Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, SACP Justus Kamugisha.
ASKARI Polisi wa Kituo cha Polisi Nyamagana jijini Mwanza, Konstebo Daud Masunga Elisha, amemuua askari mwenzake, Konstebo Petro Saimon Matiko kwa risasi na baadaye kujiua kwa risasi na kufa papo hapo.
Tukio hilo lilitokea jana saa 8.30 mchana jijini Mwanza katika eneo la Benki ya Posta Tawi la Pamba wilayani Nyamagana huku
Polisi Wauana Kwa Risasi Jijini Mwanza Wakiwa Lindoni
↧
↧
Serikali Yatangaza ‘Kuminya’ AJIRA za Wageni......Wanaoishi Nchini Bila Kibali Kukiona cha Moto
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga ameagiza waajiri kote nchini kutowapa ajira wageni kwa kazi zinazoweza kufanywa na Watanzania.
Pia, ameagiza maofisa wa Idara ya Uhamiaji kufanya operesheni maalumu kuwatimua raia wote wasio na vibali vya kuishi nchini ifikapo Januari 31, 2016.
Kitwanga ambaye alitembelea idara hiyo jana, alisema wizara yake kwa kushirikiana na
↧
Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Ijumaa Ya Disemba 25
↧
Mawaziri na Manaibu Walioteuliwa Juzi Kuapishwa Jumatatu
Tarehe 23 Desemba, 2015 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.
John Pombe Magufuli aliwateua Mawaziri wanne, Naibu Waziri mmoja na
kumhamisha Wizara Waziri mmoja.
Walioteuliwa ni Waziri wa
Maliasili na Utalii Profesa Jumanne Maghembe, Waziri wa Maji na
Umwagiliaji Mhandisi Gerson Lwenge, Waziri wa Elimu, Sayansi,
Teknolojia na Ufundi Dkt. Joyce Ndalichako na Naibu Waziri wa
↧
Serikali Yapiga Marufuku Matangazo Yote Yanayohusu Tiba asili na Tiba Mbadala Kwenye Vyombo vya Habari na Mitandao ya Kijamii.
Taarifa kutoka Wizara ya Afya kuanzia tarehe 24 Desemba 2015 imepiga
marufuku matangazo yote yanayohusu tiba asili na tiba mbadala kwenye
vyombo vya habari na mitandao ya kijamii.
Wale wote wenye vibali
wanatakiwa kuviwasilisha vibali na matangazo yao kwenye Baraza la Tiba
Asili na Tiba Mbadala ili vifanyiwe mapitio.
Utoaji wa elimu ya
afya kwa umma unaofanywa na watoa huduma za
↧
↧
Afisa wa Intelijensia wa TANAPA Aliuawa na Mfanyakazi Wake Wa Ndani Kwa Kukatwa Panga Wakati Akinywa Uji.....
Jeshi la Polisi Mkoani hapa limefanikiwa kumkamata mtu mmoja aitwaye
Ismail Swalehe Sang’wa (20) ambaye ni mwenyeji wa kijiji cha Sepuka
wilayani Ikungi katika Mkoa wa Singida kwa tuhuma za kumuua Afisa wa
Intelijensia wa TANAPA aitwaye Emily Kisamo (52).
Akizungumza
na waandishi wa habari ofisini kwake jana asubuhi , Kamanda wa Polisi
Mkoa wa Arusha Naibu Kamishna wa Polisi (DCP)
↧
Serikali Haijatoa Tamko La Kutowalipa Makocha Wa Taifa Stars
Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo inakanusha taarifa zilizoandikwa katika gazeti la Mwananchi la tarehe 24.12.2015 yenye kichwa cha habari “JPM kutolipa makocha Stars”.
Serikali kupitia Wizara inayohusika na michezo haijatoa tamko la kutowalipa makocha wanaofundisha timu ya Taifa Stars kama ilivyoripotiwa na gazeti hilo.
Suala la malipo ya makocha wa Taifa Stars
↧
Waziri Mkuu Ataka Amani ya Nchi Ilindwe......Akemea Uvaaji wa Nguo Fupi na Matumizi Ya Dawa Za Kulevya
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amewataka wananchi waendelee kulinda
amani ya nchi huku akikemea uvaaji wa nguo fupi na kuwasihi Watanzania
kujenga tabia ya kuvaa mavazi yenye kumpendeza Mungu.
Pia,
amekemea matumizi ya dawa za kulevya na mimba za utotoni akisema ni
mambo ambayo yanaepukika kwa mtu yeyote aliyelelewa katika misingi ya
kidini.
Waziri Majaliwa alisema hayo jana
↧
Serikali Yawapiga STOP Akina Lowassa Na Wenzake Kufanya Mikutano ya Hadhara
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amesema wanasiasa walioshindwa kwenye Uchaguzi Mkuu hawaruhusiwi kuitisha mikutano ya hadhara kwa ajili ya kuwashukuru wananchi kwa kuwa wanaweza kuvuruga shughuli za maendeleo.
Waziri Mkuu alisema hayo wakati akilishukuru Jeshi la Polisi wilayani Ruangwa kwa kufanya kazi ya kusimamia Uchaguzi Mkuu uliomalizika Oktoba 25 kwa CCM kushinda kiti cha urais na
↧
↧
Rais Magufuli Ashiriki Misa Ya Krismasi Kanisa La Mtakatifu Peter Jijini Dar Es Salaam Leo
Rais
Dkt John Pombe Joseph Magufuli akiwasili kushiriki Ibada ya Krismas misa
ya kwanza katika Kanisa la Mtakatifu Peter jijini Dar es salaam leo
Desemba 25, 2015.
Rais
Dkt John Pombe Joseph Magufuli, mkewe Mama Janeth Magufuli na Mke wa
Waziri Mkuu Mama Mary Majaliwa wakishiriki Ibada ya Krismas katika
Kanisa la Mtakatifu Peter jijini Dar es salaam leo Desemba 25, 2015
↧
Serikali Kuvunja Nyumba ya Waziri Mkuu wa Zamani Fredrick Sumaye.
WAZIRI Mkuu mstaafu Fredrick Sumaye, ameingia matatani baada ya kudaiwa kuvamia eneo la wazi na kuanza kuzungushia uzio, bila kufuata sheria na utaratibu wa ujenzi.
Eneo hilo la kiwanja namba 719/1/3 lililopo Mkiocheni, mtaa wa TPDC, lilikuwa likitumika kwa ajili ya michezo, mikutano ya kisiasa, pamoja na mikusanyiko mbalimbali ya kijamii.
Kufuatia tuhuma hizo, timu ya maofisa ardhi
↧
Ridhiwan Kikwete Alikana Gazeti La Mawio.......Adai aliyekuwa Anamsaidia Kufunga Viatu Sio Paul Makonda,Ni Deogratias Kessy
Mbunge wa Chalinze, Mheshimiwa Ridhiwani Kikwete amekanusha aliyekuwa anamsaidia kufunga kamba za viatu katika picha iliyochapishwa kwenye gazeti la MAWIO (picha juu) si Paul Makonda Makonda, Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni.
Akizungumza na waandishi wa habari , Ridhiwani Kikwete alisema anayeonekana akimsaidia kufunga viatu katika picha hiyo ni Deogratias Kessy, mfanyakazi katika kampuni ya
↧
Askofu Morogoro Amtaka Rais Magufuli Kuendeleza 'moto' ili Kuwadhibiti Wapiga Dili
Serikali ya awamu ya tano imeshauriwa kuendelea na adhma yake ya kudhibiti watumishi wa umma wanaotumia madaraka yao vibaya kwa maslahi binafsi.
Katika kuadhimisha sikukuu ya Krisimas mkoani Morogoro Askofu mkuu wa kanisa la KKKT Dayosisi ya Morogoro Askofu Jackob Mameo ameiomba serikali kuendelea na msimamo wake wa kuwawajibisha watumishi wanaotumia nafasi zao kwa manufaa binafsi ili
↧
↧
Familia Ya Rais Mstaafu Jakaya Kikwete Yatoa TAMKO Zito....Yasisitiza Haihusiki na Utoroshaji wa Makontena Bandarini.Mwenye Ushahidi Autoe
Mbunge wa Chalinze, Mheshimiwa Ridhiwani Kikwete, ambaye ni mtoto wa Rais Mstaafu Jakaya Mrisho Kikwete ,kwa niaba ya familia yake ametoa tamko zito kupinga tuhuma mbalimbali zinaozoelekezwa kwake na familia yake.
Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam Jana,Ridhiwani alisema baada ya Rais Kikwete kumaliza muda wa miaka 10 madarakani, baadhi ya watu wamekuwa wakiiandama familia
↧
Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumamosi Ya Tarehe 26
↧
Magufuli Awakuna Viongozi Wa Dini.....Maaskofu Wahimiza Aombewe Ili Aendelee Kutumbua Majipu
Viongozi wa makanisa mbalimbali nchini, wametoa salamu za Sikukuu ya Krismasi jana, wakielezea kufurahishwa na kasi ya utendaji kazi wa Rais John Magufuli.
Wamesisitiza waumini wao, kumuombea Rais na kuwataka wananchi kutii mamlaka, kwa kuwa yamewekwa na Mungu.
Viongozi hao pia, wamewataka watendaji wa Serikali na wananchi walioshiriki ukwepaji kodi, watubu dhambi zao na kurejesha
↧
Tanzania Yaanza Kusaka Amani Burudi......Waziri Mahiga Ateta Na Rais Nkurunziza Kwa Masaa Mawili
WAZIRI wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Dk Augustine Mahiga, amekutana na kufanya mazungumzo na Rais Pierre Nkurunziza wa Jamhuri ya Burundi, kwenye Ikulu yake jijini Bujumbura.
Taarifa ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, iliyotumwa jana kwa vyombo vya habari, ilifafanua kwamba hatua hiyo ya Dk Mahiga, ni utekelezaji wa maagizo ya Rais John Magufuli.
Kwa
↧
↧
Picha: Lowassa Aanza Kuchunga Ng'ombe Kama Alivyoahidi
Aliyekuwa mgombea wa uraisi kwa mwavuli wa UKAWA ndugu Edward Lowasa akichunga ng'ombe zake huko Handeni mkoani Tanga.
Lowassa yuko mapumzikoni na familia yake katika shamba lake la mifugo lililopo eneo la Mzeri,Handeni mkoani Tanga
↧
Nape Nnauye: Nchi ilifika pagumu, tumuombee Magufuli
Waziri wa Habari, Utamaduni, Wasanii na Michezo, Nape Nnauye amesema Watanzania wanapaswa kumuombea Rais John Magufuli ili aendelee kutumbua majipu kwani nchi ilifika pagumu baada ya wezi kuonekana wajanja.
Akizungumza wakati akizindua tamasha la Krismasi lililofanyika katika Ukumbi wa Diamond Jubilee, Dar es Salaam Nape aliyemwakilisha Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan alisema
↧
Lowassa Aibukia Kanisani Handeni Ibada Ya Krismasi......Awataka Watanzania Wadumishe Amani Na Upendo
Aliyekuwa mgombea urais kwa tiketi ya Chadema, Edward Lowassa ameibukia katika Kanisa la KKKT wilayani Handeni mkoani Tanga, kushiriki ibada ya Krismasi na kutumia nafasi hiyo kushukuru wapiga kura katika Uchaguzi Mkuu uliopita.
Wakati Lowassa akifanya hivyo, tayari Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa ametoa agizo la kupiga marufuku mikutano ya walioshindwa uchaguzi, ikiwamo kushukuru kwa kuwa
↧
More Pages to Explore .....