Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Ali Kiba: Sina Ugomvi Wowote na Diamond Platnumz, Lakini Sipo Tayari Kushiriki Tamasha Lolote Atakaloliandaa

$
0
0
Msanii wa Bongo Fleva, Ali Kiba amesema hana ugomvi na msanii mwenzie Naseeb Abdul maarufu Diamond Platnumz kama watu wanavyoongea na anafurahia mafanikio yake anayopata kupitia muziki

Kiba amewataka Watanzania wamsapoti Diamond Platnumz kwani ni msanii mzuri na anaiwakilisha nchi vizuri

Kiba amesema hayo  katika mkutano wake na waandishi wa habari uliofanyika  Novemba 8, jijini Dar es Salaam ambapo amesema hana ugomvi na Diamond isipokuwa alishamwambia hatoshiriki onesho lolote atakaloandaa

“Diamond nilishamwambia sitoweza kushiriki katika onesho lolote atakalofanya, nafurahia mafanikio anayopata, kama amepata siwezi kufanya kwasababu mimi pia nina yangu ya kuyafanikisha, hakuna ugomvi kati yetu

“Nilipomjibu nikitumia mfano wa penseli nilimaanisha kuwa aache mambo ya kitoto kwasababu nilishamjibu, mimi sio mtoto mdogo sirudii tena kujibu, mimi mwanaume na mwanaume anaongea mara moja tu

“Nafurahia sana muziki wa Diamond naomba muendelee kumsapoti kwasababu ni msanii mzuri, anafanya kazi nzuri na anawakilisha nchi yetu,” amesema Kiba.

Katika hatua nyingine, Alikiba amesema atafanya  ziara aliyoiita ‘Unforgatable’ nchini nzima akiweka kambi za kupima afya kila mkoa kwa magonjwa yasiyo ya kuambukiza.
"Kwa jinsi ambavyo mashabiki wangu wamenionesha upendo kwa miaka 17, nimeamua kuwaletea Alikiba Unforgettable Tour ambayo itakuwa na mambo mengi sana haiishii tu kuwa Concert au Tour.

"Alikiba Unforgettable Tour itakuwa na mambo makubwa matatu. 1. Ujenzi wa Ndoto kazi kwa vijana, ambapo mimi na wenzangu watakaonishika mkono tutapita mikoani kuzungumza na wanafunzi wa vyuo. Jambo namba 2 kwenye Alikiba Unforgettable Tour ni Medical Camp, hapa namshukuru Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu na jopo la madaktari, ambao watatoa mchango wa dawa kwa lengo la kutoa huduma ya afya kwa watu mbalimbali bure kabisa.", ameongeza.

Wakulima Wa Pamba Simiyu Kupata Huduma Ya Bima Ya Mazao Msimu Wa 2019/2020

$
0
0
Na Stella Kalinga, Simiyu
Shirika la Bima la Taifa (NIC)linatarajia kuanza kutoa huduma za bima ya mazao kwa wakulima wa pamba katika Wilaya ya Meatu na Maswa Mkoani Simiyu, ambapo wakulima watakuwa na uwezo wa kukata bima katika zao la pamba itakayomkinga dhidi ya majanga ukame,mvua zilizozidi kiasi , mafuriko, moto pori ,magonjwa na wadudu wasiothibitika.

Hayo yamebainishwa na Mratibu wa Bima ya mazao kutoka Shirika la Bima la Taifa (NIC),  Bw. Prosper Peter wakati akitoa mafunzo kwa  viongozi, wataalam wa Kilimo na ushirika mkoa wa Simiyu yaliyoandaliwa na NIC  yaliyofanyika Novemba 07, 2019 Mjini Bariadi kwa lengo la kujenga uelewa wa pamoja juu ya Bima ya Mazao inayotarajiwa kutolewa kwa  wakulima wa pamba mkoani Simiyu.

“Huduma ya bima ya mazao  itaanza kwanza na kumkinga mkulima dhidi ya majanga kama vile ukame , mvua zilizozidi kiasi , mafuriko, moto pori,magonjwa na wadudu wasiothibitika na itakatwa kwa pamoja kwa hiyo tutakuwa tunakinga mtaji wa mkulima aliouwekeza katika kilimo,” alisema Peter.

Aidha, Peter amesema pamoja na bima kukinga mtaji wa mkulima katika uzalishaji, NIC kwa kushirikiana na Wizara ya Kilimo itaendelea kuboresha na kuongeza wigo wa huduma za bima ya mazao kwa kuangalia mahitaji ya wakulima wa pamba kwa wakati husika  ikiwemo suala la bei.

Awali akifungua mafunzo Katibu Tawala mkoa wa Simiyu,Bw, Jumanne Sagini amesema wakulima wanakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo upatikanaji wa pembejeo, mvua iliyozidi hivyo Bima itawahakikishia kupata fidia pale wanapopata hasara inayosababishwa na changamoto hizo na kusisitiza viongozi na wataalam kutoa ushirikiano kwa NIC wanapotekeleza

Kwa upande wake mkuu wa wilaya ya Itilima, Mhe. Benson Kilangi amesema kuwa ujio wa bima ya mazao ni wa msingi hivyo ni vema NIC ikatoa bima kwa mahitaji/changamoto ambayo ni ya kipaumbele katika eneo fulani kwa kuwa changamoto za wakulima zinatofautiana, huku akitolea mfano kwa mkoa wa Simiyu kuwa ukame hauna athari sana kwenye zao la pamba.

Afisa kilimo wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi, Bibi. Suzana Sabuni amesema  kuwa ni vyema bima hiyo ijikite kwenye vipaumbele vya wakulima kutokana na mazao wanayolima ikiwa ni sambamba na kuwapata uhuru wakulima  kuchagua bima wanayoitaka

Naye afisa ushirika kutoka wilaya ya Itilima Heri Muhina ameshauri kuwa katika upande wa majanga ni vyema bima ilenge kuwasaidia katika majanga ya moto ambayo yamekuwa yakitokea kwenye baadhi ya maghala ya vyama vya ushirika (AMCOS) pindi wakulima wanapokuwa wamehifadhi pamba yao.

Akifunga kikao hicho mkuu wa wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga amesema kuwa ni vyema utekelezaji huo uanze mapema kuelekea msimu mpya wa kilimo wa mwakani 2019/ 2020 na kusisitiza wakulima wapate taarifa sahihi kwa wakati ili waweze kuifahamu vizuri kabla ya utekelezaji.

MWISHO

VIDEO Mpya ya Alikiba - Mshumaa

$
0
0
VIDEO  Mpya   ya Alikiba - Mshumaa

DC Chongolo Atekeleza Agizo La Rais Jpm La Kusimamia Kurudishwa Kwa Nyumba Ya Bibi Mwenye Miaka Zaidi Ya 80.

$
0
0
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mhe. Daniel Chongolo ametekeleza agizo la Rais Dk. John Pombe Magufuli la kusimamia kurudishwa kwa nyumba ya Bi Amina Muhenga mwenye miaka zaidi ya 80 aliyozurumiwa kwa kipindi cha miaka zaidi ya 30 iliyopita.

Rais Dk. Magufuli alitoa agizo hilo zaidi ya miezi miwili iliyopita alipokuwa kwenye ibada ya jumapili katika kanisa la mtakatifu Petro ambapo Bi Amina alimfuata na kumueleza malalamiko yake kuhusiana na nyumba yake kuchukuliwa na mtu mwingine kinyume cha taratibu na hivyo kumsababishia kukosa makazi maalumu ya kuishi.

Mhe. Chongolo alieleza kuwa baada ya Rais kutoa maagizo hayo, kwakuwa ni waisaidizi wake ,walilifanyia kazi na hivyo kufanikisha kumrudishia Bi Amina nyumba yake pamoja na hati huku utaratibu mwingine ukiendelea kufanyika.

“Baada ya kupokea malalamiko kutoka kwa Bibi, Mhe rais  kwakuwa sisi ni wasaidizi wake, alituagiza kulifanyia kazi na leo hii tumehitimisha kwa kumkabidhi hati za umiliki wa nyumba yake, na mambo mengine tunaendelea kuyakamilisha, kuanzia sasa bibi anarudi kwenye nyumba yake.” Amessema Mhe. Chongolo.

Aidha Mhe. Chongolo ameonyesha masikitiko yake ya baadhi ya wananchi wanaoishi katika Wilaya ya Kinondoni kuishi kwa ujanja ujanja na kusema kuwa kunaidadi kubwa ya watu wanaoishi kwenye mfumo huo na hivyo kutoa onyo la kuwataka kuacha mara moja tabia hiyo.

Amesema imekuwa ni jambo la kawaida kwa wananchi hao kwani kila siku ofisi yake imekuwa ikipokea malalamiko yanayohusiana na kuzurumiwa kwa nyumba zao kwakutumia kigezo cha hukumu ya Mahakama na hivyo kuacha watu wakiteseka.

Ameongeza kuwa,wakitoka Mahakamani wanakuja kuwatoa watu wenye haki, sijui niseme nini ila ukiangalia kunahali ya rushwa, ambayo imekuwa ikiwatesa sana baadhi ya wananchi, kazi yetu sisi ni kusimamia haki,nitahakikisha haki inasimamiwa na inatolewa kwa mwenye haki” amesema Mhe. Chongolo.

Kwa upande wake Bi Amina amemshukuru rais Magufuli kwa kumsaidia kupata nyumba yake, na hivyo kusema kuwa anamuombea kwa mungu aendelee kuwatumikia wanyonge.

Maswali 15 Yanayoulizwa Mara kwa Mara Kwenye Usaili ( Interviews ) na Namna ya Kuyajibu

$
0
0
Usail wa ajira (interviews) husababisha hofu na msongo wa mawazo kwa vijana wengi kabla au baada ya kutoka chumba cha usaili.

Tatizo hilo hutokana na hofu inayojenga wakati wa kujibu maswali unayoulizwa  na watu ambao wamekuzunguka wakati wa kufanyiwa usaili.

Njia moja ya kuzuia hii kutokea ni kufuatilia mfumo wa kujibu maswali.

Ifuatayo ni orodha yetu ya maswali 15 yanayoulizwa mara kwa mara kwenye interviews( Usaili) na namna ya kuyajibu;

▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬ 

1.Jitambulishe(Wewe ni Nani?)
Mara nyingi hili ni swali ambalo mtahiniwa huulizwa mara tu aingiapo kwenye chumba cha usaili. Kwa bahati mbaya watahiniwa wengi hudhani kuwa waajiri hutamani kujua majina yao. Hapana, majina yako wanayafahamu na pengine hata taarifa za ziada. Katika swali hili waajiri uhitaji kujua sifa zako zihusianazo na ajira zitakazo dhihirisha kuwa wewe ni mtu sahihi.

Mfano mtu anaweza kujibu hivi, “Jina langu ni Mti Mkavu, ni Mhitimu wa Shahada ya Masoko ya Chuo Kikuu Dodoma. Ni mtu makini, mbunifu, mchapa kazi na ninayependa watu. Pamoja na hayo ninao ujuzi usio na shaka kwenye masuala ya mawasiliano. Uwezo wangu unadhihirishwa na mrejesho ambao huwa na upata kwa kila mtu ninaye fanya naye kazi”.

Katika swali hili ni muhimu kujua kuwa halihitaji wewe kuzungumzia mambo yasiyo husiana na kazi na ajira. Kwenu mpo wa ngapi,jina la mama yako, mkoa unaotoka, kabila, kazi ya baba au mama yako havihitajiki katika taarifa unazotakiwa. 


2.Kwanini upewe ajira kwetu? | au unaweza ukaulizwa Kwa nini unahisi wewe ni mtu sahihi kwa kazi hii na siyo mwingine?

Kumbuka kuwa usaili wa kazi unahusisha ushindani hivyo swali hili linataka uoneshe utofauti ulionao. Katika kujibu swali hili zingatia mahitaji ya kazi husika kujenga hoja kwani hata kama una utofauti wa aina gani kama hautasaidia katika kufikia  malengo ya taasisi bado itakuwa ni kazi bure.

Mfano, “ Siyo kwamba mimi ni mchapakazi na mbobezi katika uhasibu pekee lakini pia ni mtu ambaye ninaweza kufanya shughuli zangu bila kusimamiwa. Mimi ni mtu wa matokeo hivyo kwa kila ambacho hufanya hulenga kutimiza malengo kwa wakati na kufikia viwango stahiki. 


"Ubora wangu unathibitishwa na tuzo kadhaa nilizowahi kupata ikiwemo mfanyakazi bora wa mwezi mara nne nilipokuwa nikifanya kazi na na Magogo Media. Hii inathibitisha kuwa mkinipa fursa hii hamtakuwa mnajaribu bali mtakuwa mnafanya maamuzi sahihi”.

3.Unajua nini kuhusu sisi?
Siku zote maandalizi ya usaili yanaenda sambamba na kutafuta taarifa sahihi za taasisi husika. Hivyo ni vyema kuhakikisha kuwa taarifa unazotoa hapa ni sahihi na muhimu katika kudhirisha kuwa ulishafanya utafiti wa kutosha kuhusu taasisi husika.

Mfano, “ Benki yenu ilianzishwa mwaka 1987 ina maono ya kuwa benki bora kuliko zote nchini kwa kutoa huduma za kifedha zinazo aminika na kufikia maeneo mengi nchini. Kwa sasa benki yenu ina matawi 700 na ATMs 500 huku ikiwa na mpango wa kufungua matawi mengine Kigoma hivi karibuni. 


Endapo mtanipa fursa ya kufanya kazi na nyinyi nitahakikisha natumia vyema uwezo wangu katika masuala ya masoko ili kuongeza wateja na kuhaikisha huduma bora mnayotoa inafahamika kwa watu wengi.”

4. Ni vitu gani unavyojivunia?
Katika swali hili waajiri huhitaji kujua mambo kadhaa ambayo unayaona kama mtaji mkubwa katika utendaji kazi. Ni vyema kukumbuka kuwa mambo utakayo yataja hapa ni yale yenye umuhimu katika kuongeza ufanisi au ubora katika kazi husika kwani kila kazi inamahitaji yake ya tofauti na kazi nyingine.

Kwa mfano, “mambo makuu mawili ninayojivunia ni ujuzi na uwezo katika huduma kwa wateja na kujisimamia katika majukumu yangu. Kila ninapowahudumia wateja huwa napokea mrejesho chanya juu ya namna wanavyoridhishwa na huduma yangu hivyo kutamani kuhudumiwa nami tena.


Hii hunifanya nijione kuwa mtu muhimu sana katika taasisi yoyote ninayofanya nayo kazi. Pia, uwezo wangu katika kufanya shughuli bila kusimamiwa au chini ya usimamizi mdogo unanifanya niwe mtu wa kuaminiwa na kutegemewa katika kufanya shughuli zangu.Haya ni baadhi ya mambo mengi yanayonifanya mimi kuwa mtu wa tofauti. Nina amini hamtaacha fursa ya kufanya kazi nami”
 

5.Udhaifu wako ni upi?
Hili ni moja ya maswali ambayo watainiwa wengi huyachukia na kuyaona kama yana lengo la kuwatafutia sababu za kuwanyima kazi. Wengine kwa lengo la kuonesha ukamilifu huthubu kusema kuwa hawana udhaifu wowote-usithubutu kusema hivyo. Kila mtu ana udhaifu wake kwani hakuna aliye mkamilifu.

Suala la msingi ni kujua namna ya kujibu suali hili. Mambo ya kuzingatia ni pamoja na kuchagua udhaifu ambao hauta athiri utendaji wako na pili hakikisha udhaifu huo unahusiana na ujuzi na sio tabia. 


Ujuzi ni rahisi kuutafuata lakini kubadilisha tabia ni ngumu zaidi hivyo usiseme kuwa wewe ni mvivu,mdokozi, na mengineyo ya kitabia. Na unapotaja udhaifu wowote kumbuka kuonesha jitihada ambazo umeshazifanya ili kudhibiti udhaifu huo.

Kwa mfano, kwa kazi ya uhasibu mtu anaweza sema, “Udhaifu nilio nao ni masuala ya ‘graphic designing’ niligundua hili nilipohitaji kuandaa tangazo kwa ajili ya ofisi niliyokuwa nikifanya nayo kazi. Hata hivyo, nimeanza kujifunza mwenyewe kupitia mtandao wa internet na naona napata mabadiliko chanya kila leo”.

Kwa jibu hili ni dhahiri kabisa graphic designing siyo mahitaji muhimu ya kazi ya uhasibu hivyo haita athiti utendaji wa kazi.


6. Kwa nini uliacha kazi yako ya mwanzo?
Hapa unahitajikua makini sana, kumbuka na epuka kuzungumza vibaya kuhusu muajiri yeyote kabla au sasa au uwezo wa muajiri. 


Hapa unaweza ukawajibu tu kwamba;" Kwa sababu ya kuboresha na kuongeza ujuzi, pia natafuta fursa bora zaidi."

7.Unatarajia kupata nini kutokana na kufanya kazi hapa? au unaweza ukaulizwa | Baada ya miaka mitatu wewe mwenyewe utakua wapi?
Ongelea unachotumaini kutimiza ila kuwa mkweli. Pia usiongee kwa ujumla. Chagua kitu maalum ambalo ni muhimu kwa kampuni alafu ilenge. Ila, uwe wazi kwa kusema itachukua muda kujifunza zaidi kuhusu kampuni ili kufanikiwa zaidi.

Kwa mfano; “Nikiwa mwalimu wa kiingereza, lengo langu ni kuongeza asilimia ya wanafunzi wanaofaulu mtihani wa taifa kuwa 85% ya darasa yangu. Najua itachukua muda kujua vizuri changamoto za wanafunzi ila, naamini nitafanikiwa”


Ni vizuri kusema kwamba unatumaini kuona uwajibikaji zaidi  katika kampuni hiyo na kuongeza thamani katika kampuni kwa mchango wako. 

8.Kwanini umekaa muda mrefu bila kupata ajira?

Wajibu kwamba; "Nilikuwa najiendeleza katika taaluma yangu "


9. Eleza namna unavyoweza kujisimamia mwenyewe
Wajibu kwamba: Nitakuwa nafanya kazi niliyopewa nikishirkiana na wasimamizi wangu na viongozi juu ya namna ya kumaliza kazi kabla ya muda uliopangwa.


10. Kitu gani kinakukera miongoni mwa wafanyakazi wenzako?

Wajibu kwamba; "Naamini katika kufanya kazi kwa pamoja. Hata kama nikikerwa na kitu chochote, huwa najaribu kuepuka isipokuwa kama ni kitu cha binafsi."

11.Unategemea kufanya kazi kwa muda gani kama ukipewa ajira?

Wajibu:Kwa muda mrefu kama nitaendelea kuongeza kitu katika taaluma yangu.

12:Je, mwenyewe unajiona kufanikiwa?

Wajibu: Ndio, ukiachana na uwezo wa taaluma yangu, nadhani nimepata watu sahihi wa kufanya nao kazi.

13. Uwezo wako ni upi katika kazi?
Wajibu: Mimi huwa naelewa na kufundishika kwa haraka na ni mchapakazi wa kweli.

14,Unapenda nafasi au cheo gani katika timu unayofanya nayo kazi?
Wajibu: Haijalishi hadi nitakapojifunza kitu kipya kwa kila mradi au kazi.

15.Je, unaswali lolote kwetu? 

Mwishoni wa interview, ni kawaida kwa mwajiri kuuliza kama una maswali kwao. Ukipewa nafasi hii, usiulizie mshaara na faida zingine. Badala yake, uliza:
  1.     Maadili ya kampuni
  2.     Aina ya uongozi
  3.     Wafanyakazi wenzako
  4.     Chochote ambacho hukuelewa kuhusu kazi hiyo.
  5.     Watakupa jibu baada ya muda gani?
==>>USIFANYE HAYA MAKOSA KATIKA SWALI HILO:
- Je, kuna fursa ya kukua / kupandishwa ngazi?
- Nitapata siku ngapi za likizo?

- waajiliwa wanafaidika vipi na kampuni hii. 

==>Tiba bora ya msongo wa interview ni kujiandaa
Ingawa interview inaweza ikakupa misongo mingi, ukijiandaa vizuri Utashangazwa na mafanikio yako.

Interview ni nafasi yako ya mwisho kumvutia mwajiri, na vidokezo vilivyoelezwa hapo juu vitakusaidia na hilo.

Kumbuka, hamna haja ya kuwa na wasiwasi ukiwa umejiandaa. 


Nakutakia Mafanikio mema kwenye Interview
▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬

👉Sasa, kwa kuwa umeshajua jinsi ya kujibu vizuri maswali ya Interview, anza kutafuta kazi unayoitaka kwa kubofya hapo chini. 


Hilo ni Jukwaa Maalumu la Ajira zote za Serikali, Makampuni Binafsi n.k. Kuna Nafasi za Kazi zaidi ya 7000 kwa ajili yako.

👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇
http://ajirazote.com/jobs


▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬

Serikali Yaanza Msako Mifuko Mbadala Isiyokidhi Viwango

$
0
0
Serikali imeanza msako wa kuwabaini waingizaji na wazalishaji wa mifuko mbadala aina ya 'non woven' isiyokidhi viwango vilivyowekwa na Shirika la Viwango Tanzania (TBS) vya chini ya GSM 70.

Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Balozi Joseph Sokoine  amesema hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma ambapo alisisitiza kuwa mifuko inayotakiwa lazima iwe na jina la mzalishaji, uzito na mawasiliano ya mzalishaji.

Sokoine alisema kuwa kumezuka wimbi la mifuko isiyokidhi viwango vilivyowekwa  hivyo matokeo yake wale ambao wameitikia wito wa kufungua viwanda vya mifuko mbadala wanakosa soko.

"Elimu kwa umma itaendelea kutolewa ili watu wajue mifuko ipi hairuhusiwi kutumika na hii itasaidia wazalishaji wa mifuko inayokidhi viwango kupata masoko na kuweza kuisambaza hadi kule kwenye changomoto na bei itakuwa ya kawaida ili kila mtu aweze kununua," alisema.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) Dkt. Samuel Gwamaka alisema kuwa zoezi la katazo la mifuko ya plastiki kupitia Kikosi kazi cha Taifa limefanikiwa kwa kiwango kikubwa.

Dkt. Gwamaka alisema kuwa kuanza sasa vifungashio vya plastiki vya katoni za maji havitaruhusiwa na kuwa badala yake yatumike maboksi kwani yanaweza kurejelezwa hivyo ni rafiki wa mazingir huku akiongeza kuwa magazeti hayaruhusiwi kufungashia bidhaa zikiwemo vyakula kama nyama kwani ni hatari kwa afya zikiwemo magonjwa ya kansa 

Alisema kwa sasa mifuko hiyo imeondolewa lakini bado kuna changamoto ya vifungashio kugeuzwa vibebeo huku akionya viwanda vya vinavyojihusisha na uzalishaji wake.

"TBS imeshatoa kanuni za namna gani mifuko mbadala inayozalishwa lakini bado tunaona mifuko hii inazalishwa kwa wingi na tunajua bayana lazima mifuko hii iwe na GSM 70 ili kuwalinda lakini wale tunaowalinda wanazalisha usiku wanapeleleka sokoni sasa Serikali haijalala tumeanza msako wa kuwabaini na tutawachukulia hatua," alionya.

Aidha Mkurugenzi huyo alisema kuwa tayari kikosi kazi hicho kimekamata kiwanda kinachozalisha mifuko hiyo kilichopo jijini Dar es Salaam na kupiga faini huku akitoa rai kwa wananchi kutoa taarifa pindi wanapoona viwanda kama hivyo na kuwa itatolewa zawadi kwao.

Mabadiliko Sekta Ya Madini Yalilenga Kuweka Umiliki Kwa Watanzania-dkt. Kalemani

$
0
0
Asteria Muhozya na Tito Mselem, Dodoma
Imeelezwa kuwa Mabadiliko Makubwa yaliyofanywa na Serikali katika Sheria ya Madini ya Mwaka 2010 na Marekebisho yake ya Mwaka 2017, yalilenga kuhakikisha rasilimali madini inabaki mikononi mwa Watanzania  chini ya Usimamizi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano  wa Tanzania.

Waziri wa Nishati Dkt. Medard Kalemani kwa niaba ya Waziri wa Madini ameieleza hayo Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo katika Semina iliyolenga kuongeza uelewa  kwa Kamati hiyo kuhusu Kanuni mbalimbali zilizoundwa zinazohusu Sekta ya Madini na kuwasilishwa na Wataalam wa Sheria wa Wizara ya Madini wakiongozwa na Mkurugenzi wa Huduma za Sheria , Edwin Igenge.
 
Kanuni zilizowasilishwa kwa kamati hiyo ni pamoja na Kanuni za Madini (Udhibiti wa Eneo la Mirerani),  Kanuni  zinazohusu  Biashara ya Almasi, Kanuni za Masoko ya Madini pamoja na  Marekebisho ya Sheria ya Madini.
 
" Mhe. Mwenyekiti kuna zaidi ya Kanuni 13 zilizoundwa amabazo zote zimelenga katika kurahisisha usimamizi wa Sekta ya Madini na kuwanufaisha Watanzania," amesema Dkt. Kalemani.
 
Aidha, ameongeza kuwa, masuala mengine ni pamoja na namna ambavyo watanzania wanashiriki katika umiliki wa asilimia 16  hadi 50  kwenye uwekezaji mkubwa katika sekta ya madini  na kueleza kuwa, awali suala hilo halikuwepo.
 
"Mhe. Mwenyekiti hii ndiyo sababu tuko hapa pamoja na Kamati yako ambayo inahusika moja kwa moja na masuala haya, ni masuala muhimu ambayo kamati yako inapaswa kuyajua," amesisitiza Dkt. Kalemani.
 
Ameongeza  suala ni usimamizi  wa sekta ya Madini kuwekwa chini ya Tume ya  Madini pamoja na  Serikali  kupitia Benki Kuu ya Tanzania kuwa  na akiba ya madini ya Dhahabu na kusema, "Mhe. Mwenyekiti suala hili lilikuwepo awali lakini sasa tumelirejesha tena''. 
 
Aidha, Waziri Kalemani amesema mabadiliko hayo yaliyofanywa katika sekta ya madini yamepelekea kupunguza nguvu ya wachimbaji wakubwa na kutoa nafasi kwa watanzania wengi kunufaika na rasilimali madini ikiwemo kuweka biashara ya madini wazi na uanzishwaji wa masoko ya madini ambayo yameleta manufaa kwa sekta.
 
katika hatua nyingine, Waziri Kalemani amesema kufuatia serikali kuweka mazingira mazuri  hususani kwa wachimbaji wadogo wa madini, serikali kupitia  Wizara ya Nishati imewezesha kufikisha nishati ya umeme kwenye migodi 32 ya wachimbaji wadogo wa madini suala ambalo linawawezesha kuchimba kwa faida na kuachana na matumizi ya mafuta. 
 
Naye, Makamu Mwenyekiti wa  Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo William Ngeleja, akizungumza  katika semina hiyo ameipongeza Serikali hususan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Magufuli kwa Maamuzi makubwa aliyoyafanya  katika Sekta ya Madini ambayo yalipelekea kufanyika kwa   Mabadiliko ya Sheria ya Madini ya Mwaka 2010 na Marekebisho yake ya Mwaka 2017 na kueleza kuwa, manufaa yake yanaonekana.
 
Pia, ameipongeza Serikali kwa uazishwaji wa Masoko ya Madini  pamoja na Ujenzi wa Ukuta unaozunguka Migodi ya Tanzanite Mirerani na kueleza kuwa, ukuta huo umeongeza tija kwa taifa kutokana na mapato yanayopatikana  baada ya udhibiti wa utoroshaji wa madini hayo  yanayopatikana Tanzania pekee ikiwemo usimamizi wa rasilimali hiyo.
 
" Mhe. Mwenyekiti kuna zaidi ya kanuni 13 zilizoundwa amabazo zote zimelenga ktika urahisisha usimamizi wa Sekta ya Madini na kuwanufaisha Watanzania, "
 
Vilevile, amesema semina hiyo imewaongezea weledi wajumbe wa kamati hiyo kuhusu mabadiliko ya  Sheria ya madini. Aidha, amempongeza Waziri Biteko kutokana na ushirikiano na usimamizi mzuri wa   rasilimali madini unaofanywa  na kusema  "Watendaji tembeeni vifua mbele mnaye kiongozi anayewawakilisha vizuri," amesema Ngeleja.
 
Pia, amechukua fursa hiyo kuipongeza Wizara ya Nishati  kwa usimamizi mzuri wa sekta ya Nishati na kusema kwamba,"Wewe Waziri Kalemani na mwenzio wa Madini mnamwakilisha vizuri Rais wetu sisi sote tunaona".
 
Aidha, kamati hiyo imeishauri Wizara  kuhusu masuala kadhaa yanayohusu sekta ya madini yakilenga katika kusimamia na kuboresha sekta  husika ili kuhakikisha kwamba rasilimali madini inawanufaisha  zaidi watanzania, ambapo Waziri Kalemani ameahidi kuufanyia kazi ushauri uliotolewa na kamat hiyo. Pia, kamati imeitaka wizara kuendelea kutoa elimu kwa wachimbaji wadogo  madini kuhusu masuala yanayohusu kodi pamoja na mambo mengine ya muhimu.
 
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Tume ya Madini Prof. Idris Kikula akijibu hoja zilizowasilishwa na Kamati hiyo, ameeleza kwamba, zipo tofauti  za kabla na baada ya kujengwa kwa Ukuta unaozunguka migodi ya Tanzanite Mirerani  na kueleza kwamba, mapato yameongezeka tofauti na ilivyokuwa awali. 
 
"Lakini Mhe. Mwenyekiti  sisi na wizara tunafanya kazi kama Timu, tunaendelea na  majukumu yetu ya usimamizi wa sekta ya madini lakini pia tayari serikali imetoa magari 36 , tumeongeza  watumishi  wapya 180  bado tunaendelea na kufanyia kazi lengo la kukusanya shilingi bilioni 470 kwa Mwaka wa Fedha 2019/20," amesema  Prof Kikula.
 
Kuhusu udanganyifu unaofanywa na baadhi ya vituo vya uchenjuaji dhahabu, amesema  Tume ya madini ilikwisha baini udanganyifu huo na suala hilo linadhibitiwa.
 
Wataalam wengine waliowasilisha Mada katika semina hiyo kutoka wizara ya madini ni pamoja na Maafisa Sheria Waandamizi Semeni Kakunda, Julieth Moshi pamoja na Afisa Sheria Godfrey Nyamsenda.
 
Wengine waliohudhuria semina hiyo ni  Wataalamu kutoka Wizara ya Madini na Tume ya Madini.

Waziri Wa Mifugo Na Uvuvi Mhe. Luhaga Mpina Atengua Uteuzi Wa Kaimu Meneja Mkuu NARCO


Waziri Lukuvi Awataka Wafugaji Kuweka Uzio Ili Kuepusha Migogoro Na Wakulima

$
0
0
Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi ameagiza wafugaji wote wanaomiliki maeneo yenye hati kuweka uzio katika maeneo yao ili kuepuka mifugo yao kwenda maeneo ya wakulima na kusisitiza kufanyika ufugaji wa kisasa.

Lukuvi alitoa agizo hilo wilayani Kilosa mkoani Morogoro wakati akizungumza na uongozi wa wilaya ya Kilosa na watendaji wa sekta ya ardhi katika wilaya hiyo akiwa katika muendelezo wa ziara ya kutatua migogoro ya ardhi katika mkoa wa Morogoro.

Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi akizungumza na uongozi wa wilaya ya Kilosa pamoja na Watendaji wa sekta ya ardhi katika wilaya ya Kilosa mkoani Morogoro wakati wa muendelezo wa ziara yake ya kutatua migogoro ya ardhi mkoani Morogoro.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Adam Mgoyi ameomba kufanyika ukaguzi wa ardhi za vijiji kwa kuwa baadhi yake watu wamejimilikisha, wameuza na mengine kufanyika mgawanyo usio sahihi.

Katika hatua nyingine Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi amesema vijijji viwili vilivyosajiliwa katika maeneo ya hifadhi wilayani Kilosa mkoa wa Morogoro vitaendelea kubaki katika maeneo hayo kufuatia Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuridhia vijiji 920 vilivyokuwa katika maeneo ya hifadhi kuendelea kubaki maeneo hayo.

Lukuvi amevitaja vijiji vya Mjambaa kilichoko katika shamba la Mbugani Estates lenye ukubwa wa ekari 1600 na kile cha Mambegwa kuwa vitaendelea kutambuliwa na kuagiza  halmashauri ya wilaya ya Kilosa kwenda kuvipima na kuanisha shughuli za kilimo na makazi katika vijiji hivyo

CAG Kichere akabidhi ofisi ya RAS Njombe

$
0
0
Na Amiri Kilagalila-Njombe
Mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali CAG Charles Kichere ameagiza watumishi wa serikali nchini kutumia pesa za serikali kwa maendeleo ya wananchi ili kukuza uchumi wa nchi na ustawi wa watu wake.

Kichere amesema serikali imekuwa ikitoa pesa nyingi kwa ajili ya miradi ya mingi ikiwemo ya maji,umeme na bara bara lakini miradi imekuwa ikishindwa kukamilika huku pesa imetolewa.

CAG Kichere ametoa maagizo hayo mkoani Njombe wakati akikabidhi ofisi kwa katibu tawala mpya wa mkoa huo Catarina Revocat huku akitolea mfano mkoa wa Njombe unaozungukwa na mito lakini bado kumekuwa na changamoto kubwa ya maji.

“Baada ya kufika huku Njombe nimejifunza mengi sana ukiwa serikali kuu huwezi kujua nini huku kinaendelea,lakini huku ndio maendeleo inatakiwa yatoke,serikali kuu imewekeza kwenye miradi mikubwa lakini huku kuna miradi midogo ya maji,umeme,barabara,afya pesa zinakuja,tuzitumie vizuri za pesa serikali zinazokuja ili tuwaletee wananchi maendeleo,nimeshuhudia pesa zinakuja lakini miradi haikamilika”anasema Charles Kichere

Aidha ameahidi kuelekeza ofisi ya mkaguzi ya taifa kuhakikisha wanafuatilia miradi yote ya maji iliyopo mkoani Njombe kuhakikisha imefanyika kikamilifu.

“Ni jambo la kusikitisha kidogo mkoa wa Njombe ambao umezungukwa na mito na mabonde mbali mbali kuna shida ya maji tatizo ni nini hasa,nitaelekeza wenzangu katika ofisi ya mkaguzi ya taifa wahakikishe wanafuatilia miradi yote ya maji mkoa wa Njombe tuhakikishe inafanyika vizuri na inawaletea manufaa wananchi wetu na tuhakikishe tunapata value for money”anasema tena Kichere

Bi.Katarina Tengia Revocati ni katibu tawala mpya wa mkoa wa Njombe mara baada ya kupokea ofisi hiyo ameahidi kufanya kazi kikamilifu kutokana na maelekezo ili kuyafikia mageuzi ya kiuchumi wananchi wa mkoa wa Njombe.

“Twende na mtazamo unaohakikisha mwananchi wa kawaida anaweza kufaidi yale mageuzi makubwa ya kiuchumi ambayo mh.Rais pamoja na uongozi mzima wa kitaifa wanayafanya”anasema Katarina

Nestory Karia ni mkaguzi wa hesabu za serikali kanda ya kusini,amesema ofisi ya mkaguzi itaendelea kushirikiana na ofisi ya katibu tawala katika kazi ili kuhakikisha hakuna halmshauri ya mkoa huo itakayoweza kupata hati chafu. Mkuu wa mko wa Njombe Christopher Ole Sendeka,amesema serikali imeendelea kutoa fedha nyingi kwa ajili ya miradi ya maendeleo katika mkoa wa Njombe hivyo kazi yao ni kuhakikisha wanasimamia miradi hiyo.

“Tuna miradi mikubwa huku inayoendelea ukiacha hiyo ya bara bara,tuna soko la kisasa jampo kuna changamoto zake,tuna ujenzi wa hospitali ya rufaa ya mkoa ambayo inajengwa kwa jumla ya bilioni saba,tunapata fedha kwa ajili ya miradi inayowagusa wananchi, kazi yetu ni kuendelea kuhakikisha tunapata value for money”anasema Ole Sendeka

Novemba 3,2019 Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Dkt.John Pombe Magufuli alifanya uteuzi wa viongozi mbali mbali akiwemo Bw.Charles Edward Kichere  kuwa mdhibiti na mkaguzi wa hesabu za serikali  akichukuwa nafasi ya Prof.Mussa Juma Assad amabye kipindi chake cha miaka  5 kilikwisha tarehe 04 Novemba 2019.

Kabla ya uteuzi Bw.Kichere alikuwa katibu tawala wa mkoa wa Njombe huku nafasi hiyo kwa sasa ikichukuliwa na Bi.Katarina Tengia Revocati aliyekuwa msajili mkuu wa mahakama ya Tanzania.

Baada ya Vyama Vya Upinzani Kujitoa, Serikali Yasema Uchaguzi Serikali za Mitaa Uko PalePale

$
0
0
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Selemani Jafo amesema Uchaguzi wa Serikali za Mitaa uko pale pale na utafanyika Novemba 24, 2019 kama ilivyopangwa licha ya vyama vingine kujitoa kwenye Uchaguzi huo.

Jafo ameyasema hayo mapema leo alipokuwa akizungumza na vyombo vya habari Ofisini kwake Jijini Dodoma kuhusu maendeleo ya  maandalizi ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa ikiwa ni pamoja na kutoa taarifa ya zoezi la uchukuaji na urejeshaji wa fomu za kugombea uongozi sambamba  na Kamati za Rufaa.

Alisema zoezi la uchukuaji wa urejeshaji wa fomu za kugombea uongozi limeenda vizuri na wananchi waliochukua fomu ni 555,036 na waliorejesha ni 539,993 sawa na asilimia 97.29 ya wananchi wote waliochukua fomu, na ambao hakurejesha ni asilimi 2.7 tu.

“Hii inaonyesha muamko mkubwa wa wananchi kutaka kuongoza katika ngazi ya Serikali za Mitaa na mchakato mzima wa uchukuaji na urejeshaji wa fomu ulienda vizuri ukiwa na Kanuni bora zaidi  kulinganisha na chaguzi zilizotangulia” alisema Jafo.

Aliongeza kuwa baada ya zoezi hili kukamilika lilifuatiwa na uteuzi ambao ulilenga kuteua wagombea wenye sifa, waliokidhi vigezo na kufuata taratibu zote za ujazaji wa fomu za kugombea na kubandiwa kwa orodha ya wagombea waliopitishwa katika hatua hiyo.

Wagombea pia walipata fursa ya kuwasilisha pingamizi zao kwa mujibu wa Kanuni na kisha kukata rufaa kwenye Kamati ya Rufaa za Wilaya zilizoundwa kwa ajili ya kuratibu rufaa za wagombea alisema Jafo.

Waziri Jafo alifafanua kuwa mpaka hivi sasa rufaa zilizowasilishwa kutoka kwenye vyama mbalimbali vya siasa ni 13,500 na zinafanyiwa kazi na Kamati za Rufaa za Uchaguzi wa Serikali za Mitaa ambapo zoezi hilo litakamilika leo hii Tarehe 09/11/2019.

Akizungumzia baadhi ya vyama kujitoa kwenye Uchaguzi ilihali wanachama wao walishateuliwa amma kuwasilisha rufaa zao kwenye Kamati  alisema kwa mujibu wa Kanuni za Uchaguzi jina la mgombea likishateuliwa linabaki kwenye karatasi za kupigia kura siku ya Tarehe 24/11/2019 hata kama chama chake kimejiengua kushiriki kwenye Uchaguzi .

Aliendelea kuelezea kuwa wakati zoezi la uteuzi na kamati za rufaa zikiendelea na kazi yake alipata fursa ya kufanya ziara katika mikoa ya Singida, Manyara, Dododma,Iringa na Njombe ambapo  alijionea baadhi ya makosa yaliyofanywa na wagombea wakati wa ujazaji wa fomu lakini pia alizungumza na Kamati za Rufaa.

Alitaja makosa yaliyobainishwa kwenye fomu za wagombea kuwa ni  “Kujaza umri mdogo kuliko umri unaostahili kwa mgombea, sehemu ya tarehe kuweka sahihi au mtu kuchukua fomu na kujidhamini mwenyewe au majina kutofautiana wakati wa kujiandikisha kwenye orodha ya mpigakura na kwenye fomu ya kugombea hivyo Wasimamizi walifanya kazi yao kwa mujibu wa miongozo na Kanuni za Uchaguzi” Alisema Jafo.

Lakini bado nafasi ilikuwepo endapo mgombea  angeona hakuteuliwa kwa kuonewa ipo Kamati ya Rufaa ambayo ingeweza kuskiliza malalamiko ya mgombea na kuyafanyia kazi alisisitiza Jafo.

“Kuanzia kesho tutaanza kutoa Taarifa ya Rufaa zilizopita na watu walioteuliwa kushiriki uchaguzi huo kupitia Kamati za Rufaa " alimalizia Waziri Jafo.

CHAUMA Nao Watangaza Kutoshiriki Uchaguzi Serikali Za Mitaa

$
0
0
Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMA) nacho kimetangaza kutoshiriki uchaguzi wa Serikali za mitaa utakaofanyika Novemba 24, 2019.

Kimetangaza uamuzi huo siku mbili baada ya Chadema na ACT-Wazalendo navyo kutangaza kutoshiriki uchaguzi huo.

Mwenyekiti wa chama hicho, Hashim Rungwe ametangaza uamuzi huo leo Jumamosi Novemba 9, 2019 akibainisha kuwa wagombea zaidi ya 250 wa chama hicho wameenguliwa bila sababu za msingi.

“Haiwezekani nchi nzima wanaokosea kujaza fomu ni watu wa upinzani tu,  na sisi tumeamua kuwa hatutashiriki uchaguzi huu.Tunaomba wagombea wetu nchi nzima wasishiriki ” amesema Rungwe.

Rungwe alitumia nafasi hiyo kuwataka wanachama wake kutulia na kuachana na masuala ya uchaguzi.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumapili November 10

Mawaziri Wa Mambo Ya Nje Wa Nchi NORDIC Na Afrika Watembelea Mradi Wa SGR

$
0
0
Mawaziri wa Mambo ya nje kutoka nchi za Nordic na Afrika watembelea Mradi wa Ujenzi wa Reli ya Kisasa – SGR kipande cha Dar es Salaam – Morogoro, kuanzia Stesheni ya Dar es Salaam hadi Vingunguti jijini Dar es Salaam Novemba 09, 2019.

Lengo la ziara hiyo ni kuona hatua kubwa ambayo serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imepiga katika kuboresha miundombinu ya usafirishaji ukizingatia miundombinu ni moja kati ya vitu muhimu katika kuimarisha uhusiano na ushirikiano baina ya nchi za Nordic na Afrika.

Mawaziri hao walipata fursa ya kuona maendeleo ya ujenzi wa stesheni ya reli ya kisasa inayojengwa eneo la stesheni jijini Dar es Salaam, daraja la treni lenye urefu wa KM 2.5 pamoja na maendeleo ya Mradi kwa ujumla kipande cha Dar es Salaam – Morogoro ambao umefikia zaidi ya 70%.

Miongoni mwa Mawaziri waliopata fursa ya kutembelea mradi ni kutoka nchini Egypt, Nigeria, Angola pamoja na Niger. Ziara hii ni matunda ya mkutano wa Mawaziri wa Mambo ya nje kutoka nchi za Nordic na Afrika uliojadili mambo kadhaa kuhusu kuboresha uhusiano na ushirikiano uliopo kati ya nchi za Afrika na nchi za Nordic uliofanyika katika ukumbi wa kimataifa wa mikutano wa Mwl. J.K Nyerere jijini Dar es salaam.

Aidha Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Reli Tanzania Ndugu Masanja Kungu Kadogosa amewashukuru Mawaziri hao kwa kuchagu kutembelea mradi wa Ujenzi wa Reli ya Kisasa kwa kuwa ipo Miradi mingi ya kimkakati.

Naye Waziri wa Mambo ya Nje nchini Nigeria Mhe. Zubairu Dada amesema kuwa amefurahishwa na emeipongeza Tanzania kwa kutumia fedha zake za ndani kujenga reli ya kiwango cha kimataifa kuanzia Dar es Salaam hadi Makutupora Singida. Ameongeza kuwa Afrika haiwezi kuendelea kusubiri maendeleo hivyo jitihada za haraka zinatakiwa kufanywa ili kuhakikisha miradi ya miundominu inakamilika haraka ili watu wapate huduma.

Serikali Kumega ekari 3000 kutoka kwenye shamba la Karamagi Kilosa

$
0
0
Na Farida Saidy- Morogoro.
Serikali ya awamu ya tano kupitia Wizara ya Ardhi, nyumba na maendeleo ya makazi imeagiza mmiliki wa shamba la Farm Africa maarufu kama shamba la Karamagi lililopo katika Halmashauri ya Wilaya Kilosa Mkoani Morogoro kutoa ekari 3000 kutoka kwenye shamba hilo ili zimilikishwe kwa wananchi wenye uhitaji wa ardhi kwa shughuli za kiuchumi.

Agizo hilo la Serikali limetolewa Novemba 8 mwaka huu na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi alipotembelea shamba hilo lenye ukubwa wa ekari elfu 13 ambapo hakuridhishwa na kasi ya uendelezaji wa eneo hilo tangu Mmiliki wa shamba hilo alipomilikishwa.

“Kwa taarifa zilizopo bwana Karamagi alimilikishwa shamba hili tangu mwaka 2012, hivyo alipaswa kila mwaka kuliendeleza shamba lake japo kwa kiwango cha moja ya nane (1/8), hii ina maana hadi kufikia mwaka huu ambapo umiliki wake umetimiza miaka minane alipaswa kukamilisha uendelezaji wa eneo hili” alisema Waziri Lukuvi,

“Kutokana na hali hii nikuagize Mkuu wa Wilaya umfikishie taarifa bwana Karamagi kwamba mimi kama Waziri wa Ardhi namuagiza atoe ekari 3000 kutoka kwenye shamba hili ili zimilikishwe kwa wananchi ili waziendeleze kwa shughuli za kilimo”, alisisitiza Waziri Lukuvi.

Sambamba na agizo hilo, Waziri Lukuvi alibainisha kuwa 2012, ni ekari 2000 pekee ndizo zilizoendelezwa kwa kupanda mazao kati ya ekari 13,000 za licha ya kipindi cha miaka minane kupita tangu mmiliki huyo alipopata uhalali wa eneo hilo mnamo mwaka shamba hilo wakati alitakiwa awe ameendeleza shamba lote kwa kipindi hicho.

Awali, kabla ya kutoa uamuzi wa kumega sehemu ya shamba hilo ekari 3000, Mhe. Lukuvi alisikiliza kero za wananchi wanaoishi jirani na shamba hilo ambao wengi walimuomba kuwasaidia kupata maeneo kwa ajili ya shughuli mbalimbali za kiuchumi ikiwemo kilimo wakitaja shamba hilo kuwa ni sababu kubwa ya kuwakosesha maeneo ya kulima
Akiongea na viongozi wa Wilaya ya Kilosa katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri hiyo, Mhe.Lukuvi alibainisha kwamba Serikali tayari imejiridhisha kuwepo uhalali wa kufutwa mashamba 48 yaliyopo katika Halmashauri hiyo ambayo hayajaendelezwa ili yagawiwe kwa wananchi wa Wilaya hiyo kwa ajili ya kuyaendeleza.

Aidha, amewataka viongozi wa Halmshauri hiyo kufuatilia mashamba mengine 24 ambayo yameonekana kutoendelezwa ili waandike ilani kwa ajili ya kuomba kufutwa na kugawiwa wananchi wenye uhitaji.

Katika hatua nyingine Waziri Lukuvi amemtaka Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Adam Mgoyi kuhakikisha suala la udalali na ukodishaji wa ardhi unaofanywa na baadhi ya viongozi wa Wilaya hiyo na kuwakosesha wananchi maeneo ya kilimo unakoma mara moja kwani suala hilo linapelekea kuibuka kwa migogoro ya ardhi Wilayani humo.

Sambamba na hayo Waziri Lukuvi amewaagiza wataalamu wa ardhi kuepuka kubadilisha hati za umiliki wa ardhi kwa wananchi watakaogawiwa maeneo yanayotokana na mashamba yaliyofutwa huku akiwataka wananchi kutouza maeneo watakayopewa kwani hiyo ni huruma ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli.
Akiendelea kutoa maagizo mbalimbali, Waziri Lukuvi amewataka wafugaji wote waliomilikishwa ardhi kihalali Wilayani Kilosa kuweka uzio katika maeneo yao ili kuzuia mifugo isitoke katika maeneo yao na kuingia katika maeneo ya wakulima ili kuepuka migogoro ya Mara kwa mara.

Amesema wakati umefika sasa kwa wafugaji kuacha ufugaji wa kizamani badala yake watumie maeneo hayo kufuga mifugo yao kisasa ndani ya eneo lenye uzio ili mifugo yao iwe na tija zaidi kwao ukilinganisha na ilivyo sasa.
Waziri Lukuvi yupo Mkoani Morogoro kwa ziara ya kikazi ya siku mbili ikiwa na lengo la kupata maoni na mapendekezo juu ya kazi ya awali iliyofanywa na tume ya uhakiki wa mashamba yasiyoendelezwa huku akishangazwa na upendeleo ulioonyeshwa katika kuyabakiza mashamba 24 ambayo yameonekana bado hayajaendelezwa.

Serikali Yakamata Pombe Kali Imetelekezwa Porini Kukwepa Kodi Shinyanga

$
0
0
Serikali mkoani Shinyanga imekamata pombe kali aina ya Shujaa, ambayo ilikuwa imetelekezwa porini eneo la Lubaga manispaa ya Shinyanga, ikiwa ndani ya gari aina ya Roli lenye namba za usajili T 391 AES, kwa madai ya kukwepa kulipa kodi.

Akitoa taarifa kwa vyombo vya habari Novemba 9, 2019 Mkuu wa mkoa wa Shinyanga Zainab Telack akiwa kwenye kituo cha Polisi wilaya ya Shinyanga, eneo ambalo gari hilo limewekwa chini ya ulinzi, amesema kuwa serikali itawashughulikia wawekezaji wote ambao wanatabia ya kukwepa kulipa kodi ya serikali.

Telack ambaye pia ni mwenyekiti wa Kamati ya ulinzi na usalama mkoa wa Shinyanga, amesema Serikali inahitaji sana wawekezaji hapa nchini ili kukuza uchumi wa taifa, lakini siyo wawekezaji wa kukwepa kodi na kufanya biashara kiujanja ujanja.

“Pombe hii kali ya Shujaa Katoni 1,490 tumeikamata ikiwa imefichwa porini eneo la Lubaga manispaa ya Shinyanga, ikiwa ndani ya gari hili ambalo mnaliona hapa, na wamiliki wa kiwanda hiki wamekuwa na tabia ya kukwepa kulipa kodi na siyo mara ya kwanza kukamatwa,”amesema Telack.

“Hivyo naagiza Mamlaka ya Mapato Tanzania TRA Kesho wafike hapa, ili kufanya tathmini ya kujua kiasi gani cha kodi ambacho watu hawa wanapaswa kulipa, ili Serikali iweze kukusanya mapato na kupata fedha za kutekeleza maendeleo kwa wananchi,”ameongeza.

Pia ameonya baadhi ya Askari Polisi kushirikiana na waharifu hao wa kiwanda cha Shujaa, na kuwapa mbinu za kukimbia ili kukwepa mkono wa Serikali, na kumuagiza Kamanda wa Jeshi hilo mkoani Shinyanga, kuwa ndani ya siku nne, wamiliki wa kiwanda hicho wawe wameshakamatwa.

Kwa upande wake Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoani Shinyanga Richard Abwao, alithibitisha kukamata Pombe hiyo ya Shujaa, na kuahidi kutekeleza maagizo hayo ya mkuu wa mkoa, huku akitoa wito kwa wamiliki hao wa kiwanda cha Shujaa wajisalimishe wenyewe kwa usalama wao kwani watakamatwa tu popote pale walipo.

Picha na Marco Maduhu- Malunde 1

Dkt. Ndugulile: Ukatili Wa Kijinsia Ni Ujambazi Mpya

$
0
0
Na Mwandishi Wetu Dodoma
Naibu Waziri wa Afya Maeandeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile amesema Mwaka 2017 Tanzania ilikuwa na matukio ya vitendo vya ukatili wa kijinsia takribani 41elfu na kati ya vitendo hivyo ukatili dhidi ya watoto pekee ni 13 elfu.

Naibu Waziri Ndugulile amesema hayo wakati akizungumza na vyombo vya habari wakati wa Semina ya wabunge wa Kamati ya Huduma na Maendeleo ya Jamii kuhusu Mkakati wa Taifa wa Kutokomeza Vitendo vya Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto Jijini Dodoma.

Aidha Naibu Waziri Ndugulile ameifananisha changamoto ya vitendo vya ukatili Nchini kuwa ni ujambazi mpya unaozidi kuwakumba wanawake na watoto kutokana na vitendo hivyo kuendelea kutokea katika maeneo mbalimbali hapa Nchini.

Dkt. Ndugulile amesema unapoongelea ukatili wa kijinsia unazungumzia maeneo makubwa matatu ambayo ni ukatili wa kimwili, kisaikolojia na ukatili wa kiakili na kuongeza kuwa changamoto ya ukatili wa kijinsia imekuwa ikiongezeka mwaka hadi mwaka.

Ameyataja matendo hayo yanayozidi kuongezeka kuwa ni mimba na ndoa za utotoni, ubakaji na ulawiti dhidi ya wanawake na watoto ndio maana ili kukabiliana na vitendo hivyo serikali tangu mwaka 2016 ilianzisha Mpango wa Taifa wa Kutokomeza Vitendo vya Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto.

Dkt. Ndugulile ameongeza kuwa juhudi za Serikali katika utoaji elimu bure hapa nchini umepunguza suala la mimba na ndoa za utotoni kwa kuwa mtoto wa kike anapozidi kukaa shuleni ndivyo uwezekano wa mimba za mapema unapozidi kuwa mdogo.

Wakati huo huo Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii Mhe. Peter Serukamba amewambia wajumbe wa Kamati hiyo na Wizara kuwa jamii bado ina mila potofu zinazoendeleza vitendo vya ukatili kama vile ukeketeji na kuwataka Wabunge kuelimisha Jamii dhidi ya Vitendo hivyo.

Aidha Mhe. Serukamba amelitaja suala la elimu kwa umma kuhusu utokomezaji wa vitendo vya ukatili kupewa kipaumbelae huku akisifu mpango wa Serikali wa kutokomeza umasikini kwa kiwango cha kaya kupitia TASAF na kuongeza kuwa umasikini pia ni chanzo cha ukatili dhidi ya wawanawake na watoto.

Naye Mshauri Mbobezi wa Sera na Mipango kutoka Shirika la Wanawake la Umoja wa Mataifa Tanzania Bi. Usu Malya amesema shirika lake litaendelea kushirikiana na Wizara ya Afya Idara Kuu Maeandeleo ya Jamii kutokomeza vitendo vya ukatili dhidi ya Wanawake na Watoto hapa nchini.

Mpango wa Taifa wa Kutokomeza Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto ulianza tangu mwaka 2016 na umewezesha kuwa na mtazamo wa pamoja katika utekelezaji wa kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na watoto na kuondoa mwingiliano, upotevu wa rasilimali watu, fedha na muda unaotumika katika kushgulikia suala moja.

Waziri Wa Kilimo Aagiza Viongozi Wa Saccos Ya Kurugenzi Jijini Arusha Wakamatwe

$
0
0
Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo-Arusha
Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga (Mb) ameliagiza jeshi la Polisi Mkoani Arusha kwa kushirikiana na Mkuu wa Upelelezi, na Kamanda wa Taasisi ya Kuzuia na kupambana na rushwa (TAKUKURU) kuwakamata viongozi mbalimbali wa Chama cha Ushirika cha Akiba na Mikopo cha Arusha Kurugenzi kutokana na ubadhilifu wa fedha za wanachama.
 
Waziri Hasunga ametoa maagizo hayo jana tarehe 9 Novemba 2019 mara baada ya kusikiliza malalamiko ya wanachama wa chama hicho wakati wa kikao kazi kilichofanyika katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha na kuhudhuriwa pia na Mkuu wa Mkoa huo Mhe Mrisho Gambo.
 
Amesema kuwa watuhumiwa hao wanapaswa kukamatwa haraka iwezekanavyo kuanzia waliokuwa viongozi mwaka 2004 mpaka 2015 ili kurudisha fedha zote walizozizihujumu za wanachama na walizokopa.
 
Wengine alioagiza wakamatwe ni pamoja na wajumbe wote wa kamati za mikopo, Kamati ya usimamizi wa SACCOS iliyokuwepo kipindi chote hicho, Wajumbe wote wa Bodi ya SACCOS iliyokuwepo awali kabla ya Bodi iliyopo sasa. 

“Tunachotaka sisi fedha zote za wanachama zirudi na hata leo wakirudisha fedha hizo hatutaendelea na kesi” Alisema
 
Pia ameagiza mwanachama wa SACCOS hiyo Bi Zainab Nassor aliyeanzisha vikundi hewa 14 akamtwe, huku wengine ni aliyekuwa Mwenyekiti wa SACCOS Dkt Freedom Makiago,  Makamu Mwenyekiti Gasto Gasper, Meneja Christina Sumaye, na wajumbe Andrea Sekidio, Joseph Kuhamwa na Mwanahamisi Gembe.
 
Katika hatua nyingine Mhe Hasunga ameagiza kukamatwa kwa aliyekuwa Mwenyekiti wa kamati ya Usimamizi Bi Mwanahawa Kombo, na wajumbe Samwel Mushy, Estomin Chang’ah. Huku akiagiza pia karani wa SACCOS hiyo Edith Malley kukamatwa.
 
Katika hatua nyingine ameagiza viongozi wote walioandikwa kwenye vikundi vya mikopo kukamatwa haraka iwezekanavyo na kuchukuliwa hatua za haraka ikiwemo kurudisha fedha za wanachama.
 
Mhe Hasunga amesema kuwa lengo la kunzishwa vyama vya ushirika ilikuwa ni kuwanufaisha wananchi kupitia umoja huo muhimu kwani mafanikio yanahusisha nguvu ya pamoja.
 
Hata hivyo ameagiza Bodi iliyopo madarakani kubainisha taarifa za kumbukumbu zote za chama hicho kwa kuonyesha idadi ya wanachama na akiba walizonazo katika chama, idadi ya hisa na kiasi cha fedha zinazodaiwa na kila mwanachama.
 
Kwa sasa chama kinadaiwa fedha kiasi cha shilingi 2,486,365.68 zilizotokana na mikopo kutoka Taasisi mbalimbali za kifedha, Amana, Akiba na Hisa za wanachama hususani wastaafu ambazo zilichukuliwa kwa kutumiwa na wahusika hao bila utaratibu na kwa malengo yao binafsi.
 
Wanachama wastaafu wanadai zaidi ya shilingi 831,764,924.87 zitokanazo na fedha za Amana walizoweka katika chama kutumia viinua mgongo vyao baada ya kustaafu utumishi, Akiba na Hisa walizowekeza tangu wajiunge na chama hicho.
 
Wanachama wanaoendelea na chama na waliojitoa wanadai zaidi ya shilingi 770,181,745.56 zitokanazo na Amana, Akiba na Hisa walizowekeza tangu wajiunge na chama hicho.
 
Kadhalika, Taasisi za kifedha zinazodai ni pamoja na (CRDB, NSSF na TUMAINI SACCOS) wanaodai zaidi ya shilingi 874,575,517.25 bakaa ya mikopo iliyotolewa bila kuzingatia utaratibu wa kifedha na kwa kutumia taarifa za udanganyifu.
 
Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga yupo Mkoani Arusha kwa ziara ya kikazi ya siku 2 kwa mualikowa Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe Mrisho Gambo ambapo pamoja na mambo mengine atashuhudia shughuli za sekta ya kilimo.

Naibu Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, Sisty Nyahoza Asema Wapinzani Wanatakiwa Kujilaumu Wenyewe kwa Kutofuata Sheria za Uchaguzi

$
0
0
Naibu Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, Sisty Nyahoza amesema malalamiko yanayotolewa na vyama vya siasa kuhusu kuenguliwa wagombea wao katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa yamesababishwa na wao wenyewe.

Miongoni mwa malalamiko ambayo yalitolewa na vyama hivyo, ni pamoja na wagombea wao kuenguliwa au kuwekewa pingamizi kwa sababu ya kukosa sifa kutokana na kukosea kujaza fomu zao.

Mengine ni wagombea kuenguliwa kwa sababu ya kujaza jina la chama kwa kifupi mfano, Chadema badala ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo au ACT Wazalendo  badala ya Alliance for Change and Transparency.

Nyahoza amesema matatizo na malalamiko mengi yanayovikumba vyama vya upinzani katika uchaguzi huu, yanatokana na kutozingatia sheria na kanuni zilizowekwa.

“Hivi vyama mara kwa mara tunaongea nao kuhusu kuzingatia sheria na kanuni, sasa kama watakuwa hawazisomi na kuzifuata watakuwa wanalalamika mara kwa mara,” alisema Nyahoza.

Kuhusu fomu inayosambaa kwenye mitandao ya kijamii ya mgombea mmoja ambaye amekatwa baada ya kuandika kwa kifupi ACT Wazalendo na kuelezwa na msimamizi wa uchaguzi huo kwamba chama hicho hakipo kwenye orodha ya msajili, alisema chama hicho kimesajiliwa kwa jina la Alliance for Change and Transparency (ACT Wazalendo) na sio ACT Wazalendo, hivyo hilo ni kosa.

“Hiyo wanayosema ni kifupi ni kama ilivyo CCM kwa Chama Cha Mapinduzi, lakini huwezi kuandika CCM tu kwani inaweza ikawa inamaanisha kitu kingine.

“Sisi kama walezi siku zote tumekuwa tukiwasisitiza kuzisoma na kuzingatia sheria, lakini kama baba unasema na mtoto hafuati matokeo yake ndiyo hayo,” alisema Nyahoza.

Alisema kuwa vyama vyote vya siasa vina wanasheria na watu waliobobea kwenye mambo hayo, ambao wana uwezo wa kuwaongoza wanachama wao katika mambo hayo muhimu.

Credit: Mtanzania

Rais Magufuli Abatilisha Ufutaji Shamba La Ekari 1000 Mvomero

$
0
0
Na Munir Shemweta, WANMM MVOMERO
Raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli amebatilisha pendekezo la kufutwa shamba lenye ukubwa wa ekari 1000 lililopo Kidunda wilayani Mvomero mkoani Morogoro linalomilikiwa na Cecilia George Rusimbi.

Uamuzi wa Dkt Mafuli kubatilisha ufutaji shamba hilo unatokana na kubainika kuwa pendekezo lililowasilishwa la kufutwa shamba hilo kwa madai ya kutoendelezwa kutokuwa za kweli na ulilenga kumdhulumu mmiliki wake.

Akitangaza uamuzi huo wa Raisi jana wilayani Mvomero, Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi alisema, baada ya kufuatilia mashamba yaliyopendekezwa kufutwa Dkt Magufuli alibaini taarifa alizopelekewa za kufuta shamba Cecilia hazikuwa sahihi na hivyo kuamua kubatilisha pendekezo lililowasilishwa kwake na kumpatia haki yake mmiliki.

Kufuatia hali hiyo Waziri Lukuvi aliwaonya Aaafisa ardhi nchini kuhakikisha wakati wa kufanya zoezi la ukaguzi/Upekuzi wa mashamba yasiyoendelezwa wanazingatia haki pamoja na kufuata sheria badala ya kufanya kazi hiyo kwa upendeleo au kumuonea mtu.

Hata hivyo, Waziri wa Ardhi alisema, utendaji kazi katika wilaya ya Mvomero umekuwa wa hovyo na usiozingatia maadili jambo linalopelekea wilaya hiyo kuongoza katika mkoa wa Morogoro kuwa na migogoro mingi ya ardhi sambamba na malalamiko mengi ya wananchi dhidi ya ofisi ya ardhi.

‘’Baadhi ya watumishi katika ofisi ya halmashauri ya wilaya ya Mvomero mnajifanya ni Maafisa ardhi au Wapima wakati hamkuajiriwa kwa nafasi hiyo, mnasaini nyaraka za ardhi na kuwaumiza wananchi’’ alisema Lukuvi

Kwa upande wake Cecilia George Rusimbi alimshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli kwa uamuzi wake wa kubatilisha ufutaji sahamba lake na kuuelezea uamuzi huo kuwa  umezingatia haki na kusikia kilio chake ambapo alisema umempa faraja baada ya kuhangaika sana kuhusiana na shamba hilo.

‘’ Nimemiliki shamba tangu mwaka 1987 na kuhangaikia hati kwa muda mrefu na nimeshangazwa kuelezwa kuwa shamba langu liko katika mpango wa kufutwa kutokana na kutoendelezwa, hii imenifanya kuishi kwa wasiwasi’’ alisema Cecilia.

Waziri Lukuvi ameagiza shamba hilo la kilimo cha Michikichi, Mitiki na Bamboo  kupangwa upya na mmiliki wake kupatiwa hati kulingana na upimaji utakaofanywa na kumtaka kuliendeleza kwa mujibu wa sheria.

Sambamba na sakata la shamba la Cecilia, Lukuvi aliagiza kupunguzwa ukubwa wa Shamba Sangasanga na Lubango lililodaiwa kuwa na ukubwa wa ekari 1,103 wakati uhalisia wa shamba hilo ni ekari 500 na kuagiza mmiliki wake kurudisha hati ili apatiwe hati ilinayolingana na uhalisia wake na ekari 603.5 zilizoongezwa zitabaki kuwa ardhi ya akiba.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Mvomero Mwl Mohamed Utaly alieleza kuwa wilaya yake ina tatizo kubwa la migogoro ya ardhi pamoja na jitihada kubwa inayofanywa na ofisi yake kukabiliana na tatizo hilo na kuongeza kuwa mingine inachochewa na uhamasishaji unaowafanya wananchi kukata tamaa.

Katika hatua nyingine Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi alitembelea ofisi ya Ardhi katika halmashauri ya Mvomero na kubaini ‘madudu’ katika ofisi hiyo ambapo alibaini baadhi ya majalada ya wananchi waliomba kumilikishwa ardhi tangu mwaka 2012 katika halmashauri hiyo kushindwa kupatiwa hati huku.

Hali hiyo ilimfanya Waziri Lukuvi kumuagiza Kaimu Kamishana Msaidizi wa Ardhi Kanda Maalum ya Morogoro Erick Makundi kuhakikisha wale wote walioomba hati na kutumiza vigezo vya kupatiwa hati wanapatiwa kufikia mwezi ujao Desemba 2019. Pia ameagiza kufuatiliwa majalada 300 ambayo wamiliki wake wamekamilisha taratibu za kupatiwa hati lakini hawajapatiwa.

Sambamba na hilo Lukuvi aliagiza wafanyakazi wa ofisi ya ardhi katika halmashauri hiyo wanaojitolea kutosaini nyaraka zozote za ardhi kwa kuwa baadhi yao wamekuwa wakishiriki kutoza tozo kwa gharama za juu za shilingi 50,000 wakati gharama halisi ni 20,000.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images