Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

TAKUKURU na POLISI Nusura Watwangane Makonde wakati Wakimgombea Shahidi.

0
0

Maafisa wa Takukuru na askari wa Jeshi la Polisi waliokuwa wakilinda eneo la Mahakama ya Wilaya ya Bukombe mkoani Geita, juzi nusura watwangane makonde wakati wakimgombea shahidi.

Tukio hilo lilianza kama masihara baada ya shahidi huyo kufika mahakamani akiongozana na maofisa wa Takukuru na ghafla mmoja wa polisi aliyemtambua, alimuweka chini ya ulinzi na kumfunga pingu.

Kamanda wa Takukuru wa wilaya hiyo, Chuzela Shija alilazimika kuingilia kati na kuwaomba polisi kumuachia mtu huyo, Paulo Sitephano ili atoe kwanza ushahidi ndipo hatua nyingine zifuate, ombi lililokubaliwa na polisi kwa kumfungua pingu huku wakimlinda asitoroke.

Sokomoko lilianza mara tu shahidi huyo alipomaliza kutoa ushahidi dhidi ya Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi ya Umoja anayetuhumiwa kuomba na kupokea rushwa ya Sh100, 000.

Polisi hao walimuwahi na kumfunga tena ili wampeleke kituoni. Kitendo hicho kiliwakera maofisa wa Takukuru ambao walitaka kuondoka na mashahidi wao wote watano walioenda nao mahakamani hapo kwa kutumia gari lao.

Maofisa hao wa Takukuru waliwasihi polisi kumuacha shahidi huyo na kuwataka wamkamate baada ya kukamilisha taratibu zao za kiofisi, ombi hilo lilikataliwa na askari hao.

“Hatuwezi kumuachia mtuhumiwa kwa sababu anatafutwa muda mrefu kwa tuhuma zilizofikishwa polisi,” alijibu mmoja wa polisi aliyekuwa na cheo cha sajenti ambaye alikataa kutaja jina lake.

Kitendo hicho kiliwakera maofisa wa Takukuru na kuamua kutumia nguvu kuwazuia polisi kuondoka na shahidi wao, hali iliyozua mtafaruku baina yao na kufikia hatua ya kukunjana mashati kabla ya kuamuliwa kuacha vitendo hivyo.

Baada ya vuta nikuvute na kurushiana maneno makali na vitisho, polisi walioongeza nguvu kwa kuita gari la doria, walifanikiwa kumchukua shahidi huyo na kumpandisha kwenye gari kabla ya kuondoka naye, huku maofisa wa Takukuru wakibaki kulalamikia ubabe wa askari hao.

Katika tukio hilo lililovuta watu wengi, baadhi ya maofisa wa Takukuru walionekana wana nguo zilizochanika, hali iliyosababishwa na mtafaruku huo.

Akizungumzia tukio hilo, mkuu wa waendesha mashtaka wa polisi mahakamani hapo, Elias Mgobela aliwatupia lawama maofisa wa Takukuru kwa kushindwa kuonyesha ushirikiano kwa askari hao wakati wa kumtia mbaroni mtuhumiwa.

“Kisheria, polisi wana haki ya kumkamata mtuhumiwa eneo lolote. Huyo shahidi wa Takukuru alikuwa akitafutwa kwa muda mrefu na polisi. Ilikuwa ni jukumu la maofisa wa Takukuru kushirikiana na polisi kufanikisha kumkamata badala ya kuzuia,” alisema.

Alisema kitendo hicho kilisababisha mmoja wa watuhumiwa aliyemtaja kwa jina moja la Lubango aliyekuwa chini ya ulinzi wa polisi kutoroka baada ya askari wengi kuelekeza nguvu kumgombea shahidi huyo.

Kwa upande wake, kamanda wa Takukuru wa wilaya, Chuzela Shija aliitupia lawama polisi akidai ilitumia ubabe, nguvu na dharau dhidi ya maofisa wake ambao hawakukataa shahidi wao kutiwa mbaroni, bali waliomba wapewe fursa ya kukamilisha taratibu za kiofisi kabla ya kumkabidhi mikononi mwao kwa tuhuma zinazomkabili.

“Isingewagharimu polisi kufuatana na maofisa wa Takukuru hadi ofisini, wakakamilisha taratibu za kiofisi na shahidi huyo, halafu wakamtia mbaroni. Ilihitajika busara ndogo sana kulimaliza suala hili, lakini bahati mbaya wenzetu walichagua kutumia ubabe na kutunishiana misuli,” alilalamika.

Katika kesi dhidi ya mwalimu huyo, Mkuu wa Wilaya ya Bukombe, Amani Mwenegoha aliieleza mahakama jinsi alivyoshiriki kuweka mtego wa kumnasa.

Mkuu huyo wa wilaya alidai kuwa aliandaa mtego huo na kufanikiwa kumtia mbaroni mtuhumiwa huyo, Daniel Nying’ati baada ya kupokea malalamiko kutoka kwa mmoja wa wananchi aliyedai kuombwa fedha ili mtoto wake apate nafasi ya kurudia darasa la saba shuleni hapo.

Akiongozwa na mwendesha mashtaka wa Takukuru, Kelvin Murusuri, shahidi huyo alidai kuwa alichukua jukumu hilo kutekeleza moja ya majukumu yake ya kupokea, kusikiliza na kutatua kero za wananchi.

Alidai Februari 8, alipokea simu kutoka kwa mwananchi aliyemtaja kwa jina la Marko Elias akimtaarifu kuombwa rushwa na mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Umoja alipoenda kuomba nafasi ya mtoto wake kurudia darasa la saba shuleni hapo.

 “Katika maelezo yake, mwananchi yule aliniambia aliombwa rushwa ya Sh150, 000, ndipo nilipomuambia aende Takukuru na kufanikisha mtuhumiwa kutiwa mbaroni,” alidai Mwenegoha.

Kwa upande wake, shahidi wa pili ambaye ni ofisa wa Takukuru, Redemta Miremi alidai Februari 8, alimpokea mwananchi aliyemtaja kwa jina la Marko Elias akidai kuelekezwa na mkuu wa wilaya kufika ofisi hizo kutoa taarifa ya kuombwa rushwa.


Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumatano ya March 16

Wanaharakati Wamjia Juu Rais Magufuli

0
0

Mtandao wa Wanawake wa Katiba na Uchaguzi, umemuomba Rais John Magufuli kusimamia kikamilifu utekelezwaji wa mikataba iliyosainiwa na Tanzania katika usawa wa kijinsia ili kupunguza pengo lililopo kuelekea usawa wa 50/50 katika nafasi za uongozi.

Maombi hayo yamekuja kufuatia uteuzi wa wakuu wa mikoa uliofanywa mwishoni mwa wiki iliyopita na wanawake waliopenya kuwa ni watano kati ya wateule 26, ikiwa ni sawa na asilimia 20.

Taarifa hiyo iliyosainiwa na Kaimu Mkurugenzi wa Mtandao wa Jinsia (TGNP), Gloria Shechambo ilielezea kuwapo kwa dalili za kuwakandamiza wanawake kutokana na idadi ndogo ya wanaoteuliwa kushika uongozi katika ngazi za uamuzi.

Mkurugenzi wa TGNP, Lilian Liundi aliwahi kusema kuna makatibu wakuu wa wizara mbalimbali na manaibu wao 50, huku wanaume wakiwa 40 sawa na asilimia 80.

Waziri Jaffo: Halmashauri ya Wilaya ya Mbarali Inanuka Ufisadi

0
0

Naibu Waziri wa Tamisemi, Utumishi na Utawala Bora, Selemani Jafo amesema Halmashauri ya Wilaya ya Mbarali mkoani Mbeya inanuka ufisadi unaofanywa na baadhi ya wakuu wa idara.

Kauli hiyo ya waziri inatokana na tuhuma za upotevu wa zaidi ya Sh800 milioni mwaka 2010/2011 zilizolenga kuboresha elimu ya sekondari wilayani Mbarali.

Fedha hizo ambazo zinaweza kutengeneza madawati 1,600 yanayotosheleza mahitaji ya wanafunzi 4,800, ikiwa dawati moja kwa bei ya soko kwa sasa ni Sh50,000 zilifujwa na watumishi ambao miongoni mwao bado wapo.

Jafo alitoa kauli hiyo juzi alipozungumza na wakuu wa idara, watumishi na madiwani wa halmashauri hiyo kwenye ziara yake iliyolenga kutoa maelekezo ya kiutendaji.

Mkurugenzi wa halmashauri hiyo, Yeremiah Mahinya alimhakikishia Jaffo kwamba watatekeleza maagizo waliyopewa kwa ufanisi na kwa muda, ikiwamo kuondokana na matumizi mabaya ya fedha za umma.

Mkuu wa wilaya hiyo, Gullamhusein Kiffu alisema mtumishi atakayeshindwa kutimiza majukumu vizuri atamchukulia hatua.

Serikali Ya Tanzania Yalilia Meno ya Tembo Yaliyochomwa Moto nchini Malawi

0
0

Serikali imeanza mazungumzo na Ubalozi wa Malawi nchini baada ya nchi hiyo kuteketeza tani 2.6 za meno ya tembo yaliyotoka Tanzania. 
 
Serikali inafanya mazungumzo hayo ili kuzuia kuchomwa kwa meno mengine yaliyopo nchini humo kwa kuwa ni kielelezo kinachohitajika mahakamani.

Mkurugenzi wa Wanyamapori wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Herman Keraryo alisema mwanasheria wa wizara alifanya mawasiliano na Mwanasheria Mkuu wa Serikali na ubalozi huo ili kuwasiliana na Mwanasheria Mkuu wa Malawi. 

Idadi ya vipande vya meno ya tembo vilivyokamatwa nchini  Malawi ni 781 na thamani yake inakisiwa kuwa  bilioni 3. 

Katika hatua nyingine; Serikali ya Kenya inatarajia kuteketeza tani 120 za meno ya tembo mwishoni mwa mwezi huu baada ya kuyakamata nchini humo. 

Mtoto wa Siku 5 Aibiwa Hospitalini Usiku Wakati Mama Yake Akiwa Amelala

0
0

Hali ya sintofahamu imeibuka katika Hospitali ya Mkoa wa Arusha ya Mount Meru baada ya mtoto mchanga wa siku tano kuibiwa wodini katika mazingira ya kutatanisha.

 Tukio hilo limezusha hofu kwa baadhi ya wazazi waliojifungua katika wodi ya wazazi hospitalini hapo wakihofia usalama wa watoto wao na kuomba Serikali kuingilia kati.

 Akisimulia tukio hilo, mama mzazi wa mtoto huyo, Sinyari Lucas ambaye ni mkazi wa Simanjiro mkoani Manyara, alisema lilitokea usiku wa kuamkia jana.

Akizungumza huku akiwa ameghubikwa na huzuni, Lucas alisema wakati akiwa kitandani muda wote kabla ya kulala alikuwa na mtoto wake.

Mumewe, Lucas Ngaraa alionyesha kushangazwa na tukio hilo kwa sababu hospitali hiyo ina ulinzi wa kutosha.

Baadhi ya wazazi waliokuwapo kwenye wodi hiyo, walisema muda wote mzazi huyo alikuwa amelala kitandani na mtoto wake, lakini usiku walishangaa kumsikia anapiga kelele.

 Mganga Mkuu Mfawidhi wa Hospitali hiyo, Dk Jackline Urio alikiri kuwapo kwa tukio hilo na kwamba, uongozi umelipokea kwa mshtuko mkubwa na unalifanyia kazi.

 Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Liberatus Sabas alisema wamepokea taarifa hizo na tayari ameagiza maofisa kwenda kufuatilia tukio hilo kwa kina.

Meya wa Jiji la Dar es Salaam Kupatikana March 22

0
0

Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam imetangaza Machi 22 kuwa ndiyo kitafanyika kikao cha Baraza la Madiwani wa Dar es Salaam kujadili ajenda moja ya uchaguzi wa meya.

Uchaguzi huo umeahirishwa mara tatu kwa sababu mbalimbali, ikiwamo zuio batili la mahakama lililowekwa na makada wa CCM, katika Mahakama Hakimu Mkazi wa Kisutu.

 Hata hivyo, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Tamisemi), George Simbachawene hivi karibuni, alisema zuio hilo ni batili na kuagiza Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kufanya uchaguzi huo kabla ya Machi 25.

Kaimu Mkurugenzi wa jiji hilo, Sarah Yohana alisema jana  kuwa uchaguzi huo utafanyika Machi 22 kuanzia saa 4.00 asubuhi ukumbi wa Karimjee.

Alisema maandalizi ya uchaguzi huo yamekamilika, ikiwamo kusambaza barua kwa viongozi wa vyama husika na wajumbe watakaoshiriki kikao hicho

Billioni 12 Zakusanywa Kutoka Kwa Wakwepa Kodi

0
0
Na Raymond Mushumbusi- MAELEZO
Serikali kupitia Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imekusanya takribani Sh. billioni 12 kutoka kwa wafanyabiashara ambao walikwepa kodi na kupewa muda wa siku 14 na Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli kulipa kodi hizo kwenye mamlaka hiyo.

Akitoa takwimu hizo jana mara baada ya kuapishwa kuwa Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Alphayo Kidata alisema, kila Mtanzania ana jukumu la kulipa kodi kwa mujibu wa sheria na sio kukwepa na amehaidi kulisimamia vizuri suala la ukusanyaji wa mapato katika sehemu mbalimbali ili kuongeza mapato ambayo yatasaidia kufanikisha maendeleo katika sekta mbalimbali.

“Tutajitahidi kwa kila namna kuwaelimisha wananchi wetu ili wafahamu wajibu wao na umuhimu katika kulipa kodi na sio kukwepa kulipa kodi na tunawaomba wananchi kila waendapo kupata huduma yoyote ile iwe katika sekta binafsi au Serikalini basi anatakiwa aombe stakabadhi za manunuzi au huduma ili tuweze kudhibiti upotevu wa kodi” alisema Kidata.

Kamishna Kidata aliongeza kwamba   mamlaka hiyo ipo kwa ajili ya kuwahudumia wananchi na kama kuna suala lolote au tatizo kuhusu kodi kuna ofisi katika mikoa yote ikiwa ni hatua ya kutatua shida zao na kama kuna mtumishi yoyote wa mamlaka hiyo atashindwa kumuhudumia mwanachi inavyotakiwa basi taarifa zitolewa mara moja kupitia namba zao zilizoko kwenye tovuti ya mamlaka hiyo, ambayo ni www.tra.go.tz ili kuimarisha huduma zetu kwa wateja.

Aidha Kamishna Mkuu huyo alisema kuwa watawachukulia hatua wale wote ambao hawatalipa au hawajalipa kodi zao kwa kuwapeleka mahakamani kwa kukaidi kulipa kodi halali kwa mujibu wa Sheria.

Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imeanzishwa kwa mujibu wa Sheria na ina mamlaka ya usimamizi wa makusanyo ya Mapato Tanzania na kwa kipindi cha hivi karibuni kumekuwa na ukwepaji wa kodi uliotokana na sakata la upotevu wa makontena katika Bandari ya Dar es Salaam hivyo kuikosesha mapato Serikali lakini jitihada thabiti zimefanywa na mamlaka hiyo kukusanya madeni kutoka kwa wakwepa kodi na kuwafikisha mahakamani ambao wamekaidi kulipa.

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL), David Mattaka Ashitakiwa Tena Kwa Uhujumu Uchumi

0
0

Mkurugenzi Mtendaji wa zamani wa Shirika la Ndege Tanzania (ATCL), David Mattaka na wenzake wawili wamepandishwa kizimbani wakikabiliwa na mashtaka sita yakiwamo ya matumizi mabaya ya madaraka, kughushi na kuisababishia hasara Serikali kupitia ukodishaji wa ndege.

Wakili Mkuu wa Serikali, Timon Vitalis akishirikiana na mawakili wa Takukuru, Joseph Kiula na Stanley Luoga waliwataja washtakiwa wengine wanaokabiliwa na kesi hiyo mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Respicius Mwijage kuwa ni Ofisa Mtendaji Mkuu Mstaafu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Manunuzi ya Umma (PPRA), Ramadhan Mlinga na Mwanasheria wa mamlaka hiyo, Bertha Soka.

Wakili Vitalis alidai kuwa Oktoba 9, 2007 katika ofisi za ATCL zilizopo wilayani Ilala, Mattaka alitumia vibaya madaraka kwa kutia saini mkataba wa ukodishaji wa ndege A320-214 iliyotengenezwa kwa namba 630 baina ya Wallis Trading Inc na ATCL.

Alidai alifanya hivyo bila ya kuzingatia Sheria ya Manunuzi ya Umma na taratibu za zabuni kwenye mchakato huo.

Pia, alidai Oktoba 27, 2007 alitumia vibaya madaraka yake kwa kutia saini cheti cha kuruhusu mchakato wa ukodishaji wa ndege hiyo bila ya kufuata ushauri wa kiufundi aliopewa na kuisababishia Serikali hasara ya dola 772,402.08 za Marekani zilizolipwa kwa kampuni ya Aeromantenimiento,S. A kama gharama za huduma ya matengenezo.

Kuhusu Mattaka, wakili huyo alidai Mahakama ya Kisutu haina mamlaka ya kumpa dhamana na kwamba, anaweza kuomba kudhaminiwa kupitia Mahakama Kuu.

Washtakiwa Mlinga na Bertha wanadaiwa kuwa Machi 19, 2008 katika ofisi za PPRA walighushi muhtasari wa kikao cha siku ukionyesha mamlaka hiyo ilijadili maombi ya ATCL juu ya kuidhinishwa kwa mkataba huo.

Washtakiwa hao walikubaliwa dhamana kwa kuwa shtaka linalowakabili linadhaminika.  Kesi hiyo iliahirishwa hadi Machi 29.

Lowassa Afunguka Mazito Kuhusu Wanachama Wanaofukuzwa CCM Wakituhumiwa Kukisaliti Chama Kwa Kumuunga Mkono Yeye

0
0

Aliyekuwa mgombea urais kwa tiketi ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Edward Lowassa amewapa neno wanachama wa CCM wanaotaka kufukuzwa ndani ya chama hicho wakituhumiwa kumuunga mkono.

Akiongea hivi karibuni katika kikao cha Baraza Kuu la chama hicho kilichofanyika jijini Mwanza, Lowassa aliwasihi watu hao kujiondoa CCM na kujiunga na Chadema kwani kuna maisha mazuri zaidi ndani ya chama hicho kikuu cha upinzania.

“Lakini hivi karibuni kuna utaratibu wa kuwafukuza kwenye chama watu ambao waliniunga mkono. Wanafukuzwa wanaambiwa ‘ondokeni mfuateni Lowassa’.

"Nasikia kuna mipango mikubwa zaidi baada ya mwezi wa sita atakapokabidhiwa Rais Magufuli… kuna mipango mikubwa zaidi ya kuwaondoa kwenye chama,” alisema Lowassa.

“Sasa mimi nawaambia kwa niaba yetu. There is life outside CCM, nawaambia tena kwa ajili yenu, waje Chadema kuna maisha mazuri tu hapa. Wasibaki huko wananyanyaswa, wanabezwa wanafanya nini… waje tushirikiane tufanye kazi,” aliongeza.

Lowassa ambaye ni Waziri Mkuu Mstaafu alieleza kuwa CCM hivi sasa wanaumia kwa sababu kuondoka kwake na kujiunga na Chadema kuliiongezea nguvu kambi hiyo ya upinzani na kupunguza ruzuku kwa kiasi kikubwa kwa chama hicho tawala.

==> Msikilize Lowassa hapo chini akiongea

Uchomaji Kituo cha Polisi Bunju A....Watuhumiwa 17 Waachiwa huru

0
0

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu imewaachia huru washtakiwa 17 kati ya 35 wanaokabiliwa na kesi ya kuchoma moto Kituo cha Polisi Bunju ‘A’ baada ya Upande wa Jamhuri kushindwa kuthibitisha mashtaka

Hukumu hiyo imetolewa mahakamani hapo na Thomas Simba, Hakimu Mkazi huku upande wa mashtaka ukiwakilishwa na Hellen Moshi, Wakili wa Serikali.

Katika kesi hiyo, Hakimu Simba amesema hatua hiyo inatokana na upande wa mashtaka kufunga ushahidi wao wakiwa na mashahidi 17 pamoja na vielelezo 19.

Amesema, kutokana na kushindwa kuthibitisha mashtaka kwa washtakiwa 17 mahakama imeamua kuwaachia huru kwa kuwa hawana hatia, huku washtakiwa waliobaki 18 wakipatikana na kesi ya kujibu.

Washtakiwa walioachiwa ni Halifan Mshengeli, Patrick Elias, Jacob Kasambo, Amos Machaka, Hamis Mohamed, Elia Nalomba, Juma Kapanga,

Wengine ni Josephine Machimo, Shadya Ismail, Aisha Husseion, Jenerose Urio, Suzan Shaulin, Mariam Mwinyi, Madgalena Nashokigwa, Mariam Rashid, Pili Ally na Said Mwindi.

Washtakiwa ambao wamepatikana na hatia baada ya kutolewa kwa ushahidi ni Yusuph Sungu, Juma Koza, Rashid Liwima, Mrisho Majaliwa, Hamis Ndege, Seleman Gwae, Baraka Nkoko, Mang’ enya Mang’enya.

Wengine ni Abuu Issa, Ramadhan Said, Rajab Ally, Ally Athuman, Abraham Nunge, Amina Matipwili, Mariam Hoza, Rehema Juma, Gudila Temba,  Veronica Ephraem (Mama Wambura).

Hakimu Simba amesema, washtakiwa hao wamepatikana na kesi ya kujibu katika mashtaka sita yanayowakabili, hivyo kutokana na wingi wa wananchi kesi hiyo itasikilizwa siku mbili mfululizo kuanzi Machi 29 hadi 30, mwaka huu kwa ajili ya kujitetea.

Baada ya kusema, hayo kuliibuka hoja za kisheria kati ya Wakili Moshi na wakili wa utetezi Felix Nkongwa kuhusu kupata dhamana kwa washitkiwa waliobaki.

Kutokana na mvutano wa hoja, Hakimu Simba amesema uamuzi wa kupata ama kutopata dhamana kwa washitakiwa hao utatolewa Machi 22, mwaka huu.

Waziri Mkuu Aagiza Kufutwa Umiliki Wa Mashamba Makubwa 11 Wilayani Ngara

0
0

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameagiza kufutwa mara moja umiliki wa mashamba makubwa 11 yenye ukubwa wa ekari 7,700  kwenye  vijiji vya Kasharazi na Rwakalemera wilayani Ngara Kagera, ambayo hayana hati na yametelekezwa.

Ametoa agizo hilo leo asubuhi  (Jumatano, Machi 16, 2016) wakati akizungumza na wakazi wa vijiji vya Kasulo na Rwakalemera katika kata ya Kasulo wilayani Ngara akiwa njiani kuelekea mkoa wa Geita.

Waziri Mkuu alilazimika kufanya mkutano huo mapema asubuhi baada ya kuamua kuitisha uongozi wa wilaya ya Ngara ufike kwenye mkutano huo ili kujibu kero za wananchi waliosimamisha msafara wake jana wakati akielekea Ngara mjini.

Uamuzi huo unafuatia hatua ya Waziri Mkuu kumwita kwenye mkutano huo Afisa Ardhi na Maliasili wa Wilaya, Bi. Betty Munuo ili aeleze chanzo cha mgogoro wa ardhi katika vijiji hivyo.

Bi. Munuo ambaye amehamishiwa wilaya hiyo Agosti, mwaka jana,  alisema aliyakuta malalamiko hayo na amefanya uchambuzi wa majina ya wamiliki wote wa mashamba na walikuwa wanapanga kuwapatia notisi ili wajieleze.

Katika orodha yake, Bi. Munuo alitaja wamiliki 18 wa mashamba makubwa lakini kati yao ni wamiliki saba tu ambao mashamba yao yana hati lakini matatu ndiyo yameendelezwa na manne hayajaendelezwa.

Mashamba yaliyoendelezwa yanatumika kwa kilimo,  ufugaji na shule. Nayo yanamilikiwa na Dayosisi ya Rulenge (shamba na. 606 lenye ekari 161 liko Mbuba); Dario Zakaria (shamba na. 639 lenye ekari 282 liko Nyakariba) na Masista wa Mt. Fransisco (shamba na. 234 lenye ekari 759 liko Kasulo).

Mashamba manne yenye hati lakini yametelekezwa ambayo yote yako kijiji cha Rwakalemera ni ya Abdallah Sadala na. 235 lenye ekari 521; Mahsen Saidi shamba na. 333 lenye ekari 458; Mshengezi Nyambele shamba na. 746 lenye ekari 388 na  Mushengezi Nyambele shamba na. 745 lenye ekari 497.

Akitangaza uamuzi wake, Waziri Mkuu aliwataja wamiliki wa mashamba yasiyo na hati kuwa ni Bw. Joseph Rugumyamheto mwenye shamba na. 527 (ekari 505 liko Rwakalemera); Bw. Nicolaus Kidenke shamba halina namba na ukubwa wake haujulikani; Bw. Gwasa Angas Sababili shamba na. 714 (ekari 236 liko Kasharazi);  na Bw. Makumi Adili Rufyega (ekari 500 liko Rwakalemera).

Wamiliki wengine ambao mashamba yao yapo kijiji cha Rwakalemera ni Paulo Shikiri ekari 250; Frank Mukama Derila ekari 750; Godfrey Kitanga ekari 800; Philemon Mpanju ekari 200; Issa Sama ekari 500; Hekizayo Mtalitinya ekari 225 na Joel Nkinga ekari 1,250.

Waziri Mkuu aliagiza ifanyike sensa ili kubaini kama wamiliki wa mashamba hayo yote ni Watanzania au la. "Haya yenye hati nataka yafanyike mapitio ya hati zao na kubainisha ni namna gani walipatiwa hati hizo. Nataka taarifa inifikie ofisini kwangu Dar es Salaam ifikapo tarehe 20 Machi, 2016," alisema.

Ili kukamilisha kazi hiyo, Waziri Mkuu ameagiza kurejeshwa mara moja kwa aliyekuwa Afisa Ardhi wa Wilaya hiyo, Bw. Enock Mponzi ambaye amehamishiwa Halmashauri ya Wilaya ya Rorya ili aje asaidie uchunguzi wa ugawaji wa maeneo hayo.

Alimtaka Mwenyekiti wa kijiji cha Rwakalemera, Bw. Brighton Kemikimba aitishe mkutano wa kijiji kabla ya tarehe 31 Machi 2016 na abainishe mashamba yote makubwa ambayo yanazidi ekari 50. Pia afuatilie kama yana kibali cha Baraza la Madiwani.

Wakati huohuo, Waziri Mkuu ameagiza kusimamishwa kazi kwa aliyekuwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ngara, Bw. Colnel Ngudungi na kutaka arejeshwe wilayani humo kujibu tuhuma za kuhusika na upotevu wa fedha za mauzo ya mbao kutoka kwenye msitu wa Rumasi, wilayani humo.

Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Kagera,  Bw. Adam Swai ameagizwa kumwandikia  barua Katibu Tawala wa Mkoa wa Shinyanga ili atekeleze maagizo hayo na Bw. Ngudungi arejeshwe Ngara kujibu tuhuma hizo. Bw. Ngudungi alihamishwa  kwenda Sekretarieti ya Mkoa wa Shinyanga,  Agosti 2015.

Akiwa njiani kuelekea Ngara jana mchana (Machi 15, 2016), waziri Mkuu alisimamishwa katika kijiji cha Rwakalemera na wananchi wenye mabango wakiomba kurejeshewa ardhi ya kijiji huku baadhi yao wakidai wanatishiwa na bunduki pindi wakisogelea mashamba hayo makubwa.

Pia walidai kuuzwa kwa msitu wa Rumasi na mapato kutojulikana yalipokwenda huku wakidai kuwa kijiji chao hakipati mapato yoyote kutokana na minada ya ng’ombe inayofayika kijijini hapo wakati sharia inataka asilimia 20 ya mapato ibakizwe kijijini.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU
JUMATANO, MACHI 16, 2016.

Mkuu Mpya Wa Mkoa wa Kagera Meja Jenerali mstaafu Salum Mustafa Kijuu Atoa Onyo Kali Kwa Majambazi na Wahalifu.

0
0

Mkuu wa Mkoa wa Kagera Meja Jenerali mstaafu Salum Mustafa Kijuu amewataka watu wote wanaopindisha sheria, majambazi na wahalifu wote kutafuta kazi nyingine halali za kufanya.

Meja Kijuu aliyasema hayo baada ya kula kiapo cha utiifu na uadilifu kuwatumikia wananchi wa mkoa wa Kagera mkoa ambao upo pembezoni mwa nchi unaokabiliwa na matukio ya mara kwa mara ya uhalifu.

''Namshukuru Mheshimiwa Rais kwa imani kubwa aliyonayo kwangu na nitafanya kazi kwa kuzingatia yale ambayo ameyasema na kuhakikisha maendeleo yanapatikana''-Amesema Meja Kijuu

''Sitakubali watu wazurure hovyo na kuacha kufanya kazi za uzalishaji na nitahakikisha napambana na wahalifu wote kwa uwezo wote nilionao"-Amesisitiza Meja Kijuu.

Aidha Rais Magufuli aliwaapisha wanajeshi wastaafu Meja Jenerali Mstaafu, Ezekiel Elias Kyunga, aliyekuwa Chuo cha Kamanda na Unadhimu (JWTZ) ambaye sasa ni Mkuu wa Mkoa wa Geita, Jenerali Mstaafu Salum Mustafa Kijuu, aliyekuwa Mkuu wa Kamandi ya Nchi Kavu ni Mkuu wa Mkoa wa Kagera.

Wengine ni Meja Jenerali Mstaafu Raphael Muhuga, aliyekuwa Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa(JKT) sasa ni Mkuu wa Mkoa wa Katavi na Brigedia Jenerali Mstaafu Emmanuel Maganga, aliyekuwa Makao Makuu ya Jeshi sasa ni Mkuu wa Mkoa wa Kigoma 

Lengo la Rais kuweka wanajeshi katika mikoa ya pembezoni ni kuleta usalama na kuimarisha amani katika mikoa hiyo.

RC Makonda Atema Cheche.......Atoa Masaa 24 Kwa Wakuu wa Idara Kumpa Ripoti ya Matatizo ya Wananchi

0
0

MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda amewagiza wakuu wa idara wa Halmashauri za jiji la Dar es Salaam kutoa ripoti za matatizo ya wananchi na jinsi walivyojipanga ndani ya masaa 24.

Makonda ameyasema hayo wakati akizungumza na watendaji wa halmashauri hizo ikiwa ni siku ya kwanza kuingia katika ofisi ya Mkuu wa Mkoa baada ya kuapishwa jana.

Makonda amesema wananchi wa Dar es Salaam wanakabiliwa na changamoto za ulinzi,maji,biashara pamoja na elimu  hivyo lazima matatizo hayo yapate ufumbuzi katika kusaidia wananchi kuondokana na changamoto hizo.

Makonda amesema kuwa kwa muda alioutoa wa masaa 24 ni mkubwa hivyo lazima wafanye kazi hiyo jinsi walivyojipanga katika kutatua changamoto hizo.

Amesema wakati umefika katika kuwatumikia wananchi kuwaondolea  kero zao ambazo zinafanya kuwa na malalamiko yasioisha.

Makonda amesema amekutana na Kamanda wa Polis wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamishina wa Jeshi la Polisi, Simon Sirro kuzungumzanaye juu ya suala la ulinzi na usalama  kwa wananchi.

Aidha amesema kuwa kukutana huko sio mara ya kwanza ataendelea ikiwa ni lengo la kuwatumikia wananchi pamoja na kutatua kero zao.

Rais Magufuli Akagua Na Kuweka Jiwe La Msingi Katika Ujenzi Wa Kituo Cha Kufua Umeme wa Megawat 240 Cha Kinyerezi II Jijini Dar Es Salaam Marchi 16,2016

0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Balozi wa Japan nchini Masaharu Yoshida, Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo, Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Dar es Salaam CCM, Ramadhan Madabida, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini Dkt. Juliana Palangyo wakikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa Ujenzi wa Kituo cha Kufua umeme cha Kinyerezi II nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Balozi wa Japan nchini Masaharu Yoshida , Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo, Mkurugenzi mkuu wa Tanesco Felchesmi Mramba wakivuta utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa Ujenzi wa Kituo cha Kufua umeme cha Kinyerezi II nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisikiliza maelezo kutoka Meneja wa Kituo cha kufua umeme cha Kinyerezi I Mhandisi John Mageni kuhusu utendaji kazi wa kituo hicho.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akitoa maelekezo kwa Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo kuhusu ujenzi wa Kituo cha Kufua umeme cha Kinyerezi I nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam.
 Meneja wa Kituo cha kufua umeme cha Kinyerezi I Mhandisi John Mageni akitoa maelekezo kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli kuhusu mitambo ya kufua umeme kwa kinyerezi I nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na wananchi wa kinyerezi hawapo pichani kabla ya kuzindua rasmi Ujenzi wa Kituo cha Kufua umeme cha Kinyerezi II nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam.
Mkurugenzi mkuu wa Tanesco Felchesmi Mramba akifafanua jinsi ujenzi wa Kituo cha kufua umeme cha Kinyerezi II kitakavyokuwa mara baada ya kukamilika mbele ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akifurahia jambo na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Dar es Salaam CCM Ramadhani Madabida kabla ya uzinduzi wa uzinduzi rasmi wa Ujenzi wa Kituo cha Kufua umeme cha Kinyerezi II nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo, Balozi wa Japan Nchini Masaharu Yoshida, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda ,Mama Janeth Magufuli wakiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa TANESCO mara baada ya kuzindua rasmi ujenzi wa Kituo cha Kufua umeme cha Kinyerezi II nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimsikiliza kwa makini mama mmoja alijitokeza kumpongeza kutokana na utendaji kazi mzuri wa Serikali yake ya awamu ya tano mara baada ya uzinduzi rasmi ujenzi wa wa Kituo cha Kufua umeme cha Kinyerezi II nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam.
Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo akimkaribisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli wakati alipowasili kwenye ofisi za kituo cha kuzalisha umeme cha Kinyerezi I nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam.
Wananchi wakishangilia wakati Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli alipokuwa akiwahutubia huko Kinyerezi nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam


Jeshi La Ulinzi La Wananchi Wa Tanzania Lakanusha Kupeleka Wanajeshi Visiwani Zanzibar.

0
0

Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) linapenda kutoa taarifa kwa Umma juu ya uvumi ulioenea katika mitandao ya kijamii kuwa, limepeleka Wanajeshi wengi visiwani Zanzibar kwa ajili ya kudhibiti Usalama wakati wa kipindi hiki cha uchaguzi marudio unaotarajia kufanyika tarehe 20 Machi, 2016

Habari hizo siyo za kweli na zina lengo la kupotosha Umma. Kimsingi JWTZ linao Wanajeshi visiwani Zanzibar wakati wote kwa majukumu yake ya msingi ya Ulinzi wa nchi yetu. 

Hivyo hakuna Mwanajeshi yeyote aliyeongezwa zaidi ya wale waliopo visiwani humo tangu awali. Taarifa hizo zipuuzwe,zisipewe nafasi yoyote ya kujenga hofu kwa Wananchi.

JWTZ linapenda kwa mara nyingine tena kuwahakikishia Wananchi kuwa wasiwe na wasiwasi wowote kuhusu ulinzi na usalama wa nchi yetu, kwani wakati wote Jeshi lao lipo imara kuwalinda.

Imetolewa  na  Kurugenzi  ya  Habari  na  Mahusiano
Makao Makuu ya Jeshi, Upanga
S.L.P  9203,   Dar es Salaam,  Tanzania.
Kwa Mawasiliano zaidi: 0784-477638.

Waziri Mwakyembe Akutana na Jaji Joseph Warioba Ili Kupata Maoni yake kuhusu Mahakama ya Mafisadi Nchini

0
0
Jaji Mstaafu Joseph Warioba amesema uamuzi wa serikali ya awamu ya tano wa kuanzisha mahakama itakayoshughulikia ufisadi, rushwa na uhujumu uchumi umekuja wakati muafaka lakini amependekeza kuwa mahakama pekee haiwezi kushughulikia suala hilo bila kushirikiana na Jeshi la Polisi na Takukuru.
 
Jaji Warioba amesema hayo leo wakati alipoalikwa Wizara ya Katiba na Sheria kwa ajili ya kutoa maoni na mapendekezo yake kuhusiana na serikali kuanzisha mahakama itakayoshughulikia Rushwa na wahujumu  uchumi.
 
“Mahakama pekee haiwezi kushughulikia ufisadi na uhujumu uchumi bila kushirikisha vyombo vingine ambavyo ni Jeshi la Polisi na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa katika kuimarisha mahakama hiyo ambayo inatarajia kuanzishwa hivi karibuni” amesema Jaji Warioba.
 
Wizara ya Katiba na Sheria imeanzisha  utaratibu wa kukutana na viongozi wa zamani ambao walishawahi kuongoza wizara hiyo kwa lengo la kupata mapendekezo, maoni na uzoefu juu ya kuanzishwa kwa mahakama. 

“Leo nimekaribishwa wizara ya Katiba na Sheria kwa lengo la kubadilishana mawazo kuhusiana na uanzishwaji wa mahakama itakayoshughulikia ufisadi, rushwa na wale wanao hujumu uchumi, huu ni uamuzi mzuri na hizi ni jitihada za wazi za serikali katika kupambana na rushwa”amesema Jaji Warioba.
 
Amesema lengo la serikali la kuanzisha kwa mahakama hiyo ni kupambana na ufisadi na tayari serikali ya awamu ya tano imeonyesha dhamira ya dhati ya kuzuia mianya ya rushwa katika ukusanyaji wa mapato.
 
Kwa upande wake, Waziri wa Sheria na Katiba , Dk Harrison Mwakyembe amesema katika kipindi kifupi cha uongozi wa rais Magufuli masuala yote ya msingi aliyoyasema wakati wa kampeni ya uchaguzi mkuu uliofanyika mwaka jana ameshaanza kuyatekeleza.
 
“Uanzishwaji wa mahakama itakayoshughulikia ufisadi na uhujumu uchumi ni miongoni mwa vipaumbele alivyovitoa rais Magufuli wakati wa kampeni hivyo kwa kiasi kikubwa yale yote ambayo aliahidi kipindi cha uchaguzi ameanza kuyatekeleza”amesema Dk Mwakyembe.
 
Amesema mbali na uanzishwaji wa mahakama hiyo, pia suala la katiba mpya litashughulikiwa lakini kwa kuanza rais Magufuli ameanza na kuwawajibisha wale wote ambao wamekiuka maadili ya kazi zao pamoja na kuanzisha mahakama itakayoshughulikia ufisadi na uhujumu uchumi.

Breaking News: Balozi Juma Mwapachu Leo Atangaza kurudi CCM...Asema Alifanya kosa Kubwa Kuhamia UKAWA

0
0
HOTUBA YA BALOZI JUMA MWAPACHU KUTANGAZA KUREJEA CCM-MIKOCHENI 16/03/2016

Ndugu zangu,
Mtakumbuka kwamba mnamo tarehe 13 Oktoba 2015, nilitangaza kuihama CCM na kurejesha kadi yangu ya uanachama kwenye ofisi ya CCM Kata ya Mikocheni. Nilitoa maelezo kwanini niliamua kujiondoa CCM (maelezo hayo pia niliyabandika katika ukurasa wangu wa facebook). 

Nilieleza kwamba CCM imepoteza mwelekeo kwa kuamua kuminyima haki ya kugombea mcha mungu Edwad Lowasa. 

Nikasema Edwad Lowasa ndiye chaguo la wana-CCM na ndiye chaguo la Watanzania. 

Nikasema nitakuwa mnafiki nikiendelea kubaki CCM huku naamini Edwad Lowasa anafaa kuwa Rais kuliko John Pombe Magufuli.

Baada ya miezi miwili ya uongozi wa Magufuli nataka niseme nilikosea sana. Nililewa mahaba ya Lowasa, nililewa ahadi ya Lowasa kunipa uwaziri wa mambo ya Nje.

Niliamini mafuriko ya Lowasa ambayo yakanifanya niamini kabisa anachukua nchi. Tulikubaliana na wenzangu kwamba wiki mbili za mwisho tuihame CCM kwa wimbi kubwa ili kuitikisa na kuitoa madarakani. Lakini baadhi wakaogopa na hadi sasa wengine wamebaki CCM na wana vyeo.

Leo natangaza kurudi CCM kwasababu nimeona kazi nzuri ya Magufuli. Nimefanya kosa kubwa katika siasa ambalo nawasihi vijana kwenye siasa wasifanye. 

Nilihama kwa kwasababu ya mtu (Lowassa). Nimerudi kwasababu ya mtu (Magufuli). Nataka niwaahidi kwamba CCM ikiweka mtu hovyo baada ya Magufuli, sitahama.

Usemi wa CCM kwamba Chama Kwanza, Mtu Baadaye sasa ndio nauona maana yake. Niliwalaumu CCM kwa kumuacha Lowassa lakini sikujua kwamba CCM ina uwezo wa miujiza wa kuibua jembe bora linaloitwa Magufuli.

Naomba mnisamehe kwa kulifanya jambo langu la kujitoa CCM na kurudi CCM kuwa jambo la kitaifa ukizingatia kwamba sikuwa na nafasi yoyote ya uongozi wa CCM wakati nahama na pia sijawahi kuwa hata Mjumbe wa NEC ya CCM na nilikuwa nje ya ulingo wa siasa za CCM kwa miaka 20. 

Niliamua kulifanya jambo kubwa ili kumsaidia Lowassa. Na sasa nimeamua kulifanya jambo kubwa ili Magufuli ajue sasa niko naye kwasababu sitaki shughuli zangu na za washirika wangu zikwamishwe na Serikali kwasababu tu huko nyuma niliamua kumsaidia swahiba wangu.

Naomba radhi kwa familia ya baba wa taifa mwalim Nyerere kwa kuitumia kisiasa siku aliyokufa (tar 14 Octoba) na kutumia msiba wake kutoa kauli za kisiasa zidi ya chama chake alichokiunda na ambacho hadi anakufa alikuwa mwanachama.

Wananchi wote tumuombee Magufuli na tumsaidie kwani tumepata nyerere mpya.

Rais Magufuli Apiga MARUFUKU Kukodi Mitambo ya Kuzalisha Umeme

0
0

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli jana tarehe 16 Machi, 2016 ameweka jiwe la msingi la ujenzi wa mradi wa kuzalisha umeme wa Kinyerezi namba mbili, uliopo katika wilaya ya Ilala Mkoani Dar es salaam, ambao utakapokamilika utakuwa na uwezo wa kuzalisha megawatts 240 za umeme.
 
Mradi huo ambao utazalisha umeme kwa kutumia gesi asilia inayosafirishwa kwa bomba kutoka Mtwara, unatarajiwa kuanza kuzalisha umeme katika kipindi cha kuanzia miezi 21 hadi 28 utakapokamilika kabisa.
 
Kuanza kwa ujenzi wa mitambo ya kuzalisha umeme huo, kunafuatia juhudi zilizofanywa na serikali ya awamu ya tano ya kufanikisha upatikanaji wa shilingi bilioni 120, ikiwa ni asilimia 15 ya fedha zilizopaswa kutolewa na Tanzania na fedha nyingine shilingi Bilioni 292 zimetolewa na Japan.
 
Mradi huu umetanguliwa na mradi wa Kinyerezi namba moja ambao una uwezo wa kuzalisha megawatts 150 za umeme, na mitambo yake tayari imeanza uzalishaji wa megawatts 105 zilizoingizwa katika gridi ya Taifa.
 
Pamoja na kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa mradi wa Kinyerezi namba mbili, Rais Magufuli amekagua mitambo ya kuzalisha umeme ya mradi wa Kinyerezi namba moja, ambapo Mkuu wa Kituo cha Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) cha Kinyerezi Mhandisi John Mageni, ametoa maelezo kuwa shirika hilo lina mpango wa kupanua uzalishaji wa umeme katika mradi huo kutoka megawatts 150 hadi kufikia megawatta 335, kwa kuongeza mitambo ya kufua umeme kwa teknolojia inayojumuisha matumizi ya gesi asilia na mvuke uzalishwao na mitambo hiyo.
 
Baadaya ya kupokea maelezo hayo, Rais Magufuli ameridhia kuwa serikali yake itatoa Dola za kimarekani milioni 20, kwa ajili ya kufanikisha upanuzi wa mradi huo na ameagiza kuwa wataalamu wa TANESCO washirikiane na Mkandalasi kuhakikisha upanuzi huo unafanyika haraka iwezekanavyo, badala ya muda wa miezi 12 uliopangwa.
 
Akizungumza na wananchi waliojitokeza katika sherehe za uzinduzi wa mradi huo, Rais Dkt. John Pombe Magufuli ameiagiza Wizara ya Nishati na Madini na TANESCO, kuanza kuachana na mitambo ya kukodi kwa ajili ya kuzalisha umeme, na badala yake nchi ijenge mitambo yake yenyewe ili kuondokana na gharama kubwa za nishati hiyo muhimu.
 
“Waziri, ukiona mtaalamu anakuletea mapendekezo ya kutaka kukodi mitambo ya kuzalisha umeme, badala ya kuleta mapendekezo ya kununua mitambo yetu wenyewe ujue mtaalamu huyo hafai, mtoe” Amesisitiza Rais Magufuli
 
Ameongeza kuwa tafiti zimethibitisha kuwa hadi sasa Tanzania ina zaidi ya futi za ujazo Trilioni 57 za gesi asilia, ambayo itazalisha umeme wa kutosheleza mahitaji ya ndani, na umeme mwingine kuuzwa nje ya nchi ikiwemo Kenya ambayo tayari imeomba kuuziwa umeme kutoka Tanzania.
 
Aidha, Rais Magufuli ametoa onyo kwa TANESCO kuwa hatarajii kusikia bwawa la maji la Mtera limeishiwa maji, kwa kuwa katika msimu huu wa mvua maeneo ya Iringa yalikuwa na mvua nyingi ambazo zimesababisha hadi mafuriko mafurukio.
 
Kwa upande wake, Waziri wa Nishati na Madini Prof. Sospeter Muhongo amesema tangu serikali ya awamu ya tano iingie madarakani, juhudi zilizofanyika zimefanikisha kuongeza uzalishaji wa umeme kutoka megawatts 800 hadi kufikia megawatts 1,000 kiasi ambacho ni pungufu kwa megawatts 20 tu, ikilinganishwa na mahitaji ya megawatts 1020 za sasa.
 
Ameongeza kuwa pamoja na kuweka jiwe la msingi la mradi wa Kinyerezi namba mbili, hivi karibuni serikali inatarajia kujenga miradi mingine ya kuzalisha umeme kwa kutumia gesi asilia, ikiwemo Kinyerezi namba tatu utakaozalisha megawatts 600, Kinyerezi namba nne utakaozalisha megawatts 300, na mingine itakayojengwa Lindi na Mtwara.
 
Prof. Muhongo amebainisha kuwa mpaka sasa gesi asilia inazalisha kati ya asilimia 50 na 60 ya umeme wote hapa nchini, Maji yanazalisha asilimia 30 hadi 40, na umeme unaozalishwa kwa mafuta hauvuki asilimia 10.
 
Sherehe hizo zimehudhuriwa na viongozi mbalimbali wakiwemo Balozi wa Japani hapa nchini Mheshimiwa Masaharu Yoshida, Wabunge wa kamati ya Nishati na Madini, wafadhili wakiwemo Benki ya Dunia, Benki ya Afrika na Shirika misaada la Japan (JICA.

Gerson Msigwa
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
Dar es salaam
16 Machi, 2016

Taarifa ya Wizara kuhusu filamu iliyompatia tuzo Elizabeth Michael "Lulu"

0
0
 TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Kumekuwa na minongono mingi kutoka kwa baadhi ya wananchi kuhusu Filamu ya Mapenzi ya Mungu ya msanii Elizabeth Michael (Lulu) iliyoshinda tuzo ya Filamu bora Afrika Mashariki mapema mwezi huu huko Lagos Nchini Nigeria katika tuzo za African Magic Views Choice Award (AMVCA).

Ili filamu ikamilike inahusisha watu mbalimbali wanaoshirikishwa kukamilisha filamu kuanzia mtoa wazo ambaye wazo hilo huwekwa katika mswada na mtaalamu jambo ambalo haliondoshi umiliki wa filamu.

Tunapenda kuufahamisha umma kuwa mmiliki halali wa Filamu ya Mapenzi ya Mungu ni Msanii Elizabeth Michael (Lulu) na ndiye aliyepata tuzo kwani ana haki zote za kupata tuzo hiyo kama mmiliki halali wa filamu hiyo.

Filamu ya Mapenzi ya Mungu imetengenezwa chini ya kampuni ya Proin Promotion na imesajiliwa kwa namba ya usajili CO831190.

IMETOLEWA NA
WIZARA YA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images