Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Uingereza ya Leo Alhamisi Ya February 25, 2016


Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya TANZANIA Alhamisi Ya Leo Februari 25

Kurasa Za Mbele Za Magazeti Ya KENYA Alhamisi ya Leo Februari 25

Steven Wasira Amkunja Shati Mwandishi Baada Ya Kesi Yake Kupinga Ushindi wa Ester Bulaya Kutupiliwa Mbali Na Mahakama

$
0
0

Mwanasiasa mkongwe nchini, Steven Wasira jana alimvamia mpigapicha wa gazeti la Mwananchi aliyekuwa akichukua picha zake wakati akitoka mahakamani, lakini akashindwa kutimiza azima yake ya kufuta picha.

Wasira, Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika wa Serikali ya Awamu ya Nne (SA4), alifanya kitendo hicho akitoka kwenye jengo la Mahakama ya Biashara ambako maombi yake ya kukata rufaa ya kupinga matokeo ya uchaguzi wa ubunge, jimbo la Bunda yalitupwa na Mahakama Kuu.

Katika kinyang’anyiro hicho cha ubunge, Wasira, ambaye amekuwa mbunge wa Mwibara tangu mwaka 1970 na baadaye mbunge wa Bunda hadi mwaka 2015, aliangushwa na Ester Bulaya wa Chadema katika uchaguzi wa Oktoba 25 mwaka jana. Waandishi kutoka vyombo mbalimbali vya habari akiwamo walishuhudia tukio hilo.

“Wasira alimkimbiza Jamson akitaka kumnyang’anya kamera, lakini hakuweza,” alisema Nyange,mwandishi  wa  gazeti  la  Mtanzania.

“Baadaye alitaka kumgonga kwa gari lake wakati akiondoka lakini ikashindikana.”

Akisimulia tukio hilo, Jamson alisema Wasira, ambaye amefanya kazi na serikali za awamu zote tangu katikati ya miaka ya 70, alichukizwa na kitendo chake cha kumpiga picha.

“Wasira alinifuata na kuniuliza sababu za kumfuatilia kila mara. Aliniuliza picha nazopiga nazipeleka wapi,” alisema Jamson.

“Njoo, njoo hapa wewe kijana. Nakuambia futa hizo picha kwa usalama wako.Hivi mnatafuta nini maana mnanifuatilia tangu nikiwa kule Mahakama Kuu hadi huku Mahakama ya biashara,” alisema Wasira

Jitihada za Wasira kumnasa Jamson ziliendelea hadi nje ya eneo la mahakama ambako alimfuata kwa kutumia gari aina ya Toyota Land Cruiser (namba tunazihifadhi).

Katika kumfuatilia, gari la Wasira nusura limgonge mpigapicha huyo, lakini waandishi wenzake walimnusuru kwa kumsukumia pembezoni mwa barabara.

Juhudi za kumpata Wasira kuzungumzia sababu za kutaka kumshambulia mpiga picha huyo kwa kuchukua picha za tukio hilo, hazikuzaa matunda.

Awali, Jaji Sirilius Matupa alitupilia mbali maombi ya ruhusa ya kukata rufaa dhidi ya uamuzi wa kufuta shauri la kupinga matokeo ya uchaguzi wa Bunda baada ya kubaini waliowasilisha maombi hayo, Magambo Masato na wenzake wanne, hawakufuata sheria.

Uamuzi huo ulisomwa na Naibu Msajili wa Mahakama Kuu, Eugenia Rujwahuka kwa niaba ya Jaji Matupa. 

Katika maombi yao ya msingi, Magambo Masato na wenzake waliiomba mahakama kutengua matokeo yaliyompa ushindi Bulaya wakidai licha ya Wasira kunyimwa haki kuhakiki na kuhesabu upya kura, mchakato wa uchaguzi huo pia uligubikwa na vitendo vya rushwa.

Akisoma maamuzi hayo kwa niaba ya Jaji Sirilius Matupa, Naibu Msajili wa Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza, Eugenia Rujwahuka alisema maombi hayo yamewasilishwa kwa kutumia kifungu cha sheria kisichohusika.

“Badala ya kuwasilisha maombi yao kwa kutumia kifungu cha 15 (c) cha Sheria ya Uchaguzi Sura namba 141, waleta maombi wametumia kifungu cha 15 (a) (b),” alisema Rujwahuka akimnukuu Jaji Matupa.

Wakati huohuo, shauri la kupinga matokeo ya uchaguzi wa jimbo la Nyamagana, iliyofunguliwa Ezekiah Wenje, imesikilizwa jana na kuahirishwa hadi Februari 29, mwaka huu.

Akiahirisha shauri hiyo iliyoahirishwa mara mbili mfululizo Jumatatu na Jumanne iliyopita, Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Sumbawanga, Kakusulo Sambo aliziagiza pande zinazohusika kuhakikisha zinakamilisha taratibu zote za kisheria ili shauri hilo lianze kusikilizwa mfululizo.

Wadaiwa 16 Waliotorosha Makontena Bandarini Kuanza Kufilisiwa Leo

$
0
0

Wadaiwa 16 waliokwepa kulipa kodi ya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), baada ya kutorosha kontena za mizigo yao kwenye Bandari Kavu (ICD) ya Azam mwishoni mwa mwaka jana, mali zao zinaanza kukamatwa leo na kufilisiwa.

Mkurugenzi wa Mtendaji wa Kampuni ya Udalali ya Yono, iliyopewa kazi ya kufuatilia wadaiwa hao wakiwemo baadhi ambao wamekamilisha malipo, Yono Kevella alisema hayo Dar es Salaam jana.

Kevela alisema kuanzia leo wanakaa na vyombo vya dola, kuanza utaratibu wa kukamata na kufilisi mali za wahusika na kuwafikisha kwenye vyombo vya sheria.

Kevela alisema hadi sasa hakuna zuio lililotolewa, linazowazuia kutekeleza wajibu wao katika kukusanya madeni hayo. Hata hivyo alisema, wengi wa wadaiwa baada ya kutolewa kwa muda huo wa siku 14, wameonesha moyo wa kulipa.

Wadaiwa 16 hawajamaliza madeni
Alitaja wadaiwa 16 ambao hawajalipa madeni yao wala kupunguza, ambao watafilisiwa wasipojitokeza kufanya malipo ni Said Ahmed Said Sh 28,249,352.50, Strauss International (45,393,769.95), Farid Abdallah Salum (52,185, 614.97).

Wengine ni Nasir Saleh Mazrui (60,105,873.77), Simbo Yona Kimaro (64,221,009.10), Ally Masoud Dama (102,586,719.22) na Juma Kassem Abdul (130,182,395.12), Salum Link Tyres (233,447,913.31) na Tybat Trading Co.Ltd (448,690,271.90).

Pia wamo IPS Roofing Co.Ltd (966,723,692.10), Tuff Tyres General Co Ltd, (7,435,254,537.03), Swalehe Mohamed Swalehe (34,687,165.00), Rushwheel Tyre General Co Ltd, (1,802,988,679.20), Said Ahmad Hamdan (68,362,558.31), Ahmed Saleh Tawred ( 59,237,578.40) na Farida Abdullah Salem Sh 75,334,871. 85.

Akizungumzia wadaiwa waliolipa ndani ya siku 14 walizopewa na zikaisha juzi, alisema wanane kati ya 24, ndiyo walijitokeza kulipa madeni baada ya kampuni yake kuwafuatilia.

Kevela alisema hadi jana zaidi ya Sh milioni 200 zimelipwa na wadaiwa hao.

Wadaiwa hao 24 walishindwa kulipa kodi kwa wakati kama walivyotakiwa kufanya, ndipo TRA ilimpa dalali huyo kazi ya kuwafilisi. Kampuni hiyo ya udalali ilitoa siku 14, kuanzia Februari 10, mwaka huu wawe wamekamilisha; muda ambao umeisha juzi.

Kevela alisema katika siku hizo 14, kati waliojitokeza kulipa,wanne kati yao wamemaliza madeni na wengine wanne wamepunguza madeni na kuahidi kumalizia kiasi kilichobaki. 

Waliomaliza madeni yao 
Wadaiwa waliolipa madeni yao yote ni Issa Ali Salim aliyekuwa akidaiwa Sh 94,543,161.96, Libas Fashion (26,593,245.78), Omary Hussein Badawy (21,346,615.40) na Zulea Abas Ali (16,760577.24).

Waliopunguza madeni yao
Waliopunguza madeni yao ni Zuleha Abbas Alli aliyelipa Sh milioni 47 na kubakiwa na deni la Sh 28,508,551, awali alikuwa akidaiwa Sh 75,508,551.88, mwingine ni Ally Awes Hamdani aliyelipa Sh milioni 17.26 awali alikuwa akidaiwa Sh 55,485,904.07).

Wengine waliopunguza kidogo ni Tifo Global Trading Co Ltd waliolipa Sh milioni mbili ilhali deni lao ni Sh 1,573,300,644.58, Lotai Steel Tanzania Ltd, waliolipa Sh milioni mbili ilhali deni lao ni Sh 5,476,475,738.19.

“Tulikabidhiwa wadaiwa 24 na TRA, waliokwepa kodi kwa kutorosha kontena katika bandari kavu ya Azam mwishoni mwa mwaka jana, sasa walipewa muda wa kulipa ila walikaidi, tukakabidhiwa tuwafilisi mali zao zote ili kulipia madeni na wamejitokeza hao na kuanza kulipa wengine wamemaliza”, alisema Kevela.

Awali wadaiwa 24, walikwepa kodi ya Sh bilioni 18.95 kwa kutorosha makontena 329 ya bidhaa zao kutoka Kampuni ya SSB ambayo ndiyo mmiliki wa bandari kavu ya (Azam ICD) na kampuni ya Regional Cargo Services.

Mapema Desemba mwaka jana aliyekuwa Kaimu Kamishna wa TRA, Dk Philip Mpango alizungumza na waandishi wa habari na kusema kampuni 15 kati ya 43, zilizokwepa kodi baada ya kutorosha kontena 329 katika ICD ya Azam, wamelipa.

Dk Mpango alisema Desemba 12, mwaka jana ndiyo ilikuwa siku ya mwisho aliyotoa Rais John Magufuli ya siku saba kwa wakwepa kodi hao 43, kulipa wenyewe kwa hiari, vinginevyo sheria zitachukua mkondo wake. Kufuatia kauli hiyo ya Rais Magufuli, wadaiwa 15 walijitokeza na kulipa na waliobaki hawakujitokeza kulipa.

Serikali Yasema Bajeti Ijayo Itatekelezwa Kwa Fedha Za Ndani

$
0
0

SERIKALI imesema bajeti ya mwaka ujao, hususani utekelezaji wa miradi yote ya maendeleo, itatekelezwa kwa fedha za ndani.

Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango alisema miradi mikubwa kama vile ujenzi wa reli ya kisasa ya kati na miradi mingine mikubwa, ndiyo itajengwa kwa fedha za msaada kutoka nje kwa kuwa nchi haiwezi kukwepa kuomba msaada kutoka nje.

Alisema hayo jana katika mji mdogo wa Holili mpakani mwa Tanzania na Kenya, baada ya kuangalia shughuli za utendaji kazi katika mpaka huo na baadaye kuzungumza na wafanyakazi wa Mamlaka ya Mapato (TRA) katika mji huo.

Alisema makusanyo ya sasa ya Sh trilioni 1.7 kwa mwezi yanayokusanywa kwa sasa nchi nzima, fedha zake zitaelekezwa kwa shughuli za maendeleo kwa mikoa yote nchini. 

Waziri huyo alisema si kweli kwamba serikali ya Rais John Magufuli haitahitaji msaada wa fedha kutoka nje. “…la hasha! ila msaada huo hautakuwa mkubwa kama zamani,” alisema waziri.

Akizungumzia bajeti ijayo, alisema fedha zake nyingi zitatokana na makusanyo ya fedha za ndani na sio za msaada kutoka nje.

Waziri huyo alisema kwa asilimia kubwa bajeti ya miradi ya maendeleo katika mikoa yote nchini, fedha zake zitakuwa ni za ndani zilizokusanywa na kiasi kidogo cha fedha kitatoka nje.

Aliwataka watumishi wote wa umma, wanaokusanya mapato katika maduhuli ya serikali, kuacha mara moja kushika na kukusanya fedha kizamani kwa kutumia stakabadhi na kuandika kwa mkono ili kuepuka ushawishi wa kutumia fedha hizo kwa njia isiyokuwa halali.

Alisema anasikitishwa na utaratibu wa ofisa uhamiaji wa kitengo viza cha mji wa Holili, kukaa na fedha zaidi ya siku tano na kutoa stakabadhi kwa mkono.

Waziri alikemea na kumtaka ofisa wa uhamiaji wa mji wa Holili, kuacha mara moja kukaa na fedha za serikali kwa zaidi ya wiki, tofauti na mtunza fedha wa TRA anayepeleka fedha benki kila siku.

Alisema utaratibu huo ulishapigwa marufuku miaka mitatu iliyopita, lakini anasikitika unaendelea katika mji wa Holili. Alimwagiza Mkuu wa Uhamiaji Mkoa wa Kilimanjaro, kubadilisha hali hiyo kwa maslahi ya serikali.

Akizungumzia uadilifu, Waziri Mpango aliwataka wafanyakazi wa TRA, kuacha kufanya kazi hiyo kwa kuwanyanyasa wafanyabiashara, kwani kufanya hivyo ni kosa kisheria. Alisema uadilifu si wa mali tu, bali uko pia katika kutenda kazi za kila siku.

Alisema pia wananchi wanapaswa kulipa kodi kwa kufurahia na kuona kodi wanayolipa inawanufaisha, ikiwa ni pamoja na kufanya maendeleo katika miradi mbalimbali.

Gesi Nyingine Yagundulika Bonde la Mto Ruvu....Ina Ukubwa wa Ujazo wa Futi Trilioni 2.17

$
0
0
Tanzania  imedhihirisha kuwa ni tajiri mkubwa wa rasilimali ya gesi asilia baada ya kugundulika kwa gesi nyingine katika bonde la mto Ruvu yenye ukubwa wa ujazo wa futi trilioni 2.17.

Ugunduzi huo wa gesi asilia umefanywa na Kampuni ya Dodsal Hydrocarbons and Power Tanzania Limited ambayo imekuwa inafanya shughuli za utafutaji wa gesi na mafuta katika Mkoa wa Pwani.

Mtendaji Mkuu wa kampuni hiyo, Pilavullathil Surendran alisema jana katika mkutano wa wawekezaji wa gesi na mafuta ulioandaliwa na Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo kuwa, thamani ya gesi iliyoko katika eneo hilo inafikia Dola za Marekani bilioni sita sawa na Sh trilioni 12.

Ugunduzi huo mpya unafanya hadi sasa Tanzania kuwa na amana ya gesi yenye ukubwa wa futi za ujazo trilioni 57.27.

Kwa upande wake, Profesa Muhongo alithibitisha kugundulika kwa gesi hiyo tangu Julai mwaka jana, lakini akaeleza kuwa Serikali imechelewa kutangaza ugunduzi huo kama inavyoagizwa na Sheria ya Mafuta ya Mwaka 2015 kutokana na shughuli za uchaguzi.

“Sheria mpya inatutaka kabla ya waziri mwenye dhamana ya gesi kutangaza ugunduzi mpya wa gesi na mafuta ni lazima athibitishiwe na mamlaka ya udhibiti wa bidhaa za Petroli na Gesi (PURA). 

“Wizara yangu itawasiliana na mwanasheria mkuu wa serikali ili kupata ushauri wa kisheria kuhusu jambo hilo na bahati nzuri tayari PURA imeshaanza kushughulikia jambo hilo na naamini kuwa nitatangaza ugunduzi huo mpya hivi karibuni,” alifafanua Profesa Muhongo.

Licha ya ugunduzi huo mpya tayari gesi imegundulika katika maeneo ya kisiwa cha Songo Songo mkoani Lindi na eneo la Mnazi Bay huko Mtwara na katika Wilaya ya Mkuranga, Pwani pia kumegundulika kiasi kikubwa cha gesi.

Wasanii Waidai Mamilioni Ya Pesa IKULU....Deni hilo Liliachwa na Rais Mstaafu Jakaya Kikwete

$
0
0

Ikulu imeahidi kufanyia kazi madai ya Chama cha Wasanii Wachoraji Tanzania (Chawata), ambayo waliyawasilisha jana, kikilalamikia ofisi hiyo katika awamu ya nne iliyokuwa chini ya Rais Jakaya Kikwete, kuwacheleweshea malipo yao ya Sh. milioni 53.6.

Kwa mujibu wa taarifa ya Chawata kwa vyombo vya habari jana, fedha hizo zimetokana na kazi za sanaa ambazo zilichukuliwa na serikali ya awamu ya nne kutoka kwa wafanyabiashara wa eneo la Mwenge jijini Dar es Salaam na kupelekwa Ikulu.

Hata hivyo, Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu, Gerson Msigwa, alithibitisha kuwapo na madai hayo na kusema kuwa yatafanyiwa kazi ndani ya wiki moja kuanzia jana.

“Ni kweli Ikulu inadaiwa, lakini ni deni la awamu ya nne, kwa hiyo tumewaomba kuwakamilishia madai yao ndani ya wiki moja, baada ya kufanya uhakiki ili kujiridhisha,” alisema Msigwa.

Awali, Katibu wa Chawata, Cuthbert Semgoja alisema waliahidiwa kulipwa fedha hizo kabla ya uchaguzi mkuu mwaka jana lakini hadi sasa hawajalipwa.

"Tuliuza kazi zetu Ikulu kwa makubaliano ya kulipwa baadaye tangu Agosti mwaka jana, hadi leo hii (jana) bado hatujaweza kupatiwa pesa zetu," alisema na kuongeza:

“Mchakato wa kazi zetu ulianza mwishoni mwa mwezi wa nane kwa kamati husika, kupitia katika maeneo ya wasanii, ili kuweza kufanya chaguzi ya sanaa wanazohitaji. Walijiridhisha kwa kuchukua baadhi ya sanaa kutoka kwa wanakikundi kwa ahadi ya kufanya malipo mara moja kabla ya uchaguzi mkuu lakini hadi sasa bado malipo hayo,” alisema Semgoja.

Alisema baada ya chama kuona muda wa malipo unakwisha, walichukua jukumu la kupiga simu kwa mhusika ambaye walikuwa wakifanya naye biashara hiyo kwa niaba ya Ikulu, lakini jibu lake lilikuwa `malipo yenu yanaandaliwa.'

“Baada ya mwezi mmoja kufanya biashara hiyo, tulianza kumpigia simu mtu mmoja ambaye ndiye alikuwa anahusika na sisi tangu mwanzo wa biashara yetu hadi mwisho, lakini majibu tunayopewa ni kusubiri tu, tumechoka sasa,” alisema.

Alisema mawasiliano waliyokuwa wanafanya na mtu kutoka Ikulu ambaye alijitambulisha (jina tunalo), ndiye aliyekuwa akiwapa majibu hayo kuhusu madai yao.

Aliongeza kuwa kulingana na ahadi waliyopewa kulipwa kabla ya uchaguzi mkuu na mlolongo wa ahadi zinazojirudia, walianza kufanya mawasiliano wao kwa wao ili  kufahamu nini kinachoendelea kuhusu malipo yao na kugundua kuwa kuna tatizo.

“Ilifika hatua simu zetu hazipokelewi, kila tunapopiga mhusika hapokei simu zetu, ndipo hapo tulipohisi kuna mchezo unaendelea kati ya mtu huyo na chama chetu,” alisema.

Waziri Mkuu Asubiriwa Kwa Mabango Kiteto

$
0
0

Wananchi  wilayani Kiteto  mkoani  Manyara  wamejiandaa  kumpokea  kwa  mabango  Waziri  Mkuu  Kassim  Majaliwa  ili  kutoa  ujumbe  wa  kuwakataa  baadhi  ya  viongozi  wa wilaya  kutokana  na   kukithiri  kwa  migogoro  ya  ardhi.

Miongoni  mwa  viongozi  wanaotajwa kuwamo  katika  ujumbe  huo  ni  Mkuu  wa  Wilaya Kanali Samweli Nzoka, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri, Bosco Ndunguru,Katibu Tawala (DAS) Nicodemus John pamoja  na  kamanda  wa  Polisi  wa  Wilaya (OCD) George Katabazi.

Hata  hivyo DC Nzoka  amepiga  marufuku  mwananchi  yeyote  kuandaa  bango  lolote  katika  ziara  hiyo  ya  Waziri  Mkuu  inayotarajiwa  kufanyika  Februari  29  mwaka  huu.

Akizungumza katika kikao  cha  baraza la  Madiwani  jana,Nzoka  alisema  hataruhusu  kuandaliwa  wala kuonyeshwa  mabango  hayo  kwani  ni  ishara  ya  vurugu  na  uvunjifu  wa  amani.

Mkuu  huyo  wa  Wilaya  alisema  anazo  taarifa  za kuwapo  watu  walioandaliwa  kutoka  wilaya  na  mikoa  ya  jirani  kwenda  Kiteto  kuzomea baadhi  ya  viongozi  wa  Wilaya katika  ziara  hiyo.

Katika  ziara  hiyo, Majaliwa  atakutana  na  kuzungumza  na  viongozi  mbalimbali  wakiwemo  madiwani, wakuu  wa  idara  na  viongozi  wa  mila  wa  jamii  ya  wafugaji

Waziri  mkuu  anategemewa  kutoa suluhisho  la mgogoro  wa  ardhi  kati  ya  wakulima  na  wafugaji  uliodumu  kwa  muda mrefu  na kusababisha  mauaji

Donald Trump Azidi Kupeta Mchujo wa Kugombea Kiti Cha Urais Marekani

$
0
0

Mgombea  urais wa Chama cha Republican, Donald Trump ameshinda katika Jimbo la Nevada nchini Marekani, na kuzidi kuimarisha uongozi wake katika mchujo wa kuwania tiketi ya chama hicho.

Tajiri huyo aliyewahi  kutamka  hadharani  kuwa atawafunga  jela  Rais  Mugabe  na Mseveni, sasa ameshinda mara tatu, kufuatia ushindi wake katika Jimbo la New Hampshire na Carolina Kusini.

Seneta Marco Rubio na Ted Cruz ambao wamekuwa wakishambuliana wiki hii wanapigania nafasi ya pili.

Maofisa wa chama hicho wamesema wanachunguza  ripoti za watu kupiga kura mara mbili huku eneo moja likidaiwa kuwa na vifaa vichache vya kupigia kura.

Baadhi ya wapiga kura  pia walidaiwa kuvaa nguo zenye picha za Trump, lakini maofisa wamesema kuwa hatua hiyo siyo kinyume na sheria

Naibu Spika Dk. Tulia Ackson Anusurika Kifo Baada Ya Kupata Ajali

$
0
0

NAIBU Spika Dk. Tulia Mwansasu, amepata ajali mkoani Mbeya alikokwenda kwa ajili ya mapumziko. Kwa mujibu wa Mkuu wa Wilaya ya Rungwe, Zainab Mbussi, Dk. Tulia alipata ajali hiyo jana wakati akitokea Mbeya mjini akielekea Kyela.

Mkuu wa wilaya alisema ajali hiyo ilitokea katika eneo la Shule ya Sekondari ya Kipoke iliyoko wilayani humo. 

Alisema maelezo ya askari wa usalama barabarani, yanaeleza kuwa chanzo cha ajali hiyo ni gari dogo lililoelezwa kuwa liliibeba familia ya mtu aliyetajwa kwa jina moja la Chacha, lililokuwa likitokea Kyela kwenda Mbeya, lilipojaribu kulipita lori na kukutana na gari la Naibu Spika.

Zainab alisema Dk. Tulia, mdogo wake pamoja na mlinzi wake waliokuwa kwenye gari lake wako salama ingawa gari hilo limeharibika vibaya sehemu za mbele.

Aidha, alisema baadhi ya abiria waliokuwa kwenye gari la Chacha wakiwemo wanawe wawili walipata majeraha na walipelekwa katika hospitali ya Mission Igogo, Kiwira.

Awali mapema jana, Dk. Tulia, alitoa msaada wa sh. milioni tano, ili kulifanyia ukarabati bweni  la Mapinduzi, ambalo alikuwa analala wakati anasoma Shule ya Sekondari ya Wasichana Loleza, iliyopo jijini Mbeya.

 Dk. Tulia ambaye alisoma shuleni hapo kuanzia kidato cha kwanza hadi cha nne, mwaka 1991 hadi 1994, pia alitoa msaada wa magunia mawili ya mchele kwa ajili ya chakula kwa wanafunzi.

Akizungumza na walimu na wanafunzi, Dk.Tulia alisema ametajiwa changamoto nyingi, zinazoikabili shule hiyo na kuwa amzichukua na kuahidi kutafuta wadau atakaoshirikiana nao ili waweze kusaidia kuzitatua.

Dk. Tulia alisema ameguswa na uchakavu wa mabweni, ambapo alipata fursa ya kuonyeshwa yakiwemo mawili aliyokuwa analala akiwa shuleni hapo, ambayo ni Kibo linaloendelea kutumika hadi sasa na lile la Mapinduzi ambalo kwa sasa halitumiki.

“Kwenye bweni nililokuwa nikikaa nimepita mwenyewe. Naahidi kushughulika na lile bweni la Mapinduzi ndilo lililo kwenye hali mbaya zaidi kiasi cha kushindwa kuendelea kutumika,” alisema Dk.Tulia.

Dk.Tulia alitoa magunia mawili ya mchele, kwa ajili ya chakula kwa wanafunzi shuleni hapo na aliwachekesha wanafunzi pale aliposema katika mambo ambayo hayajabadirika shuleni hapo ni ratiba ya kula wali mara mbili kwa wiki.

“Kwa sababu mimi dada yao nimewatembelea leo, na waswahili wanao msemo ‘mgeni njoo mwenyeji apone’, basi mimi nitawaletea magunia mawili ya mchele ili angalau kwa hizi wiki wanafunzi wawe wananikumbuka,” alisema Dk.Tulia.

Naye, mbunge wa Songwe, Philip Mulugo, alimuunga mkono Dk.Tulia kwa kuchangia sh. milioni moja, kwa ajili ya kusaidia ukarabati wa bweni hilo la Mapinduzi. 

Viongozi mbalimbali wa Chama na serikali, wakiongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Mbeya, Munasa Nyerembe, walikuwepo katika ziara hiyo na Naibu Spika kutembelea shule hiyo ambayo hivi sasa inachukua wanafunzi wa kidato cha tano na sita tu.

Taarifa Kwa Umma Toka TCU Kuhusu Mgogoro wa Chuo Cha St. Joseph (SJUIT) Kampasa ya Arusha

$
0
0

 TAARIFA KWA UMMA
MGOGORO WA CHUO KIKUU CHA MT. YOSEFU TANZANIA(SJUIT) KAMPASI YA ARUSHA

1.  Tunapenda  kuuarifu  umma  kwamba,  Chuo  Kikuu  cha  Mt.  Yosefu  Tanzania (SJUIT) Kampasi ya Arusha ni mojawapo ya vyuo vikuu vilivyosajiliwa na Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU) ambacho kilianza kudahili wanafunzi kwa mara ya kwanza mwaka wa masomo 2013/2014.

2.  Kwa mujibu wa kifungu cha 5(1) cha Sheria ya Vyuo Vikuu, Sura ya 346 ya Sheria za Tanzania, Tume ina mamlaka ya kusimamia na kudhibiti ubora na usimamizi wa uendeshaji wa Vyuo Vikuu hapa nchini.

3. Tume  inatambua  kuwa  kwa  nyakati  tofauti  kumekuwapo  na  matukio  ya migogoro baina ya uongozi wa Chuo  Arusha na wanafunzi.

Tume imekuwa ikifuatilia kwa karibu chimbuko la migogoro hiyo na kuchukua hatua stahiki ikiwa ni pamoja na kutoa maelekezo kwa uongozi wa chuo kurekebisha kasoro zinazosababisha migogoro chuoni hapo. 

Katika kutekeleza azma hiyo, hivi karibuni Tume iliunda jopo la wataalam kufanya ukaguzi wa kina katika Chuo Kikuu cha Mt. Yosefu Tanzania Kampasi ya Arusha. Ripoti ya ukaguzi huo iliwasilishwa tarehe 22/02/2016.

4.  Kwa kuzingatia utaratibu uliowekwa kisheria, ripoti hii inatakiwa kuwasilishwa na kujadiliwa na Kamati ya Ithibati ya Tume ya Vyuo Vikuu, ambayo itatoa mapendekezo kwa Tume kuhusu hatua stahiki za maamuzi. Kamati hii itakutana katika kikao cha dharura tarehe 25/02/2016 saa 3:00 asubuhi, na taarifa ya Kamati  hiyo  itawasilishwa  kwenye  Mkutano  wa  dharura  wa  Tume  tarehe hiyohiyo saa 9:00 alasiri.

5. Kwa mantiki hiyo, taarifa rasmi kuhusu maamuzi yaliyofikiwa juu ya hatma ya Kampasi hiyo ya Arusha ya Chuo cha Mt. Yosefu itatolewa siku ya Ijumaa tarehe 26/02/2016.

6.  Kwa taarifa hii, Tume inawaomba wanafunzi wote wa Chuo cha Mt. Yosefu Kampasi ya Arusha kuwa watulivu wakati huu ambapo suala lao linashughulikiwa.

7. Tume inapenda kutumia fursa hii pia kuwaarifu wanafunzi wote wa vilivyokuwa Vyuo Vikuu Vishiriki vya Sayansi za Kilimo na Teknolojia (SJUCAST) na Teknolojia ya Habari (SJUCIT), kuwa orodha ya majina yao na vyuo walivyopangiwa inapatikana  katika   tovuti  ya  Tume  ya   Vyuo   Vikuu.  Hivyo  wanashauriwa kuondoka Chuoni  mara moja na kujiandaa kwa ajili ya kuripoti katika vyuo walivyopangiwa katika muhula wa pili.

Imetolewa na


PROF. YUNUS D. MGAYA

Katibu Mtendaji

Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania

24 Februari2016

Taasisi ya TWAWEZA Yatangaza Matokeo Ya Utafiti Kuhusu Maoni ya Wananchi Juu ya Mabadiliko Kwenye Sekta Ya Elimu

$
0
0
1. Utangulizi
Mnamo mwezi Februari mwaka 2015, serikali ya Tanzania ilizindua sera mpya ya Elimu na Mafunzo. 

Sera hii imepanua wigo wa elimu ya msingi kwa kuiunganisha na elimu ya sekondari (hii ilikuwa ikitolewa bure na kwa lazima tangu mwaka 2001 baada ya kuanzishwa kwa Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi {MMEM}).

Tangu kuchaguliwa kwa Rais John Pombe Magufuli mwezi Octoba mwaka 2015, utekelezaji kikamilifu wa sera hii imekuwa moja ya ahadi kuu za serikali yake. 

Rais Magufuli aliwahakikishia wazazi wenye watoto wanaosoma katika shule za msingi na sekondari katika hotuba yake ya ufunguzi wa bunge la kumi na moja kuwa hawatapaswa kutoa michango yoyote kuanzia mwezi Januari mwaka 2016. 

Rais Magufuli pia alibainisha kuwa fedha zote zitakuwa zikipelekwa moja kwa moja shuleni, na kuongeza kuwa “Nina uhakika fedha hizo zitatumika vizuri, ole wao watakao zitumia vibaya.”

Japokuwa dhamira hii ya kutoa elimu bure mpaka kiwango cha sekondari (kidato cha nne) kwa kila mtoto wa Kitanzania ni hatua kubwa katika historia ya nchi, lakini upatikanaji fursa za elimu siyo changamoto pekee inayoukabili mfumo wa elimu nchini Tanzania. Juhudi zote zitakuwa hazina maana kwa wananchi na taifa kwa ujumla iwapo watoto wanaenda shule lakini hawajifunzi.

Hivyo basi ubora wa elimu inayotolewa ni suala muhimu pia. Ripoti ya Uwezo ya mwaka 2014 inaonesha kuwa asilimia 19 pekee ya wanafunzi wa darasa la 3 ndiyo walioweza kusoma hadithi ya Kiingereza ya kiwango cha darasa la pili 4 .

Tukiangalia ufaulu wa darasa la 7 mwaka 2015, takribani asilimia 68 ya wanafunzi waliofanya mitihani walifaulu 5 . Japokuwa hii ni ongezeko la ufaulu kwa karibu asilimia 11, bado ni idadi kubwa ya wanafunzi wasiofaulu ipasavyo.

Kutokana na umuhimu wa elimu katika maendeleo, na ukizingatia mabadiliko katika sekta ya elimu yanayoendelea nchini hivi sasa, ni vyema kufahamu mitazamo ya wananchi kuhusu mfumo wa elimu ya umma.

Wananchi wana mtazamo gani juu ya hali ya elimu iliyopo hivi sasa? Wana maoni gani juu ya walimu wa shule za umma na ubora wa elimu wanayopatiwa watoto wao? Je wana matarajio yapi kuwa elimu ya bure itaboresha elimu?

Je wazazi wamekuwa wakichangia fedha kiasi gani huko mashuleni, na nini athari za kupigwa marufuku kwa michango yote ya wazazi katika elimu? Na je fedha hizo zimetumikaje?

Muhtasari huu umebeba maoni na uzoefu wa wananchi juu ya utolewaji wa elimu ya msingi ya umma. Tunatumaini matokeo haya yatakuwa mwanzo mzuri wa kupima mafanikio ya utekelezaji wa sera hii mpya kwa siku za usoni.

Takwimu kutoka muhtasari huu zimekusanywa na Twaweza kupitia mpango wake wa Sauti za Wananchi. Sauti za Wananchi ni utafiti unaofanywa kwa njia ya simu za mkononi, wenye uwakilishi wa kitaifa. Utafiti huu unawakilisha Tanzania Bara.

Mambo muhimu kuhusu matokeo haya:

• Asilimia 76 ya wananchi wanaamini kuwa utoaji wa elimu bure utaboresha elimu.
• Asilimia 89 ya wazazi wanasema wanatoa michango ya fedha kugharamia elimu ya watoto wao waliopo shule za umma.
• Asilimia 66 ya michango ya wazazi hulipia ulinzi, asilimia 57 majaribio na asilimia 34 madawati.
• Karibu nusu ya wananchi wanaamini michango inayokusanywa shuleni haitumiki kwenye malengo husika.
• Wananchi 8 kati ya 10 wanaamini kuwa walimu hawapendi taaluma yao.
• Nusu ya wananchi wote wanaona kuwa ubora wa elimu ya msingi umezorota ama kubaki pale pale wakati nusu nyingine wanaona kuwa imeboreshwa. Hii ni ndani ya miaka 10 iliyopita.

2. Mambo sita kuhusu elimu nchini Tanzania

Jambo la 1: Wananchi wana matumaini na ahadi ya elimu bure
Asilimia 97 ya wananchi wanafahamu kuhusu ahadi ya Rais Magufuli ya kutoa elimu bure ya sekondari (kidato nne) kuanzia Januari 2016, kama ilivyoainishwa kwenye sera mpya na ilani ya chama tawala. Vilevile, asilimia 88 wana imani kuwa ahadi hii itatekelezwa kama ilivyopangwa.
Asilimia 76 ya wananchi wanaamini kuwa utolewaji wa elimu bure utaongeza ubora wa elimu kwa kuboresha mazingira ya kufundishia (asilimia 55).

Pamoja na imani hiyo, asilimia 15 ya wananchi walisema elimu ya bure haitaboresha elimu, kwa kuwa kuongezeka kwa uandikishwaji wa wanafunzi kutatumia rasilimali (fedha) nyingi 8.

Asilimia 49 walisema wanafunzi hawatafanya vizuri kutokana na kukatazwa kwa masomo ya ziada ambayo walimu waliyatumia kuwasaidia wanafunzi wasiofanya vizuri huku wakijipatia kipato cha ziada. Pamoja na hayo asilimia 22 wana hofu na upatikanaji wa vifaa vya kutosha vya kufundishia 9 .

Jambo la 2: Asilimia 89 ya wazazi huchangia elimu ya umma
Michango imekuwa ni sehemu ya mfumo wa elimu baada ya upanuzi wa Elimu ya Msingi kwa Wote. Asilimia 89 ya wazazi waliohojiwa walikiri kuchangia fedha kwenye shule za umma.

Wazazi walipoulizwa kuhusu kiwango cha fedha walichochangia, asilimia 80 walisema wamechangia TZS 50,000 ama pungufu kwa mwaka, huku asilimia 8 wakichangia zaidi ya TZS 100,000 .
Michango inayotolewa kwenye shule za umma hutumika kugharamia ulinzi (asilimia 66), majaribio (asilimia 57) na madawati (asilimia 34). Kiwango kidogo hutumika kwenye mahafali (asilimia 4) na safari za kishule (asilimia 4).

Utaratibu wa ugawaji wa fedha za ruzuku ni: asilimia 40 vitabu na nyenzo nyingine za kusomea; asilimia 20 kwa ajili ya vifaa vya kuandikia (kalamu, madaftari, penseli n.k.); asilimia 10 kwa shughuli za kiutawala na asilimia 10 kwa ajili ya makaratasi ya mitihani na uchapishaji. Hivyo basi, maamuzi ya kuwa ruzuku itumike vipi yanakuwa changamoto kwa upande wa shule zenyewe, na hata hivyo, inaonekana wazi kuwa michango hulipia vitu vingi zaidi kuliko ruzuku.


Jambo la 3: Asilimia 49 ya wazazi wanaamini michango ya wazazi haitumiki ipasavyo
Japokuwa wazazi wengi wamekuwa wakitoa michango ya ziada, asilimia 49 ya wazazi wanaamini kuwa fedha hizo hazitumiki ipasavyo. Wazazi wa mjini wana mashaka zaidi ambapo asilimia 57 wanasema hivyo ukilinganisha na asilimia 44 ya wazazi wa vijijini.

Vilevile asilimia 58 ya wananchi wanaamini kuwa michango hii haijaidhinishwa na serikali. Asilimia 89 wanaamini kuwa walimu wa shule za umma huchangisha fedha hizo kama chanzo cha kujipatia kipato cha ziada 11 .

Jambo la 4: Wananchi wanahusisha mafanikio ya ujifunzaji na juhudi za mwalimu
Wananchi walipoulizwa kuwa ni nini ambacho wanadhani kinachangia matokeo ya darasa la saba kwenye jamii yao (kuwa mazuri ama mabaya), nusu yao walihusisha matokeo na juhudi za mwalimu 12 . Asilimia 7 pekee ndio waliotaja changamoto zinazohusiana na wazazi au wanafunzi wenyewe 13 .

Cha kushangaza ni kwamba mwananchi 1 kati ya 3 hajui nini kinachangia matokeo ya kujifunza pindi watoto wanapohitimu elimu ya msingi.

Jambo la 5: Wananchi wanaamini kuwa walimu wanaona fahari juu ya taaluma yao lakini hawapendi kazi yao
Asilimia 93 ya wananchi wanaamini kuwa ualimu ni taaluma ambayo ndiyo msingi wa taifa. Japokuwa asilimia 79 ya wananchi wanaamini kuwa walimu wanaona fahari ya kile wanachokifanya, asilimia 80 wanaona kuwa walimu hawapendi kazi zao na hufanya tu kwa ajili ya kujipatia kipato. Je ni kwanini walimu wanaona fahari ya taaluma yao lakini hawapendi kazi yao?

Kwa mujibu wa baadhi ya wananchi, ni kutokana na mishahara pamoja na mazingira ya kufanyia kazi. Kwa ujumla asilimia 42 ya wananchi wanaamini kuwa walimu hawalipwi vizuri, na asilimia 34 wanaamini mazingira ya kazi ya walimu hayawapi motisha wa kufundisha.

Haya ni maoni ya wananchi wachache (wananchi wengi wanatoa kauli zinazokinzana), lakini yanaweza kutoa mwanga kwanini wananchi wanadhani walimu hawapendi kazi yao.

Wananchi walipoulizwa kuhusu vitu ambavyo vinaweza kuwaongezea walimu motisha ili kutoa elimu bora kwa wanafunzi, asilimia 56 walisema nyongeza ya mishahara na asilimia 19 walitaja uboreshaji wa mazingira ya kazi.


Jambo la 6: Maoni ya wananchi yanatofautiana juu ya ubora wa elimu ya msingi.
Wananchi walipoulizwa kuhusu ubora wa elimu, nusu yao waliamini kuwa ubora wa elimu ya msingi umezorota ama kubaki vilevile kwa kipindi cha muongo mmoja uliopita, huku nusu nyingine wakisema elimu ya msingi imeboreshwa.

Wananchi walio wengi wanaamini njia kuu ya kuboresha elimu ya msingi ni kwa kuweka mkazo kwa walimu. Ili kuboresha elimu wananchi wametoa ushauri ufuatao kwa serikali: kufuatilia utendaji wa walimu (asilimia 40), kuongeza mishahara ya walimu (asilimia 19), pamoja na kuongeza idadi ya walimu (asilimia 10). Asilimia 7 pekee ndiyo waliotaja ushirikiano kati ya
mwalimu na mzazi kama njia ya kuwawezesha watoto kujifunza.


3. Hitimisho
Serikali mpya imejikita kwenye utoaji wa elimu bure kwa shule za msingi na sekondari na wananchi wamekuwa na imani kubwa juu ya suala hilo. Wananchi wanaamini kuwa utoaji wa elimu bure utatekelezwa katika muda ulianishwa, na ubora wa elimu utaongezeka.

Wasiwasi wa wananchi unaonekana kwenye uwajibikaji wa walimu katika kufikia kiwango cha juu cha elimu. Walipoulizwa kuhusu namna ya kuboresha elimu ya msingi, wananchi walitilia mkazo kwenye mishahara ya walimu, kuongezeka kwa idadi ya walimu mashuleni na zaidi ya yote uwajibikaji
wa walimu.

Siyo wananchi pekee wanaosisitiza uwajibikaji wa walimu. Kwa mujibu wa Davidson, ukosefu wa motisha kwa walimu ni moja ya sababu kuu inayoathiri ubora wa elimu nchini Tanzania 16 .

Utafiti usio rasmi uliofanywa na Twaweza kwa walimu 272 unaonesha kuwa asilimia 96 ya walimu hao hawaridhishwi na kazi zao. 

Pia, mwalimu 1 kati ya walimu watatu alisema asingechagua tena kazi ya ualimu, huku wakitaja mazingira magumu ya kazi (asilimia 34) na mishahara midogo (asilimia 26) kama sababu kuu. Hii inadhihirisha kuwa walimu na wananchi kwa ujumla wana mitazamo inayofanana.

Kwa kuwa uongozi mpya umeweka mkazo suala la elimu, ni vizuri pia ukaanza kutatua matatizo ya walimu na kuboresha mazingira ya ufundishaji Tanzania ili kwenda sambamba na kasi ya utoaji wa elimu.

Wakati utekelezaji wa sera mpya ya Elimu ukiendelea, ni vyema kufuatilia mabadiliko yaliyofanyika na mafanikio yaliyopatikana. 

Kumekuwa na kusitasita kuhusu dhana hii ya ‘elimu bure’ ambapo viongozi wa shule wana mashaka na jinsi ambavyo TZS 10,000 kwa kila mwanafunzi mmoja kwa mwaka inaweza kutosha. Mfano mmoja ni kuhusu suala la ulinzi.

Kama ilivyoelezwa hapo juu, asilimia kubwa ya michango ya wazazi kwa mwaka 2015 imekuwa ikitumika kwenye ulinzi (asilimia 66); wakati ruzuku inayotumwa shuleni haihusishi suala la ulinzi. 

Iwapo fedha zote zilizotengwa zitapelekwa shuleni na kuwafikia wahusika kwa kiwango kilichopangwa, je kiwango hicho kitatosha kuhakikisha watoto wanajifunza?

Suala jingine la msingi ni kuhusu utunzwaji wa rasilimali. Ruzuku hapo awali zilikuwa zinapelekwa moja kwa moja shuleni mpaka mwaka kufikia mwaka 2002 zilipoanza kupelekwa kupitia kwa mamlaka zaHalmashauri za Wilaya na Miji. 

Kwa sasa mfumo umebadilika ambapo ruzuku zinapelekwa moja kwa moja shuleni. Tunaamini uamuzi wa kupeleka ruzuku moja kwa moja mashuleniumechangiwa na na kutokuwepo kwa ufanisi katika mfumo uliopita.

Kwa mfano, kati ya 2010 na 2013, kwa wastani ni TZS 2,202 pekee ndizo zilizofika shuleni kwa kila mwanafunzi.

Sera mpya ya kupeleka pesa za ruzuku moja kwa moja mashuleni unaibua maswali kadhaa. Tutahakikisha vipi upelekaji wa pesa moja kwa moja kwenye shule utatupa matokeo tofauti?

Je shule zina uwezo wa kusimamia rasilimali hizo vizuri; kuzuia ubadhirifu na upotevu na kuhakikisha zinaelekezwa kwenye matumizi ya vitu muhimu zaidi? Kuna mfumo gani uliopo kwenye ngazi ya shule, hususani katika kuhakiki maamuzi ya matumizi?

Ili kuhakikisha tunapata thamani halisi ya matumizi katika elimu, utoaji na matumizi ya fedha vinapaswa kuhakikiwa katika ngazi ya shule.

Kwa kumalizia, na la muhimu zaidi, utawala mpya umeonekana kuwa kimya kwenye suala la kuboresha matokeo ya ujifunzaji. Ongezeko la shule za msingi kwa mamilioni ya watoto wa kitanzania ni mafanikio makubwa.

Hata hivyo, baada ya miaka kumi ya sera hii, tunatilia shaka anguko la uandikishaji huo wa maelfu ya watoto pasipo kutoa fedha za kutosha, wala kutilia mkazo suala la ubora. Je kutakuwa na walimu wa kutosha kwa wanafunzi hawa? Tutahakiki vipi kama wanajifunza?

Kwa kipindi cha miaka kumi iliyopita tumeshuhudia ongezeko kubwa la shule za sekondari pamoja na wanafunzi huku ikiambatana na ongezeko kubwa la idadi ya wanafunzi wanaofanya vibaya kwenye mitihani yao ya kidato cha nne. 

Je uongozi huu umejipanga kufanya nini cha tofauti kuhakikisha kuwa Tanzania haiendelei kutengeneza wahitimu mbumbumbu?

Tutahakikisha vipi mfumo wa elimu unawapa watanzania fursa ya kuishi maisha mazuri na kuchochea maendeleo ya nchi? Pamoja na nia njema na maelezo mazuri ya Rais yanayotilia mkazo kwenye elimu na kutoa matumaini mapya, ni muhimu kuzingatia kuwa ufanisi katika sekta hii muhimu utafikiwa kwa kutumia ushirikiano na wadau wote.

Aidha, panahitaji marekebisho mapana zaidi katika mfumo wa elimu ili kufikia malengo ya elimu bure na bora, na sio bora elimu bure!

Mfuko wa Habari Tanzania (TMF ) Wasema Uko Tayari Kutoa Msaada wa Fedha Ili Kuiwezesha TBC Kutangaza LIVE Mwenendo wa Bunge

$
0
0

KILIO cha ukosefu wa fedha za kuonesha matangazo ya moja kwa moja ya Bunge la Tanzania kupitia Shirika la Utangazaji nchini (TBC) ambacho kimekuwa kikitolewa na serikali, sasa kimepata ufumbuzi.

Mfuko wa Vyombo vya Habari nchini (TMF) umeeleza kwamba upo tayari kutoa fedha zinazohitajika ili kuhakikisha haki ya Mtanzania kupata habari kupitia TBC haiingiliwi wala kubughudhiwa kwa hoja yoyote.

Endapo serikali itakubali ombo hilo, wananchi wataendelea kunufaika na vikao vya moja kwa moja vya bunge tofauti na pendekezo la serikali la kunakili baadhi ya sehemu na kisha kuoneshwa usiku.

Ernest Sungura, Mkurugenzi Mtendaji wa TMF leo jijini Dar es Salaam amewaeleza wahariri wa habari na serikali kupitia mwakilishi wake Assah Mwambene ambaye ni Mkurugenzi wa Habari Maelezo kwamba, taasisi hiyo imejipanga kusimamia na kuhakikisha Watanzania wanaendelea kupata matangazo ya moja kwa moja kutoka bungeni kupitia TBC kwa kuyagharamia.

Sungura amesema kwamba miongoni mwa malengo ya mfuko huo ni pamoja na kuleta mabadiliko katika tasnia ya habari pia kuhakikisha wananchi wanapata taarifa.

Januari mwaka huu, Nape Nnauye, Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo alitoa ufafanuzi bungeni kuhusu hatua ya serikali kusitisha matangazo ya moja kwa moja ya bunge kupitia TBC.

Miongoni mwa sababu alizozieleza ni pamoja na kuwepo kwa gharama kubwa ya Sh. 4.2 bilioni zinazotumika katika uendeshaji wa matangazo hayo ya moja kwa moja kwa mwaka pia watumishi wa serikali kushabikia bunge badala ya kuendelea na kazi ofisini.

Hatua ya serikali kusitisha matangazo hayo iliibua mjadala mkubwa bungeni huku Zitto Kabwe, Mbunge wa Kigoma Mjini (ACT-Wazalendo) akilitaka bunge kusitisha shughuli zake ili kujadili taarifa hiyo ya serikali.

Nje ya bunge mjadala huo uliendelea bila kupatikana kwa ufumbuzi ambapo TMF imedhamiria kugharamia matangazo hayo ili kuruhusu wananchi kuendelea kupata matangazo hayo kupitia TBC.

Katika mkutano huo, Mwambene amesema kwamba, serikali itafikiria namna ya kupeleka maombi TMF ya uwezeshwaji katika maandalizi ya miswada miwili ya sheria za habari ili kupitisha sheria zenye matakwa ya wadau.

Kuhusu hilo, Sungura amesema taasisi yake iko tayari kuisaidia serikali kwenye mchakato huo na hata kuitisha kongamano kubwa la wadau.

Rais Magufuli Akutana Na Rais Mstaafu Wa Awamu Ya Tatu Benjamin Mkapa Pamoja Na Mjumbe Maalum Wa Rais Wa Guinea Bisau Februari 25,2016

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akifurahia jambo wakati alipokuwa akizungumza na Rais Mstaafu wa awamu ya tatu Mheshimiwa Benjamin Wiliam Mkapa Ikulu jijini Dar es Salaam Februari 25,2016

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na Rais Mstaafu wa awamu ya tatu Mheshimiwa Benjamin Wiliam Mkapa Ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na Genarali Omar Embalo mjumbe Maalum wa Rais wa Guinea Bissau Jose Mario Vaz Ikulu jijini Dar es Salaam. Pamoja na mambo mengine Mjumbe huyo alileta salamu za pongezi kutoka kwa Rais wa Guinea Bisau.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akipokea barua kutoka Genarali Omar Embalo mjumbe Maalum wa Rais wa Guinea Bissau Jose Mario Vaz.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akimshukuru Mjumbe Maalum wa Rais wa Guinea Bissau mara baada ya kupokea barua ya Salamu na pongezi.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na Genarali Omar Embalo mjumbe Maalum wa Rais wa Guinea Bissau Jose Mario Vaz Ikulu jijini Dar es Salaam

Mabomu Ya Machozi Yarindima Jijini Mwanza Kuwatawanya Wananchi Waliotaka Kutoa Uhai wa Dereva Aliyegonga Mtoto

$
0
0

Polisi  jijini Mwanza wamewatawanya wananchi kwa mabomu katika eneo la Sinai, Mtaa wa Nyerere ‘A’ Kata ya Mabatini baada ya kutokea vurugu kutokana na mtu mmoja kugongwa na gari.

Polisi walilazimika kutumia mabomu ya machozi kutawanya watu hao wakati wakimuokoa dereva wa gari namba T. 520 CBM Mark X, Lifaty Dickson ambaye alimgonga mtoto wa miaka sita, Festo William.

Hatua hiyo ilifikiwa baada ya wananchi kuhisi kwamba polisi walitaka kumtorosha dereva huyo kwa madai ya kufanya ajali bila kukusudia.

Wananchi wanadai dereva huyo alifanya ajali baada ya kuendesha kwa mwendo kasi na hatimaye kumgonga na kumsababishia mauti motto huyo aliyekuwa Mkazi wa Kata ya Mahina.

“Mimi nilikuwa katika eneo hili la ajali ilipotokea, sasa huyu mtoto aliyefariki (Festo William) alikuwa anavuka katika eneo la watembea kwa miguu, zebra lakini huyu mwenye gari alishindwa kupunguza mwendo.

“Baada ya kuona hivyo sisi kama wananchi wapenda haki tulianza kumuadabisha huyu mtu lakini polisi wakaingilia kati na sisi hatukukubali,“ amesema shuhuda mmoja aliyetambulika kwa jina la Simon.

Justus Kamugisha, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kudai kuwa, polisi walilazimika kutumia mabomu ya machozi kumuokoa dereva wa gari hilo ambaye alikuwa akishambuliwa na wananchi.

Kamugisha amesema kuwa, polisi wake walishambuliwa kwa kupigwa mawe na wananchi hao, hivyo hawakuwa na njia yeyote ya kujiokoa tofauti na kutumia mabomu ya machozi.

“Polisi hawakuwa na njia yoyote tofauti na hiyo, waliamua kufanya hivyo ili kumuokoa dereva wa gari hilo na kuokoa raia wema wengine,” amesema Kamugisha na kuongeza kuwa watu watatu wanashikiliwa na polisi kutokana na mkasa huo.

Kurasa Za Mbele Za Magazeti Ya KENYA Ijumaa ya Leo Februari 26

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Uingereza Ijumaa Ya February 26, 2016

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya TANZANIA Ijumaa Ya Leo Februari 26

Basi La Mashimba Express La Kahama- Mwanza Lagongana Na Gari Ndogo Na Kuua Watu Wanne

$
0
0

Watu wanne wamefariki dunia katika ajali baada ya basi la Mashimba Express lililokuwa linasafiri kutoka Kahama kwenda jijini Mwanza kugongana na gari dogo  katika eneo la njia panda kuelekea wilayani Kishapu  Mkoani Shinyanga

Ajali hiyo imetokea jana jioni ambapo mashuhuda wa tukio hilo wamedai kuwa ilisababishwa  na  gari ndogo iliyokuwa katika mwendo kasi ambayo ilipoteza uelekeo na kisha kuligonga basi hilo.Watu  wawili  waliokuwa  katika  gari  hilo  akiwemo  dereva  walifariki  dunia  papo hapo

Mganga mfawidhi wa hospitali ya  rufaa ya mkoa wa Shinyanga Dkt Albert George Masigati amesema kati ya saa 12 na saa moja usiku wa kuamkia leo  walipokea miili ya marehemu wanne katika hospitali hiyo ,wote wakiwa ni wanaume na majeruhi wanane,kati yao wanawake wanne na wanaume wanne.

Hata hivyo Dkt Masigati amesema huenda idadi ya majeruhi ikaongezeka kutokana na taarifa kuwa baada ya ajali hiyo kutokea baadhi ya majeruhi walikimbizwa katika hospitali ya Kolandoto na Kishapu.

Dkt Masigati amesema hakuna majeruhi aliye katika hali mbaya na kwamba bado wanaendelea kuwafanyia uchunguzi .
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live


Latest Images