Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Kamanda Kova Ambwaga Tena Nzowa Mahakamani

$
0
0
 
Mahakama ya Rufaa Tanzania, imetupilia mbali kesi ya kugombea nyumba namba 140 iliyopo eneo la Sekei Arusha baina ya makamishna wawili wa Jeshi la Polisi, Godfrey Nzowa, ambaye ni Mkuu wa Kikosi cha Kupambana na Dawa za Kulevya na aliyekuwa Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Suleiman Kova.

Aidha, mahakama hiyo imeamuru Nzowa kulipa gharama.

Akisoma jana maamuzi ya Mahakama yaliyotolewa na majaji watatu wa vikao vya mahakama ya rufaa vinavyoendelea Jijini Arusha, ambao ni Mwenyekiti wa jopo la kikao cha mahakama ya rufaa, Jaji Mbarouk Salum Mbarouk, Mussa Kipenga na Bernad Luanda, Naibu Msajili wa Mahakama ya Rufaa Tanzania, Elizabeth Mkwizu, alisema kesi hiyo imeondolewa katika usikilizwaji wa vikao vya mahakama hiyo kwa sababu za kiufundi.

“Sababu ya kuondoa kesi hii ni mkata rufaa Nzowa… alichelewa kukata rufaa ndani ya siku 60 na hivyo kuwa nje ya sheria kama inavyotakiwa, ukitaka kukata rufaa, ukate rufaa ndani ya siku 60 tangu kesi ya msingi kutolewa hukumu,” alisema.

Mkwizu alisema mbali na kesi hiyo kuondolewa mahakamani, Mahakama ya Rufaa pia imeamuru Nzowa kulipa gharama za wajibu rufaa ambao ni Kova na Wakala wa Majengo (TBA).

Katika kesi hiyo, makamishna hao wanagombea nyumba ya serikali iliyopo maeneo ya Sekei ijini Arusha, ambapo Nzowa anapinga kuuziwa Kova nyumba hiyo ambayo wakati ikiuzwa kwa watumishi wa serikali yeye ndiye alikuwa akiishi humo.

Wakati huo Nzowa alikuwa Mkuu wa Upelelezi wa makosa ya jinai Mkoa wa Arusha (RCO), wakati Kova alikuwa ameshahamishwa kikazi mkoani Arusha.

Nyumba hiyo ni moja ya zile walizouziwa watumishi wa serikali wakati wa serikali ya awamu ya tatu, chini ya Rais Benjamin Mkapa na kusimamiwa na aliyekuwa Waziri wa Ujenzi, Rais John Magufuli.

Awali, akizungumza mahakamani hapo mbele ya majaji hao, wakili wa serikali, Sylvester Mwakitalu kwa niaba ya mjibu maombi wa pili, TBA, waliomba mahakama hiyo kutupilia mbali kesi hiyo kutokana na Nzowa kuchelewa kutoa kusudio la kukata rufaa.

Alisema upande huo wa waleta maombi, umekiuka utaratibu wa kisheria wa kukata rufaa ndani ya siku 60, ambapo wao walitoa kusudio la kukata rufaa Oktoba 3 mwaka 2014 na kwamba, Januari 2, 2015, ndipo rufaa yao iliwasilishwa kwa Msajili wa Mahakama.
 
Hoja hiyo iliungwa mkono na wakili Dilip Kesaria, anayemtetea Kamishana Suleiman Kova.

Hata hivyo, mawakili wa Nzowa, Neema Mtayangulwa na Mpaya Kamara, walipinga pingamizi hilo na kuomba mahakama hiyo iendelee usikilizwaji wa kesi kwani upande huo unachelewesha kesi pasipo sababu za msingi.

Alisema kuwa kimsingi, kusudio la kukata rufaa lilitolewa kabla ya kuanza uwasilishaji wa kesi na hivyo kesi hiyo inapaswa kusikilizwa.

Katika kesi hiyo, Kamanda Kova alijaza fomu namba 27 Mei mwaka 2002 ya kuomba kununua nyumba hiyo iliyokuwa namba 203, kabla ya kubadilishwa kuwa namba 149, akidai ni makazi yake. Aliyekuwa akiishi katika nyumba hiyo kwa muda huo ni Nzowa.

Pamoja na kujaza fomu hizo, pia Kova alitoa fedha za kununua nyumba hiyo wakati Nzowa akiishi humo.

IGP Afanya Mabadiliko Ya Makamanda Wa Polisi Kwa Baadhi Ya Mikoa

$
0
0

Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini IGP Ernest Mangu amefanya Mabadiliko kwa baadhi ya Makamanda wa Polisi wa mikoa na vikosi hapa nchini.

Mabadiliko hayo ni pamoja na aliyekuwa kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro Kamishna Msaidizi Mwandamizi SACP Leonard Paul amehamishwa  kwenda kuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga na nafasi yake kuchukuliwa na Kamishna Msaidizi Mwandamizi SACP Ulrich Matei aliyekuwa Mkuu wa Utawala Kanda Maalumu ya Dar es Salaam.  

Kamishna Msaidizi wa Polisi ACP Mihayo Msikhela  aliyekuwa kamanda wa Polisi mkoa wa Tanga amehamishwa kwenda kuwa Mkuu wa Kikosi cha Kuzuia dawa za kulevya. 
 
Aliyekuwa Kamanda wa Polisi mkoa wa kilimanjaro Kamishna Msaidizi wa Polisi ACP Ramadhani Mungi anaenda kuwa Kamanda wa Polisi Kikosi cha Bandari na nafasi yake inachukuliwa na   Kamishna Msaidizi wa Polisi ACP Wilbrod Mtafungwa ambaye alikuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Njombe. 
 
Aliyekuwa Afisa mnadhimu Mkoa wa Iringa Kamishna Msaidizi wa Polisi ACP Prudenciana Protas anakwenda kuwa Kamanda wa Polisi mkoa wa Njombe. 
 
Aliyekuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mara Kamishna Msaidizi wa Polisi ACP Philipo Kalangi amehamishiwa Makao Makuu ya Polisi na nafasi inachukuliwa na aliyekuwa Mkuu wa Upelelezi mkoa wa Shinyanga ACP Ramadhan Ng’azi.   
 
Aidha,  Kamanda wa Polisi Mkoa wa Manyara Kamishna Msaidizi wa Polisi ACP Camilius Wambura anakwenda kuwa Mkuu wa Upelelezi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam  na nafasi yake kuchukuliwa na Kamishna Msaidizi wa Polisi ACP Francis Massawe kutoka Makao Makuu ya Upelelezi Dar es Salaam. 

Aliyekuwa Afisa Mnadhimu Mkoa wa Arusha Kamishna Msaidizi wa Polisi ACP Gilles Mroto anakwenda kuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi Tarime/Rorya kuchukua nafasi ya Kamishna Msaidizi wa Polisi ACP Gemini Mushi aliyehamishiwa Makao Makuu ya Upelelezi Dar es Salaam. 
 
Wengine ni pamoja na Naibu Kamishna wa Polisi DCP Hezron Gimbi anayetoka Upelelezi Makao Makuu Dar es  Salaam kwenda kuwa Mkuu wa Utawala Kanda Maalumu Dar es Salaam pamoja na aliyekuwa Mkuu wa Upelelezi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi SACP Costantine Massawe anakwenda kuwa Mkuu wa Oparesheni wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam.

Mabadiliko hayo ni ya kawaida kwa mujibu wa Sheria,  kanuni na taratibu za Jeshi la Polisi.

 Imetolewa na:
Advera Bulimba-SSP
 Msemaji wa Jeshi la Polisi (T)

 Makao Makuu ya Polisi.

Waziri wa Elimu Profesa Joyce Ndalichako Awasimamisha Kazi vigogo watatu taasisi ya elimu

$
0
0
JOYCE Ndalichako, Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi, amewasimamisha kazi watumishi watatu wa Bodi ya Taasisi ya Elimu nchini (TET) kwa kushindwa kusimamia   sheria ya manunuzi na kazi ya uchapaji wa vitabu ili kupisha uchunguzi

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo kwa niaba ya Waziri wa Elimu, Maimuna Tarishi ambaye ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, amesema watumishi hao hawakutekeleza majukumu yao ipasavyo na kuruhusu vitabu hivyo kuchapishwa vikiwa na mapungufu.

“Mnamo tarehe 22 Januari mwaka 2016 bodi hiyo ilishauriwa kusitisha uchapaji wa vitabu uliokuwa ukifanywa na kampuni ya Yukos Enterprises Ltd baada ya kubainika kuwa na mapungufu, lakini haikusitisha,” amesema Tarishi na kuongeza.

“Serikali iliamua kusitisha uchapishaji wa vitabu hivyo ili isiendelee kupokea vitabu vyenye mapungufu, hata hivyo taasisi ya elimu haikusitisha uchapishaji wa vitabu hivyo, badala yake kampuni hiyo ilichapisha vitabu vyote ilivyopangiwa,” amesema Tarishi.

Tarishi amesema ufuatiliaji uliofanywa na wizara katika bohari ambayo ilikuwa inapokea vitabu hivyo, ulibaini kuwa vitabu vilivyowasilishwa na kampuni ya Yukos vilikuwa na kasoro.

“Kutokana na kasoro hizo, Taasisi haikutekeleza wajibu wake wa kusimamia uchapaji wa vitabu na uzingatiaji wa sheria ya manunuzi kikamilifu,” amesema.

Kutokana na mapungufu hayo, Wizara imetoa maagizo ya kuondolewa kwa baadhi ya vitabu vilivyowasilishwa kwenye bohari ya serikali ifikapo tarehe 29 Februari mwaka huu.

“ Taasisi ya Elimu iwasimamishe kazi mara moja watumishi wafuatao ambao walikuwa na jukumu la kusimamia sheria ya manunuzi na kazi ya uchapaji wa vitabu ili kupisha uchunguzi,” amesema.

Amewataja watumishi hao kuwa ni  Peter Bandio, aliyekuwa Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Vifaa vya Kielimu, Pili Magongo Mwanasheria wa TET na Jackson Mwaigonela Mkuu wa Kitengo cha Manunuzi na Ugavi.

Mapungufu yaliyoonekana kwenye vitabu hivyo ni  upungu wa mwingiliano wa rangi, upungufu wa kurasa katika vitabu, ukataji usiozingatia vipimo,vitabu kuchakaa kabla ya matumizi na mpangilo mbaya wa kurasa.

UKAWA Watoa Tamko Baada Ya Uchaguzi Wa Umeya Jijini Dar Kuhairishwa Leo

$
0
0

Uchaguzi Mkuu ulifanyika tarehe 25.10.2015 na wananchi wa Jiji la DSM Waliamua kuongozwa na UKAWA na ndio maana walichagua Madiwani na Wabunge wengi kutoka UKAWA. Kati ya Majimbo 10 ya Uchaguzi katika Jiji la DSM CCM ilipata Majimbo 3 tu baada ya kuchakachua na UKAWA ilipata yaliyosalia.
 
Hali ni hiyo hiyo kwenye kata. Wananchi waliamua kuipumzisha CCM kwa kuwa walikua wamechoshwa na uendeshaji mbaya wa Jiji la Dar es Salaam . Tangu Uchaguzi umalizike mpaka leo wananchi wanakosa huduma za Jiji kwa sababu CCM ilitaka kushinda Umeya wa Jiji kwa staili ileile waliyozoea ya goli la mkono. 
 
Mara wakaletwa wapiga kura feki kutoka Zanzibar huku Wakijua wazi kuwa TAMISEMI sio jambo la Muungano. Waziri mwenye dhamana na TAMISEMI hajawahi kutoa kauli wala kukemea hali hiyo hata siku moja huku akijua wazi kuwa vitendo hivyo vilikua ni kinyume Cha sheria za Nchi.
 
Leo tarehe 27.02.2016 tumeshuhudia Uchaguzi ukiitishwa na baada ya wajumbe Kuwasili wakakutana na kilichoitwa zuio la Mahakama la Tangu tarehe 05.02.2016 .

 Jambo hili limetokea baada ya Taarifa kusambaa jana tarehe 26.02.2016 kuwa CCM walipeleka shauri mahakamani la kuweka zuio na kuwa shauri hilo lilitupiliwa Mbali. 

Nini kinafichwa Jiji la DSM ? Tuna taarifa kuwa ni Ufisadi mkubwa uliofanywa na viongozi wa Jiji waliopita na wakishirikiana na Viongozi wa CCM kupora Mali za Jiji kama vile UDA, Mali za soko la Kariakoo, Viwanja na majengo ya Jiji. 

Pili tuna Taarifa kuwa hawataki majipu ya Jiji yatumbuliwe kwani kuna vigogo wakubwa wa CCM watatumbuliwa kutokana na kushiriki kwenye Ufisadi mkubwa ndani ya Jiji la Dar es Salaam . Mipango iliyopo.

Mkutano wa Uchaguzi Leo uliitishwa pamoja na kuwepo hicho kinachoitwa zuio la Mahakama kwa lengo la kuwaudhi Madiwani wa UKAWA ili waonekane kuwa wanafanya fujo . 

Hii ni kutokana na ukweli kuwa kama zuio lipo Tangu siku CCM wanaadhimisha miaka39 ya kuzaliwa kwake ni kwanini Mkurugenzi aliitisha mkutano wakati akijua Mahakama imeweka zuio?. 

Mpango huu umesukwa ili kuhakikisha kuwa Waziri mwenye dhamana na TAMISEMI anatengenezewa sababu za kuweza kuvunja Halimashauri ya Jiji la Dar es Salaam na kuunda Tume ya kuongoza Jiji. 
 
Ni vyema tukaweka angalizo mapema kuwa Mafisadi wana mikakati mingi sana ya kuhakikisha kuwa hawatumbuliwi Majipu. Kama Rais ambaye ndio Waziri mwenye dhamana na TAMISEMI hakubaliani na mbinu hizi za Mafisadi, aingilie Kati Mara moja na kuhakikisha kuwa Uchaguzi wa Meya unafanyika na kazi ya kutumbua majipu ya Jiji inaendelea kama ambavyo imeshaanza katika Manispaa za Ilala na Kinondoni zinazoongozwa na UKAWA .

Imetolewa na John Mrema.
Mkurugenzi wa Bunge na Halimashauri CHADEMA.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Uingereza Jumapili Ya Leo February 28, 2016

Kurasa Za Mbele Za Magazeti Ya KENYA Jumapili ya Leo Februari 28

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya TANZANIA Jumapili Ya Leo Februari 28

Waziri Mkuu Kutua Jijini Mwanza Kesho Kutwa

$
0
0

WAKAZI wa Jiji la Mwanza na vitongoji vyake wametakiwa kujitokeza kwa wingi keshokutwa ili kumpokea Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ambaye anatarajiwa kuwasili jijini hapa akitokea jijini Dar es Salaam akielekea mkoani Simiyu.
 
Hayo yameelezwa jana jijini hapa na Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Baraka Konisaga ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana, wakati alipokuwa akizungumza na wafanyabiashara wa Kamanga Feri wakati alipowaongoza kwenye shughuli ya kufanya usafi.
 
“Niwataarifu kuwa Waziri Mkuu atawasili jijini Mwanza kwa mara ya kwanza siku ya Jumanne majira ya saa 7:00 mchana akitokea jijini Dar es Salaam… akishawasili hapa ataelekea mkoani Simiyu kikazi, nawaomba muiweke moyoni siku hiyo ya Jumanne na mjitokeze kwa wingi kumlaki kiongozi wetu mpendwa, ” alisema.

Ripoti Ya Polisi Kuhusu Tukio la Ujambazi Mbagala: Waliofariki Dunia ni Watu 7........Kati Yao Majambazi ni 3, Askari 2 na Raia 2

$
0
0

Ujambazi wa kutumia vifaa vya kivita umeibuka jijini Dar es Salaam, ukiwemo uliofanyika katika uporaji wa Benki ya Access juzi, ambako majambazi walitumia bunduki za kivita aina ya SMG na mabomu ya kurusha kwa mkono.

Akizungumza jana, Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Simon Sirro, alisema mbali na uvamizi huo, pia Polisi imebaini na kukamata askari bandia, waliokuwa na sare rasmi za Jeshi la Polisi zenye vyeo na redio call, zenye uwezo wa kuingilia mawasiliano ya askari Polisi.

Akizungumzia matukio hayo, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga alisema atakutana na Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dk Hussein Mwinyi, ili Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Jeshi la Polisi, waanzishe msako wa pamoja dhidi ya wahalifu hao.

Uvamizi, mauaji Mbagala
Akisimulia ujambazi uliofanyika katika Benki ya Access Tawi la Mbagala, Kamanda Sirro alisema majambazi hao walikuwa 12, wakiwa wamepakizana kwenye pikipiki sita na walifika kwenye benki hiyo saa 8:30 mchana.

Baada ya kufika, moja kwa moja waliingia kwenye chumba cha askari wanaolinda benki na kumpiga risasi kichwani askari mwenye namba H7739 Konstebo Harid na kufa papo hapo.

Mbali na mauaji hayo, Kamanda Sirro alisema walimshambulia askari mwingine, Konstebo Shaban miguuni na kupora silaha zao na kuingia nazo ndani ya benki, ambako walimshambulia mlinzi wa kampuni binafsi ya ulinzi na raia wengine wawili na kufa papo hapo, huku wengine watano wakijeruhiwa.

Baada ya hapo kwa mujibu wa Kamanda Sirro, majambazi hao walikimbilia chumba kinachohifadhi fedha nyingi (strong room) na kukipiga risasi katika jitihada ya kutaka kuingia ndani, lakini hawakuweza kuvunja.

Kutokana na ugumu wa kuvunja chumba hicho, Kamanda Sirro alisema haraka haraka wakahamia katika kaunta za watoa fedha na kupora fedha zilizokuwepo kati ya Sh milioni 20 mpaka Sh milioni 30 na kuondoka na silaha za polisi aina ya SMG mbili na ile yao moja pamoja na pikipiki zao.

Polisi waua watatu
Kamanda Sirro alisema taarifa zilisambazwa katika vikosi vya ulinzi, ambavyo vilijiimarisha.

Alitaja Kikosi cha Mbwa na Farasi eneo la Mkuranga, ambao walijiandaa na majambazi hao walipofika kijiji cha Chui wilayani Mkuranga mkoani Pwani, walipambana na polisi na askari wakafanikiwa kuua majambazi watatu.

Mbali na kuua watatu, silaha tatu zilikamatwa ambazo ndio zile SMG mbili za Polisi, walizochukua pamoja na ile yao moja, lakini wakakutwa pia na mabomu matatu ya kutupa kwa mkono yaliyotengenezwa Urusi.

“Hawa majambazi walikuwa wamejiandaa, kwa maana walikuwa na mabomu ya kutupwa kwa mkono matatu aina ya RGD 01 ambayo ni mbinu ya kujilinda wanaposhambulia,” alisema Kamanda Sirro.

Tisa watoroka
Pamoja na kujiimarisha kwa polisi, majambazi tisa walikimbia wakaacha pikipiki zote sita za aina tofauti, ambazo ni Haojue mbili zenye namba MC 560 AED na MC 207 BAN, San LG yenye namba MC 784 BDJ, Boxer yenye namba MC 248 AXE na King Lion mbili zenye namba MC 653 BDQ na MC 853 BDR.

Kamanda Siro alisema baada ya hapo, waliendelea kuwakimbiza majambazi hao hadi wakatokomea katika Msitu wa Kongowe, ambako juhudi za kuwatafuta zilianza mara moja.

“Nawahakikishia wananchi mtandao wote wa ujambazi kwenye mabenki na maeneo mengine, tutausafisha wote kwa maana hawa wanafanya uhalifu maeneo ya Dar es Salaam na Pwani na wana ndugu zao, tutawakamata wote,” alisisitiza Kamanda Sirro.

Alisema hawawezi kuona Watanzania wakiumia na kufa kwa tamaa za wachache, wenye kupenda utajiri wa haraka.

JWTZ kazini
Akizungumza kuhusu ujambazi huo, Waziri Kitwanga alisema Polisi inajipanga upya na atazungumza na Waziri mwenzake, Dk Mwinyi kuangalia jinsi ya majeshi hayo mawili, Jeshi la Polisi na Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), watakavyofanya kazi pamoja ya msako katika misitu yote inayozunguka mikoa ya Pwani, kuanzia Bagamoyo hadi Kisarawe.

Alionya kama kuna kambi za uhalifu ndani ya misitu hiyo, zitasambaratishwa na kuomba raia wema watoe taarifa za uhalifu.

“Tutafanya operesheni kubwa na tutaifanya haraka, tunaomba wananchi watoe ushirikiano hasa waendesha bodaboda kwa maana zinatumika sana kwenye matukio haya. Mtandao wa majambazi ufahamu kwamba vyombo vya usalama havijalala, tutawamaliza wote, tutatumia nguvu zetu zote kuwamaliza na tutafanikiwa,” alisisitiza Kitwanga.

Kuhusu waendesha bodaboda, Kitwanga alisema ukaguzi wa kina unafanywa na kuwataka waendesha bodaboda hao wanaposimamishwa, wakubali na kutoa ushirikiano na wasione kama wanabughudhiwa, bali ni kuwakagua kwa sababu wahalifu hutumia vyombo hivyo zaidi kufanya matukio mabaya.

Polisi feki
Katika tukio jingine, Kamanda Sirro alisema polisi feki wanne wamekamatwa na wanashikilia kwa mahojiano, ili kubaini mtandao huo ambao unatumia sare za Polisi, redio za upepo na pingu kufanya matukio ya uhalifu.

Alisema walipata taarifa kutoka kwa raia wema ya kuwepo kwa mtandao wa askari bandia, ambao hutumia sare za jeshi hilo kufanya matukio ya uhalifu, ndipo walipowakamata hao wanne.

Kwa mujibu wa Kamanda Sirro, polisi feki watatu walikamatwa Februari 24, asubuhi saa mbili eneo la Upanga karibu na Daraja la Selander.

Alisema watuhumiwa hao baada ya kuhojiwa, walikiri kufanya matukio ya ujambazi kwa kutumia silaha na kumtaja mtuhumiwa mwenzao mmoja anayeishi Kinyerezi.

Kamanda Siro alisema Polisi walimfuata mtuhumiwa huyo nyumbani kwake Kinyerezi na walipofanya upekuzi, walimkuta na sare halisi ya Polisi, redio ya upepo na pingu.

Kamanda Sirro alisema baada ya uchunguzi, imebainika kwamba watuhumiwa hao wamekuwa wakitumia sare na vifaa hivyo vya Polisi, kufanya matukio mbalimbali ya ujambazi kwa kujiaminisha kuwa wao ni askari Polisi.

Alisema watuhumiwa hao wamekiri kufanya matukio mbalimbali, ikiwemo kuweka vizuizi katika barabara za mikoani na kufanya uporaji.

“Watuhumiwa hao wote wanahojiwa ili waeleze jinsi walivyopata sare na vifaa hivyo ya Polisi, wamekiri kufanya uhalifu maeneo mbalimbali, lakini wakati mwingine tunashindwa kukamata wahalifu kwa sababu redio call wanayotumia zinaingiliana na zetu, hivyo wanakuwa wamepata taarifa,” alisema Kamanda Sirro.

Katika tukio lingine, Februari 18 mwaka huu, watuhumiwa watatu wa ujambazi, walikamatwa eneo la Kiwalani Kwa Mkude jijini Dar es Salaam wakiwa na bastola moja.

Polisi Zanzibar Kuwahoji Watu 34 Wanaotumia Lugha ya Matusi Katika Mitandao ya Kijamii

$
0
0

JESHI la Polisi Zanzibar limetoa tahadhari kwa watumiaji wa mitandao ya kijamii ambao wanaitumia kwa kuwatukana viongozi wa kitaifa, huku likiwa na orodha ya watu 34 ambao wanatarajiwa kuhojiwa zaidi kutokana na matumizi mabaya ya mitandao hiyo.

Kauli hiyo imetolewa juzi na Naibu Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai Zanzibar (DCI), Salum Msangi alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari katika Makao Makuu ya Polisi Zanzibar.

Alisema hivi sasa baadhi ya watu wanaitumia mitandao hiyo kinyume na maadili jambo ambalo linaweza kusababisha chuki na uhasama na kwamba ni kinyume na maadili ya wananchi wa Unguja na Pemba.

Msangi alisema jeshi hilo linakusudia kuwahoji watu 34 wanaotumia mitandao hiyo ya kijamii kwa kuhamasisha vurugu pamoja na kutoa lugha za matusi kwa viongozi wa Zanzibar, jambo ambalo ni kinyume na sheria pamoja na utamaduni wa wananchi wa Zanzibar.

Alisema mara baada ya kufutwa kwa uchaguzi Mkuu wa Zanzibar uliofanyika Oktoba 25, mwaka jana, kumejitokeza baadhi ya watu na vikundi mbalimbali vinavyotumia mitandao ya kijamii kwa kuandika maneno ya matusi au kutoa video za kuzungumza zenye lugha ya matusi kwa kuwatukana watu mbalimbali hasa viongozi wa kitaifa.

“Tayari orodha ya watu hao imeshapatikana na hadi sasa Polisi inamshikilia kwa mahojiano na uchunguzi mtu mmoja ambaye anatuhumiwa kutoa moja ya video hizo zenye lugha ya matusi dhidi ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk Ali Mohamed Shein,” alisema.

Aidha alisema kuwa uchunguzi wa kitaalamu na kisayansi unaendelea na ukishakamilika jalada litafikishwa kwa Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) kwa ajili ya kulisoma na kulifikisha kwenye hatua zinazofuata.

Msangi alitoa tahadhari kwa wale wote wanaojihusisha na vitendo hivyo kwani kutumia lugha za matusi ni kosa lililoainishwa kisheria kwenye sheria ya kanuni ya adhabu, yoyote atakayetenda kitendo hicho atakamatwa na kufikishwa mbele ya vyombo vya sheria, bila ya kujali limetolewa mahali gani au wakati gani.

Hata hivyo alisema kuwa wapo watu wanaodhani kuwa demokrasia ni uhuru wa kuwatukana viongozi, jambo ambalo sio sahihi na halikubaliki kisheria na kinyume na maadili ya wananchi wa Tanzania ambao wamejengwa na utamaduni wa kuheshimu watu.

Msangi ambaye pia ni Kamishna Msaidizi wa Polisi Zanzibar, alisema orodha ya watu wanaojiuhusisha na vitendo hivyo wanayo na wataendelea kukamatwa mmoja baada ya mwingine na kuchukuliwa hatua zinazofaa kwa mujibu wa sheria.

Hivi karibuni wakati wa maadhimisho ya Siku ya Sheria, Rais wa Zanzibar Dk Ali Mohamed Shein alikemea tabia iliyojitokeza sasa ya matumizi mabaya ya mitandao.

Rais Dkt John Pombe Magufuli Awasili Arusha Kuongoza Mkutano Wa 17 Wa Kawaida Wa Wakuu Wa Nchi Wa Jumuiya Ya Afrika Mashariki

$
0
0

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amewasili Mkoani Arusha ambako pamoja na mambo mengine ataongoza Mkutano wa 17 wa kawaida wa wakuu wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki utakaofanyika Jumatano tarehe 02 Machi, 2016 Mjini Arusha.

Katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) Rais Magufuli amelakiwa na viongozi mbalimbali wa vyama vya siasa na serikali pamoja na vikundi vya burudani za ngoma kabla ya kuelekea Arusha Mjini.

Rais Magufuli ndiye Mwenyekiti wa sasa wa Jumuiya ya Afrika Mashariki inayojumuisha nchi za Tanzania, Kenya, Uganda, Rwanda na Burundi.Kabla ya kuongoza kikao hicho Rais Magufuli anatarajiwa kukutana na kufanya mazungumzo ya ana kwa ana na viongozi wakuu wa nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Tarehe 03 Machi, 2016 Rais Magufuli na Rais wa Jamhuri ya Kenya, wataweka jiwe la msingi katika mradi wa ujenzi wa barabara ya Arusha - Holili - Taveta - Voi inayoziunganisha nchi za Tanzania na Kenya.

Barabara hiyo ni sehemu ya miradi ya maendeleo ya Jumuiya ya Afrika Mashariki inayotekelezwa na nchi wanachama wa Jumuiya hiyo.

Gerson Msigwa
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU.
Dar es Salaam
28 Februari 2016

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Akagua Bandari ya Mtwara na Kunusa Harufu ya Ufisadi katika Ujenzi wa Gati 3

$
0
0

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amekagua bandari ya Mtwara na kunusa harufu ya ufisadi katika utoaji wa zabuni ya ujenzi wa gati mpya tatu.
 
Waziri Mkuu ambaye alikagua eneo la ujenzi wa gati hizo jana (Jumamosi, Februari 27, 2016), alisema anazo taarifa juu ya utolewaji wa zabuni hiyo na mzabuni ameshashinda lakini kuna madai kwamba watu wa manunuzi kupitia PPRA ndiyo wanakwamisha zabuni hiyo.

Aliwaomba wabunge wa mkoa wa Mtwara washirikiane kusimamia suala hilo ili ujenzi wake uweze kuanza mara moja na kuleta ajira kwa wana Mtwara. "Ujenzi ukikamilika siyo tu ajira zitaongezeka bali hata meli nyingi zitaleta mizigo katika bandari hii na mapato ya mkoa yataongezeka", alisema.
 
"Natambua kwamba kuna mpango wa kujenga gati nne ambapo moja kati ya hizo itajengwa na TPA (Mamlaka ya Bandari) lakini hizi tatu zilitangazwa na kupata mzabuni ambaye ni kampuni ya Hyundai kutoka Japan. Lakini hii kampuni imekuwa ikizungushwa bila sababu. Tutafuatilia kubaini tatizo liko wapi," aliongeza. 
 
"Sasa hivi tuna uwezo wa kupaki meli moja tu, lakini gati zikikamilika tutaweza kuwa na meli tatu kwa mpigo, cha msingi tusimamie maamuzi yetu kwamba lazima wafanyabiashara wa korosho watumie bandari hii kusafirisha mizigo yao na si kuipeleka kwingine."

 "Kwenye Bodi ya Korosho nako kuna majipu yanahitaji kutumbuliwa. RCC ilishakaa na kupitisha uamuzi kuwa mizigo yote ipitie bandari ya Mtwara lakini kuna watu ndani ya Bosi hiyo wanatoa vibali vya kusafirisha mizigo kupitia bandari ya Dar es Salaam."

Alimtaka mkuu wa bandari ya Mtwara (Port Master) Bw. Prosper Kimaro awe makini na watu wa kitengo cha manunuzi katika bandari hiyo kwani kimekuwa chanzo cha upotevu wa fedha za Serikali kutokana na ujanja wa watu wachache. 
 
"Hapa si kuna mtu alitaka kuiba sh. milioni 300 kwa kufoji saini za wakubwa wake? alihoji Waziri Mkuu swali ambalo lilijibiwa na Bw. Kimaro kwamba ni kweli lakini uongozi uliingilia kati kabla wizi huo haujakamilishwa.

Kuhusu fidia kwa wakazi wa vijiji vya Kisiwa na Mgao ambao wamekubali kuhama ili kupisha upanuzi wa bandari hiyo, Waziri Mkuu aliwahakikishia wabunge hao pamoja na uongozi wa bandari kwamba kiasi cha sh. bilioni 13.8/- kimekwishatengwa na Wizara na kitatolewa mapema mwezi ujao.

Alitumia fursa hiyo kusisitiza udhibiti wa bandari bubu ambazo zinatumiwa kuingiza sukari na mchele mchezo ambao unaikosesha Serikali mapato. 

"Mkuu wa Mkoa, nilikwishatoa agizo kama hilo wakati nimeenda kukagua bandari ya Tanga. Kaa na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa nanyi pia muweke mbinu za kudhibiti upenyo huu wa kuingiza bidhaa za magendo kwa sababu hawa ndiyo wanaokwepa kulipa kodi ya Serikali," alisisitiza.

Mkuu wa bandari hiyo, Bw. Kimaro wakati akitoa taarifa ya utendaji wa bandari mbele ya Waziri Mkuu, alisema bandari hiyo ilianzishwa mwaka 1950 na imekuwa inakabiliwa na ufinyu wa gati ya kuegesha meli, vifaa vya kupakulia na kupakia mizigo na kwamba hivi sasa wamekwishapata winchi ya bandarini (harbour crane) yenye uwezo wa kubeba tani 100 na tayari wako kwenye mpango wa kujenga gati moja.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
JUMAPILI, FEBRUARI 28, 2016.

DC Paul Makonda Aagiza Walimu wa Shule za Serikali Dar es salaam Wapande Daladala Bure

$
0
0

Moja ya jambo ambalo serikali ya awamu ya tano chini ya uongozi makini wa Mheshimiwa John Pombe Magufuli imelifanya kuwa kipaumbele kikubwa kwenye mipango yake ya kimaendeleo ni suala la uboreshaji wa sekta ya elimu nchini na ndio maana serikali imeanza utekelezaji wa mpango huu kwa kufuta ada zote mashuleni.

Kimsingi ni ndoto hii ya Mheshimiwa Raisi ambayo nina hakika kila mmoja wetu anaelewa ukubwa wa faida zake kwenye ujenzi wa Tanzania mpya na yenye wasomi na wataalamu wa kila namna tena wanaopatikana bila kuzingatia hali ya kipato cha familia anayotokea mwanafunzi, iliyonifanya mimi kama msaidizi wake katika nafasi ya ukuu wa wilaya nijiulize kila wakati juu ya ushiriki wangu wa kuhakikisha inatimia kikamilifu. 

Maswali ambayo yamenifikisha kwenye wazo la kuboresha sekta hii kwa kuchagua kufanya jambo ambalo wakati serikali ikiendelea kupigania changamoto nyinginezo za kuboresha ajira za walimu ikiwemo upandishwaji wa madaraja na mishahara, basi na mimi katika nafasi yangu nishiriki kwenye mchakato huu mzima kwa kutoa motisha ya usafiri wa bure kwa walimu wote wanaofundisha kwenye shule za serikali zilizopo jijini Dar es Salaam.

Kwa ufupi ni kwamba, wazo hili limejengwa juu ya msingi wa sababu kubwa tatu. Moja, kwa kuzingatia changamoto za nauli za mara kwa mara wanazolazimika kuzilipa walimu ili kuyafikia kwa wakati maeneo yao ya kufanyia kazi na pili, ni kuhakikisha mimi na serikali yangu ya wilaya ya Kinondoni tunakuwa sehemu ya juhudi za Mheshimiwa Raisi za kuboresha maslahi na mazingira ya walimu ya kufanyia kazi ili matarajio ya ndoto yake anayoipigania usiku na mchana ya kutaka kuiona sekta ya elimu nchini ikikua kwa kasi yanatimia. 

Na tatu, ni kuwafanya walimu wa wilaya ya Kinondoni na Dar es Salaam kwa ujumla kama watumishi wenzangu wa serikali nao wanafaidi sehemu ya matunda ya serikali yao ambayo kwa dhati imedhamiria kubadilisha maisha yao ili na wao waweze kubadilisha maisha ya vijana wetu kupitia taaluma.

Kwasababu hizo nilizozianisha hapo juu ninaomba kuwatangazia walimu wangu wa shule zote za serikali kuanzia za msingi mpaka sekondari ya kwamba, sasa watasafiri bure wanapokwenda kutufundishia wadogo zetu na watoto wao. 

Hii ni baada ya kufanya vikao na mazungumzo ya kina na wamiliki wa vyombo vya usafiri wa umma kupitia vyama vyao vya Darcoboa na Uwadar na hatimaye mazungumzo hayo kuitimishwa na mkutano wa vyama vyote hivyo viwili vya wamiliki wa vyombo vya usafiri ambao kwa sauti moja wamekubali kuniunga mkono kwenye utekelezaji wa wazo langu hili.

Kipekee na kwa unyenyekevu mkubwa, naomba kuchukua fursa hii kuwashukuru sana wamiliki hawa wa vyombo vya usafiri wa umma pamoja na viongozi wa vyama vya Darcoboa na Uwadar kwani walikuwa na kila sababu ya kukataa hasa ukizingatia kuwa wao ni wafanyabiashara na tena wanazo changamoto nyingi katika sekta yao ya usafirishaji, wengine wakiwa hata wamekopa kwenye mabenki ili wapate uwezo wa kufanya biashara, lakini kwenye jambo hili wote kwa umoja wao wameseme ndio na wako tayari kuanza haraka iwezekanavyo.

Utaratibu kwa walimu juu ya utumiaji wa fursa ambayo tumeipata utakuwa kama ifuatavyo:- Moja, nimemuelekeza ofisa elimu wa sekondari na shule za msingi, kutoa maelekezo kwa wakuu wa shule zote za serikali zilizopo wilayani kwangu na wilaya nyinginezo za jiji la Dar es Salaam, kutengeneza vitambulisho vya shule zao vitakavyokuwa na picha ya mwalimu, jina lake kamili, jina la shule anayofundisha, namba ya simu ya mkuu wa shule husika pamoja na saini yangu mimi mwenyewe Paul Makonda ili kuepuka udanganyifu.

Nimewataka zoezi hili walifanye na kulikamilisha ndani ya wiki moja ambapo baada tu ya kukamilika itakuwa ni furaha yangu kuwatangazia walimu wote wa shule za serikali jijini Dar es Salaam kuwa, watakuwa wakipanda daladala bure ila tu kwa siku za jumatatu mpaka Ijumaa na kwa muda wa saa kumi na moja asubuhi mpaka saa mbili asubuhi na kati ya saa tisa mpaka saa kumi na mbili jioni. Ingawa, kila mwalimu atalazimika kuonyesha kitambulisho chake alichotengenezewa kwenye shule yake pamoja na kile cha ajira ya serikali.

Imetolewa na:-
Paul Makonda
Mkuu wa wilaya – Kinondoni.

Kurasa za Mbele na Nyuma za Magazeti ya Leo ya Uingereza - Februari 29

Kurasa Za Mbele Za Magazeti Ya KENYA Jumtatu i ya Leo Februari 29


Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya TANZANIA Jumtatu Ya Leo Februari 29

Mbowe Apinga Watumishi wa Umma Kutumbuliwa MAJIPU Bila Kupewa Nafasi ya Kusikilizwa Kwanza

$
0
0

Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe, amepingana  na  sera  ya  Rais John Magufuli  ya kuwatumbua majipu watumishi wa umma wazembe na wabadhilifu wa mali za umma.

Mbowe amedai kuwa Serikali Magufuli imekuwa ikiwatimua watumishi mbalimbali wa umma bila kuwapa nafasi ya kuwasikiliza kupitia kampeni ya kupambana na ufisadi, inayotambulishwa kwa kaulimbiu ya ‘utumbuaji majipu’.

Akizungumza jana katika ibada maalumu ya shukrani kwa kumaliza uchaguzi mkuu salama, iliyofanyika kwenye Usharika wa Nshara wa Dayosisi ya Kaskazini ya KKKT na kuhudhuriwa na Mkuu wa KKKT, Askofu Dk. Frederick Shoo, na maaskofu wastaafu Dk. Erasto Kweka na Dk. Martin Shao, Mbowe alisema (wapinzani) hawaridhishwi na hatua ya serikali ya Rais Magufuli kuendeleza timuatimua na kuwasimamisha kazi watumishi wa umma 160 tangu aingie madarakani bila kuwapa nafasi ya kuwasikiliza.

Mbowe ambaye pia ni Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, alisema wapinzani wako tayari kuipongeza serikali wakati wowote inapofanya mambo mazuri kwa manufaa ya taifa, lakini kwa sharti kwamba mara zote iwe inahakikisha sheria za nchi zinasimamiwa, mali na rasilimali za umma zinalindwa na kila kitu kinafanyika kwa kuzingatia taratibu zilizopo.

"Kutokana na hali ya sintofahamu kutamalaki katika taifa kwa sasa, hakuna mtumishi wa umma aliye na amani kutokana na mfumo unaoitwa kutumbua majipu. Tunasikia watumishi wa umma wakifukuzwa kazi bila kusikilizwa.

“Mpaka sasa kuna watumishi 160 wamefukuzwa na wengine kusimmishwa. Lakini pia zaidi ya taasisi na idara za serikali zipatazo 20 hazina uongozi…hii si sahihi,” alisema.

Katika ibada hiyo, Mbowe alikuwa ameongozana na wabunge 16 na makada wengine mbalimbali wa Chadema, alitoa sadaka ya Sh. milioni 279 kwa ajili ya kusaidia ukarabati na upanuzi wa jengo la Bethel lililoko Hai.

"Sisi tunamshukuru Mungu leo kwa kuwa tuko salama ndiyo maana tunatoa sadaka. Sadaka yetu tunaielekeza kwenye upanuzi na ukarabati wa jengo hili la Betheli la Usharika wa Nshara. Kwa hiyo, nawaomba sana viongozi wa dini na Watanzania kuliombea taifa kutokana na hali inayoendelea," alisema Mbowe.

Kiongozi huyo ambaye pia ni Mbunge wa Hai, alisema wabunge 42 wa Chadema wamemuunga mkono kwa kuchangia kanisa hilo Sh. milioni 131.5; mwanasiasa mkongwe na mfanyabiashara, Philemon Ndesamburo alimchangia Sh. milioni 50; marafiki zake wa Arusha Sh. milioni 49.9; Mwenyekiti mstaafu wa Chadema, Edwin Mtei Sh. milioni mbili; makada wengine wa Chadema Sh. milioni 15 na Kamati ya Maandalizi Sh. milioni 41.

Katika hatua nyingine, Mbowe alitumia nafasi hiyo pia kuzungumzia mgogoro wa uchaguzi wa kumpata Meya wa Jiji la Dar es Salaam kwa kuitupia lawama CCM kwa madai kuwa ndio wanaokwamisha kwa maslahi yao.

Alisema jambo hilo pia linasikitisha kwa sababu sasa ni miezi minne imepita huku haki ya wananchi wa Jiji la Dar es Salaam kuwa na Meya wao ikiendelea kuminywa kutokana na CCM kutoheshimu demokrasia na kutaka waendelee kuongoza licha ya wananchi kufanya uamuzi wao kupitia sanduku la kura katika uchaguzi mkuu uliofanyika Oktoba 25, mwaka jana.

Chadema na Chama cha Wananchi (CUF) vinavyoshirikiana kupitia Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), ndivyo vyenye idadi kubwa ya madiwani kulinganisha na CCM, hivyo kwa mujibu wa Mbowe, CCM wamebaini kuwa hawawezi kushinda na sasa wanajitahidi kadri wawezavyo kukwamisha uchaguzi huo.

Halmashauri Ya Jiji la Tanga Hatarini Kufutwa

$
0
0

Wakati sakata la kumpata Meya wa Jiji la Dar es Salaam likiendelea kupamba moto baada ya mchakato huo kuwekewa zuio la mahakama juzi, serikali imetishia kuivunja Halmashauri ya Jiji la Tanga iwapo haitamaliza mgogoro wake wa kisiasa.

Akizungumza na viongozi serikali na kisiasa jijini Tanga jana, Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan, alisema serikali italazimika kuivunja halmashauri hiyo endapo mgogoro huo hautamalizwa haraka, kutokana na ukweli kwamba tangu kuanza kwa uongozi wa awamu ya tano baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka jana imeshindwa kufanya vikao vyake halali kwa mujibu wa katiba kutokana na mgogoro wa kisisa bina ya Chama Chama cha Mapinduzi (CCM) na Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa, huku wananchi wakishindwa kutatuliwa kero zao kwa wakati hivyo kuzorotesha maendeleo yao.

“Mpaka sasa jiji la Tanga hakuna uongozi uliosimama, sasa hatuwezi kwenda kwa mwendo huu, wananchi wanahitaji maendeleo na kurudia uchaguzi hatuwezi ni gharama kubwa, kilichobaki ni kuivunja halmashauri mpaka hapo muda wa kufanya uchaguzi kwa mujibu wa katiba ya nchi utakapotimia, hivyo kwa maana nyingine kama itavunjwa serikali kuu ndiyo itasimamia shughuli za jiji hili,” alisema Suluhu.

Alisema mkoa huo una mipango mbalimbali ya maendeleo lakini haiwezi kutekelezeka kutokana na mgogoro uliopo na kuwataka viongozi wa mkoa kwa kushirikiana na wazee kukaa chini kutafuta namna ya kuumaliza haraka.

“Jiji ni kioo cha mkoa mzima, sasa kama wazee hawatakaa kitako na viongozi kutafuta suluhu, basi hii mipango yenu yote ya kufufua viwanda itakuwa ni ndoto tu kwa sababu hapa mjini hakupo shwari na tunalitambua hilo,” alisema.

Mgogoro wa umeya Tanga umeibuka baada ya CCM yenye madiwani wachache kushinda nafasi hiyo dhidi ya Ukawa yenye madiwani wengi jambo ambalo linapingwa na umoja huo unaondwa na vyama vya CUF, Chadema, NCCR-Mageuzi na NLD.

Hatua kama hiyo ya kuvunja halmashauri si mara ya kwanza kutokea nchini, kwani mwaka 1996, Halmashauri ya Jiji la Dar  es Salaam ilivunjwa na serikali na badala yake ikaundwa Tume ya Jiji iliyokuwa chini ya Charles Keenja.

Makamu wa Rais pia alisema mkoa wa Tanga unakabiliwa na changamoto kubwa ya biashara ya magendo, hali ambayo inarudisha nyuma mkoa huo kiuchumi na kimaendeleo.

Kufuatia hatua hiyo aliiagiza kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa huo kutumia kila mbinu kuzuia biashara hiyo ili mkoa uweze kuimarika kiuchumi na kimapato.

Kuhusiana na suala la chakula, Makamu wa Rais alisema serikali ya awamu ya tano haitamvumilia mkuu wa mmoa yeyote wala wilaya ambaye atatoa malalamiko ya kukosekana kwa chakula kwenye eneo lake na badala yake atakuwa amejifukuzisha kazi mwenyewe.

Alisema kukosekana kwa chakula wakati viongozi wa eneo husika wana uwezo wa kujenga malambo ili kukinga maji ya mvua kipindi cha masika na kuwaelekeza wananchi kulima mazao yanayostahimili ukame, itakuwa ni kipimo chao cha uongozi na wale ambao watashindwa kupata madawati kwa ajili ya shule kwenye maeneo yao.

Awali akisoma taarifa ya mkoa wa Tanga kwa Makamu wa Rais, Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mwantumu Mahiza, alisema hali ya chakula mkoani humo hadi kufikia mwezi huu si ya kuridhisha kutokana na kuchelewa kunyesha kwa mvua msimu wa mwaka 2014/2015 na hata ziliponyesha hazikuwa na mtawanyiko mzuri.

Kinara Uporaji Benki Mbagala Atiwa Mbaroni

$
0
0

Siku nne baada ya majambazi 12 kuvamia Benki ya Access tawi la Mbagala, jijini Dar es Salaam na kuiba Sh. milioni 20 na kusababisha vifo vya watu saba, mtu anayedaiwa kuwa kinara wa uhalifu huo ametiwa mbaroni baada ya kutajwa na washirika wake, akiwamo aliyekamatwa  akiwa anafunga ndoa.

Taarifa za uhakika  zinaeleza kuwa, kinara wa ujambazi huo alikamatiwa Sinza Mori, wilaya ya Kinondoni jana, saa 11:00 jioni.

Kwa mujibu wa taarifa hizo, kikosi kinachoshirikisha askari wa majeshi mbalimbali ikiwamo, polisi na la wananchi wa Tanzania, kilinasa watu wanne kwenye sherehe ya harusi baada ya kufuatilia mawasiliano yao ya simu.

“Unajua sasa hivi hili suala linahusisha jeshi ambao wamefuatilia kwenye mtandao na kunasa simu za watu wanne ambao wamekamatwa huko Mbagala, akiwamo bwana harusi na watu wengine wanne,” kilisema chanzo cha habari hii.

Taarifa hizo zinasema baada ya watu hao kukamatwa wakiwa wanafunga ndoa msikitini, walisaidia kutoa taarifa ambazo hatimaye zilifanikisha kukamatwa kwa mtu huyo anayedaiwa kuwa ni kinara wa ujambazi huo.

Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Simon Sirro, alipoulizwa kuhusu tarifa hizo alisema bado hajazipata na kwamba yawezekana wasaidizi wake wamemkamata lakini bado hawajamfikishia taarifa.

Kinara huyo amekamatwa ikiwa imepita siku moja baada ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga, kutangaza uwezekano wa kutumia Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) kushirikiana na polisi kuwasaka wahalifu wote waliojificha kwenye misitu ya Bagamoyo na Pwani, ambako inadaiwa walikimbilia baada ya tukio la Mbagala.

Pia waziri huyo alisema katika operesheni hiyo, watakuwa wakiwasimamisha mara kwa mara watumia pikipiki kwa sababu vyombo hivyo vimekuwa vikitumiwa na majambazi katika kufanikisha matukio yao.

Kikwete: Nitaachia Uenyekiti wa CCM, Lakini Sitaacha Vikao vya Ndani CCM

$
0
0

Moja kati ya hoja zinazogonga vichwa vya baadhi ya makada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) ni mabadiliko ya Uenyekiti wa Chama hicho ambayo yatamuwezesha mzee wa Kutumbua Majipu, Rais John Magufuli kuanzisha operesheni hiyo ndani ya chama hicho.

Mwenyekiti wa CCM, Jakaya Kikwete amesema kuwa ataachia nafasi hiyo hivi karibuni na kumkabidhi Rais Magufuli, lakini alitoa angalizo kuhusu uhusika wake kwenye chama hicho baada ya kujivua kofia hiyo nzito.

Ingawa Katiba ya Chama hicho inaeleza kuwa mwenyekiti mpya atapatikana mwaka 2017, Mwenyekiti wa Chamo hicho, Dk. Jakaya Kikwete amepanga kuachia nafasi hiyo mapema (mwaka huu) kama ilivyokuwa kwa watangulizi wake.

Akiongea jana kwenye uzinduzi wa Kitabu cha maisha ya kada maarufu wa chama hicho, Marehemu Captain John Komba, Dk. Kikwete alieleza kuwa ataachia nafasi hiyo lakini hataacha kushiriki vikao vya ndani na mambo ya maamuzi ya chama hicho.

“Uenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi nitaachia, lakini mambo ya ndani yanayohusu chama hiki sitaacha kushiriki,” alisema.

Februari mwaka huu, Dk. Kikwete aliwaambia wazee wa CCM mjini Singida kuwa sherehe za kumbukumbu ya kuzaliwa kwa chama hicho mwaka huu, zilikuwa sherehe zake za mwisho akiwa kama Mwenyekiti.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images