Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Raia wa Kigeni Waushika Uchumi wa Tanzania......Ni 10% Tu Ya Watanzania Wanaomiliki Uchumi wa Nchi, Serikali Yatangaza Mkakati Kuokoa Jahazi

$
0
0

WAZIRI Mkuu Kassim Majaliwa, amesema serikali ya awamu ya tano inafanya kila juhudi kuhakikisha uchumi wake unamilikiwa na wananchi, nia ikiwa ni kuifanya nchi kuwa na uchumi wa kati.

Majaliwa aliyasema hayo jana, wakati akizindua mpango wa uwezeshaji wananchi kiuchumi, ambao pamoja na mambo mengine utatoka na mapendekezo ya nini cha kufanya kufikia malengo yake.

Kwa mujibu wa waziri mkuu, ili kufikia malengo ya mkakati huo, wadau wote hawana budi kuunganisha nguvu pamoja kuanzia ngazi ya juu hadi chini.

“Taarifa zilizopo zinaonyesha ni asilimia 10 tu ya Watanzania ndio wanaomiliki uchumi wa nchi na sera hiyo ndiyo inatoa mwongozo wa jumla unaohakikisha kwamba wananchi wanapata fursa mbalimbali za kiuchumi ambazo zitawawezesha kujenga na kufaidika na uchumi wa mchi yao,” alisema.
 
Aidha alizitaja mojawapo ya nyenzo muhimu katika kufanikisha suala hilo ni pamoja na uhakika wa masoko, riba nafuu kwa wajasiriamali, pamoja na ushirikishwaji wa viongozi wote.

“Napenda mkimaliza mkutano wenu mnipatie mapendekezo ya kile mlichokubaliana hapa, kwani nimekuwa na utaratibu kila nikifanya ziara zangu mikoani lazima nizungumze na wananchi na huwa nawaeleza haya masuala ya mipango ya serikali katika kuwawezesha,” alisema waziri mkuu.

Awali akimkaribisha waziri mkuu, Waziri wa Nchi Ofi si ya Waziri Mkuu Sera, Uratibu, Bunge, Uwezeshaji, Ulemavu Vijana na Wazee, Jenister Mhagama, alisema kuwa kuwawezesha wananchi ni hatua muhimu katika maendeleo ya taifa.
 
Katika kufanikisha azma hiyo, Waziri Jenister alisema tayari serikali imefanikiwa kutenga maeneo maalumu ya uwekezaji, ambapo vijana na wananchi kwa ujumla watapewa kipaumbele zaidi.

“Mikoa 20 tayari imeshatenga maeneo na sasa wanaweka miundombinu ambayo nia yake ni kuwasaidia wananchi kuweza kumiliki uchumi wao,” alisema.

Hatahivyo mojawapo ya changamoto inayokabili utekelezaji wa sera ya uwezeshaji wananchi kiuchumi ni ukosefu wa ajira na umasikini, ambavyo vinalikabili kundi hili muhimu.

Imeelezwa kuwa maeneo ambayo yanatajwa kama sehemu muhimu zenye kuwezesha kupatikana kwa matokeo ya haraka ni sekta ya utalii, ujenzi, usafirishaji, kilimo, madini, misitu na viwanda.

Mramba Afunguka Kuhusu Maisha Ya Gerezani.....Aishauri Serikali Kuwatumia Wafungwa Wenye Utaalumu Badala Ya Kuwarundika Gerezani

$
0
0

Aliyekuwa  Waziri wa Fedha katika Serikali ya awamu ya tatu, Basil Mramba, ameishauri Serikali kuhakikisha inawatumia wafungwa kutumikia jamii badala ya kuwarundika magerezani.

Amesema pamoja na hayo, maisha ya gerezani si salama na si njia pekee ya kumrekebisha mhalifu aliyehukumiwa na mahakama.

Kutokana na hali hiyo, alisema kuna haja kwa Serikali kuanza kutumia sheria namba 6 ya huduma kwa jamii kuwaangalia wafungwa wenye taaluma kutumika adhabu zao katika fani au taasisi za umma ili kupunguza gharama kuwahudumia watu ambao wanaweza kuisaidia jamii.

Mramba alitoa kauli hiyo jana, wakati yeye na mwenzake aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini, Daniel Yona, walipomaliza kufanya usafi katika Hospitali ya Sinza Palestina, Dar es Salaam, ikiwa ni sehemu ya kutumikia adhabu ya kifungo chao cha nje baada ya wiki iliyopita Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuridhia kuwa wanastahili kutumikia jamii kwa kipindi cha miezi sita hadi Novemba 5.

Alisema imekuwa ni kawaida jamii kuwa na mtazamo kwamba mtu yeyote anayekutwa na hatia lazima atapelekwa jela ajirekebishe na kuacha tabia aliyonayo jambo ambalo si sahihi.

“Jamii inaamini jela ni sehemu salama na mtu akishikwa na hatia kwa kosa lolote, mahala sahihi ni jela tu, kule anakutana na watu wa kila aina, wenye makosa tofauti, hali ambayo inamfanya ajifunze mambo mengine mapya.

“Unakuta mtu amefanya uhalifu wa kuiba kitu, anafungwa na kupelekwa gerezani, anakutana na majambazi sugu wanaompa mbinu zaidi, sasa akitoka jela anakuja akiwa ameiva, anarudia kwenye matukio akiwa amekamilika,” alisema Mramba.

Alisema kuwapeleka wafungwa katika huduma za kijamii kutasaidia kupunguza gharama kwa Serikali na msongamano ndani ya magereza.

Akizungumzia suala la kuwatumia wafungwa ambao ni wanataaluma, Mramba alisema sheria hiyo ikitumika vizuri italisaidia taifa kwani wapo baadhi ya wafungwa wana taaluma ya udaktari, ualimu, ufundi na uhasibu, ambao wanaweza kutumika katika fani zao kwenye taasisi za umma.

“Kuna maeneo mengine yana uhaba wa wataalamu ambao wengine wapo magerezani wanahudumiwa na Serikali kuanzia chakula, malazi na hata afya zao, hivyo wakiwatumia hao itakuwa faida kwa taifa kwa kuwa watafanya kazi bila malipo,” alisema Mramba.

Alisema suala la kuwatumia wafungwa katika huduma za kijamii si geni kwa nchi zilizoendelea ambako kwa kiasi kikubwa wamesaidia kuinua uchumi wa nchi zao.

Kwa siku ya jana, Mramba na Yona walianza kufanya usafi saa 2 asubuhi kwa kufagia nyuma ya jengo la wazazi katika hospitali hiyo.

Naye Ofisa Huduma za Jamii Mkoa wa Dar es Salaam, Deogratius Shirima, alisema gharama zinazotumika kuwahudumia wafungwa magerezani ni kubwa, hivyo ni vyema wale wanaoguswa na sheria ya huduma za jamii namba 6 ya mwaka 2002 kutumikia kifungo cha nje.

“Sheria hii ni vyema ikatumika kwa wale inaowagusa kwani itapunguza gharama za kuwahudumia magerezani, na pia adhabu wanayopata wafungwa wa nje ni wazi jamii ambayo ndiyo iliyokosewa inaona utekelezaji wake kwa uwazi,” alisema Shirima.

Alisema mataifa mengine ikiwamo nchi ya Kenya wanatumia sheria hiyo ambapo nusu ya wafungwa nchini humo wapo katika huduma za jamii.

Februari 6, mwaka huu mawaziri hao walibadilishiwa adhabu ya jela na kupewa adhabu ya kutumikia kifungo cha nje mwishoni mwa wiki iliyopita na Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, baada ya kukamilika kwa mchakato wa kufikia hatua hiyo.

Hakimu Mfawidhi wa Mahakama hiyo, Cyprian Mkeha, alisema sheria ya huduma kwa jamii namba 6 kifungu namba 3(1) ya mwaka 2002 inasema mtu yeyote anayetiwa hatiani kwa kosa ambalo adhabu yake ni miaka mitatu kushuka chini mahakama inaweza kumpa adhabu ya kutumikia jamii.

Mramba na Yona, ambao baada ya rufaa walibakiwa na adhabu ya miaka miwili, walitiwa hatiani kwa kutumia madaraka vibaya ambapo walitakiwa kumaliza kifungo Novemba mwaka huu.

Hata hivyo, hakimu huyo alisema magereza walifikisha barua mahakamani hapo Desemba 5, mwaka jana yenye kumbukumbu namba 151/DAR/3/11/223, wakipendekeza kifungo cha nje kwa mawaziri hao.

Hakimu Mkeha alisema baada ya kupokea barua hiyo, mahakama iliamuru watu wa huduma za jamii kuchunguza kama wanastahili kupewa adhabu hiyo na kwamba walifanya hivyo na kurudisha ripoti kwamba wanastahili.

Alivitaja vigezo vya kupewa adhabu hiyo kuwa ni umri ambapo Mramba na Yona wana miaka 75.

Serikali yabaini wizi wa takribani Milioni 700 ATCL....Mkurugenzi wa Fedha wa Shirika Hilo Bw.Steven Kasubi Asimamishwa Kazi Kupisha Uchunguzi

$
0
0

Serikali imebaini wizi wa  takribani  shilingi Milioni 700 katika Shirika la Ndege Tanzania (ATCL) kupitia kampuni ya Wakala wa ukatishaji tiketi ya Salama World Travel iliyopo visiwa vya Komoro.

Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam ,Waziri wa Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano Prof.Makame Mbarawa ameeleza kuwa  wizi huo umefanywa kwa kushirikiana na wafanyakazi wa shirika hilo.

“Kufuatia upotevu huo Serikali  imechukua hatua thabiti ikiwemo kumsimamisha kazi Mkurugenzi wa Fedha wa ATCL Bw.Steven Kasubi ili kupisha uchunguzi utakaofanywa na kikosi  cha polisi  kitengo cha usalama mtandaoni  ili kubaini mtandao mzima uliohusika  ” alisema Prof.Mbarawa.

Aidha aliongeza kuwa kwa utaratibu wa kawaida wa  shirika hilo wakala anapewa ruhusa ya  kuuza tiketi za ndege kuanzia kiasi cha shilingi milioni 15 tu na pale anapomaliza mauzo anarudisha fedha kwa shirika na baadaye kupewa ruhusa tena.

Prof.Mbarawa anasema kwa sasa wameanza na shirika la Ndege la Tanzania kwa kwa lengo la kulifufua kwa kununua ndege mpya na kuwa na wafanyakazi wachapakazi na waadilifu.

“Siku mbili zilizopita nilifanikiwa kukutana na menejimenti ya ATCL na kubaini mapungufu mengi na hivyo kuamua kuyafanyia kazi kwa kuhakikisha shirika hii linarudi kutenda kazi kwa udhabiti kwa kuwashughuikia wale wote wanaoenda kinyume na maadili ya utumishi wa umma” alisema Prof.Mbarawa.

Vilevile aliongeza kuwa Serikali imemuagiza  Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali(CAG) kufanya uchunguzi kwa mawakala wengine wote wa Shirika hilo kubaini kama fedha za uuzaji wa tiketi hizo zinarudishwa kama inavyotakiwa.

Prof.Mbarawa ametoa wito kwa wananchi kuachana na wizi kwa  njia ya mtandao kwa kuwa sheria ya mtandao iliyoanzishwa mwaka jana inatumika katika kuhakikisha kuwa watuhumiwa wanafikishwa katika mkondo wa sheria na kuchukuliwa hatua stahiki.

Rais Magufuli Amjulia Hali Mufti Mkuu Wa Tanzania Pamoja Na Kufanya Ukaguzi Wa Kushtukiza Katika Wodi Ya Wazazi Ya Hospitali Ya Taifa Ya Muhimbili

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ametembelea kwa ghafla wodi ya Wazazi katika Hospitali ya Taifa Muhimbili Jijini Dar es salaam, na kujionea hali ya msongamano mkubwa wa wazazi uliosababishwa na uhaba wa vitanda na nafasi finyu katika wodi hiyo.
 
Rais Magufuli aliyekuwa akitoka katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete alikokwenda kumuona na kumjulia hali Mufti wa Tanzania Sheikh Abubakar Zubery Bin Ally, amelazimika kwenda katika wodi hiyo baada ya msafara wake kusimamishwa na kundi la akina mama, waliomtaka kwenda katika wodi ya wazazi ili akajionee jinsi wazazi wanavyokabiliwa na kero mbalimbali ikiwemo ya kulala chini kutokana na kukosa vitanda.

Baada ya kujionea mwenyewe kero ya msongamano na kuzungumza baadhi wazazi waliojifungua, Rais Magufuli amewaahidi wazazi hao kuwa atashughulikia kero alizozishuhudia.

"Nimeiona hali halisi mimi mwenyewe, watu wanapata shida, watu wana mateso, na ndio maana nimeamua kuja kwa makusudi, sikuomba ruhusa ili nijionee hali ilivyo, nimejifunza mengi, ninayabeba na nitajua namna ya kuyatatua" Alisema Rais Magufuli.

Kabla ya kutembelea wodi ya wazazi, Dkt. Magufuli amemjulia hali Mufti wa Tanzania Sheikh Abubakar Zubery Ally aliyelazwa katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete ambapo  amempa pole na kumuombea apone haraka.

Pamoja na kupokea pole ya Rais, Mufti wa Tanzania ameongoza dua ya kumuombea heri Rais Magufuli ili aweze kutekeleza vyema majukumu yake katika kuwahudumia watanzania.

Dua kama hiyo pia imefanywa na wananchi wengine waliokuwa wakimsubiri nje ya majengo ya Hospitali ya Taifa Muhimbili ambapo katika dua hiyo wamemuomba Mwenyezi Mungu kumlinda na kumuongoza katika majukumu yake ya kuiongoza nchi.

"Mwenyezi Mungu mbariki Rais wetu, mpe hekima, busara na upendo katika kazi zake za kuiongoza nchi hii ili watanzania wote wanufaike" ilisema sehemu ya dua hiyo iliyoongozwa na mmoja wa akina Mama.

Gerson Msigwa
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
Dar es salaam
10 Februari, 2016. 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimjulia hali Mufti na Sheikh Mkuu wa Tanzania, Sheikh Abubakary Zubeir ambaye amelazwa kwenye Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kwa ajili ya matibabu.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimjulia hali Mufti na Sheikh Mkuu wa Tanzania, Sheikh Abubakary Zubeir ambaye amelazwa kwenye Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kwa ajili ya matibabu.
Mufti na Sheikh Mkuu wa Tanzania, Sheikh Abubakary Zubeir akimuombea Dua Rais  wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli mara baada ya Rais Dkt. Magufuli kumjulia hali Hospitalini hapo.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiombewa Dua na ndugu na jamaa mbalimbali ambao walifika Muhimbili kuwaona wagonjwa wao.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akielekea katika Wodi ya Wazazi kufanya ukaguzi wa ghafla mara baada ya kuwasili akitokea Dodoma.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na wagonjwa waliolazwa katika Wodi ya Wazazi na amewahidi kutatua kero zao ndani ya muda mfupi ujao.PICHA NA IKULU

Makampuni 210 ya Usafirishaji Na Utoaji Mizigo Bandarini Yasimamishwa Kutoa Huduma Kwa Kutowasilisha Nyaraka Za Malipo

$
0
0
Makampuni yafuatayo ya kupitisha mizigo bandarini (Clearing and Forwarding Agents) yamezuiwa kufanya kazi katika bandari zote zinazomilikiwa na TPA pamoja na washirika wake (ICS’s, CF’s na TICTS) tangu 9 Februari 2016.
 
Uamuzi huo umechukuliwa kwa sababu ya kushindwa kuwasilisha vielelezo vya malipo, kama walivyotakiwa na mamlaka ya bandari. Pia wameshindwa kufika bandarini kupokea nyaraka kadhaa kuhusiana na madeni wanayodaiwa na TPA.

==>Hii ni Orodha ya Mawakala wa kupitisha Mizigo bandarini (CLEARING & FORWARDING) waliosimamishwa kutoa huduma katika Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) Kuanzia Februari 9, 2016 ni;

1. 21st Century Freight Forwarders
2. Aristepro Investment Co. Ltd
3. Ace Exim
4. Ally Vay C & F Agency
5. A & D Holdings Ltd
6 A & G Holdings Ltd
7.ACW Investment Ltd
8.Afro Centre (T) Ltd
9.Allmol trading
10.Amico Trading Ltd
11.Avow Holding (T) Ltd
12.Afritel Systems Ltd
13.Afrovision International Co. Ltd
14.Arusha Cargo Clearing & Forwarding Ltd
15.Arusha Freight Transport Agency
16.Bakhresa Food Products Ltd
17.Boston Forwarders Ltd
18.Babylon Freight Ltd
19.Beam Tanzania Ltd
20.Best Ocean Air Ltd
21.Break Through Holdings Ltd
22.Business Service Promotion Ltd
23.B & J Co. Ltd
24.BNM Co. Ltd
25.Boneste General Enterprises Ltd
26.Blue Light Investment Ltd
27.BN Metro ( E.A) Ltd
28.Cad Mulungu Co. Ltd
29.Capital Cargo Removers Ltd
30.Cargo Stars Ltd
31.Car Freight Station ICDV
32.Clear Services Tanzania Ltd
33.Clampek (T) Ltd
34.Classic Choices Investment Ltd
35.Continetal Reliable Clearing Ltd
36.Conanza Express Ltd
37.Cos Africa Logistics Ltd
38.Cosmos Haulage Co. Ltd
39.Chissel C & F Ltd
40.Cusna Investment Ltd
41.Daffor Enterprises Ltd
42.Dynamic Freight Forwarders Ltd
43.Datar & Co. Ltd
44.Dar Es Salaam Global Access Ltd
45.Dar Coast Enterprises Ltd
46.Denilo Freight Ltd
47.Destination Tanzania Cargo Logistics
48.Divine Cargo Services Ltd
49.Dow Elef Ltd
50.Dolusi (T) Ltd
51.Dolphin Sea And Air Ltd
52.E-3 Freight Co. Ltd
53.Eagle Tallons (T) Ltd
54.Econ Consult & Trading Co. Ltd
55.Eltex Investment Ltd
56.Edams Holdings Ltd
57.Efficient Freighters (T) Ltd
58.Equity Agencies
59.Expro Freight Services Ltd
60.Evergreen General Logistics (T) Ltd
61.Enterprises Logistics Ltd
62.East African Fossils Fossils Ltd
63.Fedrol Cargo Ltd
64.Full Cargo Support Ltd
65.Freight 24/7 Ltd
66.Favre Freight Forwarders Ltd
67.Freight Forwarders (T) Ltd
68.Freedom Freight Forwarders Ltd
69.Fifa & Flow Co. Ltd
70.F.K. Farms & Co. Ltd
71.First Choice Clearing & Forwarding Ltd
72.Freight Works Ltd
73.Frafza Freight Forwarders Ltd
74.General Envirocare (T) Ltd
75.General Shami Investment Co. Ltd
76.Glory Freight Ltd
77.Grand Movers Co. Ltd
78.Gwiholoto Impex Ltd
79.GS InterTrade Co. Ltd
80.Hamymack Trading Co. Ltd
81.Hadolin (T) Ltd
82.Hasa Customs Agency (T) Ltd
83.Horizon Freight Forwarders Ltd
84.Hodari Freight Ltd
85.Hardmark Logistics Ltd
86.HK Freight Forwarders Ltd
87.Hotreef Trading Ltd
88.Home Base Tanzania Ltd
89.Ilemela Investment Ltd
90.Impact Trading And Investment Co. Ltd
91.Jambo Freight Ltd
92.Jas Express Ltd
93.Jamaap Co. Ltd
94.Joe Ocean C & F Ltd
95.Juhudi Clearing And Forwarding
96.Juni Trust Freight Tz Ltd
97.Kas Freight Ltd
98.Kahe International Ltd
99.Kassam freight Ltd
100.Kiwaepa International Co. Ltd
101.Khan's C & F Ltd
102.Kams Trading Ltd
103.Kings Freight (T) Ltd
104.K & K Cargo Logistics
105.K&K Company Ltd
106.Kadengere Traders Ltd
107.Korufreight (T) Ltd
108.Lawia (T) Ltd
109.Laz ltd
110.Lesidi General Cargo Ltd
111.Liberal International Ltd
112.LCR Limited
113.LDV Macro Investment Ltd
114.Logistics Efficiency Co. Ltd
115.Lesheti Trading Ltd
116.Lichinga (T) Ltd
117.Mambona freight Ltd
118.Mamba Enterprises Ltd
119.Maxima C & F Ltd
120.Mwaya C & F
121.Marine Air Freight Ltd
122.Maritime Shipping Consultants
123.Mechanised Cargo Systems
124.METL
125.Metrologic C &f F Ltd
126.Minex Logistics Ltd
127.Mpepa Traders Co. Ltd
128.Mogo Forwarders Ltd
129.Mokha Agency Co. Ltd
130.Mwagy Investment Ltd
131.Naito General Supplies Ltd
132.Nal Business Co. Ltd
133.Nemarts Limited
134.Neighbour Trading Co . Ltd
135.Ngaramau Contractors Ltd
136.Nutricare (T) Ltd
137.Nkira Trading Ltd
138.NM Freight Ltd
139.Overseas Hi-Tech Industrial Ltd
140.Orbit Freight Ltd
141.Pasiwa Cargo Ltd
142.P & D Freight Forwarders Ltd
143.Platinum Trading Co. Ltd
144.Palm Swift Tz Ltd
145.Quality Logistics Ltd
146.Runner Co. Ltd
147.Rungwe Trading Ltd
148.Reindeer Investment Ltd
149.Regent (T) Ltd
150.Rukwi Holdings Ltd
151.Royal Freight Ltd
152.Ruma International Ltd
153.R.H.G General Traders Ltd
154.Sky Land Across Freight
155.Sai C & F Ltd
156.Shift Cargo Ltd
157.Sachsen Spedition Ltd
158.Sahara Desert Freighters
159.Sahuse Services & Supplies Ltd
160.Selwek & Solar Forwarders Ltd
161.Sami Agency Ltd
162.Sahe C & F Ltd
163.Sangare Express Ltd
164.Sea Bridge Co. Ltd
165.Sea Air Forwarders Ltd
166.Sea Africa Cargo Freight Ltd
167.Scol (T) Ltd
168.Shakura Trading Services
169.Space Land Logistics
170.Senkondos Import & Export Ltd
171.Smith Freight Forwarders Ltd
172.Sino Logistics Ltd
173.Scanland Shipping Consultants Ltd
174.SpacelandLogistics Ltd
175.Sachsen Spedition Ltd
176.Swiftways International Ltd
177.Stepio Freight Ltd
178.Switch Trade Ltd
179.Sun Fresh Co .Ltd
180.StarVision International Ltd
181.Tanga Cargo & Trust Ltd
182.Trade Waves Investment Co. Ltd
183.Transit Ltd
184.Trident Clearing Ltd
185.Team Freight
186.Trans Net Freighters
187.Three way Shipping Service Ltd
188.Trans Pack Tanzania Ltd
189.Trans African Forwarders Ltd
190.TransBarriers Freight Ltd
191.Transit Ltd
192.Tripple D
193.Twende Freight Forwarders Ltd
194.Ujiji C & F Ltd
195.United Youth Shipping Co. Ltd
196.United family Co. Ltd
197.Uwanji General Tradersb Ltd
198.Uprising C & F Ltd
199.Upland Freight Ltd
200.Vigu Trading Ltd
201.Vamwe Investment Co. Ltd
202.Viccom resources co ltd
203.Way Logistics Ltd
204.West Freight Forwarders
205.Wings Wheels Co. Ltd
206.Walmax Freight Forwarders Co. Ltd
207.Xpress Maritime Agency Co. Ltd
208.Zappex International Ltd
209.Zaihuse C & F Ltd
210.Zzoikos (T) Ltd

F.J. Liundi
For : Port Manager
Dar es Port.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Alhamisi Ya Februari 11

Bandarini Hapakaliki.......TRA Yatangaza Kuwafilisi Wateja 24 Kwa Kutorosha Makontena

$
0
0

Mamlaka  ya Mapato Tanzania (TRA) imeikabidhi Kampuni ya Udalali ya Yono kuwafilisi wateja 24 wanaodaiwa kodi ya Sh bilioni 18.95 baada ya kutorosha makontena ya mizigo yao kwenye Bandari Kavu (ICD) ya Azam mwishoni mwa mwaka jana.

Majina ya wadaiwa hayo yametolewa jana kwenye vyombo mbalimbali vya habari, na Kampuni hiyo ya Udalali ya Yono baada ya TRA kuwakabidhi kazi ya kuwafilisi kutokana na kushindwa kutekeleza wajibu wao baada ya kupewa muda wa kulipa kodi.

Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni hiyo, Yono Kevela jana alisema wamepewa amri na TRA ya kisheria ya kukamata mali za wadaiwa na kuwafilisi ili kulipia kodi wanazodaiwa.

Kevela alisema baada ya kupata kazi hiyo, wao wameona busara kuwatangaza kwenye vyombo vya habari na kuwapa siku 14 kulipa kodi wanazodaiwa na kwamba baada ya muda huo kumalizika, hatua za kukamata mali za wadaiwa hao zitaanza na kuwafilisi.

“Tumekabidhiwa wadaiwa 24 na TRA, hawa wamekwepa kodi kwa kutorosha kontena katika Bandari Kavu ya Azam mwishoni mwa mwaka jana, sasa walipewa muda wa kulipa ila wamekaidi, sasa kazi tumepewa sisi na tutawafilisi mali zao zote ili kulipa deni hilo,” alifafanua Kevela.

==>Majina ya wadaiwa hai na kiasi cha fedha wanachodaiwa kwenye mabano ni 
  1. Zulea Abas Ali  (16,760577.24) 
  2. Omary Hussein Badawy  (21,346,615.40)
  3. Libas Fashion  (26,593,245.78)
  4. Said Ahmed Said  (28,249,352.50)
  5. Strauss International  (45,393,769.95) 
  6. Farid Abdallah Salum (52,185, 614.97)
  7. Ally Awes Hamdani  (55,485,904.07)
  8.  Nasir Saleh Mazrui  (60,105,873.77)
  9.  Simbo Yona Kimaro  (64,221,009.10)
  10.  Zuleha Abbas Alli  (75,508,551.88)
  11.  Issa Ali Salim  (94,543,161.96)
  12. Ally Masoud Dama  (102,586,719.22)
  13. Juma Kassem Abdul  (130,182,395.12)
  14.  Salum Link Tyres  (233,447,913.31)
  15. Tybat Trading Co. Ltd  (448,690,271.90)
  16. IPS Roofing Co. Ltd  (966,723,692.10)
  17. Tifo Global Trading Co Ltd (1,573,300,644.58)
  18.  Lotai Steel Tanzania Ltd (5,476,475,738.19)
  19. Tuff Tyres General Co Ltd (7,435,254,537.03)
  20.  Swalehe Mohamed Swalehe (34,687,165.00)
  21.  Rushwheel Tyre General Co Ltd, (1,802,988,679.20)
  22.  Said Ahmad Hamdan  (68,362,558.31)
  23. Ahmed Saleh Tawred  (59,237,578.40)
  24.  Farida Abdullah Salem (75,334,871. 85).
Kevela alisema wadaiwa hao wanapaswa kulipa madeni yao ndani ya siku 14 walizopewa na kwamba iwapo watashindwa kutekeleza amri hiyo, kampuni hiyo itaanza kazi ya kukamata mali zao na kuwafilisi.

Alisema ili kurahisisha kazi hiyo, Kampuni ya Said Salum Bakhresa (SSB) ambayo ndiyo mmiliki wa Bandari Kavu ya Azam pamoja na Kampuni ya Regional Cargo Services wanapaswa kutoa ushirikiano kuhakikisha wadaiwa hao wanalipa kodi walizokwepa.

“Kampuni hizo zinahusishwa na kutoroshwa kwa kontena 329 zilizokuwa Azam ICD, sasa ni vyema watoe ushirikiano ili wadaiwa walipe fedha za serikali,” alifafanua Kevela. 

Alisema baada ya muda waliotoa kumalizika, wahusika watapaswa kulipa na gharama za ziada ambazo ni pamoja na faini na usumbufu wa kuwatafuta.

Desemba 12, mwaka jana, aliyekuwa Kaimu Kamishna wa TRA, Dk Philip Mpango aliwaambia waandishi wa habari kuwa kampuni 15 kati ya 43 zilizokwepa kodi baada ya kutorosha kontena 329 katika ICD ya Azam, zimelipa.

Dk Mpango alisema Desemba 12, mwaka jana ndiyo ilikuwa siku ya mwisho aliyotoa Rais John Magufuli ya siku saba kwa wakwepa kodi hao 43 kulipa wenyewe kwa hiari, vinginevyo sheria zitachukua mkondo wake.

Kutokana na kauli hiyo ya Rais Magufuli, wadaiwa 15 walijitokeza na kulipa na waliobaki hawakujitokeza kulipa.

Majambazi Yaua Watanzania Wanne Nchini Msumbiji

$
0
0

Wafanyabiashara wanne wa Tanzania wameuwa kwa kupigwa risasi kisha kuchomwa kwa vitu vyenye ncha kali nchini Msumbiji baada ya kuvamiwa na watu wanaosadikiwa kuwa ni majambazi. 

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mtwara, Henry Mwaibambe alisema tukio hilo lilitokea usiku wa Jumatatu iliyopita katika machimbo ya dhahabu, Kijiji cha Mtoro Mtupweshi Kamprigando.

Aliwataja waliofariki dunia kuwa ni Salum Mfanga (44) Mkazi wa Temeke, Dar es Salaam, Yusuph Twalibu (34) na Mariam Ramadhani (30) wakazi wa Tanga na Hamisi Mkapira (40) wa Morogoro.

Kamanda huyo alisema kifo cha Mariam ambaye alifanikiwa kujiokoa, kilisababishwa na kukosa huduma ya haraka baada ya kuvunjika mguu.

Kamanda huyo alisema wafanyabiashara hao walivamiwa na majambazi waliokuwa na risasi pamoja na mapanga katika vibanda vya kubadilishia fedha nchini humo. “Miili ya wafanyabiashara hao ililetwa na ndugu zao ambao wanaishi Msumbiji,” alisema.

Wakizungumzia tukio hilo, Said Mfanga na Dotto Ramadhani ambao ni ndugu wa marehemu hao walisema baada ya kuwaua, majambazi hao waliwapora fedha pamoja na mabegi yao.

Watu 6 Wajeruhiwa Baada Ya Kontena Kuangukia Magari Matatu

$
0
0

Watu sita wamejeruhiwa jana baada ya Lori la Mizigo lenye namba za usalili T 493 DBR lililobeba kontena kuacha njia na kugonga magari matatu kisha kontena kudondoka katikati ya barabara ya Mandela na kusababisha msongamano kwa watumiaji wa njia hiyo.

Tukio hilo lilitokea jana saa 3:00 asubuhi eneo la Tabata Relini wilayani Ilala.

Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala, Ernest Matiku alisema watu sita ndiyo walioripotiwa polisi kuwa majeruhi, na wengine ambao idadi yao haifahamiki waliwahi hospitalini wenyewe.

Matiku alisema wanamsaka dereva wa lori hilo ambaye alikimbia baada ya kusababisha ajali hiyo.

Wakisimulia ajali hiyo, mashuhuda walisema kuwa lori hilo lilikuwa kwenye mwendo wa kasi likikimbizana na lori jingine lililobeba kontena.

Lilipofika eneo hilo hilo lenye taa za kuongozea magari, lilijaribu kukwepa daladala lililokuwa kituoni na kuparamia kingo za barabara na baadaye kupinduka.

Baada ya kuparamia na kupinduka, lori hilo lilienda kugonga magari mengine matatu yaliyokuwa katika foleni upande wa pili wa barabara.

Siku 100 za Rais Magufuli: Hospitali Ya Muhimbili Yang'aa, Mapato Yapaa na Upatikanaji wa Dawa Waongezeka Kwa Asilimi 96

$
0
0

HOSPITALI ya Taifa ya Muhimbili (MNH) iliyopo jijini Dar es Salaam imesema ndani ya siku 100 za kuwepo madarakani kwa Rais John Magufuli, imefanikiwa kuongeza mapato kwa kiwango cha asilimia 90.

Pia, imeongeza huduma za upasuaji wa dharura na pia kufanikisha upatikanaji wa dawa kwa asilimia 96. Aidha, hivi karibuni inatarajia kuanzisha chumba cha wagonjwa wanaohitaji uangalizi maalumu (ICU), kitakachokuwa na uwezo wa kulaza wagonjwa 16 kwa wakati mmoja na kuwa na vitanda kutoka nane hadi 25.

 Hayo yalisemwa na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali hiyo, Profesa Lawrence Mseru wakati akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana.

Alikuwa akieleza mafanikio ya hospitali hiyo katika siku 100 za kuwepo madarakani kwa Dk Magufuli. Dk Magufuli aliingia madarakani rasmi Novemba 5, mwaka jana baada ya kuapishwa kuongoza Serikali ya Awamu ya Tano, akipokea kijiti cha kuiongoza Tanzania kutoka kwa Rais mstaafu Jakaya Kikwete.

Akizungumzia mafanikio hayo, Profesa Mseru alisema baada ya kuongezeka kwa kasi ya usimamizi wa wafanyakazi na kupunguza kero za wafanyakazi, MNH imeongeza uzalishaji wenye tija kwani kwa Desemba mwaka jana ilizalisha mapato ya Sh bilioni 3.3 kutoka wastani wa Sh bilioni 2.7 zilizozalishwa kwa kipindi cha miezi mitano kuanzia Julai mwaka jana.

Aidha, alisema kwa Desemba mwaka jana pekee, MNH ilizalisha mapato ya Sh bilioni 3.3 na Januari mwaka huu ilizalisha Sh bilioni 4.3, ambazo ni sawa na ongezeko la asilimia 60. 

Lengo ni kufikisha Sh bilioni sita Julai mwaka huu. “Haya ni mafanikio makubwa sana kwa upande wa mapato kuwahi kupatikana katika kipindi kifupi cha miezi miwili tu. Tumeona hospitali ina fursa kiasi gani ya kuzalisha kiasi kingi cha fedha na hivyo kujitosheleza kwa kiwango kikubwa kuendesha shughuli zake,” alisisitiza Dk Mseru.

Profesa Mseru alisema baada ya agizo la Rais Magufuli la kuitaka Bohari Kuu ya Dawa Tanzania (MSD), kujenga duka la dawa katika hospitali hiyo, kwa sasa MNH imefanikisha wagonjwa kupata dawa kwa zaidi ya asilimia 96 kutoka kwenye duka hilo na maduka ya dawa ya hospitali hiyo.

Alisema wamefanikiwa kuboresha mfumo wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (Tehama) katika utoaji na uagizaji dawa, na wagonjwa wanaokosa dawa katika maduka hayo, hospitali hiyo huzitafuta na kuzinunua dawa hizo kwa ajili ya wagonjwa hao. 

Alisema kutokana na hali hiyo, kwa sasa ukosefu wa dawa hospitalini hapo, umepungua kwa kiasi kikubwa kutokana na kuimarika pia kwa utendaji ndani ya hospitali hiyo.

Akizungumzia deni la hospitali hiyo, ambalo kwa sasa ni Sh bilioni 5.7 kwa wazabuni na watu wanaopeleka bidhaa zao na huduma, Profesa Mseru alisema tayari wameanzisha mkakati wa kupunguza deni. 

“Tunaishukuru Serikali kwa kutusaidia kulilipa deni lote tulilokuwa tunadaiwa na Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) ambalo ni shilingi bilioni 4.6,” alibainisha.

Akizungumzia ongezeko la upasuaji wa dharura, Mkurugenzi huyo alisema hospitali hiyo imeamua kuanzia sasa upasuaji wowote wa dharura, utakaofanyika kwa saa 24 kupitia Idara ya Magonjwa ya Dharura.

 “Tayari tuna vyumba viwili vya kisasa vya kufanyia upasuaji huo, awali tulikuwa na chumba kimoja tu,” alieleza na kuongeza kuwa katika kuboresha huduma, pia wanatarajia kuongeza vyumba vya wagonjwa wanaohitaji uangalizi maalumu.

Kuhusu kuboresha maslahi ya wafanyakazi, alisema ndani ya kipindi cha miezi miwili menejimenti ya hospitali hiyo, imelipa wafanyakazi malimbikizo ya madai yao ambayo ni kiasi cha Sh milioni 600. 

Alisema hospitali hiyo imeanza kulipa madeni hayo, yanayotokana na fedha za mwito maalumu (on call), malipo ya wauguzi ya usiku, malipo ya posho mbalimbali hususani kwa madaktari na kada nyingine za afya zinazoshughulika na wagonjwa na likizo.

“Tumeanza kulipa fedha hizi tangu Desemba na hadi kufikia mwishoni mwa mwezi huu tunatarajia kumaliza deni hili lote. Kutokana na hatua yetu hii kwa sasa morali ya wafanyakazi imeongezeka, jambo lililosaidia kuongeza mapato ya hospitali,” alifafanua mkurugenzi huyo.

Aidha, Profesa Mseru alizungumzia maagizo ya Rais Magufuli alipotembelea ghafla hospitalini hapo Novemba mwaka jana na kusisitiza kuwa tayari hospitali hiyo imetengeneza mashine zote mbili; MRI ambayo tayari imeshapima wagonjwa 2,200 na CT Scan iliyopima wagonjwa zaidi 1,000.

Alisema kutokana na mahitaji ya vipimo kupitia mashine za CT Scan, Serikali ya Awamu ya Tano imeshanunua mashine mpya yenye uwezo wa slices 126, wakati CT Scan ya awali ilikuwa na uwezo wa slices mbili tu na ina uwezo wa kupima wagonjwa 50 ndani ya saa 24. 

Kuhusu agizo la kupunguza wagonjwa kulala chini, alisema hospitali hiyo imejitahidi kupunguza tatizo hilo, ingawa imekuwa ngumu kutokana na ongezeko kubwa la wagonjwa.

Alisema hospitali hiyo ina mpango wa kupitia upya mfumo wa muundo wa kuona wagonjwa wa nje, waliolazwa na wagonjwa wanaohitaji huduma za vipimo na uchunguzi.

 “Ndio maana tunatarajia kuzindua Mkataba wa Huduma kwa Wateja, unaonesha tumedhamiria kufanya nini na wateja watarajie nini kutoka kwetu,” alieleza.

Pia alisema wana mpango wa kupunguza wagonjwa wanaokwenda nje kupata huduma ya upandikizaji wa figo, kwani ifikapo mwishoni mwa mwaka huu, MNH itaweza kupandikiza figo nchini na kupanua huduma ya kusafisha figo kutoka uwezo wa kuwa na mashine 23 hadi 50.

Novemba 5, mwaka jana, Dk Magufuli aliapishwa rasmi kuwa Rais wa Serikali ya Awamu ya Tano. Siku nne baada ya kuapishwa kwake, alifanya ziara ya ghafla Muhimbili ambako alivunja Bodi ya Wakurugenzi ya MNH na kumuondoa madarakani Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Hospitali hiyo, Dk Hussein Kidanto.

Dk Magufuli alichukua hatua hiyo, baada ya kusikitishwa na taarifa ya kutofanya kazi kwa mashine za CT- Scan na MRI kwa takribani miezi miwili huku mashine kama hizo zikifanya kazi katika hospitali za watu binafsi.

Aidha, kiongozi huyo alihuzunishwa na hali ya huduma kwa wagonjwa, hususan wanaolala chini ikiwemo hali ya kutokujali wala kushughulikia vifaa vya kufanyia kazi.

Watu 21 Watiwa Mbaroni kwa Mauaji ya Kondoo Na Mbuzi Mvomero

$
0
0

WENYEVITI wa Serikali za vijiji vya Mkindo, Patrick Longomeza (52) na mwenzake wa Dihombo, Christian Thomas (50) pamoja na wananchi wengine 19 wanashikiliwa na Polisi kwa tuhuma za kujeruhi mifugo mali ya mwanamke mfugaji wa Kimasai, Katepoi Nuru (36) wa Kijiji cha Kambala wilayani Mvomero Mkoa wa Morogoro.

Mbali na wenyeviti wa vijiji hivyo, pia Polisi wamemtia mbaroni kinara wa uhamasishaji vijana wa kimasai kuwapiga na kuwajeruhi wakulima wanaolima katika Bonde la Mgongola, Kashu Moreto (68) kwa tuhuma za kulisha mazao na kumjeruhi mguu wa kulia, mkulima Ramadhan Juma (19), mkazi wa Dihombo.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Morogoro, Leonard Paulo alisema hayo jana wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu tukio la awali lililotokea Februari 7, mwaka huu mchana katika Kijiji cha Kambala.

Alisema kabla ya kukatwa kwa mifugo ya mwanamke huyo, kundi la ng’ombe zaidi ya 50 likiwa na wachungaji zaidi ya watatu wa Kimasai walilisha shamba la mpunga ekari moja la mkulima Rajab Issa (31) aliyewazuia na ghafla walijitokeza vijana wanaosadikiwa kuwa ni Morani wa kimasai na kuwachukua ng’ombe hao kwa nguvu.

Aliwataja wengine waliotiwa mbaroni mbali na wenyeviti hao ni Issa Ally (66), Hussein Said (25), Juhudi Amimu (25), Emily Pascal (40) na Mkude Milikioni (25) ambao wote ni wakazi wa Kijiji cha Mkindo.

Wengine waliokamatwa ni Ally Bakari (25), Gerald Mbegu (22), Miraji Noras (22), Mengi Mbegu (32), Kudura Abdi (35), na wanawake wawili Angelina Sadiki (20), Hadija Msanga (30), wote wakazi wa Kijiji cha Mkindo.

Pia wamo Mustafa Malugo (35), Charles Moris (40), Amset Alfred (42), Hassan Mohamed (46) pamoja na Hapifan Paulo ambao wote hao ni kutoka katika Kijiji cha Dihombo wilayani Mvomero.

Kamanda Paulo alisema baada ya vijana hao wa kimasai kuingia kulisha katika shamba la Issa, alijaribu kuwazuia, lakini ghalfa walijitokeza vijana wanaosadikiwa kuwa ni morani wa kimasai na kuwachukua ng’ombe hao kwa nguvu, na mkulima huyo alitoa taarifa katika Kituo cha Polisi Mvomero.

Lakini alisema Februari 8, mwaka huu mchana wakati tukio hilo likishughulikiwa, kikundi cha watu kilivamia nyumbani kwa Nuru Kipande (76) na kumkuta kumkuta Ketepoi Nuru (36) akiwa nyumbani huku mifugo aina ya mbuzi, kondoo na ndama wakiwa malishoni.

Kwa mujibu wa Kamanda, kundi hilo lilinyang’anya mifugo hiyo na kisha kumnyang’anya mwanamke huyo simu yake ya mkononi ili asiombe msaada na kisha kuipeleka mifugo hiyo porini na kuanza kuikatakata kwa vitu vyenye ncha kali .

Kamanda alisema watuhumiwa waliokamatwa wanaendelea kuhojiwa na wengine kutafutwa na wote waliohusika katika tukio hilo watafikishwa mahakamani, na kutoa onyo kwa watu wote kuacha kujichukulia sheria mkononi.

Hakimu na Ofisa Elimu Wafikishwa Mahakamani Wakidaiwa Kula Rushwa

$
0
0

Hakimu wa Mahakama ya Mwanzo Kintinku wilayani Manyoni Mkoa wa Singida, Mahando Sabato amefikishwa Mahakama ya Wilaya ya Manyoni na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), kwa tuhuma ya kuomba na kupokea rushwa ya Sh350,000.

Ilidaiwa kuwa mshtakiwa huyo, alifanya kitenda hicho ili amsaidie mlalamikaji kuifuta kesi iliyokuwa ikimkabili kijana wake.

Mkuu wa Takukuru, Wilaya ya Manyoni, Michael Sanga alidai kuwa Desemba 30, mwaka jana, ofisi yake ilipokea taarifa kutoka kwa mlalamikaji (jina limehifadhiwa), kuwa hakimu Sabato alikuwa akimuomba rushwa hiyo ili afute kesi ya wizi wa Sh400,000 iliyokuwa ikimkabili kijana wake.

Sanga alidai kuwa katika kufanikisha azma yake ya kula rushwa, hakimu huyo alifuta dhamana ya mtuhumiwa huyo na kuamuru apelekwe mahabusu ya Gereza la Wilaya ya Manyoni, kwa siku 21 wakati akiendelea na mambo mengine.

“Baada ya kubaini kwa hakimu Sabato amedhamiria kwa kiwango kikubwa kupokea rushwa hiyo, tuliweka mtego katika eneo la kituo cha mabasi cha Kintinku, ndipo tukamkamata akiwa na fedha za mtego huo wa hongo,” alidai Sanga.

Mshtakiwa huyo yupo nje kwa dhamana hadi Februari 17, kesi yake itakafikishwa mahakamani kusomewa maelezo ya awali.

Wakati huohuo, Takukuru imemfikisha kortini Ofisa Elimu Wilaya ya Kyela mkoani Mbeya, Prochesius Mguli kujibu tuhuma ya kughushi nyaraka za malipo kwa walimu 22 wa shule za sekondari wilayani humo.

Akisoma mashtaka dhidi ya mshtakiwa huyo katika Mahakama ya Wilaya ya Kyela, Ofisa wa Takukuru , Thomas Msuta alidai kuwa kati ya Agosti 18 na 30 mwaka 2012, mshtakiwa alighushi majina ya walimu hao, alidai walihudhuria semina na kuwalipa Sh3.3 milioni.

Msuta alidai mshtakiwa huyo katika ripoti yake alighushi saini za walimu hao wakati hawakushiriki kwenye semina.

Mshtakiwa yupo mahabusu baada ya kushindwa kukamilisha masharti ya dhamana.

Hakimu, Jacob Ndila aliahirisha kesi hiyo hadi Februari 17 itakapotajwa tena.

Watanzania Wapelekwa Uganda Kupiga Kura

$
0
0

Mgombea wa urais katika uchaguzi ujao nchini Uganda, Amama Mbabazi amedaia kuwa kundi la raia wa kigeni wamekuwa wakisafirishwa hadi nchini humo kwa ajili ya kumpigia kura Rais Yoweri Museveni.

Mbabazi ambaye ni mgombea huru alisema, mamia ya raia kutoka nchi za Tanzania na Rwanda wamekuwa wakiwasili nchini humo ili kukisaidia chama tawala na mgombea wake kushinda kwenye uchaguzi huo.

Mwanasiasa huyo ambaye kabla hapo alikuwa waziri mkuu chini ya utawala wa Rais Museveni, alitahadharisha wananchi kuwa macho na mwenendo huo, huku akiwataka kuchukua hatua kuzuia aina yoyote ya udanganyifu.

Waziri Mkuu huyo wa zamani ambaye alikuwa akizungumza na waandishi wa habari alisema yeye binafsi pamoja na timu yake ya kampeni itaendelea kuwa macho kufuatilia mwenendo huo.

“Watu wana njia nyingi za kufanya udanganyifu. Idadi kubwa ya Watanzania wamekuwa wakiwasili nchini kwa ajili ya kupiga kura. Pia, tumeshuhudia watu wakitoka Rwanda na kupiga kura.

"Tumebaini njama zao na sisi wananchi lazima tuwe macho kuwabaini watu hao siku ya kupiga kura itapowadia,”
alisema Mbabazi. Uchaguzi Mkuu nchini humo utafanyika Februari 18.

Majangili 9 Wanaotuhumiwa Kutungua Helkopta Wafikishwa Mahakamani

$
0
0
Watu tisa wamefikishwa mahakamani wakituhumiwa kutungua helikopta iliyokuwa ikifanya doria kwenye Pori la Akiba la Maswa wilayani Meatu, Simiyu na na kumuua rubani wake.

Mbali na kutungua chopa na kumuua rubani wake, Rogers Gower, raia wa Uingereza, watu hao pia wameshtakiwa kwa kukutwa na nyara za Serikali, kuuza na kumiliki silaha kinyume cha sheria.

Washtakiwa hao walifikishwa mbele ya Mahakama ya Mkoa wa Simiyu jana wakiwa chini ya ulinzi mkali wa polisi, huku umati wa wananchi wakifurika na kusababisha hekaheka mahakamani hapo.

Yamiko Mlekano, ambaye ni wakili mwandamizi wa Serikali, alidai kuwa washtakiwa wote kwa pamoja wanakabiliwa na kesi tatu; uhujumu uchumi, mauaji na umiliki wa silaha bila ya kibali.

Katika kesi namba mbili ya mauaji, Wakili Yamiko alidai kuwa Shija Mjika (38), Njile Gunga (28), Dotto Pangali (42) na Moses Mandagu walitungua helikopta hiyo Januari 29 kwenye Hifadhi ya Mwiba iliyoko Kijiji cha Makao wilayani Meatu na kumuua rubani Gower.

Mlekano alidai kuwa katika kesi ya uhujumu, mshtakiwa namba moja Iddy Mashaka (49) anadaiwa kujihusisha na kuratibu tukio la uhujumu uchumi kinyume na sheria.

Mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi Mwandamizi, John Nkwabi, wakili huyo alida kuwa mshtakiwa alitenda kosa hilo Januari 6 na Februari Mosi wilayani Meatu kwa kumshauri mshtakiwa namba mbili, Shija Mjika (38) kuua wanyama wasioruhusiwa.

Katika shtaka la pili, watu saba; Njile Gunga (28), Dotto Pangali (42), Moses Mandagu (48), Dotto Huya (45), Mwigulu Kanga (40), Mapolu Njige (50) na Mange Barumu (47) pia wanashtakiwa kwa kuhujumu uchumi.

Aliieleza mahakama kuwa kati ya Januari 21 na 29 katika wilayani Meatu, washtakiwa walipanga na kuratibu tukio la kuwinda wanyama aina ya tembo bila ya kibali cha Serikali.

Wakili Mlekano alidai kuwa shtaka la tatu la uwindaji wanyama wasioruhusiwa linawakabili mshtakiwa wa pili hadi tisa na wanadaiwa kutenda Januari 26 na 29 kwenye Hifadhi ya Mwiba Kijiji cha Makao wilayani Meatu wa kumuua tembo mwenye thamani ya Sh32,891,100 bila ya kibali.

Katika shtaka la nne, mshtakiwa namba mbili na tisa wanatuhumiwa kumiliki nyara za Serikali kinyume na sheria.

Washtakiwa wanadaiwa kutenda kosa hilo Januari 29 na Februari Mosi wilayani Meatu ambako walikamatwa na meno ya tembo yenye uzito wa kilo 31 na thamani ya Sh32,891,100.

Katika shtaka namba tano, Mashaka na Mjika wanashtakiwa kwa kuuzaji nyara za Serikali kinyume na sheria na kwamba walitenda kosa hilo kati ya Januari 6 na Februari Mosi wilayani Meatu.

Hakimu Nkwabi alisema washtakiwa hawatakiwi kujibu chochote kutokana na mahakama hiyo kutokuwa na uwezo wa kusikiliza kesi hiyo na aliahirisha hadi Februari 24 zitakapotajwa tena.

Katika kesi ya tatu ambayo ni kukutwa na silaha kinyume cha sheria iliyosomwa mbele ya Hakimu Mfawidhi wa Wilaya, Mary Mrio, washtakiwa wanakabiliwa na mashtaka matano.

Washtakiwa hao ni Buluma, Mjika, Pangani, Ngunga, Mandagu, Huya na Kanga ambao baadhi yao walikiri kumiliki silaha na risasi kinyume cha sheria akiwamo Njile anayedaiwa kutungua helikopta hiyo.

Washtakiwa hao walikiri mashtaka mawili ambayo ni kukutwa na bunduki aina ya Riffle 303, wakati Ngunga na Mandagu walikiri shtaka la tatu, nne na tano la kukutwa na silaha na risasi bila ya kibali.

Hata hivyo, Hakimu Mrio alishindwa kutoa hukumu kwa washtakiwa waliokiri kosa kutokana na kutokuwapo kwa vielelezo mahakamani hapo, hivyo kesi hiyo iliahirishwa hadi leo. 
Watuhumiwa wakiwa ndani ya gari la polisi, baada ya kufikishwa kituo cha polisi Bariadi wakitokea wilayani Meatu kwa ajili ya kufikishwa mahakamani.
Njile Gunga (28) Huyu ndiye Jangili anadaiwa kutungua helkopta katika pori la Akiba la Maswa lililopo katika Wilaya ya Meatu Mkoani, ambapo katika tukio hilo rubani wa helkopta hiyo Rodgers Gower (37) raia wa uingereza huku Mwenzake Nicholas Beste (43) raia wa Afrika Kusini akinususrika kifo.
Iddy Mashaka (49) ambaye ndiye alikuwa Mkuu wa kitengo cha Interejensia katika hifadhi ya taifa Ngorongoro, ambaye anadaiwa kuwa kiunganishi Mkuu wa kutekeleza tukio la kutunguliwa kwa helkpta hiyo.
Hali ya ulinzi na usalama ilivyokuwa imehimarsihwa mahakamani pamoja na kituo cha polisi Bariadi leo hii.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Elaston Mbwilo akionyeshwa watuhumiwa wa ujangili ambao walihusika kutungua Helkopta.
Watuhumiwa wakiwa Mahakamani.
Wakazi wa Mji wa Bariadi wakiwa wamefurika  katika viwanja vya Mahakama ya wilaya hiyo kushuhudia watuhumiwa hao.

Basi La Simba Mtoto Lapata Ajali Muheza Tanga....Watu 11 Wafariki Dunia

$
0
0
Ajali mbaya ya barabarani imetokea mkoani Tanga  leo asubuhi  wakati Basi la Kampuni ya Simba Mtoto ya Tanga lilipogongana na Lori uso kwa uso katika eneo la Pangamlima Wilayani Korogwe mkoani humo.

Taarifa za awali kutoka eneo la tukieo zinaeleza kuwa watu 10 wanahofiwa kupoteza maisha na wengine kujeruhiwa vibaya atika ajali hiyo.


TRA yakamata shehena kubwa ya bidhaa za magendo

$
0
0
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imefanikiwa kukamata bidhaa za magendo kwenye maeneo mbalimbali ya Ukanda  wa Bahari ya Hindi, Ziwa Victoria na mipakani.
 
Taarifa hiyo imetolewa leo na Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipa Kodi (TRA) Bw. Richard Kayombo wakati akifanya mahojiano na Mwandishi wa Idara ya Habari (MAELEZO) ofisini kwake Jijini Dar es Salaam kuhusu juhudi za operesheni ya kutokomeza bidhaa za magendo nchini.
 
Bw. Kayombo ameeleza kuwa, mkoani Lindi TRA imefanikiwa kukamata mashua katika bandari ya Lindi ambayo ilisheheni bidhaa za magendo zenye thamani ya shilingi 159,361,046.
 
Ameongeza kuwa katika operesheni hiyo, TRA imefanikiwa kukusanya kodi ya jumla ya shilingi 10,500,678 kutoka katika bidhaa zilizokuwa katika nyaraka za forodha (manifest) ambapo pia inategemea kukusanya kodi ya shilingi 19,529,500 kutoka katika bidhaa ambazo zilikuwa katika nyaraka za forodha lakini thamani yake ilikuwa chini ya bei halisi.
 
Akitaja bidhaa hizo za magendo zilizokamatwa katika mashua hiyo ni mifuko 3,725 ya sukari yenye thamani ya shilingi 127,070,562, betri katoni 50, mchele mifuko 3,087, mafuta ya kula madumu 80, majokofu manne ya mtumba, baiskeli 4 za mitumba pamoja na katoni 20 za hamira.
 
“Mashua hiyo ilikamatwa katika bandari ya Lindi tarehe1 Februari, 2016 baada ya wasamaria wema kutoa taarifa ya kuwepo bidhaa za magendo ndani ya mashua hiyo ambapo upakuaji wa shehena hiyo ulianza mara moja.’’Alisema Kayombo.
 
Ameongeza kuwa,  Jijini Dar es Salaam, TRA kwa kushirikiana na kikosi cha doria cha Jeshi la Wanamaji wameweza kukamata Jahazi lenye jina la ‘Takbiri’ lenye usajili wa namba Z-875 likiwa limesheheni lita 19,700 za dizeli ambapo thamani yake bado haijapatikana kwakuwa imepelekwa kwa Mkemia Mkuu wa Serikali kwa ajili ya Uchunguzi zaidi.
 
Aidha, majahazi mengine matatu yamekamatwa katika eneo la Kigombe mkoani Tanga ambayo yalikuwa na bidhaa za magendo yenye thamani ya shilingi 99, 682, 273, 48 ambapo ndani kulikuwa na magunia ya sukari, mchele, mafuta ya kula, matairi ya magari, nyavu za kuzuia mbu, jokofu, jiko la umeme, rangi za kupuliza, betri na biskuti. 
 
Majahazi hayo yalitaifishwa baada ya wahusika kujitosa ndani ya maji na kutoroka.
 
TRA kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi inafanya doria saa 24 kila siku katika maeneo yote yaliyoshamiri upitishaji wa bidhaa za magendo pia imeunda Kanda Maalum katika maeneo ya Mbweni, Msasani, Kunduchi pamoja na Kigamboni.

Dkt. Kigwangalla Asema Wataendelea Kumsaidia Rais Kutumbua Majipu

$
0
0

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Watoto na Wazee Dk. Hamisi Kigwangalla amesema kwamba wao kama viongozi wataendelea kumsaidia Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Mhe.Dkt. John Pombe Magufuli kutumbua majibu yanayokwamisha kutokupatikana kwa huduma bora za afya ,bila kuogopa wala kumwonea mtu kwa ajili ya maslahi ya  taifa.
 
Aidha  Dkt. Kigwangalla alisema  watafanya hivyo kwa kufuata sheria, kanuni na taratibu ili kuhakikisha kila mtu anatimiza wajibu ipasavyo.
 
Dk.Kigwangalla ameyasema hayo  leo 11 Februari wakati wa maadhimisho ya 24 ya ibada maalum ya kuwaombea  wagonjwa Duniani ambayo Kitaifa yamefanyika katika jimbo Kuu la Tabora  na baadae kwenye Hospitali ya Ndala, iliyopo Kata ya Ndala, Wilaya ya Nzega, Mkoani Tabora.
 
“ Tutaendelea kutumbua majibu bila ya kmwonea mtu kwa kuwa tunafanya hivyo kwa kuangalia sheria, kanuni na taratibu. Haiwezekani mtu akaiba dawa ambazo zinawasaidia wananchi masikini, halafu sisi tukamwaangalia tu,” alisema Dkt.Kigwangalla.
 
Alisema majipu hayo yatatumbuliwa kwa watendaji ambao watakaozembea, wasio waadili na wasiowajibika katika sekta hiyo ya afya.
 
Aliongeza kwamba Serikali ya Awamu ya Tano itakuwa inafanya kazi kwa kuwafuata wananchi hususan wanyonge (masikini) mahali walipo ili kuhakikisha baada ya miaka kumi ijayo Tanzania itakuwa na maendeleo ya kiwango cha juu.
 
Naibu Waziri huyo aliwaomba viongozi wa dini kuendelea kuwaombea kwa kuwa kazi ya kutumbua majibu si rahisi.
 
Aliuomba uongozi wa hospitali hiyo kuboresha mfumo wa ukusanyaji mapato kwa kutumia elekroniki kwa sababu umeonyesha matokeo chanya katika hospitali nyinigine.
 
Akizungumzia kuhusu suala la upungufu wa bajeti,Dkt. Kigwangalla alisema ni vema viongozi hao wadini, asasi za kijamii na taasisi zisizoza kiserikali zinazotoa huduma za afya kutafuta vyanzo mbadala vya kuongeza fedha za kuboresha huduma hizo, kwa kuwa si sekta hiyo pekee yenye changamoto hiyo.
 
Pia vipaumbele vya shughuli mbalimbali za kuwaletea maendeleo wananchi viko vingi, wakati rasimali fedha haitoshelezi.
 
Aliwataka uongozi wa hospitali hiyo na nyinginezo za mashirika ya hiari kuwasilisha taarifa za (data cleaning) UTUMISHI ikiwa ni pamoja na kuorodhesha watumishi wanaotakiwa kuondolewa kwenye malipo ya mshahara ili waweze kupatiwa kibali cha kuajiri kwani bila kufanya hivyo kibali hakitaweza kutolewa.

Dkt. Kigwangalla aliongeza kwamba hivi sasa wizara yake iko katika mchakato wa kuhakikisha Watanzania wote wanapata huduma za matibabu za  kwa kutumia mifuko ya bima ya afya. Hivyo Februari 20,mwaka huu
 
Maadhimisho hayo ni ya kila mwaka ya siku 11 Februari, Wakristo wote wanafanya sala maalum ya kuwaombea wagonjwa wanaosumbuka na maradhi na  kuwaombea wapone haraka huku wakiyapokea mateso hayo na kuyaunganisha na mateso ya kristo na kanisa lake hii ni pamoja na kuwaombea ndugu wa wagonjwa katika kuwasaidia wagonjwa wao wakati wa kuwauguza.
 
Maadhjimisho hayo yanaenda sambamba pamoja na kuwahudumia na kutoamisasada mabalimbali.
 
Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Ludocivk Mwananzila aliwataka Watanzania kuwa na tabia ya kuwatembelea wagonjwa na wafungwa ili waweze kupata faraja.
 
Kihistoria, Hospitali hiyo ya Ndala, ilianza miaka ya 1930 kama Zahanati ndogo chini ya Masista Wamissionary wa Afrika (Missionary of Our Lady of Afrika-White Sisters) katika jimbo kuu hilo la Tabora
 
Mwaka 1963 ilikuja kuwa Hospitali kamili huku ikianza na vitanda 115 na wauguzi 15 na daktari mmoja, hata hivyo hadi sasa ina jumla ya vitanda 152, wafanyakaz 125 huku wakiweza kutoa huduma kwa wagonjwa wa nje wapatao 38,917 na wagonjwa wa kulazwa 8,428.
 
Hospitali hiyona baadae ikapandishwa ngazi ya Hospitali huku ikiwa na vitanda 152 huku ikiwa na madaktari mbalimbali.
 
Wakitoa shukrani zao ni pamoja na serikali ya Tanzania kupitia wizara ya afya kwa kuweza kushirikiana bega kwa bega ikiwemo kutoa ruzuku kwa baadhi ya watumishi, posho za watumishi, vitanda vulivyohainishwa, madawa, mafunzo ya watumishi, na mambo mbalimbali

Dk. Magufuli Amtumia Salamu Za Rambirambi Mkuu Wa Mkoa Wa Tanga Kufuatia Ajali Vifo Vya Watu 11

$
0
0

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania amemtumia salamu za rambirambi Mkuu wa Mkoa wa Tanga Bi. Mwantumu Mahiza, kufuatia vifo vya watu 11 waliopoteza maisha katika ajali ya barabarani iliyosababishwa na Basi la Kampuni ya Simbamtoto kugongana uso kwa uso na Lori lililobeba mchanga katika eneo la Pandamlima, Wilaya ya Muheza Mkoa wa Tanga.

Ajali hiyo imetokeo leo tarehe 11 Februari, 2016 majira ya saa 1:15 asubuhi katika eneo hilo lenye mteremko, ambapo basi la Kampuni ya Simbamtoto lilikuwa likisafiri kutoka Tanga kwenda Dar es salaam na Lori lililokuwa limebeba mchanga, lilikuwa likielekea kiwanda cha saruji cha Tanga.

Rais Magufuli amewapa pole Ndugu, Jamaa na Marafiki wote waliofikwa na msiba huo na amewataka kuwa wavumilivu na wastahimilivu katika kipindi hiki kigumu.

"Nimepokea taarifa ya vifo hivi kwa mshituko mkubwa, na kupitia kwako Mkuu wa Mkoa wa Tanga, napenda kuwapa pole nyingi wote waliofikwa na msiba huu mkubwa na naungana nanyi katika kipindi hiki kigumu cha maombolezo" alisema Rais Magufuli.

Dkt. Magufuli amewaombea marehemu wote wapumzishwe mahali pema pepo, na amewapa pole majeruhi wote 21 walioumia katika ajali hii.

Aidha, Rais Magufuli amewakumbusha watumiaji wote wa barabara hususani madereva wa vyombo vya moto, kuwa makini watumiapo barabara kwa kuzingatia sheria zote zinazosimamia usalama barabarani ili kuepusha ajali.

Gerson Msigwa
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
Dar es salaam.
11 Februari, 2016

Waziri Mkuu Afanya Tena Ziara Ya Ghafla Bandarini.........Aibukia kitengo cha mita za kupimia mafuta Kurasini,akuta zimejaa kutu Ataka barua ya maelezo.

$
0
0

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amefanya ziara ya ghafla kwenye kitengo cha upimaji mafuta bandarini (Oil Flow Metres) na kukuta zimejaa kutu baada ya kutelekezwa kwa miaka zaidi ya mitano. Pia alitembelea mita za kupimia mafuta zinazoendelea kujengwa Kigamboni.

Aidha, Waziri Mkuu amempa saa nne tu Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Vipimo nchini (WMA), Bi. Magdalena Chuwa aandike barua ya kujieleza ni kwa nini aliamua kufunga mita hizo zisitumike kwa zaidi ya miaka mitano iliyopita na amletee barua hiyo ofisini kwake ifikapo saa 11 leo jioni.

“Nataka unieleze ni kwa nini ulitoa maelekezo ya kufunga mita hizo, na kwa nini jana uliamua kubadili uamuzi huo? Ni kwa nini umeamua kuchukua maamuzi haya baada ya kupokea ujumbe wa simu ya mkononi (sms) wakati mita zimekaa bila kufanya kazi kwa miaka mitano? Ni kwa nini umeamua kufanyia kazi ujumbe wa sms wakati unajua Serikali inafanya kazi kwa maandishi rasmi?” alisema Waziri Mkuu.

“Umesema mlikuwa mnatumia utaratibu wa kupima kwa kijiti. Huu hauna uhakika na huwezi kutegemea taarifa ya mtu mwingine au kuingia kwenye meli ya mtu na kuanza kuchukua vipimo hadi ujiridhishe. Nataka kujua ni kwa nini mlikuwa na utaratibu wa ku-bypass mafuta ili yasipite kwenye mita za kupimia mafuta? Ni kwa nini umetoa amri zianze kutengenezwa jana na siyo mwaka 2012 au 2013?” alihoji Waziri Mkuu.

Waziri Mkuu alisema mita hizo za Kurasini zilinunuliwa na Serikali kwa gharama za dola za marekani milioni 1.2 (wakati huo) na haiwezekani kuacha kuzitumia wakati watu wanachezea mifumo na kuongeza mianya ya kupoteza mapato kwa Serikali. Ameagiza mita hizo zianze kufanya kazi mara moja.

Wazir Mkuu alisema matumizi ya mita hizo yaliafikiwa na Serikali baada ya kubaini upotevu mkubwa wa kodi kwenye mafuta yanayoingizwa nchini na baada ya kuona hakuna tija ya kuendelea na ukadiriaji au kupokea taarifa za waagizaji peke yao.
 
Waziri Mkuu ambaye aliwasili Kurasini leo saaa 4: 30 asubuhi (Alhamisi, Februari 11, 2016) kwenye kitengo hicho kilichopo Kurasini (Kurasini Oil Jetty), alikagua mita hizo na kisha kwenda kukagua meli iliyokuwa ikishusha mafuta bila kutumia mita hiyo ya kupima mafuta yanayopokelewa kwa sababu mafundi walikuwa bado wanaendelea na ukarabati.

Akiwa Kurasini, Waziri Mkuu alielezwa na Bibi Chuwa kwamba mita hizo zilianza kufanyiwa ukarabati jana na leo asubuhi moja imekamilika ambayo ni ya kupokelea mafuta ya petroli. Ya dizeli ilikuwa inafunguliwa na mafundi na kukutwa imejaa kutu sababu ya kutotumika kwa muda mrefu.

“Hii ya dizeli imefunguliwa leo na ile ya mafuta ya kula, haijawahi kufanya kazi tangu ilipofungwa mwaka 2011,” alielezwa Waziri Mkuu na Kaimu Mkurugenzi wa Bandari, Eng. Aloyce Matei.

Alipoulizwa ni kwa nini aliamua kuzifungia mita hizo ziisifanye kazi, Bi. Chuwa alijibu kuwa alifikia uamuzi huo baada ya kupokea malalamiko kwamba zinawapunja wateja. Hata hivyo, hakufafanua ni wateja gani au wa aina gani.

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu Majaliwa, ametembelea na kukagua mita mpya za kupimia mafuta ambazo zinajengwa Kigamboni. Mita hizo zimegharimu dola za marekani milioni 6 (sawa na sh. bilioni 12.96/- za sasa).

Akiwa hapo, Waziri Mkuu alielezwa kwamba ujenzi huo ambao ulianza miezi nane iliyopita, unatarajiwa kukamilika ifikapo katikati ya mwezi Machi, 2016. “Tunajitahidi kazi hii ikamilike ifikapo katikati ya mwezi ujao,” alisema Eng. John Bura, Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya BQ Contractors Ltd ambayo inasimamia ujenzi wa mita hizo.

Vilevile, Waziri Mkuu alitembelea sehemu ya kuchukulia mafuta yanayotoka bandarini (TPA Manfold) iliyoko Kigamboni na kukagua mitambo ya kusambazia mafuta kwenye matenki ya mafuta ya kampuni ya TIPER yaliyoko Kigamboni yanayomilikiwa kwa ubia bainaya Serikali na kampuni ya Oryx Energies.

Katika ziara hiyo ilibainika kuwa Kampuni ya TIPER imejiunganishia bomba la moja kwa moja kutoka kwenye bomba kubwa la mafuta linalotoka bandarini hali iliyomlazimu Waziri Mkuu kuagiza kwamba bomba hilo litolewe kwenye maungio hayo ndani ya mwezi mmoja.

“Natoa mwezi mmoja hili bomba liondolewe kwenye mfumo huu na kama yapo mabomba mengine pia yaondolewe,” alisema huku akionyesha karatasi iliyokuwa mfukoni kwake yenye mchoro unaobainisha kuwa kuna bomba jingine la inchi 10 limeungwa kinyemela kwenye bomba kuu.

“Kila mmoja anapaswa aje kuchukua pale kwenye manfold ili tujue nani kachukua nini. Msajili wa Hazina hili ni eneo lako na wewe unamiliki TIPER kwa asilimia 50, hebu simamia hili. Ninyi TPA leteni mapendekezo yenu Serikalini ili tuone tunaweza kudhibiti vipi vitendo kama hivi,” alisema Waziri Mkuu.

Pia alimtaka Msajili wa Hazina, Bw. Lawrence Mafuru awasiliane na Mwanasheria Mkuu ili waangalie upya mkataba na umiliki wa matenki hayo uwe chini ya Serikali kwa asilimia 100 ili mafuta yanayoagizwa na Wakala wa Uagizaji Mafuta kwa Pamoja (Petroleum Bulk Procurement Agency) yaweze kuhifadhiwa huko.

Mapema, Waziri Mkuu ambaye alifuatana na Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Prof. Makame Mbarawa, alikagua eneo la manfold ya Mamlaka ya Bandari iliyopo Kigamboni na kukuta ni kampuni nne tu zenye matenki Kigamboni ambazo zinachukua mafuta yao hapo.

Kampuni hizo ni HASS, WORLD OIL, LAKE OIL na MOIL. TIPER haikutaka kufuata mfumo huo licha ya kuwa nafasi ya kufanya hivyo ipo. Kampuni nyingine zenye matenki yake nchi kavu, zinachukulia mafuta kwenye manfold ya Kurasini.

Askofu Gwajima, Sheikh Wa Mkoa Dar Wakwama Kumjulia Hali Mufti

$
0
0

Jopo la Madaktari wanaomtibu Mufti na Sheikh Mkuu wa Tanzania, Abubakar Zubeir  wamezuia kwa muda watu kwenda kumtembelea kiongozi huyo wa dini ili apate muda zaidi wa kupumzika.
 
Daktari wake, Profesa Mohamed Janabi jana jioni alisema: “Tumewaomba Mufti aachwe kwa muda ili apumzike. Mimi, Dk Mwanga, Dk Othman na Dk Abel tumeshauri leo (jana) apumzike na kupewa mazoezi zaidi maana watu wa madhehebu yote wamekuwa wengi mno.”

Hatua hiyo ya Dk Janabi ambaye ni Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete alikolazwa Mufti Zubeir, iliwafanya viongozi mbalimbali wa dini akiwamo, Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam Alhad Mussa Salum, Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima pamoja na Mbunge wa Kinondoni Mussa Mtulia kushindwa kumwona jana.

Viongozi hao waliowasili katika taasisi hiyo ya Muhimbili saa kumi na moja jioni, walitumia saa nzima kusubiri kama watapata ruhusa ya kumuona Mufti bila mafanikio.

“Nimekuja hapa kumuona Mufti Zubeir kama kiongozi mwenzangu wa kidini, tunamwombea heri apate ahueni,” alisema Askofu Gwajima ambaye baadaye aliamua kuondoka.

Mtulia alisema baada ya kufika hospitalini hapo wamekuta maelekezo kwamba daktari wake ameomba apumzishwe, daktari anataka apone haraka kwani wageni wamekuwa wengi.

“Nilikuja kumwona Sheikh Zubeir baada ya kufika nimeshindwa kumuona baada ya daktari wake kuomba aachwe apumzike, tunaamini tutapata muda wa kumuona baadaye Jumamosi,” alisema Mtulia.

Katibu Mkuu wa Baraza Kuu la Waislamu wa Tanzania (Bakwata), Sheikh Suleiman Lolila alisema jana kuwa hatua hiyo imekuja baada ya kuwapo na watu wengi, ndugu, jamaa na marafiki wanaotaka kumjulia hali na kumfanya akose muda wa kupumzika.

“Hali ya Mufti inaendelea vizuri, tunajua Mufti ni mtu wa watu, lakini tunataka apate muda zaidi wa kupumzika, tunachofanya ni kudhibiti wingi wa watu,”
alisema Sheikh Lolila.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live


Latest Images