Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Tangazo la Nafasi 16 za Kazi toka Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA)

$
0
0
On behalf of Tanzania Civil Aviation Authority (TCAA), Public Service Recruitment Secretariat invites qualified Tanzanians to fill 16 vacant posts mentioned below.

1.0 THE TANZANIA CIVIL AVIATION AUTHORITY, (TCAA)
The Tanzania Civil Aviation Authority, (TCAA) was established by the enactment of the Tanzania Civil Aviation Authority Act 2003 Cap 80 (R.E 2006) to regulate the civil aviation industry in the United Republic of Tanzania in order to ensure effective implementation of Standards and Recommended Practices (SARPs) as provided in the Annexes of the International Civil Aviation Organization (ICAO). The Authority is also responsible for economic regulation of the activities of persons and institutions providing air transport services and aeronautical airport services. In addition the Authority provides air navigation services in Tanzania.

1.1 AIRWORTHINESS DEVELOPMENTAL INSPECTOR - 1 POST
1.1.1 DUTIES AND RESPONSIBILITIES
i. To assist in enforcement of regulatory requirements and report deficiencies to the Supervisor;
ii. To assist in accident/incident and complaint investigations;
iii. To assist in recertification of air operators and Approved Maintenance Organizations;
iv. To assist in the review of manuals (maintenance, flight) and other documents associated with certification requirements of air operators for accuracy and compliance with Civil Aviation Regulations;
v. To assist in conducting inspections and evaluation of Approved Maintenance Organizations under supervision of a qualified inspector;
vi. To assist in evaluation of applications for issue/renewal of certificates of airworthiness;
vii. To assist in evaluation of applications for AME license issue/extension applications in accordance with procedures in Airworthiness Orders as specified in the Civil Aviation (Personnel Licensing) Regulations and Annex 1 to ICAO convention;
viii. To assist in carrying out continuous programmed surveillance to aircraft operations, air operators and approved maintenance organizations and make appropriate recommendations to the supervisor; and
ix. To assist in carrying out accident and incident investigations in accordance with procedures.

1.1.2 QUALIFICATIONS AND EXPERIENCE
i. Bachelor Degree either in Aeronautical, Mechanical, Electrical, Electronic or Telecommunication. Must have (3) three years working experience in an Aircraft Maintenance Organization as Aircraft Maintenance Engineer.
ii. For graduates, except for Aeronautical Engineers, they should have attended or be provided with a basic training in Aircraft Maintenance Engineering;
iii. For equivalent professional qualifications they should possess Aircraft Maintenance Engineer’s Licenses with ratings or appropriate approvals, commensurate with their job responsibilities, i.e., Category A or C (Mechanical) Licences with airframe and power plant ratings, category X or R (Avionics) Licence with ratings in Electrical, Instrument or Radio.

1.1.3 REMUNERATION
Attractive remuneration package in accordance with the institutions salary TCAA.SS 10

1.2 AERODROME AND GROUND AIDS DEVELOPMENTAL INSPECTOR - 2 POSTS
1.2.1 DUTIES AND RESPONSIBILITIES
i. To conduct guided safety oversight of aerodromes including certification and licensing of aerodromes;
ii. To assist assessment of applications for the initial and renewal of Aerodrome certificates and licences; and
iii. To perform any other related duties as may be assigned by immediate supervisor.

==>>Endelea Nalo kwa Kubofya Hapa

Tanzania yaitaka dunia kuiondolea vikwazo vya kuichumi Zimbabwe bila masharti

$
0
0
Na Mwandishi wetu,
Tanzania imelaani vikali vikwazo ilivyowekewa nchi ya Zimbabwe na kuitaka dunia kuiondolea nchi hiyo vikwazo hivyo bila masharti kwani haviaathiri tu Zimbabwe bali huathiri pia nchi wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC).
 
Kauli ya kulaani vikwazo hivyo imetolewa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) wakati alipokuwa akiwasilisha mada katika kongamano maalum kuhusu "vikwazo vya kiuchumi na hatma ya Afrika: Uzoefu wa Zimbabwe" leo Jijini Dar es Salaam.
 
Prof. Kabudi alisema kuwa kitendo cha dunia kuiwekea vikwazo nchi ya Zimbabwe, hakuiathiri tu Zimbabwe bali hata nchi wanachama wa SADC. 

"Tulikubaliana katika mkutano wetu wa mwezi Augosti kuwa leo tarehe 25/10/2019 kuiambia dunia kuiondolea Zimbabwe vikwazo vya kiuchumi ilivyoviwekea bila masharti..…leo siyo siku ya kuomba wala kukumbushana bali leo ni siku ya kuiambia dunia rasmi iiondolea Zimbabwe vikwazo vya kuichumi" Alisema Prof. Kabudi
 
Waziri Kabudi aliongeza kuwa "vikwazo ilivyowekewa Zimbabwe ni batili na kama Marekani na Umoja wa Ulaya wana hoja ya msingi wapeleke azimio katika baraza kuu la umoja wa mataifa na ndiyo maana katika mkutano wa SADC tuliazimia kulaani vikali Zimbabwe kuwekewa vikwazo vya kiuchumi na kuitaka dunia kuiondelea Zimbabwe vikwazo hivyo bila masharti,".
 
Pia tunasahau sababu ya msingi iliyoifikisha Zimbabwe ktk maamuzi iliyoyachukua, maamuzi hayo kiini chake kikubwa na suala la ardhi ambapo suala la ardhi ni miongozni mwa masuala ambaya hadi Zimbabwe inapata uhuru lilikuwa halijapatiwa ufunguzi. 
 
Kwa mujibu wa Prof. Kabudi, mzizi wa mambo yote haya ni sheria ya kibaguzi iliyopitishwa na waingereza kwa kusingizia kuwa wameipa Zimbabwe utawala wa ndani mwaka 1923 lakini wao walibaki na mamlaka yote juu ya ardhi. Sheria ile ilikuwa ya kibaguzi kwani ilichukua zaidi ya nusu ya ardhi yote ya Zimbabwe.
 
"Ni wajibu wetu sisi kama Tanzania kuendelea kusimama na Zimbabwe katika kuhakikisha kuwa ni jukumu letu sote kuhakikisha kuwa Zimbabwe inaondolewa vikwazo vya kiuchumi ilivyowekewa" Alisema Waziri Kabudi na kuongeza kuwa vikwazo hivyo haviiathiri tu Zimbabwe kiuchumi bala hata nchi wanachama wa SADC wanaathirika hivyo tunaitaka dunia kuindolea Zimbabwe vikwazo hivyo.
 
Katika hatua nyingine, Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamiii, Jinsia na Wazee, Prof. Jingu alisema kuwa diplomasia ya uchumi imeiwezesha Tanzania kuingia katika uwekezaji, kusaini mkataba, msaada au masoko hivyo tunapaswa kuhakikisha kuwa masuala ya kiuchumi yanapewa uzito wa hali ya juu.
 
"Vita ya kiuchumi imekuwa na athari mbalimbali kwa wananchi kijamii, kisiasa na kiuchumi kwa ujumla….vita hii ya Zimbabwe kuwekewa vita ya kiuchumi imeleta athari nyingi baadhi ni kukusekana kwa maji safi na salama, kukosekana kwa nishati ya uhakika na ongezeko la mfumuko wa bei ambao umeathiri si tu Zimbabwe, bali hata nchi wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC). 
 
Nae Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango alisema kuwa vikwazo vya kiuchumi dhidi ya Zimbabwe vimesababisha anguko kubwa na adha kwa wanachi masikini tena wasio na hatia hivyo ni vyema Afrika itambue kuwa vikwazo hivi vinaweza kutumika kama fursa ya kukuza biashara na uwekezaji miongoni mwa nchi za Afrika. 
 
"Ni muhimu nchi zetu za Afrika zifanye uchambuzi mapema ili kubaini maeneo ambayo ya kimkakati ambayo ni dhaifu na yanaweza kuwekewa vikwazo, na moja ya eneo hilo ni umiliki wa hisa katika makampuni hasa yale makubwa ya kimkakati ili tuweze kuchukua hatua stahiki za kujihami kwa kushirikisha sekta binafsi," Alisema Dkt. Mpango
 
Aliongeza kuwa, vikwazo dhidi ya Zimbawe vimewekwa kimabavu kwani havikufuata taratibu, hivyo ni wajibu wetu sisi kama nchi za SADC kusimama na Zimbabwe kuhakikisha kwamba Wazimbabwe wanarudishiwa ardhi yao na kuondolewa vikwazo vya uchumi.
 
Awali, Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Prof. William Anangisye alisema kuwa Zimbabwe inakabiliwa na vikwazo vya kiuchumi kutokana na maazimio yaliyochukuliwa na nchi za Uingereza, Marekani na Umoja wa Ulaya mwaka 2001. 
 
"Vikwazo hivi vimeathiri sana uwezo wa Serikali ya Zimbabwe kiuchumi hususani fursa za mikopo, kupata nafuu ya madeni, na zaidi kupata uwezo wa kutoa huduma kwa jamiii. Zimbabwe inapita katika kipindi kigumu cha msukosuko wa kiuchumi uliogubikwa na mfumuko wa bei, upungufu mkubwa wa bidhaa, chakula na huduma muhimu katika jamii" Alisema Prof. Anangisye
 
Kwa mujibu wa Prof. Anangisye vikwazo vya kiuchumi vipo katika makundi ambayo ni vikwazo vya biashara ambavyo vinalenga mauzo ya nje na manunuzi ya bidhaa za nchi kama ambavyo vilivyowahi kuwekwa na Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, vikwazo vya kifedha ambavyo vinalenga sekta, taasisi na mfumo mzima wa kifedha ikiwemo misaada, mikopo na mfumo mzima wa fedha za kigeni, na vikwazo vyenye malengo maalum yaani " Targerted Sanctions".
 
Kongamano hilo lilihudhuriwa na vongozi mbalimbali waandamizi wa Serikali, vyma vya siasa na ujumbe wa balozi za nchi mbalimbali hapa nchini. 
 
Katika kongamano hili, Serikali ya Chini Ikongozwa na Balozi wake nchini Tanzania, Balozi Wang Ke alisema kuwa serikali ya China inasimama pamoja na nchi za SADC katika kuhakikisha kuwa Zimbabwe inaondolewa vikwazo vya kiuchumi.
Mwisho….


Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) Lamteua Etienne Ndayiragije Kuwa Kocha Mkuu Taifa Stars

Rais Magufuli Na Mkewe Watoa Pole Kwa Familia Ya Mmoja Wa Waasisi Wa Vyama Vingi Nchini Marehemu Mzee James Mapalala

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisaini kitabu cha maombolezo nyumbani kwa Mwanasiasa Mkongwe na mmoja wa Waasisi wa Mfumo wa Vyama vingi nchini Marehemu James Mapalala Osterbay jijini Dar es salaam aliyefariki dunia Oktoba 23,2019 katika Hospital ya Kairuki jijini Dar es salaam alipokuwa akipatiwa matibabu.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimsalimia Bi. Hannah Mapalala Mke wa Marehemu James Mapalala alipokwenda na Mkewe Mama Janeth Magufuli kutoa pole nyumbani kwa Mwanasiasa Mkongwe na mmoja wa Waasisi wa Mfumo wa Vyama vingi nchini Osterbay jijini Dar es salaam aliyefariki dunia Oktoba 23,2019 katika Hospital ya Kairuki jijini Dar es salaam alipokuwa akipatiwa matibabu.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumamosi ya October 26

Waziri Wa Kilimo: Makamishna Wa Tume Ya Maendeleo Ya Ushirika Hawatekelezi Majukumu Yao Ipasavyo, Ubadhilifu Umekithiri

$
0
0
Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo-Dodoma
Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga (Mb) amesema kuwa Makamishana wa Tume ya Maendeleo ya Ushirika nchini hawatekelezi majukumu yao ipasavyo.

Amesema kuwa Mali zinaibiwa za wananchi, watu wanauziana viwanda huku Ubadhilifu ukiwa umekithiri kuliko kawaida lakini bado kuna tume ya Maendeleo ya Ushirika.

Mhe Hasunga ameyasema hayo wakati akizungumza kwenye kikao kazi cha Makamishna wa Tume hiyo katika ukumbi wa Hazina Jijini Dodoma leo tarehe 25 Octoba 2019.

Waziri Hasunga amesema kuwa jumla ya Bilioni 124 zimeibiwa kwenye vyama vya ushirika lakini hakuna hatua zilizochukuliwa, "Mnataka mpaka kuwe na posho ndipo kamati ikutane kuona ulazima wa kusimamia fedha na Mali za ushirika" Alihoji Mhe Hasunga

Aliongeza kuwa wizi wa mali na fedha hizo za ushirika ni ishara ya makamishna kutofanya majukumu yao ipasavyo hivyo jambo hilo linapelekea Wanachama kuendelea kuteseka.

"Nasikitika sana Watu walioaminiwa na kupewa dhamana wameshindwa kutekeleza majukumu yao, kwenye zao la ufuta pekee zimeibiwa Bilioni 2.5 lakini wahusika wanadunda mtaani kadhalika mazao kama ya korosho na Pamba ambapo hakuna Ushirika badala yake kuna madalali tu" Alisema

Mhe Hasunga ameongeza kuwa hakuna sababu ya kuwa na Tume ya Ushirika isiyotekeleza majukumu yake ipasavyo huku akiongeza kuwa serikali inataka kujenga ushirika lakini kuna watu kazi yao ni kubomoa, na kuweka urasimu katika utendaji.

Waziri Hasunga amemtaka Mwenyekiti wa Tume ya Maendeleo ya ushirika Dkt Titus Kanani kuchukua hatua za haraka kwa watendaji wote wa Tume hiyo ambao wameshindwa kutekeleza majukumu yao ipasavyo.

Mhe Hasunga amesema kuwa endapo ushirika utasimamiwa vizuri wananchi watakuwa na maendeleo maradufu yatakayopelekea Taifa kuendelea mbele kiuchumi.

Kadhalika ametoa nafasi ya ziada kwa Tume hiyo kufanya kazi kwa bidii na kuonyesha matokeo makubwa ya uwajibikaji vinginevyo ametishia kuivunja tume hiyo.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Tume ya Maendeleo ya Ushirika Dkt Titus Kamani amempongeza Waziri wa Kilimo kwa kukubali kushiriki katika kikao hicho huku Kamishna wa Tume hiyo Mudhihir M. Mudhihir akizungumza kwa niaba ya Makamishna wengine amehakikisha kuwa Tume hiyo itatekleza majukumu yake kwa weledi mkubwa.

Kilele Cha Wiki Ya Kisheria Wananchi 1018 Wapatiwa Msaada Kisheria

$
0
0
Na Stella Kalinga, Simiyu RS
 Msajili wa Taasisi za watoa huduma za msaada wa kisheria kutoka Wizara ya Katiba na Sheria, Bi. Felistas Mushi amesema  takribani wananchi 1018  wamepata huduma ya msaada wa kisheria katika maadhimisho ya wiki ya msaada wa kisheria tangu Oktoba 21, 2019 mpaka Oktoba 25, 2019, yaliyofanyika Kitaifa katika Uwanja wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi Mkoani Simiyu.

Mushi ametoa taarifa hiyo katika Kilele cha Maadhimisho hayo, Oktoba 25, 2019 ambapo amebainisha kuwa asilimia kubwa ya matatizo ya kisheria yalihusu migogoro ya ardhi na yameshafikishwa mahakamani  na yako katika hatua mbalimbali.

Amesema huduma walizopata wananchi katika wiki ya msaada wa kisheria ni pamoja na huduma za usuluhishi, ushauri wa kisheria, kuandaa nyaraka na maelekezo ya sehemu  sahihi ya kwenda pindi wanapopata migogoro.

“Mbali na huduma kwa wananchi mafunzo yametolewa kwa makundi mbalimbali ya watumishi wa umma wapatao 1300 wakiwemo, wajumbe wa menejimenti ya sekretarieti ya mkoa, wajumbe wa kamati ya parole, wajumbe wa mabaraza ya ardhi ya kata na vijiji, wajumbe wa kamati ya maadili ya mahakimu, askari polisi na magereza, wajumbe wa kamati za shule na watendaji wa vijiji na kata, “ alisema Mushi.

Kwa upande wake Hakimu Mary Nyangusi akimwakilisha Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya ya Bariadi, Mhe. Mary Mrio, ametoa wito kwa wananchi kuandika wosia ili kupunguza migogoro ya ardhi ambayo mingi inatokea mara nyingi wanaume( baba) wanapofariki na wake(mke) na watoto kudhulumiwa haki zao.

Adam Kisinza ni Mmoja wa wananchi waliofika kupata msaada wa kisheria katika maadhimisho hayo amesema, “nashukuru nimeelewesha ninachotakiwa kufanya maana kule kwetu baba mwenye mji anapokuwa amefariki wakabaki watoto na mama, wanakuwa hawana mamlaka juu ya mali iliyoachwa maana kila mtu anataka achukue chake wakati mzee hakuacha hata  wosia”.

Akifunga Maadhimisho ya Wiki ya Msaada wa Kisheria,Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka amesema ni vema wizara ya katiba na sheria ikaona umuhimu wa kupeleka maadhimisho ya wiki ya msaada wa huduma za kisheria katika maeneo ambayo hayajafikiwa na huduma hiyo, ili wananchi wapate uelewa wa masuala ya kisheria na kupata matokeo yatakayoonekana.

Maadhimisho ya Wiki ya Msaada wa Kisheria Kitaifa mwaka 2019 yanaongozwa na Kauli Mbiu:- “Msaada wa Kisheria kwa Maendeleo Endelevu”ambapo kilele cha maadhimisho haya kimeenda sambamba na uzinduzi wa Jarida la Msaada wa Kisheria, ambalo limezinduliwa na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka.

Ugonjwa wa Zinaa wa Kisonono (gonorrhea) : Dalili Zake, Madhara Yake Na Jinsi Ya Kujikinga

$
0
0
Kati ya magonjwa yanayoathiri watu wengi sana duniani ni magonjwa ya zinaa. Haya ni magonjwa yanayoambukizwa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine kupitia vitendo vya ngono. 

Vitendo hivi vya ngono vinaweza kuwa kujamiana, kupiga denda (kissing), vitendo vya ngono kwa kutumia mdomo (oral genital sex), kujamiana kupitia njia ya haja kubwa (anal sex) iwe kwa mwanamume na mwanamke au kati ya wanaume wenyewe na hata wale wanaotumia vifaa vya kufanyia ngono (vibrators). 

Magonjwa ya zinaa huathiri sana watu walio katika umri wa miaka 15 – 24 lakini hata kwa watu wengine ambao wana umri chini au zaidi ya huu niliotaja pia yanaonekana kwa wingi.

Kuna magonjwa ya zinaa zaidi ya ishirini yanayotambulika duniani, baadhi ya magonjwa ya zinaa ni
  1.  Kisonono (Gonorrhoea – “Gono” kama wengi wanavyopenda kuita kwa kifupi).
  2.     Chlamydia
  3.     Kaswende (Syphillis)
  4.     Human papilloma virus (HPV)
  5.     HIV/AIDS (Ukimwi/Upungufu wa kinga mwilini)
  6.     Hepatitis B, C, A
  7.     Herpes virus
  8.     Trichomoniasis
  9.     Bacteria Vaginosis
  10.     Pubic lice (chawa kwenye nywele za kinena)
  11.     Chancroid
Magonjwa mengi ya zinaa yanatibika lakini kuna baadhi ambayo hayana tiba ya uhakika kama HPV, Hepatitis B na C, na HIV. Mengine yameanza kuwa sugu kutokana na matumizi ya dawa za antibiotics bila mpangilio, magonjwa hayo ni kama gono (gonorrhoea) na nk.
 
Visababishi vya magonjwa ya zinaa
  1. Vitendo vya ngono kama nilivyoeleza hapo awali
  2. Kuanza vitendo vya ngono mapema au wakati wa umri mdogo
  3. Kuwa na wapenzi wengi
  4. Kufanya mapenzi ambao sio salama
  5. Maambukizi kupitia michibuko au sehemu zilizokatika kwenye ngozi kwa kugusana na majimaji ya aina yoyote yanayotoka kwa mtu mwenye ugonjwa wa zinaa kama damu, shahawa nk. Hii inaweza kutokea bila mtu kujua kwani mara nyingi dalili za magonjwa ya zinaa zinakuwa hazionekani kwa wanawake na hata baadhi ya wanaume.
Watu wengi huhisi kitendo cha kula denda (kissing) ni salama lakini si kama wanavyofikiria kwani baadhi ya magonjwa kama kaswende, herpes nk, yanaweza kuambukizwa kupitia njia hii. 

Soma pia:Tatizo la Kutokwa na usaha Wakati wa Kukojoa 

Kondomu husaidia kupunguza maambukizi ya magonjwa ya zinaa kama gono, Chlamydia lakini sio kinga muafaka dhidhi ya magonjwa ya zinaa kama kaswende, genital herpes, genital warts, na magonjwa ya upungufu wa kinga mwilini (AIDS).

Kisonono (gonorrhea) ni nini?
Kisonono ni ugonjwa kati ya magonjwa ya zinaa unaosababishwa na bakteria aina ya Neisseria gonorrhoeae, bakteria ambao hukuwa na kuzaliana kwa haraka katika sehemu zenye unyevunyevu na joto mwilini kama kwenye shingo ya kizazi kwa wanawake (cervix), mirija ya kupitisha mkojo au shahawa (urethra), mdomoni na kwenye puru. Maambukizi mengi kwa wanawake hutokea kwenye shingo ya kizazi (cervix). 

Asilimia 75 ya ugonjwa wa gono hutokea kwa watu wenye umri wa miaka 15 – 29, wanawake walio katika umri wa miaka 15 -19 na wanaume walio katika umri wa miaka 20 – 24 wako kwenye hatari zaidi ya kupata ugonjwa huu.
 
Ugonjwa huu huambukizwa vipi?
Ugonjwa huu huambukizwa kupitia vitendo vya ngono kupitia uke, njia ya haja kubwa (anus), kupitia mdomoni (oral sex). Ugonjwa unaweza kujitokeza kwenye sehemu za kujamiana, kwenye mdomo na kwenye puru (rectum). 

Soma Pia: Ugonjwa wa Zinaa wa Kaswende (Syphilis) : Dalili Zake, Madhara Yake Na Jinsi Ya Kujikinga 

Ugonjwa wa gono huonekana sana kwa vijana, watu wenye maisha duni kiuchumi, watu wanaoishi mijini, watu weusi na watumiaji madawa ya kulevya.
 
Dalili za ugonjwa wa kisonono
Dalili za ugonjwa wa kisonono huanza kujitokeza kuanzia siku ya 2 hadi ya 7 baada ya mtu kupata maambukizi na huweza kuchelewa kwa wanawake. Dalili ni kama zifuatazo

Kwa wanaume
  1. Kuhisi kama kichomi wakati wa kukojoa (burning sensation)
  2. Kutokwa na majimaji ya njano au meupe au ya kijani kutoka kwenye uume yanayoambatana na maumivu makali sana
  3. Wakati mwengine maumivu au kuvimba kwa korodani (swollen testicles)
  4. Maambukizi yakiwa kwenye puru (rectum) huambatana na maumivu wakati wa kujisaidia haja kubwa, kuwashwa sehemu za haja kubwa, na hata haja kubwa inaweza kutoka ikiambatana na damu, hii inatokea kwa wanaume na wanawake.
Kwa wanawake
Dalili kwa wanawake huwa si nyingi lakini wanawake wengi hawaonyeshi dalili zozote
  1. Maumivu au kuhisi kama kichomi wakati wa kukojoa
  2. Kuongezeka kwa kutoka majimaji kutoka kwenye tupu ya mwanamke ambayo ni ya njano au yamechanganyika na damu
  3. Kutokwa na damu kupitia tupu ya mwanamke kabla ya hedhi kufika.
  4. Kutokwa na damu baada ya kujamiana au baada ya tendo la ndoa
  5. Kichefuchefu
  6. Homa (fever)
  7. Kutapika
Vipimo vya ugonjwa wa kisonono
  1. Swab for culture – Kipimo hiki hufanyika maabara kwa kupandikiza bakteria baada ya kufuta sehemu za siri kwa kutumia swab ili kuona kama kuna bakteria wanaosababisha gono.
  2. Polymerase Chain Reaction (PCR)– Kipimo cha kuangalia vina saba (DNA) ya bakteria, ni ghali sana.
Tiba ya ugonjwa wa kisonono ni nini?
Tiba ya gono inahusisha na tiba ya ugonjwa wa Chlamydia kwani mara nyingi magonjwa haya huambatana kwa pamoja.Tiba hutegemea na umri wa mgonjwa na kama mtu ni mjamzito au la. 

Tiba ya gono ambayo sio sugu iliyo kwenye shingo ya kizazi (cervix), urethra na puru, dawa zinazotumika ni aina za cephalosporin dozi moja pamoja na dawa za aina ya macrolide antibiotics (mfano azithromycin) na za jamii ya penicillin (mfano doxycyclin) ili kutibu ugonjwa wa chlamydia. Mara nyingi kwa wale chini ya miaka 18 na wanawake wajawazito, hutibiwa kwa kuchomwa sindano.

Soma Pia: Saratani ya tezi dume : Madhara Yake, Dalili Zake, Chanzo na Tiba Yake

Fuata ushauri wa daktari kabla ya kutumia dawa hizi kwani dawa nyingi zina madhara kwa wajawazito (mfano doxycyclin). Ushauri nasaha hutolewa kwa wapenzi wote wawili na ni vizuri wapenzi wote wawili kutibiwa hata kama mmoja hana dalili za ugonjwa huu.
 
Madhara ya ugonjwa wa kisonono
  1. Kutoweza kuzaa kwa mwanamke (tasa) au kutoweza kutungisha mimba kwa mwanamume (infertility)
  2. Huweza kuathiri moyo (heart valves), ubongo,ngozi nk ambayo ni hatari sana kwa mtu yoyote.
  3. Madhara kwenye sehemu za maungio au jointi (joint inflammation)
  4. Kwa wanawake wale ambao hawajatibiwa wanaweza kupata ugonjwa wa PID (Pelvic Inflammatory Disease) ambao huongeza asilimia ya mwanamke kuwa tasa.
  5. Wale wanawake ambao ni wajawazito na wameambukizwa gono wako kwenye hatari ya mimba kutoka au kuzaa mapema kabla mimba haijatimiza umri wake (preterm labor).
  6. Kwa wale wanaoambukizwa gono kipindi cha kukaribia kujifungua, wanaweza kuwaambukiza watoto wao na hivyo watoto kupata ugonjwa wa uti wa mgongo (meningitis), kuwa kipofu (blindness), homa ya mapafu (pneumonia) na ugonjwa wa mifupa (septic arthritis).
Kinga ya kisonono
  1. Kutumia kondomu wakati wa kujamiana
  2. Kuwa na mpenzi mmoja mwaminifu
  3. Kuacha vitendo vya ngono kama matumizi ya vifaa vya ngono hasa kwa wanawake mfano vibrators nk.
  4. Kwa wanawake wajawazito – Hakikisha unahudhuria kliniki mapema ili upate kuchunguzwa na kupatiwa tiba muafaka kama utagundulika na ugonjwa wa gono au ugonjwa mwengine wowote.
  5. Wanawake wajawazito wanashauriwa kujifungulia hospitali ili kama mtoto ameathirika na gono apate matibabu ya haraka baada ya kuzaliwa kuepusha kuwa kipofu.
  6. Epuka kufanya ngono na mtu aliyeambukizwa gono.

Hukumu ya Jamal Malinzi na wenzake watatu Kutolewa Mwezi Ujao

$
0
0
Hatima ya Rais wa zamani wa Shirikisho la Soka (TFF), Jamal Malinzi na wenzake watatu kurudi uraiani au la itajulikana Novemba 7,mwaka huu watakaposomewa hukumu.

Malinzi na wenzake wanakabiliwa na mashtaka 20 yakiwamo ya kula njama, kughushi, kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu na utakatishaji wa fedha wa USD 173,335.

Uamuzi huo ulisomwa jana mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu Huruma Shaidi, baada ya Hakimu Mkazi Maira Kasonde aliyesikiliza kesi hiyo kuwa na udhuru.

Hakimu alisema baada ya kusikiliza ushahidi wa mashahidi wa pande zote mbili, mahakama yake itatoa hukumu mwezi ujao.

Wakili wa Serikali Ester Martin alidai kuwa kesi hiyo ilipangwa kwa ajili ya kupanga tarehe ya hukumu na kwamba upande wa Jamhuri uko tayari.

Hakimu Shaidi alisema kesi hiyo itasomwa hukumu tarehe iliyopangwa na kuamuru washtakiwa warudishwe mahabusu.

Jeshi la Polisi Lazuia Mkutano wa Mchungaji Peter Msigwa

$
0
0
Jeshi la Polisi mkoani Iringa, limezuia mkutano wa Mbunge wa Iringa Mjini (Chadema), Mchungaji Peter Msigwa, kwa madai ya kutokuwapo kwa askari wa kutosha wa kulinda mkutano huo.

Taarifa za kuzuiwa kwa mkutano huo zilisambaa kwenye mitandao ya kijamii, ikionyesha barua ya zuio kutoka polisi. Mkutano huo ulikuwa ufanyike katika viwanja vya Mwembetogwa.

Kamanda wa Polisi Mkoani Iringa, Juma Bwire, alisema marufuku hiyo ilitokana na kutokuwapo kwa askari wa kutosha kwa kuwa wako kwenye usimamizi wa mitihani ya kidato cha nne, kidato cha pili na darasa la nne pamoja na kuwapo kwa taarifa za kiintelijensia juu ya kutokea vurugu na kusababisha uvunjifu wa amani.

Kamanda huyo amesema sababu nyingine ni dalili za kuanza kampeni mapema za kuelekea uchaguzi wa Serikali za Mitaa kabla ya kalenda ya kampeni kuanza.

Kamanda huyo amebainisha kuwa sababu nyingine ni barua ya mkutano huo kutoweka wazi dhumuni la mkutano ikiwa ni kinyume cha kifungu cha 43(1)(b) cha Sheria ya Polisi na Polisi wasaidizi sura 322 kama ilivyofanyiwa marekebisho mwaka 2002.

 
Akizungumzia kuhusu kuzuiwa mikutano yake, Msigwa alisema hiyo ni kinyume cha sheria kwa kuwa Mbunge hutakiwa kutoa taarifa ili kuhakikisha usalama wa mikutano yake na si kuomba ruhusa kwa jeshi hilo.

"Mimi ni mbunge na ile ndiyo kazi yangu. Sasa kazi yao ni kulinda mikutano yangu ili pasitokee vurugu na si kuzuia." alisema Msigwa.

Meli Mpya Ya MV Victoria Tayari Imeanza Kujengwa .....Wananchi Kagera Kunufaika Tena

$
0
0
Na: Avitus Benedicto Kyaruzi,Kagera
Wakati Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais John Pombe Magufuli inaendelea kujenga miradi mikubwa ya kimkakati ya kuelekea katika uchumi wa kati bado Mkoa wa Kagera haujasaulika bali sasa wananchi wake wanakumbushwa kujiandaa kikamilifu kwa kuchapa kazi za kilimo na biashara wakati nchi inaelekea katika mapinduzi makubwa ya kiuchumi ili kutembea na kasi ya uchumi wa kati.

Ni baada ya meli ya MV Victoria meli kongwe na maarufu kwa wakazi wa Mkoa wa Kagera  kukamilika ukarabati wake ifikapo Machi 2020 na kurejea katika Ziwa Victoria kwa kufanya kazi kati ya bandari za Mwanza, Bukoba na Kemondo  kusafirisha abiria zaidi 1000 pamoja na mizigotani 200 ambapo kutakuwepo na nafuu kubwa ya bidhaa za viwandani pamoja na usafiri wa wananchi kati ya Bukoba na mwanza.

Uhakika wa meli ya MV Victoria kukamilika ukarabati wake mwakani Machi 2020 pia na ujenzi wa meli mpya ulishuhudiwa na Mkuu wa Mkoa wa Kagera Brigedia Jenerali Marco E. Gaguti pamoja na Kamati ya amani ya Mkoa wa Kagera iliyowajumuisha viongozi wa dini watatu Askofu Methodius Kilaini Askofu msaidizi Jimbo Katoliki la Bukoba, Askofu Dk. Abednego Keshomshahara  Askofu wa (KKKT) Jimbo la Kasikazini Magharibi na Sheikh Haruna Kichwabuta Sheikh wa Mkoa wa Kagera.

Mkuu wa Mkoa Gaguti akiwa katika ziara hiyo ya kutembelea na kujionea maendeleo ya ukarabati  na ujenzi wa Meli mpya pamoja na cherezo katika Bandari ya Mwanza Kusini alisema kuwa anampongeza Rais Magufuli  kwa kuleta mradi huo kwa ajili ya ukombozi wa kiuchumi  wa wananchi wa Kagera kwani utaweka usafiri wa uhakika pia alitoa wito kwa wananchi wa Kagera kujielekeza katika kazi zenye tija za kilimo na biashara na kujiandaa kutumia maboresho ya usafiri kuinua uchumi wa mkoa.

Askofu Msaidizi Methodius Kilaini baada ya kuiona miradi hiyo mitatu alisema kuwa anamshukuru Rais John Pombe Magufuli kwa kutekeleza maajabu katika miradi ya ujenzi na ukarabati wa meli, aidha alisema kuwa Mkuu wa Mkoa Gaguti amewafanyia jambo jema sana la kuwafanya wao kama viongozi wa dini wapate nguvu ya kuleta tumaini na uelekeo kwa watu na kuufanya Mkoa wa Kagera kusimama tena kiuchumi.

Askofu Dk. Keshomshahara mara baada ya kujionea ujenzi wa meli mpya na cherezo na ukarabati wa Meli ya MV Victoria alisema kuwa sasa wao kama viongozi wa dini wamepata neno la kuwaeleza waamini wao na kuwahamasisha kujiandaa kwaajili ya kuitumia fursa ya Meli hizo zikikamilika . Sheikh Haruna Kichwabuta naye alisema kuwa Rais Magufuli alihaidi wakati wa kampeini sasa ametekeleza bila ahadi hewa hasa kwa wananachi wa Mkoa wa Kagera.

Bw. Eric B. Hamissi Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Huduma za meli nchini alimshukuru Mkuu wa Mkoa wa Kagera Mhe. Gaguti kutembelea miradi hiyo ya ujenzi na ukarabati wa meli na kutoa wito kwa wananchi na viongozi wengine nchini kwenda kutembelea miradi hiyokujionea maendeleo ya ujenzi wa meli mpya na cherezo pia na ukarabati wa meli za zamani.

Bw. Eric alisema kuwa mradi  unatekelezwa na Kampuni ya JV of Gas Entec  CO. Ltd  Kang Nam Corporation na SUMA JKT  ambapo kwa ujumla utagharimu jumla ya shilingi bilioni 152 na tayari Serikali imetoa shilingi bilioni 60 wakandarasi wanadaiwa kazi hawaidai Serikali aidha, mradi umegawanyika  katika sehemu kuu nne. Kwanza ni ujenzi wa meli mpya ambayo itakuwa na uwezo wa kubeba tani 400 Abiria 1200 ikiwa na urefu wa meta 92.6, urefu kwenda juu meta 11.2 (sawa na ghorofa nne) na upana wa meta 17 na gharama yake ni shilingi bilioni 90.

Mradi wa pili ni ujenzi wa cherezo ambacho kitakuwa na uwezo wa kubeba meli zenye uzito wa tani 4000 ambapo meli mpya itakuwa na uzito wa tani 3500 tu aidha, cherezo kama  hicho hakuna katika nchi za Afrika Mashariki na Kati  na kikikamilika kitaiingizia Serikali Mapato kama kitatumika kwa kujenga meli zenye uzito mkubwa hasa kutoka nje ya Tanzania.  Mradi wa cherezo utagharimu shilingi bilioni 36 na ujenzi wake umefikia asilimia 52.

Mradi wa tatu ni ukarabati wa Meli ya MV Victoria ambao utagharimu shilingi bilioni 22.8 na ukarabati wa meli hiyo umefikia asilimia 50 ambapo inakarabatiwa ikiwa ni pamoja na kubadilishwa mfumo wake wa zamani na kuwekewa mfumo wa kidigitali. Mradi wa wa nne ni ukarabati wa meli ya Butihama ambapo mradi huo nao utagharimu shilingi bilioni 4.9 na ukarabati wake umefikia asilimia 40.

Kwa msaada wa ofisi ya mkuu wa mkoa

Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Ahudhuria Mkutano Wa Mawaziri Wa AU Mjini Addis Ababa

$
0
0
Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega yuko nchini Ethiopia ambapo anahudhuria mkutano wa mawaziri wa nchi wanachama wa Umoja wa Afrika (AU) wanaohusika na Kilimo, mifugo, uvuvi, mazingira, maji na Maendeleo Vijijini.

Mkutano huo ulioitishwa na Kamisheni ya Afrika kupitia Shirika lake la kusimamia Maendeleo ya Rasilimali za Wanyama Barani Afrika (AU-IBAR), unafanyika kwa siku mbili mjini Addis Ababa ambapo mbali na mambo mengine mkutano huo utapokea ripoti na maazimio mbalimbali kutoka kwa wataalam wa sekta hizo kujadili na kuyapitisha ili waweze kupeleka Halmadhauri Kuu ya AU kwa maamuzi na utekezaji.

Moja ya mikakati, ripoti na maazimio na mapendekezo yanayotarajiwa kujadiliwa na kuridhiwa na baraza hilo la mawaziri wa AU wa sekta ya mifugo, uvuvi, kilimo, mazingira na maji ni ripoti ya miaka miwili ya Tathmni ya Azimio la Malabo (Malabo Declaration) lenye lengo la kuondoa njaa katika bara ka Afrika ifikapo Mwaka 2025 na ripoti ya Tathnimi ya kuwasiliana na Majanga ya asili kama mafuriko na ukame.

Maazimio na mapoendekezo mengine ni ripoti ya hali ya hewa na mabadiliko ya tabia nchi, juhudi za nchi wanachama kuzuia matumizi ya bidhaa za plastiki, mkakati wa kupanda mazao yenye viini lishe vya kutosha na mkakati wa kukabiliana na upotevu wa mazao ya mimea na samaki baada ya kufunga (Post harvest Loss).

Katika kikao hicho pia kitajadili mkakati wa kupambana na magonjwa na vimelea sugu kwa mifugo, mpango wa kuanzisha maabara za kupima ubora wa chakula katika bara la Afrika, mpango wa pamoja wa kuwa na kusimamia na kuweza katika wazo la uchumi wa bahari (Blue economy), mpango mkakati wa miaka 10 kuendeleza uvuvi mdogo mdogo (small scale fisheries) na mpango mkakati wa miaka 10 wa kuendeleza sekta ya ukuzaji viumbe maji.

Mkutano huo ulifunguliwa na Balozi Bi. Josefa Correia Sacko Mkuu wa Kamisheni ya Afrika ya Kilimo na maendeleo vijijini, ambapo zaidi ya washiriki 300 kutoka nchi 49 za bara la Afrika wanahudhuria wakiwepo wawakilishi wa mashirika ya kimataifa kama FAO, WWF, Benki ya Dunia na NEPAD.

Mwisho.

Tatizo la Uhaba wa vitabu kwa wanafunzi katika shule za msingi katika Halmashauri ya Mji Kahama kuwa historia

$
0
0
NA SALVATORY NTANDU
Katika Jitihada za kukabiliana na uhaba wa vitabu vya Masomo ya sayansi na hisabati katika Halmashauri ya Mji wa Kahama mkoani Shinayanga Idara ya elimu Msingi imegawa vitabu elfu 88,652 vya darasa la awali hadi darasa la tano katika shule za msingi 72 zilizopo Halmashauri hiyo ili kukuza  kiwango cha taaluma.

Hayo yamebainishwa jana na  Afisa Elimu, Vifaa na Takwimu Mwalimu Sadick Juma,wakati akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake na kusema kuwa Vitabu hivyo ni vya masomo ya Hesabu, Kiswahili, kingereza, Sayansi, Uraia na Maadili, Maarifa ya jamii ambavyo ni maalumu kwa  wanafunzi wa darasa la awali hadi tano.

Amesema hapo awali kulikuwa na tatizo la uhaba wa vitabu ambapo wanafunzi watatu walikuwa wanatumia kitabu kimoja hivyo upatikanaji wa vitabu hivyo utakuwa suluhisho kwani kwa sasa kila mwananfunzi atakuwa anatumia kitabu chake mwenyewe.

Vitabu hivyo vimegawanyika katika makundi yafuatayo  Kiswahili darasa la tatu vitabu 2676,kusoma darasa la kwanza 4133,kuhesabu darasa la kwanza 4133,sayansi darasa la tatu 2676,hisabati darasa la tatu 2676,kiingeza darasa la tano 300.

Kiswahili darasa la nne 2739,uraia na maadili darasa la nne 2672,maarifa ya jamii darasa la tatu 114,hadithi darasa la awali 24,kifaransa hatua ya kwanza kwa darasa la kwanza hadi la tatu 277 na darasa la nne hadi la saba 277, na hisabati darasa la tatu 376

Amefafanua kuwa mbali na kugawa vitabu hivyo kwa  wanafunzi wa darasa la awali hadi latano, pia Halamshauri hiyo inatarajia kupokea vitabu vingine kwa ajili ya wanafunzi wa darasa la sita na la saba huku asilimia kubwa ya vitabu hivyo vikiwa vya masomo y sanyansi na hisabati.

Katika Hatua nyingine Mwalimu Juma  Hata amesema  kuwa, mbali nakutoa vitambu hivyo bado wanakabiliwa na  uhaba wa walimu katika shule za msingi ambapo mwaka jana wa 2018 Halmashauri ya mji wa kahama ilipokea walimu 20 wapya  ambapo wanauhitaji wa walimu zaidi ya 600.

Mwalimu Juma alitolea mfano Shule ya msingi Mhungula inawanafunzi 4000uhitaji wawalimu 88 na walipo 39, na Shule ya Msingi majengo inajumla ya wanafunzi 2800 na inauhitaji wa walimu 64 na walipo ni 36 laki shule hizi zimeonekana kufanya vizuri katika mtihani mbalimbali ya kitaifa.

Amesema Katika matokeo ya darasa la saba mwaka huu ,shule tatu kati ya shule za msingi 72 za serikali zilizopo Halmashauri ya mji wakahama zimefanya vizuri katika mtihani wa darasa la saba ambazo ni shule ya msingi Kinaga iliyoshika nafasi ya kwanza katika Halmasghauri hiyo,Kilima B, Majengo pamoja na Kahama B,na shule zilizofanya vibaya ni shule ya msingi Bukooba, Mpera, Bujika na Shule ya msingi Nyandekwa.

Waziri Mkuu Amwakilisha Rais Magufuli Katika Mkunao Wa 18 Wa Wakuu wa nchi na Serikali wa nchi zisizofungamana na upande wowote (NAM)

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa leo Oktoba 26, 2019 anatarajiwa kumwakilisha Rais Dkt. John Pombe Magufuli katika Mkutano wa 18 wa Wakuu wa nchi na Serikali wa nchi zisizofungamana na upande wowote (NAM) kutoka Afrika na kwingineko duniani utakaofanyika Baku, Azerbaijan.

Mkutano huo unalenga kujadili namna ya kutatua changamoto za kisiasa, kiuchumi na kijamii zinazokabili nchi wanachama wa NAM katika nyakati za sasa, pamoja na na kujadili masuala mbalimbali yanayohusu maslahi ya nchi wanachama wa umoja huo.

Waziri Mkuu aliwasili nchini Azerbaijan jana (Ijumaa, Oktoba 25, 2019) na alipokelewa na Naibu Waziri Mkuu wa Azerbaijan, Bw. Ali Ahmadov pamoja na viongozi wengeine wa Serikali hiyo. Mapokezi hayo yalifanyika katika uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Heydar Aliyev.

Ajenda za mkutano huo ni kupokea ripoti za mkutano wa maandalizi wa Mawaziri, kupokea ripoti ya mkutano wa maandalizi wa Maafisa Waandamizi, uchaguzi wa nchi zitakazokuwa wajumbe katika ofisi ya uratibu wa shughuli za NAM, New York kwa kipindi cha mwaka 2019-2022.

Mbali na ajenda hizo, pia ajenda nyingine za mkutano huo ni kupokea ripoti za shughuli za umoja huo zilizotekelezwa chini ya Mwenyekiti wa NAM, Venezuela, mjadala mkuu, pamoja na kupitisha maandiko yatokanayo na mkutano.

Mheshimiwa Majaliwa ameambatana na Naibu Waziri Mambo ya Nje na Ushirkiano wa Afrika ya Mashariki, Dkt. Damasi Ndumbaro na Balozi wa Tanzania Nchini Urusi ambale pia ni Balozi wa Azerbaijan, Meja Jenerali Mstaafu, Simon Mumwi.

Awali, Waziri Mkuu alikuwa Sochi nchini Urusi ambako pia alimwakilisha Rais Dkt. John Magufuli katika Mkutano wa Uchumi kati ya Urusi na Afrika (Russia - Africa Economic Forum) na baadae Mkutano wa wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Mataifa ya Afrika uliofunguliwa na Rais wa Urusi Vladimir Putin.

 (mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
JUMAMOSI, OKTOBA 26, 2019

Ndege ya pili Boeing 787-8 Dreamliner yaondoka Marekani....Kutua nchini leo mchana

$
0
0
Ndege mpya ya pili aina ya Boeing 787-8 Dreamliner iliyonunuliwa na Serikali kwa ajili ya Shirika la Ndege Tanzania (ATCL) imeondoka nchini Marekani jana Ijumaa, Oktoba 25, 2919 kuja Dar es Salaam Tanzania.

Ndege hiyo kubwa yenye uwezo wa kuchukua abiria 262 inatarajiwa kutua katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam leo mchana Oktoba 26, 2019.

Ndege hiyo itapokelewa na wananchi wakiongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli.

Hii inakuwa ndege ya 8 kati ya ndege 11 zilizonunuliwa na Serikali kwa lengo la kuimarisha Shirika la Ndege Tanzania (ATCL), kukuza utalii na uchumi.

Watatu Kizimbani kwa Kukutwa na Tausi wa Ikulu

$
0
0
Watu watatu wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisitu wakikabiliwa na mashtaka matano likiwemo la  kukutwa na ndege watatu aina ya tausi waliokuwa Ikulu wenye thamani ya zaidi ya Sh3.4milioni.

Washtakiwa hao wanaokabiliwa na kesi hiyo ya uhujumu uchumi namba 116/2019 ni David Graha, Mohamed Hatibu na Mohamed Ally.

Mbele ya Hakimu Mkazi, Vick Mwaikambo, Wakili wa Serikali Mkuu, Faraja Nchimbi alisema  Juni Mosi 2015 na Oktoba 14, mwaka huu jijini Dar es Salaam, washtakiwa walijihusisha na mtandao wa uhalifu ambapo wanadaiwa kuratibu genge la uhalifu wakijihusisha na biashara ya ndege aina ya Tausi bila kibali cha Mkurugenzi wa Wanyamapori.

Katika shitaka la pili, Nchimbi amedai katika tarehe hizo washitakiwa walikutwa na ndege watatu aina ya tausi wenye thamani ya USD 1,500 ambazo ni sawa na Sh milioni 3.4 mali ya serikali bila kuwa na kibali.

Pia Oktoba 14, mwaka huu maeneo ya Mikocheni jijini Dar es Salaam, mshtakiwa Ally alikutwa na ndege watatu aina ya Tausi wanaopatikana Ikulu, ambao aliwapata kwa njia zisizo halali huku katika shtaka la tano, washtakiwa i Graha na Hatibu katika tarehe hizo hizo walijipatia Sh 300,000 huku wakijua fedha hizo ni mazalia ya kosa la wizi.

Hata hivyo, washtakiwa hawakuruhusiwa kujibu chochote kwa sababu mahakama hiyo haina mamlaka ya kusikiliza kesi ya uhujumu uchumi.

Kwa mujibu wa upande wa mashtaka, upelelezi wa shauri hilo bado haujakamilika hivyo waliomba tarehe nyingine kwa ajili ya kutajwa na kuzingatia kwamba mashitaka hayo hayana dhamana.

Kesi hiyo imeahirishwa hadi Novemba 7 mwaka huu kwa ajili ya kutajwa na washitakiwa walirudishwa rumande kwa sababu mashitaka hayo hayana dhamana.

Mvua yasababisha mafuriko wilayani Korogwe.....Mamia ya abiria wakwama

$
0
0
Mamia ya abiria waliokuwa wanasafiri kutoka Arusha, Kilimanjaro na nchi jirani na waliotoka Dar es Salaam kuelekea mikoa mbalimbali wamekwama tangu jana mchana Ijumaa Oktoba 25, 2019 wilayani Korogwe na Handeni Mkoa wa Tanga.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, Edward Bukombe, amesema kuwa Jeshi la Polisi mkoani humo linaendelea kuimarisha usalama kwa abiria wote, waliokwama kuendelea na safari baada ya maji kujaa juu ya daraja ili kuepusha madhara makubwa hususani wale ambao watalazimisha kuvuka.

Kauli hiyo ameitoa leo ambapo amesema kuwa abiria ni wengi kwani wanaongezeka kila muda na kwamba wameshindwa kupata idadi kamili ya watu waliokwama kwa hizo pande zote mbili.

"Bado njia haijafunguka kule Handeni tulikokuwa tunapategemea kupita daraja lilishakatika kabisa kwahiyo hakuna mawasiliano na hii ya Segera - Korogwe na yenyewe bado maji yanapita juu, kwahiyo tunasubiri maji yapungue ili tuone uimara wa daraja na gari kama zinaweza zikapita", amesema Kamanda Bukombe.

"Tunachokifanya kwa sasa ni kuimarisha ulinzi ili yasiwepo madhara ya kuibiwa na wale ambao huwa wanataka kuvuka kwa kutumia nguvu'', ameongeza.

Inakadiriwa kuwa abiria zaidi ya 5,000, kutoka mikoa ya Arusha, Kilimanjaro na hata nchi jirani na wale waliokuwa wanatoka Dar es Salaam kwenda katika mikoa hiyo wamekwama siku ya jana ya Oktoba 25, 2019, wilayani Korogwe na Handeni, kufuatia mvua kubwa inayonyesha na kupelekea maji kujaa juu ya daraja na huku lingine likisombwa na maji.
 

LIVE: Hafla Ya Mapokezi Ya Ndege Mpya Boeing 787-8 Dreamliner Ya Air Tanzania

$
0
0
LIVE: Hafla Ya Mapokezi Ya Ndege Mpya Boeing 787-8 Dreamliner Ya Air Tanzania

Nafasi Mbalimbali za Kazi Zilizotangazwa Leo TANROADS, Chuo Kikuu SAUT, Mamlaka Ya Usafiri Wa Anga -TCAA

$
0
0
==>>Nafasi Mpya za kazi  Zilizotangazwa na TANROADS - Mtwara.

👉Wanahitajika Watu wa fani Mbalimbali.
👉Elimu ni kuanzia kidato cha Nne
👉Deadline; 01 November 2019.

Kujua jinsi ya kutuma maombi, <<Bofya Hapa>>
▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬

==>>Nafasi Mpya za  kazi Zilizotangazwa na Chuo Kikuu cha St. Augustine University of Tanzania (SAUT) - Mwanza.

👉Wanahitajika Watu wa Fani Mbalimbali
👉Mwisho wa Kutuma Maombi ni tarehe; 01 November 2019.

Kujua jinsi ya kutuma maombi, <<Bofya Hapa>>
▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬

==>>Nafasi 16  Za Kazi toka Mamlaka Ya Usafiri Wa Anga -TCAA

👉Wanahitajika Watu wa Fani Mbalimbali
👉Elimu: kuanzia ya Cerificate /Diploma
👉Deadline: November 06,2019

Kujua jinsi ya kutuma maombi, <<Bofya Hapa>>
▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬

Tanzania Yataka Vikwazo Dhidi Ya Cuba Na Zimbabwe Viondolewe

$
0
0
SERIKALI ya Tanzania imelaani vikwazo vya kiuchumi vilivyowekwa na Serikali ya Marekani dhidi ya Cuba na Zimbabwe kwa sababu vinadhoofisha biashara, uwekezaji na ustawi wa wananchi na imetaka vikwazo hivyo viondolewe.

Tamko hilo limetolewa leo (Jumamosi, Oktoba 26, 2019) na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa kwenye Mkutano wa 18 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Nchi Zisizofungamana na Upande Wowote (NAM) ulioanza leo huko Baku, Azerbaijan.

“Vizuizi na vikwazo vya kiuchumi vilivyowekwa dhidi ya Cuba na Zimbabwe vinadhoofisha maendeleo ya uchumi, uwezo wa kufanya biashara, fursa za uwekezaji na ustawi wa wananchi wake.”

“Tanzania inaungana na Jumuiya ya Kimataifa kutaka yawepo majadiliano ya msingi ambayo yataondoa vizuizi kwa Serikali ya Cuba na vikwazo kwa Serikali ya Zimbabwe ili kuleta mabadiliko ya kiuchumi kwa manufaa ya watu wa nchi hizo,” amesema.

Mwaka 2001, Marekani na Jumuiya ya Ulaya (EU) ziliweka vikwazo vya kiuchumi dhidi ya Zimbabwe baada ya Serikali ya nchi hiyo chini ya uongozi wa Rais Robert Mugabe kuamua kuchukua ardhi yote iliyokuwa ikimilikiwa na wageni.

Waziri Mkuu ambaye anahudhuria mkutano huo wa Wakuu wa Nchi na Serikali kwa niaba ya Rais Dkt. John Pombe Magufuli, aligusia mambo kadhaa ikiwemo mabadiliko ya tabianchi, masuala ya Sahara Magharibi, usalama wa Palestina na msimamo wa Tanzania kwenye Umoja wa Nchi Zisizofungamana na Upande Wowote (NAM).

Kuhusu mabadiliko ya tabia nchi, Waziri Mkuu amesema suala hilo ni mojawapo ya changamoto kubwa zinazoikabili dunia na wanadamu kwa sasa. “Tunaiomba Jumuiya ya Kimataifa iweke njia muafaka ambazo zitasadia kurekebisha tishio ambalo tunakabiliana nalo hivi sasa. Tunazitaka nchi zilizoendelea zitimize ahadi zao na michango ya kifedha, zisaidie kujenga uwezo na kutoa wataalamu watakaozisaidia nchi zinazoendelea,” amesema.

Akizungumzia Sahara Magharibi, Waziri Mkuu amesema suala la kujitawala kwa nchi hiyo limeingia sura mpya baada ya Morocco kujiunga tena na Umoja wa Afrika na kwamba hivi sasa imekuwa mjumbe wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa.

“Ipo fursa kubwa hivi sasa kwa Umoja wa Mataifa pamoja na mjumbe maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ya kuweza kushirikiana na chombo kipya cha Troika kilichoundwa na Umoja wa Afrika katika kuliangalia suala zima la Sahara Magharibi. Tanzania inaunga mkono jitihada hizo,” amesema Waziri Mkuu.

Kwenye suala la Palestina, Waziri Mkuu amesema Tanzania inatambua kwamba nchi hiyo ina haki ya kufurahia amani na uhuru wake kama ilivyo kwa Israeli, kwa mujibu wa mkataba wa Umoja wa Mataifa. “Ni matumaini yetu kwamba kuendelea kuwepo kwa jitihada za kimataifa, mgogoro huo utapatiwa ufumbuzi katika muda muafaka na mataifa haya mawili yataishi kwa amani na utulivu.”

Waziri Mkuu alitumia fursa hiyo kuelezea msimamo wa Tanzania kwenye umoja huo na kusisitiza kwamba Tanzania bado ina imani na chombo hicho. “Tanzania itaendelea kuheshimu kazi zinazofanywa na umoja huu kama ambavyo tumekuwa tukifanya kwa miaka 58 iliyopita. Tunaomba ushirikiano baina ya nchi za Kusini uimarishwe. Ushirikiano baina ya nchi zinazoendelea na zilizoendelea nao pia uimarishwe.”

Amesema: “Serikali ya Tanzania inapongeza uhusiano ulipo baina ya Umoja wa Nchi Zisizofungamana na Upande Wowote (NAM), kundi la nchi 77 (G77) na China na kwamba tunatamani ujizatiti zaidi kutetea maslahi ya umoja huu ambao wanachama wake wengi ni nchi zinazoendelea.”

Waziri Mkuu Majaliwa ameambatana na Naibu Waziri Mambo ya Nje na Ushirkiano wa Afrika ya Mashariki, Dkt. Damas Ndumbaro na Balozi wa Tanzania nchini Urusi ambaye pia ni Balozi wa Azerbaijan, Meja Jenerali Mstaafu, Simon Mumwi.

(mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images