Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Majangili Waliotungua Helkopta Wahukumiwa Miaka 15 Jela

$
0
0

Mahakama ya Wilaya ya Bariadi imewahukumu watu wanne, mmoja kifungo cha miaka 20 jela na watatu miaka 15 kila mmoja waliostakiwa kuwa kutungua helikopta kwenye Pori la akiba Maswa wilayani Meatu na kusababisha kifo cha rubani wake baada ya kupatikana na hatia ya kukutwa na silaha.

Akisoma hukumu hiyo jana, Hakimu Mfawidhi wa Wilaya hiyo, Mary Mrio alisema anawapa adhabu hiyo washtakiwa hao baada ya kukiri kosa la kukutwa na silaha hiyo kinyume cha sheria na hivyo kutoisumbua mahakama.

Katika hukumu hiyo, Njile Gunga ambaye anadaiwa kutungua ndege hiyo Januari 29 atatumikia kifungo cha miaka 20, huku akisubiri kesi nyingine mbili ya mauaji ya rubani huyo na uhujumu uchumi ambazo zitatajwa Mahakama ya Mkoa wa Simiyu.

Juzi washtakiwa hao, Shija Mjika, Dotto Pangani, Njile Ngunga na Moses Mandagu, walikiri kukutwa na silaha, lakini Hakimu Mrio hakuweza kutoa hukumu kwa kuwa ushahidi ulikuwa haujawasilishwa mahakamani. Baada ya kuwasilishwa ushahidi huo jana, alitoa hukumu hiyo ambayo inatokana na mashtaka matano dhidi yao.

Wakili Mwandamizi wa Serikali, Yamiko Mlekano alitaja makosa hayo kuwa ni kumiliki na kukutwa na silaha kinyume cha sheria.

Shtaka la tatu ni kukamatwa na risasi tano za bunduki aina ya rifle, shtaka ambalo Pangali na Gunga walikiri.

Katika shtaka la nne linalowakabili washtakiwa wote wanne, Wakili Mlekano alidai ni umiliki risasi kinyume cha sheria, ambazo walikamatwa nazo Februari 8 na bunduki aina ya Rifle 303.

Washtakiwa hao waliomba kupunguziwa adhabu kwa kile walidai ni mara yao ya kwanza kutenda makosa kama hayo, lakini Mlekano aliomba mahakama kutoa adhabu kali ili iwe fundisho kwa wengine.

Hakimu Mrio alisema kwa kosa la kwanza, pili na nne mahakama inawahukumu kifungo cha miaka mitano jela kila mmoja, kosa la tatu miaka mitano au kulipa faini ya Sh10 milioni.

Profesa Maghembe Amng’oa Mhifadhi Mkuu wa Hifadhi ya Kilimanjaro (Kinapa), Erastus Lufungulo

$
0
0

Waziri wa Maliasili na Utalii, Profesa Jumanne Maghembe amemuondoa Mhifadhi Mkuu wa Hifadhi ya Kilimanjaro (Kinapa), Erastus Lufungulo na kutoa maagizo mazito kwa kampuni za wazawa.

Maghembe amemuondoa Lufungulo Kinapa na kumrudisha makao makuu ya Shirika la Hifadhi za Taifa (Tanapa) baada ya kufanya mabadiliko kwenye baadhi ya hifadhi hizo nchini na nafasi yake kuchukuliwa na Betrita Loibooki aliyekuwa Mkuu wa Hifadhi ya Arusha.

Pia, Maghembe ametoa muda hadi Mei, mwaka huu kwa kampuni za wazawa zinazohudumia watalii wanaopanda Mlima Kilimanjaro kuboresha huduma, vinginevyo ataruhusu ushindani wa kibiashara.

Vilevile, amezitaka kampuni za utalii kuwalipa wapanda mlima mishahara waliyokubaliana na Serikali na hataki kusikia wanapunjwa ujira wao.

Waziri huyo alitoa maagizo hayo katika kikao cha wadau wa utalii wanaohudumia watalii Mlima Kilimanjaro na kusisitiza kuwa wasipoboresha huduma kwa kiwango cha kimataifa, ataruhusu ushindani na kampuni za nje.

Mbali na kufanya mabadiliko hayo, ameuagiza uongozi wa Tanapa kufanya haraka mabadiliko ya watumishi waliopo sehemu za kuingilia watalii za Kinapa.

Profesa Maghembe alisema sababu nyingine iliyochangia kushuka kwa idadi ya watalii ni wageni kupata huduma duni ikiwamo chakula ambacho hakina hadhi ya kimataifa.

“Nataka niwaambie, kuanzia mwezi Mei kama hamjaboresha chakula kwa watalii, mishahara kwa wapanda milima na kuwapa mavazi ya kujikinga na baridi nitaruhusu ushindani,” alisema.

Mkurugenzi Mkuu wa Tanapa, Allan Kijazi, aliahidi kuitisha kikao cha wadau wote wa utalii kabla ya Mei ili kujadili changamoto na maagizo hayo ya waziri.

Msemaji wa Wapanda Mlima Kilimanjaro na Meru, James Mwamatego alisema kwa muda mrefu wameomba kupatiwa mikataba ya ajira, lakini baadhi ya wamiliki wa kampuni za utalii wamegoma. 

Mwenyekiti wa Chama cha Huduma za Utalii Mkoa wa Kilimanjaro (Kiato), Amos Lufungilo alisema wapo baadhi ya raia wa kigeni wanaomiliki nyumba ‘bubu’ za kulala wageni na kufanya biashara ya kuongoza watalii.

Moto Waua Askari Polisi Na Mpenzi Wake

$
0
0

ASKARI wa kike wa Usalama Barabarani, Attuganile Mwakibete (37) na mpenzi wake Sunday Mhagama (36), wameteketea kwa moto baada ya nyumba walimokuwa ndani kuungua.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Rukwa, Jacob Mwaruanda alisema tukio hilo lilitokea Februari 2, mwaka huu saa 7:15 mchana katika kitongoji cha Maporomoko, Kata na Tarafa ya Laela Wilaya ya Kipolisi ya Laela.

Inadaiwa kuwa nyumba hiyo iliyoteketea kwa moto ambayo askari Attuganile alikuwa amepanga vyumba viwili, ni mali Yaiyela Mwamahonje aliyokuwa akiishi na watoto wake wawili wadogo ambao wamenusurika kufa, licha ya kuwemo ndani ya nyumba hiyo wakati wa ajali hiyo.

Taarifa za uhakika zinaeleza kuwa Mhagama aliyekuwa rafiki wa trafiki huyo wa kike, ni mkazi wa Mbeya ambako mkewe anaishi, na alikuwa na mazoea ya kumtembelea mpenzi wake huyo mara kwa mara.

Inadaiwa askari Attuganile alikuwa ameachana na mumewe wa ndoa. “Vyumba viwili yaani sebule na chumba walimokuwemo Attuganile na Mhagama viliwaka moto baada ya jenereta lililokuwa likifanya kazi likiwa sebuleni humo kulipuka na kuwajeruhi vibaya,” alieleza.

Kwa mujibu wa Kamanda Mwaruanda, Attuganile alifariki dunia Februari 8, mwaka huu saa 2:30 asubuhi akipatiwa matibabu katika Hospitali ya Mkoa wa Rukwa mjini Sumbawanga.

Mhagama alikimbizwa na kulazwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mbeya jijini Mbeya ambako alifariki dunia Februari 9, mwaka huu. Kamanda Mwaruanda alisema uchunguzi wa tukio hilo unaendelea.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Ijumaa Ya Februari 12

Waziri Nchemba Afanya Ziara Ya Kushtukiza Saa Saba Usiku Machinjio Ya Ukonga Mazizi Na Kufukuza Viongozi Wote Wa Machinjio

$
0
0
Waziri wa Kilimo na Mifugo Mwigulu Nchemba amefanya ziara ya Kushtukiza saa saba usiku wa kuamikia leo katika Machinjio ya Ukonga Mazizi.

Katika ziara hiyo, Waziri Nchemba  amekamata
ng'ombe 200 wakiwa wanaingizwa kwenye machinjio bila kibali halali, na kati yao ni ng'ombe 20 tu ndo walikuwa na kibali cha kuchinjwa, hivyo ushuru  wa ng'ombe 180  ulikuwa  unatafunwa  na  watumishi  waovu.
 
Baada  ya  kubaini  hali  hiyo,Waziri Nchemba ameufukuza  uongozi wote  wa  machinjio  hayo  na  kuagiza  vyombo  vya  dola  viwakamate  viongozi  wote waliohusika  na  kuwafikisha  mahakamani.


Maalim Seif Aiandikia Barua Tume ya Uchaguzi Zanzibar (Zec)

$
0
0

Mgombea urais wa Zanzibar kupitia Chama cha Wananchi (CUF), Maalim Seif Sharif Hamad, ameithibitishia rasmi Tume ya Uchaguzi Zanzibar (Zec) kujiondoa kuwania wadhifa huo katika Uchaguzi wa marudio utakaofanyika Machi 20, mwaka huu.

Mbali na Maalim Seif, wagombea wote wa chama hicho wa nafasi ya Uwakilishi na Udiwani wamejiondoa kwa kuwasilisha barua rasmi kuwa hawatoshiriki uchaguzi huo wa marudio wa Zanzibar.

Mkurugenzi wa Mipango na Uchaguzi wa CUF, Omar Ali Shehe, amesema Maalim Seif amewasilisha waraka wa barua wa kujiondoa kwa Zec, Febuari 8, mwaka huu.

Amesema hatua aliyochukuwa mgombea huyo ni utekelezaji wa wa azimio la Baraza Kuu la Uongozi la Taifa la CUF kutoshiriki uchaguzi mkuu wa marudio visiwani hapa.

Shehe alisema kuwa Zec imetakiwa kutotumia jina wala picha za Maalim Seif  na taarifa zozote katika karatasi za wapigakura kabla ya kufanyika uchaguzi huo.

Alisema kuwa katika Barua yake Maalim seif amesisitiza kuwa uchaguzi wa Oktoba 25 mwaka jana ulikuwa uchaguzi huru na wa haki na Mwenyekiti wa tume ya Uchaguzi ya Zanzibar Jecha salim Jecha hakuwa na mamlaka ya Kikatiba na sheria kufuta matokeo ya Uchaguzi huo.

Hata hivyo Mkurugenzi wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar Salum Kassim alisema jana kuwa ni mapema kueleza vyama vingapi vimekamilisha kuthibitisha wagombea wake kama wapo hai na watashiriki uchaguzi kabla ya kufanyika Machi 20, mwaka huu.

BASATA yaufungia wimbo wa Nay wa Mitego ‘Shika Adabu Yako’

$
0
0

Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) limeufungia rasmi wimbo wa ‘Shika Adabu Yako’ ulioimbwa na Msanii Nay wa Mitego kutokana na ukiukwaji mkubwa wa maadili, kashfa, uchochezi, kudhalilisha watu na kuhatarisha amani na utengamano miongoni mwa wasanii na jamii kwa ujumla.

Sambamba na kuufungia wimbo huo, BASATA litampa karipio kali Msanii huyo na kumwagiza kuacha mara moja kujihusisha kwa namna yoyote na tabia ya kuutangaza wimbo au kuusemea katika vyombo vya habari vinginevyo hatua kali zaidi na za kisheria zitachukuliwa.

Ieleweke kwamba kwa mujibu wa kifungu cha 4 (1) (j) cha sheria ya BASATA namba 23 ya mwaka 1984, Baraza limepwa mamlaka ya kuratibu na kufuatilia mienendo ya mtu yeyote anayehusika na kazi za Sanaa na kuhakikisha linalinda maadili ya kitaifa miongoni mwa Wasanii wanapokuwa jukwaani au wanapobuni kazi yoyote ya Sanaa.

Aidha, kifungu cha 4 (2) cha sheria hii kinalipa Baraza nguvu ya kisheria kufanya jambo lolote lile kuliwezesha kufanya majukumu yake kwa faida na ustawi wataifa.Baraza la Sanaa la Taifa limekuwa likipokea simu za maswali na malalamiko kadhaa kutoka kwa waandishi wa habari na wadau wa Sanaa ambao kwa njia moja ama nyingine wameguswa na kuchukizwa na kazi hiyo ambayo si tu inadhalilisha tasnia ya Sanaa bali inawafanya watu makini kuanza kuhoji hadhi ya msanii, weledi na taaluma ya Sanaa kwa ujumla.

BASATA mara kadhaa limekuwa likikemea na kuchukua hatua kadhaa dhidi ya tabia hii chafu ambayo ilianza kujitokeza kwenye kampeni za uchaguzi mkuu wa mwaka jana wa 2015. Kukemea huku ni kwa msingi mmoja kwamba asili ya tasnia hii ya Sanaa ni kuelimisha jamii, kukosoa pale kunapokuwa na tatizo, kuburudisha na kujenga jamii yenye staha, umoja wa kitaifa, mshikamano na amani.

Ni wazi wasanii wengi wanafanya kazi zao vizuri, kwa kubuni kazi zenye ubora, zenye kujenga jamii na zaidi zinazoburudisha rika zote kiasi cha kuzifanya zililetee heshima taifa. Kati ya hawa wengi, kuna wachache ambao wanaipaka matope tasnia ya Sanaa na kwa kiasi kikubwa wanaonesha wazi kutokuwa na nia njema.

Kwa mantiki hii BASATA halitavumilia hawa ‘wasanii’ wachache ambao wanataka kuigeuza tasnia ya Sanaa na wasanii genge la wahuni, wasio na staha, wa kudharaulika  na waliojipanga kuibomoa jamii na kuharibu amani na utulivu uliopo nchini.

BASATA linapenda kueleza yafuatayo:
1.Vyombo vya habari viwe vya kwanza kuchuja maudhui ya kazi yoyote ya Sanaa kabla ya kuingia kwenye mtego wa kuwa mawakala wa uharibifu wa jamii kupitia kucheza kazi chafu za Sanaa. BASATA lilishaziandikia radio zote kuzishauri kuwa na kamati za maudhui ya kazi za Sanaa lakini inashangaza baadhi ya vyombo vya habari vinakuwa vya kwanza kushabikia nyimbo hizo chafu na kuwapa muda mrefu wa mahojiano wasanii hao na baadaye kurudi BASATA kuhoji uhalali wa nyimbo husika. Hii si sawa hata kidogo.

2.Serikali ya awamu ya tano chini ya Rais Dkt. John Pombe Magufuli imejipanga kuwajengea mazingira bora ya utendaji Wasanii wote nchini kupitia kuboresha miundombinu ya Sera, Sheria na Kanuni. Hata hivyo, uwepo wa Wasanii kama hawa unafanya jamii kuhoji hadhi ya wasanii, nafasi yao katika jamii na kwa maana hiyo kukatisha tamaa juhudi za kuipa msukumo sekta hii maana wadau wakuu ambao ni wasanii wanaanza kuoneasha kuwa mawakala wa uharibifu wa jamii.

3.BASATA linawataka wasanii kujiuliza mara mbili kabla ya kubuni kazi zao za Sanaa. Wafikirie wazazi, ndugu, jamaa na marafiki zao watazipokeaje? Wavae nafasi ya wale wanaowatukana na kuwadhalilisha, Waelewe kwamba Sanaa si uwanja wa kutusi na kudhalilisha watu hata kidogo. Ikitokea wale wanaotukanwa na kudhalilishwa kughafilika Sanaa itakuwa uwanja wa vita. Hili halikubaliki.

4.Tunafahamu kuna wasanii wamekuwa wakifanya hivyo makusudi kutafuta ‘umaarufu uchwara’ ambao wanadhani utakuja kutokana na kuzungumziwa sana. Tunapenda kusema wazi kwamba umaarufu hauji kwa upuuzi wa namna hiyo unakuja kwa msanii mwenyewe kujiheshimu, kujituma, kubuni kazi bora na zenye kulifahamu vema soko la ndani na la kimataifa.
 
SANAA NI KAZI TUIKUZE, TUILINDE NA KUITHAMINI

Godfrey L. Mngereza
KATIBU MTENDAJI, BASATA

Watendaji Wakuu wa Wakala Wa Vipimo Nchini Wasimamishwa Kazi Kupisha Uchunguzi Wa Upotevu Wa Mafuta Bandarini

$
0
0

SERIKALI imeamua kuwasimamisha kazi watendaji wawili kutoka Wakala wa Vipimo nchini (WMA) kuanzia leo ili kupisha uchunguzi wa upotevu wa mafuta bandarini kutokana na zuio la kufunga kwa mita kwa zaidi ya miaka mitano.

Waliosimamishwa kazi ni Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Vipimo nchini (WMA), Bi. Magdalena Chuwa na Meneja Vipimo Kitengo cha Bandari, Bi. Bernadina Mwijarubi. Bi. Mwijarubi ndiye anashughulikia kitengo cha mafuta bandarini.

Akitangaza uamuzi huo kwenye kikao cha Makatibu Wakuu kilichofanyika leo (Ijumaa, Februari 12, 2016) ofisini kwake Magogoni jijini Dar es Salaam, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amemwagiza Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara, Dk. Adelhelm Meru awaandikie barua za kuwasimamisha kazi ili kupisha uchunguzi huo.

“Katibu Mkuu Viwanda, waandikie barua za kuwasimamisha kazi ili kupisha uchunguzi. Katika kipindi hiki hawatatakiwa kusafiri kwenda popote hadi uchunguzi utakapokamilika. Pia utafute mtu wa kukaimu nafasi hiyo ili kazi ziendelee,” alisema.

Waziri Mkuu pia amesema ofisi yake itawaandikia barua ofisi ya TAKUKURU na polisi ili wafuatilie suala hilo mara moja na ikithibitika kuwa walihusika hatua rasmi zitachukuliwa na ikithibitika hawakuhusika basi watarudishwa.

Waziri Mkuu pia aliagiza mfumo wa upimaji mafuta kwa kutumia flow meters uendelee kutumika na ule upimaji wa kukadiria uache kutumiwa mara moja.

Jana (Alhamisi, Februari 11, 2016) Waziri Mkuu alifanya ziara kukagua flow meters za zamani zilizopo Kurasini (Kurasini Oil Jetty) na kisha akatembelea na kukagua flow meters mpya ambazo zinajengwa Kigamboni. Mita hizo zimegharimu dola za marekani milioni 6 (sawa na sh. bilioni 12.96/- za sasa).

Pia Waziri Mkuu alitembelea sehemu ya kuchukulia mafuta yanayotoka bandarini (TPA Manfold) iliyoko Kigamboni na kukagua mitambo ya kusambazia mafuta kwenye matenki ya mafuta ya kampuni ya TIPER yaliyoko Kigamboni yanayomilikiwa kwa ubia baina ya Serikali na kampuni ya Oryx Energies.

Katika ziara hiyo ilibainika kuwa Kampuni ya TIPER imejiunganishia bomba la moja kwa moja kutoka kwenye bomba kubwa la mafuta linalotoka bandarini hali iliyomlazimu Waziri Mkuu kuagiza kwamba bomba hilo litolewe kwenye maungio hayo ndani ya mwezi mmoja.

“Jana niliagiza kuwa bomba hilo ling’olewe. Nimetoa mwezi mmoja ili kurekebisha mfumo huo. Simamieni vizuri na kuhakikisha kuwa na wao pia wanarudi kwenye manfold kama ilivyo kwa wengine,” alisema Waziri Mkuu.


IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU, 2 MTAA WA MAGOGONI,
S.  L. P. 3021, 11410 DAR ES SALAAM.
IJUMAA, FEBRUARI 12, 2016.

CCM Yalaani Vikali Kitendo Cha Kuwekwa Alama ya X Kwenye Nyumba Za Wafuasi Wake

$
0
0

CHAMA CHA MAPINDUZI kimelaani vikali kitendo cha kuwekwa alama ya X kwenye nyumba za wafuasi wake Kisiwani Pemba.

Pia CCM imesikitishwa na kulaani vikali kitendo cha kuchoma moto tawi la CCM la Kengeja.

Katibu wa Kamati Maalum ya NEC Bi Waride Bakari Jabu akizungumza na wanahabari ofisini kwake Kisiwandui amesema kitendo cha kuchoma moto ofisi za CCM na kuweka X nyumba za wafuasi wa CCM maeneo ya Mtambile, Kengeja, Minazini, na Kangani katika Wilaya ya Mkoani kuna lengo la kuvunja Amani na Usalama visiwani humo.

CCM imetoa wito kwa wazanzibar hasa wafuasi wa CCM kupuuza vitendo hivyo na kutolipa kisasi na badala yake waelekeze nguvu katika maandalizi ya uchaguzi wa marudio uliotangazwa kufanyika Machi 20.

Lakini pia CCM inatoa wito kwa vyombo vya Ulinzi na Usalama kuhakikisha kuwa wanafanya kazi yao kwa umakini zaidi ili kuzuia uhalifu na njama za kuvuruga amani Visiwani, Zanzibar.

Siku 100 Za Rais Magufuli Ikulu

$
0
0

Ni kweli siku hazigandi kwamba Rais John Magufuli aliyeingia madarakani baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 25 mwaka jana, ametimiza siku 100 leo. 

Tangu alipotoa hotuba yake siku ya kuapishwa na ile ya uzinduzi wa Bunge la 11, Rais Magufuli  amejitahidi kuishi katika maneno yake kwa kutenda kile anachokisema.

Miongoni mwa mambo aliyoahidi ni kupambana na rushwa pamoja janga la dawa za kulevya, akisema dawa za kulevya zimeathiri vijana wengi, hivyo akaahidi kushughulikia mtandao huo na wakubwa wanaohusika.

 Kwa upande wa rushwa, Rais Magufuli aliahidi kupambana na ufisadi na rushwa na katika kutekeleza hilo, alisema ataunda mahakama maalumu ya kushughulikia wezi wakubwa yaani mafisadi.

 Pia aliahidi kuwashughulikia wafanyakazi wazembe ili Serikali yake isiendelee kulea watu wanaolipwa mishahara tu wakati hawafanyi kazi yoyote.

Katika kubana matumizi ya serikali, aliahidi kudhibiti warsha ambazo hazina umuhimu katika Serikali wala kuongeza ufanisi kwa wafanyakazi.

Aliahidi pia kudhibiti safari za nje, ambazo zimekuwa zikigharimu Serikali fedha nyingi ambazo zingeweza kutumika katika shughuli mbalimbali za kimaendeleo.

Rais Magufuli pia alisema Serikali yake itaongeza wigo katika ukusanyaji wa mapato, ukizingatia kuwa kodi ni kitu muhimu na ni lazima zikusanywe.

Aliahidi kufufua viwanda viliyobinafsishwa, ambavyo baadhi alidai vimegeuzwa mazizi ya mbuzi wakati waliopewa kwa madhumuni ya kuviendeleza.

Aliahidi pia kushughulika na kero zinazolalamikiwa kutendwa na polisi, hospitali, mizani, Mahakama, maliasili na vilio vya wachimbaji.

Tayari Rais Magufuli ametenda yale ambayo aliyaahidi kwa Watanzania. Amebana matumizi ya serikali kwa kudhibiti safari zisizo na tija, matumizi yasiyo ya lazima, ameshughulikia watumishi wazembe, ameshughulikia mafisadi ndani ya serikali na kutoa elimu ya bure.

 Alivyoanza kazi
Mara tu baada ya kuingia ofisini, alimuapisha Mwanasheria Mkuu, George Masaju aliyemteua muda mfupi tu baada ya kuapishwa.

Katika siku zake hizo za mwanzo, alitumia mtindo wa kufanya ziara za kushtukiza katika taasisi mbalimbali za Serikali pamoja na kukemea viongozi wazembe na wanaoendekeza ufisadi na rushwa serikalini.

Mtindo wake huo, ukatumiwa pia na watendaji wengine wa Serikali wakiwamo mawaziri na wakuu wa mikoa na wengine.

Katika siku zake hizo za mwanzo, Rais Magufuli pia alifanya mabadiliko makubwa Ikulu kwa kufuta baadhi ya vitengo, kikiwamo cha lishe na benchi la wageni na kuagiza wananchi wote wenye matatizo waanzie ngazi za chini.
 
Atoa Msimamo wake
Novemba 7, mwaka jana akiwa Ikulu, Dar es Salaam, alikutana na watumishi wa Serikali ikiwa ni pamoja na manaibu katibu wakuu, manaibu wakuu na watendaji wakuu wa Serikali.

Katika kikao hicho, aliwataka kujiandaa kufanya kazi kwa ufanisi katika Serikali ya awamu ya tano chini yake. huku akiwasisitiza juu ya dhamira yake ya kuendeleza kaulimbiu yake ya “Hapa kazi tu”.

Kikao hicho pia kiliudhuriwa na Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Profesa Benno Ndulu na aliyekuwa Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Rished Bade ambapo alitoa mwelekeo wa Serikali anayoitaka.

Afuta Safari za Nje
Rais Magufuli alitumia kikao hicho kutangaza kufuta safari zote za nje ya nchi hadi hapo atakapolitolea suala hilo uamuzi mwingine, na kueleza shughuli zote zinazotakiwa kufanywa nje ya nchi zifanywe na kusimamiwa na mabalozi wa Tanzania wanaowakilisha nchi.

Alisema mtumishi atasafiri nje iwapo kutatokea jambo la dharura, na lazima kibali kitolewe na yeye, Katibu Mkuu Kiongozi au Makamu wa Rais.

Badala yake aliwataka watendaji hao kufanya zaidi ziara za kwenda vijijini ili kuzijua na kutatua kero za wananchi.

Hadi sasa, Rais Magufuli bado hajakwenda safari yoyote ya nje ya nchizaidi ya kuwatuma Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa kwenda kumwakilisha kwenye shughuli mbili tofauti.

Safari zake  ndani ya nchi
Novemba 20, mwaka jana, Rais Magufuli alisafiri kwa mara ya kwanza nje ya Dar es Salaam alipokwenda mkoani Dodoma ambako alifungua Bunge la 11.

Katika mkutano wake, Rais Magufuli alijikuta akisusiwa hotuba yake na wabunge wa upinzani waliokuwa wakipinga uteuzi wake na kutomtambua Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein kama rais halali, baada ya kufutwa matokeo ya Uchaguzi Mkuu wa Zanzibar.

Januari 12, mwaka huu, Rais Magufuli alisafiri kwa ndege ya kukodi kwenda Zanzibar ambako alihudhuria maadhimisho ya miaka 52 ya Mapinduzi ya Zanzibar.

Januari 21, mwaka huu alifanya ziara ya kwanza mkoani Arusha, ambako alikwenda pia katika Chuo cha Maofisa wa Kijeshi (TMA) Monduli kutunuku vyeo askari wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) baada ya kuhitimu mafunzo, huku naye akiwa amevalia sare za jeshi hilo.

Februari 5, mwaka huu pia Rais Magufuli alisafiri kwa gari kutoka Dar es Salaam kwenda mkoani Singida kuhudhuria maadhimisho ya miaka 39 ya Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Akataa sherehe ya kifahari Bungeni
Rais alionekana tofauti na viongozi wengine waliomtangulia baada ya kuifanya sherehe ya kuzindua Bunge kutokuwa ya kifahari na hivyo akaokoa Sh milioni 251, ambazo aliagiza zikanunue vitanda Hospitali ya Taifa Muhimbili.

Jumla ya vitanda 300, magodoro 300, viti maalumu vya wagonjwa 30, vitanda vya kubeba wagonjwa 30 na mashuka 1,695.

Afuta gwaride la Uhuru
Novemba 9, mwaka jana, Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Sefue, alitangaza kuwa Rais Magufuli aliamua kufuta shamrashamra za Sikukuu ya Uhuru na kwamba fedha zitakazookolewa atazipeleka sehemu nyingine.

Fedha Sh bilioni nne zilizopaswa kutumika kugharimia shamrashamra za Siku ya Uhuru, ambazo zingefanyika tarehe 9 Desemba 2015, Rais aliamuru zitumike kufanya upanuzi wa barabara ya Mwenge hadi Morocco jijini Dar es Salaam yenye urefu wa kilometa 4.3.

Baraza la Mawaziri
Desemba 10, mwaka jana, Rais Magufuli alitangaza baraza lake la mawaziri ambalo alianza kwa kuteua mawaziri 19, ingawa wizara ni 18. Mawaziri sita kati ya hao ni wanawake.

Katika uteuzi wake, aliacha wazi nafasi nne za uwaziri kwa madai alikuwa akitafuta watu watakaofaa kuteuliwa kuongoza wizara husika.

Wizara ambazo hakuteua mawaziri katika baraza lake la awali alilolitangaza ni Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi, Wizara ya Fedha na Mipango, Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano na Wizara ya Maliasili na Utalii.

Desemba 23, mwaka jana ikiwa ni siku 13 tangu alipotangaza Baraza la Mawaziri, Rais Magufuli alikamilisha baraza lake kwa kuwataja mawaziri wanne waliokuwa wamebakia.

Uteuzi wa Rais Magufuli umekuwa wa tofauti ambapo viongozi wengi aliowateua kushika nafasi mbalimbali ni wasomi wa ngazi ya uprofesa na udaktari.

Mabalozi Wapigishwa  Kiapo cha Utii
Katika mwendelezo wa kuhakikisha kuwa wale anaowateua wanakubaliana na kasi yake, Rais Magufuli aliwapa kiapo cha utii makatibu wakuu wa wizara na manaibu wao.

Akiwaapisha kiapo hicho aliwaeleza wazi kwamba yule atakayeshindwa kufanya kazi ni bora ajiondoe mwenyewe na kupisha wengine watumikie wananchi. 

Majipu 152  Yatumbuliwa
Ndani ya siku hizi 100  za  uongozi  wa  Rais  Magufuli, watumishi wa umma 152  wamefukuzwa  kazi  kutokana na kasoro mbalimbali za kiutendaji.

Hao ni watumishi waliotimuliwa kwa majina au vyeo vyao, lakini ukijumlisha na wengine waliosimamishwa au kufukuzwa kwa matamko bila kutajwa majina, idadi ni kubwa zaidi.

Watumishi hao wamesimamishwa na baadhi wamefukuzwa kazi kutokana na tuhuma mbalimbali za kukiuka Sheria ya Manunuzi ya Umma, Rais kutoridhishwa na utendaji wao, wizi kwenye taasisi zao, ukwepaji kodi, tuhuma za ubadhirifu wa fedha za umma na utovu wa nidhamu.

1.Muhimbili
Hatua za kusimamisha na kutimua zilianza siku nne tu baada ya Rais kuapishwa, ambapo Novemba 9, 2015 Kaimu Mkurugenzi wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH), Hussein Kidanto, alihamishwa na bodi iliyokuwa na wajumbe 11 ilivunjwa.

2.TRA
Rais Magufuli alimsimamisha kazi Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato (TRA), Rished Bade Novemba 27.

3.Bodi ya TPA
Desemba 7, mwaka jana, Magufuli alivunja bodi ya Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) pamoja na kutengua uteuzi wa Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi, Dk Shaaban Mwinjaka, Mwenyekiti wa Bodi ya Bandari, Profesa Joseph Msambichaka na Mkurugenzi Mkuu wa Bandari, Awadh Massawe.

Pia, aliwasimamisha kazi wasimamizi wanane wa Bandari Kavu (ICD). Jumla ya waliotimuliwa TPA na TRA ni watu 47.

4.Takukuru
Akiendelea na kasi yake, Desemba 16, 2015 Rais alitengua uteuzi wa nafasi nyeti ya Mkurugenzi wa Takukuru, Dk Edward Hoseah. Rais alisema alichukua hatua hiyo baada ya kutoridhishwa na utendaji wa Takukuru chini ya mkurugenzi huyo.

Maofisa wengine wa taasisi hiyo walisimamishwa kazi kwa kukiuka maagizo yaliyohusu safari za nje.

Waliosimamishwa kazi ni Mary Mosha, Ekwabi Mujungu, Doreen Kapwani na Rukia Nikitas, wakiwa watumishi waandamizi wa taasisi hiyo.

5.Rahco
Rais JPM alimsimamisha kazi Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni Hodhi ya Rasilimali za Reli Tanzania (Rahco), Benhadard Tito, Desemba 23, 2015 kwa kile kilichoelezwa ni “ukiukwaji mkubwa wa taratibu za ununuzi” katika mchakato wa utoaji wa zabuni ya ujenzi wa reli ya kati.

Pia alivunja bodi ya Rahco yenye wajumbe wanane na bodi ya TRL yenye wajumbe wanane pia.

6. Katibu Tawala Mwanza 
Akiendelea na kasi hiyo, Januari 15, alitengua uteuzi na kumfukuza kazi Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza, Faisal Issa kutokana na “utovu mkubwa wa nidhamu” aliounyesha katika kikao cha cha kamati ya ulinzi kilichofanyika mjini Mwanza. 

7.Idara ya Uhamiaji 
Rais Magufuli alimsimamisha kazi Kamishna Mkuu wa Uhamiaji, Sylvester Ambokile na Kamishna wa Uhamiaji anayeshughulikia utawala na fedha, Piniel Mgonja Januari 21 ili kupisha uchunguzi baada ya kubaini dosari kadhaa kwenye ofisi hiyo.

8.NIDA
Januari 25, Dk Magufuli alitengua uteuzi wa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (Nida), Dickson Maimu kutokana na matumizi yasiyoridhisha ya Sh179 bilioni.

Wengine waliosimamishwa Nida ni Joseph Makani ambaye ni mkurugenzi wa Tehama, Rahel Mapande (ofisa ugavi mkuu), Sabrina Nyoni (mkurugenzi wa sheria) na George Ntalima, ofisa usafirishaji.

Pia, aliwarudisha nyumbani mabalozi wawili, Dk Batilda Buriani aliyekuwa Japan, Dk James Msekela (Roma, Italia). Pia, Peter Kallaghe (Uingereza) na kurejeshwa Wizara ya Mambo ya Nje, Afrika Mashariki na Ushirikiano, Kikanda na Kimataifa.

                          Dunia nzima Yamkubali
Kutokana na kasi yake ya mabadiliko ya kweli ya uongozi wake, hasa kudhibiti matumizi na kuelekeza fedha katika huduma za kijamii, Rais Magufuli amekuwa gumzo kwenye anga za kimataifa.

Uongozi wake umeelezwa kuwa wa mfano, kwani miongoni mwa mambo anayoyafanya, yanagusa ulimwengu na anatekeleza yote bila kufanya safari yoyote ya nje ya nchi kama wanavyofanya viongozi wengine.

Tangu aingie madakarani, amedhibiti mabilioni ya fedha na kuzielekeza katika kuboresha huduma za afya, ikiwamo kuongeza upatikanaji wa dawa za kupunguza makali ya Ukimwi (ARV’s), ruzuku ya shule na miundombinu ya barabara.


                        Changamoto: Sakata  la  Zanzibar
Pamoja na yote, suala la kufutwa kwa Uchaguzi Mkuu wa Zanzibar limekuwa likiitesa Serikali ya Rais Magufuli.

Wakati Chama Cha Mapinduzi kikitaka uchaguzi huo urudiwe, Chama cha Wananchi (CUF) kimeendelea kushikilia msimamo wake kuwa hakitakubali marudio ya uchaguzi huo na hakitashiriki.

CUF wanaamini Rais Magufuli pekee ndiye anayeweza kumaliza mzozo huo ulioibuka visiwani humo, lakini kiongozi huyo hajazungumza lolote hadi hivi sasa tangu Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC), Jecha Salim Jecha alipotangaza kufutwa na kurudiwa kwa uchaguzi huo.

Kuendelea kuwako kwa mgogoro huo, ni wazi kwamba kunaitia doa Serikali ya Dk. Magufuli nje ya nchi.
                     

Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue akitoa taarifa ya siku 100 za kwanza za Serikali ya awamu ya tano Ikulu jijini Dar es salaam leo Ijumaa Februari 12, 2016

$
0
0

Tazama video hii ya Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue akitoa taarifa ya siku 100 za kwanza za Serikali ya awamu ya tano Ikulu jijini Dar es salaam leo Ijumaa Februari 12, 2016

TAKUKURU Yawafikisha Mahakamani Vigogo 11 wa Kampuni ya Reli (TRL)

$
0
0

Hatimaye vigogo 11 wa Kampuni ya Reli (TRL) waliosimamishwa kazi hapo awali wamepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu wakishtakiwa na makosa tisa yakiwemo matumizi mabaya ya madaraka yaliyopelekea manunuzi ya mabehewa mabovu 25 kinyume na utaratibu.

Washtakiwa hao ni pamoja na  Kipallo Aman Kisamfu  (Mtendaji Mkuu), Jasper Hurbert Kisiraga (Mkurugenzi Mkuu wa Ndani), Ngoso Joseph Ngosomwiles (Mhandisi Mkuu wa Mitambo), na Mathias Andrew Massae.

Wengine ni pamoja na Muungano Kaupunda, Paschal Mafikiri, Kedmon Mapunda, Felix Kashaigili, Lowland Simtengu, Joseph Syaizyagi, na Charles Ndege.

Akiwasomea mashtaka mbele ya Hakimu Mkazi Emillius Mchauru, Mwendesha mashtaka wa TAKUKURU, Maxilmillian Ari amesema washtakiwa walitenda makosa hayoa kati Januari 1, 2013 na Mei 31, 2014.

Maximillian alisema mshtakiwa wa kwanza Kipallo Kisamfu akiwa kama Mtendaji Mkuu alitumia vibaya madaraka yake kwa makusudi kwa kushindwa kuhakikisha mkataba wa tenda no. PA/113/2012-13/ME/G/OE/013 unatekelezwa kwa mujibu vigezo na masharti ya utoaji tenda na kukiuka kifungu cha 33(k) na 44(1) na (3) cha Sheria ya Manunuzi na kusababisha Kampuni ya M/S Hindustan Engineering and Industries Ltd kujinufaisha kutokana na mkataba huo.

Ilidawa pia kuwa mshtakiwa namba 6, Paschal Mafikiri akiwa kama Injinia Mkuu alitumia vibaya nafasi yake kwa kupitisha michoro na dizaini za mabehewa aina ya Ballast Hopper Bogie Wagons (BHB) iliyoandaliwa na Kampuni ya M/S Hindustan Ltd ambazo zilikuwa kinyume na vigezo na masharti ya mkataba katika tenda tajwa.

Mwendesha mashtaka wa TAKUKURU aliiambia mahakama kuwa washtakiwa wa pili na wa tatu (Jasper Kisanga na Mathias Massae), wakiwa kama Mhasibu Mkuu na Mhandisi Mkuu wa TRL, walitumia vibaya nafasi zao kwa makusudi kwa kuidhinisha malipo ya kiasi cha Dola za Marekani 1,280,593.75 kwenda Kampuni ya M/S Hindustan Ltd bila ya kuthibitisha ufanisi wa mabehewa 25 aina ya Ballast Hopper Bogie Wagons ndani ya muda wa uangalizi (warranty period), kinyume na Sheria ya Manunuzi.

Vilevile mshtakiwa wa 4, Muungano Kaupunda, akiwa kama Fundi Mkuu wa TRL alitumia vibaya nafasi yake kwa kuruhusu Kampuni ya M/S Hindustan Ltd kuanza utengenezaji wa mabehewa hayo 25 bila ya kujiridhisha kama vigezo na masharti vya utolewaji wa tenda hiyo vilifatwa kama inavyoainishwa na Sheria.

Kwa mujibu wa mwendesha mashtaka, washtakiwa wa 4,7,8,9 na 10 kama wajumbe wa kamati ya uthibitisho na huku wakijua wanatenda kosa walitumia vibaya nafasi zao kwa kushauri na kupendekeza Kampuni ya M/S Hindustan Ltd kushinda tenda tajwa kinyume na Sheria ya Manunuzi.

Washtakiwa wote walikana mashtaka yao na mshtakiwa 3, 4, na 11 walifanikiwa kupata dhamana baada ya kutimiza masharti ya kuwa na wadhamini wa kuaminika watatu watakaosaini dhamana ya Shilingi Milioni Kumi kila mmoja ikiwa ni pamoja na kuwasilisha hati zao za kusafiria mahakamani.

Washtakiwa wengine 8 walirudishwa rumande kwa kushindwa masharti ya dhamana huku wengine wakiwa hawana wadhamini kabisa hadi hapo kesi yao itakapotajwa tena Februari 25, mwaka huu.

Machi 21, 2013, TRL iliingia mkataba wa kununua mabehewa hayo aina ya Ballista Hopper Bogie (BHB) kutoka Kampuni ya M/S Hingustan Engineering and Industrial Limited ya nchini India kwa ajili ya kutumika katika uimarishaji wa njia za Reli ya Kati na yaliwasili Julai, 2014.

Hata hivyo, baada ya kuanza kazi yalilalamikiwa kuwa hayakuwa na ubora unaotakiwa na aliyekuwa Waziri wa Uchukuzi, Dkt. Harrison Mwakyembe aliunda kamati kwa ajili ya kuchunguza tuhuma hizo na kamati hiyo ilikabidhi ripoti yake Desemba 1, 2014 na Waziri huyo kuahidi kuishughulikia bodi ya zabuni ya TRL.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumamosi Ya Februari 13

Watu 20 Wafikishwa Mahakamani Kwa Kukatakata Mapanga Mbuzi Na Kondoo Mvomero

$
0
0

Wakulima 20 wamefikishwa mahakamani kujibu shitaka la kukatakata na kuua mifugo, huku mfugaji mmoja akitakiwa kujibu mashtaka matatu ya kuharibu mali, kulisha mifugo kwenye shamba la mpunga na kumshambulia mmiliki wa shamba.

Washitakiwa hao walifikishwa kwenye mahakama mbili tofauti; wakulima walipanda kizimba cha Mahakama ya Wilaya ya Morogoro, huku wafugaji wakisomewa mashtaka yao mbele ya Hakimu Ivan Msaki wa Mahakama ya Mkoa wa Morogoro.

Akisomewa mashtaka mbele ya Hakimu Mkazi, Regina Futakamba, wakili wa Serikali, Edger Bantulaki alidai kuwa Februari 8, wakulima hao kwa pamoja walikatakata mbuzi na kondoo wenye thamani ya Sh6,140,000 mali ya Ketepoi Nuru, mkazi wa kijiji cha Kambala wilayani Mvomero.

Hata hivyo, washtakiwa hao walikana mashtaka hayo na hivyo kurudishwa mahabusu kutokana na kushindwa kukamilisha masharti ya dhamana. Kesi yao itatajwa tena Februari 25.

Ili wapewe dhamna washtakiwa hao walitakiwa kuwa na wadhamini wawili wanaoishi mkoani Morogoro na kila mdhamini awe na kitambulisho pamoja na mali yenye thamani ya Sh3,070,000.

Mbele ya Hakimu Msaki, wakili huyo pia alimsomea mashtaka matatu Kasho Mereto, akidai kuwa alilisha mifugo kwenye shamba la mpunga na kuharibu mazao yenye thamani ya Sh300,000, kuharibu baiskeli na kumshambulia mmiliki wa shamba hilo, Rajabu Issa, mkazi wa kijiji cha Dihombo wilayani Mvomero.

Mfugaji huyo alikana shtaka na yuko nje kwa dhamana. Kesi hiyo itatajwa Februari 29.

Utafiti: Umaarufu Wa Lowassa Waporomoka, Magufuli Apaa

$
0
0

Matokeo ya utafiti mpya uliofanywa mapema mwezi huu yanaonyesha kuwa umaarufu wa Rais John Magufuli umeongezeka kufikia asilimia 74.5, akimuacha mbali mpinzani wake wa karibu kwenye Uchaguzi Mkuu, Edward Lowassa.

Magufuli alishinda mbio za urais kwenye Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 25, akipata asilimia chache kuliko wagombea wengine kutoka CCM, lakini amejiongezea umaarufu kutokana na hatua ambazo amekuwa akichukua tangu alipoapishwa Novemba 5, 2015.

Katika uchaguzi huo, Dk Magufuli alipata kura milioni 8.8 sawa na asilimia 58.47, akifuatiwa na Lowassa aliyepata kura milioni 6.07, sawa na asilimia 39.97.

Lakini utafiti huo uliofanywa na taasisi ya Ms Infotrak Researc and Consultant na Ms Midas Touche East Africa kwa kuwahoji watu 1,200 wenye umri wa zaidi ya miaka 18 katika kanda sita na mikoa 15, unaonyesha kuwa Magufuli ameongeza umaarufu kwa takriban asilimia 20, huku Lowassa akishuka kwa asilimia 20 pia.

Katika utafiti huo, Lowassa anaonekana kushuka hadi asilimia 20.1.

Wengine waliotajwa katika orodha hiyo ni Anna Mghwira aliyepata asilimia 1.1, Hashimu Rungwe (0.4), Fahmi Dovutwa (0.2), Lutalosa Yemba (0.1), Janken Kasambala (0.1) na Machmillan Lyimo aliyepata asilimia 0.0. Asilimia 3.5 ya walioulizwa swali hilo walikataa kujibu.

Vilevile, wananchi walipouliza iwapo Uchaguzi Mkuu ukifanyika leo wangemchagua nani kati ya makada waliojitokea kugombea urais mwaka jana, wengi wamemtaja Magufuli.

Matokeo hayo yanaonyesha kwamba wanawake wengi ndiyo wanamuunga mkono Magufuli ikilinganishwa na wanaume. 

Asilimia 77.9 ya wanawake wanasema wapo tayari kumchagua tena kuwa Rais iwapo kutakuwa na uchaguzi mpya, wakati wanaume wanaosema hivyo ni asilimia 71.5 pekee.

Kinyume na ilivyo kwa Magufuli, utafiti umebaini kwamba Lowassa anapendwa zaidi na wanaume huku asilimia 22.6 wakisema wapo tayari kumchagua kuwa rais. Ni asilimia 17.4 ndiyo wametoa maoni kama hayo kwa Magufuli.

Kwa upande wa kanda; Kanda ya Zanzibar ndiyo inayoongoza kwa ‘kumkubali’ Magufuli ikiwa na asilimia 91.6, ikifuatiwa na Kanda ya Kati yenye asilimia 81.6, Kanda ya Kaskazini (77%), Kanda ya Pwani (72.7) na Kanda ya Ziwa asilimia 67.6.

Alipoulizwa kuhusu matokeo ya utafiti huo, mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Mzumbe, Profesa George Shumbuso alisema kuongezeka kwa umaarufu wa Rais Magufuli kunatokana na utendaji wake kugusa kero za wanyonge.

Alisema Watanzania wengi hata wale waliokuwa wakiunga mkono vyama vya upinzani, wameanza kukubaliana na Magufuli kutokana na namna alivyoweza kufanya mambo makubwa na yenye umuhimu kwa Taifa ndani ya muda mfupi.

“Hakuna Rais aliyefanya mambo makubwa namna hii ndani ya siku 100 ndiyo maana wanyonge wameonekana kumkubali kwa sababu amegusa na kuonyesha wazi nia ya kumaliza changamoto zao,” alisema.

“Hata ikitokea uchaguzi ukafanyika sasa nina uhakika Magufuli atashinda kwa sababu wananchi wamebaini wazi kuwa anachokizungumza ndicho anachomaanisha. Si siasa kama ambavyo imezoeleka kwa wanasiasa wengine.”

Kauli hiyo iliungwa mkono na mwenyekiti wa Tanzania Labour Party na mbunge wa zamani wa Vunjo, Augustine Mrema aliyesema kuwa Watanzania walifanya uchaguzi sahihi kumuweka Magufuli madarakani.

Alisema katika kipindi cha siku 100 kiongozi huyo amefanya miujiza ambayo hakuna Mtanzania ambaye alifikiria kuwa ingeweza kufanyika.

Watu 7 Wafikishwa Mahakamani Kwa Kuvunja Ofisi Ya TRA Makao Makuu Na Kuiba Kompyuta

$
0
0

Watu saba, wakiwamo walinzi wawili wa Suma JKT, wamefikishwa Mahakama ya Wilaya ya Ilala kujibu mashtaka matatu ya kuvunja ofisi ya Makao Makuu ya Mamlaka ya Mapato nchini (TRA) na kuiba kompyuta na runinga.

Washtakiwa hao wanadaiwa kuiba kompyuta aina ya Dell na televisheni moja aina ya Samsung vyenye thamani ya Sh4.2 milioni mali ya TRA.

Mwendesha mashtaka wa Serikali, Hilda Kato aliwataja washtakiwa hao kuwa ni Joseph Kaitila (24) na Hussein Komba (25) ambao ni walinzi wa Suma JKT, ambalo ni shirika la uzalishaji mali la Jeshi la Kujenga Taifa (JKT). 

Wengine ni Iman Litonto, ambaye ni mfanyabiashara Rajabu Libila (33), Vedasto Mkude (56), mkazi wa Yombo Vituka na madereva, Omary Dikachite (30) na Jumanne Maulid (36).

Akisoma hati ya mashtaka mahakamani hapo, Wakili Kato alidai katika shtaka la kwanza, Januari 19 mwaka huu washtakiwa kwa pamoja walikula njama za kutenda kosa na shtaka la pili washtakiwa hao walivunja ofisi ya Makao ya TRA iliyopo Mtaa wa Sokoine Drive Inn na la tatu ni kuiba vifaa hivyo.

Washitakiwa hao walikana mashtaka hayo na Hakimu Mkazi Flora Mjaya aliahirisha kesi hiyo hadi Februari 25.

Washtakiwa sita walirudishwa rumande baada ya kushindwa kutimiza masharti ya dhamana.

AKA & Diamond Platnumz – Make Me Sing (Official Video)

$
0
0
Heavy collaboration alert, South Africa meets East Africa as one of South Africa’s finest rappers – AKA linked up with Tanzania’s finest – Diamond Platnumz on “Make Me Sing”, the video was  shot on location in Johannesburg, South Africa
 
Enjoy!

Mwanamke Aliyemkaba Jambazi Na Kumpora Bunduki Aina Ya SMG Azawadiwa Laki 5 Na Jeshi La Polisi

$
0
0
Mwanamke aliyepambana na jambazi na kufanikiwa kumnyang’anya bunduki aina ya SMG, Sophia Manguye (46), amepewa zawadi ya Sh 500,000 na Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu Tarime/Rorya, Gemini Mushy.

Mwanamke huyo ambaye aliomba Serikali kumpa silaha ili kujilinda, alisema kuwa hajaridhika na zawadi hiyo kwa kuwa kama asingemmudu jambazi huyo watu wengi wangepoteza maisha.

Hata hivyo, Mushy alimwomba Manguye kupokea kiasi hicho japokuwa ni kidogo kwa kuwa ni zawadi kutoka ofisi yake.

Tukio hilo lilitokea Februari 9, saa 2.42 usiku, baada ya watu watatu kufika dukani kwake, mmoja wao akiwa na bunduki kisha kumwamuru atoe fedha alizokuwa nazo.

Manguye alisema alichukua Sh80,000 alizokuwa nazo na kumkabidhi jambazi huyo, lakini hakuridhika na kumlazimisha aongeze kiasi kingine.

“Nilipandwa hasira nikanyanyuka wakati jambazi anainama kuangalia kwenye kiboksi cha fedha, nikamkamata kifuani na kung’ang’ania mkanda wa bunduki, akaanza kunivuta kwenda nje, nami nikamvutia ndani, lakini alifanikiwa kunitoa nje akaniangusha chini, lakini sikuachia mkanda wa bunduki,” alisema Manguye na kuongeza:

“Aliposikia wananchi wameanza kupiga yowe akaniachia na kutoa mkanda wa silaha begani, akakimbia na kuniachia bunduki. Wakati huo huo jambazi mwingine alikuwa amekamatwa kwenye duka la Zaituni Magasi, wananchi walipofika wakaanza kumshambulia, wakati huo taarifa ilikuwa tayari imetolewa Kituo cha Polisi Sirari, wakafika kumchukua,” alisema.

Hii ni mara ya pili kwa Manguya kuvamiwa na majambazi wenye silaha, ambapo mwaka 2014 alivamiwa dukani kwake na majambazi waliokuwa na bunduki, lakini alifanikiwa kumpiga kwa kigoda aliyekuwa na bunduki na alianguka chini.

Magasi alisema wakati wa tukio hilo, alikuwa amevamiwa na majambazi waliokuwa na bunduki, mapanga na nondo.

“Wakati anatoka mvunguni mdogo wangu alimkamata kwa nyuma na kummudu huku akipiga kelele, watu wakafika wakaanza kumpiga hadi akazimia, polisi walipofika wakamwokoa kwani kidogo wamuue,” alisema. 

ZEC Yagoma Kuondoa Picha ya Maalim Seif Kwenye Karatasi za Kura........CUF Yasema Ipo Tayari Kwa Mazungumzo ila Sio Kurudia Uchaguzi

$
0
0
Zikiwa  zimebaki siku chache kabla ya kurudiwa kwa uchaguzi Zanzibar, Makamu wa Kwanza wa Rais Maalim Seif Sharrif Hamad amehoji sababu za chama tawala, CCM kuhofia CUF kuongoza visiwa hivyo.

Maalim Seif, ambaye aligombea urais wa Zanzibar katika uchaguzi wa Oktoba 25 ambao matokeo yake yalifutwa, pia amesema endapo CCM itasitisha uchaguzi huo uliopangwa kufanyika siku 36 zijazo, CUF watakuwa tayari kufanya mazungumzo lakini si kwa wakati huu ambao maandalizi ya kupiga kura yanaendelea.

Akizungumza na waandishi wa habari jana, katibu huyo mkuu wa CUF aliitoa hofu CCM kuwa chama chake hakina ajenda ya kulipiza kisasi.

Matokeo ya uchaguzi wa Rais wa Zanzibar, wawakilishi na madiwani yalifutwa na Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi (ZEC), Jecha Salum Jecha siku ambayo chombo hicho kilitakiwa kumtangaza mshindi, na mwezi uliopita alitangaza Machi 20 kuwa siku ya uchaguzi wa marudio visiwani humo.

Wakati CUF ikipinga vikali kufutwa matokeo na kutangaza tarehe mpya, Serikali imesema kuna nafasi ya kufanya mazungumzo kabla ya uchaguzi wa marudio kwa kuwa kuna muda  mrefu wa kufanya hivyo.

Jecha alitangaza uamuzi huo wakati tayari matokeo ya urais ya majimbo 31 yalishatangazwa, na ya majimbo tisa yaliyosalia yalishahakikiwa, huku washindi wa viti vya uwakilishi na udiwani wakiwa wametangazwa na kupewa vyeti vya ushindi. 

“Sijui kwa nini CCM wanaogopa sisi tukiongoza?” alihoji Maalim Seif kwenye mkutano huo na waandishi akiwa pamoja na aliyekuwa mgombea urais wa Jamhuri ya Muungano kwa tiketi ya Chadema, Edward Lowassa.

“Wana wasiwasi gani, kwamba CUF ikiongoza kutatokea nini? Sisi hatuna ajenda ya kulipiza kisasi,” alisema.

Katika mkutano huo, Maalim Seif mbaye pia ni katibu mkuu wa chama hicho alisema kama CCM ina wasiwasi na idadi ya wajumbe wa Baraza la Wawakilishi kwenye Serikali ya Umoja wa Kitaifa (SUK), haina budi kuondoa shaka kwa kuwa idadi kwa pande zote inakaribiana.

“Hawa wanahisi hawatapata uwakilishi mkubwa, lakini mbona miaka yote tunakuwa na idadi isiyopishana ya wawakilishi?” alihoji.

Kuna Vitisho  Zanzibar 
Katika mkutano huo, Maalim Seif alisema kumekuwapo vitendo vya wananchi kupigwa na vikundi vya watu wasiojulikana. 

Alidai wafanyakazi wa Serikali na taasisi zake wameamrishwa kupeleka vitambulisho vyao vya kazi na vya kura serikalini ili vikahakikiwe.

“Hii si mara ya kwanza wafanyakazi wa Serikali kutakiwa kupeleka vitambulisho, sisi tunajua kuwa wanataka wawatishe kuwa watajua nani kapiga kura na nani hajapiga,” alisema na kusisitiza:

“Hii ni kama kitisho cha kuwalazimisha wakapige kura, zaidi hasa hizo ni dhuluma ambazo wananchi wanafanyiwa.”

Kadhalika Maalim Seif alizungumzia uwapo wa watu wanaovaa soksi usoni na kuwashambulia raia, akisema Serikali haijachukua hatua stahiki kudhibiti hali hiyo.

Alisema watu hao ambao wamepachikwa jina la mazombi, wamevamia maeneo kadhaa kama Baraza la CUF, Jang’ombe na yaleambayo yana wafuasi wa chama hicho kikuu cha upinzani visiwani humo.

“Wanawapiga watu, wanawajeruhi na wanaiba mali, lakini inashangaza sana mambo haya na si Serikali wala polisi iliyochukua hatua,” alisema.

Maalim Seif alisema amezungumza na Rais wa Zanzibar, Dk Ali Mohamed Shein kuhusu matukio hayo ya uharamia wanaofanyiwa wananchi, lakini hakuna hatua zinazochukuliwa.

Alisema CCM wanatafuta sababu ili machafuko zaidi yatokee visiwani humo wapate kisingizio.

Aliwataka wafuasi wa CUF kuvumilia hali hiyo ili nchi isiingie kwenye machafuko kama yaliyotokea mwaka 2000, wakati watu zaidi ya 20 waliuawa na wengine kukimbilia Shimoni, Mombasa nchini Kenya ambako waliishi kama wakimbizi.

 Lowassa Azungumza
Kwa upande wake, Lowassa aliwataka viongozi wa ngazi za juu wachukue   hatua kumaliza mgogoro wa Zanzibar.

“Hili tulichukulie kwa umakini sana. Viongozi wafanye vikao vya maridhiano, tunaipenda sana amani tuliyonayo,” alisema.

Lowassa alisema anashangazwa na jinsi CCM wanavyoshindwa kuheshimu makubaliano ya SUK na kukataa kukubali matokeo. 

ZEC  yagoma  kuondoa  picha  ya  Maalim 
Wakati huohuo, habari zinaarifu kuwa Tume  ya  Uchaguzi  Zanzibar( ZEC)  imegoma  kuondoa  picha  za  wagombea  Urais,Udiwani  na Uwakilishi  kutoka  vyama  vilivyotangaza  kutoshiriki  uchaguzi  wa  marudio,ikiwemo  jina  na  picha  Maalim Seif Sharif Hamad.

Hilo  lilifahamika  jana mjini Unguja  baada  ya  kigogo  mmoja  wa  ZEC ambaye  hakuwa  tayari  kutaja  jina  kusema  kuwa  sheria  hazimruhusu  mgombea  yeyote  kujitoa  mwenyewe  kwa  utashi  wake  binafsi.

Kiongozi  huyo  alisema  kwa  mujibu  wa  kifungu  cha  36  cha  sheria  ya  uchaguzi  namba  11  ya  mwaka  1984,mgombea  hawezi  kujiondoa  kwa  utashi  wake  baada  ya  Tume  kukamilisha  kazi    ya  uteuzi  ambayo  ilifanyika  kabla  ya  Oktoba  25  mwaka  jana.

"Ieleweke  kwamba mgombea  urais  anaweza  kujiondoa  katika  kinyang'anyiro  kwa  kuwasilisha  taarifa  za  maandishi  yeye  mwenyewe  ofisi  za  ZEC  kabla  ya  saa 10  jioni  ya  siku  ya  uteuzi." Alisema  ofisa  huyo  akinukuu  kifungu  cha  katiba.

Alisema  uteuzi  wa  mgombea  mwingine  unaweza  kufanyika  ndani  ya  siku 21  kama  mgombea  hatafariki dunia,lakini  hakuna  ruhusa  ya  kujitoa  kabla  ya  kukamilika  kwa  uchaguzi.

Alisema  ZEC  tayari  imeviandikia  vyama  kuvitaka  vithibitishe  iwapo  wagombea  wao  wangali  hai  au  kuna  waliofariki dunia, na si kutaka  kufahamu  kama  watashiriki  uchaguzi  wa  marudio  au  la.

Mkurugenzi  wa  Mipango  na  Uchaguzi CUF  anena
Mkurugenzi  wa  Mipango  na  Uchaguzi  wa  CUF, Omar Ali Shehe  amesema  ZEC  inasuka  mkakati  wa  siri  wa  kutaka  kuzitumia  picha  na  taarifa  za  wagombea wao  kwa  lengo  la  kuidanganya  dunia  na  jumuiya  za  kimataifa  kwamba  CUF  walishiriki  uchaguzi  huo.

Shehe  amesema  CUF  kilitangaza  mapema  kabisa  kutoshiriki  uchaguzi  wa  marudio,hivyo  dunia  nzima  inaelewa  kabisa  kwamba  CUF  haishiriki  uchaguzi  huo  na  kitendo  cha  kuendelea  kuchapisha  picha  na  taarifa  za  wagombea  wao  katika  karatasi  za  wapiga  kura  si  sahihi.

Mufti Mkuu wa Tanzania Sheikh Abubakar Zuberi bin Ally Aruhusiwa kutoka hospitali....Aitaka Serikali iboreshe hospitali za ndani

$
0
0
Mufti wa Tanzania, Sheikh Abubakary Zubeir, ameitaka Serikali iweke mikakati thabiti ya kuzipa uwezo hospitali za ndani ili kupunguza gharama kwa Watanzania wengi kwenda kutafuta matibabu nje ya nchi.

Mufti aliyasema hayo jana muda mfupi baada ya kuruhusiwa kutoka katika Hospitali ya Taifa Muhimbili, Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete alikokuwa amelazwa kwa takribani wiki moja akipatiwa matibabu.

Alisema kuna haja ya hospitali kubwa kama Muhimbili kuangaliwa kwa jicho la tatu ili iweze kutoa huduma za kimataifa, hilo litawezekana endapo kutakuwa na vitendea kazi vya kutosha na madaktari kufanya kazi katika mazingira mazuri.

Mufti alisema kwa kufanya hivyo Watanzania watarudisha imani kwa hospitali za nyumbani na madaktari wake, tofauti na hali ilivyokuwa miaka ya karibuni ambapo wengi walikuwa wakikimbilia nje ya nchi kwa ajili ya kutafuta matibabu.

“Binafsi nilikuwa siamini kama naweza kutibiwa hapa nchini, tayari nilishakata tiketi kwa ajili ya kwenda nje ya nchi lakini nashukuru Mungu siku moja kabla ya safari nilihakikishiwa kwamba naweza kupata matibabu hapa.

“Niwasihi Watanzania wenzangu kuamini kwamba Tanzania nayo tuna madaktari bingwa wengi ambao wanafanya kazi nzuri, muhimu kwa Serikali ni kuwaboreshea mazingira ya kufanya kazi,”alisema Sheikh Zubeir 
Kwa upande wake Waziri wa Afya,Ustawi wa Jamii, Jinsia na Watoto, Ummy Mwalimu alisema ni matarajio ya Serikali kuona viongozi wote wanatibiwa hospitali za nyumbani, jambo litakalowashawishi Watanzania wengine kuamini huduma zinazotolewa.

Alisema kwa viongozi wakubwa kama Mufti kutibiwa nchini kumewasukuma kuongeza vifaa na huduma bora zaidi, ili kuifanya Muhimbili kuwa miongoni mwa taasisi zinazoheshimika.

“Kama Mufti ametibiwa hapa nyumbani kuna sababu gani ya kupeleka watu nje, kwa sasa tumepata hamasa ya kuongeza vitendea kazi na huduma, ili Muhimbili iendelee kuheshimika na ivuke mipaka itoe huduma ndani na nje ya nchi,” alisema Mwalimu 
Akitoa salamu za Bakwata Katibu Mkuu wa Baraza hilo, Suleiman Said Lolila alimshukuru Rais John Magufuli kwa kufanikisha matibabu ya Mufti.

“Madaktari wamefanya kazi kubwa tuna kila sababu ya kushukuru kwa hilo na Watanzania wote kwa ujumla kwa dua zao hatimaye leo Mufti ameruhusiwa kurudi nyumbani,” alisema Lolila 

 Waziri wa Afya na Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu akimualika Mufti Mkuu Sheikh Abubakar Zuberi bin Ally kuongea na wanahabari katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI iliyopo Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) baada ya madaktari kumruhusu kurejea nyumbani baada ya afya yake kuimarika.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images