huko,” alisema Rais Magufuli wakati akizindua ujenzi wa kituo cha umeme cha mradi wa Kinyerezi ll utakaokuwa ukizalisha megawati 280 kwa mwaka jijini Dar es Salaam jana.

“Hayo mawazo yafe, sasa tuwe na mawazo ya kujenga mitambo yetu. Cha kuazima ni kibaya. Hivi sasa vya kukodi na vya kuazima achaneni navyo. Nendeni na mawazo ya kujenga mitambo yetu.

“Tumechoka kuchezewa. Kuna miradi hapa ya hovyo kweli. Kila siku inazaa matatizo. Kwa hiyo Mheshimiwa Waziri (Muhongo) lisimamie hilo. " Alisema Rais Magufuli

Alisema Profesa Muhongo akipata ushauri kutoka kwa wataalamu wake kuhusu miradi ya kukodi mitambo, atambue kuwa hawafai. “Ujue huyo si mtaalamu mzuri, ikiwezekana mtoe. Wataalamu wako wakuletee mawazo ya kujenga mitambo yetu,” alisema. 

Rais Magufuli alisema ni lazima ufike wakati Tanzania iwe na umeme wa uhakika tena wa kujitegemea.

 “Si umeme kwa kukodisha- kodisha. Umeme ni wa kutumia watu.Na ndiyo maana kumekuwa na matatizo mengi. Mara IPTL mara nini. Ni kwa sababu tulizoea umeme wa kukodisha kwa wafanyabiashara,” alisema. 

Kampuni ya IPTL iliingia kwenye mgogoro na Serikali baada ya kudaiwa kuwa inaitoza Tanesco tozo kubwa gharama za uwekezaji kuliko makubaliano ya mkataba. 

Wakati wa kashfa ya escrow, zaidi ya Sh300 bilioni zilizokuwa zimewekwa kwenye akaunti hiyo kusubiri kumalizika kwa mgogoro wa kimkataba baina ya IPTL na Tanesco zilichotwa na kuonekana zikiingia kwenye akaunti za mawaziri, majaji, wabunge na watumishi waandamizi wa Serikali, jambo lililolifanya Bunge limlazimishe Profesa Muhongo awajibike kwa kushindwa kusimamia fedha za Serikali. 

 Profesa Muhongo alijiuzulu, lakini akateuliwa na Rais Magufuli kurudi kwenye nafasi hiyo na jana mkuu huyo wa nchi hakusita kummwagia sifa. 

 “Wizara ya Nishati mmenifurahisha sana. Tuachane na mitambo ya kukodi. Tumechoka kufanya biashara na wawekezaji wa ajabu ajabu. Halafu tunalipia capacity charges za ajabu na umeme unakuwa juu. Tunawapa shida Watanzania wa maisha ya chini,” alisema Magufuli. 

“Nendeni kwa kasi ya hapa kazi tu. Na ndiyo maana niliamua kumrudisha Profesa Muhongo hapo. Wakati mwingine vitu vizuri vinapigwa vita. Sichagui mwanasiasa. Mimi nataka mtu mchapa kazi. Maendeleo hayana chama.”

Akizungumzia ujenzi wa kituo cha Kinyerezi ll utakaogharimu dola 344 za Marekani (sawa na Sh688 bilioni), Rais alisema amefarijika kuona ndani ya muda wake mfupi akiwa madarakani amealikwa kuweka jiwe la msingi kwenye mradi huo.

 Alisema Serikali ya Japan ilitoa dola 292 milioni za Marekani na Tanzania ilitakiwa kutoa dola 52 milioni za Marekani sawa na asilimia 15, lakini ikashindikana na kutakiwa wasubiri. 

“Baada ya makusanyo kuimarika tulipoingia madarakani mwezi Novemba na Desemba mwaka jana, tulitoa maelekezo na hizo dola 52 milioni sawa Sh110 bilioni za Tanzania na zikapatikana ndiyo maana leo tupo hapa kuweka jiwe la msingi kwa ajili ya mradi huu kuanza,” alisema.

 “Hivi sasa tuna uwezo wa kuzalisha megawati 1,200 hadi 1,500 za umeme kwa mwaka. Sasa tumefikia 1026. Hiyo ina maana kuwa kila Mtanzania kwa sasa anatumia wastani wa wati 30 kwa mwaka,” alisema. 

Pia alisema amefurahi kupata taarifa kuwa mradi ya Kinyerezi l utaongezewa uwezo wa uzalishaji kutoka megawati 150 hadi 335. 

“Nimeambiwa mkandarasi anataka dola 20 milioni za Marekani (sawa na Sh 40 bilioni). Sasa kama tuliweza kutoa hela kwa ajili ya Kinyerezi II, hatuwezi kushindwa kuongeza kwa ajili ya Kinyerezi l. Hiyo hela tutatafuta hata mwezi huu tutampa,” alisema.

Mkuu wa Wilaya Asuluhisha Ugomvi wa Takukuru na Polisi Ambao Walikunjana Mashati wakigombea Shahidi Mahakamani

$
0
0

Mkuu wa Wilaya ya Bukombe mkoani Geita, Amani Mwenegoha ameingilia kati kwa kuwasuluhisha maofisa wa Takukuru na polisi waliokunjana mashati wakimgombea shahidi katika eneo la Mahakama ya Hakimu Mkazi wilayani hapa.

“Nimelazimika kuita kikao cha dharura cha kamati ya ulinzi na usalama kujadili suala hili linalotishia kuvuruga uhusiano mwema kati ya taasisi hizi mbili zinazopaswa kushirikiana,” alisema Mwenegoha.

Alisema kabla ya tukio hilo, Machi 8 mwaka huu, ofisi yake ilipokea malalamiko kutoka Takukuru kuwa baadhi ya maofisa wa polisi walivuruga upelelezi na ushahidi wa kesi ya tuhuma za rushwa inayomkabili mmoja wa walimu wa shule za msingi.

 “Baada ya kikao cha zaidi ya saa nne kuanzia saa 11 jioni hadi saa mbili usiku, pande zote zimezika tofauti na nimewapa onyo mkuu wa polisi wa wilaya na mwenzake wa Takukuru nikiwataka kuwasimamia vyema maofisa waliopo chini yao kuepusha tukio kama lile,” alisema mkuu huyo wa wilaya. 

Miongoni mwa makubaliano yaliyofikiwa katika kikao hicho ni polisi na Takukuru kuheshimiana na kushirikiana kutekeleza majukumu yao. 

“Nimeagiza OCD na mkuu wa PCCB waitishe vikao vya haraka vya ndani kujadili suala hili na kuwekana sawa,” alisema. 

Mwenegoha alisema amewapa wakuu wa taasisi hizo muda wa siku tano kuanzia Jumanne iliyopita kukamilisha vikao vyao vya ndani na kutoa mrejesho kwenye kikao cha kamati ya ulinzi na usalama jinsi walivyoshughulikia suala hilo lililoitia aibu Serikali baada ya watumishi wake kukunjana mashati hadharani. 

Alisema kitendo cha askari polisi kumkamata na kumfunga pingu shahidi wa Takukuru, Paulo Stephano kabla ya kutoa ushahidi hakikuwa cha kiungwana wala kuheshimu mamlaka nyingine ya Serikali na kimetoa taswira kuwa jeshi hilo lililenga kudhoofisha ushahidi wa taasisi hiyo.

 “Haikubaliki polisi kumvamia shahidi wa Takukuru, kumweka chini ya ulinzi, kumfunga pingu na kumtupia kwenye gari lao hata kabla hajatoa ushahidi,” alifafanua. 

Kikao cha kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya hiyo kitakachopokea taarifa ya vikao vya ndani vya Takukuru na polisi namna walivyoshughu-likia suala hilo kitafanyikaMarch 18,mwaka huu.

Ujue Mfumo wa Nguvu za Kiume Unavyofanya Kazi Na Jinsi Ya Kukabiliana na Tatizo la Upungufu wa Nguvu za Kiume

$
0
0

Ukosefu  na/ama  upungufu wa  nguvu  za  kiume, ni tatizo linalo  wakabili  mamilioni  ya  wanaume duniani.

Tatizo  la  ukosefu/upungufu  wa  nguvu  za  kiume ni  nini  ?

Ukosefu  ama  upungufu  wa  nguvu za  kiume  ni  ile  hali  ya  mwanaume  kutokuwa  na  uwezo  wa kufanya  tendo  la  ndoa  kwa  ukamilifu

HATUA  MBILI  MUHIMU  KATIKA  KUSIMAMA  KWA  UUME

Ili  mwanaume   aweze  kufanya  tendo  la  ndoa  na  andelee  kufanya  tendo  la  ndoa, ni  lazima  uume wake  upitie  hatua  kuu  mbili  kama  ifuatavyo :

Hatua  ya  kwanza, ni  lazima  uume  wake  uweze  kusimama  barabara  na  kuwa  mgumu  kama  msumari.

Na  hatua  ya  pili  ni  lazima, uume  wake  uendelee  kusimama  kwa  muda  mrefu  wakati  wa  tendo  la  ndoa.  Hatua  zote  mbili  zinapo  kamilika, ndipo  tunapo  pata  kitu  kinaitwa  STRONGER  AND  LONGER  ERECTION

JINSI  HATUA  ZA  KUSIMAMA  KWA  UUME  ZINAVYO  TOKEA.

1. HATUA   YA  KWANZA:
DAMU  KUTIRIRIKA  KWA  KASI KUINGIA  NDANI  YA  MISHIPA  YA  UUME  NA  KUUFANYA  UUME  KUSIMAMA  NA  KUWA  MGUMU.

Unapopata  wazo  la  kufanya  tendo  la  ndoa, mishipa  ya  fahamu iliyopo  kwenye  ubongo,  hupeleka  ishara  kwenye  mishipa  ya  uti  wa  mgongo, ambayo  nayo  hupeleka  taarifa  hadi  kwenye  mishipa  ya  uume. 
 
Taarifa  inapofika  kwenye  mishipa  ya  uume  huifanya  mishipa hiyo  ku-relax  na  hatimaye   kufanya  mishipa  ya  ateri  kufunguka  na  kutanuka. Mishipa  ya  ateri  inapo  tanuka  na  kufunguka, huruhusu  damu  kuingia  kwa  kasi  ndani  ya  mishipa  ya  uume  na  hivyo  kuufanya  huume  kusimama.

Ni  muhimu  kujua  kuwa, mishipa  ya  uume  inapo relax  hupelekea  kuisukuma na  hatimaye  kuiziba  mishipa  ya  vena  iliyo  karibu  na  mishipa  ya  uume  na  hivyo  kuiondolea  uwezo  wa  kunyonya  damu  iliyomo  ndani  ya  mishipa  ya  uume  na  kuipeleka  sehemu  nyingine  za  mwili.

N.B: Kazi  kubwa  ya  mishipa  ya  vena  ni  kunyonya  damu  iliyomo  ndani  ya  mishipa  ya  uume  na  kuipeleka  katika  sehemu  nyingine  za  mwili.  Au  kwa  lugha  nyingine  unaweza  kusema, kazi  kubwa  ya  mishipa  ya  vena  ni  kuhakikisha  hakuna  damu  kwenye  mishipa  ya  uume.

2. HATUA  YA  PILI  :
DAMU  KUENDELEA  KUHIFADHIWA  KATIKA  UUME  WAKATI  UUME  UKIWA  UMESIMAMA  NA  HIVYO  KUUFANYA  UUME  UENDELEE  KUDUMU  KATIKA  TENDO LA NDOA   KWA  MUDA  MREFU.

Uume  ulio  simama, ili  uendelee  kusimama, ni  lazima  mishipa  ya  vena  isiwe  na  uwezo   wa  kunyonya  damu  kutoka  katika  mishipa  ya  uume  na  kuipeleka  katika  sehemu  nyinginezo  za  mwili. .

Mishipa  ya  Vena  ndio  inayo  husika  na  kunyonya  damu  kutoka  kwenye  mishipa  ya  uume na  kupeleka  sehemu  nyingine  za  mwili.  Ili  uume  uendelee  kusimama  lazima  mishipa  hii  ya  vena  iwe imezibwa. Ili  iweze  kuzibwa   ni  lazima  misuli  laini  ya  kwenye  uume  iwe - ime  relax na  hivyo  kuifanya  mishipa  ya  vena  kushindwa  ku  nyonya  damu  kutoka  kwenye  uume.

Endapo  mishipa  ya  vena  itazibuka , basi  itanyonya  na  kutoa  damu yote  kutoka  kwenye  mishipa  ya  uume uliosimama  na  kuipeleka  sehemu  nyinginezo  za  mwili  na  hatimaye  uume  huo ulio simama  na  utasinyaa  mara  moja.

JINSI  UUME  UNAVYO  SIMAMA  NA  KUSISIMKA.
Tumeisha  zifahamu  hatua  mbili  muhimu  katika  kusimama  kwa  uume

Jinsi  Uume  unavyo  simama: Katika  uume  kuna chemba  yenye  mishipa  laini  sana, ambayo  ndio  huufanya  uume  kusimama.

Mishipa  hii  ipo kama  sponji  hivyo  huweza  kunyauka  na  kutanuka.

Damu  inapoingia  ndani  ya  mishipa  hii  huufanya  uume  kusimama  na  kuwa  mgumu  kama  msumari.

Damu  inapoendelea  kuhifadhiwa  ndani  ya  mishipa  hii  wakati  wa  tendo  la  ndoa, huufanya  uume  uendelee  kusimama.

Mwanaume  unapo  patwa  na  wazo la  kufanya  tendo  la  ndoa, mishipa  ya  fahamu  iliyo  kwenye  ubongo  hupeleka  ishara  kwenye  uti  wa mgongo, ambao  nao  hufikisha   taarifa  kwenye  mishipa  ya  uume.

Taarifa  ikisha  fika  kwenye  mishipa  ya  uume, huifanya  mishipa  ya  uume  ku-relax  na  mishipa  ya  uume  inapo  relax, hufanya  mambo  makuu  mawili;

i. Kwanza  hufanya  mishipa  ya  ateri  kufunguka na  hivyo  damu  kutiririka  kwa  kasi  sana  kuingia  kwenye  mishipa  ya  uume

( Mishipa  ya  ateri  ndio  inayo  tumika  kama  njia  ya  kuingiza  damu  kwenye  uume. Bila  mishipa  ya  ateri  imara  na  yenye  afya, damu  haiwezi kuingia  kwenye  mishipa  ya  uume, na  damu  isipoweza kuingia  kwenye  mishipa  ya  uume, basi  uume  hauwezi  kusimama )

ii.Pili huibana  mishipa  ya  vena  na  hivyo  kuizuia    kunyonya  damu  kutoka  kwenye  uume  na  kuipeleka  kwenye  sehemu nyingine  za  mwili. Matokeo  yake  kuufanya  uume  uendelee  kusimama  kwa  muda  mrefu  wakati  wa  tendo  la  ndoa.

Kumbuka ,kazi  kubwa  ya  mishipa  ya  neva  iliyo  karibu  na  mishipa ya  uume, ni kunyonya  damu kutoka  ndani  ya  mishipa  ya  uume  na  kuipeleka  kwenye  sehemu  nyingine  za  mwili. Kwa  lugha  nyingine, kazi  kubwa  ya  mishipa  ya  vena  ni  kuhakikisha  hakuna  damu  kwenye  mishipa  ya  uume ulio simama.

Kadri  damu  inavyo  zidi  kuingia  ndani  ya mishipa  ya  uume, ndivyo  uume  unavyo  zidi  kuwa  mgumu  na  kukakamaa.

Na  kadri  damu  inavyo  hifadhiwa  ndani  ya  mishipa  ya  uume, ndivyo  uume  unavyo endelea  kusimama  wakati  wa  tendo  la  ndoa kwa  muda  mrefu.

Baada  ya  kumaliza  kufanya  tendo  la  ndoa,mishipa  ya  uume inarudi  katika  hali  yake  ya  kawaida (inanyauka ), ikisha  nyauka, mishipa  ya  ateri  inanyauka  pia, vena  zinafunguka  na  kunyonya  damu  katika  mishipa  ya  uume  na  kuirejesha  katika  sehemu nyinginezo  za  mwili  na  hatimaye  uume  kurudi  katika  hali  ya  kawaida  ( Flaccid ).

Hali  hii  itaendelea  kujirudia  kwa  kadri  utakavyo  kuwa  ukiendelea  kufanya  tendo  la  ndoa.

Mambo  Muhimu  Katika  Kuufanya Uume  Usimame na  Kuendelea  kudumu  katika  kusimama  kwa  muda  mrefu wakati  wa  tendo  la  ndoa.

Ili  uume  uweze  kusimama  imara  kama  msumari na  uendelee  kusimama  imara  na  kwa  muda  mrefu  wakati  wa  tendo la  ndoa, ni  lazima  mambo  yafuatayo yawepo.

1.Mishipa ya   uume iliyo  imara  na  yenye  afya  njema.
2.Mfumo   mzuri  wa damu  katika   mwili  mzima.
3.Mtiririko  imara  wa  damu kuingia  na  kutoka  ndani  ya  mishipa  ya  uume.
4.Ushirikiano  wenye  afya  kati  ya  mishipa  ya  fahamu  ya  kwenye  ubongo  (nerves), mishipa  ya  kwenye  uti  wa  mgongo  pamoja  na  mishipa  ya  kwenye  uume.

Ili  mwanaume  aweze  kuwa  imara  katika  tendo  la  ndoa, ni  lazima  mambo  manne  niliyo yataja  hapo  juu  yawe  sawa  sawa  bila  hitilafu  yoyote. Kinyume  chake, mwanaume  hawezi  kuwa  na  nguvu  za  kiume.

MAMBO   YANAYO SABABISHA   UKOSEFU/UPUNGUFU  WA  NGUVU  ZA  KIUME.
Tumeshajua   nguvu za  kiume  ni  nini, jinsi  uume  unavyo  simama, hatua  za  kusimama  kwa  uume, pamoja  na  mambo  yanayo  fanya  uume  uweze  kusimama  na  kuwa  na  uwezo  wa  kuendelea  kusimama  wakati  wa  tendo  la  ndoa.

Ni  vyema  tukajua  mambo  yanayo  sababisha  kushindwa  kusimama  kwa  uume, mambo  yanayo  sababisha  uume  ushindwe kuendelea  kusimama  kwa  muda  mrefu  wakati  wa  tendo  la  ndoa   pamoja  na  mambo  yanayo  fanya  mtu  ashindwe  kurudia  tendo  la  ndoa.

Yafuatayo  ni  mambo  yanayo  sababisha  ukosefu wa  nguvu  za  kiume.

1. MAGONJWA  YANAYO  SHAMBULIA  MFUMO  WA  DAMU  PAMOJA  NA  MISHIPA  YA  DAMU.

Damu  ndio  nishati  inayo wezesha  kusimama  kwa  uume  na kuufanya  kuwa  mgumu na  imara  kama  msumari.

Damu  ndio  nishati  inayo weza   kuufanya  uume uendelee kusimama  wakati  wa  tendo  la  ndoa.

Damu  ndio  nishati  inayo  upa  uume  uimara  na  uwezo  wa  kurudia  tendo  la  ndoa  zaidi  ya  mara  moja.

Hivyo  basi  ili  uume  uweze  kuwa  imara na  wenye  nguvu, pamoja  na  kuwa  na  uwezo  wa  kumudu  na  kustahimili   tendo  la  ndoa  wakati  wowote , basi  ni  lazima   mwanaume  awe  na mfumo  imara  wa  damu  utakao  ruhusu  kutiririka  kwa  damu  kwenda  katika  sehemu mbalimbali  za  mwili  ikiwamo  uume.

Ili  mfumo  uweze  kuwa  imara  ni  lazima  mhusika  awe  na  damu  ya  kutosha, na  pili  awe  na  mishipa  ya  damu  yenye  afya.

Katika  mwili  wa  mwanadamu,kuna  mishipa  inayo  tumika  kusafirisha  damu  kutoka  katika  sehemu moja  ya  mwili kwenda  katika  sehemu  nyingine  ya  mwili  ikiwemo  uume. Mishipa  hiyo  ni  kama  vile  vena (veins), atery ( ateri) na  capillary  ( kapilari )

Mishipa  hii  ya  damu  inapaswa  kuwa  imara  na  yenye  afya  njema  wakati  wote.   Mishipa  hii  ikipatwa  na  hitilifu, basi  itazuia  kusafirishwa  kwa  damu  katika  sehemu  mbalimbali za  mwili  wa  mwanadamu  na  hatimaye  kufanya  suala  la  kuwa  na  nguvu  za  kiume  kwa  mhusika  kuwa  ugumu  kwa  sababu   ya  kushindwa  kupeleka  damu  kwenye  mishipa  ya  uume.

Magonjwa  kwenye  mishipa  ya  damu  huzuia   kutirika  kwa  damu kwenye  ogani  muhimu   kama  vile  moyo, ubongo na  figo.

VIASHIRIA  VYA  MAGONJWA  KWENYE  MISHIPA  YA  DAMU.
Utajuaje  kwamba  una  magonjwa  kwenye  mishipa  yako  ya  damu ?

Ukiwa  una  matatizo  yafuatayo ya  kiafya, ni  ishara  kwamba, una  magonjwa  kwenye  mishipa  yako  ya  damu:

1.  Kolestrol ( Ama  lehemu  kwenye  damu )
Kolestrol  nyingi  kwenye  damu, huzuia  kutiririka  kwa  damu. Kolestrol  ikizidi  kwenye  damu,  hupelekea  kuziba   mishipa  ya  ateri  ambayo  kazi  yake  ni  kupeleka  damu  kwenye  uume. Matokeo  yake  ni  mhusika  kutokuwa  na  uwezo  wa  kusimamisha  uume  wake barabara  kwa  sababu uume  hauwezi  kusimama  bila  damu  kuingia  ndani  ya  mishipa  ya  uume.  
 
Hivyo  basi pamoja  na  dawa  ya  nguvu  za  kiume, yakupasa  kutibu  kolestrol. Unaweza  kuondoa  kolestrol  kwenye  damu  kwa  kutumia  dawa  mbali  za  asili  kama  vile mdalasini,uwatu, habbat sodah  etc.  Jinsi  ya  kujitibu  kolestrol  kwa  kutumia dawa asilia  tafadhali  tembelea


2. Shinikizo  Kubwa  la  Damu
Shinikizo  Kuu la  Damu husababisha  mishipa  ya  ateri  ambayo  hutiririsha  damu  iingiayo  kwenye  uume  kuziba  na  kushindwa kutanuka  kwa  kiwango  inachotakiwa  kutanuka.

Pia  huifanya  mishipa  laini  katika  uume   kushindwa  ku-relax  na  hivyo  kushindwa  kuizuia  mishipa  ya  vena  ya  kunyonya  damu  kutoka  kwenye  mishipa  ya  uume  na  kuipeleka  kwenye  maeneo  mengineyo  ya  mwilini.

Matokeo  yake  kunakuwa hakuna  kiasi  cha  kutosha  cha  damu  iingiayo  kwenye  uume  na  hivyo  kufanya  uume  ushindwe  kusimama.

Vile  vile  hata  kiasi  kidogo  cha  damu  kinacho  ingia  kwenye  uume, kinashindwa  kuendelea  kuhifadhiwa  ndani  ya  uume  wakati uume  ukiwa  umesimama, na  matokeo yake  ni  uume  kusinyaa  ndani  ya  kipindi kifupi  sana  tangu  usimame.

Pamoja  na kutumia  dawa  ya  nguvu  za  kiume, unapaswa   pia  kutumia  dawa  asilia  kujitibu  tatizo  la  shinikizo  kuu  la  damu.

Kufahamu  jinsi  ya  kujitibu  tatizo  la  shinikizo  la  damu  kwa  njia  ya  asilia, tembelea :


3.  Ugonjwa  wa  kisukari :
Ugonjwa  wa  kisukari  ni  miongoni  mwa  vyanzo  vikuu  vya  tatizo  la  ukosefu wa  nguvu  za  kiume.  Kusimama  kwa  uume  kunategemeana  na  kutiririka  kwa  damu  mwilini. Kisukari  huathiri  mishipa  ya  damu pamoja  na  usambazaji  wa  damu  kwenye  ogani  muhimu  mwilini  kama  vile  moyo, ubongo, figo  na  uume.

Kiukweli, mwanaume  mwenye  kisukari  yupo  katika  risk  kubwa  ya  kupatwa  na  tatizo  la  ukosefu  wa  nguvu  za  kiume,m tena  katika  kiwango  kikubwa  sana.

Unashauriwa pamoja  na kutumia  dawa  ya  nguvu  za  kiume, tumia  pamoja  na  dawa  mbalimbali  za  asili  kwa  ajili  ya  kubalance  sukari  yako mwilini. 
 
Zipo  dawa  mbalimbali  za  asili  zinazo  saidia  kubalance  kiwango  cha  sukari  mwilini. Dwa  hizo  ni  pamoja na mdalasini, unga  wa  uwatu, mbegu  za  uwatu, manjano, majani  ya  manjano,mbegu  za  katani, nakadhalika.
 
 Namna  ya  kutumia  dawa  hizo  kujitibu  tatizo  la  sukari, tafadhali  tembelea :http://neemaherbalist.blogspot.com/2015/07/jitibu-kisukari-presha-shinikizo-la.html

4. Magonjwa  ya  figo
Tatizo  la  ugonjwa  wa  figo  huathiri  vitu vingi  ambavyo  ni  muhimu  sana  katika  kuufanya  uume  uweze  kusimama  na  kuendelea  kudumu  katika  kusimama.

Tatizo  la  figo, huathiri  homoni, huathiri kutiririka   kwa  damu  kwenda  kwenye  mishipa  ya  uume. Huathiri  mfumo  wa mishipa  ya  neva  pamoja  na  nishati  ya  mwili mzima.

Pamoja  na  dawa  ya  kutibu  tatizo  la  nguvu  za  kiume, unapaswa  pia, kutibu  tatizo  la  figo.
 
 Kufahamu  jinsi  ya  kujitibu  magonjwa  mbalimbali  ya  figo  kwa  kutumia  dawa  mbalimbali  asilia, tembelea : http://neemaherbalist.blogspot.com/2015/07/jitibu-kisukari-presha-shinikizo-la.html

5.  Ugonjwa  wa  moyo
Moyo  ndio  supplier  mkubwa  wa  damu  katika  sehemu  mbalimbali  za  mwili.  Ugonjwa  wa  moyo  hupunguza  uwezo  wa  moyo  kusambaza  damu  kwenye  mishipa  mbalimbali  ya  damu  na  hivyo  kuathiri  utendaji  kazi  wa  mishipa ya  damu  kama  vile  ateri  na  vena.
 
 Matokeo  yake  ni  mishipa  hiyo  kushindwa  kupeleka  damu  ya  kutosha  katika  uume  pamoja  na  kushindwa  kuifanya  mishipa  ya  uume  kurelax na  matokeo  yake,. Ukosefu  wa nguvu  za  kiume. 
 
Hivyo  basi, pamoja  na  dawa  ya  nguvu  za  kiume, unapaswa  pia   kutibu  tatizo  la  moyo. Kufahamu  jinsi  unavyo  weza  kutibu  ugonjwa  wa  moyo  kwa  dawa  asilia, tembelea :


6.  Kupwaya  kwa  mishipa  ya  vena.
Kazi  kubwa  ya  mishipa  ya  vena  kwenye  uume   kunyonya  damu  iliyomo  ndani  ya  mishipa  ya  uume  na  kuipeleka  katika  sehemu  nyingine  za  mwili. 
 
 Mishipa  ya  vena  iliyopo  karibu  na  uume  kazi  yake  kubwa  ni  kuhakikisha  hakuna  damu  yoyote  kwenye  mishipa  ya  uume. ( KUMBUKA  KUWA  DAMU  NDIO  HUFANYA  UUMU  USIMAME, HIVYO  CHOCHOTE  KILE  KITAKACHO  FANYA  DAMU  ISIKAE  NDANI  YA  MISHIPA  YA  UUME , KITAFANYA  UUME  USINYAE  )

Ili  uume  uendelee  kusimama  ni  lazima, mishipa  ya  vena  isiwe  na  uwezo  wa  kunyonya  damu  kutoka  kwenye  mishipa  ya  uume  kupeleka  nje  ya  mishipa  ya  uume.

Na  ili  mishipa  ya  vena  isiwe  na  uwezo  wa    kunyonya  damu  kutoka  kwenye   mishipa  ya  uume  ulio  simama  na  kuipeleka  kwenye  sehemu  nyingine  za  mwili,  ni  lazima  mishipa  ya  uume  iwe  imara  na  thabiti  isiyo  na  hitilafu  yoyote  ile.

Mishipa  ya  vena  ikipwaya, mwanaume  hutokuwa  na  uwezo  wa  kusimamisha  uume  wako, na  ikitokea  umefanikiwa  kuusimamisha  basi  utasimama  ukiwa  legelege  sana  na  utasinyaa  ndani  ya  muda  mfupi  sana, kwa  sababu  damu  iliyo  ingia  ndani  ya  uume  wako  na  kuufanya  usimame, itanyonywa  ndani  ya  muda  mfupi  sana  na  kutolewa  nje  ya  mishipa  ya  uume  na  hivyo  kuufanya  uume  wako  usimame.

Tatizo  la  kupwaya  kwa  mishipa  ya  vena  linasababishwa  na  kupiga  punyeto  kwa  muda  mrefu  pamoja  na  ugonjwa  wa  kisukari.

KUPIGA  PUNYETO  KWA  MUDA  MREFU:  Kupiga  punyeto  kwa  muda  mrefu  ni  moja  kati  ya  vyanzo  vikuu  vya  tatizo  la  la  ukosefu  wa  nguvu  za  kiume.  Asilimia  kubwa  ya  vijana  wenye  tatizo  la  ukosefu  wa  nguvu  za  kiume, linasababishwa  na  upigaji  wa  punyeto  kwa  muda  mrefu.

JINSI  PUNYETO  INAVYO  SABABISHA  UKOSEFU  WA  NGUVU  ZA  KIUME.

Unapopiga  punyeto  unakuwa  unaiminya  mishipa  ya  uume   ambayo  ndio  inaufanya  uume  usimame.

Matokeo  yake  unaifanya  mishipa  hiyo  ilegee na  kutokuwa  na  uwezo  wa  kusimama  tena.

Mishipa  ya  uume  iliyo  legea  kutokana  na  upigaji  punyeto, huleta  madhara  yafuatayo  :

i. Huondoa  uwezo  wa  mishipa  ya  uume  kurelax.
( Unapopata  wazo  la  kufanya  tendo  la  ndoa, mishipa  ya  uume  ina relax  , mishipa  iki  relax  husababisha  mishipa  ya  ateri  kupanuka  na  kuruhusu  damu  kingie  ndani  ya  mishipa  ya  uume  na  hatimaye  kuufanya  uume  usimame  na  kuwa  mgumu)

ii.Mishipa   ya  kiume  ikishindwa  ku relax  husababisha  mishipa  ya  ateri  kuziba

iii. Mishipa  ya  ateri  ikiziba, damu  haiwezi  kutiririka  kuingia  kwenye  mishipa  ya  uume, na  hata  ikitokea  damu  imeingia  ndani  ya  mishipa  ya  uume  basi  huingia  kiasi  kidogo sana   tena  kwa  presha  ndogo  sana  hivyo  basi  hata  kama  uume  utasimama   basi  utasimama  ukiwa  legelege  sana

iv.Mishipa  ya  uume  ikishindwa  kurelax  basi  haitakuwa  na  uwezo  wa  kuipush  na  kuiziba  mishipa  ya  vena  ambayo  ndio  hunyonya  damu  kutoka  kwenye  mishipa  ya  uume  ulio  simama. Matokeo  yake  basi, damu  kidogo  iliyo  ingia  ndani  ya  mishipa  ya  uume  na  kuufanya  uume  kusimama, hunyonywa  na  kutolewa  nje  ya  mishipa  ya  uume  ndani  ya  sekunde  chache  sana  na  hivyo  kuufanya  uume usinyae  ndani  ya  muda  mfupi  sana.

v.         Mishipa  ya  uume  kulegea
vi.       Uume  kurudi ndani  na  kusinyaa  na  kuwa  kama  uume  wa  mtoto

6. Tatizo  la  unene  kupita  kiasi : Tatizo  la  unene  na  uzito  kupita  kiasi  ni  miongoni  mwa  mambo  yanayo  sababisha  upungufu  wa  nguvu  za  kiume. Unene  kupita  kiasi  humuweka  mtu  katika  hatari  ya  kupatwa  na  magonjwa  kama  vile  kisukari, presha, moyo  na  shinikizo  kuu  la  damu. 
 
Na  magonjwa  ya  kisukari, moyo,presha  na  shinikizo  la  damu  husababisha  upungufu na  ukosefu  wa  nguvu  za  kiume, na  hivyo  kumuweka  muhusika  katika  hatari  kuu  ya  kupatwa  na  tatizo  la  ukosefu/upungufu  wa  nguvu  za  kiume.

Hivyo  basi  kwa  wewe  mwenye  tatizo  la  unene  na  uzito  kupita  kiasi , pamoja  na  kutumia  tiba  ya  nguvu  za  kiume,  ni  vyema  ukafanya  na  mpango  wa  kupunguza  unene  na  uzito  wako.

JINSI  YA  KUPUNGUZA  UZITO  NA  UNENE  KWA  KUTUMIA  TIBA  ASILIA, TAFADHALI  TEMBELEA:


7.   Matatizo  Katika  mfumo  wa  Ubongo
Uume  hauwezi  kusimama   bila  ya  kuwa  na  ushirikiano  na  ubongo.  Ili mtu  uume  uweze  kusimama, mtu  lazima  apate  wazo  la  kufanya  tendo  la  ndoa  (UBONGO  UNA HUSIKA  HAPO ), akishapata  wazo, ubungo  hupeleka  ishara  kwenye  mishipa  ya  fahamu  iliyopo  katika  uti  wa  mgongo  ambayo  nayo hupeleka  taarifa  kwenye  mishipa  ya  uume  then  uume  usimama.   
 
Hivyo  basi  ili  mtu  aweze  kuwa  na uwezo  wa kusimamisha  uume  wake  ni lazima  kuwa  na  mawasiliano  mazuri  na  imara  kati  ya mishipa  ya  fahamu ( ubongo ), mishipa  ya  kwenye  uti  wa  mgongo   na  mishipa  ya  kwenye    uume.  Bila  ushirikiano  kati  ya  vitu  hivyo  vitatu, uume  hauwezi  kusimama.

Magonjwa  yanayoweza  kuathiri  ushirikiano  kati  ya  mishipa  ya  ubongo  na  mishipa  ya  uume, yanaweza  kusababisha  kushindwa  kusimama  kwa  uume.

Magonjwa  hayo  ni  pamoja  na  kiharusi,kupoteza  kumbukumbu  (  Alzheimer ), multiple  sclerosis pamoja  na  ugonjwa  wa  Parkinson.

Ni  vyema  mgonjwa  akatibiwa  kwanza  magonjwa  hayo  kabla  ya  kuanza  kutumia  dawa  ya  nguvu  za  kiume.  Kufahamu  jinsi  ya  kujitibu  magonjwa  tajwa  hapo  juu  kwa  njia  asilia,tafadhali  tembelea

Mambo   mengine  yanayo  sababisha  ukosefu  na  upungufu  wa  nguvu  za  kiume, ni  pamoja  na  maumivu & majeraha  kwenye  uti  wa  mgongo,  chango  la  kiume , ngiri  na  matatizo  katika  homoni.

VIASHRIA  VYA  MTU  MWENYE  TATIZO  LA  UKOSEFU/UPUNGUFU  WA  NGUVU  ZA  KIUME.

Mtu  mwenye  tatizo  la  ukosefu  wa  nguvu  za  kiume  huwa  na  dalili  zifuatazo ;

1. Kushindwa  kabisa  kusimamisha  uume  wake
2. Uume  kusimama  ukiwa  legelege
3. Kuwahi  kumaliza  tendo  la  ndoa
4. Mwanaume  kutokuwa  na uwezo  wa  kufanya  tendo  la  ndoa  katika  baadhi  ya  staili  ( Mara  nyingi   mwanaume  huyu huwa  na  uwezo  wa  kufanya  tendo  la  ndoa    staili  moja  tu ).  
 
Hapa  mwanaume  anakuwa  na  uwezo  wa  kufanya  tendo  la  ndoa  kwa  staili  ya   “ missionary” pekee.  Ikibadilishwa   staili, mwanaume  anakuwa hana  tena  uwezo  wa  kusimamisha  uume  wake  japo  katika  hali  ya lege  lege

5. Uume  kutokuwa  na  uwezo  wa  kusimama  wenyewe   bila  kushikwashikwa  ama  kutomaswa kwa  muda  mrefu.

6. Uume  kusinyaa  ukiwa  ndani  ya  mwanamke.

7. Uume  kusinyaa, pindi  inapotokea  activity  yoyote  ya  kiungo  ama  ogani  nyingine  ya  mwanaume  wakati  wa  tendo  la  ndoa. Kwa  mfano, wakati  wa  tendo  la  ndoa, ikitokea  mwanaume  amekohoa  au  kupiga  chafya, uume  nao  unasinyaa.

8. Uume  kusinyaa  mara  tu  baada  ya kutolewa  ndani  ya  uke ( Kwa  mfano  kama  unafanya  tendo  la  ndoa, halafu  uume  ukatoka  nje, kitendo  cha  kuushika  kuurudisha ndani, tayari  una  sinyaa )

9. Kutokuwa  na  uwezo  wa  kurudia  tendo  la  ndoa.
10.  Kupatwa  na  maumivu  wakati  wa  tendo  la  ndoa.

VIASHIRIA  VYA  MWANAUME  ASIYE 
NA  TATIZO  LA UKOSEFU  WA  NGUVU  ZA  KIUME.
Mwanaume  asiye  na  tatizo  la  ukosefu  wa  nguvu  za  kiume, huonyesha  ishara  zifuatazo ;

i. Uume  husimama  ukiwa  imara  kama  msumari.

ii.Hukaa  kifuani  kwa  muda  mrefu  ( Wastani  ni  kati  ya  dakika  20  hadi  45  )

iii.Huweza  kurudia  tendo  la  ndoa  zaidi  ya  mara  tatu  bila  misuli  ya  uume  kuchoka.

iv. Huweza  kufanya  tendo  la  ndoa  kwa  staili  yoyote  ile

v. Uume  husimama  wenyewe  bila  kushikwa  shikwa  wala  kuwa  stimulated  kwa  namna  yoyote  ile

vi.Kwa  ufupi  anakuwa  na  uwezo  wa  kufanya na  kukamilisha  tendo  la  ndoa  kwa  uukamilifu  mkubwa.

TIBA  ASILIA  YA  TATIZO  LA  UKOSEFU/UPUNGUFU  WA  NGUVU  ZA  KIUME.
Dawa  asilia  ya  JIKO   ni  dawa  asilia  inayo  tibu  na  kuponyesha  kabisa  tatizo  la  ukosefu  wa  nguvu  za  kiume.

MFUMO   WA  DAWA
Dozi  ya  dawa  ya  JIKO ni  mkusanyiko  wa  dawa  nne  asilia  zenye  uwezo  mkubwa  sana  katika kutibu  na  kuponyesha  kabisa  tatizo  la  ukosefu/upungufu  wa  nguvu  za  kiume.

Dawa  hizi  zipo  katika  mfumo  wa  MIZIZI  na  UNGA  UNGA.

JINSI   DOZI  YA  DAWA  YA  JIKO  INAVYO  FANYA  KAZI.
Dozi  ya  dawa  ya  JIKO  inafanya  kazi  zifuatazo  katika  mwili  wa  mwanadamu.

KAZI  INAYO  FANYWA  NA  DAWA  YA  JIKO .
Dawa  ya  JIKO  inasadia  katika  mambo  makuu yafuatayo:

1.  Inasaidia   kuimarisha  mishipa  ya  uume  ulio legea  na  hivyo  kuufanya  uume  uwe  na uwezo  wa  kusimama  barabara  kama  msumari  wakati  wa  tendo  la  ndoa.

2. Inasaidia  kusafisha  mishipa  ya  kwenye  uume  na  hivyo  kusaidia  katika  kuongeza  kasi  ya  msukumo  wa  damu  kwenye  mishipa  ya  kwenye  uume.

3. Huongeza  damu  mwilini

4. Husaidia  kuongeza  msukumo (pressure)  wa  damu  kwenye  mishipa  ya  uume  na  hivyo  kuufanya  uume  kuwa  na  nguvu  za  ajabu.

5. Huipa  misuli  ya  uume  uwezo  wa  kuziba  wa  kuizuia  mishipa  ya  vena   kunyonya  damu  kwenye  mishipa  ya  uume  wakati  wa  tendo  la  ndoa  na  matokeo  yake  kukupa  uwezo  wa  kufanya  tendo  la  ndoa  kwa  muda  mrefu( Kuzuia  hali  ya  kufika  kileleni  haraka  )

6. Husaidia  kurelax  mind  na  hivyo  kumfanya  mtu  awe  na  uwezo  wa  kuconcentrate  wakati  wa  tendo la  ndoa   bila  kuathiriwa  na  msongo  wa  mawazo

7.  Hurejesha, kuimarisha  na  kuboresha  ushirikiano  kati  ya  mishipa  ya  fahamu  ya  kwenye  ubongo  (nerves), mishipa  ya  kwenye  uti  wa  mgongo  pamoja  na  mishipa  ya  kwenye  uume

8. Humfanya  mwanaume  awe  na  uwezo  wa  kurudia  tendo  la  ndoa  mara  nyingi  zaidi  bila  kuchoka.
9. Husaidia  kuongeza  hamu  ya  tendo  la  ndoa.

10.Husaidia  kuurudisha  nje  uume  ulio ingia  ndani.

11. Husaidia  kutibu  side effects  za  punyeto  na  matumizi  ya  muda  mrefu  ya dawa  kali  za  (za  kizungu ) za  kuongeza  nguvu  za  kiume.

12. Husaidia  kutibu  chango  la  kiume.
13. Dawa  hii  huwasaidia  hata  wanawake  wanao sumbuliwa  na  tatizo  la  ukosefu  wa  hamu ya  tendo  la  ndoa.

BEI  YA  DAWA:  Dozi  ya  dawa  ya  JIKO  inapatikana  kwa  gharama  ya  SHILINGI  ELFU  THEMANINI  TU  (Tshs.80,000/=)

DAWA  HII  IMETHIBITISHWA  NA  MKEMIA  MKUU  WA  SERIKALI.

MAHALI  TUNAPOPATIKANA :
Dozi  ya  dawa  ya  JIKO, inatolewa  na  duka  la  dawa  asilia  la  NEEMA  HERBALIST    NUTRITIONAL  FOODS  CLINIC. Tunapatikana  jijini  DAR ES  SALAAM, katika  eneo  la UBUNGO    karibu  na  SHULE  YA  MSINGI  UBUNGO  NATIONAL  HOUSING  nyuma  ya  jengo  la  UBUNGO  PLAZA.

Kwa  wasio  weza  kufika  ofisini  kwetu, tunatoa  huduma  ya kuwapelekea  dawa  mahali  walipo  ( DELIVERY )

Kwa  wateja  waliopo  nje  ya  DAR  ES  SALAAM, watatumiwa  dawa  kwa  njia  ya  mabasi, wateja  waliopo  Zanzibar, watatumiwa  dawa  kwa   njia  ya  boti  na  kwa  wateja  waliopo  Ulaya, America  na  Arabuni, watatumiwa  dawa  kwa  njia  ya  DHL  au POSTA.

WASILIANA  NASI  KWA  SIMU  NAMBA
0766  53  83  84.
Na  kwa  maelezo  zaidi  kuhusu  huduma  zetu, endelea  kutembelea:

www.neemaherbalist.blogspot.com

Rais Magufuli na Mkewe Wavutiwa na kipindi cha Clouds 360 mpaka Wameamua Kupiga Simu LIVE Studio....Wasikilize hapa

$
0
0

Rais John Magufuli na Mkewe, Mama Janeth leo amekuwa Rais wa kwanza Tanzania kupiga simu ya surprise moja kwa moja kwenye kituo cha runinga kama mtazamaji wa kawaida akichangia yaliyokuwa yanajadiliwa kwenye kipindi.

Magufuli amezungumza moja kwa moja na watangazaji wa kipindi cha ‘360’ cha Clouds TV akiwapongeza kwa kazi nzuri wanayoifanya ikiwa ni pamoja na namna walivyochambua magazeti na mijdala mingine. Moja kati ya mijadala hiyo ilikuwa mjadala uliohusu ziara yake Benki Kuu.

Rais Magufuli pia aliisifu ‘Clouds Media Group’ kwa namna wanavyofanya kazi akiigusia tukio la ‘Malikia wa Nguvu’ lililolenga kutambua mchango wa wanawake nchini katika kuzitambua fursa na kuzifanyia kazi ipasavyo.

==> Msikilize Rais Magufuli akiongea live na watangazaji wa clouds

Kiongozi wa CUF Aliyetangaza Kuwa Wafuasi wa Chama Hicho Wamekimbilia Porini Akamatwa na Polisi

$
0
0

Ikiwa ni siku tatu tangu Mkurugenzi wa Habari Uenezi na Mawasiliano ya Umma wa Chama cha Wananchi (CUF), Hamad Masoud Hamad, atangaze kuwa baadhi ya wananchi wa Zanzibar wanakimbilia porini kuhofia usalama wao, ametiwa mbaroni.

Kukamatwa kwa Masoud sasa kunafanya idadi ya viongozi wa chama hicho waliotiwa mbaroni na kuhojiwa polisi kufikia wanne tangu kufutwa kwa matokeo ya Uchaguzi Mkuu Oktoba 28, mwaka jana.

Viongozi wengine waliohojiwa na Polisi na kuachiwa kwa dhamana ni Naibu Katibu Mkuu, Nassor Ahmed Mazrui, Mkurugenzi wa Mipango na Uchaguzi, Omar Alin Shehe na mshauri wa mikakati wa chama hicho, Eddy Riyami.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja, Mkadam Khamis Mkadam, jana alithibitisha kukamatwa kwa Masoud, ambaye ni Waziri wa zamani wa Miundombinu na Mawasiliano katika Serikali ya Umoja wa Kitaifa.

Alisema kiongozi huyo alikamatwa na kitengo cha upelelezi nyumbani kwake mtaa wa Mbweni mjini Zanzibar jana.

Alisema kwa sasa anashikiliwa katika Kituo cha Polisi cha Mwembe Madema ili kusadia uchunguzi juu ya taarifa alizotoa katika mkutano wake na waandishi wa habari na kuzungumzia hali ya amani ya Zanzibar na wananchi wake.

“Tunamshikilia kwa uchunguzi, kuna mambo ya msingi tunaona yanahitaji kufanyiwa uchunguzi na yeye kusadia polisi uchunguzi wake,” alisema Mkadam.

Kufuatia kukamatwa huko kwa Masoud, CUF imelaani kitendo hicho na kusema kuwa kamata kamata hiyo inawalenga viongozi wa chama hicho na wanachama wake pekee.

Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho, Mazrui alisema matukio yote ya uvunjifu wa amani yaliyotokea visiwani hapa, yamekuwa yakihusishwa  na CUF na Jeshi la Polisi huwakamata viongozi wa chama hicho pekee.

“Tunasema huu ni uonevu wa hali ya juu, maana viongozi na wafuasi wa CUF pekee ndio wanaoshikiliwa na Jeshi la Polisi, hii yote inatokana na uchaguzi wa marudio, hivyo  kutoshiriki kwetu kwa uchaguzi isiwe sababu ya kuadhibiwa,” alisema.

Aidha, alisema suala la kushiriki au kutoshiriki katika uchaguzi ni hiari ya mtu, hivyo kwa wale ambao hawatashiriki uchaguzi huo, wasiadhibiwe wala wasidhalilishwe na wale ambao wametangaza kushiriki waende wakapige kura.

Kwa upande wa mke wa Masoud, Rahma Issa, alisema askari kazu wasiopungua sita wakiwa na silaha za moto mbili walifika nyumbani jana saa moja asubuhi na kudai wanamhitaji mumewe.

Alisema baada ya kubisha hodi, kijana wake mmoja alifungua mlango na kisha askari watatu waliingia ndani mmoja akiwa na silaha ya moto kifuani.

“Baada ya kuamshwa na kutoka chumbani walimwambia yupo chini ya ulinzi anahitajika kituo cha polisi,” alisema Rahma.

Hata hivyo, alisema baada ya kumkamata, hawakumwambia sababu ya kukamatwa kwake, lakini baada ya kuwauliza wanampekeka kituo gani walimwabia Kituo cha Polisi Mwembe Madema, Zanzibar.

Naye Mkurugenzi wa Mipango na Uchaguzi wa CUF, Omar Ali Shehe, alisema vitendo vya kukamatwa viongozi wa CUF ni mwendeleo wa Serikali ya CCM kuwanyanyasa viongozi na wanachama wake chama hivyo visiwani hapa.

Alisema vitendo vnavyoendelea kufanywa na Jeshi la Polisi vinakwenda kinyume cha misingi ya demokrasia na haki za binadamu.

Shehe alisema matunda ya Serikali ya Umoja wa Kitaifa ya kujenga amani na umoja wa kitaifa yameanza kuvurugwa tangu kuingia mgogoro wa uchaguzi mkuu.

Taarifa Ya TRA Kuhusu Tishio la wafanyabiashara kufunga maduka

$
0
0

Mojawapo ya wajibu wa kisheria wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ni kukagua taarifa za wafanyabiashara ili kuhakiki usahihi wa kumbukumbu za biashara. 

Katika kutekeleza zoezi hili, TRA imechukua hatua mbalimbali ikiwemo kuwaelimisha wafanyabiashara juu ya umuhimu wa kutunza kumbukumbu za biashara na kusisitiza utumiaji wa mashine za kielektroniki za kodi (EFDs). 

Wakati wa kutekeleza jukumu hilo TRA ilibaini wafanyabiashara wengi wanakiuka sheria za kodi kwa kutokutoa risiti, hivyo wamekuwa wanachukuliwa hatua stahiki kwa mujibu wa sheria.

Vilevile Mamlaka ya Mapato Tanzania imebaini kuwa kuna njama ya baadhi ya wafanyabiashara kuhamasisha wenzao nchi nzima kufunga biashara kwa makusudi endapo tutaendelea na ufuatiliaji na uhakiki wa bidhaa zilizouzwa bila kutolewa risiti na kutekeleza agizo la serikali la kusitisha matumizi ya kodi elekezi kwa bidhaa zinazoingizwa nchini. Njama hizi ni ukiukwaji wa sheria na hazipaswi kuvumiliwa.

Wafanyabiashara na wananchi wote kwa ujumla wanafahamishwa kwamba kutokutoa risiti baada ya kufanya mauzo au kutoa huduma ya kibiashara ni kosa la jinai linalostahili adhabu. 

Hivyo wafanyabiashara wanatahadharishwa kutofunga maduka kutokana na sababu zinazotolewa na wafanyabiashara wanaofanya njama hizo.

Endapo TRA itawabaini wafanyabishara wanaokula njama hizi itachukua hatua kali za kisheria dhidi yao ambazo zitapelekea kuzuiwa kufanya biashara moja kwa moja hapa nchini.
 
TRA inatoa wito kwa wananchi wote kudai risiti kila wanapofanya manunuzi na kutoa taarifa za wafanyabiashara ambao hawatoi risiti. Vilevile wanaombwa kutoa taarifa katika ofisi yoyote ya TRA za kuwafichua wafanyabiashara wanaokula njama za kuhamasisha wenzao nchi nzima kufunga biashara kwa makusudi.

Taarifa hizi zinaweza kutolewa pia kupitia namba za simu zifuatazo: 0800780078 au 0800750075.

Barua pepe
Huduma@tra.go.tz
au services@tra.go.tz

“Pamoja Tunajenga Taifa Letu”
Alphayo J. Kidata
KAMISHNA MKUU

Mahakama Yataka Upelelezi wa Kesi Ya Wabunge Halima Mdee, Mwita Waitara na Saed Kubenea Ukamilike Haraka

$
0
0

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imeutaka upande wa mashtaka kukamilisha upelelezi haraka ili kesi inayowakabili wabunge watatu wanaotokana na Ukawa na madiwani wao ianze kusikilizwa.

Washtakiwa hao ni pamoja na Mbunge wa Kawe, Halima Mdee, Mwita Waitara (Ukonga) na Saed Kubenea (Ubungo).

Madiwani wanaoshtakiwa katika kesi hiyo ni Ephrein Kinyafu (Kimara), Manase Njema (Kimanga, Tabata) na kada wa chama hicho, Rafii Juma.

Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba alitoa kauli hiyo jana baada ya Wakili wa Serikali, Mbunito Aloyce kudai kesi ilikuja kwa ajili ya kutajwa kwa kuwa upelelezi wake haujakamilika na kuomba ipangiwe tarehe nyingine.

Wakili Peter Kibatala anayewatetea washtakiwa hao, aliuomba upande wa mashtaka kuanza kuisikiliza kesi hiyo kwa sababu washtakiwa walikamatwa haraka haraka na usikilizaji wake uwe vivyo hivyo.

Washtakiwa hao wanaodaiwa kumjeruhi Katibu Tawala wa Mkoa wa Dar es Salaam, Theresa Mmbando katika vurugu zilizotokea Februari 27,2016 Ukumbi wa Karimjee kwenye Uchaguzi wa meya na naibu meya wa jiji la Dar es Salaam, wanatetewa na Mawakili Peter Kibatala na John Malya. Kesi hiyo imeahirishwa hadi Aprili 18.

Miss Tanzania kuanza tena Machi 19 mwaka huu

$
0
0

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye anatarajiwa kuwa mgeni Rasmi katika ufunguzi wa Mashindano ya Miss Tanzania mwaka 2016  yatakayofanyika Machi 19, 2016 jijini Dar es Salaam.

Akizungumzia mashindano hayo leo jijini Dar es Salaam Mkurugenzi wa Lino International Agency Limited kampuni inayoandaa  mashindano hayo Bw. Hashim Lundenga amesema kuwa uzinduzi huo kwa mwaka 2016 utakuwa wa aina yake tofauti na miaka iliyopita.

“Tunatarajia kutangaza kamati mpya ya Miss Tanzania siku hiyo ya uzinduzi, kamati ya Miss Tanzania itakuwa na jukumu la kuusaidia uongozi wa Miss Tanzania katika shughuli nzima za kuratibu na kusimamia mashindano hayo.” alisema Lundenga.

Lundenga ameongeza kuwa, katika uzinduzi huo wadau mbalimbali wa tasnia ya urembo wakiwemo wabunifu wa mavazi, mawakala wanaoandaa mashindano ya Miss Tanzania katika ngazi mbalimbali hapa nchini watakutana .

Aidha  amesema uzinduzi wa Miss Tanzania mwaka 2016 umedhaminiwa na makampuni ya Ramada Resorts Dar, Naf Beach Hotel Mtwara, Kitwe General Trader, CXC Africa, MMI Tanzania, Mwandago Invesment Ltd, Break Point na GSM Media.

Vilevile uzinduzi huo utahamia mkoa wa Arusha mara tu baada ya kufanyika  mkoa wa Dar es Salaam. Wasanii Linah Sanga anayeimba nyimbo za kizazi kipya na Wanne Star msanii wa ngoma za asili watatoa burudani katika uzinduzi huo.

Mashindano ya Miss Tanzania yalifungiwa kwa miaka miwili mfululizo na Baraza la Sanaa Tanzania (BASATA) Desemba 22, 2014 kutokana na kukiuka Sheria, Kanuni na Taratibu za uendeshaji matukio ya Sanaa nchini, kutokuwasilisha nyaraka mbalimbali za shindano lake hususan mikataba ya washiriki pamoja na kutumia mawakala wasiosajiliwa na kupewa vibali vya BASATA.

Mashindano hayo yamefunguliwa tena na BASATA Agosti, 2015 baada ya mwandaaji wake LINO International Agency Limited kufuata taratibu ikiwemo kuomba radhi  na kuyafanyia kazi baadhi ya mapungufu yaliyojitokeza pamoja na kutekeleza masharti aliyopewa.

CUF Watoa Tamko Jipya......Wampinga Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Aliyesema jana kuwa Kuna Amani ya Kutosha Zanzibar

$
0
0
Naibu Katibu Mkuu wa CUF (Bara) , Magdalena Sakaya akionyesha picha ya mhanga wa vipigo zanzibar.
****
WAKATI uchaguzi wa marudio ukitarajiwa kufanyika jumapili visiwani Zanzibar, Chama Cha Wananchi (CUF) kimesema kuwa haki za binadamu zimeendelea kuminywa kwa kiasi kikubwa visiwani humo huku wafuasi wa chama hicho wakilengwa zaidi.

Naibu Katibu Mkuu wa CUF (Bara) , Magdalena Sakaya, ameyasema hayo leo wakati alipozungumza na waandishi wa habari kwenye Makao Makuu ya Ofisi za Chama hicho zilizopo Buguruni  jijini hapa.

Magdalena amesema kuwa Tanzania imeridhia mikataba mbalimbali ya kimataifa ya haki za binadamu hivyo mambo yanayotokea Zanzibar ni ya kushangaza na hayapaswi kufumbiwa macho kwa ustawi wa Taifa.

Amesema kuwa baada ya CUF kutangaza kujitoa kwenye kinyang’anyiro cha uchaguzi wa marudio , wananchi wa Zanzibar wamekuwa wakiishi kwa hofu huku vikundi vya matukio ya uhalifu maarufu’mazombi’ yakipiga watu pasipo na kuchukuliwa hatua zozote na vyombo vya usalama.

“Mara kwa mara tumekuwa tukiwaambia jeshi la polisi kuhusiana na haya mazombi ila cha kushangaza hadi leo hakuna taarifa yoyote iliyotolewa kuhusiana na kukamatwa kwa makundi hayo ya mazombi,”alisema.

Chama hicho kimesema kuwa viongozi wao kadhaa wamekamatwa kwa nyakati tofauti ambapo jana Mkurugenzi wa Habari na Uenezi Taifa -Hamad Masoud, alikamatwa na kuwekwa kizuizini na Polisi baada ya kutoa taarifa ya matukio mbalimbali yanayoendelea visiwani humo ambayo ni ya kinyume na haki za binadamu.

“Jambo la kushangaza kila tukio baya likitokea wanasingiziwa wafuasi wetu, mara kwa mara wamekuwa wakikamatwa na tangu januari hadi sasa zaidi ya wafuasi 60 wamekamatwa kwa madai ya kuhusika na uvunjifu wa amani,”alisema.

“Sisi tumeamua kujitoa kwenye uchaguzi huo ili wananchi wetu wawe huru na kuwaepusha kwenye vurugu, kwa hiyo
Chama cha Mapinduzi kisiwalazishe wananchi kufanya mambo ambayo wenyewe hawako tayari kuyafanya na kuyaona ni kinyume na Katiba, kwa sababu uchaguzi huo wa marudio ni haramu.

“Asilazimishwe mbuzi kunywa maji wakati hana kiu,”alisema Magdalena na kuongeza kuwa wangetegemea uchaguzi huo kufanyika kwa amani baada ya kutangaza kujitoa mapema mwaka huu.
Magdalena alisema kuwa yapo maeneo kadhaa visiwani humo wananchi wamepigwa marufuku ya kutoonekana wakitembea kuanzia saa mbili usiku hatua inayosababisha hata wengine kushindwa kwenda kufanya ibada.

Akizungumzi kauli ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga, ya kusema kuwa hakuna watu wanaopigwa visiwani humo, Kiongozi huyo wa Chama alipinga madai hayo na kusema kuwa ni hatari kuudanganya umma kwa kuficha ukweli na kuacha watanzania wateswe.

Aliishauri Serikali kuhakikisha kuwa usalama wa wananchi visiwani humo unaimarishwa kwa kufuata misngi ya haki za binadamu na utawala bora, pia ichukue hatua dhidi ya ‘mazombi’ ambayo yamekuwa yakiripotiwa kupiga watu kwa nyakati tofauti. 

Mwigulu Nchemba aonya kuhusu mauaji ya kisiasa

$
0
0

WAZIRI wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi,  Bw. Mwigulu Nchemba amesema hakuna chama cha siasa ambacho kinaweza kuthaminishwa na maisha ya mwanadamu na kwamba wananchi hawana sababu ya kupigana na kutoana uhai kwa sababu ya ushabiki wa vyama.
 
Ametoa kauli hiyo jana mchana (Alhamisi,  Machi 17, 2016) wakati akizungumza na mamia ya wakazi wa mji mdogo wa Katoro, wilayani Geita alipopewa nafasi kuwasalimia wananchi kwenye mkutano wa Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa. 
 
“Duniani kote hakuna chama cha siasa kinaweza kuwa na thamani sawa na maisha ya mwanadamu au damu ya mwanadamu. Ninazungumza hili nikihusisha na matukio ya hivi karibuni hapa Geita na kule Tunduma ambako raia wetu walipoteza maisha kwa sababu ya tofauti za kisiasa, “alisema.
 
Aliwauliza wananchi hao ni kwa nini wanapigana hadi kutoana uhai wakati wao (wananchi) hawaendi bungeni. “Ninyi mnaopigana hakuna hata mmoja wenu anayeingia bungeni lakini sisi tukikutana kule bungeni tunasalimiana na kugongeshana glasi. "
 
Akitolea mfano kauli hiyo, Waziri Mwigulu alisema wakati waneenda kwenye msiba wa wana CCM waliouawa huku Tunduma, baada ya mazishi yeye na Mwenyekiti wa CHADEMA, Bw. Freeman Mbowe pamoja na wanasiasa wengine walikaa na kula nyama za kuchoma hadi saa usiku.
 
“Nini kinachowafanya muwe maadui wa siasa kiasi hicho?” alihoji na kuongeza:

 “Mnasababisha watoto wasio na hatia tena wasiojua siasa wawe yatima. Duniani siasa hazina tofauti kama zilivyo mechi za mpira. Leo unavaa jezi hii na kesho jezi ile. Acheni kufanya uadui katika siasa”, alionya.
 
Wakati huohuo,  Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema atamtuma Waziri wa Nishati na Madini, Prof.  Sospeter Muhongo aende Geita keshokutwa (Jumamosi, Machi 19, 2016) ili akasikilize malalamiko ya wananchi hao juu ya suala la magwangala.
 
Magwangala ni mchanga uliochimbwa mgodini na kuchujwa na sasa unatakiwa kuchujwa tena ili utolewe mabaki ya madini na wachimbajiwadogo wadogo.

“Nimemuita Profesa Muhongo aje na timiu yake ya wakurugenzi pamoja na wataalamu wa STAMICO ili waje wakamilishe suala hili. Najua lilikwishaanza kughughulikiwa tangu Makamu wa rais alipopita hapa mwezi uliopita na sasa nimeambiwa kuwa limefikia asilimia 75 ya utekelezaji,” alisema.

Waziri Mkuu amemaliza ziara ya mkoa huo na alirejea jijini  Dar es salaam jana jioni

Kiwanda Cha Rhino Cement Cha Tanga Chafungiwa Kwa Uharibifu Wa Mazingira

$
0
0

Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Raisi Muungano na Mazingira Mh. Luhaga Mpina (MB) amekifungia kiwanda cha kuzalisha cement na chokaa kilichopo jijini Tanga cha Rhino Cement, jana jioni kutokana na kile kinachodaiwa kuwa ni uharibifu na uchafuzi wa mazingira na kuvunja sheria ya usimamizi wa mazingira ya mwaka 2004 na kanuni zake.
 
Mh. Mpina amechukua uamuzi huo, baada ya kupokea malalamiko kutoka kwa wananchi wa kata ya maweni kupitia diwani wa kata hiyo Bw. Joseph Colvas na kujionea mwenyewe namna ambavyo kiwanda hicho kinavyo achilia moshi mzito kwenda angani, pamoja na vumbi lisilovumilika kusambaa katika maeneo ya makazi ya wanachi wa kata hiyo ikiwa ni pamoja na kusambaa katika maeneo ya shule ya sekondari ya Don Bosco ambapo, Mh. Mpina ameelezwa kuwa athari zitokanazo na uachiachi wa hewa hiyo chafu angani si tu kwa watoto wa shule zinazozunguka kata hiyo bali pia ni kwa viumbe hai na mazingira.

Kwa upande wake Afisa Afya wa jiji la tanga aliyejulikana kwa jina moja la bwana Kizito alimuelezea Naibu Waziri Mpina kuwa ni kweli kiwanda hicho kimekuwa kikifanya uchafuzi huo wa mazingira, na Afisa uendeshaji kutoka Baraza la Taifa na HIfadhi ya Mazingira NEMC Bw. Novatus Mushi ameeleza kuwa kiwanda hicho kimeshawahi kutozwa faini ya shilingi milioni kumi na saba (17) kwa kosa la kuchelewa kulipa ada ya mwaka ya mazingira pamoja na uharibifu wa mazingira uliokuwa ukifanywa na kiwanda hicho kwa upande wa kuzalisha chokaa.
 
Mh. Mpina ameelekeza Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira ( NEMC) kukifunga kiwanda hicho kisiendelee na uzalishaji kwa muda usiopungua miezi mitatu, na kulitaka baraza hilo lijiridhishe na kufuatilia namna kiwanda hicho kinavyotakiwa kutekeleza sheria ya mazingira kwa kujenga mfumo wa kisasa wa kutoa taka zitokanazo na uzalishaji kiwandani hapo pamoja, na kupima vumbi na moshi utokao kiwandani hapo kama hautakuwa na madhara na athari kwa mazingira na viumbe hai. Kinyume na hapo kiwanda hicho kitafungiwa moja kwa moja.
 
Aidha, akitolea mfano wa kiwanda cha bonite bottles cha mjini moshi kwa kuwa kinara katika upandaji miti na utunzaji wa mazingira, mh Mpina alivitaka viwanda vingine viige mfano wa kiwanda hicho cha coke cola.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Ijumaa ya March 18

Afungwa Kifungo cha Maisha Jela Kwa Kusafirisha Kilo 21 za Mirungi

$
0
0

Mahakama Kuu Kanda ya Moshi, imemfunga jela maisha mfanyabiashara, Silay Maulid Jumanne (35) baada ya kupatikana na hatia ya kusafirisha kilo 21 za majani ya mirungi.

Hukumu hiyo iliyotolewa jana na Jaji Mfawidhi wa mahakama hiyo, Aishiel Sumari, ni ya kihistoria katika vita dhidi ya dawa za kulevya nchini kwani haijawahi kutolewa tangu Tanzania ipate Uhuru.

Wengi wa wanaokamatwa na mirungi, hushtakiwa kwa kupatikana na mirungi, shtaka ambalo husikilizwa na mahakama za chini tofauti na kusafirisha ambalo husikilizwa na Mahakama Kuu.

Kutokana na mazoea hayo, washtakiwa wengi wanaopatikana na hatia kwa kosa la kupatikana na mirungi, huishia kupigwa faini hatua inayoelezwa kuchangia kushamiri kwa matumizi ya mirungi.

Hata hivyo, mshtakiwa huyo jana hakuamini masikio yake pale Jaji Sumari alipomweleza kuwa adhabu ya kusafirisha mirungi kama ilivyo dawa nyingine za kulevya ni kifungo cha maisha jela.

Akitoa adhabu hiyo, Jaji Sumari alisema upande wa mashtaka ukiongozwa na Wakili Mwandamizi wa Serikali, Tamari Mndeme umejenga kesi hiyo na kuishawishi Mahakama pasi na kuacha shaka.

Upande wa mashtaka ukiongozwa na Wakili Mndeme akisaidiwa na mwenzake Kassim Nassir, ulidai kuwa Septemba 7, 2013, mshtakiwa alikamatwa na vifurushi 21 vya Mirungi.

Kwa mujibu wa mashtaka hayo, mshtakiwa alikamatwa kituo kikuu cha mabasi mjini Moshi, akiwa kwenye harakati za kusafirisha mirungi hiyo kwenda kuiuza jijini Arusha.

Jaji Sumari alisema ushahidi wa mashahidi watano wa upande wa mashitaka, umethibitisha kuwa mshtakiwa alikamatwa na begi la rangi ya kijani likiwa na mirungi hiyo.

Alisema licha ya mshtakiwa aliyekuwa akitetewa na Wakili Martin Kilasara, kujitetea kuwa hakukamatwa stendi kuu bali eneo la Majengo mjini Moshi, ushahidi umethibitisha alikamatwa stendi kuu.

“Baada ya kusikiliza ushahidi, mashahidi wamethibitisha ulikamatwa Stendi Kuu Moshi, ushahidi huo uliungwa mkono na kondakta wa basi na dereva teksi aliyekuchukua,” alisema.

Jaji Sumari alisema polisi hawakuwa na sababu yoyote ya msingi ya kumbambikia shtaka mshtakiwa huyo, kama alivyojaribu kujitetea na kusisitiza kuwa ushahidi ulikuwa madhubuti dhidi yake.

“Kulikuwa na tofauti ndogondogo kama begi lilibebwa na nani kutoka stendi, au kutoka kwenye basi kwenda kwenye teksi lakini zilikuwa ni tofauti ndogo hazikuharibu mizizi mikuu ya ushahidi,” alisema.

Kwa mujibu wa Jaji Sumari, ukiacha ushahidi huo, ungamo la mshtakiwa linaongeza nguvu na kushabihiana na ushahidi uliotolewa na mashahidi.

Jaji Sumari alisema mirungi ni dawa za kulevya zenye madhara, ushahidi wa Mkemia Mkuu wa Serikali, ulibainisha matumizi yake humfanya mtumiaji kuwa mtegemezi wa dawa hizo.

“Matumizi ya dawa za kulevya yanaathiri jamii ulim wengu mzima hasa vijana, hivyo sheria hii ilitungwa ikizingatia uhai wa binadamu ndiyo maana imeweka adhabu kali,” alisema.

Jaji Sumari alimweleza mshtakiwa huyo ambaye muda wote alikuwa akijifuta jasho na kunywa maji, kuwa mtu yeyote anayepatikana akisafirisha mirungi na dawa nyingine ni kufungwa jela maisha.

Hukumu hiyo ilionekana kuwa gumzo katika viunga vya mahakama hiyo jana, huku wanasheria wakisema inapeleka ujumbe kwa jamii kutodharau kosa linalohusiana na mirungi.

Mwenyekiti wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) Tawi la Moshi, David Shilatu alisema hukumu hiyo ni ya kwanza kutolewa na ya aina yake Tanzania.

“Kwa sheria zetu hizi na marekebisho yake, mirungi nayo inaangukia daraja la dawa za kulevya, kwa hiyo upande wa mashtaka ukithibitisha ulikuwa unasafirisha adhabu ni kubwa,” alisema Wakili Shilatu.

Shilatu alisema ingawa mshtakiwa anayo haki ya kukata rufaa, lakini hukumu hiyo itoshe kupeleka ujumbe kwa jamii kwamba matumizi ya mirungi na usafirishaji wake ni kosa la jinai nchini.

Umoja wa Rufaa za Wananchi Tanzania Wawaomba Wazanzibar Wajitokeze Kwa Wingi Kupiga Kura Tarehe 20

$
0
0
Viongozi wa muungano wa vyama vya siasa uitwao Umoja wa Rufaa za Wananchi Tanzania wamewaomba Wazanzibari kukamilisha haki yao ya kupiga kura katika uchaguzi wa marudio ili wapate viongozi wa kuwaletea maendeleo

Ujumbe wa watu saba wa umoja huo ukiongozwa na John Shibuda wa Ada Tadea, ulitoa kauli hiyo jana ulipokutana kwa mazungumzo na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Ali Iddi ofisini kwake Vuga Mjini Zanzibar.

Taarifa iliyotolewa na Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais, ilisema ujumbe huo ni kutoka vyama visivyokuwa na wabunge ambavyo ni UPDP, Sau, UDP na Ada-Tadea.

Msimamo wa vyama hivyo unakinzana na ule wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) uliotoa tamko la kususia uchaguzi huo wa marudio.

Kwa upande wake John Cheyo alisema upigaji kura ndiyo njia pekee itakayotoa mwanga kwa wananchi wa Zanzibar kuamua wapi wanataka kuelekea katika mustakabali wa maisha yao ya baadaye.

Wakati huohuo, vyama 12 visivyo na uwakilishi bungeni vimetoa tamko la kushiriki uchaguzi huo vikisema hoja za kugomea uchaguzi huo hazina mashiko.

 Vyama vilivyotoa tamko hilo ni CCK, Sau, Ada-Tadea, TLP, AFP, UPDP, Demokrasia Makini, NRA, UMD, Chausta, DP na ADC ambacho mgombea urais Zanzibar ni Hamad Rashid aliyejiengua CUF miaka miwili iliyopita. 

Mansoor Yussuf Himid Ambaye ni Mshauri wa Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF) Akamatwa Na Jeshi La Polisi

$
0
0

Jeshi la Polisi linamshikilia mwanasiasa Mansoor Yussuf Himid kwa mahojiano kuhusiana na kulipuliwa kwa maskani ya CCM, Kisonge Michenzani mjini Unguja.

Mansoor, ambaye ni mshauri wa Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Maalim Seif Sharif Hamad alipigiwa simu jana jioni na polisi kwa ajili ya mahojiano katika kituo cha Madema.

Kukamatwa kwa Mansoor kumekuja siku chache baada ya Jeshi hilo kuwakamata wafuasi wengine 42 akiwamo Kaimu Mkurugenzi wa Habari, Uenezi na Mawasiliano ya Umma, Hamad Masoud akituhumiwa kutoa taarifa kwamba kuna watu wamekimbilia porini na wengine wamekwenda Mombasa.

Wafuasi hao 42 ambao bado wanashikiliwa ni kutokana na kuhusishwa na tukio la kulipuliwa nyumba ya Kamishina wa Polisi, Hamdan Omar Makame.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mjini Magharibi, Mkadam Khamis Mkadam jana alithibitisha kukamatwa kwa Mansoor na kwamba ni kutokana na hali ya matukio ya milipuko na mambo mengine, hivyo wanahitaji kupata maelezo ya kina kabla ya kumwachia.

Alisema lengo la kumshikilia Mansoor si kumkomoa bali ni kupata ufafanuzi na maelezo kwani hivi sasa kutokana na hali na matamshi ambayo huwa yanatolewa katika mitandao ya kijamii, Jeshi la Polisi linayafuatilia kwa kina kuyachunguza.

“Kwa hivyo tunataka maelezo na tukishapata maelezo yake tutaamua kama ni kumwachia au la, lakini kwa sasa tunamhitaji kwa kuisaidia polisi kwenye upelelezi,” alisema Mkadam.

Tukio hilo limekuja saa chache baada ya Naibu Katibu Mkuu wa CUF Bara, Magdalena Sakaya kulalamikia dalili za wazi za uvunjifu wa haki za binadamu Zanzibar zinazofanywa na vyombo vya dola dhidi ya wafuasi wao kwa kivuli cha utunzaji wa amani.

Akizungumza jana jijini Dar es Salaam, Sakaya aliisihi Serikali ya Rais John Magufuli kuingilia kati kwani wananchi wanaweza kuchoshwa na vitendo hivyo na kuleta uvunjifu zaidi wa amani. 

Sakaya alisema kuwa wanaamini mambo yote hayo yanatokea kutokana na msimamo wao wa kutokubali kushiriki uchaguzi wa marudio unaofanyika Jumapili hii.

Uchaguzi huo wa marudio unafanyika baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 25 mwaka jana kufutwa na Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC), Jecha Salim Jecha kutokana na kile alichodai kukithiri kwa ukiukwaji wa taratibu na sheria za uchaguzi.

Sakaya alisema kuwa kuna vitendo vingi wanafanyiwa wafuasi wa CUF visiwani humo vikiwamo vya kupigwa na vikundi vya uhalifu vinavyoitwa ‘mazombi’, kuchomewa nyumba na kutiwa ndani kwa viongozi wa chama hicho kwa visingizio vya kushiriki uhalifu.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images