Mgombea urais wa Zanzibar kwa tiketi ya CUF, Maalim Seif Sharif Hamad, ameitisha mkutano wa waandishi wa habari na kusema kuwa baada ya chama chake kukusanya fomu zote za matokeo kutoka vituoni, yeye amepata kura 200,007 dhidi ya kura 178,363 za mgombea wa CCM anayetetea nafasi yake, Dk. Ali Mohammed Shein.
Aidha, akiongea na wanahabari, Maalim Seif Sharif Hamad ameitaka Tume ya
Maalim Seif Sharif Hamad Ajitangazia Ushindi wa Urais Zanzibar..
↧
↧
Mabomu ya Machozi Yarindima Zanzibar Kuwatawanya Wafuasi wa CUF Walioingia Barabarani Kushangilia Ushindi wa Maalim Seif Sharif Hamad
Hali ya Usalama Zanzibar sio nzuri, Polisi amelazimka kutumia mabomu ya machozi kuwatawanya wafuasi wa CUF walioingia barabarani kushangilia ushindi wa Maalim Seif Sharif Hamad ambaye amejitangazia ushindi hata kabla ya ZEC kumaliza kutangaza matokeo.
Mabomu ya machozi yamepigwa kwa wingi katika mji wa Chakechake baada ya wananchi kukaidi amri halali
↧
Update Za Matokeo Malimbali Ya Ubunge na Udiwani Zinapatikana Hapa....Karibu
Jimbo la Mkinga
Mgombea wa Ubunge kupitia CCM jimbo la Mkinga Dustan Kitandula ameshinda na kutangazwa rasmi kuwa mbunge wa jimbo hilo
Jimbo la Mbinga Mjini
Mgombea wa Ubunge kupitia CCM jimbo la Mbinga Mjini Sixtus Mapunda ameshinda na kutangazwa rasmi kuwa mbunge wa jimbo hilo
Jimbo la Musoma Mjini
Ubunge: Vicent Nyerere(Chadema) 25,925 na Vedastus Mathayo(CCM) 32,839.
↧
Lowassa Kaongea na Vyombo vya Habari Mchana Huu........Kasemaje?? Bofya Hapa
Nimewaita kueleza masikitiko yetu mawili haswa katika upande wa jeshi la Polisi. Tuna vijana wetu wanaofanya kazi za IT kwa kujitolea maeneo ya kinondoni na kijitonyama jumla ya vituo vitatu.
Hawa vijana wanafanya uzalendo,kushiriki katika uchaguzi wa nchi yao,na kujenga historia moya ya nchi yao,tendo la kuwakamata si la haki kabisa
Wamewavamia na kuwakamata kwa kosa la human trafficking
↧
CCM Waongea na Vyombo vya Habari.....Wamesema Hadi sasa Wameshinda Majimbo 176 kati ya 264
CCM inapenda kutoa taarifa ifuatayo kwa wanachama, wapenzi na washabiki wake na kwa umma Watanzania.
Tathmini ya Upigaji Kura
Kama tulivyoeleza jana, tumeridhishwa na amani na utulivu uliotawala katika sehemu kubwa ya nchi yetu wakati wa zoezi la upigaji kura. Licha ya changamoto zilizojitokeza, ambazo baadhi zimeshughulikiwa, kwa jinsi zoezi la kupiga na kuhesabu kura lilivyoendeshwa
↧
↧
Mabula ashinda ubunge jimbo la Nyamagana
Mgombea wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Stanslaus Mabula ametangazwa mshindi wa mbio za ubunge katika jimbo la Nyamagana mkoani Mwanza kwa kupata kura 81, 170 dhidi ya mbunge anayemaliza muda wake, Ezekiel Wenje (Chadema) aliyepata kura 79, 280.
Akitangaza matokeo hayo usiku wa kuamkia leo, msimamizi wa uchaguzi wa Jimbo la Nyamagana, Peter Mainya, amesema jumla ya wagombea saba walichuana
↧
Mbatia atwaa Vunjo, Komu mshindi Moshi Vijijini
Tume ya Uchaguzi (NEC) imemtangaza James Mbatia wa NCCR Mageuzi kuwa mbunge mteule wa jimbo la Vunjo huku kada wa Chadema, Anthony Komu naye akiibuka mshindi katika jimbo la Moshi Vijijini lililokuwa linaongozwa na Waziri wa zamani wa Biashara na Viwanda, Dk. Cyril Chami kupitia CCM.
Akitangaza matokeo ya majimbo hayo mawili mkoani Kilimanjaro kuamkia leo, msimamizi Fulgence Mponji,
↧
Matokeo Ya Uchaguzi: Mawaziri Watano wa Serikali Ya CCM Wang'oka
Mawaziri watano wa Serikali inayomaliza muda wake wameanguka kwenye uchaguzi majimboni mwao, sambamba na wagombea wengine maarufu wa Bunge lililopita baada ya matokeo ya kura zilizopigwa Jumapili kuanza kutangazwa jana.
Mawaziri hao wanaungana na wabunge wengine maarufu wa Bunge la Kumi walioshindwa kutetea majimbo yao, wakiwamo wa kambi ya upinzani ambao wameangushwa na wagombea wa CCM.
↧
CCM Walalamikia Kitendo Cha Maali Seif Sharif Hamad Kujitangaza Mshindi......Wadai Walikamata Kura Feki za CUF Zanzibar
Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar kimesema, Maalim Seif amevunja katiba na sheria kwa kujitangaza mshindi kabla ya matokeo halali ya Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (Zec).
Akizungumza na waandishi wa habari kwenye makao makuu ya chama hicho Kisiwandui, mkoa wa Mjini Magharibi Unguja jana, Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho Zanzibar, Vuai Ali Vuai, alisema kwa mujibu wa Katiba ya Zanzibar ya
↧
↧
Kilimanjaro Yavunja Rekodi ......Majimbo 7 kati ya 9 Yanyakuliwa na Wapinzani
Mkoa wa Kilimanjaro, umevunja rekodi ya uchaguzi mkuu wa kwanza wa vyama vingi mwaka 1995 baada ya upinzani kunyakua majimbo saba kati ya majimbo tisa.
Mwaka 1995, upinzani ulinyakua majimbo sita ya Hai,Siha,Rombo, Moshi Vijijini, Moshi mjini na Vunjo na kuiachia CCM majimbo ya Mwanga, Same Mashariki na Magharibi.
Lakini kati ya mwaka 2000 na 2010, CCM ikafanikiwa kukomboa majimbo ya
↧
LIVE: Matokeo Rasmi ya Urais kwa Mujibu wa NEC (Official Results) - Uchaguzi Mkuu 2015
Tunawaletea matokeo rasmi kwa nafasi ya Urais kwa mujibu wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, NEC kama yanavyotangazwa.
Tembelea ukurasa huu mara kwa mara kwa updates zaidi
==================================
October 27, 2015 - Saa 8.40 Mchana
Jimbo la Fuoni-Mjini Magharibi
Magufuli (CCM): 956
Lowassa (CHADEMA):420
Jimbo la Kikwajuni-Mjini Magharibi
Magufuli (CCM):6,317
Lowassa
↧
Mabasi Ya Zacharia Express Yapigwa Mawe kwa Ushabiki wa Kisiasa
Mabasi mawili ya Kampuni ya Zacharia Express mali ya Pita Zacharia mkazi wa Tarime mjini yanayofanya safari zake Tarime-Mwanza yameharibiwa kwa kupondwa na mawe kwa kile kinachoelezwa ni ushabiki wa kisiasa.
Kamanda wa polisi mkoa wa kipolisi Tarime/Rorya Lazaro Mambosasa alisema kuwa Octoba 26, majira ya saa tisa mchana katika kijiji cha sokoni,Kata ya Sirari,Wilayani Tarime Gari
↧
JWTZ Yavamia Kijiji Kuondoa Vizuizi Barabarani
Vijana wa Jeshi la Wananchi jana walivamia nyumba za wananchi waliokaribu na barabara kuu ya kutoka Mbeya kwenda Malawi katika wilaya ya Rungwe na kuwataka waamke kuondoa vizuizi vya moto, magogo na mawe vilivyokuwa kwenye barabara hiyo.
Kazi hiyo ilifanywa baada ya vijana wanaodaiwa kuwa wafuasi wa Ukawa kuweka vizuzi vya moto, magogo na mawe kwenye barabara hiyo ikiwa ni ishara ya
↧
↧
Waangalizi wa Umoja wa Ulaya Watoa Maoni Kuhusu Uchaguzi Mkuu Tanzania:
Waangalizi wa Umoja wa Ulaya wamesema uchaguzi wa Tanzania kwa kiasi kikubwa umeendeshwa vizuri lakini kasoro kadhaa zimesababisha baadhi ya wanasiasa kutilia shaka uhuru wa Tume za Uchaguzi NEC na ZEC.
Katika tamko lao la awali mbele ya waandishi wa habari waangalizi hao wamesema kuwa uchaguzi wa mara hii ulikuwa na ushindani mkali huku kukishuhudiwa idadi kubwa ya watu wakijitokeza
↧
Wassira: Sikubalini na Matokeo ya Ester Bulaya....Nimehujumiwa
Saa chache baada ya Msimamizi wa Uchaguzi kumtangaza Ester Bulaya wa
Chadema kuwa mshindi katika jimbo la Bunda Mjini, aliyekuwa mbunge wa
Jimbo hilo na mpinzani wake mkuu Stephen Wassira amejitokeza na kupinga
matokeo hayo.
Wassira amedai kuwa matokeo hayo sio halali na kwamba kuna hujuma zimefanywa ili kumuangusha na kumpendelea Esther Bulaya.
Wassira
ambaye pia alikuwa Waziri
↧
Mbunge Amkaba Koo Msimamizi Wa Uchaguzi Akidai Hati Yake
Ili kupata hati ya ushindi Mbunge Mteule wa jimbo la Serengeti Mkoa wa Mara Marwa Ryoba (Chadema)alilazimika kumkaba Msimamizi wa Uchaguzi jimbo hilo,baada ya kutomkabidhi hati yake ya ushindi.
Tukio hilo lililovuta umati mkubwa wa watu wakishinikiza msimamizi huyo atoe hati lililazimu polisi kupiga mabomu ya machozi ili kutawanya watu ambao walikuwa wamezunguka uzio wa ofisi ya Mkurugenzi
↧
Idd Azzan wa CCM Aanguka Kinondoni, Cuf yachukua Jimbo
Wimbi la vyama vya upinzani kushinda ubunge jijini Dar es Salaam limeendelea baada ya mgombea ubunge kwa tiketi ya Chama cha Wananchi (CUF), Maulid Mtulia kutangazwa mshindi wa nafasi hiyo katika jimbo la Kinondoni, akimshinda mgombea wa CCM, Idd Azzan.
Akitangaza matokeo hayo usiku wa kuamkia leo, msimamizi wa uchaguzi katika jimbo hilo ambaye pia ni mkurugenzi wa manispaa ya Kinondoni,
↧
↧
UKAWA Wasema Hawayatambui Matokeo ya Urais Yanayotangazwa na NEC
Chadema kwa kushirikiana na vyama vinavyounda Ukawa, leo wanakutana kujadili mwenendo waliouita usio halali wa kutangaza matokeo, wakiituhumu Tume ya Uchaguzi (NEC), CCM na Jeshi la Polisi kushirikiana kuhujumu matokeo.
Viongozi hao wa Ukawa, Freeman Mbowe, ambaye ni mwenyekiti wa Chadema, James Mbatia (mwenyekiti, NCCR Mageuzi) na Profesa Abdallah Safari, ambaye ni mjumbe wa Kamati Kuu ya
↧
Lowassa na Magufuli Waendelea Kuchuana Vikali
Wagombea wa CCM na Chadema wanaendelea kuchuana vikali kwenye mbio za urais baada ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kutangaza matokeo ya majimbo 113.
Hadi jana jioni kwa mujibu wa matokeo yaliyotangazwa na NEC, mgombea wa CCM, Dk John Magufuli alikuwa anaongoza kwenye majimbo mengi akifuatiwa na Edward Lowassa anayegombea kwa tiketi ya Chadema, akiungwa mkono na vyama vingine vitatu vya
↧
NEC Yajibu Malalamiko Ya Ukawa
Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji Damian Lubuva amejibu malalamiko yaliyotolewa na viongozi wa vyama vya upinzani vinavyounda Ukawa, kuhusu utofauti kati ya baadhi ya matokeo yanayotangazwa na Tume hiyo na yale yaliyokuwepo vituoni.
Akiongea hivi punde kabla ya kuanza kutangaza matokeo mengine ya majimbo 54, Jaji Lubuva amekanusha taarifa zilizotolewa jana na viongozi wa Ukawa
↧
More Pages to Explore .....