Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Mbuzi Na Kondoo 200 Wakatwakatwa Mapanga Wakituhumiwa Kuvamia Shamba La Mkulima Huko Mvomero Morogoro

$
0
0

Zaidi ya Mbuzi na kondoo 200 huko Dihinda mvomero Mkoani Morogoro wamekatwa katwa na walinzi wa jadi kutoka Gairo wanaojulikana kwa jina la Mwanu ' 
 
Taarifa zinadai kuwa mifugo hiyo ilikula nusu ekari ya mazao ya mkulima mmoja kijijini hapo na taarifa zikawafikia walinzi hao ambao walifika na kukatakata mifugo hiyo mali ya mama mmoja mjane mfugaji wa jamii ya kimasai
 
Lakini Inadaiwa kuwa mifugo ya mama huyo haikuhusika kula mazao hayo bali ni mifugo ya mfugaji mwingine.
 
Waziri mwenye dhamana kupitia wizara ya mifugo na kilimo hivi sasa ameelekea eneo la tukio .

Tiba Ya Kunenepesha Uume Wakati Wa Tendo La Ndoa

$
0
0
Tiba  hizi  uufanya  uume  Kunenepa  wakati  wa  tendo  la  ndoa  na  mhusika  anatakiwa  kuwa  anazitumia  kila  anapotaka  kufanya  tendo  la  ndoa.
 ================================

1.   AINA  YA  KWANZA  ;
Chukua  zubadi  za  baharini  kiasi  cha  robo  kilo, kisha  ziponde  ponde   hadi zilainike  kabisa  na  kuwa  unga  unga, kisha  changanya  na  asali robo.

MATUMIZI  YAKE :  Lisaa  limoja  kabla  ya  kukutana  na  mwanamke, tumia  kuuchua  uume  wako  kwa  muda  wa  dakika  kumi  hadi  kumi  na  tano.  Utakapo muingilia  mke  wako, uume  wako  utanenepa  na  kututumka  isivyo  kawaida.
 
Utakuwa  unafanya  hivyo  kila  mara  utakapo hitaji  kumuingilia  mwanamke.

2. AINA  YA  PILI :   Chukua  dawa  inaitwa  filfil  nyeupe, changanya  na  dawa  inaitwa  sambalu, khulinjani  pamoja na   miski  kwa  vipimo  vinavyo  lingana, kisha utachanganya na  asali pamoja  na  dawa  inaitwa  zanjabila marbiy.
 
MATUMIZI : Tumia  kuuchua  uume  wako   kwa  muda  wa dakika  tano  hadi  kumi, nusu  saa  kabla  haujamuingilia  mke  wako. Ama  kwa  hakika, uume  wako  utanenepa  na  kututumka  sana wakati wa  tendo.

3. AINA  YA  TATU:  Chukua  dawa  ya asili  inaitwa  Ilqu, kiasi  cha  robo kilo, itie  kwenye  birika ama  chupa  ya  glasi,  kisha  changanya  na  dawa  inaitwa  mbomboto ( tumia  mbomboto yenye  joto ) , utaacha mchanganyiko  wako  kwa  muda  wa  siku  ishirini  na  moja. Baada  ya  siku  ishirini na  moja, dawa  zako  zitakuwa  zimechanganyikana na  kuwa  kama  mafuta.
 
MATUMIZI : Tumia   kuuchua  dhakari  yako  kwa  muda  wa  dakika  ishirini hadi  thelathini, kisha  kaa  nusu  saa  halafu  nenda  kamuingilie  mkeo.  Dhakari yako, itanenepa  na  kurefuka.
 
Baada  ya  kumaliza  tendo, utatakiwa  kuichua  dhakari  yako  kwa  kutumia  juisi  ya  zabibu  ili kuufanya  urudi  katika  hali  yake  ya  kawaida.

4. AINA  YA  NNE  :   Chukua qadbwib ya  kiwindwa  cha  mnyama  pori, chukua  qadbwib ya  mnyama  anaye  fugwa kama  vile  n’gombe  au mbuzi, pamoja  na  qadbwib   ya  dhi-ibu, kisha  pika kwenye  maji  lita  tano. Utachemsha  dawa zako mpaka  maji  lita  tano  yapungue na  kubaki nusu  yake .
 
Baada  ya  hapo, utachukua  punje  za ngano  kiasi  cha  kilo tatu, halafu  utaziloweka  kwenye  dawa  yako  kwa  muda  wa masaa matatu.

Baada  ya  masaa  matatu, zitoe  hizo  punje  za  ngano  na  uzisafishe  halafu  chukua  kuku  jike  mweusi  asie  kuwa  na  doa  la  rangi  nyingine, kuku  huyo  utamtia  kwenye  banda  maalumu  la  kufugia  na  utakuwa  unamlisha  hizo  punje  za  ngano  kwa  muda  wa  siku  saba . 

( HAKIKISHA  KUKU  WAKO  ANAMALIZA  KULA  PUNJE  ZOTE KILO TATU  NDANI  YA  SIKU  SABA  ).
 
Baada  ya  siku  saba, utamchinja  kuku  wako  na  kumla  peke yako. Hakika  uume  wako   utakakamaa, utanenepa na  kurefuka kwa  kiasi kikubwa  sana.

5. NJIA  YA  TANO.
Chukua   kijiko  kimoja  kikubwa  cha  unga  wa  mdalizi, changanya  kwenye  kikombe  kikubwa  chenye  maji  ya  moto, koroga  kisha  kunywa  mara  tatu  kwa siku, asubuhi, jioni  na  usiku  kwa  muda wa  siku  saba, halafu siku  ya  saba  ikifika , utachukua  maji  ya  fatiru.
 
Utatumia  kuchua  dhakari  yako  kwa  maji  ya  fatiru  hadi  utakapo  ona   kichwa  cha  dhakari yako kimebadilika  rangi  na  kuwa  nyekundu.
 
Kama wewe  ni mwarabu,  muhindi  au  ngozi  nyeupe  yoyote, uume  dhakari  yote  itabadilika  na  kuwa  na  rangi  nyekundu.
 
Dhakari  yako  ikisha  badilika  na  kuwa  na  rangi  nyekundu, utaichua kwa  kutumia  asali  iliyo  changanywa  na  tangawizi  kwa  muda  wa  dakika  kumi.
 
Baada  ya  hapo, nenda  kamuingilie  mwanamke . Uume  wako, utakakamaa, utanenepa  na  kurefuka  kwa  namna  itakayo  kushangaza.

6.   NJIA  YA  SITA :
Chukua filifili nyeupe, changanya na  sambal  katika  vipimo   sawa, ponda  ponda  kupata  unga wake  halafu  changanya  na  asali  ya  zanjabiila  murbiy  kisha  tumia  kuchua  dhakari  yako kwa  muda  wa  dakika  thelathini. Dhakari  yako  itanenepa  na  kurefuka  kwa  kiasi  kikubwa  sana   kila  utakapo  kuwa  uki muingilia  mwanamke  wako.

7.NJIA  YA  SABA :  Kuchanjiwa  kwa  dawa inaitwa  miyegea.  Unatafutwa  mti  wa  myegea  ambao  unaanza  kuchipukia, halafu utomvu  wake  anachanjiwa  mwanaume  kwenye  dhakari. Basi  kila  tunda  la  mti  huo  litakapo  kuwa  linaongezeka  ndivyo, uume  wa  mwanaume  huyo  unakuwa  unaongezeka. ( TIBA  HII, HUTOA  MATOKEO  YA  KUDUMU )

( Kwa  watakao  hitaji  huduma  ya  kuchanjiwa, wawe  tayari  kusafiri  hadi  kijijini  )

8.  NJIA  YA  NANE :  Kunywa  maji  yaliyo  changanywa  na  unga  wa  mdalizi, pamoja  na  mizizi  saba  ya  mti  unaitwa  “MWAMBAMJI “. Hakika  uume  wako  utanenepa  na  kurefuka  wakati wa  tendo  la  ndoa.

KWA  MAHITAJI  YA  MOJA  WAPO KATI  YA  DAWA  ZILIZO  TAJWA  HAPO   WASILIANA  NA  DR. MUNGWA  KABILI, KWA  SIMU  NAMBA   0744 000 473.
 
NAPATIKANA  JIJINI  DAR  ES  SALAAM.
NA KWA  TAARIFA  ZAIDI  KUHUSU  HUDUMA  ZANGU, TEMBELEA  KILA  SIKU :

Jeshi la Polisi kikosi cha Wanamaji Lakamata Mafuta ya Wizi aina ya Diesel Katika Bandari ya Dar es Salaam

$
0
0

Jeshi la Polisi kitengo cha majini limekamata tani zipatazo 20 za mafuta ya Dizeli yaliyokuwa katika Jahazi lililokuwa kando ya bandari ya Dar es Salaam likijiandaa kwa safari ya kwenda Zanzibar.
 
Mkuu wa Kitengo hicho cha polisi cha wanamaji Bwana Mboje John Kanga amesema watu watano wanashikiliwa kuhusiana na tukio hilo na uchunguzi zaidi unaendelea.

Rais Magufuli Atuma Salamu za Pole Kwa Mke wa Waziri Mkuu Mstaafu Mama Tunu Pinda Aliyepata Ajali ya Gari Jana

$
0
0

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, amemtumia salamu za pole Mke wa Waziri Mkuu Mstaafu Mama Tunu Pinda aliyepatwa na ajali ya gari, iliyotokea jana tarehe 08 Februai, 2016 akiwa safarini kutoka Dodoma kwenda Dar es salaam.

Ajali hiyo imetokea katika eneo la Mkundi lililopo katika Manispaa ya Morogoro ambapo gari aliyokuwa akisafiria Mama Tunu Pinda, ilipinduka baada ya kumgonga mwendesha pikipiki aliyeingia ghafla barabarani.

Katika salamu hizo alizozituma kupitia kwa Waziri Mkuu Mstaafu Mheshimiwa Mizengo Kayanza Peter Pinda, Rais Magufuli amesema amepokea kwa mshtuko taarifa za kutokea kwa ajali hiyo na amemuombea Mama Pinda na Majeruhi wengine kupona haraka.

"Kupitia kwako Mheshimiwa Waziri Mkuu Pinda, naomba unifikishie pole nyingi kwa mkeo Mama Pinda kwa kuumia katika ajali hii, na namuomba Mwenyezi Mungu awaponye majeruhi wote ili waweze kuendelea na shughuli zao za kila siku" alisema Rais Magufuli.

Mama Tunu Pinda anaendelea kupata matibabu Jijini Dar es salaam, na hali yake inaendelea vizuri.

Gerson Msigwa
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
Dodoma
09 Februari, 2016

Update: Waziri Mwigulu Nchemba Amefika Eneo la Mapigano ya Wakulima na Wafugaji na Kuamuru Mambo Haya

$
0
0
Waziri wa Kilimo, Uvuvi na Mifugo, Mwigulu Nchemba ametembelea Kijiji cha Kigurukwa mjini Morogoro kulikotokea mapigano ya Wakulima na Wafugaji yaliyosababisha kuuawa kwa mbuzi takribani 200.

Waziri Mwigulu ameagiza Kamati ya Ulinzi ya Mkoa kuhakikisha wote waliohusika katika tukio hilo wanakamatwa na kuchukuliwa hatua za kisheria. 
 
Pia ameagiza kutekelezwa haraka hukumu ya mahakama iliyotolewa mwaka 2005 iliyoagiza kuwekwa kwa mipaka kati ya eneo la wafugaji na wakulima

Picha: Edward Lowassa Amjulia Hali Mafti Mkuu wa Tanzania Sheikh Aboubakary Zubeiry Aliyelazwa Muhimbili

$
0
0
Aliekuwa  mgombea urais kwa tiketi ya Chadema ,Edward Lowassa  leo amemtembelea Mufti Mkuu wa Tanzania Sheikh Aboubakary Zubeiry aliyelazwa Hospitali  ya Muhimbili baada ya kufanyiwa upasuaji wa tumbo juzi

Adhabu Ya Kifungo Cha Nje Kwa Mujibu Wa Sheria Ya Huduma Kwa Jamii

$
0
0
Kwa mujibu wa kifungu na 3(2) (a) cha Sheria ya Huduma kwa Jamii ya mwaka 2002 kifungo cha nje ni utaratibu ambao unampa fursa mfungwa kutumikia kifungo chake nje ya gereza kwa kufanya shughuli/kazi zisizo na malipo kwa manufaa ya jamii.
 
Utaratibu huu hutolewa kwa wafungwa ambao vifungo vyao havizidi miaka mitatu bila kujali wana faini au hawana. Wapo wahalifu wanaohukumiwa moja kwa moja mahakamani kwenda kutumikia kifungo cha nje na wengine huingia gerezani kwanza na baadaye utaratibu wa maombi maalum hufanyika ili mfungwa husika kwenda kutumikia kifungo kwa utaratibu huo.
 
Sheria ya Magereza Sura ya 58 kifungu Na. 52 (1) (2) inatoa utaratibu wa kumuondoa mfungwa aliyepo gerezani huku akiwa ana sifa ya kutumikia kifungo chake kwa utaratibu wa huduma kwa jamii.
 
Kifungu hicho cha Sheria kinaeleza kuwa pale ambapo Mkuu wa gereza atajiridhisha kuwa kuna mfungwa ambaye ana sifa ya kutumikia kifungo chake chini ya utaratibu wa huduma kwa jamii, atamshauri mfungwa huyo juu ya utaratibu huo kwa kuzingatia sifa alizonazo na ikiwa mfungwa huyo ataridhia kuachiliwa kwake katika utaratibu wa huduma kwa jamii, Mkuu wa Gereza atawasilisha maombi maalum katika Mahakama iliyomfunga kwa ajili ya maandalizi ya kuachiliwa kwa mfungwa huyo katika utaratibu wa huduma kwa jamii.
 
Mahakama baada ya kupokea maombi hayo, itafanya uchunguzi kulingana na kifungu Namba 3 cha Sheria ya Huduma kwa jamii na ikijiridhisha kuwa mfungwa husika ana sifa za kutumikia katika utaratibu wa Huduma kwa jamii, Mahakama husika itatoa amri ya kuachiliwa kwa mfungwa huyo chini ya utaratibu huo.
 
Aidha, Usimamizi na Utekelezaji wa adhabu hii husimamiwa na Idara inayojitegemea ya Huduma kwa Jamii iliyopo chini ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
 
Mfungwa anayetumikia kifungo cha nje ni lazima aishi kwa kufuata Sheria na masharti aliyopangiwa. Masharti hayo ni kuwa chini ya uangalizi maalum, kutoondoka nje ya Mkoa bila kibali na kuhakikisha kuwa hatendi kosa lolote mpaka muda wake wa kifungo chake utakapokamilika.

Imetolewa na;
Lucas Mboje, Mrakibu Msaidizi wa Magereza,
Afisa Habari wa Jeshi la Magereza,
DAR ES SALAAM
09 Februari, 2016

TPDC yakanusha taarifa iiliyochapishwa kwenye Gazeti la Mtanzania la Jumapili tarehe 7 Februari 2016

$
0
0

Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC), linapenda kuchukua fursa hii kukanusha taarifa iiliyochapishwa kwenye Gazeti la Mtanzania la Jumapili tarehe 7 Februari 2016 Toleo Na: 8087 lenye kichwa cha habari ‘TPDC kwafukuta’.  Taarifa hii si sahihi na ina lengo la kulichafua Shirika na kuupotosha umma wa Watanzania.

TPDC ni Shirika la Umma, linalomilikiwa kwa asilimia mia moja na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, hivyo taratibu za kuliendesha Shirika hufuata sheria, taratibu na kanuni za nchi.

Hii ina maana kwamba, taratibu za kupata Kampuni ya kufanya Utafiti wa Vitalu vya mafuta na gesi kwa kutumia teknolojia ya ‘Airborne Gravity Gradiometry’   ilifuata sheria ya manunuzi ya umma ya mwaka 2011 pamoja na kanuni za manunuzi ya umma za mwaka 2013.

Aidha, tungependa kuwafahamisha watanzania kwamba taarifa iliyotolewa na gazeti la Mtanzania zilikuwa zina lengo la kupotosha umma kwani zoezi zima la kutafuta mkandarisi lilikuwa la wazi na lilihusisha kampuni tatu ambazo ni Bell Geospace ya Marekani, CGG ya Ufaransa na ARKEX ya Uingereza ambazo ndizo kampuni pekee zenye uwezo wa kutumia teknolojia tajwa hapo juu.

Kutokana na kuwepo kwa kampuni tatu tu hapa dunia zenye utaalamu uliohitajika, Shirika liliwasiliana na kampuni husika kwa mujibu wa kanuni ya manunuzi  ya umma ya mwaka 2013 namba 152(1) (b) ili kuwasilisha taarifa za kiufundi na kifedha  kwa TPDC.

Baada ya taratibu hizo za manunuzi kufanyika, ndipo kutokana na tathimini iliyofanyika, Kampuni ya CGG ndiyo iliyopewa kazi ya kufanya utafiti maeneo yafutayo; Eyasi – Wembere iliyopo Manyara, na Mandawa Mkoani Lindi wakati Lake Tanganyika North iliyopo Kigoma, ilifanywa na kampuni ya Bell Geospace.

“Airbone Gravity Gradiometry” ina gharama nafuu, inachukua eneo kubwa la utafutaji na kwa kipindi kifupi sana. Ni aina ya teknolojia inayotafiti maeneo mapya ya utafutaji na yale ambayo tayari yameshaonyesha dalili nzuri za utafutaji wa hapo awali. Imechukua miezi mitatu tu kwenye maeneo tajwa hapa nchini kukamilisha kazi ya kukusanya data.

TPDC inakanusha vikali kuwepo kwa shinikizo toka kwa Mtu au Taasisi yoyote katika kufanikisha zoezi hili, aidha Shirika linasisitiza kuzingatiwa kwa utaratibu wa sheria za manunuzi na hivyo kuwataka Watanzania kupuuza taarifa hizi zilizotolewa na gazeti la Mtanzania kwani ni za uzushi na upotoshaji mkubwa.

Tunawaomba wadau wote wa sekta ndogo ya mafuta kuendelea kufanya kazi za utafiti, utafutaji na uendelezaji wa sekta nzima ya gesi asilia.

“Gesi Asilia kwa Maendeleo ya Taifa”

Imetolewa na:
Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji
Shirika la Maendeleo ya Petroli ya Tanzania

Jaji Mkuu Wa Tanzania Mhe. Mohamed Chande Othman Amshukuru Rais Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli Kwa Kutimiza Ahadi Yake

$
0
0

Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Mohamed Chande Othman amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.John Pombe Magufuli kwa kutimiza ahadi yake ya kuipatia Mahakama kiasi cha shilingi Bilioni 12.3 alizoahidi wakati wa maadhimisho ya Siku ya Sheria Februari 4, 2016 jijini Dar es salaam.
 
Amesema Fedha hizo zitatumika  katika utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwemo uboreshaji wa miundombinu ya Mahakama na ujenzi wa Mahakama mpya katika maeneo mbalimbali nchini.
 
Akitoa shukrani hizo leo jijini Dar es salaam Mhe.Othman amesema kuwa kwa mara ya kwanza tangu mwaka 2012 Mahakama imepata asilimia 100 ya fedha zote za Maendeleo zilizokasimiwa na Bunge kwenye Bajeti yake ya mwaka 2015/2016.
 
Amesema  kupatikana kwa fedha hizo ambazo ni za Maendeleo kutasaidia kufufua miradi ya ujenzi iliyosimama, kufufua Mahakama ambazo zilikua hazifanyi kazi kwa sababu ya uchakavu na kuipatia Mahakama fursa zaidi ya kutoa huduma bora kwa wananchi kwa kuwasogezea huduma za Haki karibu katika maeneo wanayoishi.
 
Mhe.Othman ameeleza kuwa kwa kipindi cha bajeti za miaka 3 mfululizo kuanzia mwaka 2012 /2013 hadi 2014/2015  Mahakama ilikua ikipokea fedha pungufu ya kiasi kilichopangwa katika Bajeti hali iliyochangia kuzorota kwa shughuli za Mahakama.
 
” Kwa mara ya kwanza Mahakama tumepata asilimia 100 ya Bajeti yetu ya mwaka 2015/2016 kutoaka Serikalini, mwaka 2012/2013 tulipata shilingi bilioni 26.9 ikiwa ni pungufu ya bajeti yetu kwa asilimia 78, mwaka 2013/2014 tukapata Bilioni 42.7 pungufu kwa asilimia 82 na mwaka 2014/2015 tulipewa shilingi  bilioni 41.5 ambayo ni pungufu kwa asilimia 92 “
 
Akizungumzia miradi ya ujenzi wa majengo mapya ya Mahakama amesema kuwa tayari Mahakama ina michoro ya ramani za majengo yatakayojengwa katika maeneo mbalimbali ambayo hayakuwa na huduma hiyo ikiwemo mikoa 12 kati ya 25 ambayo haina Mahakama Kuu, wilaya 22 kati ya 133 ambazo hazina Mahakama za Wilaya pamoja na kuongeza Mahakama za Mwanzo ambazo ziko 976 kufikia kata zote 3,957.
 
Kuhusu  Mradi wa ujenzi wa  jengo la Makao Makuu ya Mahakama utakaofanyika katika uwanja wa Chimala jijini Dar es salaam amesema  utahusisha  maeneo mbalimbali ya utoaji huduma za Kimahakama na kuongeza kuwa  Mahakama itajenga  jengo lenye viwango kwa kuwatumia Wakandarasi  na wataalam wa kitanzania watakaojenga  Mahakama nzuri na yenye viwango kwa gharama  nafuu.
 
“Mahakama tutatoa kipaumbele kwa wataalam wetu wa ndani ili waweze kutujengea Mahakama zetu, tunalenga kuwafikishia huduma zetu katika maeneo wanayoishi  tunao mfano mzuri wa Mahakama ya mwanzo ya Dumila iliyoko Morogoro, Mahakama hii imejengwa kijijini ni ya kisasa” Amesisitiza Mhe.Othman.
 
Kwa upande wake Waziri wa Katiba na Sheria Dkt. Harrison Mwakyembe amesema kuwa Serikali itaendelea  kushirikiana na Mahakama ya Tanzania ili kuwezesha ufanisi wa shughuli zake kwa kuhakikisha kuwa kiwango cha fedha za Bajeti kinachopitishwa kwa ajili ya kuhudumia shughuli za  Mahakama kinafika kwa wakati.
 
Akizungumzia kuhusu uanzishwaji wa Mahakama ya Mafisadi, amesema uanzishwaji wake uko katika hatua nzuri na wakati ukifika wananchi watataarifiwa kama ilivyoahidiwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kuungwa mkono na Mahakama ya Tanzania.
 
Naye Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip  Mpango, akizungumzia fedha za Maendeleo zilizotolewa  na Mhe.Rais amesema kuwa lengo la ahadi ya Rais kwa Mahakama ilikua ni kuhakikisha Haki inapatikana kwa wananchi kwa Wakati na kwamba miongoni mwa vitu vilivyokua vikichelewesha haki kwa watanzania walio na mashauri Mahakamani ni ukosefu wa fedha na uchakavu wa miundombinu.
 
Amesema Serikali inaendelea kujenga uwezo wa kifedha ili kuimarisha huduma katika mihimili yote ikiwemo Bunge na Mahakama huku msisitizo ukiwekwa katika kukusanya mapato ya ndani.
 
“Kwa kushirikiana na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) tuna dhamira ya dhati ya kukusanya mapato ya ndani ili kujenga uwezo wa Serikali tutawabana wote waliokuwa wanakwepa kulipa kodi na hili tutalisimamia kikamilifu”
 
Amesema utoaji wa Haki ni moja ya ukuzaji wa maendeleo ya nchi na kuongeza kuwa Mahakama ya Tanzania inafanya kazi nzuri pamoja na ufinyu wa bajeti yake.

Waziri Wa Maliasili Na Utalii Prof. Jumanne Maghembe Azungumzia Tukio La Kushambuliwa Helkopta Ya Doria Iliyopelekea Kifo Cha Rubani Wake.

$
0
0


 
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI KUHUSU TUKIO LA KUSHAMBULIWA KWA HELKOPTA YA DORIA NA KUUAWA KWA RUBANI ROGERS GOWER TAREHE 29/01/2016

1.0 UTANGULIZI

Itakumbukwa kuwa mnamo tarehe 29/01/2016 lilitokea tukio la kuhuzunisha ambapo majangili walishambulia helikopta iliyokuwa inafanya doria katika maeneo ya Pori la Akiba Maswa na Ranchi ya Wanyamapori ya Mwiba. Shambulio hilo lilisababisha kifo cha Rubani Bw. Rogers Gower raia wa Uingereza na kuharibika vibaya kwa helkopta hiyo baada ya kuanguka. Aidha, katika tukio hilo Bw. Nick Desta aliyekuwa pamoja na Bw. Rogers aliweza kunusurika na kukimbizwa Nairobi kwa ajili ya matibabu zaidi.

Tarehe 30/01/2016 nilitembelea eneo la tukio ili kujionea hali halisi na kutoa tamko la serikali. Haiyumkini, kutokana na kuguswa na kadhia hiyo, Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John P. Magufuli alitoa maelekezo kwa Wizara ya Maliasili na Utalii ya kuanza kufanya msako haraka wa kuhakikisha kuwa wahalifu hao wanakamatwa na kufikishwa kwenye vyombo vya Sheria. Aidha, Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Major Gen. Gaudence Millanzi akifuatana na Mwenyekiti wa Bodi  ya Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA), Major Gen. Hamisi Semfuko na baadhi ya watendaji wa Wizara walitembelea eneo hilo tarehe 02 hadi 03/02/2016.

Napenda kuwajulisha kuwa, katika ziara zote mbili tuliweza kushuhudia namna watendaji wa Wizara ya Maliasili na Utalii (Pori la Akiba Maswa, Kikosi Dhidi Ujangili Bunda, Hifadhi ya Taifa Serengeti na Mamlaka ya Hifadhi Ngorongoro)  kwa kushirikiana na vyombo vya Ulinzi na Usalama vya Taifa na vya Mkoa wa Simiyu na Wilaya ya Meatu na Maofisa kutoka Makao Makuu ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Viongozi  wa FRIEDKIN CONSERVATION FUND, Bw. Dan Friedkin na Bw.  Pratik Patel na watumishi wengine kwa pamoja walisaidiana sana katika kuendesha msako kwa juhudi kubwa na weledi wa hali ya juu. Kazi hii ilifanyika usiku na mchana katika mazingira magumu na hatarishi. Mara kadhaa watendaji hao wamekuwa wanalazimika kuvuka makorongo na mito yenye maji mengi kwa kuogelea kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha katika maeneo hayo.

Mtakumbuka kuwa taarifa zilizopatikana baada ya tukio hilo la kusikitisha zilibainisha kuwa majangili waliohusika na tukio hilo walikuwa watatu (03) na kwamba walikuwa na bunduki mbili aina ya rifle zenye ukubwa wa mtutu (calibre) wa 303 na .458 mtawalio. Aidha, wakati wa tukio hilo, majangili hao tayari walikuwa wamefanikiwa kuua tembo mmoja na kutoweka na meno yake mawili.

2.0 HATUA ZILIZOFIKIWA:
Kama mlivyosikia kwenye taarifa iliyotolewa na Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Simiyu, sote kwa pamoja tunafarijika kuwajulisha kuwa jitihada zilizofanyika za kuwasaka wahalifu hao ndani ya kipindi cha wiki moja zimeleta matokeo mazuri ambapo:

·watuhumiwa wote muhimu (key suspects) waliotajwa kuhusika na tukio hilo wamekamatwa na wote wamekiri kuwepo kwenye tukio. Mmojawapo anatuhumiwa kuhusika moja kwa moja na kufyatua risasi iliyosababisha kuanguka kwa ndege hiyo na hatimaye kifo cha rubani.

·  bunduki mbili zilizotumika aina ya Rifle Calibre 303 na .458 zinazoshukiwa kutumika kwenye uhalifu huo zimekamatwa pamoja na risasi 5 za .458 na moja ya 303;

·   meno mawili ya tembo aliyeuawa siku ya tukio yenye uzito wa kilo 31 yamekamatwa;

·   pikipiki moja ambayo inashukiwa kuhusika katika tukio hilo na matukio mengine ya uhalifu imekamatwa;

·  raia wema wanaendelea kutoa taarifa zinazobainisha kuwepo kwa mtandao mkubwa wa ujangili katika Mkoa wa Simiyu na maeneo ya jirani. Taarifa hizo zimesaidia kupanua wigo wa operesheni na kuwezesha kuboresha mbinu za mapambano dhidi ujangili.

3.0 MPANGO MAHSUSI WA WIZARA KUIMARISHA MAPAMBANO DHIDI  UJANGILI NA USAFIRISHAJI HARAMU WA MAZAO YA WANYAMAPORI NA MISITU

Tukio hili limetoa funzo kubwa kwa nchi yetu na linadhihirisha kuwa hivi sasa  baadhi ya majangili wamefikia hatua ya kujijengea uthubutu na ujasiri wa kutisha.

Kutokana na mazingira haya, Wizara ya Maliasili na Utalii imeamua kurejea (review) kwa haraka na kwa upana zaidi mbinu na mikakati yake ya vita dhidi ujangili wa wanyamapori na mazao ya misitu pamoja na usafirishai haramu wa mazao ya wanyamapori na misitu  kwa kufanya yafuatayo:

1.   Kukamilisha haraka uanzishaji wa Kikosi Maalum cha Kupambana na Uhalifu  wa wanyamampori (Wildlife Crime Unit);

2.   Kikosi hiki kitaundwa kwa kushirikisha Taasisi zote za Wizara (Idara ya Wanyamapori, Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA), Hifadhi za Taifa (TANAPA), Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA) na Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS). Aidha, kitafanya kazi kwa karibu na Vyombo vya Ulinzi na Usalama, Sheria, Mamlaka ya Bandari, Viwanja vya Ndege, Mamlaka ya Mapato Tanzania, Taasisi za Uhifadhi za ndani na nje ya Nchi na wadau wengine wa Uhifadhi;

3.   Kikosi hiki kitakuwa na jukumu la kuratibu na kufuatilia utendaji wa vikosi vidogo (Taskforce Coordinating Groups TCGs)) vilivyoundwa kwenye kanda nane za kiikolojia (ecosystem approach) ili kukabili kwa haraka nyendo zote za ujangili wa wanyamapori, uvunaji na usafirishaji haramu wa mazao ya wanyamapori na misitu;

4.   Kuharakisha ukamilishaji wa kubadilisha muundo wa utendaji kazi wa Wahifadhi Wanyamapori kutoka mfumo wa Kiraia  kuelekea mfumo wa Jeshi Usu (Paramilitary);

5.   Kuharakisha usimikaji wa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA) iliyozinduliwa Oktoba 2015 katika jitihada za kuimarisha na kuboresha uwekezaji binafsi wa Serikali katika maeneo yaliyopo nje na ndani ya Hifadhi za Taifa na Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorogoro;

6.   Kurejesha utaratibu wa kuwa na kada ya walinzi wa misitu (Forest Rangers) ambao watakuwa na uwezo wa kutumia silaha ambapo pamoja na kudhibiti uvunaji haramu wa misitu, utapanua wigo wa kukabili ujangili katika Hifadhi za Misitu;

7.   Kuishauri serikali kuangalia upya endapo bado kuna sababu za msingi kwa wananchi kuendelea kununua na kumiliki bunduki zenye mitutu mikubwa. Uamuzi huu unatokana na kuongezeka kwa matukio ya kukamatwa kwa silaha hizo zikiwa zinatumika kwenye vitendo vya uhalifu nje ya mikono ya wamiliki halali;

8.   Kuboresha utendaji kazi wa wahifadhi kwa kuwapatia mafunzo ya mbinu mpya za ukusanyaji habari na ufuatiliaji wa nyendo za majangili (intelijensia), kukusanya na kutunza kumbukumbu za ushahidi na kuendesha mashtaka (Inteligence, investigation and prosecution);


9.   Kuimarisha upatikanaji wa vifaa vya kisasa ikiwa ni pamoja na kuwashirikisha wadau wa uhifadhi katika kuchangia ununuzi/upatikanaji wa vifaa hivyo ili kukabili kasi ya mbinu mpya zinazotumiwa na majangili na wasafirishaji haramu wa mazao ya wanyamapori na misitu;
10.                Kwa kuwa katika Operesheni hiyo, wako Askari wa Wanyamapori wanaotuhumiwa kushiriki katika uhalifu wa kijangili, askari hao watafikishwa katika Mahakama ya kijeshi ili kukabiliana na mashitaka ya kijeshi ya kukiuka kiapo na dhamana waliyopewa.


4.0 HITIMISHO
Napenda kutumia fursa hii kutambua na kuwapongeza watendaji wote, Uongozi wa Mkoa wa Simiyu na Wilaya ya Meatu.  Napenda kupongeza na kuishukuru  Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Jeshi la Polisi, Jeshi la Wananchi, Usalama wa Taifa Shirika la Friedkin Foundation  na  wadau wengine wote walioshiriki katika msako huu hadi kufanikisha na kutimiza azma iliyokusudiwa na Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Dkt. John Pombe Magufuli pamoja na Watanzania wote wenye mapenzi mema na Taifa letu.

Kama nilivyotangulia kueleza, pamoja na mazingira magumu yaliyojitokeza wakati wa kutekeleza kazi hii, washiriki wote waliweza kuendesha operesheni hii kwa ari kubwa na weledi wa hali ya juu hadi kukamilisha lengo kuu  ndani ya kipindi kifupi. Aidha, naomba kuwashukuru wananchi wote ambao kwa namna ya pekee waliweza kutoa ushirikiano kwa kutoa taarifa muhimu zilizoweza kufanikisha lengo hili.

Pia nawashukuru wadau wote walioweza kutoa michango ya hali na mali kwa watendaji wa operesheni hii. Michango yao ilikuwa chachu kwa washiriki wa operesheni kuwajengea mazingira kuendelea kujituma kwa kupunguza makali ya ugumu wa mazingira wakati wanatekeleza jukumu hili.  Aidha, natoa wito kwa wananchi wote waendelee kuisaidia Wizara katika vita hii kubwa ya kukabili ujangili na usafirishaji haramu wa rasilimali zetu.


Imetolewa na:
Waziri wa Maliasili na Utalii
09/02/2016


Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumatano Ya Februari 10

Kesi Ya Kamanda Godfrey Nzowa Dhidi Ya Kamanda Suleiman Kova Kuunguruma Leo

$
0
0

Kesi ya maofisa wawili waandamizi wa polisi kutaka kuuziwa nyumba ya Serikali inaanza kunguruma leo katika kikao cha Mahakama ya Rufaa mjini Arusha.

Wanaopambana katika kesi hiyo ni Mkuu wa Kikosi cha Kupambana na Dawa za Kulevya, Godfrey Nzowa anayemshtaki kamanda mstaafu wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova.

Mwenyekiti wa Jopo la Majaji wa Mahakama ya Rufaa waliopo Arusha, Jaji Mbarouk Salum Mbarouk alisema juzi kuwa jumla ya kesi 50 zitaanza kusikilizwa wiki hii.

Alisema kati ya kesi zitakazosikilizwa, tisa ni za madai, 18 za jinai na 23 za maombi ya madai.

Mbali na Jaji Mabrouk, wengine wanaotarajiwa kusikiliza kesi hizo ni Jaji Musa Kipenka na Jaji Bernard Luanda.

Lowassa Atakiwa Kuvisaidia Vyombo Vya Dola Kukabiliana na Tishio La Kundi la al Qaeda Kuingia Nchini

$
0
0

WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Mohamed Aboud Mohamed amemtaka Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa kutoa taarifa za kuwapo kwa tishio la kundi la al Qaeda kuingia nchini kwa vyombo vya ulinzi na usalama ili vyombo hivyo, vishughulikie hatari hiyo.

Aboud amesema kwa kuwa Lowassa anaelewa madhara ya ugaidi na ana taarifa za kina kuhusu kundi hilo, ni vyema akazipeleka kwenye vyombo vya usalama.

“Kuna nchi za jirani ambazo zimekumbwa na madhara ya ugaidi, sasa kama kuna watu kama akina Lowassa na wengine wenye maono kama hayo au kuwa na taarifa za ziada za magaidi basi wapeleke Jeshi la Polisi ili zifanyiwe kazi,” alisema Aboud

Mwishoni mwa wiki, Lowassa ambaye alikuwa mgombea urais kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) katika uchaguzi mkuu wa mwaka jana, alionya kuwa ipo hatari Zanzibar ikatumiwa kuwa njia ya kuingia magaidi wa aina ya Al-Qaeda nchini.

Lowassa alidai kuwa hilo linaweza kufanyika, endapo jitihada maalumu hazitafanyika sasa katika kumaliza mkwamo wa kisiasa visiwani humo na kuzuia uwezekano wa kuvunjika kwa hali ya amani.

Lakini, Waziri Aboud aliyewahi kuwa Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi katika Serikali ya Awamu ya Nne, alisisitiza kuwa Zanzibar ina amani na utulivu na kuwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) imejipanga kuhakikisha hali ya utulivu na amani inaendelea kudumu.

“Kama serikali kupitia vyombo vyake vya usalama, vina utaratibu wake wa kuhakikisha inashughulikia watu wote wanaofanya uhalifu na vitendo vya uvunjifu wa amani kwa mujibu wa taratibu za nchi,” alieleza.

Alisema SMZ itahakikisha inatekeleza agizo la Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) la kufanyia uchaguzi wa marudio na kuwapo kwa vitisho kutoka kwa baadhi ya vyama vya upinzani.

“Tutatekeleza agizo la Tume ya Uchaguzi (ZEC) na niwahakikishie wananchi kuwa Zanzibar itaendelea kuwa na amani na utulivu kuanzia sasa, wakati wa kupiga kura na baada ya kupiga kura na kupokea matokeo,” alibainisha.

Zanzibar inatarajia kufanya uchaguzi wa marudio wa kuchagua Rais wa Zanzibar, Wawakilishi na Madiwani Machi 20, mwaka huu, baada ya ule uliofanyika Oktoba 25, mwaka jana kufutwa siku tatu baadaye kwa tangazo la Mwenyekiti wa ZEC, Jecha Salim Jecha kutokana na kuwapo kwa kasoro kadhaa.

Dk Phillip Mpango Akataa Kuwa Waziri OmbaOmba......Asema Serikali Haipo Tayari Kukubali Ndoa Za Mashoga Kisa Misaada Ya Wahisani

$
0
0

WAZIRI wa Fedha na Mipango, Dk Phillip Mpango amesema hatua ya Serikali ya kukusanya kodi kwa nguvu kwa baadhi ya wafanyabiashara waliotorosha makontena bila kulipiwa ushuru, haikuwa lengo la kumkomoa mtu, bali ililenga kukusanya fedha za Serikali yenye lengo la kuifanya nchi iache utegemezi wa wahisani.

Waziri huyo ambaye jana alikutana na makundi mbalimbali ya wafanyabiashara ofisini kwake Dar es Salaam, alisema yeye kama waziri wa fedha asingependa kuwa waziri ombaomba kwa wahisani, ambao alidai baadhi yao wana masharti magumu, ambayo hayatekelezeki kwa maadili ya Watanzania.

“Nimewasindikiza wenzangu huko nje kuomba fedha sasa nimechoka, nataka kutembea kifua mbele, maana wana masharti magumu, wengine wanataka turuhusu homosexual (ndoa za jinsia moja), masharti haya kwa kweli yanakera sana,” alisema Dk Mpango ambaye katika serikali iliyopita alikuwa Katibu Mtendaji wa Tume ya Mipango.

Dk Mpango aliongeza kuwa ili nchi isonge mbele, ni lazima ikusanye kodi ya kutosha; na jana aliahidi kuchukua hatua kadhaa, zitakazoiwezesha sekta binafsi kuwa mhimili wa kuimarisha uchumi wa nchi ili kufikia malengo ya kuifanya Tanzania kuwa nchi yenye kipato cha kati.

Alisema Rais John Magufuli ni kiongozi ambaye akilala na kuamka, anawaza namna ambavyo atawahudumia wananchi wake, ambao wengi wako kwenye dimbwi la umaskini. 

Alisema Rais atafanikiwa tu, pale Serikali yake itakusanya kodi ya kutosha na kuwahudumia wananchi hao.

“Kuna minong’ono kwamba eti Serikali ya Awamu ya Tano inawanyanyasa wafanyabiashara wakubwa na kwamba hatua tulizochukua kukusanya kodi, ililenga kuwadhalilisha baadhi ya wafanyabiashara, hii sio kweli kabisa,” alisema Dk Mpango.

Dk Mpango alisema Serikali ya Awamu ya Tano, inatambua umuhimu wa wafanyabiashara, hivyo wizara yake itakuwa ya mwisho kuchukua hatua za kuwanyanyasa. 

“Nawahakikishia kwamba nina dhamira ya dhati ya kufanya kazi kwa kushirikiana na ninyi wafanyabiashara wakubwa na wadogo ili tutimize ndoto ya Rais,” alisema.

Alisema serikali yoyote duniani ni lazima ikusanye kodi, hivyo aliwahakikishia wafanyabiashara hao kuwa kama bado kuna wafanyabiashara wanaokwepa au hawataki kulipa kodi kwa mujibu wa sheria, serikali haitakuwa tayari kuwavumilia.

Dk Mpango alisema idadi ya watu wanaolipa kodi kwa sasa nchini bado wachache, hivyo aliwaagiza wafanyabiashara wote kujisajili wapatiwe Namba ya Utambulisho wa Mlipa Kodi (TIN).

Pia, aliwataka waache tabia ya kufanya udanganyifu kwa kuwa na vitabu vingi vya utunzaji wa kumbukumbu za biashara. Aliwaagiza kuhakikisha wanatoa stakabadhi na suala hilo lisiwe hiyari.

“Tunajua kwamba mnatoa vitisho kwa wanunuzi kuwa kama wanataka risiti bei ni ya juu, hiki mnachofanya ni hatari kwa nchi,” alisema na kuwataka wote watumie mashine za EFD na serikali inaendelea na mpango wa kununua zingine ili wagawiwe bure.

Aliwataka kutoa taarifa kwa Kamishna Mkuu wa TRA, kama kuna mfanyakazi wa Mamlaka ya Mapato (TRA) au wa Halmashauri ya Wilaya, ambaye atadai hongo au atawanyanyasa wakati wa kudai kodi.

Katika kutekeleza hilo, aliwapatia namba zake pamoja na za Kamishna na kuwataka waache tabia ya kutoa rushwa ili wasilipe kodi.

 Dk Mpango alisema baada ya wafanyabiashara kufanya kikao na Rais Magufuli, Serikali imeunda kikosi kazi kushughulikia kero zote, zilizotolewa na Baraza la Biashara na mojawapo ni kufuta utiriri wa kodi ili kuwapa wepesi wawekezaji kufanya biashara nchini na kumpungumzia mzigo mkulima.

Vyama 9 Havitashiriki Uchaguzi wa Marudio Zanzibar

$
0
0
Maalim Seif Sharif Hamad

Vyama tisa vya siasa kati ya 14 vilivyoshiriki Uchaguzi Mkuu Zanzibar mwaka jana vimeungana na CUF kutoshiriki uchaguzi wa marudio uliopangwa kufanyika Machi 20, hadi utakapopatikana mwafaka wa kumaliza mgogoro wa kisiasa.

Mratibu wa umoja wa vyama hivyo, Kassim Bakari Ali alisema jana kuwa vyama hivyo vilikutana Unguja na kupitisha maazimio mawili ya kutoshiriki uchaguzi huo. 

Vyama hivyo ni UMD, Jahazi Asilia, Chaumma, UPDP, DP, CCK na ACT Wazalendo. Ushiriki wa vyama vya ADC na CCK bado una utata kutokana na wagombea wake kutangaza kushiriki licha ya vyama vyao kuwa na msimamo tofauti, hali iliyosababisha wagombea hao kusimamishwa.

Vyama ambavyo vimetangaza kushiriki marudio hayo hadi sasa ni CCM, Tadea, TLP, Sau na AFP. 

Kwa kipindi cha miezi miwili iliyopita, Zanzibar imeendelea kuwa kwenye mgogoro wa kisiasa kati ya vyama vikubwa vinavyounda Serikali ya Umoja wa Kitaifa (SUK) baada ya CUF kususia marudio ya uchaguzi baada ya ule wa awali kufutwa na Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC), Jecha Salim Jecha.

Akitaja maazimio ya vyama hivyo, Kassim alisema wamekubaliana kutoshiriki marudio ya uchaguzi huo hadi mgogoro wa CCM na CUF utakapomalizika na wameunda kamati ya wajumbe 18 ya wenyeviti na makatibu wa kila chama ili kuanzisha meza ya kutafuta suluhu ya mvutano uliopo kati ya CCM na CUF.

 “Tutaanza kukaa na viongozi wa vyama hivyo kila upande kujua ni nini hasa hatima ya mvutano huo na tunajikwamuaje,” alisema.

Ali ambaye pia ni mwenyekiti wa Jahazi Asilia alisema mgogoro wa Zanzibar utamalizwa na Wazanzibari wenyewe, hivyo ni vyema viongozi hao wa kisiasa wakajenga uvumilivu katika kutafuta mwafaka.

Alisema tatizo la vyama hivyo siyo kushiriki marudio ya uchaguzi huo tu bali ni kuangalia chanzo na hatima ya mgogoro huo kwa masilahi ya Wazanzibari.

Mwenyekiti wa CCK, Constatine Akitanda aliwaambia waandishi wa habari kuwa uamuzi wa kusimamishwa uanachama kwa mgombea wake wa urais, Ali Khatibu Ali, unakwenda sanjari na kutoshiriki uchaguzi hadi maridhiano ya CUF na CCM yapatikane.

Mgombea urais wa Zanzibar kupitia AFP, Said Soud Said alisema jana kwamba, chama hicho kimekubali kurudia uchaguzi huo.

 “Lengo la chama chetu ni kushika dola, sasa tusiposhiriki itakuwaje? Kwanza hatuamini kama CUF haijatendewa haki kwa sababu ni kweli kulikuwa na udhaifu, mfano vurugu za kituo cha kupigia kura cha Matrekta Wawi,” alisema.

Mwenyekiti wa TLP, Augustine Mrema alisema kama vyama hivyo viliiamini ZEC katika uchaguzi uliopita, vinatakiwa kuiamini kwenye marudio hayo kwa kuwa hakuna mbadala.

“Naomba wakubali kurudia uchaguzi kwani ‘maji yalishamwagika na kuzoleka haiwezekani... Nani aliyekwenda mahakamani kupinga? Wanachoogopa kurudia ni kitu gani kama walishinda?” alihoji Mrema.

Profesa Muhongo: Sijawahi Kupokea Rushwa wala 10% Ya Mwekezaji

$
0
0

WAZIRI wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo, amesema hajawahi kupokea rushwa kwa mtu yeyote wala asilimia 10 ya wawekezaji wa miradi mbalimbali ya umeme nchini.

Aidha, ametaka kuachwa kuingizwa kwa masuala ya siasa kwenye umeme, kwani umeme ni suala linalohitaji utaalamu zaidi na si maneno.

Alitoa kauli hizo juzi wakati akizungumza na wazalishaji wa umeme kwenye mkutano uliofanyika Mtera.

Mimi hakuna mtu yeyote dunia nzima aliyewahi kunipa rushwa, nia yangu ni kuhakikisha taifa linapata umeme ikiwa ni pamoja na kuongeza wawekezaji, sihitaji hela ya mtu,” alisema Profesa Muhongo.

Pia alisema baadhi ya mitandao ya kijamii, imekuwa ikiripoti kuwa amewaita wazalishaji hao ili wamlipe asilimia 10 ; na kusema jambo hilo si la kweli hata kidogo.

“Kwenye masuala mengine ya mtandao ambayo hayana ukweli wowote muwe mnajitetea,” alisema Profesa Muhongo. “Acheni kuingiza masuala ya siasa kwenye umeme,” alionya.

Jeshi La Polisi Zanzibar Lasema Halitambui Uwepo Wa Mazombi....... Lapiga Marufuku Mtu Aliyepigwa Na Zombi Kutibiwa Bila Kuwa Na PF3

$
0
0

Jeshi la Polisi Zanzibar limewataka madaktari kuacha kuwahudumia watu wanaokwenda hospitali baada ya kupigwa na kikundi cha watu wasiojulikana cha mazombi bila ya kuwa na fomu ya matibabu (PF3).

Akizungumza na wanahabari mjini Unguja jana, Mkurugenzi wa Upelelezi Zanzibar, Salum Msangi alisema matukio ya watu kujeruhiwa na kutopeleka taarifa polisi yanachangia kuendeleza uhalifu.

Alisema taswira ya haraka wanayoipata ni kwamba inawezekana watu wanaotendewa vitendo hivyo ni wahalifu ambao wamekutana na wahalifu wenzao hivyo kuhofia kutoa taarifa ili uhalifu wao usibainike hali inayosababisha kunung’unika pembeni bila ya kufikisha taarifa maeneo sahihi ili zifanyiwe kazi.

“Kwa mujibu wa taratibu zilizopo ni kwamba mtu yeyote anayefanyiwa kitendo cha kihalifu anapaswa kutoa taarifa kwenye kituo cha polisi ili uchunguzi au upelelezi ufanyike kubaini wahalifu hao,” alisema Msangi.

Alisema iwapo polisi itambaini daktari atakayetoa tiba kwa watu hao bila PF3 itamchukulia hatua.

Alisisitiza polisi kutowatambua mazombi hao ambao huvaa soksi nyeusi usoni, wakiwa na silaha wanazotumia kuwashambulia watu kwa vile wanaofanyiwa vitendo hivyo hawatoi taarifa.

Alisema kumejitokeza mambo matatu; vipeperushi vyenye vitisho, mazombi na kuwekwa alama za X kwenye baadhi ya nyumba hasa Pemba na kutoa tahadhari kwa mtu yeyote anayehusika, kikundi au jumuiya inayojihusisha na utoaji wa vitisho hivyo kuacha mara moja kabla ya jeshi hilo kuchukua hatua kali dhidi.

Akivisoma vipeperushi hivyo, Msangi alisema kuna vikaratasi vimesambazwa vyenye ujumbe usemao ipo siku itakuwa kweli ‘One Day Yes’ kingine “Kutangazwa uchaguzi siyo kufanyika uchaguzi.”

Shahidi : Nilimsikia Kubenea akimwambia DC Paul Makonda ni kibaka,mjinga, mpumbavu na cheo chenyewe kapewa.

$
0
0

Mratibu Msaidizi wa Jeshi la Polisi, ASP Denis Mujumba, 39 ameieleza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuwa akiwa Mkuu wa Upelelezi Magomeni alimsikia Mbunge wa Jimbo la Ubungo Saed Kubenea akimwambia Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda kuwa DC gani kibaka, mjinga, mpumbavu na cheo chenyewe kapewa.

ASP Mujumba aliyasema hayo  jana mbele ya Hakimu Mkazi, Thomas Simba wakati akitoa ushahidi wake katika kesi ya kutoa lugha chafu inayomkabili Kubenea dhidi ya Mkuu wa huyo wa Wilaya.

Akiongozwa na Wakili wa Serikali Mwandamizi, Kishenyi Mutalemwa, Mujumba alidai kuwa baada ya Kubenea kuyatoa maneno hayo huku akionekana mwenye hasira, Makonda akiwa amesimama alishangaa, akakunja mikono yake na akawa anamsogelea Kubenea.

“Nikaona watarushiana ngumi, nikamsihi Mkuu wa Wilaya Makonda aondoke wakati huo watu walianza kushangilia huku wengine wakisikitika,” alidai shahidi huyo wa tatu wa upande wa mashtaka.

Alidai kuwa alimgeukia Kubenea na kumwambia kitendo alichofanya cha kutoa matamshi hayo ametenda kosa la jinai, akamkamata na kumpeleka kituo cha polisi Magomeni kwa mahojiano.

Baada ya kutoa ushahidi huo, Wakili wa Kubenea, Peter Kibatala alimuuliza shahidi huyo kuwa ilikuwaje hadi Kubenea akayatamka maneno hayo.

Akijibu swali hilo, Mujumba alidai kuwa ni baada ya Makonda kumnyima nafasi Kubenea ya kuzungumza na wafanyakazi waliokuwa katika mgomo kwenye Kiwanda cha Tooku Garments Co. Limited. 

Pia Wakili Kibatala aliuliza kwamba siku hiyo kulikuwepo na waandishi lakini alipataje picha za video na sauti kutoka kwa waandishi wa habari?

Mujumba: Ni kweli kulikuwepo na waandishi na kwamba niliwasiliana na waandishi hao ili wanipe ushahidi wa picha, sauti au video. Waandishi walinijibu kuwa hawana ushahidi huo.

Kibatala: je ulikwenda na askari wangapi?

Mujumba: nilikwenda na askari wanane au tisa.

Kibatala: wataje majina

Mujumba: Ni Sajenti Peter, PC Hamis, Joachim na Doel.

Kibatala: Shahidi hajui askari wake kwani anajua jina moja tu la mwanzo na hajataja wote.

Maswali haya yalisababisha Mjumba kukunja sura na kutoa sauti ya juu huku akitaka kubishana, Hakimu Simba alimtaka aache kubishana

Wakili Kibatala kwa kutumia sheria Namba 155(a) aliiomba mahakama kuonesha picha za ushahidi zilizokuwa zianonesha hali halisi ya tukio.

Wakili huyo aliinesha mahakama picha ambazo zilionesha kuwepo kwa askari walioshika bunduki na kumzingira Kubena, kwenye picha hiyo Mujumba hakuwemo.

Hapo awali Mujumba aliieleza mahakama kwamba yeye ndiye aliyemsihi Kubenea aende naye kwenye Kituo cha Polisi Magomeni, hivyo Wakili Kibatala aliongeza kuwa, kwa kutokuwepo kwenye picha ile Mujumba alitoa maelezo ya uongo. 

Hakimu Mkazi hata hivyo, baada ya shahidi huyo kutoa ushahidi wake, Hakimu Simba alihairisha kesi hiyo hadi tarehe 15 na 16 Aprili mwaka huu.

Wanafunzi 21 Wafukuzwa Shule Kwa Muda Usiojulikana.......Kosa Lao Ni Kuvaa "YeboYebo", Mwalimu Wa Zamu Alizichukua na Kuzichoma Moto

$
0
0
Wanafunzi wapatao 21 wanaosoma Shule ya Msingi Kilambo cha Mkolechi, Kata ya Kala mwambao mwa Ziwa Tanganyika wilayani Nkasi, wamefukuzwa shule kwa muda usiojulikana kwa kuvaa viatu maarufu yeboyebo.

Imeelezwa kwamba yeboyebo hizo zilikusanywa na kuchomwa kwa kile kilichoelezwa kwamba ni kunatokana na waraka uliotolewa na Ofisa Elimu Halmashauri ya Nkasi (Msingi) ukipiga marufuku wanafunzi kuvaa aina hiyo ya viatu shuleni.

Hata hivyo,jana  Ofisa Elimu Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi (Msingi), Misana Kwangula, alikanusha kutoa waraka huo kwa shule hiyo.

“Sina taarifa rasmi ila jana jioni (Jumatatu) alinipigia simu mkazi mmoja akinitaarifu kwamba kuna mwalimu wa shule ya msingi Kilambo cha Mkolechi amechoma moto viatu vya wanafunzi kwa madai kuwa ofisa elimu (msingi) ametoa waraka kwamba wanafunzi hawatakiwi kuvaa yeboyebo shuleni…

“Hakuna waraka wala marufuku yoyote iliyotolewa, isitoshe sio sahihi hata kidogo wala sio kitu kizuri kuchoma vifaa walivyonavyo wanafunzi…. Sasa kama amewachomea wanafunzi hao viatu hivyo vya yeboyebo basi awanunulie viatu vya ngozi,” alisema Kwangula.

Mkasa huo wa wanafunzi hao kufukuzwa shule na kuchomewa yeboyebo walizovaa ulitokea juzi wakati wanafunzi hao walipofika shuleni wakiwa wamevaa viatu hivyo. 

Inaelezwa kwamba mwalimu wa zamu, Baraka Mwakasege aliwazuia kuingia darasani, badala yake akawaamuru wavue viatu vyao.

Taarifa kutoka shuleni hapo zinaeleza kuwa, baada ya hatua hiyo, mwalimu huyo wa zamu alizikusanya yeboyebo na kuzitia kiberiti kisha akawafukuza wanafunzi hao kwa muda usiojulikana hadi wazazi na walezi watakapowanunulia viatu vya ngozi.

Mwalimu Mkuu wa shule hiyo, Posian Ally alikanusha kumtuma mwalimu wa zamu kuwafukuza wanafunzi hao shule kwa muda usiojulikana wala kuteketeza kwa moto yeboyebo zao.

 Alisema ataitisha kikao ili kujadili suala hilo na kwamba mwalimu huyo akibainika kutenda kosa hilo ataamriwa kuwanunulia watoto hao viatu vingine.

Mkuu Mpya Wa Chuo Kikuu Cha Dar (UDSM) Rais mstaafu Jakaya Kikwete Atembelea Chuo Hicho Na Kujionea Hali Halisi Ilivyo

$
0
0

MKUU mpya wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) ambaye ni Rais mstaafu Jakaya Kikwete, ametembelea chuo hicho kujifunza na kujionea hali halisi ilivyo, kabla ya kukabidhiwa rasmi wadhifa huo.

Kikwete aliyekuwa Rais wa Awamu ya Nne, ameteuliwa hivi karibuni na Rais John Magufuli kushika wadhifa huo, baada ya kufariki kwa Balozi Fulgence Kazaura mwaka 2013.

 Akiwa chuoni hapo majira ya mchana, Kikwete alitembelea Chuo cha Uhandisi, Jengo jipya la Sayansi, kumbi za mihadhara za Yombo na eneo ambalo itajengwa maktaba mpya ya kisasa.

Akiwa katika Ukumbi wa Yombo, aliwaambia wanafunzi kuwa Rais John Magufuli amempa kazi ya kuwa mkuu wa chuo, hivyo amefika hapo kujionea hali halisi kabla ya kukaa na viongozi kutengeneza chuo hicho kiwe bora zaidi.

Akiondoka katika eneo la ukumbi huo, baadhi ya wanafunzi walimfuata na kumweleza kuwa zaidi ya miezi miwili hawajapewa fedha za kujikimu, hivyo aliwaahidi kuwasaidia kwa kulisemea sehemu husika.

Baada ya ziara hiyo, Kikwete alikutana na watendaji mbalimbali wa chuo hicho na kuwaeleza kuwa ujio huo umempa kukifahamu chuo hicho kwa sehemu. “Nimefurahi fursa hii ya kutembea leo (jana) kabla ya siku rasmi ya kukabidhiwa uongozi wa chuo.

"Bado natamani Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kiwe bora kuliko vyote nchini. Sina maana vingine vitakuwa duni, hapana. Ila kiwe ni chuo kinachotoa viongozi. Mtu akitaka kiongozi aanzie kumtafuta kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, akikosa ndio aende chuo kingine.

"Na hivyo vyuo vingine watafute maeneo ambayo watayakomalia ili nao wafuatwe,” alisema Kikwete ambaye alisoma hapo katika miaka ya 1970. 

Alisema amesikia kilio cha wanafunzi hao baada ya kumwambia hali ni tete kwa kuwa hawajapata fedha, hivyo japo hajakabidhiwa rasmi nafasi hiyo, ataanza na hilo ili vijana wasome vizuri.

Aliahidi kurudi kabla ya mwezi huu kuisha ili akutane na viongozi mbalimbali, lengo ni kukielewa vizuri kabla ya kukabidhiwa rasmi.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images