Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Fahamu Zaidi Kuhusu Ugonjwa Wa Mshipa Wa Ngiri (Hernia/Hydrocele)

$
0
0
Tatizo la Ngiri Linavyosababisha Upungufu wa Nguvu za Kiume na Maumbile Kusinyaa, Dalili zake Hizi Hapa..

Ngiri au Hernia ni aina ya ugonjwa ambao unampata mtu baada ya misuli au kuta za tishu mwilini zinazoshikiria au kubeba viungo (organs) fulani mwilini kupoteza uimara wake au kuwa na uwazi (Opening) na hivyo kusababisha viungo hivyo kutoshikiriwa ipasavyo katika sehemu vinapostahili kuwepo.

Katika mwili wa binadamu, maeneo ambayo tatizo hili hutokea mara kwa mara ni maeneo ya tumboni, katika eneo la kinena, eneo la paja kwa juu na pia ngiri inaweza kutokea katika eneo ambalo mtu alifanyiwa upasuaji (operesheni).

Dalili za Ngiri
Tumbo kuunguruma, kiuno kuuma, kupata choo kama cha mbuzi, kushindwa kufanya tendo la ndoa, mishipa ya maumble ya kiume kulegea, kutokuwa na hamu ya kurundia tendo la ndoa, korondani moja kuvimba, mgongo kuuma.

Dalili zingine za ugojwa wa ngiri ni pamoja na;

Uvimbe unaoteremka kuingia ndani ya korodani unaojulikana kitaalamu kama Direct Scoratal inguinal Hernia.


Uvimbe unaojitokeza tumboni na kuteremka hadi ndani ya korodani, uvimbe huu hauumi na unaweza kurudishwa kwa urahisi iwapo mgonjwa atalala chali na kusukuma kwa vidole, uvimbe huu.


Na pindi ukikubali kurudi ndani ndipo unapoitwa Reduible direct scrotal inguinal hernia.


Na pia endapo utashindikana kurudi tumboni ndipo unapoitwa Irreduible direct scrotal inguinal hernia.


Ugojwa huu wa ngiri unaweza kutibika

Kwa Ushauri na Msaada wa Wasaliana na  0713785111

Rais Magufuli Aongoza Maelfu ya Watanzania Kupokea ndege mpya ya Serikali ya Boeing 787-8 Dreamliner Jijini DAR Leo

$
0
0
Na Mwandishi Wetu,MAELEZO
RAIS Dkt. John Magufuli amesema Tanzania itaendelea kutekeleza kwa kasi kubwa miradi ya maendeleo nchini kwa kuwa Serikali imeimarisha nidhamu katika usimamizi na matumizi ya rasilimali zilizopo pamoja na ukusanyaji wa kodi.

Akizungumza katika hafla ya upokeaji wa ndege mpya ya Serikali ya Boeing 787-8 Dreamliner katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere leo Jumamosi (Oktoba 26, 2019) Jijini Dar es Salaam, Rais Magufuli aliwataka Watanzania kujivunia na kuendelea kuiunga mkono Serikali yao kwa kuwa imedhamiria kuwaletea maendeleo ya kweli na ya haraka.

Rais Magufuli alisema Tanzania na Bara la Afrika kwa ujumla lina uwezo wa kufanya mambo makubwa  nay a haraka kutokana na kubarikiwa na rasilimali nyingi ikiwemo madini na hivyo Serikali ya Awamu ya Tano itaendelea kusimamia rasilimali hizo ili ziweze kuleta manufaa yaliyokusudiwa kwa wananchi walio wengi.

‘’Watanzania sisi ni matajiri tunaweza kufanya mambo makubwa na kununua vitu vizito kama ndege hizi, na tukiamua tunaweza kinachotakiwa sasa ni kuweza kuwa na matumizi mazuri ya fedha zinazopatikana kutokana na kodi tunazokusanya kutoka kwa wananchi wetu’’ alisema Rais Magufuli.

Aliongeza kuwa malengo ya Serikali ya Awamu ya Tano ni kuhakikisha kuwa sekta ya usafiri wa anga inapiga hatua kubwa ya maendeleo nchini na kwa kufanya hivyo Serikali imekusudia kuliwezesha Shirika la Ndege Nchini ATCL kuweza kutekeleza mipango na mikakati mbalimbali iliyojiwekea.

Akifafanua zaidi Rais Magufuli alisema ATCL kwa sasa ina jumla ya ndege 7 kati ya ndege 11 zilizopangwa kununuliwa na Serikali, hivyo aliitaka Menejimenti ya Shirika hilo kujipanga vizuri ili kuhakikisha kuwa linamudu ushindani wa kibiashara uliopo nchini ikiwemo kuimarisha mtandao wa usafirishaji abiria katika soko la ndani na nje ya nchi.

Kwa mujibu wa Rais Magufuli alisema ndege hiyo mpya ya Boeing 787-8 Dreamliner ni ndege kubwa ya kisasa yenye uwezo wa kubeba abiria 262 ikiwemo abiria 22 wa daraja la juu pamoja abiria 240 katika daraja la kawaida, hivyo kuitaka ATCL kuweka mipango na mikakati endelevu ya kuhakikisha itangaza vyema vivutio vya utalii vilivyopo nchini.

‘ATCL hamna budi kujiendesha kibiashara na mnapaswa kutambua ndege hii ni mali ya Serikali na si ya ATCL hivyo na hilo linajionesha katika mkataba tuliosaini baina ya Katibu Mkuu Kiongozi na Katibu Mkuu (Uchukuzi), hivyo hakikisheni mnafikia malengo yote tuliyowekeana’’ alisema Rais Magufuli.

Kwa upande wake Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Dkt. Leonard Chamuriho alisema Shirika la ATCL limeendelea kutekeleza kwa mafanikio makubwa Mpango Mkakati wa Shirika hilo, ambapo sasa limeweza kufikia mafanikio ya asilimia 73 la usafirishaji wa abiria katika soko la ndani.

Aidha Dkt. Chamuriho anaongeza kuwa kutokana na kuongezeka kwa idadi ya safari za abiria nje ya nchi, Shirika hilo pia limefanikiwa kuongeza idadi ya upokeaji wa shehena za mizigo kutoka nchini India na kufikia tani 178 na kuzisafirisha katika nchi mbalimbali ikiwemo Zambia.

Aliongeza kuwa Shirika hilo limepanga kushirikiana na Taaasisi ya Sekta Binafsi Nchini (TPSF) pamoja na Chemba ya Biashara,Viwanda na Kilimo Tanzania (TCCIA) kwa ajili ya kuweka nguvu na mkakati wa pamoja wa kuhakikisha kuwa inatanua mtandao wa usafirishaji wa shehena za mizigo nchini India.

Kuhusu soko la ndani, Dkt.Chamuriho aliongeza kuwa Shirika hilo limeweza kuongeza kituo cha usafirishaji wa abiria katika Kituo cha Mpanda Mkoani Rukwa pamoja na kupanga kuongeza idadi ya miruko ya ddege kutoka Dar es Salaam-Dodoma kufikia mara nne kwa siku ifikapo mwezi Desemba mwaka huu.

Naye Kaimu Balozi wa Marekani Nchini , Dkt. Imni Patterson aliipongeza Serikali ya Awamu ya Tano kutokana na juhudi na hatua mbalimbali za makusudi inazochukua katika kuimarisha sekta ya usafiri wa anga kwani kwa kufanya hivyo kutaweza kutangaza sekta ya utalii pamoja na kuimarisha uchumi.

MWISHO

Kamati Ya Bunge Ya Katiba Na Sheria Yaridhishwa Na Utekelezaji Wa Mfuko Wa Maendeleo Ya Vijana

$
0
0
Na; Mwandishi Wetu
Kamati ya Bunge ya Katiba na Sheria imeridhishwa na utekelezaji wa Mfuko wa Maendeleo ya Vijana “Youth Development Fund” unaoratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu katika kuchochea maendeleo ya shughuli za kiuchumi za vijana.

Hayo yameelezwa na Mwenyekiti wa kamati hiyo ya kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria Mhe. Najma Giga (Mb) wakati kamati hiyo ilipokutana kwa lengo la kufuatilia utekelezaji wa mfuko wa maendeleo ya vijana katika ukumbi wa Katiba na Sheria Bungeni Jijini, Dodoma.

Akizungumza wakati wa kikao hicho alisema kuwa Mfuko wa Maendeleo ya Vijana umekuwa ni kielelezo tosha kwa serikali katika kuonyesha dhamira ya dhati ya kuwasaidia vijana sambamba na kuendeleza miradi yao ya kiuchumi.

“Tunapongeza Ofisi ya Waziri Mkuu kwa kusimamia vizuri mfuko wa Maendeleo ya vijana kwa kuwa umeendelea kuwa chachu kwa vijana kuanzisha makampuni na vikundi vya uzalishaji mali katika ngazi ya halmashauri za wilaya, miji na manispaa ambazo zimeibua fursa ya ajira kwa vijana,” alisema Mheshimiwa Giga

Aliongeza kuwa kupitia mfuko huo vijana waendelee kuhamasishwa zaidi kujishughulisha na kubuni miradi mbalimbali ya kiuchumi na aliwataka kuongeza ubunifu katika shughuli zao za uzalishaji mali.

Aidha alitoa wito kwa vijana waliopata mikopo hiyo kuitumia vizuri mikopo hiyo kwa kuwa inamanufaa ili waweze kunufaika nayo pia kuifanya miradi yao kuwa endelevu.

Akielezea kuhusu mfuko huo wa Maendeleo ya Vijana Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Sera, Bunge, Kazi, vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama alieleza kuwa lengo la kuanzishwa mfuko maendeleo ya vijana na Serikali mwaka 2013 ilikuwa ilikuwa kuwawezesha vijana kupata mitaji yenye masharti nafuu.


“Katika kipindi cha miaka mine ya Serikali ya awamu ya tano yaani mwaka 2015 – 2018 jumla ya bilioni 2 zimetolewa katika vikundi vya vijana 533 vyenye idadi ya vijana 3,780 katika halmashauri 128 nchini,” alisema Mhagama

Akielezea miradi ya vijana iliyoweza kunufaika na mikopo ya mfuko huo ikiwemo Kilimo, Ufugaji, Viwanda vya kuchakata (Ngozi, Madini, kusindika mazao ya chakula, vifaa vya ujenzi, kutengeneza taulo za kike, kusindika chakula cha mifugo), Makampuni yanayotoa huduma za mawasiano, makampuni yanayotoa huduma za kifedha na makampuni yanayotoa huduma za elimu.

Alieleza kuwa Serikali inaendelea kuwahamasisha vijana pamoja na wenye ulemavu kuendelea kuchangamkia fursa ya mikopo hiyo ambayo imekuwa kielelezo katika kubadili mtazamo wa vijana kujijengea dhana ya kujitegemea na kukuza vipato vyao.

“Mwaka huu wa fedha 2019/2020 Serikali inatarajia kutoa mikopo yenye thamani ya shilingi milioni 850 kwa vikundi vya vijana 224 katika halmashauri za wilaya 56, kwa dhamira hii njema ya serikali ni wakati muafaka vijana wakawa wabunifu katika kuanzisha miradi yenye tija itakayowawezesha kukopesheka,” alieleza Mhagama

Aidha aliwashauri vijana walionufaika na mfuko huo wahakikishe wanarejesha mikopo hiyo kwa wakati ili mfuko huo uweze kuwa endelevu na manufaa kwa vijana.

MWISHO

Serikali Yaelekeza Kukamilika Kwa Ujenzi Wa Kiwanda Ili Kukuza Soko La Mifugo Nchini

$
0
0
Na. Edward Kondela
Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo) Prof. Elisante Ole Gabriel ameuelekeza uongozi unaosimamia ujenzi wa kiwanda cha kusindika nyama cha Eliya kinachojengwa katika Wilaya ya Longido Mkoani Arusha kuhakikisha unakamilisha ujenzi wa kiwanda hicho mapema mwanzoni mwa mwaka 2020 ili kiweze kuleta tija kwa taifa na wafugaji wanaoishi katika Mkoa wa Arusha, mikoa ya jirani na nchi ya jirani ya Kenya.

Prof. Gabriel amesema hayo jana (24.10.2019) mara baada ya kutembelea ujenzi wa kiwanda hicho akiwa pamoja na uongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Longido na kukuta tayari ujenzi wa kiwanda umefikia asilimia 90 ambapo mitambo mbalimbali imeanza kufungwa katika kiwanda ambacho kitakuwa na uwezo wa kuchinja ng’ombe 500 kwa siku na mbuzi takriban Elfu Mbili kwa siku.

Katibu mkuu huyo ametoa wito kwa wadau wa mifugo kujipanga vizuri namna ya kutumia fursa ya uwepo wa kiwanda hicho ili wafugaji na wafanyabiashara waweze kuuza mifugo katika kiwanda hicho ambacho kitaongeza ajira na kukuza sekta ya mifugo nchini.

Awali akizungumza na wakuu wa idara na vitengo wa Halmashauri ya Wilaya ya Wilaya ya Longido kabla ya kutembelea ujenzi wa kiwanda hicho, Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo) Prof. Elisante Ole Gabriel amepokea maoni ya namna ya kudhibiti vitendo vya kutorosha mifugo mipakani hali inayochangia kuikosesha serikali mapato ambapo elimu imesisitizwa kwa watu wanaoishi mipakani.

Prof. Gabriel amesema Wizara ya Mifugo na Uvuvi inazidi kuchukua maoni ya namna ya kuhakikisha vitendo vya utoroshaji wa mifugo hususan katika mpaka wa Namanga ambao ni kati ya mipaka ya nchi za Tanzania na Kenya vinadhibitiwa ili kuhakikisha mapato ya serikali hayapotei pamoja na kusimamia  viwanda vya kusindika nyama kikiwemo cha Eliya kinachotarajia kukamilika mapema mwaka 2020 kinapata mifugo ya kutosha kutoka Mkoa wa Arusha na mikoa ya jirani ili kusindika nyama katika kiwanda hicho.

Mwisho.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumapili October 27

BREAKING: Majina Ya Wanafunzi Waliopata Mkopo Awamu Ya Pili 2019/20

$
0
0
Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) imetoa orodha ya majina ya wanafunzi 11,378 wa mwaka 2019/2020 waliopata mkopo wa awamu ya pili.

Mkurugenzi mtendaji wa HESLB,  Abdul-Razaq Badru ametoa taarifa  Jumamosi Oktoba 26, 2019 na kubainisha kuwa waliopata mikopo hadi sasa ni 42,053 wa mwaka wa  kwanza. Amesema mkopo waliopata ni sawa na Sh148,56 bilioni.

Badru amesema mwaka 2019/20, Serikali imetenga Sh450 bilioni kwa ajili ya wanafunzi 128,285.

Amebainisha kuwa kati ya wanafunzi hao,  zaidi ya 45,000 ni wa mwaka wa kwanza na  83,285 ni wanafunzi wenye mikopo wanaoendelea na masomo.

Taarifa Ya Kusitishwa Kwa Huduma Za Usafiri Wa Reli Ukanda Wa Kaskazini (Tanga & Kilimanjaro)

RC Mtaka: TRA Ongezeni Elimu Ya Kodi Ya Majengo

$
0
0
Na Veronica Kazimoto, Simiyu
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Anthony Mtaka ameipongeza Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kwa kuhamasisha wananchi kulipa kodi ya majengo na kuishauri kuongeza elimu zaidi juu ya umuhimu wa kodi hiyo.

Akizungumza ofisini kwake wakati timu ya maofisa wa TRA kutoka mkoani Simiyu na Makao Makuu Dar es Salaam walipomtembelea kwa ajili ya kumpa taarifa ya semina za wafanyabiashara zilizofanyika mkoani humo, Mtaka amesema licha ya kazi kubwa ya uhamasishaji wa kodi ya majengo inayofanyika, bado kuna baadhi ya maeneo ambapo wananchi hawajapata elimu ya kutosha kuhusu kodi hiyo.

“TRA mnajitahidi sana kuhamasisha kodi ya majengo lakini bado kuna maeneo mengi elimu hii haijafika kama inavyotakiwa hivyo tumieni kila njia ya mawasiliano kuhakikisha kuwa elimu ya kodi ya majengo inawafikia wananchi wote,” alisema Mtaka.

Aidha, Mtaka ameongeza kuwa, kuna haja ya Mamlaka ya Mapato Tanzania kufungua ofisi katika baadhi ya wilaya ambazo hakuna ofisi za TRA ili kusogeza huduma karibu na wananchi ikiwa ni pamoja na kodi ya majengo. 

“Kuna baadhi ya wilaya hazina ofisi za TRA hapa nchini, kwa mfano mkoani kwangu Simiyu, kuna Wilaya ya Itilima na Busega ambazo hazina ofisi za TRA na hivyo wananchi wa wilaya hizi hulazimika kufuata huduma kwenye ofisi za TRA zilizoko makao makuu ya mkoa,” alifafanua Mtaka.

Naye, Meneja wa Elimu kwa Mlipakodi kutoka TRA Makao Makuu Diana Masalla amemshukuru Mkuu wa Mkoa huo kwa ushirikiano anaoutoa kwa TRA katika kutekeleza majukumu yake ya ukusanyaji mapato mkoani humo.

Mamlaka ya Mapato Tanzania ndio yenye jukumu la kukusanya kodi ya majengo kisheria na viwango vya kodi hiyo ni shilingi 10,000 kwa nyumba za kawaida, shilingi 20,000 kwa ghorofa zima katika Halmashauri za Wilaya na shilingi 50,000 kwa kila sakafu ya ghorofa katika Majiji, Miji na Manispaa.

Mwisho.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumatatu October 28

Trump atangaza kuuawa kwa kiongozi wa IS Abu Bakr al-Baghdadi Syria

$
0
0
Rais wa Marekani Donald Trump amethibitisha kuwa vikosi maalum vya Marekani vimemuua kiongozi wa kundi linalojiita Dola la Kiislamu – IS Abu Bakr al-Baghdadi kaskazini mwa Syria

"Jana usiku, Marekani ilifikisha mwisho safari ya gaidi nambari moja duniani," alisema Trump. "Al-Baghdadi amefariki dunia"

"Alifika mwisho wa handaki wakati mbwa wetu wakimfukuza,” Aliongeza Trump. Al-Baghdadi aliripua mabomu aliyokuwa amejifunga mwilini wakati wanajeshi walipomkaribia. Mlipuko huo uliwauwa wanawe watatu.

Vikosi maalum vya Marekani viliweza kumtambua Baghdadi dakika 15 baada ya kuuawa kwa kufanya vipimo vya vinasaba – DNA katika eneo la shambulizi hilo. Uchunguzi huo wa DNA ulikuwa muhimu ikizingatiwa kuwa al-Baghdadi alikuwa ametangazwa kuuawa mara kadhaa. Hakukuwa na hasara yoyote kwa upande wa Marekani wakati wa operesheni hiyo.

Trump amesema katika Ikulu ya White House kuwa "idadi kubwa ya wapiganaji wa al-Baghdadi na marafiki waliuawa, wakati watoto 11 wadogo wakihamishwa kutoka kwenye nyumba walimokuwa, bila kujeruhiwa.

Amesema dunia sasa ni mahala salama, na kuwa "matukio hayo ni ukumbusho mwingine kuwa tutaendelea kuwawinda magaidi waliobaki wa IS hadi mwisho.”

Trump ameipongeza Urusi, Uturuki, Syria na Iraq klwa ushirikiano wao. Wizara ya Ulinzi ya Uturuki imesema katika taarifa kuwa Uturuki na Marekani zilibadilishana taarifa kuhusu shambulizi hilo lililoongozwa na Marekani mkoani Idlib, Syria. Kamanda wa vikosi vya Syrian Democratic – SDF, Mazloum Abdi ameandika kwenye Twitter kuwa kifo cha al-Baghdadi kilikuwa matokeo ya ushirikiano wao na Marekani.

Kwa miezi mitano kumekuwa na ushirikiano wa pamoja wa taarifa za kijasusi na uchunguzi mahsusi, hadi tulipofanikisha operesheni ya pamoja ya kumuua Abu Bakr al-Baghdadi,” Aliandika Abdi.

Al-Baghdadi amekuwa mafichoni mwa miaka mitano. Kuna wakati Marekani ilitangaza zawadi ya dola milioni 25 kwa yeyote ambaye alikuwa na taarifa ambazo zingesaidia kupatikana kwake.


Credit;DW

Waziri Lugola Aagiza Polisi Kuwakamata Wabadhirifu Wa Vyama Vya Ushirika

$
0
0
Na Felix Mwagara, MOHA, Bunda.
WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola ameliagiza Jeshi la Polisi nchini kuwakamata viongozi wa vyama vya ushirika nchini ambao wamekuwa wakihujumu fedha za wakulima.

Waziri Lugola ametoa kauli hiyo, katika Mkutano wa Viongozi wa Wilaya ya Bunda, Mkoani Mara, jana, kufuatia Mkuu wa Wilaya ya Bunda, Lydia Bupilipili kuwakamata viongozi wa vyama vya ushirika walioshindwa kurejesha fedha za Serikali zaidi ya bilioni moja na milioni mia nne atua ambayo imemfanya.

“Nawaagiza Polisi kuendesha operesheni ya kuwakamata wabadhirifu wa fedha na mali mbalimbali za umma, na agizo hili si la hapa Bunda tu, bali nchi nzima, makamanda wawasake na kuwatia mbaroni ili iwe fundisho kwa watu wenye tabia hizo,” alisema Lugola.

Pia Waziri Lugola, alitoa onyo kali kwa viongozi wa vyama vya ushirika kote nchini kuwa Serikali ya awamu ya tano kupitia Wizara yake haitamuacha mtu salama atakayechezea fedha za Serikali.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Bunda, Lydia Bupilipili alisema wamewakamata viongozi wa vyama vya ushirika walioshindwa kurejesha fedha za Serikali na watawafikisha mahakamani.

“Fedha za vyama vya ushirika zimeliwa, tukaamua kuwakamata watuhumiwa wote na tayari tumefanya hizo, na tutawafungulia mashataka ili iwe fundisho kwa wananchi ambao wanatabia ya kuchukua fedha za umma,” alisema Lydia.

Waziri Lugola yupo Wilayani Bunda kwa ajili ya ziara ya kikazi, kuzungumza na wananchi, na pia kutatua kero mbalimbali zinazohusu Wizara yake Wilayani humo.

Kamati Ya Bunge Yaipongeza Ofisi Ya Waziri Mkuu Kwa Mkakati Wa Ajira Na Uwezeshaji Vikundi Vya Vijana

$
0
0
Na; Mwandishi Wetu
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria imeipongeza Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu kwa mikakati iliyoweka katika kuwajengea uwezo vijana kujiajiri na uwezeshwaji kiuchumi kwa vijana kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Vijana “Youth Development Fund” na Mikopo kupitia mapato ya ndani ya halmashauri.

Akizungumza wakati wa ziara ya ukaguzi wa miradi ya vijana katika Mkoa wa Morogoro, Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Katiba na Sheria Mhe. Najma Giga ameipongeza Serikali kwa mikakati iliyokuja nayo katika kutatua changamoto ya ukosefu wa ajira kwa vijana kwa kuwajengea mazingira wezeshi na yanayowahamasisha kuanzisha miradi mbalimbali ya kiuchumi.

“Matokeo ya utekelezaji wa mikakati hiyo tumeona kwa kiasi kikubwa imewawezesha vijana kutambua taratibu rasmi za kupata mikopo yenye riba nafuu na ambayo imewasaidia kuazisha miradi ya kiuchumi,” alisema Mheshimiwa Giga.

Aliongeza kuwa Serikali iendelee kutenga bajeti zaidi ya uwezeshwaji wa vikundi vya vijana kwa kuwa vina tija na vinapunguza tatizo la ajira kwa vijana kwa kiasi kikubwa.

Sambamba na hayo Kamati hiyo iliitaka Ofisi ya Waziri Mkuu kuendelea kutoa maelekezo katika halmashauri zote kuelimisha vijana zaidi ili waweze kutambua taratibu za kupata mikopo kupitia mfuko wa maendeleo ya vijana na asilimia 10 ya mikopo ambayo utolewa kwa Vijana 4%, Wanawake 4% na Wenye Ulemavu 2% kupitia mapato ya ndani ya halmashauri.

Akitoa maelezo ya Ofisi ya Waziri Mkuu, Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Kazi, Vijana na Ajira Mhe. Anthony Mavunde ameihakikishia Kamati ya Bunge kwamba Serikali itaendelea kuviwezesha kiuchumi vikundi vya vijana katika mkakati wa kuhamasisha vijana kujiajiri lakini pia kuwajengea uwezo wa kiuchumi vijana ili nao pia washiriki kikamilifu katika mnyororo mzima wa uchumi wa viwanda ambapo matarajio ni kwamba ifikapo mwaka 2025 zaidi ya asilimia 40 ya nguvukazi iwe imeajiriwa kwenye sekta ya viwanda.

“Serikali iliazisha mfuko wa maendeleo ya vijana na programu mbalimbali ili kuwawezesha wananchi hususan vijana kuweza kupata mahitaji ya mitaji ya kuanzisha shughuli za kiuchumi zitakazo waingizia kipato,” alisema Mavunde

Akitolea mfano mafunzo ya kilimo cha kisasa kwa vijana kutumia teknolojia ya kitalu nyumba ni mkakati mzuri ambao Serikali imekuja nao katika kutatua tatizo la ajira kwa vijana kupitia sekta ya kilimo.

Aidha, Naibu Waziri Mavunde aliwahamasisha vijana kuandaa maandiko ambayo yataelezea shughuli zenye tija wanazotaka kuzifanya katika kujileta maendeleo ili waweze kupata mikopo kupitia Mfuko wa Maendeleo ya vijana na Mikopo kupitia mapato ya ndani ya halmashauri itakayowasaidia kuendesha shughuli zao. 

Kwa nyakati tofauti vijana wa Mkoa wa Morogoro wameishukuru Serikali kwa uwezeshaji kupitia Mfuko wa maendeleo ya vijana na kuomba kuwezeshwa zaidi ili kukidhi matarajio yao ya uanzishwaji wa viwanda katika kuunga mkono jitihada za Serikali ya Tano katika uchumi wa viwanda.

Viwanda Vinavyotumia Malighafi Za Mifugo Kutambuliwa Ili Kufikia Uchumi Wa Kati

$
0
0
Na. Edward Kondela
Serikali imewataka maafisa mifugo wote nchini katika maeneo yao ya kazi kufuatilia idadi ya viwanda vinavyotumia malighafi ya mifugo ambavyo vinafanya kazi pamoja na ambavyo havifanyi kazi kufahamu changamoto  zake ili ziweze kutafutiwa ufumbuzi na viwanda hivyo vianze kufanya kazi kuendana na azma ya serikali ya kufikia uchumi wa kati unaotegemea viwanda ifikapo Mwaka 2025.

Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo) Prof. Elisante Ole Gabriel amebainisha hayo jana (27.10.2019) katika Wilaya ya Simanjiro Mkoani Manyara wakati alipotembelea kiwanda cha kuchakata mazao ya mifugo cha Rotiana Social Investment ambacho kwa sasa hakifanyi kazi na baadhi ya mitambo yake kuharibika na vifaa vingine kudaiwa kuibiwa na baadhi ya watu waliokuwa wakikisimamia kiwanda hicho.

Prof. Gabriel amesema lengo la Wizara ya Mifugo na Uvuvi ni kuhakikisha inasimamia vyema azma ya serikali kuhakikisha viwanda vya malighafi za mifugo vinafanya kazi na kutaka maafisa hao wa mifugo kushirikiana na maafisa kutoka Taasisi ya Biashara, Viwanda na Kilimo (TCCIA) katika kubaini changamoto mbalimbali zinazovikabili viwanda hivyo.

“Kwa kushirikiana na ofisi ya mkuu wa Mkoa wa Manyara umuliki wa mitambo lazima uweze kufahamika kisheria umekaaje na kuhakikisha viwanda ambavyo vimekuwa vikichakata mazao ya mifugo vinafanya kazi ili mnyororo wa mazao ya mifugo uendelee kufanya kazi na kufikia uchumi wa kati 2025 kupitia viwanda.” Amesema Prof. Gabriel

Kuhusu kiwanda cha Rotiana Social Investment chenye eneo la Hekari 12,500 Prof. Gabriel ameutaka uongozi wa Mkoa wa Manyara kuendelea kufuatilia kwa kina umiliki wa ardhi wa eneo hilo kisheria kutokana na kiwanda hicho kutofanya kazi baada ya kuibuliwa na Taasisi ya Ilaramatak Lorkornei na Stitching Her Groen Wout ya nchini Uholanzi na kufunguliwa kiwanda mwaka 2011 ambapo kwa sasa hakifanyi kazi.

Kiwanda hicho ambacho kina uwezo wa kuchinja ng’ombe zaidi ya 300 kwa siku na pamoja na mifugo mingine wakiwemo mbuzi katibu mkuu huyo ametaka pia uongozi wa Mkoa wa Manayara kufuatilia kwa kina umiliki wa mitambo hiyo kisheria na hatimaye kiwanda hicho kiweze kufanya kazi baada ya taratibu za kisheria kukamilika.

Bibi Mary Kisyoki ambaye amewahi kuwa mmoja wa viongozi wa Shamba la Rotiana linalomiliki kiwanda cha Rotiana Social Invetment ameshukuru uongozi wa Mkoa wa Manyara na TCCIA katika kufuatilia kiwanda hicho ambapo amesema kupitia serikali ya awamu ya tano ataendelea kusimamia ukweli ambao amekuwa akiusimamia katika kulinda mali za kiwanda hicho zinasimamiwa vyema na hatimaye kiweze kufanya kazi.

Amesema katika kipindi chote mara baada ya kiwanda hicho kusimama kufanya kazi amekuwa akihakikisha mali za kiwanda hazizidi kuibiwa au kuharibiwa na baadhi ya watu.

Kwa upande wake Katibu Mtendaji wa TCCIA Mkoa wa Manyara Bibi Mwanahamisi Hussein ametoa wito kwa makatibu wenzake wa mikoa na wilaya kuzidi kutoa ushirikiano kwa serikali na sekta binafsi na kujikita kuangalia fursa na changamtoto zilizopo ili kuweza kuzitatua zikiwemo za wafugaji na kuhakikisha jamii inapata faida kutokana na yale wanayosimamia.

Aidha ameishuru Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwa kuweza kufuatialia masuala mbalimbali kwa kuweza kufanyia kazi yale ambayo yamekuwa yakifikishwa katika wizara hiyo likiwemo la kutofanya kazi kwa kiwanda cha Rotiana Social Investmant suala ambalo amekuwa akilisimamia ili kuhakikisha kiwanda hicho kinafahamika umiliki wake na hatimaye kiweze kufanya kazi.

Mwisho.

Hatima Ya Wanafunzi Wanaotuhumiwa Kumuuwa Mwanafunzi Mwenzao Yaanza Kuonekana

$
0
0
Na Silvia Mchuruza,Bukoba.
KESI ya mauaji inayowakabili wanafunzi wa shule ya Sekondari ya Katoro Islamic ya mkoani Kagera wanaotuhumiwa katika mauaji ya mwanafunzi mwenzao, Mudy Muswadiku imeharishwa hadi Novemba 11 mwaka huu kutokana na upelelezi kutokamilika.

Kesi hiyo ya mauaji namba 18/2019 inayosikilizwa na Hakimu Frola Kaijage imetajwa tena leo (jana) katika Mahakama ya Wilaya Bukoba mkoani Kagera ambapo Wakili wa Serikali, Juma Mahona amesema upelelezi wa kesi hiyo unakaribia mwishoni.

Mahona alisema watuhumiwa hao wakiwa gerezani hivi karibuni walitembelewa na Mkuu wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai Mkoa (RCO) ambapo alisema shauri la watuhumiwa hao liko katika hatua ya mwisho.

“Kwa utaratibu wa makosa ya namna hii RCO anapokamilisha upande wake analeta jarada kwetu na likishafika kwetu tunalipitia ili kuandaa nyaraka kwa ajili ya kupeleka shauri hilo Mahakama Kuu.

Hivyo tumewaambia watuhumiwa wawe wavumilivu, taratibu hizo zitakapokamilika tutawajulisha na kupeleka nyaraka Mahakama Kuu na zikitoka Mahakama Kuu na kurudi Mahakama ya Wilaya hapo ndipo upelelezi utakuwa umekamilika,” Alieleza Mahona.

Kwa upande wa watuhumiwa waliokuwa wakisoma kidato cha nne kufanya mitihani wa Taifa unaotarajia kuanza Novemba 4 mwaka huu, Mahona amesema hawezi kuzungumzia suala hilo maana watuhumiwa waliiomba Mahakama iwaruhusu kufanya mtihani huo.

“Waliiomba Mahakama hivyo wa kulizungumzia suala hilo ni Mahakama yenyewe,” alisema.

Watuhumiwa katika kesi hiyo ya mauaji ya mwanafunzi Mudy aliyekuwa anasoma kidato cha nne katika shule ya sekondari ya Katoro Islamic ya mkoani Kagera ni wanafunzi Sharifu Amri (19), Fahadi Abdulazizi Kamaga (20), Husama Ramadhan (17), Sharifu Huled (19), Abdalah Juma (19) na Hussein Mussa (20), Majaliwa Abud (35) mwalimu na Badru Issa Tibagililwa (27) mlinzi.

Kesi hiyo imehairishwa hadi Novemba 11 mwaka huu ambapo pia itatajwa tena kwani Mahakama hiyo haina mamlaka ya kusikiliza shitaka hilo na watuhumiwa wamerudishwa rumande hadi siku kesi itakapotajwa tena.

Mauji hayo yalitokea Aprili 14 mwaka katika shule ya sekondari ya Katoro Islamic iliyoko katika Halmashauri ya Bukoba Vijijini mkoani Kagera.

Rais Magufuli apokea hati za utambulisho za Mabalozi wa Umoja wa Ulaya, Finland na Rwanda. Ikulu Jijini Dar es Salaam.


Zoezi La Kuchukua Na Kurejesha Fomu Za Kugombea Uchaguzi Serikali Za Mitaa Kuanza Kesho 0ktoba 29,2019

$
0
0
Na.Faustine Gimu Galafoni,Dodoma.
Waziri wa Nchi,Ofisi ya Rais ,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe.Seleman Jafo ametangaza siku maalum ya Uchukuaji wa Fomu za Kuwania uongozi Serikali za Mitaa kuwa ni kuanzia Kesho Oktoba,29,2019 .
 
Akizungumza na waandishi wa habari leo Oktoba ,28,2019 Jijini Dodoma ,Mhe.Jafo amesema zoezi la uchukuaji wa fomu hizo  pamoja na kuzirudisha litadumu kwa muda wa siku saba kuanzia Oktoba 29,2019 hadi Novemba 4,2019.
 
Hivyo Waziri Jafo amesema muda huo ni Muafaka kwa wagombea mbalimbali kuchukua fomu  na kurudisha ndani ya Muda husika kama ilivyopangwa.

Aidha,Waziri  Jafo amewataka wakuu wa wilaya na wakuu wamikoa kote nchini kuhakikisha wanasimamia suala la ulinzi ,usalama na amani katika zoezi hilo.
 
Fomu hizo zitatolewa katika ofisi za wasimamizi  Wa Uchaguzi ambao ni watendaji wa mitaa na  vijiji.

Hata hivyo,Waziri Jafo amesema nafasi mbalimbali zimezibwa pale ambapo pako wazi   kwa watendaji wa Mitaa na wapo watumishi wa umma wamekaimu nafasi hizo.

Ikumbukwe kuwa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa unatarajia kufanyika Novemba ,24,2019.

Waitara Amewaomba Wananchi Kuchagua Viongozi Wenye Hofu Ya Mungu

$
0
0
Na Paschal Dotto-MAELEZO.
Katika kuelekea uchaguzi wa Serikali za Mitaa ambao utafanyika nchi nzima Novemba 24, 2019, Naibu Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mhe. Mwita Waitara amewaomba viongozi wa Dini kuwahamsisha wananchi kuchagua viongozi weneye Mungu.

Akizungumza katika Mkutano wa Kujadili namna Taasisi za Dini zinzvyochangia Ujenzi wa Uchumi wa Viwanda uliofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Julius Nyerere (JNICC) Jijini Dar es Salaam, Mhe. Waitara amesema kuwa ni muhimu kuwachagua viongozi wenye hofu ya Mungu na waadilifu kwa wananchi ili kuiunganisha Serikali katika kuleta maendeleo kwa wananchi.

“Viongozi wa Dini nyie mnahubiri amani na haki, watu wakipata haki maana yake nchi inatulia, kwa hiyo hakikisheni mnawahubiria watu wenu kuhusu kuchagua viongozi walio na hofu ya Mungu ambao pia ni waadilifu kwa wananchi ili kuondoa migogoro mbalimbali ambayo imekuwa ikisababishwa na viongozi wala rushwa kwenye mitaa yetu ikiwemo ile ya ardhi”, ameeleza Mhe.Waitara.

Waziri Waitara alisema kuwa viongozi waadilifu huwa wanawajibika bila shida yeyote, kwa hiyo ni muhimu kuunganisha juhudi za Mhe. Rais John Pombe Magufuli kwa wananchi kwani uwajibikaji wake ni mkubwa katika kuwaletea maendeleo wananchi.

Alianisha sifa nzuri za kiongozi kuwa ni yule mwenye maono, maamuzi sahihi, anayesimamia maono na maamuzi yake, sifa ambazo Rais Magufuli anazo, kwa hiyo ili kuendelea kuleta maendeleo ni lazima viongozi wa Serikali za Mitaa ambako maendeleo yaanzia wawe waadilifu na wenye hofu ya mungu.

Waziri Waitara alisema kuwa mpaka Oktoba 17, 2019 wananchi milioni 19,686,000 walikuwa wamejiandikisha, sawa na asilimia 86 ikilinganishwa na mwaka 2014 ambapo wananchi Milioni 11 walijiandikisha sawa na asilimia 63.

Aidha Waitara alisema kuwa katika hatua za uchaguzi huo wagombea wataanza kuchukua fomu za kugombea kuanzia oktoba 29, 2019 na kwamba itakapofika Novemba 5, 2019 wasimamizi wa Uchaguzi watabadika majina ya wagombea kwa hiyo viongozi wa dini wanatakiwa kuwasaidia wananchi kujua kiongozi mwadilifu na pia kusali kwa ajili ya kupata kiongozi bora katika mitaa mbalimbali nchini.

Waziri Waitara alisema kuanzia Novemba 17 hadi 23, 2019, itakuwa ni muda wa kampeni ambapo amewataka wagombea kuomba kura kwa kujenga hoja kwa wananchi na kuwataka Wakuu wa Mikoa na Viongozi wa Dini kusimamia kikamilifu suala ya amani wakati wa kampeni.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda alisema kuwa watu wanatakiwa kubadilika na kufuata kasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na wasaidizi wake kwani wanakimbizana kuwaletea maendeleo wananchi.

“Kuna watu bado hajabadilika na hawataki kubadilika, lakini ukiangalia makusudi ya Rais wetu, Makamu wake, Waziri Mkuu na Mawaziri wanakimbizana kuleta matokeo kwa wananchi, lakini huku chini ni shida kidogo, kwa hiyo nawaomba viongozi wetu wa Dini tuwahamasishe wananchi wetu Novemba 24, 2019 wajitokeze kuwachagua Wenyeviti wa Serikali za Mitaa wenye hofu ya Mungu”, alieleza Makonda.
 

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumanne October 29

Mwakyembe: Ni heshima kutembelewa na Miss World 2018

$
0
0
Na Eleuteri Mangi, WHUSM, Arusha
Ni heshima kubwa kwa Tanzania kutembelewa na Mwenyekiti na Mwendeshaji wa Shindano la Miss World Bi Julia Morley pamoja na Mshindi wa Miss World 2018 Vanessa Ponce.
 
Hayo yamesemwa na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe wakati wa uzinduzi wa taulo za kike zinazojulikana kama Uhurupads uliofanyika leo katika shule ya sekondari Moshono iliyopo jijini Arusha.
 
“Ujio wao leo hapa Arusha, ni heshima kwa taifa. Katika mataifa yote duniani, wameichagua Tanzania, hii ni heshima kubwa na wametuletea zawadi ya Uhurupads ambazo zitawaweka huru watoto wetu katika kutimiza ndoto zao hasa wanapokuwa shuleni” amesema Waziri Dkt. Mwakyembe.

Aidha, Waziri Dkt. Mwakyembe amesema kuwa bidhaa ya taulo hizo alizozindulia  ni rafiki kwa mazingira kwa kuwa zinaweza kutunzwa mahali popote na zisiwe na madhara kwenye mazingira kwa kuwa haina  mchanganyiko wowote wa plastiki. Taulo hizo zinazotengenezwa na kikundi cha wanawake 12 kiachojulikana kama timu ya Uhuru Kit Ltd ambao wanaunga mkono juhudi za Serikali katika kutunza mazingira kwa marufuku ya matumizi ya mifuko ya plastiki nchini Julai, 2019.
 
Katika kuhakikisha Tanzania inatumia vema fursa ya ujio wa Mshindi wa Miss World 2018 Vanessa Ponce wa Mexico, Dkt. Mwakyembe amesema kuwa Serikali itaandaa ziara maalum kwa Uongozi wa Miss World ukiongozwa na Mwenyekiti na Mwendeshaji wa Shindano la Miss World Bi Julia Morley kutembelea vivutio mbalimbali vya utalii nchini ikiwemo mbuga za Serengeti, hifadhi ya Ngorongoro pamoja na mji wa kihistoria wa Zanzibar.
 
“Uwepo wa Miss World 2018 Vanessa Ponce, dunia nzima macho yao yapo hapa nchini, ni vema kuitangaza nchi yetu kimataifa kupitia ujio wake” amesema Waziri Dkt. Mwakyembe.

Kwa upande wake Mwenyekiti na Mwendeshaji wa Shindano la Miss World Bi Julia Morley amesema kuwa amefurahishwa na hatua zinazochukuliwa na Serikali ya Tanzania ambapo ni mara ya kwanza kwake kuja nchini.
 
“Nimefurahi sana Tanzania ni nchi nzuri, nilipopanda ndege kuja hapa nilipata matangazo yanayosisitiza marufuku ya kutumia mifuko ya plastiki, Serikali imefanya vizuri kujali kutunza mazingira” alisema Bi Julia Morley.

Nao Miss World 2018 Vanessa Ponce kutoka Mexico pamoja na Miss Tanzania 2019 Sylivia Sebastian wamesema kuwa urembo ni heshima, UhuruPads zitawasaidia wasichana kupata elimu wakiwa huru wakizingatia kauli mbiu ya ‘Uzuri wenye malengo.’ 
 
Uzinduzi huo ulihudhuriwa na Mwenyekiti na Mwendeshaji wa shindano la Miss World Bi Julia Morley, Mshindi wa Miss World 2018 Vanessa Ponce kutoka Mexico, Mshindi wa Miss Tanzania 2019 Sylivia Sebastian Bebastian Bebwa pamoja, mwandaaji wa Mashindano ya Miss Tanzania Bi. Basilla Mwanukuzi pamoja na walimu na wanafunzi wa shule ya sekondari Moshono ya jijini Arusha.

Umoja wa Ulaya waurefusha tena muda wa Brexit

$
0
0
Umoja wa Ulaya umekubali  kuchelewesha kwa muda wa miezi mitatu Uingereza kujitoa kutoka Umoja huo hadi Januari 31.

Kiasi siku tatu kabla ya tarehe ya mwisho ya Uingereza kujitoa kutoka Umoja wa Ulaya hapo Oktoba 31, mchakato wa Brexit bado haujulikani mwelekeo wake wakati wanasiasa wa Uingereza hawako karibu ya kufikia muafaka juu ya vipi, lini na hata iwapo hatua ya kuachana na Umoja wa Ulaya itawezekana.

Mataifa 27 ya Umoja wa Ulaya yanamefikia makubaliano kuchelewesha Brexit hadi Januari 31, pamoja na uwezekano wa Uingereza kujitoa mapema iwapo bunge la Uingereza litaidhinisha makubaliano ya kujitoa.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images