Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Corruption Watch Yapinga Hukumu Ya Ufisadi Wa Benki ya Standard Dhidi Ya Serikali Ya Tanzania

$
0
0

Hukumu ya kesi ya rushwa ya mkopo uliotolewa na Benki ya Standard ya nchini Uingereza kwa Serikali ya Tanzania imepingwa na taasisi ya kimataifa inayopambana na ufisadi, Corruption Watch, ikisema kuwa benki hiyo ilijisalimisha kuepuka adhabu kali.

Hukumu hiyo inatokana na kashfa ya ufisadi ambayo benki hiyo ilihusika baada ya kushinda zabuni ya kuitafutia Tanzania mkopo wa dola 600 milioni za Marekani (sawa na Sh1.2 trilioni) kwa mauzo ya hatifungani kwa ajili ya miradi ya maendeleo, lakini ikaliingiza tawi lake la hapa nchini, Stanbic katika kupata kamisheni, kinyume na taratibu.

Katika makubaliano hayo haramu, kampuni ya EGMA ililipwa dola 6 milioni (sawa na Sh1.2 bilioni) kwa maelezo kuwa ilitoa huduma za ushauri.

Taarifa ya awali iliyotolewa na Taasisi ya Uchunguzi wa Makosa Makubwa ya Ufisadi (SFO) ya Uingereza, ilibainisha kuwa EGMA haikutoa ushauri wowote na kuhusishwa kwake ilikuwa ni njia ya kuwanufaisha viongozi wa Serikali waliokuwa na mamlaka na taratibu za kukamilisha muamala huo.

Kwa mujibu wa Corruption Watch, baada ya taarifa hiyo ya SFO, benki hiyo ilipaswa kushtakiwa mahakamani ili hatua za kisheria zichukue mkondo wake, lakini Standard Bank ilitumia Sheria ya Ufisadi nchini humo kumtaka Mwendesha Mashtaka wa Serikali kutofanya hivyo na kufanikiwa kumshawishi.

Kwa mara ya kwanza katika historia ya Uingereza, Jaji Mwandamizi wa Mahakama ya Southwark Crown, Brian Leveon aliidhinisha na kutumia Sheria ya Makubaliano ya Kutoshtakiwa (DPA) kuilipisha faini Benki ya Standard na hivyo kukwepa kushtakiwa na kukumbana na adhabu za mahakamani.

Hii ni mara ya kwanza kwa Uingereza kutumia sheria hiyo kwa moja ya kampuni zake kubwa, jambo lililosababisha wadau na wanaharakati wanaopinga ufisadi wa kitaasisi, kuikosoa hukumu hiyo kwa maelezo kuwa inaikandamiza Tanzania, ambayo ni nchi maskini inayoingizwa kwenye vitendo vya rushwa kwa mipango kutoka nje ya mipaka yake.

Taasisi ya Corruption Watch ya nchini humo imesema benki hiyo haistahili kupata unafuu unaotokana na sheria hiyo ya DPA kwa maelezo kwamba iliratibu rushwa hiyo na maofisa wake walihusika, hivyo haikustahili kupewa adhabu ndogo kwa kutumia sheria hiyo.

“Serikali ya Tanzania haitaridhika na uwajibikaji wa benki hii katika kukabiliana na uhalifu ilioutenda. Corruption Watch inaona kuwa Tanzania imepunjwa kiasi inachostahili kulipwa kutokana na ufisadi huu,” inasema taarifa ya Corruption Watch ya mwezi Desemba.

Katika kuthibitisha udogo wa fidia ambayo benki hiyo imekubali kuilipa Tanzania, taasisi hiyo imeeleza kuwa malipo halali yangeweza kuzidi mara kumi ya makadirio ya awali, endapo madhara yote ya udanganyifu uliofanywa yangezingatiwa.

Inasisitiza kuwa faini hiyo ilitakiwa ifike dola 80 milioni (zaidi ya Sh160 bilioni) pamoja na riba ya faida ya dola 10 milioni (zaidi ya Sh20 bilioni) kutokana na kilichochumwa na taasisi hiyo ya fedha.

Wakati hapa nyumbani Serikali ikiwa imetangaza kuwachukulia hatua za kisheria maofisa wake wote waliohusika kwenye sakata hilo, akiwamo aliyekuwa Kamishna wa Mamlaka ya Mapato nchini (TRA) ambaye pia likuwa mwenyekiti wa EMGA, Harry Kitilya, hakuna hatua zozote zilizochukuliwa dhidi ya maofisa wa benki hiyo walioratibu upatikanaji wa hatifungani hiyo.

“Hakuna mtu yeyote aliyechukuliwa hatua za kisheria ama na benki yenyewe au mahakama kutokana na uzembe wa kushindwa kuzuia vitendo vya rushwa. Watu hawa wangali wanahudumu katika vyeo vya juu kwenye sekta ya huduma ya fedha hapa Uingereza. Wanapaswa kuchunguzwa kwa lengo la kuwapunguzia heshima yao ya kitaaluma,” inasema taarifa hiyo.

Kuhusu utekelezaji wa sheria uliotumika mpaka Benki ya Standard ikapewa DPA, taasisi hiyo imelalamikia utegemezi wa uchunguzi uliofanywa na benki husika juu ya kashfa hiyo. 

Imeeleza kuwa upo uwezekano mahakama na umma wakawa hawajaelezwa kinagaubaga uovu uliofanywa na kampuni hiyo.

Kwa vile uamuzi huu wa DPA ni wa kwanza kutolewa Uingereza na kutakiwa kutumika kama rejea kwa matukio yatakayofuata, taasisi hiyo imeonya kuhusu kifungu cha 7 cha Sheria ya Ufisadi kinachotoa adhabu kwa kampuni au mfanyakazi wake anayeshindwa kudhibiti vitendo vya rushwa dhidi ya wateja wake.

“Kitendo cha kushindwa kuwachukulia hatua maofisa waliohusika ni kosa kubwa kisheria na kitaaluma,” inasema ripoti hiyo ya Corruption Watch UK.

“DPA hii inadhihirisha kuwa kifungu cha 7 cha Sheria ya Ufisadi ndicho kinachotoa adhabu ndogo kwa wavunjaji wake, hivyo kutia wasiwasi kama kweli Uingereza imedhamiria kukomesha rushwa miongoni mwa kampuni zake.”

Inasema kuwa benki hiyo iliamua kutumia DPA kukwepa mkono wa mahakama ili kulinda maslahi yake ambayo ni pamoja na leseni ya biashara katika Jiji la Westminster, mpango wake wa kuuza hisa zake kwa benki ya China ya ICBC pamoja na kuendelea kuimiliki hatifungani ya Tanzania. 

==>Hivi ni baadhi ya Vipande vya Ripoti hiyo 


Mwalimu Mkuu Ashushwa Cheo na Kukamatwa na Takukuru Kwa Rushwa ya KUKU

$
0
0

Mkuu wa Wilaya ya Bukombe mkoani Geita, Amani Mwenegoha amemvua wadhifa wake Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Sinamila, Mashaka Lusotola na kumrudisha kuwa mwalimu wa kawaida.

Hatua hiyo ilikuja baada Mwenegoha kubaini kuwa walimu wa shule hiyo wamekuwa na tabia ya kuwaagiza kuku, wazazi wanaowaandikisha wanafunzi wa darasa la kwanza.

Mwenegoha alichukua maamuzi hayo, baada ya kuthibitisha kuwa mwalimu huyo mkuu, ameshindwa kudhiti tabia hiyo ya walimu walio chini yake.

Akizungumzia kusimamishwa kwake, Mwalimu Lusotola alisema amefurahi na kufananisha adhabu hiyo na kumpiga teke chura.

Tayari mwalimu huyo amekamatwa na Taasisi ya Kuzuia na Kupamaba na Rushwa (Takukuru), leo anatarajia kwenda kuandikisha maelezo, huku akisisitiza kuwa hajaomba kitu chochote kwa wazazi.

Askofu Gwajima Azushiwa Kifo

$
0
0

Kiongozi wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Askofu Josephat Gwajima, jana alizushiwa kuwa amefariki dunia.

Taarifa hizo zilizozagaa katika mitandao ya kijamii zilieleza kuwa Askofu Gwajima alifariki dunia katika hospitali ya TMJ, Mikocheni jijini Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa taarifa hizo zilienea  kuanzia ya saa tano asubuhi, zilieleza kuwa Askofu Gwajima alifariki dunia kwa shinikizo la damu. 
 
Hata hiyo, taarifa hizo zilikanushwa vikali na mwanasheria wake, wakili wa kujitegemea Peter Kibatala.

Kibatala jana alisema taarifa hizo ni za uzushi ambao haelewi chanzo chake.

“Nimesikitishwa na taarifa hizi na nimepigiwa simu nyingi sana leo kuniuliza juu ya kifo cha Askofu Gwajima na nimebaki nashangaa kwani ni mzima wa afya,”alisema Kibata.

Majira ya jioni jana picha zilizoenea kwenye mitandao ya kijamii ziliomwonyesha Askofu Gwajima akiwa mkoani Kigoma kwa ziara ya kikazi.

Wingu Zito Laendelea Kutawala Ufisadi Wa Mabilioni NIDA....Yadaiwa Kitambulisho Kimoja Kimegharimu Sh 89,800

$
0
0
Wingu  zito limetanda ndani ya Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) kuhusu matumizi ya  Sh bilioni 179.6 ambako kila kitambulisho  cha taifa kimegharimu Sh 89,800 zikiwamo gharama za utawala

Hayo yamebainika  siku chache baada ya Rais Dk. John Magufuli kushangazwa na watendaji wa mamlaka hiyo ikizingatiwa vitambulisho vilivyokwisha kutengenezwa hadi sasa havifiki   milioni mbili na havina saini.

“Utaona ugumu wa kuongoza, nchi inatawaliwa na madudu ya kila aina.  Wapo watu wanacheza na fedha wanavyotaka wakati wapo watu masikini sana  wengine wanataka bodi zao wakakae Ulaya.

“Hapo ndipo tulipofikia, wengine wanalipwa mshahara wa Sh milioni 35 kwa mwezi…naomba mniombee kabla ya kunihukumu, toeni hukumu kwa haki kwa hawa wanaotaka kuifikisha nchi pabaya, toeni hukumu zao haraka,” alisema.

Rais Dk. Magufuli, licha ya kushangazwa na hali hiyo, alisema Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) ilipewa Sh bilioni 70 lakini iliweza kutengeneza vitambulisho   23,253,982 ambavyo vilikuwa na saini ya kila mpiga kura na kila kimoja kimegharimu Sh 3,010.

Kutokana na hali hiyo, tofauti ya gharama kati ya kitambulisho kimoja cha NIDA na cha NEC ni Sh 86,790.

Pamoja na hayo, hivi sasa Watanzania wanasuburi   ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Profesa Juma Assad, kuhusu  matumizi ya fedha hizo za NIDA.

Januari 26 mwaka huu, Rais Magufuli alitangaza kumsimamisha kazi ili kupisha uchunguzi dhidi yake, Mkurugenzi Mkuu wa NIDA, Dickson Maimu.

Maimu alisimamishwa kazi pamoja na maofisa wengine wanne, kwa tuhuma za ubadhirifu wa fedha za Serikali.

Maofisa hao ni Mkurugenzi wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano, Joseph Makani, Ofisa Ugavi Mkuu, Rahel Mapande, Mkurugenzi wa Sheria, Sabrina Nyoni na Ofisa Usafirishaji, George Ntalima.

Akitangaza uamuzi huo, Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Sefue, alisema taarifa zilizomfikia Rais zinaonyesha kuwa NIDA hadi wakati huo ilikuwa imetumia Sh bilioni 179.6, kiasi ambacho ni kikubwa.

Alisema Rais angependa ufanyike uchunguzi na ukaguzi kujua jinsi fedha hizo zilivyotumika, maana amekuwa akipokea malalamiko ya wananchi kuhusiana na kasi ndogo ya utoaji wa Vitambulisho vya Taifa.

Licha ya kumuelekeza Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali, afanye ukaguzi maalumu wa hesabu za NIDA  ukiwamo ukaguzi wa “value for money” baada ya kuthibitisha idadi halisi ya vitambulisho vilivyotolewa hadi sasa, pia aliitaka Takukuru ifanye uchunguzi kujiridhisha kama kulikuwa na vitendo vya rushwa au la.

Credit: Mtanzania

Mawaziri Yona na Mramba Waanza Kutumikia Kifungo cha nje...Wakabidhiwa Vifaa vya Usafi

$
0
0

Mawaziri wa zamani Basil Pesambili Mramba na Daniel Yona wameripoti leo katika hospitali ya Sinza Palestina na kukabidhiwa vifaa kwa ajili ya kufanya usafi.

Mwishoni mwa wiki iliyopita, mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu iliridhia Mawaziri hawa  wastaafu kutumikia adhabu ya kifungo cha nje kwa kufanya usafi katika maeneo ya kijamii ikiwemo Hospitali ya Sinza Palestina.

Ahadi Ya Sh.bilioni 12.3 Ya Rais Dk. John Pombe Magufuli Ya Maombi Ya Uendeshaji Wa Mahakama Yatimia Leo.

$
0
0

WIZARA ya Fedha na Mipango imetoa sh.bilioni 12.3 kwa ajili shughuli za mahakama ikiwa ni sehemu ya ahadi ya  Rais Dk. John Pombe Magufuli aliyoiahidi katika kilele cha maadhimisho ya  siku ya mahakama.

Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam, Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Philip Mpango amesema fedha hiyo imetolewa kwa kutimiza ahadi ya Rais ya uendeshaji wa shughuli za mahakama.

Mpango amesema kuwa ahadi ya Rais ilikuwa ni ya siku tano ambazo zimetimia kwa kutoa hundi ya sh.bilioni 12.3 ambazo zitakwenda kufanya kazi iliyokusudiwa.

Amesema kuwa Wizara ya Fedha na Mipango kutokana na ahadi hiyo imefanya kuweka wazi juu ya fedha hizo kwa waandishi wa habari.

Nae Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria, Amon Mpanju amesema lengo ni kuongeza kasi kwa mashauri yaliyopo kuondoshwa  pamoja na waliokwepa kodi  yashughulilikiwe.

Ahadi ya Rais ilitolewa baada ya maombi ya Jaji Mkuu, Othman Chande katika maadhimisho ya  kuanza kwa mwaka wa mahakama kudai kuwa wana uhaba fedha za maendeleo  katika kuweza kuendesha shughuli za kimahakama.
Waziri wa Fedha Mipango, Philip Mpango (Katikati) akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo, kuhusiana na kutimiza ahadi aliyoiahidi Rais  Dkt. John Pombe Josef Magufuli alipoahidi katika maadhimisho ya siku ya mahakama hapa nchini. Kulia ni Naibu waziri wa katiba na sheria, Amon Mpanju na kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango Dkt. Servacius Likwelile.
Mtendaji mkuu wa Mahakama Hussein Kattanga (kushoto)akimshukuru Rais  Dkt. John Pombe Josef Magufuli kwa kutimiza ahadi yake aliyoiahidi siku ya maadhimisho ya siku ya mahakama. kulia ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango Dkt. Servacius Likwelile.

Kamati kuu ya CCM, yateua wagombea wa kujaza nafasi mbali mbali zilizo wazi

$
0
0
 TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Jana tarehe 07/02/2016 Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa ilikuwa na kikao maalum cha siku moja mjini Dodoma. Kikao hicho kiliongozwa na Mwenyekiti wa Taifa wa CCM Dr. Jakaya Mrisho Kikwete. 

Kikao hicho kilikuwa na kazi ya kuteua wagombea wa nafasi mbalimbali zilizo wazi za uongozi ndani ya CCM mikoani na wilayani ambazo uteuzi wake upo kwenye Mamlaka ya Vikao vya Chama Taifa.

Nafasi hizi wazi zimetokana na sababu mbalimbali zikiwemo vifo na baadhi ya viongozi kukihama Chama na kujiunga na vyama vingine. Hivyo, nafasi zilizofanyiwa uteuzi na wagombea wake ni kama ifuatavyo:-

I.     UENYEKITI WA CCM MKOA.

1.      ARUSHA
(i)      Michael Lekule Laizer
(ii)     Emanuel Makongoro Lusenga
(iii)   John Pallangyo

2.   SHINYANGA
(i)      Hassan Ramadhani Mwendapole
(ii)     Mbala Kashinje Mlolwa
(iii)   Erasto Izengo Kwilasa

3.   SINGIDA
(i)    Hanje Narumba Barnabas
(ii)   Misanga Mohamed Hamis
(iii)  Mlata Martha Moses
(iv)  Kilimba Juma Hassan

II.     UJUMBE WA HALMASHAURI KUU YA CCM TAIFA NEC

1.       NYAMAGANA
(i)    DR. Sillinus Elias Nyanda
(ii)   Jamal abdul Babu
(iii)  Kelebe Bandoma Lutelil
(iv)  Patrick Kambarage Nyabugongwe

2.       KAHAMA
(i)   Pili Yakanuka Izengo
(ii)  Paschal Ndibatyo Mayengo
(iii) Sweetbert Charles Nkuba

3.       MONDULI
(i)  Namelock Edward Sokoine

III.    UENYEKITI WA CCM WILAYA

1.       MONDULI
(i)  Loata Erasto Sanare

2.       SUMBAWANGA MJINI
(i)  Chami Slegried Mask
(ii) Godfrey Mwimanzi Mwikala

IV. KATIBU WA UCHUMI NA FEDHA MKOA WA KILIMANJARO

(i)    Shadrack Amani
(ii)   Chata Madata Joseph
(iii)  Karia Ahmed Mahamoud

V.      KATIBU WA SIASA NA UENEZI MKOA WA ARUSHA
(i)   Semmy Rabson Kiondo
(ii)  Shaban Omari Mdoe
(iii) Veraikunda Zablon Urio

VI.     UENYEKITI WA UVCCM WA MKOA

1.   ARUSHA
(i)            Erick Edward
(ii)            Lengai Loy Thomas
(iii)          Mwanzani Omar

  2.   KILIMANJARO
(i)      Amaly T.Mathew
(ii)     Frank Lumisha Nkya
(iii)   Juma Rahibu Juma

2.   SHINYANGA
                (i)   Mabembela Joseph Elias
                (ii)  Mipanda kali Dalushi
                (iii) Ndasa Jeremiah Damian
                (iv) Shigela Reubeen Bernard

Ratiba ya chaguzi hizo itatolewa wiki hii mwishoni.

Kamati Kuu pia imepokea taarifa ya maandalizi ya uchaguzi wa marudio Zanzibar na kuridhishwa na maandalizi hayo na kuwatakia kila la kheri Wazanzibar katika Uchaguzi huo.

Wakati huo huo, Kamati Kuu imetoa pole kwa Jeshi la Polisi nchini kufuatia vifo vya Askari Polisi watatu vilivyotokea tarehe 06/02/2016 mjini Singida kutokana na ajali wakati Askari hao wakitimiza wajibu wao kwenye maadhimisho ya miaka 39 ya kuzaliwa kwa CCM. Kamati Kuu inawapa pole wafiwa wote na kuwaombea majeruhi wote kupona haraka.

Imetolewa na:-

Nape Moses Nnauye
KATIBU WA HALMASHAURI KUU YA TAIFA,
ITIKADI NA UENEZI
08/02/2016

Mke wa Waziri Mkuu Mstaafu Mizengo Pinda Apata Ajali Mbaya ya Gari

$
0
0

Mtu mmoja amefariki dunia na wengine wanne wamejeruhiwa akiwemo mke wa waziri mkuu mstaafu Mizengo Pinda Mama Tunu Pinda baada ya gari walilokuwa wakisafiria kumgonga mwendesha pikipiki wakati akikatisha barabara katika eneo la Mkundi barabara ya Morogoro Dodoma manispaa ya Morogoro. 

Ajali hiyo imetokea majira ya saa nane mchana katika eneo la Mkundi ikihusisha gari lenye namba za usajili STK 9242 gari la mke wa waziri mstaafu Mizengo Pinda likitokea Dodoma kwenda jijini Dar-es-Salaam  na pikipiki

Majeruhi wengine wa ajali hiyo ni dereva wa gari hilo Bw Anjelo Mwisa, mlinzi wa mke wa waziri mkuu mstaafu Gaudensi Tembo na kijana wa familia ya Mama Tunu Pinda Bwana Gilbert Sampa.

Kwa upande wake mganga mfawidhi wa hospitali ya rufaa mkoa wa Morogoro Dr Rita Liamuya amesema hali ya mke wa waziri mkuu mstaafu na majeruhi wengine zinaendelea vizuri na kueleza kuwa  majeruhi hao wanatarajia kuhamishiwa jijini Dar-es-Salaam kwa matibabu zaidi.

Mke Wa Rais Mama Janeth Magufuli Amtembelea Mufti Mkuu Wa Tanzania Sheikh Abubakar Zubeiry Hospitali Muhimbili.

$
0
0

Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akimjulia hali Mufti Mkuu wa Tanzania Sheikh Abubakar Zubeiry aliyelazwa kwa matibabu katika taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili.
 
Pamoja naye ni Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Watoto na Wazee Mhe Ummy Mwalimu, Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe George Masaju pamoja na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi hiyo Profesa Mohamed Janabi leo Jumatatu February 8, 2016.
 


Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akisindikizwa wakati wa kuondoka baada ya kumjulia hali Mufti Mkuu wa Tanzania Sheikh Abubakar Zubeiry aliyelazwa kwa matibabu katika taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili.
 
Pamoja naye ni Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Watoto na Wazee Mhe Ummy Mwalimu na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi hiyo Profesa Mohamed Janabi  leo Jumatatu February 8, 2016.

Mwalimu Mkuu Avuliwa Wadhifa Wake Baada Ya Kuchelewa Kikao Cha Mkuu wa Wilaya

$
0
0

Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Butinzya, amevuliwa wadhifa huo kwa madai ya kuchelewa kuhudhuria kikao kilichoitishwa na Mkuu wa Wilaya ya Bukombe, Amani Mwenegoha.

Utekelezaji wa kumvua madaraka mwalimu huyo, Mathias Mazuri, ulifanywa na Ofisa Elimu Shule za Msingi wa wilaya hiyo, Shadrack Kabanga.

Mwalimu Mazuri alichelewa kikao kilichoitishwa na Mwenegoha Februari 6, kikiwa na lengo la kudhibiti fedha za ruzuku ya Serikali na kwamba adhabu hiyo ni fundisho kwa watumishi wengine.

Akitangaza kumvua wadhifa huo mbele ya walimu wakuu wenzake, Kabanga alisema Shule ya Butinzya ipo karibu na eneo la mkutano na wezake waliotoka mbali walifika saa 3:00 asubuhi yeye saa 6:00 mchana.

“Sikubali, huu ni muda wa kubadilika siyo kuleana, nakuvua wadhifa kuanzia sasa siyo Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Butinzya,” alisema.

Mwalimu Mazuri alijitetea kuwa kuchelewa kwake kulitokana na pikipiki yake kuharibika njiani, utetezi huo ulitupiliwa mbali na ofisa elimu.

Mkuu wa wilaya hiyo, Mwenegoha aliwataka walimu kutumia vizuri fedha za ruzuku na kwamba, wasichangishe wazazi kutokana na uhaba wa posho za madaraka.

Mwenegoha alipiga marufuku kuwadai wanafunzi fedha za masomo ya ziada.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumanne Ya Februari 9

Rais Magufuli Atoa kauli Kuhusu Mgogoro wa Kisiasa visiwani Zanzibar, Asema Hakuna Suluhu zaidi ya Kurudia Uchaguzi.

$
0
0

Rais John Magufuli amesema kuwa hana mamlaka yoyote ya kuingilia suala la uchaguzi wa Zanzibar.
 
Rais Magufuli aliyaeleza hayo  jana katika hotuba yake kwa mabalozi mbalimbali wanaoziwakilisha nchi zao hapa Tanzania iliyosomwa kwa niaba yake na waziri wa mambo ya nje, ushirikiano wa Afrika Mashariki, kikanda na kimataifa Balozi Augustine Mahiga  jana ikulu jijini Dar es salaam.
 
Katika hotuba hiyo, Rais Magufuli aliwaeleza mabalozi hao kuwa licha ya Tanzania kuwa nchi moja, Zanzibar ina mfumo wake wa siasa, ina serikali yake, Katiba yake na pia tume yake ya uchaguzi inayojitegemea.
Alisema tume hiyo ilifuta uchaguzi kutokana na mapungufu yaliyojitokeza kisiwani Pemba, na kwamba tayari tarehe mpya ya uchaguzi wa marudio imekwisha tangazwa kwa mujibu wa Katiba ya Zanzibar.
 
Alosema mazungumzo ya kutatua mgogoro huo yalifanyika bila mafanikio ambapo chama kikuu cha upinzani (CUF) kimeendelea kupinga uchaguzi wa marudio huku vyama vingine kikiwemo chama tawala vikionesha uhitaji wa uchaguzi huo wa marudio.
 
Alisema kwa hali ilivyo, busara inahitajika ili kunusuru suala hilo, na kwamba kususia uchaguzi siyo suluhu bali kutumia nafasi iliyopo sasa kujadili namna ya kuufanya uchaguzi wa marudio kuwa huru na wa haki.
 
Aliwaeleza mabalozi hao kuwa serikali pamoja na watanzania walio wengi wangependa kuona CUF inathibitisha madai yake ya kushinda uchaguzi huo kupitia sanduku la kura katika uchaguzi wa marudio.
 
“Tunakiasa chama cha CUF kama ambavyo watanzania wengi wangependa kuona, kuthibitisha madai ya ushindi wao katika sanduku la kura, hakuna jinsi nyingine ya kutatua suala hili zaidi ya kukubali kufanya uchaguzi wa marudio” ilisema sehemu ya hotuba hiyo.
 
Magufuli amewahakikishia mabalozi hao kuwa nchi ni salama na hali ya amani na utulivu ni ya kuridhisha katika kipindi hiki cha kuelekea katika uchaguzi wa marudio.
 
Fungua PDF ifuatayo kusoma hotuba yake kamili:- 
 

Hashim Rungwe Akosoa kauli za Rais Magufuli Kuhusu idara ya Mahakama, asema Zinaingilia Uhuru wa Mahakama.

$
0
0

Mwenyekiti wa chama cha ukombozi wa umma CHAUMA Hashim Rungwe amesema kauli iliyotolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzani Dkt John Pombe Magufuli wakati wa maadhimisho ya siku ya Mahakama nchini iliingilia uhuru wa mahakama.

Mwenyekiti wa chama cha ukombozi wa umma CHAUMA Hashim Rungwe amesema kauli iliyotolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzani Dkt John Pombe Magufuli wakati wa maadhimisho ya siku ya Mahakama nchini iliingilia uhuru wa mahakama.

Akielezea utata uliojitokeza katika hotuba hiyo Rungwe amesema hotuba hiyo ilionekana kama kuifundisha mahakama wajibu wake jambo ambalo lina utata katika uongozi wa kisheria lakini hata hivyo Rungwe ameielezea hotuba hiyo kuwa itaongeza uwajibikaji katika mahakama na haki kupatikana kwa wakati.

Wakati wa siku ya maadhimisho ya siku ya mahakama Alhamisi iliyopita, Rais Magufuli aliahidi kuipatia idara ya mahakama fedha kwa ajili ya kuendesha shuhguli za mahakama na kuitaka mahakama hiyo kuharakisha kusikiliza kesi mbalimbali ikiwa ni pamoja na kesi za watuhumiwa wa kukwepa kulipa kodi.

Jaji Mihayo Amtetea Rais Magufuli........ Asema Sio Dikteta na Kauli Yake Kuhusu Mahakama Ilikuwa Ni Kuwataka Majaji Wafanye Kazi Kwa Bidii

$
0
0

Siku tatu baada ya Rais John Magufuli kueleza kuwa yeye si kichaa, si dikteta wala mnyama, Jaji Thomas Mihayo ameungana na mkuu huyo wa nchi akisema hajauona udikteta wake.

Jaji Mihayo alikuwa akifafanua kauli alizotoa Rais Magufuli kwenye kilele cha Siku ya Sheria, wakati alipomuahidi Jaji Mkuu Othman Chande Sh12.3 bilioni za kuendeshea shughuli za mahakama na kumtaka aharakishe kushughulikia kesi za ufisadi ili Serikali iokoe Sh1 trilioni, ambazo kati ya hizo atatoa Sh250 bilioni kwa ajili ya Idara ya Mahakama.

Rais pia alitaka kesi ambazo watuhumiwa wanakamatwa na ushahidi, zifikishwe mahakamani mara moja na kuamuliwa, lakini akataka asichukuliwe kuwa ni dikteta kutokana na maamuzi yake.

“Ninapochukua hatua mimi si mnyama, si dikteta, si shetani. Ni mpole kweli, lakini inafika mahali lazima nifanye (uamuzi). Yanayofanyika serikalini ni mambo ya ajabu sana, nataka kutoa sadaka yangu, inawezekana hata nikifa naweza kuwa rais wa malaika,” alisema.

Kauli hiyo imeibua mjadala miongoni mwa wanasheria wanaodai Rais anaingilia uhuru wa mahakama kwa kutaka uamuzi wa kesi hizo ufanywe kwa utashi wa Serikali, huku baadhi ya hatua kali anazochukua zikielezewa kuwa zina harufu ya udikteta. 

Lakini jana, mkuu huyo wa nchi alipata mtetezi wakati Jaji Mihayo alipoongea na waandishi kufafanua kauli hiyo ya Siku ya She ria, akisema Rais dikteta ni yule asiyefuata misingi ya sheria.

“Wanaosema Magufuli ni dikteta hawawajui madikteta. Hakuna kiongozi dikteta Afrika Mashariki isipokuwa Idi Amini tu,” alisema jaji huyo mstaafu ambaye alisema ameamua kutoa ufafanuzi huo baada ya kuona mjadala mkubwa kuhusu kauli hiyo ya Rais na kupata baraka kutoka kwa Jaji Mkuu, Othuman Chande.

Jaji Mihayo, ambaye ni mwenyekiti wa majaji wastaafu, alihoji inawezekanaje kiongozi ambaye mataifa mengine wanatamani akaongoze nchi yao angalau kwa miezi miwili, aonekane kuwa ni dikteta.

“Magufuli anafuata sheria kwa sababu hajafanya jambo lolote ambalo linamfanya awe juu ya sheria. Sijawahi kusikia kasema mfunge huyu au kusema sheria hii isitumike na hii itumike” alisema.

Alisema ni kawaida kwa viongozi wanaokemea uovu kuonekana kama madikteta kwa sababu wanataka kuondoa rushwa.

Kadhalika, Jaji Mihayo alisema anaupenda utendaji kazi wa Magufuli ili wanaokiuka sheria wawajibishwe na walalahoi wapate haki yao.

Magufuli na Mahakama 
Kuhusu ahadi yake ya kuipa Idara ya Mahakama Sh12.3 bilioni ili izitumie kwenye shughuli zake na agizo la kuharakisha uamuzi wa kesi 442 ili Serikali iokoe Sh1 trilioni, Jaji Mihayo alisema kitendo hicho hakiingilii uhuru wa mahakama bali ni katika kuhakikisha kesi zinamalizwa kwa wakati na serikali inakusanya mapato ya kutosha.

“Maneno ya Rais ya kuwataka majaji wamalize kesi kwa haraka na kuwaahidi kiasi kile cha fedha, si kuwahonga bali ni motisha na mbinu ya kukusanya mapato,” alisema.

Alisema kauli ya Rais isitafisriwe kuwa ni lazima Serikali ishinde kesi dhidi ya rufaa ya kodi, bali alitaka majaji wafanye kazi zao kwa wepesi zaidi.

Akifafanua kesi za rufaa za kodi, Jaji Mihayo alisema mashauri hayo yatakusanya fedha nyingi kwa hata kama wanaodaiwa watashinda, kisheria ni lazima watoe theluthi ya kodi wanayodaiwa.

Jaji Mihayo pia alisema maneno ya Magufuli yasichukuliwe kuwa yatawavuruga majaji kwa sababu wanafanya kazi yao kwa kufuata kanuni na sheria.

“Uhuru wa mahakama upo ‘guaranteed (umehakikishwa)’ na katika kifungu namba 107 (a) cha Katiba ya Jamhuri ya Muungano.Hata kama Rais akiamrisha vipi, kama ni kitu ambacho ni kinyume na utaratibu, hakiwezi kutekelezwa” alisema.

Kuhusu Magufuli kuwachukulia hatua majaji na mahakimu 502 ambao hawajafikia malengo ya kumaliza kati ya kesi 250 na 260 kwa mwaka, Jaji Mihayo alisema JPM alionyesha kukerwa na ucheleweshaji wa kesi na wala si kuingilia uhuru wa mahakama.

Alisema hata Jaji Mkuu Othman Chande alishachukua hatua kwa kuwataka mahakimu hao watoe maelezo kabla sheria haijachukua mkondo wake.

“Tatizo la ucheleweshaji wa kesi ni kubwa, si dogo kama unavyofikiria ndiyo maana linamkera JPM,” alisema.

Utendaji wa mawaziri, wakuu wa mikoa 
Kadhalika Jaji Mihayo pia alizungumzia pia jinsi mawaziri wa JPM wanavyotoa kauli za kuwafukuza kazi au kuwasimamisha watendaji wa Serikali, akisema siasa inatawala kuliko sheria.

Alisema kisheria kiongozi wa Serikali hawezi kusimamishwa kazi au kufukuzwa bila maandishi.

“Watendaji hawatachukuliwa hatua bila kauli ya waziri kuwa katika maandishi, hilo jambo halichukuliwi kijumla tu,” alisema.

Alisema Katibu Mkuu Kiongozi akimsimamisha au kumfukuza mtu kazi, hilo linakuwa limeshafanyiwa kazi kwa kina.

“Vinginevyo, huwezi kumfukuza mtu kazi bila mchakato na uchunguzi wa kuhakiki kama ni kweli ana haki ya kusimamishwa au kufukuzwa,” alisema.

Jeshi La Polisi Lakamata Majangili 9 Waliotungua Helkopta na Bunduki 29.....Miongoni Mwa Waliokamatwa ni Mhifadhi wa hifadhi ya Ngorongoro

$
0
0
Siku chache baada ya kutokea tukio la majangili katika pori la akiba Maswa wilaya ya Meatu Mkoani Simiyu, kuitungua ndege (helikopta) iliyokuwa doria na kuaawa kwa rubani wake Rodgers Gower (37),  watu 9 wamekamatwa kuhusika na tukio hilo.

Katika watuhumiwa hao mmoja ni Mhifadhi wa hifadhi ya taifa ya Ngorongoro kitengo cha Interejensia, ambaye alitajwa kuwa mhusika Mkuu wa kufanikisha tukio hilo sambamba na kukamatwa mganga wa jadi.

Akitoa taarifa mbele za waandishi wa habari ofisini kwake jana, Kamanda wa polisi Mkoani Simiyu Lazaro Mambosasa alisema kuwa kukamatwa kwa watuhumiwa hao kumetokana na jeshi hilo kufanya kazu usiku na mchana  kwa kushirikiana na wananchi, pamoja na uongozi wa TANAPA.

Kamanda Mambosasa alisema watuhumiwa wote walikamatwa na kukiri kuhusika na tukio hilo, huku akieleza kuwa msako mkubwa uliofanywa na jeshi hilo mara baada ya tukio kutokea chini ya Mkuu wa upelelezi Mkoa Jonathan Shana.

Alisema katika msako huo baadhi ya watuhumiwa walibainika kuwa kiungo kikubwa kufanikisha tukio hilo kwa kutoa mbinu za uharifu, huku wakijihusisha na matukio ya ujangili kwa muda mrefu.

Aliongeza kuwa baadhi yao walibainika kuwa waganga wa jadi, ambapo walikuwa wakitoa dawa kwa majangili za kuosha silaha, ikiwa ni pamoja na  kuosha na kusafisha miili yao ili wasiweze  kukamatwa.

Mambosasa aliwataja watuhumiwa hao kuwa ni Shija Mjika (38), Njile Gonga (28) Mhazabe, Masasi Mandago (48) pamoja na Dotto Pangali (41) , ambao ndio walihusika kutungua helkopta hiyo.

Wengine ni Iddi Mashaka (49) ambaye Kamanda Mambosasa alimtaja kuwa Mhifadhi wa hifadhi ya taifa ya Ngorongoro Kitengo cha Intelijensia na ndiye alikuwa kiungo Mkuu wa tukio hilo.

Aliwataja wengine kuwa ni Mapolu Njige (50) ambaye ni mganga wa jadi aiyekuwa anatumika kutoa dawa za kutokamatwa kwa majangili hao, Mwigulu Kanga (40) , Dotto Huya (45) , Pamoja na Mange Balumu.

Aidha Mambosasa alisema kuwa Mtuhumiwa Dotto Pangali alikamatiwa katika wilaya ya Kishapu Mkoa wa Shinyanga mnamo tarehe 7/02/216 na kufanyiwa upekuzi nyumbani kwake ambapo alikutwa na bunduki aina ya Riffle yenye namba .7209460 CAR Na.63229.

Mkuu huyo wa polisi alisema Mtuhumiwa huyo alikiri bunduki hiyo kutumika katika tukio la kuuawa kwa rubani huyo, ambapo ilibainika kuwa bunduki hiyo inamilikiwa na Mange Magima ambaye pia amekamatwa.

Alisema msako uliendelea nyumbani kwa Pangali na kufanikiwa kukamatwa kwa bunduki nyingine aina ya Riffle Na3478 CAR 458 ikiwa na risasi 6 ambayo ilibainika kumilikiwa na Nghomango Jilala ambaye mpaka sasa hajakamatwa.

Alieleza kuwa jeshi hilo liliendelea kupata taarifa ambapo mnamo tarehe 29/01/2016 walikamatwa Shija Mjika, Njile Gonga, pamoja na Masasi Mandago wakiwa na meno ya tembo 2 yakiwa na uzito wa Kilo 31 yakiwa yamefichwa chini ya daraja katika kijiji cha Itaba.

Aidha Mambosasa alieleza kuwa baada ya kukamatwa kwa wahusika wote ilibainika kuwa bunduki zilizotumika katika tukio hilo zinamilikiwa kihalali na watu ambao waliomba kuzimiliki kwa ajili kujilinda.

“Mbali na tukio hilo bunduki nyingi wamiliki wake wanawaazimisha majangili kwa ajili ya kutumika kwa uhalifu pamoja na kuua wanyama ndani ya hifadhi…lakini na hao wamiliki wanalipwa pesa baada ya uhalifu kufanyika” ,alisema.

Alisema baada ya kubaini hilo kulifanyika msako mwingine kwa wanaomiliki silaha, ambapo alisema asilimia kubwa wanaishi karibu na hifadhi, na jumla ya bunduki 27 zimekamatwa na mara baada ya uchunguzi wamiliki watarudishiwa.

“Tunajiandaa kupeleka zuio la silaha mahakamani ili kubaini kama wana sifa za umiliki…lakini mbali na hilo sasa kutaanzishwa oparesheni kwa watu wote wanaomiliki silaha hasa maeneo ya hifadhi kwa ajili ya kuwanyanganya”, alisema.
 
Mkuu huyo wa polisi alisema kuwa upelelezi juu ya tukio hilo umekamilika na watuhumiwa wote watafikishwa mahakamani leo Jumanne ili kujibu tuhuma zinazowakabili, ambapo alioomba mahakama kuharakisha hukumu kwa vile uchunguzi umekamilika.

Kwa upande wake Mhifadhi mkuu wa Serengeti William Mwakilema amelipongeza jeshi la polisi ambapo amesema tukio hilo lilipotokea liliwasikitisha sana kwani hasara ilipatikana kutokana na kutunguliwa kwa helkopta.

Mnamo tarehe 29/01/2016 saa 11:30 jioni katika eneo la Gululu lililopo ndani ya hifadhi ya Maswa kata ya Mwangudo wilaya ya Meatu Mkoani Simiyu, majangili waliipiga risasi ndege (helkopta) 88HFCG iliyokuwa doria na kusababisha kifo cha rubani wake Rodgers Gower (37) raia wa uingereza huku Mwenzake Nicholas Beste (43) raia wa Afrika Kusini akinususrika kifo. 


Mahakama Yatoa siku Saba Marekebisho kesi ya Augustine Mrema Kupinga Ushindi wa James Mbatia

$
0
0

Mahakama Kuu Kanda ya Moshi imetoa siku saba kwa mawakili waandamizi wa Serikali kutoa majibu ya kuendelea kusikilizwa kwa kesi ya aliyekuwa mgombea wa ubunge Jimbo la Vunjo wa TLP, Augustine Mrema .

Januari 18, mwaka huu, mahakama ilimpa siku 12 Mrema kwenda kufanya marekebisho ya maombi yake aliyokuwa amepeleka mahakamani hapo ya kupinga matokeo yaliyompa ushindi mbunge James Mbatia (NCCR Mageuzi).

Akitoa uamuzi huo mbele ya wakili mwandamizi wa Serikali, Omary Kibwana akisaidiana na Glory Efatha, Jaji Benedict Mwingwa alisema kwa siku saba mawakili hao watatakiwa kupeleka majibu ili kesi hiyo iweze kuendelea kusikilizwa.

Jaji alisema Februari 18, mwaka huu ndiyo siku ambayo watasikiliza kesi hiyo baada ya mawakili hao kupeleka majibu mahakamani hapo na Februari 15.

Awali, mawakili hao waliiomba mahakama kupewa muda wa kutosha wa kujibu maombi ya marekebisho hayo ili kesi iweze kuendelea kusikilizwa.

Wakili anayemwakilisha Mbatia, Youngsevia Msuya aliiomba mahakama hiyo kusikiliza kesi hiyo Februari 18 badala ya Februari 15.

Awali, Mrema ambaye pia ni Mwenyekiti wa Taifa wa TLP, alifungua kesi hiyo kupinga ushindi wa Mbatia aliyepata kura 60,187 dhidi ya kura 16,617 za Mrema katika Uchaguzi Mkuu uliofanyika nchini Oktoba 25, mwaka 2015.

Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni Yaunda Kanuni Zitakazowaongoza Wabunge Wake

$
0
0

Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni (KUB) imeunda kanuni zitakazowaongoza wabunge wake kuendesha shughuli mbalimbali za chombo hicho cha uwakilishi.

Kaimu Katibu Mkuu wa Chadema, Salum Mwalimu aliwaambia wanahabari jana kuwa kanuni hizo ambazo zimeundwa kwa kushirikisha vyama vyote vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) zitasaidia kuondoa holela iliyokuwa ikijitokeza awali ndani ya KUB.

Mwalimu, ambaye chama chake ndiyo kinaongoza kambi hiyo, alisema Chadema inaipongeza hatua hiyo kwa kuwa imeonyesha kuzaa matunda katika mkutano wa pili wa Bunge la 11 uliomalizika wiki iliyopita.

Kanuni hizo za kambi rasmi ya upinzani, kwa mujibu wa Mwalimu zimeanzishwa kwa kufuata kanuni ya 16, ibara ya 4 ya Kanuni za Kudumu za Bunge ambayo inasema:

“Vyama vya siasa vyenye uwakilishi bungeni vinaweza kutunga kanuni za vyama vya kwa ajili ya uendeshaji bora wa shughuli za vyama hivyo bungeni.”

Mwalimu alisema kanuni hizo tayari zimeshasaidia uteuzi wa wawakilishi katika vyombo vya kimataifa kupitia Bunge.

Alisema katika utaratibu wa kanuni hizo mpya jambo likishaamriwa kwenye vikao vya umoja huo hakuna mtu wa kupinga na ikitokea mbunge husika akazivunja hatua za kinidhamu zitachukuliwa. 

“Kwa sasa hamna tena songombingo ya kupata nafasi za uwakilishi ndani ya Bunge. Likipita jambo ndani ya caucus (kikao cha chama) basi limepita...hakuna tena kuvujisha siri ndiyo maana safari hii hata waandishi ilikuwa vigumu kupata taarifa za ndani,” alisema.

 Akizungumzia umeya Dar es Salaam alisema kuna hila za wazi za kutaka kuongeza wajumbe wasiotakiwa katika uchaguzi hasa kutoka Ilala na Kinondoni.

Hali ya Mufti Mkuu Abubakar Zuberi Yaimarika Baada Ya Kufanyiwa Upasuaji Wa Tumbo

$
0
0

Hali ya Mufti wa Tanzania, Sheikh Mkuu wa Tanzania Abubakar Zuberi ambaye amelazwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) kwa matibabu inaendelea vizuri.

Ofisa Uhusiano wa MNH, Neema Mwangomo jana alisema mufti amelazwa katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete   na alifikishwa  Hospitalini  hapo  juzi. 

Jana, viongozi  mbalimbali  wa  serikali  akiwemo  Waziri Mkuu Kassim Majaliwa walimtembelea  kumjulia hali  Mufti Zeburi

Pia,baadhi ya waumini wa Kiislamu jana mchana walionekana nje ya jengo hilo wakitaka kufahamu maendeleo ya afya ya kiongozi wao huyo. 

Watendaji wa Sekta ya Afya waaswa kuota taarifa sahihi juu ya idadi ya wagonjwa wa Kipindupindu

$
0
0

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu amewataka watendaji wa Serikali na Sekta ya Afya kuwajibika ipasavyo kwa  kutoa taarifa sahihi juu ya idadi ya wagonjwa wa kipindupindu nchini.

Akitoa tamko kuhusu mwenendo wa ugonjwa wa kipindupindu nchini pamoja na tahadhari ya ugonjwa wa Zika jana  jijini Dar es salaam Mhe. Ummy alisema kuwa watendaji watakaoficha taarifa za wagonjwa katika maeneo yao watawajibishwa.

“Mojawapo wa changamoto katika mapambano ya kudhibiti mlipuko huu wa kipindupindu ni utoaji wa idadi pungufu au kutotoa kabisa taarifa za wagonjwa wa kipindupindu hivyo kupelekea kutokuwa na mafanikio katika mikakati iliyowekwa” alisema Waziri Ummy.

Aidha, alitoa wito kwa sekta nyingine kushirikiana na Wizara kupambana na ugonjwa huo ili kukabiliana  na baadhi ya changamoto zinazowakabili watoa huduma za afya na elimu walioko katika maeneo mbalimbali nchini.
 
“ Jukumu la kupambana na mlipuko wa ugonjwa huu si la Wizara ya Afya pekee  naomba sekta nyingine ikiwemo Maji, Miondombinu, Biashara Elimu na Mazingira tushirikiane kwa pamoja ili kuutokomeza ugonjwa huu”.

Mbali na hayo Mhe. Ummy alieleza kuwa takwimu za kuanzia tarehe 1 hadi 7 februari mwaka huu zinaonyesha kuwa idadi ya wagonjwa wa kipindupindu imepungua kutoka 459 ya wiki iliyoisha tarehe 31 Januari hadi 258 ambapo ni sawa na punguzo la asilimia 44%.

Hata hivyo Wizara imewatoa hofu wananchi na kuwakumbusha kuendelea kuchukua tahadhari dhidi ya ugonjwa wa Homa ya Zika pamoja na magonjwa mengine yanayoenezwa na Mbu.

Taarifa Kwa Umma Kutoka Ofisi Ya Makamu Wa Rais

Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images