Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Waziri Wa Kilimo Mhe Hasunga Apiga Marufuku Biashara Ya Rumbesa Nchini

$
0
0
Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo-Karatu
Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga (Mb) jana tarehe 11 Novemba 2019 amewataka wakuu wa mikoa yote nchini kwa kushirikiana na kamati za ulinzi za mikoa na wilaya kuwakamata wafanyabiashara wote nchini wanaonunua mazao kwa wakulima kwa njia ya Rumbesa.

Ametoa agizo hilo wakati akiwa katika ziara ya kikazi linalohusisha vipimo vya ujazo wa mazao ikiwemo kupiga marufuku ujazaji wa rumbesa na mizani isiyotenda haki kwa wakulima.

Alisema kuwa Rumbesa, na mizani isiyokuwa ya haki kwa wakulima ni kosa kisheria, hivyo kamati za siasa za mikoa, wilaya, kata na matawi zinapaswa kusimamia jambo hilo na kuwataka kutoa taarifa ili wananchi wanyonge wasiendelee kunyanyasika.

Wakizungumza kwenye mkutano huo ulioongozwa na Waziri wa Kilimo pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe Mrisho Gambo, wakulima wa Kijiji cha Mang’ola wamesema kuwa mifuko inayotumika kufungashia vituguu inakuwa na ujazo mkubwa kuanzia kilo 120 hadi 180  wakati wa kuwapimia wafanyabiashara.

Aidha, wamesema kuwa gharama za uzalishaji zimekuwa juu hivyo kwa kuuza vitunguu au mazao mengine kwa rumbesa kunawatia hasara na kushindwa kurudisha gharama za uzalishaji jambo ambalo limewafanya kuiomba serikali kuingilia kati.

Katika hatua nyingine Mhe Hasunga ameiagiza Tume ya umwagiliaji nchini kufika katika eneo maalumu la kilimo cha vitunguu Mang'ola katika Wilaya ya Karatu mkoani Arusha  kubaini maeneo ya kuchimba visima vya maji ili wakulima waweze kunufaika na kilimo.“Kuna haja ya kujenga mabwawa na kuweka kingo za kuzuia maji ili kuimarisha sekta ya kilimo nchini” Alisisitiza

Amewahakikishia wakulima hao kuwa Wizara ya Kilimo kwa kushirikiana na wizara ya Maji, Wizara ya nchi Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na serikali za mitaa (TAMISEM) pamoja na Halmashauri za wilaya itaweka mkakati madhubuti wa kuwasaidia wakulima ili waweze kuzalisha mazao ya kilimo katika kipindi cha mwaka mzima tofauti na kufanya kilimo cha kutegemea msimu wa mvua ambao ni mara moja kwa mwaka.

Pia ametoa mwito kwa wadau wa sekta ya kilimo na maendeleo kujitokeza kwa ajili ya kuchimba visima na mabwawa yatakayonusuru upotevu wa maji katika wilaya ya Karatu.

Ebitoke amvamia Mlela na Mpenzi Wake kwa fujo mbele ya Waandishi wa Habari

$
0
0
Mchekeshaji Ebitoke ameuvamia mkutano wa Mwigizaji Yusuph Mlela na Waandishi wa Habari Dar es salaam na kutaka kupigana na Mlela na Mpenzi wake mpya ambae alikua ameongozana nae kwenye mkutano huo na Waandishi wa Habari ikiwa ni siku chache tu toka Mlela adaiwe kuachana na Ebitoke..

Ebitoke amesikika akisema; “Mwacheni nimwonyeshe”, huku akitukana matusi ya nguoni licha ya kudhibitwa na mabaunsa.

Kaka wa Ebitoke naye amesikika akimwambia Mlela, “Umemuharibia maisha mdogo wangu” huku waandishi wa habari na wasanii wenzake waliokuwepo wakibaki wameduwaa.

Waziri Jafo Atoa Maelekezo Mapya Uchaguzi Serikali za Mitaa

Rais Magufuli Kuzindua Kitabu cha Maisha ya Mkapa Kesho Jumanne

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumanne November 12

Waziri Mbarawa Afuta Mamlaka Za Maji 36

$
0
0
Na.Alex Sonna,Dodoma
Katibu mkuu wizara ya Maji Profesa Kilila Mkumbo,amesema serikali imefuta mamlaka za maji safi na usafi wa mazingira 36 na sasa zitahudumiwa na mamlaka za makao makuu ya mikoa 25, zilizoundwa na kuongezewa majukumu ya utoaji huduma katika maeneo yake

Hayo ameyasema jana jijini Dodoma wakati alipokuwa akitoa taarifa ya Wizara juu ya maboresho ya muundo mpya wa mamlaka za maji safi na usafi wa mazingira nchini.

Prof.Mkumbo,amesema kuwa katika kuimarisha uendesahiji wa sekta ya usambazaji maji na usafi wa mazingira mijini, Waziri wa maji Profesa Makame Mbarawa, kwa mamalaka aliyonayo kwa mujibu wa sheria ameongeza maeneo ya huduma za maji.

“Kwa mujibu wa sheria ya huduma za maji na iusafi wa mazingira Na 5, ya mwaka 2019 ameongeza maeneo ya huduma kwa baaadhi ya mamalaka za maji na usafi wa mazingira nchini aidha Waziri wa maji ameanzisha na kufuta baadhi ya mamlaka za maji na usafi wa mazingira nchini”amesema Prof.Mkumbo

Hata hivyo amesema kuwa kwenye mabadiliko hayo kutakuwa na mamlaka za maji safi na usafi wa mazingira 25, katika ngazi ya makao makuu au miji mikuu ya mikoa.

Hata hivyo ameongeza kusema kuwa mamlaka hizo zitahudumia halmashauri zilizopo katika miji mikuu,makao na makuu ya mikoa husika.

“Aidha baadhi ya mamlaka za maji safi na usafi wa mazingira katika ngazi hii zimeongezewa maeneo ya huduma na kuunganishwa na baadhi ya miji midogo katika mikoa husika au mikoa ya jirani,”amesisitiza

Prof.Mkumbo amezitaja baadhi ya mamlaka za maji na usafi wa mazingira za mikoa zilizoongezewa majukumu kuwa ni pamoja na mamlaka ya maji na usafi wa mazingira Dar es saalam (DAWASA) ambayo itahudumia hadi maeneo ya Bagamoyo, Kibaha, Kisarawe na Mkuranga.

Nyingine ni Mamlaka ya maji na usafi wa mazingira mkoa wa Dodoma (DUWASA), ambayo nayo pia itahudumia eneo lake la jiji pamoja na miji ya Kongwa, Bahi na Chamwino

Mamlaka ya maji na usafi wa mazingira Mrogoro (MORUWASA) ambayo imeongezewa miji ya Kilosa na Mikumi.

Nyingine ni Mamalaka ya maji na usafi wa mazingira ya Mwanza (MWAUWASA) ambayo itahudumia halmashauri ya jiji la Mwanaza na manispaa zake na mji wa Magu, Nansio na Ngudu

Hata hivyo amesema kuwa Vmamalaka za maji na usafi wa mazingira za miji midogo ya wilaya 40, zitasimamiwa na mamlaka ya maji vijijini (RUWASA).

Baadhi ya mamlaka za maji na usafi wa mazingira zilizofutwa kati ya 36, ni pamoja na Kibaha WSSA, Kongwa WSSA, Chamwino WSSA, Kilosa, Kyela WSSA, Mikumi WSSA, Pangani WSSA, Magugu WSSA.

Amesema kuwa lengo la Serikali kufanya hivyo ni kuongeza ufanisi na kupunguza matumizi ya fedha .

Wimbo Mpya: Rayvanny – I Love You

$
0
0
Wimbo Mpya: Rayvanny – I Love You

Mfumuko Wa Bei Wa Taifa Waongezeka Hadi Asilimia 3.6 % Kutoka Asilimia 3.4

$
0
0
Na: Mwandishi Wetu, MAELEZO -Dodoma
Mfumuko wa bei wa Taifa kwa kipimo cha mwaka unaoishia mwezi Oktoba 2019 umeongezeka hadi asilimia 3.6 kutoka asilimia 3.4 mwaka ulioishia mwezi Septemba 2019 ikiwa ni ongezeko la asilimia 0.2. 
 
Akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari kutangaza takwimu za bei, Kaimu Mkurugenzi wa Takwimu za Jamii na Sensa ya Watu, Bibi. Ruth Minja amesema kuwa ongezeko hilo limetokana na kasi ya bei za bidhaa na huduma kwa mwaka ulioishia mwezi Oktoba, 2019 imeongezeka ikilinganishwa na kasi iliyokuwepo kwa mwaka ulioishia mwezi Septemba2019. 
 
Fahirisi za Bei zimeongezeka hadi 115.84 mwezi Oktoba, 2019 kutoka 111.83 mwezi Oktoba, 209 
 
“Ongezeko hili la mfumuko wa bei limetokana na ongezeko la bei za bidhaa za Vyakula na Vinywaji Baridi  ambapo mfumuko wa bei kwa mwezi Oktoba, 2019 umeongezeka hadi asilimia 5.1 toka asilimia 4.0 mwezi Septemba, 2019.” Alisema Bibi. Ruth. 
 
Aidha amesema kuwa mfumuko wa bei kwa bidhaa na huduma zote ambazo hazijumuishi chakula na nishati kwa mwezi Oktoba, 2019 umepungua kidogo hadi asilimia 2.6 kutoka asilimia 2.6 kutoka  asilimia 2.7 Septemba, 2019 
 
Fahirisi za Bei kati ya mwezi Septemba, 2019 na mwezi Oktoba, 2019 zimepungua kwa asilimia 0.1 ambapo badiliko ni sawa na badiliko lilivyokuwa kati ya mwezi Agosti, 2019 na mwezi Septemba 2019 
 
Alizitaja baadhi ya bidhaa zilizochangia kupungua kwa fahirishi kuwa ni pamoja na mafuta ya taa kwa asilimia 2.5, dieseli kwa asilimia 2.1, petrol kwa asilimia 4.0. vifaa kwa ajili ya uchakataji wa taarifa kama kompyuta kwa asilimia 5.1 na baadhi ya huduma binafsi. 
 
Tanzania kupitia Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) ambayo ndiyo mamlaka ya kutangaza takwimu pamoja na nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki imekuwa na utaratibu wa kutangaza matokeo ya mfumuko wa bei  kila mwezi ambapo ambapo mfumuko wa bei katika nchi hizo utangazwa. 
 
Mwisho


LIVE: Uzinduzi Wa Kitabu Cha "My Life My Purpose" Cha Rais Mstaafu Mhe. Benjamini Mkapa.

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli anashiriki hafla ya uzinduzi rasmi wa kitabu cha Historia ya maisha ya Mhe. Benjamin William Mkapa Rais Mstaafu wa awamu ya tatu wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania katika Ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) Jijini Dar es salaam.Kitabu kianitwa "MY LIFE MY PURPOSE"

Nafasi 150 za Kazi Zilizotangazwa Wiki Hii....Zipo za Umoja wa Mataifa, WHO, Benki Mbalimbali za Tanzania Na Zingine

$
0
0


1. Associate Criminal Analyst At United Nations | Tanzania Jobs 

2. Finance and Administrative Assistant at Heifer International 

3. Finance Assistant at Heifer International | Tanzania Jobs 

4. Job Opportunity at WHO | Finance Assistant 

5. Associate Legal Officer at United Nations | Job Opportunities

6. Job Opportunity at Oxfam Tanzania | Country Funding & Partnerships Lead 

7. Job Opportunity at Standard Chartered | Head, Safety and Security 

8. Job Opportunity at THPS | LIS Global Super User and Networking Assistant 

9. Job Opportunity at Yara International | Customer Service Manager 

10. Job Opportunity at THPS | LIS Database Administrator and Networking Program Officer 

11. Job Opportunity at ActionAid Tanzania | Information Technology Coordinator 

12. Job Opportunity At Aga Khan | Clinical Epidemiologist, Medical College 

13. Job Opportunities at Tanga UWASA | Drivers II 

14.Job Opportunity at Tanga UWASA | Customer Service Manager 

15.Job Vacancy at Geita Gold Mining (GGML) | Superintendent UG Planning 

16.Job Opportunity at Tanzania Revenue Authority (TRA) | Assistant Lecturer 

17.Job Opportunity | Estate Officer At Mbeya University November 

18.Artisan II Jobs (Masonry-2 And Plumber-1) At Mbeya University 

19.Technician II Jobs (Civil) At Mbeya University

20
.New Job Opportunity at Institute of Adult Education (IAE) | Deputy Director (Academic, Research And Consultancy) 

21.Airport Services Duty Officer at Qatar Airways  

22.Job Opportunity at ICAP | Strategic Information (SI) Specialist, Tanzania 

23.Job Opportunity at ICAP | Project Director for Health Information Systems (HIS), Tanzania 

24.Job Opportunity at ICAP | Zonal Project Manager 

25..Job Vacancy at Kazini Kwetu Limited | Depot Accountants 
▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬   


==>>World Wide Fund for Nature

👉Deadline; November 15, 2019 

Kujua jinsi ya kutuma maombi, <<Bofya Hapa>> 
▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬   

==>>Nafasi za Kazi International Rescue Committee (IRC) Tanzania

👉Wanataka Procurement Officer – Goods & Services


Kujua jinsi ya kutuma maombi, <<Bofya Hapa>> 
▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬  
 
==>>Nafasi za Kazi Railway Children Africa (RCA)

👉Deadline; 14 November 2019

Kujua jinsi ya kutuma maombi, <<Bofya Hapa>> 
▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬  
 
==>>Nafasi za Kazi Ubalozi wa Marekani Nchini Tanzania

👉Deadline; November 19,2019

Kujua jinsi ya kutuma maombi, <<Bofya Hapa>> 
▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬   

==>>Nafasi za Kazi Oxfam Tanzania

👉Deadline; November 15,2019

Kujua jinsi ya kutuma maombi, <<Bofya Hapa>> 
▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬  

==>>Nafasi Mpya za kazi  Iringa katika shirika la Kimataifa FHI 360 Tanzania
👉Wanataka watu wa fani Mbalimbali
👉Deadline ni; November 23, 2019 

Kujua jinsi ya kutuma maombi, <<Bofya Hapa>> 
▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬ 

Kuangalia Nafasi Zingine Mpya Zilizotangazwa wiki hii <<INGIA HAPA>> 

Taarifa MUHIMU Toka Benki Kuu ya Tanzania

January Makamba Kutoa Hatima Yake Kisiasa Mwezi ujao

$
0
0
Mbunge wa Bumbuli, January Makamba amesema kwa sasa bado hana uhakika kama atagombea tena ubunge katika uchaguzi mkuu ujao mwaka 2020.

Makamba ametoa kauli hiyo kupitia ukurasa wake wa Twitter ambapo amesema atafanya uamuzi Desemba mwaka huu atakapokuwa mapumzikoni.

“Sina uhakika juu ya hili, sina hakika kama nitahitaji tena kugombea ubunge mwakani. Nitafanya maamuzi sahihi nikiwa mapumzikoni Desemba mwaka huu,” ameandika Makamba.

Makamba amewahi kuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Muungano, kabla Rais Dk. John Magufuli hajatengua uteuzi huo mapema mwaka huu!

Pia amewahi kugombea urais kupitia tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM) mwaka 2015, lakini alibwagwa kwenye kura za maoni

Faida za muungano wa Tigo na Zantel kwa watumiaji wa simu za mkononi nchini

$
0
0

Imetangazwa mapema wiki hii kuwa kampuni mbili kubwa za mawasiliano ya simu nchini Tanzania za Tigo na Zantel zimeungana.

Muungano huo wa kampuni hizi mbili unafanya ziunganishe huduma zao maeneo yote mawili ya Muungano kwa maana ya Bara na Visiwani na ni muungano ambao umekuwa ukisubiriwa kutokea. 

Mapema mwaka huu wakurugenzi wa kampuni hizo mbili waliweka bayana kusudio hilo la kuungana katika mahojiano na jarida maarufu duniani la Forbes toleo maalumu la kujenga Tanzania yenye mafanikio.

Waliweka wazi namna gani muungano huo utaleta faida kwa wateja wa kampuni hizo mbili kupitia kuboresha huduma kwa kiwango cha juu na sekta ya mawasiliano ya simu za mkononi kwa ujumla. 

Swali ni je muungano huu una faida gani hasa kwa mteja?  

Kwa ufupi, wateja wa kampuni hizi zote mbili sasa wataweza kufurahia huduma bora zaidi ambazo zitatolewa kutokana na muungano huu. Muungano huu unaleta nguvu za kampuni zote mbili pamoja na kutoa kilicho bora zaidi kote bara na visiwani, mijini na vijijini. Pia unaongeza wigo wa kufanya biashara toka pande zote mbili. Lakini ni vyema pia kufahamu faida hizi za muunganiko si tu kwa wateja wa Tigo na Zantel pekee. 

Akielezea kuhusu muungano huu, Mkurugenzi Mtendaji wa Tigo Tanzania , Simon Karikari, amesema kuwa anaamini “utatengeza sekta bora zaidi ya mawasiliano ya simu za mkononi nchini Tanzania kwa sasa na siku za usoni.” Ameongeza pia kuwa soko lenye kampuni zilizoungana kama hivi litasukuma mbele ubunifu. 

Wataalamu wa uchumi na teknolojia wameweka bayana athari hasi za kuwa na soko vipande vipande au lenye kampuni nyingi za mawasiliano ya simu za mkononi mijawapo ikiwemo kushindwa kuwekeza mitaji mikubwa yenye kukuza tija kwa mtumiaji kwa muda mrefu. 

Muungano wa Tigo na Zantel ni hatua kubwa na muhimu katika kukuza sekta ya mawasiliano ya simu za mkononi nchini Tanzania na kuleta mabadiliko chanya katika sekta hii. Sasa zimebaki kampuni tano badala ya sita kutokana na kuondoka kwa kampuni ya Smart mwezi jana. Hatua ya Tigo na Zantel sio tu muhimu kwa wateja wao bali pia uchumi wa nchi na sekta ya mawasiliano kwa ujumla.

Wadau Waliomba Bunge Kuridhia Itifaki Ya Mitandao Ya Tehama

$
0
0
Na Prisca Ulomi, WUUM
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Isack Kamwelwe amewasilisha Itifaki ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ya Mitandao ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (EAC Protocol on ICT Networks) kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu ili waweze kuipitia na kuridhia kabla ya kuiwasilisha kwenye Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Baada ya Kamwelwe kuwasilisha Itifaki hiyo mbele ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu chini ya Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Selemani Kakoso, Kamati ilipokea Itifaki hiyo na kualika wadau wa Sekta ya Mawasiliano ili waweze kufika mbele ya Kamati hiyo na kutoa maoni yao.

Kamwelwe aliwaeleza wajumbe wa Kamati hiyo kuwa madhumuni ya Itifaki hiyo ni kuendeleza uunganishaji wa miundombinu ya TEHAMA mipakani; kuwezesha matumizi ya pamoja ya miundombinu ya TEHAMA, ikiwa pamoja na masafa na namba; kuwezesha matumizi ya huduma za mitandao ya TEHAMA bila upendeleo; kuendeleza matumizi ya huduma za mitandao ya TEHAMA Serikalini na kwenye sekta binafsi ikijumuisha Serikali Mtandao, Biashara Mtandao, mfumo wa “Geospatial Information.

System (GIS)” na utangazaji; kuwianisha sera, sheria na programu za TEHAMA
zitakazowezesha kufikiwa kwa malengo ya itifaki; kutoa elimu bora na mafunzo
yanayohitajika kwa ajili ya uongozi wa kimkakati, usimamizi, utafiti na ujuzi katika eneo la mitandao ya TEHAMA ndani ya Jumuiya; kuendeleza mashirikiano baina ya sekta ya umma na binafsi; kuwezesha upatikanaji wa mawasiliano kwa wote hususan kuunganisha visiwa na nchi zisizopakana na bahari; na kuhakikisha usalama na ubora wa huduma za mawasiliano na kuwezesha matumizi salama ya mtandao.

Aliongeza kuwa kwa upande wa Tanzania, nchi yetu imejiimarisha kwa kuweka
miundombinu muhimu ya TEHAMA ambayo ni pamoja na Mkongo wa Taifa wa
Mawasiliano ambao umejengwa na kufika katika Mikoa 26 ya Tanzania Bara pamoja na Zanzibar na kufikisha kwenye maeneo tisa ya mipaka na nchi jirani ikiwemo Kenya, Rwanda, Burundi na Uganda ambapo kuna watoa huduma za mawasiliano wa nchi hizo wanaotumia Mkongo wa Taifa. Pia, nchi za Rwanda, Uganda, Zambia na Malawi zinategemea uwepo wa miundombinu ya TEHAMA ya Tanzania kuwasiliana kimataifa.

Vilevile, watoa huduma wa nchini Kenya wanatumia Mkongo wa Taifa wa Tanzania kupitisha mawasiliano yake kwenda nchi nyingine. Miundombinu mingine iliyopo ni Kituo cha Taifa cha Kuhifadhi Data, Vituo sita vya maunganisho ya watoa huduma za intaneti (Internet Exchange Point – IXPs), miundombinu ya utangazaji pamoja na Mfumo wa Kuratibu na Kusimamia Mawasiliano (Telecommunication Traffic Monitoring System-TTMS). Pia, Serikali inaendalea kukamilisha Mkakati wa Taifa wa Mtandao wa
Kasi (National Broadband Strategy).

Wakitoa maoni yao kuhusu Itifaki hiyo mbele ya wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, wadau mbali mbali wakiwemo Kampuni ya Simu ya Airtel, Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL), Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) na Kituo cha Taifa cha Kuhifadhi Data (NIDC) wameridhia Itifaki hiyo na kuomba Bunge kupitia Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu iliridhie na kupitisha Itifaki hiyo Meneja wa Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano, Adin Mgendi alisema kuwa, “Itifaki hii nimekuja wakati muafaka, Tanzania imekuwa mdau wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, imejenga miundombinu na kuwezesha nchi za jirani zisizopakana na bahari kupata
mawasiliano.

Itifaki hii itatuweka mahali pazuri na tutashirikiana vema, kwa sasa
tunaingia makubaliano baina ya nchi mbili na kupeleka mawasiliano, ila tukitofautiana hakuna pa kwenda, ila kupitia itifaki hii tutaendelea kufungua masoko EAC na nchi za SADC ambapo hadi sasa tumeunga Malawi na tunaendelea Msumbiji,”.

Naye Mkuu wa Kitengo cha Usimamizi na Utekelezaji wa TCRA, Dkt. Phillip
Filikunjombe alisema kuwa Itifaki hii ikipitishwa, nchi wanachama wa EAC tutakuwa na fursa ya kukaa pamoja na kuja na sheria zinazofanana na zinazoendana na matakwa ya nchi yetu katika kudhibiti uhalifu mtandaoni

Filikunjombe alifafanua kuwa Tanzania tumefunga mtambo wa TTMS ambapo Itifaki hii inazungumzia mifumo ya kudhibiti usalama wa mtandao kwa kuwa Tanzania sio kisiwa na uhalifu mtandao hauna mipaka, tutahakikisha nchi za wenzetu wanakuwa na mifumo yenye viwango vinavyohitajika kudhibiti usalama kwa kuwa hawana mfumo kama TTMS hivyo tutahakikisha nao wanafunga mifumo ya kudhibiti uhalifu wa mtandao na usalama.

Mwakilishi wa Airtel, Delfina Martin alisema kuwa kampuni yao imeridhia Itifaki hii na itapunguza gharama za mawasiliano kwa wateja wao wanaowasiliana kutoka nchi moja kwenda nchi nyingine kwa kuwa hadi sasa Airtel wapo nchi 16 za Afrika na wana makubaliano ya moja kwa moja ya kutumia miundombinu na huduma za mawasiliano.

Baada ya kupokea maoni ya wadau, Kakoso amesema kuwa Kamati yake imeridhia Itifaki hiyo na itawasilisha taarifa yake Bungeni na kuunga mkono Serikali kupitia Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano ili Itifaki hiyo iweze kuridhiwa kupitishwa na Bunge

Rais Magufuli Awataka Viongozi Wajenge Utaratibu wa Kuandika Vitabu

$
0
0
Rais  Magufuli amewataka viongozi wastaafu nchini kujenga utaratibu wa kuandika vitabu vinavyohusu maisha yao ili viwe chachu kwa vijana wanaotamani kuingia katika masuala ya uongozi.

Ametoakauli hiyo leo Jumanne Novemba 12, alipokuwa akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa kitabu cha historia ya maisha ya Rais Mstaafu, Benjamin Mkapa kilichopewa jina la ‘My life my purpose’ iliyofanyika Jijini Dar es salaam na kuhudhuriwa na viongozi wengine mbalimbali wakiwemo marais wastaafu, Ali Hassan Mwinyi, Jakaya Kikwete na Rais wa Zanzibar, Dk. Ali Mohamed Shein.

“Ninawahimiza viongozi wastaafu wengine kuiga mfano wa mzee Mkapa kwa kuandika vitabu ili uzoefu wao katika uongozi uwe chachu kwa vijana wetu wanaoinukia kwenye uongozi, nimefurahi kusikia kuwa mchato wa kukamilisha kitabu cha Mzee Mwinyi uko mbioni kukamilika na Mzee Kikwete pia anaendelea na uandishi wa kitabu chake.

“Uandishi wa vitabu usiishie kwa viongozi wastaafu wa nafasi za urais tu tunataka na viongozi wengine nitafurahi kusoma kitabu cha Mzee Warioba, Maalim Seif, Job Ndugai na wengine wengi kwani haya ni masuala muhimu katika historia na maendeleo yetu,” amesema Rais Magufuli.

CUF Nao Wajitoa Uchaguzi Serikali za Mitaa.....Waitaka Serikali Kutotumia Nembo Yake

$
0
0
Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF) Prof. Ibrahim Lipumba amesema Chama chake hakitoshiriki kwenye uchaguzi wa Serikali za Mitaa na hakiutambui uchaguzi huo unaotarajiwa kufanyika Mwezi huu mwishoni kwa madai ya ukiukwaji wa Haki na Sheria katika mchakato wake

Profesa Lipumba ametoa msimamo huo  leo Jumanne Novemba 12, 2019  wakati akitoa maazimio ya kikao cha baraza kuu la uongozi la CUF.

CUF kinakuwa chama cha siasa cha sita kujitoa katika uchaguzi huo baada ya Chadema, ACT-Wazalendo, NCCR-Mageuzi, UPDP na Chauma.

Katika maelezo yake Profesa Lipumba amesema  baraza hilo limetafakari kwa kina na kuona hakuna umuhimu kushiriki uchaguzi baada ya hoja zao tatu walizoziwasilisha serikalini kutofanyiwa kazi.

Profesa Lipumba amewataka asilimia nne ya wagombea wa chama hicho waliopitishwa kugombea kujitoa na kuiomba Tamisemi kutotumia nembo ya chama hicho kwenye uchaguzi huo.

Bunge lapitisha Sheria ya kuruhusu watu kujipima UKIMWI

$
0
0
Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, tayari limeipitisha rasmi sheria inayompa mamlaka, mtu kujipima mwenyewe Virusi vya Ukimwi kwa kutumia sampuli zinazotoka kwenye kinywa, pamoja na sheria inayoruhusu kijana kuanzia miaka 15, kupima Ukimwi bila ridhaa ya mzazi.

Sheria hiyo imepitishwa leo Novemba 12, 2019, na kwamba sheria hiyo itasaidia watu kujitambua hali zao mapema, hususani wanaume na kundi la vijana, ambalo kwa sasa ndilo linaloongoza kuwa na waathirika wengi wa ugonjwa huo.

Akizungumza bungeni Dodoma, Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt Faustine Ndugulile, amesema kuwa tayari Wizara imekwishajipanga juu ya upatikanaji wa vipimo hivyo na tayari imeshaanza kufanya majaribio ya mifumo hiyo ikiwa ni pamoja na kuangalia mapokea kutoka kwa wananchi.

"Vipimo hivi havitakuwa vinatumia damu, vitakuwa vinatumia sampuli ya kinywa na hii watu watapima hata kabla ya kujamiiana na watakapobaini wamepata changamoto hizo wanakuja katika vituo vya kutoa huduma za afya ili kujiridhisha,vijana wengi wameanza kuathirika na kujamiiana wakiwa na umri mdogo, sasa tunatoa fursa kwa vijana kuanzia miaka 15 kupima Ukimwi bila ridhaa ya mzazi wake" amesema Waziri Dkt Ndugulile.

Rais Magufuli Asimulia Alivyopewa SUMU Dodoma.....Ataja sababu ya kutowasifia sana wateule wake.

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, amesema kuwa hapendi kuwapongeza sana wateule wake, kwakuwa hatua hiyo ilimfanya achukiwe na viongozi wenzake alipokuwa Waziri wa Ujenzi baada ya yeye kupongezwa na Rais Mstaafu, Benjamini Mkapa alipofanya vizuri.

Rais Magufuli ametoa kauli hiyo leo Novemba 12, 2019, wakati akizungumza kwenye uzinduzi wa Kitabu cha Rais Mstaafu Benjamin Mkapa, ambapo amesema anamshukuru kiongozi huyo kwa kuwa shujaa katika uongozi wake licha ya changamoto alizozipitia.

“Nakumbuka Mzee Mkapa pale tulipofanya kazi vizuri alifurahi na baadae akatamka mimi kuwa askari wake wa mwamvuli namba moja kwa kufanya kazi nzuri ya barabara, siwezi kusahahu suala hilo maishani mwangu kwasababu licha ya dhamira yake njema liliniletea mimi matatizo nilianza kuaona dalili za baadhi ya mawaziri tena wengine wa ngazi za juu kabisa kuanza kunichukia na baada ya hapo nikanyweshwa sumu Dodoma ambayo alimanusura iondoe uhai wangu lakini kwa neema za Mwenyezi Mungu nikakiepuka kifo.

“Baada ya tukio la kunusurika kifo nilimwendea Mzee Mkapa kumuelezea dhamira yangu ya kutaka kujiuzulu nakumbuka siku hiyo aliniangalia kwa jicho la baba na mwana akinihurumia na pia kunipa ujasiri na baada ya dakika chache aliniambia nanukuu “John kafanye kazi ukimtanguliza Mungu” na baada ya hapo nikapewa ulinzi nikaendelea kuchapa kazi,” amesema Rais Magufuli.

Aidha Rais Magufuli ameongeza kuwa, "Hilo suala lilinifunza sana hata mimi sasa hivi siwasifii sana wateule wangu, kwa sababu yasije yakawakuta yaliyotaka kunikuta mimi".

Kutana na Mohamedi Buruhani Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH .....Anauwezo wakufanya Dua mbalimbali Na Kutafsiri Ndoto

$
0
0
Kutana  na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH Mohamedi Buruhani Mtabibu wa Nyota za Binadamu  Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika..

JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na  Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na Mohamed Buruani Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. 

Anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO . Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine? Muone akutatulie ..Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.

Mohamed Buruhan Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..

Anatibu kwa Kutumia  Vitabu vya QUR-AN, Anatafsiri Ndoto. ,Kusafisha nyota, Mvuto wa Mwili na Biashara, ...Miguu kufa ganzi na mengi zaidi (+255  715971688 au (+255  756914036

NB: TIBA KWA DINI ZOTE NA IMANI ZOTE...

Serikali Kuanzia Mwakani Kuanza Kupima Ardhi Nyote Nchini

$
0
0
Na Ahmed Mahmoud Arusha
SERIKALI imesema kuwa kipindi cha miaka 10 ijayo kuanzia mwakani itahakikisha eneo lote nchini linapimwa na kutengenezewa misingi ya matumizi bora ya Ardhi kwa lengo la kuondoa migogoro na kuongeza thamani ya Ardhi sanjari na kutoa hati miliki.

Aidha zoezi hilo la kupanga matumizi sahihi ya Ardhi linaenda sambamba na kuowanisha sera za watumiaji wa rasilimali  mbalimbali kama vile misitu maji madini ambazo zote zipo kwenye Ardhi hivyo kuona umuhimu wa kupanga kwa ujumla matumizi sahihi ya Ardhi.

Akizungumza kwenye mkutano wa majadiliano ya mandhari ya mazingira na matumizi sahihi ya Ardhi kwa nchi za Afrika unaoshirikisha nchi zaidi ya 20 za bara la Afrika Waziri wa Ardhi nyumba na makazi William Lukuvi alisema kuwa mkutano huo ni muhimu na umekuja wakati muafaka serikali ikiwa kwenye mchakato wa kuandaa upimaji wa Ardhi nchini.

“Tumeshafanikiwa kwenye wilaya tatu nza mkoa wa Morogoro ambazo ni Malinyi Ulanga na Kilombero kupanga kila kipende cha Ardhi na kuwezesha kutoa hati zaidi ya laki tano za kimila kwa kipndi ncha miaka minne sasa tuaenda kwenye ajenda kubwa ya kupanga kupima na kumilikisha ardhi ya Tanzania” Alisema Lukuvi

Kwa Upande wake Mkurugenzi wa Tume ya Taifa mipango ya matumizi bora Ardhi chini ya wizara ya Ardhi Dkt.Steven Nindi alisema kuwa eneo la Tanzania lina ukubwa wa takribani kilomita za mraba zipatazo  milioni moja hivyo katika mkutano huu wanaangazia namna ya kupata rasilimali fedha na rasilimali watu ili kuharakisha zoezi zima la upangaji,usimamizi na utekelezaji wa matumizi bora ya Ardhi.

Alisema lengo ni kuhakikisha Ardhi nzima hapa nchini inapimwa na kupangwa matumizi bora na endelevu kwa maendeleo endelevu ya rasilimali za misitu maji madini kuhakikisha tunakuwa na sera moja itakayosaidia kuondoa wigo na kuhimiza fursa kwa matumizi bora ya rasilimali mbali za ardhi.

Nae Mwenyekiti wa Tume ya taifa ya Mipango ya Matumizi  bora ya Ardhi ,Wakili Fidelis Mutakyamilwa  alisema katika muda wa miaka kumi Taznania itakuwa imekamilisha mpango wa matumizi bora ya Ardhi ambayo itasaidia kuondoa migogoro ya muda mrefu hapa nchini.

Amesema kuwa mkoa wa Morogoro na Arusha inaongoza kwa migogoro ya ardhi hususani Rasilimali mifugo kwa mkoa wa Arusha iliyopeleka migorogoro ya wafugaji na wakulima wakigombea malisho huku wengine wakiwa ndani ya hifadhi hivyo kuleta changamoto baina ya Tanapa NCAA na wafugaji.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images