Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Uzalishaji Makaa Ya Mawe Waongezeka Nchini

$
0
0
Na Asteria Muhozya
Imeelezwa kuwa, wastani wa uzalishaji wa Makaa wa Mawe nchini umekuwa ukiongezeka tofauti na ilivyokuwa  awali huku sababu kadhaa zikichangia ongezeko la uzalishaji huo ikiwemo mazingira mazuri ya uwekezaji, zuio la  Serikali kuingiza makaa ya mawe kutoka nje, ongezeko la viwanda vinavyotumia makaa ya mawe na  kuboreshwa kwa mundombinu ya usafirishaji. 
 
Hayo yamebainishwa na Kamishna wa Madini Mhandisi David Mulabwa wakati akiwasilisha kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kuhusu  hatua zilizofikiwa katika  uendelezaji wa miradi ya makaa ya mawe kwa niaba ya Waziri wa Madini.
 
Mhandisi Mulabwa amesema katika kipindi cha miaka 8 kuanzia mwaka 2011 hadi 2018, uzalishaji uliongezeka kutoka tani 81,384.67 mwaka 2011 na kufikia  627, 651.00 mwaka 2018, ikiwa ni  wastani wa takribani tani 52,304.25 kwa mwezi.
 
‘’ Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kipindi cha miezi 9 kwa mwaka 2019, uzalishaji  uliongezeka  hadi kufikia tani 543,621.39 ikiwa ni wastani wa tani 60,402.38 kwa mwezi,’’ amesema Mhandisi Mulabwa.
 
Ameongeza kuwa, pamoja na ongezeko la uzalishaji huo, bado ni mdogo ikilinganishwa na kiasi cha makaa ya mawe kinachokadiriwa kuwepo nchini. Amesema Tanzania inakadiriwa kuwa na mashapo ya makaa ya mawe  yanayofikia tani bilioni 1.9 na yaliyothibitishwa ni tani bilioni 1.4 huku ikitajwa kuwa nchi yenye akiba kubwa ya makaa hayo  kwa nchi za Afrika Mashariki.
 
‘’ Mheshimiwa Mwenyekiti akiba kubwa zaidi kwa sasa inapatikana katika bonde la Mchuchuma ambapo kuna akiba ya zaidi ya tani milioni 400,’’ amesema Mhandisi Mulabwa.
 
Akizungumzia  mwenendo wa mauzo amesema kipindi cha kuanzia  mwezi Julai, 2018 hadi  Juni, 2019 kiasi cha makaa ya mawe kilichozalishwa na kuuzwa  ni tani 799,628.41 zenye thamani ya shilingi 102,922,127,876.61. Ameongeza kati ya kiasi hicho kilichozalishwa, tani 421,400.07 ziliuzwa nchini na tani 378,2228.34 ziliuzwa katika masoko ya  nje ya nchi
 
Ameeleza kutokana na mauzo hayo, Serikali ilipata kiasi cha  shilingi 4, 116,885, 115.06 , ambapo shilingi 3,087,663,836. 30 ni mapato yatokanayo na mrabaha na  shilingi 1,029,221,278.77 ni mapato yatkanayo na ada ya ukaguzi.kipindi cha kuanzia mwezi Julai.
 
Kuhusu uzalishaji wa makaa ya mawe kwa mwaka wa fedha 2019/20, kuanzia mwezi Julai 2019 hadi Septemba 2019 amesema  kiasi kilichozalishwa katika migodi yote ni tani 157,341 zenye thamani ya shilingi 16,691,662,474. 
 
‘’ Mhe. Mwenyekiti kutokana na mauzo hayo serikali ilikusanya mapato ya shilingi 949,834,017.71 ambapo shilingi  807,074,032.73 ni mapato yatokanayo na malipo ya mrabaha na shilingi 142,759,984.98 ni mapato yaliyotokana na ada ya ukaguzi.
 
Akizungumzia hatua zilizochukuliwa na serikali kuendeleza miradi ya makaa ya mawe amesema kuwa ni pamoja na kuendelea kuhamasisha uanzishwaji wa Viwanda mbalimbali ili kujenga uchumi wa viwanda; kuendelea kusimamia tafiti maeneo mbalimbali ili kupata taarifa sahihi za kiasi cha mashapo na ubora wa makaa ya mawe nchini; wizara kwa kushirikiana na taasisi nyingine za serikali imeendelea kuboresha mazingira ya biashara katika sekta ya makaa ya mawe; serikali imeendelea kufuatilia uanzishwaji wa miradi ya makaa ya mawe ya Mchuchuma na Liganga na kuendelea kuweka zuio la uingizwaji   wa makaa ya mawe kutoka nje ya nchi ili kuongeza biashara ya makaa ya mawe yanayozalishwa nchini.
 
Aidha, ameyataja baadhi ya mafanikio kuwa ni pamoja na kuongeza kwa matumizi ya makaa ya mawe yanayozalishwa nchini kufuatia zuio la uingizaji wa makaa ya mawe kutoka nje,  kuongezeka kwa kiasi cha makaa ya mawe yanayozalishwa hapa nchini kutoka wastani wa tani 81,384.67 kwa mwaka 2011 hadi kufikia tani 627,651.00 mwaka 2018 kutokana na ongezeko la watumiaji wa ndani.
 
Pia, ameyataja mafanikio mengine kuwa ni pamoja na  kuongezeka kwa biashara ya makaa ya mawe ndani  na nje ya nchi, ambapo watumiaji wa nishati ya makaa ya mawe wameendelea kuongezeka kutokana na upatikanaji wake, kuongezeka kwa mapato ya serikali kutokana na uuzaji wa makaa ya mawe na kuongezeka kwa ajira kutokana na shughuli za uchimbaji wa makaa ya mawe ambapo hadi kufikia Septemba 2019, takribani watu 500 wameajiriwa katika migodi mbalimbali  ya uchimbaji wa makaa ya mawe.
 
Kwa upande wa Kamati ya Bunge baada ya kupkea taarifa hiyo, Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Dustan Kitandula imeitaka wizara kuweka msukumo mkubwa wa uanzishwaji wa miradi ya Linganga na Mchuchuma pamoja na mradi wa Kiwira kutokana na manufaa yake kiuchumi. 
 
Akijbu hatua zilizochukuliwa na wizara, Waziri wa Madini Doto Biteko amesema tayari wizara kwa upande wake imekwishafanya masuala yote yanayohitaji msukumo wa wizara katika miradi husika huku mengine yakisimamiwa na mamlaka nyingine hata hivyo ameeleza kuwa serikali inaendelea kuyafanyia kazi ili kuwezesha miradi hiyo kutekelezwa.
 
Naye, Naibu Waziri wa Madini Stanslaus Nyongo ameileza Kamati hiyo kuhusu hatua kadhaa zilizochukuliwa na wizara katika kuboresha miundombinu ya barabara katika maeneo ya uchimbaji wa makaa ikiwemo ya kilomita 8 kutoka Kiwira mpaka Kabulo na kueleza kuwa, tayari serikali imekwisha tenga shilingi Bilioni 2 kwa ajili ya ujenzi wa barabara na shilingi bilioni 1.5 kwa ajili ya ujenzi wa daraja. 
 
Vikao kati ya  Kamati, Wizara na taasisi zake vimeanza Oktoba 28, 2019 na vinatarajiwa kuhitimishwa Novemba 1,2019.

Wanawake Washauriwa Kujitokeza Na Kuogombea Nafasi Mbalimbali Za Uongozi

$
0
0
Wanawake Mkoani Kagera wametakiwa kujitokeza kwa wingi kugombea nafasi mbalimbali katika uchaguzi wa Serikali za mitaa unaotarajia kufanyika mnamo septemba 24 mwaka huu.
 
Hayo yamebainishwa na Mbunge wa viti maalumu kutoka Manispaa ya Bukoba mkoani Kagera kupitia chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema Mh Conchester Rwamulaza wakati akiongea na mpekuzi blog kuelekea katika uchaguzi wa serikali za mitaa utakaofanyika mapema mwaka huu.
 
Mh Conchester amesema kuwa wanawake wengi wamekuwa na hofu ya kutotaka kugombea nafasi mbalimbali za uongozi na kuongeza kuwa wanayo nafasi kubwa yakuweza kugombea nafasi za uongozi kwa mwaka huu  kwa ajili ya maedeleo ya nchi kwa kuwa wana kauli mbiu ya wanawake wanaweza na kusema kuwa isiwe kauli ya maneno bali ata kwa vitendo.
 
Amesema kuwa ushindani wa mwaka huu ni mkubwa na watu wengi wana mwamuko wa kugombea kwa ajili ya maendeleo ya nchi na kuongeza kuwa uongozi unaanzia chini katika ngazi ya vitongoji na vijiji kwa kuwa viongozi hao wanakuwa karibu na wananchi.
 
Aidha Mh Conchester ameongeza kuwa wananchi wajitokeze  kwa wingi mnamo septemba 24 mwaka huu kuweza kupiga kura huku wakitambua umuhimu wa uchaguzi huo na akiwataka wananchi kutobeza uchaguzi huo kwa kuwa ni muhimu sana.
 
Pia mh Conshester amesema kuwa  ili jambo la wanawake kujitokeza kugombea nafasi mbali mbali lifanikiwe inabidi akina baba kutowakataza wanawake  kugombea katika uchaguzi huo ili waweze kutimiza malengo yao.


Mkuchika Asema Wanaowahamisha Watumishi Vituo Vya Kazi Kabla Hawajathibitishwa Atawashughulikia.

$
0
0
Na.Faustine Gimu Galafoni,Dodoma
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Utumishi na Utawala Bora, Kepteni George  Mkuchika amesema atawashughulikia wale wote anaohamisha watumishi vituo vya kazi kabla hawajathibitisha kwani ndio wanaochangia kuwepo kwa changamoto ya baadhi ya Mikoa kuwa na upungufu wa watumishi.

Akizungumza Jijini hapa jana wakati akizindua Baraza Kuu la nne la Wafanyakazi katika Utumishi wa Umma Kepteni Mkuchika amewataka utumishi wa Umma kutambua kuwa kila wakati wanapaswa kuwa tayari kufanya kazi mahali popote kwa ajili ya kuwatumikia wananchi.

Amesema katika ziara yake Mikoani amegundua Mikoa ya pembezoni ina uhaba mkubwa wa watumishi, akitolea mfano Wilaya ya Tunduru Mkoani Ruvuma ambayo ina watumishi chini ya asilimia 50.

Kuhusu suala la Rushwa, amesema taasisi zilizopo chini ya Ofisi Rais zinatakiwa kuwa kioo katika kukema vitendo vya rushwa, kwani Ofisi hiyo ndio inayoshughulikia wasiowaadilifu na si kujihusisha na vitendo hivyo.

Kwa pande wake Makamu Mwenyekiti wa Baraza hilo Leah Ulaya amesema watumishi wa Umma wanajua kazi kubwa inayofanywa na Rais katika kuleta maendeleo kwa wananchi hivyo wataendelea kufanyakazi kwa weledi na uadilifu ili kuunga mkoni juhudi za Seriali.

Kuhusu malalamiko yaliyopo kwa watumishi wanaopandishwa madaraja lakini kiwango cha mshahara hakibadiliki,Wizara hiyo amewahakikishia kuwa suala hili litapatiwa ufumbuzi haraka iwezekanavyo, huku ikimesema kuondolewa kwa watumishi 19,708 waliobainika kuwa na  vyeti vya kughushi kupitia zoezi la uhakiki kumeifanya Serikali kuokoa kiasi cha Sh 19.838 bilioni.
Mwisho.

Heri Ya Kuzaliwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr John Pombe Magufuli

$
0
0
Leo Oktoba 29, 2019, Rais Magufuli anasherehekea kumbukizi ya siku yake ya kuzaliwa. 

Rais Magufuli alizaliwa tarehe kama ya leo Oktoba 29, 1959 na ametimiza miaka 60, tunamtakia afya njema na Mungu azidi kumuongoza katika majukumu yake.

Muungano wa Tigo na Zantel unavyokusudia kuboresha soko la mawasiliano nchini

$
0
0
Sekta ya mawasiliano ya simu za mkononi imekua kwa kiasi kikubwa sana katika kipindi cha muongo mmoja uliopita.

Katika kipindi hiki cha ukuaji huu makampuni ya simu yametanua wigo wa huduma na matumizi ya simu za mkononi imekuwa sehemu muhimu ya maisha ya kila siku kwa mamilioni ya Watanzania tofauti na zamani ambapo simu ilikuwa kama anasa na ni wachache tu waliweza kuwa nazo. Maendeleo haya yanazidi kukua siku hadi siku kutokana na kuongezeka kwa ubunifu katika teknolojia. 

Simu ya mkononi sasa imebadilika na kuwa si tu kifaa cha kupiga, kupokea na kutuma meseji baina ya watumiaji lakini pia imeleta mapinduzi katika namna tunavyoweka akiba ya fedha, kulipana, kulipa bili mbalimbali na kuendesha maisha yetu ya kila siku.  
 
Mfano wa namna ambavyo simu za mkononi zimebadili maisha yetu ni kampuni ya Tigo Tanzania. Mfumo wa Tigo Pesa wa kutuma na kupokea pesa unatupa nafasi ya kutumiana na kupokea pesa bila haja ya kwenda na kupanga foleni benki.

Vivyo hivyo wenye maduka na biashara mbalimbali nao wametengenezewa mfumo wa Tigo Pesa Merchant ambao unawapa uwezo wa kupokea malipo kutoka wateja wote wa Tigo Pesa ambao kwa sasa ni zaidi ya watu milioni 16.   

Tigo Tanzania pia ni moja ya makampuni yanayoongoza kwa kutoa huduma ya 4G ambayo ni teknolojia yenye ina kasi zaidi katika mawasiliano nchini.

 Huduma hii inakupa uhakika wa kutazama vitu kama videos mtandaoni bila wasiwasi wa kukwama kwama au hata kufanya mikutano kwa njia ya video (conferencing)

Hata hivyo katika siku za karibuni umekuwepo wasiwasi kwamba sekta ya mawasiliano ya simu za mkononi imejaa watoa huduma ambao wengi hawana tija na wasiolipa soko afya katika kuhudumia wateja.

Hali hii inaelezwa kuleta changamoto kwa ubunifu na utoaji huduma wenye tija na viwango bora kwa wateja. 

Katika sekta nyingi za uchumi uwepo wa watoa huduma wengi huwa ni faida kwa mteja. Bahati mbaya ukweli huu haupo kwenye sekta ya mawasiliano ya simu za mkononi. 

Utafiti unaonyesha kuwa kupunguza idadi ya watoa huduma katika sekta ya mawasiliano ya simu za mkononi huwezesha makampuni machache yalipo sokoni kuongeza faida ambayo huwawezesha kuwekeza zaidi katika mitambo na teknolojia yenye kutoa huduma bora zaidi kwa wateja wake. 

Katika soko la Tanzania, siku za karibuni zimekuwepo hatua mbalimbali za kibiashara kupunguza watoa huduma ili kuongeza uwekezaji kwenye teknolojia na ubora wa huduma kwa wateja.

Makampuni mawili ya Tigo Tanzania na Zantel yamekuwa na mjadala kuungana. 

Hatua hii ya Tigo Tanzania na Zantel kuungana ni habari njema sana kwa wateja wa Zantel. Maana yake ni kwamba sasa wateja hao wa Zantel wataweza kufurahia huduma zote ambazo sasa wateja wa Tigo Tanzania wanazipata.

Muungano huo pia utasaidia sekta ya mawasiliano ya simu za mkononi nchini kuendelea kuwa bunifu na kutoa huduma bora kwa mamilioni ya wateja wake nchi nzima.

UVCCM: Wanaosaka Ubunge Kwa Njia Ya Rushwa Kukiona Cha Mtema Kuni

$
0
0
NA FREDY MGUNDA,IRINGA.
MWENYEKITI wa umoja wa vijana wa ccm (UVCCM) mkoa wa Iringa Kenani Kiongosi amewataka wanasiasa mbalimbali wanaousaka ubunge wa jimbo la Iringa Mjini  kufuata misingi ya chama ili wapite kwenye kanuni na taratibu za chama.

Akizungumza na viongozi wa UVCCM mkoa wa Iringa Kihongosi alisema kuwa viongozi wote wanaoutafuta ubunge katika jimbo la Iringa mjini wanatakiwa kufuata utaratibu unatakiwa na chama cha mapinduzi ili kumpata kiongozi bora.

“Katika kipindi cha miaka kumi sasa tumekuwa tukipoteza jimbolaIringa mjini kwa kuwa na makundi kutokana na viongozi warafi na waroho wa madaraka kwakutoa rushwa kwa wapiga kura ili waweze kupata ubunge,kwa sasa hatuwezi kukubali swala hilo kwa kuwa tunahujumiwa kutokana na makundi ambayo yamekuwa yakitokeza kipindi cha uchaguzi” alisema Kihongosi

Kihongosi alisema kuwa kumekuwa na viongozi wanaoutaka ubunge Iringa Mjini wameanza kufanya kazi wanavyojitakia wao bilakufuata njia sahihi ambazo zinatakiwa,badala yake wamekuwawakitoa fedha kwa baadhi ya wadau kwa lengo la kutengeneza makundi ambayo hayana faida kwa wananchi wa Manispaa ya Iringa.

Aidha Kihongosi aliwataka vijana wa chama cha mapinduzi kukataa mara moja kutumika kuwa daraja kuwatafutia ubunge viongozi ambao hawana msaada katika jumuiya katika kuleta maendeleo kwa vijana ambao ndio wamekuwa wakitumia kuleta ushindi kwamgombea wa chama cha mapinduzi.

“Vijana acheni mara moja kutumika kwa viongozi wasaka tonge ambao wamekuwa wakipata madaraka hawakumbuki mchango wa vijana wakati wa kukitafuta cheo chake”alisema Kihongosi

Kihongosi alisema mwaka 2015 kulikuwa namakundi makubwa mawili ambayo yalikuwa katika ya wenyeviti na makatibu na kupelekea kupoteza jimbo la Iringa Mjini na kulikuwa na mvurugano mkubwa kweli ambao ulimpa tena ubunge Mchungaji Petter Msigwa.

“Nitasikitika sana kuona kijana mmoja ambaye ni kiongozi kumbeba mgombea furani,nikikutambua mapema nitakupeleka kwenye kamati husika na tutakuondoa kwenye nafasi ambayo uponayo hivi sasa ili usituvuruge kwenye harakati zetu za kulikomboa jimbo la Iringa Mjini” alisema Kihongosi

Taarifa Kwa Umma; Gavana Wa BOT Hajafungua Akaunti Ya “Facebook”

$
0
0
Benki Kuu ya Tanzania (BoT) inapenda kuutangazia umma kwamba Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Prof. Florens Luoga, hajafungua akaunti ya mtandao wa kijamii wa Facebook, kinyume na taarifa na picha zinazojitokeza katika katika mtandao huo kwa jina lake.

Kwa taarifa hii, tunapenda kuutangazia umma kupuuza chochote kinachopatikana katika akaunti hiyo bandia inayojiita Florence Luoga, na ambayo inatumia picha mbalimbali za Gavana wa BoT kinyume cha sheria.

Aidha, Benki Kuu ya Tanzania inapenda kuwapa pole watu wote ambao kwa namna moja ama nyingine wameathirika kutokana na yote ambayo yamejitokeza katika akaunti hiyo bandia, ikiwemo kutumia jina la Gavana Luoga kutapeli na hata kutumiwa ujumbe wa matusi.

Pamoja na taarifa hii, hatua za kisheria zinaendelea kuchukuliwa ili kumbaini mhalifu huyu kwa kutumia akaunti hiyo kuchafua sifa ya Gavana Luoga katika jamii.

Tunauhakikishia umma kwamba, Gavana Luoga hajafungua akaunti kwa jina hilo na hivyo taarifa zozote zinazotolewa kwenye akaunti hiyo ya Facebook hazina uhusiano wowote na Prof. Florens Luoga.

Waziri Lugola Ayasimamisha Magari Yaliyotaka Kusababisha Ajali......Dereva Wa Basi Akamatwa, Abiria Warudishiwa Nauli

$
0
0
Na Felix Mwagara, MOHA, Busega.
WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola ameyakamata magari mawili yaliyotaka kusababisha ajali kwa kufukuzana na kulazimisha kuovateki bila ya kuwa na tahadhari katika barabara kuu ya Mwanza Mara.

Magari hayo ni basi lililokuwa na abiri liitwalo Manoni Safaris lenye namba za usajili T800DCU, pamoja na lori namba T865CVJ, yaliyokuwa yanatokea Mwanza kuelekea Mkoani Mara, yalipofika Kijiji cha Nyashishi, Wilayani Busega Mkoani Simiyu yakiwa mwendokasi yakawa yanalazimisha kuovateki bila kuwa na tahadhari.

Waziri huyo  akiwa safarini akitokea Wilayani Bunda, leo, alishuhudia magari hayo yakiwa mwendokasi na yakilazimisha kuovateki hali iliyosababisha magari yaliyokuwa yanatokea Mkoani Mara kuyakwepa kwa shida ili kuepusha ajali isitokee.

Baada ya tukio hilo, Waziri huyo alimwelekeza dereva wake kugeuza gari na kuyakimbiza magari hayo hasa basi hilo Manoni Safaris lenye namba za usajili T800DCU, ambalo ndilo lililokuwa na makosa dereva akijua magari yanakuja mbele yake lakini akawa analazimisha kuovateki akilikimbiza lori ambalo lilikua mbele yake.

“Huyu dereva hana tahadhari na mtu hatari sana, alitaka kutuua na pia kuua abiria wa basi hili, lazima afunguliwe mashtaka apelekwe mahakamani na iwe fundisho kwa madereva wazembe wa aina hii, na nimeambiwa na abiria hapa kuwa aliwapuuza baada ya kuambiwa apunguze mwendo,” alisema Lugola.

Waziri huyo alimkamata dereva wa basi hilo na kumtaka atoe leseni yake, kabla ya kupelekwa Kituo cha Polisi Busega kwa ajili ya kufunguliwa mashtaka, na alielekeza abiria wa basi hilo warudishiwe nauli zao na watafutiwe basi lingine ili waendelee na safari.

Dereva wa basi hilo, Marijani Saidi alikiri kufanya kosa na alimuomba msamaha Waziri huyo, hata hivyo alikataliwa kutokana na kuvunja sheria za usalama barabarani na kutaka kusababisha ajali.

Akizungumzia tukio hilo, abiria wa basi hilo, Mwita Machela, alisema walimtaka dereva huyo kuacha kuendesha mwendokasi lakini aliwapuuza na kuendelea na safari.

“Waziri yupo sahihi kutusimamisha maana ametuokoa pia, huyu dereva alikua mwendokasi, tulimuonya aache lakini hakutusikiliza, sasa haraka yake imeishia hapa, na sisi tumepotezewa muda wetu kutokana na uzembe wake,” alisema Lugola.

Waziri Lugola alisimamia kondakta wa basi hilo akiwarudishia nauli abiria hao, pamoja na kuhakikisha wanapandishwa katika mabasi yaliyokua yanapita katika barabara hiyo.

Nafasi Mbalimbali za Kazi Zilizotangazwa na Coca Cola Tanzania, Tigo Tanzania, Vodacom Tanzania, Umoja wa Mataifa na Zingine Kibao

$
0
0
==>>Nafasi za Kazi za  Kujitolea SNV( Wanatakiwa watu 8)


👉Volunteers wanahitajika Dar,Moshi,Mbeya,Dodoma,Katavi, Songea
👉Deadline; November 3, 2019

Kujua jinsi ya kutuma maombi, <<Bofya Hapa>> 
▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬  

==>>Coca Cola Tanzania Wametangaza Nafasi Mpya ya Kazi

👉Wanataka; Distribution Driver 
👉Deadline; November 5, 2019 

Kujua jinsi ya kutuma maombi, <<Bofya Hapa>> 
▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬  
 
==>>Tigo Tanzania Wametangaza Nafasi Mpya ya Kazi

👉Wanataka;Commercial Execution Specialist 

Kujua jinsi ya kutuma maombi, <<Bofya Hapa>> 
▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬  
 
==>>Vodacom Tanzania Wametangaza Nafasi Mpya ya Kazi

👉Wanataka; M-PESA Agents – MPESAN
👉Deadline; November 1,2019

Kujua jinsi ya kutuma maombi, <<Bofya Hapa>> 
▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬  

==>>Tangazo la Nafasi za Kazi Umoja wa Mataifa Katika Shirika la Kuhudumia Wakimbizi (UNHCR)

👉Deadline ni; November 11, 2019
👉Kituo cha Kazi ni Kigoma,Tanzania

Kujua jinsi ya kutuma maombi, <<Bofya Hapa>> 
▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬  

 ==>>Shirika la REPOA Limetangaza Nafasi Mpya za Kazi

👉Deadline ni; November 11, 2019
👉Wanawake Watapewa Kipaumbele zaidi

Kujua jinsi ya kutuma maombi, <<Bofya Hapa>> 
▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬  

==>>Nafasi Mpya za kazi  Iringa katika shirika la Kimataifa FHI 360 Tanzania
👉Wanataka watu wa fani Mbalimbali
👉Deadline ni; November 23, 2019 

Kujua jinsi ya kutuma maombi, <<Bofya Hapa>> 
▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬ 

==>>Nafasi Mpya za kazi  Zilizotangazwa na TANROADS - Mtwara.

👉Wanahitajika Watu wa fani Mbalimbali.
👉Elimu ni kuanzia kidato cha Nne
👉Deadline; 01 November 2019.

Kujua jinsi ya kutuma maombi, <<Bofya Hapa>>
▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬

==>>Nafasi Mpya za  kazi Zilizotangazwa na Chuo Kikuu cha St. Augustine University of Tanzania (SAUT) - Mwanza.

👉Wanahitajika Watu wa Fani Mbalimbali
👉Mwisho wa Kutuma Maombi ni tarehe; 01 November 2019.

Kujua jinsi ya kutuma maombi,<<Bofya Hapa>>
▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬

==>>Nafasi 16  Za Kazi toka Mamlaka Ya Usafiri Wa Anga -TCAA

👉Wanahitajika Watu wa Fani Mbalimbali
👉Elimu: kuanzia ya Cerificate /Diploma
👉Deadline: November 06,2019

Kujua jinsi ya kutuma maombi, <<Bofya Hapa>>
▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬

Bilioni 10 Za Rais Magufuli Zaanza Kazi Ruvuma

$
0
0
Na Mwandishi Wetu,Ruvuma
Shilingi Bilioni 10 zilizotolewa mwanzoni mwa mwaka huu na Rais Dkt. John Pombe Magufuli kwa ajili ya Ujenzi wa Nyumba za Askari wa Vyeo vya chini zimeanza kutumika mkoani Ruvuma huku jumla ya nyumba sita zikiwa zimejengwa katika wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma.

Rais Magufuli aliahidi kutoa kiasi hicho cha fedha wakati akizindua Kituo cha Polisi cha Utalii na Diplomasia jijini Arusha mwezi April mwaka huu.

Akizungumza leo wakati wa ziara ya ukaguzi wa nyumba hizo mkoani Ruvuma, Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,Mhandisi Hamad Masauni alisema tayari nyumba hizo zimekamilika na tayari ujenzi unaendelea mikoa yote nchini ambako ilibainika kuna changamoto ya makazi ya askari

“Rais wetu aligundua changamoto ya askari wetu hawa hasa wa vyeo vya chini,akatoa kiasi cha shilingi bilioni kumi kwa jeshi la polisi,leo nimefika hapa kuangalia matumizi ya fedha hizo na nimeridhishwa na hatua ya ujenzi ulikofikia kwani nyumba zimekamilika na tayari nimeona baadhi askari wetu washahamia,”alisema Masauni

“….tunatembea nchi nzima kuona nyumba hizo zimefikia hatua gani lengo ni kuona askari wetu wanahama katika makazi duni na kuhamia nyumba hizi mpya ambazo serikali ya awamu ya tano imedhamiria kuondoa hiyo changamoto.” Aliongeza Masauni

Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma,Kamishna Msaidizi Simon Marwa alisema wanamshukuru Mheshimiwa Rais Dkt. John Magufuli kwa kiasi hicho cha fedha ambapo wao walipata mgao wa Shilingi Milioni 150/=  huku akitaja idadi ya nyumba walizojenga.

“Nyumba zishakamilika na askari wa vyeo vya chini wameshahamia kama maelekezo ya Mheshimiwa Rais yalivyosema, hapa kuna nyumba sita ambazo kuna vyumba viwili vya kulala, sebule na chumba cha kulala kwa kila nyumba,” alisema RPC Simon

Kamanda Simon alisema mkoa wa Ruvuma una wilaya tano za Songea, Tunduru, Mbinga, Namtumbo na Nyasa huku mapendekezo ya nyumba hizo kwa mkoa huo zikijengwa wilayani Namtumbo ambako changamoto ya makazi ilikua kubwa tofauti na wilaya zilizobakia.

Fahamu Zaidi Kuhusu Ugonjwa Wa Mshipa Wa Ngiri (Hernia/Hydrocele)

$
0
0
Ngiri au Hernia ni aina ya ugonjwa ambao unampata mtu baada ya misuli au kuta za tishu mwilini zinazoshikiria au kubeba viungo (organs) fulani mwilini kupoteza uimara wake au kuwa na uwazi (Opening) na hivyo kusababisha viungo hivyo kutoshikiriwa ipasavyo katika sehemu vinapostahili kuwepo.

Katika mwili wa binadamu, maeneo ambayo tatizo hili hutokea mara kwa mara ni maeneo ya tumboni, katika eneo la kinena, eneo la paja kwa juu na pia ngiri inaweza kutokea katika eneo ambalo mtu alifanyiwa upasuaji (operesheni).

Dalili za Ngiri
Tumbo kuunguruma, kiuno kuuma, kupata choo kama cha mbuzi, kushindwa kufanya tendo la ndoa, mishipa ya uume kulegea, kutokuwa na hamu ya kulundia tendo la ndoa, korondani moja kuvimba, mgongo kuuma.

Dalili zingine za ugojwa wa ngiri ni pamoja na;
Uvimbe unaoteremka kuingia ndani ya korodani unaojulikana kitaalamu kama Direct Scoratal inguinal Hernia.


Uvimbe unaojitokeza tumboni na kuteremka hadi ndani ya korodani, uvimbe huu hauumi na unaweza kurudishwa kwa urahisi iwapo mgonjwa atalala chali na kusukuma kwa vidole, uvimbe huu.


Na pindi ukikubali kurudi ndani ndipo unapoitwa Reduible direct scrotal inguinal hernia.


Na pia endapo utashindikana kurudi tumboni ndipo unapoitwa Irreduible direct scrotal inguinal hernia.


Ugojwa huu wa ngiri unaweza kutibika

Kwa Ushauri na Msaada  Wasaliana na 
0713785111

Taarifa Ya Kusitishwa Kwa Huduma Za Usafiri Wa Reli Ukanda Wa Kaskazini (Tanga & Kilimanjaro)

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Arejea Nchini

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa, Ieo Oktoba 29, 2019 amerejea nchini akitoka Baku nchini, Azerbijan ambako alimwakilisha Rais Dkt. John Pombe Magufuli katika mkutano wa 18 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Nchi zisizofungamana na upande wowote.

Baada ya kuwasili katika uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Waziri Mkuu amepokelewa na Naibu Spika wa Bunge Dkt. Tulia Ackson Mwansasu pamoja na viongozi wengine wa Mkoa wa Dar es salaam.

Awali, Mheshimiwa Majaliwa alimwakilisha Rais Dkt. John Pombe Magufuli katika Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Mataifa ya Afrika na Urusi uliofanyika katika mji wa Sochi nchini Urusi.

 (mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU

Ofisi Ya Makamu Wa Rais Yakutana Na Kamati Ya Kudumu Ya Bunge Ya Viwanda, Biashara Na Mazingira.

$
0
0
Imebainika kuwa Sera ya Usimamizi wa Mazingira (1997) na Sheria ya Usimamizi wa Mazingira Na.20 ya mwaka 2004 (Sura ya 191) ndio muundo muhimu wa usimamizi wa mazingira nchini. 
 
Hayo yamesemwa hii leo na Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Mussa Sima mara baada ya kuwasilisha taarifa ya utekelezaji wa mpango wa pili wa Maendeleo wa miaka mitano katika Sekta ya Mazingira mbele ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira jijini Dodoma.
 
Naibu Waziri Sima amesema katika  kuhusisha masuala ya kuimarisha usimamizi wa rasilimali
Ofisi yake imeandaa Sera, Sheria na Mikakati inayohusiana na uhifadhi wa Rasilimali za  Misitu, vyanzo vya Maji, Ardhi oevu, Wanyamapori, Gesi asilia, Madini na Nishati.
 
Mambo mengine yaliyotekelezwa ni pamoja na kuongoa mifumo ikolojia ya majini iliyoharibika ili kuwepo kwa huduma bora kwa afya ya jamii na ikolojia; kuhifadhi rasilimali za bahari kwa maendeleo endelevu, Miradi na kampeni mbalimbali zimetekelezwa  zikilenga kupunguza uharibifu wa ardhi kwa maendeleo endelevu. 
 
Aidha katika kuimarisha mifumo ya kijamii ya usimamizi wa rasilimali, Naibu Waziri Sima amesema Ofisi yake imeimarisha usimamizi wa mazingira katika maeneo mbalimbali ya nchi kupitia Mradi wa Bonde la Ziwa Nyasa, Mradi wa kurejesha ardhi iliyoharibika, Mradi wa usimamizi endelevu wa ardhi, ambayo yote inasimamiwa na Ofisi yake.
 
Katika jitihada za kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi, Ofisi ya Makamu wa Rais imeandaa miradi mbalimbali na kukuza teknolojia za nishati jadidifu zinazoweza kurejereshwa (biogas, petroli gesi (LPG), nishati ya jua,pepo na joto la ardhi) pamoja na kusaidia programu za utafiti, kukuza teknolojia mpya, mbegu bora, udhibiti wa wadudu waharibifu, na mbinu bora za kilimo.
 
Wakichangia wasilisho hilo Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira Mhe. Suleiman Saddiq na Kanali Mstaafu Masoud Ali ameishauri Serikali kuwa na Mikakati thabiti ya kuzuia uharibifu wa Mazingira nchini ikiwa ni pamoja na kuhakikisha ushirikishwaji wa wananchi katika kutunza rasilimali za misitu, ardhi na mazingira yanayowazunguka kwa kushirikiana na wakaguzi wa Mazingira.
 
Kamati ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira hii leo imepokea taarifa  ya Ofisi ya Makamu wa Rais –Mazingira kuhusu utekelezaji wa wa Mpango wa miaka mitano wa Maendeleo kwa Sekta ya Mazingira (Mafanikio na changamoto) pamoja na Ripoti ya hali ya mazingira Nchini.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatano October 30


Maambukizi Ya Vvu Yapungua Kwa Asilimia 2.3

$
0
0
Na WAMJW- DSM
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu amesema kuwa maambukizi ya VVU yamepungua kutoka asilimia 7 mwaka 2003/4 hadi asilimia 4.7 mwaka 2016/17.

Waziri Ummy amesema hayo jana wakati wa mkutano wa kujadili maendeleo ya utekelezaji wa sera ya pamoja ya ushirikiano na Serikali ya Marekani kupitia PEPFAR cop 19 kuhusiana na masuala ya VVU na UKIMWI uliofanyika jijini Dar Es Salaam. “Kuanzia huduma za UKIMWI zianze kutolewa nchini tumeshuhudia mafanikio makubwa kwa upande wa kupunguza maambukizi kutoka asilimia 7 mwaka 2003/4 hadi asilimia 4.7 mwaka 2016/17". Amesema Waziri Ummy.

Aidha, Waziri Ummy amesema kuwa Serikali ya Tanzania kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa maendeleo ikiwemo PEPFAR inaendelea kupanga mikakati mbalimbali ya kudhibiti maambukizi ya UKIMWI, kutoa huduma na matibabu kwa watu wanaoishi na virusi.

Mbali na hayo Waziri Ummy amedai kuwa Serikali imefanikiwa kutoa huduma za utambuzi na matibabu, huku akisisitiza kuwa dhana ya kwamba UKIMWI ni ugonjwa wa kifo imeisha.

Hata hivyo, Waziri  Ummy amesema, kufikia mwezi Septemba mwaka 2019 idadi ya watu waliopima na kujua afya zao imefikia asilimia 77.2 na kati yao asilimia 98 wanaendelea na huduma za VVU pamoja na matumizi ya ARV.

Kwa upande wake Balozi wa Marekani nchini Dr. Inmi Patterson amesema Serikali ya Marekani itaendelea kushirikiana na Serikali ya Tanzania katika mapambano dhidi ugonjwa wa UKIMWI na ameipongeza Serikali kupitia Wizara ya Afya kwa jitihada kubwa inazofanya kwa kushirikiana na wadau mbalimbali katika kudhibiti maambukizi na kutoa huduma bora za VVU kwa watu waliogundulika na maambukizi.

Mkutano huo ulijumuisha wadau mbalimbali akiwemo mwakilishi wa Shirika la Afya duniani nchini Tanzania Dkt. Tigest Ketsela pamoja na wataalam kutoka Wizara ya Afya wakiongozwa na Mkurugenzi wa kinga Dkt. Leonard Subi, Ofisi ya Rais TAMISEMI, Tume ya kudhibiti na kupambana na UKIMWI (TACAIDS) pamoja na wadau mbalimbali.

Dr Gwajima: Tusimhujumu Rais, Komesheni Ubadhirifu wa Dawa

$
0
0
Na Atley Kuni- TAMISEMI.
Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Dkt. Dorothy Gwajima, amewataka Wafamasia wa Mikoa kote nchini kupambana na kukomesha watu wanaofanya ubadhilifu wa dawa zinazotolewa na serikali kwenda kwenye sehemu za kutolea huduma za afya sambamba na kutafsiri falsafa ya hapa kazi tu kwa vitendo.

Akizungumza katika kikao kazi cha wataalam hao kinachofanyika mjini Dodoma, alisema Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli ametekeleza vema ilani ya Chama cha Mapinduzi kwakuijali na kuipa kipaumbele sekta ya afya na ndio maana katika mwaka wa fedha 2019/20 serikali imepitisha bajeti ya Shilingi bilioni 57.4 ambapo katika mgawanyo eneo la dawa ni miongoni mwa vipaumbele vitatu vilivyo pewa umuhimu.

“Sasa tusimhujumu Mhe. Rais ambaye ameshafanya kazi kubwa na sisi tuliomo ndani ambao tumewekwa kusimamia tunaujuzi na utaalam sehemu ambayo yeye hawezi kuingia, watu wanaiba dawa tunawaangalia, wanaiba vitendanishi tunawaangalia, tutakuwa hatutimizi wajibu wetu kama matazamia yake naya wanachi yanavyotaka” alisema Gwajima.

Gwajima amewataka Wafamasia hao kutumia mfumo wa Ugavi wa dawa wa (elmis) ambao kimsingi taarifa zote za dawa zinaingizwa na kutumika kama muhtadha wa kuombea dawa kwa kila robo. Alisema mfamasia wa Mkoa atakuwa na wajibu wa kuhalalisha maombi ya dawa kwenda MSD kila mara, huku akiitaja mikoa ya kuanzia katika zoezi hilo ni pamoja na Singida, Dodoma, Manyara, Kagera na Geita.

“Tunataka kufanyika kwa Medicine Audit kila robo na taarifa yake kwa kila mkoa iwasilishwe OR-TAMISEMI” alisema Gwajima na kuongeza kuwa “lengo ni kuchakata taarifa za mifumo ya dawa ili kubaini kama kuna hazina ya dawa za kutosha au lah, ili kuweza kusaidia maeneo ambayo yanaupungufu wa dawa.” Alisisitiza Gwajima.

Katika hatua nyingine Gwajima alisema Serikali hivi sasa ipo katika maboresho makubwa ya mfumo wa uendeshaji wa shughuli za Afya (Government of Tanzania Health Management Information System-GoTHOMIS) ambao baada ya kukamilika kwake mfumo utatoa taarifa nyingi za makusanyo ya fedha za dawa mpaka ngazi ya mtumiaji wa mwisho.

Awali kabla yakumkaribisha Mgeni Rasmi, Mkurugenzi wa Idara ya Afya na Ustawi wa Jamii OR-TAMISEMI, Dkt. Ntuli Kapologwe, alisema Sekta ya Afya imekuwa miongoni mwa sekta zilizo pewa kipaumbele na Mhe. Rais hivyo kama wataalam lazima tuoneshe kwa vitendo kuwa Mhe. Rais hajakosea katika hili.

“Mtakumbuka ziara ya mwanzo kabisa Mhe. Rais, alijielekeza katika sekata hii muhimu kwa mustakabali wa maendeleo nchi hasa wakati huu tunapoelekea katika uchumi wa kati ifikapo 2025. Lakini hakuishia hapo toka ameingia madarakani imeendelea kutenga fedha kwaajili ya kujenga na kukarabati vituo vya kutolea huduma za afya, ambapo katika mwaka wa fedha 2017/18 vituo vya afya 352 zikiwepo Hospitali 9, Vituo vya Afya 304 na Zahanati 39 zilikarabatiwa, lakini hivi sasa vituo vinavyo jengwa na kukarabatiwa vimefikia 470 zikiwemo hospitali 67 mpya za Halmashauri ambazo zitakuwa na idara kamili ya dawa” alisema Kapologwe.

Kikao cha Wafamasia kimetayarishwa na Ofisi ya Rais TAMISEMI kwa ushirikiano na wadau wa maendeleo, lengo likiwa nikuweka mipango ya kuhakikisha mianya ya ubadhilifu wa dawa inakomeshwa lakini pia kuweka mikakati endelevu ya upatikanaji wa dawa katika sehemu zote za kutolea huduma za afya.

Taarifa Kwa Umma: Usitumie Progaramu Za Simu,Whatsap Zilizoghushiwa Kuwa Za NIDA

Mwenyekiti Tume Ya Madini Afanya Ziara Dodoma

$
0
0
Na Greyson Mwase, Dodoma
Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula amefanya ziara Wilayani Dodoma Mjini lengo likiwa ni kukagua shughuli za uchimbaji wa madini  ya ujenzi pamoja na kutatua kero mbalimbali.

Katika ziara yake Profesa Kikula aliambatana pamoja na Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Dodoma, Jonas Mwano na maafisa kutoka Makao Makuu ya Tume ya Madini.

Mara baada ya kuwasili katika Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Mjini, Patrobass Katambi na kupokelewa na Katibu Tawala wa Wilaya hiyo, Michael Maganga, Profesa Kikula alianza ziara yake kwa kutembelea  kituo cha ukaguzi wa madini ujenzi cha Nala kilichopo nje ya jiji la Dodoma na kutembelea baadhi ya machimbo ya mchanga.

Akiwa katika machimbo ya mchanga yanayomilikiwa na kampuni ya Tripple I General Supply Limited yaliyopo katika eneo la Mbalawala, Wilayani Dodoma Mjini mara baada ya kupokea taarifa ya uendeshaji wa shughuli zake, Profesa Kikula aliitaka kampuni hiyo kuhakikisha inaandaa mkataba na kusaini kati yake na wanakijiji wanaozunguka kampuni hiyo kwa ajili ya utoaji wa huduma za jamii (corporate social responsibility) na kuepuka migongano.

“Ni vyema kampuni ikahakikisha kunakuwepo na mkataba au muhtasari unaotambulika kisheria kwa ajili ya makubaliano ya maeneo ambayo kampuni itasaidia kijiji katika kipindi fulani kulingana na vipaumbele vya wananchi,” alisema Profesa Kikula.

Profesa  Kikula alisisitiza kuwa, ni vyema wananchi wakanufaika na rasilimali za madini  kwa kupata huduma za jamii kutoka kwa wawekezaji ikiwa ni pamoja na shule, vituo vya afya, miundombinu, maji na kuendelea kusema kuwa kampuni inatakiwa kuwashirikisha wananchi kwa kuwapa fursa ya kutoa huduma kwenye kampuni kama vile vyakula, ajira.

Awali akitoa taarifa kwa Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula, Mkurugenzi wa Kampuni ya Tripple I General Supply Limited,  Maglan Kipuyo alimpongeza Mwenyekiti kwa ziara yake na kusisitiza kuwa kupitia ziara zake, kero mbalimbali zimekuwa zikitatuliwa pamoja na kupewa elimu bora ya namna ya kuchimba madini ya ujenzi kwa kufuata Sheria ya Madini na kanuni zake.

Akielezea mafanikio ya kampuni yake, Kipuyo alisema tangu kuanzishwa kwa kampuni mapema mwaka huu kampuni imefanikiwa kutoa ajira zaidi ya 200, ununuzi wa mabati kwa ajili ya ujenzi wa Ofisi ya kijiji cha Mbalawala na kuboresha miundombinu ya barabara.

Alitaja mafanikio mengine kuwa ni pamoja na malipo ya  wastani wa shilingi milioni 15 kama mrabaha kwa Ofisi ya Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Dodoma kwa kila mwezi na kuanza kwa mchakato wa ujenzi wa kisima cha maji kitakachowanufaisha wanakijiji wa Mbalawala.

Aidha, Kipuyo aliongeza kuwa mafanikio mengine ni pamoja na  kuwezesha wenye viwanda vidogo vya kufyatulia matofali mkoani Dodoma kupata mchanga.

Katika hatua nyingine Profesa Kikula alimtaka Afisa Madini wa Mkoa wa Dodoma, Jonas Mwano kuendelea kutoa elimu kwa wachimbaji wa madini ya ujenzi kuhusu umuhimu wa kutoa huduma kwa jamii (corporate social responsibility) kwa wananchi wanaozunguka migodi yao kama Sheria ya Madini na kanuni zake inavyofafanua.

Profesa Kikula pia alitembelea machimbo ya mchanga yanayomilikiwa na  Wema Msuya yaliyopo katika eneo la Mundemu Wilayani Dodoma Mjini na kusisitiza umuhimu wa wachimbaji wa madini ya mchanga kuchimba kwa kufuata Sheria ya Madini na kanuni zake pamoja kuzingatia suala la usalama na utunzaji wa mazingira.

“Mbali na kuchimba mchanga na kulipa mapato Serikalini ni vyema mkahakikisha suala la usalama kwenye shughuli zenu linazingatiwa na kuepusha ajali zinazoweza kujitokeza,”alisema Profesa Kikula.

Naye Meneja wa machimbo hayo, Richard Tairo  mbali na kumpongeza Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula kwa kufanya ziara na kutatua changamoto mbalimbali mara moja alimhakikishia ushirikiano kati ya wachimbaji wa madini ujenzi na Serikali ili Sekta ya Madini  iwe na mchango mkubwa kwenye ukuaji wa uchumi wa nchi.

Wakati huo huo Profesa Kikula alitembelea viwanda vya kufyatulia matofali vilivyopo katika maeneo ya Vyeyula na Mlimwa C Wilayani Dodoma Mjini ili kujionea namna shughuli zinavyoendeshwa pamoja na ulipaji wa kodi Serikalini.

Profesa Kikula aliitaka Ofisi ya Afisa Madini wa Mkoa wa Dodoma kusimamia kwa karibu zaidi na kuwa wabunifu kwenye zoezi la ukusanyaji wa kodi mbalimbali ili  Serikali iweze kupata mapato yake stahiki.

Wananchi waliovamia Mpaka wa Tanzania na Zambia Watii Agizo la Rais la Kubomoa

$
0
0
Zaidi ya asilimia 80 ya Wananchi waliovamia Mpaka wa Tanzania na Zambia eneo la Tunduma wametii agizo la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli na kubomoa majengo na vibanda vyao ili kuacha Mpaka wazi.

Mkuu wa Mkoa wa Songwe Brig. Jen. Nicodemus Mwangela ameyasema hayo mara baada ya kukagua maendeleo ya utekelezaji wa agizo la Rais na kukuta wananchi wametii na wamebomoa.

“Ninawapongeza wananchi wa Tunduma kwakuwa wameitikia agizo la Rais na utekelezaji unakwenda vizuri sana, nyumba na vibanda vingi vimebomolewa na watu wanahamisha bidhaa na vifaa ambavyo watavitumia wakienda sehemu nyingine, hivyo ninawapongeza sana kwa Mwitikio mzuri.”, amesema Brig. Jen. Mwangela.

Ameongeza kuwa kutokana na kuridhishwa na kasi ya kubomoa ameamua kuwaongezea siku tatu ambazo zitatumika kumalizia kuhamisha bidhaa na vifaa kutoka katika eneo la mpaka na baada ya hapo chochote kitakachobaki hapo kitabomolewa na serikali.

Brig. Jen. Mwangela amesema wananchi waliobaki wanapaswa kuondoka na kuacha Mpaka wazi kwakuwa vyombo vya Ulinzi na Usalama kwenye mipaka waweze kutekeleza majukumu yao bila bila kukwamishwa na kituo pia hakutaruhusiwa shughuli za biashara katika eneo la Mpaka.

Naye Kamanda wa Polisi Mkoa wa Songwe George Kyando amesema Jeshi la Polisi limerahisishiwa namna ya kupambana na uhalifu na kuzuia Magendo kutokana na kushafishwa eneo la mpaka.

Kyando amesema anampongeza Rais Magufuli kwa amri ya kusafisha mpaka huo kwani hali ya amani itazidi kuimarika katika eneo hilo na pia ameshuhudia zoezi la kubomoa likifanyika kwa amani.

Afisa Uhamiaji Mkoa wa Songwe Philon Kyetema amesema kabla ya usafishaji wa Mpaka, zoezi la kupambana na wahamiaji haramu lilikuwa gumu kwakuwa walikuwa wanaweza kuingia na kutoka nchi jirani kwa urahisi kupitia vichochoro.

Amesema Wananchi wa Tunduma wategemee hali kuimarika Zaidi kwakuwa sasa wataweza kufanya ukaguzi wakati wote na kwa kutumia njia mbalimbali kama magari pikipiki na hata kwa miguu kwakuwa wamerahisishiwa mazingira ya kufanyia kazi.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images