Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Ajali Yaua Watu Watatu Arusha

$
0
0
Jeshi la Polisi mkoani Arusha linamshikilia dereva wa gari ndogo aina ya Toyota Salon yenye namba za usajili T.213, Deogratius Thomas Kiwale, aliyesababisha vifo vya watu watatu na kujeruhi wawili baada ya gari lake kuacha njia na kugonga wafanyabiashara na watembea kwa miguu.

Taarifa hiyo imetolewa Novemba 9, 2019 na Kamanda wa Polisi mkoani humo ACP Jonathan Shanna, ambapo amesema kuwa ajali hiyo imetokea usiku wa kuamkia jana  majira ya saa 1:00 usiku, katika barabara ya Arusha Moshi maeneo ya Manchester, Kata ya Sekei Halmashauri ya Jiji la Arusha.

"Chanzo cha ajali hiyo ni uzembe wa dereva kushindwa kulimudu gari lake hali iliyopelekea vifo na majeruhi, Dereva wa gari hilo amekamatwa na pindi upelelezi utakapokamilika atafikishwa mahakamani kwa hatua zaidi za kisheria" amesema ACP Shanna.

ACP Shanna ameyataja majina ya watu waliofariki na kupatwa na majeraha katika ajali hiyo kuwa ni Gudla Mashanga, mfanyabiashara na mkazi wa Sanawari, Honorina Zakaria, mfanyabiashara na mkazi wa Sanawari, Amina Hassan mkazi wa Moivo, ambapo majeruhi ni Rogath Minja, mfanyabiashara na mkazi wa Sanawari na Renatha Thadei ambaye pia ni mfanyabiashara na mkazi wa Sekei.

Kwa mujibu wa Kamanda Shanna, miili ya marehemu imehifadhiwa katika hospitali ya Mount Meru, na majeruhi pia wamelazwa katika hospitali hiyo kwa ajili ya matibabu zaidi.

Uteuzi Mpya Uliofanywa Na Rais Magufuli Mchana Huu

Scholarships for Tanzanian Students| Ufadhili wa Kusoma Nje ya Nchi (Unalipiwa Kila Kitu) | Deadline ni Mwakani 2020

$
0
0
📚 FURSA ZA UFADHILI  WA KUSOMA NJE YA NCHI

▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬

    🎓Tanzanian Scholarships


Kama wewe ni Mtanzania mwenye Ndoto ya Kusoma nje ya Nchi lakini hukuwa na uwezo, basi hii ni Nafasi yako. Kuna Nafasi Nyingi sana za Ufadhili zimetangazwa (Scholarships)


 Zote Hizo ni Full Funded( Unalipiwa kila Kitu) Japo kuna zingine utachangia kidogo 

_______________________ 

Bado hujachelewa, Deadline ni kuanzia Mwezi huu wa  kumi na moja  hadi Mwakani-2020
._______________________ 


1.Global Scholars Program- Clark University USA 

2.Hong Kong PhD Fellowship Scheme for International Students

3.Clarendon Fund Scholarships, University of Oxford, UK

4.Holland Scholarship for Non EEA International Students

5.Justus & Louise van Effen Excellence Scholarships in Netherlands

6.Oxford Pershing Square Graduate Scholarships in UK

7.Emile-Boutmy Scholarship in France for Non EU Students

8.Karen McKellin International Leader of Tomorrow Award, University of British Columbia

9.Weidenfeld-Hoffman Scholarships and Leadership Program

10.Radboud Scholarship Programme | Netherlands

11.Global Minds Doctoral Scholarships Programme at KU Leuven

12.Chalmers IPOET Scholarships for International Students

13.ETH Zurich Excellence Masters Scholarships

14.Maastricht University Holland High Potential Scholarships for International Students

15.Uppsala University Global Scholarships

16.University of Twente Scholarships (UTS)

Bofya hapo chini kujua zaidi
👇👇👇👇👇👇👇👇


http://ajirazote.com/scholarship/

Chadema waitaka serikali kutotumia jina na nembo ya chama chao kwenye Uchaguzi wa Serikali za Mitaa

$
0
0
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetaka Serikali kutotumia nembo na jina la chama hicho kwenye karatasi za kupigia kura katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa utakaofanyika Novemba 24, mwaka huu.

Naibu Katibu Mkuu (Bara), wa chama hicho, John Mnyika amesema amesema hayo leo Jumapili Novemba 10, jijini Dar es Salaam wakati akizungumza na waandishi wa habari.

Amesema sababu ya uamuzi huo ni kutokana na wao kujiengua katika kinyang’anyiro hicho hivyo wagombea wao wasiwepo katika fomu hizo za kupigia kura.

“Kesho Novemba 11, tutamuandikia barua Waziri wa Tamisemi (Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa), Suleiman Jaffo, kuacha kutumia jina nembo ya chama chetu.

“Pia tunamuomba Rais Dk. John Magufuli, kuingilia kati ukiukwaji wa sheria unaoendelea kwenye uchaguzi huo kama alivyohamasisha wakati wa uandikishaji,” amesema Mnyika.

Waziri Jafo Atengua Maamuzi Yote.......Kaagiza Wagombea Wote Waliongeliwa Uchaguzi Serikali za Mitaa Warudishwe

$
0
0
Waziri wa Nchi ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe. Selemani Jafo ametangaza kuwaruhusu wagombea wote waliochukuwa fomu na kuzirejesha kwa ajili ya kugombea nafasi mbalimbali katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa unaotarajiwa kufanyika nchini Tanzania Novemba 24, 2019 na amefuta maamuzi yote yaliyofanywa na wasimamizi wa uchaguzi Nchini kote ya kuwaengua wagombea wa vyama mbalimbali. 

Waziri Jafo ametoa uamuzi huu  leo November 10, 2019 jijini Dodoma alipokuwa akizungumza na wanahabari leo

“Natoa Muongozo Wagombea wote waliochukuwa fomu na kuzirejesha waruhusiwe kushiriki uchaguzi huo, waingie ulingoni, hakuna kutafuta sababu, labda kama sio Raia wa Tanzania, hajajiandikisha Kwenye Mtaa husika, amejiandikisha mara mbili au hajadhaminiwa na Chama chake

“Wote waliochukua na kurejesha fomu wanaingia ulingoni na ratiba za kampeni zitaanza kupokelewa, hakuna kuweka mpira kwapani, hakuna kuruka kenchi,hakuna kukimbiana wote watashiriki Uchaguzi huu wa Serikali za Mitaa, hakuna kutafuta visingizio tena

“Kwahiyo nafuta maamuzi yaliyofanywa na Wasimamizi wa Uchaguzi Nchini kote ya kuwaengua Wagombea wa Vyama mbalimbali, tunafanya hivi Kwa busara, tusijiangalie sisi kama Viongozi wa Vyama mbalimbali, tuangalie watu ambao wapo kule chini wanataka kushiriki uchaguzi huu

“CHADEMA na ACT walitangaza kujiondoa, cha ajabu mpaka jana kuna Wanachama wa Vyama hivyo bado walikuwa wanaendelea kupeleka fomu, kwa hiyo licha ya utashi wa Viongozi, kule site hali ni tofauti watu wanataka kushiriki uchaguzi ndo maana nimetoa muongozo huu wa kuwaruhusu” Amesema Waziri Jafo

Tangazo La Kuwarejesha Wagombea Wasio Na Makosa Ya Kikanuni Kwenye Uchaguzi Wa Serikali Za Mitaa 2019

$
0
0
Zoezi la Uchukuaji fomu, Urudishaji fomu, Uteuzi, Pingamizi na Rufaa lilianza tarehe 29/10/2019 na kumalizika tarehe 9/11/2019.
 
Katika zoezi hilo jumla ya wananchi 555,036 kutoka Vyama mbalimbali vya Siasa walifanikiwa kuchukua fomu za kugombea. Na jumla ya wananchi 539,993 sawa na asilimia 97.3 walifanikiwa kurejesha fomu.
 
Wagombea kutoka Chama cha Mapinduzi waliochukua fomu walikuwa 412,872 (asilimia 74), Chama cha Demokrasia na Maendeleo walikuwa 105,937 (asilimia 19), Chama cha Wananchi CUF walikuwa 24,592 (asilimia 4), ACT Wazalendo walikuwa 8,526 (asilimia 1.5), NCCR – Mageuzi walikuwa 2,244 (asilimia 0.4) na Vyama vingine vyenye usajili
wa kudumu walichukua chini ya asilimia 0.1 kwa kila chama.
 
Katika zoezi zima la kuchukua na kurejesha fomu kulikuwa na changamoto kubwa kwa wagombea wengi kufanya makosa mengi ya kikanuni yaliyopelekea wengi wao kutoteuliwa. 

Baadhi ya makosa hayo ni pamoja na kujidhamini wenyewe, kutojaza fomu namba IV, kutofautiana kwa majina, kutojaza fomu kwa ukamilifu, kuandika umri, kukosea umri (mfano amezaliwa mwaka 2019) na makosa mengine mengi mbalimbali. Hii ilitokana na baadhi ya vyama kushindwa kuwajibika ipasavyo katika kuwaelekeza wanachama wao. Kutokana na hali hiyo pingamizi na rufaa mbalimbali zipatazo 15,380 ziliwasilishwa.
 
Hadi zoezi la maamuzi ya rufaa mbalimbali lilipohitimishwa tarehe 9/11/2019, jumla ya rufaa 4,921 (32%) zilipitishwa na zilizobaki zilikosa sifa kwa sababu mbalimbali.
 
Katika mchakato huo wa kuchukua na kurudisha fomu Chama cha Mapinduzi kimefanikiwa kupita bila kupingwa katika maeneo mbalimbali kwakuwa hapakuwa na mgombea yoyote kutoka Chama cha Upinzani. Kwa upande wa Wenyeviti wa Vijiji Chama cha Mapinduzi kimepita bila kupingwa katika vijiji 6,248 kati ya vijiji 12,319 sawa na asilimia 51. 

Kwa upande wa Mitaa Chama cha Mapinduzi kimepita bila kupingwa katika Mitaa 1,169 kati ya Mitaa 4,263 sawa na asilimia 27 Kwa upande wa Vitongoji Chama cha Mapinduzi kimepita bila kupingwa katika Vitongoji 37,505 kati ya Vitongoji 64,384 sawa na asilimia 58. Kwa upande wa Wajumbe wa kundi la wanawake jumla ya wajumbe 64,085 wamepita bila kupingwa na wajumbe kundi mchanganyiko jumla ya wajumbe 75,560 wamepita bila kupingwa.
 
Kwa kuwa imeonekana wazi wananchi kutoka vyama mbalimbali wamekuwa na nia kubwa ya kugombea nafasi mbalimbali za uongozi licha ya vyama vyao kutokuweka umuhimu katika kuwaelekeza vyema wanachama wao juu ya ujazaji fomu kwa mujibu wa Kanuni. 

Mamlaka ya Uchaguzi imeona ni vyema wananchi hao kupewa nafasi ya kushiriki katika Uchaguzi kwani imejidhihirisha wazi hata baada ya vyama viwili vilivyojitoa bado wanachama wao waliendelea kuwasilisha rufaa zao ili wapewe nafasi ya kushiriki katika uchaguzi.
 
Kwa mujibu wa Kanuni za Uchaguzi wa Serikali za Mitaa Mwaka 2019 Tangazo la Serikali Na. 371 la Mwaka 2019 Kanuni ya 49, Tangazo la Serikali Na. 372 la Mwaka 2019 Kanuni ya 51, Tangazo la Serikali Na. 373 la Mwaka 2019 Kanuni ya 52, na Tangazo la Serikali Na. 374 la Mwaka 2019 Kanuni ya 52 ninatoa muongozo kwamba Wagombea wote ambao walioteuliwa na kudhaminiwa na vyama vyao na kufanikiwa kurejesha fomu zao za uteuzi kwa Msimamizi Msaidizi wa Uchaguzi katika kipindi kilichokuwa kimepangwa cha kuchukua na kurejesha fomu kilichoanza tarehe 29*/10/2019 na kumalizika tarehe 04/11/2019 kwa Tangazo hili wanapewa sifa ya kupigiwa kura na wananchi wa Kijiji, Mtaa, au Kitongoji husika kwa ajili ya Uchaguzi huu wa Serikali za Mitaa wa Mwaka 2019 isipokuwa tu kama atakuwa amekutwa na mambo yafuatayo:
 
1. Siyo Raia wa Tanzania,
2. Hajajiandikisha katika Kijiji, Mtaa, au Kitongoji husika,
3. Amejiandikisha mara mbili,
4. Amejidhamini Mwenyewe,
5. Hajadhaminiwa na chama chake cha Siasa,
6. Wamerejesha fomu watu zaidi ya mmoja kutoka chama kimoja kwa nafasi inayofanana ya Mwenyekiti wa Kijiji, Mtaa, au Kitongoji kwa Kijiji, Mtaa, au Kitongoji husika. Msimamizi Msaidizi hata wajumuisha wagombea hao katika orodha ya wanaopaswa kupigiwa kura,
7. Amejitoa kwa mujibu wa Kanuzi za Uchaguzi wa Serikali za Mitaa Tangazo la Serikali Na. 371 la Mwaka 2019 Kanuni ya 19, Tangazo la Serikali Na. 372 la Mwaka 2019 Kanuni ya 20, Tangazo la Serikali Na. 373 la Mwaka 2019 Kanuni ya 20, na Tangazo la Serikali Na. 374 la Mwaka 2019 Kanuni ya 20.
 
Msimamizi wa Uchaguzi ataanza kupokea ratiba za kampeni kutoka katika Vyama vya Siasa kuanzia leo hii tarehe 10/11/2019 hadi kesho jioni kwa ajili ya kuziunganisha.
 
Tarehe ya matukio na shughuli zingine zote zinazohusu Uchaguzi huu zitaendelea kwa mujibu wa Kanuzi za Uchaguzi wa Serikali za Mitaa wa Mwaka 2019.
 
Selemani S. Jafo (Mb.)
WAZIRI WA NCHI – TAMISEMI
10 Novemba, 2019

Vilio na huzuni vyatawala tena mgodi wa Imalanguza Geita

$
0
0
Na Issa Mtuwa “WM” - Geita
Majonzi na huzuni vimetawala kwenye mgodi wa wachimbaji wadogo wa Imalanguza wilaya ya Geita kata ya Lwamgasa katika Kijiji cha Imalanguzu, mara baada ya kuwasili Naibu Waziri wa Madini Stanslausi Nyongo mgodini hapo akiwa na viongozi wengine waandamizi wa Wizara ya Madini, uongozi wa mkoa na viongozi wa dini kwa ajili ya kwenda kusitisha shughuli za uokoaji wa wachimbaji wadogo wawili Karos Msukuma Paulo mwenyeji wa Chato na Kulwa Joseph Mahungija mwenyeji wa Busolwa Nyang’wale waliofukiwa kifusi siku ya tarehe 1/10/2019.
 
Usitishaji wa zoezi hilo umefanyika tarehe 9/11/2019 ikiwa ni siku 39 tangu wachimbaji hao wafukiwe na kifusi kutokana na uwepo wa changamoto mbalimbali zilizo jitokeza katika kipindi chote cha uokoaji. Ripoti maalam ya timu ya wataalam wa uokoji imeeleza kuwa kumekuwa na changamoto nyingi wakati wote wa ukoji zilizopelekea kuwa na ugumu wa kuwaokoa wachimbaji hao. 
 
Akiwasilisha taarifa ya wataalam wa uokoaji iliyoishauri serikali kusitisha kwa zoezi hilo la uokoaji kwa Naibu Waziri wa Madini Stanslaus Nyongo,  mkuu wa wilaya ya Geita Josephat Maganga amemwambia Naibu Waziri wa Madini kuwa miongoni mwa changamoto zilizojitokeza wakati wa uokoaji ni pamoja na uwepo wa maji chini ya mgodi, mwingiano wa magogo mbalimbali chini ya shimo la mgodi, na kutokuwa na usalama katika eneo hilo hata kwa vyombo vya uokoaji.
 
Maganga aliongeza kuwa, kulikuwa na wataalam wa makundi mbalimbali ya uokoaji na vifaa vya kutosha kutoka kwa jeshi na uokoaji, mgodi wa dhahabu wa Geita (GGM), na makampuni mengine kutoka kwenye migodi mbalimbali, lakini pamoja na juhudi zote hizo imeshindikana kupatikana kwao.
 
Taarifa hiyo iliendelea kusema kuwa  siku ya tukio hilo, kwenye shimo hilo kulikuwa na wachimbaji 5 ambapo 3 kati yao waliokolewa siku hiyo hiyo na wawili hawakuweza kupatikana hadi zoezi hilo la uokoaji linasitishwa.
 
Kwa upande wake Naibu Waziri Nyongo, akiongea kwa masikitiko na majozi kwenye hadhara hiyo, Nyongo amesema kwanza lililotokea ni bahati mbaya na kwamba serikali imesikitishwa na tukio hilo na kwamba iko pamoja wafiwa na wachimbaji wote.
 
Ameongeza kuwa, serikali inathamini sana hata uhai wa mtu mmoja kuliko dhahabu au madini yote yaliko chini na ndio maana inasisitiza wachimbaji kuchimba kwa kufuata utaratibu na sharia ili wachimbe kwa kuzingaatia usalama ili kuepukana na majanga kama hayo. 
 
Nyongo ametowa kauli ya serikali ya kuhitimisha shughuli za uokoaji na kutoa maelekezo kuhusu eneo hilo ambalo wachimbaji hao wamefukiwa na kifusi.
 
“Na sasa tunakwenda kufanya ibada ya kwenda kuwazika wenzetu, viongi wetu wa dini wako hapa watatuongoza katika ibada hiyo kwa ajili ya maombi. Natamka kuwa, shughuli zote za uchimbaji katika eneo ambalo tunaamini kuwa ndipo wezentu hawa wapo, basi eneo hilo litambuliwe rasmi kuwa ndio kabuli lao na kama kuna undelezaji wa shughuli ya uchimbaji utaendelea katika eneo lingine na kwa utaratibu mwingine.” alisema Nyongo.
 
Nyongo pia alitoa maagizo kwa afisa madini mkazi mkoa wa Geita na timu yake kusimamia usitishwaji wa shughuli za uchimbaji katika eneo hilo mpaka pale hatua za uzingatiaji usalama ziwe zimefuatwa ili kuepusha ajali nyingine.
 
Kwa upannde wake Mchungaji Nuhu Suleman alie ongoza ibada hiyo ya kuwaombea marehemu alisema, hapana budi kumshukuru mungu kwa kila jambo na kila jambo hukusudiwa na mungu. Amewakumbusha waumini wote kumuelekea mungu kwani yeye ndie mwenye upekee na ufalme na kwamba maisha ya binaadamu yana ukomo ni vyema kila mmoja akajiandaa na safari hiyo.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumatatu November 11


Mikopo Ya Elimu Ya Juu Yafikia Sh. Bilioni 162.8 .....Ni Kwa Wanafunzi 46,838 Wa Mwaka Wa Kwanza Kwa Mwaka 2019/2020

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema hadi kufikia Novemba 3, mwaka huu, Serikali imekwishatoa mikopo ya sh. bilioni 162.8 kwa wanafunzi 46,838 wa mwaka wa kwanza nchini kote.

“Kwa mwaka 2019/2020, Serikali imetenga jumla ya shilingi bilioni 450 kwa ajili ya mikopo kwa wanafunzi walengwa 128,285. Na hadi tarehe 3 Novemba, 2019 wanafunzi 46,838 wa mwaka wa kwanza kwa mwaka 2019/2020, walikuwa wamepewa mikopo inayofikia shilingi bilioni 162.8,” amesema.

Ametoa kauli hiyo jana jioni (Jumapili, Novemba 10, 2019) wakati akizungumza na maelfu ya waumini waliohudhuria Baraza la Maulid kitaifa katika viwanja vya Benki Kuu (BoT) Capripoint, jijini Mwanza.

Waziri Mkuu ambaye alikuwa mgeni rasmi kwa niaba ya Rais Dkt. John Magufuli, amesema Serikali inatambua kuwa utoaji wa huduma ya elimu ni gharama na kuwa baadhi ya wananchi hawawezi kumudu gharama hizo, hivyo ikaamua kuanzisha utaratibu wa kutoa mikopo ya elimu ya juu kupitia Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu.

“Mikopo inayotolewa na Serikali, huongozwa na Sheria ya Bodi ya Mikopo (Sura 178) inayotaja vigezo vya wahitaji na wenye udahili lakini wasio na uwezo wa kumudu gharama zote au sehemu ya gharama za mafunzo au kwenye maeneo ya kipaumbele ikiwemo yatima na wanaotoka familia zenye kipato duni.”

“Hata, hivyo Serikali inaendelea kufanyia kazi maoni na mapendekezo ya wadau mbalimbali ili kuboresha mfumo wa utoaji mikopo ya elimu ya juu. Nitumie nafasi hii kuwapongeza sana BAKWATA kwa kuweka mkakati wa kuunga mkono jitihada za Serikali katika eneo hili.”

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amewataka viongozi mbalimbali watumie maadhimisho ya mazazi ya Mtume Muhammad (S.A.W) kama chachu ya kujiuliza juu ya uongozi wao, na kwa kiasi gani uongozi wao unaacha alama kwa wale wanaowaongoza.

“Kipindi hiki tunachoadhimisha mazazi ya Mtume huyu mbora wa darja, hebu nasi kama viongozi wa waumini tujiulize na tujitathmini, je, ni kwa kiasi gani tunamuenzi kwa kufuata mwenendo mzima wa Mtume Muhammad Swalla Allahu Alayh Wasallam. Je, ni kwa kiasi gani uongozi wetu umekuwa ni wenye kuacha athari njema kwenye nyoyo na fikra za waumini?”

Amesema wataalamu, waandishi na watafiti wa masuala ya uongozi walitumia muda mwingi kumsoma Mtume Muhammad (S.A.W). “Sababu kubwa iliyowavutia kumtafiti, kumsoma na hata kumuandikia makala na vitabu mbalimbali ni mafanikio makubwa aliyoyapata katika uongozi wake. Itoshe tu kusema kwamba Mtume Muhammad Swalla Allahu Alayh Wasallam alikuwa ni mtu wa familia na kiongozi makini kabisa.”

Aliwataka watambue kwamba mtu anaweza kuteuliwa kuwa sheikh au imamu lakini hawezi kuwa kiongozi bora mpaka pale uteuzi au kuchaguliwa kwake utakapothibiti katika nyoyo na fikra za wale anaowaongoza.

“Nitoe rai kwamba wakati tunapoelekea kwenye uchaguzi wa viongozi wa BAKWATA kwa ngazi mbalimbali baadaye mwaka huu, suala la kumuogopa Allah mtukufu na kufuata mwenendo wa bwana Mtume Muhammad Swalla Allahu Alayh Wasallam uwe ndiyo mwongozo wetu wa kuwapata viongozi,” alisisitiza.

Mapema, akitoa salamu za BAKWATA Taifa, Katibu Mkuu wa BAKWATA, Ustaadh Nuhu Jabir Mruma alisema Baraza hilo limeanzisha vikundi 82 vya uzalishaji vinavyojishughulisha na kazi za bustani na shamba darasa.

Kuhusu masuala ya utoaji wa haki na sheria, Katibu Mkuu huyo alisema watu 59,824 walipatiwa msaada wa kisheria na wataalamu wasaidizi wa sheria (paralegals) 79 katika maeneo mbalimbali nchini.

Alisema Desemba mwaka huu, BAKWATA itafanya uchaguzi katika ngazi mbalimbali. “Kupitia chaguzi hizo, tunatarajia kupata viongozi wabunifu, waadilifu na wachapakazi. Ninawasihi Waislamu wenye sifa wajitokeze kugombea nafasi husika.”

Pia alitumia fursa hiyo kuwaomba Waislamu wote wajitokeze kwa wingi kushiriki uchaguzi wa viongozi wa Serikali za Mitaa utakaofanyika Novemba 24, mwaka huu ili watumie haki yao ya kuchagua viongozi wanaofaa. “Kuacha kupiga kura ni kuwapa wengine fursa wakuchagulie viongozi wanaowataka. Tuepuke kuchaguliwa viongozi tusiowataka,” alisema.

(mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU

Mke wa Waziri Mkuu: Watoto Wenye Mahitaji Maalumu Wasitengwe

$
0
0
MKE wa Waziri Mkuu Mama Mary Majaliwa ametoa wito kwa wazazi na walezi watoto wenye mahitaji maalumu  kutowaficha na kuwatelekeza na badala yake wawape nafasi ya kupata elimu kwa sababu ni haki yao ya msingi.

Mama Majaliwa ambaye pia ni Mlezi wa Umoja wa Wake wa Viongozi (New Mellenium Women Group), ametoa wito huo jana (Jumapili, Novemba 10, 2019), wakati alipokabidhi majengo ya madarasa manne na matundu ya vyoo kumi kwa Kituo cha Watoto Wenye Ulemavu cha Buhangija mkoani Shinyanga yaliyojengwa na umoja huo.

Mama Majaliwa amesema si vyema kuwatenga au kuwakatia tamaa watoto wenye ulemavu kwani wao pia ni watoto sawa na watoto wengine, hivyo wanastahili kupewa haki zote bila kubaguliwa.

Amesema hatua waliyochukuwa akinamama wa umoja huo inaunga mkono jitihada za serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Dkt. John Pombe  Magufuli za kuwapatia watoto wa kitanzanai elimu bure na katika mzingira mazuri.

Mgeni rasmi katika makabidhiano hayo, Waziri wa Elimu, Sayansi na Tekinolojia, Profesa, Joyce Ndalichako ameupongeza umoja  huo kwa shughuli mbalimbali za kijamii ikiwemo kuwajali watoto wenye mahitaji maalumu.

Profesa Ndalichako amesema katika  kipindi  cha  mwaka  2019/2020  Serikali imetenga  jumla  ya  sh 3,809,758,460.00  kwa  ajili ya  kununua  na  kusambaza  vifaa  vya  kufundishia na  kujifunzia  pamoja  na  vifaa  visaidizi  kwa  ajili  ya wanafunzi  wenye  mahitaji  maalum  (wakiwemo Albino),  katika  shule  na  vitengo  vya  elimu  maalum. 

Waziri huyo ameongeza kuwa pamoja  na  juhudi  hizo  za Serikali, bado wanafurahi wanapopata  michango  kama  huo uliotolewa leo. "Wito  wangu kwenu tusichoke  kuwasaidia  hawa  watoto  wetu.  Napenda kuwakumbusha  na  kusisitiza  kwamba  Watu  wenye Ulemavu wanahitaji  msaada  mkubwa  kutoka kwenu."

"Tuwasaidie  na  tushirikiane  kuwapatia mahitaji  yao  muhimu  ikiwa  ni  pamoja  na  elimu, huduma  za  afya  na  mazingira  mazuri  ya kuwawezesha  kuishi  bila  ya  matatizo. Serikali  kwa upande  wake itaendelea  kujitahidi kwa  uwezo kutoa  fursa  zinazojali  mahitaji  yao."

Amesema madarasa  pamoja  na  vyoo alivyokabidhiwa  leo kwa niaba ya uongozi  wa  kituo  cha Buhangija na  Kikundi  cha  New  Millenium ni  tunu kwao na  wananchi  wa  Shinyanga  na  ni  sadaka kwa watoto wa Buhangija, hivyo,  ameutaka uongozi wa  Mkoa  na  Uongozi  wa  Kituo  kwa  pamoja washirikiane  kuyatunza  vizuri  ili yaweze  kutumika kwa  muda  mrefu.

Akitoa taarifa ya ujenzi huo kwa mgeni rasmi, Katibu Tawala wa Mkoa wa Shinyanga, Albert Msovela amesema fedha zilizotumika kwa ajili ya ujenzi wa madarasa manne ni sh. 65m,884,523/= ambapo kila chumba cha darasa kimejengwa kwa wastani wa sh. 16,471,130.

Amesema ujenzi wa vyumba kumi vya vyoo  unaendelea na ukikamilika utagharimu sh.26, 271,922.44 na kwamba vyoo hivyo vitakuwa vya kisasa vikiwa na maji ndani pamoja na masinki ya kunawia ili kukidhi mahitaji ya watoto wenye ulemavu.

LIVE: Kinachoendelea Bungeni Muda Huu

$
0
0
LIVE:  Kinachoendelea Bungeni Muda Huu

Watu Wasiojulikana Wachoma Moto Ofisi Ya Mtendaji wa Kata ya Soweto katika Manispaa ya Moshi.

$
0
0
Watu wasiojulikana wamechoma moto ofisi ya Serikali ya mtendaji wa kata ya Soweto katika Manispaa ya Moshi.

Taarifa kutoka eneo la tukio zinaeleza kuwa watu hao walichoma ofisi hiyo kwa kutumia mafuta ya petroli na kusababisha baadhi ya nyaraka na samani za ofisi kuungua.

Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Dk. Anna Mghwira, alithibitisha jana kupokea taarifa za uhalifu huo, muda mfupi baada ya kuzuru eneo la Wailes, lilipo jengo hilo.

Katika taarifa yake, Mghwira ameagiza kufanyika uchunguzi wa kina ili kubaini wahusika wa tukio hilo, huku akisema ni mapema mno kulihusisha na masuala ya siasa.

Watu hao wanadaiwa kuichoma moto ofisi hiyo, Novemba 9, mwaka huu usiku.

“Ni kweli mimi na kamati yangu ya ulinzi na usalama mkoa, nilipokea taarifa hizo jana usiku kwamba kuna watu wasiojulikana wamechoma Ofisi ya Mtendaji wa Kata ya Soweto iliyoko eneo la Wailes, Manispaa ya Moshi na kuunguza nyaraka za serikali.

"Nimesha vielekeza vyombo vya ulinzi na usalama kuanza uchunguzi mara moja ili kubaini kiini cha uhalifu huo. Mpaka sasa kuna watu kadhaa wameshakamatwa na wanashikiliwa na Jeshi la Polisi kwa ajili ya mahojiano."

Kwa mujibu wa Dk. Mghwira, tukio la kuteketezwa kwa ofisi hiyo liligunduliwa na mtu mmoja aishie jirani na ofisi hiyo, ambaye anadai kusikia harufu ya petroli na ya vitu vinavyochomwa moto.

“Jirani huyo alihisi kuna taka zinachomwa ndipo akaamua kuchungulia kupitia dirishani na kuona ofisi ya mtendaji ikiwa imeshika moto, hapo hapo, ndipo alipotoka nje na kupiga kelele, kitendo ambacho kilisababisha wananchi wenzake kutoka nje na kuuzima moto huo na kisha kufanikiwa kupunguza athari zilizoanza kujitokeza,” alisema Mkuu huyo wa Mkoa.

Pia Dk. Mghwira alisema wahalifu hao baada ya kutekeleza nia hiyo ovu, waliacha katika eneo la tukio kibiriti na kipande cha msokoto wa bangi.

Alipoulizwa kama nyaraka zilizounguzwa ni zinazohusiana na masuala ya uchaguzi, Mkuu huyo wa Mkoa alisema nyaraka nyingi zilizoteketea ni za masuala ya afya.

Alizitaja baadhi ya nyaraka zilizokuwa karibu na dirisha ambalo lilianza kuteketea kwa moto kuwa zinazohusiana na zoezi la chanjo ya rubella, surua na polio, iliyofanyika hivi karibuni.

CCM Nao Kutoa Tamko Kesho Kutwa Kuhusu Uchaguzi Serikali za Mitaa

$
0
0
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Humphrey Polepole amesema chama hicho kwa sasa kinaendelea kufuatilia muenendo wa zoezi zima la uchaguzi wa Serikali za Mitaa, na kinatarajia kutoa tamko lake Novemba 13, 2019.

Polepole ametoa kauli hiyo Leo Novemba 11, 2019 kupitia ukurasa wake wa Twitter, huku zoezi zima la uchaguzi huo likiwa limekumbwa na changamoto kadhaa ikiwemo wagombea wengi wa vyama mbalimbali kuenguliwa.

Kutokana na changamoto hizo, jana Waziri wa Nchi ofisi ya Rais TAMISEMI, Mhe. Selemani Jafo alitengua maamuzi yote na kuamua kuwaruhusu wagombea wote nchini waliochukua fomu na kuzirejesha kushiriki uchaguzi wa Serikali za Mitaa bila kujali kama walienguliwa isipokuwa kwa wale wasio raia wa Tanzania, hawakujiandikisha au wamejiandikisha mara mbili.

Waziri Wa Kilimo Aagiza Viongozi Wa Chama cha Akiba na mikopo na Chama cha Ushirika wa Ayalabe Dairy Wakamatwe

$
0
0
Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo-Arusha
Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga (Mb) ameliagiza jeshi la Polisi Mkoani Arusha kwa kushirikiana na Mkuu wa Upelelezi, na Kamanda wa Taasisi ya Kuzuia na kupambana na rushwa (TAKUKURU) kuwakamata viongozi mbalimbali wa Chama cha Akiba na mikopo cha Ayalabe na na Chama cha Ushirika wa Ayalabe Dairy kutokana na ubadhilifu wa fedha za wanachama wa vyama hivyo.
 
Waziri Hasunga ametoa maagizo hayo jana tarehe 10 Novemba 2019 wakati mara baada ya kusikiliza malalamiko ya wanachama wa vyama hivyo wakati wa kikao kazi kilichofanyika katika eneo la uwanja wa vyama hivyo Wilayani Karatu ikiwa ni siku ya pili ya ziara yake ya kikazi ya siku mbili mkoani Arusha.
 
Waziri Hasunga ameagiza viongozi hao kukamatwa haraka iwezekanavyo kwani dhamira ya serikali ya awamu ya tano ya kuanzisha vyama vya ushrika ni kuwanufaisha wananchi kupitia umoja huo.
 
Viongozi hao ni Wajumbe wa Bodi ya AYALABE SACCOS ambao ni aliyekuwa Mwenyekiti Ndg Christopher Kastuli, Aliyekuwa Makamu Mwenyekiti Ndg Yuda Moratha, Waliokuwa makatibu Bi Maria Lohay na Anastazia Evodi pamoja na wajumbe Eustela Kastuli, Faustini Tekko, Ludovick Marmo, Tarsila Visent na Costantine Matle.
 
Wengine ni waliokuwa wajumbe wa Chama cha Ushirika wa Ayalabe Dairy ambao ni aliyekuwa Mwenyekiti wa chama hicho Yuda Moratha, aliyekuwa Makamu mwenyekiti Faustine Tekko, aliyekuwa katibu wa chama hicho Ndg Yasinta Faustin, na wajumbe ambao ni EufrasiaAntony, Israel Sarwat, Evarist Sulle, Florance Neston na Eustela Kastuli.
 
Waziri Hasunga ameagiza pia kukamatwa viongozi wote wa makampuni yaliyochukua hela kinyume na taratibu za ushirika, kampuni hizo ambazo ni Shimaswa na Teddy Agrovet.
 
Katika hatua nyingine ameagiza Ndg Blanka Michael akamatwe kutokana na kukodisha eneo la Chama cha Ushirika wa Ayalabe Dairy pasipo kufuata utaratibu wa kisheria.
 
Katika mkutano huo pia Mhe Hasunga ameagiza kuwekwa kizuizini viongozi na wajumbe wa kamati ya usimamizi wa Chama cha Akiba na mikopo cha Ayalabe ambao ni aliyekuwa Mwenyekiti Ndg Lazaro Titus Lazaro  na wajumbe Joseph Bayo na Eudesi Jonas.
 
Waziri Hasunga ameuagiza uongozi uliopo wa Chama cha Ushirika cha akiba na mikopo cha Ayalabe kusitisha mara moja kulipa deni la mkopo waliochukua wa shilingi 500,00,000 kutoka Benki ya TIB kwa kutumia hati za majengo ya Ayalabe Dairy mpaka serikali itakapojiridhisha kama mkopo huo ni halali.
 
Ameagiza watuhumiwa hao wote wafunguliwe kesi ya uhujumu uchumi na watakaoweza kurudisha fedha za wanachama waweze kusamehewa. Pia ameuagiza uongozi wa wilaya ya Karatu na Tume ya Maendeleo ya Ushirika kuhakikisha kuwa wanasimamia ukarabati wa kiwanda cha Ayalabe Diary na kufikia mwezi Januari 2020 kianze kufanya kazi.
 
Chama cha Ushirika wa maziwa cha Ayalabe kilipokea kiasi cha shilingi 513,407,077 kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Karatu kupitia miradi ya ASDP na DADPS tangu mwaka 2009 hadi 2013 kwa ajili ya ujenzi wa kuboresha kiwanda cha maziwa ambapo hata hivyo baada ya kufanyiwa uchunguzi na ukaguzi kilibainika kuwa na ubadhilifu wa Tshs 147,126,000 huku chama cha Ushirika wa Akiba na Mikopo (SACCOS) chenyewe kilikuwa na akiba za wanachama ambazo ni shilingi 11,015,000 na hisa zao zilikuwa Tshs 2,830,000, huku kikiwa kimechukua mkopo wa Tshs 500,000,000 kutoka Benki ya TIB.

Serikali Yatoa Kauli Mahindi Kupanda Bei

$
0
0
Serikali imesema licha ya bei ya mahindi kuwa juu, haitaingilia kupunguza bei kwani ni nafasi ya wakulima kupata bei wanayotaka.

Naibu Waziri wa Kilimo nchini Tanzania, Hussein Bashe ametangaza msimamo huo bungeni leo Jumatatu Novemba 11, 2019 wakati akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Busega (CCM), Dk Rafael Chegeni.

“Sasa hivi bei ya vyakula inazidi kupanda na ukiangalia wananchi wengi wanaadhirika na hali hii, gunia la mahindi sasa ni karibu Sh. 100,000 je serikali ina mkakati gani wa kupunguza gharama hizi kwa wananchi,” alihoji Dk. Busega.

Akijibu swali hilo Bashe amesema msimamo wa serikali ni kutokuingilia kushusha bei ya mazao kwa kuwa wakulima wameshapata hasara na hivyo watapunguza gharama za uzalishaji na kuruhusu ushindani katika soko.

“Hatutaingilia kupunguza bei ya mazao kwasababu wakulima wa nchi hii kwa muda mrefu wamepata hasara, huu ni msimamo wa serikali na ieleweke hivyo, njia ya pili tunahamsisha Watanzania kuongeza uzalishajikwani supply ikiwa kubwa demand ikiwa ndogo mazao yatashuka bei.

“Ni bunge hili hili mwaka jana wakati bei ya mahindi kwa mkulima ilikuwa sh. 150 wakasema kwanini tunafunga mipaka, sisi kama serikali hatua tunazozichukua kupunguza gharama za bei sokoni ni pamoja na kupunguza gharama za uzalishaji, kuruhusu soko kushindana, kwahiyo hatutaingilia kushusha bei, tunayo National Food Reserve Agency na niwaambie wabunge na wakuu wa mikoa pale wanapoona kuna upungufu wa mazao ya chakula sokoni wawasiliane na mawakala hao ili wasambaze chakula katika maeneo hayo,” amesema Bashe.

Serikali Yapiga Hatua Kubwa Urejeshwaji Wa Kodi Ya Ongezekola Thamani

$
0
0
Na. Peter Haule, WFM, Dodoma
Serikali imefanikiwa kuwarejeshea wafanyabiashara na wawekezaji Kodi ya Ongezeko la Thamani-VAT baada ya uhakiki wa madai yao kwa lengo la kuimarisha kipato cha mtu mmoja mmoja na uwekezaji nchini.

Hayo yamesemwa bungeni Jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji, wakati akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Viti maalum, Mhe. Khadija Nassir Ali, aliyetaka kujua namna Serikali ilivyojipanga kurejesha Kodi ya Ongezeko la Thamani kwa wawekezaji ili kuimarisha uwekezaji.

Dkt. Kijaji alisema kuwa, Serikali imelipa zaidi ya asilimia 90 ya VAT kwa watu waliokuwa wakidai Serikali baada ya kufanyika kwa uhakiki wa madai hayo, uhakiki unaendelea kwa asilimia kumi iliyobaki ili kujiridhisha kabla ya kufanya malipo.

“Tulikua na changamoto kubwa ya udanganyifu kwenye eneo la urejeshwaji wa Kodi ya Ongezeko la Thamani, hivyo Serikali ilianza mkakati wa kujiridhisha na kila muamala unaoletwa ili kuweza kuirejesha kwa wazalishaji, wanunuzi pamoja na viwanda vilivyopo nchini”, alieleza Dkt. Kijaji.

Aidha, akijibu swali la Msingi la Mbunge wa Busega, Mhe. Dkt. Raphael Chegeni, aliyetaka kujua maana ya dhana ya ukuaji wa uchumi kwa kuoanisha na Maisha ya wananchi, Dkt. Kijaji alisema kuwa dhana hiyo inatafsiriwa kwa kuangalia upatikanaji, ubora na gharama ya huduma za jamii zinazotolewa na Serikali.

Alisema baadhi ya huduma hizo ni pamoja na elimu, afya, maji, umeme na miundombinu ya usafiri na usafirishaji inayosaidia kupunguza gharama za usafirishaji wa bidhaa na na matengenezo ya vyombo vya usafiri.

Dhana nyingine ya kutafsiri ukuaji wa uchumi na maisha ya wananchi ni ushiriki wa wananchi wenyewe katika shughuli za kiuchumi hivyo ukuaji wa uchumi ni matokeo ya ushiriki wa wananchi katika uzalishaji mali na huduma.

Alisema kuwa wananchi wanaoshiriki katika shughuli za uchumi wananufaika kwa tafsiri ya dhana ya ukuaji wa uchumi kupitia huduma za kijamii zinazotolewa na Serikali pamoja na matokeo ya shughuli zinazofanywa na mwananchi.

Serikali ya Awamu ya Tano imeendelea kufanya jitihada za kuweka mazingira wezeshi ya uwekezaji na biashara ili kila mtanzania aweze kutumia kikamilifu fursa zilizopo katika uzalishaji na huduma.

Naibu Waziri Dkt. Kijaji alisema kuwa uwekezaji katika viwanda utaongeza ajira na uzalishaji katika Sekta ya kilimo kwa kuwa Sekta hiyo inaajiri idadi kubwa ya watu nchini.

Mwisho

Polisi Arusha Wafanikiwa Kukamata Bunduki Mbili Za Kivita Na Nyara Za Serikali

$
0
0
Na Ahmed Mahmoud Arusha
JESHI la polisi mkoani hapa limefanikiwa kukamata bunduki mbili za kivita pamoja na nyara za serikali ambazo ni nyama ya twiga pamoja na vipande viwili vya meno ya tembo sanjari na silaha za jadi yakiwemo mapanga,sime na visu.

Kamanda wa jeshi la polisi mkoani hapa,Jonathan Shana alizitaja silaha hizo kuwa ni AK 47 yenye namba 174364 ikiwa na risasi 6 kwenye magazine na G3 yenye namba A36011858 ikiwa na risasi 9ndani ya magazine na kwamba zilikamatwa katika eneo la Naani lililopo katika mpaka wa Tanzania na Kenya tarafa ya Loliondo Mkoani hapa.

Alisema kukamatwa kwa silaha hizo kunatokana na ushirikiano kati ya jeshi la polisi,Tanapa,Hifadhi ya Ngorongoro,kikosi dhidio ya ujangili(KDU)Kanda ya kaskazini na kikosi kazi cha taifa kinachopambana na ujangili kanda ya ziwa katika operesheni inayorndelea huko Loliondo.

“Bunduki hizo zilipatikana baada ya majibizano ya risasi baina ya kikosi kazi hicho kabambe na majangili mara baada ya kuona mashambulizi yamezidi majangili hao walitelekeza silaha hizo na kukimbilia nchi jirani,hata hivyo kikosi kikosi hicho kilifanikiwa kumjeruhi kwa risasi jangili mmoja ambaye pia alifanikiwa kukimbia huku akivuja damu”alisema Shana.

Kamanda huyo wa polisi aliongeza kuwa mnamo tarehe 10 mwezi wa 11 mwaka huu katika eneo la Oleng’usa kijiji na kata ya oloipiri ndani ya eneo la pori tengefu la Loliondo walifanikiwa kukamata watu wawili wanaojihusisha na ujangili ambao ni Yamhanga Mwita(19)na Chacha
Marwa(20) wakazi wa Serengeti Mkoani Mara wakiwa wameuwa Twiga.

Alisema kuwa watuhumiwa hao walikutwa wakiwa wanaendelea kuanika nyama hizo porini kwa ajili ya kusafirisha baada ya kuwa wamezikata vipande vipande ambapo ndio waliokutwa na panga,sime mbili,kisu tochi pamoja na nyaya za kutegea wanyama zikiwa katika mafungu saba.

Kuhusu meno ya tembo alisema kuwa tarehe 10 mwezi wa 11 mwaka huu majira ya 17:40,maeneo ya mbuyuni wilayani Arumeru waliwakamata watu watano wakiwa na meno hayo pamoja na pikipiki mbili aina za Kinglion namba T917 BUA na Sunlag namba MC 819 ACD ambapo walitokea wilayani Simanjiro mkoani Manyara walipokuwa wameyahifadhi na kwamba walikuja
Mkoani hapa kwa ajili ya kuyauza.

Kadhalika Kamanda Shana alisema kuwa polisi inawashikilia Juma Yahaya(33)na Amani Mbise(32) wanaojishughulisha na kusajili laini za simu,wakazi wa jijini hapa kwa tuhuma za kutumia jina la Gavana wa benki kuu ya Tanzania(BOT)Profesa Frorence Luoga katika mitandao ya kijamii na kuwatapeli watu mbalimbali kwa kutumia jina hilo ambapo baada ya upelelezi wamekiri kosa hilo.

“Baada ya kuwapekuwa watuhumiwa tuliwakuta na simu 6,mashine mbili ya kusajili kwa alama za vidole,laini mbalimbali,vitambulisho 9 ya wateja ambao walishawasajilia laini zao za simu na kwamba tumebabaini mtuhumiwa huyu anamiliki jumba la kifahari eneo la Sombetini jijini hapa hali ambayo aiendani na kipato chake”alisema

Aliongeza kuwa pia jeshi la polisi kwa kushirikiana na Idara ya ya ustawi wa jamii jiji la Arusha imefanya operesheni ya kuwaondoa watoto wadogo wanaofanya biashara mbalimbali ikiwemo kubebeshwa mizigo kati masoko mbalimbali ya jijini hapa ambapo waliwakamata watoto 105 ambapo kati yao 46 wana umri chini ya miaka 18 na 59 wana umri wa zaidi ya
miaka 18.

Ofisi ya Afisa Mtendaji kata ya Mlali Morogoro Yachomwa Moto

$
0
0
Watu wasiojulikana wamevamia na kuchoma moto Ofisi ya Afisa Mtendaji kata ya Mlali wilaya ya Mvomero mkoani Morogoro, na kuteketeza Nyaraka na baadhi ya samani ambapo tayari watu watatu wanashikiliwa na jeshi la Polisi wakihusishwa na tukio hilo la kiharifu akiwemo Diwani wa kata hiyo,Frenk Mwananjinje.

Taarifa zinaeleza kuwa tukio la kuvamiwa na kuchomwa moto kwa ofisi hiyo, limetokea majira ya  saa 9:00 usiku wa kuamkia Novemba 11, 2019, ambapo zimeshuhudiwa nyaraka mbalimbali zikiwa zimeteketea vibaya na baadhi ya samani ikiwemo Viti, Meza.

Mkuu wa mkoa wa Morogoro Loata ole Sanare amefika katika eneo la tukio na kuweka wazi kuwa watu waliotekeleza uharifu huo watakamatwa mara moja na kuwajibishwa kwa mujibu wa sheria.

Afisa Mtendaji wa kata hiyo ambaye pia ni msimamizi wa uchaguzi, amedai kuwa hivi karibuni alipokea vitisho kutoka kwa mmoja wa wagombea akimtuhumu kutotenda haki katika mchakato wa uchaguzi wa serikali za mitaa.

CAG Kichere atambulishwa Bungeni

$
0
0
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Charles Kichere leo Jumatatu Novemba 11, 2019 ametambulishwa rasmi bungeni jijini Dodoma, ambapo Spika Job Ndugai ameahidi kuwa, bunge litampatia ushirikiano mkubwa. 

"Nataka nimuhakikishie kuwa, Bunge litakupa ushirikiano wa kila aina na wala hatuna tatizo na ofisi ya CAG kwa hiyo tutakuwa pamoja," amesema Ndugai.

Spika amesema leo mchana atakutana na CAG na wenyeviti wa kamati pamoja ili wajadiliane pamoja na kuzungumza baadhi ya mambo.

Aliyekuwa Rais wa TFF Jamal Malinzi afungiwa na FIFA miaka 10 .....Apigwa Faini ya Bilioni 1

$
0
0
Shirikisho la Soka Ulimwenguni (FIFA) limemfungia kwa miaka kumi (10) aliyekuwa Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania, Jamal Malinzi baada ya kumkuta na hatia ya matumizi mabaya ya fedha na kughushi nyaraka.

Mbali na adhabu hiyo, Malinzi pia amepigwa faini ya CHF 500,000 za Uswisi ambazo ni zaidi ya shilingi bilioni 1.1 za Kitanzania, baada ya uchunguzi wa Kamati ya Maadili ya FIFA uliobaini kuwa Malinzi alihusika katika matumizi mabaya ya fedha za FIFA (FIFA Financial Assistance Programme (FAP) funds), fedha za CAF.

Matumizi mengine aliyohusishwa ni fedha za TFF pamoja na kughushi nyaraka za maazimio ya Kamati ya Utendaji ya TFF kati ya mwaka 2013 na 2017.

Adhabu hiyo inaanza kufanya kazi kuanzia Novemba 8, 2019 na tayari Malinzi mwenyewe ameshajulishwa.

“Kamati imemkuta na hatia ya kuvunja kanuni ya 24 inayohusu kughushi nyaraka, na kanuni ya 28 inayohusu matumizi mabaya ya fedha katika kanuni za maadili ya FIFA toleo la mwaka 2018 na hivyo inamfungia miaka kumi kujihusisha za shughuli zote za soka Kitaifa na Kimataifa”, imeeleza sehemu ya taarifa iliyotolewa leo na FIFA.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images