Jeshi
la polisi mkoa wa Morogoro limeanza kufanya oparesheni ya kuwatafuta
watuhumiwa waliohusika na mauaji ya watu watatu wakiwemo wakulima
wawili na mfugaji mmoja, kufuatia mapigano yaliyozuka kati ya wakulima
na wafugaji katika bonde la matembele linalounganisha kijiji cha
Mabwegere na Mbigiri wilayani kilosa mkoani Morogoro.
Mkuu wa wilaya ya Kilosa Elis Tarimo
Oparesheni ya kuwasaka wauaji Morogoro yaanza
↧
↧
Kijiji Chaunganishwa na Umeme wa Kutumia Kuni
Wakazi wa kijiji cha Uchindile wilayani Ifakara mkoani Morogoro wamepata umeme unaozalishwa kwa kutumia kuni baada ya kuzinduliwa kwa mtambo wa 10kW uliotolewa na kampuni ya kimataifa ya Camco Clean Energy.
Mtambo huo wenye thamani ya zaidi ya Sh milioni 75 ulizinduliwa na Mwakilishi wa Shirika la Misaada la Marekani (USAID), Rogness Swai katika hafla iliyohudhuriwa na wadau mbalimbali wa
↧
JKT Yawasuta Wahitimu Wanaotaka Kuandamana kudai Ajira
Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) limewataka vijana waliomaliza katika jeshi hilo, kutambua kuwa walikula kiapo cha utii wakati wa kuhitimu mafunzo, hivyo suala la kuandamana ni kinyume na kiapo chao.
Vijana hao waliotumikia Jeshi la Kujenga Taifa Operesheni za nyuma na kumaliza mkataba wa miaka miwili, wameambiwa shinikizo lao la kulazimisha ajira kwa kuandamana ni kinyume cha sheria za nchi.
↧
Baba Mzazi wa Mtoto Albino Aliyeuawa Geita Atiwa Mbaroni
Mtoto Yohana Bahati mwenye ulemavu wa ngozi (albino), aliyetekwa katika Kijiji cha Ilelema wilayani Chato katika Mkoa wa Geita, mwili wake umekutwa ukiwa umefukiwa huku umenyofolewa miguu na mikono.
Polisi imesema baba mzazi wa mtoto huyo, Bahati Misalaba na mkazi wa kitongoji cha Mapinduzi katika kijiji cha Lumasa, wilayani Chato, wamekamatwa kwa ajili ya uchunguzi zaidi.
Mwili wa
↧
Papaa Msofe Ashindwa kutokea Mahakamani
Mfanyabiashara mashuhuri, Marijan Abubakar maarufu kama Papaa Msofe (50) anayekabiliwa na kesi ya mauaji, ameshindwa kufika mahakamani kwa kuwa anaumwa.
Kesi hiyo ilitajwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu lakini Wakili wa Serikali Hellen Moshi alidai bado upelelezi haujakamilika na kwamba Papaa Msofe hakufika mahakamani, kwa kuwa wamepata taarifa kuwa anaumwa.
Hakimu Mkazi
↧
↧
Japan Yajitosa Tatizo la Kukatikakatika Umeme Dar
Tatizo la kukatika kwa umeme katika Jiji la Dar es Salaam litakwisha baada ya Serikali ya Japan kupitia Shirika lake la Maendeleo la JICA kutoa msaada wa zaidi ya Sh bilioni 66, kwa ajili ya ukarabati na ujenzi wa vituo vipya vya kupozea umeme jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), Felchesmi Mramba alisema hayo alipokuwa akizungumza na waandishi
↧
RITA Yaanza kutoa vyeti vya Kuzaliwa Kinondoni
Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA), unategemea kuanza rasmi mkakati wa kuwasajili na kuwapa vyeti vya kuzaliwa wanafunzi wa shule za msingi za Manispaa ya Kinondoni na mpango huo utatekelezwa katika takribani shule 140 zenye wanafunzi wapatao 155,944.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari na kitengo cha mawasiliano cha wakala huyo, lengo la usajili huo katika
↧
Ajali ya Basi la Kidia Yaua Watu Wawili na Kujeruhi 45
Watu wawili wamekufa papo hapo huku wengine 45 wakijeruhiwa baada ya basi la abiria lililokuwa likitokea Dar es Salaam kwenda Mwanza kugongana uso kwa uso na lori katika kijiji cha Vikonje wilayani Chamwino mkoani Dodoma.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, David Misime, alisema kuwa ajali hiyo ilitokea jana saa 7.05 mchana wakati basi la Kidia lenye namba za usajili T663 AXL kugonga lori
↧
Mwanamke Amuua Mwanamke Mwenzake kwa Kummwagia Mafuta ya taa na Kumchoma Moto baada ya Kumfumania na Mumewe
Mkazi wa kijiji cha Ibosa, kata ya Nyakato, Bukoba Vijijini, Amelia Richard (50) anatuhumiwa kumuua mwanamke mwenzake kwa kummwagia mafuta ya taa na kumchoma moto baada ya kumfumania na mumewe.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kagera, Henry Mwaibambe alitaja tukio hilo ni la Februari 15, mwaka huu saa 3 usiku katika kijiji cha Ibosa kata ya Nyakata Bukoba vijijini.
Alimtaja aliyeuawa
↧
↧
Watu Wawili Wafariki Dunia Wakiiba Mafuta Kwenye Lori Lililopinduka jijini Mbeya.....18 Wamejeruhiwa Vibaya
Takribani miaka 15 imepita tangu ilipotokea ajali katika kijiji cha Idweli wilayani Rungwe mkoa wa Mbeya, iliyosababisha vifo vya watu walioungua wakichota petroli kwenye gari lililopinduka.
Hata hivyo, tukio la namna hiyo limejirudia tena kijijini hapo na safari hii watu wawili, wamekufa na wengine 18 kujeruhiwa wakati wakichota mafuta kwenye gari lililopinduka.
Lori hilo lilikuwa
↧
Wanasiasa Wahusishwa Mauaji ya Albino Nchini.....Tangu 2006 hadi sasa Albino 76 Wameauawa Kikatili
Wanasiasa wamenyooshewa vidole, wakihusishwa na mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi baada ya matukio hayo kuhusishwa na harakati za kuelekea katika uchaguzi mkuu.
Vyama vya watu wenye ulemavu pamoja na baadhi ya wadau kutoka vyama vya siasa, vimetaka Serikali kutopuuzia dhana hiyo ya kuhusisha harakati za kisiasa na mauaji hayo.
Aidha, Chama cha Walemavu wa Ngozi Tanzania, kimesema
↧
Uteuzi wa Paul Makonda Kuwa Mkuu wa Wilaya Wapingwa Kila Kona.....Anatuhumiwa Kumpiga Warioba na Kumtusi Lowassa Hadharani
Uteuzi wa Makonda ambao umefanywa na Rais Kikwete, unaonesha kuwashitua wengi; hali ambayo imefanya watu wengi kumbeza hasa kupitia mitandao ya kijamii.
Baadhi ya wanaobeza, wanadai kwamba Makonda hana sifa ya kuongoza wilaya kubwa kama Kinondoni, ambayo ina changamoto na migogoro mingi ya ardhi.
Makonda ambaye ni Katibu wa Chipukizi na Uhamasishaji wa UVCCM, jina lake limekuwa
↧
Muimbaji wa Chamber Squad Mez B afariki dunia
Muimbaji wa kundi la Chamber Squad, Maze B, amefariki leo saa nne
asubuhi, kwa mujibu wa mtu aliyekuwa akimuuguza.
Msanii huyo aliyewahi
kufanya vyema na wimbo wake ‘Fikiria’ alikuwa amelazwa katika hospitali
ya Mwananchi mjini Dodoma.
Mez B aliyezaliwa kwa jina la Moses Bushagama alikuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa Pneumonia.
Hivi karibuni aliongea na E-News ya EATV na
↧
↧
Hospitali za Mikoa 25 Kuboreshwa
Hospitali 26 za rufaa katika mikoa 25 nchini, zitafanyiwa maboresho ili zitoe huduma bora za afya kupitia mradi wa Japan International Co-operative Agency (JICA) kwa kushirikiana na Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii.
Akizungumza katika mkutano wa tathimini ya miradi mingine ya afya iliyotekelezwa, mwakilishi wa shirika la Jica, Kuniaki Amatsu alisema mpango huo umeonesha ufanisi mkubwa
↧
EWURA Yapitisha Kanuni za Tozo Huduma ya Gesi
Bodi ya wakurugenzi ya Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma ya Nishati na Maji (EWURA) imepitisha maombi ya Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) kuhusu kanuni za tozo za huduma ya kuchakata na kusafirisha gesi asilia.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini, Mkurugenzi Mkuu EWURA, Felix Ngamlagosi alisema TPDC iliiomba Ewura kuidhinisha vipengele vya kanuni ya kurekebisha tozo za
↧
Clouds Media Group Wakanusha Kuuzwa kwa Rostam Aziz
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Clouds Media Group, Joseph Kusaga amesema kuwa habari zilizoenea mtaani kwamba kampuni hiyo imeuzwa ni za uzushi na kuwataka Watanzania wazipuuze.
Kampuni hiyo ambayo inamiliki Clouds FM, Clouds Tv na Choice FM ilidaiwa kuuzwa kwa Rostam Aziz ambaye ni mmoja wa wafanyabiashara maarufu na kada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Kusaga (pichani) alisema
↧
Serikali Kuajiri Walimu Wapya 35,000 Mwaka huu
Waziri Mkuu Mizengo Pinda, amesema Serikali imepanga kuajiri walimu zaidi ya 35,000 kwa ajili ya shule za sekondari, ili kukabiliana na tatizo la uhaba wa walimu nchini.
Alitoa kauli hiyo jana jioni wakati akizungumza na mamia ya wakazi wa kata ya Kiwere, baada ya kukagua ujenzi wa maabara na kuzindua nyumba nne za walimu kwenye Shule ya Sekondari ya Kiwere, tarafa ya Kalenga, wilayani
↧
↧
Lowassa Azidi Kushawishiwa Atangaze Nia Ya Kuwania Urais
MWENYEKITI wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilayani Kishapu mkoani Shinyanga, Shija Ntelezu, ameungana na baadhi ya wana CCM wengine kumuomba Waziri Mkuu mstaafu Edward Lowassa, ajitokeze kutangaza nia ya kugombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake juzi, Ntelezu alisema kwa niaba ya wana Kishapu wenzake anamuomba Lowassa baada ya
↧
Mkuu wa Kituo cha Polisi Ilembula Njombe Afungwa Jela Miaka 30 kwa kosa la Kumbaka Mahabusu
Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa ya Njombe,
imemhukumu aliyekuwa mkuu wa kituo cha Polisi Ilembula kifungo cha
miaka 30 jela, baada ya kukutwa na hatia ya kumbaka mtuhumiwa aliyekuwa
ndani ya mahabusu.
Hukumu hiyo ilitolewa na Hakimu Augustine Rwezile, baada ya mshtakiwa huyo James Nyambenga
kukiri kosa hilo mahakamani, ambapo mshakiwa huyo anadaiwa kumtoa
msichana huyo kwenye chumba
↧
Koti la Wassira: Kambi ya Membe Lawamani
Tukio la takribani wiki mbili zilizopita
lililofanywa na Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Steven
Wassira,(pichani) la kukosea kufunga vifungo vya koti lake katika
mkutano wa Injili wa dhehebu la Wasabato uliofanyika Februari 7, mwaka
huu, limeipa lawama kambi ya kusaka urais inayoongozwa na Waziri wa
Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernand Membe.
Wafuasi wa Waziri
↧