Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Vigogo Watatu Wa Mradi wa Mabasi Yaendayo Haraka (DART) Wafikishwa Mahakamani

$
0
0

Vigogo watatu wa Mradi wa Mabasi Yaendayo Haraka (DART), akiwemo Mtendaji Mkuu wa mradi huo, Asteria Mlambo, wamepandishwa kizimbani, kwa tuhuma za kuisababishia serikali hasara ya Sh milioni 83.5.

Mbali na Asteria, washitakiwa wengine wanaokabiliwa na mashitaka hayo ya uhujumu uchumi ni Mkurugenzi wa Fedha na Utawala, Evodius Katale, Mwanasheria Mkuu wa mradi huo, Francis Kugesha na Mkurugenzi wa kampuni ya Yukan, Yuda Mwakatobe.

Walifikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam jana na kusomewa mashitaka matatu mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Respicius Mwijage.

Walisomewa mashitaka na wakili kutoka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Jackline Nyantori akisaidiwa na Estazia Wilson na Stellah Mafuru.

Nyantori alidai kati ya Septemba Mosi na Oktoba Mosi 2013, Kinondoni Dar es Salaam, Asteria, Katale na Kugesha wakiwa wafanyakazi wa mradi huo, walishindwa kutekeleza majukumu yao vizuri na kuisababishia serikali hasara ya Sh milioni 83.5.

Katika mashitaka yanayomkabili Mwakatobe, inadaiwa Juni 29, 2005 katika ofisi za kodi Ilala, Dar es Salaam, alitoa taarifa za uongo kwa maofisa wa Mamlaka ya Mapato (TRA), wakati akiwasilisha taarifa ya fedha ya mwaka 2004 na ya 2005 ya kampuni yake ya Yukan Business, jambo lililosababisha alipe kodi ndogo.

Awali, Wakili Nyantole alidai kuwa Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP) amewasilisha hati ya kuruhusu mahakama hiyo, kusikiliza kesi hiyo ya uhujumu uchumi hivyo washitakiwa wataruhusiwa kujibu mashitaka yao.

Washitakiwa walikana mashitaka na upande wa Takukuru ulidai kuwa upelelezi wa kesi hiyo haujakamilika, pia hawana pingamizi ya dhamana kwa washitakiwa.

Hakimu Mwijage alisema Asteria, Katale na Kugesha watapata dhamana endapo kila mmoja atakuwa na mdhamini mmoja anayefanyakazi serikalini au kwenye taasisi inayofahamika, atakayesaini hati ya Sh milioni 15. Pia kila mshitakiwa awasilishe Sh milioni 15 au hati isiyohamishika yenye thamani ya Sh milioni 15.

Kwa upande wa Mwakatobe, dhamana yake ipo wazi endapo atapata mdhamini mmoja mwenye barua kutoka taasisi inayofahamika, asaini hati ya Sh milioni tano.

Wote waliachiwa kwa dhamana baada ya kutimiza masharti. Asteria na Katale wametakiwa kuwasilisha hati hizo Machi 3 mwaka huu. Kesi itatajwa tena Machi 9 mwaka huu.

Vigogo Watatu Wanusuru Nyumba ya Dk. Slaa Iliyokuwa Imeuzwa Kwa Mnada Baada ya Kushindwa Kurudisha Mkopo

$
0
0

Vigogo watatu nchini wamejitosa kunusuru nyumba ya ya aliyekuwa Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasi na Maendeleo (Chadema), Dk. Willbrod Slaa kwa kumchangia Sh milioni 300.

Hatua hiyo inaelezwa inatokana na maombi ya mmoja wa watu wa karibu wa Dk. Slaa, kuwaomba vigogo hao kunusuru nyumba hiyo iliyopo Mtaa wa Mtipwa, Mbweni jijini Dar es Salaam, ambayo iliuzwa kwa mnada.

Nyumba hiyo ilinunuliwa kwa mnada mwishoni mwa mwaka jana na mfanyabiashara Hussein Ndama, ambaye aliinunua kwa Sh milioni 110.

Baada ya kuuzwa kwa nyumba hiyo zilianza juhudi kutoka kwa watu waliokuwa karibu na Dk. Slaa kwa kutaka kuikomboa, huku mfanyabiashara huyo akigoma kuiuza kwa bei aliyonunulia na kutaka kuiuza kwa Sh milioni 500.

Taarifa hizo zinaeleza kuwa, wakati vigogo hao wakijitosa, mawakili wa mke wa Dk. Slaa pia walifanya kazi kubwa, ili kurejesha nyumba hiyo mikononi mwa familia ya Dk. Slaa.

Chanzo cha kuaminika kimesema  kuwa, baadhi ya vigogo hao kutoka Chama Cha Mapinduzi (CCM), waliamua kuingilia kati na kulazimika kuchanga fedha za kukomboa nyumba hiyo.

“Baada ya taarifa za nyumba kutoka kwa watu wa karibu na Dk. Slaa, viongozi watatu waliingilia kati na kuanza kutoa michango yao ambapo zilipatikana Sh milioni 300.

“Vigogo hawa watatu, wawili ni viongozi wa juu wa chama tawala na mmoja ni kiongozi wa ngazi za juu katika shirika la umma (jina linahifadhiwa), na kila mmoja alitoa shilingi milioni 100.

“… tena hilo halikufanyika hivi hivi ila nguvu kubwa ilitumika kuhakikisha hao viongozi wanawasiliana na Ndama (Hussein), ili kumwomba alegeze msimamo wake kuhusu bei ya nyumba aliyonunua. 

“Baada ya majadiliano marefu, Ndama alikubali ingawa kwa masharti zaidi.

"Wakati hilo likifanyika pia mawakili wa mke wa Dk. Slaa walifanya kazi kubwa ili kuweza kurejesha nyumba hiyo katika mikono ya familia ya Dk. Slaa,” kilisema chanzo .

Chanzo hicho kilisema jitihada za vigogo hao zilimfanya Ndama maarufu kwa jina la ‘Ndama mutoto ya ng’ombe’ alegeze masharti ya kiwango cha fedha alichohitaji na hivyo kukubali dau la Sh milioni 300.

Nyumba ilipotoka
Katibu Mkuu huyo wa zamani wa Chadema, Dk. Slaa na mkewe Josephine Mushumbusi walinunua nyumba hiyo namba 74694, iliyopo katika kiwanja namba 117, kitalu ‘1’ Mbweni JKT.

Nyumba hiyo ilinunuliwa na wawili hao Mei 8, mwaka 2012 kutoka Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), kwa gharama ya Sh milioni 117.859.

Dk. Slaa aliwahi kukaririwa na vyombo vya habari Septemba 4, mwaka jana alipokuwa akitangaza kujitoa Chadema, akimshukuru Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe kwa kumsaidia sehemu ya fedha za kununulia nyumba hiyo.

Licha ya sintofahamu hiyo, Dk. Slaa alisema hana ugomvi na Mbowe ambaye pia ni Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni.

“Ninamuheshimu sana Mbowe, sina ugomvi naye maana hata nyumba ninayoishi amehusika kunichangia na hata kunisaidia mambo mengi,” alisema Dk. Slaa.

Jinsi Nyumba ilivyouzwa kwa mnada
Mfanyabishara huyo alinunua nyumba hiyo Desemba 27, mwaka jana kwa mnada uliosimamiwa na kuendeshwa na Dalali wa Mahakama, Bilo Star kwa ajili ya kufidia deni la mkopo wa Sh milioni 52.999 ambalo lilitakiwa kulipwa kufikia Novemba 26, mwaka jana katika Benki ya Equity ya jijini Dar es Salaam.

Inadaiwa kwamba mke wa Dk. Slaa, Josephine Mushumbusi, ndiye aliyetoa hati hiyo ya nyumba kama dhamana ya mkopo huo uliochukuliwa na mtu anatajwa kwa majina ya Salehe Swedi Nehale wa Kampuni ya ujenzi ya T/A Nehale Building Material Supplies.

Safari ya Nje
Septemba 8, mwaka jana Dk. Slaa, alisema anakwenda Marekani pamoja na familia yake kwa mapumziko.

Akiwa nchini humo kwa ajili ya mapumziko na kujiendeleza katika kozi fupi katika tasnia ya Sheria na Lugha, Dk Slaa alisema nyumba yake itakuwa chini ya ulinzi wa Jeshi la Polisi.

Akizungumza katika mahojiano yaliyorushwa kituo cha televisheni cha Azam, mwanasiasa huyo, alisema akiwa mapumzikoni Marekani, nyumba yake itakuwa inalindwa na Jeshi la Polisi kutokana na vitisho ambavyo amekumbana navyo tangu alipoamua kuachia ngazi Chadema.

“Ninatishiwa maisha, ni lazima nichukue hadhari….., ninatishiwa kupigwa mawe.Ni kweli ninalindwa na usalama,” alisema Dk. Slaa akiwa anahojiwa na mwanahabari nguli, Tido Mhando.

Credit: Mtanzania

Majina Ya Mawaziri MAJIPU Yakabidhiwa Kwa Waziri Mkuu......Ni Wale Waliogoma Kutangaza Mali Zao

$
0
0

Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma imemkabidhi Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa majina ya baadhi ya mawaziri na naibu mawaziri ambao hawajajaza fomu za mali wanazozimiliki kama sheria inavyowataka.
 
Akizungumza jana kwenye semina ya mawaziri na naibu mawaziri, Kamishina wa Sekretarieti hiyo, Jaji mstaafu Salome Kaganda alisema viongozi hao wanajua umuhimu wake lakini wanapuuza.

“Sheria hii ya Maadili ya Viongozi wa Umma inajulikana, lakini jambo la kushangaza wapo baadhi ya mawaziri na manaibu ambao hawajajaza, kwa ruhusa yako nitakukabidhi majina yao, sisi tunafanya kazi kwa mujibu wa sheria, hivyo anayekiuka anapaswa kuadhibiwa,” alisema Jaji Kaganda bila kutaja majina hayo.
 
Kifungu cha 9 cha sheria hiyo kinataka katika kipindi cha siku 30 baada ya kupewa wadhifa, kila mwisho wa mwaka na mwisho wa kutumikia wadhifa wake kiongozi husika anatakiwa kupeleka tamko la maandishi la mali zake.
 
Sheria hiyo inafafanua kuwa mali hizo ni pamoja na rasilimali zake au mume au watoto wenye umri usiozidi miaka 18 ambao hawajaoa au kuolewa.

Alisema fomu hizo lazima zijazwe na viongozi na wananchi wanaruhusiwa kwenda kuzihakiki wakitoa sababu za msingi, lakini sheria hiyo hairuhusu waende kutangaza na wakifanya hivyo hatua zinachukuliwa dhidi yao.
 
“Hapo ndipo wananchi wengi huwa hawatuelewi kwa kuwa wanapenda kujua mali ambazo viongozi wao wanamiliki,” alisema. 

Alisema Sekretarieti kwa kutambua umuhimu wa viongozi hao kuzingatia sheria na maadili, ndiyo sababu imeandaa semina hiyo baada ya kupata ufadhili kutoka Shirika la Misaada ya Maendeleo la Marekani (USAID), wakiamini kuwa yatasaidia kuwakumbusha.

Wadaiwa 16 Waliotorosha Makontena Bandarini Waanza Kufilisiwa ......Jana Zimekamatwa Kontena 9 za Mabati Ambazo Zitauzwa Kufidia Deni

$
0
0

MaliI zenye thamani ya Sh bilioni sita za baadhi ya wadaiwa 16, waliokwepa kulipa kodi ya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), baada ya kutorosha kontena za mizigo yao kwenye Bandari Kavu (ICD) ya Azam mwishoni mwa mwaka jana, zimekamatwa jana na zinafilisiwa.

Aidha, mali nyingine za thamani ya Sh bilioni 7.4 zimebainishwa na muda wowote kuanzia leo zitakamatwa ili kufilisiwa kwa lengo la kulipa kodi inayodaiwa na TRA.

Hayo yalibainishwa Dar es Salaam jana na Mwenyekiti wa Bodi ya Kampuni ya Udalali ya Yono, iliyopewa kazi ya kufuatilia wadaiwa hao, Yono Kevella alipokuwa akizungumzia kuanza kwa kazi ya kukamata mali za wadaiwa hao na kufilisiwa.

Kevela alisema baada ya kuisha muda wa siku 14, walioutoa kwa wadaiwa 24 kulipa madeni yao ya Sh bilioni 18.95, hadi juzi ni wadaiwa nane tu waliweza kulipa, hivyo hao 16 hawakulipa na mali zao ndio zimeanza kukamatwa na kufilisiwa.

Aliwataja wadaiwa ambao mali zao zimekamatwa na wamekubali wenyewe zifilisiwe kulipa deni hilo kuwa ni Tifo Global Trading Co Ltd wanaodaiwa Sh bilioni 1.57 na Lotai Steel Tanzania Ltd wanaodaiwa Sh bilioni 5.47.

Alisema wadaiwa hao ni wawekezaji kutoka China na wamekubali kwa hiari yao mali zao zifilisiwe kulipa deni wanalodaiwa. 

Mali zilizokamatwa na ziko tayari chini ya kampuni hiyo ya Yono ni kontena tisa za mabati, zenye thamani ya Sh bilioni sita.

"Nitumie fursa hii kuwaalika wananchi wote wanaohitaji mabati waje ofisi za kampuni yetu kununua mabati hayo, yako mengi ni kontena tisa, tunachofanya si kumuonea mtu, bali tunatekeleza wajibu wetu tuliopewa wa kuhakikisha kodi ya serikali inalipwa”, alisema Kevella.

Alisema kazi ya kukamata mali za wadaiwa wengine 14, zinaendelea na ndani ya wiki moja kazi hiyo itakuwa imekamilika na iwapo wahusika wote hawatapatikana, Kampuni ya SSB ambayo ndiyo mmiliki wa bandari kavu ya (Azam ICD) na kampuni ya wakala wa forodha ya Regional Cargo Services, watahusika kulipa deni linalobaki.

"Kwa wale tutakaoshindwa kuwapata au kukamata mali za kutosha kulipa deni wanalodaiwa, mmiliki wa bandari kavu ya Azam ICD, na kampuni ya wakala wa forodha ya Regional Cargo Services, watapaswa kulipa”, alisisitiza Kevella.

Kevella alisema jana jioni walitarajia kukamata mali nyingine za Sh bilioni 7.4 za mdaiwa Tuff Tyres General Co Ltd, ambaye amekimbilia kufungua ombi mahakamani lakini Mahakama haijatoa uamuzi.

Alisema wameshazibainisha mali za mdaiwa huyo, ikiwa ni pamoja na jengo la ghorofa, matairi na nyumba iliyopo Msasani, ambazo zote kwa pamoja zikifilisiwa zitalipa deni la Sh bilioni 7.4 anazodaiwa.

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa apokea mchango wa vifaa vya bilioni 10/= vya mahospitalini kutoka Azam, Coke na Pepsi

$
0
0

Umoja wa Wazalishaji Vinywaji laini umetoa msaada wa vifaatiba vyenye thamani ya Sh10 bilioni vilivyopokelewa na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa.

Vifaatiba vilivyopokelewa jana ni pamoja na mashine za aina mbalimbali kama utra sound, mashine za kustulia moyo, vitanda vya watoto njiti, vitanda vya kujifungulia, vitanda 80 vya kawaida na magodoro yake, ambavyo viliwekwa kwenye makontena 20.

“Haijapata kutokea msaada mkubwa kama huu,” alisema Majaliwa kwenye hafla hiyo iliyofanyika kwenye ghala la Bohari Kuu ya Dawa (MSD) iliyoko Mabibo, Ubungo jijini Dar es Salaam. 

 “Natoa wito kwa makampuni mengine binafsi kuunga mkono jitihada za Serikali.”

Msaada huo wa vifaa tiba unawalenga zaidi watoto na wajawazito, ikiwa ni jitihada za kuunga mkono juhudi za Rais John Magufuli katika kuboresha huduma za afya.

Msemaji wa umoja huo, Erastus Mtui kutoka Coca Cola Kwanza alisema msaada huo umelenga kusaidia watoto na wajawazito pamoja na wagonjwa wengine kama wa moyo.

“Tumelenga hasa vifaa vya watoto na wajawazito. Hii yote ni katika kuunga mkono jitihada za Rais Magufuli kwani anaboresha afya na kutokomeza rushwa, hii inayaokoa zaidi makampuni ya uzalishaji nchini,” alisema Mtui.

Akizungumza kwenye hafla hiyo, Majaliwa alizipongeza sekta binafsi kwa kushirikiana na Serikali kukabiliana na changamoto katika sekta ya afya.

Alisema vifaa hivyo vimekuja wakati mwafaka kwa kuwa vitawezesha vituo kutoa huduma bora za afya.

“Mtakumbuka kwamba hivi karibuni Rais Magufuli alihamasisha maboresho ya Hospitali ya Taifa ya Muhimbili na hasa wodi ya wazazi, hatua hii mliyoichukua ya kutoa msaada wa vifaa hivi ni sehemu ya kumuunga mkono,” alisema Waziri Mkuu.

Alisema Serikali kupitia MSD itahakikisha vifaa hivyo vinasam bazwa kwenye vituo husika kwa umakini mkubwa, hasa maeneo yenye mahitaji makubwa.

Alisema tayari kuna orodha ya awali katika mikoa ya Dodoma, Geita, Katavi, Lindi, Kilimanjaro, Mara, Mbeya, Shinyanga na Tanga.

Naye Mkurugenzi Mkuu wa MSD, Laurean Bwanakunu alisema bohari imedhamiria kusambaza dawa na vifaa tiba vya kutosha kwenye kanda nane za nchi, lakini changamoto kubwa ni jinsi ya kuzihifadhi.

“Ukubwa wa ghala hili la vifaa tiba ni mita za mraba 19,650 na hapa panatugharimu kiasi cha Sh2.5 bilioni. Na iwapo tutaendelea kuhifadhi hapa, itatulazimu kulipia Sh4 bilioni,” alisema Bwanakunu na kuongeza kuwa:

“Kwa hiyo changamoto ni kupata eneo la kujenga ghala. Wizara ya Ardhi ikitupatia eneo, tunategemea kuanza ujenzi mara moja.” 

Wafanyakazi PSI wasimamisha ziara
 Wafanyakazi wa kampuni ya PSI walisimamisha msafara wa Waziri Mkuu kwa kuziba barabara wakati akiondoka, wakitaka wamuambie kero wanazokumbana nazo kazini.

Wafanyakazi hao walitoa kero zao mbalimbali ikiwa ni pamoja na kulipwa malipo kiduchu kiasi cha Sh5,750 kwa siku, huku wakinyimwa kushiriki kuchangia mfuko wa hifadhi ya jamii wa PPF.

“Shida yetu kubwa ni mshahara. Tangu mwaka 2013 tunalipwa Sh5,750 mpaka leo na kwa miaka yote hiyo watu hawashiriki PPF,” alisema Amini Athuman ambaye ni mfanyakazi wa PSI.

“Wote ni vibarua, hakuna aliyeajiriwa hapa. Pia kinamama wajawazito hawalipwi chochote wakienda kujifungua, mtu anafukuzwa kazi bila kosa lolote bosi akiamua.”

Akijibu malalamiko hayo, Waziri Mkuu alisema ameyapokea na kwa kuwa Serikali ya Awamu ya Tano ilishajipa kazi ya kusikiliza kero za wananchi na wafanyakazi, lazima tatizo hilo litatuliwe.

“Nawasihi kesho (leo) mje kazini asubuhi saa 2:00 asubuhi na Waziri ya Kazi, Jenister Mhagama atakuwa hapa kwa kuwa mmelalamika kwamba hata makato ya PPF hayakatwi. Namsihi kiongozi ayaandike vizuri malalamiko ili akija asome kwa umakini na utatuzi utapatikana kesho hiyohiyo. Nawasihi msigome kufanya kazi,” alisema. 

Rais Magufuli aagiza mawaziri wasiolejesha hati za tamko la mali na ahadi ya uadilifu kufanya hivyo kabla ya saa 12 jioni leo - la sivyo Watafutwa Kazi

$
0
0

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. John Pombe Magufuli amesema mawaziri ambao hawajajaza Tamko la Rasilimali na Madeni wawe wamejaza fomu hizo na kuzirejesha katika Ofisi za Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Dar es Salaam ifikapo leo saa 12.00 jioni (Ijumaa, Februari 26, 2016).

Agizo hilo la Rais limetolewa leo na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa mbele ya waandishi wa habari katika mkutano uliofanyika ofisini kwake, Magogoni jijini Dar es Salaam.

“Mheshimiwa Rais ameelekeza mawaziri ambao hawajajaza tamko la rasilmali au hati ya ahadi ya uadilifu wafanye hivyo na kuzirejesha kabla saa 12 jioni na Waziri ambaye atashindwa kutekeleza agizo hili atakuwa amejiondoa mwenyewe kwenye nafasi yake,” amesisitiza Waziri Mkuu.

Waziri Mkuu amesema wakati akifungua mafunzo ya Mawaziri na Naibu Waziri kuhusu Mwongozo wa Maadili ya Viongozi wa Umma na Utekelezaji wa Ahadi ya Uadilifu yaliyofanyika Ikulu jana (Alhamisi, Februari 25, 2016) alikabidhiwa majina ya Mawaziri na Naibu Mawaziri ambao hawajawasilisha Tamko la Rasilimali na Madeni kwa Kamishna wa Maadili.

Amewataja mawaziri wanaotakiwa kurejesha fomu za tamko la rasilimali pamoja na hati ya ahadi ya uadilifu kuwa ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Bw. Charles Kitwanga na Waziri wa Nchi (OMR – Muungano na Mazingira), Bw. January Makamba.
 
 Wengine ni Waziri wa Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Ushirikiano wa Kikanda na Kimataifa, Dk. Augustine Mahiga ambaye anatakiwa kurejesha hati ya ahadi ya uadilifu kwa viongozi wa umma na Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi, Prof. Joyce Ndalichako ambaye anatakiwa kutoa tamko la rasilmali na madeni.

Kwa upande wake, Naibu Waziri wa  Nchi (OMR – Mazingira), Bw. Luhaga Mpina anatakiwa kurejesha fomu za tamko la rasilmali na madeni pamoja na hati ya ahadi ya uadilifu kwa viongozi wa umma

==> Tazama video hii kumsikiliza Waziri mkuu akuongea.

Agizo la Rais Magufuli Laanza kutekelezwa ......Waziri Mahiga arudisha Fomu , Kitwanga Ang'aka Jina Lake Kutajwa

$
0
0
Baada ya waziri mkuu kutaja majina ya mawaziri wanne na naibu waziri mmoja ambao hawajarudhisha fomu za Sekretariati ya maadili ya umma na kutakiwa wawe wamerejesha fomu hizo kabla ya  saa kumi na mbili jioni ijumaa ya leo mpaka sasa ni waziri mmoja aliyetii agizo hilo

Aliyerudisha fomu hizo ni Waziri wa Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Ushirikiano wa Kikanda na Kimataifa, Dk. Augustine Mahiga ambapo amekiri kuwa ni kweli alikuwa hajarudisha fomu hizo kutokana na majukumu ya kazi yaliyokuwa yamembana

Waziri wa mambo ya ndani Charles Kitwanga yeye  ameshangaa jina lake kutajwa wakati tayari ameshazirudisha fomu hizo. Amesema hivi sasa  ameelekea ofisi za Sektretariati ya maadili kuwasilisha malalamiko yake

Naibu Waziri wa  Nchi (OMR – Mazingira), Bw. Luhaga Mpina yeye amesema kuwa atawahisha kurudisha fomu hizo kabla ya saa kumi na mbili jioni.

Breaking News: TCU Yakifuta Chuo Kikuu cha St. Joseph Kampasi ya Arusha.......Wanafunzi Watahamishiwa Vyuo Vingine

$
0
0
1.Tunapenda kuuarifu umma kwamba, Chuo Kikuu cha Mt. Yosefu Tanzania (SJUIT) Kampasi ya Arusha ni mojawapo ya vyuo vikuu vilivyosajiliwa na Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU) ambacho kilianza kudahili wanafunzi kwa mara ya kwanza mwaka wa masomo 2013/2014.


2.Kwa mujibu wa kifungu cha 5(1) cha Sheria ya Vyuo Vikuu, Sura ya 346 ya Sheria za Tanzania, Tume ina mamlaka ya kusimamia na kudhibiti ubora na usimamizi wa uendeshaji wa Vyuo Vikuu hapa nchini.
 

3.Kwa muda mrefu na kwa wakati tofauti kumekuwapo na matukio ya migogoro baina ya uongozi wa Chuo Kikuu cha Mt. Yosefu Kampasi ya Arusha na wanafunzi. 

Kwa kipindi hiki chote Tume imekuwa ikifuatilia kwa karibu chimbuko la migogoro hiyo na kuchukua hatua stahiki ikiwa ni pamoja na kutoa maelekezo kwa uongozi wa chuo kurekebisha kasoro zinazosababisha migogoro chuoni hapo.

Kwa sehemu kubwa migogoro hiyo imekuwa ikitokana na matatizo ya ubora, uongozi, ukiukwaji wa sheria na taratibu za uendeshaji wa chuo kikuu kama zilivyobainishwa na Sheria ya Vyuo Vikuu. 

Hata hivyo jitihada za Tume ya Vyuo Vikuu kukitaka Chuo Kikuu cha Mt. Yosefu Tanzania (SJUIT) Kampasi ya Arusha kuhakikisha kuwa elimu inayotolewa katika Kampasi hii inakidhi viwango vya ubora vilivyowekwa na Tume hazikupewa uzito stahiki na uongozi wa chuo.
 

4.Hivi sasa Kampasi ya Arusha ina jumla ya wanafunzi 1557 wanaosoma programu za masomo ya ualimu wa sayansi zifuatazo:
5.Kutokana na yaliyobainishwa hapo awali, tunapenda kuuarifu umma kwamba, Tume imejiridhisha kuwa Kampasi ya Arusha ya Chuo Kikuu cha Mt. Yosefu Tanzania imepoteza sifa na vigezo vya kuendelea kutoa elimu ya chuo kikuu. 

Kwa kuzingatia ukweli kwamba wanafunzi ndio waathirika wakuu wa matatizo yaliyopo kwenye Kampasi hii, Tume imeamua kama ifuatavyo:
 

a)Imefuta kibali kilichoanzisha Kampasi ya Arusha ya Chuo Kikuu cha Mt. Yosefu Tanzania (SJUIT) na kuidhinisha uhamisho wa wanafunzi wote waliokuwa wanasoma katika Kampasi hiyo ya Arusha kwa gharama za Chuo Kikuu cha SJUIT. Orodha ya majina yao na vyuo watakavyopangiwa itatangazwa na kuwekwa katika tovuti ya Tume ya Vyuo Vikuu hivi punde.
 

b)Imefuta udahili wa wanafunzi wapya katika programu ya shahada ya miaka mitano ya ualimu wa sayansi. Na kwamba, wanafunzi wanaoendelea na masomo katika programu hii watahamishiwa katika Kampasi ya Luguruni, Dar es Salaam, na watalazimika kwanza kuhitimu katika ngazi ya Stashada (Diploma) kama ilivyokuwa imeidhinishwa na Tume hapo awali. Utaratibu wauhamisho wa wanafunzi wa programu hii utatangazwa hivi punde na kuwekwa katika tovuti ya Tume ya Vyuo Vikuu.
 

c) Imeidhinisha wanafunzi wa mwaka wa kwanza ambao hawakuweza kupata udahili katika vyuo vikuu vingine, kutoka katika kundi la wapatao 500 waliofukuzwa chuoni kutokana na migogoro iliyojitokeza katika Kampasi ya Arusha mwezi Juni, 2015 kuendelea na masomo katika vyuo watakavyopangiwa baada ya taratibu za uchambuzi wa taarifa zao kukamilika. Orodha ya majina yao na vyuo watakavyopangiwa itatangazwa na kuwekwa katika tovuti ya Tume ya Vyuo Vikuu hivi punde.
 

6.Kufuatia uamuzi huu, wanafunzi wote wanaosoma katika Chuo Kikuu cha Mt. Yosefu Kampasi ya Arusha wanaarifiwa kuwa watahamishiwa kwenye vyuo vikuu vingine vinavyofundisha programu za masomo zinazofanana na masomo wanayosoma hivi sasa chini ya utaratibu na masharti yafuatayo:
 

 i)Wanafunzi wote wanapaswa kuondoka chuoni mara moja baada ya kukamilisha taratibu za kukabidhi mali na vifaa vingine vya chuo kwa mujibu wa taratibu zilizowekwa.
 

 ii)Wanafunzi wote wanatakiwa kuripoti kwenye vyuo watakavyopangiwa wakati wa kufunguliwa kwa muhula (semester) wa pili. Tarehe halisi ya kuanza kwa muhula wa pili kwa kila chuo watakachopangiwa itatangazwa na kuwekwa kwenye tovuti ya Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania.
 

 iii)Wanafunzi wanaosoma shahada ya miaka mitatu ya ualimu wa sayansi katika masomo yafuatayo watahamishiwa katika Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM):

     a)Bachelor of Science in Education with Mathematics & Chemistry;

   b)Bachelor of Science in Education with Physics & Chemistry, na

   c)Bachelor of Science in Education with Physics & Computer Science.
 

 iv)Wanafunzi wanaosoma shahada ya miaka mitatu ya ualimu wa sayansi na Kompyuta (Bachelor of Science in Education with Mathematics & Computer Science) watahamishiwa katika Chuo Kikuu cha Kikatoliki cha Ruaha (RUCU):
 

 v)Wanafunzi wanaosoma shahada ya miaka mitatu ya ualimu wa sayansi katika masomo yafuatayo watahamishiwa katika Chuo Kikuu cha Kikatoliki cha Mwenge (MWECAU):

  a)Bachelor of Science in Education with Physics & Mathematics; na

  b)Bachelor of Science in Education with Biology & Chemistry.

vi)Orodha ya wanafunzi waliohamishwa na majina ya vyuo vikuu walivyohamishiwa itatangazwa na kuwekwa kwenye tovuti ya Tume ya Vyuo Vikuu hivi punde.
 

 vii)Wanafunzi wote waliohamishwa ambao hawakukamilisha mitihani yao ya mwisho wa muhula wa kwanza, au hawakufanya kabisa mitihani hiyo, watatakiwa kufanya mitihani hiyo katika vyuo vikuu watavyohamishiwa kwa utaratibu maalum utakaondaliwa na chuo husika.

 viii) Kila mwanafunzi anawajibika kutunza kumbukumbu zake zote muhimu za maendeleo ya kitaalama kwa ajili ya matumizi ya baadaye, ikiwa ni pamoja na matokeo ya mitihani aliyokwishafanya.
 

ix)Wanafunzi wote ambao ni wanufaika wa Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu, mikopo yao itahamishiwa katika vyuo wakapokuwa wamehamishiwa.
 

7.Kampasi nyingine za Chuo Kikuu cha SJUIT (Luguruni na Boko – Dar es Salaam; na Makambako – Njombe) zitaendelea na masomo kama kawaida.
 

8.Kwa taarifa hii, vyuo vikuu vyote nchini vinakumbushwa kufuata sheria na kuzingatia utoaji wa elimu inayokidhi viwango vya ubora vinavyokubalika kitaifa na kimataifa. Tume haitasita kuchukua hatua stahiki kwa chuo kikuu chochote kitakachobainika kutoa elimu isiyokidhi viwango vya ubora kwa kisingizio cha aina yoyote.
 

Imetolewa na

PROF. YUNUS D. MGAYA
Katibu Mtendaji
Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania 
26 Februari 2016




Orodha Ya Majina ya Wanafunzi wa St. Joseph Kampasi ya Songea Waliohamishiwa Vyuo Vingine Baada ya TCU Kukifuta Chuo Hicho

$
0
0
http://www.tcu.go.tz/images/pdf/Students%20from%20SJUCAST%20&%20SJUCIT%20%20to%20other%20institutions_25_02_2016.pdf

The Tanzania Commission for Universities (TCU) wishes to inform the general public and particularly students, who were undertaking their studies at St Joseph University College of Agricultural Sciences and Technology (SJCAST) and St Joseph University College of Information Technology (SJCIT) in Songea, that we have transferred the respective students to other universities. 

These students are required to report to the receiving institutions upon the opening of the second semester.

The dates for opening of the second semester for each receiving institution will soon be communicated through TCU website and websites of respective institutions.
 
Meanwhile, TCU hereby releases the list of names of the transferred students, which contains receiving institutions and the programmes they have been transferred to.
 
TCU would also like to inform respective students including those with Diplomas that there are names of some students, which are yet to be posted as we are continuing with the verification of their data. 

These names shall be posted as soon as the verification exercise is completed.
 
For further information or clarification please contact the Tanzania Commission for Universities through the following numbers;
 
Landline: +255 (0) 222 772 657 
Hotlines : +255 (0) 683 921 928
                +255 (0) 675 077 673

Mawaziri Wote Waliopewa Hadi Leo Jioni Kujaza Na Kurejesha Tamko La Mali Na Madeni, Hati Ya Uadilifu Wametekeleza Agizo La Rais Katika Muda Muafaka

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema agizo lilitolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. John Pombe Magufuli la kuwataka mawaziri ambao hawajajaza Tamko la Rasilimali na Madeni wakamilishe kabla ya saa 12 leo jioni limetekelezwa.

Waziri Mkuu amepokea barua kutoka kwa Kamishna wa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma, Jaji (Mst.) Salome Kaganda ikithibitisha kuwa mawaziri na naibu mawaziri wote wametekeleza agizo hilo.

“Hadi kufikia saa 9.30 leo alasiri (Ijumaa, Februari 26, 2016) mawaziri wote walikuwa wamekamilisha fomu zao za kuzikabidhi katika Ofisi za Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma,” alisema Waziri Mkuu.

Rais Magufuli leo asubuhi alitoa maelekezo kwamba Mawaziri ambao hawajajaza Tamko la Rasilimali na Madeni ifikapo leo Ijumaa tarehe 26 Februari, 2016 saa 12.00 jioni wawe wamejaza na kurejesha Fomu ya Tamko la Rasilimali na Madeni katika Ofisi za Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Dar es Salaam. Waziri ambaye atashindwa kutekeleza agizo hili atakuwa amejiondoa mwenyewe kwenye nafasi yake.

Mawaziri waliotakiwa kurejesha fomu za tamko la rasilimali pamoja na hati ya ahadi ya uadilifu kuwa ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Charles Kitwanga na Waziri wa Nchi (OMR – Muungano na Mazingira), Mhe. January Makamba. 
 
Wengine ni Waziri wa Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Ushirikiano wa Kikanda na Kimataifa, Dk. Augustine Mahiga ambaye alitakiwa kurejesha hati ya ahadi ya uadilifu kwa viongozi wa umma na Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi, Prof. Joyce Ndalichako ambaye alitakiwa kutoa tamko la rasilmali na madeni.

Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Nchi (OMR – Mazingira), Mhe. Luhaga Mpina alitakiwa kurejesha fomu za tamko la rasilmali na madeni pamoja na hati ya ahadi ya uadilifu kwa viongozi wa umma.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,2 MTAA WA MAGOGONI,
S.  L. P. 3021,11410 DAR ES SALAAM.
IJUMAA, FEBRUARI 26, 2016

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Uingereza Jumamosi YaLeo February 27, 2016

Kurasa Za Mbele Za Magazeti Ya KENYA Jumamosi ya Leo Februari 27

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya TANZANIA Jumamosi Ya Leo Februari 27

Meneja Vipindi wa kituo cha televisheni cha East Africa (EATV) Afikishwa Mahakamani Kwa Kuhifadhi Raia Wa Kigeni

$
0
0

WATU wawili akiwemo Meneja Vipindi wa kituo cha televisheni cha East Africa (EATV), Lidya Igarabuza (37) wamepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu wakikabiliwa na mashitaka mawili likiwemo la kuishi nchini bila kibali.

Igarabuza ambaye ni mtanzania na raia wa Kenya, David Wachila (36), ambaye anadaiwa kuwa ni DJ wa muziki katika kituo hicho cha televisheni, walifikishwa mahakamani hapo jana na kusomewa mashitaka mbele ya Hakimu Mkazi Mkazi, Kwey Rusema.

Wakili wa Serikali kutoka Idara ya Uhamiaji, Khadija Masoud alidai kuwa Februari 25, mwaka huu katika maeneo ya Mikocheni A, Wachila akiwa raia wa Kenya, alikutwa akiishi nchini bila kibali jambo ambalo ni kinyume cha Sheria za Uhamiaji. Katika mashitaka yanayomkabili, Igarabuza anadaiwa kumhifadhi Wachila jambo ambalo ni kinyume cha sheria.

Inadaiwa Februari 25, mwaka huu huko maeneo ya Mikocheni, Igarabuza alikutwa amemhifadhi Wachila huku akijua jambo hilo ni kinyume cha sheria. Washitakiwa walikiri kutenda makosa hayo.

Wakili Masoud aliiomba mahakama ipange tarehe nyingine kwa ajili ya kuwasomea maelezo ya awali. Hakimu Rusema aliahirisha kesi hiyo hadi Machi Mosi, mwaka huu. Igarabuza aliachiwa kwa dhamana wakati mshitakiwa Wachila akirudishwa rumande kwa kukosa wadhamini.

Nape Nnauye Ataka Magazeti Ya Serikali Yamsaidie Rais Magufuli Kutumbua Majipu Kwa Kuibua Uozo Serikalini

$
0
0

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye ametaka magazeti ya Serikali kumsaidia Rais John Magufuli, kutumbua majipu kwa kuibua uozo serikalini.

Akizungumza katika kikao cha wafanyakazi wa Kampuni ya Tanzania Standard (Newspapers) Ltd Dar es Salaam jana, inayochapisha magazeti ya Daily News, HabariLeo na Spotileo, Nape ametaka magazeti hayo yasimung’unye maneno kwa kuandika ukweli; kwenye nyeusi yaandike nyeusi na kwenye nyeupe, yaandike nyeupe.

Alisema vyombo vya habari vya Serikali vina wajibu wa kumsaidia Rais kutumbua majipu kwa kuandika habari bila woga, upendeleo wala kuomuonea mtu, ili kama kuna dosari ziko mahali ziibuliwe kwa lengo la kupata suluhu.

“Unajua vyombo vya habari vinaaminika na vinasomwa na wengi na hasa wananchi wanapotaka ukweli wa jambo, wanaangalia kama limeandikwa, sasa kama jambo litaandikwa kwa kufichwa fichwa haitaisaidia Serikali, kama ni nyeusi sema nyeusi, kama ni nyeupe sema nyeupe na hiyo ndiyo suluhu,” alisisitiza Nape.

Alisema majipu yanayoendelea kutumbuliwa na Rais, mengine yanaibuliwa na vyombo vya habari na ili kumsaidia na kusaidia Taifa, vyombo vya habari vya Serikali lazima viibue hayo, pia viaminiwe mpaka na watumishi wa Serikali, wavitumie kuibua uozo.

Nape alisisitiza kwamba kuficha ukweli kwenye jambo ovu, ni kuendelea kuharibu hivyo kuibuliwa kwa maovu kutaisaidia Serikali na watendaji wake kuchukua hatua madhubuti.

 “Kuna hili jambo la baadhi ya watendaji kusema mfumo hautaki hili, hakuna cha mfumo ni maneno yao wanayatumia kama kichaka cha kufanya uchafu,” alisema Nape.

Nape alitoa onyo kwa watendaji wa serikali kuacha tabia ya kuzuia habari zisitoke kwa maslahi yao na kutaka wenye pingamizi ya kutoka kwa habari, wawasiliane naye na si kuingilia chombo cha habari.


TANESCO Yapeleka Maombi ya Kupandisha Bei Ya Umeme

$
0
0

SHIRIKA la Umeme (Tanesco) limepeleka maombi kwa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (Ewura), kuomba kupandisha bei ya nishati hiyo, kinyume na matakwa ya Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo ya kushusha bei hiyo.
 
Taarifa ya Ewura kwa umma iliyotolewa kwenye vyombo vya habari jana, imeeleza kuwa maombi hayo yamepokewa Jumatano ya wiki hii na kutaka wadau kujitokeza kujadili uhalali wa nyongeza hiyo siku mkutano huo utakapoitishwa.
 
“Mamlaka inaanzisha mchakato wa kupata maoni ya wadau, ili kujua uhalali wa maombi ya nyongeza ya bei za huduma iliyoyapokea kutoka Tanesco,” imeeleza taarifa hiyo.
 
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, Tanesco iliwasilisha ombi husika kulingana na Sheria ya Umeme namba 131, inayoitaka Ewura kufanya mabadiliko ya bei zinazotozwa na mtoa huduma mara moja kila baada ya miaka mitatu.
 
“Pendekezo la wastani wa badiliko la bei za umeme ni asilimia 1.1 kuanzia Aprili mosi 2016 na asilimia 7.9 kuanzia Januari mosi 2017,” limeeleza tangazo hilo.
 
Mapendekezo hayo japo ya kisheria, lakini yanapingana na msimamo wa Waziri Muhongo, ambaye tangu alipoapishwa kushika wadhifa huo, alielezea kusudio lake la kutaka bei ya nishati hiyo ishushwe.
 
Profesa Muhongo alikwenda mbali na kuagiza Tanesco, Ewura na Shirika la Maendeleo ya Petroli (TPDC), kumpelekea mapendekezo ya kushuka kwa bei ya umeme kuanzia mwanzoni mwa mwaka huu.
 
Katika maagizo hayo, Profesa Muhongo alihoji kwa nini bei ya umeme isishuke, wakati gharama za uzalishaji wa umeme wa kutumia mafuta zimeshuka kutokana na kupungua kwa bei ya mafuta katika soko la dunia.
 
Kutokana na maombi hayo ya Tanesco, Ewura imewataka wadau wa nishati wanaopenda kutoa maoni yao kwa maandishi, kufanya hivyo kwa kutuma maoni yao kwa Mkurugenzi Mkuu wa Ewura, ghorofa ya saba jengo la LAPF Pensions Fund Tower, mkabala na Kijiji cha Makumbusho, Kijitonyama Dar es Salaam.
 
Kwa watakaotuma kwa njia ya posta, wameombwa kufanya hivyo kwa kutumia Sanduku la Posta 72175, Dar es Salaam, Tanzania, simu namba (+255-22) 2123853-4; Fax namba (+255-22) 2123180; Barua pepe info@energyregulators.org au tovuti http://www. energyregulators. org.
 
Taarifa hiyo imeeleza kuwa mamlaka hiyo pia, itaitisha mikutano ya wazi ili kukusanya maoni kuhusu mapendekezo hayo kutoka kwa wadau mbalimbali, wakiwamo Baraza la Wawakilishi wa Watumiaji wa Huduma (CCC); Baraza la Ushauri la Serikali (GCC) pamoja na wananchi kwa ujumla.

CUF Kuandamana Kupinga Marudio Ya Uchaguzi Zanzibar

$
0
0

CHAMA cha Wananchi (CUF) Bukoba kimejiandaa kufanya maandamano ya amani keshokutwa, kwa ajili ya kupinga kufanyika upya uchaguzi wa Zanzibar unaotarajiwa kuwa Machi mwaka huu.

Kimeiomba pia serikali ya awamu ya tano, kuchukua uamuzi wa kumtambua Maalim Seif Sharif Hamad kuwa ndiye mshindi wa uchaguzi wa urais Zanzibar na kuwa hakiko tayari kurudia uchaguzi huo tena.

Akizungumza na waandishi wa habari juu ya msimamo wa chama hicho, Kaimu Mwenyekiti wa chama hicho Saverina Mwijage, alisisitiza kuwa kamwe chama hicho hakitakuwa tayari kurudia uchaguzi huo uliotangazwa na Tume ya uchaguzi ya Zanzibar (ZEC) kuwa utafanyika Machi 20,kwa kile kinachodaiwa ni kufutwa uchaguzi wa Oktoba 25,mwaka jana.

“Tumedhamiria kuandamana ili kumfikishia ujumbe wetu Rais John Magufuli kupitia kwa Mkuu wa mkoa wa Kagera, John Mongella lengo letu hasa ni kupinga uchaguzi wa Zanzibar. Hali ya Zanzibar kwa sasa haiko shwari, watu wanatishiwa maisha yao, wanaishi kwa hofu juu ya maisha,” alisisitiza.

Mwijage ambaye pia ni Makamu Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wanawake wa CUF Taifa, alisema chama hicho kinatambua uchaguzi ulishakwisha na tume hiyo ilishatoa vyeti kwa walioshinda, kwa mantiki hiyo CUF inamtambua Maalim Seif kuwa alishinda katika uchaguzi huo.

Alisema maandamano hayo yanatarajiwa kuanzia saa 4:00 asubuhi hadi saa 9:00 alasiri na baadaye utakuwepo mkutano wa hadhara katika Uwanja wa Mashujaa Mayunga ulioko mjini Bukoba ili kuutangazia umma juu ya msimamo wa chama hicho na baada ya hapo watazunguka katika wilaya za Muleba, Missenyi na Karagwe.

Majambazi Dar es Salaam Yavamia Benki Ya Access....Yaua Mlinzi na Kupora Pesa, Polisi Wapambana Nayo na Kuyaua

$
0
0

Majambazi  ambao  idadi  yao  haikufahamika  wakiwa  na  mabomu  na  bunduki  za  kisasa  jana  walivamia  Benki  ya  Access  tawi  la Mbagala  ambako  walipora  viroba vya   fedha, kuua  mlinzi  na  baadae wanne  kati  yao  waliuawa  na  jeshi  la  polisi.

Watu  walioshuhudia  tukio  hilo  walisema  baada  ya  majambazi  hao  kufika  katika  benki  hiyo  kwa  bodaboda  nne  majira  ya saa  nane  mchana,yalimuua  mlinzi  wa  benki  hiyo, kusha  kubomoa  kwa  risasi  mlango  wa  vioo  na  kuingia  ndani  na  kuzua taharuki  kubwa

Mashuhuda  hao  walisema, katika  tukio  hilo  lililodumu  kwa  karibu saa  moja,mmoja  wa  majambazi  hao  aliyekuwa  amevaa  kininja,alikuwa barabarani  akiamuru  magari  kupita  haraka  huku  akifyatua  risasi  hovyo.

Ilielezwa  kuwa, jambazi  huyo  aliyeonekana  kuwa  na  uzoefu  wa  matumizi  ya  bunduki  alikuwa  akifyatua  risasi  kwa  kutumia  mkono  mmoja  na  ndiye  aliyewajeruhi  baadhi  ya  wapita  njia.

Hivyo,wakati  uporaji  ukiendelea  na  jambazi  huyo  akiimarisha  ulinzi  barabarani  baadae  hakukuwa  na  magari  wala  pikipiki  zilizokuwa  zikipita.

Mfanyabiashara  wa  duka  la  vifaa  vya  ujenzi  jirani  na  benki  hiyo,Ramadhani Tairo  alisema  baada  ya  jambazi  huyo  kuliona  gari  la  polisi  likielekea  eneo  la  tukio,alifyatua  risasi  na kulipiga  kabla  halijafika.Gari  hilo  lilipoteza  mwelekeo  na  kutumbukia  mtaroni.

Tairo  alisema  mbali  na  jambazi  huyo  kulipiga  risasi  gari  la polisi  pia  alilirushia  bomu  la  mkono,lakini  liliangukia  barabarani  bila  kuripuka.Polisi  walifanikiwa  kulilipua  bomu  hilo  baadae  likiwa  halijasababisha  madhara  kwa wananchi  waliofika  kushuhudia  tukio  hilo.

Mkazi  mwingine  wa  eneo  hilo,Rebecca  Maliva  alisema  majambazi  walioingia  ndani  ya  benki  hiyo  walioneka  wakitoka  na  viroba  vitatu vya  fedha  ambavyo  walivipakata kwenye  pikipiki  na  kuondoka  kwa  kasi  kuelekea  Mkuranga kupitia  barabara  ya  Kilwa.

Rebecca  alisema  polisi  zaidi  walifika  kwenye  eneo  hilo  wengine  wakiwa  kwenye  pikipiki  na  kuanza  kuwafukuza  majambazi  hao  ambapo  walipofika  eneo  la  shule  ya  St. Marry's,walitupa  kiroba  kimoja  cha  fedha  ambacho  wananchi  waliokuwa    jirani  waligombania  na  kuchukua  fedha  zilizokuwemo  na   kisha  kila  mmoja  kukimbia  na  burungutu  la  noti.

Baada  ya  nusu  saa  wakati  umati  ukiwa  bado  upo  kwenye  benki  hiyo,magari  ya  polisi  yalipita  katika eneo  hilo  yakitokea  eneo  la  Mkuranga  yakiwa  yamebeba  miili  ya  majambazi  yaliyouawa.

Magari  hayo  yalikuwa  yakisindikizwa  na  vijana  wa  bodaboda  waliokuwa  wakishangilia  kazi  iliyofanywa  na  polisi.

Kamanda  wa  p[olisi  kanda  maalum ya  Dar es Salaam, Simon Sirro  alizungumzia  kwa  ufupi  tukio  hilo n kwamba  majambazi  manne  yaliuawa  na  kukamata  silaha  tatu,lakini  hakutaka  kuingia  kwa  ndani  akisema  atatoa  taarifa  zaidi  leo

Wafanyabiashara ya Sukari Wamchokonoa Rais Magufuli...... Wapandisha Bei Kiholela, Bodi Yakana Upungufu wa Sukari Nchini

$
0
0
SASA ni wazi kwamba wafanyabiashara wa sukari nchini wameamua kuanzisha vita na Rais John Magufuli, kwa kuamua kuficha bidhaa hiyo na hivyo kuadimika katika soko na kupanda bei.

Hatua hiyo ya wafanyabiashara imekuja baada ya Rais Magufuli kupiga marufuku  uagizwaji  holela wa sukari kutoka nje, isipokuwa kwa kibali maalum cha Ikulu

Jana Bodi ya Sukari ililazimika kuitisha mkutano na waandishi wa habari na kueleza kile walichokibaini baada ya kuwapo kwa taarifa kuwa bidhaa hiyo imeadimika.

Akitoa tamko kwa niaba ya Bodi ya Sukari na wazalishaji bidhaa hiyo, Mwenyekiti wa bodi ya Wakurugenzi wa Kiwanda cha Sukari cha Kilombero, Ami Mpungwe, alisema tangu Rais Magufuli alipotangaza utaratibu huo  wamebaini kuwa baadhi ya wafanyabiashara wameanza kufanya mipango ya kuhujumu taratibu hizo.

Alisema wafanyabiashara hao wameamua kuficha bidhaa hiyo ili kuwaaminisha wananchi kwamba sababu kubwa ya kuadimika kwa sukari inachangiwa na uamuzi huo wa rais.

Kabla ya uamuzi huo haujafikiwa na Rais Magufuli, wafanyabiashara wengi wa bidhaa hiyo walikuwa hawalipi kodi hali iliyochangia kufanya biashara hiyo kiholela huku wakipata faida nyingi na kuinyima mapato Serikali.

Hili linathibitishwa na kauli iliyotolewa na Mpungwe jana ambaye aliwanyooshea vidole waziwazi wafanyabiashara hao kwamba walikuwa wakinufaika na uingizaji holela wa sukari bila kulipia kodi na kwamba hata wanachokifanya sasa cha kupandisha bei ya sukari ni mbinu chafu ili kudhoofisha juhudi za Serikali za kuendeleza viwanda vya ndani kwa nia ya kujinufaisha wao binafsi.

“Wameanzisha kampeni za kuwatia hofu wananchi wakiwaonyesha sukari imeadimika kutokana na agizo lililotolewa na Serikali la kudhibiti uingizaji sukari nchini,” alisema Mpungwe.

“Miongoni mwa vitendo hivyo ni kuficha maghalani na kuendesha propaganda kwamba bei ya sukari imepanda na wapo waliopandisha kwa ghafla bei ya sukari kwa madai kwamba kuna upungufu viwandani na wengine wakiwalaghai watu kwamba bei wanayonunulia viwandani imepanda,” alisema Mpungwe na kusisitiza kuwa wanaofanya hujuma hiyo watachukuliwa hatua za kisheria.

Mwenyekiti huyo wa Bodi ya sukari nchini, alisema wazalishaji nchini wanatambua kwamba viwanda vyote vya wasambazaji vinauza sukari kati ya shilingi 1,700 na 1,800 kwa kilo na hakuna kilichopandisha bei tangu tamko la Rais lilipotoka.

“Hali ya uzalishaji sukari msimu huu 2015/2016 ni nzuri na msimu utafungwa Aprili kupisha matayarisho ya msimu mpya 2016/2017 Mei na Juni 2016 kama ilivyo taratibu kwa kila mwaka na viwanda vina akiba ya tani 32,000 za sukari inayoendelea kuuzwa,” alisema na kuongeza:

“Kiwanda cha sukari cha TPC kilichopo Moshi na kile cha Kagera vinaendelea kuzalisha sukari hadi Aprili 2016 na Serikali imeshatangaza utaratibu wa uagizaji wa sukari ambao utahakikisha sukari inayoruhusiwa kuingizwa nchini na kiasi kinachohitajika kuziba mahitaji ya wakati viwanda vinapokuwa vimefunga uzalishaji.”

Aliongeza kuwa kutokana na utaratibu huu mpya wa kuweka uwazi katika usimamizi wa bidhaa ya sukari, utasaidia kwa kiwango kikubwa kudhibiti sukari ya magendo na kuhakikisha inayoingia ni ile iliyoruhusiwa kwa kulipiwa kodi.

Mwenyekiti huyo alisema Bodi ya sukari na wazalishaji wanawahakikishia Watanzania kwamba hali ya upatikanaji wa sukari nchini ni nzuri na wao kwa kushirikiana na vyombo husika vya Serikali watahakikisha wanaendelea kuwa na sukari ya kutosha kwa muda wote.

Hivi karibuni Rais Magufuli alitoa kauli ya kupiga marufuku uingizwaji wa sukari kutoka mataifa ya kigeni ili kuvilinda viwanda vya sukari nchini ambavyo vimeathiriwa na uingizaji wa sukari ya bei rahisi kutoka nje.

Rais huyo alisema Taifa haliwezi kufikia malengo yake ya kuimarisha viwanda vya ndani iwapo viwanda vya sukari nchini havitalindwa na kuwezeshwa dhidi ya uingizaji huo.

Rais Magufuli alielezea kuwepo kwa viwanda nchini ambavyo hununua miwa kutoka kwa wakulima wadogo wadogo na viwanda hivyo huzalisha sukari, lakini pia ajira ni chanzo cha mapato ya Serikali.

Alisema ingawa ipo hifadhi ya kutosha ya sukari lakini wapo watu serikalini wanaotoa vibali vya kuingiza sukari kutoka nje.

Aliwaelezea watu hao kama ni sehemu ya kukandamiza juhudi za Serikali hali iliyosababisha kuchukua hatua ya kuzuia utolewaji wa vibali kuruhusu uingizaji wa sukari, hadi itakapotokea mahitaji maalumu.

Alisema wapo baadhi ya wafanyabiashara wasiowaaminifu ambao wamekuwa wakiingiza sukari nchini iliyoisha muda wake wa matumizi na haifai kutumiwa na binadamu.

Mahitaji ya sukari nchini ni tani 420,000 ambako tani 170,000 zinatumiwa kwa mahitaji ya nyumbani na nyingine iliyobaki hutumiwa viwandani.

Alisema viwanda vya hapa nchini vimekuwa vikizalisha tani 300,000 hali inayosababisha kuwepo kwa upungufu wa tani 290,000 kila mwaka kwa matumizi ya nyumbani na yale ya viwandani.

Vurugu Kubwa Zaibuka Wakati wa Uchaguzi wa Meya wa Jiji la Dar es Salaam

$
0
0
VURUGU kubwa zimetokea wakati wa Uchaguzi wa meya wa Jiji la Dar es Salaam mara baada ya uchaguzi huo kuhairishwa  tena kwa mara ya nne leo,huku Jeshi la Polisi likivamia ukumbi wa Karimjee na kuanza kupambana na Madiwani na wabunge wa Muunganiko wa umoja wa Vyama vinavyounda  UKAWA.

Tukio hilo la aina yake limetokea leo katika ukumbi wa Karimjee  jijini Dar es salaam mara baada ya mkurugenzi wa Jiji kutangaza kuahirisha uchaguzi huo kwa madai ya uchaguzi  kuwekewa pingamizi na CCM mahakamani.

Jambo hilo liliwachukiza   madiwani wa UKAWA ambao walidai kuwa hawajapata barua ya pingamizi hilo, hivyo wakataka waruhusiwe kufanya uchaguzi peke yao kwa kuwa akidi ya madiwani kufanya uchaguzi ilikuwa imetimia.

Wakati UKAWA  wakijiiandaa kufanya uchaguzi huo  wenyewe ,Polisi zaidi ya 15 walivamia ukumbi huo na kuwataka madiwan hao waondoke ukumbini,jambo lilowachukiza tena na kuibua patashika ndani ya ukumbi.

Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images